Yuda 1:7-8
[7]Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele. [8]Kadhalika na hawa, katika kuota kwao, huutia mwili uchafu, hukataa kutawaliwa, na kuyatukana matukufu.
[7]Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele.
[8]Kadhalika na hawa, katika kuota kwao, huutia mwili uchafu, hukataa kutawaliwa, na kuyatukana matukufu.
Maandiko hayo, yanazunguzia tabia ya watu waasi ambao wameshaijua kweli lakini wamependa kuendelea katika dhambi zao.
Hivyo katika andiko hilo anasema katika kuota kwao huutia mwili uchafu…sasa huko kuota kunakozungumziwa hapo sio ile hali ya kulala na kuota ndoto…hapana bali ni maono yao, yaani ndoto zao za jinsi watakavyokuwa baadaye, namna wanavyojiona baadaye..sasa hiyo namna ndio sio nzuri bali ni ya kujitia mwili uchafu.
Kuutia mwili uchafu ni ile hali ya kuruhusu matendo yote ya mwilini kukutawala…matendo hayo yanazunguziwa vema katika Wagalatia 5:19-21
[19]Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, [20]ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, [21]husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.
[19]Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
[20]ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
[21]husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.
Haya ndio watu wanayoyaona mbele yao, wanayoyawaza na kuyatazamia wakati wote, wanayoyaota yaje kutokea..
Fikra za watu wengi leo ni ili baadaye waishi kiasherati, wafanye anasa kwa pombe, ulafi, waibe..
Hii ni kutufunulia pia kunajisika sio mpaka mtu akatende jambo lenyewe bali ile kulitamania, tu au kulitarajia mbeleni…tayari ameshajinajisi.
Jiulize kuota kwako ni kupi? Kama mtoto wa Mungu, lazima tujue sisi yatupasa kuota maendeleo ya kazi ya Mungu, kuota ukuaji wa kiroho, kuota upendo, kuota kuingia mbingu mpya na nchi mpya,..namna hiyo humfanya mtu kuendelea katika utakaso.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Yuda alimaanisha nini kusema “wokovu ambao ni wetu sisi sote”
KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 13 (Kitabu cha Hosea).
Print this post
2 Wafalme 3:16-17
[16]Akasema, BWANA asema hivi, Fanyeni bonde hili lijae mahandaki. [17]Kwa kuwa BWANA asema hivi, Hamutauona upepo, wala hamtaiona mvua, ila bonde hilo litajaa maji; nanyi mtakunywa, ninyi, na ng’ombe zenu, na wanyama wenu.
[16]Akasema, BWANA asema hivi, Fanyeni bonde hili lijae mahandaki.
[17]Kwa kuwa BWANA asema hivi, Hamutauona upepo, wala hamtaiona mvua, ila bonde hilo litajaa maji; nanyi mtakunywa, ninyi, na ng’ombe zenu, na wanyama wenu.
Ilifika wakati wana wa Israeli, walikwama, baada ya kuona wapo katika eneo ambalo ni kame kupita kiasi, na hawana msaada, nguvu zimewaishia maadui zao wapo karibu kuwaangamiza..
Wakalia sana, Lakini baadaye wakapata akili ya kumlingana Mungu kwa kuulizia kupitia nabii wake Elisha. Lakini maagizo waliyopewa hayakuwa bado marahisi sana, kama walivyotegemea.
Hawakufanyiwa muujiza wa maji kutokea mwambani kama kipindi cha Musa, au mvua kushuka mbinguni…bali waliambiwa wachimbe mahandaki…yaani mashimo makubwa sana…pale jangwani..
Fikiri umechoka umeishiwa nguvu, halafu unaambiwa uchimbe mashimo..upige sururu chini, upige jembe chini, utoe jasho la kutosha si jambo jepesi..
Lakini baadaye tunaona Mungu anawaambia hamtaona mvua bali hayo mabonde yote yatajaa maji. Na ndivyo ilivyokuwa. Kwa waliochimba sana walipata maji sana, kwa waliochimba kidogo walipokea maji sawasawa na mashimo yao.
Je nini Bwana alikuwa analifundisha kanisa lake.
Katikati ya jangwa, Si muda wa kulia na kusumbuka, kinyume chake shika jembe lako, chepe lako anza kuchimba mashimo.
Kwanini watu wengi hawaioni mvua ya Mungu ya neema au baraka za rohoni zikidumu kwao lakini kwa wengine hudumu…sio kwamba Mungu anaupendeleo…hapana…bali wale wengine tayari wameshachimba mashimo marefu ya kuhifadhi maji mengi…Kwasababu mvua au umande wa Mungu sikuzote hushuka au hupanda juu ya nchi yote lakini wale wenye visima ndio hudumu na maji yake mda mrefu kwa wengine hudumu tu kwa muda mfupi pale juu, baadaye kidogo hupotelea ardhini…
Kuchimba handaki ni kudumu sana katika maombi, pamoja na kutendea kazi kile ulichokitaka kwa Mungu…
Kwa mfano unamwomba Mungu akupe mke/mume mwema, labda leo huoni kutokea kwa yoyote upo jangwani tu, unakaribia kukata tamaa…hakikisha unazidisha sana maombi, lakini pia unajitunza na kuanza kujifunza mafunzo ya kuwa mke/mume mwema, unaonyesha kivitendo zile sifa za mke mwema/mume mwema anazopaswa awe nazo kibiblia, kwamfano wewe ni mwanamume unafahamu kuwa yapo majukumu ya kibaba mbele yako, kwamba unapaswa uwajibike kwa kipato cha familia yako, lakini hilo kama hulisumbukii na bado unatarajia Bwana akuletee mke..ni kweli atakuletea, atapandisha umande wa maji juu ya nchi lakini hatimaye atashindwa kudumu na wewe katika hatua za awali akiona huwezi kusimama kwenye wajibu wako…baadaye utalalamika mbona wanawake wananikimbia..vilevile mwanamke akikosa tabia njema..wanaume watakuja na kumkimbia baadaye…kwasababu hakuwa na muda wa kujichimbia mahandaki yake, kitabia.
Kila eneo liwe la kihuduma, kikazi, kiafya..wekeza sana kwenye mahandaki kwasababu mvua/ umande utakuja tu…kwasababu kwa Mungu kushusha baraka si jambo la kulisumbukia sana, yeye anawanyeshea mvua waovu na wema alisema hivyo (Mathayo 5:45) bali kuzihifadhi hizo baraka ndio ugumu ulipo.
Mwanzo 2:6
[6]ukungu ukapanda katika nchi, ukatia maji juu ya uso wote wa ardhi.
Wekeza kwenye maombi na kutendea kazi imani yako kwa vitendo. Zaidi ya kutarajia tu Mungu atende mwenyewe.
Bwana akubariki
Huu ni mfululizo wa masomo yawahusuyo watumishi wa Mungu.
Kuna makosa mengi yapo miongoni mwa mitazamo yetu sisi (watumishi wa Mungu), tunadhani mafanikio ni pale hasaa huduma yetu inaposhawishi mioyo ya wengi …pale tunapoona umati unaipokea, na kuishangilia.
Lakini tukifuatilia huduma za manabii wengi wa Mungu, kwenye biblia kama vile Isaya na Ezekieli, Yeremia hawakuwa na mafanikio makubwa ya mahubiri yao, kama tunavyodhani hivi leo, kinyume chake waliishia kukataliwa, kuteswa na kuuliwa, kwa ufupi huduma zao ziliwavunja sana moyo, lakini kwasababu aliyewatuma ni Bwana, injili yao imesimama vizazi na vizazi mpaka leo..
Walijua wanakwenda kuhubiri kwa watu ambao wana mioyo migumu sana…na Mungu aliwaeleza kabisa, lakini walifanya hivyo kwa uaminifu wote, kana kwamba wanauokoa umati wa watu.
Yeremia 7:27
[27]Nawe utawaambia maneno hayo yote; lakini hawatakusikiliza, nawe utawaita; lakini hawatakuitikia.
Ezekieli 2:3-7
[3]Akaniambia, Mwanadamu, nakutuma kwa wana wa Israeli, kwa mataifa wanaoasi, walioniasi mimi; wao na baba zao wamekosa juu yangu, naam, hata hivi leo. [4]Na wana hao wana nyuso zisizo na haya, na mioyo yao ni migumu. Mimi nakutuma kwa hao; nawe utawaambia, Bwana MUNGU asema hivi. [5]Nao, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia, (maana ndio nyumba ya kuasi hao), hata hivyo watajua ya kuwa nabii amekuwako miongoni mwao. [6]Na wewe, mwanadamu, usiwaogope hao, wala usiyaogope maneno yao, ijapokuwa miiba na michongoma i pamoja nawe, nawe unakaa katikati ya nge; usiyaogope maneno yao, wala usifadhaike kwa sababu ya nyuso zao, wajapokuwa ni nyumba yenye kuasi. [7]Nawe utawaambia maneno yangu, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia; maana hao wanaasi sana.
[3]Akaniambia, Mwanadamu, nakutuma kwa wana wa Israeli, kwa mataifa wanaoasi, walioniasi mimi; wao na baba zao wamekosa juu yangu, naam, hata hivi leo.
[4]Na wana hao wana nyuso zisizo na haya, na mioyo yao ni migumu. Mimi nakutuma kwa hao; nawe utawaambia, Bwana MUNGU asema hivi.
[5]Nao, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia, (maana ndio nyumba ya kuasi hao), hata hivyo watajua ya kuwa nabii amekuwako miongoni mwao.
[6]Na wewe, mwanadamu, usiwaogope hao, wala usiyaogope maneno yao, ijapokuwa miiba na michongoma i pamoja nawe, nawe unakaa katikati ya nge; usiyaogope maneno yao, wala usifadhaike kwa sababu ya nyuso zao, wajapokuwa ni nyumba yenye kuasi.
[7]Nawe utawaambia maneno yangu, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia; maana hao wanaasi sana.
Hakuna jambo linaloumiza kwa mtumishi wa Mungu pale unapoona unahubiria jamii kubwa ya watu lakini matokeo yoyote huoni kwao,…Ni vema ufahamu kuwa Mungu hakutumi ukawe mshawishi, anakutuma ukawe mwaminifu kwa kazi yake.
Kushindwa kwako katika huduma sio, kukosa watu wa kukusikiliza au watu kupungua kwenye huduma yako, kushindwa kwako ni kukosa uaminifu..hilo tu.
Leo hii ungewekwa kwenye nafasi ya Nuhu ambaye aliuhubiria ulimwengu kwa miaka mia moja na ishirini, na kuambulia tu familia yake, ungeshamkimbia Mungu siku nyingi na kusema sijatumwa, ungewekwa kwenye nafasi ya Yeremia, Mika, sefania ungesema huyu si Mungu, ni akili zangu zimenituma, ungesema ninachofanya ni uwendawazimu…hii sio huduma lazima kuna shida mahali, haiwezekani watu hawataki kugeuka, na kutubu, ungewekwa nafasi ya Musa ungesema hawa nilionao sio watu wa Mungu ni kizazi cha nyoka, pamoja na ishara zote na miujiza…lakini bado wanatengeneza ndama wa shaba, wanaasi, wananung’unika…najitaabisha bure tu.
Kama mtumishi wa Mungu jitahidi sana kuwa mwaminifu, hata kama huoni ukuaji wowote, au mafanikio yoyote ya machoni, ya kuokoka kwa watu wengi…wewe ifanye kazi yake, mtumikie yeye, timiza ratiba zako. mtumikie Mungu kwa mtazamo huo wa uaminifu na sio wa matokeo, utadumu na hutapindishwa na chochote.
Kwani thawabu yako ni kubwa mbinguni.
Mungu akubariki sana.
MHESHIMU MCHUNGAJI WAKO.
SIKU ZA WATUMISHI WA MUNGU.
KARAMA TUZIPATAZO KWA MSAADA WA WATU WENGI.
Wagalatia 1:10
[10]Maana, sasa je! Ni wanadamu ninaowashawishi, au Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa hata sasa nawapendeza wanadamu, singekuwa mtumwa wa Kristo.
Kuna dhambi moja ya kale, ambayo imekuwa sugu sana, na kibaya zaidi imekuwa tishio kubwa kwa mwanadamu, hata kumfanya ashindwe kabisa kuyatenda mapenzi ya Mungu, haijalishi atamaanisha kiasi gani, dhambi yenyewe si zile tunazozifahamu, kama vile uzinzi, uongo, n.k., Hapana bali ni dhambi ya “kuwapendezesha wanadamu”
Ni dhambi ya kufanya jambo kwa hofu ya kuchukiwa na watu, kufikiriwa vibaya na watu. Hofu ya Kutengwa na watu, kudharauliwa na watu.
Ni kufanya jambo machoni pa watu ili utukuzwe, uonekane mkuu, uonekane ni wa rohoni, uonekane unajua kuliko wengine… ni kuwa radhi kuvumiliana na vilivyo kinyume na Mungu ilimradi tu mbele za watu, usipoteze heshima yako.
Bwana Yesu alijua moyo wa mwanadamu unafurahia hali hii, upo radhi kufanya vitu kinafki, bila kujali haja ya Mungu ni nini.
Mathayo 6:2,5
[2]Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu… [5]Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao.
[2]Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu…
[5]Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao.
Ni hali mbaya sana, Mahali pengine waliogopa kumkiri hadharani kwasababu watapoteza heshima zao za kikuhani machoni pa watu..
Yohana 12:42-43
[42]Walakini hata katika wakuu walikuwamo wengi waliomwamini; lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakumkiri, wasije wakatengwa na sinagogi.
Madhara ya dhambii hii ni kwamba, Tunaweza tukayapindisha maandiko tusiongee ukweli wote, tuhubiri injili ya juu juu, injili ya vichekesho, tusikemee aina Fulani ya dhambi kwasababu zitawafanya watu wainamishe vichwa vyao, matokeo yake wasije kanisani.
Hali hii inatufanya tuwe na kigeugeu, ilimvaa hata Petro, wakati ule alipoketi na wayahudi, anasema hivi, alipokutana na Watu wa mataifa anasema vingine kwa hofu ya wayahudi, mpaka Paulo alipomwona akamkemea mbele ya wote. (Wagalatia 2:11)
Tunaogopa kuvaa mavazi ya kujisitiri yasiyokuwa na mvuto machoni pa watu, lakini mbele za Mungu yanapendeza, kisa tutaonekana washamba, wazee. Nuru yetu inashindwa kuangaza ulimwenguni.
Ijapokuwa Bwana Yesu aliwapenda sana wanadamu, lakini hakuishi kwa kuziangalia hisia zao zinasemaje, kwasababu sifa za wanadamu, hazitabiriki, leo watakusifia, kesho watakuchukia.. Alipoingia Yerusalemu walimwita mbarikiwa Hosana, wiki moja baadaye wakasema Asulubiwe.. Lakini katika nyakati zote hizi hatuoni Bwana Yesu akigeuka, akipindisha pindisha msimamo wake, alipotukanwa, hakutazama umati unasemaje, aliutazama utukufu wa Mungu unamwelekezaje.
Hii huitwa hofu ya mwanadamu, Tunasahau kuishi kwa hofu ya Mungu, yaani Mungu anasemaje, Anajisikiaje, tunawaza sana wanadamu wanasemaje, wanafikirije..Hatupaswi kuwafanya watu sanamu zetu.
Ili tushinde hii hali kwanza ni lazima tujue kuwa kumpendezesha kila mtu ni jambo ambalo haliwezekani, hivyo usiogope kufikiriwa kivingine pale unapokusudia kuishi maisha yampendezayo Mungu.
Lakini pia ni lazima ufahamu, wanadamu hawana sifa za kweli, za kudumu, hivyo acha kufanya vitu, kuwaridhisha, ilihali unajua wewe mwenyewe unaumia ndani kwa ndani, na mwisho jitahidi kufanya mambo yako kwa msukumo wako mwenyewe sirini, bila watu kukutazama, hapo utaua sifa za wanadamu, utaanza kuishi kwa kumwangalia Mungu.
MWONGOZO WA MAOMBI YA WAHUDUMU/ WASIMAMAO MADHABAHUNI.
Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)
USIONDOE ALAMA YA MPAKA ILIYOWEKWA NA MABABA.
WhatsApp
Huu ni mfululizo wa masomo maalumu ya wanawake, ikiwa utapenda kupata madarasa mengine mengi ya nyuma wasiliana nasi kwa namba zilizo chini ya somo hili.
Mariam ni mwanamke ambaye Mungu alimchagua kipekee kuwa mfano bora wa kuigwa wa namna wanawake wa kikristo wanavyopaswa kuwa.
Mariamu alijitunza usichana wake, lakini pia sifa nyingine kubwa aliyokuwa nayo, hakuwa mtu wa kuwaza ki-akili bali aliwaza kwa moyo. Kila jambo lililomfikia halikuishia akilini tu, kwamba ni hoja nzuri tu, au kwamba inaingia akilini, hapana bali alijifunza kulishusha mpaka moyoni, kulitafakari …Na hilo lilimsaidia sana kuwa mwanamke bora…
Embu tafakari haya matukio machache, mwitikio wake ulivyokuwa;
Luka 1:28-29
[28]Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe. [29]Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani?
[28]Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe.
[29]Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani?
Luka 2:17-19
[17]Walipomwona wakatoa habari waliyoambiwa juu ya huyo mtoto. [18]Wote waliosikia wakastaajabu kwa hayo waliyoambiwa na wachungaji. [19]Lakini Mariamu akayaweka maneno hayo yote, akiyafikiri moyoni mwake.
[17]Walipomwona wakatoa habari waliyoambiwa juu ya huyo mtoto.
[18]Wote waliosikia wakastaajabu kwa hayo waliyoambiwa na wachungaji.
[19]Lakini Mariamu akayaweka maneno hayo yote, akiyafikiri moyoni mwake.
Luka 2:48-51
[48]Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni. [49]Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu? [50]Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia. [51]Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake.
[48]Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni.
[49]Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu?
[50]Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia.
[51]Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake.
Hiyo ni kuonyesha ilikuwa ni desturi ya maisha yake, kufikiri kutoka kilindi cha moyoni mwake sio kwa akili zake…
Wazia zaidi, Mariamu aliposalimiwa alijiuliza salama hii, lengo lake ni nini? nyuma ya salamu kuna lengo gani, Mwisho wake ni upi.. hakupokea salamu, ilimradi salamu kisa inamtakia mema…aliivunja vunja kwanza..Na huko ndio kuwaza kwa moyo.
Mabinti wengi leo hii wanaingia kwenye mitego ya kulaghaiwa kwa kutowaza kutoka moyoni..hujiulizi iweje mtu usiyemjua aje kukupa tu salamu ya zawadi, akusifie, na wewe hufikiri salamu hii ni ya namna gani…
Hujiulizi huyu mtu nia yake ni nini? Anatarajia nini kwangu, kumbuka salamu sio lazima tu ije kwa maneno, yaweza kuja kwa kupewa lifti, kupewa nafasi ya upendeleo, kulipiwa manunuzi fulani, dada kuwa makini na salamu hizo, hata kama umeolewa kuwa makini sana. Ni kweli si zote ni mbaya lakini jiulize maudhui yake ni nini? Waza moyoni mwako, Nia ni nini?.
Kama mama yetu Hawa pale bustanini angejiuliza salamu za nyoka ni za namna gani, sote tusingekuwa kwenye matatizo tuliyonayo sasa.
Halikadhalika Mariamu, hakuyaacha maneno yenye jumbe za Mungu yampite hivi hivi, mahali ambapo hajaelewa alihifadhi ndani yake akitumai upo wakati ataelewa vema kwa jinsi anavyozidi kutafakari…alihifadhi matukio yake yote moyoni..
Lakini wanawake wengi wa leo, wanahifadhi maneno yasiyo na maana, utaona moyoni mwao yamejaa maneno waliyosengenywa, waliyoaabishwa, waliodhalilishwa..hayo ndio yanawaganda lakini si maneno ya Mungu..
Wanatumia vibaya nafasi hizo, Na matokeo yake kinachotoka nje ya mioyo yao ni wivu, uchungu, hasira, chuki, masengenyo, badala ya mafunuo, upendo, hekima, na adabu.
Tumia moyo wako kwa lengo la kupambanua na kuhifadhi mambo mema…sio maovu.
Ifike wakati, unasema…lile hubiri lililohubiriwa mwaka juzi mpaka leo linanitafakarisha, lile ono Mungu alilonionyesha utotoni linanirudia rudia akilini, yale maonyo ya mhubiri tuliyokemewa kipindi kile yanazunguka ndani yangu hata sasa siwezi yasahau…
Hayo ndio mambo ya kubeba..
Geuka fikiri kama Mariamu..
Shalom
MAOMBI MAALUMU YA WA-WAMAMA / WANAWAKE WA KANISANI.
MAPAMBO YA WANAWAKE WALIOUKIRI UCHAJI WA MUNGU.
MASOMO MAALUMU KWA WANAWAKE.
2 Yohana 1:10-11
[10]Mtu akija kwenu, naye haleti mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani mwenu, wala msimpe salamu. [11]Maana yeye ampaye salamu azishiriki kazi zake mbovu.
[10]Mtu akija kwenu, naye haleti mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani mwenu, wala msimpe salamu.
[11]Maana yeye ampaye salamu azishiriki kazi zake mbovu.
Ni salamu ya namna gani ambayo ililengwa hapo?
JIBU: Ukisoma habari yote tokea juu utaona mtume Yohana anazungumzia kundi la wadanganyifu ambao walitokea wengi duniani wakati ule, ni kundi la watu waliopinga kuja kwa Yesu katika mwili kwa namna ya kibinadamu, akasema hao ndio wapinga Kristo.
Na mbeleni akatoa katazo la kutowakaribisha hata majumbani kwao, wala kuwapa salamu, maana kuwapa salamu ni kushiriki kazi zao mbovu.
Swali je ni salamu ya namna gani ililengwa hapo.?
Salamu zinazozungumziwa hapo si salamu hizi za kijamii za “umeamkaje, au shikamoo, au za mchana” hapana bali ni salamu za kiroho ambazo hata wakati ule wayahudi walipozisema zilimaanisha ushirika mmoja katika kiimani. Kwamfano, walipokutana walibusiana na kusema “Amani ya Bwana iwe pamoja nawe”..
Sasa salamu kama hiyo utajiuliza ni bwana yupi ikiwa huyo mwingine haamini katika fundisho kama lenu.. ukimsalimia basi unakubaliana na bwana wake ambaye hajaja katika mwili. Tayari umeshazishiriki kazi zake.
Ni sawa na leo labda tuseme unakutana na watu wanaomwamini kweli Yesu, lakini Yesu ambaye hajafufuka, yupo kaburini mpaka sasa, halafu anakuja anakusalimia “Bwana Yesu asifiwe” na wewe unasema Amina..Mtu mgeni akipita akakusikia atajua kuwa mna imani moja kuhusu Yesu Kristo ambaye hajafufuka.
Hivyo hata kwa wakati huu, salamu zetu za kiroho zisimame mahali ambapo tunajua imani tulio nayo kuhusu Kristo ni moja.
Kwasababu salamu tu, hutangaza, zina nguvu kama lilivyo fundisho.
ANDALIZI LA MWISHO LA UJIO WA MPINGA KRISTO.
JAWA SANA MOTO ULAO.
Jina la Bwana wetu YESU KRISTO libarikiwe, karibu katika kujifunza Biblia.
Upo usemi usemao “wanadamu tumeumbiwa maradhi”..Usemi huu ni wa hekima za ulimwengu, ambao Biblia inasema ni upuuzi mbele za Mungu (1Wakorintho 3:19).
Ni kweli maradhi yapo lakini hatupaswi kuyakiri na kuyakumbutia kama sehemu yetu, (ikiwa tumeshampokea YESU) ….hata kama yapo ndani yako si sahihi kusema “hayo ni ya kwako” au “umeumbiwa”, ni kauli ambayo ni hatari sana.
Kwanini Maradhi si sehemu yetu tuliomwamini YESU? Na kwanini hatupaswi kutawaliwa nayo?.
Hebu tujifunze kidogo historia ya Maradhi mabaya na hatari kibiblia.
Kipindi wana wa Israeli wanatoka MISRI, kuelekea nchi ya Ahadi, Kanaani, Mungu aliwaambia yale maradhi yaliyokuwa yanawapata MISRI hayatawafuata Kaanani..
Kumbukumbu 7:15 “Na Bwana atakuondolea ugonjwa wote; wala hatatia juu yako MARADHI YO YOTE MABAYA UYAJUAYO YA MISRI, lakini atayaweka juu ya wote wakuchukiao”.
Maana yake ni kwamba wakiwa Misri pamoja na kwamba walikuwa katika utumwa wa mwilini lakini pia Misri ILITAWALIWA NA MAGONJWA YA KUTISHA (Soma Kutoka 15:26 na Kumbukumbu 28:60).
Misri haikuwa sehemu salama kiroho na hata kimwili, kulikuwa kuna mlipuko wa magonjwa ya ajabu na ya kutisha, ambayo hayo yalitokana na miungu wa Misri waliyokuwa wakiiabudu..Na Bwana aliwaonya wana wa Israeli kwamba wakirudi kuitumikia hiyo miungu basi yale maradhi ya MISRI yatavuka kuwafuata waendako.
Kumbukumbu 28:60 “Naye atakurejezea maradhi yote ya Misri juu yako uliyokuwa ukiyaogopa, nayo yataambatana nawe. 61 Tena kila ugonjwa, na kila pigo yasiyoandikwa katika kitabu cha torati hii, atakutia nayo Bwana juu yako, hata utakapokwisha kuangamizwa”.
Kumbukumbu 28:60 “Naye atakurejezea maradhi yote ya Misri juu yako uliyokuwa ukiyaogopa, nayo yataambatana nawe.
61 Tena kila ugonjwa, na kila pigo yasiyoandikwa katika kitabu cha torati hii, atakutia nayo Bwana juu yako, hata utakapokwisha kuangamizwa”.
Kwahiyo tunachoweza kuona ni kuwa “Magonjwa yote asili yake ni Misri”, na Mungu aliyaweka kwa waMisri kutokana na maisha yao ya kuabudu miungu (shetani)..
Sasa swali kwanini yatutawale sisi ambao hatuabudu miungu ya Misri, na wala hatupo Misri, vile vile kama yanavyowatawala waMisri (watu ambao hawamjui Mungu)?
Ni swali la kutafakari sana..
Ukiona kuna ugonjwa unakusumbua miaka mingi, na umejaribu kutumia matibabu ya hospitalini yaliyo halali lakini tatizo linabaki kuwa sugu, au linakwenda baada ya muda linarudi..hebu wakati wa leo simama na kusema “imetosha”.
Huenda hujajua tu haki yako ndio maana ibilisi anakutesa na kukusumbua…anakujengea saikolojia kwamba huo ugonjwa ni wa kwako na huwezi kupona.. Leo hii simama na kusema “Magonjwa ya Misri si sehemu yangu”.
Kama umeokoka kweli kweli, usikae ukiri kwa kinywa chako, au uamini moyoni mwako kuwa “magonjwa ni sehemu yako”.. anza kuanzia leo kufuta kalenda za kwenda hospitali hospitali kila mara.
Tatizo linalowakabili watu wengi waliookoka ni kuamini na kujiwekea matumaini katika madawa na mahospitali, sio vibaya kuamini hivyo, lakini kunadumaza imani yako kwa MUNGU na kuyapa nafasi magonjwa ya Misri juu yako.
Si kila dalili tu ya mafua unayoyasikia unakimbilia dawa!..si kila homa tu inayokupata unakimbilia hospitalini utaacha lini hiyo tabia?.. Hufanyi dhambi lakini unadumaza imani yako.
Jenga tabia ya kuamini kuwa ninaweza kuwa na afya na uzima bila ya madawa wala hospitali, kwasababu wewe sio Mmisri, kwahiyo Maradhi ya Misri hayakuhusu, wala taarifa za maradhi ya Misri si sehemu yako.
Afya yako ni ya muhimu sana, ukiwa na maradhi hata uwezo wako wa kiutendaji kiroho unakuwa hafifu, hivyo usikubali hata kidogo, maandiko yanatufundisha hivyo kwamba ni mapenzi ya Mungu tuwe na afya zetu..
3Yohana 1:2 “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo”
Ikiwa una maradhi yanayokuonea leo kwa imani fuatisha maneno yafuatayo na yatakuacha haraka sana..
Sema “Bwana YESU ninasogea mbele zako, ninaomba unisamehe nilipofungua mlango wa maradhi katika maisha yangu, lakini pia naomba unisamehe nilipopungukiwa imani, siku leo ninakiri uzima na afya, ninayakataa maradhi yote ya Misri juu ya mwili wangu, kwakuwa mimi sio Mmisri, kuanzia leo mimi ni mzima na wala sitasumbuka tena, ninaomba na kuamini katika jina kuu lako Bwana YESU KRISTO. Amen”
Nini maana ya kuinuliwa juu ya nchi? (Yohana 12:32).
JINSI MATENDO YA IMANI YANAVYOWEZA KULETA UTAMBULISHO MPYA KWA MTU.
UTAIKUZAJE IMANI NDANI YAKO?
Je ni kweli imani ya mtu ndiyo itakayomuokoa, na si kitu kingine?
Je! Imani ya mitume ipo katika maandiko?
Jina la Bwana YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze maandiko..
shetani hana jipya zaidi ya kunakili (kucopy) vile vilivyopo na kuvutumia kinyume.
Kwamfano kafara za wanyama kama mbuzi na kondoo kwaajili ya utakaso hazikuanzia kwa shetani, bali zilianza kwa MUNGU, ambapo katika Agano la kwanza (yaani Agano la kale) damu za wanyama hao zilitumika kwaajili ya utakaso, lakini sasa Agano jipya hazitumiki tena kwani Damu ya YESU ni bora zaidi ya damu za wanyama.
Kwahiyo shetani anachokifanya ni kunakili kilichokuwa kinatumika zamani (kisicho na matumizi tena) na kukileta siku za mwisho kwaajili ya matumizi yake, ndio maana utaona waganga wa kienyeji na wachawi ndio sadaka zao hizo.
Sasa sio tu hilo, lakini pia katika utumishi, shetani anayo desturi ya kutengeneza nakala..
Kwa namna gani?
Hebu turejee ile habari ya yule mchawi aliyeitwa.. “Bar-YESU” katika Matendo 13?..tuzisome habari zake kidogo kisha tuendelee mbele..
Matendo 13:6 “Walipokwisha kupita katikati ya kisiwa chote mpaka Pafo, wakaona mtu mmoja, mchawi, nabii wa uongo, Myahudi jina lake BAR-YESU; 7 mtu huyu alikuwa pamoja na liwali SERGIO PAULO, mtu mwenye akili. Yeye liwali akawaita Barnaba na Sauli waje kwake, akataka kulisikia neno la Mungu”
Matendo 13:6 “Walipokwisha kupita katikati ya kisiwa chote mpaka Pafo, wakaona mtu mmoja, mchawi, nabii wa uongo, Myahudi jina lake BAR-YESU;
7 mtu huyu alikuwa pamoja na liwali SERGIO PAULO, mtu mwenye akili. Yeye liwali akawaita Barnaba na Sauli waje kwake, akataka kulisikia neno la Mungu”
Huyu “Bar-Yesu” ni nabii wa uongo na ni mchawi, lakini ajabu ni kwamba jina lake limebeba jina la YESU ndani yake.. Je unaelewa maana ya Bar-Yesu?.. maana yake ni “Mwana wa YESU” hiyo ndio tafsiri yake..
Kwahiyo huyu mchawi na nabii wa uongo, alikuwa ni mtu anayemjua YESU na anayedai kufundisha habari za YESU, lakini nyuma yake alikuwa ni mwongo.
Na jambo jingine la ajabu ni kwamba huyu Bar-Yesu alikuwa ni mwalimu wa kiroho wa mtu mmoja aliyeitwa “Sergio-Paulo”… Je unaelewa maana ya Sergio-Paulo?…maana yake ni “Mhudumu-Paulo”..
Kwahiyo wakati YESU wa Mnazareti, anammiliki Paulo mtumishi wa Mungu, yupo mtu anaitwa Bar-YESU anayemmiliki Sergio Paulo.
Kwahiyo hapa kuna “Sergio-Paulo” na “Bar-Yesu” na kuna “Paulo” na “YESU”. Kuonyesha kuwa shetani hana jipya zaidi ya kunakili vile vilivyopo vilivyo halali na kuvigeuza kwa matumizi yake.
Maandiko yanasema hivyo…
2Wakorintho 11:14 “Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru. 15 Basi si neno kubwa watumishi wake NAO WAKIJIGEUZA WAWE MFANO WA WATUMISHI WA HAKI, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao”.
2Wakorintho 11:14 “Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.
15 Basi si neno kubwa watumishi wake NAO WAKIJIGEUZA WAWE MFANO WA WATUMISHI WA HAKI, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao”.
Kwahiyo si kila anaitwa mtumishi wa YESU ni mtumishi kweli wa YESU, vile vile si kila anayejiita ni Mkristo, ni Mkristo kweli kweli, ni muhimu kuwa macho sana, na kujua vipimo halisi vya kuwatambua manabii wa uongo, waalimu wa uongo, wachungaji wa uongo, waimbaji wa uongo pamoja na wakristo wa uongo.
Na kipimo hiko si kingine zaidi ya NENO LA MUNGU, baada ya kujaa Roho Mtakatifu, Neno la MUNGU pekee ndio kipimo cha kumjua huyu ni wa MUNGU au wa ibilsi, hii ni sauti ya Mungu au ya ibilisi.
Je umeokoka?.. unao uhakika wa kwenda mbinguni ikitokea parapanda imelia leo?
Kama bado haujampa YESU maisha yako, bado parapanda haijalia leo, lakini muda wowote mambo yanabadilika, hivyo fanya mabadiliko kabla ya mabadiliko makuu kutokea.
JIHADHARI NA ROHO YA YEZEBELI.
Roho ya Malipizi/ roho za malipizi ni nini?
MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.
MKUU WA UZIMA AKUWEKE HURU.
UNAMALIZAJE MWAKA WAKO, JE NA MUNGU AU SHETANI?
Mfundishe mtoto namna ya kutumia jina la Yesu katika kutenda mambo yake yote.
Kuishi ni tufoauti na kuwa na uhai. Hata mti ni hai, lakini hauishi. Kuishi ni maisha, yaani unasifa ya kuwa na mfumo au ustaarabu Fulani ambao unatembea nao, unaweza kuchagua mahali pa kukaa, unafanya kazi, unapumzika, unajenga, unapanda, unajichagulia burudani mfano miziki, michezo, vyakula, unafanya ibada, unauza, unanunua.. mambo kama hayo kiumbe kikitenda tunasema kinaishi.
Lakini kuwa kifungoni, ndani ya gereza huoni jua wala mwezi siku zako zote uwapo duniani, hatuwezi kusema unaishi, tunasema wewe upo hai, lakini hauishi.. Au unapokaa kwenye kitanda cha wagonjwa mauti-uti, umepooza, huwezi kuongea wala kutembea, umekata kauli, kwa sikuzote uwapo duniani, hayo si maisha ijapokuwa upo hai.
Sasa kuna maneno Yesu aliyasema, ambayo si wengi hujaelewa kwa undani na upana.. Tusome;
Yohana 11:25-26
25 Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi; 26 naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo?
Hii kauli ukiisoma vizuri, unaweza ukasema inajichanganya, Embu tafakari, jambo la kwanza Yesu anasema, tukimwamini tukifa tutakuwa tunaishi, lakini pia tukiwa hai na kuamini hatutakufa kabisa hata milele.
Je! Sisi tuliomwamini hatufi?
Jibu ni Ndio hatufi kabisa, bali tunahamishwa makao. Hicho kinachoitwa kifo, ni macho ya wanadamu yanaona hivyo, lakini sisi tunakuwa kama tumefumba macho, kisha tukafumbua na kujikuta katika ulimwengu mwingine kabisa, Ndio maana lugha ambayo hutumika kueleza hali hiyo kwa watakatifu ni kulala (Matendo 7:54-60, 1Kor 15:51-58, Yohana 11:11-19)
Sisi tuliomwamini Yesu hatutaona kitu kinachoitwa kaburi, wala hatutajikuta kwenye gereza Fulani , bali kwenye ulimwengu mwingine mzuri sana uitwao pepo, sio tukiwa hai, bali tukiwa tunaishi kabisa huru.
Maana yake, tunaendeleza maisha, ikiwa kuna kutembea, huku na huko au kushughulika kwa vitu vya kimbingu, kufanya hivi, kufanya vile..Tutakuwa tunayafanya. Hayo ndio maisha anayosema mtu akimwamini yeye, ajapokufa (lala), atakuwa anaishi.. Si atakuwa na uhai
Tutakaa huko pepo, kwa kipindi chote, ambacho tunamsubiria Yesu, kulikamilisha kusudi la watakatifu wote, kisha baadaye,(mwisho ukifika), atakuja mwenyewe kuwachukua walio hai Pamoja na miili yetu tuliyoiacha duniani, na sote kwa Pamoja tutaanza ziara mpya ya kuelekea mbingu ya tatu. Makao yetu ya milele yalipo (2Wakorintho 12:2-4)
Lakini waovu wanapokufa, wenyewe watajiona kwanza wakiingia makaburini, kisha wakishuka kuzimu, Uhai wao ukitunzwa kwenye vifungo vya giza wasijue chochote, wala wasitende kazi yoyote, mpaka siku ya hukumu itakapofika, ambapo watatolewa huko kisha watasimama kwenye kiti cha enzi cheupe cha mwana-kondoo kwa ajili ya hukumu, (Ufunuo 20) baada ya kuhukumiwa ndipo watakapotupwa kwenye ziwa la moto, na kuangamia milele.
Sasa wakiwa huko kuzimu, ambapo kwa jina lingine kunaitwa Jehanamu, ni mahali pa shida, dhiki nyingi na mateso yasiyoelezeka, huko hakuna maisha, ni mateso tu vifungoni.
Hivyo ndugu, unapomwamini Yesu ipo faida kubwa zaidi ya unavyofikiri, unapokea MAISHA YA MILELE, Tangu ukiwa hapa duniani, ndani yako hakuna kitu kinachoitwa kifo, wala hutakihisi hata kidogo. Kwanini leo usimkaribishe maishani mwako? Ikiwa upo tayari basi wasiliana nasi kwa namba hizi kwa ajili ya mwongozo wa sala ya Toba, bure.
Au sema sala hii kwa Imani, na Moja kwa moja Yesu ataingia moyoni mwako.
AINA ZA FARAJA BWANA AZIACHILIAZO KWA WATUMISHI WAKE.
TAFUTA UTAKASO WA SEHEMU KUU NNE ZA MWILI WAKO.
ASIYEMPENDA BWANA NA AWE AMELAANIWA.