Category Archive Home

Kuadibu ni nini kibiblia? (Zaburi 94:12)

Kitendo cha kumtia mtu adabu ndio kuadibu. Maana yake kuchukua hatua za makusudi kuadhibu, au kukaripia, au kuonyoosha mwenendo lakini kwa lengo la kujenga sio kulipiza kisasi.

Neno hilo utalipata kwenye vifungu hivi.

Zaburi 94:12

[12]Ee BWANA, heri mtu yule umwadibuye, Na kumfundisha kwa sheria yako; 

Zaburi 94:10

[10]Awaadibuye mataifa asikemee? Amfundishaye mwanadamu asijue? 

Mungu akiitwa Baba, basi tujue kuwa sisi ni watoto wake, na kama ni watoto wake basi atatuadabisha pale tunapokosea..

Kubali kuadibiwa na Bwana…

Shalom.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Beliari ni nini? (2Wakorintho 6:15)

‘laana ya torati’ maana yake ni nini?

Mapokeo ni nini?

Print this post

MUNGU AUMBAYE TENA.

Biblia inatuonyesha Mungu ndiye muumba wa vitu vyote 

Mwanzo 1:1 Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.

Lakini hatujui ni nini kilitokea baadaye kikaifanya dunia kuwa ukiwa, mpaka akaanza kuirekebisha tena dunia aliyoiumba mwanzo.. 

Kwasababu mstari wa 2..unasema nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji, 

Mungu akaanza tena kuifanya ikaliwe na watu, akaleta tena nuru kutoka kwenye giza, akayatenga maji, na kuyaweka sehemu stahiki,  akalitokeza anga..akamuumba mwanadamu.

Dunia ikawa nzuri tena, lakini baadaye mwanadamu akaasi, akaiharibu duniani, mpaka ikaangamia kwa maji. 

Bado Mungu hakuikatia tamaa dunia yake, akawaongeza, Nuhu na wazao wake, baadaye akamchagua Ibrahimu ili kumwandaa mkombozi atakayeikomboa dunia kikamilifu, akaja Kristo ulimwenguni ndio mwokozi wetu.

Watu wakaokolewa, ijapokuwa waliendelea kuiharibu dunia, bado Mungu akawa kwenye mwendelezo wa uumbaji wake unaoharibiwa .

Na kama tunavyojua Kristo aliahidi kurudi tena duniani mara ya pili, kuwanyakua watu wake, kisha kuukarabati huu ulimwenguni na kuufanya kuwa mbingu mpya na nchi mpya.(Ufunuo 21)

Hivyo kama ukichunguza asili ya tabia ya Mungu, si kufanya kitu mara moja, kisha pale kinapoharibika anakikatia tamaa ..

Hapana utaona hukiumba tena na tena na tena…kwa miaka na miaka na miaka..tena huanzia mbali sana mpango wake wa ukarabati..

Na sisi ni lazima tujue tumeumbwa kwa mfano wake na sura yake..ikiwa unaona hakuna mwenye hekima duniani  kumzidi Mungu, na kila lifanyalo ni bora, na kamilifu basi jifunze kuiga tabia zake ufanikiwe…

Mungu wetu alikuwa na siku moja katika juma ya kupumzika, wewe si ‘busy’ zaidi ya Mungu mpaka siku zote saba katika juma, mwaka mzima unafanya kazi mpaka unakosa muda wa kumwabudu Mungu wako.

Vivyo hivyo ni lazima kutambua kuwa kazi zake zimepitia changamoto nyingi sana za kuharibiwa zaidi ya zako lakini amekuwa katika uumbaji wake kila siku..Na wewe pia kuharibiwa kwa maono yako, si sababu ya kukata tamaa na kusema sitaendelea mbele…inuka anza tena na tena..

Unamtumikia Mungu, ile huduma iliyokaa ndani yako, ni kama imekufa, mwanzoni uliona hatua lakini sasa huoni, pengine ni kutokana na kuwa umedhulumiwa, umeibiwa, umefukuzwa..inuka tena na tena, anza upya..

Kuacha kazi uliyokwisha itaabikia na kuitolea jasho jingi, ni ishara ya kuwa bado tabia ya Mungu haijaumbika ndani yako.

Kumbuka mpaka leo hii Mungu anaendelea kufanya uumbaji wake, ijapokuwa kazi hizo zingepeswa zikamilike tangu kule mwanzo…Wewe ni nani usifanye matengenezo yako yaliyokufa kila siku?

Anza sasa. Fanya kazi na Mungu.

Shalom.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MBONA MMESIMAMA HAPA MCHANA KUTWA BILA KAZI?

USIMPE MWANAO VITU SASA.

Print this post

UPANGA USHIKAMANAO NA MKONO

2 Samweli 23:9-10

[9]Na baada yake kulikuwa na Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu waliokuwa pamoja na Daudi; walipowatukana Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko ili kupigana, na watu wa Israeli walikuwa wamekwenda zao; 

[10]huyo aliinuka, akawapiga Wafilisti hata mkono wake ukachoka, na mkono wake ukaambatana na upanga; naye BWANA akafanya wokovu mkuu siku ile; nao watu wakarudi nyuma yake ili kuteka nyara tu. 

Kibaolojia mwili wa mwanadamu unapokamata kitu, kwa muda mrefu sana, kwa nguvu, huwa unatabia ya kukakamaa katika hali hiyo hiyo hata kama mtu huyo hatakuwa na nia ya kuendelea kukishikilia kitu hicho.

Ndicho kilichomkuta huyu shujaa wa Daudi, alipokutana na jeshi la wafilisti angali yupo peke yake. Aligundua kitu pekee ambacho kingeweza kumtetea ni upanga wake. Hivyo aliukamata kwa nguvu sana bila kuuachia, akaanza kupambana na wafilisti wale kwa muda mrefu,  hakujua kuwa mkono wake utabakia katika hali ile ile…yeye aliendelea tu kupigana vita, mpaka  baadaye aliposhangaa  kuona hana jitihada yoyote tena ya kuushika upanga, ni kama vile ulikuwa ni sehemu ya kiungo chake…kazi yake ilikuwa ni kurusha tu mkono kuupeleka anapotaka, huku upanga ukiwa tu pale pale kiganjani hautoki…

Kikawaida hali ikishafikia hatua hiyo huwa inamgharimu mtu masaa mengi hata siku,  ili kung’atuka kutoka kwenye kitu kilichoshikamana naye..wakati mwingine ili kuharakisha uponyaji, wengine hutumia maji ya uvuguvugu na kuchua kiganja kwa muda baadaye kunyosha kidole kimoja baada ya kingine…

Sasa askari wa mwilini ni kivuli cha mtu wa rohoni. Yeye naye ana mikono na analazimika wakati wote kuwa na upanga…Lakini si upanga tu, wa kushika, bali ule Ugandao na mkono. 

Waefeso 6:11-14,17

[11]Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. 

[12]Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. 

[13]Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama. 

[14]Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,..

[17]Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu; 

Kama maandiko yanavyotuonyesha hapo Mtu wa rohoni, hulazimika kubeba upanga wake, ambao ni Neno la Mungu.

Tunapoonyesha nia ya kuling’ang’ania Neno la Mungu, mwanzoni ni kama tutatumia jitihada zetu, lakini haitakuwa hivyo mbeleni …baadaye litashikamana na sisi..maana yake haitakuwa jitihada tena kuliishi.

Jambo lolote la kiroho, mfano maombi ya masafa marefu, mwanzoni ukianza utaona kama ni jitihada zinatumika lakini ukiendelea mara mbili, mara tatu utaona ni kawaida..

Mambo yote ya rohoni iwe ni upendo, unyenyekevu, utaanza kwa jitihada fulani lakini Kwasababu umekusudia tu kung’ang’nia kwa nguvu, utagandamana navyo.

Kumbuka hakuna wepesi wowote utakuja bila mtu kutia nia kwanza. Anza sasa kutendea kazi Neno la Mungu.

Bwana akubariki.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:


 

Print this post

MAISHA YA IMANI NI KAMA SIFA YA MTI.

Mti una sifa moja, hautembei kutoka sehemu moja Kwenda nyingine, Utaupanda eneo fulani, utaridhika kubakia hapo hapo, haijalishi ni pabaya kiasi gani, utaenda utarudi miaka na miaka utaukuta pale pale, tofauti na viumbe hai vingine, ambavyo vyenyewe, vikiona hali si nzuri ya mahali, huama na Kwenda kutafuta makazi pengine. Lakini Mti hauna sifa hiyo, na bado utaendelea kustawi na kuwepo kwa miaka mingi zaidi ya viumbe hai vingine,  haijalishi ni kipindi gani kitapita.

Siri ya mti ipo wapi?

Jibu ni kwenye mizizi yake. Ijapokuwa hautembei kwa juu, lakini chini unatembea. Kwa juu utauna upo pale pale, lakini kwa chini mizizi yake ina mwendo, kila siku inaendelea katika safari ya huku na huko kutafutia virutubisho na maji.

Ni nini Bwana anatufundisha katika maisha ya mti.

Yeye hutupanda apendako.

Leo hii ni rahisi kulalamika, kwanini nimezaliwa hili taifa, kwanini hili kabila, kwanini hii familia, kwanini hii jinsia, kama ningezaliwa kwenye nchi ile, kabila lile, familia ile yenye Uchumi mkubwa ningekuwa mbali sana, ningestawi vizuri sana, ningeimarika kiroho kwa kasi kubwa mno… Kama umekuwa na Mawazo hayo, basi kuna tatizo la kiufahamu.

Mafanikio ya mwanadamu hayapo katika mazingira yake sasa. Mafanikio yake yapo katika mizizi yake rohoni. Mti ukikosa mizizi, hata uwe kwenye udongo mzuri kiasi gani hauwezi kukua popote.

Kama mwamini fahamu mzizi uliyopewa inauwezo wa kukustawisha popote, isipokuwa sifa yake ni ile ile yaani huwa haionekani kwa juu, hukaa matopeni, na huzidi Kwenda chini kila siku sio kurudi juu. Vivyo hivyo na sisi tujue nguvu yetu ipo rohoni, (pasipoonekana), Na katika unyenyekevu kwa Mungu wetu kila siku, ndivyo tutakavyoleta ustawi mema wa maisha yetu.

Kunyenyekea kiroho ni mjumuiko wa mambo : kumkubali Kristo, kutii maagizo yake (ikiwemo maombi, ushirika), kuliishi Neno, na kumtumikia yeye.

Huko ndiko kurefusha mizizi.

2 Wafalme 19:30

[30]Na mabaki yaliyookoka ya nyumba ya Yuda yatatia mizizi chini, na kuzaa matunda juu. 

Kristo alipaswa aishi Yerusalemu, mji  wenye sifa za kiroho na kisomi, lakini alipelekwa Nazareti , mji mnyonge, lakini huko huko alimzalia Mungu matunda, kwasababu mizizi yake ilienea sana.

Yusufu aliuuzwa utumwani, akawa msikwao, asiye na makazi kule Misri, lakini aliendea kuiimarisha mizizi yake, ijapokuwa kwa nje, hakukuonekana dalili ya badiliko lolote, lakini hatimaye, Mungu akamwinua akawa, mkuu kule kule Misri, Ndivyo ilivyokuwa kwa Danieli, Ayubu na watumishi wa Mungu.

Kabla ya kulalamikia mazingira, jiuliza kwanza je! Mizizi yangu, ipo sawa? Kwasababu haiwezekani mizizi ikawa sawa, mti ukafa. Haiwezekani ukawa mtakatifu halafu ukamezwa na mazingira.

Imarisha kiroho chako.

Shalom.

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Print this post

MIINGILIANO MINGINE, IPOKEE KAMA MWITO WA KI-MUNGU.

Ni kawaida Mtu mwenye malengo yake au mpangilio wa ratiba zake, mfano  kukatokea mvurugano fulani mambo mengine yakaingilia ratiba zake huwa anakereka sana, na kujiona ameshindwa,  kusimamia maono yake.

Lakini kama mwana wa Mungu, si kila wakati mwingiliano wa vitu, ni kutoka kwa adui. Wakati mwingine ni kwa Mungu, hivyo kuliko kulaumu, kuvunjika moyo au kuchukia embu tulia kisha litazame kama mwito wa ki-Mungu, kutimiza kusudi fulani.

Kwamfano kuna wakati Petro alialikwa kwenye nyumba ya Kornelio, katikati ya somo lake, pengine hata watu hawajaelewa vizuri, Roho Mtakatifu akawashukia watu waliokuwa pale wakaanza kunena kwa lugha kabla hata ya kubatizwa, au kuhubiriwa toba, na kuwekewa mikono.

Kama mhubiri angeweza  kusema, “Naomba kuwe na utulivu” tusikilize Neno, …lakini Petro alibakia tu kushangaa jambo lile, liliwezekanikaje kwa haraka vile kwa mataifa wasiomjua Mungu kujazwa Roho.,Akaendelea kumwacha Mungu afanye kazi zake.

Bwana Yesu hakuwa mtu wa kulaumu au kukatiza kila mvurugano uliokuja mbele yake, bali alijifunza kutulia na kumsikia Mungu, wenda yupo nyuma ya mwingiliano huo.

Kwa mfano Wakati fulani alikuwa anaelekea Tiro na Sidoni kuwatafuta kondoo  waliopotea wa Israelitu, lakini mwanamke mmoja ambaye si mwisraeli aliingilia ziara yake, na kutaka kuhudumiwa…Mwanzoni Yesu hakumsemesha kitu, watu wakasema..achana naye anatupigia kilele, lakini Yeye akatulia kwa muda na kuanza kuhojiana naye..mwishowe akamtendea muujiza ambao mpaka leo tunausoma kama fundisho la imani. Kama angesema achana na mimi, ni marufuku kukusikiliza akaendelea na safari yake…kusudi la Mungu la siku hiyo lisingetimia.

Mathayo 15:22-28

[22]Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo. 

[23]Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu. 

[24]Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. 

[25]Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie. 

[26]Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa. 

[27]Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao. 

[28]Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile. 

Miujiza mingi ya Yesu ilifanyika nje ya ratiba alipokuwa njiani kuelekea katika ziara zake, mafundisho mengine aliyafundisha kulingana na matukio aliyopishana nayo, si yale aliyokusudia kuwaambia watu.

Hii ni kuonyesha kuwa na sisi, sehemu kubwa ya mwito wa Mungu unaweza kuwa katika mambo yanayotuingilia kila siku..

Unaweza kupangilia fedha yako, kwa wiki nzima au mwaka mzima ufanyie hivi au vile…lakini ikatokea tu mtoto wa mjomba ni mgonjwa inahitaji fedha ya matibabu, na ukalazimika kuitoa karibu yote, sasa ni rahisi kulalamika mbona nikiweka malengo sifikii…mbona nikipata tu kinatoka…mbona nikipata kitu kinang’ang’aniwa  na wengine, mimi sivitumii.

Kabla hujahuzunika Jifunze kuusikia mwito wa Mungu nyuma ya mivurugano hiyo, kwasababu sehemu kubwa ya maisha yetu ni mivurugano, Na huko huko Mungu hutimiza makusudi yake.

Bwana akubariki.

 

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

JINSI MWANADAMU ANAVYOUHARIBU USO WAKE.

Zawadi kubwa na ya kipee alipewa  mwanadamu na Mungu, iliyomtofautisha na viumbe vingine vyote, (vya mbinguni na duniani) basi ni Uso wa Mungu.

Ni mwanadamu pekee ndiye aliyeumbwa kwa mfano na sura ya Mungu (Mwanzo 1:27-28).

Biblia inaposema sura, inafananisha na mfano wa kioo,  pale mtu anapojitazama kwenye kioo, anaiona taswira yake vilevile kama yeye alivyo, ikiwa ni mwenye chunusi, basi ataiona chunusi yake kwenye kile kioo, ikiwa ni mweupe vivyo hivyo ndivyo atakavyojiona.

Kwahiyo sisi ni taswira ya Mungu kabisa, lakini ifahamike kuwa taswira hiyo sio hii ya nje, yaani pua, mdogo, masikio, hapana bali ile ya ndani, yaani tabia na sifa alizonazo Mungu, sisi pia tunazo.

Sasa kazi kubwa ya shetani, aliyokuwa nayo kwa Mwanadamu ni kumbadilisha SURA yake. Ili ifanane na kitu kingine tofauti na Mungu.

Na alijua njia pekee na kubwa ambayo hubadili taswira ya mtu, ni IBADA.

Yaani kile ambacho mwanadamu anakiabudu basi moja kwa moja hufanana nacho, wala si kile anachokitazama, au anachokishika, au anachokiangalia Hapana bali kile akifanyiacho ibada, moja kwa moja kinambadilisha taswira yake.

Ndio maana amri ya kwanza na ya pili ambayo Mungu aliwapa watu wake (Kutoka 20), ni kuhakikisha hawajifanyii sanamu ya kuchonga ya aina yoyote na kuiabudu, wala hawawi na miungu mingine, ila yeye.

Kwanini? Kwasababu wamwabudupo yeye, hudumisha tabia zake, na mwonekano wake ndani yao.Lakini wanadamu walipoanza kuabudu miungu, mfano wa Baali, Arishtoreth, n.k. hawakujua kwamba moja kwa moja wanafanana nazo.

Zaburi 115: 4-8

4 Sanamu zao ni fedha na dhahabu, Kazi ya mikono ya wanadamu.
5 Zina vinywa lakini hazisemi, Zina macho lakini hazioni,
6 Zina masikio lakini hazisikii, Zina pua lakini hazisikii harufu,
7 Mikono lakini hazishiki, miguu lakini haziendi, Wala hazitoi sauti kwa koo zake.
8 WAZIFANYAO WATAFANANA NAZO, Kila mmoja anayezitumainia

Maandiko yanasema hapo, wazifanyao, hufanana nazo, maana yake Walikuwa vipofu rohoni, viziwi rohoni, wamepooza, kabisa, hawana uhai, ndio maana hata walipokuwa wakihubiriwa Habari za hukumu na manabii hawakuelewa wala kuona ni kitu, hata Kristo alipokuja duniani bado hawakutambua wakati wa kujiliwa kwao, sio kwamba walikuwa wanafanya makusudi, lakini ni kwasababu waliabudu miungu isiyo hai, waliabudu mashetani yasiyojua kesho yao itakuwaje, mizimu isiyojua amani ya kweli ina Ladha gani, mapepo yasiyoweza kuganga mioyo ya watu, mwishowe wakafanana nao, wakawa wakatili, wauaji, wenye wivu .

Lakini tunaposoma biblia tunadhani sanamu ziliabudiwa zamani tu, Hapana, hata sasa sanamu zipo, ambapo zinawakilishwa na vitu vyote vinavyochukua nafasi ya Mungu katika mioyo ya wanadamu.

Fedha, ni sanamu, ukiiabudu ujue utafanana nayo, simu/TV yaweza kuwa sanamu, inapochukua muda wako mwingi, kutazama maudhui zake, na kuacha kabisa kumtafuta Mungu, umeshakuwa mfu hata kama unatembea,  mtu anaweza kuwa sanamu, unapomtegemea yeye zaidi ya Mungu, hapo hesabu umelaaniwa.

Lakini unapomwabudu Mungu, yaani unapomtegemea, unapomtii, unapomtumikia, unapomsujudia, ufahamu kuwa ndivyo unavyofanana na yeye, na hatimaye utakuwa hai kama yeye alivyo hai, sikuzote. Mungu anaishi milele, na wewe vivyo hivyo, Mungu ni mweza, na wewe utakuwa vivyo hivyo, Mungu ni mwenye upendo na wewe utakuwa kama yeye. Mungu ni mtakatifu, ni wa rehema, ndivyo na wewe utakuwa kama yeye. Ibada yako kwa Mungu isiibiwe na kitu chochote.

Bwana akubariki.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUSUDI LA MUNGU NYUMA YA SAFARI.

AINA ZA FARAJA BWANA AZIACHILIAZO KWA WATUMISHI WAKE.

MTU WA NNE, ANADHIHIRISHWA KWA MOTO

Print this post

WATAKATIFU BABELI.

Moja ya ombi kubwa la watu wa Mungu, pale wanapojikuta wameokoka, ni kubadilishwa mazingira waliyopo, wapelekwe kwenye mazingira mengine yenye uwepo wa karibu zaidi na Mungu, Kwasababu wakiangalia kwa sehemu kubwa mambo ambayo yanawakosesha huchangiwa na mazingira yao. Mazingira husika yanaweza kuwa mitaa wanayoishi, shule wanazosoma, maeneo ya kazi/ biashara walipo, watu wanaowazunguka, hata nchi yanayotokea.

Hii ni hali ya kawaida, na hufikia hatua wengi kuwaza mioyoni mwao, “Kama ningekuwa eneo Fulani, basi ningekuwa na mahusiano ya karibu na Mungu, ningekuwa mwombaji sana, ”

Lakini Je! Kuwaza hivyo ni sahihi?

Ndio kuwaza kubadilishwa mazingira yanayokosesha, ni vema, lakini kuwaza kuwa Hapo ulipo huwezi kumpendeza Mungu kwa viwango vyote ni uongo,. Kwasababu maandiko yanatuonyesha Mungu amewaweka watumishi wake katika mazingira yote, yaani mazingira rafiki na yale yasiyo rafiki, kwa mapenzi yake, na kuthibitisha kuwa kote kote, kumpendeza Mungu kunawezekana. Kwasababu dunia moja.

Bwana aliwaweka watakatifu Babeli, alikuwepo Shedraka, Meshaki, Abednego na Danieli.

Hawa waliishi katika taifa la kipagani usiokuwa wa kawaida,ni taifa lenye shinikizo kubwa la mtu kuabudu miungu hata kama hapendi, lenye mikorogo ya kila namna ya maovu. Lakini watu hawa walisimama vema na Bwana.

Waliwezaje?

Yafuatayo ni mambo ambayo yaliyatenda mpaka ufanikiwa kuishi katika viwango vyote vya ukamilifu.

1) Waliitangaza Imani yao mapema.

Mwanzoni kabisa akina Danieli walipochukuliwa Babeli, na kusomeshwa elimu ya wakaldayo,tunaona walipewa vyakula ambavyo ni najisi, lakini Danieli alisimama mapema na kumwomba msimamizi, kulishwa vyakula vingine visivyo najisi. Na Mungu akawa Pamoja nao. Wakatambulika tangu mapema kuwa wao ni watumishi wa wayahudi wasiojichangamana na desturi za kimataifa.

Hawakungoja, miaka ipite baadaye..bali mezani tu, wanaanza kutangaza misimamo yao.

Danieli 1:8-9

[8]Lakini Danieli aliazimu moyoni mwake ya kuwa hatajitia unajisi kwa chakula cha mfalme, wala kwa divai aliyokunywa; basi akamwomba yule mkuu wa matowashi ampe ruhusa asijitie unajisi. 

[9]Basi Mungu alimjalia Danieli kupata kibali na huruma machoni pa huyo mkuu wa matowashi. 

Hii ni desturi ambayo na sisi, kama watoto wa Mungu babeli, tuwapo katikati ya wasioamini, tujitambulishe mapema. Hiyo itasaidia sana wao kutokukuhusisha katika matendo yao ya giza wakijua kuwa wewe ni mwamini.

Wengi wameshindwa kung’atuka katika mazingira mabovu kwasababu ya kushindwa kujitambulisha wao ni akina nani, kwa wanaowazunguka.

2) Walikuwa waombaji

Danieli akiwa Babeli, alijijengea desturi na kutwa mara tatu, kupiga magoti na kuomba, akijua kuwa nguvu ya kusimama na kuendelea mbele ilitegemea sana maombi…

Ijapokuwa alikuwa na majukumu makubwa kama waziri katika taifa lakini hakuruhusu muda wake mahususi wa maombi kuibwa.

Danieli 6:10

[10]Hata Danieli, alipojua ya kuwa yale maandiko yamekwisha kutiwa sahihi, akaingia nyumbani mwake, (na madirisha katika chumba chake yalikuwa yamefunguliwa kukabili Yerusalemu;) akapiga magoti mara tatu kila siku, akasali, akashukuru mbele za Mungu wake, kama alivyokuwa akifanya tokea hapo. 

Vivyo hivyo na sisi tuwapo popote pasipofaa, hatuwezi sema hatuna muda wa sala. Ikiwa umebanwa upo muda wa chakula cha mchana kazini unaweza tumika nafasi kusogea mahali tulivu na kuomba.

3) Walikubali kujitwika misalaba yao.

Kujitwika msalaba maana yake ni kukubali kuipokea imani kwa gharama yoyote ile, yaani kama ikitokea nitatengwa kwasababu ya imani yangu, nitafungwa, nitauawa..Je nipo tayari?

Ndivyo ilivyokuwa kwa Meshaki, shedraka, Abednego, Danieli, Yusufu.

Wote hawa walikubali kutupwa kwenye matanuru ya moto, kwenye magereza, matanuru ya simba, walipojaribiwa.

Vivyo hivyo na sisi, lazima tufahamu mapema kuwa, imani haipendwi, ulimwengu sio rafiki kwetu, kama ikitokea tunalazimishwa kuikana imani je! Tutachukua hatua gani?

Wengine wameshindwa na majaribu mbalimbali ya Babeli, wameanguka katika uzinzi,wizi, upagani kwa sababu tu ya kuhofia kupoteza kazi zao, familia zao, heshima zao, mali zao, uhai wao.

Ili uweza kuishi vema Babeli, ufahamu huu wa kujitwika msalaba ni lazima uwe nao tangu mwanzo kabisa wa kuamini kwako. Kumbuka sikuzote nguvu ya kuushinda ulimwengu upo katika msalaba.

4) Waliwajibika kwa bidii na uaminifu.

Utaona hawakuwa wavivu, au walegevu, au watu wasiokuwa na shughuli zao maalumu, bali waliwajibika..Danieli pamoja na wenzake walisoma ili kupata elimu na kuwajibika katika shughuli za kifalme mpaka wakaonekana hakuna wa kufanana na wao kwa hekima na ujuzi, 

Yusufu naye alisimama kwenye majukumu yake, wala hakuna mahali alionekana mlegevu. Na wote hawa walitanguliza uaminifu.

Walijua kabisa kutowajibika ni mlango mwingine wa shetani, kuinua majaribu.

Waefeso 4:27-28

[27]wala msimpe Ibilisi nafasi. 

[28]Mwibaji asiibe tena; bali afadhali afanye juhudi, akitenda kazi iliyo nzuri kwa mikono yake mwenyewe, apate kuwa na kitu cha kumgawia mhitaji. 

Hivyo na sisi pia tuwapo kwenye Babeli zetu, tuwe makini kuwajibika kwa bidii na uaminifu, tuepuke uvivu, kama watoto wa Mungu ni wajibu kujishughulisha.

Tukifanikiwa kuwa na uwiano huo mzuri, Neema ya Mungu itatusaidia.

Bwana akubariki.

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MNARA WA BABELI

Ipi tofauti ya Falme, Mamlaka na Wakuu wa giza (Waefeso 6:12)

KWA KUWA FURAHA YA BWANA NI NGUVU ZENU. 

Print this post

MWENENDO WA KORA NA WATOTO WAKE.

Chanzo kibaya, Haimaanishi mwisho mbovu, chanzo chaweza kuwa bora lakini mwisho ukawa mbovu, Vilevile chanzo chaweza kuwa kibovu, mwisho ukawa mzuri.

Moja kati ya watu waliofanya uasi mkubwa mpaka Mungu akawaangamiza kwa kuwashusha kuzimu moja kwa moja wakiwa wazima, basi alikuwa ni Kora na jamii ya watu wake.

Ni mtu ambaye anatajwa hata baadaye katika agano jipya (Yuda:1:11), kama kielelezo akifananishwa na watu waasi waliopotoka wa siku za mwisho, kwasababu ya maasi yake kuwa makubwa yenye kuambukiza.

Hesabu 16:31-33

[31]Basi ilikuwa, hapo alipokwisha kusema maneno haya yote, nchi iliyokuwa chini yao ikapasuka; 

[32]nchi ikafunua kinywa chake, na kuwameza, na watu wa nyumba zao na wote walioshikamana na Kora, na vyombo vyao vyote. 

[33]Basi wao, na wote waliokuwa nao, wakashukia shimoni wali hai; nayo nchi ikawafunika wakaangamia kutoka mle mkutanoni. 

Lakini ijapokuwa wazazi walifanya vibaya…watoto hawakufuata njia za baba yao (Hesabu 26:11)

Kinyume chake baadaye tunaona wazao wa kora wakaambata na Bwana kwa  bidii mpaka wakawa sehemu takatifu ya Mungu, yaani waimbaji wa hekaluni.

Nafasi iliyo takatifu sana.

1 Nyakati 6:31–38, 

Wengine wakawa wafungua malango ya nyumba ya Mungu (1 Nyakati 9:19)

Na Kama hilo halitoshi Sehemu nyingi za  Zaburi zilitungwa na wana wa Kora. Mfano wa hizo ni

(Zaburi 42, 44, 45, 46, 47, 48, 49, 84, 85, 87, 88).

 Huu ni mchango mkubwa sana kwenye ufalme wa Mungu. Ambao mpaka sasa tunakula matunda yake.

Lakini si rahisi kukubali kama hao ni wana wa mtu mwasi Kora. Ni sawa na leo usikie wana wa Yezebeli ni manabii wa Bwana.., wana wa Elima-mchawi ni mitume wa Kristo.

Tufahamu kuwa rehema za Mungu, haziathiriwi na asili, au mwanzo mbovu. Maadamu moyo umegeuka kweli kweli, Bwana huanza historia mpya.

Hapo mwanzo uliitwa Kora lakini leo ukigeuka utaitwa Musa, uliitwa Sauli leo utaitwa Paulo.

Sahau yaliyopita, anza ukurasa mpya na Bwana. Wazazi wako walikosea, hata na wewe mwenyewe ukakosea, ukapata sifa mbaya, ukawa kama mfu, . LEO HII, kubali toba ya kweli, uwe kiumbe kipya, ukubaliwe na Bwana, upendwe na Bwana, utumiwe na Bwana, hata kama una asili ya sifa mbaya.

Je upo tayari leo kukata shauri kwa kutubu na kumpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yako?

Kama ndio basi hapo ulipo piga magoti kisha sema sala hii kwa imani kutoka moyoni ukimaanisha kabisa kutaka ukombozi wa nafsi yako leo. SEMA;

Bwana Yesu, asante kwa upendo wako mkuu, kwa kuja duniani kunikomboka maisha yangu, katika dhambi na hukumu. Leo hii nimeamini kwa moyo wangu wote, na kupokea msamaha wa dhambi upatikanao kwa dhabihu ya damu yako takatifu. Kuanzia leo mimi ni mwana wa Mungu, nimemkataa shetani na kazi zake zote. Karibu Roho Mtakatifu ndani yangu. Ufanye makao yako sasa, nitembee kwa nguvu zako, na kukutumikia. Nimeomba nikiamini katika jina la Yesu Kristo.

Amen

Mpaka hapo utakuwa umepokea msamaha wa dhambi, hivyo hatua zinazofuata na malezi ya kiroho ili umjue Mungu, ukue kiroho, Na ubatizo ikiwa bado hujabatizwa.

Kwa mawasiliano. 

Piga namba hizi : +255789001312 / +255693036618

Lakini tembelea tovuti yetu yenye mafundisho mengi zaidi ya elfu tano (5000), upate kujifunza kufuatana na mada mbalimbali za kiroho.

Mungu akubariki.

ashirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Print this post

Biblia ina maana gani inaposema katika kuota kwao huutia mwili unajisi?

Yuda 1:7-8

[7]Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele. 

[8]Kadhalika na hawa, katika kuota kwao, huutia mwili uchafu, hukataa kutawaliwa, na kuyatukana matukufu. 

Maandiko hayo, yanazunguzia tabia ya watu waasi ambao wameshaijua kweli lakini wamependa kuendelea katika dhambi zao.

Hivyo katika andiko hilo anasema katika kuota kwao huutia mwili uchafu…sasa huko kuota kunakozungumziwa hapo sio ile hali ya kulala na kuota ndoto…hapana bali ni maono yao, yaani ndoto zao za jinsi watakavyokuwa baadaye, namna wanavyojiona baadaye..sasa hiyo namna ndio sio nzuri bali ni ya kujitia mwili uchafu.

Kuutia mwili uchafu ni nini?

Kuutia mwili uchafu ni ile hali ya kuruhusu matendo yote ya mwilini kukutawala…matendo hayo yanazunguziwa vema katika Wagalatia 5:19-21

[19]Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, 

[20]ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, 

[21]husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu. 

Haya ndio watu wanayoyaona mbele yao, wanayoyawaza na kuyatazamia wakati wote, wanayoyaota yaje kutokea..

Fikra za watu wengi leo ni ili baadaye waishi kiasherati, wafanye anasa kwa pombe, ulafi, waibe..

Hii ni kutufunulia pia kunajisika sio mpaka mtu akatende jambo lenyewe bali ile kulitamania, tu au kulitarajia mbeleni…tayari ameshajinajisi.

Jiulize kuota kwako ni kupi? Kama mtoto wa Mungu, lazima tujue sisi yatupasa kuota maendeleo ya kazi ya Mungu, kuota ukuaji wa kiroho, kuota upendo, kuota kuingia mbingu mpya na nchi mpya,..namna hiyo humfanya mtu kuendelea katika utakaso.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Yuda alimaanisha nini kusema “wokovu ambao ni wetu sisi sote”

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 13 (Kitabu cha Hosea).

Print this post

SHIKA JEMBE NA SURURU CHIMBA MAHANDAKI. 

2 Wafalme 3:16-17

[16]Akasema, BWANA asema hivi, Fanyeni bonde hili lijae mahandaki. 

[17]Kwa kuwa BWANA asema hivi, Hamutauona upepo, wala hamtaiona mvua, ila bonde hilo litajaa maji; nanyi mtakunywa, ninyi, na ng’ombe zenu, na wanyama wenu. 

Ilifika wakati wana wa Israeli, walikwama, baada ya kuona wapo katika eneo ambalo ni kame kupita kiasi, na hawana msaada, nguvu zimewaishia maadui zao wapo karibu kuwaangamiza..

Wakalia sana, Lakini baadaye wakapata akili ya kumlingana Mungu kwa kuulizia kupitia nabii wake Elisha. Lakini maagizo waliyopewa hayakuwa bado marahisi sana, kama walivyotegemea.

Hawakufanyiwa muujiza wa maji kutokea mwambani kama kipindi cha Musa, au mvua kushuka mbinguni…bali waliambiwa wachimbe mahandaki…yaani mashimo makubwa sana…pale jangwani..

Fikiri umechoka umeishiwa nguvu, halafu unaambiwa uchimbe mashimo..upige sururu chini, upige jembe chini, utoe jasho la kutosha si jambo jepesi..

Lakini baadaye tunaona Mungu anawaambia hamtaona mvua bali hayo mabonde yote yatajaa maji. Na ndivyo ilivyokuwa. Kwa waliochimba sana walipata maji sana, kwa waliochimba kidogo walipokea maji sawasawa na mashimo yao.

Je nini Bwana alikuwa analifundisha kanisa lake.

Katikati ya jangwa, Si muda wa kulia na kusumbuka, kinyume chake shika jembe lako, chepe lako anza kuchimba mashimo.

Kwanini watu wengi hawaioni mvua ya Mungu ya neema au baraka za rohoni zikidumu kwao lakini kwa wengine hudumu…sio kwamba Mungu anaupendeleo…hapana…bali wale wengine tayari wameshachimba mashimo marefu ya kuhifadhi maji mengi…Kwasababu mvua au umande wa Mungu sikuzote hushuka au hupanda juu ya nchi yote lakini wale wenye visima ndio hudumu na maji yake mda mrefu kwa wengine hudumu tu kwa muda mfupi pale juu, baadaye kidogo hupotelea ardhini…

Kuchimba handaki ni kudumu sana katika maombi, pamoja na kutendea kazi kile ulichokitaka kwa Mungu…

Kwa mfano unamwomba Mungu akupe mke/mume mwema, labda leo huoni kutokea kwa yoyote upo jangwani tu, unakaribia kukata tamaa…hakikisha unazidisha sana maombi, lakini pia unajitunza na kuanza kujifunza mafunzo ya kuwa mke/mume mwema, unaonyesha kivitendo zile sifa za mke mwema/mume mwema anazopaswa awe nazo kibiblia, kwamfano wewe ni mwanamume unafahamu kuwa yapo majukumu ya kibaba mbele yako, kwamba unapaswa uwajibike kwa kipato cha familia yako, lakini hilo kama hulisumbukii na bado unatarajia Bwana akuletee mke..ni kweli atakuletea, atapandisha umande wa maji juu ya nchi lakini hatimaye atashindwa kudumu na wewe katika hatua za awali akiona huwezi kusimama kwenye wajibu wako…baadaye utalalamika mbona wanawake wananikimbia..vilevile mwanamke akikosa tabia njema..wanaume watakuja na kumkimbia baadaye…kwasababu hakuwa na muda wa kujichimbia mahandaki yake, kitabia.

Kila eneo liwe la kihuduma, kikazi, kiafya..wekeza sana kwenye mahandaki kwasababu mvua/ umande utakuja tu…kwasababu kwa Mungu kushusha baraka si jambo la kulisumbukia sana, yeye anawanyeshea mvua waovu na wema alisema hivyo (Mathayo 5:45) bali kuzihifadhi hizo baraka ndio ugumu ulipo.

Mwanzo 2:6

[6]ukungu ukapanda katika nchi, ukatia maji juu ya uso wote wa ardhi. 

 

Wekeza kwenye maombi na kutendea kazi imani yako kwa vitendo. Zaidi ya kutarajia tu Mungu atende mwenyewe.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

 

Print this post