Kuishi ni tufoauti na kuwa na uhai. Hata mti ni hai, lakini hauishi. Kuishi ni maisha, yaani unasifa ya kuwa na mfumo au ustaarabu Fulani ambao unatembea nao, unaweza kuchagua mahali pa kukaa, unafanya kazi, unapumzika, unajenga, unapanda, unajichagulia burudani mfano miziki, michezo, vyakula, unafanya ibada, unauza, unanunua.. mambo kama hayo kiumbe kikitenda tunasema kinaishi.
Lakini kuwa kifungoni, ndani ya gereza huoni jua wala mwezi siku zako zote uwapo duniani, hatuwezi kusema unaishi, tunasema wewe upo hai, lakini hauishi.. Au unapokaa kwenye kitanda cha wagonjwa mauti-uti, umepooza, huwezi kuongea wala kutembea, umekata kauli, kwa sikuzote uwapo duniani, hayo si maisha ijapokuwa upo hai.
Sasa kuna maneno Yesu aliyasema, ambayo si wengi hujaelewa kwa undani na upana.. Tusome;
Yohana 11:25-26
25 Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi; 26 naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo?
Hii kauli ukiisoma vizuri, unaweza ukasema inajichanganya, Embu tafakari, jambo la kwanza Yesu anasema, tukimwamini tukifa tutakuwa tunaishi, lakini pia tukiwa hai na kuamini hatutakufa kabisa hata milele.
Je! Sisi tuliomwamini hatufi?
Jibu ni Ndio hatufi kabisa, bali tunahamishwa makao. Hicho kinachoitwa kifo, ni macho ya wanadamu yanaona hivyo, lakini sisi tunakuwa kama tumefumba macho, kisha tukafumbua na kujikuta katika ulimwengu mwingine kabisa, Ndio maana lugha ambayo hutumika kueleza hali hiyo kwa watakatifu ni kulala (Matendo 7:54-60, 1Kor 15:51-58, Yohana 11:11-19)
Sisi tuliomwamini Yesu hatutaona kitu kinachoitwa kaburi, wala hatutajikuta kwenye gereza Fulani , bali kwenye ulimwengu mwingine mzuri sana uitwao pepo, sio tukiwa hai, bali tukiwa tunaishi kabisa huru.
Maana yake, tunaendeleza maisha, ikiwa kuna kutembea, huku na huko au kushughulika kwa vitu vya kimbingu, kufanya hivi, kufanya vile..Tutakuwa tunayafanya. Hayo ndio maisha anayosema mtu akimwamini yeye, ajapokufa (lala), atakuwa anaishi.. Si atakuwa na uhai
Tutakaa huko pepo, kwa kipindi chote, ambacho tunamsubiria Yesu, kulikamilisha kusudi la watakatifu wote, kisha baadaye,(mwisho ukifika), atakuja mwenyewe kuwachukua walio hai Pamoja na miili yetu tuliyoiacha duniani, na sote kwa Pamoja tutaanza ziara mpya ya kuelekea mbingu ya tatu. Makao yetu ya milele yalipo (2Wakorintho 12:2-4)
Lakini waovu wanapokufa, wenyewe watajiona kwanza wakiingia makaburini, kisha wakishuka kuzimu, Uhai wao ukitunzwa kwenye vifungo vya giza wasijue chochote, wala wasitende kazi yoyote, mpaka siku ya hukumu itakapofika, ambapo watatolewa huko kisha watasimama kwenye kiti cha enzi cheupe cha mwana-kondoo kwa ajili ya hukumu, (Ufunuo 20) baada ya kuhukumiwa ndipo watakapotupwa kwenye ziwa la moto, na kuangamia milele.
Sasa wakiwa huko kuzimu, ambapo kwa jina lingine kunaitwa Jehanamu, ni mahali pa shida, dhiki nyingi na mateso yasiyoelezeka, huko hakuna maisha, ni mateso tu vifungoni.
Hivyo ndugu, unapomwamini Yesu ipo faida kubwa zaidi ya unavyofikiri, unapokea MAISHA YA MILELE, Tangu ukiwa hapa duniani, ndani yako hakuna kitu kinachoitwa kifo, wala hutakihisi hata kidogo. Kwanini leo usimkaribishe maishani mwako? Ikiwa upo tayari basi wasiliana nasi kwa namba hizi kwa ajili ya mwongozo wa sala ya Toba, bure.
Au sema sala hii kwa Imani, na Moja kwa moja Yesu ataingia moyoni mwako.
Bwana akubariki
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
AINA ZA FARAJA BWANA AZIACHILIAZO KWA WATUMISHI WAKE.
TAFUTA UTAKASO WA SEHEMU KUU NNE ZA MWILI WAKO.
ASIYEMPENDA BWANA NA AWE AMELAANIWA.
Print this post
Maisha ya Imani, hayafuti dhiki, hayafuti hisia za kibinadamu, haijalishi mtu atakuwa na ukomavu mkubwa kiasi gani, bado mahangaiko ya ndani na nje, zipo nyakati atakutana nayo.
Mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo, pamoja na kuwa walitumiwa na Mungu kipekee sana na neema ya Mungu kubwa kukaa juu yao. Bado walikiri kwa wazi kabisa bila maficho dhiki ziliwasonga kote kote,
2 Wakorintho 7:5
[5]Kwa maana hata tulipokuwa tumefika Makedonia miili yetu haikupata nafuu; bali tulidhikika kote kote; nje palikuwa na vita, ndani hofu.
Paulo anasema nje kulikuwa na vita, maana yake maadui, walioshindana naye, kuipinga imani, kutaka kumuua, kumfunga walikuwa ni wengi sana…lakini pia ndani anasema kulikuwa na hofu si nje tu,..akiwa na maana hofu ya kwenye nafsi..mfano wa hizi ni kama vile hofu za majukumu, hofu za kusalitiwa, hofu za kuvunjwa moyo, kuachwa peke yako, za kuvamiwa na wezi, mashaka ya ugenini, kushtakiwa, hofu za mwili kudhoofika, kuugua n.k. ambazo kimsingi kazi yake ni kukufanya ukate tamaa, usisonge mbele, usizae matunda.
Ndivyo ilivyo hata kwa watumishi wa Mungu wa kweli leo, mbele ya macho ya watu wanaweza kuonekana ni watu walio- mbali na mateso, lakini kwa mujibu wa kibiblia mioyoni mwao, vipo vita vingi na hofu kote kote…
Sasa swali ni je! Wanaweza kuishi na kuendelea na imani au huduma bila kukata tamaa wakiwa katika viwango vilevile ilihali nje vita ndani hofu?
Jibu ni kuwa Bwana..huwatumia faraja kwa njia mbalimbali, na faraja hizo ni kama zifuatazo;
Paulo katika dhiki zake anasema;..Mungu, mwenye kuwafariji wanyonge, alitufariji kwa kuja kwake Tito.
2 Wakorintho 7:5-7
[5]Kwa maana hata tulipokuwa tumefika Makedonia miili yetu haikupata nafuu; bali tulidhikika kote kote; nje palikuwa na vita, ndani hofu. [6]Lakini Mungu, mwenye kuwafariji wanyonge, alitufariji kwa kuja kwake Tito. [7]Wala si kwa kuja kwake tu, bali kwa zile faraja nazo alizofarijiwa kwenu, akituarifuhabari ya shauku yenu, na maombolezo yenu, na bidii yenu kwa ajili yangu, hata nikazidi kufurahi.
[6]Lakini Mungu, mwenye kuwafariji wanyonge, alitufariji kwa kuja kwake Tito.
[7]Wala si kwa kuja kwake tu, bali kwa zile faraja nazo alizofarijiwa kwenu, akituarifuhabari ya shauku yenu, na maombolezo yenu, na bidii yenu kwa ajili yangu, hata nikazidi kufurahi.
Ni ukweli usiopingika zipo nyakati ambazo unajihisi kama kuishiwa nguvu ya kuendelea aidha na wokovu au huduma, kwasababu ya hali fulani ngumu zinazokuzunguka..
Majira kama haya, Mungu hufanya njia, habari njema za faraja zinaweza kukufikia na kukutia nguvu na hatimaye kuendelea mbele kwa hamasa mpya.
Kwamfano Paulo alikuwa katika nyakati hizo mbaya, akiona kama taabu yake kwa Mungu ni bure, hakuna matunda, lakini ghafla analetewa taarifa na Tito ya wanafunzi wake huko Korintho wamebadilika, wamesimama imara zaidi sana wana shauku naye. Hilo lilimtia nguvu tena hata kujiona tena hayupo katika dhiki.
Kwamfano unaweza ukawa unafanya huduma kwa muda mrefu, na pengine huoni matokeo uliyoyategemea, lakini ghafla unakutana na mtu anakuambia nimebadilishwa sana na huduma yako au mafundisho yako. Wakati ule unafanya maombezi nilipona ile ugonjwa, ulipokuwa unahubiri niliguswa moyoni na sasa nimeokoka.
Hiyo ni faraja kubwa sana, na kama ulikuwa umelegea unaamka tena unasema…oh! Kumbe Bwana yupo pamoja nami.
Nyakati za uzito, nyakati za dhiki, Bwana huachilia mafunuo kwa njia mbalimbali ili kukufariji katika wokovu wako au huduma yako aidha anaweza kutumia ndoto au maono, au Neno, au hata fundisho fulani kama hili unalolisoma sasa…
Paulo alipokuwa kama mfungwa anaelekea Rumi, njiani Meli ilipata shida mpaka wakakata tamaa ya kuishi..lakini Mungu alimtokea na kumtia nguvu kwa maono.
Matendo ya Mitume 27:23-24
[23]Kwa maana usiku huu wa leo malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye, alisimama karibu nami, [24]akaniambia, Usiogope, Paulo, huna budi kusimama mbele ya Kaisari; tena, tazama, Mungu amekupa watu wote wanaosafiri pamoja nawe.
[23]Kwa maana usiku huu wa leo malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye, alisimama karibu nami,
[24]akaniambia, Usiogope, Paulo, huna budi kusimama mbele ya Kaisari; tena, tazama, Mungu amekupa watu wote wanaosafiri pamoja nawe.
Ni kawaida ya Mungu, kutufariji kwa njia za mafunuo, wewe ni mchungaji Bwana kukuonyesha ukichunga watu wengi, litakuwa ni jambo la kawaida, au anaweza kukupa andiko ambalo, litakupa sababu ya kusimama au kuendelea mbele. Au wakati mwingine hata kutumia mtumishi wake kukufundisha, na lile fundisho likawa ni nanga kubwa sana kwako, kutembea katika aina yoyote ya mapito.
Hii ni namna nyingine ambayo Mungu huwafariji watumishi wake, huwafungulia milango ya kifedha, aidha kusaidiwa na watu wa amani mahali fulani kimahitaji.
2 Wakorintho 11:9
[9]Nami nilipokuwa pamoja nanyi na kuhitaji sikumlemea mtu. Maana hao ndugu waliokuja kutoka Makedonia walinipa kadiri ya mahitaji yangu; nami katika mambo yote najilinda nafsi yangu nisiwalemee hata kidogo; tena najilinda.
Ni kawaida ya Mungu, nyakati fulani kufungua milango ya kupokea vitu kwa watu wake, lengo lake ni kukufariji, kukutia moyo ili usonge mbele katika kazi yake.
Hii ni njia nyingine ambayo Bwana huitumia sana, kutukumbusha mioyoni mwetu kuwa hizi taabu ni za kitambo, Bwana wetu ametuandalia makao na siku moja atarudi, nasi tutaishi naye milele na milele mbinguni.. katika maisha ya milele yasiyokuwa na fujo..Bwana anataka tuyakumbuke hayo, tufarijike.
1 Wathesalonike 4:16-18
[16]Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. [17]Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. [18]Basi, farijianeni kwa maneno hayo.
[16]Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.
[17]Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.
[18]Basi, farijianeni kwa maneno hayo.
Sikuzote kumbuka kuwa furaha yetu, urithi wetu, utajiri wetu upo kule ng’ambo unatungoja, hapa duniani ni wasafiri, hivyo hatutaona shida tuwapo katika dhiki za muda mfupi…Ni sawa na umeingia katika nyumba ya wageni, halafu ukaona mazingira si safi, aidha ya choo au vyumba..huwezi kulalamika na kuanza kusoneneka na kutaabika sana, kana kwamba umeingia kwenye matatizo makubwa…hapana utavumilia tu.kwasababu unajua hapo sio kwako, unapita tu utalala siku moja kesho yake utaondoka..na kurudi kwako palipo pasafi..hivyo utavumilia.
Bwana akutie nguvu. Songa mbele katika imani.
Amen.
MAANA HUYAWAZI YALIYO YA MUNGU, BALI YA WANADAMU
WALAKINI MIMI SI PEKE YANGU.
LAKINI DAUDI ALIJITIA NGUVU KATIKA BWANA, MUNGU WAKE.
(Masomo maalumu ya utakaso)
Jina la Bwana na Mwokozi YESU KRISTO libarikiwe. Karibu tujifunze Biblia, Neno la MUNGU wetu lililo Taa na Mwanga wa Njia yetu.
Je unazijua sehemu Nne (04) za Mwili wa Bwana YESU zilizotobolewa na kumwaga damu pale msalabani?.. Basi kama huzifahamu sehemu hizo ni 1)Kichwa, 2)Mikono, 3)Ubavu na 4)Miguu.
Tutazame moja baada ya nyingine, na pia tujifunze kwanini ni viungo hivyo ndio vilimwaga damu na kwanini vinahitaji utakaso sana.
1.KICHWA
Maandiko yanatuonyesha kuwa Bwana YESU alivikwa taji ya Miiba ..
Mathayo 27:28 “Wakamvua nguo, wakamvika vazi jekundu. 29 Wakasokota taji ya miiba, wakaiweka juu ya kichwa chake, na mwanzi katika mkono wake wa kuume; wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki, wakisema, Salamu, Mfalme wa Wayahudi!”
Mathayo 27:28 “Wakamvua nguo, wakamvika vazi jekundu.
29 Wakasokota taji ya miiba, wakaiweka juu ya kichwa chake, na mwanzi katika mkono wake wa kuume; wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki, wakisema, Salamu, Mfalme wa Wayahudi!”
Kwanini sehemu hii ya kichwa ilimwagika damu?.. Ni kwasababu kichwani ndiko kwenye ufahamu wa mtu, na milango yote ya ufahamu kama macho, masikio, pua na ulimi vipo huko.. na kwa kupitia vitu hivyo watu wanafanya dhambi, kwamfano kupitia ulimi mtu atasema uongo, atatukana, atakejeli n.k,
Kupitia macho mtu atatazama kwa kiburi sawasawa na (Mithali 6:17), kupitia macho mtu ataangalia uchafu, na pia kupitia masikio mtu atasikiliza mabaya, usengenyaji, njama mbaya n.k
Kwahiyo ni lazima Damu ingekota usoni kutakasa uso wa Bwana kwani dhambi zetu zote alizibeba yeye
2. UBAVU.
Biblia pia inatuonyesha kuwa Ubavuni mwa YESU palitokea damu..
Yohana 19:33 “Lakini walipomjia Yesu na kuona ya kuwa amekwisha kufa, hawakumvunja miguu; 34 Lakini askari mmojawapo alimchoma ubavu kwa mkuki; na mara ikatoka damu na maji”.
Yohana 19:33 “Lakini walipomjia Yesu na kuona ya kuwa amekwisha kufa, hawakumvunja miguu;
34 Lakini askari mmojawapo alimchoma ubavu kwa mkuki; na mara ikatoka damu na maji”.
Sasa kwanini ubavuni?.. Ni kwasababu ubavuni ndipo Moyo wa mtu ulipo, na hata wale Askari wa kirumi walikusudia kuhakiki kifo cha Bwana YESU kwa kumpiga mkuki katika moyo..
Na moyo ndio ubebao mawazo yote ya mtu ikiwemo mawazo mabaya..
Mathayo 15:19 “Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano”
Kwahiyo kulikuwa na sababu kwanini damu itokea moyoni ni kuonyesha utakaso wa Moyo..
3. MIKONO
Pia Biblia inatuonyesha kuwa mikono ya Bwana YESU ilitoka damu..
Yohana 20:25 “Basi wanafunzi wengine wakamwambia, Tumemwona Bwana. Akawaambia, Mimi nisipoziona mikononi mwake kovu za misumari, na kutia kidole changu katika mahali pa misumari, na kutia mkono wangu katika ubavu wake, mimi sisadiki hata kidogo”.
Kwanini mikono?.. Kwasababu mikono ndio inayoshika, inayofanya kazi za kila namna, (zilizo njema na mbovu)…watu wanafanya mauaji kwa kutumia mikono yao, kwa ufupi mikono ni nyenzo kubwa ya mabaya ndani ya mtu ndio maana katika ile ile Mithali maandiko yanasema, moyo uwazayo mabaya ni machukizo kwa Bwana..
Mithali 6:16 “Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake. 17 macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia; 18 moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu”
Mithali 6:16 “Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake.
17 macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia;
18 moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu”
4. MIGUU
Biblia inatuonyesha sehemu nyingine ya mwisho ya mwili wa Bwana YESU iliyomwagika damu ni miguu..
Luka 24:38 “Akawaambia, Mbona mnafadhaika? Na kwa nini mnaona shaka mioyoni mwenu? 39 Tazameni mikono yangu na miguu yangu, ya kuwa ni mimi mwenyewe. Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo”.
Luka 24:38 “Akawaambia, Mbona mnafadhaika? Na kwa nini mnaona shaka mioyoni mwenu?
39 Tazameni mikono yangu na miguu yangu, ya kuwa ni mimi mwenyewe. Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo”.
Miguu ni kiungo kingine chenye kuutia mwili mzima unajisi..watu wanatumia miguu kukimbilia mabaya, kukimbilia uzinzi, mauaji, ulevi n.k
Mithali 6:16 “Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake. 17 Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia; 18 Moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu”
17 Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia;
18 Moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu”
Sasa viungo hivi ni lazima vitakaswe kwa damu ya YESU, na vinatakaswaje?
Vinatakaswa kwanza kwa kumwamini Bwana YESU KRISTO, na kuomba na kuacha dhambi.. zingatia hili neno “kuacha dhambi” kupitia viungo hivyo.
Angalia miguu yako inachokimbilia, je ni chema au ni kibaya.. jiuepushe miguu yako na njia za wakosaji, angali macho yako yanachokitazama ni chema au kibaya, jiepushe na kutazama mambo yasiyofaa, vivyo hivyo na mikono yako na moyo wako, angalia sana unavyovifuatilia na kuvifanya.
Mwisho, kumbuka tunaishi katika siku za mwisho, na Kristo amekaribia sana kurudi, wakati wowote parapanda ya mwisho italia na hukumu ya mataifa itaanza, je umejiandaaje?
Shalom
USHUHUDA WA MATENDO NI MKUU KULIKO WA MANENO.
UZURI WA MAJIVU.
IPO NJIA YA MKATO YA KUFIKA KIWANGO VYA MBALI VYA KIROHO.
Na kipenu ni nini (Isaya 1:8)
Wokovu wa milele/ Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?
WhatsApp
Mathayo 8:29
[29]Na tazama, wakapiga kelele, wakisema, Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?
Mashetani yanajua kila jambo lipo katika mpangilio wa muda wake, yanajua kuwa tayari hukumu ilishatolewa ya wao kutupwa katika ziwa la moto lililo hatma yao ya milele..
Lakini utekelezaje wake, utakuja baadaye, ambao utakuwa ni mwisho wa dunia, utakao asisiwa na Bwana Yesu Kristo mwenyewe.(Mathayo 25:41)
Wengi tunadhani mapepo, hushindana na sisi, kwa kutuonea wivu, hilo ni kweli kwa sehemu, lakini sababu kubwa ya mapepo na shetani kushindana na sisi…ni wao kujilinda…na adhabu ijayo.
Na wanajua mwanadamu ndiye anayeweza kuiharakisha hiyo siku au kuikawiisha hiyo siku. Ndio maana yanafanya kazi kubwa sana kuwaharibu wanadamu ili siku hiyo isifike upesi.
Hizi ni njia tatu mapepo, hufanya kwa watu ili kukawiisha muhula wao usiwafikie haraka.
1) Kuchochea maovu.
2) Kukengeusha Imani za watu
3) Kukawisha injili
Maovu mengi, humsukuma Mungu kuwa mvumilivu na wanadamu, ili wafikie toba wasiangukie hukumu ya mapepo..Kama wanadamu wasingekuwa na shingo ngumu, mwisho wa dunia na hukumu yao ingeshafika zamani sana.. hivyo mapepo wanabuni kazi mbalimbali ili kuwafanya wanadamu wazidi kupotoka.
2 Petro 3:9-11
[9]Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba. [10]Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea. [11]Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,
[9]Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.
[10]Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.
[11]Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,
Luka 18:8
[8]Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?
Kristo anatarajia kanisa lake kusimama katika msingi wa imani kamili ambayo haijaharibiwa wala kuvurugwa na mapokeo na mafundisho ya uongo.. hii ndio sababu ya shetani kuinua makundi ya manabii wa uongo, kufundisha injili nyingine ambayo Kristo hajaileta duniani. Matokeo yake ndio kuwa na kundi kubwa la wakristo lakini dhaifu wasio tayari kumlaki Bwana mawinguni.
Mathayo 24:14
[14]Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.
Injili ya kweli adui huipiga vita vikubwa..Na wanajua ikihubiriwa ulimwenguni kote, basi ushuhuda wa Mungu utakuwa umefika na hakuna atakayekuwa na udhuru.
Sasa mimi na wewe hatuna budi kusimama katika utakatifu lakini pia imani na injili kuisambaza ili watu waokolewe…
Kumbuka tayari tupo kwenye siku za mwisho, Amka simama na Bwana.
MAPEPO YANATAFUTA HIFADHI NDANI YAKO KWA BIDII SANA.
Je mkristo anaweza akawa na mapepo?
Shetani anaishi wapi, Je! Amefungwa au yupo kuzimu?
1 Petro 1:23-25
[23]Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima, lidumulo hata milele. [24]Maana, Mwili wote ni kama majani, Na fahari yake yote ni kama ua la majani. Majani hukauka na ua lake huanguka; [25]Bali Neno la Bwana hudumu hata milele. Na neno hilo ni neno lile jema lililohubiriwa kwenu.
[23]Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima, lidumulo hata milele.
[24]Maana, Mwili wote ni kama majani, Na fahari yake yote ni kama ua la majani. Majani hukauka na ua lake huanguka;
[25]Bali Neno la Bwana hudumu hata milele.
Na neno hilo ni neno lile jema lililohubiriwa kwenu.
Neno la Mungu linatuonyesha mtu aliyeokoka, anatambulika kuwa amezaliwa mara ya pili kwa mbegu isiyo haribika…lakini wengi hawajui makusudi ya kuzaliwa kwa mbegu hiyo ni nini?
Kabla ya kuona mbegu isiyo haribika, ifahamu kwanza mbegu iharibikayo ni ipi..
Katika habari hiyo tunaonyeshwa mbegu iharibikayo mfano wake ni ile ya mwanadamu .maana yake ni kuwa wewe ulizaliwa kwa mbegu ambayo inaanza katika mtoto, kisha ujana wenye nguvu, lakini baadaye utaishia na kuchakaa, na kuchoka kwa kuishiwa nguvu na hatimaye kufa…ndio hapo anasema mwili wote ni kama nyasi hukauka na kuanguka…kwasababu asili ya mbegu hii si ya kudumu daima.
Vivyo hivyo na mbegu nyingine zote za hapa duniani mfano, za wanyama, samaki, mimea zote ni mbegu ziharibikazo huisha ubora kulingana na wakati.
Lakini ukizaliwa kwa mbegu isiyo haribika maana yake ni kuwa ubora wako haupungui wala hauishi kulingana na wakati ..
Mtu aliyezaliwa kwa mbegu hii ambayo ni Neno la Mungu…huwa hazeeki rohoni, haishiwi nguvu wala hafi kiroho..
Lakini utashangaa mtu anasema kazaliwa mara ya pili, hapo mwanzoni alianza vizuri sana na Bwana, anaomba, anasoma Neno, amesimama, anamtumikia Bwana kwa bidii na uaminifu, lakini baada ya muda anaanza kupoa, hatimaye anaacha hata kuabudu na mwisho anakufa kiroho….miaka miwili nyuma alikuwa ameokoka lakini leo ni mtu mwingine kabisa…hapo ni lazima ujiulize je huyu mtu alizaliwa kwa mbegu ipi?
Kama ni mbegu isiyoharibika mbona wokovu wake unaharibika kulingana na wakati ..kikawaida mwamini kwenye maisha ya kiroho hufanyika upya siku baada ya siku, huama kutoka utukufu mmoja hata mwingine imani moja hata nyingine…lakini wewe unaharibika siku baada ya siku, je wewe ni mbegu gani?
2 Wakorintho 3:18
[18]Lakini sisi sote, kwa uso usiotiwa utaji, tukiurudisha utukufu wa Bwana, kama vile katika kioo, tunabadilishwa tufanane na mfano uo huo, toka utukufu hata utukufu, kama vile kwa utukufu utokao kwa Bwana, aliye Roho.
2 Wakorintho 4:16
[16]Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku.
Ikiwa unajiona wewe umezaliwa kwa mbegu isiyoharibika, basi onyesha hivyo kwa ubora wako wa kiroho na kiiamani kila siku…ikiwa ni mchungaji onyesha mwendelezo wa kulisimamia kundi la Mungu katika nyakati zote iwe ni ngumu na nyepesi, ikiwa ni mwinjilisti, hupaswi kuacha kuhubiri maisha yako yote, ikiwa ni mhudumu wa kanisani, simama katika nafasi yako kwa ubora wote…usiseme yatosha, usiseme nimechoka,.kwasababu hukuzaliwa kwa mbegu ichokayo, isinyaayo, bali kwa Neno la Mungu lidumulo milele. Ikiwa ni mwombaji, usianze kusema hapo zamani mimi nilikuwa nina uimara kimaombi, kinyume chake onyesha vitendo, hata sasa moto wako ni ule ule tena na zaidi.
Unyesha ubora huo na amani ya Bwana iwe pamoja nawe.
Maran Atha.
Shuhuda za Mungu ni zipi?
Bawa la mbuni hufurahi; Lakini mabawa yake na manyoya yake, je! Yana huruma?
TIA MIZIZI CHINI, ILI UZAE MATUNDA JUU.
Jina la Bwana YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu wetu lilo njia na Mwanga wa njia yetu (Zab. 119:105).
Je! Umeokoka na kuna dhambi ambayo bado hujaiacha na hujui ufanye nini?.. Twende pamoja katika ujumbe huu utapata kitu au suluhisho la tatizo ulilo nalo.
Awali ya yote ni muhimu kufahamu kuwa, mtu anapoamua kwa dhati kabisa kutoka moyoni mwake kumfuata YESU, basi zile dhambi zote zilizokuwa zinamtesa ni lazima zife ndani yake!, lakini inapotokea mtu kaokoka lakini bado mambo ya kale yanamsumbua kuna SHIDA!
Fanya hivi ili upone hilo tatizo… ACHA HIYO DHAMBI!..ACHA KUITUMIA HIYO DHAMBI!. Huenda bado hujaelewa.. ni hivi.. ACHA HIYO DHAMBI.
Kitu chochote ukiacha kukitumia kinaisha nguvu na hatimaye kinakufa kabisa/kinapotea…hata chuma kisipotumika kinapata kutu na hatimaye kuharibika kabisa..Moto usipochochowa unakufa (Soma Mithali 26:20) na Dhambi isipotumika inakufa…Hiyo ndio tabia ya dhambi wengi tusiyoijua.. kuwa dhambi ina tabia ya KUFA.
Warumi 6:11 “Vivyo hivyo ninyi nanyi jihesabuni kuwa WAFU KWA DHAMBI na walio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu”.
Ukitaka kushinda dhambi ya “Kujichua”.. “Acha Kujichua”… Ukitaka kuacha dhambi ya Uzinzi acha uzinzi, ukitaka kuacha dhambi ya ulevi, acha ulevi, ukitaka kuacha matusi, acha kutukana, ukitaka kuacha hasira acha hasira..
Mithali 28:13 “Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye NA KUZIACHA atapata rehema”.
Utauliza.. “nitaachaje”.. Wazo linapokuja kichwani la kwenda kufanya hivyo, unaanza kulikataa likiwa huko huko kichwani, na kukubaliana na matokeo ya maumivu, kwasababu inakuhitaji kuingia gharama kushindani na dhambi….lakini ukijilegeza na kuitii dhambi itazidi kustawi ndani yako.
Ukishaikataa kichwani, ni wakati wa kuutiisha mwili wako, na kusema utafanya unachokisema wewe na unachokitaka na sio mwili unachokitaka!… nakuhakikishia ukimaanisha kufanya hivyo, dhambi itakosa nguvu ndani yako!.. Kwani unapoamka kila siku asubuhi na kukatisha usingizi wako ili uwahi kwenye majukumu yako, mwili huwa unapenda??..
Huwa haupendi katika siku za mwanzo lakini unakuwa unajilazimisha tu…mpaka ile ratiba inapokaa akilini kiasi kwamba unafika wakati ukifika tu ule muda wa kuamka usingizi wenyewe unakata..kwanini!..ni kwasababu tayari umeshauua usingizi majira yale uliyozoea kuamka.. kwahiyo ukifika tu huo wakati hauhitaji kengele, tayari kengele ipo kwenye ubongo wako na usingizi unakuwa haupo huo muda..
Na dhambi ni hivyo hivyo, unaiacha na kuilazimisha isikae maishani mwako, na mwisho itakufa tu… mahali pale ulipozoa kukutana ili kulewa, zikifika zile saa hata kiu haipo, mitaa ambayo ulikuwa ukikatiza ni lazima utamani kulewa, sasa utaikatiza bila shida yoyote.
Aina ya watu ambao ulikuwa ukiwaona huwezi kuvumilia, unawaka tamaa…utafika wakati utawaona ni watu wa kawaida sana, tena utajishangaa ulikuwa ni mtu wa namna gani?
Rushwa ulizokuwa unakula, ambazo huwezi kufanya jambo bila kuhonga, utajishangaa hutamani tena kuchukua/kutoa rushwa..
Lakini ni lazima uingie gharama katika hatua za awali, usikubali kujilegeza.. na kusubiri muujiza wa wewe kuacha hayo…amua kubadilika kwa KUACHA DHAMBI.. ACHA DHAMBI, ACHA DHAMBI..Hakuna dawa nyingine zaidi ya hii ACHA!, na MUNGU atakusaidia..
Shalom.
MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.
Je tamaa ni dhambi kulingana na Yakobo 1:15?
Ipi tofauti kati ya sadaka ya dhambi na sadaka za hatia?
NITAACHAJE DHAMBI?.
Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.
SWALI: Mara nyingi biblia inataja “shuhuda za Mungu” Je hizi shuhuda ni zipi?
Mfano katika vifungu vifuatavyo Neno hilo utaliona;
Zaburi 119:2
[2]Heri wazitiio shuhuda zake, Wamtafutao kwa moyo wote.
Zaburi 119:22
[22]Uniondolee laumu na dharau, Kwa maana nimezishika shuhuda zako.
Zaburi 119: 24
[24]Shuhuda zako nazo ndizo furaha yangu, Na washauri wangu.
Zaburi 119:99
[99]Ninazo akili kuliko wakufunzi wangu wote, Maana shuhuda zako ndizo nizifikirizo.
Soma pia…Zab 119:119, 144, 132:12
Hizi shuhuda ni zipi?
Shuhuda ni neno linalozaa ushuhuda au kushuhudia.
Ni kitendo cha kuthibitisha ukweli wa jambo.
Kwamfano nikisema yule “mtu ni mkarimu”. Hapo nimemshuhudia kwasababu nimeona kitu hicho ndani yake, aidha amenitendea mimi ukarimu au kamtendea mwingine..
Tofauti na kama angejisemea mwenyewe..
Hivyo Mungu naye ana vitu amevihakiki kuwa ni kweli, na hizo ndizo zinazoitwa shuhuda zake..
Mpaka jambo Mungu amelihakiki mwenyewe ni kutuhakikishia kuwa hatupotei tukilifuata, tofauti na kama tungeshuhudiwa na wanadamu…kwasababu shuhuda za wanadamu zina udanganyifu mwingi nyuma yake.
Yesu Kristo ni mwana wa Mungu na ndiye uzima wetu.
1 Yohana 5:7-12
[7]Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli. 9… Tukiupokea ushuhuda wa wanadamu, ushuhuda wa Mungu ni mkuu zaidi; kwa maana ushuhuda wa Mungu ndio huu, kwamba amemshuhudia Mwanawe. [10]Yeye amwaminiye Mwana wa Mungu anao huo ushuhuda ndani yake. Asiyemwamini Mungu amemfanya kuwa mwongo, kwa kuwa hakuuamini huo ushuhuda ambao Mungu amemshuhudia Mwanawe. [11]Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe. [12]Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima.
[7]Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli.
9… Tukiupokea ushuhuda wa wanadamu, ushuhuda wa Mungu ni mkuu zaidi; kwa maana ushuhuda wa Mungu ndio huu, kwamba amemshuhudia Mwanawe.
[10]Yeye amwaminiye Mwana wa Mungu anao huo ushuhuda ndani yake. Asiyemwamini Mungu amemfanya kuwa mwongo, kwa kuwa hakuuamini huo ushuhuda ambao Mungu amemshuhudia Mwanawe.
[11]Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe.
[12]Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima.
Huu ndio ushuhuda mkuu wa Mungu, na huu ndio tuliopewa tuuhubiri kwa ulimwengu pia kwamba kwa Yesu kuna ukombozi, na uzima..
Matendo ya Mitume 4:33
[33]Na mitume wakatoa ushuhuda wa kufufuka kwake Yesu kwa nguvu nyingi, na neema nyingi ikawa juu yao wote.
Sisi (tulioamini) ni wana wa Mungu Huu ni ushuhuda mwingine wa Mungu mwenyewe ndani yetu kupitia Roho wake Mtakatifu.
Warumi 8:16-17
[16]Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; [17]na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye.
[16]Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu;
[17]na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye.
Si Kristo tu peke yake ni mwana wa Mungu, na sisi pia tunapomwamini tunafanyika watoto wake (Yohana 1:12 )watoto wa Mungu mfano wa Kristo.
Hivyo tunapopitia mateso kama yeye, hatupaswi kuwa na hofu au manung’uniko, kinyume chake ndio tujipige vifua vyetu kushangilia, kwani hata yule wa pekee(Yesu), aliyapitia hayo…kwasababu kama vile alivyopata mateso na alivyorithi utukufu vivyo hivyo na sisi tutarithi utukufu wake.
Mungu anataka tutembee kwa ujasiri hapa duniani, tusiishi kama yatima, tuishi tukijua kuwa tunaye Baba mbinguni anayetutazama na kujishughulisha sana na mambo yetu yote, kwasababu yeye mwenye ametuthibitisha kuwa sisi ni wana wake…Kama yeye ametuthibitisha nafsi yako kwanini ipinge? Wanadamu kwanini wapinge, ulimwengu kwanini upinge?
Hivyo kwa hitimisho ni kuwa tunaposema tumezishika shuhuda zake maana yake ni kuwa tumeamini wokovu na uzima utokao kwa Kristo Yesu, lakini pia tumekubali kuwa wana wa Mungu, yaani tukubali dhiki kwa ajili ya jina lake, tuishipo maisha ya kumpendeza yeye, lakini pia kupokea tumaini la utukufu lililo mbele yetu.
DHAMBI HAIWEZI KUKAA NA MSHAHARA WAKO.
USHUHUDA WA RICKY:
FUNGUA KINYWA CHA ROHO MTAKATIFU KIHUDUMU.
Jibu: Turejee..
Kumbukumbu la Torati 11:15 “Nami nitakupa nyasi katika MAVUE yako kulisha wanyama wako wa mifugo, nawe utakula na kushiba”.
“Mavue” ni kiswahili kingine cha “mashamba”….shamba likiwa moja linaitwa “VUE” yakiwa mengi “MAVUE”.
Kwahiyo hapo anaposema “Nitakupa nyasi katika mavue yako”.…maana yake nitakupa nyasi katika mashamba yako.
Hii ni ahadi ya Mungu kwa wana wa Israeli, na ni ahadi ya MUNGU kwetu pia, ikiwa tutayashinda
Tuanzie ule mstari wa 13..
Kumbukumbu 11:13-15 “Tena itakuwa, mtakaposikiza kwa bidii maagizo yangu niwaagizayo leo, kwa kumpenda BWANA, Mungu wenu, na kumtumikia kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote, 14 ndipo nitakapowapa mvua ya nchi yenu kwa wakati wake, mvua ya masika, na mvua ya vuli, upate kuvuna nafaka yako, na divai yako, na mafuta yako. 15 Nami nitakupa nyasi katika MAVUE YAKO kulisha wanyama wako wa mifugo, nawe utakula na kushiba”.
Kumbukumbu 11:13-15 “Tena itakuwa, mtakaposikiza kwa bidii maagizo yangu niwaagizayo leo, kwa kumpenda BWANA, Mungu wenu, na kumtumikia kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote,
14 ndipo nitakapowapa mvua ya nchi yenu kwa wakati wake, mvua ya masika, na mvua ya vuli, upate kuvuna nafaka yako, na divai yako, na mafuta yako.
15 Nami nitakupa nyasi katika MAVUE YAKO kulisha wanyama wako wa mifugo, nawe utakula na kushiba”.
Neno hili pia tunalisoma katika
Maandiko yafuatayo…
1Samweli 25:15 na 1Samweli 30:11.
Je umempokea Bwana YESU KRISTO?..
Kama bado unasubiri nini mpendwa?..Fahamu ya kuwa kwa jinsi unavyozidi kuendelea kuishi maisha ya dhambi
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea.
Neno utakaso mara nyingi, tunalitazama katika jicho la Mungu kututakasa sisi(1Thes 5:23), lakini pia sisi kujitakasa wenyewe (1Petro 1:22), lakini tunasahau kuwa Kristo naye tunamtakasa… maandiko yanasema hivyo katika,
1 Petro 3:14
[14]Lakini mjapoteswa kwa sababu ya haki mna heri. Msiogope kutisha kwao, wala msifadhaike; bali mtakaseni Kristo Bwana mioyoni mwenu.
Kama Kristo anatakaswa? Swali ni je! Anatakaswaje wakati yeye ni mkamilifu?
Hapo anasema;
‘mtakaseni Kristo Bwana mioyoni mwenu’.
Kumbe ni mioyoni mwetu, sio kwamba yeye mwenyewe tumtakase mahali alipo(hawezi kutakaswa kwasababu yeye ni msafi). Mioyo yetu ndio humfanya aonekane kivingine.
Kutakasa ni kukifanya kitu kiwe kisafi au kiwe kikamilifu tena, kurejee katika hadhi yake iliyopotezwa.
Sasa kumtakasa Yesu moyoni, ni sawa na kumfanya Yesu awe jasiri tena, ajae utukufu wake, ajawe na raha na fahari yote ndani ya mtu.
Haya ni mambo ambayo ukiyatenda/ kuyakubali basi unamtakasa sana Yesu moyoni mwako
Sawasawa na hilo andiko hapo juu anasema..
Zipo nyakati ambazo utachukiwa bure kwasababu umekataa uongo, au utafukuzwa kazi kwasababu umekataa rushwa, au utafungwa kwasababu unahubiri injili ,au utapigwa kwasababu unakemea dhambi..
Nyakati kama hizi wengine huzikwepa, na kuamua kusimama na maovu ili tu kuepusha madhara yatakawapata… hawajui kuwa wanamweka Kristo kando.
Matokeo yake Yesu anakosa kutukuzwa ndani yetu, kwasababu yeye naye alikubali kuteswa kwa kusimamia ukweli na haki, akapigwa, akasulubiwa kwa kifo cha aibu.. Hivyo atakapoona watu pia wanafuata Nyayo zake, hutakasika sana, hujitukuza sana ndani ya huyo mtu, hujithibitisha kuwa kazi yake kamilifu huendelea kumulika gizani.
Hivyo usikwepe mapito yenye gharama, wala usihuzunishwe nayo maadamu ni haki unayoisimamia. Mtakase Kristo.
Lakini pia..
Waefeso 1:6-7
[6]Na usifiwe utukufu wa neema yake, ambayo ametuneemesha katika huyo Mpendwa. [7]Katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao ukombozi wetu, masamaha ya dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake.
[6]Na usifiwe utukufu wa neema yake, ambayo ametuneemesha katika huyo Mpendwa.
[7]Katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao ukombozi wetu, masamaha ya dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake.
Kwa jinsi unavyoitambua kazi ya Kristo aliyoitenda kwa ajili yako pale msalabani kwamba kwa kupigwa kwake umepokea neema na ukombozi kupitia msamaha wa dhambi ndivyo unavyomtakasa Kristo moyoni mwako.
Tumia muda mwingi kutafakari juu ya neema ya wokovu, kisha msifu na kumtukuza na kumshukuru juu ya hilo. Kristo anapoona umeithamini kazi yake, huinuka sana moyoni mwako.
Utakumbuka yule mwanamke kahaba na Miriamu ndugu yake Martha walivunja vibweta vya marhamu vyenye thamani nyingi, wakampaka Yesu kichwani na miguuni, mpaka wengine wakasema ni upotevu mkubwa sana..lakini Yesu alipoona alisema wametenda kazi njema juu yake, (Marko 14:3-9, Luka 7:36-50).
Jifunze kumtolea Kristo sadaka zaidi hata kipimo chako cha sikuzote, sio kwamba unamshawishi Yesu kwa vitu, (yeye hashawishi na hivyo)..Lakini anapendezwa sana, na watoaji, anatakasika sana pale unapofanya kitu cha ziada kwa ajili ya Mungu wako. Jifunze kutoa sana sadaka.
Yesu anajaa utukufu na waombaji…utakumbuka alikuwa na mitume kumi na wawili…lakini waliokuwa tayari kudumu naye katika masafa ya ndani ya kimaombi walikuwa ni watatu; yaani Petro Yohana na Yakobo.
Na wakati ule alipopanda juu ya ule mlima mrefu(Mathayo 17), ghafla walimwona katika utukufu mwingine wa ajabu, nguo zake zilikuwa zikimeta-meta kwa weupe mkuu.. wakashangaa na kuingiwa na hofu..
Lakini Yesu asingeweza kubadilika mbele yao, kama wangekuwa mbali na yeye katika maombi.
Hivyo unapozama sana katika uombaji, ndivyo unavyomtakasa Kristo ndani yako. Anajiona safi na mkamilifu.
Kwa hitimisho ni kuwa, unapokubali mateso pamoja na Yesu, unapo msifu sana kwa kazi yake ya msalaba, unapotoa sadaka zako nyingi na unapokuwa mwombaji.
Moyoni unahesabika kuwa unamtakasa Bwana wako sana.
Shalom, Mungu akubariki.
WALAWI WALIKUWA WENYE MIOYO YA ADILI KWA KUJITAKASA KULIKO MAKUHANI.
Kanisa kama sehemu ya maisha ya mwamini mpya.
SHUGHULIKA NA HASIRA INAYOKAA KIFUANI
Kama ni msomaji wa biblia, Neno hilo utakutana nalo katika baadhi ya vifungu kwenye Zaburi..
Zaburi 11:2
[2]Maana, tazama, wasio haki wanaupinda uta, Wanaitia mishale yao katika upote, Ili kuwapiga gizani wanyofu wa moyo.
Zaburi 21:12
[12]Kwa maana utawafanya kukupa kisogo, Kwa upote wa uta wako ukiwaelekezea mishale.
Upote ni ule uzi mwembamba unaofungwa kwenye uta, ambao mshale huwekwa pale kwa kuvutwa na kurushwa.
Upote hutengenezwa kwa ngozi na wakati mwingine kamba za mimea imara.. ni lazima utengenezwe kwa malighafi imara, ili isikatike pale unapovutwa.
Kwasababu hizi ni zana za kivita…kiroho hufunua pale mbili. Adui hutengeneza upote wake, ambao hurushia watu mishale ya moto ili kuwaua kiimani (Waefeso 6:16), ili kuweza kuishinda, biblia inatufundisha daima tuibebe ngao ya Imani.
Lakini pia Bwana Yesu anao upote wake ambao kwa huo hutupa silaha zake kwa adui zetu, sawasawa na hiyo Zaburi 21:12, Na silaha za Kristo zina nguvu sana sio tu kumlenga adui lakini pia kuangusha ngome.
Maboma na makao ya shetani.
2 Wakorintho 10:4-5
[4](maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;) [5]tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;
[4](maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)
[5]tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;
Lakini Nguvu ya silaha hizi hutegemea na hali ya mtu kiroho katika maeneo matatu;
1) kimaombi,
2)Utakatifu
3) Injili.
Mwamini wa namna hii ambaye huchukia dhambi, huubiri injili na huzingatia kudumu katika maombi ya masafa,
Kiroho ni askari imara na mwenye silaha zenye nguvu sana, ziwezazo kumuharibu ibilisi.
Kuwa askari kamili wa Kristo
Mtambo/mitambo ni nini kibiblia?
Kutawa ni nini? Sawasa na Luka 1:24