Category Archive Home

JINSI MWANADAMU ANAVYOUHARIBU USO WAKE.

Zawadi kubwa na ya kipee alipewa  mwanadamu na Mungu, iliyomtofautisha na viumbe vingine vyote, (vya mbinguni na duniani) basi ni Uso wa Mungu.

Ni mwanadamu pekee ndiye aliyeumbwa kwa mfano na sura ya Mungu (Mwanzo 1:27-28).

Biblia inaposema sura, inafananisha na mfano wa kioo,  pale mtu anapojitazama kwenye kioo, anaiona taswira yake vilevile kama yeye alivyo, ikiwa ni mwenye chunusi, basi ataiona chunusi yake kwenye kile kioo, ikiwa ni mweupe vivyo hivyo ndivyo atakavyojiona.

Kwahiyo sisi ni taswira ya Mungu kabisa, lakini ifahamike kuwa taswira hiyo sio hii ya nje, yaani pua, mdogo, masikio, hapana bali ile ya ndani, yaani tabia na sifa alizonazo Mungu, sisi pia tunazo.

Sasa kazi kubwa ya shetani, aliyokuwa nayo kwa Mwanadamu ni kumbadilisha SURA yake. Ili ifanane na kitu kingine tofauti na Mungu.

Na alijua njia pekee na kubwa ambayo hubadili taswira ya mtu, ni IBADA.

Yaani kile ambacho mwanadamu anakiabudu basi moja kwa moja hufanana nacho, wala si kile anachokitazama, au anachokishika, au anachokiangalia Hapana bali kile akifanyiacho ibada, moja kwa moja kinambadilisha taswira yake.

Ndio maana amri ya kwanza na ya pili ambayo Mungu aliwapa watu wake (Kutoka 20), ni kuhakikisha hawajifanyii sanamu ya kuchonga ya aina yoyote na kuiabudu, wala hawawi na miungu mingine, ila yeye.

Kwanini? Kwasababu wamwabudupo yeye, hudumisha tabia zake, na mwonekano wake ndani yao.Lakini wanadamu walipoanza kuabudu miungu, mfano wa Baali, Arishtoreth, n.k. hawakujua kwamba moja kwa moja wanafanana nazo.

Zaburi 115: 4-8

4 Sanamu zao ni fedha na dhahabu, Kazi ya mikono ya wanadamu.
5 Zina vinywa lakini hazisemi, Zina macho lakini hazioni,
6 Zina masikio lakini hazisikii, Zina pua lakini hazisikii harufu,
7 Mikono lakini hazishiki, miguu lakini haziendi, Wala hazitoi sauti kwa koo zake.
8 WAZIFANYAO WATAFANANA NAZO, Kila mmoja anayezitumainia

Maandiko yanasema hapo, wazifanyao, hufanana nazo, maana yake Walikuwa vipofu rohoni, viziwi rohoni, wamepooza, kabisa, hawana uhai, ndio maana hata walipokuwa wakihubiriwa Habari za hukumu na manabii hawakuelewa wala kuona ni kitu, hata Kristo alipokuja duniani bado hawakutambua wakati wa kujiliwa kwao, sio kwamba walikuwa wanafanya makusudi, lakini ni kwasababu waliabudu miungu isiyo hai, waliabudu mashetani yasiyojua kesho yao itakuwaje, mizimu isiyojua amani ya kweli ina Ladha gani, mapepo yasiyoweza kuganga mioyo ya watu, mwishowe wakafanana nao, wakawa wakatili, wauaji, wenye wivu .

Lakini tunaposoma biblia tunadhani sanamu ziliabudiwa zamani tu, Hapana, hata sasa sanamu zipo, ambapo zinawakilishwa na vitu vyote vinavyochukua nafasi ya Mungu katika mioyo ya wanadamu.

Fedha, ni sanamu, ukiiabudu ujue utafanana nayo, simu/TV yaweza kuwa sanamu, inapochukua muda wako mwingi, kutazama maudhui zake, na kuacha kabisa kumtafuta Mungu, umeshakuwa mfu hata kama unatembea,  mtu anaweza kuwa sanamu, unapomtegemea yeye zaidi ya Mungu, hapo hesabu umelaaniwa.

Lakini unapomwabudu Mungu, yaani unapomtegemea, unapomtii, unapomtumikia, unapomsujudia, ufahamu kuwa ndivyo unavyofanana na yeye, na hatimaye utakuwa hai kama yeye alivyo hai, sikuzote. Mungu anaishi milele, na wewe vivyo hivyo, Mungu ni mweza, na wewe utakuwa vivyo hivyo, Mungu ni mwenye upendo na wewe utakuwa kama yeye. Mungu ni mtakatifu, ni wa rehema, ndivyo na wewe utakuwa kama yeye. Ibada yako kwa Mungu isiibiwe na kitu chochote.

Bwana akubariki.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUSUDI LA MUNGU NYUMA YA SAFARI.

AINA ZA FARAJA BWANA AZIACHILIAZO KWA WATUMISHI WAKE.

MTU WA NNE, ANADHIHIRISHWA KWA MOTO

Print this post

WATAKATIFU BABELI.

Moja ya ombi kubwa la watu wa Mungu, pale wanapojikuta wameokoka, ni kubadilishwa mazingira waliyopo, wapelekwe kwenye mazingira mengine yenye uwepo wa karibu zaidi na Mungu, Kwasababu wakiangalia kwa sehemu kubwa mambo ambayo yanawakosesha huchangiwa na mazingira yao. Mazingira husika yanaweza kuwa mitaa wanayoishi, shule wanazosoma, maeneo ya kazi/ biashara walipo, watu wanaowazunguka, hata nchi yanayotokea.

Hii ni hali ya kawaida, na hufikia hatua wengi kuwaza mioyoni mwao, “Kama ningekuwa eneo Fulani, basi ningekuwa na mahusiano ya karibu na Mungu, ningekuwa mwombaji sana, ”

Lakini Je! Kuwaza hivyo ni sahihi?

Ndio kuwaza kubadilishwa mazingira yanayokosesha, ni vema, lakini kuwaza kuwa Hapo ulipo huwezi kumpendeza Mungu kwa viwango vyote ni uongo,. Kwasababu maandiko yanatuonyesha Mungu amewaweka watumishi wake katika mazingira yote, yaani mazingira rafiki na yale yasiyo rafiki, kwa mapenzi yake, na kuthibitisha kuwa kote kote, kumpendeza Mungu kunawezekana. Kwasababu dunia moja.

Bwana aliwaweka watakatifu Babeli, alikuwepo Shedraka, Meshaki, Abednego na Danieli.

Hawa waliishi katika taifa la kipagani usiokuwa wa kawaida,ni taifa lenye shinikizo kubwa la mtu kuabudu miungu hata kama hapendi, lenye mikorogo ya kila namna ya maovu. Lakini watu hawa walisimama vema na Bwana.

Waliwezaje?

Yafuatayo ni mambo ambayo yaliyatenda mpaka ufanikiwa kuishi katika viwango vyote vya ukamilifu.

1) Waliitangaza Imani yao mapema.

Mwanzoni kabisa akina Danieli walipochukuliwa Babeli, na kusomeshwa elimu ya wakaldayo,tunaona walipewa vyakula ambavyo ni najisi, lakini Danieli alisimama mapema na kumwomba msimamizi, kulishwa vyakula vingine visivyo najisi. Na Mungu akawa Pamoja nao. Wakatambulika tangu mapema kuwa wao ni watumishi wa wayahudi wasiojichangamana na desturi za kimataifa.

Hawakungoja, miaka ipite baadaye..bali mezani tu, wanaanza kutangaza misimamo yao.

Danieli 1:8-9

[8]Lakini Danieli aliazimu moyoni mwake ya kuwa hatajitia unajisi kwa chakula cha mfalme, wala kwa divai aliyokunywa; basi akamwomba yule mkuu wa matowashi ampe ruhusa asijitie unajisi. 

[9]Basi Mungu alimjalia Danieli kupata kibali na huruma machoni pa huyo mkuu wa matowashi. 

Hii ni desturi ambayo na sisi, kama watoto wa Mungu babeli, tuwapo katikati ya wasioamini, tujitambulishe mapema. Hiyo itasaidia sana wao kutokukuhusisha katika matendo yao ya giza wakijua kuwa wewe ni mwamini.

Wengi wameshindwa kung’atuka katika mazingira mabovu kwasababu ya kushindwa kujitambulisha wao ni akina nani, kwa wanaowazunguka.

2) Walikuwa waombaji

Danieli akiwa Babeli, alijijengea desturi na kutwa mara tatu, kupiga magoti na kuomba, akijua kuwa nguvu ya kusimama na kuendelea mbele ilitegemea sana maombi…

Ijapokuwa alikuwa na majukumu makubwa kama waziri katika taifa lakini hakuruhusu muda wake mahususi wa maombi kuibwa.

Danieli 6:10

[10]Hata Danieli, alipojua ya kuwa yale maandiko yamekwisha kutiwa sahihi, akaingia nyumbani mwake, (na madirisha katika chumba chake yalikuwa yamefunguliwa kukabili Yerusalemu;) akapiga magoti mara tatu kila siku, akasali, akashukuru mbele za Mungu wake, kama alivyokuwa akifanya tokea hapo. 

Vivyo hivyo na sisi tuwapo popote pasipofaa, hatuwezi sema hatuna muda wa sala. Ikiwa umebanwa upo muda wa chakula cha mchana kazini unaweza tumika nafasi kusogea mahali tulivu na kuomba.

3) Walikubali kujitwika misalaba yao.

Kujitwika msalaba maana yake ni kukubali kuipokea imani kwa gharama yoyote ile, yaani kama ikitokea nitatengwa kwasababu ya imani yangu, nitafungwa, nitauawa..Je nipo tayari?

Ndivyo ilivyokuwa kwa Meshaki, shedraka, Abednego, Danieli, Yusufu.

Wote hawa walikubali kutupwa kwenye matanuru ya moto, kwenye magereza, matanuru ya simba, walipojaribiwa.

Vivyo hivyo na sisi, lazima tufahamu mapema kuwa, imani haipendwi, ulimwengu sio rafiki kwetu, kama ikitokea tunalazimishwa kuikana imani je! Tutachukua hatua gani?

Wengine wameshindwa na majaribu mbalimbali ya Babeli, wameanguka katika uzinzi,wizi, upagani kwa sababu tu ya kuhofia kupoteza kazi zao, familia zao, heshima zao, mali zao, uhai wao.

Ili uweza kuishi vema Babeli, ufahamu huu wa kujitwika msalaba ni lazima uwe nao tangu mwanzo kabisa wa kuamini kwako. Kumbuka sikuzote nguvu ya kuushinda ulimwengu upo katika msalaba.

4) Waliwajibika kwa bidii na uaminifu.

Utaona hawakuwa wavivu, au walegevu, au watu wasiokuwa na shughuli zao maalumu, bali waliwajibika..Danieli pamoja na wenzake walisoma ili kupata elimu na kuwajibika katika shughuli za kifalme mpaka wakaonekana hakuna wa kufanana na wao kwa hekima na ujuzi, 

Yusufu naye alisimama kwenye majukumu yake, wala hakuna mahali alionekana mlegevu. Na wote hawa walitanguliza uaminifu.

Walijua kabisa kutowajibika ni mlango mwingine wa shetani, kuinua majaribu.

Waefeso 4:27-28

[27]wala msimpe Ibilisi nafasi. 

[28]Mwibaji asiibe tena; bali afadhali afanye juhudi, akitenda kazi iliyo nzuri kwa mikono yake mwenyewe, apate kuwa na kitu cha kumgawia mhitaji. 

Hivyo na sisi pia tuwapo kwenye Babeli zetu, tuwe makini kuwajibika kwa bidii na uaminifu, tuepuke uvivu, kama watoto wa Mungu ni wajibu kujishughulisha.

Tukifanikiwa kuwa na uwiano huo mzuri, Neema ya Mungu itatusaidia.

Bwana akubariki.

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MNARA WA BABELI

Ipi tofauti ya Falme, Mamlaka na Wakuu wa giza (Waefeso 6:12)

KWA KUWA FURAHA YA BWANA NI NGUVU ZENU. 

Print this post

MWENENDO WA KORA NA WATOTO WAKE.

Chanzo kibaya, Haimaanishi mwisho mbovu, chanzo chaweza kuwa bora lakini mwisho ukawa mbovu, Vilevile chanzo chaweza kuwa kibovu, mwisho ukawa mzuri.

Moja kati ya watu waliofanya uasi mkubwa mpaka Mungu akawaangamiza kwa kuwashusha kuzimu moja kwa moja wakiwa wazima, basi alikuwa ni Kora na jamii ya watu wake.

Ni mtu ambaye anatajwa hata baadaye katika agano jipya (Yuda:1:11), kama kielelezo akifananishwa na watu waasi waliopotoka wa siku za mwisho, kwasababu ya maasi yake kuwa makubwa yenye kuambukiza.

Hesabu 16:31-33

[31]Basi ilikuwa, hapo alipokwisha kusema maneno haya yote, nchi iliyokuwa chini yao ikapasuka; 

[32]nchi ikafunua kinywa chake, na kuwameza, na watu wa nyumba zao na wote walioshikamana na Kora, na vyombo vyao vyote. 

[33]Basi wao, na wote waliokuwa nao, wakashukia shimoni wali hai; nayo nchi ikawafunika wakaangamia kutoka mle mkutanoni. 

Lakini ijapokuwa wazazi walifanya vibaya…watoto hawakufuata njia za baba yao (Hesabu 26:11)

Kinyume chake baadaye tunaona wazao wa kora wakaambata na Bwana kwa  bidii mpaka wakawa sehemu takatifu ya Mungu, yaani waimbaji wa hekaluni.

Nafasi iliyo takatifu sana.

1 Nyakati 6:31–38, 

Wengine wakawa wafungua malango ya nyumba ya Mungu (1 Nyakati 9:19)

Na Kama hilo halitoshi Sehemu nyingi za  Zaburi zilitungwa na wana wa Kora. Mfano wa hizo ni

(Zaburi 42, 44, 45, 46, 47, 48, 49, 84, 85, 87, 88).

 Huu ni mchango mkubwa sana kwenye ufalme wa Mungu. Ambao mpaka sasa tunakula matunda yake.

Lakini si rahisi kukubali kama hao ni wana wa mtu mwasi Kora. Ni sawa na leo usikie wana wa Yezebeli ni manabii wa Bwana.., wana wa Elima-mchawi ni mitume wa Kristo.

Tufahamu kuwa rehema za Mungu, haziathiriwi na asili, au mwanzo mbovu. Maadamu moyo umegeuka kweli kweli, Bwana huanza historia mpya.

Hapo mwanzo uliitwa Kora lakini leo ukigeuka utaitwa Musa, uliitwa Sauli leo utaitwa Paulo.

Sahau yaliyopita, anza ukurasa mpya na Bwana. Wazazi wako walikosea, hata na wewe mwenyewe ukakosea, ukapata sifa mbaya, ukawa kama mfu, . LEO HII, kubali toba ya kweli, uwe kiumbe kipya, ukubaliwe na Bwana, upendwe na Bwana, utumiwe na Bwana, hata kama una asili ya sifa mbaya.

Je upo tayari leo kukata shauri kwa kutubu na kumpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yako?

Kama ndio basi hapo ulipo piga magoti kisha sema sala hii kwa imani kutoka moyoni ukimaanisha kabisa kutaka ukombozi wa nafsi yako leo. SEMA;

Bwana Yesu, asante kwa upendo wako mkuu, kwa kuja duniani kunikomboka maisha yangu, katika dhambi na hukumu. Leo hii nimeamini kwa moyo wangu wote, na kupokea msamaha wa dhambi upatikanao kwa dhabihu ya damu yako takatifu. Kuanzia leo mimi ni mwana wa Mungu, nimemkataa shetani na kazi zake zote. Karibu Roho Mtakatifu ndani yangu. Ufanye makao yako sasa, nitembee kwa nguvu zako, na kukutumikia. Nimeomba nikiamini katika jina la Yesu Kristo.

Amen

Mpaka hapo utakuwa umepokea msamaha wa dhambi, hivyo hatua zinazofuata na malezi ya kiroho ili umjue Mungu, ukue kiroho, Na ubatizo ikiwa bado hujabatizwa.

Kwa mawasiliano. 

Piga namba hizi : +255789001312 / +255693036618

Lakini tembelea tovuti yetu yenye mafundisho mengi zaidi ya elfu tano (5000), upate kujifunza kufuatana na mada mbalimbali za kiroho.

Mungu akubariki.

ashirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Print this post

Biblia ina maana gani inaposema katika kuota kwao huutia mwili unajisi?

Yuda 1:7-8

[7]Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele. 

[8]Kadhalika na hawa, katika kuota kwao, huutia mwili uchafu, hukataa kutawaliwa, na kuyatukana matukufu. 

Maandiko hayo, yanazunguzia tabia ya watu waasi ambao wameshaijua kweli lakini wamependa kuendelea katika dhambi zao.

Hivyo katika andiko hilo anasema katika kuota kwao huutia mwili uchafu…sasa huko kuota kunakozungumziwa hapo sio ile hali ya kulala na kuota ndoto…hapana bali ni maono yao, yaani ndoto zao za jinsi watakavyokuwa baadaye, namna wanavyojiona baadaye..sasa hiyo namna ndio sio nzuri bali ni ya kujitia mwili uchafu.

Kuutia mwili uchafu ni nini?

Kuutia mwili uchafu ni ile hali ya kuruhusu matendo yote ya mwilini kukutawala…matendo hayo yanazunguziwa vema katika Wagalatia 5:19-21

[19]Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, 

[20]ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, 

[21]husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu. 

Haya ndio watu wanayoyaona mbele yao, wanayoyawaza na kuyatazamia wakati wote, wanayoyaota yaje kutokea..

Fikra za watu wengi leo ni ili baadaye waishi kiasherati, wafanye anasa kwa pombe, ulafi, waibe..

Hii ni kutufunulia pia kunajisika sio mpaka mtu akatende jambo lenyewe bali ile kulitamania, tu au kulitarajia mbeleni…tayari ameshajinajisi.

Jiulize kuota kwako ni kupi? Kama mtoto wa Mungu, lazima tujue sisi yatupasa kuota maendeleo ya kazi ya Mungu, kuota ukuaji wa kiroho, kuota upendo, kuota kuingia mbingu mpya na nchi mpya,..namna hiyo humfanya mtu kuendelea katika utakaso.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Yuda alimaanisha nini kusema “wokovu ambao ni wetu sisi sote”

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 13 (Kitabu cha Hosea).

Print this post

SHIKA JEMBE NA SURURU CHIMBA MAHANDAKI. 

2 Wafalme 3:16-17

[16]Akasema, BWANA asema hivi, Fanyeni bonde hili lijae mahandaki. 

[17]Kwa kuwa BWANA asema hivi, Hamutauona upepo, wala hamtaiona mvua, ila bonde hilo litajaa maji; nanyi mtakunywa, ninyi, na ng’ombe zenu, na wanyama wenu. 

Ilifika wakati wana wa Israeli, walikwama, baada ya kuona wapo katika eneo ambalo ni kame kupita kiasi, na hawana msaada, nguvu zimewaishia maadui zao wapo karibu kuwaangamiza..

Wakalia sana, Lakini baadaye wakapata akili ya kumlingana Mungu kwa kuulizia kupitia nabii wake Elisha. Lakini maagizo waliyopewa hayakuwa bado marahisi sana, kama walivyotegemea.

Hawakufanyiwa muujiza wa maji kutokea mwambani kama kipindi cha Musa, au mvua kushuka mbinguni…bali waliambiwa wachimbe mahandaki…yaani mashimo makubwa sana…pale jangwani..

Fikiri umechoka umeishiwa nguvu, halafu unaambiwa uchimbe mashimo..upige sururu chini, upige jembe chini, utoe jasho la kutosha si jambo jepesi..

Lakini baadaye tunaona Mungu anawaambia hamtaona mvua bali hayo mabonde yote yatajaa maji. Na ndivyo ilivyokuwa. Kwa waliochimba sana walipata maji sana, kwa waliochimba kidogo walipokea maji sawasawa na mashimo yao.

Je nini Bwana alikuwa analifundisha kanisa lake.

Katikati ya jangwa, Si muda wa kulia na kusumbuka, kinyume chake shika jembe lako, chepe lako anza kuchimba mashimo.

Kwanini watu wengi hawaioni mvua ya Mungu ya neema au baraka za rohoni zikidumu kwao lakini kwa wengine hudumu…sio kwamba Mungu anaupendeleo…hapana…bali wale wengine tayari wameshachimba mashimo marefu ya kuhifadhi maji mengi…Kwasababu mvua au umande wa Mungu sikuzote hushuka au hupanda juu ya nchi yote lakini wale wenye visima ndio hudumu na maji yake mda mrefu kwa wengine hudumu tu kwa muda mfupi pale juu, baadaye kidogo hupotelea ardhini…

Kuchimba handaki ni kudumu sana katika maombi, pamoja na kutendea kazi kile ulichokitaka kwa Mungu…

Kwa mfano unamwomba Mungu akupe mke/mume mwema, labda leo huoni kutokea kwa yoyote upo jangwani tu, unakaribia kukata tamaa…hakikisha unazidisha sana maombi, lakini pia unajitunza na kuanza kujifunza mafunzo ya kuwa mke/mume mwema, unaonyesha kivitendo zile sifa za mke mwema/mume mwema anazopaswa awe nazo kibiblia, kwamfano wewe ni mwanamume unafahamu kuwa yapo majukumu ya kibaba mbele yako, kwamba unapaswa uwajibike kwa kipato cha familia yako, lakini hilo kama hulisumbukii na bado unatarajia Bwana akuletee mke..ni kweli atakuletea, atapandisha umande wa maji juu ya nchi lakini hatimaye atashindwa kudumu na wewe katika hatua za awali akiona huwezi kusimama kwenye wajibu wako…baadaye utalalamika mbona wanawake wananikimbia..vilevile mwanamke akikosa tabia njema..wanaume watakuja na kumkimbia baadaye…kwasababu hakuwa na muda wa kujichimbia mahandaki yake, kitabia.

Kila eneo liwe la kihuduma, kikazi, kiafya..wekeza sana kwenye mahandaki kwasababu mvua/ umande utakuja tu…kwasababu kwa Mungu kushusha baraka si jambo la kulisumbukia sana, yeye anawanyeshea mvua waovu na wema alisema hivyo (Mathayo 5:45) bali kuzihifadhi hizo baraka ndio ugumu ulipo.

Mwanzo 2:6

[6]ukungu ukapanda katika nchi, ukatia maji juu ya uso wote wa ardhi. 

 

Wekeza kwenye maombi na kutendea kazi imani yako kwa vitendo. Zaidi ya kutarajia tu Mungu atende mwenyewe.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

 

Print this post

Huduma ya kuendelea kuwa mwaminifu pale wachache wanapokusikiliza.

Huu ni mfululizo wa masomo yawahusuyo watumishi wa Mungu. 

Kuna makosa mengi yapo miongoni mwa mitazamo yetu sisi (watumishi wa Mungu), tunadhani mafanikio ni pale hasaa huduma yetu inaposhawishi mioyo ya wengi …pale tunapoona umati unaipokea, na kuishangilia.

Lakini tukifuatilia huduma za manabii wengi wa Mungu, kwenye biblia kama vile Isaya na Ezekieli, Yeremia hawakuwa na mafanikio makubwa ya mahubiri yao, kama tunavyodhani hivi leo, kinyume chake waliishia kukataliwa, kuteswa na kuuliwa, kwa ufupi huduma zao ziliwavunja sana moyo,  lakini kwasababu aliyewatuma ni Bwana,  injili yao imesimama vizazi na vizazi mpaka leo..

Walijua wanakwenda kuhubiri kwa watu ambao wana mioyo migumu sana…na Mungu aliwaeleza kabisa, lakini walifanya hivyo kwa uaminifu wote, kana kwamba wanauokoa umati wa watu.

Yeremia 7:27

[27]Nawe utawaambia maneno hayo yote; lakini hawatakusikiliza, nawe utawaita; lakini hawatakuitikia. 

Ezekieli 2:3-7

[3]Akaniambia, Mwanadamu, nakutuma kwa wana wa Israeli, kwa mataifa wanaoasi, walioniasi mimi; wao na baba zao wamekosa juu yangu, naam, hata hivi leo. 

[4]Na wana hao wana nyuso zisizo na haya, na mioyo yao ni migumu. Mimi nakutuma kwa hao; nawe utawaambia, Bwana MUNGU asema hivi. 

[5]Nao, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia, (maana ndio nyumba ya kuasi hao), hata hivyo watajua ya kuwa nabii amekuwako miongoni mwao. 

[6]Na wewe, mwanadamu, usiwaogope hao, wala usiyaogope maneno yao, ijapokuwa miiba na michongoma i pamoja nawe, nawe unakaa katikati ya nge; usiyaogope maneno yao, wala usifadhaike kwa sababu ya nyuso zao, wajapokuwa ni nyumba yenye kuasi. 

[7]Nawe utawaambia maneno yangu, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia; maana hao wanaasi sana. 

Hakuna jambo linaloumiza kwa mtumishi wa Mungu pale unapoona unahubiria jamii kubwa ya watu lakini matokeo yoyote huoni kwao,…Ni vema ufahamu kuwa Mungu hakutumi ukawe mshawishi, anakutuma ukawe mwaminifu kwa kazi yake.

Kushindwa kwako katika huduma sio, kukosa watu wa kukusikiliza au watu kupungua kwenye huduma yako, kushindwa kwako ni kukosa uaminifu..hilo tu.

Leo hii ungewekwa kwenye nafasi ya Nuhu ambaye aliuhubiria ulimwengu kwa miaka mia moja na ishirini, na kuambulia tu familia yake, ungeshamkimbia Mungu siku nyingi na kusema sijatumwa, ungewekwa kwenye nafasi ya Yeremia, Mika, sefania ungesema huyu si Mungu, ni akili zangu zimenituma, ungesema ninachofanya ni uwendawazimu…hii sio huduma lazima kuna shida mahali, haiwezekani watu hawataki kugeuka, na kutubu, ungewekwa nafasi ya Musa ungesema hawa nilionao  sio watu wa Mungu ni kizazi cha nyoka, pamoja na ishara zote na miujiza…lakini bado wanatengeneza ndama wa shaba, wanaasi, wananung’unika…najitaabisha bure tu.

Kama mtumishi wa Mungu jitahidi sana kuwa mwaminifu, hata kama huoni ukuaji wowote, au mafanikio yoyote ya machoni, ya kuokoka kwa watu wengi…wewe ifanye kazi yake, mtumikie yeye, timiza ratiba zako. mtumikie Mungu kwa mtazamo huo wa uaminifu na sio wa matokeo, utadumu na hutapindishwa na chochote.

Kwani thawabu yako ni kubwa mbinguni. 

Mungu akubariki sana.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MHESHIMU MCHUNGAJI WAKO.

SIKU ZA WATUMISHI WA MUNGU.

KARAMA TUZIPATAZO KWA MSAADA WA WATU WENGI.

Print this post

AU NATAKA KUWAPENDEZA WANADAMU?

Wagalatia 1:10

[10]Maana, sasa je! Ni wanadamu ninaowashawishi, au Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa hata sasa nawapendeza wanadamu, singekuwa mtumwa wa Kristo.

Kuna dhambi moja ya kale, ambayo imekuwa sugu sana, na kibaya zaidi imekuwa tishio kubwa kwa mwanadamu, hata kumfanya ashindwe kabisa kuyatenda mapenzi ya Mungu, haijalishi atamaanisha kiasi gani, dhambi yenyewe si zile tunazozifahamu, kama vile uzinzi, uongo, n.k., Hapana bali ni dhambi ya “kuwapendezesha wanadamu”

Ni dhambi ya kufanya jambo kwa hofu ya kuchukiwa na watu, kufikiriwa vibaya na watu. Hofu ya Kutengwa na watu, kudharauliwa na watu.

Ni kufanya jambo machoni pa watu ili utukuzwe, uonekane mkuu, uonekane ni wa rohoni, uonekane unajua kuliko wengine… ni kuwa radhi kuvumiliana na vilivyo kinyume na Mungu ilimradi tu mbele za watu, usipoteze heshima yako.

Bwana Yesu alijua moyo wa mwanadamu unafurahia hali hii, upo radhi kufanya vitu kinafki, bila kujali haja ya Mungu ni nini.

Mathayo 6:2,5

[2]Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu…

[5]Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao.

Ni hali mbaya sana, Mahali  pengine waliogopa kumkiri hadharani kwasababu watapoteza heshima zao za kikuhani machoni pa watu..

Yohana 12:42-43

[42]Walakini hata katika wakuu walikuwamo wengi waliomwamini; lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakumkiri, wasije wakatengwa na sinagogi.

Madhara ya dhambii hii ni kwamba, Tunaweza tukayapindisha maandiko tusiongee ukweli wote, tuhubiri injili ya juu juu, injili ya vichekesho, tusikemee aina Fulani ya dhambi kwasababu zitawafanya watu wainamishe vichwa vyao, matokeo yake wasije kanisani.

Hali hii inatufanya tuwe na kigeugeu, ilimvaa hata Petro, wakati ule alipoketi na wayahudi, anasema hivi, alipokutana na Watu wa mataifa anasema vingine kwa hofu ya wayahudi, mpaka Paulo alipomwona akamkemea mbele ya wote. (Wagalatia 2:11)

Tunaogopa kuvaa mavazi ya kujisitiri yasiyokuwa na mvuto machoni pa watu, lakini mbele za Mungu yanapendeza, kisa tutaonekana washamba, wazee. Nuru yetu inashindwa kuangaza ulimwenguni.

Ijapokuwa Bwana Yesu aliwapenda sana wanadamu, lakini hakuishi kwa kuziangalia hisia zao zinasemaje, kwasababu sifa za wanadamu, hazitabiriki, leo watakusifia, kesho watakuchukia.. Alipoingia Yerusalemu walimwita mbarikiwa Hosana, wiki moja baadaye wakasema Asulubiwe.. Lakini katika nyakati zote hizi hatuoni Bwana Yesu akigeuka, akipindisha pindisha msimamo wake, alipotukanwa, hakutazama umati unasemaje, aliutazama utukufu wa Mungu unamwelekezaje.

Hii huitwa hofu ya mwanadamu, Tunasahau kuishi kwa hofu ya Mungu, yaani Mungu anasemaje, Anajisikiaje, tunawaza sana wanadamu wanasemaje, wanafikirije..Hatupaswi kuwafanya watu sanamu zetu.

Ili tushinde hii hali kwanza ni lazima tujue kuwa kumpendezesha kila mtu ni jambo ambalo haliwezekani, hivyo usiogope kufikiriwa kivingine pale unapokusudia kuishi maisha yampendezayo Mungu.

Lakini pia ni lazima ufahamu, wanadamu hawana sifa za kweli, za kudumu, hivyo acha kufanya vitu, kuwaridhisha, ilihali unajua wewe mwenyewe unaumia ndani kwa ndani, na mwisho jitahidi kufanya mambo yako kwa msukumo wako mwenyewe sirini, bila watu kukutazama, hapo utaua sifa za wanadamu, utaanza kuishi kwa kumwangalia Mungu.

Wagalatia 1:10

[10]Maana, sasa je! Ni wanadamu ninaowashawishi, au Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa hata sasa nawapendeza wanadamu, singekuwa mtumwa wa Kristo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MWONGOZO WA MAOMBI YA WAHUDUMU/ WASIMAMAO MADHABAHUNI.

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

USIONDOE ALAMA YA MPAKA ILIYOWEKWA NA MABABA.

Print this post

KUWEKA MAMBO MOYONI, NI TABIA YA MARIAMU.

Huu ni mfululizo wa masomo maalumu ya wanawake, ikiwa utapenda kupata madarasa mengine mengi ya nyuma wasiliana nasi kwa namba zilizo chini ya somo hili.

Mariam ni mwanamke ambaye Mungu alimchagua kipekee kuwa mfano bora wa kuigwa wa namna wanawake wa kikristo wanavyopaswa kuwa.

Mariamu alijitunza usichana wake, lakini pia sifa nyingine kubwa aliyokuwa nayo, hakuwa mtu wa kuwaza ki-akili bali aliwaza kwa moyo. Kila jambo lililomfikia halikuishia akilini tu, kwamba ni hoja nzuri tu, au kwamba inaingia akilini, hapana bali alijifunza kulishusha mpaka moyoni, kulitafakari …Na hilo lilimsaidia sana kuwa mwanamke bora…

Embu tafakari haya matukio machache, mwitikio wake ulivyokuwa;

Luka 1:28-29

[28]Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe. 

[29]Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani? 

Luka 2:17-19

[17]Walipomwona wakatoa habari waliyoambiwa juu ya huyo mtoto. 

[18]Wote waliosikia wakastaajabu kwa hayo waliyoambiwa na wachungaji. 

[19]Lakini Mariamu akayaweka maneno hayo yote, akiyafikiri moyoni mwake. 

Luka 2:48-51

[48]Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni. 

[49]Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu? 

[50]Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia. 

[51]Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake. 

Hiyo ni kuonyesha ilikuwa ni desturi ya maisha yake, kufikiri kutoka kilindi cha moyoni mwake sio kwa akili zake…

Wazia zaidi, Mariamu aliposalimiwa alijiuliza salama hii, lengo lake ni nini? nyuma ya salamu kuna lengo gani, Mwisho wake ni upi.. hakupokea salamu, ilimradi salamu kisa inamtakia mema…aliivunja vunja kwanza..Na huko ndio kuwaza kwa moyo.

Mabinti wengi leo hii wanaingia kwenye mitego ya kulaghaiwa kwa kutowaza kutoka moyoni..hujiulizi iweje mtu usiyemjua aje kukupa tu salamu ya zawadi, akusifie, na wewe hufikiri salamu hii ni ya namna gani…

Hujiulizi huyu mtu nia yake ni nini? Anatarajia nini kwangu, kumbuka salamu sio lazima tu ije kwa maneno, yaweza kuja kwa kupewa lifti, kupewa nafasi ya upendeleo, kulipiwa manunuzi fulani, dada kuwa makini na salamu hizo, hata kama umeolewa kuwa makini sana. Ni kweli si zote ni mbaya lakini jiulize maudhui yake ni nini? Waza moyoni mwako, Nia ni nini?.

Kama mama yetu Hawa pale bustanini angejiuliza salamu za nyoka ni za namna gani, sote tusingekuwa kwenye matatizo tuliyonayo sasa.

Halikadhalika Mariamu, hakuyaacha maneno yenye jumbe za Mungu yampite hivi hivi, mahali ambapo hajaelewa alihifadhi ndani yake akitumai upo wakati ataelewa vema kwa jinsi anavyozidi kutafakari…alihifadhi matukio yake yote moyoni..

Lakini wanawake wengi wa leo, wanahifadhi maneno yasiyo na maana, utaona moyoni mwao yamejaa maneno waliyosengenywa, waliyoaabishwa, waliodhalilishwa..hayo ndio yanawaganda lakini si maneno ya Mungu..

Wanatumia vibaya nafasi hizo, Na matokeo yake kinachotoka nje ya mioyo yao ni wivu, uchungu, hasira, chuki, masengenyo, badala ya mafunuo, upendo, hekima, na adabu.

Tumia moyo wako kwa lengo la kupambanua na kuhifadhi mambo mema…sio maovu.

Ifike wakati, unasema…lile hubiri lililohubiriwa mwaka juzi mpaka leo linanitafakarisha, lile ono Mungu alilonionyesha utotoni linanirudia rudia akilini, yale maonyo ya mhubiri tuliyokemewa kipindi kile yanazunguka ndani yangu hata sasa siwezi yasahau…

Hayo ndio mambo ya kubeba..

Geuka fikiri kama Mariamu.. 

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAOMBI MAALUMU YA WA-WAMAMA / WANAWAKE WA KANISANI.

MAPAMBO YA WANAWAKE WALIOUKIRI UCHAJI WA MUNGU.

MASOMO MAALUMU KWA WANAWAKE.

Print this post

Maana yeye ampaye salamu azishiriki kazi zake mbovu. 

2 Yohana 1:10-11

[10]Mtu akija kwenu, naye haleti mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani mwenu, wala msimpe salamu. 

[11]Maana yeye ampaye salamu azishiriki kazi zake mbovu. 

 Ni salamu ya namna gani ambayo ililengwa hapo?

JIBU: Ukisoma habari yote tokea juu utaona mtume Yohana anazungumzia kundi la wadanganyifu ambao walitokea wengi duniani wakati ule, ni kundi la watu waliopinga kuja kwa Yesu katika mwili kwa namna ya kibinadamu, akasema hao ndio wapinga Kristo.

 Na mbeleni akatoa katazo la kutowakaribisha hata majumbani kwao, wala kuwapa salamu, maana kuwapa salamu ni kushiriki kazi zao mbovu.

Swali je ni salamu ya namna gani ililengwa hapo.?

Salamu zinazozungumziwa hapo si salamu hizi za kijamii za “umeamkaje, au shikamoo, au za mchana” hapana bali ni salamu za kiroho ambazo hata wakati ule wayahudi walipozisema zilimaanisha ushirika mmoja katika kiimani. Kwamfano, walipokutana walibusiana na kusema “Amani ya Bwana iwe pamoja nawe”..

Sasa salamu kama hiyo utajiuliza ni bwana yupi ikiwa huyo mwingine haamini katika fundisho kama lenu.. ukimsalimia basi unakubaliana na bwana wake ambaye hajaja katika mwili. Tayari umeshazishiriki kazi zake.

Ni sawa na leo labda tuseme unakutana na watu wanaomwamini kweli Yesu, lakini Yesu ambaye hajafufuka, yupo kaburini mpaka sasa, halafu anakuja anakusalimia “Bwana Yesu asifiwe” na wewe unasema Amina..Mtu mgeni akipita akakusikia atajua kuwa mna imani moja kuhusu Yesu Kristo ambaye hajafufuka.

Hivyo hata kwa wakati huu, salamu zetu za kiroho zisimame mahali ambapo tunajua imani tulio nayo kuhusu Kristo ni moja.

Kwasababu salamu tu, hutangaza, zina nguvu kama lilivyo fundisho. 

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ANDALIZI LA MWISHO LA UJIO WA MPINGA KRISTO.

JAWA SANA MOTO ULAO.

Print this post

USIYAKUBALI MARADHI YA MISRI

Jina la Bwana wetu YESU KRISTO libarikiwe, karibu katika kujifunza Biblia.

Upo usemi usemao “wanadamu tumeumbiwa maradhi”..Usemi huu ni wa hekima za ulimwengu, ambao Biblia inasema ni upuuzi mbele za Mungu (1Wakorintho 3:19).

Ni kweli maradhi yapo lakini hatupaswi kuyakiri na kuyakumbutia kama sehemu yetu, (ikiwa tumeshampokea YESU) ….hata kama yapo ndani yako si sahihi kusema “hayo ni ya kwako” au “umeumbiwa”, ni kauli ambayo ni hatari sana.

Kwanini Maradhi si sehemu yetu tuliomwamini YESU? Na kwanini hatupaswi kutawaliwa nayo?.

Hebu tujifunze kidogo historia ya Maradhi mabaya na hatari kibiblia.

Kipindi wana wa Israeli wanatoka MISRI, kuelekea nchi ya Ahadi, Kanaani, Mungu aliwaambia yale maradhi yaliyokuwa yanawapata MISRI hayatawafuata Kaanani..

Kumbukumbu 7:15 “Na Bwana atakuondolea ugonjwa wote; wala hatatia juu yako MARADHI YO YOTE MABAYA UYAJUAYO YA MISRI, lakini atayaweka juu ya wote wakuchukiao”.

Maana yake ni kwamba wakiwa Misri pamoja na kwamba walikuwa katika utumwa wa mwilini lakini pia Misri ILITAWALIWA NA MAGONJWA YA KUTISHA (Soma Kutoka 15:26 na Kumbukumbu 28:60).

Misri haikuwa sehemu salama kiroho na hata kimwili, kulikuwa kuna mlipuko wa magonjwa ya ajabu na ya kutisha, ambayo hayo yalitokana na miungu wa Misri waliyokuwa wakiiabudu..Na Bwana aliwaonya wana wa Israeli kwamba wakirudi kuitumikia hiyo miungu basi yale maradhi ya MISRI yatavuka kuwafuata waendako.

Kumbukumbu 28:60  “Naye atakurejezea maradhi yote ya Misri juu yako uliyokuwa ukiyaogopa, nayo yataambatana nawe.

61 Tena kila ugonjwa, na kila pigo yasiyoandikwa katika kitabu cha torati hii, atakutia nayo Bwana juu yako, hata utakapokwisha kuangamizwa”.

Kwahiyo tunachoweza kuona ni kuwa “Magonjwa yote asili yake ni Misri”, na Mungu aliyaweka kwa waMisri kutokana na maisha yao ya kuabudu miungu (shetani)..

Sasa swali kwanini yatutawale sisi ambao hatuabudu miungu ya Misri, na wala hatupo Misri, vile vile kama yanavyowatawala waMisri (watu ambao hawamjui Mungu)?

Ni swali la kutafakari sana..

Ukiona kuna ugonjwa unakusumbua miaka mingi, na umejaribu kutumia matibabu ya hospitalini yaliyo halali lakini tatizo linabaki kuwa sugu, au linakwenda baada ya muda linarudi..hebu wakati wa leo simama na kusema “imetosha”.

Huenda hujajua tu haki yako ndio maana ibilisi anakutesa na kukusumbua…anakujengea saikolojia kwamba huo ugonjwa ni wa kwako na huwezi kupona.. Leo hii simama na kusema “Magonjwa ya Misri si sehemu yangu”.

Kama umeokoka kweli kweli, usikae ukiri kwa kinywa chako, au uamini moyoni mwako kuwa “magonjwa ni sehemu yako”.. anza kuanzia leo kufuta kalenda za kwenda hospitali hospitali kila mara.

Tatizo linalowakabili watu wengi waliookoka ni kuamini na kujiwekea matumaini katika madawa na mahospitali, sio vibaya kuamini hivyo, lakini kunadumaza imani yako kwa MUNGU na kuyapa nafasi magonjwa ya Misri juu yako.

Si kila dalili tu ya mafua unayoyasikia unakimbilia dawa!..si kila homa tu inayokupata unakimbilia hospitalini utaacha lini hiyo tabia?.. Hufanyi dhambi lakini unadumaza imani yako.

Jenga tabia ya kuamini kuwa ninaweza kuwa na afya na uzima bila ya madawa wala hospitali, kwasababu wewe sio Mmisri, kwahiyo Maradhi ya Misri hayakuhusu, wala taarifa za maradhi ya Misri si sehemu yako.

Afya yako ni ya muhimu sana, ukiwa na maradhi hata uwezo wako wa kiutendaji kiroho unakuwa hafifu, hivyo usikubali hata kidogo, maandiko yanatufundisha hivyo kwamba ni mapenzi ya Mungu tuwe na afya zetu..

3Yohana 1:2 “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo”

Ikiwa una maradhi yanayokuonea leo kwa imani fuatisha maneno yafuatayo na yatakuacha haraka sana..

Sema “Bwana YESU ninasogea mbele zako, ninaomba unisamehe nilipofungua mlango wa maradhi katika maisha yangu, lakini pia naomba unisamehe nilipopungukiwa imani, siku leo ninakiri uzima na afya, ninayakataa maradhi yote ya Misri juu ya mwili wangu, kwakuwa mimi sio Mmisri, kuanzia leo mimi ni mzima na wala sitasumbuka tena, ninaomba na kuamini katika jina kuu lako Bwana YESU KRISTO. Amen”

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya kuinuliwa juu ya nchi? (Yohana 12:32).

JINSI MATENDO YA IMANI YANAVYOWEZA KULETA UTAMBULISHO MPYA KWA MTU.

UTAIKUZAJE IMANI NDANI YAKO?

Je ni kweli imani ya mtu ndiyo itakayomuokoa, na si kitu kingine?

Je! Imani ya mitume ipo katika maandiko?

Print this post