Wagalatia 1:10
[10]Maana, sasa je! Ni wanadamu ninaowashawishi, au Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa hata sasa nawapendeza wanadamu, singekuwa mtumwa wa Kristo.
Kuna dhambi moja ya kale, ambayo imekuwa sugu sana, na kibaya zaidi imekuwa tishio kubwa kwa mwanadamu, hata kumfanya ashindwe kabisa kuyatenda mapenzi ya Mungu, haijalishi atamaanisha kiasi gani, dhambi yenyewe si zile tunazozifahamu, kama vile uzinzi, uongo, n.k., Hapana bali ni dhambi ya “kuwapendezesha wanadamu”
Ni dhambi ya kufanya jambo kwa hofu ya kuchikiwa na watu, kufikiriwa vibaya na watu. Hofu ya Kutengwa na watu, kudharauliwa na watu.
Ni kufanya jambo ili machoni pa watu ili utukuzwe, uonekane mkuu, uonekane ni wa rohoni, uonekane unajua kuliko wengine… ni kuwa radhi kuvumiliana na vilivyo kinyume na Mungu ilimradi tu mbele za watu, usipoteze heshima yako.
Bwana Yesu alijua moyo wa mwanadamu unafurahia hali hii, upo radhi kufanya vitu kinafki, bila kujali haja ya Mungu ni nini.
Mathayo 6:2,5
[2]Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu… [5]Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao.
[2]Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu…
[5]Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao.
Ni hali mbaya sana, Mahali pengine waliogopa kumkiri hadharani kwasababu watapoteza heshima zao za kikuhani machoni pa watu..
Yohana 12:42-43
[42]Walakini hata katika wakuu walikuwamo wengi waliomwamini; lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakumkiri, wasije wakatengwa na sinagogi.
Madhara ya dhambii hii ni kwamba, Tunaweza tukayapindisha maandiko tusiongee ukweli wote, tuhubiri injili ya juu juu, injili ya vichekesho, tusikemee aina Fulani ya dhambi kwasababu zitawafanya watu wainamishe vichwa vyao, matokeo yake wasije kabisani.
Hali hii inatufanya tuwe na kigeugeu, ilimvaa hata Petro, wakati ule alipoketi na wayahudi, anasema hivi, alipokutana wa Watu wa mataifa anasema vingine kwa hofu ya wayahudi, mpaka Paulo alipomwona akamkemea mbele ya wote. (Wagalatia 2:11)
Tunaogopa kuvaa mavazi ya kujisitiri yasiyokuwa na mvuto machoni pa watu, lakini mbele za Mungu yanapendeza, kisa tutaonekana washamba, wazee. Nuru yetu inashindwa kuangaza ulimwenguni.
Ijapokuwa Bwana Yesu aliwapenda sana wanadamu, lakini hakuishi kwa kuziangalia hisia zao zinasemaje, kwasababu sifa za wanadamu, hazitabiriki, leo watakusifia, kesho watakuchukia.. Alipoingia Yerusalemu walimwita mbarikiwa Hosana, wiki moja baadaye wakasema Asulubiwe.. Lakini katika nyakati zote hizi hatuoni Bwana Yesu akigeuka, akipindisha pindisha msimamo wake, alipotukwana, hakutazama umati unasemaje, aliutazama utukufu wa Mungu unamwelekezaje.
Hii huitwa hofu ya mwanadamu, Tunasahau kuishi kwa hofu ya Mungu, yaani Mungu anasemaje, Anajisikiaje, tunawaza sana wanadamu wanasemaje, wanafikirije..Hatupaswi kuwafanya watu sanamu zetu.
Ili tushinde hii hali kwanza ni lazima tujue kuwa kumpendezesha kila mtu ni jambo ambalo haliwezekani, hivyo usiogope kufikiriwa kivingine pale unapokusudia kuishi maisha yampendezayo Mungu.
Lakini pia ni lazima ufahamu, wanadamu hawana sifa za kweli, za kudumu, hivyo acha kufanya vitu, kuwaridhisha, ilihali unajua wewe mwenyewe unaumia ndani kwa ndani, na mwisho jitahidi kufanya mambo yako kwa msukumo wako mwenyewe sirini, bila watu kukutazama, hapo utaua sifa za wanadamu, utaanza kuishi kwa kumwangalia Mungu.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Mafundisho mengine:
MWONGOZO WA MAOMBI YA WAHUDUMU/ WASIMAMAO MADHABAHUNI.
Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)
USIONDOE ALAMA YA MPAKA ILIYOWEKWA NA MABABA.
Print this post
Huu ni mfululizo wa masomo maalumu ya wanawake, ikiwa utapenda kupata madarasa mengine mengi ya nyuma wasiliana nasi kwa namba zilizo chini ya somo hili.
Mariam ni mwanamke ambaye Mungu alimchagua kipekee kuwa mfano bora wa kuigwa wa namna wanawake wa kikristo wanavyopaswa kuwa.
Mariamu alijitunza usichana wake, lakini pia sifa nyingi kubwa aliyokuwa nayo, hakuwa mtu wa kawaza ki-akili bali aliwaza kwa moyo. Kila jambo lililomfikia halikuishia akilini tu, kwamba ni hoja nzuri tu, au kwamba inaingia akilini, hapana bali alijifunza kulishusha mpaka moyoni, kulitafakari …Na hilo lilimsaidia sana kuwa mwanamke bora…
Embu tafakari haya matukio machache, mwitikio wake ulivyokuwa;
Luka 1:28-29
[28]Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe. [29]Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani?
[28]Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe.
[29]Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani?
Luka 2:17-19
[17]Walipomwona wakatoa habari waliyoambiwa juu ya huyo mtoto. [18]Wote waliosikia wakastaajabu kwa hayo waliyoambiwa na wachungaji. [19]Lakini Mariamu akayaweka maneno hayo yote, akiyafikiri moyoni mwake.
[17]Walipomwona wakatoa habari waliyoambiwa juu ya huyo mtoto.
[18]Wote waliosikia wakastaajabu kwa hayo waliyoambiwa na wachungaji.
[19]Lakini Mariamu akayaweka maneno hayo yote, akiyafikiri moyoni mwake.
Luka 2:48-51
[48]Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni. [49]Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu? [50]Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia. [51]Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake.
[48]Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni.
[49]Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu?
[50]Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia.
[51]Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake.
Hiyo ni kuonyesha ilikuwa ni desturi ya maisha yake, kufikiri kutoka kilindi mwake sio kwa akili zake…
Wazia zaidi, Mariamu aliposalimiwa alijiuliza salama hii, lengo lake ni nini? nyuma ya salamu kuna lengo gani, Mwisho wake ni upi.. hakupokea salamu, ilimradi salamu kisa inamtakia mema…aliivunja vunja kwanza..Na huko ndio kuwaza kwa moyo.
Mabinti wengi leo hii wanaingia kwenye mitego ya kulaghaiwa kwa kutowaza kutoka moyoni..hujiulizi iweje mtu usiyemjua aje kukupa tu salamu ya zawadi, akusifie, na wewe hufikiri salamu hii ni ya namna gani…
Hujiulizi huyu mtu nia yake ni nini? Anatarajia nini kwangu, kumbuka salamu sio lazima tu ije kwa maneno, yaweza kuja kwa kupewa lifti, kupewa nafasi ya upendeleo, kulipiwa manunuzi fulani, dada kuwa makini na salamu hizo, hata kama umeolewa kuwa makini sana. Ni kweli si zote ni mbaya lakini jiulize maudhui yake ni nini? Waza moyoni mwako, Nia ni nini?.
Kama mama yetu Hawa pale bustanini angejiuliza salamu za nyoka ni za namna gani, sote tusingekuwa kwenye matatizo tuliyonayo sasa.
Halidhalika Mariamu, hakuyaacha maneno yenye jumbe za Mungu yampite hivi hivi, mahali ambapo hajaelewa alihifadhi ndani yake akitumai upo wakati ataelewa vema kwa jinsi anavyozidi kutafakari…alihifadhi matukio yake yote moyoni..
Lakini wanawake wengi wa leo, wanahifadhi maneno yasiyo na maana, utaona moyoni mwao yamejaa maneno waliyosengenywa, waliyoaabishwa, waliodhalilishwa..hayo ndio yanawaganda lakini si maneno ya Mungu..
Wanatumia vibaya nafasi hizo, Na matokeo yake kinachotoka nje ya mioyo yao ni wivu, uchungu, hasira, chuki, masengenyo, badala ya mafunuo, upendo, hekima, na adabu.
Tumia moyo wako kwa lengo la kupambanua na kuhifadhi mambo mema…sio maovu.
Ifike wakati, unasema…lile hubiri lililohubiriwa mwaka juzi mpaka leo linanitafakarisha, lile ono Mungu alilonionyesha utotoni linanirudia rudia akilini, yale maonyo ya mhubiri tuliyokemewa kipindi kile yanazunguka ndani yangu hata sasa siwezi yasahau…
Hayo ndio mambo ya kubeba..
Geuka fikiri kama Mariamu..
Shalom
MAOMBI MAALUMU YA WA-WAMAMA / WANAWAKE WA KANISANI.
MAPAMBO YA WANAWAKE WALIOUKIRI UCHAJI WA MUNGU.
MASOMO MAALUMU KWA WANAWAKE.
2 Yohana 1:10-11
[10]Mtu akija kwenu, naye haleti mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani mwenu, wala msimpe salamu. [11]Maana yeye ampaye salamu azishiriki kazi zake mbovu.
[10]Mtu akija kwenu, naye haleti mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani mwenu, wala msimpe salamu.
[11]Maana yeye ampaye salamu azishiriki kazi zake mbovu.
Ni salamu ya namna gani ambayo ililengwa hapo?
JIBU: Ukisoma habari yote tokea juu utaona mtume Yohana anazungumzia kundi la wadanganyifu ambao walitokea wengi duniani wakati ule, ni kundi la watu waliopinga kuja kwa Yesu katika mwili kwa namna ya kibinadamu, akasema hao ndio wapinga Kristo.
Na mbeleni akatoa katazo la kutowakaribisha hata majumbani kwao, wala kuwapa salamu, maana kuwapa salamu ni kushiriki kazi zao mbovu.
Swali je ni salamu ya namna gani ililengwa hapo.?
Salamu zinazozungumziwa hapo si salamu hizi za kijamii za “umeamkaje, au shikamoo, au za mchana” hapana bali ni salamu za kiroho ambazo hata wakati ule wayahudi walipozisema zilimaanisha ushirika mmoja katika kiimani. Kwamfano, walipokutana walibusiana na kusema “Amani ya Bwana iwe pamoja nawe”..
Sasa salamu kama hiyo utajiuliza ni bwana yupi ikiwa huyo mwingine haamini katika fundisho kama lenu.. ukimsalimia basi unakubaliana na bwana wake ambaye hajaja katika mwili. Tayari umeshazishiriki kazi zake.
Ni sawa na leo labda tuseme unakutana na watu wanaomwamini kweli Yesu, lakini Yesu ambaye hajafufuka, yupo kaburini mpaka sasa, halafu anakuja anakusalimia “Bwana Yesu asifiwe” na wewe unasema Amina..Mtu mgeni akipita akakusikia atajua kuwa mna imani moja kuhusu Yesu Kristo ambaye hajafufuka.
Hivyo hata kwa wakati huu, salamu zetu za kiroho zisimame mahali ambapo tunajua imani tulio nayo kuhusu Kristo ni moja.
Kwasababu salamu tu, hutangaza, zina nguvu kama lilivyo fundisho.
Shalom.
ANDALIZI LA MWISHO LA UJIO WA MPINGA KRISTO.
JAWA SANA MOTO ULAO.
Jina la Bwana wetu YESU KRISTO libarikiwe, karibu katika kujifunza Biblia.
Upo usemi usemao “wanadamu tumeumbiwa maradhi”..Usemi huu ni wa hekima za ulimwengu, ambao Biblia inasema ni upuuzi mbele za Mungu (1Wakorintho 3:19).
Ni kweli maradhi yapo lakini hatupaswi kuyakiri na kuyakumbutia kama sehemu yetu, (ikiwa tumeshampokea YESU) ….hata kama yapo ndani yako si sahihi kusema “hayo ni ya kwako” au “umeumbiwa”, ni kauli ambayo ni hatari sana.
Kwanini Maradhi si sehemu yetu tuliomwamini YESU? Na kwanini hatupaswi kutawaliwa nayo?.
Hebu tujifunze kidogo historia ya Maradhi mabaya na hatari kibiblia.
Kipindi wana wa Israeli wanatoka MISRI, kuelekea nchi ya Ahadi, Kanaani, Mungu aliwaambia yale maradhi yaliyokuwa yanawapata MISRI hayatawafuata Kaanani..
Kumbukumbu 7:15 “Na Bwana atakuondolea ugonjwa wote; wala hatatia juu yako MARADHI YO YOTE MABAYA UYAJUAYO YA MISRI, lakini atayaweka juu ya wote wakuchukiao”.
Maana yake ni kwamba wakiwa Misri pamoja na kwamba walikuwa katika utumwa wa mwilini lakini pia Misri ILITAWALIWA NA MAGONJWA YA KUTISHA (Soma Kutoka 15:26 na Kumbukumbu 28:60).
Misri haikuwa sehemu salama kiroho na hata kimwili, kulikuwa kuna mlipuko wa magonjwa ya ajabu na ya kutisha, ambayo hayo yalitokana na miungu wa Misri waliyokuwa wakiiabudu..Na Bwana aliwaonya wana wa Israeli kwamba wakirudi kuitumikia hiyo miungu basi yale maradhi ya MISRI yatavuka kuwafuata waendako.
Kumbukumbu 28:60 “Naye atakurejezea maradhi yote ya Misri juu yako uliyokuwa ukiyaogopa, nayo yataambatana nawe. 61 Tena kila ugonjwa, na kila pigo yasiyoandikwa katika kitabu cha torati hii, atakutia nayo Bwana juu yako, hata utakapokwisha kuangamizwa”.
Kumbukumbu 28:60 “Naye atakurejezea maradhi yote ya Misri juu yako uliyokuwa ukiyaogopa, nayo yataambatana nawe.
61 Tena kila ugonjwa, na kila pigo yasiyoandikwa katika kitabu cha torati hii, atakutia nayo Bwana juu yako, hata utakapokwisha kuangamizwa”.
Kwahiyo tunachoweza kuona ni kuwa “Magonjwa yote asili yake ni Misri”, na Mungu aliyaweka kwa waMisri kutokana na maisha yao ya kuabudu miungu (shetani)..
Sasa swali kwanini yatutawale sisi ambao hatuabudu miungu ya Misri, na wala hatupo Misri, vile vile kama yanavyowatawala waMisri (watu ambao hawamjui Mungu)?
Ni swali la kutafakari sana..
Ukiona kuna ugonjwa unakusumbua miaka mingi, na umejaribu kutumia matibabu ya hospitalini yaliyo halali lakini tatizo linabaki kuwa sugu, au linakwenda baada ya muda linarudi..hebu wakati wa leo simama na kusema “imetosha”.
Huenda hujajua tu haki yako ndio maana ibilisi anakutesa na kukusumbua…anakujengea saikolojia kwamba huo ugonjwa ni wa kwako na huwezi kupona.. Leo hii simama na kusema “Magonjwa ya Misri si sehemu yangu”.
Kama umeokoka kweli kweli, usikae ukiri kwa kinywa chako, au uamini moyoni mwako kuwa “magonjwa ni sehemu yako”.. anza kuanzia leo kufuta kalenda za kwenda hospitali hospitali kila mara.
Tatizo linalowakabili watu wengi waliookoka ni kuamini na kujiwekea matumaini katika madawa na mahospitali, sio vibaya kuamini hivyo, lakini kunadumaza imani yako kwa MUNGU na kuyapa nafasi magonjwa ya Misri juu yako.
Si kila dalili tu ya mafua unayoyasikia unakimbilia dawa!..si kila homa tu inayokupata unakimbilia hospitalini utaacha lini hiyo tabia?.. Hufanyi dhambi lakini unadumaza imani yako.
Jenga tabia ya kuamini kuwa ninaweza kuwa na afya na uzima bila ya madawa wala hospitali, kwasababu wewe sio Mmisri, kwahiyo Maradhi ya Misri hayakuhusu, wala taarifa za maradhi ya Misri si sehemu yako.
Afya yako ni ya muhimu sana, ukiwa na maradhi hata uwezo wako wa kiutendaji kiroho unakuwa hafifu, hivyo usikubali hata kidogo, maandiko yanatufundisha hivyo kwamba ni mapenzi ya Mungu tuwe na afya zetu..
3Yohana 1:2 “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo”
Ikiwa una maradhi yanayokuonea leo kwa imani fuatisha maneno yafuatayo na yatakuacha haraka sana..
Sema “Bwana YESU ninasogea mbele zako, ninaomba unisamehe nilipofungua mlango wa maradhi katika maisha yangu, lakini pia naomba unisamehe nilipopungukiwa imani, siku leo ninakiri uzima na afya, ninayakataa maradhi yote ya Misri juu ya mwili wangu, kwakuwa mimi sio Mmisri, kuanzia leo mimi ni mzima na wala sitasumbuka tena, ninaomba na kuamini katika jina kuu lako Bwana YESU KRISTO. Amen”
Nini maana ya kuinuliwa juu ya nchi? (Yohana 12:32).
JINSI MATENDO YA IMANI YANAVYOWEZA KULETA UTAMBULISHO MPYA KWA MTU.
UTAIKUZAJE IMANI NDANI YAKO?
Je ni kweli imani ya mtu ndiyo itakayomuokoa, na si kitu kingine?
Je! Imani ya mitume ipo katika maandiko?
WhatsApp
Jina la Bwana YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze maandiko..
shetani hana jipya zaidi ya kunakili (kucopy) vile vilivyopo na kuvutumia kinyume.
Kwamfano kafara za wanyama kama mbuzi na kondoo kwaajili ya utakaso hazikuanzia kwa shetani, bali zilianza kwa MUNGU, ambapo katika Agano la kwanza (yaani Agano la kale) damu za wanyama hao zilitumika kwaajili ya utakaso, lakini sasa Agano jipya hazitumiki tena kwani Damu ya YESU ni bora zaidi ya damu za wanyama.
Kwahiyo shetani anachokifanya ni kunakili kilichokuwa kinatumika zamani (kisicho na matumizi tena) na kukileta siku za mwisho kwaajili ya matumizi yake, ndio maana utaona waganga wa kienyeji na wachawi ndio sadaka zao hizo.
Sasa sio tu hilo, lakini pia katika utumishi, shetani anayo desturi ya kutengeneza nakala..
Kwa namna gani?
Hebu turejee ile habari ya yule mchawi aliyeitwa.. “Bar-YESU” katika Matendo 13?..tuzisome habari zake kidogo kisha tuendelee mbele..
Matendo 13:6 “Walipokwisha kupita katikati ya kisiwa chote mpaka Pafo, wakaona mtu mmoja, mchawi, nabii wa uongo, Myahudi jina lake BAR-YESU; 7 mtu huyu alikuwa pamoja na liwali SERGIO PAULO, mtu mwenye akili. Yeye liwali akawaita Barnaba na Sauli waje kwake, akataka kulisikia neno la Mungu”
Matendo 13:6 “Walipokwisha kupita katikati ya kisiwa chote mpaka Pafo, wakaona mtu mmoja, mchawi, nabii wa uongo, Myahudi jina lake BAR-YESU;
7 mtu huyu alikuwa pamoja na liwali SERGIO PAULO, mtu mwenye akili. Yeye liwali akawaita Barnaba na Sauli waje kwake, akataka kulisikia neno la Mungu”
Huyu “Bar-Yesu” ni nabii wa uongo na ni mchawi, lakini ajabu ni kwamba jina lake limebeba jina la YESU ndani yake.. Je unaelewa maana ya Bar-Yesu?.. maana yake ni “Mwana wa YESU” hiyo ndio tafsiri yake..
Kwahiyo huyu mchawi na nabii wa uongo, alikuwa ni mtu anayemjua YESU na anayedai kufundisha habari za YESU, lakini nyuma yake alikuwa ni mwongo.
Na jambo jingine la ajabu ni kwamba huyu Bar-Yesu alikuwa ni mwalimu wa kiroho wa mtu mmoja aliyeitwa “Sergio-Paulo”… Je unaelewa maana ya Sergio-Paulo?…maana yake ni “Mhudumu-Paulo”..
Kwahiyo wakati YESU wa Mnazareti, anammiliki Paulo mtumishi wa Mungu, yupo mtu anaitwa Bar-YESU anayemmiliki Sergio Paulo.
Kwahiyo hapa kuna “Sergio-Paulo” na “Bar-Yesu” na kuna “Paulo” na “YESU”. Kuonyesha kuwa shetani hana jipya zaidi ya kunakili vile vilivyopo vilivyo halali na kuvigeuza kwa matumizi yake.
Maandiko yanasema hivyo…
2Wakorintho 11:14 “Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru. 15 Basi si neno kubwa watumishi wake NAO WAKIJIGEUZA WAWE MFANO WA WATUMISHI WA HAKI, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao”.
2Wakorintho 11:14 “Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.
15 Basi si neno kubwa watumishi wake NAO WAKIJIGEUZA WAWE MFANO WA WATUMISHI WA HAKI, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao”.
Kwahiyo si kila anaitwa mtumishi wa YESU ni mtumishi kweli wa YESU, vile vile si kila anayejiita ni Mkristo, ni Mkristo kweli kweli, ni muhimu kuwa macho sana, na kujua vipimo halisi vya kuwatambua manabii wa uongo, waalimu wa uongo, wachungaji wa uongo, waimbaji wa uongo pamoja na wakristo wa uongo.
Na kipimo hiko si kingine zaidi ya NENO LA MUNGU, baada ya kujaa Roho Mtakatifu, Neno la MUNGU pekee ndio kipimo cha kumjua huyu ni wa MUNGU au wa ibilsi, hii ni sauti ya Mungu au ya ibilisi.
Je umeokoka?.. unao uhakika wa kwenda mbinguni ikitokea parapanda imelia leo?
Kama bado haujampa YESU maisha yako, bado parapanda haijalia leo, lakini muda wowote mambo yanabadilika, hivyo fanya mabadiliko kabla ya mabadiliko makuu kutokea.
JIHADHARI NA ROHO YA YEZEBELI.
Roho ya Malipizi/ roho za malipizi ni nini?
MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.
MKUU WA UZIMA AKUWEKE HURU.
UNAMALIZAJE MWAKA WAKO, JE NA MUNGU AU SHETANI?
Mfundishe mtoto namna ya kutumia jina la Yesu katika kutenda mambo yake yote.
Kuishi ni tufoauti na kuwa na uhai. Hata mti ni hai, lakini hauishi. Kuishi ni maisha, yaani unasifa ya kuwa na mfumo au ustaarabu Fulani ambao unatembea nao, unaweza kuchagua mahali pa kukaa, unafanya kazi, unapumzika, unajenga, unapanda, unajichagulia burudani mfano miziki, michezo, vyakula, unafanya ibada, unauza, unanunua.. mambo kama hayo kiumbe kikitenda tunasema kinaishi.
Lakini kuwa kifungoni, ndani ya gereza huoni jua wala mwezi siku zako zote uwapo duniani, hatuwezi kusema unaishi, tunasema wewe upo hai, lakini hauishi.. Au unapokaa kwenye kitanda cha wagonjwa mauti-uti, umepooza, huwezi kuongea wala kutembea, umekata kauli, kwa sikuzote uwapo duniani, hayo si maisha ijapokuwa upo hai.
Sasa kuna maneno Yesu aliyasema, ambayo si wengi hujaelewa kwa undani na upana.. Tusome;
Yohana 11:25-26
25 Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi; 26 naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo?
Hii kauli ukiisoma vizuri, unaweza ukasema inajichanganya, Embu tafakari, jambo la kwanza Yesu anasema, tukimwamini tukifa tutakuwa tunaishi, lakini pia tukiwa hai na kuamini hatutakufa kabisa hata milele.
Je! Sisi tuliomwamini hatufi?
Jibu ni Ndio hatufi kabisa, bali tunahamishwa makao. Hicho kinachoitwa kifo, ni macho ya wanadamu yanaona hivyo, lakini sisi tunakuwa kama tumefumba macho, kisha tukafumbua na kujikuta katika ulimwengu mwingine kabisa, Ndio maana lugha ambayo hutumika kueleza hali hiyo kwa watakatifu ni kulala (Matendo 7:54-60, 1Kor 15:51-58, Yohana 11:11-19)
Sisi tuliomwamini Yesu hatutaona kitu kinachoitwa kaburi, wala hatutajikuta kwenye gereza Fulani , bali kwenye ulimwengu mwingine mzuri sana uitwao pepo, sio tukiwa hai, bali tukiwa tunaishi kabisa huru.
Maana yake, tunaendeleza maisha, ikiwa kuna kutembea, huku na huko au kushughulika kwa vitu vya kimbingu, kufanya hivi, kufanya vile..Tutakuwa tunayafanya. Hayo ndio maisha anayosema mtu akimwamini yeye, ajapokufa (lala), atakuwa anaishi.. Si atakuwa na uhai
Tutakaa huko pepo, kwa kipindi chote, ambacho tunamsubiria Yesu, kulikamilisha kusudi la watakatifu wote, kisha baadaye,(mwisho ukifika), atakuja mwenyewe kuwachukua walio hai Pamoja na miili yetu tuliyoiacha duniani, na sote kwa Pamoja tutaanza ziara mpya ya kuelekea mbingu ya tatu. Makao yetu ya milele yalipo (2Wakorintho 12:2-4)
Lakini waovu wanapokufa, wenyewe watajiona kwanza wakiingia makaburini, kisha wakishuka kuzimu, Uhai wao ukitunzwa kwenye vifungo vya giza wasijue chochote, wala wasitende kazi yoyote, mpaka siku ya hukumu itakapofika, ambapo watatolewa huko kisha watasimama kwenye kiti cha enzi cheupe cha mwana-kondoo kwa ajili ya hukumu, (Ufunuo 20) baada ya kuhukumiwa ndipo watakapotupwa kwenye ziwa la moto, na kuangamia milele.
Sasa wakiwa huko kuzimu, ambapo kwa jina lingine kunaitwa Jehanamu, ni mahali pa shida, dhiki nyingi na mateso yasiyoelezeka, huko hakuna maisha, ni mateso tu vifungoni.
Hivyo ndugu, unapomwamini Yesu ipo faida kubwa zaidi ya unavyofikiri, unapokea MAISHA YA MILELE, Tangu ukiwa hapa duniani, ndani yako hakuna kitu kinachoitwa kifo, wala hutakihisi hata kidogo. Kwanini leo usimkaribishe maishani mwako? Ikiwa upo tayari basi wasiliana nasi kwa namba hizi kwa ajili ya mwongozo wa sala ya Toba, bure.
Au sema sala hii kwa Imani, na Moja kwa moja Yesu ataingia moyoni mwako.
Bwana akubariki
AINA ZA FARAJA BWANA AZIACHILIAZO KWA WATUMISHI WAKE.
TAFUTA UTAKASO WA SEHEMU KUU NNE ZA MWILI WAKO.
ASIYEMPENDA BWANA NA AWE AMELAANIWA.
Maisha ya Imani, hayafuti dhiki, hayafuti hisia za kibinadamu, haijalishi mtu atakuwa na ukomavu mkubwa kiasi gani, bado mahangaiko ya ndani na nje, zipo nyakati atakutana nayo.
Mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo, pamoja na kuwa walitumiwa na Mungu kipekee sana na neema ya Mungu kubwa kukaa juu yao. Bado walikiri kwa wazi kabisa bila maficho dhiki ziliwasonga kote kote,
2 Wakorintho 7:5
[5]Kwa maana hata tulipokuwa tumefika Makedonia miili yetu haikupata nafuu; bali tulidhikika kote kote; nje palikuwa na vita, ndani hofu.
Paulo anasema nje kulikuwa na vita, maana yake maadui, walioshindana naye, kuipinga imani, kutaka kumuua, kumfunga walikuwa ni wengi sana…lakini pia ndani anasema kulikuwa na hofu si nje tu,..akiwa na maana hofu ya kwenye nafsi..mfano wa hizi ni kama vile hofu za majukumu, hofu za kusalitiwa, hofu za kuvunjwa moyo, kuachwa peke yako, za kuvamiwa na wezi, mashaka ya ugenini, kushtakiwa, hofu za mwili kudhoofika, kuugua n.k. ambazo kimsingi kazi yake ni kukufanya ukate tamaa, usisonge mbele, usizae matunda.
Ndivyo ilivyo hata kwa watumishi wa Mungu wa kweli leo, mbele ya macho ya watu wanaweza kuonekana ni watu walio- mbali na mateso, lakini kwa mujibu wa kibiblia mioyoni mwao, vipo vita vingi na hofu kote kote…
Sasa swali ni je! Wanaweza kuishi na kuendelea na imani au huduma bila kukata tamaa wakiwa katika viwango vilevile ilihali nje vita ndani hofu?
Jibu ni kuwa Bwana..huwatumia faraja kwa njia mbalimbali, na faraja hizo ni kama zifuatazo;
Paulo katika dhiki zake anasema;..Mungu, mwenye kuwafariji wanyonge, alitufariji kwa kuja kwake Tito.
2 Wakorintho 7:5-7
[5]Kwa maana hata tulipokuwa tumefika Makedonia miili yetu haikupata nafuu; bali tulidhikika kote kote; nje palikuwa na vita, ndani hofu. [6]Lakini Mungu, mwenye kuwafariji wanyonge, alitufariji kwa kuja kwake Tito. [7]Wala si kwa kuja kwake tu, bali kwa zile faraja nazo alizofarijiwa kwenu, akituarifuhabari ya shauku yenu, na maombolezo yenu, na bidii yenu kwa ajili yangu, hata nikazidi kufurahi.
[6]Lakini Mungu, mwenye kuwafariji wanyonge, alitufariji kwa kuja kwake Tito.
[7]Wala si kwa kuja kwake tu, bali kwa zile faraja nazo alizofarijiwa kwenu, akituarifuhabari ya shauku yenu, na maombolezo yenu, na bidii yenu kwa ajili yangu, hata nikazidi kufurahi.
Ni ukweli usiopingika zipo nyakati ambazo unajihisi kama kuishiwa nguvu ya kuendelea aidha na wokovu au huduma, kwasababu ya hali fulani ngumu zinazokuzunguka..
Majira kama haya, Mungu hufanya njia, habari njema za faraja zinaweza kukufikia na kukutia nguvu na hatimaye kuendelea mbele kwa hamasa mpya.
Kwamfano Paulo alikuwa katika nyakati hizo mbaya, akiona kama taabu yake kwa Mungu ni bure, hakuna matunda, lakini ghafla analetewa taarifa na Tito ya wanafunzi wake huko Korintho wamebadilika, wamesimama imara zaidi sana wana shauku naye. Hilo lilimtia nguvu tena hata kujiona tena hayupo katika dhiki.
Kwamfano unaweza ukawa unafanya huduma kwa muda mrefu, na pengine huoni matokeo uliyoyategemea, lakini ghafla unakutana na mtu anakuambia nimebadilishwa sana na huduma yako au mafundisho yako. Wakati ule unafanya maombezi nilipona ile ugonjwa, ulipokuwa unahubiri niliguswa moyoni na sasa nimeokoka.
Hiyo ni faraja kubwa sana, na kama ulikuwa umelegea unaamka tena unasema…oh! Kumbe Bwana yupo pamoja nami.
Nyakati za uzito, nyakati za dhiki, Bwana huachilia mafunuo kwa njia mbalimbali ili kukufariji katika wokovu wako au huduma yako aidha anaweza kutumia ndoto au maono, au Neno, au hata fundisho fulani kama hili unalolisoma sasa…
Paulo alipokuwa kama mfungwa anaelekea Rumi, njiani Meli ilipata shida mpaka wakakata tamaa ya kuishi..lakini Mungu alimtokea na kumtia nguvu kwa maono.
Matendo ya Mitume 27:23-24
[23]Kwa maana usiku huu wa leo malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye, alisimama karibu nami, [24]akaniambia, Usiogope, Paulo, huna budi kusimama mbele ya Kaisari; tena, tazama, Mungu amekupa watu wote wanaosafiri pamoja nawe.
[23]Kwa maana usiku huu wa leo malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye, alisimama karibu nami,
[24]akaniambia, Usiogope, Paulo, huna budi kusimama mbele ya Kaisari; tena, tazama, Mungu amekupa watu wote wanaosafiri pamoja nawe.
Ni kawaida ya Mungu, kutufariji kwa njia za mafunuo, wewe ni mchungaji Bwana kukuonyesha ukichunga watu wengi, litakuwa ni jambo la kawaida, au anaweza kukupa andiko ambalo, litakupa sababu ya kusimama au kuendelea mbele. Au wakati mwingine hata kutumia mtumishi wake kukufundisha, na lile fundisho likawa ni nanga kubwa sana kwako, kutembea katika aina yoyote ya mapito.
Hii ni namna nyingine ambayo Mungu huwafariji watumishi wake, huwafungulia milango ya kifedha, aidha kusaidiwa na watu wa amani mahali fulani kimahitaji.
2 Wakorintho 11:9
[9]Nami nilipokuwa pamoja nanyi na kuhitaji sikumlemea mtu. Maana hao ndugu waliokuja kutoka Makedonia walinipa kadiri ya mahitaji yangu; nami katika mambo yote najilinda nafsi yangu nisiwalemee hata kidogo; tena najilinda.
Ni kawaida ya Mungu, nyakati fulani kufungua milango ya kupokea vitu kwa watu wake, lengo lake ni kukufariji, kukutia moyo ili usonge mbele katika kazi yake.
Hii ni njia nyingine ambayo Bwana huitumia sana, kutukumbusha mioyoni mwetu kuwa hizi taabu ni za kitambo, Bwana wetu ametuandalia makao na siku moja atarudi, nasi tutaishi naye milele na milele mbinguni.. katika maisha ya milele yasiyokuwa na fujo..Bwana anataka tuyakumbuke hayo, tufarijike.
1 Wathesalonike 4:16-18
[16]Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. [17]Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. [18]Basi, farijianeni kwa maneno hayo.
[16]Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.
[17]Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.
[18]Basi, farijianeni kwa maneno hayo.
Sikuzote kumbuka kuwa furaha yetu, urithi wetu, utajiri wetu upo kule ng’ambo unatungoja, hapa duniani ni wasafiri, hivyo hatutaona shida tuwapo katika dhiki za muda mfupi…Ni sawa na umeingia katika nyumba ya wageni, halafu ukaona mazingira si safi, aidha ya choo au vyumba..huwezi kulalamika na kuanza kusoneneka na kutaabika sana, kana kwamba umeingia kwenye matatizo makubwa…hapana utavumilia tu.kwasababu unajua hapo sio kwako, unapita tu utalala siku moja kesho yake utaondoka..na kurudi kwako palipo pasafi..hivyo utavumilia.
Bwana akutie nguvu. Songa mbele katika imani.
Amen.
MAANA HUYAWAZI YALIYO YA MUNGU, BALI YA WANADAMU
WALAKINI MIMI SI PEKE YANGU.
LAKINI DAUDI ALIJITIA NGUVU KATIKA BWANA, MUNGU WAKE.
(Masomo maalumu ya utakaso)
Jina la Bwana na Mwokozi YESU KRISTO libarikiwe. Karibu tujifunze Biblia, Neno la MUNGU wetu lililo Taa na Mwanga wa Njia yetu.
Je unazijua sehemu Nne (04) za Mwili wa Bwana YESU zilizotobolewa na kumwaga damu pale msalabani?.. Basi kama huzifahamu sehemu hizo ni 1)Kichwa, 2)Mikono, 3)Ubavu na 4)Miguu.
Tutazame moja baada ya nyingine, na pia tujifunze kwanini ni viungo hivyo ndio vilimwaga damu na kwanini vinahitaji utakaso sana.
1.KICHWA
Maandiko yanatuonyesha kuwa Bwana YESU alivikwa taji ya Miiba ..
Mathayo 27:28 “Wakamvua nguo, wakamvika vazi jekundu. 29 Wakasokota taji ya miiba, wakaiweka juu ya kichwa chake, na mwanzi katika mkono wake wa kuume; wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki, wakisema, Salamu, Mfalme wa Wayahudi!”
Mathayo 27:28 “Wakamvua nguo, wakamvika vazi jekundu.
29 Wakasokota taji ya miiba, wakaiweka juu ya kichwa chake, na mwanzi katika mkono wake wa kuume; wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki, wakisema, Salamu, Mfalme wa Wayahudi!”
Kwanini sehemu hii ya kichwa ilimwagika damu?.. Ni kwasababu kichwani ndiko kwenye ufahamu wa mtu, na milango yote ya ufahamu kama macho, masikio, pua na ulimi vipo huko.. na kwa kupitia vitu hivyo watu wanafanya dhambi, kwamfano kupitia ulimi mtu atasema uongo, atatukana, atakejeli n.k,
Kupitia macho mtu atatazama kwa kiburi sawasawa na (Mithali 6:17), kupitia macho mtu ataangalia uchafu, na pia kupitia masikio mtu atasikiliza mabaya, usengenyaji, njama mbaya n.k
Kwahiyo ni lazima Damu ingekota usoni kutakasa uso wa Bwana kwani dhambi zetu zote alizibeba yeye
2. UBAVU.
Biblia pia inatuonyesha kuwa Ubavuni mwa YESU palitokea damu..
Yohana 19:33 “Lakini walipomjia Yesu na kuona ya kuwa amekwisha kufa, hawakumvunja miguu; 34 Lakini askari mmojawapo alimchoma ubavu kwa mkuki; na mara ikatoka damu na maji”.
Yohana 19:33 “Lakini walipomjia Yesu na kuona ya kuwa amekwisha kufa, hawakumvunja miguu;
34 Lakini askari mmojawapo alimchoma ubavu kwa mkuki; na mara ikatoka damu na maji”.
Sasa kwanini ubavuni?.. Ni kwasababu ubavuni ndipo Moyo wa mtu ulipo, na hata wale Askari wa kirumi walikusudia kuhakiki kifo cha Bwana YESU kwa kumpiga mkuki katika moyo..
Na moyo ndio ubebao mawazo yote ya mtu ikiwemo mawazo mabaya..
Mathayo 15:19 “Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano”
Kwahiyo kulikuwa na sababu kwanini damu itokea moyoni ni kuonyesha utakaso wa Moyo..
3. MIKONO
Pia Biblia inatuonyesha kuwa mikono ya Bwana YESU ilitoka damu..
Yohana 20:25 “Basi wanafunzi wengine wakamwambia, Tumemwona Bwana. Akawaambia, Mimi nisipoziona mikononi mwake kovu za misumari, na kutia kidole changu katika mahali pa misumari, na kutia mkono wangu katika ubavu wake, mimi sisadiki hata kidogo”.
Kwanini mikono?.. Kwasababu mikono ndio inayoshika, inayofanya kazi za kila namna, (zilizo njema na mbovu)…watu wanafanya mauaji kwa kutumia mikono yao, kwa ufupi mikono ni nyenzo kubwa ya mabaya ndani ya mtu ndio maana katika ile ile Mithali maandiko yanasema, moyo uwazayo mabaya ni machukizo kwa Bwana..
Mithali 6:16 “Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake. 17 macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia; 18 moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu”
Mithali 6:16 “Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake.
17 macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia;
18 moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu”
4. MIGUU
Biblia inatuonyesha sehemu nyingine ya mwisho ya mwili wa Bwana YESU iliyomwagika damu ni miguu..
Luka 24:38 “Akawaambia, Mbona mnafadhaika? Na kwa nini mnaona shaka mioyoni mwenu? 39 Tazameni mikono yangu na miguu yangu, ya kuwa ni mimi mwenyewe. Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo”.
Luka 24:38 “Akawaambia, Mbona mnafadhaika? Na kwa nini mnaona shaka mioyoni mwenu?
39 Tazameni mikono yangu na miguu yangu, ya kuwa ni mimi mwenyewe. Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo”.
Miguu ni kiungo kingine chenye kuutia mwili mzima unajisi..watu wanatumia miguu kukimbilia mabaya, kukimbilia uzinzi, mauaji, ulevi n.k
Mithali 6:16 “Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake. 17 Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia; 18 Moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu”
17 Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia;
18 Moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu”
Sasa viungo hivi ni lazima vitakaswe kwa damu ya YESU, na vinatakaswaje?
Vinatakaswa kwanza kwa kumwamini Bwana YESU KRISTO, na kuomba na kuacha dhambi.. zingatia hili neno “kuacha dhambi” kupitia viungo hivyo.
Angalia miguu yako inachokimbilia, je ni chema au ni kibaya.. jiuepushe miguu yako na njia za wakosaji, angali macho yako yanachokitazama ni chema au kibaya, jiepushe na kutazama mambo yasiyofaa, vivyo hivyo na mikono yako na moyo wako, angalia sana unavyovifuatilia na kuvifanya.
Mwisho, kumbuka tunaishi katika siku za mwisho, na Kristo amekaribia sana kurudi, wakati wowote parapanda ya mwisho italia na hukumu ya mataifa itaanza, je umejiandaaje?
USHUHUDA WA MATENDO NI MKUU KULIKO WA MANENO.
UZURI WA MAJIVU.
IPO NJIA YA MKATO YA KUFIKA KIWANGO VYA MBALI VYA KIROHO.
Na kipenu ni nini (Isaya 1:8)
Wokovu wa milele/ Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?
Mathayo 8:29
[29]Na tazama, wakapiga kelele, wakisema, Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?
Mashetani yanajua kila jambo lipo katika mpangilio wa muda wake, yanajua kuwa tayari hukumu ilishatolewa ya wao kutupwa katika ziwa la moto lililo hatma yao ya milele..
Lakini utekelezaje wake, utakuja baadaye, ambao utakuwa ni mwisho wa dunia, utakao asisiwa na Bwana Yesu Kristo mwenyewe.(Mathayo 25:41)
Wengi tunadhani mapepo, hushindana na sisi, kwa kutuonea wivu, hilo ni kweli kwa sehemu, lakini sababu kubwa ya mapepo na shetani kushindana na sisi…ni wao kujilinda…na adhabu ijayo.
Na wanajua mwanadamu ndiye anayeweza kuiharakisha hiyo siku au kuikawiisha hiyo siku. Ndio maana yanafanya kazi kubwa sana kuwaharibu wanadamu ili siku hiyo isifike upesi.
Hizi ni njia tatu mapepo, hufanya kwa watu ili kukawiisha muhula wao usiwafikie haraka.
1) Kuchochea maovu.
2) Kukengeusha Imani za watu
3) Kukawisha injili
Maovu mengi, humsukuma Mungu kuwa mvumilivu na wanadamu, ili wafikie toba wasiangukie hukumu ya mapepo..Kama wanadamu wasingekuwa na shingo ngumu, mwisho wa dunia na hukumu yao ingeshafika zamani sana.. hivyo mapepo wanabuni kazi mbalimbali ili kuwafanya wanadamu wazidi kupotoka.
2 Petro 3:9-11
[9]Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba. [10]Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea. [11]Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,
[9]Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.
[10]Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.
[11]Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,
Luka 18:8
[8]Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?
Kristo anatarajia kanisa lake kusimama katika msingi wa imani kamili ambayo haijaharibiwa wala kuvurugwa na mapokeo na mafundisho ya uongo.. hii ndio sababu ya shetani kuinua makundi ya manabii wa uongo, kufundisha injili nyingine ambayo Kristo hajaileta duniani. Matokeo yake ndio kuwa na kundi kubwa la wakristo lakini dhaifu wasio tayari kumlaki Bwana mawinguni.
Mathayo 24:14
[14]Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.
Injili ya kweli adui huipiga vita vikubwa..Na wanajua ikihubiriwa ulimwenguni kote, basi ushuhuda wa Mungu utakuwa umefika na hakuna atakayekuwa na udhuru.
Sasa mimi na wewe hatuna budi kusimama katika utakatifu lakini pia imani na injili kuisambaza ili watu waokolewe…
Kumbuka tayari tupo kwenye siku za mwisho, Amka simama na Bwana.
MAPEPO YANATAFUTA HIFADHI NDANI YAKO KWA BIDII SANA.
Je mkristo anaweza akawa na mapepo?
Shetani anaishi wapi, Je! Amefungwa au yupo kuzimu?