Title April 2021

TABIA KUU TATU ZA WAHUBIRI WALIORUDI NYUMA NA KUMWACHA MUNGU.

Muhubiri/ Mtumishi yeyote aliyerudi nyuma na kusahau kusudi lake tayari anageuka kuwa nabii wa uongo, kumbuka pia, biblia inapotaja nabii wa uongo, haimaanishi tu mtu Yule mwenye karama ya kinabii, hapana! Bali neno hilo ni neno la kiujumla linaloweza kumaanisha aidha Mwalimu wa uongo, au mchungaji wa uongo, au mtume wa uongo, au muinjilisti wa uongo, au hata muimbaji wa uongo, wote hao ni manabii wa uongo kibiblia.

Leo tutajifunza tabia kuu tatu za wahubiri waliorudi nyuma. Ambapo tukizijua tabia hizo zitatusaidia kujihadhari na upotevu wao.

 1. Tabia ya kwanza, huwa hawahubiri na wala hawapendi kuhubiri kuwa hizi ni siku za Mwisho,

2. Tabia ya pili, wanashambulia watumishi wanaohubiri kuhusu siku za mwisho.

3. Tabia ya tatu, ni watu wa kupenda anasa, aidha kwa siri au kwa wazi.

Hizo ndio tabia kuu tatu za manabii, waalimu, wainjilisti, au wachungaji waliorudi nyuma na kugeuka kuwa wa uongo! ambapo kitambo sana walishaliacha kusudi la Mungu na kufuata mambo yao.

Sasa hebu tusome mfano ufuatao ambao Bwana Yesu aliutoa, kuhusu watumishi waliorudi nyuma.

Mathayo 24:44 “Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja.

45  Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, ambaye bwana wake alimweka juu ya nyumba yake, awape watu chakula kwa wakati wake?

46  Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo.

47  Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote.

48  Lakini mtumwa yule mbaya akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia;

49  akaanza kuwapiga wajoli wake, na kula na kunywa pamoja na walevi;

50  bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua,

51  atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”

Bwana alitoa mfano huo kwa wanafunzi wake tu!..na kwa makutano yote.. Akimaanisha kuwa unawahusu mitume tu! Na wote ambao wameitwa katika kuifanya kazi ya kulisha kondoo wa Mungu. Huu ni tofauti na ule mfano wa mpanzi, ambao Bwana aliwaambia watu wote, (yaani makutano pamoja na wanafunzi), lakini mfano huu aliwatenga wanafunzi wake na kuwaambia wao peke yao. Na katika mfano huo alilinganisha utumishi aliowapa wa kwenda kuhubiri na utumishi wa mtu aliyeajiri wafanyakazi katika nyumba yake. Ambapo hiyo nyumba inaonekana ni kubwa mfano wa kasri ambayo ina watu wengi (wageni pamoja na wenyeji) vile vile ina wafanyakazi wengi tofauti tofauti, wapo wapishi, wapo wanaofua nguo, wapo walinzi, wapo wanaofanya usafi n.k

Lakini katika huo mfano tunaona mwenye nyumba ni kama alisafiri, na akawaachia majukumu kila mfanyakazi, na hakuwaambia ni lini atarudi, Hivyo kila mfanyakazi kwa nafasi yake alipaswa afanye kwa uaminifu, kwasababu hajui ni lini Bwana wake atakuja. Lakini akatokea mtumwa mmoja miongoni mwao, ambaye kazi yake ilikuwa ni ya upishi, ambapo aliachiwa posho ya kutosha ya kununua chakula apikie watu wa ile nyumba wale kila siku washibe, lakini kinyume chake alipoona Bwana wake anachelewa, alikengeuka na kuanza kuwazuilia chakula watu wa pale nyumbani, lakini haikuishia hapo akaanza kuwapiga wajoli wake, Neno mjoli maana yake ni “mfanyakazi-mwenza”.. yaani mtu anayefanya kazi pamoja na wewe anaitwa “mjoli wako”.

Kwahiyo huyu mpishi akaanza kuwapiga wale wafanyakazi wengine, pengine wale waliokuwa walinzi, au wanaofanya usafi n.k. Na mpaka mtu afikie hatua ya kuwapiga wafanyakazi wenzake maana yake ni kwamba tayari kuna vitu wale wenzake wanafanya ambavyo hakubaliani navyo. Maana yake wenzake ni waaminifu katika kazi zao lakini yeye si mwaminifu ndio maana anagombana nao, na hata kufikia kuwapiga.

Maana yake ni nini mfano huo?

Ukiona mtumishi kasahau Ono la Msingi la kwamba BWANA WAKE ANARUDI SIKU YOYOTE, na kugeukia mambo mengine. Tambua kwamba hiyo ndio dalili ya kwanza ya Mtumishi aliyerudi nyuma.

> Ukiona hakubaliani na kwamba Kristo wakati wowote anarudi, badala yake anahubiri na kuishi maisha kana kwamba Kristo atarudi miaka elfu5 mbele…Jitenge naye! Kwasababu Kitambo sana kashaliacha kusudi lake, na hivyo atakupoteza.

> Ukiona hakukumbushi kwamba siku yoyote kuanzia muda huu parapanda italia, kimbia! Jiokoe nafsi yako.

> Ukiona anakuhubiria vitu vya kidunia tu!..njoo upate mke, njoo upate nyumba, gari, mali.. na wala hakwambii kuwa hizi ni nyakati za mwisho, na dalili zote za kurudi kwake zimetimia.. Jiokoe nafsi yako ndugu!

2. Tabia ya pili: Ukiona anawapiga wajoli wake (yaani wale watumishi wanaosimamia kweli) jihadhari naye. Utauliza anawapigaje?..Anawapiga kwa kuwarushia maneno!!, na kuwadharau. Na ni kwanini anafanya hivyo?.. ni kwasababu ameona wamekuwa waaminifu katika nafasi zao na yeye kashatoka kwenye mstari kitambo, hivyo atakapoona wengine wanahubiri kwa nguvu kwamba Kristo yupo mlangoni, atakwenda kinyume nao kwa nguvu!.. kwasababu yeye bado anatamani udunia. Hiyo ni dalili ya pili.

> Hivyo ukiona anashambulia sana mahubiri au wahubiri wanaohubiri kuhusu kurudi kwa Yesu. Jihadhari na huyo mtumishi. Ukiona anakuambia Yesu harudi leo wala kesho, hivyo endelea na maisha yako kama kawaida, jiokoe nafsi yako!.

3. Na tabia ya tatu na ya mwisho: Ni watu wa kupenda anasa. Katika huo mfano utaona anasema “anaacha kwenda kugawa chakula, anakula na kunywa na walevi”

> Ukiona mhubiri anapenda kusifia sifia vitu vya kiulimwengu kama magari, nyumba, mavazi, umaarufu, mwonekano, hiyo ni dalili mojawapo ya kwamba ni mtu wa anasa. Anaweza asikiri kwa kinywa lakini maisha yake ya siri ni ya anasa. Na mahubiri yake yatakuwa ni ya kutukuza mambo hayo hayo tu!.. Atakuwa anafanya juu chini ili awe maarufu, ili awe na mali nyingi, atabadilisha mpaka mtindo wa mahubiri ilimradi tu akusanye fedha, na umaarufu kutoka kwa watu. Ukiona hiyo dalili, jihadhari kwasababu tayari kasharudi nyuma. Kashaliacha kusudi aliloitiwa.

Lakini Bwana alisema maneno haya..

Mathayo 24:50 “bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua,

51  atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”

Hapo Bwana anaanza kwa kusema “atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua”. Ndugu hao manabii na watumishi wanaokuhubiria kuwa Kristo harudi, wala haji leo wala kesho!!.. Kristo kasema mwenyewe atakuja siku wasiyoidhania… wakati wanadhani ndio wakati wa kujiongezea mali, ghafla Kristo atatokea, na atawakata vipande viwili. Je! Wewe unayewategemea hao utakuwa wapi siku hiyo???. Geuka! Mtazame Kristo yupo mlangoni kurudi, achana na wahubiri hao waliorudi nyuma, hawana tumaini lolote, siku yao itakuja ghafla na Kristo atawahukumu.

Na tena anasema atawakata vipande viwili: Kwanini viwili na si kumi?..na kwasababu wanajifanya kutumika upande wa Bwana na wakati huo huo wanazitumikia tamaa zao (wanatumikia mabwana wawili kwa wakati mmoja), hivyo zamani, adhabu ya mtu anayekamatwa anatumikia falme mbili kwa wakati mmoja ilikuwa ni kukatwa vipande viwili, kwasababu ni mnafiki na msaliti. Hivyo na Bwana atawakata vipande viwili watumishi wote wanaotumikia tumbo na huku wanasimama kuhubiri, atawakata vipande viwili wahubiri wote wanaodharau ujio wake.

Ndugu hizi ni nyakati za mwisho, Yesu anarudi, kizazi tunachoishi ni kizazi cha hatari kuliko vyote, kwasababu dalili zote za kurudi kwake zimeshatimia, Ugonjwa uliosambaa sasa ujulikanao kama corona ni mojawapo ya Tauni zilizotabiriwa kutokea kipindi kifupi kabla ya kurudi kwa Yesu mara ya pili (Soma Luka 21:11), na zaidi ya yote, Israeli imeshakuwa Taifa, wakati wowote unyakuo wa kanisa utatokea.

Luka 12:35 “Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka;

36  nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara.

37  Heri watumwa wale, ambao bwana wao ajapo atawakuta wanakesha. Amin, nawaambieni, atajifunga na kuwakaribisha chakulani, atakuja na kuwahudumia”

Kama hujampokea Yesu, wakati wako ndio sasa na si kesho, hapo ulipo piga magoti, kisha omba rehema kwa Bwana Yesu, naye atakusamehe..na pia acha maovu yote uliyokuwa unayafanya kwa vitendo, kama ulikuwa unatazama filamu za kidunia unaacha na kuzifuta kwenye kifaa chako, kama ulikuwa unazini na kufanya uasherati unaacha kwa vitendo, kama ni binti ulikuwa unavaa vibaya, ikiwemo nguo zinazobana na suruali, na kama ulikuwa unapaka wanja, na kuvaa wigi, hereni, na kujichubua,na mambo mengine yote yanayofanana na hayo ya kidunia unayaacha, na unabeba msalaba wako unamfuata Yesu. Na baada ya hapo, bila kukawia tafuta ubatizo sahihi wa maji tele na kwa jina la Yesu, kwaajili ya ondoleo la dhambi zako (Matendo 2:38).

Na kama ukifanya hayo yote  kwa Imani, Roho Mtakatifu atakuthibitisha kwa kukupa amani, na furaha isiyoelezeka, na pia atakupa uwezo wa kuushinda ulimwengu, na atakuongoza katika kuyaelewa maandiko.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Muhubiri/ Mtumishi yeyote aliyerudi nyuma na kusahau kusudi lake tayari anageuka kuwa nabii wa uongo, kumbuka pia, biblia inapotaja nabii wa uongo, haimaanishi tu mtu Yule mwenye karama ya kinabii, hapana! Bali neno hilo ni neno la kiujumla linaloweza kumaanisha aidha Mwalimu wa uongo, au mchungaji wa uongo, au mtume wa uongo, au muinjilisti wa uongo, au hata muimbaji wa uongo, wote hao ni manabii wa uongo kibiblia.

Leo tutajifunza tabia kuu tatu za wahubiri waliorudi nyuma. Ambapo tukizijua tabia hizo zitatusaidia kujihadhari na upotevu wao.

 1. Tabia ya kwanza, huwa hawahubiri na wala hawapendi kuhubiri kuwa hizi ni siku za Mwisho,

2. Tabia ya pili, wanashambulia watumishi wanaohubiri kuhusu siku za mwisho.

3. Tabia ya tatu, ni watu wa kupenda anasa, aidha kwa siri au kwa wazi.

Hizo ndio tabia kuu tatu za manabii, waalimu, wainjilisti, au wachungaji waliorudi nyuma na kugeuka kuwa wa uongo! ambapo kitambo sana walishaliacha kusudi la Mungu na kufuata mambo yao.

Sasa hebu tusome mfano ufuatao ambao Bwana Yesu aliutoa, kuhusu watumishi waliorudi nyuma.

Mathayo 24:44 “Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja.

45  Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, ambaye bwana wake alimweka juu ya nyumba yake, awape watu chakula kwa wakati wake?

46  Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo.

47  Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote.

48  Lakini mtumwa yule mbaya akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia;

49  akaanza kuwapiga wajoli wake, na kula na kunywa pamoja na walevi;

50  bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua,

51  atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”

Bwana alitoa mfano huo kwa wanafunzi wake tu!..na kwa makutano yote.. Akimaanisha kuwa unawahusu mitume tu! Na wote ambao wameitwa katika kuifanya kazi ya kulisha kondoo wa Mungu. Huu ni tofauti na ule mfano wa mpanzi, ambao Bwana aliwaambia watu wote, (yaani makutano pamoja na wanafunzi), lakini mfano huu aliwatenga wanafunzi wake na kuwaambia wao peke yao. Na katika mfano huo alilinganisha utumishi aliowapa wa kwenda kuhubiri na utumishi wa mtu aliyeajiri wafanyakazi katika nyumba yake. Ambapo hiyo nyumba inaonekana ni kubwa mfano wa kasri ambayo ina watu wengi (wageni pamoja na wenyeji) vile vile ina wafanyakazi wengi tofauti tofauti, wapo wapishi, wapo wanaofua nguo, wapo walinzi, wapo wanaofanya usafi n.k

Lakini katika huo mfano tunaona mwenye nyumba ni kama alisafiri, na akawaachia majukumu kila mfanyakazi, na hakuwaambia ni lini atarudi, Hivyo kila mfanyakazi kwa nafasi yake alipaswa afanye kwa uaminifu, kwasababu hajui ni lini Bwana wake atakuja. Lakini akatokea mtumwa mmoja miongoni mwao, ambaye kazi yake ilikuwa ni ya upishi, ambapo aliachiwa posho ya kutosha ya kununua chakula apikie watu wa ile nyumba wale kila siku washibe, lakini kinyume chake alipoona Bwana wake anachelewa, alikengeuka na kuanza kuwazuilia chakula watu wa pale nyumbani, lakini haikuishia hapo akaanza kuwapiga wajoli wake, Neno mjoli maana yake ni “mfanyakazi-mwenza”.. yaani mtu anayefanya kazi pamoja na wewe anaitwa “mjoli wako”.

Kwahiyo huyu mpishi akaanza kuwapiga wale wafanyakazi wengine, pengine wale waliokuwa walinzi, au wanaofanya usafi n.k. Na mpaka mtu afikie hatua ya kuwapiga wafanyakazi wenzake maana yake ni kwamba tayari kuna vitu wale wenzake wanafanya ambavyo hakubaliani navyo. Maana yake wenzake ni waaminifu katika kazi zao lakini yeye si mwaminifu ndio maana anagombana nao, na hata kufikia kuwapiga.

Maana yake ni nini mfano huo?

Ukiona mtumishi kasahau Ono la Msingi la kwamba BWANA WAKE ANARUDI SIKU YOYOTE, na kugeukia mambo mengine. Tambua kwamba hiyo ndio dalili ya kwanza ya Mtumishi aliyerudi nyuma.

> Ukiona hakubaliani na kwamba Kristo wakati wowote anarudi, badala yake anahubiri na kuishi maisha kana kwamba Kristo atarudi miaka elfu5 mbele…Jitenge naye! Kwasababu Kitambo sana kashaliacha kusudi lake, na hivyo atakupoteza.

> Ukiona hakukumbushi kwamba siku yoyote kuanzia muda huu parapanda italia, kimbia! Jiokoe nafsi yako.

> Ukiona anakuhubiria vitu vya kidunia tu!..njoo upate mke, njoo upate nyumba, gari, mali.. na wala hakwambii kuwa hizi ni nyakati za mwisho, na dalili zote za kurudi kwake zimetimia.. Jiokoe nafsi yako ndugu!

2. Tabia ya pili: Ukiona anawapiga wajoli wake (yaani wale watumishi wanaosimamia kweli) jihadhari naye. Utauliza anawapigaje?..Anawapiga kwa kuwarushia maneno!!, na kuwadharau. Na ni kwanini anafanya hivyo?.. ni kwasababu ameona wamekuwa waaminifu katika nafasi zao na yeye kashatoka kwenye mstari kitambo, hivyo atakapoona wengine wanahubiri kwa nguvu kwamba Kristo yupo mlangoni, atakwenda kinyume nao kwa nguvu!.. kwasababu yeye bado anatamani udunia. Hiyo ni dalili ya pili.

> Hivyo ukiona anashambulia sana mahubiri au wahubiri wanaohubiri kuhusu kurudi kwa Yesu. Jihadhari na huyo mtumishi. Ukiona anakuambia Yesu harudi leo wala kesho, hivyo endelea na maisha yako kama kawaida, jiokoe nafsi yako!.

3. Na tabia ya tatu na ya mwisho: Ni watu wa kupenda anasa. Katika huo mfano utaona anasema “anaacha kwenda kugawa chakula, anakula na kunywa na walevi”

> Ukiona mhubiri anapenda kusifia sifia vitu vya kiulimwengu kama magari, nyumba, mavazi, umaarufu, mwonekano, hiyo ni dalili mojawapo ya kwamba ni mtu wa anasa. Anaweza asikiri kwa kinywa lakini maisha yake ya siri ni ya anasa. Na mahubiri yake yatakuwa ni ya kutukuza mambo hayo hayo tu!.. Atakuwa anafanya juu chini ili awe maarufu, ili awe na mali nyingi, atabadilisha mpaka mtindo wa mahubiri ilimradi tu akusanye fedha, na umaarufu kutoka kwa watu. Ukiona hiyo dalili, jihadhari kwasababu tayari kasharudi nyuma. Kashaliacha kusudi aliloitiwa.

Lakini Bwana alisema maneno haya..

Mathayo 24:50 “bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua,

51  atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”

Hapo Bwana anaanza kwa kusema “atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua”. Ndugu hao manabii na watumishi wanaokuhubiria kuwa Kristo harudi, wala haji leo wala kesho!!.. Kristo kasema mwenyewe atakuja siku wasiyoidhania… wakati wanadhani ndio wakati wa kujiongezea mali, ghafla Kristo atatokea, na atawakata vipande viwili. Je! Wewe unayewategemea hao utakuwa wapi siku hiyo???. Geuka! Mtazame Kristo yupo mlangoni kurudi, achana na wahubiri hao waliorudi nyuma, hawana tumaini lolote, siku yao itakuja ghafla na Kristo atawahukumu.

Na tena anasema atawakata vipande viwili: Kwanini viwili na si kumi?..na kwasababu wanajifanya kutumika upande wa Bwana na wakati huo huo wanazitumikia tamaa zao (wanatumikia mabwana wawili kwa wakati mmoja), hivyo zamani, adhabu ya mtu anayekamatwa anatumikia falme mbili kwa wakati mmoja ilikuwa ni kukatwa vipande viwili, kwasababu ni mnafiki na msaliti. Hivyo na Bwana atawakata vipande viwili watumishi wote wanaotumikia tumbo na huku wanasimama kuhubiri, atawakata vipande viwili wahubiri wote wanaodharau ujio wake.

Ndugu hizi ni nyakati za mwisho, Yesu anarudi, kizazi tunachoishi ni kizazi cha hatari kuliko vyote, kwasababu dalili zote za kurudi kwake zimeshatimia, Ugonjwa uliosambaa sasa ujulikanao kama corona ni mojawapo ya Tauni zilizotabiriwa kutokea kipindi kifupi kabla ya kurudi kwa Yesu mara ya pili (Soma Luka 21:11), na zaidi ya yote, Israeli imeshakuwa Taifa, wakati wowote unyakuo wa kanisa utatokea.

Luka 12:35 “Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka;

36  nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara.

37  Heri watumwa wale, ambao bwana wao ajapo atawakuta wanakesha. Amin, nawaambieni, atajifunga na kuwakaribisha chakulani, atakuja na kuwahudumia”

Kama hujampokea Yesu, wakati wako ndio sasa na si kesho, hapo ulipo piga magoti, kisha omba rehema kwa Bwana Yesu, naye atakusamehe..na pia acha maovu yote uliyokuwa unayafanya kwa vitendo, kama ulikuwa unatazama filamu za kidunia unaacha na kuzifuta kwenye kifaa chako, kama ulikuwa unazini na kufanya uasherati unaacha kwa vitendo, kama ni binti ulikuwa unavaa vibaya, ikiwemo nguo zinazobana na suruali, na kama ulikuwa unapaka wanja, na kuvaa wigi, hereni, na kujichubua,na mambo mengine yote yanayofanana na hayo ya kidunia unayaacha, na unabeba msalaba wako unamfuata Yesu. Na baada ya hapo, bila kukawia tafuta ubatizo sahihi wa maji tele na kwa jina la Yesu, kwaajili ya ondoleo la dhambi zako (Matendo 2:38).

Na kama ukifanya hayo yote  kwa Imani, Roho Mtakatifu atakuthibitisha kwa kukupa amani, na furaha isiyoelezeka, na pia atakupa uwezo wa kuushinda ulimwengu, na atakuongoza katika kuyaelewa maandiko.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Gidamu ni nini? Kwanini Yohana alisema hastahili kuzilegeza gidamu za Yesu?

SWALI: Kwanini Yohana alisema hastahili kulegeza gidamu ya viatu vya Yesu, gidamu ni nini?

Gidamu ni mikanda maalumu ya viatu,

Viatu vya zamani vilikuwa havina muonekano kama tulionao sasa hivi, ambao vingi vinatengenezwa kwa muundo wa kutumbukiza tu mguu,, vya zamani vilikuwa zinashikiliwa na mikanda maalumu, au kamba maalumu, ambazo zinazungushwa kwenye miguu, ili kuwezesha kiatu kisitoke, sasa hiyo mikanda ndio inayoitwa Gidamu. tazama picha juu..

Neno hilo utalipata kwenye vifungu hivi;

Marko 1:7 “Akahubiri akisema, Yuaja nyuma yangu aliye na nguvu kuliko mimi, ambaye mimi sistahili kuinama na kuilegeza gidamu ya viatu vyake.

8 Mimi niliwabatiza kwa maji; bali yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu”.

Luka 3:16 “Yohana alijibu akawaambia wote, Kweli mimi nawabatiza kwa maji; lakini yuaja mtu mwenye nguvu kuliko mimi, ambaye mimi sistahili kuilegeza gidamu ya viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto”;

Mathayo 3.11 “Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto”.

Tukirudi kwenye swali kwanini Yohana Mbatizaji alisema hastahili kulegeza gidamu ya viatu Yesu?

Zamani na hata sasa kazi ya kufunga na kufungua mikanda/kamba za viatu ni kazi zinazofanywa na watumwa wa chini sana,  Wanachofanya ni kumwandalia bwana wao viatu, kisha kumvisha, na baadaye kuwavua tena pindi watakaporudi kutoka katika mihangaiko yao, na kuvichukua viatu hivyo mpaka sehemu ya usafi na kuhakikisha  wanaviosha, vinakuwa maridadi, kisha wanarudi kuwavisha tena bwana zao, hiyo ndio inakuwa ni kazi yao muda wote, siku zote.

Kwa desturi wa wayahudi kazi kama hii haikufanywa na mtumwa wowote wa kiyahudi, kwasababu ni kazi nyonge, dhaifu na ya kudharaulika, ilikuwa inafanywa na wakaanani tu(Watu wa mataifa mengine waliokuwa wanaishi Israeli wakati ule).

Sasa Yohana kusema hastahili kulegeza hata gidamu ya viatu vya Yesu, ni kuonyesha kutostahili kwake, kuifanya hata ile kazi ndogo sana ya Yesu Kristo, kwasababu Kristo ni mkuu kupita kiasi. Hivyo hata ile kazi inayoonekana ni ya kudharaulika sana kwake ni kubwa sana, kiasi cha kumfanya ajione hastahili kuifanya. Huo ni unyenyekevu wa hali ya juu sana na hofu aliyokuwa nayo Yohana kwa ajili ya Bwana wake Yesu Kristo.

Na matokeo yake, hatushangai ni kwanini Bwana Yesu alimfanya kuwa mtangulizi wake, na zaidi ya yote akamshuhudia kuwa katika uzao wa wanawake hakuwahi kutokea mtu aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni kuliko yeye. Hiyo yote ni kwasababu aliithamini sana hata ule wito mdogo sana wa Bwana Yesu.

Je na sisi tunaweza kuwa kama Yohana mbatizaji?..Kama tutashindwa kupiga deki kanisa la Bwana, au kuosha choo,  tutawezaje, kufanywa watangulizi wake..Tutawezaje kuonyeshwa siri za ndani za ufalme wa mbinguni kama alivyoonyeshwa Yohana, kama tutazidharau hata zile kazi zake ndogo.

 Thamini Gidamu za Yesu!

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Tofauti kati ya lijamu na hatamu ni ipi kibiblia?

Mtu mwenye “kitango” ni mtu wa namna gani kibiblia?

UFUNUO: Mlango wa 1

Amri zilizo ndogo alizozizungumzia Yesu ni zipi?

Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Israeli wote wataokolewa siku ya mwisho kulingana na Warumi 11:26?

Jibu: Tusome,

Warumi 11:25 “ Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.

26 Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake”

Ni kweli upo unabii wa Israeli wote kuokolewa katika siku za mwisho, kuna kipindi ambacho injili itahamia katika Taifa la Israeli baada ya unyakuo kupita!..wakati huo kanisa la mataifa litakuwa limeshanyakuliwa, Ndipo injili itaanza kuhubiriwa tena katika Taifa la Israeli na wale manabii wawili tunaowasoma katika kitabu cha Ufunuo 11, watahubiri kama nyakati za Yohana Mbatizaji isipokuwa zama hizo itakuwa ni kwa ishara nyingi na miujiza mfano wa ile ya Musa na Eliya.

Na kupitia injili ya hao manabii wawili, waisraeli wengi watamkubali Yesu kama Masihi, kumbuka kwasasa wayahudi wengi (yaani waisraeli wengi), hawaamini kuwa Yesu Yule aliyekuja na kufa na kufufuka kuwa ndiye Masihi aliyetabiriwa na manabii zamani, wanaamini kuwa Masihi bado hajaja, na Yesu sio Masihi, hivyo wanamsubiria mwingine!!..Biblia inasema macho yao yamefumbwa wasimtambue Yesu kuwa ndiye Masihi, ili sisi watu wa mataifa tupate neema. (Warumi 11:30-31).

Sasa swali la Msingi hapo, ni je Israeli wote wataokolewa?..hata kama ni watenda maovu?..na je kitendo tu cha kuzaliwa  Muisraeli tayari umeshapewa tiketi ya kuurithi uzima  wa milele?.

Jibu ni La!… Sio wote watakaookolewa, kwasababu wapo waisraeli wasioamini kabisa hata kama Mungu yupo, wapo wachawi na manabii wa uongo katikati ya jamii za Israeli mfano wa akina Bar-Yesu (Matendo 13:6), hao hawataokolewa na wataenda katika ziwa la moto, kama hawatatubu!..

Sasa kwanini hapo biblia iseme ni  “Israeli wote”, na si baadhi!.. kama watakuwepo baadhi ambao hawataokolewa?, kwanini iseme wote?.. Ili kuelewa vyema tusome mstari ufuatao.

Warumi 9:6  “Si kana kwamba neno la Mungu limetanguka. MAANA HAWAWI WOTE WAISRAELI WALIO WA UZAO WA ISRAELI.

7  Wala hawawi wote wana kwa kuwa wazao wa Ibrahimu, bali, Katika Isaka wazao wako wataitwa; ”

Unaona hapo?.. Sio Waisraeli wote ni waisraeli, ni sawa na kusema “Si wote wanaojiita au wanaojulikana kuwa ni wakristo ni wakristo”. Sasa hivi duniani kuna zaidi ya mabilioni ya wakristo. Lakini kiuhalisia “Wakristo wa kweli ni wachache”, ni wale wanaozishika amri za Mungu na kufanya mapenzi yake, hao wengine ni wakristo jina tu!. Kwahiyo kwenye biblia kungekuwa na mstari unaosema “wakristo wote wataokolewa” bila shaka, ingekuwa imemaanisha “wale wakristo wa kweli” na si wakristo jina!.. mtu anayejiita mkristo lakini mchawi, hawezi kuurithi uzima wa milele, mtu anayejiita mkristo lakini ni mzinzi vivyo hivyo!

Kadhalika biblia iliposema “Israeli wote wataokolewa” ilimaanisha wale “wale waisraeli kweli kweli” ambao wanakwenda katika sheria za Mungu bila kupinda panda. Hao ndio wote watakaookolewa. Mfano wa hao ni wakina Nathanieli katika Yohana 1:47 “Basi Yesu akamwona Nathanaeli anakuja kwake, akanena habari zake, Tazama, MWISRAELI KWELI KWELI, hamna hila ndani yake”

 Lakini wengine wasiompenda Mungu, maana yake ni waisraeli jina tu!, Lakini sio waisraeli hasa!!, hao hawataokolewa, Ndicho Mtume Paulo alichokuwa anakimaanisha hapo katika Warumi 9:6 kuwa “….HAWAWI WOTE WAISRAELI WALIO WA UZAO WA ISRAELI”.

Vivyo hivyo hawawi wote wakristo, walio wa uzao Kristo!!. Walio uzao wa Kristo ni wale waliozaliwa mara ya pili, hao ndio Wakristo, wengine ni wakristo jina tu!..

Je wewe ni Mkristo halisi au mkristo jina tu!.. Mkristo jina ni Yule anayekwenda kanisani lakini anafanya uzinzi kwa siri, ni yule mwenye jina la kikristo lakini ni mtu wa kidunia, mkristo jina ni Yule anayeupenda ulimwengu kuliko kumpenda Mungu, mkristo jina ni yule asiyechukua msalaba wake na kumfuata Yesu. Lakini mkristo kweli kweli ni Yule aliyeukataa ulimwengu, anayejitwika msalaba wake kila siku na kumfuata Yesu kwa gharama zozote.

Bwana atusaidie tuwe wakristo halisi!

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

AINA TATU ZA WAKRISTO.

AINA TATU ZA WAKRISTO.

Je Musa kumwoa Sipora, Mkushi alifanya dhambi?

LIPI TUNAJIFUNZA KWA WALIOMWONA YESU ALIYEFUFUKA?

Rudi nyumbani

Print this post

Ayari ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Ayari ni mtu aliyekosa utu,  mchoyo  na asiyejali watu,  anayejipenda mwenyewe, na mwenye hasira nyingi na madanganyifu. Kwa ufupi ni mtu asiyependa watu kwa ujumla.

Mfano wa watu hawa katika biblia ni Nabali, ambaye pamoja na kwamba Daudi na wenzake walimfanyia wema mwingi, hakujali kuwastahi hata kwa maji au kwa chakula (1Samweli 25).. na mwingine ni yule Tajiri wa Lazaro ambaye aliishi hapa duniani katika maisha ya anasa na ya ubinafsi, akafa katika dhambi zake, akaenda kuzimu.(Luka 16)

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi kwenye biblia;

Isaya 32:5 “Mpumbavu hataitwa tena mwungwana, WALA AYARI HATASEMWA KWAMBA NI KARIMU.

6 Maana mpumbavu atanena yaliyo upumbavu, na moyo wake utafanya maovu, ili kutenda hila na kusema yasiyo kweli juu ya Bwana, ili kuziacha nafsi za watu wenye njaa hazina kitu, na kukikomesha kinywaji chake mwenye kiu.

7 Tena VYOMBO VYAKE AYARI NI VIBAYA; hutunga hila mbaya, ili kuwaangamiza wanyonge kwa maneno ya uongo, mtu mhitaji ajaposema maneno yenye haki.

8 Bali mwungwana huwaza mambo ya kiungwana, naye hushika sana mambo ya kiungwana”.

Kwa mfano katika habari hiyo, kama ukianzia  mistari ya juu mstari wa kwanza utapata picha kamili ni nini kilikuwa kinazungumziwa,  anasema..

Isaya 32:1 Tazama, mfalme atamiliki kwa haki, na wakuu watatawala kwa hukumu.

Huo ni unabii unaomzungumzia Kristo katika utawala wake wa amani utaokuja huko mbeleni, kwasababu yeye ndiye atakayemiliki kama mfalme, Na katika huo utawala wake, hakutakuwa na kupindisha haki, kama ilivyo sasahivi, kwa sasahivi fisadi ndio anaonekana mwerevu, Mtu mbinafsi, ndiye anayeonekana  ana akili. Wapumbavu ndio wanaopewa uongozi, mtoa rushwa ndiye anayeonekana  ni mkarimu, Ayari (mtu asiyependa watu) ndio anayehesheshimika na kuogopeka katika jamii n.k.

Lakini katika huo utawala wa Amani wa miaka 1000 wa Yesu Kristo hapa duniani, hilo jambo halitakuwepo,  anasema..

“Mpumbavu hataitwa tena mwungwana, wala AYARI hatasemwa kwamba ni karimu”.

Hii ikiwa na maana kuwa watenda haki ndio watasifika katika haki yao, bali watendao uovu, watakutana na fimbo ya chuma ya Yesu Kristo, (Ufunuo 2:27).

Fahamu kuwa, kwa Mungu hakuna upendeleo, hata leo hii ikiwa utakufa katika hali yako ya dhambi, hakuna nafasi ya pili, kama umestahili mbingu, utakwenda mbinguni, kama umestahili Jehanum, utakwenda Jehanum, nafasi ya kutubu ipo leo, haipo baada ya kufa, hivyo mgeukie Yesu Kristo ayaokoe Maisha yako. Kwasababu hizi ni siku za mwisho.. Wakati ambao mtu kufanya dhambi ndio anasifiwa.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

YESU NI MFALME WA AINA GANI KWAKO? 

JE NI KWELI SAMAKI NGUVA YUPO?

Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki;

Alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru

Mafundisho

Rudi nyumbani

Print this post

YESU NI MFALME WA AINA GANI KWAKO? 

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tuyatafakari maandiko pamoja.

Je Bwana Yesu ni Mfalme katika maisha yako?..Kama una tabia zifuatazo, hajawa bado Mfalme kwako, haijalishi utamkiri kiasi gani.

Kama unamtafuta kwaajili ya faida zako za kimwili, ikiwemo kupata mali, kupata mke, kupata mume, kupata kupata watoto, kupata umaarufu, na mambo mengine yote ya kimwilini , Tambua kuwa yeye si mfalme kwako, haijalishi utamtangaza kwa watu kuwa ni mfalme kwako, lakini yeye hakujui!!.

Utauliza tunasoma wapi katika maandiko?.. Hebu tukitafakari kisa kifuatacho kwa ufupi kisha tutapata majibu…

Yohana 6:10  “Yesu akasema, Waketisheni watu. Na mahali pale palikuwa na majani tele. Basi watu waume wakaketi, wapata elfu tano jumla yao.

.11  Basi Yesu akaitwaa ile mikate, akashukuru, akawagawia walioketi; na kadhalika katika wale samaki kwa kadiri walivyotaka.

12  Nao waliposhiba, aliwaambia wanafunzi wake, Kusanyeni vipande vilivyobaki, kisipotee cho chote.

13  Basi wakavikusanya, wakajaza vikapu kumi na viwili, vipande vya mikate mitano ya shayiri vilivyowabakia wale waliokula.

14  Basi watu wale, walipoiona ishara aliyoifanya, walisema, Hakika huyu ni nabii yule ajaye ulimwenguni.

15  Kisha YESU, HALI AKITAMBUA YA KUWA WALITAKA KUJA KUMSHIKA ILI WAMFANYE MFALME, AKAJITENGA, AKAENDA TENA MLIMANI YEYE PEKE YAKE”.

Hebu jiulize, kwani! Bwana Yesu, hataki au hapendi kuitwa Mfalme??.. Hata hivyo ndicho anachokitengeneza sasa, anatengeneza ufalme wake, na yeye ndiye atakuwa Mfalme wa wafalme. Lakini hapa tunaona anaukataa na kuukimbia ufalme??..Ni kwanini?..Jibu ni rahisi, ni kwasababu yeye hatengenezi wala hatafuti ufalme wa kidunia.

Yohana 18:33  “Basi Pilato akaingia tena ndani ya Praitorio, akamwita Yesu, akamwambia, Je! Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?

34  Yesu akamjibu, Wewe wasema hivi kwa nafsi yako, au watu wengine walikuambia habari zangu?

35  Pilato akajibu, Ama! Ni Myahudi mimi! Taifa lako na wakuu wa makuhani ndio waliokuleta kwangu. Umefanya nini?

36  Yesu akajibu, UFALME WANGU SIO WA ULIMWENGU HUU. Kama ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, watumishi wangu wangenipigania, nisije nikatiwa mikononi mwa Wayahudi. Lakini ufalme wangu sio wa hapa”

Hiyo ndio sababu aliwakimbia wale makutano waliotaka kumfanya awe mfalme wao… Waliona wakimpata atawasaidia kujenga miji yao, atawasaidia kunyanyua uchumi wa nchi yao, atawasaidia kupata fedha nyingi, atawasaidia kutokomeza umasikini.  Lakini Yesu aliwakimbia… na walimtafuta kwa bidii na walipompata sehemu nyingine aliwaambia maneno yafuatayo..

Yohana 6:24  “Basi mkutano, walipoona ya kuwa Yesu hayuko huko wala wanafunzi wake, waliingia mashuani wenyewe, wakaenda Kapernaumu wakimtafuta Yesu.

25  Hata walipomwona ng’ambo ya bahari, walimwambia, Rabi, wewe umekuja lini hapa?

26  Yesu akawajibu, akasema, AMIN, AMIN, NAWAAMBIENI, NINYI MNANITAFUTA, SI KWA SABABU MLIONA ISHARA, BALI KWA SABABU MLIKULA ILE MIKATE MKASHIBA.

27  Msikitendee kazi chakula chenye kuharibika, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele; ambacho Mwana wa Adamu atawapa, kwa sababu huyo ndiye aliyetiwa muhuri na Baba, yaani, Mungu”.

Na jitihada zao zote za kumtafuta awe mfalme, hata hakuwa mfalme wao, Yesu aliwaepuka. Kilichowatokea wale ndicho kinachotutokea kanisa la sasa. Biblia inasema…

Waebrania 13:8  “YESU KRISTO NI YEYE YULE, JANA NA LEO NA HATA MILELE.

9  Msichukuliwe na mafundisho ya namna nyingine nyingine, na ya kigeni; maana ni vizuri moyo ufanywe imara kwa neema, wala si kwa vyakula, ambavyo wao waliokwenda navyo hawakupata faida”.

 Ndugu Bwana Yesu hajabadilika kama watu wanavyombadilisha sasa, Ni yeye Yule, jana, na leo na hata milele!!!…maana yake tabia zako ni zile zile hazijabadilika, kama aliwakimbia wale makutano, waliotaka kumfanya mfalme wao, atatukimbia na sisi pia vile vile, kama tukimwendea kwa mtindo ule.

Kama Bwana Yesu atawakana siku ile watu waliotoa pepo kwa jina lake, na huku mioyo yao ipo mbali naye??..si zaidi wewe aliyekupa mali leo na bado ni mlevi?. Hao amewapa uwezo wa kutoa pepo lakini kawakana mwisho wa siku?..jiulize wewe uliyepewa nyumba na gari na tumbo lako kufunguliwa na bado unavaa kidunia, jiulize utasilimika vipi siku ile?, wewe uliyeponywa kimiujiza na bado hutaki kujikana nafsi yako na kumfuata Yesu, utasalimika vipi?, wewe uliyeponywa ugonjwa kimiujiza na bado hutaki kuuacha ulimwengu, jiulize utasalimikaje siku ile?..

Unadhani Bwana kukupa wewe mali, au mtoto, au kukuponya ugonjwa wako uliokuwa sugu, ndio kitu cha kwanza anachokitafuta kwako??..lengo la kukufanyia hayo ni ili tu ugeuke! Utubu na uwe mkamilifu kama yeye na si kwa lengo lingine. Ukitafsiri kwamba Bwana kakuponya ugonjwa wako kwasababu anapendezwa na wewe..fahamu kuwa umepotea!..Ukitafsiri kuwa Bwana kaifanikisha biashara yako kwasababu eti anataka uwe bilionea, fahamu kuwa umepotea!!.. Ameifanikisha hiyo biashara yako kusudi kwamba utubu na umrudie yeye, uwe mkamilifu. Lakini ukidhani kuwa ni kwasababu amependezwa na wewe, na moyoni ukijitumainisha kwamba ni mfalme wako, na Bwana wako, siku ile atakukana, pamoja na kwamba ni yeye ndiye aliyekufanikisha!!

Kama hujampokea Yesu maishani,  mlango wa neema bado upo wazi, ingawa hautakuwa hivyo siku zote. Huu ni wakati wako wa kumpokea Yesu, kwa kumwamini moyoni mwako, na kukiri kwa kinywa chako, na kuamua kwa dhati kuacha dhambi zote ulizokuwa unazifanya.. Unaziacha kwa vitendo, kama ulikuwa ni mlevi unavunja vikao na makundi yote ya ulevi, kama ulikuwa ni kahaba, unachoma nguo zote za kikahaba ulizokuwa unavaa ikiwemo suruali zote, na lipstick, wanja na mengineyo, kama ulikuwa unasikiliza miziki ya kidunia unaifuta yote katika simu yako, au popote pale ulipoihifadhi, kama ulikuwa ni shabiki wa mambo ya kidunia kama mipira, filamu, na mambo yanayofanana na hayo, unayaacha yote.

Na baada ya kufanya hivyo unatafuta ubatizo sahihi, kama bado hujabatizwa, kumbuka ubatizo sahihi ni ule wa maji tele, na kwa jina la Yesu Kristo, na baada ya hapo Bwana atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu, ambaye atakuongoza katika kuijua kweli yote ya maandiko, na kukusaidia kuushinda ulimwengu.

Bwana akubariki.

afadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Je! tunapaswa kukiamini Kitabu cha Henoko?

SWALI: Kitabu cha Henoko ndio kitabu kipi hicho, Je! Sisi kama wakristo tunapaswa kukiamini?


JIBU: Kitabu cha Henoko ni moja ya vitabu vya Apokrifa ambavyo viliandika kati ya miaka 200 kabla ya Kristo(KK), na  miaka 400 baada ya Kristo(WK). Vitabu hivi  vinaaminiwa na baadhi ya wakristo kuwa  vilihifadhiwa kwa siri, kutokana na kuwa vilikuwa na siri za ndani sana kuhusu Mungu na historia ya ulimwengu kwa ujumla, kiasi kwamba havikuweza kujumuishwa moja kwa moja kwenye biblia yenye vitabu 66 ambayo tunayo hivi sasa.

Lakini si kweli, vitabu hivi havikujumuishwa katika biblia takatifu kwasababu vilikuwa na siri za Mungu hapana badala yake vilionekana kujaa habari nyingi za kutungwa, ambazo zinakinzana na misingi ya imani ya Kikristo.

Sasa tukirudi katika hichi kitabu cha Henoko, kiligunduliwa kwenye miaka ya 1700 huko Ethiopia, baadaye kikasafirishwa mpaka Uingereza kwa ajili ya kutafsiriwa katika lugha nyingine, Kitabu hichi kilijulikana kama Henoko wa  Kwanza (1Henoko), kwasababu kulikuja kuwa pia na matoleo mengine yaliyofuata baadaye.

Vipande vya nyaraka vya kitabu hichi pia viligunduliwa huko Israeli mnao mwaka 1947, kwenye mapango yalikuwa katika fukwe za bahari ya chumvi (dead sea), Na kwenye mapango hayo kulionekana pia machapishi ya vitabu vyote vya agano la kale isipokuwa tu kitabu cha Esta, inasadikika ni vitabu ambavyo vilikuwa vimehifadhiwa huko na watu wa kale ambao waliishi kabla hata ya Kristo kuja duniani.

Sasa kitabu hiki kinamueleza Henoko ambaye alikuwa ni mtu wa saba kutoka Adamu kama tunavyosoma katika biblia Mwanzo 5:18-24…Henoko hakuonja mauti kama ilivyokuwa kwa wanadamu wengine, bali alinyakuliwa kama Eliya. Hiyo imekuwa ikawafanya watu wengi waamini kuwa mtu huyu alipewa siri nyingi za rohoni na kuziandika kwa ajili ya watu wa baadaye.

Hivyo kitabu hichi kilipogunduliwa, kilidhaniwa  kuwa mwandishi wake  ni Henoko, japo hilo jambo halikuthibitika kuwa ni kweli. Kitabu hichi kimejaa historia zinaeleza visa vya dunia ya kwanza kugharikishwa na maji, kinasema baadhi malaika wa Mungu  ambao walikuwa ni waangalizi wa huku ulimwenguni, ambao idadi yao ilikuwa ni 200 waliwaona binti za wanadamu, kisha wakawatamani, , hivyo wakashauriana washuke duniani wajitwalie wake, waishi nao, na kweli wakafanya hivyo  wakashuka duniani wakawapa mimba wanawake, ndio wakazaa wale majitu ambayo tunayasoma katika Mwanzo 6

Zaidi ya yote, malaika hawa kwa kuwa walikuwa na ujuzi, wakawafundisha wanadamu, kubuni silaha za chuma, kufanya uharibifu, wengine wakawafundisha wanadamu kufanya uchawi, na wengine kusoma nyota za mbinguni. Pamoja na hayo watoto wao waliowazaa wakawa wakatili kupita kiasi, ndio wale wanefili, wakawa wanaharibu kila kitu ikiwemo mimea, wanyama, mpaka wanadamu. Urefu wa majitu hayo ulikuwa ni futi 4500, sawa na Jengo la ghorofa 415. Jambo ambalo ni ngumu kusadikika,  Hakuna kiumbe cha namna hiyo kinaweza kuzaliwa na mwanamke. Japo wanefili kweli walikuwa ni wakubwa lakini sio kwa kiwango hicho.

Baadaye baadhi ya malaika wa mbinguni wakampelekea Mungu habari zao,  lakini Mungu akakataa kuwasamehe, akawafunga katika vifungo vya giza, ndio hapo Mungu akamwambia Henoko kuwa atakwenda kuiangamiza dunia kwa gharika.  Hii ndio habari ambayo inafahamika sana

Zipo habari nyingine katika kitabu hicho ambazo kiuhalisia hazina uhalisia wowote  na maandiko.

Tunapaswa tujue vitabu hivi vimejaa hadithi nyingi za kutungwa, ambazo ni sumu kwa Mkristo, na ndio maana huwezi kuziona vikijumuishwa katika biblia yenye vitabu 66 vilivyovuviwa na Roho Mtakatifu, kwasababu vinakinzana na misingi ya kweli ya maandiko.

Bwana Yesu alisema..

Mathayo 22:29 “Yesu akajibu, akawaambia, Mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu.

30 Kwa maana katika kiyama hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika mbinguni”.

Unaona? Hakuna andiko lolote linaloonyesha kuwa malaika wanaoa, au wanazaliana, malaika hawakuumbiwa viungo vya uzazi kama tulivyonavyo sisi, hawahitaji kuzaliana, wao tayari walishaumbwa, ndivyo walivyo na idadi yao tayari ipo kamili, Lakini kusema walishuka duniani, ni fundisho la uongo ambalo wakristo wengi wanaliamini mpaka leo, na chanzo chake walikitoa katika hichi kitabu cha Henoko.

Waliowaona binti za wanadamu wakawatamani, walikuwa ni watakatifu wa Mungu, ambao hao hawakujichanganya na mambo ya ulimwengu tangu mwanzo, bali walitumia sehemu kubwa ya maisha yao, kuliita jina la Bwana na kumwabudu Mungu soma Mwanzo 4:26 utalithibitisha hilo ndio ule  uzao wote wa Sethi (Wakina Henoko, Methusela, Na Nuhu).. Lakini binti za wanadamu walikuwa ni watu wa kidunia tu, ambao walitokea katika ule uzao wa Kaini..hao ndio tangu mwanzo walikuwa na ujuzi mkubwa, na hodari na pia wakatili ukisoma pale Mwanzo 4:16-23 utaona ni jinsi gani, uzao wa Kaini ulivyokuwa hodari, wenye ujuzi mwingine, lakini pia mwovu kwa uuaji, kama Baba yao alivyokuwa.

Baadaye sasa walipojichanganya mbegu ndipo Mungu akakasirika, akaghahiri na kuuangamiza ulimwengu wote, ni sawa na leo hii, Mungu aone, watakatifu wake wote, wanaiga na kufanya mambo ya ulimwengu, wanawake wanavaa vimini, wanatembea nusu uchi barabarani, wanaume watakatifu wanakuwa mashoga n.k. kiasi kwamba huwezi kuona tofauti yoyote kati yao na ulimwenguni, hapo kinachofuata ni Mungu kuuteketeza ulimwengu, ndivyo ilivyokuwa kwa watu wa kipindi kile. Watakatifu walijitofautisha kabisa na wana wa ulimwengu..

Hivyo hakuna sababu ya mkristo kuamini, moja kwa moja vyanzo ambavyo havipo katika biblia, kwasababu vingi kati ya hivyo vinakasoro nyingi na vimejaa hadithi nyingi zilizotungwa na wanadamu lakini sio kwa uvuvio wa Roho Mtakatifu.

Kwamfano kwasasa Kanisa Katoliki, limeamua kuchukua baadhi ya hivi vitabu vya Apokrifa na kuviongezea kwenye biblia takatifu yenye vitabu 66, kufikia 73. Vitabu vyenyewe ikiwemo Yudithi, Baruku, Yoshua bin Sira, Wamakabayo 1&2,  Hekima.

Vitabu hivi vinakinzana na misingi ya imani, kwamfano, vinafundisha kwenda toharani, yaani mtu mwenye dhambi anaweza kwenda mbinguni tena, lakini baada ya kupitishwa mahali panapoitwa toharani ili kutakaswa,.,Fundisho lingine ni kuwa Mungu, anasikia maombi ya wafu, mambo ambayo ni uongo, biblia inasema, mtu ameandikiwa kuishi mara moja na baada ya kifo ni hukumu (Waebrania 9:27).

Kwahiyo, vitabu vya Aprokifa, sio vya kuviamini, kama uaminivyo biblia, iwe ni kitabu cha Henoko, au kingine chochote kile nje ya vitabu 66 vya biblia sio vya kuiamini vinamakosa mengi na wakati mwingine vimejaa uongo mwingi, ambao unapotosha kabisa.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Kitabu cha YASHARI kinachozungumziwa katika 2Samweli 1:17-18, ni kitabu gani?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Chuo cha vita vya Bwana ni kipi?(Hesabu 21:14)

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 7 (Yeremia na Maombolezo)

UNYAKUO.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi nyumbani

Print this post

Je Mungu aliumba watu wengine kabla ya Adamu?

SWALI: Je Mungu aliumba watu wengine kabla ya Adamu?, maana tunasoma katika Mwanzo 1:27, alimwumba mwanamke na mwanamke, na tena tunaona anaumba tena mtu mwingine (Adamu) katika Mwanzo 2:7.


Jibu: Kitabu cha Mwanzo Mlango wa Kwanza kimezungumzia uumbaji wa Mungu kwa muhtasari  (yaani kwa ufupi), lakini tunapokwenda katika Mlango wa pili, ndio tunaona uumbaji ukielezewa kwa urefu zaidi. Kwahiyo mlango wa kwanza ni muhtasari wa uumbaji, ndio maana utaona vitu vinaelezewa kwa ufupi tu…Kwamfano utaona Mungu anasema..

Mwanzo 1:11 “Mungu akasema, Nchi na itoe majani, mche utoao mbegu, na mti wa matunda uzaao matunda kwa jinsi yake, ambao mbegu zake zimo ndani yake, juu ya nchi; ikawa hivyo

12 Nchi ikatoa majani, mche utoao mbegu kwa jinsi yake, na mti uzaao matunda, ambao mbegu zake zimo ndani yake, kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema,

13 Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya tatu.”

Hapo, uumbaji wa miti na mimea umeelezewa kwa kifupi sana, haijaelezwa ilitokeaje tokeaje… sasa ili tujue kwa undani zaidi, hiyo miti ilitokeaje tokeaje, ndipo tunakwenda katika mlango wa 2 wa kitabu hicho hicho cha mwanzo, tunaona ikielezewa vizuri zaidi..

Mwanzo 2:4 “Hivyo ndivyo vizazi vya mbingu na nchi zilipoumbwa. Siku ile Bwana Mungu alipoziumba mbingu na nchi

5 hapakuwa na mche wa kondeni bado, wala mboga ya kondeni haijachipuka bado, kwa maana Bwana Mungu hajainyeshea nchi mvua, wala hapana mtu wa kuilima ardhi;

6 ukungu ukapanda katika nchi, ukatia maji juu ya uso wote wa ardhi”

Unaona?..Kumbe Mungu aliposema nchi itoe majani na mche utoao mbegu, siku ile ile aliinyeshea nchi mvua na ndipo nchi ikazaa miti na mimea kadha wa kadha… Maana yake hakusema tu itokee halafu ikatokea kama tulivyosoma hapo katika hiyo Mwanzo 1:11, bali kulikuwa na hatua (process). Ambazo ndizo tulizokuja kuzisoma katika hiyo Mwanzo mlango wa pili.

Kadhalika Mungu aliposema katika Mwanzo 1:27 kwamba… “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba”.

Tunaona hapo uumbaji wa mtu umeelezwa kwa ufupi tu, haijaeleza ni jinsi gani huyo mtu alivyoumbwa, mwanaume na mwanamke walitokeaje tokeaji …je! Wote waliumbwa pamoja?..na je waliumbwa kwa malighafi gani?. Sasa majibu ya maswali hayo ndio tunayapata katika Mlango wa pili wa kitabu hicho hicho.. tusome,

Mwanzo 2:4 “Hivyo ndivyo vizazi vya mbingu na nchi zilipoumbwa. Siku ile Bwana Mungu alipoziumba mbingu na nchi

 5 hapakuwa na mche wa kondeni bado, wala mboga ya kondeni haijachipuka bado, kwa maana Bwana Mungu hajainyeshea nchi mvua, wala hapana mtu wa kuilima ardhi;

 6 ukungu ukapanda katika nchi, ukatia maji juu ya uso wote wa ardhi.

7 BWANA MUNGU AKAMFANYA MTU KWA MAVUMBI YA ARDHI, AKAMPULIZIA PUANI PUMZI YA UHAI; MTU AKAWA NAFSI HAI.

 8 Bwana Mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa Edeni, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya”.

Umeona hapo, biblia inasema Bwana Mungu akamfanya mtu kutoka kwenye mavumbi ya ardhi, jambo ambalo halikutajwa katika ile Mwanzo 1:27, na ukiendelea kusoma katika Mwanzo 2:18-24, utaona jinsi uumbaji wa mwanamke ulivyokuwa, kwamba alitwaliwa kutoka kwa mwanaume (ubavuni mwa mwanaume), jambo ambalo halikuelezwa katika ile Mwanzo 1:27.

Kwahiyo kitabu cha Mwanzo mlango wa kwanza ni muhtasari tu wa uumbaji, umeelezea kwa ufupi sana, na mlango wa pili ndio umeelezea kwa undani kidogo. Ni sawa na unaposoma kitabu Fulani labda cha jeografia, unapokifungua mwanzo kabisa utakutana na “yaliyomo”/“table of content”. Lengo la lile ni kukupa muhtasari na kukuongoza utakachokwenda kukisoma.. Na utaona kila kichwa kimeelezea kwa ufupi sana, lakini utakapokwenda katika kurasa zenyewe utaona mada zimeelezewa kwa urefu sana. Ndicho kilichopo katika kitabu cha Mwanzo mlango wa Kwanza..na wa pili..

Hivyo si kweli kwamba kuna watu wengine waliumbwa kabla ya Adamu. Adamu na Hawa ndio wanadamu wa kwanza kuumbwa.. Na walipoasi waliondolewa katika ile bustani ya Mungu Edeni, na kuanzia huo wakati, wote tunaozaliwa tunakuwa tunalibeba anguko lake. Mpaka tutakapozaliwa mara ya pili katika uzao wa Adamu wa pili Yesu Kristo, ambaye yeye hakutenda dhambi hata mara moja, ambaye alijaribiwa kama Adamu lakini hakutenda dhambi, huyo pekee ndiye amewekwa kuwa ukombozi kwetu.

Kila amwaminiye maandiko yanasema atapata ondoleo la dhambi zake, naye atakuwa haishi chini ya laana bali chini ya Baraka, lakini wote wasiomwamini hawatapata ondoleo la dhambi zao, na siku ya mwisho watatupwa katika ziwa lile la moto, aliloandaliwa shetani na malaika zake.

Je wewe ni mmoja wa waliomwamini au ambao hawajamwamini?.. Kama bado tambua kuwa upo chini ya laana ya anguko la Adamu, na hakuna namna yoyote unaweza kuhesabiwa haki bila kumpokea Yesu maishani mwako, haijalishi utafanya mangapi mazuri, kama humtaki Yesu hutamwona Mungu, kwasababu yeye ndiye Njia ya kufika mbinguni, wala hakuna mwingine.

Hivyo mpokee leo kwa kutubu dhambi zako zote, na kwa kudhamiria kuziacha kabisa na baada ya toba yako hiyo, nenda katafute ubatizo sahihi, kumbuka ubatizo sahihi ni ule wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo ambalo ndio jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu. Kwa kukamilisha hatua hizo tatu, yaani Imani, ubatizo na kupokea Ujazo wa Roho Mtakatifu, utakuwa umeukamilisha wokovu wako na Roho Mtakatifu atakuongoza katika kuijua kweli yote na kukupa nguvu za kuishinda dhambi.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Je! Adamu alikuwa na mwanamke mwingine anayeitwa Lilith?

MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.

Majina mbalimbali ya Mungu na maana zake.

VAZI KUU AMBALO MUNGU AMETUANDALIA KILA MMOJA WETU.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Rudi nyumbani

Print this post

“Yodi” ni nini kama tunavyoisoma katika Mathayo 5:18?

Jibu: Tusome,

Mathayo 5:18 “Kwa maana, amin, nawaambia ,Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka,yodi moja wala nukta moja ya torati haitaoondoka ,hata yote yatimie”.

Yodi ni neno lililotumika katika lugha ya Kiswahili cha zamani, lenye maana ya “herufi ndogo”.. kwa lugha ya kiingereza ni “small letter”. Katika sentensi yoyote huwa kunakuwa na herufi kubwa na herufi ndogo, sasa zile ndogo ndio zinazoitwa “yodi”.. Mfano tunaposema neno “Yesu ni Mungu”..Herufi kubwa hapo ni hiyo “Y” na “M” lakini hizo nyingine zote zilizosalia kama “e” “s” “u” “n” “i”  “u” ni YODI.

Kwahiyo Bwana Yesu aliposema kwamba hakuna hata “yodi” moja wala nukta itakayoondolewa hata yote yatimie maana yake.. ni kwamba hakuna herufi yoyote (hata ile iliyo ndogo kuliko zote, ‘yodi’) itakayobadilishwa katika maneno ya torati, kwasababu maneno ya Mungu hayabadilii. Ndio maana ukianzia juu kidogo utaona anasema hakuja kuitangua torati bali kuitimiliza..

Mathayo 5:17 “Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza.

18 Kwa maana, amin, nawaambia ,Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati haitaoondoka ,hata yote yatimie”.

Mathayo 24:35 “Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe”.

Pale torati iliposema “usizini”..Bwana Yesu hakuja kulibadilisha hilo andiko, bali alikuja kulitimiliza kwa kusema “mtu amtazamaye mwanamke amekwisha kuzini naye nafsini mwake”. Hapo hajaondoa chochote, bali ameongezea dawa. Torati inaposema “usiue” Bwana Yesu alisema “amwoneaye ndugu yake hasira hana tofauti na muuaji, hivyo itampasa hukumu tu kama muuaji”. Hapo hajaitangua wala kulibadilisha bali ameitimiliza, na sheria nyingine zote za kwenye torati ni hivyo hivyo..

Je wewe bado una chuki kwa ndugu zako au maadui zako?,ukijitumainisha kwamba wewe si muuaji?.. bado unatamani ukijitumainisha kwamba wewe sio mzinzi??, bado unavaa nusu uchi,na suruali ukijitumainisha kwamba wewe si kahaba?? (kasome Mithali 7:10 ujipime kama wewe ni kahaba au la kwa mavazi yako), bado unajichua na kunatazama pornography ukijitumainisha kwamba wewe si mwasherati?, bado ni mshabiki wa mambo ya kidunia kuliko kitu kingine chochote ukijitumainisha kwamba wewe si wa kidunia??.

Kama unafanya mojawapo ya hayo, au yote, wakati wa kumkaribisha Mwokozi ndani ya maisha yako ni huu?..Usingoje kesho wala baadaye, saa ya wokovu ni sasa, na wakati uliokubaliwa ndio huu.. wakati wa kukimbilia Kalvari, Bwana akuokoe na kukutua mzigo ndio huu, sio kesho, kwasababu hujui kesho yako itakuwaje, labda leo ndio mwisho wako wa kuishi duniani, au leo ndio siku parapanda ya mwisho itakapolia, jiulize, unyakuo leo ukipita utakuwa wapi??.. Hivyo fanya uamuzi wa kumgeukia Yesu leo kwa kutubu dhambi zako zote kwake, na kwenda kubatizwa katika ubatizo wake wa maji tele (Yohana 3:23), na kwa jina la Yesu Kristo (Matendo 2:38), na Bwana atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu, atakayekuongoza katika kweli yote ya maandiko.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Kwanini Yesu aliwakataza mitume wake kumdhihirisha?

Mlima Gerizimu na Ebali ni ipi, na umuhimu wao rohoni ni upi?

Amri zilizo ndogo alizozizungumzia Yesu ni zipi?

RUDI KUMPA MUNGU UTUKUFU.

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki;

SWALI: Warumi 5:7 “Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki; lakini yawezekana mtu kuthubutu kufa kwa ajili ya mtu aliye mwema”.

Bwana Yesu asifiwe mtumishi wa Mungu, Naomba ufafanuzi wa hilo andiko na pia nipate  kujua tofauti kati ya mtu mwenye haki na mtu mwema.


JIBU: Pamoja na kwamba Bwana Yesu kuja hapa duniani kuwaokoa watu waliopotea kabisa, (yaani watu wenye dhambi wasio na vimelea vyovyote wa utu, kama vile wauaji, wahalifu, mafisadi n.k.) alikuja pia kuwaokoa watu walio wema.

Sasa tukirudi kwenye mstari huo tunaona mwandishi anajaribu kutofautisha  kati ya mtu mwema na mtu mwenye haki.

Mtu mwenye haki ni yupi?

Mtu mwenye haki ni mtu mkamilifu sana, asiyekuwa na kosa lolote mbele za Mungu, Mtu wa namna hii kiuhalisia hajawahi kuwepo tangu duniani iumbwe. Kama wangekuwepo hakukuwa na sababu ya Yesu Kristo kushuka hapa duniani, na kufa kwa ajili yao, wapate wokovu, ya nini sasa? Wakati tayari wanaoukamilifu wote ndani yao..hakuna doa lolote ndani yao?

Na ndio maana hapo inasema.. ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki..

Lakini mtu mwema, ni mtu ambaye sio mwovu sana, ni mtu ambaye anajaribu kuishi maisha ya kawaida tu katika jamii, anajiheshimu, anawasaidia wengine, anao utu, anajitahidi kutenda mema kwa bidii na kufanya mambo yake kwa utulivu bila kuvunja sheria yoyote ya jamii husika au nchi n.k. Lakini katika jitihada zake zote, bado hajaweza kufikia kipimo cha yeye kuwa mtu mwenye haki mbele za Mungu..Yaani nguvu zake bado hazijajitosheleza kumfanya awe mkamilifu..hao ndio watu wema mwandishi anaowazungumzia hapo. Na ndio maana ukianzia mstari wa juu anasema;

Warumi 5:6 “Kwa maana HAPO TULIPOKUWA HATUNA NGUVU, wakati ulipotimia, Kristo alikufa kwa ajili ya waovu.

7 Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki; lakini yawezekana mtu kuthubutu kufa kwa ajili ya mtu aliye mwema”.

Unaona anasema “hapo tulipokuwa hatuna nguvu”, ikiwa na maana tulishajaribu kujitahidi kwa nguvu zetu na kwa matendo yetu kumpendeza Mungu lakini bado tukashindwa kuufikia ule ukamilifu…Na  ndio Kristo alikuja kutufia pale msalabani, ili sasa kwa kumwamini tu yeye, tuhesabiwe haki mbele za Mungu.

Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa, kama tungekuwa wenye haki, basi Kristo asingekuja duniani, lakini kwasababu sote tumepungukiwa na utukufu wa Mungu,  (nikiwa na maana watu waovu sana na wa kawaida), Sote tunamuhitaji Kristo ayabadilishe maisha yetu. Kwasababu pasipo yeye, haijalishi tuna dini nzuri kiasi gani, tunafanya mazuri kiasi gani,  tunasaidia maskini wengi kiasi, bado hutuwezi kumpendeza Mungu, bila Kristo. Kwasababu hayo tayari yalishashindikana tangu zamani.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

JE NI KWELI SAMAKI NGUVA YUPO?

USIOMBE MAOMBI YASIYOKUWA NA MAJIBU NA WALA USIMTUKANE MUNGU.

Alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru

ESTA: Mlango wa 4

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

KOIKOI ANGANI AJUA NYAKATI ZAKE ZILIZOAMRIWA.

Yeremia 8:7 “Naam, koikoi angani ajua nyakati zake zilizoamriwa; na hua na mbayuwayu na korongo huangalia wakati wa kuja kwao; bali watu wangu hawazijui amri za Bwana”.

Koikoi, mbayuwayu na korongo ni ndege wa ajabu sana, ni ndege wenye uwezo wa kusoma majira ya dunia, Na hiyo imewasaidia sana, kuishi maisha ya salama salmini huku duniani, pasipo kukumbana na changamoto zozote  zisizo na maana.

Hawa ni ndege ambao kikikaribia kipindi cha baridi wanahama wote waeneo yao wanayoishi kwa muda, na kusafiri umbali mrefu sana, kwenye pembe ya pili ya dunia kutafuta msimu tulivu aidha wa vuli au  wa joto ulipo wakatulie, kisha baadaye hali ya baridi ikishakwisha wanarudi katika makazi yao ya awali kuendelea na maisha yao ya kawaida.

Kumbuka baridi tunayoizungumzia ni ile baridi haswaa, ya kutengeneza barafu iliyopo huko nchi za ulaya, ambayo hata mtu wa kawaida akikaa nje masaa machache tu anageuka kuwa jiwe la barafu, haijalishi atavaa masweta makubwa kiasi gani.. Baridi ya namna hiyo watu wanaoishi huko wanatumia muda wao mwingi kuwepo ndani, na hata kazi zao wanazifanyia ndani katika nyumba zilizojengwa kitaalamu kuhifadhi joto ndani, kwani nyumba za kawaida kama hizi zetu, kule hazijengwi kwasababu zinapitisha baridi, kiasi kwamba ukibaki ndani yake, ukakaa huko mpaka asubuhi ukiamka umeganda. Huku kwetu Afrika hatuna baridi ya namna hiyo.

Sasa, ndege hawa, wanaelewa kabisa kwa namna ya kawaida hawawezi kuishi katika mazingira hayo ya baridi kali, kwasababu hata viota vyao vitaganda.. Sasa ili kulitatua hilo tatizo inawagharimu wahame kwa muda, ndio hapo wanasafiri maelfu ya kilometa wanakuja mpaka huku kwetu Afrika, au nchi nyingine zenye joto, wanakaa  huko mpaka msimu wa baridi  utakaposhakwisha kule Ulaya ndio wanarudi sasa, kuendeleza maisha yao ya sikuzote.

Sasa Mungu ametumia mfano wa ndege hawa wasio na akili, kutushangaa sisi wanadamu wenye akili timamu kwanini hatujui hukumu zake alizoziweka hapa duniani..anasema..

“Naam, koikoi angani ajua nyakati zake zilizoamriwa; na hua na mbayuwayu na korongo huangalia wakati wa kuja kwao; bali watu wangu hawazijui amri za Bwana”

Hii ikiwa na maana tunashindwa kujua wakati wa neema ni upi, na wakati wa hukumu za Mungu ni upi.. Sisi tupo tu hatujui majira yetu, tunadhani wakati wote, hii neema ya wokovu itaendelea kuwepo, tunadhani wakati wote, hali itakuwa kama ilivyo sasa hivi, utahubiriwa injili kama unavyohubiriwa sasa hivi..

Ndugu yangu, fahamu kuwa neema hii inakwenda kuisha siku sio nyingi, Dhiki kubwa ambayo haijawahi kutokea tangu dunia iumbwe na wala haitakaa iwepo itakwenda kutokea ulimwenguni kote..Dalili zote zinaonyesha, pengine katika wakati wetu huu tunaoishi tutayashuhudia hayo..Haya majira ya neema ndio yanaishia hivyo, muda huu tulionao ni wa nyongeza tu, dunia ingepaswa iwe imeshakwisha tangu zamani, lakini kwasababu tu ile nuru ndogo ya jioni ipo ndio maana unaona mambo bado yapo hivi..

Tumeshafikia wakati ambao Yesu hatuhubirii  tena injili ya kutuvuta kwenye wokovu, kama ilivyokuwa zamani bali anatuhubiria injili ya kuthibitisha ulichokiamini. Sikiliza anavyosema..

Ufunuo 22:10 “Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.

11 Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa.

12 Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo”.

Unaona, hiyo yote ni kwasababu ya unafki tulionao sasa, kwasababu kama tunaweza kuyatambua majira ya nchi, kwamba huu ni msimu wa masika na hivyo tunaanza kuyaandaa mashamba yetu kabla ya mvua kunyesha, au tunahama mabondeni mapema mafuriko yasitukute, inakuwaje basi, tunashindwa kuzitambua siku hizi kuwa ni siku za mwisho? Korona inakufundisha nini? Vimbunga vinakufundisha nini, Hili wimbi la manabii wa uongo unaloliona leo hii limezuka duniani kwa ghafla linakufundisha nini? . Bado tu huoni, hizo ni dalili za wazi kabisa ambazo zinatutambulisha kuwa tukio la unyakuo lipo karibu?

Yesu alisema..

Luka 12:54 “Akawaambia makutano pia, Kila mwonapo wingu likizuka pande za magharibi mara husema, Mvua inakuja; ikawa hivyo.

55 Na kila ivumapo kaskazi, husema, Kutakuwa na joto; na ndivyo ilivyo.

56 Enyi wanafiki, mwajua kuutambua uso wa nchi na mbingu; imekuwaje, basi, kuwa hamjui kutambua majira haya”?

Itakuwa ni ajabu sana tukishindwa akili na akina koikoi. Tujitathimini sana, tuamke katika usingizi huu mzito, hukumu ya Mungu juu ya ulimwengu wote ipo karibu. Kama upo nje ya safina, anza safari upesi, mkimbilie Kristo kwa kumaanisha kabisa kwa moyo wako wote akuokoe, kwasababu hatuna muda mrefu hapa duniani,

 mbingu na nchi zitapita lakini maneno ya Bwana Yesu hayatapita milele.

Mbingu ipo,lakini pia kuzimu ipo, uchaguzi ni wa wako,

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

WAENDEE WANA WA ISAKARI, UWE SALAMA.

KWASABABU MUDA TULIOBAKIWA NAO SI MWINGI.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

Rudi nyumbani

Print this post