Kwanini Yesu aliwakataza mitume wake kumdhihirisha?

Kwanini Yesu aliwakataza mitume wake kumdhihirisha?

SWALI: Shalom ndugu wapendwa! Naomba kuuliza kwa nini Yesu awakataze akina Petro wasiseme kwa watu kwamba yeye ni KRISTO kama ilivyo kwenye Mathayo 16:20

JIBU:

Kwa faida ya wengi tusome habari yote inayoelezea hilo tukio..

Mathayo 16:13 “Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani?

14 Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii.

15 Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?

16 Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.

17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.

18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.

19 Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni.

20 NDIPO ALIPOWAKATAZA SANA WANAFUNZI WAKE WASIMWAMBIE MTU YE YOTE ya kwamba yeye ndiye Kristo”.

Sasa ukisoma vitabu vyote vya injili utagundua sio tu katika tukio hilo aliwakataza wanafunzi wake wasimdhihirishe, bali pia yapo matukio mengine mbalimbali aliwakataza watu wasimdhihirishe, utaona kuna wakati aliwazuia makutano aliowaponya wasimtangaze..(Mathayo 8:4) Wakati mwingine aliyazuia pia  mapepo aliyoyatoa yasimtangaze,

Marko 3:11 “Na pepo wachafu, kila walipomwona, walianguka mbele yake, wakalia wakisema, Wewe ndiwe Mwana wa Mungu. 12 Akawakataza sana, wasimdhihirishe”.

na pia utaona kuna wakati Bwana alipojidhihirisha kwa mitume wake, wale 3 kule mlimani kwa mavazi ya kumeta-meta aliwaambia maneno hayo hayo.

Lakini kwanini awazuie watu kumdhihirisha?

Sio kwamba aliogopa, au alikuwa hataki kujulikana hapana, lakini aliwazuia kwasababu Ushuhuda wake ulikuwa bado haujakamilika. Ilimpasa kwanza ayatimize yote aliyoandikiwa kama mkombozi wa huu ulimwengu, kisha yakishakamilika, ndipo sasa habari hizo zihubiriwe rasmi kwa watu wote, Na ndio maana utaona sehemu nyingine anasema, subirini mpaka nitakapofufuka kutoka katika wafu ndipo mhubiri habari zangu, myasimulie haya.

Mathayo 17:5 “Alipokuwa katika kusema, tazama, wingu jeupe likawatia uvuli; na tazama, sauti ikatoka katika lile wingu, ikasema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye; msikieni yeye.

6 Na wale wanafunzi waliposikia, walianguka kifulifuli, wakaogopa sana.

7 Yesu akaja, akawagusa, akasema, Inukeni, wala msiogope.

8 Wakainua macho yao, wasione mtu ila Yesu peke yake.

9 Na walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu aliwaagiza, akasema, MSIMWAMBIE MTU YE YOTE HABARI YA MAONO HAYO, HATA MWANA WA ADAMU ATAKAPOFUFUKA KATIKA WAFU.

Hapo ndio lile Neno la Yesu alilolisema katika Mathayo 10:27 lilipokuja kutimia..

Mathayo 10:27 “Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru; na msikialo kwa siri, lihubirini juu ya nyumba”.

Ni jambo la kawaida hata sasa  kitu chochote ambacho kitatumiwa na uma, huwa kinajaribiwa kwanza na watu wachache, kisha kikishathibitishwa, au kukamilishwa ndipo kinapoachiwa kwa uma mzima kutumiwa.

Hivyo, sababu ya yeye kuzuia mambo yake mengi yasidhihirishwe kwa wakati ule ni kwasababu ushuhuda wake ulikuwa haujamilika bado. Lakini sasa umeshakamilika na ndio maana tunazitangaza habari za Yesu wazi wazi kwa wote bila kumficha mtu chochote.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.

Nini maana ya “Tumejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii”?

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Kwanini  vizazi vya ukoo wa Yesu vinajipinga katika Mathayo na Luka.

Kiango na Pishi ni nini (Mathayo 5:15)?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Anonymous
Anonymous
2 years ago

Thanks n be blessed.