Title June 2024

Je kumwimbia Mungu kwa kucheza ni sahihi kibiblia?

Jibu: Kuna mambo makuu mawili ya kuzingatia katika kulitafakari hili.

    1. KWANINI UNACHEZA

    2. NACHEZAJE

Tutazame moja baada ya lingine.


     1. KWANINI UNACHEZA!

Tafakari umempa mtoto kitu anachokipenda, au mwanamichezo kashinda mchezo wake, au mwanafunzi kapata taarifa za kufaulu mitihani yake, huwa ipo furaha ambayo inaweza kumpelekea kuruka ruka kwa shangwe.

Sasa furaha ya namna hiyo inayompelekea kuruka rukwa kwa shangwe haina nia ya Maonyesho, au majivuno, bali ni mwitikio wa jambo jema linaloendelea au lililotokea.

Na kadhalika tunapofanyiwa jambo na MUNGU (Ambaye kwaasili huwa haishi matukio wala miujiza) zipo hisia zinazoambatana na shangwe, ambapo shangwe hiyo inaweza kuambatana na kuimba kwa kuruka ruka kama ndama!.

Raha ya namna hii inayoambatana na kuruka ruka na kucheza cheza tutaipata Zaidi siku ile tutakapomaliza mwendo, na kutangaziwa na BWANA KWAMBA TUMESHINDA!!, NA HIVYO TUNAUINGIA ULE MJI MTAKATIFU, NA KUKAA HUKO MILELE… Hapo baba, au mama hata kama hupendi kucheza utacheza tu!!.

Malaki 4:2 “Lakini kwenu ninyi mnaolicha jina langu, jua la haki litawazukia, lenye kuponya katika mbawa zake; nanyi mtatoka nje, NA KUCHEZA-CHEZA KAMA NDAMA WA MAZIZINI”.

Sasa ikiwa kuna ahadi ya sisi kucheza cheza huko mbeleni tutakapomaliza maisha haya na kutangaziwa ushindi.. vipi vipindi vidogo vidogo ambavyo Mungu anatupa ushindi hapa duniani?.. kwamba tulikuwa tunaumwa kiwango cha kufa, sasa Bwana katuponya, ndoa zilikuwa zinayumba sasa Bwana kazisimamisha.

Watoto walikuwa wanasumbua sasa Bwana kawatengeneza, Wokovu ulikuwa huna sasa Bwana kakupa… Kwasababu kama hizo wakati mwingine shangwe inaweza kuzidi mpaka kufikia hatua ya kucheza na kuruka ruka kama ndama huku ukimwimbia Bwana. (Hapo inakuwa ni wewe na Bwana na si wewe na mtu).

Unapozitafakari hizo sababu na nyingine nyingi, hauhitaji au husubiri uambiwe umshangilie Mungu, bali hiyo hali itatoka tu yenyewe ndani yako, na wala haitakuwa na lengo la kutazamwa na watu.

      2. UNACHEZAJE

Hili ni jambo la pili la kuzingatia.. UNACHEZAJE!!.. Ukiona unatafuta mtindo/style ya kucheza wakati wa Sifa, hapo kuna jambo la kutafakari!!!.. Sifa zinazozalika kwa kutafakari matendo makuu ya Mungu, hazinaga step, hazinaga kanuni maalumu, na pia zina staha!!..

Huwezi kumshangilia Bwana kwa staili za disko,..huwezi kutikisa makalio kama wafanyavyo wanenguaje wa disko..huwezi kucheza kwaito, na kushikana shikana na mwingine kama watu wa duniani wafanyavyo.. wengine wapo nusu uchi halafu wanasema wanacheza!..hiyo ni hatari sana.

Sifa za namna hiyo sio kutoka katika roho, bali na za NIA ya mwilini,..ambazo lengo lake kuu ni kutazamwa  na watu na kusifiwa nao au kuwapendeza..na ndizo ambazo mkristo hapaswi kuzifanya.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba iwe katika kuabudu, au kusifu, au kuruka ruka ni lazima yote yafanyike kwa staha na kwa utukufu wa Mungu.

Wafilipi 4:8 “Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je tunaruhusiwa kushirikiana na wasanii wa kidunia katika kumwimbia Mungu?

Jicho kucheza ni ishara ya nini?

NAFASI YAKO NI IPI KATIKA MWILI WA KRISTO?

Nini maana ya Shangwe ya waovu ni kwa muda kidogo Ayubu 20:4

HAUWEZI KURUKA MADARASA YA MUNGU!

Rudi Nyumbani

Print this post

Ukaufu ni nini? (Kumbukumbu 28:22).

Swali: Ukaufu ni nini na Koga ni nini kama tunavyosoma katika Kumbukumbu 28:22?


Jibu: Turejee.

Kumbukumbu 28:22 “Bwana atakupiga kwa kifua kikuu, na kwa homa, na kwa kuwashwa, na kwa hari ya moto, na kwa upanga, na kwa UKAUFU, na kwa KOGA; navyo vitakufukuza hata uangamie”

“Ukaufu” ni ugonjwa wa mazao unaotokana na utandu (fangasi), tazama picha juu. Ugonjwa huu unaposhambulia zao la nafaka basi linapata mabaka mabaka na kisha kunyauka na mwishowe kutozalisha chochote.

Sasa hapo Bwana alikuwa anasema na watu wake  Israeli (ambao ni sisi pia) kwamba tutakapomwacha Bwana na kufuata miungu mingine na kuiabudu basi tutakuwa tumefungua milango ya laana juu ya maisha yetu,  kwani tutapigwa kwa magonjwa ya mwilini lakini pia mazao ya mashamba yetu yatapiwa kwa magonjwa.. na pia tutapigwa kwa misiba na majanga ya nchi.

Mfano wa magonjwa ya mwilini ni hayo yaliyotajwa hapo (Kifua kikuu, homa na kuwashwa).. na mfano wa magonjwa yatakayoshambulia mimea yetu hata tusipate chakula ni hayo yaliyotajwa hapo (Koga na UKAUFU),

Koga ni utandu mweupe unaoshambulia mimea ambao nao pia ukikamata zao la chakula, basi zao lile linadhoofika na hatimaye kufa. (Tazama picha chini).

koga ni nini

Lakini pia mfano wa majanga nchi yatakayotupata ikiwa tutamwacha Bwana ni hayo yaliyotajwa hapo juu (hari ya moto na upanga)..Hari ya moto inayozungumziwa hapo ni vipindi vya ukame na jua kali na upanga unaozungumziwa hapo ni vita (au umwagaji damu).

Na sio kwa mambo hayo tu, bali pia kwa mambo mengine mengi yaliyotajwa hapo katika Kumbukumbu 28 na yasiyotajwa… yote yatatupata ikiwa tutamwacha BWANA MUNGU WETU, na kujitumainisha katika mambo mabaya…

Kumbukumbu 28:58 “Kama hutaki kutunza kufanya maneno yote ya torati hii yaliyoandikwa katika kitabu hiki, upate kulicha jina hili la fahari na utisho, Bwana, MUNGU WAKO;

59 ndipo atakapofanya Bwana mapigo yako yawe ya ajabu, na mapigo ya uzao wako, mapigo makubwa kwa kweli, ya kudumu sana, na magonjwa mazito ya kudumu sana.

60 Naye atakurejezea maradhi yote ya Misri juu yako uliyokuwa ukiyaogopa, nayo yataambatana nawe.

61 Tena kila ugonjwa, na kila pigo yasiyoandikwa katika kitabu cha torati hii, atakutia nayo Bwana juu yako, hata utakapokwisha kuangamizwa”.

Lakini kinyume chake, ikiwa tutamtii Bwana MUNGU WETU, na kwenda katika njia zake, basi tutafanikiwa sana kufungua milango ya Baraka nyingi, wala hatutapatwa na hayo yote (Saswasawa na Kumbukumbu 28:1-14)

Bwana atusaidie na kutuneemesha.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAGONJWA YAKUPATAYO MARA KWA MARA.

Kwanini kuwe na kitabu Cha kumbukumbu la Torati na kwanini kiitwe vile?

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

ATAANGAMIZWA NA KUTENGWA NA WATU WAKE.

Ukoma wa nyumba ulifunua nini zamani?

Rudi Nyumbani

Print this post

KILA SILAHA ITAKAYOFANYIKA JUU YAKO HAITAFANIKIWA.

Jina la BWANA wetu YESU KRISTO lihimidiwe daima.

Neno la Mungu linasema..

Isaya 54:17 “KILA SILAHA ITAKAYOFANYIKA JUU YAKO HAITAFANIKIWA Kila na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa Bwana, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema Bwana”.

Hapo anasema “kila silaha itakayofanyika haitafanikiwa” na si “kila shambulizi halitafanikiwa”.. Maana yake katika tu mwanzo wa maandalizi ya silaha, huo ndio hautafanikiwa!..

Kivipi?

Silaha za zamani zilikuwa ni Mikuki, Panga na Mishale na nyinginezo baadhi ambazo zote zilikuwa zinatengenzwa kwa vyuma na Wahunzi..(Sasa kufahamu mengi kuhusu Wahunzi na jinsi wanavyofua vyuma basi fungua hapa >>> Mhunzi ni nani? (Isaya 54:16) ).

Hivyo Wahunzi walikuwa wanayeyusha chuma kisha wanakitengeneza kwa umbile la silaha waitakayo kama ni panga, au kisu au mkuki.. Sasa hapa biblia inasema silaha yoyote inayotaka kutengenezwa na hawa wahunzi, haitafanikiwa..

Maana yake wahunzi wakiwa katika zile hatua za kuyeyusha chuma, basi hawafanikiwa kufikia hitimisho la kuikamilisha  ile silaha, maana yake shughuli yao itaishia katikati na hakuna silaha yoyote itakayozaliwa. (aidha wakiwa katika utengenezaji wataungua moto, au watapungukiwa na malighafi, au watapata hitilafu nyingine yoyote ambayo itawafanya wasilamize ile kazi).

Watabaki na chuma kisicho na umbile lolote la kisu, au sime, au panga au mkuki..

Isaya 54:16-17 “Tazama, nimemwumba MHUNZI avukutaye moto wa makaa, akatoa silaha kwa kazi yake; nami nimemwumba mharibu ili aharibu…kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa”

Vile vile na agano Mungu analoingia na watumishi wake ni agano la namna hiyo hiyo, maana yake hawataona hata dalili ya silaha juu ya maisha yao kwani Bwana ataziharibu kabla hazijakamilika…

Kama ni uchawi ndio silaha ya adui, basi wakati tu unapikwa huko kwenye vibuyu na miti, na makaburini na habarini au katika madhabahu za baali basi utaungua moto kabla haujakamilika (wala hutajua kama kuna mashambulizi yalikuwa yameandaliwa dhidi yako, hutaona hata hiyo dalili..mambo yanaharibika kabla hayakamilika)… baadaye sana ndio utakuja kusikia ushuhuda kwamba kuna njama zilipangwa juu yako na zikashindikana (kama Bwana ataruhusu ujue).

Kama magonjwa ndio silaha ya adui anayoisuka juu yako, akiwa katika kiwanda chake cha kukutengenezea hayo, Bwana atasimama kinyume chake na kuziharibu hizo hila, na hutaona chochote na wala kujua chochote kwani hata dalili haitaonekana.

Kama ni kuondolewa kazi ndio silaha ya adui, basi kabla hata hiyo mipango kukamilika, itafutwa na Bwana na kuharibiwa..(utakuja kujua tu baadaye kama Bwana ataruhusu ujue).

Na hiyo ndio sababu kwanini kuna umuhimu wa kumshukuru Mungu kila wakati kwani kuna vitu vingi sana Bwana anatuepusha navyo pasipo hata kuona dalili yake..

Kama ni visa ndio silaha ya adui ili upotezi hiki au kile Bwana alichokupa, basi kabla hivyo visa havijakamilika Bwana ataviharibu.. Hiyo ndio maana ya “kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa”.

Lakini hiyo ni kama wewe ni mtumishi wa Mungu (Maana yake unayempendeza Mungu na kuyafanya mapenzi yake)

Isaya 54:17 “SILAHA ITAKAYOFANYIKA JUU YAKO HAITAFANIKIWA Kila na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa Bwana, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema Bwana”

Lakini kama upo nje ya Kristo, basi fahamu kuwa kila silaha itakayofanyika juu yako itafanikiwa na itakudhuru.. Hivyo usiruhusu silaha yoyote ifanikiwe juu yako… Ni sharti iharibiwa ikiwa katika hatua zake za matengenezo, na wenye nguvu za kuweza kuharibu silaha hizo ni wale tu walio ndani ya imani.

Je umempokea Bwana YESU?.. Kama bado huu si wakati wa kupoteza muda, wala kungoja ngoja..ni wakati wa kujiokoa nafsi yako, wala si wakati wa kutazama nyuma, kama mke wa Lutu, bali ni wakati wa kupiga mbio na kuikimbia Sodoma..

Luka 17:32  “Mkumbukeni mkewe Lutu.

33  Mtu ye yote atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza; na ye yote atakayeiangamiza ataiponya”

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.

TUZIDI KUWA HODARI KATIKA BWANA.

Mata ni nini (Mwanzo 27:3).

Kombeo ni nini? Teo ni nini katika biblia?

Fahamu ni nani aliye mwandishi wa kitabu cha Mathayo.

Rudi Nyumbani

Print this post

Mhunzi ni nani? (Isaya 54:16)

Jibu: Turejee..

Isaya 54:16 “Tazama, nimemwumba MHUNZI avukutaye moto wa makaa, akatoa silaha kwa kazi yake; nami nimemwumba mharibu ili aharibu”

Mhunzi/ Wahunzi  wanaozungumziwa katika biblia ni watu “wanaofua Vyuma, shaba, fedha au dhahabu”. Maana yake wanaviyeyusha vyuma hivyo au madini hayo na kuyaumba kwa maumbile mbalimbali kama silaha na urembo.

Tofauti ya Mhunzi na mfinyanzi, ni kwamba Mfinyanzi yeye anashughulika na udongo, anafanya kazi ya kutengeneza vyombo au zana kupitia udongo, (Soma Isaya 41:25, Isaya 64:8 na Yeremia 18:6) lakini “Mhunzi” yeye anatumia vitu vya metali kama vyuma, fedha, shaba au dhahabu kutengeneza vito au zana za kazi au silaha.

Mistari mingine katika biblia inayotaja Wahunzi (wafua vyuma/dhahabu/shaba au fedha) ni pamoja na 1Samweli 13:19, 2Wafalme 24:16, Isaya 44:12, Isaya 46:6, Yeremia 24:1, Zekaria 1:20, Matendo 19:24, na 2Timotheo 4:14.

Je umempokea BWANA YESU?. Kama bado fahamu kuwa upo katika hatari kubwa yenye mwisho mbaya, ni vyema ukafanya maamuzi leo ya kumpokea YESU kama BWANA na MWOKOZI wa maisha yako, kabla ya kumaliza muda wako wa kuishi, kwani hakuna nafasi ya pili baada  ya kifo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Sala ya baraka (Hesabu 6:24-26).

NDUGU,TUOMBEENI.

KWANINI NABII ISAYA ALIAGIZWA KUHUBIRI UCHI?

Mchuuzi ni nani? (Hosea 12:7).

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 12 (Kitabu cha Isaya)

Rudi Nyumbani

Print this post

Majumbe ni watu gani? (Mwanzo 36:15).

Jibu: Turejee..

Mwanzo 36:15 “Hawa ndio MAJUMBE wao wana wa Esau; wana wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau; JUMBE Temani, JUMBE Omari, JUMBE Sefo, JUMBE Kenazi,

16 JUMBE Kora, JUMBE Gatamu, jumbe Amaleki. Hao ndio MAJUMBE, waliotoka kwa Elifazi katika nchi ya Edomu. Hao ni wana wa Ada”.

Jumbe/Majumbe ni “WAKUU WA KOO” (machifu),

Majumbe walikuwa ni watu wenye heshima katika ukoo, na walijulikana sana katika nchi yote… na pia Majukumu yao yalikuwa ni kutatua migogoro ya kifamilia, na migawanyo ya ardhi kwa familia.

Katika biblia majumbe waliokuwa maarufu ni Majumbe wa wana wa Esau, (Hawa ndio waliokuwa Majumbe maarufu na wenye heshima kuliko Majumbe wa kabila nyingine za watu).. Jamii yao iliwapa heshima Majumbe hawa kiasi kwamba wakajulikana mpaka nje ya mipaka.

Kutoka 15:14 “Kabila za watu wamesikia, wanatetemeka, Wakaao Ufilisti utungu umewashika.

15 Ndipo MAJUMBE WA EDOMU wakashangaa, Watu wa Moabu wenye nguvu tetemeko limewapata, Watu wote wakaao Kanaani wameyeyuka”.

Sehemu nyingine katika biblia zilizotaja Majumbe ni pamoja 1Nyakati 1:51-54, Esta 1:3, Esta 9:3

Lakini pamoja na kwamba “Majumbe wa Esau” walikuwa maarufu na waliojulikana sana na wenye heshima, lakini kutoka huko hakutoka “MKUU WA UZIMA (YESU KRISTO), lakini badala yake kutoka katika Ukoo mdogo sana, (wa Majumbe ya Yuda), alitoka Mwokozi wa ulimwengu, Haleluya!!..

Mathayo 2:5 “Nao wakamwambia, Katika Bethlehemu ya Uyahudi; kwa maana ndivyo ilivyoandikwa na nabii,

6  Nawe Bethlehemu, katika nchi ya Yuda, HU MDOGO KAMWE KATIKA MAJUMBE WA YUDA; Kwa kuwa kwako atatoka mtawala Atakayewachunga watu wangu Israeli”.

Je umemwamini Bwana YESU?.. Kama bado fahamu kuwa tunaishi majira ya kurudi kwake, na ule mlango unazidi kuwa mwembamba kila siku na ile njia ya upotevuni inazidi kuwa pana kwa kadiri muda unavyozidi kwenda, hivyo usikawie kusimama katika wokovu, muda umebaki mchache sana.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

SAUTI NI SAUTI YA YAKOBO, LAKINI MIKONO NI YA ESAU.

MWINUE YESU KRISTO KATIKA MAISHA YAKO.

JE! UNA MHESHIMU MUNGU?

Heshima ni nini kibiblia?

SINA PESA SASA, YESU ATANISAIDIA NINI?

Rudi Nyumbani

Print this post

Sifa na Lami ni nini? (Kutoka 2:3).

Swali: Sifa na Lami ni nini kama tunavyosoma katika Kutoka 2:3

Jibu: Turejee..

Kutoka 2:3 “Na alipokuwa hawezi kumficha tena, akampatia kisafina cha manyasi akakipaka SIFA NA LAMI, akamtia mtoto ndani yake, akakiweka katika majani kando ya mto”

“Sifa” inayozungumziwa hapo sio “Utukufu” bali ni aina ya “Nta” inayopatikana/kuzalishwa na aidha mimea au mafuta. Mfano wa Nta ya mimea ni ile inayotokea katika baadhi ya mashina na miti (Tazama picha chini).

nta  ya mimea biblia

Lakini Nta ya “Sifa” ni ile inayopatikana kutoka katika mabaki ya “Makaa ya mawe” ambayo ni nyepesi kuliko Lami. (Tazama picha chini)

sifa ni nini biblia

Na “Lami” ni Nta nzito Zaidi inayoganda ambayo kimwonekano ni nyeusi na inapatikana katika hali ya uasili au baada ya kuchujwa kwa mafuta ya petroli kiwandani.

Lami inapatikana katika uasili wake maeneo ya bahari ya chumvi (Sidimu)mpakani mwa nchi ya Israeli na Yordani..

Mwanzo 14:10 “Na bonde la Sidimu lilikuwa limejaa MASHIMO YA LAMI. Nao wafalme wa Sodoma na Gomora wakakimbia, wakaanguka huko, nao waliosalia wakakimbia milimani”

“Lami” kimwonekano ni nzito kuliko “Sifa” na rangi yake ni nyeusi kama tu “Sifa”. (Tazama picha chini).

lami ni nini

Biblia inatabiri siku ya mwisho (ya kisasi cha Mungu) juu ya wanadamu wote watendao maasi, dunia itapigwa (kwa kuunguzwa kwa moto) na vijito na ardhi yote itakuwa Lami.

Isaya 34:8 “Maana ni siku ya kisasi cha Bwana, mwaka wa malipo, ili kushindania Sayuni.

9 Na vijito vyake vitageuzwa kuwa lami, na mavumbi yake yatageuzwa kuwa kiberiti, NA ARDHI YAKE ITAKUWA LAMI IWAKAYO”.

Sasa kufahamu kwa mapana kwanini Safina ile iliyomficha Musa ilipakwa Sifa pamoja na Lami?.. na ni ufunuo gani uliopo nyuma yake?, fungua hapa >>>>SAFINA NI NINI?

sifa ni nyeusi

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Sifa ni nini?

Nini maana ya Mithali 27:21  inaposema “mtu hujaribiwa kwa sifa zake?”

NI NINI KINATOKA KINYWANI MWA MTOTO WAKO?

MALAIKA NI WALIMU WA SIFA KWETU, TUJIFUNZE KWAO!

TENDA JAMBO LA ZIADA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Sakitu ni nini? (Ayubu 38: 29)

Sakitu ni BARAFU INAYOANGUKA KUTOKA JUU, ambayo mara nyingi inafunika mimea, au barabara au nyumba katika nchi zenye baridi kali. (Tazama picha juu).

Ayubu 38: 29 “Barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na SAKITU YA MBINGUNI ni nani aliyeizaa?

30 Maji hugandamana kama jiwe, Na uso wa vilindi huganda kwa baridi”.

Neno hili limeonekana pia katika Kutoka 16:14, ambapo biblia inaonyesha ile MANA ilifanan na sakitu kimwonekano (ingawa haikuwa sakitu).

Kutoka 16:14 “Na ulipoinuka ule umande uliokuwa juu ya nchi, kumbe! Juu ya uso wa bara kitu kidogo kilichoviringana, kidogo kama SAKITU juu ya nchi.

15 Wana wa Israeli walipokiona, wakaambiana, Nini hiki? Maana hawakujua ni kitu gani. Musa akawaambia, Ndio mkate ambao Bwana amewapa ninyi, mle”

Ingawa Mana haikuwa sakitu (barafu) lakini ilibeba tabia za sakitu, kwani Sakitu (barafu) inapopigwa jua inayeyuka, na ile Mana ilikuwa ina tabia hiyo hiyo, jua lilipozuka ilikiyeyusha.

sakitu ni mana

Kutoka 16:21 “Basi wakaokota asubuhi baada ya asubuhi, kila mtu kama ulaji wake ulivyokuwa; na hapo jua lilipokuwa ni kali, kikayeyuka”.

Kujua ni ufunuo gani uliopo nyuma ya MANA, fungua hapa >>>MANA ILIYOSHUSHWA KUTOKA MBINGUNI.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

USIWE NA TAMAA YA CHAKULA KINGINE.

JE UMEUFIKIA ULE UTUKUFU HALISI WA MANA? 

NYOTA YA ASUBUHI.

NI NANI ATAKAYETUTENGA NA UPENDO WA KRISTO?

MWONGOZO WA MAOMBI YA ASUBUHI.

Rudi Nyumbani

Print this post

JE UMEUFIKIA ULE UTUKUFU HALISI WA MANA? 

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, karibu katika kujifunza Neno la uzima.

Ni vizuri kufahamu mana waliyopewa wana wa Israeli jangwani, ijapokuwa ilikuwa ni ileile lakini haikuwa na ubora sawa. Utajiuliza kwa namna gani?

  1. Ipo mana iliyodumu kwa siku moja (1): Ndio ile waliyokuwa wanaiokota kila siku asubuhi, na kuipika, jua lilipozuka iliyeyuka, lakini pia iliposazwa siku ya pili yake ilivunda.
  2. Mana ya pili ni ile iliyodumu kwa siku mbili(2). Mungu aliwaangiza siku moja kabla ya sabato waokote mana ile, ambayo wataila, mpaka siku ya sabato, na itakuwa sawa. Lakini ikisazwa hadi siku ya tatu, inavunda.
  3. Mana ya tatu, ilidumu daima: Hii haikuharibika kwa vizazi vyote. Ni ile aliyoambiwa Musa aichukue na kuihifadhi ndani ya sanduku la agano. Iwe kumbukumbu kwa vizazi vyote vijavyo.

Habari hiyo utaisoma kwenye Kutoka 16:19-36

Je hili hufunua nini katika agano jipya?

Mana ya kwanza:

Kama vile tunavyojua mana ni chakula walichopewa na Mungu wakile na kuishi, katika mazingira magumu (ya jangwani).Na katika hiyo hawakuugua, wala miguu yao kupasuka.

Vivyo hivyo kwa sasa Mana ni chakula cha rohoni ambacho tumepewa tukile sisi tuliookoka, katika huu ulimwengu wa upotovu, ili katika hicho tusiathiriwe na dhambi au mauti, mpaka siku ya ukombozi wetu.

na chakula chenyewe ni “ufunuo wa Yesu Kristo” au kwa lugha nyingine ni “Neno la Mungu lililofunuliwa”(Yohana 6: 30-35)

Mtu yeyote anayeokoka, lazima ajue hapaswi kukaa tu, na kusema imekwisha, Yesu aliyamaliza yote. hapana vinginevyo atakufa kiroho. Bali anapaswa aanze kula NENO (ndiyo mana) ili aukulie wokovu, kama Israeli walivyokula jangwani. Na hiyo huchangiwa na kufundishwa injili ya kweli kutoka kwa walimu sahihi, huku na yeye mwenyewe akionyesha bidii katika kutamani kufundishwa pamoja na kusoma Biblia kila siku.

Sasa mtu kama huyu rohoni akifanya hivyo anaonekana anakula mana lakini sasa mana yake kwa mwanzoni, humtia nguvu ya kitambo kidogo, ni sawa na mtu anayekunywa maziwa na yule anayekula ugali ipo tofauti, ni kweli vyote vinafaa mwilini lakini vyote vina nguvu tofauti.

Ndivyo ilivyo kwa mtu aliye mchanga kiroho, hufunuliwa  lile neno la awali (Maziwa).

Hivyo fadhili za Mungu zitamlinda mtu huyu, siku kwa siku kwa jinsi anavyozidi kufundishwa na kujisomea, ndio maana Mtu aliyemchanga kiroho akikosa Neno au fundisho kwa muda mrefu, ni rahisi sana kufa, Haiwezekani mtu akasema nimeokoka halafu hana habari na kufundishwa. Kujipima kama wewe ni hai au umekufa angalia usomaji wako/kujifunza kwako Neno.

Mana ya pili:

Lakini kwa jinsi mtu huyu anavyojenga uhusiano wa karibu na Mungu wake siku baada ya siku, basi Neno lile linapokea nguvu, ya kumuhifadhi kwa kipindi kirefu kidogo,. Wana wa Israeli kwasababu walikuwa wanaingia  katika sabato kwa Mungu wao,ili kumwabudu na kumsifu, ile mana ilipokea nguvu kwa hiyo siku yao ya sabato haikuharibika.

Halikadhalika na mtu awapo katika kujibidiisha na kazi ya Mungu, utumishi wa Mungu, huduma ya Mungu. Lile Neno linapokea nguvu ya kumuhifadhi wakati wote huo ahudumupo. Maana yake uwezo wa kuhifadhiwa na Mungu unakuwa mkubwa. Huyu mtu anayejibiisha na Mungu, hawi mwepesi kuanguka dhambini, hawi mwepesi kurudi nyuma ovyo, hawi mwepesi kushambuliwa na mwovu hata kukosa shabaha kabisa, hawi mwepesi kupungukiwa kabisa.

Fadhili za Mungu hukaa juu yake, huyu mtu kwa wakati wote amtumikapo Mungu kwa moyo wa dhati, au azingatiapo ibada nyingi. Mungu humuhudumia yeye. Lakini kwamfano akianza kupoa, na kulegea, ataanza kuona tu nguvu za Mungu zinaisha ndani yake ukame unatokea, uzito unakuja, ugumu unaamka tena ndani yake. Hufananishwa na kile chakula alichopewa Eliya na malaika, akaweza kuenda na nguvu ya chakula hicho kwa siku arobaini. Hiyo ndio mana ya pili ambayo Bwana atakulisha wewe utumikaye mbele zake.

Mana ya Tatu:

Lakini ile mana ambayo hudumu milele. Utakumbuka kuwa sharti yake ni ikae ndani ya sanduku. Na sanduku letu ni Kristo, ambaye ndani yake hazina zote za hekima na maarifa  zimesitika (Wakolosai 2:3).

Kwa jinsi mtu unavyoendelea kudumu ndani ya Kristo, kwa uaminifu, kwa wakati fulani mrefu, Bwana hujifunua kikamilifu kwao. Na hapo fadhili za Mungu hazikomi, wala kupungua juu yao milele. kwasababu wameufikia ule utukufu halisi wa Mana iliyofichwa, ambayo si kila mtu anaifikia. Hatua hii, humfanya huyo mtu wakati wote kuwa chini ya fadhili nyingi za Mungu, neema nyingi zinakuwa juu yake, sikuzote ni kwenda mbele tu hakuna kurudi nyuma, wala kupoa, wala hakuna siku atapoa ki-upendo kwa Mungu, Mungu atajifunua kwake kwa namna yake mwenyewe.

ndio maana alitoa ahadi hiyo kwa kanisa la Pergamo akasema..

Ufunuo 2:17

[17]Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. YEYE ASHINDAYE NITAMPA BAADHI YA ILE MANA ILIYOFICHWA, nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua mtu ila yeye anayelipokea.

Kushinda nini?

Ukianzia juu (Ufunuo 2:12-17) utaona anasisitiza,

kutoikana imani na kuendelea kuwa mwaminifu, kwa kutojichanganya na mafundisho ya uongo, ambayo yanakufanya usiwe mtakatifu Rohoni. Mafundisho hayo yalifananishwa na yule Balaamu aliyewaletea Israeli wanawake wa kimataifa ili wawaoe  kisha wafundishwe kuabudu miungu, ili wamkosee Mungu. Ndugu epuka mafundisho ya kidunia, baki kwenye Neno likufanyalo kuwa mtakatifu, tembea katika huo. Fahamu tu Mana hiyo ipo sandukuni imefichwa, si kila mtu anaweza kuifikia hivyo huna budi na wewe kuingia humo, kwa kuishi maisha ya kumtii Kristo. Fikia utukufu huo wa mana.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

USIWE NA TAMAA YA CHAKULA KINGINE.

MNGOJEE BWANA

CHAKULA CHA ROHONI.

(Opens in a new browser tabUSIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Mchuuzi ni nani? (Hosea 12:7).

Swali: Mchuuzi maana yake nini kama tunavyosoma katika Hosea 12:7? na je tunaruhusiwa kuwa wachuuzi?


Jibu: Turejee.

Hosea 12: 7 “Ni MCHUUZI, mizani ya udanganyifu i mkononi mwake; anapenda kudhulumu”

Mchuuzi ni mtu anayefanya biashara ya kununua bidhaa na kuzisafirisha kwenda kuziuza mahali pengine hususani nje ya nchi yake.

Utalisoma neno hili tena katika kitabu cha Wimbo ulio bora 3:6, Ezekieli 27:3,  Ezekieli 27:20-22 na Isaya 23:8.

Swali ni je biblia inaturuhusu wakristo kuwa Wachuuzi (yaani biashara ya kutoka nchi moja kwenda nyingine)?

Jibu ni ndio inaruhusu!, isipokuwa katika biashara yoyote ile ni muhimu kuzingatia viwango vya utakatifu na ukamilifu, Uchuuzi wowote ukihusisha rushwa au biashara haramu ni kosa kibiblia, na pia ni hatari kama maandiko yanavyosema katika Ezekieli 28:18.

Ezekieli 28:18 “Kwa wingi wa maovu yako, KATIKA UOVU WA UCHUUZI WAKO, umepatia unajisi patakatifu pako; basi nimetokeza moto kutoka ndani yako, nao umekuteketeza, nami nimekufanya kuwa majivu juu ya nchi, machoni pa watu wote wakutazamao.

19 Wote wakujuao kati ya kabila za watu watakustaajabia; umekuwa kitu cha kutisha, wala hutakuwapo tena hata milele”

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 13 (Kitabu cha Hosea).

Sala ya baraka (Hesabu 6:24-26).

Je! Karamu za ‘Idi’ ndio zipo hizo tunazozisoma katika Hosea (12:9)

Je ni halali kwa mkristo kufanya biashara ya Forex?

Kalafati ni nini? (Ezekieli 27:9)

Rudi Nyumbani

Print this post

KUWA NA JUHUDI KATIKA ROHO.

Jina la Bwana wetu YESU KRISTO libarikiwe. Karibu tujifunze biblia Neno la Mungu wetu lililo Mwanga wa njia yetu na Taa iongozayo miguu yetu (Zaburi 119:105).

Wengi tuna juhudi katika “mwili” lakini hatuna juhudi katika “roho”. Juhudi katika mwili ni nzuri na inafaa lakini ile ya roho ni bora Zaidi na inafaa sana. Kwasababu biblia inasema Roho ndiyo inayoutia uzima (Yohana 6:63).

Sasa Neno la Mungu linasema..

Warumi 12:11 “kwa bidii, si walegevu; MKIWA NA JUHUDI KATIKA ROHO ZENU; mkimtumikia Bwana”.

Sasa hizi juhudi katika roho ni zipi?..

   1. JUHUDI KATIKA MEMA.

1Petro 3:13 “Naye ni nani atakayewadhuru, mkiwa wenye juhudi katika mema”.

Matendo mema ni pamoja na kuwasaidia wanyonge (masikini, wayatima na wajane), kusamehe na mengineyo..

    2. JUHUDI KATIKA KUPENDANA.

1Petro 4:8 “Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi.

9  Mkaribishane ninyi kwa ninyi, pasipo kunung’unika”

Mtu mwenye juhudi katika roho ni yule pia mwenye juhudi katika kuutafuta upendo.

    3. JUHUDI KATIKA KUMTUMIKIA MUNGU.

Kazi ya Mungu si lazima iwe ule ya kusimama mimbarini na kuhubiri/kufundisha.. Lakini pia ile ya kusafisha nyumba ya Mungu, ni kazi yenye thawabu kubwa na heshima kubwa kwa Mungu… Ukiwa na juhudi katika kumtumikia Mungu kwa njia hiyo pasipo kusukumwa au kukumbushwa kumbushwa bali unajituma wewe mwenyewe, basi hapo unaonyesha juhudu uliyonayo katika roho, na ukomavu wako kiroho.

   4. JUHUDI KATIKA KUOMBA.

Ikiwa utaweza kuomba kila siku kwa muda usiopungua lisaa limoja, hiyo ni ishara kubwa ya kuwa una juhudi katika roho, lakini kama kuomba kwako ni mpaka jumapili kwa jumapili, basi kuna ulegevu ulio ndani yako.

   5. JUHUDI KATIKA KUSOMA NENO.

Mtu mwenye kutia bidii katika kujua mafunuo yaliyo ndani ya biblia kwa njia ya kujifunza na kutafiti na kurudia rudia kutafakari yale aliyoyasoma na kujifunza, mtu wa namna hiyo kibiblia ni mwenye juhudi katika roho na si mlegevu.

Wakolosai 3:16 “Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu”.

   6. JUHUDI KATIKA KUMTOLEA MUNGU.

Sadaka inakamilisha ibada kwa mkristo yoyote yule (ikiwemo mchungaji, mwalimu, nabii, mwinjilisti au mtumishi mwingine yoyote). Na mtu mwenye bidii nyingi katika kumtolea Mungu, mtu huyo kulingana na biblia ni mwenye juhudi katika roho.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwa namna gani mauti ya wacha Mungu ina thamani machoni pake? (Zaburi 116:15).

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

IKIWA MWENYE HAKI AKIOKOKA KWA SHIDA, MWENYE DHAMBI ATAONEKANA WAPI?

TABIA ZA NJIA YA MUNGU KWA MKRISTO

Ni kwa namna gani, upendo husitiri wingi wa dhambi? (1Petro 4:8).

Rudi Nyumbani

Print this post