Category Archive Uncategorized

Fahamu mana ya Zaburi 48:14 Yeye ndiye atakayetuongoza

SWALI: Ipi tafsiri ya Zaburi 48:14 ?

[14]Kwa maana ndivyo alivyo MUNGU, Mungu wetu. Milele na milele  Yeye ndiye atakayetuongoza.


JIBU: Mwandishi anajivunia sifa ya Mungu wao wa milele. kwamba ndiye atakayewaongoza.

Akiwa na maana atayewaongoza katika mambo yao yote, kwamba kamwe hawezi kuwaacha, atakayewaongoza njia sahihi ya uzima, njia sahihi ya kupigana vita, ya kujenga na kupanda.

Ndivyo ilivyokuwa kwa wana wa Israeli. Mungu alikuwa nao jangwani kwa nguzo ya moto na wingu kuwaongoza, aliwapelekea malaika wake kuwalinda, aliwafundisha namna ya kupata faida katika shughuli zao, akawainulia na waamuzi, pamoja na wafalme na manabii kuwachunga na mwisho akawaletea mkombozi, ambaye ndio ukamilifu wa yote. Kuonyesha wema wake na kiu yake ya kuwaongoza  watu wake.

Hata sasa, sifa yake ndio hiyo hiyo, ndio maana na sisi tuna ujasiri wa kusema…

‘Yeye ndiye atakayetuongoza’.Sio tu kwa wakati huo, bali mpaka siku ya kufa kwetu.

Alipokuja mwokozi hakutuacha hivi hivi kama mayatima, bali alituachia msaidizi ambaye anatuongoza na kututia katika kweli yote, ndiye Roho Mtakatifu.

Yohana 16:13

[13]Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.

Bwana akubariki.

Je umempokea Yesu?  Kama bado ni nini unasubiri ? Fungua hapa kwa mwongozo wa sala  ya toba ya imani. >>>>KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MANA ILIYOSHUSHWA KUTOKA MBINGUNI.

Fahamu maana ya Mhubiri 10:9 Mwenye kuchonga mawe ataumizwa kwayo;

Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?

Rudi Nyumbani

Print this post

‘Waibao watu ‘ sawasawa na 1Timotheo 1:10 humaanisha nini?

SWALI: Biblia inapowataja ‘waibao watu ‘ sawasawa na 1Timotheo 1:10 humaanisha nini?


JIBU: Tusome;

1 Timotheo 1:8-10

[8]Lakini twajua ya kuwa sheria ni njema, kama mtu akiitumia kwa njia iliyo halali;

[9]akilifahamu neno hili, ya kuwa sheria haimhusu mtu wa haki, bali waasi, na wasio wataratibu, na makafiri, na wenye dhambi, na wanajisi, na wasiomcha Mungu, na wapigao baba zao, na wapigao mama zao, na wauaji,

[10]na wazinifu, na wafiraji, na WAIBAO WATU, na waongo, nao waapao kwa uongo; na likiwapo neno lo lote linginelo lisilopatana na mafundisho yenye uzima;

Tangu zamani dhambi ya wizi, haikuwa tu katika vitu na mali, bali ilikuwa hata katika watu. Ndio kilele cha juu kabisa cha wizi.

Wizi huu ulikuwa na  malengo mbalimbali mojawapo ilikuwa ni kuwapeleka vitani, lakini pia kuwauza kama watumwa. Kama tunavyofahamu katika historia bara la Afrika lilikumbwa na tatizo hili, katika karne ya 17, waafrika wengi waliibiwa, na kuuza katika mabara ya ulaya.

Lakini kwa nyakati hizi wizi huu, umekuwa mbaya zaidi, kwasababu watu hawaibi tena watu kwa lengo la kuwatumikisha, bali kwa lengo la kuwafanyisha biashara ya kikahaba, wengine kuwaua ili wachukue viungo vyao kwa kazi za kishirikina, wengine wauze viungo vyao vya ndani kama vile figo, ili wapate fedha.

Jambo ambalo ni baya sana, ndio maana kwenye maandiko katika enzi za agano la kale adhabu ya wizi wa watu  haikuwa ndogo bali kifo.

Kumbukumbu la Torati 24:7

[7]Mtu akionekana anamwiba nduguze mmojawapo katika wana wa Israeli, akamfanya kama mtumwa, au kumwuza; na afe mwivi huyo; ndivyo utakavyoondoa uovu katikati yako.

Lakini sisi katika agano jipya, hatuna ruhusa ya kuua watu wa namna hiyo, isipokuwa tuonapo vitendo kama hivyo vikitokea ni ripoti katika vyombo vya dola, hapo utaisaidia jamii, kudhibiti uovu kama huo Lakini pia kumwomba Mungu, aiondoe roho hii chafu isiwepo katikati ya  jamii zetu, ili kuiponya kuiponya jamii.

Na Mungu atakubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea. Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ALIJARIBIWA SAWASAWA NA SISI KATIKA MAMBO YOTE.

Je! Malaika wanazaliana?

USIZISHIRIKI DHAMBI ZA WATU WENGINE.

Mikono iliyotakata ni mikono ya namna gani? (1Timotheo 2:8).

Rudi Nyumbani

Print this post

Je ni sawa kuukubali udhaifu kama mtume Paulo alivyojisifia kwa huo? (2Wakorintho 12:9-10)

SWALI: Je udhaifu ni jambo la kulikubali? Kama tunavyoona mtume Paulo akiusifia katika;

2 Wakorintho 12:9-10
[9]Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juuyangu.

[10]Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu.

Paulo Hajisifii udhaufu, kana kwamba ni mzuri wa kuvutia, hapana hakuna udhaifu ulio mzuri umfanyao mtu ajiivunie huo……lakini linapokuja eneo la Mungu, udhaifu humnyenyekesha mtu, na hivyo humfanya mtu huyo kutegemea zaidi nguvu za Mungu, kuliko uweza wake mwenyewe ndicho kilichokuwa kwa Paulo.

Anasema hakuwa mtu mwenye ujuzi wa maneno, au utashi mwingi wa kitume kama wanavyodhaniwa watumishi wa Mungu wote kuwa nao.

2 Wakorintho 10:10

[10]Maana wasema, Nyaraka zake ni nzito, hodari; bali akiwapo mwenyewe mwilini ni dhaifu, na maneno yake si kitu.

Lakini katika udhaifu huo wa kunena, maelfu ya watu walikuja kwa Kristo, katika udhaifu huo wa kimwili miujiza mikubwa ilifanyika kwa mikono yake. Hivyo akamshukuru Mungu kwa hilo, ili watu wasidhani ni kwa uwezo wake au kipawa chake fulani maalumu aliweza kuyafanikisha hayo.

Ndivyo tunavyojifunza hata kwa Musa, Mungu kumtumia kwa viwango vile haikuwa katika uweza wake wowote, kwasababu alikiri mbele za Mungu yeye sio mnenaji.(Kutoka 4:10), lakini pia Mungu alimshuhudia kuwa ni mpole kuliko watu wote waliokuwa duniani kipindi kile. Tofauti labda na makuhani wengine au manabii waliokuja au kuwepo kabla yake.(Hesabu 12:3)

hata leo, pale tunapojiona ni wadhaifu fulani mbele za Mungu kimaumbile au kiusemi, au kihali, hapo ndipo mahali pazuri pa kitumiwa na yeye. Usifadhaike wala usife moyo ukasema mimi siwezi, amini tu, kwasababu yeye hategemei ulichonacho, bali Neno lake moyoni mwako, ukiliweka yote yawezekana kwako. Amini tu.

1 Wakorintho 1:26-29

[26]Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa;

[27]bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu;

[28]tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko; [29]mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu. 

fuatilia ushuhuda hizi zitakujenga..

USHUHUDA WA RICKY:

JE UDHAIFU WANGU UNAWEZA KUZUIA INJILI?

Lakini hilo halimaanishi kwamba udhaifu wowote ni mzuri, kwamba tujivunie katika hayo, hapana hakuna raha katika ulemavu, au katika ububu, au katika upofu..Lakini tujapo kwa Kristo ni mtaji mzuri wa Mungu kututumia. Hiyo ni kutudhuhirishia kuwa kwa Mungu hakuna kiungo hata kimoja ambacho hakiwezi kumtumikie yeye. Sote kwa pamoja tuwe na elimu tusiwe na elimu, tuwe na afya tusiwe na afya, tuwe na vijijini tuwe mijini, tunajukumu la kumtumikia Mungu, na kufanya vema kabisa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.


Mafundisho mengine:

MUNGU ALIVICHAGUA VITU AMBAVYO HAVIKO.

USIMLAANI KIZIWI, WALA USITIE KWAZO MBELE YA KIPOFU.

Ipi tofuati ya “Kutakabari” na “kutakabali”?

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mhubiri 10:15 Kazi yao wapumbavu huwachosha kila mmoja,

SWALI: Je, mstari huu tunaousoma kwenye Mhubiri 10:15 una maana gani?

Mhubiri 10:15

[15]Kazi yao wapumbavu huwachosha kila mmoja, Maana hajui hata njia ya kuuendea mji.


JIBU: Kwa namna ya kawaida ya kibinadamu tunajua watu wengi hutamani kuishi mijini kuliko mashambani. Kwasababu mijini huduma zote hupatikana, na ni mahali pa raha. Hata kazi, mtu anazozifanya mashambani, wengi wao ni ili matunda yake wakayafurahie mjini, Au wakaziuze bidhaa zao huko wawe matajiri.

lakini tengeneza picha mtu, ambaye anajitaabiisha kufanya kazi kwa lengo la kuzifurahia mjini, halafu hajui njia ya kufika huko, kinyume chake ndio anakwenda mbali zaidi na mji, anaelekea majangwani au mabondeni?  ni wazi kuwa mtu kama huyo  hawezi kuwa na raha katika kazi yake, kwasababu taabu yake haina faida, alikosa malengo au hakuwa na maarifa sahihi.

Ni ufunuo gani upo nyuma yake?

Na sisi pia tuliomwamini Kristo. Tuna mji ambao tunatarajia kuungia, ndio ule Yerusalemu mpya ishukayo kutoka mbinguni kwa Baba..

Ufunuo  21:2-3

[2]Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe. 

 [3]Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. 

Anaendelea kusema…

Ufunuo  22:14-15

[14]Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake. 

[15]Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.

Huo ndio ule mji halisi ambao hata Ibrahimu aliona, ikamfanya aishi maisha kama ya mpitaji hapa duniani.

Waebrania 11:8-10

[8]Kwa imani Ibrahimu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka asijue aendako. 

 [9]Kwa imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi, kama katika nchi isiyo yake, akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile ile. 

 [10]Maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu. 

Umeona na sisi ili tuweze kuonekana tumestahili kuuingia katika mji huo wa mbinguni hatuna budi tuwe tumeokolewa na YESU KRISTO. Kwasababu yeye ndio NJIA ya kuuingia mji.

Ukiwa nje ya Kristo tafsiri yake wewe ni mpumbavu, kwasababu taabu yako yote ya hapa duniani, haikufikishi popote haikuepeki mjini mwa Mungu, itakuchosha tu, utakuwa na magorofa, utaijaza akaunti fedha, utakuwa ni miradi mikubwa lakini mwisho utakufa, na kwenda kaburini. Lakini ukiiona njia na kuifuata Yerusalemu basi hufanyi kazi ya bure, unapojiwekea hazina kule hufanya kazi ya kushosha, ni uzima baada ya kifo. Utafaidi matunda yake

Je umeokoka?

Ikiwa bado na unatamani kufanya hivyo, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala hiyo >>>  KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Yerusalemu ni nini?

KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI

(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)Maana ya Mhubiri 1:9 “wala jambo jipya hakuna chini ya jua”. (Opens in a new browser tab)

MJI WENYE MISINGI.(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Je! Malaika wanazaliana?

Wapo wanaodhani kuwa malaika wanao uwezo wa kuzaliana sawasawa na habari ya wana wa Mungu na binti za wanadamu inayozungumzwa  katika kitabu cha Mwanzo.

Mwanzo 6:1-3,  Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao,

2 wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.

3 Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.

Kwa habari hiyo wengi hufikiri, hao wana wa Mungu walikuwa ni malaika, ukweli ni kwamba hawakuwa malaika bali wanadamu. Yesu alisema, tutakapofika mbinguni, hatutaoa wala kuolewa, tutafanana na malaika, Kuonyesha kuwa malaika hawazaliani. (Mathayo 22:30)

Vilevile katika habari hiyo hatuoni kwamba malaika wakiadhibiwa, bali wanadamu, kuonyesha kuwa ni jambo la kibinadamu. Kwa urefu wa fundisho hilo, fungua hapa >>> WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.

Viungo vya uzazi viliumbwa mahususi kwa viumbe wa ulimwenguni, kwa lengo la kuijaza nchi. Lakini vya mbinguni havikuumbwa kwa utaratibu kama huu wa kwetu.

Hivyo kwa hitimishi ni kuwa malaika watakatifu hawazaliani. Kwasababu wao ni viumbe vya rohoni, waishio milele. Hivyo hawahitaji kuzaliana.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je! mbinguni kuna malaika wa kike?. Na je! tukifika mbinguni tutafanana wote?

Je malaika wote wana wabawa?

KUNDI LA MALAIKA WALETAO MABAYA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Tafsiri ya Mithali 27:18 Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake;

SWALI: Maana ya Mithali 27:18 Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake; Naye amhudumiaye bwana wake ataheshimiwa.


JIBU: Mstari huo una vipengele viwili cha kwanza ni Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake

Na cha pili ni naye amhudumiaye bwana wake ataheshimiwa.

Tukianzana na hicho cha kwanza. Tufahamu kuwa Mungu ameiandika injili yake sio tu kwenye kitabu chake, bali pia kwenye vitu vya asili, ndio maana Yesu alitumia mifano mingi ya namna hiyo, kuzungumza nao habari zake mwenyewe. Kuanzia wakulima, mimea, wanyama, wafanya biashara, wafalme n.k.

Sasa hapa anasema yeye atunzaye mtini atakula matunda yake. Kumbe kula matunda ni “kutunza”. Usipotunza huwezi pata chochote. Ili uone kazi yako, utaiwekea mbolea, utaipalilia, utaipiga dawa n.k. Na mwisho utakuwa mvumilivu aidha miaka mitatu/ minne ukisubiri  mazao.

Halidhalika rohoni. Sisi kama watoto wa Mungu (tuliookolewa), kila mmoja wetu anao “mtini” moyoni mwake, na huo si mwingine zaidi ya Yesu Kristo. Wengi wasichojua ni kwamba Kristo huanza kama kichanga, kisha huwa kijana mdogo, baadaye huwa mtu mzima, na mwisho huanza kutenda kazi zake. Kama tu alivyokuwa hapa duniani alivyoishi na Mariamu na Yusufu, hakuanza kufanya chochote pindi anazaliwa.

Hivyo usipomlea ipasavyo hutafaidi matunda yake vema. Ndio mfano wa mpanzi ambao Yesu mwenyewe aliutoa, akasema zile mbegu ziliporushwa nyingine zikaishia njiani, nyingine kwenye miamba, nyingine kwenye miiba, na nyingine kwenye udongo mzuri, moja ikazaa thelathini, nyingine sitini, nyingine mia. Akatoa ufafanuzi wake, kwamba zile zilizofanikiwa kuzaa, ni kwamba zilichangiwa na KUVUMILIA (Luka 8:15). Sasa kuvumilia nini? Kuvumilia  hatua zote tatu za mwanzo, yaani dhiki kwa ajili ya Kristo, kujiepusha na anasa, udanganyifu wa mali, na uvivu wa kulitendea kazi Neno.

Ukuaji wa kiroho tafsiri yake ni ‘Kristo kukua ndani yako’. Ukiona upo  ndani ya wokovu kwa miaka mingi, halafu huoni matunda yoyote ya wokovu wako, katika ufalme wa Mungu, tatizo linakuwa hapo, hukuwa na nafasi ya kuutunza mtini wako.

Ukiokoka, ni lazima bidii ya kusoma Neno iwe ndani yako kila siku, usiwe mvivu wa maombi, vilevile epuka maisha ya kidunia, na ubize uliopitiliza, ambao unakufanya hata nafasi ya Mungu wako unakosa. Ukizingatia hayo, baada ya kipindi Fulani utaona Kristo anavyojengeka nafsini mwako , na kukutumia.

Lakini pia sehemu ya pili inasema naye amhudumiaye bwana wake ataheshimiwa,. Ni hekima ya kawaida, ukiwa mfanyakazi mwema kwa bwana wako, hawezi kukuchikia kinyume chake atakupa heshima yako, lakini pia na watu wengine wote wa nyumbani kwake watafanya hivyo.

Si zaidi Mungu?

Heshima hasaa kwa Mungu wako, sio kumwambia “Shikamoo” au kuomba kwa sauti ya unyenyekevu, au kuinamisha kichwa uwapo ibadani. Heshima yake hasaa ni pale unapomtumikia, unapotii agizo lake la kuwaeleza wengine habari za injili, na pale naposimama katika nafasi yako kwenye mwili wa Kristo.

Tutafute kuheshimiwa na Bwana kwa kuwashuhudia wengine injili.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MTINI, WENYE MAJANI.

Biblia imemaanisha nini kusema Nyoka atakula mavumbi?(Opens in a new browser tab)

(Opens in a new browser tab)Je ile habari ya mtini kunyauka inajichanganya?(Opens in a new browser tab)

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo.

SWALI: Nini maana ya mstari huu Yohana 12:35

Basi Yesu akawaambia, Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru hiyo, giza lisije likawaweza; maana aendaye gizani hajui aendako.

JIBU:  Yesu alipokuwa duniani, alijilinganisha na Nuru ya uimwengu huu (jua), Yohana 11:9-10…Na hivyo mara kwa mara katika mafundisho yake aliwasisitiza wayahudi juu ya jambo hilo, lakini hawakulielewa.

kwa kawaida jua huwa halizimi, lakini pia huwa halitulii mahali pamoja(kwa jinsi ya kawaida). Litachomoza, litazama,.litaendelea hivyo hivyo katika mzunguko wake. Wakati linaangaza upande mmoja, upande mwingine wa dunia ni giza.

Sasa wayahudi walipomwona Kristo, wengine walimpokea, wengine walimpinga, wengine walimwonea wivu, wengine walimwita mchawi.

Lakini wote hawa, Neema bado ilikuwa juu yao. Bado Kristo alikuwa anawakusanya kama vile kuku akusanyaye vifaranga vyake chini ya mbawa zake (Luka 13:34). Yesu hakudhubutu kwenda kuhubiri kwenye mataifa mengine ambayo yalihitaji hata kumfanya mfalme, ijapokuwa walikuwa wanampinga vikali.

Sasa ndio hapa akawaambia..kwambo hili halitaendelea sana…kuna wakati pia nuru hii  mnayoiona sasa itawafikie na wengine..

ndio hapo akawaambia..

“Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru hiyo, giza lisije likawaweza; maana aendaye gizani hajui aendako”.

Maana yake ni kuwa anawaambia aminini mapema, kwasababu nguvu hii inayowalilia mioyoni mwenu itaondoka … Mkikataa neema, mkikataa kujazwa Roho,  Kamwe hamtaweza kulishinda giza kwa nguvu zenu.

Na tunaona ni kweli, jambo hilo liliendelea kwa kipindii kifupi, baada ya Kristo kufufuka, na kupaa, injili kidogo kidogo ikaanza kutoka kwa wahayudi.ikaenda kwa watu wa mataifa yaani mimi na wewe..

Tangu ule wakati, wa mitume, mpaka leo hii inakaribia sasa miaka 2000, wayahudi bado hawajafumbuliwa macho, kwasababu wokovu ni neema kuamini. Sio utashi wa mtu.

Sasa leo hii sisi watu wa mataifa tunayo injili, lakini kanuni ya Nuru ni ileile, huzunguka. Na kwetu pia haitadumu milele. Mungu aliahidi ule mwisho unapokaribia kufika (ambao ndio huu) atawarudia tena Israeli kwa kipindi kifupi. na hivyo kwa upande wetu, hakutakuwa na neema tena ya wokovu itakayokuwa imesalia..

Warumi 11:25-26

[25]Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.

[26]Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa,

Mwokozi atakuja kutoka Sayuni;

Atamtenga Yakobo na maasia yake.

Hii ni kutufunisha pia Bwana hasemi na wayahudi tu, bali na anasema sisi pia…

Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru hiyo, giza lisije likawaweza; maana aendaye gizani hajui aendako.

Je unaenda katika nuru hiyo? Kama bado wasubiri nini. Geuka leo uoshwe dhambi zako upokee uzima wa milele, usipofanya hivyo kamwe huwezi kulishinda giza.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine

MZEITUNI HALISI UTAKAPOPACHIKWA.

Nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho,

(Opens in a new browser tab)Mistari ya biblia kuhusu maombi.(Opens in a new browser tab)

AGIZO LA UTUME.(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Je! Ni dhambi kutumia njia za kisasa za uzazi wa mpango.

Kwanza ni vema kufahamu uzazi wa mpango ni nini na kama ni dhambi au la!.

Uzazi wa mpango ni kuzaa kwa mpangilio ulioutaka wewe, kwamfano ukijiwekea malengo ya kuzaa watoto 30, huo ni uzazi wa mpango maadamu yalikuwa ni malengo yako, au ukijiwekea malengo ya  kuzaa mmoja maisha yako yote huo pia ni uzazi wa mpango. Kinyume chake uzao usio wa mpango, ni ule wa  kutojali idadi ya watoto utakaouzaa, wala kutojali muda wa uzaaji wako.

Lakini je! Jambo hili linaruhusiwa na Mungu?

Ukweli ni kwamba uzazi wa mpango si dhambi. Kwasababu gani?

Licha ya kwamba Mungu ameweka maagizo yake kupitia biblia takatifu, lakini pia, ameweka hekima yake kupitia mambo ya asili (1Wakorintho 11:14, Warumi 1:20), Hivyo mambo ya asili yanatufundisha pia agizo la Mungu .

Si kila wakati mama atashika ujauzito, bali upo wakati wa hatari na wakati usio wa hatari. Sasa kwa hekima huo tayari ni utaratibu Mungu kamwekea mtu, atambue majira yake, achukue tahadhari. Umeona? Kwa namna nyingine Mungu anasema, kuna majira utapata mtoto, na kuna majira hutapata mtoto. Hivyo uamuzi ni wako, ukitaka kuzingatia mazunguko huo, ni wewe, usipojali pia ni wewe.

Sasa mtu ambaye anayechagua kuzingatia mzunguko huo wa asili wa Mungu, huyo tayari yupo katika uzazi wa mpango. Na pia ni agizo la Mungu tuwe na uwezo wa kuwatunza wale wa nyumbani kwetu (1Timotheo 5:8)

Lakini je! Vipi ambao wanatumia njia za kisasa za uzazi wa mpango je na wao wapo sawa?

Tukisema njia za kisasa, ni kama zile za kutumia vidonge, kutumia sindano, kutumia vizuizi kama mipira (kwa wanaume na wanawake), kuweka kitanzi, na kuweka vipandiki/vijiti.  Zote hizi ni njia za kisasa.

Hapa ni lazima tufahamu pia lengo ni nini?. Bila shaka lengo ni lile lile moja la uzazi wa mpango kwa wanandoa, na si vinginevyo. Lakini mwanadamu ameamua kutumia njia zake za kisasa, ili kufanikisha hilo?

Je! Ni kosa?

Ili kujibu swali hilo, tufikirie pia mambo mengine ya kisasa, leo hii tuna vitu vingi vya kisasa vimebuniwa na wanadamu, kwamfano kuna kuku wa kienyeji lakini pia wapo wa kisasa, kuna mchicha wa kienyeji lakini pia ipo ya kisasa, kuna matunda ya kienyeji lakini pia yapo ya kisasa. Je! Ni dhambi kutumia vitu hivyo, kwasababu vimebuniwa na mwanadamu?

Jibu ni hapana.

Lakini vinaweza kuwa na madhara yake, kwasababu mwanadamu hawezi kuumba kitu kiukamilifu. Ndio maana asilimia kubwa ya vitu hivi vya kisasa, huwa si vizuri kiafya. Vivyo hivyo katika matumizi ya njia za kisasa za uzazi wa mpango. Yaweza isiwe dhambi kwako kutumia. Lakini madhara ya kiafya, pia waweza kukumbana nayo. Wengine hupata shida ya vizazi, wengine ugumba kabisa kulingana na njia iliyotumika, lakini wengine hawapatwi na madhara. Hivyo amani ya Kristo iamue ndani yako.

Lakini ile y asili ni bora zaidi. Ukitumia njia ya kalenda, ni salama lakini pia Mungu ametubunia hiyo, ukijizoesha kuifuatilia utaweza tu kupangilia uzazi wako.

Lakini fahamu pia uzazi wa mpango, maadamu amani ya Kristo imeamua moyoni mwako, si dhambi mbele za Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je ni halali kwa mkristo kufanya biashara ya Forex?

JE! KUBET NI DHAMBI?

Je Kutoa Mimba ni dhambi?

Rudi Nyumbani

Print this post

Elewa tafsiri ya Mithali 27:22 Hata ukimtwanga mpumbavu kwa mchi kinuni.

SWALI: Nini tafsiri ya Mithali 27:22

Hata ukimtwanga mpumbavu kwa mchi kinuni pamoja na ngano; Upumbavu wake hautamtoka.


JIBU: Kama tunavyojua mtwangio na kinu ni vyombo vinavyotumika kuponda-ponda nafaka ngumu kuwa unga, au wakati mwingine mimea migumu kuwa milaini. Mfano wa kisamvu ambacho ili kiweze kulika, majani yake huwezi yapika hivyo hivyo huna budi kuyatwanga twanga kidogo, yalainike ndipo upike ule.

Na vivyo hivyo, nafaka kama mahindi, au ngano, ili viweze kulika zamani vilikuwa vinatwangwa kwenye vinu ,tofauti na sasa vinasagwa na mashine.

Sasa katika mithali hiyo, Mungu anatoa, asili ya mtu mpumbavu, kwamba hata akitwangwa, mfano wa ngano kinuni, huo upumbavu hauwezi kumtoka. Yaani njia gani ya lazima itumike bado hawezi kuacha upumbavu.

Sasa ni vizuri kufahamu, mpumbavu ni nani?

Mpumbavu kibiblia sio mtu Fulani mjinga tu hapana, bali ni Neno pana, linalolenga kuanzia

mtu anayesema hakuna Mungu (zaburi 14:1)

Mtu mgomvi (Mithali 9:13),

Mtenda maovu (Mithali 10:23)

Anayejiona njia yake ni sawa machoni pake (Mithali 12:15)

Mwenye kiburi (Mithali 14:3)

Mwenye dharau (Mithali 15:5)

Yaani kwa kifupi mpumbavu ni mtu ambaye hana Mungu ndani yake. Kwasababu dhambi ndani ya mtu ndio chanzo cha Upumbavu wote.

Sasa mtu kama huyu, hakuna kitu kinachoweza kuutoa upumbavu huo ndani yake, waweza kusema elimu, lakini ni watu wangapi wameelimika, lakini walevi, watukanaji, mashoga. Hata atwangwe vipi kinuni hawezi lainika, ikiwa hajui ni kipi sahihi kinachoweza kutoa upumbavu huo.

Kumfunga mwizi, hakumfanyi wizi au tamaa ya kuiba itoke ndani yake, mara ngapi unasikia mwizi katoka jela, karudia wizi wake, au ni kiongozi ambaye anaaminiwa awe kielelezo cha kupambana na ufisadi, lakini yeye ndio anakamatwa katika ufisadi, au teja ametolewa hospitalini karudia, tena madawa la kulevya. Ndio maana jamii ijapojaribu kudhibiti vitendo viovu, bado haviishi, bali hubadilika tu maumbile. Kwasababu mpumbavu hata atwangwe kinuni, hawezi geuka, hakuna nidhamu inayoweza mbadilisha. Huwezi acha mwenendo wake mbovu kwa semina za kijamii, au kuwekewa sheria

Je! Ni kipi kinachoweza kumgeuza?

Ni Yesu Kristo tu. Yeye ndiye aliyetiwa mafuta, na Mungu kuwaokoa watu wa Mungu na kuwafungua. Amwaminiye  na kudhamiria moyoni mwake kumfuata, basi atageuzwa moja kwa moja na kuwa mtu mwingine, huo ni uhakika.

Alisema.

Yohana 1:12  Bali wote waliompokea aliwapa UWEZO wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.

Ni ahadi yake kuwa Ukimwamini jambo la kwanza ni kukusamehe dhambi zako, kwasababu ndio jambo lililomfanya aende msalabani kwa ajili yako miaka elfu mbili iliyopita,. Unakuwa huhesabiwi dhambi tena, unahesabiwa haki bure kwa neema yake. Lakini sambamba na hilo anakupa UWEZO wa kuwa kama yeye kwa nguvu za Roho wake Mtakatifu atakayemwachia ndani yako, pindi tu unapoamini.

Na baada ya hapo utashangaa tu unavyoanza kubadilika moyoni mwako.

Zingatia tu toba ya kweli, pamoja na ubatizo sahihi (kuzamishwa katika maji mengi kwa jina la Yesu Kristo). Na kumtii yeye.

Upumbavu utakutoka.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Fahamu Maana ya Mithali 18:13 Yeye ajibuye kabla hajasikia, Ni upumbavu na aibu kwake.

HAUWEZI KURUKA MADARASA YA MUNGU!

Nini maana ya Mithali 9:13 Mwanamke mpumbavu hupiga kelele, Ni mjinga, hajui kitu?

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 26:2 Kama shomoro katika kutanga-tanga kwake,

SWALI: Nini maana ya Mithali 26:2

Kama shomoro katika kutanga-tanga kwake, Na kama mbayuwayu katika kuruka kwake; Kadhalika laana isiyo na sababu haimpigi mtu.


JIBU: Mungu anafananisha laana isiyo na sababu na ndege wanaotanga-tanga angani.

Kama tunavyojua ndege hawa aina ya shomoro na mbayuwayu, kila siku tunawaona wanaruka angani, kila siku tunawaona wapo hari-hari, wanaonekana kama wapo buzy, lakini katika kazi zao zote, na juhudi zao zote, na mikakati yao yote, kamwe huwezi ona yanaleta madhara yoyote kwa mwanadamu. Hata kama utawaharibia viota vyao, hata kama watakauwa na hasira na wewe, huwezi ona wanamshambulia mwanadamu, kwasababu uwezo huo hawana. Huwezi wafikiria na kila wanapokuona wanakimbia. Wewe mwenyewe ukiwaona huwezi kuwaogopa, tofauti na ukimwona nyoka, utajidhatiti asikuume. Lakini ndege huvai ‘chapeo’ kichwani kujilinda naye asikuume, kwasababu hana madhara.

Ndivyo Mungu anavyotufundisha, laana zisizo na sababu, haziwezi kukupata ni kama ndege tu angani, zitapita, na kuendelea na shughuli zake, kamwe haziwezi kukupata ikiwa wewe ni mtakatifu, Hii ni kutufundisha kuwa hatupaswi kuwa waoga wa maneno ya watu  (laana) ambayo hayana sababu.

Ukiona laana imekupata basi  ujue kulikuwa na sababu nyuma yake, (lakini sio tu maneno matupu mtu anayoyatoa), mfano wa laana hizi ni ile ya Elisha aliyowalaani wale vijana 42, walioraruliwa na dubu. Kwasababu walimdhihaki. (2Wafalme 2:22-25)

Lakini mfano wa laana zisizo na sababu, ni ile Goliathi aliyomlaani Daudi kwa miungu yake, ambayo  ilikuwa ni kazi bure..

1Samweli 17:42 Hata Mfilisti alipotazama huku na huku, akamwona Daudi akamdharau; kwa kuwa ni kijana tu mwekundu, tena ana sura nzuri.  43 Mfilisti akamwambia Daudi, Je! Mimi ni mbwa hata umenijia kwa fimbo? Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake

Ni mfano mwingine ni ile Balaamu mchawi alivyojaribu kuwalaani Israeli ikashindakana, kwasababu huwezi laani vilivyobarikiwa. (Hesabu 23)

Hata leo, ikiwa wewe umeokoka, hupaswi kuogopa, maneno yoyote iwe ya waganga au wanadamu. Kwasababu wewe tayari ni mbarikiwa. Ni ajabu sana kuona mkristo,  analia na kutetemeka, eti! Mchawi kamwambia mwaka huu hautaisha atakuwa watoto wake wote watakuwa wamekufa!!. Mzee wa mila kamwambia atapata ajali kwasababu hakutambika kijijini mwaka huu.

Mwingine anawaza, mzazi kamwambia hatafanikiwa kwasababu kaamua kuokoka. Haa! Unaogopa nini hapo?. Hizo ni laana zisizo na sababu. Ishi kwa amani zione tu kama ndege wa angani ambao hukai kuwafikiria kama watakushambulia siku moja.

Ukiokolewa na Kristo umebarikiwa, wewe sio wa kunenewa maneno ovyo ovyo tu, na yakatokea. Wewe ni uzao wa kifalme usiotetemeshwa, ngome imara isiyoangushwa. Mwamba mgumu usiogharikishwa. Yatambue mamlaka na nguvu ulizopewa ndani ya Kristo. Usiogope!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Elewa maana ya Mithali 26:2 Kama shomoro katika kutanga-tanga kwake,

Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani,

Maana yake nini, Mwe na hofu wala msitende dhambi? (Zaburi 4:4)

NUHU WA SASA.

Rudi Nyumbani

Print this post