Category Archive Uncategorized

BWANA ni mtu wa vita,  BWANA ndilo jina lake.(Kutoka 15:3)

SWALI: Naomba kufahamu maana ya huu mstari..Kwanini biblia imtaje Mungu kama mtu, angali maandiko yanasema yeye sio mtu.

Kutoka 15:3

[3]BWANA ni mtu wa vita,  BWANA ndilo jina lake.


JIBU: Neno hilo halimaanishi kuwa Mungu ni mtu, Bali biblia hutumia mifano halisi ya kibinadamu kuwasilisha picha Fulani Rohoni..

Kwamfano ukisoma andiko lingine linalopatikana katika Mithali 30:26, utaona mnyama anayeitwa Wibari anatajwa kama mtu..

Mithali 30:26

[26]Wibari ni watu dhaifu;  Lakini hujifanyia nyumba katika miamba.

Tunafahamu kabisa wanyama hawa wibari(Pimbi) sio watu, isipokuwa kwa wingi wa akili zao, mwandishi anawafananisha na watu, Ni kwasababu gani? Ni Kwasababu ijapokuwa ni waoga, wadhaifu, wanawindwa na kila mnyama mkali..lakini hawajengi nyumba zao zao katika sehemu dhaifu kama kwenye viota, au kwenye mashimo, au vichaka, ambapo ni rahisi kuvamiwa au kuharibiwa na majanga, Bali wanaweka makazi Yao katika miamba mikubwa iliyojificha sana  Mahali ambapo ni ngumu adui kuwashambilia.. wanafananishwa na watu waliojenga maisha yao juu ya MWAMBA, pekee yaani Yesu Kristo

Mathayo 7:24  “Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba; 25  mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba”

Hivyo tukirudi katika andiko hilo, anaposema “BWANA ni mtu wa vita”. Anajaribu kumfananisha Bwana na shujaa wa kivita, jemedari mwenye uzoefu mkubwa sana katika vita vikali, mfano wa Sauli, au Daudi, ambao walikuwa wanasimama mstari wa mbele katika vita, ili sisi tupate picha jinsi gani Mungu wetu alivyo mkuu sana, pale anapoitwa Bwana wa Majeshi, tumwelewe uweza wake wa kutupigania na kutusaidia kuangusha ngome za ibilisi jinsi ulivyomkubwa haijalishi zimekita mizizi kiasi gani.

Zaburi 24:8 “Ni nani Mfalme wa utukufu? Bwana mwenye nguvu, hodari, Bwana hodari wa vita”

Hivyo mstari huo hakumaanisha kuwa yeye ni mtu.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Ufunuo 12 inaelezea vita vya wakati upi?

Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza

NIMEAZIMIA KUWAKUSANYA MATAIFA. NIPATE KUWAMWAGIA GHADHABU YANGU

Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?

VITA DHIDI YA MAADUI

Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?

NA WATU WOTE WALIKUWA WAKIAMKA MAPEMA, WAENDE HEKALUNI.

Shetani anaishi wapi, Je! Amefungwa au yupo kuzimu?

Rudi nyumbani

Print this post

Kama ndege aendaye huko na huko mbali na kitundu chake;

SWALI: Nini maana ya huu mstari?

Mithali 27:8 “Kama ndege aendaye huko na huko mbali na kitundu chake; Ndivyo alivyo mtu aendaye huko na huko mbali na mahali pake”

JIBU: Hapa Sulemani alikuwa anajaribu kueleza jinsi tabia ya ndege inavyoweza kufananishwa na tabia ya mkristo katika maisha yake hapa duniani. Kwa kawaida ndege anapotoka katika kiota chake, huwa na lengo la aidha kutafuta chakula, au kukiendeleza kiota chake, au kujipumbuzisha mahali Fulani kwa muda. Hivyo huwa anaenda na kurudi, anaenda na kurudi kwa siku hata mara 10 na zaidi, anaweza kufanya hivyo.

 Lakini wakati huo huo, awapo katika mazingira ya kuzunguka huko na huko, hukutana na hatari nyingi sana. Aidha Maadui au mitego. Hivyo asipokuwa makini anaweza asirudi, kabisa nyumbani kwake.

Hivyo ndivyo alivyo mkristo, ambaye misingi yake ni “biblia na Kanisa”. Ukweli ni kwamba si kila wakati atakuwa katikati ya watakatifu, au atakuwa uweponi akimsifu Mungu na kumwimbia, au akilitafakari Neno la Mungu. Zipo nyakati atatoka kwa muda ataenda kazini, atatoka kwa muda ataenda shambani pengine kujitafutia rizki, ataenda shuleni masomoni na kama si hivyo basi kwa namna moja au nyingine atajihusisha na mambo ya kijamii, kama kutembelea jamaa, na ndugu, majirani n.k.

Sasa awapo katika mazingira haya anafananishwa na ndege atokaye katika kiota chake na kuzunguka huko na huko. Hivyo anapaswa awe na busara kwa sababu huko nje, zipo hatari nyingi sana za yeye kunaswa na adui asipokuwa makini.

Ni lazima ajiwekee mipaka, si kila biashara afanye, si kila jambo la kidunia analoletewa mbele yake ajihusishe nalo, si kila mazungumzo ayaongee. Bali muda wote awapo nje, atambue kuwa makao yake ni KANISANI awezapo kufanya ibada, na kujumuika na watakatifu wenzake. Muda wote atambue usalama  wake ni katika Neno la Mungu basi. Alale katika hilo na aamke katika hilo.

Akitafutacho huko nje ajue ni kwa lengo la kuendeleza tu kiota chake (kazi ya Mungu), na sio vinginevyo. Mtu huyo akizingatia vigezo hivyo atakuwa salama. Lakini watu wengi wamenaswa na ulimwengu. Hata Kanisani hawaonekani tena baada ya kupata kazi, Upendo wao kwa Mungu umepoa pale walipokutana na marafiki Fulani wapya, muda wa maombi wanakosa kisa wapo buzy na mihangaiko ya maisha. Kauli zao zimebadilika, kwasababu muda mwingi wamekaa na watu wenye mizaha, na matusi, hadi na wao wakajifunza lugha zao.

Biblia inatuambia,

Waefeso 5:15  “Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; 16  mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu. 17  Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana.

Anasema tena..

Wakolosai 4:5  “Enendeni kwa hekima mbele yao walio nje, mkiukomboa wakati. 6  Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea munyu, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu”.

Hivyo tuwapo nje ya uwepo wa Bwana, tujichunge, tujizuie, tuwe na kiasi, tutakuwa salama. Ili tusijikute tunanaswa katika mitego ya ibilisi.(Mithali 1:17,  7:22)

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mambo yale yaliyo mbali, na yale yaendayo chini sana,

Dia ni nini katika biblia? (Mithali 13:8)

Mithali 24:17 inamaana gani kusema Tengeneza kazi yako huko nje?

Nini maana ya “Atamwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake”. (2Wathesalonike 2:8).

Aibusu midomo atoaye jawabu la haki (Mithali 24:26)

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

Marijani ni nini katika biblia(Ayubu 28:18,Mithali 8:11)?

Rudi nyumbani

Print this post

Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo; Lakini hukumu zake zote ni za BWANA.

SWALI: Nini maana ya huu mstari?

Mithali 16:33

[33]Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo; Lakini hukumu zake zote ni za BWANA.

JIBU: Kura zilipigwa kwa namna mbalimbali zamani, njia iliyokuwa nyepesi ndio hiyo ambayo kipande cha shuka, au nguo, iliyofumwa vilitumiwa kukusanya kura za watu mbalimbali ambazo ziliandikwa katika vipande vya vibao vidogo vidogo, au mawe kisha hukorogwa, na lile litakalotoka la kwanza au kuchukiliwa humo basi ndio kilichosahihi..

Wengine walitumia makopo, wengine kofia, kisha kuzikoroga kura na ile itakayotoka au kuchaguliwa cha kwanza huko ndio huaminika kuwa chaguo sahihi

Hivyo, zipo nyakati ambazo Mungu aliruhusu baadhi ya mambo yaamuliwe kwa kura kama vile kugawanya nchi n.k.Soma(Hesabu 26:55, Yoshua 18:6-10)Lakini si kila jambo, mengi Mungu alitoa majibu kwa njia ya moja kwa moja, kwa kufunuliwa aidha kwa kupitia manabii au maono au ndoto.

Sasa tukirudi katika mstari huo..

Anaposema..

Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo; Lakini hukumu zake zote ni za BWANA.

Maana yake ni kuwa Japokuwa kupiga kura ni tendo linaloonekana la kibinadamu lakini ikiwa linafanyika katika Bwana, majibu ya kweli hutoka kwake.

Yule atakayechaguliwa, au kile kitakachopendekezwa, ndio jibu sahihi kutoka kwa Bwana.

Katika Biblia tunaona mtume Mathiya alichaguliwa kwa kura, lakini kabla ya kupiga kura ile, mitume walimtanguliza kwanza Mungu katika uchaguzi wao,waliomba na kumsihi Bwana aingilie uchaguzi wao..kisha kila mmoja akaandika pendekezo lake na jawabu likatoka na ndio likawa kweli jibu sahihi la Mungu.

Matendo 1:23-26

[23]Wakaweka wawili, Yusufu, aitwaye Barsaba, aliyekuwa na jina la pili Yusto, na Mathiya.

[24]Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuonyeshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili,

[25]ashike mahali katika huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe.

[26]Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye akahesabiwa kuwa pamoja na mitume kumi na mmoja.

Wakati mwingine tunaweza kulaumu, viongozi tuliowachagua, tukasema waliiba kura n.k. lakini kama Mungu asingetaka wawepo pale wasingekuwepo tu, kwasababu yeye ndio anayewamilikisha watawala haijalishi watakuwa ni waovu au wema..

Danieli 2:21

[21]Yeye hubadili majira na nyakati; huuzulu wafalme na kuwamilikisha wafalme; huwapa hekima wenye hekima; huwapa wenye ufahamu maarifa;

Hii ni kuonyesha uhuru wa Mungu wa kuchagua, yapo mambo kwetu tutaona kama tumeamua sisi, au yametokea kwa bahati, lakini kumbe ni Mungu kapanga..kwake yeye vitu havitokei kwa bahati, bali vyote chini ya makusudi yake.Mungu ndiye ayaruhusuyo yote..

Utukufu una yeye milele na milele.

Amina.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?

NINI KINAFUATA SIKU ILE ILE YA KUOKOKA!

kwanini yule kijana aliitupa ile nguo ya kitani chini na kukimbia uchi?

HAKUVAA NGUO SIKU NYINGI.

Ni kura ya aina gani waliipiga wale watu waliosafiri na Yona?

NI WAPI UTAKUTANA NA MALAIKA WA BWANA?

Rudi nyumbani

Print this post

TABIA ZA NJIA YA MUNGU KWA MKRISTO

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo.

Biblia inatuambia Yesu ndiye njia na kweli na uzima. (Yohana 14:6)

Ni kweli wakristo wengi tunamtambua yeye kama njia, lakini hatujui tabia ya hii njia kwa undani jinsi ilivyo kwetu sisi wakristo.

Tofauti na hizi njia tuzijuazo, kwamfano ukitaka kutoka Daresalaam kwenda Morogoro, ni rahisi kuifuata hiyo barabara, au kuielewa kwasababu daima ipo palepale haibadiliki, watu wote tunaipita hiyo kila siku, tumeshaikariri, tunajua vituo vyake vyote vya njiani,  tunaweza hata kukadiria ni muda gani tutakaoutumia kumaliza safari yetu.

Lakini vipi kuhusu njia ya Mungu kwa wakristo. Je na yenyewe inakaririka, au inazoeleka, au ipo palepale?

Maandiko yanatupa majibu; tusome;

Warumi 11:33

Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! Hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazitafutikani!

Hapo anasema “Njia zake hazitafutikani”

Ndugu Bwana alichotuhakikishia ni , usalama na mwisho mwema wa safari yetu ya wokovu endapo tutaamua kumfuata YESU kwa mioyo mikamilifu. Lakini hakutuhakikishia kuwa njia zetu sote kwa pamoja zitafanana. Kwamba sote tukitoka hapa tutapita pale, kisha tutamalizia na pale.

Ni Mungu ndiye anayemchagulia kila mtu mapito yake kwa jinsi apendavyo yeye. Mwingine akishaokoka Bwana atampitisha mashariki kwenda Magharibi, mwingine ataanza naye kusini kwenda kaskazini, na ndio hapo utaona, mmoja ataanza kwa kupoteza kila kitu, mwingine Mungu atambariki atamfanikisha katika maisha yake atakuwa bilionea, mwingine atakuwa na maisha ya kawaida, mwingine atakuwa na ya chini. Mwingine atakuwa na afya sikuzote, mwingine atakuwa na magonjwa yasiyotibika na Bwana hamwondolei kwa kipindi fulani kirefu.

Lakini katika mapito hayo yote, Kristo atahakikisha kuwa anampa nguvu ya kuweza kukabiliana au kuchukuliana na hayo mazingira  bila kukengeuka au kuona ni mzigo mkubwa sana kwake.

Tatizo kubwa la  watakatifu ni kuwa tunataka njia zetu ziwe kama za mtu fulani pale tunapodhamiria.

Sote tunataka tuwe mabilionea kama Sulemani. Ndugu mawazo ya kumpangia Mungu ni wapi akupitishe yatakugharimu. Kwasababu njia zake hazikaririki, hazitafutikani, wala hazichunguziki. Atakupitisha ajuapo yeye, sio ujuapo wewe.

Kuna mmoja atakuwa kama Yohana mbatizaji, hali wala hanywi anakaa majangwani, kuna mwingine atakuwa kama Bwana Yesu anakula na kunywa..kikubwa ni matokeo ya wito ndicho kitakachoeleza wito wa mtu huyo ni kweli au la. Wote wawili Yohana na Bwana Yesu walikuwa na mafanikio makubwa katika huduma zao, japo mapito tofauti, hivyo kila mmoja wito wake ulikuwa ni wa kweli.

Njia za Mungu kwetu sisi hazichunguziki, kaa katika nafasi yako na wito wako, mwamini Bwana hapo hapo ulipo ikiwa kweli umeokoka na umemanisha kumfuata Yesu, kamwe usijilinganishe na mkristo mwingine, kisa yeye ni tajiri kuliko wewe, au ana uwezo wa kuhubiri sana kuliko wewe.

Mtazame Yesu tembea katika njia yake aliyokupangia, hata kama ni mlemavu, isiwe sababu ya wewe kupoteza uelekeo wa wokovu katika maisha yako.Kila pito la mtu, lina sehemu kubwa mbeleni kulisaidia kanisa la Kristo. Maisha yako ni ushuhuda wa kuwaponya wengine mbeleni. Hujui kwanini Mungu akupitishe katika mapito hayo. Hivyo acha kuzikariri njia za Bwana…

Sulemani alikuwa ni mtu mwenye akili nyingi, ambazo alipewa na Mungu, akili za kuweza kuchunguza kila kitu kilicho duniani, lakini alipofika katika njia za Mungu alikiri kuwa hakuna anayeweza kuzielewa alisema..

Mhubiri 8:17 “basi, niliiona kazi yote ya Mungu, ya kuwa haitafutikani na mwanadamu kazi inayofanyika chini ya jua; kwa sababu mwanadamu na akijisumbua kadiri awezavyo kuitafuta, hata hivyo hataiona; naam, zaidi ya hayo, mwenye hekima ajapodhania ya kuwa ataijua, lakini yeye hataweza kuiona”.

Sasa ni kwa namna gani hazitafitikani?

Ni kwasaababu nyakati nyingine Mungu anakupitisha mahali usipopatarajia, wana wa Israeli hawakujua kuwa wangeelekezwa baharini walipokuwa wanatoka Misri, lakini ndio ilikuwa njia ya Bwana kwao. Unaweza kuelekezwa na Mungu, mahali ambapo hakuna dalili yoyote ya wewe kutoka kumbe ndio Mungu kakusudia upite hapo, aonyeshe maajabu yake.

Pili wakati mwingine Mungu anatabia ya kuvuruga mipango yetu. Kanisa la kwanza lilkuwa linakwenda vizuri, katika raha yote, lakini Mungu akamnyanyua Paulo alitese kanisani mpaka Kifo cha Stefano. Kanisa likaogopa nikaondoka Yerusalemu. Kumbe nyuma ya kutawanyika kule kulikuwa na kusudi la Mungu injili ihubiriwe dunia nzima. Paulo alipomaliza kusudi hilo akageuzwa na yeye moyo akawa mhubiri. Njia za Mungu hazichunguziki.

Hata wewe mambo yako yanaweza kwenda sawa, halafu ghafla Mungu akayavuruga, lakini mwisho wake ukawa mwema. Kupata na kupoteza, nyakati za raha na shida, milima na mabonde..tarajia katika safari hii ya ukristo..Njia za Mungu hazichnguziki.

Lakini katika yote Bwana anasema.. Sisi tulioamua kumfuata yeye kwa mioyo yetu yote kamwe hatutakaa tupotee katika njia hiyo hata  kama tutakuwa hatueleweki, tutakuwa wajinga kiasi gani, hatutakaa tupotee, lakini tutafikia tu mwisho mwema kwasababu nji hiyo ni salama sana na hakika.

Isaya 35:8

[8]Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, Njia ya utakatifu; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; wasafirio, wajapokuwa wajinga, hawatapotea katika njia hiyo.

Anasema pia…

Yeremia 29:11

[11]Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema BWANA, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.

Wote waliomfuata Yesu, waliofaida yake, katika kila pito. Jitwike msalaba wako mfuate Yesu. Kwasababu yeye ndio Njia pekee ya kufika mbinguni na kuumaliza mwendo wako salama.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MATARAJIO YA KILA MWANADAMU DUNIANI NI YAPI?

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

MBINGUNI YUPO NANI SASA?

Je Mungu ana njia ngapi za kuzungumza?

Dia ni nini katika biblia? (Mithali 13:8)

Mofa ni nini? na inafunua nini kiroho?(1Samweli 28:24).

Kujazi ni nini? (Mathayo 6:4)

Zile Rangi saba za Upinde wa Mvua zinawakilisha nini?

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

Rudi nyumbani

Print this post

Yeremia alikuwa na umri gani alipoitwa?

JIBU: Maandiko hayaweki wazi ni katika umri gani Yeremia aliitwa isipokuwa watafiti wengi ya Biblia wanakadiria Yeremia aliitwa katika umri wa miaka 20, au chini kidogo ya hapo, pengine 17

Biblia inachosema tu..alipoitwa aliitikia kwa kusema mimi ni MTOTO…Ikiwa na maana kuwa alijiona  umri wake ulikuwa bado haujakidhi vigezo vya kumtumikia Mungu..

Yeremia 1:4 “Neno la Bwana lilinijia, kusema,  5 Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.  6 Ndipo niliposema, Aa, Bwana MUNGU! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto.  7 Lakini Bwana akaniambia, Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru”.

Na hiyo pengine kwasababu aliona historia ya manabii wengi walioitwa walikuwa tayari ni watu wazima,

Pili Yeremia yeye alizaliwa katika familia ya kikuhani, na alijua umri wa kuhani kutumika Mungu ni kuanzia miaka 25 na kuendelea sawasawa na (Hesabu 4:3). Hivyo huwenda yeye hakuwa katika umri huo, ndio maana akawa na ujasiri wa kumwambia Mungu mimi bado ni mtoto.

Hivyo na sisi tunajifunza nini?

Kwa Bwana hakuna umri maalumu au  wakati maalumu wa kuitwa..Uonapo unavutwa umwamini Yesu, saa hiyo hiyo itikia wito huo, kama Yeremia, neema hiyo haitadumu milele. Ikiwa utapuuzia kwa kusema Aah, Muda bado ngoja kwanza nifikishe umri Fulani, ngoja kwanza nijenge nyumba, ngoja kwanza nipate kazi, ngoja kwanza niondoke kwa wazazi. Fahamu kuwa una dalili kubwa ya kuipoteza neema ya Mungu. Saa ya wokovu ni sasa, wakati uliokubalika ndio huu. Maneno ya Mungu yanapokuchoma, tambua huo ndio wakati wako. Itikia sauti hiyo, badilika, tumika, tii. Na Bwana atayashughulikia hayo yaliyosalia.

Bwana akubariki

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?

Raheli aliwalilia vipi watoto wake?

Matowashi ni wakina nani?

Historia ya wimbo wa tenzi – Ndio dhamana Yesu wangu

Je ni kweli miaka yetu ya kuishi ni 80 tu (kulingana na Zaburi 90:10).

Nabii Elisha alikuwa ana maana gani kulia na kusema”Gari la Israeli na wapanda farasi wake”?

Maswali na Majibu

HISTORIA YA ISRAELI.

Rudi nyumbani

Print this post

YESU KATIKA USINGIZI WAKE.

Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo.

Naamini kuwa ulishawahi kusoma katika maandiko kuwa kuna mahali Yesu alilala. Lakini ulishawahi kujiuliza ni kwanini habari ile iandikwe kulikuwa na umuhimu gani?

Kumbuka kila tukio lililoandikwa katika biblia limebeba somo kwetu sisi watakatifu.

Jambo pekee lililomfanya Yesu alale usingizi  mzito namna ile, sio kuchoka kama wengi wanavyodhani, kuna nyakati nyingi Yesu alikuwa anachoka kuliko hata hapa, lakini alikuwa halali, anapanda mlimani kuomba…lakini ni nini kilichompelekea alale?

Jambo lililompa Yesu usingizi mzito, ni ile DHORUBA iliyoanza kule baharini.

Marko 4:36-39

[36]Wakauacha mkutano, wakamchukua vile vile alivyo katika chombo. Na vyombo vingine vilikuwako pamoja naye.

[37]Ikatokea dhoruba kuu ya upepo, mawimbi yakakipiga chombo hata kikaanza kujaa maji.

[38]Naye mwenyewe alikuwapo katika shetri, amelala juu ya mto; wakamwamsha, wakamwambia, Mwalimu, si kitu kwako kuwa tunaangamia?

[39]Akaamka, akaukemea upepo, akaiambia bahari, Nyamaza, utulie. Upepo ukakoma, kukawa shwari kuu.

[40]Akawaambia, Mbona mmekuwa waoga? Hamna imani bado?

Umeona hapo, hakuna mahali popote biblia inarekodi Yesu alipitiwa na usingizi,  isipokuwa hapo kwenye dhoruba kuu.

Wakati wengine wanahangaika na matatizo, hawapati usingizi, wanapambana na changamoto zao..upande wa pili wa Yesu mambo ni tofauti,kule kuyumba kwa chombo kumbe ndio kulikuwa kunavuta usingizi vizuri.

Lakini ni nini Bwana anataka tujifunze juu ya tabia hii ya Kristo?

Ni kwamba hata yeye akiwa amejaa vizuri ndani yetu, tutadhihirisha tabia kama zake.

Ni kwanini leo hii tuna hofu ya maisha, tuna hofu ya kesho, tutaishije, tutakula nini, tutavaa nini? tuna hofu ya wezi, tuna hofu na kufukuzwa kazi, tuna hofu ya magonjwa?

Ni kwasababu Kristo hajajaa ndani yetu vizuri, ni kwasababu hatujapokea uhakika wa kuwa salama daima.

Wakristo wengi, wakiwa kwenye matatizo, mbalimbali hawana raha, wanapoteza utulivu..wanahangaika huku na kule kama wakina Petro. Hii ni hali ya kawaida ya kibinadamu. Lakini Yesu anaweza kukupa usingizi katikati ya tufani na dhoruba..endapo atajaa ndani yako vizuri.

Unachopaswa kufanya ni jiachie tu kwa Yesu, mwache yeye ahangaike na hiyo tufani, itaisha tu yenyewe, haitadumu muda mrefu, atakufungulia mlango wa kutoka katika hilo jaribu, haijalishi ni kubwa kiasi gani.

Jiachie tu kwa Yesu mtafakari yeye muda wote, muwaze yeye na uweza wake, Kama hujaokoka, hakikisha unafanya hivyo sasa, hivyo kwa jinsi utakavyokuwa unaendelea kumsogelea yeye ndivyo atakavyokupa wepesi kwa kukabiliana na mambo yote, na changamoto zote unazokutana nazo..Na hatimaye zitaisha tu bila hata kusumbuka kwasababu yeye yupo kazini.

Mkaribie Yesu sasa acha kuzitegemea akili zako mwenyewe..Naye atakusaidia, yeye mwenyewe anasema;

Mathayo 11:28-29

[28]Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

[29]Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu

Anasema pia..

Mathayo 6:31-34

[31]Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?

[32]Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.

[33]Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.

[34]Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.

Mkaribie Yesu, Akutue mizigo. Akupe uzingizi, akupe raha.

Zaburi 127:2 “Kazi yenu ni bure, mnaoamka mapema, Na kukawia kwenda kulala, Na kula chakula cha taabu; Yeye humpa mpenzi wake usingizi”

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

NA WATU WOTE WALIKUWA WAKIAMKA MAPEMA, WAENDE HEKALUNI.

Dia ni nini katika biblia? (Mithali 13:8)

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

KATAA KUWA EUTIKO, WA KUSINZIA IBADANI.

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

Rudi nyumbani

Print this post

Je watu wa kale walitumia vifaa gani kuandikia?

Watu wa kale walitumia wino, na kalamu pamoja na karasati kuweka kumbukumbu zao kama tunavyofanya sasa..

Isipokuwa wino wao, kalamu zao na karatasi zao zilikuwa tofauti na hizi tunazotumia sasa..

Mtume Yohana katika nyaraka zake aliandika hivi; 

3 Yohana 1:13

[13]Nalikuwa na mambo mengi ya kukuandikia, lakini sipendi kukuandikia kwa wino na kalamu. 

Kuonyesha kuwa unandishi wao ulitegemea wino na kalamu, kama tu huu wetu.

Je! Wino wa kale ulitengenezwaje?

Tofauti na huu wa kwetu unaotengenezwa na kemikali mbalimbali..wino wa zamani ulikuwa unatengenezwa na MASINZI. Masinzi hayo yalikuwa yanavunwa aidha kutoka  katika mafuta yaliyochomwa au kuni pale yanapoganda katika chombo kama sufuria kwa pembeni.

Wino wa kale

Sasa yalipokusanywa kama poda, baadaye yanachanganywa na gundi inayotoka katika mmea wa mpira..lengo la kufanya hivyo ni kuufanya wino huo ushikamane vizuri ili  wakati wa uandishi wino usitapakae ovyo.

Hivyo mwandishi anapoununua wino huo anachofanya ni kuchanganya na maji, kisha kutumia kalamu yake kuchovya na kuandika katika hilo karatasi lao.

Je! Kalamu zao ziliundwaje

Tofauti na kalamu zetu hizi, ambazo zinatengenezwa kwa mirija ya pastiki na chuma. Kalamu za zamani ziliundwa na mmea ujulikanao kama MWANZI ambayo hata huku sehemu kadhaa hutumika.. Mianzi hii ilichongwa kwa pembeni kuacha ncha. Ili kuruhusu wembambea wa uandishi katika karatasi  kama tu kalamu zetu za kisasa zilivyo.Tazama picha.

Kalamu za kale

Je karatasi za kale zilikuwaje?

Karatasi za zamani zilfanana hizi isipokuwa zrnyewe zilikuwa ni nene, ziliundwa na mmea ujulikanao kama mafunjo(Ayubu 8:11).

Mmea huu ulichongwa kulingana na ukubwa wa karatasi, kisha kuchanjwa chanjwa katika vipisi vidogo, ambavyo baaadaye vililowekwa katika maji ili vilainike..kisha vinawekwa katika ubao ulionyooka, kisha vinalazwa kipisi kimoja baada ya kingine, na vingine kupita kwa kukatiza..kisha panawekwa ngozi ya mnyama kwa juu , na baada ya hapo kukandamizwa, ili vipisi hivyo vishikane,

Na kuachwa siku kadhaa, baadaye wakitoa, tayari karatasi hiyo nene hutokea… ngumu na imara kuliko hata hizi tulizonazo sasa. Ndizo walizotumia watu wa kale kuandikia.

karatasi za kale

Bwana akubariki.

Je! Umeokoka? Je! Unatambua kuwa unyakuo wa kanisa upo karibu? Umejiandaaje? Ikiwa bado hujafanya hivyo na unahitaji msaada huo, basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi;

Maran Atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU.

BWANA alimaanisha nini kwenye mstari huu Marko 2:21″ Hakuna mtu ashonaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kukuu?

Yerusalemu ni nini?

Kaniki ni nini katika biblia? (Yeremia 8:21).

Karismatiki ni nini?

KALAMU YENYE UONGO YA WAANDISHI IMEIFANYA KUWA UONGO.

Rudi nyumbani

Print this post

Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.

Zaburi 147:3 Huwaponya waliopondeka moyo, Na kuziganga jeraha zao.  4 Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.  5 Bwana wetu ni mkuu na mwingi wa nguvu, Akili zake hazina mpaka.

Ukitazama juu unaona nyota nyingi sana zisizo na idadi, mbali na hizo zilizo ndani ya upeo wa macho yetu, lakini pia zipo nyingine tusizoziona ambazo idadi yake ni mabilioni kwa mabilioni, matrilioni kwa matrilioni,..

Lakini hapa Mungu anatupa siri ya uweza wake, anasema zote hizo amezihesabu na kuzipa majina,..

Sasa Kwanini atuambie jambo kama hilo?

Ni kutuaminisha kuwa ikiwa anazifahamu  nyota zote zilizo mbali, nje-ndani, atashindwaje kutufahamu sisi? Atashindwaje kuziona taabu zetu na shida zetu, atashindwaje kuyaona mateso yetu na majeraha yetu?

Hivyo hapo anaposema ‘Huwaponya waliopondeka moyo, Na kuziganga jeraha zao’. Anamaanisha, huweza kutufanya upya, endapo tutamkaribia.

1Petro 5:7  ‘huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu’.

Mkaribie Kristo akuponye kwasababu yeye yupo karibu sana na wewe zaidi ya nyota za angani.

Utukufu na uweza vina yeye milele na milele amina.

Maombi Yangu:

“Baba mwema, tumeona uweza wako, juu ya ulimwengu wako uliouumba, kwamba hakuna lolote usilolijua,wala usiloliweza, na sasa ninakukaribia Baba wa Upendo, kama ulivyoahidi kwenye Neno lako kwamba utaziganga jeraha zangu, Naomba sasa niponye moyo wangu, na mwili wangu, nifanye upya tena, nisimame mbele zako, nikutumikie. Ni katika jina la Yesu naomba nikiamini. Amen.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NYOTA ZIPOTEAZO.

UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?

Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?

MUNGU WETU, JINSI LILIVYO TUKUFU JINA LAKO DUNIANI MWOTE!

UNAMCHUKULIA YESU KWAKO KAMA NANI?

Agano ni nini? na kuna aina ngapi za maagano?

Mofa ni nini? na inafunua nini kiroho?(1Samweli 28:24).

NIMEOKOKA, ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA NITAKWENDA WAPI.

Rudi nyumbani

Print this post

Ni kosa gani alilolifanya Eli, ilihali aliwaonya watoto wake?

SWALI: Kwanini Mungu alimuadhibu Eli kwa kosa la kutowaonya watoto wake, angali tunasoma katika maandiko aliwaonya hapo kabla?

Tusome;

1Samweli 2:22 Basi Eli alikuwa mzee sana; naye alisikia habari za mambo yote ambayo wanawe waliwatenda Waisraeli; na jinsi walivyolala na wanawake waliokuwa wakitumika mlangoni pa hema ya kukutania. 

23 Akawaambia, Mbona mnatenda mambo kama hayo? Maana nasikia habari za matendo yenu mabaya kwa watu hawa wote.  24 Sivyo hivyo, wanangu, kwa maana habari hii ninayoisikia si habari njema; mnawakosesha watu wa Bwana. 

25 Mtu mmoja akimkosa mwenzake, Mungu atamhukumu; lakini mtu akimkosa Bwana, ni nani atakayemtetea? Lakini hawakuisikia sauti ya baba yao, kwa sababu Bwana amekusudia kuwaua.

Lakini Hapa Mungu anasema…

1Samweli 3:12 Siku hiyo nitayatimiza maneno yale yote niliyoyasema juu ya Eli katika habari za nyumba yake, tangu mwanzo hata mwisho. 

13 Kwa maana nimemwambia ya kwamba nitaihukumu nyumba yake milele, kwa ajili ya ule uovu alioujua; kwa kuwa wanawe walijiletea laana, wala yeye HAKUWAZUIA. 

14 Na kwa hiyo nimeapa juu ya nyumba ya Eli, ya kwamba uovu wa nyumba ya Eli hautasafika kwa dhabihu wala kwa sadaka hata milele.


JIBU: Kibiblia “Kuonya” sio tu kusema kwa mdomo, bali pia kuchukua hatua stahiki, endapo maonyo hayatatekelezwa. Eli ni kweli aliwaonya watoto wake, kwa dhambi walizokuwa wanazifanya madhabahuni pa Mungu, lakini aliendelea kuwaangalia, wakifanya mambo yao maovu bila kuwaondoa katika nafasi zao. Ndio maana hapo kwenye 2Samweli3:13 Mungu anamwambia Samweli, kwamba HAKUWAZUIA. Hakuwaondoa katika kazi ya utumishi, Pengine kwasababu ni watoto wake, warithi wake, akawastahi zaidi ya  Mungu. Hivyo wakati wa adhabu ulipofika yeye naye alishiriki adhabu ile.

Hili ni funzo, pia kwa viongozi wote wa imani, nyakati hizi tunazoishi, kanisa limegeuzwa kama mahali pa kila mtu kujiamulia jambo lake, na viongozi wanaona wanafumbia macho. Utakuta mchungaji ni mzinzi, lakini askofu akipata taarifa, badala wamwondoe katika ofisi ile, wanamwonya tu, kisha wanamuhamisha dayosisi, wanamstahi, na akifika kule anaendelea na maovu yake, anahamishwa tena dayosisi.

Utakuta watoto wa wachungaji, ni walevi, hawana maadili, lakini wanaendelea kubaki katika nafasi za wazee wa kanisa au waimbaji kwaya. Mchungaji akiambiwa, anachokifanya ni kuwaonya tu, lakini bado wanaendelea kushika nafasi hizo za madhabahuni. Hii ni hatari. Mungu anataka hatua stahiki zifuatane na maonyo kama hakuna mabadiliko.

Hivyo kama wewe ni kiongozi, kumbuka maonyo yako ni lazima yaambatane na vitendo.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwanini Kuhani wa Mungu Eli alikufa kwa kuvunjika shingo?

IKABODI MAANA YAKE NI NINI?

NA NENO LA BWANA LILIKUWA ADIMU SIKU ZILE.

NI NINI KINATOKA KINYWANI MWA MTOTO WAKO?

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.

IELEWE SAUTI YA MUNGU.

NINI MAANA YA SISI KUWA WATOTO WA MUNGU?

Rudi nyumbani

Print this post

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU BARAKA

Baraka ni karama ya Mungu, na kila mmoja wetu aliyekombolewa na Yesu, ahadi hiyo ni yake. Baraka zimegawanyika mara mbili, zipo baraka za mwilini, na baraka za rohoni. Lakini kubwa zaidi ni zile za rohoni. Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyoeleza Baraka za Mungu. Lakini pia ikiwa utapenda kupata vifungu mbalimbali, pamoja na mafundisho mazuri ya Neno la Mungu, bofya link hii uweze kujiunga na kundi letu la Whatsapp>>> WHATSAPP GROUP

Wafilipi 4:19  “Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu”

Yakobo 1:17  “Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka”.

Hesabu 6: 24 “Bwana akubarikie, na kukulinda;  25 Bwana akuangazie nuru za uso wake, na kukufadhili;  26 Bwana akuinulie uso wake, na kukupa amani”

3Yohana 1:2  “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo”

2Wakorintho 9:8  “Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema;”

Kumbukumbu 28:2 “na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako.  3 Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani.  4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako.  5 Litabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga.  6 Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo”.

Waefeso 1:3 ” Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo;”

Mathayo 6:30 ” Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba? 31  Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini? 32  Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote. 33  Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa. 34  Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake”

Malaki  3:10 “Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la”.

Zaburi 20:4 “Akujalie kwa kadiri ya haja ya moyo wako, Na kuyatimiza mashauri yako yote”.

Mathayo 5:6  “Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa”.

Mithali 16:3 “Mkabidhi Bwana kazi zako, Na mawazo yako yatathibitika”

Yeremia 17:7 “Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake”

Pia Kwa wokovu/ maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU WATOTO.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU KIFO.

MISTARI YA BIBLIA YA FARAJA.

MISTARI YA BIBLIA YA UPONYAJI.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU UPENDO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

Rudi nyumbani

Print this post