Title September 2021

FAHAMU JINSI MUNGU NA SHETANI WANAVYOZUNGUMZA NA WATU.

Ulishawahi kuyatafakari kwa makini haya maneno ya Bwana Yesu?

Yohana 8:38 “Niliyoyaona kwa Baba ndiyo niyanenayo; nanyi vivyo hivyo mliyoyasikia kwa baba yenu ndiyo myatendayo”.

Maneno hayo aliwaambia wayahudi (Mafarisayo na waandishi) kipindi kile walipotaka kumuua?. Lakini unaweza kujiuliza ni lini walishakaa chini na kumsikiliza shetani, akizungumza nao kisha akawapa maagizo ya kumwangamiza Bwana Yesu? Ni lini?

Hatuwezi kudhani kuwa shetani alishawahi kukaa chini, na kuanza kunong’ona kwenye masikio yao, na kuwaambia “sasa wanangu wakati wa kumuua Yesu umefika haya nendeni”, Hilo halipo, lakini Bwana Yesu hawezi kusema uongo, ni lazima aliwaona wakimsikiliza shetani, kisha wakaitii sauti yake, na wakafanikiwa kuyafanya yale yote waliyoagizwa na shetani kutenda.. Na ndio maana ukiendelea kusoma pale, utaona anasema..

Yohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na TAMAA ZA BABA YENU NDIZO MPENDAZO KUZITENDA. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo”.

Ndugu, sauti ya shetani, kamwe usitazamie utaisikia katika maono au ndoto, au kwa mapepo, hali kadhalika sauti ya Mungu vivyo hivyo, Utaisikia sauti ya Mungu kwa kutazama tu yale Mungu anatenda.. Vilevile utaisikia na kuielewa sauti ya shetani pale unapotazama ni nini anatenda..

Kwamfano, tukianzana na hawa wayahudi, ilifikia wakati walimwonea Yesu wivu kisa Mungu anamtumia kwa ukamilifu wote kuwavuta watu wote kwenye nuru, hapo ndipo wakaingiwa na wazo la kutaka kumuua, wazo ambalo walishawahi kuona watu fulani huko nyuma wakilifanya likawaletea matunda, na wao pia wakalichukua. Kumbe hawajui hilo wazo ndio sauti ya shetani yenyewe ikiwapa maelekezo.

Hata leo, wazo la wewe kutaka kurudi nyuma kuzini, tayari hiyo ni sauti ya shetani, na ndio hapo unaitii kwa kuanza kutazama picha za ngono mitandaoni,  unafanya punyeto, unakwenda disco, unatazama muvi zenye maudhui ya mapenzi mapenzi wakati wote, hujui kuwa ni tamaa za ibilisi unazozifanya.. yaani katika ulimwengu wa roho, Yesu anakuona umeketi na shetani kwenye meza moja, ukimsikiliza sauti yake kwa makini sana.

Lakini vivyo hivyo kwa watoto wa Mungu pia kanuni ni ile ile, nao wanamsikiliza Mungu kwa kumtazama vile atendavyo, Kama vile Bwana Yesu alivyosema “Niliyoyaona kwa Baba ndiyo niyanenayo”. Sio maono, hapana, Bwana aliona kazi nyingi za Mungu ulimwenguni hivyo akaziiga akazitenda..

Kwamfano moja ya kazi ambazo Yesu aliziona Baba yake anazifanya akaiga ni pamoja na kuwa na HURUMA,  KUSAMEHE, KUWAPENDA MAADUI na KUFADHILI hata kwa wasio na shukrani.

Luka 6:35 “Bali wapendeni adui zenu, tendeni mema, na kukopesha msitumaini kupata malipo, na thawabu yenu itakuwa nyingi; nanyi mtakuwa wana wa Aliye juu, kwa kuwa yeye ni mwema kwa wasiomshukuru, na waovu.

36 Basi, iweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma.

Unaona, hivyo na wewe ukionyesha tabia hizo, kuonyesha fadhili kwa watu wasio na malipo kwako, basi rohoni unaonekana umeketi na Mungu kwenye meza moja ukimsikiliza kwa makini akikupa maagizo ya kufanya, hiyo ni zaidi ya sauti, au ndoto, au maono elfu kumi, unayoweza kuyasikia.

Mathayo 5:46 “Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?

47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?

48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.

Kwahiyo, tujifunze kuitambua sauti ya Mungu wetu kwa kuzitazama kazi zake, vilevile tujifunze kuielewa sauti ya adui yetu ibilisi, ili tuweze kumkwepa na yeye, kwasababu kamwe tusitazamie, sikumoja atakuja kutunong’oneza kwenye masikio yetu “nenda ukazini”, hilo halipo.

Je! Umeokoka? Je! Unafahamu kuwa tupo katika muda wa nyongeza tu, siku yoyote Kristo anarudi. Unasubiri nini huko nje? Utajisikiaje usikie unyakuo umepita halafu wewe umebaki, utamweleza nini Bwana Yesu. Tubu dhambi zako leo kwa kumaanisha kabisa kumrudia Mungu wako, injili tuliyobakiwa nayo sio ya kubembelezewa wokovu tena, ni wewe mwenyewe kuona na kuchukua hatua. Muda umeisha.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Je ni kweli imani ya mtu ndiyo itakayomuokoa, na si kitu kingine?

UNYAKUO.

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?

Rudi nyumbani

Print this post

Kisima cha joka na lango la jaa ni nini?(Nehemia 2:13)

SWALI:Bwana Yesu asifiwe naomba kuelewa “Kisima cha joka”  na “lango la jaa” vina maana gani kama tunavyosoma katika Nehemia 2:13


JIBU: Nehemia alipopata taarifa juu ya uharibifu wa mji wa Yerusalemu, alifunga na kumwomba Mungu kwa muda mrefu, ili aende kuujenga tena mji huo, ndipo Mungu akasikia maombi yake na kumfungulia mlango wa kwenda Israeli kwa ajili ya kazi hiyo ya ukarabati.

Sasa kama tunavyosoma alipofika,hakusubiri sana, bali aliondoka usiku wa tatu yeye ni baadhi ya watu wachache, ili kuuchunguza kwanza mji, jinsi kuta zake zilivyoharibiwa. Na kati ya sehemu tano (5) alizopita mojawapo ilikuwa ni hapo penye kisima cha joka, na lango la jaa.

Kisima cha joka: Ni kisima kilichokuwa kando ya kuta za mji, kinaaminika, kiliitwa hivyo kutokana na umbile la mdomo wake jinsi ulivyofanana na nyoka., japo wengine wanaamini kuwa hapo kale kilitumiwa na wapagani kwa ajili ya miungu yao ya majini, waliyoitambua kwa jina la joka. Hivyo jina la kisima hicho liliendelea kuwa hilo hadi wakati wa baadaye, Japo hilo halijathibitishwa ni kulingana tu na mapokeo kwasababu biblia haijaeleza sababu ya kuitwa vile.

Lango la Jaa: Jaa kwa jina lingine ni jalala, hivyo, lango hili lilitumika kutolea uchafu wote wa mji (kinyesi). Huko nako Nehemia alifika.

Nehemia 2:11 Basi nikafika Yerusalemu, nikakaa huko muda wa siku tatu.

12 Kisha nikaondoka usiku, mimi na watu wachache pamoja nami; wala sikumwambia mtu neno hili alilolitia Mungu wangu moyoni mwangu, nilitende kwa ajili ya Yerusalemu; wala hapakuwa na mnyama pamoja nami, ila mnyama yule niliyempanda mwenyewe.

13 Nikatoka nje usiku, kwa njia ya LANGO LA BONDENI, nikashika njia IENDAYO KISIMA CHA JOKA, na LANGO LA JAA; nikazitazama kuta za Yerusalemu, zilizokuwa zimebomoka; na malango yake yameteketezwa kwa moto.

14 Kisha nikaendelea mpaka lango la chemchemi, na ziwa la mfalme; lakini hapakuwa na nafasi ya kupita kwa yule mnyama aliyekuwa chini yangu.

15 Kisha nikapanda usiku kando ya kijito, nikautazama ukuta; kisha nikarudi nyuma, nikaingia kwa lango la bondeni, nikarejea hivyo.

Lakini  baada ya hayo yote tunaona, Nehemia haraka na mapema alianza ujenzi wa kuta za mji. Na kazi ikaja kukamilika kwa ufasaha wote,licha ya kupitia vipingamizi na vikwazo vingi kutoka kwa maadui zao.

Ni ujumbe gani tunaupata kutoka katika mawazo hayo ya Nehemia?

Ni kwamba hatuwezi kukarabati kitu bila kujua uharibifu wake upo wapi. Ni jinsi gani wakristo, tunapaswa tufumbue macho yetu tuone, uharibifu shetani aliousababisha kwenye kazi ya Mungu, jinsi watoto wanavyoharibiwa, jinsi vijana walivyopotoka kila kukicha, jinsi maasi yanavyoendelea kanisani.., Tukiyaona hayo hapo ndipo wote kwa pamoja tutaona sababu ya kumtumikia Mungu, kwa ushirikiano.

Vinginevyo tutaona kila siku mambo yote ni sawa tu, kama wale watu wa Mji Nehemia alivyowakuta wame RELAX.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Jaa ni nini katika biblia?

“Shinikizo” ni nini kibiblia, Na maana yake rohoni ni ipi?

Nini maana ya Dirii, Chepeo na Utayari?

Jehanamu ni nini?

UFUNUO: Mlango wa 12

Rudi nyumbani

Print this post

Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?

SWALI: Wale  Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo au ni mfano wa picha tu? Na je! wanyama wataenda mbinguni?


Jibu: Awali ya yote ni muhimu kufahamu kuwa viumbe vyote na kila kitu tunachokiona duniani kimeumbwa kwa taswira ya viumbe na vitu vya mbinguni.

Kuanzia mwanadamu mpaka wanyama, ndege pamoja na mimea na vito, vyote vimeumbwa kwa taswira ya vitu vya mbinguni… Isipokuwa vya mbinguni vina utukufu mwingi kuliko vya duniani.

Kwamfano tukianza na mwanadamu.. Maandiko yanasema kaumbwa kwa “sura na mfano wa Mungu”.. Maana yake kimwonekano, mwanadamu anafanana na Mungu, lakini si Mungu.

Kadhalika tukimtazama ng’ombe, simba na tai.. Nyuso zao hizo zimeumbwa kwa taswira ya aina fulani ya malaika waliopo mbinguni, wajulikanao kama Makerubi.. Kwasababu Makerubi wana nyuso Nne, maandiko yanasema hivyo.

Ufunuo 4:6 “Na mbele ya kile kiti cha enzi kulikuwa na mfano wa bahari ya kioo, kama bilauri; na katikati ya kile kiti cha enzi, na pande zote za kile kiti, WALIKUWAKO WENYE UHAI WANNE, wamejaa macho mbele na nyuma.

7 NA HUYO MWENYE UHAI WA KWANZA ALIKUWA MFANO WA SIMBA; NA MWENYE UHAI WA PILI ALIKUWA MFANO WA NDAMA; NA MWENYE UHAI WA TATU ALIKUWA NA USO KAMA USO WA MWANADAMU; NA MWENYE UHAI WA NNE ALIKUWA MFANO WA TAI ARUKAYE”.

Kadhalika wapo farasi wa kimbinguni, (Ufunuo 19:14) na wapo wa kiduniani.. na vile vile vipo vito vya kimbinguni na vya kiduniani..

Kwahiyo, tukirudi kwenye swali letu? Je ni mbinguni wapo kweli wale wenye uhai wanne?, jibu ni ndio wapo! na si nadharia tu!.. tukifika huko tutawaona.. Nabii Ezekieli aliwaona kwenye maono, Yohana naye aliwaona na sisi pia tutawaona.

Na kama hivyo ndivyo, je wanyama nao wataenda mbinguni?

Jibu ni hapana! Hakuna Twiga, wala mbwa, wala simba, wala ng’ombe wala tai arukaye, atakayeenda mbinguni.. Hivyo vyote ni viumbe vya kidunia.. vimeumbwa kutoka mavumbini, na havina nafsi iliyo hai.. maana yake vikifa vimekufa vinarudi mavumbini, havina ufufuo..Na mavumbi hayawezi kuingia mbinguni.

Ni mwanadamu peke yake aliye na ahadi ya kuingia mbinguni, (Na si wanadamu wote bali wale waliooshwa dhambi zao kwa damu ya Mwanakondoo) ambapo siku ya unyakuo itakapofika watafufuliwa na kisha kuvaa miili ya kimbinguni, lakini hawataingia mbinguni na hii miili ya mavumbi.. bali watabadilishwa na kuvikwa ya kimbinguni.

1Wakorintho 15:50 “Ndugu zangu, nisemayo ni haya, ya kuwa nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu; wala uharibifu kurithi kutokuharibika.

51 Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika,

52 kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika.

53 Maana sharti huu uharibikao uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa uvae kutokufa”.

Sasa wanyama wenyewe hawana hiyo ahadi ya kufufuliwa na kuvikwa miili ya utukufu, na wala Kristo hajawafia wao.. ndio maana unaona hakuna mahali popote katika maandiko, inayoonyesha mfano wa mnyama yoyote kufufuliwa.

Na kama wapo wanadamu tu ambao wataikosa mbingu.. mnyama ni nani aweze kuingia?

Waliokombolewa kwa damu ya mwanakondoo, hao peke yao ndio walioahidiwa kwenda mbinguni.. lakini wanadamu wengine wote, ikiwemo wanyama na miti, na nzige, na bakteria hawana nafasi mbinguni..wakifa wamekufa, kama vile mti ukifa unavyopotea, hauna ufufuo wowote.

Sehemu pekee ambayo maandiko yanasema wanyama watakuwepo, ni katika ule utawala wa miaka elfu, hapa duniani tutakapotawala na Kristo. Huko ndiko wanyama watakuwepo. Kwa maelezo marefu kuhusu utawala huu unaweza  kuupata kupitia hapa > Utawala wa miaka elfu

Lakini itoshe kusema tu kwamba! Mbinguni hakitaingia kinyonge

Ufunuo 21:27 “Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo”.

Je na wewe unafanya machukizo? Je umeokoka?.. kama bado basi fahamu kuwa hutakwenda mbinguni, kwasababu huko haviingi vinyonge na wafanyao machukizo, huko hawaingii waasherati, walevi, wazinzi, watu wanaoupenda ulimwengu kuliko kumpenda Mungu.. n.k

Hivyo mpokee Yesu leo, uoshwe dhambi zako, ili uwe na uhakika wa kuingia mbinguni katika makao ya furaha ya daima.

Unyakuo upo karibu na Bwana yuaja.


Mada Nyinginezo:

Naomba kufahamu maana ya “sura ya kijiti” katika Marko 12:26.

Biblia inamaanisha nini inaposema “Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake”?

Je! Kuna malaika wangapi mbinguni?

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

Bahari mbalimbali zilizoorodheshwa kwenye biblia.

Rudi Nyumbani:

Print this post

UTAYAFIKIAJE MANENO SAFI YA MUNGU?

Watu wengi wanasoma biblia lakini si wote wanayafikia maneno SAFI YA MUNGU. Jambo ambalo watu wengi hatujui ni kuwa tunadhani, tunapoisoma biblia kwa mara moja, tayari tumeshayafikia “maneno safi ya Mungu”, yale yenye uwezo wa kubadilisha Maisha yetu katika ubora wote.

Ni vizuri ukafahamu hii biblia tunayoisoma, haipo wazi kama unavyodhani, ni kitabu kilichoficha maneno SAFI YA MUNGU (Pure word of God), Ambayo hayapatikani hivi hivi tu, kwa usomaji wa kawaida tuliouzoea sikuzote. Watu ambao wanauwezo wa kufikia hapa, basi Maisha yao ya kiroho yanakuwa na mageuzi makubwa sana, kutokana na nguvu ya Neno hilo.

Leo kwa neema za Bwana tutaona mtu anawezaje kuyafikia maneno haya;

Biblia imefananisha Neno la Mungu na madini ya fedha (Silver), sehemu nyingine na Dhahabu.

Sasa ukisoma, Zaburi 12:6 inasema..

Zaburi 12:6 “Maneno ya Bwana ni maneno safi, Ni fedha iliyojaribiwa kalibuni juu ya nchi; Iliyosafishwa mara saba”.

Maana yake ni kuwa, ili uweze kufahamu haya “Maneno safi ya Mungu” yanapatikanaje, unapaswa utazame jinsi Fedha/dhahabu safi, inavyopatikana na kusafishwa.

Kwa kawaida, madini haya yanapochimbwa, huwa hayang’ai kama unavyoona katika maduka ya VITO vya thamani. Bali yanakuwa kama miamba tu, au maudongo udongo, yaani dhahabu halisi inakuwa imechanganyikana sana na uchafu wa aina  mbali mbali.

Hivyo wanachokifanya ili kuitoa takataka hizo katikati ya madini, ni kwenda kuiyeyusha katika joto kali sana. Hiyo inapelekea, uchafu kujitenga na fedha, kwani zile takataka zote zinapanda juu, na ile fedha/dhahabu, inabaki chini, kisha wanauzoa ule uchafu wote uliokuja juu, baadaye wanaicha igande tena kisha inatokea dhahabu yenyewe.

Sasa kwa kawaida,wafua fedha/dhahabu, wengine wanairudia hiyo hatua mara mbili au tatu, na kwa jinsi wanavyoirudia mara nyingi na kuondoa hata zile takataka ndogo sana, ndivyo, dhahabu hiyo inavyozidi kuleta mng’ao mzuri sana na wakuvutia sana.

Hivyo Mungu alitumia mfano huo kuonyesha pia jinsi NENO LAKE SAFI, linavyopatikana. Ni kama fedha iliyosafishwa MARA SABA katika moto,. Ikiwa na maana kuwa, zipo hatua saba, za kulifikia NENO safi la Mungu, alilokusudia limletee matokea makubwa katika Maisha yake..

Sasa hii mara saba, mtu anaifikiaje?

Ukiwa ni mtu wa kusoma biblia mara moja tu, na kujiona kuwa tayari umeshajua kila kitu, ufahamu kubwa hapo bado hujalifikia hili Neno safi la Mungu. Kulifikia kunahitaji utulivu, na pia kulitafakari tena na tena, na tena, na tena, kila siku, na sio kusoma tu kama gazeti.

Kwamfano leo unaweza kusoma habari za wana wa  Israeli jinsi Mungu alivyowatoa katika nchi ya Misri, kwa mara ya kwanza ukaielewa kama stori tu, lakini ukigotea hapo, ukasema tayari nimeshaelewa hapo, sina haja ya kurudia tena siku nyingine.. Nakuambia biblia kwako itakuwa haina tofauti na vitabu kingine cha kihistoria ulichowahi kusoma huko nyuma.

Lakini ukasema siku nyingine nitatafakari, kisha ukamwomba Mungu, na kukaa katika utulivu ukairudia habari ile, utaona jambo jipya, limefunuliwa ndani yako, ambalo hukuwahi kulijua hapo mwanzo..

Wakati mwingine tena ukamwomba Roho Mtakatifu akusaidie, kisha ukarudia tena kusoma habari ile ile, utashangaa jambo lingine jipya unalipata ambalo siku za nyuma hukulipata..

Hivyo hivyo unavyozidi kuendelea, kurudia na kurudia ndivyo unavyolisafisha Neno la Mungu ndani yako,, Na matokeo yake ni kuwa, nguvu za Neno lake zinapenya katika roho yako, na kuleta mabadiliko makubwa sana, maishani mwako.

Shida inakuja pale, tunapodhani tumeimaliza biblia yote, pale tunaposoma habari Fulani na kujisemea moyoni, Aaah, tayari, yule kipofu Yesu aliishia kumpaka mate machoni akapona.. hivyo tunapita juu juu tu, kama sio kuiruka habari yote.

Wakati mwingine kanisani, unafundishwa, somo ambalo pengine ulishawahi kulisikia huko nyuma, na wewe badala ya kuwa mtulivu rohoni kusikiliza kwa makini, unasema, tayari hili nalifahamu..

Kumbuka, maneno safi ya Mungu, yanapatikana katika matanuru saba.

Hivyo natumai, kuanzia sasa sote, tutaacha kuwa wavivu wa kuyatafakari maandiko. Kwasababu lengo letu ni kuona nguvu za  Neno la Mungu kweli zikifanya katika Maisha yetu ya wokovu. Tujitahidi sana kujifunza biblia.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

EPUKA KUPELELEZA KILA KITU MUNGU ANACHOKUAHIDIA.

Biblia inamaana gani kusema “vipo sita, naam saba”?

IEPUKE GHADHABU YA MUNGU.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

Je Adamu na Hawa, walikuwa hawafanyi mema kabla ya kula tunda?

SWALI: Ni mema gani na mabaya gani, Adamu na Hawa waliambiwa watayajua?, Kwasababu Kama ni mema siwalikuwa wanayafanya hapo kabla?


JIBU: Ili tuweze kuelewa vizuri, tujifunze katika mifano ya kawaida ya maisha.

Haiwezekani mtu kujijua kwamba yeye ni mrefu kama hajakutana na mtu mfupi katika maisha yake..

Yeye siku zote atajiona yupo kawaida tu..lakini siku atakapokutana na aliowazidi kimo ndipo atakapojijua kumbe yeye ni mrefu.

Kadhalika haiwezekani kujijua kama kwasasa una afya kama hujawahi kupitiaga kuumwa…zaidi ya yote hutajua hata maana ya kuwa na afya ni nini.

Lakini siku ile utakapougua na hamu yote ya kula kupotea, ndipo utakapojijua kuwa kumbe siku kadhaa nyuma ulikuwa ni mwenye afya sana.

Vile vile haiwezekani kujijua kuwa unatenda wema kama hujawahi kuujua ubaya…

Wewe utakuwa unaufanya tu! Na kuona kawaaida, Lakini hutajua kama unachofanya ni kitu chema…siku utakapokuja kuuona ubaya, ukifanywa na mwingine..ndipo utakapojua kuwa kumbe wewe ulikuwa mwema. N.k

Sasa hiyo ni mifano tu ya kimaisha,Sasa tukirudi pale Edeni,jambo ni lile lile, Adamu na Hawa walikuwa wanatenda mema lakini walikuwa hawajijui kama wanatenda mema, mpaka siku walipofanya ubaya na kuona madhara yake.

Ndio maana Mungu aliwakataza Adamu na Hawa wasile yale matunda, maana yake wasiujaribu ubaya…kwasababu siku watakapoujaribu ndipo watakapojijua kuwa kumbe siku kadhaa nyuma walikuwa katika mema.

Maana yake watajujua kumbe walikuwa katika utakatifu..

Hiyo ndio maana ule mti ukajulikana kama ni mti wa UJUZI WA MEMA NA MABAYA …Na si mti tu wa UJUZI WA MABAYA..hapana! bali mema na mabaya.. kwasababu mambo hayo mawili yanakwenda pamoja…hayaachani…

Kadhalika na sisi tunapokuwa dhambini tunakuwa tunajiona tupo sawa na njia zetu hizo, Hatujioni kama tupo hatarini, wala matatizoni, tunaona ni kawaida maisha ndivyo yalivyo..

Lakini siku tunapompokea Yesu, na kuonja Mema.. ndipo macho yetu yanafumbuliwa na kuelewa kwamba kumbe maisha tuliyokuwa tunaishi yalikuwa ni maisha mabaya, yalikuwa yana kasoro nyingi, yalikuwa ni ya mateso, yalikuwa ya tabu na hatari…lakini tulipokuwa huko dhambini tulikuwa hatulioni hilo..

Na YESU KRISTO, Ndiye ule MTI WA UZIMA.
Kwamba kila atakayeonja matunda ya mti ule hatatamani tena mabaya..na macho yake yatafumbuliwa, na kujitambua na hivyo kujitenga mbali na dhambi..

Adamu na Hawa walipokula na kujijua kuwa wapo dhambini walitamani kurudi, lakini walishindwa kwasababu njia ilifungwa.

Lakini sasa njia imefunguliwa, ipo wazi na njia hiyo si nyingine zaidi ya YESU KRISTO.
Ni kwasababu gani leo unaona ulevi unaoufanya ni kawaida?..ni kwasababu bado hujampokea Yesu na macho yako kufumbuliwa..siku utakapoocha kipawa cha Roho Mtakatifu ndipo utajiona kuwa hizo pombe zilikuwa ni sumu, huo uasherati ulikuwa ni kitanzi na wala hauna raha yoyote zaidi ni mateso..

Ndipo utakapojua kuwa kumbe maisha ya chuki, vinyongo na visasi yalikuwa ni maisha ya shida.

Bwana leo anatuita wote..na anasema tuonje!..Maana yake tujaribu kula matunda hayo ya mti wa uzima, tuone kama tutatamani kubaki dhambini.

Zaburi 34:8 “Onjeni mwone ya kuwa BWANA yu mwema; Heri mtu yule anayemtumaini”.

Je! Umempokea Kristo?

Kama bado mlango wa kutubu upo wazi sasa, lakini hautakuwa hivyo siku zote. Mpokee Yesu leo akutue mizigo na utapata raha ambayo hujawahi kuipata.

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu”

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

JINSI EDENI ILIVYOKUWA.

Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

JIFUNZE KUELEWA MAANA YA KUOA/KUOLEWA KABLA YA KUINGIA HUKO.

MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA.

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

Rudi nyumbani

Print this post

YAPO MAJIRA YA KUONJWA NA BWANA.

Bwana alisema…

Zaburi 34:8

[8]Onjeni mwone ya kuwa BWANA yu mwema; 

Heri mtu yule anayemtumaini.

Maana yake ni kuwa Mungu ametoa nafasi kwa kila mtu ambaye yupo mbali na neema  kuonja au kujaribu kwanza uzuri ulioko ndani yake kabla hajauingia moja kwa moja..kwamfano kujaribu kungalia kama ndani ya Kristo kuna furaha, au amani, au upendo n.k.

Na pale mtu anapoona kuwa ipo basi anawajibika kumuishia Mungu maisha yake yote, lakini kama hajaiona basi anaruhusiwa kughahiri uamuzi wake..Na Ukweli ni kwamba hakuna aliyemjaribu Kristo akatamani kutoka baada ya hapo.

Lakini sio sisi tu tunaonja vya Mungu.. Mungu naye pia anayotabia ya kutuonja sisi auminifu wetu na uelekevu wetu kwake kama tunakidhi kweli vigezo vya yeye kutupa moja kwa moja kile tulichomuomba…au kutukaribia moja kwa moja milele.

Sasa hatua kama hii ukishafikia tambua kuwa unapaswa ung’ang’ane kweli kweli kwasababu huwa hakiwi kipindi cha raha sana.

Tukirudi kwenye biblia…tunaona wana wa Israeli walipotoka Misri, Mungu alikuwa nao karibu katika kiila hatua waliyopiga, walichokitaka walikipata wala hawakuachwa bila majibu..mpaka wanavuka bahari ya shamu wote wakawa wanamwimbia Mungu na kumchezea kwa shangwe kwa jinsi alivyowatendea miujiza mikubwa..Hivyo hilo likamvutia Mungu sana..Mungu akashawishika kushuka atembee nao milele katika furaha na raha..

Lakini kabla ya yeye kufanya vile ilimpasa kwanza AWAONJE..aone kama ni kweli wamekidhi vigezo vya yeye kuwa Mungu wao au la.

Hivyo alichofanya ni kuwaacha siku tatu kwa Kiu kule janwani pindi tu walipovuka bahari ya shamu, jambo ambalo hawajawahi kulipitia kabisa maisha yao yote tangu walipoanza kutembea na Mungu.. 

Tusome…

Kutoka 15:22-25

[22]Musa akawaongoza Israeli waende mbele kutoka Bahari ya Shamu, nao wakatokea kwa jangwa la Shuri; wakaenda safari ya siku tatu jangwani wasione maji.

[23]Walipofika mahali palipoitwa Mara hawakupata kuyanywa yale maji ya Mara, kwa kuwa yalikuwa machungu; kwa ajili ya hayo jina lake likaitwa Mara.

[24]Ndipo watu wakamnung’unikia Musa, wakisema, Tunywe nini?

[25]Naye akamlilia BWANA; BWANA akamwonyesha mti, naye akautia katika hayo maji, maji yakawa matamu. Basi akawawekea amri na hukumu huko, AKAWAONJA HUKO.

Unaona mstari wa 25 inasema Mungu akawaonja huko.kama kweli walimpenda kutoka moyoni au ni kwa miujiza tu..au kwa mikate tu..au kwa mafanikio tu..

Lakini tunaona wana wa Israeli walinung’unika badala ya kujinyenyekeza..Hivyo Mungu hakuona ukamilifu ndani yao.akajua kumbe walimpendea kwasababu walipata  raha tu lakini sio kwasababu ni Mungu wao..Laiti wangejinyenyeza ni wazi kuwa tangu ule wakati na kuendelea wasingekaa kusikia kitu kinachoitwa shida au taabu au masumbufu…

Ndugu yangu..Mungu akidhamiria kushuka kwako moja kwa moja kukaa na wewe au kukupa kitu fulani ulichomuomba ni sharti kwanza AKUONJE..uaminifu wako kama alivyofanya kwa Ibrahimu kumtoa mwanae Isaka..Hiyo ndio kanuni yake ambayo wana wa Israeli walishindwa kuielewa..

Soma pia Kumbukumbu 8:1-3 utaona Bwana akilisisitiza neno hilo hilo..

Hivyo ndugu uliyeokoka..lijue jambo hilo, liweke akiba moyoni mwako. Kabla hujawa rafiki wa Mungu wa milele ni sharti kwanza akuonje..ukikidhi vigezo basi ndio kimekuwa chako milele.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

BIRIKA LA SILOAMU.

USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

UFUNUO: Mlango wa 14

KUOTA MAFURIKO,KUOTA MAJI MENGI,KUOTA MAWIMBI.

Rudi nyumbani

Print this post

Risasi inayotajwa kwenye Ezekieli 27:12 ni ya namna gani?

 Je! ni risasi hizi tunazozijua za bunduki, au ni risasi ya namna gani?.


Jibu: Katika biblia kuna maneno yaliyotumika ambayo yakiletwa katika nyakati zetu, yanabadilika maana kabisa.. kwamfano utaona Neno “fisadi” likitajwa katika biblia.. Maana halisi ya neno hilo sio “mtu anayedhulumu fedha za umma”.. Bali maana halisi ya neno hilo ni “mtu anayefanya uasherati uliovuka mipaka”.

Hali kadhalika kuna neno kama “Fedha”.. Neno hili kama lilivyotumika nyakati za kale ni tofauti na linavyotumika leo, Leo hii ukizungumzia Fedha, moja kwa moja akili zinakwenda katika “Hela” iwe ya noti au sarafu. . Lakini kiuhalisia maana halisi ya neno Fedha sio “Hela”.. Bali ni madini aina ya “Fedha” kama vile yalivyo madini aina ya dhahabu.. Hata pale katika maandiko Bwana aliposema Fedha na dhahabu ni mali yangu,(Hagai 2:8) hakumaanisha “Hela na dhahabu”… bali alimaanisha madini aina ya fedha, na madini aina ya dhahabu, ndio mali za Bwana. ..

Sasa kwanini madini haya ya fedha leo ndio yamegeuzwa maana na kuwa Hela/pesa?..kiasi kwamba hela yoyote leo inaitwa fedha.

 Ni kwasababu tangu zamani hata sasa malighafi inayotumika kutengenezea sarafu nyingi, ni madini hayo ya fedha.. utaona sarafu nyingi, kama zile za sh.10, au 20 au 500 hazijatengenezwa kwa chuma, wala dhahabu bali zimetengenezwa kwa madini ya fedha,..hivyo hiyo ikafanya Hela zote zijulikane kama fedha..siku hizi hata Noti zote zinajulikana kama ni fedha, jambo ambalo kiuhalisia sio sawa.

Na madini ya fedha yanaweza kutumika kwa matumizi mbalimbali sio tu kutengenezea sarafu, bali pia vyombo vya chakula, urembo n.k..isipokuwa tumizi lililo maarufu ni hilo la kutengenezea Sarafu.

Kwa mantiki hiyo hiyo pia kwa Neno “Risasi”. Leo hii ukitaja neno risasi moja kwa moja akili za wengi zinakwenda kwenye kile kipande kidogo cha chuma kinachotoka ndani ya bunduki.

Lakini kiuhalisia hiyo sio maana ya Risasi.. Risasi ni aina nyingine ya madini, ijulikanayo kwa jina hilo.. kama vile ilivyo fedha, dhahabu, almasi, chuma, shaba  n.k.. Vivyo hivyo kuna madini aina ya Risasi ambayo kwa lugha ya kiingereza yanaitwa “Lead”.

Na madini haya yajulikanayo kama Risasi yanamatumizi mengi mbali mbali kama vile Fedha ilivyokuwa na matumizi mbali mbali sio tu kutengeneza sarafu, bali pia vitu vingine.. Kadhalika madini haya ya Risasi matumizi yake ambayo ni maarufu leo hii ni kutengenezea hicho kisilaha kidogo kijulikanacho kama risasi leo… lakini hayo sio matumizi pekee ya madini hayo, bali ina matumizi mengine mengi ambayo ndio hasaa yaliyokuwa yanatumika enzi za zamani.

Nyakati za biblia madini hayo ya Risasi, yalikuwa yanatumika sana sana katika kutengenezea vyombo vya kupikia, na kuhifadhia vitu vya moto sana, kwasababu yalikuwa ni magumu kuyeyuka hata kwa moto mkubwa, madini ya chuma yanawahi kuyeyuka kabla ya Risasi, kadhalika madini haya yalitumika kwaajili ya maandishi, yalikuwa ni bora kwa kuhifadhi maandishi kwa muda mrefu, tofauti na mengine yote. (Ayubu 19:24).

Hivyo yalikuwa ni madini ya kibiashara sana enzi za zamani na hata sasa.. Nyakati hizi yamezidi matumizi mpaka kufikia kutengeneza vifaa vya kisilaha kama hizi risasi zinazotumika katika bunduki.

Katika biblia madini hayo yameonekana yakitajwa katika sehemu kadhaa..

Ezekieli 27:12 “Tarshishi alikuwa mfanya biashara kwako, kwa sababu ya wingi wa utajiri wa kila aina; kwa fedha, na chuma, na bati, na risasi, walifanya biashara, wapate vitu vyako vilivyouzwa”.

Unaweza kuyapata pia katika vitabu vifuatavyo… Hesabu 31:22, Yeremia 6:29 na Zekaria 5:7

Lakini katika roho sisi watu wa Mungu tunafananishwa na vitu hivyo vya thamani.. kama fedha, dhahabu, almasi n.k

Kama vile chuma na dhahabu ili viwe imara na ili ving’ae ni lazima vipitishwe kwenye moto, na watu wa Mungu waliookoka ili wawe wa thamani mbele za Mungu ni lazima wapitishwe kwenye moto (yaani majaribu mbali mbali).

Kadhalika ili risasi iwe bora ni lazima ipitishwe nayo kwenye moto.. Na sisi tunafananishwa na risasi za Bwana.. na matumizi makubwa ya risasi katika zama zetu hizi ni SILAHA, Kadhalika na sisi ni silaha za Bwana, dhidi ya majeshi yote ya adui..Ili tuwe imara hatuna budi kupitishwa katika moto.. Ndivyo maandiko yanavyosema…

Ezekieli 22:18 “Mwanadamu, nyumba ya Israeli imekuwa taka za fedha kwangu; wote wamekuwa shaba, na bati, na chuma, NA RISASI, kati ya tanuu; wamekuwa taka za fedha.

19 Basi Bwana MUNGU asema hivi; Kwa sababu ninyi nyote mmekuwa taka za fedha, tazama, nitawakusanya kati ya Yerusalemu.

20 Kama vile watu wakusanyavyo FEDHA, NA SHABA, NA CHUMA, NA RISASI, NA BATI, KATI YA TANUU, ILI KUVIFUKUTIA MOTO NA KUVIYEYUSHA; ndivyo nitakavyowakusanya ninyi katika hasira yangu, na ghadhabu yangu, nami nitawalaza huko, na kuwayeyusha.

21 Naam, nitawakusanya, na kuwafukutia moto wa ghadhabu yangu, nanyi mtayeyushwa kati yake”.

Je umempokea Yesu?.. je wewe ni dhahabu safi?, ni fedha safi?, ni Risasi safi kwa Bwana?.. kama bado unasubiri nini?..Unawezaje kuishi maisha ya namna hayo yasiyo na thamani yoyote mbele za Mungu..Mpokee Kristo leo, na ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo, upate ondoleo la dhambi, na Bwana atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu, atakayekuongoza katika kweli yote.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Ni kwa namna gani malaika wa mbinguni wanaweza kutuhubiria sisi injili?

APENDAYE FEDHA HASHIBI FEDHA.

Fuawe ni nini? Kama tunavyosoma katika Isaya 41:7

KUNA UMUHIMU WA KUWA MTU WA KURIDHIKA.

ONDOA TAKATAKA KATIKA FEDHA, NA CHOMBO KITATOKEA KWA MTAKASAJI.

Ufisadi una maanisha nini katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Neno Saumu lina maana gani katika biblia?

JIBU: Saumu ni neno lenye asili ya lugha ya “kiaramu” lenye maana ya “kujizua kufanya jambo/kitu fulani kwa ajili ya ibada”.

Hivyo pale mtu anapoacha kula kwa kipindi fulani, kwa ajili ya sala..Mtu huyo yupo katika saumu.au kwa jina tulilolizoea tunasema yupo katika mfungo.

Neno hilo utalipata katika vifungu hivi kwenye biblia..

Zekaria 8:19

[19]BWANA wa majeshi asema hivi, Saumu ya mwezi wa nne, na saumu ya mwezi wa tano, na saumu ya mwezi wa saba, na saumu ya mwezi wa kumi, zitakuwa furaha na shangwe, na sikukuu za kuchangamkia, kwa nyumba ya Yuda; basi zipendeni kweli na amani.

Yoeli 1:14

[14]Takaseni saumu, iteni kusanyiko la dini, 

Wazee na wakusanye wenyeji wote wa nchi; Waende nyumbani kwa BWANA, Mungu wenu, Na kumlilia BWANA,

Soma pia Yoeli 2:15.utaliona neno hilo.

Saumu ya kweli ni ipi?

Lakini pia tofauti na wengi tunavyodhani..kwamba saumu inayompendeza Mungu ni ile ya chakula tu..ni kweli hiyo anaitazama lakini sio kiini cha saumu anayotaka kuiona ndani ya mtu.. Saumu anayoipokea ni ile ya kufunga vifungo vya uovu na dhambi.

Isaya 58:3-8

[3]Husema, Mbona tumefunga, lakini huoni? Mbona tumejitaabisha nafsi zetu, lakini huangalii? Fahamuni, siku ya kufunga kwenu mnatafuta anasa zenu wenyewe, na kuwalemea wote watendao kazi kwenu.

[4]Tazama, ninyi mwafunga mpate kushindana na kugombana, na kupiga kwa ngumi ya uovu. Hamfungi siku hii ya leo hata kuisikizisha sauti yenu juu.

[5]Je! Kufunga namna hii ni SAUMU niliyoichagua mimi? Je! Ni siku ya mtu kujitaabisha nafsi yake? Ni kuinama kichwa kama unyasi, na kutanda nguo za magunia na majivu chini yake? Je! Utasema ni siku ya kufunga, na ya kukubaliwa na BWANA?

[6]Je! Saumu niliyoichagua, siyo ya namna hii? Kufungua vifungo vya uovu, kuzilegeza kamba za nira, kuwaacha huru walioonewa, na kwamba mvunje kila nira?

[7]Je! Siyo kuwagawia wenye njaa chakula chako, na kuwaleta maskini waliotupwa nje nyumbani kwako? Umwonapo mtu aliye uchi, umvike nguo; wala usijifiche na mtu mwenye damu moja nawe?

[8]Ndipo nuru yako itakapopambazuka kama asubuhi, na afya yako itatokea mara; na haki yako itakutangulia; utukufu wa BWANA utakufuata nyuma ukulinde.

Umeona? Hivyo na wewe ufungapo basi fahamu kuwa Mungu anatazamia kuona mageuzi makubwa ya maisha yako dhidi ya dhambi na kutenda haki. Usifunge tu kidini ili kutumiza sheria.Funga kwa lengo la kuwa mkamilifu mbele zake.

Vinginevyo unaweza ukafunga hata siku 40 usiku na mchana bila kula, kama Musa na Mungu bado akaona unafanya kazi bure.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

KWARESMA IPO KIMAANDIKO?

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

Mafundisho

Rudi nyumbani

Print this post

MWISHO WA MAVUNO, NI MWISHO WA DUNIA.

Si kila tunayemuhubiria, ni lazima tuone matokeo ya papo kwa papo ya badiliko.. Ni kweli tunatamani iwe hivyo kwa watu wote , na wakati mwingine ukiwa kama muhubiri unaweza kuvunjika moyo, pale ambapo unazunguka kila mahali, mwezi mzima, au mwaka mzima, kuhubiri, halafu hufanikiwi kupata tunda lolote la kudumu, au hata ukiyapata basi ni machache sana, ukilinganisha na nguvu ulizowekeza hapo.

Lakini ukiwa katika hali kama hiyo, jambo ambalo unapaswa usilitoe katika akili yako ni kuwa, mwisho wa mavuno sio siku hiyo unayohubiri, mwisho wa mavuno sio leo uliyopo mkononi mwako. Mwisho wa mavuno utakuwa ni siku ile ya mwisho, Mungu atakapotuma malaika zake, kuyatenganisha magugu na ngano. Na ngano kuziweka ghalani,  sio sasa.

Mathayo 13:39b … mavuno ni mwisho wa dunia; na wale wavunao ni malaika….

49 Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki,

Kwahiyo ndugu, huyo mtu unayemshuhudia/ unaowashuhudia, ikiwa hawaonyeshi badiliko leo, bado wewe endelea kuhubiri, kwasababu wakati wa kuhitimisha kila kitu bado. Pengine leo unapanda mbegu, mwingine kesho atatia maji, au wewe unatia maji leo, mwingine atapalilia, au wewe utapalilia mwingine atamalizia kuvuna,.kabla ya mwisho wa mavuno kufika.

Kwahiyo, usivunjwe moyo sana, mwisho wa dunia bado, japo upo karibu sana, hivyo wewe endelea kuingaza nuru ya Kristo katika hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho, hata kama matunda hutayaona sasa. Mwachie Mungu amalize kazi zake. Kwasababu Biblia inasema..

Mhubiri 11: 4 Mwenye kuuangalia upepo hatapanda; Naye ayatazamaye mawingu hatavuna.

Songa mbele. Tangaza habari za Kristo.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?

AHADI YA ROHO ILIYOSALIA SASA KWA KIPINDI CHETU.

Ahera ni wapi? Kama tunavyosoma katika biblia.

UPO UMUHIMU MKUBWA WA KUMTOLEA BWANA!

Rudi nyumbani

Print this post

UPO UMUHIMU MKUBWA WA KUMTOLEA BWANA!

Jina la Mwokozi wetu, Yesu libarikiwe..
Karibu tujifunze biblia, leo tutajifunza jambo dogo, linalohusiana na faida za kumtolea Bwana.

Moja ya mambo ambayo shetani kayakoroga sana katika Ukristo na nje ya ukristo, ni suala la utoaji.

Shetani hataki watu wanaomjua Mungu wawe watoaji na hata wale wasiomjua Mungu wawe watoaji.

Kwasababu anajua hata mtu asiyemjua Kristo akiwa mtoaji, basi atapata thawabu kwa hicho…kwahiyo atajitahidi kumpandikizia mtu roho ya kutokutoa kwa gharama zozote, hata akisikia jambo lolote linalohusiana na kutoa asisikilize, na hata achukie kabisa.

Lakini nataka nikuambie.. Chochote unachokitoa aidha kwa Bwana au kwa mtu , kina thamani kubwa sana kwake yule unayekipokea…Kama ni Kristo au kama ni mwanadamu mwenzako.

Sijui kama umewahi kupitia mazingira fulani ambayo upo katika hali ya kuhitaji sana, halafu anatokea mtu anakusaidia, au anakukopesha…kuna furaha fulani unaipata isiyokuwa ya kawaida.

Sasa wengi wetu tunafikiri ni sisi tu waanadamu ndio tunapitia hayo mazingira ya kupungukiwa na kuhitaji msaada..Lakini leo nataka nikuambie ya kwamba futa hayo mawazo… Hata Kristo naye ambaye ni Mungu, anapitia hayo mazingira kila siku, na anatafuta watu wa kumsaidia, Ingawa yeye ana kila kitu..

Kikawaida ukiwa na mtoto au watoto wanaokupenda na wewe unawapenda, halafu uwaone wanapitia shida..ni wazi kuwa wewe ndio utateseka zaidi na kupitia shida zaidi..kwasababu kwanza ni damu yako, na vile vile wapo moyoni mwako..

Na Kristo naye ni hivyo hivyo, wale wote ambao wapo katika agano la damu yake, na wapo moyoni mwake, na yeye yupo mioyoni mwao..wanapopitia matatizo ni yeye ndiye anayekuwa katika shida..zaidi hata ya yule anayepitia shida.

Kwahiyo hata Kristo naye anapitia shida hata sasa, ndivyo maandiko yanavyosema..

Mathayo 25:41 “Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;

42 kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe;

43 nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama.

44 Ndipo hao pia watajibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie?

45 Naye atawajibu, akisema, Amin, nawaambia, Kadiri msivyomtendea mmojawapo wa hao walio wadogo, hamkunitendea mimi.

46 Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa mmilele”.

Umeona?

Na “Wadogo” wanaozungumziwa hapo sio wale watu wanaosimama njiani na kuomba, ambao wengi wao ni watu wakidunia na walevi, watukanaji, na hata wengine wanamtukana Kristo hadharani..

Bali “wadogo”, Kristo anawaozungumzia hapo ni wale ambao “Ndani yao yupo Kristo wa kweli”… Lakini wapo katika mahitaji pengine kutokana na kuishikilia imani yao, wapo vifungoni pengine kutokana na kuhubiri injili, hawana chakula, mavazi n.k kutokana na mambo ya kiimani wanayoyafanya. Hao ndio ambao ukiwasaidia unakuwa umemsaidia Kristo mwenyewe…Kwasababu Kristo yupo ndani yao.

Sasa kuna aina ya mahubiri, yameenea sana leo, kwamba watu wote waliompokea Kristo, hawapitii kabisa kipindi cha kuwa na mahitaji.. Nataka nikuambie hiyo injili si ya ukweli..watu waliookoka watapitia vipindi vyote, vya kupungukiwa na vya kuongezekewa, watapitia vipindi vya magonjwa, watapitia vipindi vya vifungo, na dhiki kwasababu bado wapo ulimwenguni..Lakini hiyo haimaanishi kuwa hawatapitia pia vipindi vya raha, watavipitia lakini pia vya dhiki watakutana navyo.

Sasa katika wakati kama huo, ambao unaona watu wa Mungu wapo katika hali ya kuhitaji, huo ndio wakati wa kujizombea baraka..kwasababu ukiwasaidia hao, umemsaidia Kristo mwenyewe..Mungu anaruhusu watu wake wawe hivyo, sio kwamba hawezi kuwatajirisha ghafla la!..bali anawafanya hivyo, ili watu wengine wapate nafasi ya kubarikiwa kwa kuwasaidia.

Kwahiyo ndugu usikwepe hata kidogo kumtolea Bwana kwasababu kuna thawabu kubwa, Bwana Yesu mwenyewe alisema maneno haya…

Marko 9:41 “Kwa kuwa ye yote atakayewanywesha ninyi kikombe cha maji, kwa kuwa ninyi ni watu wa Kristo, amin, nawaambia, hatakosa thawabu yake”.

Na hilo sio jukumu la kundi fulani tu la watu, kwamba ni watu fulani wenye uwezo ndio wanapaswa wamtolee Bwana..Au kwamba ni washirika na waumini tu, hapana!..bali ni la watu wote, walio wahudumu na wasio wahudumu…Watumishi na wasio watumishi. Wote hatuna budi kumtolea Bwana kwa namna hiyo, kama tunataka kubarikiwa.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

DALILI ZIPI ZITAMTAMBULISHA MTU KUWA AMEFANYIKA KIUMBE KIPYA?

Zile Rangi saba za Upinde wa Mvua zinawakilisha nini?

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

Katika (Mathayo 25:8 na Marko 16:8) Wale wanawake walitangaza kufufuka kwa Bwana au walikaa kimya?

MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

Rudi nyumbani

Print this post