Je! Kuna malaika wangapi mbinguni?

Je! Kuna malaika wangapi mbinguni?

Biblia haijatoa idadi kamili ya malaika Mungu aliowaumba, inatumia neno “MAJESHI” ambayo majeshi yenyewe  hayo yapo maelfu kwa maelfu.

Waebrania 12:22 “Bali ninyi mmeufikilia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na MAJESHI ya malaika ELFU NYINGI”,

Umeona ni wengi sana kiasi kwamba hata mwandishi ameshindwa kutoa idadi kamili ya majeshi hayo, anaishia kusema tu elfu NYINGI..maana yake hayahesabiki.

Sehemu nyingine, inasema  idadi yake ni elfu mara elfu na elfu kumi mara elfu kumi..utaona hapo mwandishi bado  anapata shida kuelezea idadi hiyo  kamili ya malaika hao, jinsi walivyo wengi, Ni malfu mengi yanayojizidisha, na kujizidisha na kujizidisha..

Ufunuo 5:11 “Nikaona nikasikia sauti ya malaika wengi pande zote za kile kiti cha enzi, na za wale wenye uhai, na za wale wazee, na hesabu yao ilikuwa elfu kumi mara elfu kumi na elfu mara elfu,”

Katika biblia Malaika wapo wa aina tofauti tofauti,

Wapo malaika wa Sifa: Hawa wapo mbele za Mungu usiku na mchana kuilinda enzi yake, ndio wale Maserafi na makerubi; ambao tunawasoma kwenye biblia. Ezekieli 1:4-28, Isaya 6:2-6

Wapo malaika wa vita: Mfano wa hawa ni Mikaeli na malaika zake: 2Wafalme 6:17, Ufunuo 12:7, Yeremia 5:14, 38:17, Hosea 12:5

Wapo malaika wajumbe: Mfano wake ni  Gabrieli. Danieli 8:16, 9:21, Luka 1:19,26.

Wapo malaika wa vitu vya asili tu: kama vile moto, maji n.k. Ufunuo 16:5, 14:18

Wapo malaika wa ulinzi, (Mji, na mataifa): Danieli 4:13

Wapo malaika wa ulinzi (wanadamu): Mathayo 18:10, Zaburi 34:7

Wapo malaika wa Huduma (watumishi):  Matendo 5:19, 7:30, 8:26, 12:15, 27:23,Waebrania 1:14,

Wapo malaika wa mapigo: Zaburi 78:49, Ufunuo 16

Wapo malaika wa uponyaji: Yohana 5:4, Isaya 6:7

Pamoja na hayo wapo pia malaika walioasi. Ambao biblia inatuambia walikuwa ni theluthi tu ya malaika wote waliokuwa mbinguni. Na hao idadi yao haihesabiki, katikati yao kuna ambao wapo vifungoni saa hii wanasubiria hukumu ya mwisho, (Yuda 1:6)  

Wengine wapo  vifungoni lakini watakuja kuachiliwa kwa muda kidogo wafanye kazi duniani kwa muda mfupi kisha wataondolewa(Ufunuo 9:1-11),

na wengine wapo  bado hapa hapa duniani wakizurura zurura tu kuwaharibu watu, na kusababisha maovu duniani..

Jaribu tu kutengeneza picha tu  yale mapepo yaliyomwingia Yule kichaa, kule makaburini, Yesu alipowauliza jina lako nani, yakasema LEGIONI, yaani jeshi, yakimaanisha hatuhesabiki..Sasa Kama ndani ya mtu mmoja yanaweza kukaa mapepo yasiyohesabika, jiulize mapepo yaliyopo ndani ya watu wote ambao hawajampa Kristo maisha yao leo hii yapo mangapi?

Hivyo hiyo inafanya idadi ya malaika  ambao Mungu aliwaumba kuwa nyingi sana isiyoweza kuhesabika, hata zaidi ya idadi ya wanadamu wote walioishi na wanaoishi duniani tangu dunia iumbwe.

Hiyo ni kutuonyesha jinsi Mungu alivyojawa na uweza na nguvu na utukufu.

Zaburi 139:17 “Mungu, fikira zako zina thamani nyingi kwangu; Jinsi ilivyo kubwa jumla yake!

18 KAMA NINGEZIHESABU NI NYINGI KULIKO MCHANGA; NIAMKAPO NIKALI PAMOJA NAWE”.

JINA LA BWANA LIHIMIDIWE DAIMA.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nitaitofautishaje sauti ya Malaika na ya Roho Mtakatifu?

Kwanini Mungu anasema “Afanyaye malaika zake kuwa pepo”?

MALAIKA WAPELELEZI WA HUKUMU WANAPITA SASA.

 KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA.

UTAWALA WA MIAKA 1000.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments