SWALI: Naomba kufahamu Biblia unapozungumzia kuhusu kupewa jina jipya inamaanisha nini?
JIBU: Kazi ya jina sio tu kumtambulisha au kumtofautisha mtu mmoja na mwingine. Bali jina linasimama pia kueleza Wasifa wa mtu,
Hivyo jina la mtu linapobadilika, aidha Wasifa pia hubadilika.
Kwamfano Ibrahimu alipobadilishwa jina kutoka Abramu na Kuwa Ibrahimu ni kwasababu alikuwa anaenda kuwa Baba wa mataifa mengi.(Mwanzo 17:5)
Vilevile Sarai kuitwa Sara. Ni kwasababu anaenda kuwa mama wa mataifa mengi..(Mwanzo 17:15)
Sauli kuwa Paulo kwasababu anaenda kuwa mtume kwa mataifa.(Matendo 13:9)
Vivyo hivyo tunaona Mungu katika maandiko Akijitambulisha kwa majina mbalimbali, lengo sio kuonyesha uzuri au upekee wa majina yake hapana bali kutambulisha wasifa wake.
Kwamfano alipojitambulisha kama Yehova rafa, alisimama kama Mungu mponyaji..Yehova yire Mungu atupaye, Yeshua(Yesu), kama Mungu atuokoaye.
Tukirudi kwa wakati wa sasa Biblia Inatuonyesha kuwa Kristo atakaporudi mara ya pili atakuja na jina lingine jipya. Ambalo ndio tunangojea kuona utukufu wake, mamlaka yake na nguvu zake.
Ufunuo wa Yohana 3:12
[12]Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya.
Jina hili halitakuwa Yesu,tulitumialo sasa ambalo linawasifa wa wokovu, lililojikita katika kiwakomboa na kuwafungua wanadamu katika mauti na vifungo vya kila namna.
Lakini hilo linalokuja litakuwa ni jina lenye uweza Mwingi, la kifalme, la kiutawala zaidi. Wakati huo Kristo hataonekana tena kama mwanakondoo mpole, asimamaye kutuombea kwa Baba N.k..hapana ataonekana katika taswira mpya kabisa ya kifalme, na zaidi ya hapo (Ufunuo 19:11-16), sawasawa na hilo jina lake litakavyokuwa.
Ndio maana kuna umuhimu sana kuokoka sasa, angali neema na msamaha upo katika jina la YESU, kwasababu atakaporudi mara ya pili,na jina jipya hatajua kusamehe ni nini, bali mambo mengine mapya yatakuwa wanaendelea..Usipookoka leo hakuna wokovu siku ya mwisho.
Vilevile wale watakaoshinda Kristo ana ahidi kuwapa majina mapya ya kipekee, ambayo yatawanafisisha kipekee mbele ya Kristo.
Ufunuo wa Yohana 2:17
[17]Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua mtu ila yeye anayelipokea.
Ndugu Utukufu Unaokuja wa Kristo ni mkuu sana, ni heri ukose vyote sasa, lakini usikose mbingu Mpya na nchi mpya na ile Yerusalemu mpya ishukayo kutoka kwa Baba mbinguni.
Siku hizi ni za mwisho, unyakuo umekaribia sana. Mambo ya umilele yanakaribia kuanza. Bado unaendelea kung’ang’ana na ya kidunia? tubu leo mgeukie Kristo.
Bwana akubariki.
Amen.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Majina mbalimbali ya Mungu na maana zake.
JE NI LAZIMA KUBADILISHA JINA BAADA YA KUOKOKA?
Nini maana ya “Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi”?
SWALI: Je mtu anaweza akawa hajaokoka akaombea mtu na Pepo likamtoka, na pia mtu anaweza akawa ameokoka akaombea mtu na pepo lisitoke ?
JIBU: Kuhusu swali la kwanza linalosema je mtu anaweza akawa hajaokoka kisha akaenda kuombea mtu mwenye pepo na hatimaye likamtoka?
Jibu ni la!, haiwezekani mtu ambaye hajaokoka, akawa na uwezo wa kutoa pepo, kwasababu pale alipo yupo chini ya vifungo vya ibilisi, haiwezekani akaenda kumfungua mtu ambaye ni mfungwa mwenzake, inahitaji mtu aliye huru ndio aweze kufanya hivyo.
Bwana Yesu alisema…
Marko 3:23-27
[23]Akawaita, akawaambia kwa mifano, Awezaje Shetani kumtoa Shetani?
[24]Na ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, ufalme huo hauwezi kusimama;
[25]na nyumba ikifitinika juu ya nafsi yake, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
[26]Na kama Shetani ameondoka juu ya nafsi yake, akafitinika, hawezi kusimama, bali huwa na kikomo.
[27]Hawezi mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu, na kuviteka vitu vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu; ndipo atakapoiteka nyumba yake.
Ni hatari huyo mtu akijaribu kufanya hivyo, kwasababu anaweza kukutana na madhara kama yaliyowakuta wale wana wa Skewa.(Matendo 19:13-16).
Kuhusu swali la pili linalouliza Je mtu ambaye ameokoka anaweza akaombea na pepo lisitoke?
Jibu ni ndio Ikiwa mtu huyo anakiwango kidogo cha imani, si mapepo yote yanaweza yakatoka, kwasababu mashetani yanatofautiana kimadaraja (Mathayo 12:43-45), yapo yenye nguvu kubwa ya ukinzani, mengine huitwa wakuu wa giza, mengine wafalme na wenye mamlaka. (Waefeso 6:12)
Hivyo inahitaji nguvu zaidi za kiimani ambazo zinakuja kwa njia ya mifungo na maombi.
Ndio maana mitume kuna mahali walitoa kweli pepo wengi lakini kuna mahali hawakuweza kwasababu ya uhaba wa maombi. (Mathayo 17:14-21)
Lakini uhalisia ni kuwa mtu yeyote aliyeokoka, haijalishi amedumu sana katika wokovu au ni mchanga. Anayo mamlaka ndani yake ya kutoa pepo lolote lile, isipokuwa anahitaji pia na maombi ile mengine yasishindikane kwake.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Swali: Maana ya Madhali ni nini kama ilivyotumika hapo katika Zaburi 21:11
Jibu: Turejee…
Zaburi 21:11 “Madhali walinuia kukutenda mabaya, Waliwaza hila wasipate kuitimiza”.
Neno “Madhali” limeonekana mara moja tu kwenye biblia yote, na maana yake ni “Ingawa” Hivyo Kiswahili kingine cha neno “Ingawa” ni “Madhali” …
Kwahiyo maandiko hayo yanaweza kuweleweka pia hivi…“Ingawa walinuia kukutenda mabaya, Waliwaza hila wasipate kuitimiza”.
Madhara yanayonuiwa na watu wabaya, ikiwa tupo ndani ya Kristo, hayataweza kushinda juu yetu, haijalishi yataonekana yamekomaa kiasi gani.
Je umempokea BWANA YESU?..
Unao wokovu ndani yako?
Waebrania 10:37 “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia”.
Maran atha
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Swali: Tunasoma Simeoni alipomwona mtoto YESU, Alikiri kuuona Wokovu wa MUNGU, sasa swali ni Wokovu gani huo alioupata?
Jibu: Tuanzie ule mstari wa 25 ili tuweze kuelewa vyema…
Luka 2:25 “Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
26 Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana.
27 Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria,
28 yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema,
29 Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako, Kwa amani, kama ulivyosema;
30 KWA KUWA MACHO YANGU YAMEUONA WOKOVU WAKO,
31 Uliouweka tayari machoni pa watu wote;
32 Nuru ya kuwa mwangaza wa Mataifa, Na kuwa utukufu wa watu wako Israeli”
Sasa hapo hajasema AMEUPATA WOKOVU..La! bali anasema “MACHO YANGU YAMEUONA WOKOVU”.. kuuona wokovu na kuupata wokovu ni vitu viwili tofauti…
Wokovu wa Mungu unapatikana kupitia mmoja tu, naye ni YESU KRISTO (Matendo 4:12),..Baada ya YESU kusulibiwa ndipo watu wakaanza kuupata wokovu, lakini kabla ya hapo waliusikia na kuuona tu,…waliousikia ni manabii wa kale na watu wote wa agano la kale, na waliouona ni watu waliokuwepo kipindi BWANA YESU anazaliwa, na walioupata ni wote waliomwamini baada ya kufufuka kwake.
Sasa utauliza vipi waliokufa katika haki wakati wa agano la kale, je hawakupata wokovu kabisa katika kipindi chao?… Jibu ni kwamba baada ya kufa kwao wokovu wao ulikuwa haujakamilika, lakini KRISTO aliposhuka kuzimu na kuchukua mamlaka yote ya walio hai na waliokufa, ndipo wokovu wao ukakamilika (maana yake wakaupata wokovu).
1Petro 1:10 “Katika habari ya wokovu huo manabii walitafuta-tafuta na kuchunguza-chunguza, ambao walitabiri habari za neema itakayowafikia ninyi.
11 Wakatafuta ni wakati upi, na wakati wa namna gani ulioonywa na Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao, ambaye alitangulia kuyashuhudia mateso yatakayompata Kristo, na utukufu utakaokuwako baada ya hayo.
12 Wakafunuliwa ya kuwa si kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili yenu walihudumu katika mambo hayo, ambayo sasa yamehubiriwa kwenu na wale waliowahubiri ninyi Injili kwa Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni. Mambo hayo malaika wanatamani kuyachungulia”.
Kwahiyo Simoni aliuona Wokovu, kwakuwa anayebeba wokovu (YESU KRISTO) yupo pale.
Na wote tunaomwamini sasa, tunapokea wokovu wa roho zetu.
Je umempokea YESU?… Je umeoshwa dhambi zako kwa damu yake?
Matendo 4:12 “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo”
Maran atha.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
FAHAMU KANUNI ZA KUZISUBIRIA AHADI ZA MUNGU?
Nini tofauti ya haya maneno. 1) KUOKOKA, 2) WOKOVU, 3) KUONGOKA.?
Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?
UKIAMINI NA UKIMKIRI YESU KWA KINYWA CHAKO, UTAOKOKA.
Musa alikuwa na sababu kadha wa kadha za yeye kufanye vile, ikiwemo
Kutoka 3:11
[11]Musa akamwambia Mungu, Mimi ni nani, hata niende kwa Farao, nikawatoe wana wa Israeli watoke Misri?
Musa aliogopa, kwenda kuwahubiria watu juu ya Mungu Ambaye hakulijua jina lake, kwani zamani zile, miungu yote ilifahamika kwa majina, hivyo alijiona kama kwenda kuwaambia watu habari za Mungu asiyejulikana jina lake, ni kama anawafedhehi.
Kutoka 3:13 Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n’nani? Niwaambie nini?
Kutoka 4:1
[1]Musa akajibu akasema, Lakini, tazama, hawataniamini, wala hawataisikia sauti yangu; maana watasema, BWANA hakukutokea.
Kwasababu alikuwa hana ishara yoyote ya ki-Mungu ndani yake.
Kutoka 4:10
[10]Musa akamwambia BWANA Ee Bwana, mimi si msemaji, tokea zamani, wala tokea hapo uliposema na mtumishi wako; maana mimi si mwepesi wa kusema, na ulimi wangu ni mzito.
Pamoja na Mungu kumwakikishia kuwa atakuwa naye na kumsaidia lakini Musa bado akakataa, ndipo Mungu akaghadhibika na kumletea nduguye Haruni, kama msaidizi wake.
Jambo ambalo halikuwa mpango wa awali wa Mungu, kwani uongozi wa Haruni hakuwa kusudi kamilifu la Bwana. Sababu kadha wa kadha zilizowapelekea wana wa Israeli kupata adhabu, zilikuwa ni pamoja na uongozi dhaifu wa Haruni. Utakumbuka wakati Musa amepanda juu mlimani kuchukua zile mbao mbili za amri 10, Haruni aliachiwa uongozi kwa muda, watu walipomfuata Kwa ajili ya hatma zao, akasikiliza mapendekezo yao akawaundia sanamu ya ndama ili waiabudu, ikapelekea Mungu kuwaangamiza wana wa Israeli wengi sana, (Kutoka 32:1-6) mzizi huo ni kutokana na kutokutii kwa Musa, halikadhalika sababu ya Musa kutoiona nchi ya ahadi ilichangiwa pia na uongozi hafifu wa Haruni, kwani kule Meriba kosa alilofinya Musa la kuchukua utukufu wa Mungu, alihusika na Haruni pia. (Hesabu 20:10-12)
Hivyo ni wazi kama angekuwa na imani na Mungu, mengi yasingetokea mbeleni. Hata wakati huu wa sasa, wengi wetu tumejikuta katika machaguzi ya pili ya Mungu kwasababu tu, ya kumpotezea imani, kuwa anaweza kutenda kusudi lake lote hata katika Madhaifu yetu.
Mwamini Mungu mtegemee yeye tu.
Shikilia vifungu hivi vikusaidie.
Mithali 3:5
[5]Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
Isaya 6:8
[8]Kisha nikaisikia sauti ya Bwana, akisema, Nimtume nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu? Ndipo niliposema, Mimi hapa, nitume mimi.
2 Timotheo 1:7
[7]Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini Mungu alimchagua Musa, na si mtu mwingine?
Je ni sala gani inahitajika kabla ya kumchinja mnyama katika ukristo?
Je maombi ya mlimani yana ulazima wowote kwa mkristo?
Mungu hakumchagua Musa kwasababu ya wema, au kipawa, au ujuzi fulani aliokuwa nao tofauti na wengine. Hapana almchagua ili ‘kutumiza kusudi lake la kuchagua’ ambalo tunalisoma kwa urefu katika (Warumi 9:11-17). Linalomaanisha Mungu humchagua mtu na kumfanya awe kama anavyotaka mwenyewe, na sio kwa jinsi Yule mtu atakavyo. Kwamfano alimchagua Farao, kisha akamwekea moyo mgumu,ili atimize kusudi lake mwenyewe, kujichotea utukufu kwa mapigo yale kumi,aliyoyaachia kwa wamisri, vivyo hivyo na kwa Musa alimchagua na kumpa neema ile kubwa ya hofu ya Ki-Mungu na upole ili atimize kusudi lake la kuwakomboa wana wa Israeli.
Lakini hakuwa na tendo lolote jema alilowahi kutenda lililomshawishi Mungu amchague yeye tofauti na wengine.
Na ndivyo anavyofanya hata sasa kwa wanadamu wote. Tunaokolewa na kutumiwa na Mungu kwa neema tu, na si kwasababu ya matendo Fulani mema tuliyowahi kumtendea Mungu.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Nini tofauti ya Majira na Wakati?
Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?
NAAM, HATA WABAYA KWA SIKU YA UBAYA.
Swali: Je sisi wakristo tunapaswa tuombe sala gani kabla kumchinja mnyama?, maana Imani nyingine tunaona kabla kuchinja wanatanguliza sala.
Jibu: Katika biblia hatujapewa maagizo yoyote ya kuomba sala, au kukiri maneno Fulani kabla ya kumchinja mnyama. Ndio zipo Imani zinazoelekeza kufanya hivyo, lakini si Biblia takatifu.
Maagizo tu yaliyopo katika biblia ni kushukuru kabla ya kula..lakini kupiga sala kabla ya kuchinja hatujapewa kwani hatuendi kutoa sadaka kwa miungu bali ni kwaajili ya kitoweo.
Katika agano la kale, wanyama waliombewa kabla ya kuchinjwa iwapo wanaenda kutolewa kama sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana (dhabihu).
Walawi 4:32 “Naye akileta mwana-kondoo kuwa sadaka ya dhambi, ataleta wa kike mkamilifu.
33 Naye ataweka mkono wake kichwani mwake sadaka ya dhambi, kisha atamchinja awe sadaka ya dhambi, mahali hapo wachinjapo sadaka ya kuteketezwa”.
Lakini katika agano jipya dhabihu ya mwili wa YESU ilishatolewa, (hiyo ndio dhabihu kamilifu)…sasa wanyama wanachinjwa kwaajili ya vitoweo, na si kwaajili ya sadaka.. na hakuna sala yoyote inayotangulia, na hata wanaoomba hizo dua bado kuna viumbe vitawafunga katika sheria hiyo, kwamaana samaki au dagaa au wadudu kama kumbikumbi au senene unawaombeaje dua kabla ya kutoa uhai wao?… utaombea dagaa mmoja mmoja??..ni jambo lisilowezekana vinginevyo hatutakula kabisa.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba hakuna sala inayotangulia kabla ya kuchinja au kuutoa uhai wa kiumbe chochote kwaajili ya chakula.. Na kufahamu kwa urefu kama wakristo anaruhusiwa kula nyama ya mnyama aliyechinjwa kwa dua, basi fungua hapa >>UKWELI KUHUSU UISLAMU Sehemu ya Pili: (Jiwe/Jabali la Kaaba).
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Jibu: Turejee..
Mwanzo 15:16 “Na kizazi cha nne kitarudi hapa, maana haujatimia uovu wa Waamori bado”.
Ili tuelewe vizuri tuanzie ule mstari wa 13..
Mwanzo 15:13 “Bwana akamwambia Abramu, Ujue hakika ya kwamba uzao wako utakuwa mgeni katika nchi isiyo yake, watawatumikia watu wale, nao watateswa muda wa miaka mia nne.
14 Hata na taifa lile, watakaowatumikia, nitawahukumu; baadaye watatoka na mali mengi.
15 Lakini wewe utakwenda kwa baba zako kwa amani, utazikwa katika uzee mwema.
16 NA KIZAZI CHA NNE KITARUDI HAPA, MAANA haujatimia uovu wa Waamori bado”
Katika mistari hiyo Bwana MUNGU anamwambia Abramu kuhusiana na uzao wake kwamba utaenda utumwani katika nchi isiyo yake (ambayo ni nchi ya Misri) na utamtumikia Farao kwa muda wa miaka 400, na baada ya miaka hiyo watatoka Misri.
Sasa wakati Bwana anamwambia Abramu hayo maneno, Abramu alikuwa tayari yupo katika nchi hiyo ya ahadi, isipokuwa bado alikuwa hajaimiliki kwani uzao wake ulikuwa bado mdogo na ilikuwa ni sharti uende kwanza Misri, ukaongezeke huko na kukua, ndio maana Mungu anamwambia kuwa utapelekwa utumwani na kisha utarudi tena katika hiyo nchi Abramu aliyopo muda huo, na itawaondoa wenyeji wa nchi hiyo.
Sasa swali nini maana ya “Kizazi cha Nne kitarudi”..
Jibu: Zamani kizazi kimoja kilihesabika kwa miaka 100, hiko ni kizazi kimoja, kwahiyo vizazi vinne maana yake ni miaka 400.. na mwisho wa hiyo miaka 400 ndio wana wa Israeli walitoka Misri.
Lakini swali lingine ni hili: Ni kwasababu gani uzao wa Abramu ukae Misri miaka muda mwingi hivyo? (400).. Jibu tunalipata katika ule mstari wa 16 unasema..“Na kizazi cha nne kitarudi hapa, maana haujatimia uovu wa Waamori bado”
Kumbe ilihitajika UOVU WA WAAMORI UTIMIE!!..Na hiyo yote ni kuonyesha huruma za MUNGU, kwamba si mwepezi wa hasira, mpaka aachilie ghadhabu yake maana yake ni kwamba kiwango cha maasi kimezidi sana..kile kikombe cha ghadhabu kinakuwa kimejaa..
Kwahiyo hapo aliposema haujatimia uovu wa Waamori, maana yake kiwango cha maasi cha Waamori bado hakikuwa kingi kiasi cha kupigwa na MUNGU.. Lakini baada ya miaka 400 kile kiwango cha maovu na maasi ya Waamori, na ya watu wengine waliokuwa wanaishi Kanaani kilifika kilele, na ndipo MUNGU akaachilia hukumu yake kwa kuwaondoa.
Utazidi kuona MUNGU anawakumbusha wana wa Israeli kuwa sababu ya wenyeji wa Kanaani kuondolewa katika ile nchi, si kwasababu ya utakatifu wa wana wa Israeli, bali ni kwasababu ya maasi ya waliokuwa wanaikalia ile nchi.
Kumbukumbu 9:3 “Basi jua siku hii ya leo kuwa Bwana, Mungu wako, ndiye atanguliaye kuvuka mbele yako kama moto uteketezao; atawaangamiza, tena atawaangusha mbele yako; ndivyo utakavyowafukuza na kuwapoteza upesi, kama alivyokuambia Bwana.
4 USISEME MOYONI MWAKO, BWANA, MUNGU WAKO, ATAKAPOKWISHA KUWASUKUMIA NJE MBELE YAKO, UKASEMA, NI KWA HAKI YANGU ALIVYONITIA BWANA NIIMILIKI NCHI HII; KWANI NI KWA AJILI YA UOVU WA MATAIFA HAYA BWANA AWAFUKUZA NJE MBELE YAKO.
5 Si kwa haki yako, wala kwa unyofu wa moyo wako, hivi uingiavyo kuimiliki nchi yao; lakini ni kwa uovu wa mataifa haya Bwana, Mungu wako, awafukuza nje mbele yako; tena apate kuliweka imara hilo neno Bwana alilowaapia baba zako Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo.
6 Basi jua ya kuwa Bwana, Mungu wako, hakupi nchi hii nzuri uimiliki kwa ajili ya haki yako, kwa maana u taifa lenye shingo ngumu”.
Umeona?… Na MUNGU ni yule yule hajabadilika, kama alivyowavumilia Waamori, na waanaki na Wahiti waliokuwa wanaikalia ile nchi ya ahadi kwa miaka 400, anatuvumilia hata sasa, lakini uvumilivu wake ni ili sisi tutubu, kwasababu hapendi hata mmoja apotee..
Warumi 2:4 “Au waudharau wingi wa wema wake na ustahimili wake na uvumilivu wake, usijue ya kuwa wema wa Mungu wakuvuta upate kutubu?
5 Bali kwa kadiri ya ugumu wako, na kwa moyo wako usio na toba, wajiwekea akiba ya hasira kwa siku ile ya hasira na ufunuo wa hukumu ya haki ya Mungu”.
Je umeitikia wito wa YESU?, Kama bado hujageuka na kumfuata YESU basi usipoteze muda Zaidi, huu ndio wakati, duniani imefikia kilele kabisa cha maovu na maasi, muda wowote parapanda italia na kile kikombe cha ghadhabu ya MUNGU kitamiminwa duniani.
Bwana atusaidie tusiwe miongoni mwa watakaokabiliana na mkono wa BWANA.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
SWALI: Yusufu aliwezaji kutafsiri ndoto? Je ni kwa hekima aliyokuwa nayo au kwa kuangalia ishara fulani, au kwa usomaji wa vitabu, au kwa saikolojia?
JIBU: Biblia inatuonyesha sifa kuu, ya Yusufu iliyokuwa ndani yake ni uwezo wa kutafsiri ndoto.
Lakini swali linaloulizwa je uwezo huo alitolea wapi, ulikuwa ndani yake mwenyewe au ulitoka kwingine.
Tukisoma Mwanzo 41:15, tunaweza kupata majibu;
Farao akamwambia Yusufu, Nimeota ndoto, wala hakuna awezaye kunifasiria; nami nimesikia habari zako, ya kwamba, usikiapo ndoto, waweza kuifasiri.16 Yusufu akamjibu Farao, akisema, Si mimi; Mungu atampa Farao majibu ya amani.
Hapo Yusufu anasema si mimi, Mungu atampa Farao majibu. Kuonyesha kuwa uwezo huo ulitoka kwa Mungu wala sio katika akili zake, elimu , saikolojia , au hekima ya kibinadamu.
Alimtegemea Mungu asilimia mia kumfunulia, mfano tu wa Danieli alipokwenda kuomba juu ya tafsiri ya ndoto ya Nebukadreza katika sala akafunuliwa. Ndivyo ilivyokuwa kwa Yusufu, katika kutafsiri ya ndoto ya Farao, pamoja na za wale watumishi wawili wa mfalme waliokuwa wanahudumu mezani pa mfalme. Hakubuni tu tafsiri kulingana na mazingira, bali alifunuliwa moja kwa moja aidha kwa ndoto au kuona maono.
Lakini ni kwanini Yusufu apokee neema hiyo kirahisi kwa Mungu, tofauti na wengine.
Jibu lipo katika TABIA yake, Ni wazi Roho ya Mungu huvutika sana katika tabia njema ya mtu. Yusufu tangu udogo alijitahidi kujiepusha na tabia zisizofaa, jambo lililopelekea mpaka ndugu zake kumchukia kwasababu alikuwa anatoa siri za mambo yao mabaya, hata alipouzwa kwa akida wa Farao, bado aliendeleza tabia yake ileile, pale mke wa Potifa alipomtamani akakataa, mwishowe akatupwa gerezani. Kwa njia hiyo Yusufu hakuacha kulitunza joto la ROHO ndani yake. Mfano tu wa Danieli naye, ambaye hakutaka kujitia unajisi kwa vyakula vya kifalme, na ndani ya hakukuonekana kosa lolote (Danieli 6:3).
Akashuhudiwa na mfalme kuwa Roho njema sana, na iliyo bora inakaa ndani yake.
Danieli 5:12 kwa kuwa roho njema kupita kiasi, na maarifa, na ufahamu, na uwezo wa kufasiri ndoto, na kufunua maneno ya fumbo, na kufungua mafundo, zilionekana katika Danieli huyo, ambaye mfalme alimwita Belteshaza. Basi na aitwe Danielii, naye ataionyesha tafsiri.
Hivyo ili na sisi tushiriki sehemu bora na njema za vipawa mbalimbali vya Roho Mtakatifu, hatuna budi kujijenga kimwenendo, katika maisha matakatifu yampendezayo Mungu.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je! habari ya Yusufu, inabeba ujumbe gani kwa agano jipya?
KWA KUWA ROHO BORA ILIKUWA NDANI YAKE.
JIBU: Safina ya Nuhu ilikuwa ni mfano wa Meli kubwa iliyojengwa katika deka tatu, ambayo vipimo vyake vilikuwa ni mikono mia tatu urefu wake, na mikono hamsini upana, na mikono thelathini kwenda juu.
Mwanzo 6:13 Mungu akamwambia Nuhu, Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia.14 Ujifanyie safina ya mti wa mvinje; fanya na vyumba ndani ya safina, ukaifunike ndani na nje kwa lami. 15 Hivi ndivyo utakavyoifanya; mikono mia tatu urefu wa safina, mikono hamsini upana wake, na mikono thelathini kwenda juu kwake.
Ambayo kwa vipimo vya sasa ni sawa na makadirio ya;
> Mita 137 urefu
> Mita 23 upanda
> Mita 14 kimo.
Ukubwa wa ile Safina, kwa sasa tunaweza kuifananisha na hizi meli kubwa za mizigo.
Yapo mambo manne ya kufahamu;
1). Jambo la kwanza ni kuwa hawakuingizwa wengi wengi, bali wawili wawili, na wengine saba saba, hivyo ni idadi ndogo tu ya kila jamii ndio iliyoingizwa.
2) Lakini pia kuna uwezekano Nuhu aliwaingiza wale wadogo wadogo tu, na sio wale wakubwa, Hivyo ikaachilia nafasi ya wanyama wote kujitosheleza ndani ya safina.
3) Tatu alipoambiwa awaingize wanyama kwa “namna” zao, (Mwanzo 6:20). Kwa lugha ya kibiblia si lazima imaanishe kila familia za wanyama ziingie, mfano familia mbalimbali za mbwa, wenye manyoya marefu, wenye asili ya ufupi, wawindaji, n.k. hapana, bali walipoingizwa mbwa, ni namna moja tu, iliwakilisha wote, Na baadaye walipoongozeka waliweza kuonekana wa maumbile tofauti tofauti tena, hilo linawezekana, ni sawa na sisi wanadamu tulitoka katika asili ya baba mmoja na mama mmoja, lakini leo hii kuna waafrika, wazungu, wachina, waarabu n.k. Hivyo ikiwa aliwaingiza kwa njia hiyo basi kisayansi inawezekana kabisa.
4) Lakini hoja ya mwisho iliyo na nguvu kuliko zote, ni kuwa hata kama ni namna zote na familia zao waliingia, bado Mungu anaweza kufanya mambo ambayo mwanadamu hawezi kuyafanya, ikiwa katika uzazi wa mwanaume mmoja Mungu amehifadhi mamilioni ya mbegu za kibinadamu, na ndani ya tumbo la mwanamke mmoja hadi watoto tisa wanakaa kwa ujauzito mmoja. Hivyo hatuwezi kushangaa, Mungu kuvihifadhi viumbe vyote katika meli ile, inayoonekana haijitoshelezi. Kwasababu yeye ni Mungu asiyeshindwa na chochote.
Ni kwa yeye haathiriwi na nafasi ya udogo au ukubwa, kusudi lake litasimama tu. Kwa vile vichache vilivyokuwa kwenye safina, ulimwengu leo umejawa na viumbe vingi na watu wengi. Wengine wanasema mimi nabanwa na muda hivyo siwezi kumtumikia Mungu, mimi nabanwa na masomo hivyo siwezi kufanya kitu kwa Mungu, mimi nimefungwa gerezani, siwezi kulitimiza kusudi lolote la Mungu. Ndugu Neno la Mungu halifungwi.
Ndugu Paulo alifungwa gerezani akazuiwa kwenda kuhubiri injili katika mataifa kama ilivyo desturi yake, lakini akiwa gerezani aliandika nyaraka ambazo mpaka leo hii zinaendelea kuhubiri injili, zaidi hata ya ziara zake.
Amini uweza wote wa Mungu mahali popote ulipo, bila kuathiriwa na mazingira.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NUHU ALIJENGA SAFINA KWA MIAKA MINGAPI?
SAFINA NI NINI?
Mvinje ni mti gani? (Mwanzo 6:14)