Hii ni mistari ya biblia inayogusia utoaji wa sadaka wa namna mbalimbali.
Mithali 3:9 Mheshimu Bwana kwa mali yako, Na kwa malimbuko ya mazao yako yote. 10 Ndipo ghala zako zitakapojazwa kwa wingi, Na mashinikizo yako yatafurika divai mpya.
Mwanzo 4: 3 Ikawa hatimaye Kaini akaleta mazao ya ardhi, sadaka kwa Bwana. 4 Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. Bwana akamtakabali Habili na sadaka yake; 5 bali Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana.
Kutoka 25:2 Waambie wana wa Israeli kwamba wanitwalie sadaka; kila mtu ambaye moyo wake wampa kupenda mtatwaa kwake sadaka yangu.
2Wakorintho 9:7 Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.
Kumbukumbu 16:17 Kila mtu na atoe kama awezavyo, kwa kadiri ya baraka ya Bwana, Mungu wako, alivyokupa
Kutoka 35:5 Katwaeni kati yenu matoleo kwa Bwana; mtu awaye yote aliye na moyo wa kupenda, ayalete matoleo; dhahabu na fedha na shaba;
2Nyakati 31: 5 Mara ilipotangaa amri, wana wa Israeli wakatoa kwa wingi malimbuko ya nafaka, na divai, na mafuta, na asali, na mazao yote ya mashamba; na zaka za vitu vyote wakazileta nyingi.
Zaburi 50:14 Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru; Mtimizie Aliye juu nadhiri zako.
Walawi 22: 29 Tena mtakapomchinjia Bwana dhabihu ya shukrani, mtamchinja ili mpate kukubaliwa. 30 Italiwa siku iyo hiyo; msisaze kitu chake hata asubuhi; mimi ndimi Bwana.
Malaki 3:10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.
Walawi 27: 30 Tena zaka yote ya nchi, kama ni mbegu ya nchi, au kama ni matunda ya nchi, ni ya Bwana; ni takatifu kwa Bwana.
Marko 12:43 Akawaita wanafunzi wake, akawaambia, Amin, nawaambia, Huyu mjane maskini ametia zaidi kuliko wote wanaotia katika sanduku la hazina; 44 maana hao wote walitia baadhi ya mali iliyowazidi; bali huyu katika umaskini wake ametia vyote alivyokuwa navyo, ndiyo riziki yake yote pia.
Wafilipi 4:18 Lakini ninavyo vitu vyote na kuzidi, tena nimejaa tele; nimepokea kwa mkono wa Epafrodito vitu vile vilivyotoka kwenu, harufu ya manukato, sadaka yenye kibali, impendezayo Mungu.
Luka 6:38 Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.
Pamoja na kuwa na sadaka za aina nyingi, lazima tufahamu, Sadaka halisi zimpendezazo Mungu. Na ya kwanza ni Yesu Kristo. Yeye alitolewa kwetu kama dhabihu kamilifu kwa ajili ya dhambi zetu. Hivyo mtu yoyote anayeitoa sadaka hii kwa Mungu basi, hukubaliwa na yeye asilimia mia. Na tunaitoa kwa kumpokea mioyoni mwetu kama Bwana na mwokozi wa maisha yetu. Imefanyika bora kuliko dhabihu zote na matoleo yote.
Waebrania 10: 4 Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi. 5 Kwa hiyo ajapo ulimwenguni, asema, Dhabihu na toleo hukutaka, Lakini mwili uliniwekea tayari;
Sambamba na hizo, sadaka nyingine zilizobora kuliko matoleo ni pamoja na kujitoa miili yetu katika utakatifu, kutenda haki, kuonyesha fadhili na rehema, kwa Bwana.
Warumi 12:1 Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.
Hosea 6:6 Maana nataka fadhili wala si sadaka; na kumjua Mungu kuliko sadaka za kuteketezwa.
Mika 6:6 Nimkaribie Bwana na kitu gani, na kuinama mbele za Mungu aliye juu? Je! Nimkaribie na sadaka za kuteketezwa, na ndama za umri wa mwaka mmoja? 7 Je! Bwana atapendezwa na elfu za kondoo waume, au na elfu kumi za mito ya mafuta? Je! Nimtoe
mzaliwa wangu wa kwanza kwa kosa langu, mzao wa mwili wangu kwa dhambi ya roho yangu? 8 Ee mwanadamu, yeye amekuonyesha yaliyo mema; na Bwana anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!
Je! Unatoa sadaka zote hizi? Kwa Bwana?
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NINI NI KILICHOMFANYA IBRAHIMU AKUBALI KUMTOA MWANAWE SADAKA?
Swali: Katika kitabu cha Mwanzo tunaona viumbe vyote viliumbwa na Mungu kwa kutamka tu Neno!, lakini kwa mwanadamu haikuwa hivyo, alimwumba kwa mikono yake, je sababu ni nini?
Jibu: Turejee
Mwanzo 1:19 “Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya nne.
20 MUNGU AKASEMA, Maji na yajawe kwa wingi na kitu kiendacho chenye uhai, na ndege waruke juu ya nchi katika anga la mbingu.
21 MUNGU AKAUMBA nyangumi wakubwa, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho, ambavyo maji yalijawa navyo kwa wingi kwa jinsi zao, na kila ndege arukaye, kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
22 Mungu akavibarikia, akisema, Zaeni, mkaongezeke, mkayajaze maji ya baharini, ndege na wazidi katika nchi.
23 Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya tano.
24 MUNGU AKASEMA, Nchi na izae kiumbe hai kwa jinsi zake, mnyama wa kufugwa, nacho kitambaacho, na wanyama wa mwitu kwa jinsi zake; ikawa hivyo
25 MUNGU AKAFANYA mnyama wa mwitu kwa jinsi zake, na mnyama wa kufugwa kwa jinsi zake, na kila kitu kitambaacho juu ya nchi kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.”
Hapa tunasoma kwamba MUNGU AKASEMA, na kisha MUNGU AKAFANYA.. Kwahiyo kumbe MUNGU alianza kwanza kwa kusema ndipo “akafanya”..Naam hata wewe unaweza kusema “utajenga nyumba” ikawa ni kauli, na wakati utakapofika ukaanza kukusanya malighafi na kuitengeneza ile nyumba.. Kwahiyo kuna “KUSEMA” na “KUFANYA” ndiyo kanuni Bwana MUNGU aliyoenda nayo pia.
Sasa biblia haijaeleza kwa urefu alifanyaje fanyaje, kwenye huo udongo wakatokea wanyama, na viumbe..Kwamba ile kauli ya kinywa chake ndio ilienda kubadili ule udongo na kuwa Twiga, na Simba, na Tembo, au kwamba baada ya kusema alienda kuchukua udongo kwa vidole vyake na kufanya wanyama wale wote hakuna anayejua, lakini tunachojua ni kwamba wanyama walitokea ardhini kwa neno lake hilo.
Lakini tukiendelea na mstari wa 26 alipomwumba mtu, tunaona jambo jipya.. MUNGU ANASEMA, na kisha ANAUMBA kwa maelezo marefu zaidi tofauti na ilivyokuwa kwa wanyama.
Mwanzo 1:26 “MUNGU AKASEMA, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
27 MUNGU AKAUMBA mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba”.
Soma tena Mwanzo 2:7 na Isaya 45:12 utaona maelezo ya ziada juu ya uumbaji wa mtu.
Kwa wanyama Bwana MUNGU hakuelezea kawaumba kwa mfano wa kitu gani, na kwa sura ya kitu gani, huenda labda waliumbwa kwa mfano wa baadhi ya viumbe vya mbinguni (kwani kuna malaika mbinguni wenye uso kama wa tai, na wengine wenye uso kama wa simba na ndama, na pia mbinguni kumetajwa uwepo wa farasi, soma Ezekieli 1:10, Ufunuo 4:7 na Ufunuo 19:11), lakini hiyo yote biblia haijaeleza, ni makisio tu..
Lakini alipoumbwa mwanadamu, biblia imetoa maelezo ya wazi kabisa ziada kaumbwa kwa mfano wa MUNGU, na kwa sura ya MUNGU, kuonyesha umaalumu wake na utofauti wake na viumbe vingine vyote.
Na kama jinsi MUNGU alivyo Mkuu mbinguni na tena anatawala mbinguni, hali kadhalika na yule aliyetengenezwa kwa mfano wake duniani, atakuwa na nguvu na utawala kama wa kwake duniani.
Mwanzo 1:27 “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.
28 Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi”.
Lakini pamoja na kwamba Adamu aliumbwa ili atawale duniani, bado alimwuzia shetani nafasi yake hiyo, lakini habari njema ni kwamba YESU KRISTO alishinda na kuirejesha nafasi ya mwanadamu ya utawala..
Na wote wamwaminio Bwana YESU wanatawala naye si tu duniani, bali hata mbinguni.. kwani tumeketi naye mbinguni katika ulimwengu wa roho.
Waefeso 2:5 “ hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema.
6 Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu”
Lakini ukiwa nje ya Kristo, huna mamlaka yoyote, kwani shetani ndiye anayekutawala..Mpokee leo KRISTO na upande viwango vingine vya kiroho.
Maran atha.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
1Samweli 1:5 Hana akajibu, akasema, Hasha! Bwana wangu, mimi ni mwanamke mwenye roho ya huzuni, mimi sikunywa divai wala kileo, ila nimeimimina roho yangu mbele za Bwana.
Divai na kileo ni vinywaji vya kulewesha, na vyote vilitumika zamani katika Israeli, ambavyo hata sasa vinatumika.
Tofauti kati ya Divai na kileo ni hii;
Divai, ilichachushwa kutoka katika matunda ya zabibu tu.
Kwa wayahudi divai ilikuwa kama kinywaji cha kitamaduni kilichotumika sana sana katika karamu mbalimbali za kijamii, tunaona mfano wa sherehe ile aliyoalikwa Bwana Yesu kule Kana, katikati ya sherehe walitindikiwa Divai, ndipo Yesu akaenda kuyageuza yale maji kuwa divai. Kuonyesha kuwa divai ilikuwa ni kinywaji kilichoruhusiwa kitamaduni Israeli, katika karama. (Yohana 2)
Lakini pia ilikuwa kama kinywaji cha kiibada, katika karamu za kidini, kwa mfano sikukuku za pasaka, wana wa Israeli walikunywa divai pamoja na mikate isiyotiwa chachu. Tunaona hilo Kristo alilidhihirisha kipindi kile cha pasaka alipoketi na wanafunzi wake akawapa mkate na divai, kama ishara ya mwili wake na damu yake, imwagikayo kwa ajili ya ondoleo la dhambi za watu wengi. (Mathayo 26.27-29)
Lakini pia divai ilisimama kama kiashiria cha furaha, au baraka.
Zaburi 104: 15 Na divai imfurahishe mtu moyo wake. Aung’aze uso wake kwa mafuta, Na mkate umburudishe mtu moyo wake.
Mvinyo ulitengenezwa kwa ngano, shayiri, makomamanga, au tende tofauti na divai iliyozalishwa katika zabibu tu.
Mvinyo ulikuwa na kilevi kikali kuliko divai, na matumizi yako hayakuwa rasmi Israeli, Ilitumika sana sana katika karamu za ulafi na ulevi, lakini sio katika shughuli zozote za kijamii au kidini.
Makuhani hawakuruhusiwa kuinywa walipokuwa wakihudumu katika hema (Walawi 10:9)
Lakini maandiko yanasema nini kuhusu ulevi?
Mithali 20:1 Mvinyo hudhihaki, kileo huleta ugomvi; Na akosaye kwa vitu hivyo hana hekima.
Katika andiko hilo tunaona Hana, aliposhutumiwa na Eli kuhusu ulevi, yeye akamwambia mimi sikunywa divai wala kileo. Kuonyesha kuwa alitilia umakini ibada yake na sala zake kwa Mungu.
Hata leo, ni vema tufahamu kuwa hatulewi tena kwa mvinyo, bali kwa Roho Mtakatifu tuliyepewa ndani yetu (Waefeso 5:18), Yeye ndiye divai yetu na mvinyo yetu.
Hivyo ni wajibu wa mwamini yoyote kudumu katika Maombi, kutafakari Neno, na ibada, ili ajazwe vema Roho.
Mungu akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Paulo alimwambia Timotheo atumie mvinyo kidogo kwa ajili ya tumbo lake, Je! tunaruhusiwa na sisi pia kutumia pombe?
Je! mabalasi Bwana Yesu aliyoyatumia kugeuzia maji kuwa divai, yalitumika tu kwa kazi hiyo?
Kwanini Bwana YESU ageuze maji kuwa Divai? Na ni ujumbe gani tunapata?
Swali: Kwenye Mathayo 20:20-25 Mke wa Zebedayo anamwendea YESU na wanawe akimuomba wakae pande zote za YESU na awape mamlaka alizonazo ila YESU akamwambia hana amri juu ya jambo hilo lakini huku kwenye Luka 23:39 anamwambia mmoja wa wale wanyang’anyi leo hii utakuwa na mimi peponi, naomba ufafanuzi wa mwingiliano huo wa maandiko….Je biblia inajichanganya kwa maneno hayo???…
Jibu: Turejee mistari hiyo..
Mathayo 20:20 “Ndipo mama yao wana wa Zebedayo akamwendea pamoja na wanawe, akamsujudia, na kumwomba neno.
21 Akamwambia, Wataka nini? Akamwambia, Agiza kwamba hawa wanangu wawili waketi mmoja mkono wako wa kuume, na mmoja mkono wako wa kushoto, katika ufalme wako.
22 Yesu akajibu akasema, Hamjui mnaloliomba. Je! Mwaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi? Wakamwambia, Twaweza.
23 Akawaambia, Hakika mtakinywea kikombe changu; lakini kuketi mkono wangu wa kuume na mkono wangu wa kushoto, sina amri kuwapa, bali watapewa waliowekewa tayari na Baba yangu.
24 Na wale kumi waliposikia, waliwakasirikia wale ndugu wawili”.
Hapa tunaona Bwana anatamka kuwa “Hana amri ya kuwaketisha vijana hao upande wa kuume na kushoto katika ufalme wake”
Tusome tena Luka 23:39
Luka 23:39 “Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi.
40 Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo?
41 Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.
42 Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.
43 YESU AKAMWAMBIA, AMIN, NAKUAMBIA, LEO HIVI UTAKUWA PAMOJA NAMI PEPONI.”
Sasa swali ni kwanini KRISTO awe na amri juu ya huyu mhalifu na asiwe amri juu ya wale Vijana wa Zebedayo?.
Jibu ni kwamba “walichokiomba wana wa Zebedayo ni tofauti na alichokiomba huyu mhalifu”.. Wana wa Zebedayo wenyewe waliomba nafasi za ukubwa ndani ya ufalme wa mbinguni (kwamba watakapofika mbinguni wakawazidi wengine wote ikiwemo akina Petro na mitume wengine na hata sisi watu wa kizazi hiki)…
Lakini huyu Mhalifu yeye hakuomba ukubwa wowote ndani ya ufalme wa mbinguni kwamba akawe nani huko anakokwenda bali aliomba tu nafasi ya kuuingia ule ufalme wa mbinguni, (habari za kwenda kuwa nani huko aendako hilo hakujali, alichokitamani na kuuingia tu ule ufalme).
Na KRISTO alimpa hiyo nafasi kwani hiyo AMRI anayo kwa watu wote watakaokiri makosa yao Ikiwa na kumwamini Bwana YESU kama alivyofanya huyu Mhalifu. (Na KRISTO alimwambia vile kwasababu alijua hatakengeuka tena, kwani maisha yake ndio yalikuwa yanaenda kuisha, alikuwa amebakisha masaa machache tu ya kuishi).
Lakini wana wa Zebedayo, tayari walikuwa wameshajiwekea hakika wa kuuingia ufalme wa mbinguni, kwasababu walishamwamini Bwana YESU na kutubu kitambo kirefu….na hivyo wakaenda mbali zaidi si kuomba kuuingia ufalme wa mbinguni, bali kuomba nafasi za juu katika huo ufalme wa mbinguni watakaouingia… Jambo ambalo KRISTO asingeweza kuwaahidia.
Ni sawasawa na mwanafunzi anayemwomba mwalimu ampe zawadi ya nafasi ya kwanza darasani na ilihali bado hajafanya mtihani.. Ni wazi kuwa mwalimu hawezi kumpa hiyo zawadi, kwani bado hajafanya/kumaliza mtihani…Matokeo yatakapotoka ndio yatakayoeleza kama anastahili hiyo zawadi ya nafasi ya kwanza au la!.
Na KRISTO hakuwa na amri ya kuwapa hizo nafasi walizokuwa wanazitaka kwani vita vya imani bado walikuwa hawajavimaliza, na ule mwisho bado haujafika, ambapo kazi ya kila mtu itakapopimwa na kupewa thawabu,
Siku ile kama watakuwa wamefanya bora kuliko wengine wote watapata hiyo nafasi waliyoiomba (ya kuketi mkono wa kuume na kushoto), lakini kama watatokea wengine watakaofanya vema kuliko wao, basi wataikosa na nafasi hizo watapewa wengine.
Je umeokoka?
Je unajua kuwa YESU KRISTO anarudi!… na dalili za kurudi kwake karibia zote zimeshatimia?..Je unafahamu kuwa kuishi maisha ya uvuguvugu ni laana? Soma Ufunuo 3:14, leo unaenda kanisani kesho unaenda bar, asubuhi unaimba kwaya, jioni miziki ya kidunia, kwenye kabati una nguo za heshima, na nguo za kikahaba.. Huo wote ni uvuguvugu ambao Bwana YESU alisema matokeo yake ni kutapikwa.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Swali: Kuna uhusiano gani kati ya aina ya maisha anayoishi mtu na ile siku aliyozaliwa?.. Kwanini Ayubu anailaani ile siku aliyozaliwa na ule usiku ilipotungwa mimba? (Ayubu 3:1-6).
Jibu: Turejee..
Ayubu 3:1 “Baada ya hayo Ayubu akafunua kinywa chake, na kuilaani siku yake.
2 Ayubu akajibu, na kusema;
3 Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi, Na ule usiku uliosema, Mtoto mume ametungishwa mimba.
4 Siku hiyo na iwe giza; Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie.
5 Ishikwe na giza, giza tupu, kuwa yake; Wingu na likae juu yake; Chote kiifanyacho siku kuwa giza na kiitishe.
6 Tena usiku huo, na ushikwe na giza kuu; Usihesabiwe katika siku za mwaka; Wala kutiwa katika hesabu ya miezi”.
Sababu kuu ya Ayubu kuilaani siku aliyozaliwa ni kutokana na majaribu aliyoyapitia!.. Ya kupoteza mali zake pamoja na watumwa wake, lakini pia ya kupoteza watoto wake na zaidi sana kupatwa na magonjwa.
Hali hiyo ya mapito magumu ndiyo iliyomfanya Ayubu ailaani siku yake ya kuzaliwa… Maana ya kulaani hapo “ni kutotamani kuzaliwa”, kwamba ni “kosa kubwa limefanyika yeye kuzaliwa/kuja duniani”.
Lakini pamoja na kwamba Ayubu aliilaani siku yake ya kuzaliwa bado hakumlaani MUNGU, wala kumwazia mabaya.. ndio maana hapo anasema… “Siku hiyo (ya kuzaliwa) Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie”.. kitendo hiko cha kumhusisha MUNGU katika kauli yake hiyo ni kuonyesha Ayubu alimheshimu MUNGU.
Lakini swali ni Je! jambo hilo Ayubu alilolifanya ni sahihi? Na Je na sisi pia tunaweza kuzilaani siku zetu tulizozaliwa ikiwa tutapitia majaribu yanayofanana au kukaribia kufanana na ya Ayubu?..
Jibu ni hapana! hatupaswi kuzilaani siku zetu tulizozaliwa, vile vile Ayubu hakufanya jambo lililo jema machoni pa BWANA kwa kauli ile!.. kwani tunaona ijapokuwa Ayubu hakumlaani MUNGU kwa kinywa chake lakini kitendo pia cha kuilaani siku yake ya kuzaliwa kilikuwa ni kosa, wala haikuwa ni busara kusema vile, bali alinena pasipo maarifa, ingawa nia yake ya ndani haikuwa ovu kama ile ya mke wake..
Ayubu 35:16 “Ndiposa Ayubu hufunua kinywa chake kwa ubatili; Huongeza maneno pasipo maarifa”.
Kwahiyo alinena hayo maneno pasipo maarifa, ndio maana mwishoni tunaona baada ya kutokewa na MUNGU katika upepo wa kisulisuli na kusahihishwa alitambua makosa yake ya kuwa maneno aliyoyatoa yalikuwa yana kasoro (yasiyo na maarifa) na alitubu..
Ayubu 42:1 “Ndipo Ayubu akamjibu Bwana, na kusema.
2 Najua ya kuwa waweza kufanya mambo yote, Na ya kuwa makusudi yako hayawezi kuzuilika.
3 Ni nani huyu afichaye mashauri bila maarifa? KWA MAANA, NIMESEMA MANENO NISIYOYAFAHAMU, MAMBO YA AJABU YA KUNISHINDA MIMI, NISIYOYAJUA.
4 Sikiliza, nakusihi, nami nitanena; Nitakuuliza neno, nawe niambie.
5 Nilikuwa nimesikia habari zako, kwa kusikia kwa masikio; Bali sasa jicho langu linakuona.
6 KWA SABABU HIYO NAJICHUKIA NAFSI YANGU, NA KUTUBU Katika mavumbi na majivu”.
Umeona hapo?, Ayubu anakiri makosa aliyoyafanya ya kusema maneno asiyoyajua, na anamaliza kwa kutubu. Ikimaanisha kuwa nasi hatupaswi kusema maneno kama hayo. Kukosoa siku uliyozaliwa bado kwa namna moja au nyingine ni kumkosoa MUNGU, Hata kama hatutalihusisha jina la MUNGU katika kukosoa kwetu huko, bado hatupaswi kulaani, kwasababu kila kitu kinakuja kwa makusudi..
Ikiwa unaona unapitia majaribu mazito usiojua mwanzo wake wala mwisho wake, suluhisho si kuikimbilia siku uliyozaliwa na kuilaani, au kujijutia kuzaliwa!.. hiyo haisaidii kitu, kwani hiyo siku imeshapita na haiji tena mbeleni,.. zaidi sana badala ya kulaani, ni vizuri kutafuta kujua chanzo cha majaribu hayo ni nini, kwa kujinyenyekeza mbele za MUNGU.
Na MUNGU kwakuwa ni mwaminifu kwetu na mwenye upendo, hawezi kamwe kutuacha muda mrefu katika mitihani mkubwa wa kutokuelewa sababu ya majaribu yanayotukabili, ni lazima tu ataonyesha njia na kutufunulia sababu ya mapito tupitayo….hivyo ni suala la kujinyenyekeza tu na kumngoja BWANA, Na si kulaani…
Laiti Ayubu angejua kuwa muda mchache tu umebaki wa MUNGU kwenda kumrudishia vile alivyovipoteza mara dufu, asingesema yale maneno ya laana,… lakini tunajua alisema vile pasipo maarifa ili baadaye na sisi pia tuje kujifunza.. ma ndio maana baadaye alitubu na MUNGU akamsamehe..
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Wana kumi na mbili wa Yakobo ndio waliozaa makabila 12 ya Israeli. Majina yao ni kama yafuatavyo;
Zipo kazi au majukumu ambayo makabila yote yaliwajibika kuyatekeleza mfano wa hayo ni kama kumwabudu Mungu, kuihudumia hema, ambayo baadaye ikawa hekalu, ulinzi kwa taifa (msaada wa kijeshi), kuendeleza Sheria ya Mungu kwa vizazi vyote.
Lakini pamoja na hayo, yapo majukumu ambayo yalitekelezwa Zaidi na kabila husuka kuliko mengine. ambapo mengine yaliagizwa na Mungu Moja kwa moja na mengine yalikuja Kama kipawa, walichokirimiwa . Na hatimaye yakawa ni majukumu yao.
Reubeni alipaswa kuwa na jukumu la kiuongozi, kama mzaliwa wa kwanza, lile kusudi lote la ukuhani lingepaswa liwe la lake lakini kwasababu alizini na mke wa Baba yake, akapoteza haki ya mzaliwa wa kwanza akaondolewa nafasi hiyo (mwanzo 35:22, 49:3-4).
Ijapokuwa alishushwa daraja lake. Bado alibakia kutimiza kusudi la kiulinzi upande wa mashariki mwa Israeli kwani jeshi lake, lilikiwa na watu hodari, lakini hawakuwa viongozi wa kijeshi.
Kabila la Simeoni nalo lingepaswa lichukue nafasi kuu katika Israeli, lakini lilishushwa chini kwasababu ya ukatili wao pamoja na Lawi, walipokwenda kuwaua wale washekemu ambao hawakustahili Kufanyiwa mauaji yale, kwa kosa la kumnajisi dada yao.(Mwanzo 34)
Hivyo kabila hili halikuwa na uongozi wowote wa kiroho katika Israeli, zaidi lilimezwa katika kabila la Yuda, kutimiza unabii wa Baba yao (Mwanzo 49:5-7), likabakia kuwa mchango kwenye eneo la kijeshi Israeli.
Lawi lilichukua nafasi ya kikuhani, lilihudumu katika hema na Hekalu, kufanya Upatanisho kwa wana wa Israeli, kwa sadaka mbalimbali pamoja Kufundisha Torati. (Kutoka 32:26-29).
Lawi hawakuwa urithi Israeli, bali walisambazwa katika makabila yote ya Israeli, kama Simeoni, kutimiza unabii wa Baba yao juu ya hasira walioionyesha Isiyo na huruma.(Mwanzo 49:5-7)
Kabila la Yuda lilisimama Kama kabila la Kifalme, na la kikuhani halisi wa milele (2Samuel 7:16)
Ndilo lililoandaa njia ya masihi kuja Duniani,(Mwanzo 49:10).Yuda lilichukua nafasi zote za juu, kutokana na kuwa Reubeni, Lawi na Simeoni kupoteza uwezo wa kuzishika, kwa matendo yao yasiyofaa.
Kabila Hili lilikuwa pia na askari hodari wa vita, na likasimama Kama kitovu cha kiutalawa, kivita na kiibada katika Israeli. Halikadhalika Yuda ilisimama kutunza urithi wa Israeli kwa vizazi vingi baada ya kutawanywa Kwenye mataifa yote, ndio lenyewe tu lililoweza kurudi Israeli.(Mwanzo 49:9-12)
Kabila la Dani lilikuwa na jukumu la kimahakama katika Israeli, (Mwanzo 49:16-18). Lilikuwa ninasimama katika nafasi ya maamuzi. Kuhakikisha Sheria na taratibu zake zinafuatwa ipasavyo.
Lakini pia lilisimama kusaidia Israeli, mahali popote walipoweka marago na kuondoka lilihusika kukusanya vitu vyote muhimu, na kuhakikisha watu wasiojiweza wanatembea Na kundi. (Hesabu 10:25).
Pamoja na hilo lilisimama kama mashujaa wa nyuma wa jeshi la Israeli, pale linapokwenda vitani lilisimama kulinda dhidi ya wavamizi wa nyuma.
lakini baadaye lilikuja kupoteza sifa yake ya kiuamuzi, kwasababu ya kwenda kusimamisha miungu ya kigeni na kuiabudu (Waamuzi 18).
Kabila la hekima na nguvu.
Ni kabila Ambalo lilikuwa na mchango mkubwa Katika eneo la kivita. Tunaweza kuona katika kipindi cha waamuzi kabila hili kwa uongozi wa Debora na Baraka (Waamuzi 4:6), lilimshinda Sisera.
Lakini lilisimama Kama washauri wa kiroho kwa Israeli.
Mwanzo 49:21
[21]Naftali ni ayala aliyefunguliwa; Anatoa maneno mazuri.
Katika wakati wa Kristo, eneo La wanaftali ambalo lilikuwa sehemu ya Galilaya lilidharauliwa sana, na kuonekana nyonge,(Yohana 1:46,7:52) si tu kimaendeleo lakini pia kuwa na wapagani wengi, lakini ndio mahali Ambapo palikuwa mji wa makazi ya Masihi Yesu Kristo, sawasawa na unabii alioutoa Isaya.(Mathayo 4:13-16).
Gadi lilikuwa hodari katika vita, lisilojisalimisha kirahisi kwa maadui, lilisimama Kama Walinzi wa lango la mashariki la taifa la Israeli, pembezoni mwa Reubeni.
Mwanzo 49:19
[19]Gadi, jeshi litamsonga, Lakini atawasonga wao mpaka visigino.
Ni kabila ambalo halikujikita Sana katika mchango Wa kijeshi. Bali Lilikuwa ni kabila la kibiashara Tajiri, lenye kulinda uchumi wa nchi.
Mwanzo 49:20
[20]Asheri, chakula chake kitakuwa kinono, Naye atatoa tunu za kifalme.
Ni kabila Lilipewa neema katika kutambua Nyakati na kutoa mashauri sahihi ya kufanya. lilisimama kama washauri Wa taifa.
1 Mambo ya Nyakati 12:32
[32]Na wa wana wa Isakari, watu wenye akili za kujua nyakati, kuyajua yawapasayo Israeli wayatende; vichwa vyao walikuwa watu mia mbili na ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao.
Walichangia maaskari wa vita, kwasababu walikaa katika fukwe, iliwafanya wawe hodari katika biashara na uchuuzi.
Mwanzo 49:13 Zabuloni atakaa pwani ya bahari, Naye atakuwa kama pwani za kuegesha merikebu, Na mpaka wake utakuwa kando ya Sidoni.
Ni kabila lililopewa nguvu, kiutawala na kijeshi , lilitimiza kusudi la kulisimamisha taifa la Israeli, hata wakati Israeli ilipogawanyika, makao makuu ya kabila zile 10, yalikuwa Ni samaria mji wa Efraimu. (Mwanzo 49: 22-26)
Ni kabila Lililokirimiwa watu hodari wa vita watumiao mashoto (Waamuzi 20:16), ambao walisimama vema katika vita, ijapokuwa lilikuwa dogo, lililojichanganya katika kabila la Yuda ndio kabila la kwanza kutoa mfano Israeli (Sauli), na baadaye mtume Paulo.
La kujifunza: Kuwa mdogo haimaanishi kuwa utakuwa wa mwisho. Bwana anasema walio wa mwisho Watakuwa wa kwanza na wa kwanza watakuwa wamwisho.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Yakobo alimaanisha nini kusema ‘ndipo BWANA atakuwa Mungu wangu’ Mwanzo 28:21
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Swali: Biblia imeandikwa na watu, (kama Paulo, Petro, Musa, Daudi na wengineo) je tutaamini vipi kitu kilichoandikwa na wanadamu kuwa ni kweli,? vipi kama wametoa tu kwenye akili zao, kwanini tukiamini kitabu cha namna hiyo, chenye mikono ya wanadamu?
Jibu: Kabla ya kujibu swali hili, tusome kwanza maandiko yafuatayo…
Yohana 14:11 “Mnisadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu; la! Hamsadiki hivyo, SADIKINI KWA SABABU YA KAZI ZENYEWE”
Hapa Bwana YESU anatoa njia za sisi kumwamini yeye, kwamba kama hatutamwamini kwa yeye kutuambia kwa mdomo wake mwenyewe, basi tumwamini kupitia zile kazi anazozifanya ambazo ni ishara na miujiza.
Hiyo hakika ni hekima kuu sana!… kwamba kama sisi ni kazi sana kumwamini yeye kwa maneno ya kinywa chake, basi tuzipime zile kazi anazozifanya ikiwa ni halisi na za kweli, basi tumwamini kwahizo pasipo hata maneno yake.
Vile vile na hata kuhusiana na waandishi wa Biblia, kama hatuwaamini kuwa wameandika mambo waliyovuviwa na MUNGU, basi kupitia matokeo ya kazi hizo, (jinsi yanavyobadilisha watu wengi leo, na kuponya watu wengi) basi tuamini.
Labda hujaelewa vizuri, tafakari tena mfano huu.
Umeletewa kitabu cha Fizikia, ambacho kimsingi kimeandikwa na watu wengi, ambapo ndani ya kitabu hiko waandishi wameeleza kanuni/fomula za kuunda ndege inayoruka juu sana, sasa kitabu kama kitabu kinakuambia kuwa kwa kupitia kanuni hii inawezekana kutengeneza chombo na kuruka juu mawinguni..(hayo ni maneno ya waandishi wa kitabu, ambao ni wanasayansi).
Sasa kwa maneno yao hivyo tu, hatuwezi kuamini, au tuseme ni ngumu kuamini!, kwamba huwenda yakawa ni maneno ya kutunga tu, au ya watu waliorukwa na akili… lakini anapotokea mtu na kutengeneza chombo kinachoruka angani kupitia kanuni za wanasayansi hao walizoziandika kwenye kitabu chao hiko, basi ndipo tunaweza kuamini kuwa waliyokuwa wanayasema ndani ya kitabu ni kweli, kwani tumeona kabisa ndege ikiruka kupitia kanuni walizoziandika kupitia kile kitabu.
Vile vile tunaweza tusiyaamini maneno ya Paulo, au ya Petro au ya Daudi au ya Mtume mwingine yoyote ndani ya biblia, lakini tutakapoyaona yametumiwa na wengine na kuleta matokeo kama waliyoyasema ndani ya kitabu cha biblia tutawaamini.
Sasa maneno yao (Paulo, Petro, Daudi na wengineo) yamewekwa katika matendo na majaribio ya mamilioni ya watu, na yameleta matokeo yale yale waliyoyasema hao Mitume ndani ya biblia, hicho ndicho kinachotufanya tuwaamini kuwa waliyokuwa waliyoyaandika ni kweli, na uzuri ni kwamba hata mimi na wewe tumepewa nafasi ya kuyatafiti maneno hayo kama ni kweli au uongo..
Walisema na kuandika ndani ya kitabu (biblia) kuwa kwa jina la YESU pepo wanatoka, leo tumejaribu na tumeona ni kweli, na maelfu ya watu wamejaribu na kuona ni kweli, hivyo basi maneno yao ndani ya biblia ni kweli!.
Mitume waliandika kuwa Aminiye na kubatizwa atapokea zawadi ya Roho Mtakatifu (Matendo 2:38), jambo hilo tumelihakiki wenyewe kuwa ni kweli, na wewe unaweza kulihakiki kuwa ni kweli, sasa kuna sababu gani ya kutoaiamini biblia, ijapokuwa imeandikwa na watu?.. kama watu wanaishuhudia kweli, basi kinachofuatwa ni ile kweli wanaousema na si watu.
Ukiona mtu anasema mwanasayansi aliyetoa kanuni ya kuunda ndege ni mwongo na katunga, na huku ndege zinaonekana zikiruka, basi mtu huyo anayepinga huwenda anamatatizo ya afya ya akili, na anahitaji msaada, vile vile ukiona mtu anapinga elimu inayotolewa na mitume wa kwenye biblia na huku matokeo ya elimu hiyo yanaonekana wazi kwa macho, basi mtu huyo huwenda anayo matatizo pia ya afya ya akili za rohoni au hata ya mwilini, anahitaji msaada.
2Petro 1:20 “Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu.
21 Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, WAKIONGOZWA NA ROHO MTAKATIFU”.
Biblia si kitabu kilichoandikwa kwa fikra za watu, kama ulikuwa unafikiri hivyo, basi leo hii anza kubadili mtazamo wako na fikra zao, anza kuisoma Biblia kwa mtazamo mwingine na utamwona MUNGU na si Mtu, kwa msaada wa njia bora ya kusoma biblia tutafute inbox.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Jibu: Mpaka kufikia mwaka 2024 biblia imetafsiriwa kwa lugha 756, hivyo kuna tafsiri Zaidi ya 756 mpaka sasa duniani kote.
Sasa kwa asili biblia iliandikwa kwa lugha kuu tatu, ambazo ni KIEBRANIA (Agano la Kale), lugha ya KIARAMU (Sehemu za Agano la kale na jipya) pamoja na lugha ya KIYUNANI AU KIGIRIKI (Agano jipya), Hizo ndizo lugha kuu tatu zilizoandikia biblia ya kwanza, na haikuandikwa kwa lugha ya kiingereza wala Kiswahili, wala lugha nyingine yoyote tofauti na hizo tatu.
Sasa kuna tafsiri nyingi za biblia siku hizi za leo kwasababu kadhaa, na sababu hizo zipo tatu (3)..
1)Tofauti za lugha, 2) Maendeleo ya Lugha 3) Mitazamo ya kidhehebu.
Hizo ndizo sababu kuu tatu,.. hebu tutatame moja baada ya nyingine.
1. Tofauti za Lugha
Kwasababu biblia kwa asili iliandikwa kwa lugha ya Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki. Zipo jamii za watu zisizozungumza lugha hizo, na kwasababu ni lazima watu wote, ulimwenguni kote walisikie Neno la Mungu, ni lazima tafsiri iwepo,….na watalisikiaje na kulielewa wasipolisikia kwa lugha yao na kulisoma kwa lugha yao?..
Hiyo ndiyo ikawa sababu ya Biblia ya kwanza yenye lugha hizo tatu, kutafsiriwa kwa lugha nyingine mbali mbali ikiwemo lugha yetu ya Kiswahili, Hebu tafakari laiti isingetafsiriwa kwa lugha yetu, biblia kwetu ingekuwa ngumu kiasi gani leo?.. Hivi ilivyo tu tayari ni ngumu!… vipi kama tungekuwa tunaisoma kwa lugha nyingine?? Si hali ingekuwa mbaya Zaidi??…kwasababu ingetupasa tukajifunze kwanza lugha hizo tatu, jambo ambalo lingekuwa gumu sana kwa wengi!.
Kwasababu ya shida hiyo, ndipo Bwana MUNGU wetu kupitia Roho wake Mtakatifu alitangulia kuachilia uwezo wa lugha na tafsiri zake ile siku ya Pentekoste, (soma Matendo 2) kuonyesha kuwa sasa Neno linapaswa lihubiriwe kwa watu wote na lugha zote, na ndipo zikaja tafsiri hizo.
2. Maendeleo ya Lugha.
Hii ni sababu ya pili ya uwepo wa tafsiri nyingi, utaona tayari kuna tafsiri moja ya lugha husika, tuchukue mfano lugha ya Kiswahili, halafu baada ya muda unaona kuna tafsiri nyingine zinaongezeka tofauti na hiyo ya kwanza na tena kwa lugha hiyo hiyo ya Kiswahili.
Sasa hiyo inatokana na kukua kwa lugha, kwani lugha siku zote inakuwa (inaongezeka misemo na maneno), na kwasababu hiyo basi tafsiri nyingi zinatokea na bado zitaendelea kutokea,
3. Mitazamo ya Kidhehebu na Theolojia
Kutokana na ongezeko la Madhehebu mengi yenye itikadi zinazotofautiana, imechangia pakubwa kutokea kwa tafsiri mpya kila siku kulingana na misimamo ya dhehebu husika. Kwani tafsiri nyingine zinaegemea mapokeo ya dhehebu hilo, kwamfano utaona dhehebu la katoliki linatumia biblia yenye vitabu vingine vya Deuterokanoni, ambavyo vinafanya jumla ya vitabu 72, tofauti na Biblia ya asili yenye vitabu 66.
Zipo na sababu nyingine ndogo ndogo ikiwemo mbinu za kutafsiri, kwamba wengine wanatafsiri neno kwa neno, na wengine wanatafsiri sentensi nzima na kuleta maana ya ujumla, na sababu nyingine ni mapendekezo ya lugha laini kwaajili ya watoto, zenye kutumia tafsida na zisizotumia lugha za ukali na kuogopesha. Hizi zote ndizo zinazochangia ongezeko la tafsiri za biblia kila siku.
Lakini swali je! Ni tafsiri ipi iliyo sahihi na isiyo na sumu kwa mkristo?
Mara nyingi kitu cha asili kinakuwa ni bora kuliko kile kilichochujwa Zaidi.. Tafsiri iliyo bora na yenye kufaa kuliko zote ni ile yenye lugha tatu (Kiebrania, Kiaramu na kiyunani), lakini kwasababu ni ngumu sisi kukijua kiyunani, na kiebrania kifasaha, basi tafsiri inayofuata kwa Ubora ni ile ya kwanza kabisa iliyotafsiriwa katika yetu lugha husika, kwamfano kwa sisi tunaozungumza Kiswahili, tafsiri ya kwanza kabisa na bora kwa lugha yetu ni ile ya SWAHILI UNION VERSION (SUV), ambayo ndiyo inayotumika sasa kwa wingi, inayoanza na…
Mwanzo 1:1 “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.
2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.”
Hiyo ndiyo tafsiri iliyo bora, tafsiri nyingine zinazofuata baada ya hapo faida yake inakuwa ni ndogo ukilinganisha na hasara…kwani zinabadilishwa maana na zinatengenezwa kwa kuegemea dini Fulani, na katika lugha nyingine ni hivyo hivyo, ile ya kwanza ni bora Zaidi kuliko zilizoendelea kufuata.
Kwahiyo kwa hitimisho, Tafsiri sahihi yenye kumfaa mtu ni ile ya kwanza (yenye kiebrania, kiyunani na kigiriki) ikiwa mtu atakuwa ana uwezo wa kuzielewa lugha hizo, lakini kama hana uwezo basi ile tafsiri ya kwanza kabisa iliyotafsiriwa kwa lugha yake, ni bora Zaidi.
Je umempokea Bwana YESU kikweli kweli?
Je unajua kuwa tunaishi katika siku za kurudi kwa pili kwa Bwana YESU na unyakuo upo karibu?, Je unajua kuwa kama huna Roho Mtakatifu huwezi kuiona mbingu (Warumi 8:9).. sasa kama bado hujaokoka unasubiri nini?,
Warumi 13:11 “Naam, tukiujua wakati, kwamba saa ya kuamka katika usingizi imekwisha kuwadia; kwa maana sasa wokovu wetu u karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini
12 Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru.
13 Kama ilivyohusika na mchana na tuenende kwa adabu; si kwa ulafi na ulevi, si kwa ufisadi na uasherati, si kwa ugomvi na wivu.
14 Bali mvaeni Bwana Yesu Kristo, wala msiuangalie mwili, hata kuwasha tamaa zake”.
Maran atha.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine: