Category Archive Roho Mtakatifu

KUWA NA  MAFUTA YOTE YA ROHO MTAKATIFU NDANI YAKO.

Moja ya maeneo ambayo yamekuwa na uelewa mchanga katika ukristo, ni pamoja na eneo la Roho Mtakatifu. Wengi tunachofahamu kuhusiana na huduma ya Roho Mtakatifu ni kunena kwa lugha tu! Basi. Lakini hilo ni tone moja kati ya bahari kubwa, tunahitaji kumwelewa kwa mapana na marefu ili tujue utendaji kazi wake ulivyo kwa wanadamu na ulimwengu.

Kipo kitabu cha Roho Mtakatifu, ikiwa utapenda kukipata wasiliana nasi kwa namba zilizo chini ya chapisho hili/ au tutumie ujumbe whatsapp.

Leo  tutaona sehemu mojawapo ambayo inahusiana na mafuta ya Roho Mtakatifu.  Unaweza ukajiuliza, kwanini kila mara watu waliposhukiwa na Roho Mtakatifu, maandiko yanatumia neno “wakajazwa”, na sio neno kama ‘wakavikwa’  au labda ‘wakalishwa’. Kwasababu tukisema wakavishwa maana yake tunamfanya yeye kuwa kama nguo, au tukisema wakalishwa tunamfanya yeye kuwa kama chakula. Lakini tukisema wakajazwa tunamfanya yeye kuwa kama kimiminika, na hicho si kingine zaidi ya MAFUTA. Roho Mtakatifu anakuja kwetu kama MAFUTA. Ni vema kulitambua hilo!

Sasa si watu wote wanayo mafuta yote ya Roho Mtakatifu kama Bwana Yesu alivyokuwa,. Leo tutaona aina mbalimbali za mafuta hayo, kisha tujitahidi tuyapokee yote kwa msaada wa Roho.

1.Mafuta ya nguvu

Haya yanapatikana katika UMOJA.

Zaburi 133:1 Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza, Ndugu wakae pamoja, kwa umoja.  2 Ni kama mafuta mazuri kichwani, Yashukayo ndevuni, ndevu za Haruni, Yashukayo mpaka upindo wa mavazi yake.

Maana yake ni kuwa jinsi watakatifu wanavyoshirikiana  pamoja kwa umoja, rohoni, yanaonekana ni mafuta mengi yanashuka katikati yao, mengi kiasi cha kufika hata katika upindo wa mavazi. Wanatiwa mafuta, na hayo ni ya nguvu. Kwasababu palipo na umoja ndipo penye nguvu.

Na ndio maana siku ile ya pentekoste, Mungu aliwakutanisha kwanza mahali pamoja wakawa wapo orofani pale sio katika kupiga zoga, hapana, bali katika kusali na kuomba, na kutafakari maneno ya Bwana(Matendo 1:12-14). Na ghafla, wakashangaa, katika siku ya kumi, Roho Mtakatifu amewashukia wote wakajazwa nguvu. Wakawa mashahidi wa Bwana tangu siku ile  na kuendelea (Matendo 2).

Jambo kama hilo utalithibitisha tena katika Matendo 12:14, walipokuwa wamekaa pamoja kumwomba Mungu, mahali pale pakatikiswa, wajazwa Roho Mtakatifu wakanena Neno la Mungu kwa ujasiri. Hivyo hivyo na sisi  tupenda ushirika na wengine, hususani katika kuomba na kufunga. Tukiwa watu wa namna hii tutajazwa mafuta haya na tutapokea ujasiri mwingi sana katika wokovu wetu.

Soma (Mhubiri 4:12)

2. Mafuta ya shangwe

Haya yanapatikana katika usafi na utakatifu.

Waebrania 1:8  Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi,Mungu,ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili. 9  Umependa haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio

Shangwe ni ile furaha iliyopitiliza, inayodhihirika hata mpaka kwa nje. Halikadhalika Roho Mtakatifu naye anayo shangwe yake, ambayo hiyo inazidi hata hii ya kidunia, kwasababu ya kwake inakufanya ufurahi sio tu katika raha bali mpaka katika majaribu. (Luka 10:21)

Kwamfano utaona Bwana Yesu alikuwa nayo hata pale msalabani.

Wakolosai 2:15  akiisha kuzivua enzi na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba huo.

Tukiwa watu wa kupenda haki(utakatifu), mafuta haya Roho anayaminina, mioyoni mwetu. Maisha yetu yanakuwa ni ya furaha tu, daima, vipindi vyote. Haijalishi mauvimu, kero, udhia, yataonekana kwa nje, lakini rohoni ni shangwe nyingi za Roho Mtakatifu, ndivyo Mungu alichokiweka ndani ya Kristo na kwa wakatifu wa kale ( Matendo 13:52, Waebrania 11:13, , Mathayo 5:12).

Hivyo Tuchague kupenda maisha ya haki ili tuyapate mafuta haya. Ni muhimu sana, ukipoteza furaha ya wokovu, huwezi kusonga mbele.

3. Mafuta ya upambanuzi

Haya yanaachiliwa katika kulitunza Neno la Mungu ndani yako.

1Yohana 2:26  Nimewaandikia haya katika habari za watu wale wanaotaka kuwapoteza. 27  Nanyi, mafuta yale mliyoyapata kwake yanakaa ndani yenu, wala hamna haja ya mtu kuwafundisha; lakini kama mafuta yake yanavyowafundisha habari za mambo yote, tena ni kweli wala si uongo, na kama yalivyowafundisha, kaeni ndani yake.

Kumbuka biblia ni sauti ya Mungu katika maandishi, hivyo unavyoiweka moyoni mwako, ndivyo inavyoumbika  na kuwa sauti kamili ya Mungu. Na hiyo ndio itakayokufudisha, na kukusaidia kupambanua, ikiwa wewe ni mkristo na una miaka  mingi katika wokovu halafu hujawahi kuisoma BIBLIA yote, bado kuna viwango Bwana hawezi kusema na wewe.  Lakini Unavyozidi kujifunza Neno ndivyo mafuta haya yanavyoachiliwa ndani yako kukufundisha. “Huna Neno, huna sauti ya Mungu”

4. Mafuta ya kuhudumu

Haya huachiliwa katika kuwekewa mikono na wakufunzi wako, au kuombewa na kanisa (wazee wa kanisa).

Huu ni utaratibu mwingine Mungu ameuachilia, katika kanisa, vipo vitu ambavyo huwezi kuvipokea wewe tu mwenyewe. Bali kutoka kwa waliokutangulia kiimani.

Elisha alitiwa mafuta na Eliya, akasimama mahali pake kihuduma (1Wafalme 19:15-16)

Musa aliwatia mafuta wale wazee 70, sehemu ya roho yake ikawaingia (Hesabu 11:16-25)

Daudi na Sauli wote walitiwa mafuta ya Samweli, ndipo wakapokea nguvu kutoka kwa Mungu, kutumika. (1Samweli 15:1, 16:12,)

Vilevile Timotheo, aliwekewa mikono na mtume Paulo  (2Timotheo 1:6), akapokea neema ya kuyasimamia makanisa ya Kristo, mahali pa Paulo.

Vivyo hivyo na wewe usikwepe, wala usimdharau kiongozi wako wa kiroho, hata kama atakuwa ana madhaifu. Anayo sehemu yake aliyopewa na Mungu kwa ajili yako. Jinyenyekeze omba akuwekee mikono neema ya Mungu ijae ndani yako ya kuhudumu, ili Bwana akunyanyue katika viwango vya juu zaidi.

Hivyo kwa kuzingatia aina hizo 4, tukazipokea basi tutamsogelea Bwana katika mafuta mengi sana ya juu. Mfano wa Bwana wetu Yesu Kristo. Roho Mtakatifu atajifunua zaidi ndani yetu.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

TUUTAFUTE UMOJA WA ROHO.

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

Nini maana ya’Shangwe ya waovu ni kwa muda kidogo’Ayubu 20:4

Wakapaka mafuta watu wengi waliokuwa wagonjwa, wakawapoza

Je tunaruhusiwa kujipaka mafuta au kujipulizia marashi?

Masihi ni nani?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini tofauti kati ya Kipawa na Karama?

Jibu: Ili tuelewe vizuri tofauti ya haya maneno mawili “kipawa na karama” hebu tuutafakari mfano ufuatao;

Watu wawili wamepewa zawadi ya magari ya kutembelea, tena yanayofanana, kila mmoja la kwake.. Ila wa kwanza akalitumia lile gari kwa faida yake yeye, yaani kumrahisishia usafiri, na kwa matumize yake binafsi…..na wa pili akalichukua lile gari alilopewa na kwenda kulifanya kuwa gari la kuwasaidia wagonjwa mahospitalini (ambulance) tena bure…

Sasa kibiblia Magari waliyopewa hawa watu wawili ndiyo yanayofananishwa na  VIPAWA vya Mungu,  lakini huyo wa pili aliyelifanya gari lake kuwa gari la huduma (msaada kwa wengine), gari lake hilo ndilo linalofananishwa na KARAMA, kwasababu alilitoa kwaajili ya kuwasaidia wengine na si kwa faida yake yeye… Yeye alikuwa radhi atembee kwa miguu, lakini si wagonjwa wasifie nyumbani kwa kukosa usafiri wa haraka kufika katika vituo vya huduma..

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Kipawa ni zawadi ya kipekee kwa Mtu anayopewa na Mungu , lakini karama imeenda mbali zaidi;ni zawadi ya kipekee kwa Mtu kutoka kwa Mungu yenye lengo la kuwasaidia wengine (kuwanufaisha wengine).

Kwamaana hata asili ya neno lenyewe karama ni “kukirimu” na kukirimu maana yake ni kusaidia..na mtu anayekirimu ndio anaitwa Mkarimu.

Na leo hii kuna watu wengi wenye vipawa makanisani lakini hawana karama!… Wengi leo wana vipawa vya kuimba lakini hawana karama ya kuimba…

Wana vipawa vya kunena kwa lugha lakini hawana karama ya kunena, wana vipawa vya kutabiri lakini hawana karama za kutabiri..

kwasababu gani?…Ni kwasababu vile vipawa wanavitumia kwa faida zao wenyewe na si kwa faida ya mwili wa Kristo…wanavitumia kwaajili ya umaarufu wao na kwa matumbo yao, na si kwaajili ya kuujenga mwili wa Kristo.

1 Wakorintho 14:12 ”Vivyo hivyo na ninyi, kwa kuwa mnatamani sana kuwa watu wenye karama za roho, takeni kwamba mzidi sana kuwa nazo ili kulijenga kanisa”.

Hapo anasema “ili kulijenga kanisa”, na si kwaajili yetu…

Jitazame!..Je kipawa ulichonacho ni kwa kukunufaisha wewe au wengine?..

Je kipawa ulichonacho cha kuimba, kufundisha au kuhubiri au kuimba au unabii.. je kinafanya kazi ya kuujenga mwili wa Kristo au kujenga umaarufu wako na kujaza tumbo lako?..na kujiongezea utukufu?.

Kama kipawa chako kinakunufaisha wewe zaidi ya wengine, kama hakilitukuzi jina la Yesu, bali kinakutukuza wewe zaidi….basi tambua ya kuwa bado hauna Karama yoyote!…haijalishi unafanya miujiza kiasi gani, haijalishi unajua kuimba kiasi gani au unasifiwa na watu wote duniani..bado huna karama ya Roho.

Kifanye kipawa chako kuwa Karama!!.

Na madhara ya kutokuwa na karama yoyote maana yake hutakuwepo “karamuni” siku ile!!…Kwasababu watakaoalikwa katika karamu ya Mwanakondoo ni wale waliokuwa na karama na walizitumia vizuri kwa manufaa ya mwili wa Kristo…Kwasababu hata mzizi wa neno hilo karamu ni “karama”.

Je unataka karama za Rohoni basi Kifanye kipawa chako kuwa baraka kwa wengine..

1 Wakorintho 12:4 “Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule.

5 Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule.

6 Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.

7 Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho KWA KUFAIDIANA”.

Nataka tuutazame huo mstari wa mwisho unaosema “KWA KUFAIDIANA”.

Hapo mwisho anasema “kwa kufaidiana”

Siku zote kuwa mtu mwenye Nia ya kuujenga mwili wa Kristo, kuwa na nia ya kuwasaidia wengine pasipo kutegemea faida wala malipo!..na Kipawa chako Bwana atakigeuza kuwa KARAMA.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?

USINIE MAKUU.

KUOTA UNAENDESHA GARI.

NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.

Rudi nyumbani

Print this post

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe,

Leo tutajifunza jinsi ya kuuvuta uwepo wa Roho Mtakatifu karibu nasi. Yapo mambo makuu matatu yanayovuta uwepo wa Mungu karibu nasi.

  1. MAOMBI

Hili ni jambo la kwanza linalohifadhi uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yetu. Tunapoingia kwenye maombi Roho Mtakatifu anazidi kusogea karibu nasi,  anasogea kuomba pamoja na sisi (Warumi 8:26) na vile vile anasogea kuzungumza na sisi.

Kama wewe ni msomaji wa biblia utakumbuka kipindi, Bwana Yesu anabatizwa katika mto Yordani na Yohana, utaona Roho Mtakatifu alishuka juu ya Bwana kwa mithili ya HUA (Yaani Njiwa).

Lakini katika tukio hilo kuna siri moja imejificha pale, ambayo ukisoma kwa haraka haraka unaweza usiigundue. Na siri yenyewe ni MAOMBI!. Utaona baada ya Bwana kutoka majini, na kusogea pembeni utaona alianza KUOMBA!, na wakati akiwa katika maombi, ndipo Mbingu zilipofunguka na Roho Mtakatifu kushuka juu yake.

Luka 3:21 “Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, NAYE ANAOMBA, mbingu zilifunuka;

22 Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili, kama hua; sauti ikatoka mbinguni, Wewe ndiwe Mwanangu, mpendwa wangu; nimependezwa nawe”.

Umeona? Ni wakati alipokuwa anaomba ndipo Roho Mtakatifu alishuka juu yake, na sio wakati anabatizwa tu peke yake.

Vile vile utaona kipindi cha Pentekoste, Mitume na wanafunzi wengine wapolikuwa wamekusanyika mahali Pamoja katika ghorofa wakidumu katika kusali, na kule kule ndipo Roho Mtakatifu akashuka juu yao na kuwajaza nguvu (Soma Matendo 1:13-14, Matendo 2:1-2).

Na sehemu nyingine nyingi, utona kuwa Roho Mtakatifu alishuka wakati watu wakiwa kwenye maombi..

Matendo 4:31 “Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri”.

Vile vile na sisi tukitaka kuuvuta uwepo wa Roho Mtakatifu hata tumuhisi ndani yetu, au katikati yetu basi hatupaswi kuyakwepa MAOMBI, kadhalika tukitaka tumsikie anataka nini kwetu au anasema nini, njia pekee ni Maombi!

Sasa inawezekana hujui namna ya kuomba, ni rahisi sana.. Kama utatamani kupata mwongozo wa namna ya kuomba basi tutumie ujumbe inbox, ili tuweze kukutumia somo linalohusu “Njia bora ya kuomba”

  1. KUSOMA NENO.

Hii ni njia nyingine ya Muhimu ya kuuvuta uwepo wa Roho Mtakatifu karibu nasi. Kazi mojawapo ya Roho Mtakatifu ni kutuongoza na kututia katika Kweli yote (Yohana 6:13-14), na Kweli ni Neno la Mungu (Yohana 17:17). Hivyo tunapotenga muda wa kuishika biblia na kuisoma kwa lengo la kujifunza, basi Roho Mtakatifu anasogea karibu nasi sana. Ni lazima atusogelee kwasababu ndio kazi yake yeye kutufundisha na kutufunulia maandiko.

Tunaweza kujifunza kwa yule Mkushi aliyekuwa anarudi nchini kwao, ambapo njiani alijikuta anafungua kitabu cha Isaya 53, kilichokuwa kinazungumzia Habari za Masihi, Yesu lakini hakuwa na ufunuo wowote juu ya hilo, Ndipo Roho Mtakatifu akaingia kazini kujisogeza karibu naye ili amtie katika kweli yote!!..

Roho Mtakatifu akaanzaa kuzungumza kwanza na Filipo siku kadhaa kabla hata ya Mkushi huyo kufikiria kusoma hilo andiko, Roho Mtakatifu akaanza kutengeneza njia ya kumkaribia Mkushi huyo, akamwambie Filipo ashuke njia ya jangwa, na alipokutana na yule Mkushi yupo matatani haelewi maandiko, ndipo Roho Mtakatifu akaanza kuzungumza kupitia kinywa cha Filipo. Na hatimaye kumfunua macho yake na kumtia katika kweli yote.

Matendo 8:29 “Roho akamwambia Filipo, Sogea karibu na gari hili, ukashikamane nalo.

30 Basi Filipo akaenda mbio, akamsikia anasoma chuo cha nabii Isaya; akanena, Je! Yamekuelea haya unayosoma?

31 Akasema, Nitawezaje kuelewa, mtu asiponiongoza? Akamsihi Filipo apande na kuketi pamoja naye.

32 Na fungu la Maandiko alilokuwa akilisoma ni hili, Aliongozwa kwenda machinjoni kama kondoo, Na kama vile mwana-kondoo alivyo kimya mbele yake amkataye manyoya, Vivyo hivyo yeye naye hafunui kinywa chake.

33 Katika kujidhili kwake hukumu yake iliondolewa. Ni nani atakayeeleza kizazi chake? Kwa maana uzima wake umeondolewa katika nchi.

34 Yule towashi akamjibu Filipo, akasema, Nakuomba, nabii huyu; asema maneno haya kwa habari ya nani; ni habari zake mwenyewe au za mtu mwingine?

35 Filipo akafunua kinywa chake, naye, akianza kwa andiko lilo hilo, akamhubiri habari njema za Yesu.

36 Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe?

37 Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]

38 Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.

39 Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi”.

Roho wa Yesu ni yule yule na tabia zake ni zile zile, tukitaka atukaribie, tumsikie, au tumwone basi ni lazima pia tuwe wasomaji wa Neno.

  1. KUHUBIRI/KUSHUHUDIA.

Agizo kuu ambalo Bwana alilotupatia ni kupeleka injili ulimwenguni kote.

Marko 16:15 “Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.

16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”.

Kwanini kuhubiri/kumshuhudia Yesu kunamsogeza Roho Mtakatifu karibu nasi?. Kwasababu kila tunapofika mahali na kushuhudia tunafanyika vyombo vya Roho Mtakatifu, Hivyo Roho Mtakatifu hana budi kila wakati kuwa nasi kwasababu wakati wote tunatumika kama vyombo vyake, hakuna wakati uwepo wake utakaa mbali na sisi!..

Mathayo 10:18 “nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa.

19 Lakini hapo watakapowapeleka, msifikiri-fikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema.

20 KWA KUWA SI NINYI MSEMAO, BALI NI ROHO WA BABA YENU ASEMAYE NDANI YENU”.

Kwahiyo kama wakati wote tutakuwa katika hayo mazingira ya kumshuhudia Kristo, maana yake wakati wote, kinywa kitakachokuwa kinasema ndani yetu ni kinywa cha Roho Mtakatifu, hivyo uwepo wake utakuwa nasi muda wote!, lakini kama hatutakuwa katika mazingira yoyote ya kumshuhudia Kristo ni ngumu Roho Mtakatifu kuwa na sisi, kuzungumza kupitia vinywa vyetu, au kusema nasi!.

Je! Na wewe leo Umempokea Yesu?

Na kama ndio je! Wewe ni MWOMBAJI?..wewe ni MSOMAJI WA NENO?…wewe ni MSHUHUDIAJI?. Kama hufanyi hayo basi, uwepo wa Roho Mtakatifu utawezaje kuusikia?, vile vile sauti yake utaweza kuisikia?!.

Leo shetani kawafanya wakristo wengi wasiwe Waombaji?..utakuta mkristo mara ya mwisho kutenga angalau lisaa limoja kuomba yeye binafsi hata hakumbuki!, (yeye atakuwa anapenda kusikiliza na kusoma mahubiri tu!, na kuombewa lakini kuomba mwenyewe hataki/hawezi), Utakuta mkristo mara ya mwisho kusoma Neno binafsi ni muda mrefu sana, leo hata ukimuuliza mkristo biblia ina vitabu vingapi hajui, ukimpa biblia afungue kitabu cha Yeremia atapepesuka nusu saa hajui kilipo mpaka akaangalie kwenye index, hiyo ni kuonesha ni jinsi gani biblia ni kitabu-baki tu kwake!, na si kila kitu kwake!.

Leo hii ukimwuliza mkristo mara ya mwisho kuzungumza na mtu mwingine Habari za wokovu, au kumshuhudia Kristo, hana hiyo kumbukumbu!, lakini shuhuda za mipira, na za Maisha ya watu wengine zimejaa katika kinywa chake!..

Kumbuka Bwana anatamani yeye kuwa karibu na sisi kuliko sisi tunavyotamani yeye awe karibu nasi, hivyo ni wajibu wetu kuongeza bidii katika kuomba, kusoma Neno, kushuhudia Pamoja na kuishi Maisha matakatifu.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

Shekina ni nini? Na Je! Utukufu wa shekina unamaana gani?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

1Wakorintho 12:3 “Kwa hiyo nawaarifu, ya kwamba hakuna mtu anenaye katika Roho wa Mungu, kusema, Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu.”

Katika hali ya kawaida kila mtu anaweza kusema “Yesu ni Bwana”, hata watu wa kidunia, wanaweza kulitamka hilo neno, lakini wasiwe wamemaanisha, au wamejua uzito wake, wakawa wamelitaja tu.. Lakini kwa mtu ambaye amempokea Roho Mtakatifu, na kufunuliwa kwa Roho kuwa Yesu ni nani, kwanini amekuja duniani, kwanini  amwage damu yake, afe na kufufuka, na yupo wapi sasahivi?..Mtu wa namna hiyo kama akitamka “Yesu ni Bwana”,… kutamka kwake kunakuwa na maana sana na nguvu kubwa. Kwasababu amekutamka katika Roho.

Hivyo Mtu anayetaja “Yesu ni Bwana” katika Roho Mtakatifu ni lazima atakuwa ni mtakatifu, kwasababu amemjua Mungu, kadhalika atakuwa anamheshimu Mungu na kumwogopa, kutokana na ufunuo mzito alioupata kumhusu Yeye (Yesu).

Lakini Yule anayesema  tu “Yesu ni Bwana” bila Roho, maana yake hamjui Yesu, hana mpango na maneno yake, hana  ufunuo wowote alioupata unaomfanya  yeye aseme hivyo, mtu wa namna hiyo kutamka kwake hakuna manufaa yoyote, ndio maana hapo biblia inasema.. “mtu hawezi kusema Yesu ni Bwana isipokuwa katika Roho Mtakatifu”..maana yake atakuwa anasema tu kimdomo, na si kwa kuelewa na kumaanisha.

Bwana Yesu alisema maneno haya…

Mathayo 7:21 “SI KILA MTU ANIAMBIAYE, BWANA, BWANA, ATAKAYEINGIA KATIKA UFALME WA MBINGUNI; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

22  Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23  Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”

Umeona?.. Kusema tu “Yesu ni Bwana” bila ya kuwa na badiliko halisi la ndani, ambalo hilo linaletwa na Roho Mtakatifu mwenyewe, ni kazi bure!.. Vile vile huwezi kuwa na Roho Mtakatifu halafu useme Bwana Yesu kalaaniwa.. hilo haliwezekani.

Hivyo ili tuyafanye mapenzi ya Mungu, na maneno ya midomo yetu pamoja na sala zetu zikubalike mbele za Mungu, hatuna budi kuzaliwa mara ya pili, na kuzaliwa mara ya pili kunakuja kwa kutubu dhambi, kwa kumaanisha kuziacha, na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi pamoja na kupokea Roho Mtakatifu.

Baada ya hapo, lolote tunalolitamka la kumwadhimisha Mungu, kumsifu, kumwomba, na kumkiri linakuwa katika Roho, na hivyo linaleta matokeo makubwa sana. Lakini kama hatutatubu kwa kumaanisha kuacha dhambi, hata sala zetu zinakuwa ni bure, hata sifa zetu kwake zinakuwa ni bure…

2Timotheo 2: 19  “Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu”

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Kwanini Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake wasichukue chochote isipokuwa fimbo tu?

DAMU YA YESU INANENAJE MEMA KULIKO YA HABILI?

YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.

TOFAUTISHA KATI YA MAFUNDISHO YA YESU, NA YA WAANDISHI.

Rudi nyumbani

Print this post

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

Moja ya mambo muhimu kuyafahamu pia ni  kuhusu Roho Mtakatifu. Kwasababu Roho Mtakatifu ndio ukamilifu wa sauti ya Mungu kwetu..

Sasa kabla ya kwenda kuzitazama kazi kuu tatu za Roho Mtakatifu, hebu tuweke msingi kidogo wa kuufahamu utendaji kazi wa Mungu, katika ofisi zake tatu.

Wakati wa agano la kale, Mungu alizungumza na watu kutoka mbinguni, mwanzo wa agano hili jipya Mungu akazungumza na sisi ndani ya mwili wa Bwana Yesu.(Waebrania 1:2), na baadaye akazungumza na sisi kupitia Roho Mtakatifu. Ni sawa na kusema.. Mungu alizungumza nasi akiwa juu yetu(Kama Baba), kisha akazungumza nasi akiwa pamoja nasi katika mwili wa kibinadamu (Imanueli) na mwisho Mungu anazungumza ndani yetu kama(Roho Mtakatifu).

Katika hatua hizi tatu, hatua hiyo ya mwisho ndio hatua kamilifu kuliko nyingine zote, kwasababu Ni sauti ya Mungu iliyo karibu sana na sisi kuliko ilivyokuwa juu yetu (kama Baba), au ilivyokuwa pamoja nasi (kama mwana).

Ni sawa mtu azungumze na wewe kwa sauti kuu akiwa juu kabisa kwenye gorofa, kiasi kwamba humuoni ila unachoweza kusikia ni sauti yake tu na wewe upo chini ya hilo ghorofa, bila shaka kuna maneno ambayo unaweza usiyasikie vizuri kwasababu yupo mbali,  hivyo maneno mengine unaweza kuyaelewa kinyume na alivyosema.. Lakini huyo mtu atakapotoka huko aliko na kushuka chini ukamwona, akawa kama mita 5 kutoka mahali ulipo, akizungumza na wewe ni rahisi kumsikia vizuri kuliko alivyokuwa kule juu, ambapo ulikuwa unasikia sauti tu na sasa unamsikia na kumwona, lakini pia bila shaka wakati anazungumza kuna maneno unaweza usiyasikie vizuri, hata wewe unapozungumza na mtu aliye karibu na wewe ni lazima utapitia vipindi vichache vichache vya kuomba arudie alichosema…

Lakini hebu tafakari tena endapo huyo huyo mtu akikukaribia sana kiasi kwamba mdomo wake unafika katika sikio lako, bila shaka hapo utakuwa unamsikia vizuri zaidi kuliko alivyokuwa mita mbili mbele yako..hapo huwezi kumwambia arudie rudie yale anayoyasema.. Hivyo utamsikia vizuri kuliko kawaida, na utamwelewa, kwasababu amesogea karibu sana na wewe.

Na utendaji kazi wa Mungu ni hivyo hivyo, Roho Mtakatifu ni sauti ya Mungu iliyo karibu sana na sisi, haijaishia kusikika masikioni tu, bali inasikika hadi mioyoni mwetu. Ni sauti isiyo na chenga chenga. Sauti ya Bwana Yesu ilikuwa ni kamilifu, lakini ilikuwa na chenga chenga kwetu, hatukuweza kumwelewa vizuri kwasababu alikuwa anazungumza nje ya miili yetu. Ndio maana ilimpasa Bwana aondoke ili Yule Roho aje juu yetu.

Yohana 16:7 “ Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu”.

Umeona hapo? Bwana hana budi kuondoka ili Roho Mtakatifu aje…(Na kumbuka Roho Mtakatifu ndiye Yule Yule Bwana Yesu mwenyewe, isipokuwa anakuja katika roho (soma 2Wakorintho 3:17),

Sasa baada ya kuelewa hayo, twende kwa pamoja tukazitazame kazi kuu tatu za Roho Mtakatifu kwa ulimwengu.

1) Kazi ya kwanza ni kuuhakikisha ulimwengu kwa habari ya DHAMBI  2) Atauhakikisha kwa habari ya HAKI   3) Atauhakikisha kwa habari ya HUKUMU.

Hizi ndio kazi kuu tatu za Roho Mtakatifu kwa Ulimwengu, tutaziangalia moja baada ya nyingine.

1. Kwa habari ya dhambi:

Yohana 16:8 “Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu.

9  Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi”

Kuhakikisha maana yake ni “kuweka sawa jambo”. Kitu ambacho hakikukaa vizuri sasa kimewekwa vizuri maana yake kitu hicho“kimehakikiwa”. Kadhalika Hapo Bwana Yesu anasema huyo Roho atakapokuja atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, maana yake hapo kwanza yeye alizungumza kuhusu dhambi lakini hakueleweka vizuri, lakini atakapokuja huyo Roho ataizungumzia vizuri dhambi kwa sauti ya ukaribu zaidi, na atafanya wengi kuelewa dhambi ni nini, kuliko jinsi wangemwelewa Bwana.

  Ndio maana Bwana Yesu anasema hapo… “Kwa habari ya dhambi, KWA SABABU HAWANIAMINI MIMI ”… maana yake yeye aliihubiri sana kuhusu dhambi, lakini watu hawakumwamini. Hivyo Roho Mtakatifu atakuja kuielezea vizuri na wengi wataamini. Na kumbuka dhambi ni “kutomwamini Mwana wa Mungu, kwamba yeye ndiye mkombozi wa ulimwengu. Hiyo ndiyo dhambi…hayo mengine kama uasherati, wizi, uchawi, uuaji n.k ni matokeo ya dhambi. Kwahiyo Bwana Yesu alihubiri sana kwamba “kila amwaminiye atapata uzima wa milele lakini Yule asiyemwamini atahukumiwa, maana yake atakuwa na dhambi”. Lakini pamoja na kuyasema hayo sana kwa kipindi cha miaka mitatu na nusu, si wengi waliomwamini, ndio maana injili haikufika duniani kote, kipindi Bwana Yesu yupo duniani anahubiri. Ni wachache tu ndio waliokuwa wanaisikia sauti yake, wengine walikuwa hawamwelewi.

Lakini baada ya Roho Mtakatifu kushuka siku ile ya Pentekoste, Petro alivyosimama siku ile kuhubiri habari ya dhambi, biblia inasema watu zaidi ya elfu tatu waliokoka ndani ya siku moja.(Matendo 2:41). Na wakati miezi miwili tu nyuma, Bwana Yesu alizungumza maneno hayo hayo, tena mji ule ule Yerusalemu, lakini waliishia kumsulubisha, kwasababu hawakumwelewa.

Yohana 12:37  “Walakini ajapokuwa amefanya ishara nyingi namna hiyo mbele yao, hawakumwamini;

38  ili litimie lile neno la nabii Isaya alilolisema, Bwana, ni nani aliyezisadiki habari zetu; Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani?”

Lakini miezi miwili tu baadaye kama tunavyosoma katika kitabu cha Matendo 2, Roho Mtakatifu alipozungumza kwa kinywa cha Petro, wale ambao hawakumwamini Bwana Yesu Yerusalemu, walianza kumwamini kwa kasi sana.

2. Kwa habari ya HAKI.

Yohana 16:10  “kwa habari ya haki, kwa sababu mimi naenda zangu kwa Baba, wala hamnioni tena”

Katika kipengele ambacho Bwana hakukigusia kabisa wakati yupo hapa duniani, ni kipengele cha HAKI. Na haki inayozungumziwa hapo, ni haki ile ipatikanayo kwa njia ya IMANI. Hii Bwana hakuigusia kabisa, na lengo la kutoielezea hii ni kwasababu ya ugumu wa mioyo ya watu, Ndio maana aliwaambia “yapo mambo ya kuwaambia lakini kwa wakati huo wasingeweza kustahimili,mpaka huyo Roho atakapokuja”

Yohana 16:12  “Hata bado nikali ninayo mengi ya kuwaambia, LAKINI HAMWEZI KUYASTAHIMILI HIVI SASA.

13  Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake”.

Umeona jambo mojawapo ambalo wasingeweza kustahimili endapo wangeambiwa ni hilo la “HAKI”. Laiti Bwana angewafunulia siri Mitume kwamba, sisi watu wa mataifa nasi ni warithi wa ahadi za Mungu, kwamba kwa NEEMA tunahesabiwa HAKI kwa Kumwamini Yesu, kwamba na sisi ni warithi wa ahadi za Mungu, ni dhahiri kuwa wangerudi nyuma. Wangesema Bwana Yesu kachanganyikiwa. Yule aliyemwita Yule mwanamke wa kimataifa “Mbwa” halafu leo anamwita “mrithi”?.. Yule ambaye aliwatuma na kuwaambia “msifike miji ya mataifa kuhubiri (Mathayo 10:5)” ghafla anawaita tena mataifa ni warithi!!… Yule aliyesema “sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli (Mathayo 15:24)”. Leo hii yeye ndio atutume sisi huko kwao kuhubiri??.. Hakika amechanganyikiwa.

Hivyo Bwana aliliacha hilo hakuwaambia mitume, pamoja na mengine mengi ili yaje kufunuliwa na Roho Mtakatifu baada ya kuondoka kwake. Kwasababu kwa uchanga waliokuwa nao Mitume, wangeambiwa hizo siri, wangemwacha Bwana na kurudi nyuma (wasingeweza kustahimili)

Na siku ya kuifunua hiyo siri  ya HAKI YA MUNGU ilipofika, Roho Mtakatifu alimfunulia kwanza Mtume Petro, kipindi kile cha lile ono la Kornelio, na baada ya hapo alikuja kumfunulia tena Mtume Paulo hiyo siri..

Hebu soma hichi kisa taratibu..

Matendo 11:1  “Basi mitume na ndugu waliokuwako katika Uyahudi wakapata habari ya kwamba watu wa Mataifa nao wamelipokea neno la Mungu.

2  Na Petro alipopanda kwenda Yerusalemu, wale walio wa tohara wakashindana naye,

3  wakisema, Uliingia kwa watu wasiotahiriwa ukala nao.

4  Petro akaanza kuwaeleza kwa taratibu, akasema,

5  Nalikuwa katika mji wa Yafa, nikiomba, roho yangu ikazimia, nikaona maono; chombo kinashuka, kama nguo kubwa inatelemshwa kutoka mbinguni kwa pembe zake nne, kikanifikilia.

6  Nikakitazama sana, nikifikiri, nikaona wanyama wa nchi wenye miguu minne, na wanyama wa mwituni, nao watambaao, na ndege wa angani.

7  Nikasikia na sauti ikiniambia, Ondoka, Petro, ukachinje ule.

8  Nikasema, Hasha, Bwana, kwa maana kitu kilicho kichafu au kilicho najisi hakijaingia kabisa kinywani mwangu.

9  Sauti ikanijibu mara ya pili kutoka mbinguni, Alivyovitakasa Mungu, usivinene wewe najisi.

10  Jambo hili likatendeka mara tatu, kisha vitu vyote vikavutwa tena juu mbinguni.

11  Na tazama, mara hiyo watu watatu wakasimama mbele ya nyumba tuliyokuwamo, waliotumwa kwangu kutoka Kaisaria.

12  Roho akaniambia nifuatane nao, nisione tashwishi. Ndugu hawa sita nao wakaenda pamoja nami, tukaingia katika nyumba ya mtu yule;

13  akatueleza jinsi alivyomwona malaika aliyesimama nyumbani mwake na kumwambia, Tuma watu kwenda Yafa ukamwite Simoni aitwaye Petro,

14  atakayekuambia maneno ambayo yatakuokoa, wewe na nyumba yako yote.

15  Ikawa nilipoanza kunena, Roho Mtakatifu akawashukia kama alivyotushukia sisi mwanzo.

16  Nikalikumbuka neno lile la Bwana, jinsi alivyosema, Yohana alibatiza kwa maji kweli, bali ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.

17  BASI IKIWA MWENYEZI MUNGU AMEWAPA WAO KARAMA ILE ILE ALIYOTUPA SISI TULIOMWAMINI BWANA YESU KRISTO, MIMI NI NANI NIWEZE KUMPINGA MUNGU?”

Umeona hapo? Kornelio ambaye ni mtu wa Mataifa anapokea Roho Mtakatifu  baada ya kuamini, tena Roho Yule Yule waliyepokea wakina Petro walio waisraeli,  bila shaka Petro alijua ni kwanini Bwana Yesu hakuwaambia hiyo siri wakati wapo duniani, alijua ingekuwa ni ngumu wao kumeza!… Maana unaona hapo juu tu kama tulivyosoma, mitume wengine walipopata habari ya kwamba Petro kaingia kwa watu wa mataifa, walishindana naye vikali..Mpaka Petro alipowaelezea kwa utaratibu..

Hiyo ndiyo siri ya Mungu ambayo ilisitirika tangu zamani, kwamba sisi watu wa MATAIFA, ni warithi wa ahadi za Mungu, kwamba tunahesabiwa HAKI YA KUURITHI UZIMA WA MILELE bure kwa njia ya IMANI YA KUMWAMINI YESU, Mitume hapo kabla walidhani wokovu ni kwaajili yao tu! (Wayahudi), lakini kumbe sivyo!.. hata watu wa mataifa pia..

Mtume Paulo naye aliielezea siri hii katika Wakolosai 1:26-27,  na katika Waefeso 3:6, unaweza kuisoma mistari hiyo binafsi.

Hiyo ndio maana Bwana Yesu akasema kwamba…. “kwa habari ya haki, kwa sababu mimi naenda zangu kwa Baba, wala hamnioni tena”…..Maana yake alipaswa aelezee hiyo Haki, lakini anaondoka anakwenda kwa Baba na wala hawatamwona tena, na wala hataielezea hiyo siri, lakini Roho atakuja kuliweka hilo sawa!..maana yake atalifunulia kanisa.

3. Kwa habari ya HUKUMU.

Yohana 16:11  “kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa”.

Hapo mkuu wa Ulimwengu anayezungumziwa ni  “shetani”. Na Bwana Yesu anasema…Mfalme wa ulimwengu amekwishahukumiwa.. Sasa hukumu inayozungumziwa hapo si ile ya ziwa la moto, (Hiyo ni kweli ilishapitishwa kitambo), lakini hukumu inayozungumziwa hapa si hiyo, bali ni hukumu ya kunywang’anywa mamlaka ya ulimwengu!!. Na kwamba mamlaka yote ya Duniani amekabidhiwa Yesu.

 Na mamlaka hayo shetani aliyapoteza wakati Bwana Yesu akiwa hapa duniani!. Kwajinsi alivyoutoa uhai wake kwaajili ya wengi, akakabidhiwa mamlaka yote ya mbinguni na duniani.

Mathayo 28:18 “Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, NIMEPEWA MAMLAKA YOTE MBINGUNI NA DUNIANI”.

Sasa atakapokuja Roho Mtakatifu, ataliweka hilo sawa katika mioyo ya watu wengi, Watu wataelewa kwa undani ni kwa jinsi gani sasa hivi YESU NDIYE ANAYETAWALA MBINGUNI NA DUNIANI, NA HAKUNA MFALME MWINGINE KAMA YEYE. Mitume hawakumwelewa Bwana Yesu vizuri wakati wakiwa naye!!. Walikuja kumwelewa vizuri baada ya kuondoka kwake!. Kwamba alikuwa ni nani?.. Yule Yohana ambaye alikuwa anaegemea kifuani pa Yesu, ambaye alikuwa anamwona Bwana Yesu kama kaka yake tu! (Yohana 13:23)… Huyo huyo anakuja kumwona Bwana Yesu katika kisiwa cha Patmo kama miale ya moto, na anaanguka chini ya miguu yake kama mtu aliyekufa!! (Kasome Ufunuo 1). Roho Mtakatifu anamfunulia Yule Yule Yesu kama Mfalme wa wafalme, ambaye enzi na mamlaka yote ni zake.

Waefeso 1:20 “aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho;

21 juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia;

22  AKAVITIA VITU VYOTE CHINI YA MIGUU YAKE, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo

23  ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote”

Hivyo Roho Mtakatifu, atakapokuja atauonyesha ulimwengu kuwa YULE mkuu wa ulimwengu, shetani…hata kitu! Mbele za Bwana, kashashindwa…

Yohana 14:30 “ Mimi sitasema nanyi maneno mengi tena, kwa maana yuaja mkuu wa ulimwengu huu, wala hana kitu kwangu”

Hana mamlaka yoyote juu ya wote waliomwamini Yesu..kashahukumiwa na kunyang’anywa mamlaka ya duniani na kuzimu. Wafu wote wanamilikiwa na Bwana Yesu (Warumi 14:9), maana yake ni kwamba mfano wa jambo lililotokea kwa Samweli, kuletwa juu na yule mchawi, kwasasa haliwezekani tena, kwasababu mkuu wa ulimwengu kashahukumiwa (kashanyang’anywa hayo mamlaka), anayewamiliki wafu wote kwasasa ni Mkuu wa Uzima, YESU!. Huyo pekee yake ndiye mwenye mamlaka ya kuileta roho ya mtu  juu na kuishusha chini, yeye peke yake ndiye mwenye mamlaka na uwezo wa kufufua au kuua!.

Kwahiyo kwa kazi hizo tatu ambazo Bwana Yesu alizozitaja, ndizo zinazokamilisha ushuhuda kamili wa Roho Mtakatifu kwa ulimwengu!!..

Na Roho huyo ndiye anayeshuhudia hata sasa…Na anashuhudia kwa vinywa vya watumishi wake waliojazwa na Roho Mtakatifu, Kwamba Kristo ni kweli!, na Watu wote kutoka mataifa yote na makabila yote anawapokea na kuwakubali na kuwahesabia Haki ya kupata uzima wa milele endapo watamjia, Kadhalika Bwana YESU ndiye mmiliki wa mbingu na nchi na shetani hana kitu mbele zake. Hivyo yeye ndio tumaini pekee la kulikimbilia na kulitegemea.

Je umezitii ushuhuda hizo za Roho Mtakatifu???.. kwa Kumpokea Yesu maishani mwako na kutubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha kabisa???, kumbuka yeye anapokea watu wote haijalishi ni kutoka Taifa gani, wala kabila gani.

 Kama bado hujamwamini, basi fahamu kuwa umeukataa ushuhuda wa Roho Mtakatifu maishani mwako.. Na hivyo utakuwa na HATIA kubwa, kwasababu Roho Mtakatifu amezungumza na wewe kwa sauti ya kueleweka kabisa, hivyo umeukataa ushuhuda ulio mkamilifu kabisa.

 Hivyo mpokee leo Yesu maishani mwako, Ukubali ushuhuda wa Roho Mtakatifu, ili ufanikiwe katika roho yako, biblia inasema yeye Roho Mtakatifu anatutamani kiasi cha kutuonea wivu, anatamani aingie ndani yako kuliko wewe unavyotamani aingie ndani yako, hivyo ulichobakisha tu ni kutii!.. kwa kutubu dhambi zako na kwenda kubatizwa ubatizo sahihi, kama bado hujabatizwa. Kumbuka ubatizo sahihi ni ule wa maji mengi (Yohana 3:23), na kwa jina la Yesu Kristo (Matendo 2:38).

Na baada ya hapo, Neema ya kipekee ya Bwana itakuwa nawe daima.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

UTENDAJI KAZI MWINGINE WA ROHO MTAKATIFU USIOUFAHAMU.

KWASABABU MUDA TULIOBAKIWA NAO SI MWINGI.

UTAKASO NI SEHEMU YA MAISHA YA MKRISTO YA KILA SIKU.

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

Rudi nyumbani

Print this post

UTENDAJI KAZI MWINGINE WA ROHO MTAKATIFU USIOUFAHAMU.

Ulishawahi kujiuliza ni kwanini Roho Mtakatifu alicheleweshwa kushuka juu ya mitume ikawachukua muda mrefu  kidogo, Na hata baada ya Yesu kufufuka tunaona iliwapasa tena kungojea kwa muda wa siku 50? Ulishawahi kujiuliza ni kwanini? Sio kwamba walikuwa hawastahili kupokea Roho Mtakatifu tangu zamani, hapana lakini ndio tabia ya Roho Mtakatifu aliyojiwekea, na anafanya hivyo kwasababu zake maalumu.

Hawi mwepesi sana kushuka juu ya mtu kwa haraka kwasababu anajua akishashuka huwa hashuki kwa kipimo au nusunusu, au kuchunguza chunguza. Na ndio maana Bwana Yesu alisubiri kwanza, wanafunzi wake wakamilishwe katika madarasa yake, ili kusudi kwamba watakaposhukiwa na Roho kile kilicho ndani yao kitendeke kwa ufasaha ziadi kama kilivyokusudiwa.

Roho Mtakatifu anafananishwa na MVUA,  Na kama tunavyojua mvua sikuzote ikishuka huwa haichagui hapa kuna ngano au magugu, au mboga, au bangi, au mbigili kazi yake ni kwenda kustawisha tu, hiyo ndio kazi yake. Hivyo ni wajibu wa mwenye shamba kuhakikisha kitu alichokipanda shambani kwake ni chenye manufaa, ahakikishe shamba lake amelipalilia vya kutosha, kwamba hakuna mbegu za magugu chini ya ardhi,vinginevyo itakuwa ni kwa hasara yake mwenyewe pale mvua itakaponyesha na kustawisha magugu badala ya chakula.

Na ndivyo Roho Mtakatifu alivyo, anaposhuka juu ya mtu au kanisa, huwa anakuza au kukiwezesha kile ambacho kimeshapandwa ndani yake. Na ndio maana anaitwa msaidizi, Sasa Kama ulitubu dhambi zako, ukawa unaishi maisha matakatifu, ukawa unabidii katika kumtafuta Mungu, basi Roho akija juu yako, anaikuza hiyo mbegu iliyopo ndani yako, kuwezesha kumjua Mungu zaidi na kuishi hayo maisha kwa viwango vingine vya juu sana.

Na ndio hapo atakuongezea vipawa na karama ili kuhakikisha unafikia pale ambapo umepakusudia na Mungu ufike na hata zaidi. Lakini pale atakaposhuka juu yako, na bado haujajiweka tayari kwa Mungu, kinyume chake, ni mzinzi, au unayo mambo yako ya kidunia, na bado unasema ni  mkristo, atakuja kweli na akija hatakufanya uwe mtakatifu bali atakufanya uwe mwovu zaidi. Hapo ndipo wengi wetu hatujui. Tendo hili katika biblia sehemu nyingine imeitwa “nguvu ya upotevu” itokayo kwa Mungu.. Soma 2Wathesalonike 2:10-12

Utajiuliza ni wapi tena jambo  hilo tena italipata katika biblia,  Embu vitafakari  hivi vifungu, hususani hivyo vilivyo katika herufi kubwa.

Waebrania 6.4 “Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,

5 na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,

6 wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.

7 MAANA NCHI INAYOINYWA MVUA INAYOINYESHEA MARA KWA MARA, NA KUZAA MBOGA ZENYE MANUFAA KWA HAO AMBAO KWA AJILI YAO YALIMWA, HUSHIRIKI BARAKA ZITOKAZO KWA MUNGU;

8 BALI IKITOA MIIBA NA MAGUGU HUKATALIWA NA KUWA KARIBU NA LAANA; AMBAYO MWISHO WAKE NI KUTEKETEZWA”.

Embu jiulize upo katika kanisa muda mrefu, unasema umeokoka, unasali, unafanya ushirika, unaimba kwaya n.k. lakini bado una maisha ya dhambi ya siri siri unayoyajua wewe.. Unatazamia nini pale Roho Mtakatifu atakaposhuka juu yako au juu ya kanisa, upaliliwe kitu gani?

Roho Mtakatifu anaposhuka ndani ya kanisa lake kulinyeshea mvua, halafu anakukuta, wewe ni gugu umepandwa ndani yake, ujue kuwa mvua hiyo itaistawisha gugu, lizidi kustawi zaidi ili siku ya kuteketezwa na kutupwa motoni likapate adhabu iliyokubwa zaidi. Ili kutimiza andiko hili;

Mathayo 13:24 “Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;

25 lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.

26 Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.

27 Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu?

28 Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, Basi, wataka twende tukayakusanye?

29 Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo.

30 Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu”.

Kumbuka kilichomfanya mfalme Sauli ashukiwe na Roho mbaya kutoka kwa Mungu, ni tabia yake ya wivu na ile ya kudharau maagizo ya Mungu, hivyo ile Roho njema ya Mungu iliposhuka juu yake na kukutana na tabia yake mbaya, ndio ikamfanya awe mbaya, kutaka kumwangamiza Daudi. Lakini kama angekuwa ni mtiifu kwa Mungu na mwenye upendo, Roho ya Mungu ingekutana na tabia hiyo njema na kumfanya kuwa mfalme Hodari zaidi na mshupavu kama alivyokuwa hapo mwanzoni. Hiyo ndio sababu kwanini biblia ilikuwa inasema “Roho mbaya kutoka kwa Mungu” ilikuwa inamjia Sauli..Hizi ndio sababu.(1Samweli 16:14-23)

Hata sasa, tunapaswa tujiangalie sana mienendo yetu katika kanisa, wapo watu baada ya kukaa kanisani   ndio wamezidi kuwa wabaya zaidi, wanafanya mambo ambayo hata watu wa kidunia hawafanyi, kama ulikuwa huji sababu ndio hii. Sasa usidhani mtu kama huyo alianza tu kuwa mbaya, hapana, bali alidharau maagizo ya Mungu, akawa anafanya mambo yasiyofaa kidogo kidogo hivyo hivyo, na mwisho wa siku akajikuta anayafanya kwa nguvu zaidi,..Hajui kuwa tayari kashapotea milele, Na biblia inasema mtu akishafikia hatua hiyo, hawezi kufanywa upya tena atubu, anasubiria kwenda tu katika ziwa la moto. Kwahiyo tujitathimini ni mbegu za aina gani zipo ndani yetu. Ili tuwe na amani pale Roho anaposhuka juu yetu, kutuwezesha zaidi.

Tukipanda mbegu njema katika utakatifu, Roho Mtakatifu atatufanya kuwa watakatifu zaidi, tukipanda katika imani,atatuongezea imani zaidi, tukipanda katika upendo vivyo hivyo, katika kulitafakari Neno lake, atatuongezea mafunuo mengi zaidi n.k. Huo ndio uzuri wa Roho Mtakatifu, ndio maana anaitwa msaidizi.

Yohana 16:13 Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.

Hivyo katika hili eneo tunapaswa tuwe makini sana, hata Bwana Yesu alituonya hivyo. Ni heri ukafanya mizaha katika mambo ya kidunia, lakini sio ndani ya kanisa la Kristo. Kwasababu huko ndani Roho Mtakatifu yupo kuwezesha watu, kwahiyo angalie zisije zikawa ndio dhambi zako zinawezeshwa huko.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

NI KWA NAMNA GANI ROHO HUTUTAMANI KIASI CHA KUONA WIVU?

Mungu anaposema “nitaliweka jina langu” ana maana gani?

MTEGO HUTEGWA BURE, MBELE YA MACHO YA NDEGE YE YOTE.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini tofauti kati ya Roho Mtakatifu na Roho Takatifu?

JIBU: Roho Mtakatifu na Roho Takatifu ni kitu kimoja, inategemea neno hilo limetumika wapi

Roho wa Mungu anapozungumza ndani yetu, au kutuongoza, au kutufundisha..anakuwa kama ni mtu yupo ndani yetu akifanya hizo kazi..anakuwa kama ni mtu mwingine mpole ndani yetu anazungumza nasi, anatufundisha, anatushauri, anatufariji, anatutia moyo, anatuongoza n.k..Hivyo hiyo tabia ya kuwa kama mtu wa pili ndani yetu, ndiyo inayofanya biblia sehemu zote iitaje Roho ya Mungu, kwa cheo cha uutu. (yaani Roho M-takatifu).

Hali kadhalika, linapokuja suala la tabia ya Roho ya Mungu, ni sahihi kabisa kusema Roho ya Mungu ni Roho Takatifu, ni Roho Nyenyekevu, ni Roho Tulivu, Ni roho Njema (Danieli 5:12) n.k Hapo hatujaivisha uutu lakini tumeielezea sifa yake.

Yapo madhehebu yanayofanya mambo haya yawe magumu kwa maneno hayo mawili, na hata mengine yamebadilisha biblia zao, kila mahali palipoandikwa kwenye biblia neno Roho Mtakatifu, yamebadilisha na kuweka Roho Takatifu..Hivyo kwao ni kosa kutumia neno Roho Mtakatifu mahali popote. Vile vile yapo mengine ni kosa kutumia neno Roho Takatifu. Pasipo kujua kwamba maneno yote mawili ni sahihi, inategemea ni wapi yametumika.

Kumbuka pia ni wajibu wa kila mmoja aliyeokoka kuwa na Roho Mtakatifu.

Mungu atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JE WAJUA?

MAKEDONIA.

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

Yuko azuiaye sasa hata atakapoondolewa! ni nani huyo?

JE VIBWENGO NI KWELI VIPO?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nitaitofautishaje sauti ya Malaika na ya Roho Mtakatifu?

JIBU: Mungu anaweza kuzungumza na mtu moja kwa moja, au akatumia malaika wake kumpa mtu ujumbe au akamtumia mwanadamu…na mara chache sana anaweza kutumia hata wanyama (Hesabu 22:30). Au vitu vya asili (Ayubu 12:7-9).

Sasa wanadamu na wanyama ni viumbe wa mwilini, Mungu hawezi kuzitumia roho zao kuzungumza na sisi…kwamfano Mungu hawezi kutumia roho yangu au ya mtu fulani kuzungumza na roho ya mtu mwingine…akitaka kuzungumza na mtu, atampa ujumbe katika roho, mtumishi wake, kisha huyo mtumishi atautoa huo ujumbe kwa mhusika. Ni Roho Mtakatifu pekee na Malaika watakatifu ndio wenye huo uwezo wa kuzungumza na sisi kwa njia hiyo ya rohoni kwasababu wao ni wa rohoni..

Malaika anaweza kuonekana kama mtu na kumpa mtu ujumbe na vile vile anaweza kuzungumza na mtu moja kwa moja kwenye roho yake bila kutumtokea wala kuonekana.

Jambo la muhimu la kufahamu ni kwamba…Malaika wa Mungu hawazungumzi kitu kama watakavyo wao…kila wanachokisema au kila ujumbe wanaotupa ni ujumbe kutoka kwa Roho Mtakatifu kama ulivyo (haujaongezwa wala kupunguzwa). Kwahiyo sauti zao ni sauti za Roho Mtakatifu mwenyewe…Ikiwa na maana kuwa Malaika anapozungumza na wewe rohoni, ujue kuwa ni Roho Mtakatifu anazungumza na wewe, kwasababu Malaika anazungumza kitu alichoambiwa na Roho Mtakatifu akiseme vile vile.

Kwamfano hebu tusome mistari michache ifuatayo..

Mwanzo 22:10 “Ibrahimu akanyosha mkono wake, akakitwaa kisu ili amchinje mwanawe.

11 Ndipo MALAIKA WA BWANA AKAMWITA KUTOKA MBINGUNI, AKASEMA, IBRAHIMU! IBRAHIMU! NAYE AKASEMA, MIMI HAPA.

12 Akasema, Usimnyoshee kijana mkono wako, wala usimtendee neno; kwa maana sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee.

13 Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama, kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.

14 Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-yire,kama watu wasemavyo hata leo,Katika mlima wa BWANA itapatikana.

15 MALAIKA WA BWANA AKAMWITA IBRAHIMU MARA YA PILI KUTOKA MBINGUNI

16 akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema Bwana, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,

17 katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao”

Umeona katika tukio hilo…hapo ni Malaika wa Bwana anazungumza na Ibrahimu kama Mungu mwenyewe…kiasi kwamba ni ngumu kujua kama huyo ni Malaika au Mungu anayezungumza hapo..

Tusome tena..

Kutoka 3:1 “Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu.

2 MALAIKA WA BWANA AKAMTOKEA, KATIKA MWALI WA MOTO uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea. 3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei

4 Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa.

5 Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu.

6 TENA AKASEMA, MIMI NI MUNGU WA BABA YAKO, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu”.

Wengi wetu tunaijua hii habari ya Musa kuona kijiti kilichokuwa kinaungua lakini hakiteketei, na wengi wetu tunajua kwamba ni Mungu ndiye aliyemtokea Musa…lakini kiuhalisia sio Mungu aliyemtokea Musa…Bali ni Malaika wa Mungu ambaye alibeba maneno ya Mungu kama yalivyo, ndiye aliyemtokea Musa katika kile kijiti kilichokuwa kinawaka lakini hakiteketeiSiku zote Malaika anapotoa ujumbe ni kama tu msemaji wa Raisi anayesoma waraka wa Raisi mbele ya watu..atasoma mpaka sahihi ya mwisho iliyoandikwa (mimi Raisi nimesema haya yote yaafanyike)!…

Tusome tena..

Waamuzi 2:1 “Kisha malaika wa Bwana alikwea juu kutoka Gilgali kwenda Bokimu. Akasema, Mimi nimewaleta ninyi mkwee juu kutoka nchi ya Misri, nami nimewaleta hata nchi niliyowaapia baba zenu; nami nilisema, Mimi milele sitalivunja hilo agano langu nililoagana nanyi”.

Umeona na hapo? Malaika anasema “Mimi nimewatoa Misri na kuwaleta katika nchi niliyowaapia baba zenu,…milele sitalivunja hilo agano langu nililoagana nanyi”. Ukitafakari hakuna mahali popote Malaika alishaingia agano na wana wa Israeli, ni Mungu ndiye aliyeingia agano na wana wa Israeli..Kwahiyo hapa ni Malaika anazungumza ujumbe wa Mungu, ni kama vile anarudia kuzungumza kile kitu Mungu alichomwambia azungumze..(Ni kama vile anasoma waraka).

Malaika mara nyingi hawana hichi kitu cha “Mungu kasema”…wenyewe wanarudia kuzungumza kile Mungu alichokisema…Hivyo hiyo inafanya kuwa ngumu sana kuitofautisha sauti ya Roho Mtakatifu na ya malaika…Kwani Malaika atakapozungumza nawe katika roho yako hatasema…Mungu kasema fanya hivi au vile….utasikia tu sauti inasema “Mimi Bwana nimesema”..na wewe unaweza kudhani ni Bwana kazungumza nawe kumbe ni Malaika wake.

Sasa kilicho cha muhimu sio kutafuta kujua kuzitofautisha hizi sauti kwasababu haisaidii chochote…kilicho cha muhimu ni kujifunza kutii kile unachoambiwa…iwe ni Roho Matakatifu kazungumza kupitia kinywa cha malaika au kazungumza yeye mwenyewe moja kwa moja…kilicho cha muhimu na maana kwetu ni kukitii kile tulichokisikia maadamu tumehikiki ni Ujumbe kutoka kwa Mungu…

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Je! kuchora tattoo ni dhambi?

KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.

WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.

USIPUNGUZE MAOMBI.

SHETANI ANAITHAMINI HATA MAITI YAKO.

IKIMBIE DHAMBI KWA GHARAMA ZOZOTE ZILE!

KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Leo tutaona kimaandiko ni jinsi gani Roho wa Mungu anavyowasaidia watu kuyaelewa maandiko. Watu wengi, wanaposoma biblia na kuona kama ni ngumu haieleweki hususani vile vitabu vya manabii, kama vile Danieli, Isaya, Ezekieli, Yeremia, Zekaria, Ufunuo na vinginevyo, basi wanakata tamaa kabisa ya kuvimaliza, wanaona ni afadhali tu waache, au wanaona pengine hawastahili kufahamu habari zile kwasasa ni za watumishi Fulani tu, au viongozi Fulani wa dini waliokomaa ndio wanaouwezo wa kuelewa.

Lakini nataka nikuambie kutolielewa Neno la Mungu, sio ujinga, bali Mungu mwenyewe ndio karuhusu sehemu nyingine kulifunga kwa makusudi maalumu ili awafunulie wale waliotayari kujifunza (Danieli 12:4, Mathayo 13:11-14). Hivyo leo tutaangazia mfano mmoja wa kwenye biblia ili na wewe kwa kupitia habari hii, upate motisha ya kupenda kujifunza Neno la Mungu peke yako ukiongozwa na Roho Mtakatifu mwenyewe.

Sasa tukisoma kile kitabu cha Matendo ya Mitume tunaona habari ya mtu mmoja aliyetoka Kushi kwenda kuhiji Yerusalemu, Mtu huyu hakuwa myahudi, wala hakuwa chini ya viongozi wa kidini wa kiyahudi kama Gamalieli na wenzake, bali alikuwa ni kiongozi tu mkuu wa nchi hiyo ya Kushi (ambayo kwasasa ni nchi ya Ethiopia), lakini mtu huyu alimpenda Mungu wa Israeli, na hiyo ikawa inamfanya kila wakati wa sikukuu za kiyahudi na yeye awe anapanda Yerusalemu kuungana na wayahudi wengine kumwabudu Yehova.

Lakini pia alikuwa ni mtu aliyependa kujifunza maandiko. Tunasoma alipokuwa anarudi kutoka Yerusalemu akiwa kwenye gari lake, safarini kurejea nyumbani, biblia inatuambia mule ndani ya gari lake alikuwa akisoma vitabu vya manabii vya agano la kale..Kitabu cha Isaya sura ile ya 53, Mtu huyu alikuwa hayaelewi haya maandiko hata kidogo, pengine alikuwa anayasoma kwa kuyarudia tena na tena,labda pengine atapata tafsiri yake, au ufunuo..akifikiria habari ile ilikuwa inamzungumzia nani, anawaza moyoni mwake, mistari ile inamaanisha nini,..

Sasa kwa kitendo tu kama kile cha kutia nia kutaka kujua maana ya maneno yale..Hapo hapo Roho Mtakatifu akaanza kufanya kazi, akaanza kumwandalia mwalimu wa kumfundisha tokea mbali sana na yeye alipokuwepo.. Roho Mtakatifu akamtafutia mtu, akampata Filipo.. Filipo akiwa huko Samaria akihubiri na kubatiza watu, Roho Mtakatifu akamkatisha kazi yake, na kumwambia anza safari kuelekea mahali pasipo kuwa na watu, Kusini Njia ya jangwa la Gaza, Wakati anaondoka pengine Filipo anawaza kichwani kwake mbona Mungu anafanya niache maelfu ya watu huku Samaria na kuniambia niende huku mahali pasipokuwa na watu..Lakini yeye alitii kwasababu alijua Mungu anamakusudio yake, pengine alidhani huko anapokwenda atakutana na watu wengi zaidi ya wale aliowaacha Samaria,..Akasafiri kupita jangwa lile mpaka akafika mahali akaliona gari Fulani kwa mbali njiani, Roho Mtakatifu akamwambia lisogelee karibu kabisa..Na yeye akalisogelea, alipolisogelea akamwona mtu ndani yake yupo bize akisoma kwa sauti kitabu cha Isaya sura ile ya 53…

Ndipo kuanzia hapo Filipo akaanza kuzungumza naye tusome..

Matendo 8:26 “Malaika wa Bwana akasema na Filipo, akamwambia, Ondoka ukaende upande wa kusini hata njia ile itelemkayo kutoka Yerusalemu kwenda Gaza; nayo ni jangwa.

27 Naye akaondoka, akaenda; mara akamwona mtu wa Kushi, towashi, mwenye mamlaka chini ya Kandake malkia wa Kushi, aliyewekwa juu ya hazina yake yote; naye alikuwa amekwenda Yerusalemu kuabudu,

28 akawa akirejea, ameketi garini mwake akisoma chuo cha nabii Isaya.

29 Roho akamwambia Filipo, Sogea karibu na gari hili, ukashikamane nalo.

30 Basi Filipo akaenda mbio, akamsikia anasoma chuo cha nabii Isaya; akanena, Je! Yamekuelea haya unayosoma?

31 Akasema, Nitawezaje kuelewa, mtu asiponiongoza? Akamsihi Filipo apande na kuketi pamoja naye.

32 Na fungu la Maandiko alilokuwa akilisoma ni hili, Aliongozwa kwenda machinjoni kama kondoo, Na kama vile mwana-kondoo alivyo kimya mbele yake amkataye manyoya, Vivyo hivyo yeye naye hafunui kinywa chake.

33 Katika kujidhili kwake hukumu yake iliondolewa. Ni nani atakayeeleza kizazi chake? Kwa maana uzima wake umeondolewa katika nchi.

34 Yule towashi akamjibu Filipo, akasema, Nakuomba, nabii huyu; asema maneno haya kwa habari ya nani; ni habari zake mwenyewe au za mtu mwingine?

35 Filipo akafunua kinywa chake, naye, akianza kwa andiko lilo hilo, akamhubiri habari njema za Yesu.

36 Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe?

37 Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]

38 Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.

39 Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.

Unaweza kuona hapo, Mkushi Yule sio tu aliishia kuyaelewa maandiko yale bali maandiko yale bali pia yalimpelekea kupata mpaka na ubatizo. Lakini hiyo yote ni kwasababu alitia nia moyoni mwake ya kutaka kuyatafakari maandiko kufahamu maana ya yale yaliyoandikwa. Na ndipo akafunuliwa mambo ambayo, hata kuhani mkuu kule Yerusalemu alikuwa hayajui, viongozi wote wa dini na waandishi wanayasoma kila siku lakini hawayaelewi..anakuja kufunuliwa mkushi ambaye hana ujuzi wowote na torati.

Vivyo hivyo na wewe na mimi, Kama umeokoka na unaye Roho Mtakatifu ndani yako, sio wakati wa wewe kukaa kungojea fundisho Fulani uletewe na mhubiri Fulani, au mchungaji Fulani tu peke yake,..Anza kwa kujijengea utaratibu wa wewe mwenyewe kuyatafakari maandiko binafsi kwa bidii na kumwomba Mungu akufunulie, ndipo hapo Mungu atakapotumia njia zake yeye mwenyewe alizozipanga kukufunulia, aidha kwa ufunuo au kwa muhubiri, hapo ndipo utakapopata uhakika kuwa Roho Mtakatifu amesema na wewe.. Wapo wengine wanasema nilikuwa ninautafakari sana mstari Fulani jana usiku, lakini sikuelewa, ghafla kesho yake nikasikia mhubiri Fulani anauhubiri mstari ule ule au nikakutana na mafundisho yale yale,.Hiyo ni ishara kuwa Mungu amemfunulia maana ya mstari ule. Sasa zipo njia nyingine nyingi ambazo Mungu anaweza kumfunulia mtu ikiwa tu atataka yeye mwenyewe kufahamu.

Lakini usikae tu bila kujishughulisha, kusubiria tu kufundishwa wakati wote, ujue kuwa yapo mambo ambayo Roho Mtakatifu anataka kukufundisha wewe kama wewe, vile vile anataka kukujengea uwezo wa wewe kuisikia sauti yake. Hivyo kama wewe umeshaokoka anza kuchukua hatua ya kuyatafakari maandiko bila kuogopa hichi ni kitabu cha manabii kisichoeleweka, au sio, suala la kutafsiri sio lako bali ni la Mungu, yeye mwenyewe ndiye atakayekufungulia njia zake za kuliewa.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312

Mada Nyinginezo:

SEHEMU YA MAANDIKO ILIYOFICHWA.

KITABU CHA UZIMA

WAKAMTUKANA MUNGU, WALA HAWAKUTUBU.

Nifanye nini ili niondokane na Hofu maishani mwangu?

Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?

 

KUOTA UNAKULA CHAKULA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Roho Mtakatifu ni nani?.

Watu wengi wanajiuliza Roho Mtakatifu ni nani? Jibu  rahisi ni kuwa Roho Mtakatifu ni Roho ya Mungu, Mungu anayo Roho kama vile mwanadamu alivyo na roho, hakuna mwanadamu yeyote asiye na roho.

Na Biblia inasema katika Mwanzo 1:26 kwamba Mwanadamu aliumbwa kwa mfano na sura ya Mungu. Ikiwa na maana kuwa kama mwanadamu ana nafsi halikadhalika Mungu naye anayo nafsi, na kama mwanadamu anayo roho vilevile na Mungu naye anayo Roho. Kwasababu tumeumbwa kwa sura yake na kwa mfano wake. Na kama vile mwanadamu anao mwili halikadhalika Mungu naye anao mwili.

Na Mwili wa Mungu si mwingine zaidi ya ule uliodhihirishwa pale Kalvari miaka 2000 iliyopita. Nao ni mwili wa Bwana Yesu Kristo, hivyo Yesu Kristo ndiye Mungu mwenyewe aliyedhihirishwa katika Mwili. Hivyo aliyemwona Yesu amemwona Mungu (Yohana 14:8-10)

1Timotheo 3:16 “Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu”.

Huyo ni Yesu anayezungumziwa hapo.

Na kadhalika roho iliyokuwepo ndani ya Mwili wa Bwana Yesu Kristo ndio Roho ya Mungu na ndiye ROHO MTAKATIFU MWENYEWE. Tunalithibitisha hilo katika kitabu cha.

Matendo 16:6 “Wakapita katika nchi ya Frigia na Galatia, wakikatazwa na Roho Mtakatifu, wasilihubiri lile neno katika Asia.

7 Walipofika kukabili Misia wakajaribu kuenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu hakuwapa ruhusa,

8 wakapita Misia wakatelemkia Troa”.

Sasa utauliza kama Roho wa Yesu ndiye Roho Mtakatifu iweje mahali pengine Bwana Yesu anaonekana amejaa Roho Mtakatifu?. Na mahali pengine anaonekana Roho Mtakatifu akishuka juu yake?

Jibu ni kwamba, Roho wa Mungu hana mipaka kama roho zetu sisi wanadamu zilivyo na mipaka, sisi wanadamu Mungu alivyotuumba roho zetu mipaka yake ni katika miili yetu.

Haziwezi kutenda kazi nje ya fahamu zetu au miili yetu.Haiwezekani niongee na wewe hapa na wakati huo huo roho yangu ipo China. Hilo haliwezekani kwetu sisi wanadamu, isipokuwa kwa Mungu linawezekana. Roho wake anauwezo wa kuwa kila mahali, ndio maana wewe uliopo Tanzania utasali muda huu na mwingine aliyepo China atasali na mwingine aliyeko Amerika atakuwa anamwabudu Mungu muda huo huo na wote Roho Mtakatifu akawasikia na kuwahudumia kila mtu kivyake. Huyo huyo anao uwezo wa kuwepo mbinguni, na duniani ndani ya Mwili wa Bwana Yesu na wakati huo huo kuzimu, hakuna mahali asipofika.

Ndio maana utaona alikuwa ndani ya Kristo, na bado akashuka juu ya Kristo, na akaachiliwa juu yetu siku ile ya Pentekoste.

Hiyo ndiyo tofauti ya Roho wa Mungu na roho ya mwanadamu. Roho zetu zina mipaka lakini Roho wa Yesu hana mipaka.

Na ni kwanini Roho wa Yesu anajulikana kama Roho Mtakatifu?

Ni kwasababu yeye ni Roho Takatifu, hiyo ndio sifa kubwa na ya kipekee Roho wa Yesu aliyoibeba..Yeye ni mtakatifu na hachangamani na uchafu.

Na ndio maana uthibitisho wa Kwanza kabisa wa Mtu aliyempokea Roho Mtakatifu ni kuwa Mtakatifu. Umepokea uwezo wa kufanyika mwana wa Mungu, unakuwa kama YESU. Naamini mpaka hapo utakuwa umeshafahamu Roho Mtakatifu ni nani?

Je! Umepokea moyoni mwako? kama bado ni kwanini? Biblia imesema ahadi hiyo ni ya bure na tunapewa bila malipo, kwa yeyote atakayemwamini.

Matendo 2:39 “Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”.

Gharama za kumpata huyo Roho si fedha bali ni Uamuzi tu! Ukimtafuta Mungu kwa bidii utampata Neno lake linasema hivyo..

Hivyo kanuni rahisi sana ya kumpata ni KUTUBU kwanza: Yaani unamaanisha kuacha dhambi kwa vitendo, kisha kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji tele (Yohana 3:23) na kwa jina la Yesu kwaajili ya ondoleo la dhambi kulingana na Matendo 2:38 ili kuukamilisha wokovu wako. Na Roho Mtakatifu ataingia ndani yako, atakayekupa uwezo wa kuwa kama yeye alivyo yaani Mtakatifu. Vilevile atakushushia na karama zake za Roho kwa jinsi apendavyo yeye juu yako. Hapo ndipo utakapopokea uwezo wa kuwa shahidi wake

Kumbuka biblia inasema wote wasio na Roho Mtakatifu hao sio wake (Soma Warumi 8:9), Hivyo ni wajibu wetu sote kumtafuta Roho Mtakatifu kwa bidii sana. Kwasababu hutaweza kumjua Mungu, wala kupokea uwezo wa kuishinda dhambi kama huna Roho Mtakatifu ndani yako.

Bwana akubariki.

Maran Atha !jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?

JE UNATAMANI KUMJUA MUNGU, NA HUJUI PA KUANZIA?

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

ROHO HUTUOMBEA KWA KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA!

KAMA MUNGU ANABORESHA KAZI ZAKE, KWANINI WEWE USIBORESHE ZA KWAKO?.

Rudi Nyumbani:

Print this post