Nitaitofautishaje sauti ya Malaika na ya Roho Mtakatifu?

by Admin | 25 June 2020 08:46 pm06

JIBU: Mungu anaweza kuzungumza na mtu moja kwa moja, au akatumia malaika wake kumpa mtu ujumbe au akamtumia mwanadamu…na mara chache sana anaweza kutumia hata wanyama (Hesabu 22:30). Au vitu vya asili (Ayubu 12:7-9).

Sasa wanadamu na wanyama ni viumbe wa mwilini, Mungu hawezi kuzitumia roho zao kuzungumza na sisi…kwamfano Mungu hawezi kutumia roho yangu au ya mtu fulani kuzungumza na roho ya mtu mwingine…akitaka kuzungumza na mtu, atampa ujumbe katika roho, mtumishi wake, kisha huyo mtumishi atautoa huo ujumbe kwa mhusika. Ni Roho Mtakatifu pekee na Malaika watakatifu ndio wenye huo uwezo wa kuzungumza na sisi kwa njia hiyo ya rohoni kwasababu wao ni wa rohoni..

Malaika anaweza kuonekana kama mtu na kumpa mtu ujumbe na vile vile anaweza kuzungumza na mtu moja kwa moja kwenye roho yake bila kutumtokea wala kuonekana.

Jambo la muhimu la kufahamu ni kwamba…Malaika wa Mungu hawazungumzi kitu kama watakavyo wao…kila wanachokisema au kila ujumbe wanaotupa ni ujumbe kutoka kwa Roho Mtakatifu kama ulivyo (haujaongezwa wala kupunguzwa). Kwahiyo sauti zao ni sauti za Roho Mtakatifu mwenyewe…Ikiwa na maana kuwa Malaika anapozungumza na wewe rohoni, ujue kuwa ni Roho Mtakatifu anazungumza na wewe, kwasababu Malaika anazungumza kitu alichoambiwa na Roho Mtakatifu akiseme vile vile.

Kwamfano hebu tusome mistari michache ifuatayo..

Mwanzo 22:10 “Ibrahimu akanyosha mkono wake, akakitwaa kisu ili amchinje mwanawe.

11 Ndipo MALAIKA WA BWANA AKAMWITA KUTOKA MBINGUNI, AKASEMA, IBRAHIMU! IBRAHIMU! NAYE AKASEMA, MIMI HAPA.

12 Akasema, Usimnyoshee kijana mkono wako, wala usimtendee neno; kwa maana sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee.

13 Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama, kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.

14 Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-yire,kama watu wasemavyo hata leo,Katika mlima wa BWANA itapatikana.

15 MALAIKA WA BWANA AKAMWITA IBRAHIMU MARA YA PILI KUTOKA MBINGUNI

16 akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema Bwana, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,

17 katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao”

Umeona katika tukio hilo…hapo ni Malaika wa Bwana anazungumza na Ibrahimu kama Mungu mwenyewe…kiasi kwamba ni ngumu kujua kama huyo ni Malaika au Mungu anayezungumza hapo..

Tusome tena..

Kutoka 3:1 “Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu.

2 MALAIKA WA BWANA AKAMTOKEA, KATIKA MWALI WA MOTO uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea. 3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei

4 Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa.

5 Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu.

6 TENA AKASEMA, MIMI NI MUNGU WA BABA YAKO, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu”.

Wengi wetu tunaijua hii habari ya Musa kuona kijiti kilichokuwa kinaungua lakini hakiteketei, na wengi wetu tunajua kwamba ni Mungu ndiye aliyemtokea Musa…lakini kiuhalisia sio Mungu aliyemtokea Musa…Bali ni Malaika wa Mungu ambaye alibeba maneno ya Mungu kama yalivyo, ndiye aliyemtokea Musa katika kile kijiti kilichokuwa kinawaka lakini hakiteketeiSiku zote Malaika anapotoa ujumbe ni kama tu msemaji wa Raisi anayesoma waraka wa Raisi mbele ya watu..atasoma mpaka sahihi ya mwisho iliyoandikwa (mimi Raisi nimesema haya yote yaafanyike)!…

Tusome tena..

Waamuzi 2:1 “Kisha malaika wa Bwana alikwea juu kutoka Gilgali kwenda Bokimu. Akasema, Mimi nimewaleta ninyi mkwee juu kutoka nchi ya Misri, nami nimewaleta hata nchi niliyowaapia baba zenu; nami nilisema, Mimi milele sitalivunja hilo agano langu nililoagana nanyi”.

Umeona na hapo? Malaika anasema “Mimi nimewatoa Misri na kuwaleta katika nchi niliyowaapia baba zenu,…milele sitalivunja hilo agano langu nililoagana nanyi”. Ukitafakari hakuna mahali popote Malaika alishaingia agano na wana wa Israeli, ni Mungu ndiye aliyeingia agano na wana wa Israeli..Kwahiyo hapa ni Malaika anazungumza ujumbe wa Mungu, ni kama vile anarudia kuzungumza kile kitu Mungu alichomwambia azungumze..(Ni kama vile anasoma waraka).

Malaika mara nyingi hawana hichi kitu cha “Mungu kasema”…wenyewe wanarudia kuzungumza kile Mungu alichokisema…Hivyo hiyo inafanya kuwa ngumu sana kuitofautisha sauti ya Roho Mtakatifu na ya malaika…Kwani Malaika atakapozungumza nawe katika roho yako hatasema…Mungu kasema fanya hivi au vile….utasikia tu sauti inasema “Mimi Bwana nimesema”..na wewe unaweza kudhani ni Bwana kazungumza nawe kumbe ni Malaika wake.

Sasa kilicho cha muhimu sio kutafuta kujua kuzitofautisha hizi sauti kwasababu haisaidii chochote…kilicho cha muhimu ni kujifunza kutii kile unachoambiwa…iwe ni Roho Matakatifu kazungumza kupitia kinywa cha malaika au kazungumza yeye mwenyewe moja kwa moja…kilicho cha muhimu na maana kwetu ni kukitii kile tulichokisikia maadamu tumehikiki ni Ujumbe kutoka kwa Mungu…

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Je! kuchora tattoo ni dhambi?

KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.

WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.

USIPUNGUZE MAOMBI.

SHETANI ANAITHAMINI HATA MAITI YAKO.

IKIMBIE DHAMBI KWA GHARAMA ZOZOTE ZILE!

KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/06/25/nitaitofautishaje-sauti-ya-malaika-na-ya-roho-mtakatifu/