Category Archive Roho Mtakatifu

TUNAMHITAJI SANA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUYAELEWA MAANDIKO.

Katika biblia nzima hakuna mahali utaona pametabiriwa kwa wazi kuwa Kristo atakaa kaburini siku tatu, na baada ya siku ya tatu atafufuka. Hakuna mahali popote kwenye Biblia palipoandikwa ufunuo huo…Tunaona unabii wa Kristo kuzaliwa na Bikira uliandikwa wazi katika Isaya 7:14 kwamba atazaliwa na Bikira, kadhalika unabii wa Kristo kuzaliwa Bethlehemu ya Uyahudi ulitabiriwa wazi katika kitabu cha Mika.

Mika 5: 2 “Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele”…

Kadhalika unabii wa Bwana Yesu kuteswa kwa ajili ya dhambi zetu uliandikwa wazi katika Isaya

Isaya 53:4 “Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.

5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.

Na Nabii nyingine Nyingi zimuhusuzo Yesu ziliandikwa wazi hata za kuja kwake mara ya pili…Lakini katika unabii wa kukaa kaburini siku tatu, huo haukuandikwa wazi..Uliihitaji Ufunuo wa kipekee wa Roho ili kuujua…Kwasababu Yesu mwenyewe alisema ilipaswa yote yatimie yaliyoandikwa na Manabii, Torati na Zaburi. Na pia ulipaswa utimie unabii alioandikiwa yeye kuhusu kukaa kaburini siku tatu.

Luka 24:44 “ Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika TORATI YA MUSA, NA KATIKA MANABII NA ZABURI.

45 Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko.

46 Akawaambia, NDIVYO ILIVYOANDIKWA, KWAMBA KRISTO ATATESWA NA KUFUFUKA SIKU YA TATU;”

Sasa ni wapi palipotabiriwa kuwa Kristo atakaa kaburini siku tatu?

Pasipo ufunuo wa Roho hakuna mtu angejua kuwa Yesu Kristo alitabiriwa hayo, hata Wanafunzi wa Yesu walikuwa hawajui, si Zaidi Mafarisayo..Lakini tunaona Roho Mtakatifu mwenyewe alifichua fumbo hilo na kutuonesha sisi katika maandiko kuwa ni wapi Kristo alitabiriwa kukaa siku tatu kaburini…tunasoma katika..

Mathayo 12:39 “Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona.

40 Kwani kama vile Yona alivyokuwa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la nyangumi, hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku tatu mchana na usiku katika moyo wa nchi”

Unaona? Kumbe Maisha ya Yona yalikuwa ni UFUNUO WA YESU KRISTO kukaa kaburini siku tatu?? Nani alikuwa analijua hilo?? Hata Yona mwenyewe alikuwa halijui.

Sasa kama Maisha ya Yona yalikuwa yamebeba siri nzito namna ile, inayomhusu Yesu….ya Yusufu yatakuaje? Ya Musa yatakuaje?, ya Ayubu na Danieli yatakuwaje?..Tunamhitaji Roho Mtakatifu atufunulie maandiko tuweze kumwelewa. Hakika pasipo yeye hatutaelewa chochote katika maandiko.

Yohana 14:26 “Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia”.

Ukisoma tena katika maandiko utaona Bwana YESU alikuwa yupo tayari kutueleza pia mambo ya mbinguni, lakini kwa kutokuamini kwetu, hakutueleza(Yohana 3:12),.. Lakini Kristo mwenyewe aliahidi kuwa huyo Roho Mtakatifu atakapokuja atayatwaa yaliyo yake na kutupasha sisi habari,(Yohana 16:14).

Umeona umuhimu wa kuwa na Roho Mtakatifu sasa?, Swali ni Je! Umempata?..Na hata kama unaye je! amejaa kwa wingi ndani yako? Bwana atusaidie!

Kama hujampa Yesu Kristo Maisha yako, mlango wa Neema bado upo wazi, lakini hautakuwa hivyo siku zote.Tubu kwa kumaanisha kuacha dhambi kama hujatubu, na zingatia kutafuta ubatizo sahihi, wa kuzama mwili wote majini na kwa jina la Yesu Kristo kulingana na Matendo 2:38. Na yeye mwenyewe atakupa kipawa cha Roho Mtakatifu bure kama alivyoahidi katika Neno lake kwa wale wote waaminio.

Maran atha!

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

UMUHIMU WA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUZAA MATUNDA.

JE! HIZI ROHO SABA ZA MUNGU NI ZIPI? NA JE ZINATOFAUTIANA NA ROHO MTAKATIFU?

DHAMBI YA KUMKUFURU ROHO MTAKATIFU NI IPI?

UKIAMINI NA UKIMKIRI YESU KWA KINYWA CHAKO, UTAOKOKA.

JE! BIKIRA MARIA NI MALKIA WA MBINGUNI?


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

MATUNDA 9 YA ROHO MTAKATIFU

Uthibitisho wa kwanza wa mtu kuwa na Roho Mtakatifu ni Utakatifu atakaouonesha, na Utakatifu kwa ujumla ndio tunda la Roho. Na uthibitisho wa Pili ndio karama aliyo nayo…. Na Mtu Mtakatifu ni lazima aoneshe vitu 9 vifuatavyo..pamoja na vingine vingi, lakini hivi 9 ndio msingi wa UTAKATIFU WA MTU.

  1. UPENDO
  2. FURAHA
  3. AMANI
  4. UVUMILIVU
  5. UTU WEMA
  6. FADHILI
  7. UAMINIFU
  8. UPOLE
  9. KIASI

Tabia hizi 9 zinapatikana kutoka katika kitabu cha Wagalatia..

Wagalatia 5:22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,

23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria. 

Mtu Mwenye Roho Mtakatifu lazima awe navyo hivi vyote kwa pamoja! hapaswi kukosa hata kimoja..kwasababu vyote kwa pamoja ndio vinaitwa TUNDA LA ROHO, na si MATUNDA YA ROHO…Ikiwa na Maana ni lazima viende kwa pamoja.

Ubarikiwe.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

FAIDA ZA MAOMBI.

HATARI YA KUTOKUITAFAKARI BIBLIA VIZURI?

EPUKA KUTOA UDHURU.

JE! NI SAHIHI KUJIPA CHEO MFANO MIGHTY PROPHET, CHIEF APOSTLE N.K?

BIBLIA INAKATAZA KUAPA KABISA, LAKINI KWANINI WATU WANAAPA MAHAKAMA?


Rudi Nyumbani:

Print this post

UMUHIMU WA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUZAA MATUNDA.

Shalom mtu wa Mungu, karibu tutafakari maandiko pamoja.
 
Biblia inasema katika Kitabu cha Yohana 15:16 kwamba “Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda; na matunda yenu yapate kukaa; ili kwamba lo lote mmwombalo Baba kwa jina langu awapeni”
 
Tumepewa jukumu la kuzaa matunda, na matunda hayo yamegawanyika katika sehemu kuu mbili, sehemu ya kwanza ni matunda ya Haki, ambayo hayo yanatokana na utakatifu, tunayasoma hayo katika
Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, 23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria”.
 
Na aina ya pili ya Matunda, ni matunda ya KAZI, ambayo hayo yanatokana na kuwaleta watu kwa Kristo,
 
Wafilipi 1:21 “Kwa maana kwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faida.
 
22 Ila ikiwa kuishi katika mwili, kwangu mimi ni matunda ya kazi; basi nitakalolichagua silitambui.”
 
Hivyo Kristo ametuweka tuzae aina hizi mbili za matunda…Matunda ya HAKI na Matunda ya KAZI..Hivi viwili vinakwenda pamoja…Na vyote vinahitaji Mafuta ya Roho Mtakatifu ili viweze kufanyika. Ili tuwe watakatifu tunahitaji Mafuta ya Roho Mtakatifu…Kwasababu kama jina lake lenyewe lilivyo..Roho Mtakatifu, hivyo kila ampataye yeye ni lazima atakuwa mtakatifu tu.
 
Kadhalika ili tuweze kuleta matunda mengi kwa Kristo tunamhitaji Roho Mtakatifu, kwasababu yeye ndiye anayehusika katika kumshawishi mtu ndani ya moyo wake amgeukie Kristo.. 1 Wakorintho 2:4 “Na neno langu na kuhubiri kwangu hakukuwa kwa maneno ya hekima yenye kushawishi akili za watu, bali kwa dalili za Roho na za nguvu”
Na leo tutajifunza umuhimu wa Roho Mtakatifu katika kuzaa matunda katika hizi siku za mwisho.
Kazi ya kuwavuta watu kwa Kristo imefananishwa na kazi ya uvuvi…Sharti ni kwamba ili mtu akavue samaki ni lazima atimize masharti makuu 5..
 
Sharti la kwanza ni lazima awe na mtumbwi unaoelea, sharti la pili ni lazima awe anajua kuogolea, sharti la tatu ni lazima awe na nyavu au ndoano, sharti la 4 Ni lazima aende usiku na sharti la 5 na la mwisho ni lazima awe na TAA..Akitimiza masharti hayo 5 basi ni lazima apate samaki..hawezi kukosa chochote aendapo anavua baharini…
 
Masharti hayo hayo pia yanatumika katika roho kwa uvuvi wa watu…
 
Sharti la kwanza: Kama vile mvuvi ni lazima awe na mtumbwi unaoelea na ni lazima akae juu ya huo mtumbwi ili aweze kuvua…vivyo hivyo katika Uvuvi wa watu ni lazima mtu awe juu ya Mtumbwi unaoitwa YESU KRISTO, na ni lazima mtu awe juu ya huo mtumbwi sio mbali au nje ya huo mtumbwi…huko nje ni kwa watu wasiomjua Mungu, ulimwengu unafananishwa na bahari ambayo imejaa watu wasiomjua Mungu ambao wanahitajika kuvuliwa..Hivyo haiwezekani mtu aliye nje ya Kristo kuwahubiria watu waje kwa Kristo kama vile ilivyo ngumu mvuvi kuwa nje ya mtumbwi na kuvua samaki.
 
Sharti la pili: Ni lazima mvuvi awe anajua kuogelea kabla hajaenda kuvua samaki…awe na uwezo endapo ikitokea ajali akaanguka ghafla majini awe na uwezo wa kurudi tena mtumbwini…sio endapo Kazama ndio anapotelea huko moja kwa moja…Kadhalika na mvuvi wa Roho za Watu ni lazima awe na uwezo wa kujihadhari na dunia, kwasababu dunia ni kama bahari, ukizama na ukiwa hujui namna ya kujitoa huko unazama moja kwa moja na kufia huko…Kwahiyo Ni kama tunaonywa kamwe tusidhubutu kwenda kuhubiri injili kama tunajua hatujaacha sisi wenyewe mambo ya ulimwengu huu, kama tunajua hatuwezi kuushinda na kujinusuru na ulimwengu…ni afadhali tusiende kuhubiri injili kabisa kuliko kwenda na kuzama huko… kwasababu endapo tukianguka tunakuwa tumeanguka moja kwa moja hakuna kurudi tena..
 
2 Petro 2:20 “Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia machafu ya dunia kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, kama wakinaswa tena na kushindwa, hali yao ya mwisho imekuwa mbaya kuliko ile ya kwanza.
 
21 Maana ingekuwa heri kwao kama wasingaliijua njia ya haki, kuliko kuijua, kisha kuiacha ile amri takatifu waliyopewa”
 
Sharti la Tatu: Ni lazima mvuvi awe na ndoano au nyavu…Ndoano au nyavu zinawakilisha Neno la Mungu, pamoja na ishara na miujiza…Vitu hivi biblia inasema waaminio wote vitaambatana nao…Ni lazima tulifahamu Neno ndipo tuende kuwahubiria wengine…
 
Sharti la Nne: Ni lazima mvuvi aende usiku kuvua, wavuvi wote wanaomaanisha kupata samaki huwa hawaendi mchana kwani wanajua hawatapata kitu, ni lazima aende usiku, kadhalika hata wakati huu wa sasa tunapaswa tuende ulimwenguni kote kulikojaa giza…Matendo ya dhambi yote ni matendo ya giza, na dunia yote imejaa giza kutokana na dhambi za wanadamu…lakini leo Utashangaa mtu anapambania awe mhubiri kanisani kila siku, lakini hataki kwenda mitaani mahali ambapo makahaba wapo, mahali penye giza…tukihubiri kanisani mahali ambapo kuna mwanga ni sawa tunaingia na mshumaa ndani ya nyumba ambayo tayari ina bulb inayowaka sana..Hivyo ni lazima tuenda na mitumbwi yetu, na nyavu zetu sehemu zenye giza mbali sana huko kuvua roho za watu. Na sisi wenyewe tukijihadhari tusipotelee huko.
 
Na Sharti la Tano Na la mwisho: Ni lazima mvuvi aende na TAA..Nyavu peke yake haitoshi kuwaleta samaki, ndoano peke yake haitoshi inahitajika taa…Wataalamu wa masuala ya uvuvi wanasema wakati wa usiku samaki wanapenda kufuata mahali penye mwangaza, hivyo wavuvi wengi hutwaa taa zao juu na kwenda nazo vilindini na hivyo samaki wanapoiona ile Nuru wanaisogelea na hivyo kunaswa…Na sisi tunahitaji Taa yenye Mafuta ili kuwavuta samaki wengi kwenye nyavu zetu, NA Mafuta yanawakilisha Roho Mtakatifu. Hivyo tunahitaji Roho Mtakatifu sana ili Taa zetu ziwe zinawaka sana, katika dunia hii ya giza ili waovu waonapo wamgeukie Bwana.
 
Wafilipi 2:15 “….mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao MNAONEKANA KUWA KAMA MIANGA KATIKA ULIMWENGU”
 
Ukiwa na Mtumbwi, ukiwa na ndoano, ukiwa na nyavu, na ukiwa na ujuzi wote wa kuogelea, kama huna TAA ni kazi bure…utakuwa umwekwenda baharini kubarizi tu na si kuvua..Kadhalika hata tukiwa na tumempa Bwana Maisha yetu, hata tukiwa tunalijua Neno vizuri na kujiepusha na dunia vizuri kama hatuna Roho Mtakatifu, kamwe shughuli ya kuwaleta wengine kwa Kristo itakuwa ngumu sana kwetu.
Hivyo leo tunajifunza tumtafute sana Roho Mtakatifu ajae ndani yetu, kwa maana pasipo yeye hakuna mtu yeyote atakaye vutwa kwa Mungu.
 
Yohana 6: 44 “Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho”.
Bwana akubariki sana. Wahubirie na wengine habari njema, waujue wokovu wa Bwana Yesu.
 
Bwana akubariki.



Mada nyinginezo:

TUTAWEZAJE KUMZALIA MUNGU MATUNDA?

TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.

UMUHIMU WA KUISHI MAISHA YAMPENDEZAYO MUNGU SASA.

MUNGU MWENYE HAKI.

MLINZI, NI HABARI GANI ZA USIKU?

LILE TUMAINI LILILO NDANI YETU LINAPOULIZIWA.

NGUVU YA UPOTEVU.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! hizi roho saba za Mungu ni zipi? na je zinatofautiana na Roho Mtakatifu?

Swali ambalo ni wajibu wetu sote kulijua ni juu ya Roho saba za Mungu, kwamba zenyewe ni nini na zinatendaje kazi. Na pia ni muhimu kufahamu juu ya makanisa saba

JIBU: Tukisoma mandiko yanatuambia kuwa Mungu ni mmoja, agano la kale linatuthibitishia hilo, (Kumb 6:4), vile vile agano jipya linatuthibitishia hilo, tukisoma katika (Marko 12:29) pale Bwana Yesu alipofuatwa na Yule mwandishi na kuulizwa ni amri ipi iliyo ya kwanza alijibu..


“….Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja; 30 nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.”

Hivyo maagano yote mawili yanathitisha kuwa Mungu ni mmoja, lakini sasa kwanini tunamwona YESU kama Mungu, kwanini tunamwona Roho kama Mungu, tena tukiendelea kusoma tunaziona kuna Roho nyingine saba za Mungu, swali ni je! hawa wote wametokea wapi, ikiwa Mungu ni mmoja?.Hili ni moja ya swali lililoleta migawanyiko mikubwa sana sio tu katika ukristo, bali hata kwa wale wasioamini limewafanya wazidi kwenda mbali zaidi kwa kushindwa kuelewa utendaji kazi wa Mungu.

Tukiweza kujua kuwa kitu kinachoitwa Dhambi na kutengwa mbali na uso wa Mungu ndicho chanzo kilichopelekea tumwone Mungu katika taswira nyingi tofauti tofauti, tukilifahamu hilo basi hatutashindwa kumwelewa Mungu katika nafasi yake ya Uungu.. Na ameamua kufanya hivyo makusudi kwa lengo la kuturejesha sisi asingefanya hivyo leo hii tungekuwa makapi sisi. Laiti kama tusingeanguka katika dhambi, tungemwona Mungu na kuzungmza na Mungu kama yeye tu tusingejua kitu kingine cha ziada kumuhusu yeye, tabia zake zilivyo.

Kwamfano kulikuwa hakuna sababu ya Mungu kuutafuta mwili na kuiweka Roho yake mwenyewe ndani yake aje asulibiwe ili atupatanishe sisi na yeye kama tusingepotea katika dhambi, vile vile kulikuwa hakuna haja ya Roho Mtakatifu kuwa msaidizi wetu kama tungekuwa tunazungumza na Mungu uso kwa uso kama ilivyokuwa pale Edeni Adamu alipokuwa anazungumza na Mungu..

Ni sawa tu ni kifaa kinachoitwa simu, kama sio suala la umbali kati ya mtu mmoja na mwingine, simu isingehitajika katika jamii, kusingekuwa na haja ya wewe kuisikia sauti yangu kwenye kifaa kinachoitwa simu..Lakini je! Fikiria pia siku ile uliposikia mimi ninazungumza ndani ya kifaa kile, je ulisema nimegawanyika?, na kuwa wawili, kwamba mimi unayeniona tukizungumza uso kwa uso ni tofauti na Yule unayenisikia kwenye kifaa-simu? Ukweli ni kuwa utasema ni kifaa tu lakini mimi ni Yule Yule..Na ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana Yesu kuja kwake duniani, ..yule ni Mungu yule yule kauvaa mwili lakini sio MUNGU wa pili katika UUNGU, kama wengi wanavyodhani…YESU na Mungu BABA, sio Mtu na Mtu mwenzake, Ni Mungu yule Yule mmoja isipokuwa amekuja kwetu katika vazi lingine.
Kwa maelezo marefu ya kufahamu kwanini Yesu alikuja duniani, tutumie ujumbe inbox tukutumie somo lake..

Vivyo hivyo na Roho wake Mtakatifu, Yule sio Nafsi ya Tatu katika uungu bali ni ofisi ya tatu ya Mungu Yule Yule mmoja katika hatua zake za kuturejesha sisi katika mstari wake wa ukamilifu..Kama tusingekuwa katika hali ya dhambi na kumsahau Mungu, basi hakukuwa na haja ya sisi kupewa msaidizi, lakini Mungu aliona ajitoe sehemu ya nafsi yake iliyo moja aje kwetu kama Roho Mtakatifu ili atukumbushe yale yote Bwana Yesu aliyotuagiza.(Yohana 14:26).

Vile vile Roho Mtakatifu alipoachiwa pale Pentekoste, hakuachiwa kwa mtu mmoja mmoja tu peke yake kama wengi wanavyodhani, bali aliachiwa pia na kwa kanisa kwa ujumla..Hivyo kulikuwa na makanisa tofauti tofauti kulingana na wakati na majira..Sasa Roho huyu huyu aliyetenda pia kazi tofauti tofauti kulingana na kanisa husika..Ndio yale makanisa saba tunayoyasoma katika kitabu cha ufunuo sura ya 2&3, ..


Ufunuo 1:4 Yohana, kwa yale makanisa saba yaliyoko Asia; Neema na iwe kwenu na amani, zitokazo kwake yeye aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja; na zitokazo kwa roho saba walioko mbele ya kiti chake cha enzi;

makanisa saba

Sasa biblia inaposema Roho saba za Mungu nadhani utakuwa umeelewa kuwa hakuna tena Roho nyingine 7 zilizo mbele za Mungu, bali ni Roho Yule Yule mmoja akitenda kazi katika yale makanisa saba, Biblia inasema pia ndio macho 7 ya Mungu (Ufunuo 5:6), Na Taa 7 za moto (Ufunuo 4:5).
Kwa maelezo marefu juu ya nyakati saba za Kanisa,pia tutumie ujumbe inbox tukutumie somo lake..

Hivyo hizo zote ni hatua za Mungu za utendaji kazi lakini ni yeye Yule Yule, Mungu mmoja, hajagawanyika..


Lakini Swali lingine mtu anaweza kuuliza je! Tunafanya makosa kumwabudu YESU au Roho Mtakatifu? Jibu ni hapana, unapomwabudu Bwana YESU umemwabudu Mungu Yule Yule mmoja, Unapomwabudu Roho Umemwabudu Mungu Yule Yule mmoja, ni ofisi tu imebadilika, lakini Mungu ni Yule Yule umwabuduye..

Hivyo YESU ni Mungu mwenyewe katika mwili (1Timotheo 3:16), Roho Mtakatifu ni Mungu mwenyewe katika roho, vile vile zile Roho 7 za Mungu ndio Yule Yule Roho mmoja na ndio Mungu mwenyewe YEHOVA muumba wa mbingu na nchi, Hana mwanzo wala hana mwisho, ALFA NA OMEGA. Haleluya!

Je unampenda kwa moyo wako wote? Jibu unalo.


Ubarikiwe.


Mada zinazoendana:

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?

JINA LA MUNGU NI LIPI?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

ACHENI MJUE YA KUWA MIMI NI MUNGU.

MJUE SANA YESU KRISTO.

MUNGU KUSEMA NA WEWE PEKEE, HAITOSHI KUKUPA USHINDI.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Je kunena kwa Lugha mpya kukoje?

Swali: Je hizi lugha ni zipi, na je! ni lazima kila mkristo aliyepokea Roho Mtakatifu anene kwa lugha mpya

JIBU: Hili ni moja ya jambo linalowachanganya wengi sana, Na nilinichanganya hata mimi pia kwa muda mrefu, na lingine linalofanana na hili ni juu ya uthibitisho halisi wa mtu kuwa amepokea Roho Mtakatifu ni upi?..

Lakini napenda ufahamu kuwa tukiweza kutofautisha kati ya hivi vitu viwili yaani “vipawa vya Roho Mtakatifu” na “Roho Mtakatifu” mwenyewe tutaweza kuondoa huu utata kwa sehemu kubwa sana.. Biblia inasema Kunena kwa lugha ni moja ya karama ya Roho Mtakatifu kama zilivyokarama nyingine, mfano Unabii, miujiza, uponyaji, ualimu, uinjilisti n.k. Lakini hatutaenda sana huko turudi kwenye msingi wa swali letu linalouliza juu ya Kunena kwa Lugha. Tukirudi nyuma kidogo kabla siku ile Bwana Yesu kupaa, aliorodhesha baadhi ya ishara ambazo zitaambata na wale wote waliomwamini na mojawapo ya ishara hizo alisema watanena kwa lugha mpya.

Marko 16:17 “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;

18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya”.

Sasa Neno “Lugha mpya”, ni Neno lisilo na mipaka (Halifungiki), yaani kwa ufupi Lugha yoyote usiyoijua wewe ukiinena kwako ni Lugha mpya, iwe ni ile iliyopo katika nchi yako, au nje ya nchi yako, au iwe ya ulimwengu huu au sio ya ulimwengu huu maadamu hauitambui bado kwako ni Lugha mpya. Hivyo ukisoma maandiko utaona ulikuwa ni mpango wa Roho Mtakatifu tangu zamani, kuwa utafika wakati atazungumza na watu wote wa ulimwenguni kwa lugha tofauti, unabii huo unaweza kuusoma katikaIsaya 28: 11 “La, bali kwa midomo ya watu wageni, na kwa lugha nyingine atasema na watu hawa;”Sasa utagundua kumbe lengo la kwanza Roho Mtakatifu kusema kwa lugha gheni katikati ya watu ni ili kuwavuta kwake wamwamini.

Hapa ni lazima atumie lugha za kibinadamu, Mfano dhahiri ni kile kilichotokea Siku ile ya Pentekoste, Walijikuta wote wanazungumza Lugha za mataifa mengine ya mbali na wale waliokuwa wanasikia wote walishikwa na butwaa na kusema hakika haya matendo makuu ya Mungu..Na kwa kitendo kile tu maelfu ya watu walivutwa Kwa Kristo.Na jambo hili liliendelea kwa muda mrefu sana.

Na pia kusudi la pili la lugha hizi Roho Mtakatifu kuziachia duniani ni ili kudhihirisha uwepo wake katikati ya waaminio, Hapa ndipo mtu anajikuta ananena lugha asiyoifahamu kwa uweza wa Roho wa Mungu..kuna Lugha za kimbinguni pia, ambazo hizo hazina matunda yoyote kwa watu wasioamini, na ndio maana Mtume Paulo alionya akasema ikiwa mtu atajikuta katika hali kama hii basi na anyamaze na anene na nafsi yake mwenyewe na Mungu wake kwa jinsi anavyojaliwa, vinginevyo ataonekana kama mwendawazimu kama akifanya hivyo katikati ya watu wasioamini, na Mungu sikuzote ni Mungu wa utaratibu. (1Wakorintho 14:28).

Fikiri mtu asiyeujua kabisa Ukristo, anaingia kanisani ghafla anashangaa watu wanaanza kuzungumza lugha zisizoeleweka…moja kwa moja atahisi amekutana na watu pengine ni wendawazimu au wanaabudu miungu..lakini akiingia na kusikia lugha yake pale inaongelewa katika ufasaha wote na anayeiongea sio hata wa jamii ya watu wake..Na maneno anayoongea ni ya kumtukuza Mungu..atashangaa sana na kuogopa kusema huu ni muujiza?..na hivyo atajua mahali pale kuna uwepo Fulani wa kiMungu na hivyo atatubu na kumgeukia Mungu. Na kusema kuwa kila mwaminio ni lazima anene kwa lugha mpya, kauli hiyo inapingana kabisa na maandiko.

Kumbuka kuwa mtu haneni lugha kama apendavyo yeye, au ajisikiavyo yeye bali ni kama vile Roho ANAVYOMJALIA MTU KUTAMKA (Soma Matendo 2:4), kama tu vile mtu asivyoamua kuona maono mpaka Mungu amwonyeshe na lugha ndio ziko hivyo hivyo..Vinginevyo mtu utakuwa ananena tu kwa akili zake, na ndivyo watu wengi walivyofanya leo hii, ambayo yanafanya tunaonekana kama watu waliorukwa na akili..

Kunena kwa lugha ni kipawa cha Mungu na Mungu anakigawa kwa jinsi apendavyo yeye mwenyewe, mmoja atampa lugha mpya, mwingine unabii, mwingine tena uponyaji, mwingine uongozi, wingine matendo ya miujiza, mwingine kufundisha n.k..lakini wote hatuwezi kuwa manabii, au wote waalimu au wote wenye kufanya matendo ya miujiza au wote wenye kunena kwa lugha au wote wachungaji.

1Wakorintho 12.27 “Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake.

28 Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha.

29 Je! Wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni waalimu? Wote wanatenda miujiza?

30 Wote wana karama za kuponya wagonjwa? WOTE WANENA KWA LUGHA? Wote wafasiri?.”

Na jambo lingine la muhimu la kufahamu ni kuwa mtu anaweza kuwa na ananena kwa lugha mpya lakini bado asiwe na Roho Mtakatifu ndani yake, kama tu vile mtu anaweza akawa ni nabii, akaona maono yote duniani, na asiwe nabii wa kweli, kama tu vile mtu anaweza akaponya magonjwa kwa karama Mungu aliyompa na kufanya miujiza mingi isiyokuwa ya kawaida na bado Kristo asimtambue.(Mathayo 7:21). 

Hivyo usijisifie karama, kwasababu Roho Mtakatifu sio karama yeye ni zaidi ya hicho, ikiwa utapenda kupata maelezo marefu juu ya uthibitisho fasaa unaomtambulisha mtu kuwa amepokea Roho Mtakatifu atanitumia ujumbe inbox, nikutumie somo lake.

Hivyo kwa kumalizia ikiwa wewe ni mmojawapo wa waliokirimiwa kipawa hichi Unaponena kwa lugha mwombe pia Mungu akupe kutafsiri, Sehemu hii inaonekana kwa wachache katika kanisa lakini ndio inayofaa zaidi, kuliko kunena tu maneno yasiyojulikana kanisani mbele ya watu, kwasababu hilo linaweza kuwa na manufaa tu kwako mwenyewe lakini lisiwe na msaada wowote kwa wengine.

Lakini kama litaambatana na tafsiri hilo linafaa sana na lina nguvu kwasababu linalijenga kanisa la Kristo kwa ujumla.

1Wakorintho 14:27 “Kama mtu akinena kwa lugha, wanene wawili au watatu, si zaidi, tena zamu kwa zamu, na mmoja na afasiri.

28 Lakini asipokuwapo mwenye kufasiri na anyamaze katika kanisa; aseme na nafsi yake tena na Mungu.”

Jivunie karama yako ikiwa inalijenga kanisa la Kristo, na sio kwa kujionyeshea kuwa ni hodari wa kunena, Mtume Paulo alijisifia zaidi ya mtu yoyote, lakini alisema ni heri anene maneno matano lakini yanalifaa kanisa kuliko kunena maneno Elfu kwa lugha.

Bwana akubariki.

[embedyt] https://www.youtube.com/watch?v=-v8ToQZwJho[/embedyt]


Mada zinazoendana:

JE! NI LAZIMA WATU WOTE WANENE KWA LUGHA?

JE! KARAMA NI UTHIBITISHO WA KUWA NA MUNGU?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

UPEPO WA ROHO.

ROHO MBAYA KUTOKA KWA BWANA.

SEHEMU ISIYO NA MAJI.


Rudi Nyumbani:

Print this post

HATUA ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUTUONGOZA.


Jina la Bwana Yesu Kristo, libarikiwe…

pamoja na kazi nyingine nyingi anazozifanya Roho Mtakatifu juu ya mtu aliyemwamini Yesu Kristo, nyingine ni kumwongoza katika kuijua kweli yote…Hilo tunalisoma katika..

Yohana 16:13“ Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake”

Neno kuongoza halina tofauti sana na kuelekeza, yaani mtu anayekuelekeza jambo Fulani hatua kwa hatua, mpaka kufikia hitimisho analotaka yeye ufikie, hana tofauti na mwongozaji…na kazi ya mwelekezaji au mwongozaji, sio tu kuonesha njia pekee bali hata kurekebisha baadhi ya makosa..Kwamfano mtu anapotaka kukuongoza kufika mahali Fulani, halafu wewe unampa mashauri yako ya njia ya kuipitia, ni wazi kuwa kama hayo mashauri yako sio sahihi basi atakurekebisha kwa nia ya kukuelekeza njia iliyo bora zaidi.

Na ndivyo ilivyo kwa Roho Mtakatifu, yeye ni mwongozaji wetu, na Roho Mtakatifu ndio jambo la kwanza kabisa mtu aliyemwamini Kristo anapaswa kuwa naye…Biblia inasema mtu asiye na Roho Mtakatifu huyo sio wake (Warumi 8:9) Ikiwa na maana kuwa mtu asiye na Roho Mtakatifu, hakuna uongozi wowote wa KiMungu unaoendelea juu ya Maisha yake..Ni kupotea tu!.

Hivyo mtu aliyeamini, katika hatua za awali kabisa, anakuwa hajui vitu vingi, hiyo ni kawaida kabisa, anakuwa kama mtoto mdogo aliyezaliwa, ambaye hajui chochote katika maisha haya, na vivyo hivyo mtu aliyezaliwa mara ya pili anakuwa ni mdhaifu katika roho. Lakini pamoja na udhaifu huo kunakuwa na kitu ndani yake kinachomfanya aelewe mambo mengi kwa muda mfupi kwasababu anakuwa na moyo wa unyenyekevu wa kutaka kujua au kufahamu Zaidi kuhusu Mungu, kama mtoto mchanga… hiyo Kiu ni ambayo Roho Mtakatifu kaiweka mwenyewe ndani ya mtu, ili itumike katika mstari wa kuwa chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu.

Roho Mtakatifu anaanza kumvuta, kidogo kidogo na kumtoa hatua moja hadi nyingine, aielekee njia ya utakatifu, ndio hapo mtu ataanza kutoka katika ulimwengu na kuona sababu ya kutafuta kanisa Fulani ambalo angalau ataweza kuipooza ile kiu iliyopo ndani yake ya kutaka kumjua Mungu…Atatoka kwenye dhambi na hatimaye kujiunga kanisa Fulani, atapata vitu ndani ya lile kanisa ambavyo vitamsisimua sana na kumfanya kukua kiroho kwa kiwango Fulani..na atakapofika mahali na kuona hali yake ya kiroho ipo pale pale, baada ya kukaa muda mrefu, kuna kitu kitamwambia hapo ulipo bado unahitaji kuwa na Mungu zaidi…..hiyo nguvu itamsukuma kutafuta hazina mpya ya chakula cha kiroho kwa hali na mali, utaona anazidi kutafuta mahali ambapo atapata chakula kilichobora zaidi…lengo lake sio kuhama kanisa au dhehebu hapana!.

Bali lengo lake ni kupata kuweka sawa hatima ya Maisha yake ya kiroho…Tofauti na wengi wanaohama makanisa sasahivi ni kwasababu tu wamesengenywa kidogo, au kwasababu wanahitilafiana na mchungaji wake kwa masuala ambayo hata sio ya kiimani, au kwasababu wanakemewa waache dhambi, au kwasababu wanataka kuolewa au kuoa, au kwasababu wamechoka tu kukaa pale na hivyo wanajaribu ladha mpya n.k…

Aliye na Roho Mtakatifu kweli haondoki mahali kwasababu kama hizo…Kinachomwondoa sehemu moja hadi nyingine ni ile kiu iliyopo ndani yake ya kutaka kumjua Mungu Zaidi, na anakuwa hana kiburi…Mahali alipokuwa anakaa hapo kwanza walikuwa hawana utaratibu wa maombi ya mfungo, hivyo anaona kuna kitu ndani ya roho yake kimepunguka anahitaji kuwa mwombaji zaidi na msomaji wa maandiko zaidi, kwahiyo anatafuta mahali ambapo atakuwa mwombaji Zaidi…Au mahali alipo kuna mchanganyiko wa Neno la Mungu na mambo ya ulimwengu huu hivyo anaondoka kwenda kutafuta mahali atakapoishibisha roho yake na Neno lisilochanganywa.

Au pengine mahali alipokuwa anakaa hakukuwa na desturi za kwenda kufanya uinjilishaji, na yeye anaona kuna kiu ndani yake ya kwenda kuwahubiria wengine habari njema popote pale, na hivyo mahali alipo haiwezekani kufanya hivyo, kwahiyo anaondoka kwenda mahali ambapo atatimiza agizo hilo la Bwana Yesu la kwenda kuhubiri injili kwa kila kiumbe..

Au pengine mahali alipokuwepo kunafanyika ibada za sanamu, na baada ya kuyachunguza maandiko vizuri anaona si sawa kufanya jambo hilo, na hivyo anaondoka kwenda kutafuta mahali ambapo hataabudu sanamu tena n.k.

Sasa katika hatua zote hizo utaona mtu huyu wa Mungu anaweza akawa ameshatembea sehemu nyingi zote akitafuta kukaa mahali salama….Na anavyozidi kusogea mbele ndivyo anavyozidi kuwa bora zaidi katika Imani. Na mtu anayekua kutoka sehemu moja hadi nyingine anakuwa hatamani tena kurudia yale ya nyuma…kwamfano mahali alipokuwepo ni mahali ambapo palikuwa hakuna utaratibu wa kusali au kuomba, wala palikuwa hakuna msisitizo wa kuishi maisha matakatifu akishatoka hapo hawezi tena kutamani kurudia hapo..

Sasa jambo hilo la kutoka sehemu moja hadi nyingine kwa lengo la kutafuta Usalama wa maisha yako ya kiroho, na si sababu nyingine tofauti na hizo…sio dhambi! Bali ni kazi ya Roho Mtakatifu katika kukuongoza na kukuweka katika kweli yote…

Hiyo ndio kazi ya Roho Mtakatifu kutuhakikisha hatukwami sehemu moja kila siku bali tunakuwa kuufikia utimilifu,

Kosa moja linalofanyika na watu wengi, ni kujaribu kutafuta dhehebu Fulani la kuhamia na kutafuta lililobora zaidi ya lingine kwa kuangalia watu wengi wanakwenda wapi, au kwa kusikiliza ushauri wa watu, au kwa kuangalia uzuri wa kanisa….lakini hawasikilizi msukumo wa Roho Mtakatifu ndani yao, ambaye huyo ndiye angewaongoza katika kuwatia kwenye kweli yote…

Binafsi nimekutana na watu wengi, wakiniuliza nimeamini sasa nihame hapa niende kanisa gani?…Binafsi huwa nakosa jibu la hili swali..kwasababu Mungu hakuanzisha madhehebu, na Roho Mtakatifu hamwongozi mtu kwenda kwenye dhehebu lolote bali anamwongoza katika kuijua kweli…..Hiyo njaa na kiu ya Neno la Mungu ndio inayomsukuma mtu kutoka sehemu moja hadi nyingine kutafuta chakula, hivyo hata kama akikutana na chakula kilichochacha mbele yake atakula tu kwa huo muda ilimradi aweze kuishi..

Kanisa sio suluhisho la kuishi katika mapenzi ya Mungu, bali Roho Mtakatifu ndio suluhisho, unapokaa chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu kwa kuyasoma maandiko ndivyo unavyompa nafasi Roho Mtakatifu kukuonesha ni wapi ulikuwa unakosea, na ni wapi unapaswa urekebishe na ni wapi pa kukaa palipo salama…lakini sio kutafuta ushauri kutoka kwa watu, au kwa kuangalia ni wapi wengi wanakwenda. Wengi wanaofanya hivyo hakuna chochote katika maisha yao kitakachobadilika kwasababu ni sawa na wamehama dini moja na kujiunga na nyingine…huko wanakokwenda wanakwenda kuwa washirika wa dini tu na si wakristo halisi, na kuvamiwa na roho ya udhehebu ambayo ndiyo roho ya mpingakristo….roho ya kusema dini yangu inafundisha hivi, au dhehebu halisemi hivyo n.k Kumbuka madhehebu ya Mafarisayo na Masadukayo ndiyo yaliyoongoza kumpinga Bwana Yesu katika huduma yake…sasa roho hiyo hiyo ndiyo iliyopo katika madhehebu (yaani watu walioacha uongozi wa Roho Mtakatifu na kuwa washirika au washabiki wa dini)..Bwana alipokuwa anawaambia Mafarisayo hivi wenyewe wakawa wanasema Musa hakutufundisha hivyo, kwahiyo ikawafanya kuwa mbali na Mungu kuliko hata watu wa Ulimwengu wasio mjua Mungu, hiyo yote ni kutokana na Udhehebu na Udini uliokuwa ndani yao.

Ndio maana Biblia inatuambia tutoke huko (Ufu.18:4), Tunapomgeukia Roho Mtakatifu na kufuata uongozi wake ndio kutoka kwenyewe kunakozungumziwa hapo…yeye ndiye kiongozi wetu ambaye kila siku anarekebisha makosa yetu kulingana na Biblia na kutuweka katika mstari.

Usianze kutafuta kanisa la kwenda sasa, anza kutafuta maandiko yanasemaje kwanza…ndipo Roho atapokuongoza pa kwenda, Roho Mtakatifu anawaongoza watu wanaosoma maandiko sio wanaotafuta makanisa…

Bwana akubariki sana. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOKUJA JUU YA MTU.

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

MIISHO YA ZAMANI.

ROHO I RADHI, LAKINI MWILI NI DHAIFU.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Kuna tofauti kati ya UBATIZO wa Roho Mtakatifu na UPAKO wa Roho Mtakatifu.

Watu wanachanganyikiwa wakidhani kuwa na upako, au nguvu za Roho Mtakatifu, ndio Umebatizwa na Roho Mtakatifu. Lakini hii sio kweli, mtu anaweza kuwa na upako wa Roho Mtakatifu, akaponya magonjwa, akafufua wafu, akanena kwa lugha, akaona maono, akatabiri au kuota ndoto na ikaja kutokea, na bado asiwe amebatizwa na Roho Mtakatifu. Tunaona kabla ya Pentekoste wanafunzi wa Yesu ikiwemo Yuda aliyemsaliti Bwana walikuwa wanafanya ishara zote hizi na bado walikuwa hawajabatizwa na Roho wa Mungu..

Biblia inasema Mathayo 5:45

“…..maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.”

Hii ni SIRI kubwa sana inayozungumzwa hapo, Bwana anaachia nguvu zake kwa waovu na wema, anaachilia nguvu zake za uponyaji,miujiza, kwa wote waovu na wema n.k. Hivyo kigezo cha mtu kufanya ishara na miujiza si tiketi ya yeye kuwa mwana wa Mungu, Bwana aliwaambia wanafunzi wake..

Luka 10:20″ Lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.”

Unaona alituambia tusifurahi kwa sababu miujiza inatendeka na sisi bali kwasababu majina Yetu yameandikwa mbinguni hii ikiwa na maana,tunapaswa tufarahi tunapokuwa na mahusiano na Mungu na uhakika wa kwenda mbinguni na sio tunapokuwa na uwezo wa kutoa pepo au kufanya miujiza.

Katika kipindi hichi cha mwisho shetani amefanikiwa kuwadanganya wengi kwa njia hii, kwa kushindwa kutofautisha ubatizo halisi wa Roho Mtakatifu na Upako wa Roho Mtakatifu, si jambo la kushangaza kuona mtu anatoka kuvuta sigara na akaenda kunena kwa lugha, nabii katoka kuzini na bado akaenda kutoa unabii na huo unabii ukatimia kama ulivyo, mtu katoka kwenye ufisadi na akaenda kumwombea mtu akafufuka na bado anaota ndoto, ishara na miujiza vikifuatana naye, mtu katoka kutukana na bado akaenda kufundisha,na kutoa mapepo na bado nguvu za Mungu zikashuka na watu wakafunguliwa katika vifungo vyao..

lakini hiyo sio uthibitisho ya kwamba mtu huyo amepokea Roho Mtakatifu usidanganyike. Mungu anaweza kutumia chombo chochote kutenda kazi yake kama chombo cha kuazima tu, kazi ya hicho chombo ikiisha Mungu anaondoka. Kwa mfano tunaona katika biblia Mungu alimtumia Punda kuzungumza na Balaamu, lakini baada ya kuupeleka ujumbe yule punda akarudia katika hali yake ya mwanzo ya upunda.

Hivi ndivyo watu wanavyotumiwa na Mungu kama vyombo vya kuazima lakini wasiwe watu halisi wa Mungu, wamenyeshewa tu ile mvua ya upako ambayo inawanyeshea wote waovu na wema. Hii ni SIRI kubwa watu wanapaswa waijue.

Bwana Yesu alisema

Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?
23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.”

Mstari huu unajieleza wazi kabisa juu ya watu wanaojidhani kuwa wanafanya miujiza na ishara ndio uthibitisho kuwa wao ni wana wa Mungu.

LAKINI UBATIZO WA ROHO MTAKATIFU NI UPI?

Uthibitisho wa Roho Mtakatifu pale anaposhuka juu yako anakufanya uwe kiumbe kipya (uzaliwe mara ya pili), anasafisha ile hali ya kutamani dhambi na kukufanya uwe mtakatifu na pia atakuongoza katika kuijua kweli yote tusome..

 Yohana 16:12 “Hata bado nikali ninayo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili hivi sasa.
13 Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.
14 Yeye atanitukuza mimi, kwa kuwa atatwaa katika yaliyo yangu na kuwapasha habari”.

Jambo la kwanza Mkristo yeyote aliyepokea Roho Mtakatifu lazima Roho amuongoze katika kuijua ukweli, ikiwemo uelewa wa maandiko,kiu na shauku ya kumjua Mungu siku baada ya siku.na kufanywa ufanane na Yesu Kristo. Roho ya mafunuo itakuja juu yake, Hatafungwa na mambo ya dini bali na NENO la Mungu tu, na Roho atamweka mbali na ulimwengu, yaani kiu ya kuupenda mambo ya ulimwengu itaanza kufa ndani yake.

Jambo lingine ni Roho atashuhudia ndani yake kuwa yeye ni Mwana wa Mungu ( atakushuhudia katika maisha unayoishi)

Warumi 8:15 “Kwa kuwa hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba, yaani, Baba.
16 Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu”;

Mtu huyo ataondokewa na hofu ya maisha kwa kuwa anajua anaye baba mbinguni, na Baba anamshuhudia ya kuwa yeye ni mtoto wake ndani yake. 

Kuna watu angali wakijidanganya kuwa wana Roho Mtakatifu lakini wamekosa haya mambo, ndani yao tamaa ya mambo ya ulimwengu imewavaa, Hawana uhusiano wowote  wao na Baba yao wa mbinguni, hofu na masumbufu ya maisha haya yamewasonga kana kwamba hawana Baba mbinguni, Wanalipinga siku zote NENO la Mungu, kuthibitisha dini zao na madhehebu yao(mfano wa mafarisayo na masadukayo), Hawapendi kuijua kweli halisi ya injili inayowapeleka watu mbinguni bali injili za pesa na mafanikio ya ulimwengu huu tu.

Sasa watu kama hao ni dhahiri kuwa hawajashukiwa na Roho wa Mungu bado, haijalishi wanafanya miujiza kiasi gani. Sio kwamba kuwa na hizo ishara ni mbaya, tofauti ni hii hawa wanakuwa wamenyeshewa mvua tu lakini hawana Roho, na wale waliobatizwa kweli kweli wanakuwa na vyote, 

Hivyo basi Roho wa Mungu anaposhuka juu ya mtu kwa mara ya kwanza huyo mtu anaweza akaanza kunena kwa lugha, au kuona maono, au kutabiri au akapata msisimko, au kushukiwa na nguvu za Mungu nyingi ndani yake,au akapata hisia ya tofauti ambayo hakuwahi kuisikia hapo kabla, wengine wakati Roho akishuka juu yao amani ya kipekee inawashukia,wengine hawasikii chochote lakini watafahamu kwa jinsi Roho wa Mungu anavyougua ndani yao, haya yote ni udhihirisho wa nje ambao hata wale wengine(magugu) wanaweza kuupata.

Lakini uthibitisho halisi ni jinsi maisha yako yatakavyokuwa yanaanza kubadilishwa na kufanywa kiumbe kipya siku baada ya siku kwa kutakaswa kwa Neno. na ubatizo wa Roho Mtakatifu unaambatana na karama za Mungu lakini kama tulivyosema mtu anaweza kuonyesha zile karama za Roho na asiwe amebatizwa na Roho Mtakatifu.

Na kuna mtazamo pia ya kuwa “kunena kwa lugha” kuwa ndio uthibitisho wa mtu kupokea Roho Mtakatifu, mtazamo huu si kweli mtu anaweza kunena kwa Lugha na asiwe amepokea Roho Mtakatifu kwasababu hichi ni kipawa cha Roho na kinamshukia yeyote kwa jinsi Roho alivyomjalia mtu, kumbuka hata mashetani wananena kwa lugha, Na kipawa hichi sio lazima kila mtu awe nacho,

kwasababu biblia inasema 

1wakoritho12:28 “Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha.
29 Je! Wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni waalimu? Wote wanatenda miujiza?
30 Wote wana karama za kuponya wagonjwa? Wote wanena kwa lugha? Wote wafasiri”?

Si unaona hapo sio wote wenye hicho kipawa cha kunena kwa Lugha. Kwahiyo mtu anaweza akabatizwa na Roho Mtakatifu na asinene kwa lugha, bali akaonyesha karama nyingine tofauti na hiyo, aidha unabii, au karama ya uponyaji, au neno la maarifa, au miujiza n.k. kwa jinsi Roho atakavyokujalia.. Mafundisho ya kwamba kila mtu lazima anene kwa lugha sio sahihi mwisho wa siku kama mtu hajapewa hicho kipawa anaishia kunena kwa akili zake tu, na kutakuwa hakuna kufasiri 1wakoritho 14.

Kwahiyo mpendwa kama haujabatizwa na Roho Mtakatifu mwombe Bwana naye atakupa Luka 11:9-13..”Nami nawaambia, Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa. Kwa kuwa kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.

Maana ni yupi kwenu aliye baba, ambaye mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe au samaki, badala ya samaki atampa nyoka? Au akimwomba yai, atampa nge? Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?” 

Kumbuka kutoa zaka, kusaidia yatima, kuhudhuria ibada kila jumapili, hayo hayatoshi hata watu wasioamini wanafanya hayo na zaidi ya hayo(mfano mzuri ni waislamu)

soma….

Mathayo 5:20″ Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni. “

Hii haki inakuja kwa kuzaliwa mara ya pili, hauwezi kuingia katika ufalme wa mbinguni pasipo hiyo, na ukishabatizwa na Roho Mtakatifu ndio kuzaliwa mara ya pili.

Matendo 2:38 “Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.”

Kumbuka Roho mtakatifu ndiye MUHURI wa Mungu, (maana ya neno MUHURI ni kwamba “KAZI IMEKAMILIKA JUU YAKO”).waefeso 4:30 “Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi”. Pasipo huyo hauwezi kwenda mbinguni, kwa sababu biblia inasema warumi 8:9 “……….Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake”. 

Mungu akubariki!

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

HATUA ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUTUONGOZA

ACHENI MJUE YA KUWA MIMI NI MUNGU.

JE! KARAMA NI UTHIBITISHO WA KUWA NA MUNGU?

JIPE MOYO.

BWANA ALIPOSEMA “SIKUJA KUTANGUA TORATI BALI KUITIMILIZA” ALIKUWA ANAMAANISHA NINI?

rejeabiblia.com


Rudi Nyumbani

Print this post

6# SWALI : Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni ipi?

JIBU: Tukisoma;

Mathayo 12:25-32 ” Lakini Mafarisayo waliposikia, walisema, Huyu hatoi pepo, ila kwa Beelzebuli mkuu wa pepo.

25 Basi Yesu akijua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, hufanyika ukiwa; tena mji au nyumba yo yote ikifitinika juu ya nafsi yake, haitasimama.

26 Na Shetani akimtoa Shetani, amefitinika juu ya nafsi yake; basi ufalme wake utasimamaje?

27 Na mimi nikitoa pepo kwa Beelzebuli, je! Wana wenu huwatoa kwa nani? Kwa sababu hiyo hao ndio watakaowahukumu.

28 Lakini mimi nikitoa pepo kwa Roho wa Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia.

29 Ama awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuviteka vyombo vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Ndipo atakapoiteka nyumba yake.

30 Mtu asiye pamoja nami yu kinyume changu; na mtu asiyekusanya pamoja nami hutapanya.

31 Kwa sababu hiyo nawaambia, KILA DHAMBI, NA KILA NENO LA KUFURU, watasamehewa wanadamu, ILA KWA KUMKUFURU ROHO HAWATASAMEHEWA.

32 Naye mtu ye yote atakayenena neno juu ya Mwana wa Adamu atasamehewa, bali yeye atakayenena neno juu ya Roho Mtakatifu hatasamehewa katika ulimwengu wa sasa, wala katika ule ujao. “

Tunavyosoma mistari hiyo tunaona kabisa wale Mafarisayo walikuwa wanajua Bwana Yesu ni kweli alikuwa anatoa pepo, na kutenda mambo yote kwa uweza wa Roho wa Mungu, lakini wao kwa ajili ya wivu, na kwa tamaa zao wenyewe,ili tu wawavutie watu kwao, wakakusudia kwa makusudi kabisa, wawageuze watu mioyo ili watu wasimuamini Bwana Yesu,wawaamini wao, na ndipo wakaanza kutoa maneno ya makufuru wanawaambia watu kuwa BWANA anatoa pepo kwa uwezo wa belzebuli mkuu wa Pepo angali ndani ya mioyo yao walikuwa wanajua kabisa anachofanya ni kwa uweza wa Roho wa Mungu.

Ukweli wa jambo hilo unajidhihirisha kwa Nikodemo ambaye naye alikuwa ni mmoja wa wale mafarisayo alipomwendea Yesu usiku na kumwambia

Yohana 3:1-2″Basi palikuwa na mtu mmoja wa Mafarisayo, jina lake Nikodemo, mkuu wa Wayahudi.

2 Huyo alimjia usiku, akamwambia, RABI, “TWAJUA” YA KUWA U MWALIMU, UMETOKA KWA MUNGU; KWA MAANA HAKUNA MTU AWEZAYE KUZIFANYA ISHARA HIZI UZIFANYAZO WEWE, ISIPOKUWA MUNGU YU PAMOJA NAYE. “

kwahiyo unaona walikuwa wanajua kabisa lakini kwa ajili ya wivu wakaanza kuzusha maneno ya uongo juu ya kazi ya Roho wa Mungu, sasa huko ndiko kumkufuru Roho Mtakatifu. hivyo basi Bwana Yesu alitoa angalizo tunapozitazama kazi za Mungu, pale mtu mwenye Roho wa Mungu anatenda kazi za Mungu kweli huku tunajua ni Mungu ndiye anayefanya kazi ndani yake, na kuanza kusema yule ni mchawi, au anatumia uchawi, au mshirikina, au tapeli, au mwizi, ili tu watu wasiziamini kazi za Mungu au vinginevyo, au unaanza kuzusha propaganda za uongo juu yake, pengine kwa kusudi la kumkomoa! hapo ndugu utakuwa unajimaliza mwenyewe. (Ni kweli si watumishi wote ni wa Mungu,hao ni sawa kuufunua uovu wao). Lakini Hapa tunamzungumzia yule unayemfahamu kabisa ni mtumishi wa BWANA,..wewe hujui umewakosesha wangapi, ambao kwa kupitia yeye, watu wengi wangeokolewa? kufanya hivyo ni hatari sana tuwe makini.

Hivyo hii dhambi unawahusu wale wanaozipinga kazi za Mungu kwa makusudi kabisa (Mfano wa mafarisayo). Hao kwao hakuna msamaha, hawawezi tena kutubu hata iweje wanachongojea ni ziwa la moto.

Lakini shetani naye anapenda kulitumia hili neno kuwafunga watu wajione kuwa wamemkufuru Roho Mtakatifu na kwamba dhambi zao hazisameheki hata wafanyeje,
Hii inakuja sana sana kwa watu waliowachanga ki-imani, kuna shuhuda nyingi za watu waliofungwa na shetani kwa namna hiyo wakidhani kuwa dhambi zao hazisameheki, kuna watu wamekata tamaa wanajiona kwa wingi wa dhambi zao, Mungu hawezi kuwasemehe tena, pengine wameua, wametoa mimba sana, n.k, Sasa jambo la namna hii likija katika mawazo yako likatae linatoka kwa yule mwovu kukufanya wewe ujione kuwa Mungu hawezi kukusamehe umemkufuru, hivyo usijisumbue kutubu kwasababu Mungu hatakusikiliza.

Kumbuka kama tulivyosema Dhambi hii inakaa kwa wale watu ambao ndani yao mioyo ya toba imekufa, au hofu ya Mungu haipo tena kwao, watu waliojikinai, wanaompinga Mungu katika fikra zao japo kuwa walimjua Mungu na uweza wake wote, wanazipotosha kazi za Mungu kwa makusudi kwa faida zao wenyewe,ili wawavute watu kwao, au wawe washirika wao na sio kwa Mungu. Hivyo basi kitendo tu cha wewe kuwa na hii hofu ya kumwogopa Mungu ujue Roho wa Mungu anatenda kazi ndani yako na hayo mawazo ya kwamba umemkufuru Roho Mtakatifu yapinge huyo ni adui ndio moja ya njia zake hizo ili usiufikie wokovu na anapenda kuwatesa watu wengi katika andiko hili.

Ubarikiwe sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada zinazoendana:

DHAMBI YA MAUTI

DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI.

DHAMBI ZINAZOTANGULIA NA ZINAZOFUATA.

DHAMBI ISIYO NA MSAMAHA.


Rudi Nyumbani:

Print this post