Title March 2021

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

SWALI: Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “Kwa kuwa kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu? (Luka 23:31)


JIBU: Tunaona sehemu mbalimbali katika biblia Bwana Yesu alijifananisha na MTI, utaona kuna mahali anasema mimi ni mzabibu wa kweli, mtu akikaa ndani yake huzaa sana.(Yohana 15:1-8), Sehemu nyingine katika kitabu cha Ufunuo Yesu anajulikana kama mti wa Uzima (Ufunuo 22:2).Akiwa na maana kuwa yeye ni kama mti ulio hai mbichi, utoao matunda,..wenye maneno ya uzima, wenye ishara na miujiza mingi ya wazi, aliyewaponya watu wote waliomwendea bila kushindwa na chochote. Aliyewaweka huru waliokuwa wanasumbuliwa na mateso, na mapepo, aliyekuwa na uwezo wa kuwasamehe watu dhambi zao, Mtu ambaye hakuwahi kuwa na doa lolote la dhambi hapa duniani, lakini hilo halikuwa na thamani machoni pao, badala yake walimdhihaki, na kumpiga na kumuua.

Mti mbichi ambao haukustahili kuchomwa moto, lakini waliuchoma moto.. vipi kuhusu miti mikavu isiyozaa,wakiiona si ndo wataifanyia zaidi. Pengine Hawataikata hata, bali wataichomea pale pale ilipo kama kuni angali imesimama,.

Na sisi ndio kama hiyo miti mikavu, ambao tumezaliwa katika dhambi, ambao hatuna ishara kama za Yesu, hatufanyi uponyaji mkuu kama wa Bwana Yesu, tunamkosea Mungu mara kwa mara, hatutoi maneno ya uzima yanayowaokoa watu muda wote, tunajikwaa kila wakati, tunategemea vipi ulimwengu utatupokea?. Tusidhani kuwa chochote tutakachojitahidi kukitenda kwa ajili ya Kristo kitakuwa ni kitu cha kupendwa sana na wao.

Yeye mwenyewe alisema..

Yohana 15:18 “Iwapo ulimwengu ukiwachukia, mwajua ya kuwa umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi.

19 Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia.

20 Likumbukeni lile neno nililowaambia, Mtumwa si mkubwa kuliko bwana wake. Ikiwa waliniudhi mimi, watawaudhi ninyi; ikiwa walilishika neno langu watalishika na lenu.

21 Lakini haya yote watawatenda kwa ajili ya jina langu, kwa kuwa hawamjui yeye aliyenipeleka”.

Kwahiyo  maneno hayo ni kuwa Bwana Yesu alikuwa anatoa tu angalizo, kwamba yatakapotutokea tusiogope au tusidhani kuwa sisi hatupendwi na Mungu au tumekosea sehemu fulani na ndio maana yametukuta kama hayo,  hapana badala yake tujue kuwa kama alivyoyapitia yeye ndivyo tutakavyoyapitia na sisi pia.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UFUNUO: Mlango wa 22

KWASABABU MUDA TULIOBAKIWA NAO SI MWINGI.

MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.

Ni kweli Waliolala Katika Kristo Wamepotea?(1Wakor 15:18)

VIKAANGUKA MACHONI PAKE VITU KAMA MAGAMBA.

Rudi nyumbani

Print this post

Adhama ni nini katika biblia?

Adhama ni neno lenye maana ya “Uzuri wa hali ya juu sana”. Na huu uzuri ni Bwana Yesu tu peke yake ndio anao, yeye ndiye mwenye adhama.

Zaburi 93: 1 “Bwana ametamalaki, amejivika adhama, Bwana amejivika, na kujikaza nguvu. Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike;

2 Kiti chako kimekuwa thabiti tokea zamani; Wewe ndiwe uliye tangu milele”

Mistari mingine michache inayozungumzia adhama ni kama ifuatayo..

Zaburi 96:6 “Heshima na adhama ziko mbele zake, Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake”.

Zaburi 104:1 “ Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Wewe, Bwana, Mungu wangu, Umejifanya mkuu sana; Umejivika heshima na adhama.

2 Umejivika nuru kama vazi; Umezitandika mbingu kama pazia;”

Isaya 33:21 “ Bali huko Bwana atakuwa pamoja nasi, mwenye adhama; mahali penye mito mipana na vijito, pasipopita mashua na makasia yake; wala hapana merikebu ya vita itakayopita hapo”.

2Wakorintho 4:7 “Lakini tuna hazina hii katika vyombo vya udongo, ili adhama kuu ya uwezo iwe ya Mungu, wala si kutoka kwetu”.

Mistari mingine iliyotaja neno hilo ni pamoja na 1Nyakati 16:27, Zaburi 21:5, Zaburi 113:3,  Zaburi 148:13 na Zaburi 29:4.

Hivyo Bwana Yesu, peke yake ndiye mwenye heshima yote na adhama yote, na wala hakuna mwingine.

Ufunuo 5:9 “Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa”

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 10 (Kitabu cha Zaburi).

Nini maana ya..“wakiwazuia watu wasioe” (1Timotheo 4:1)

UTUKUFU NA HESHIMA.

Rudi nyumbani

Print this post

2Samweli 24:1-14,inasema ni jambo la kutisha kuangukia katika mkono wa Bwana je! inakinzana na Waebrania 10:31?.

SWALI: Katika 2Samweli 24:1-14, Hapo tunaona Daudi anasema, afadhali kuangukia katika mkono wa Bwana, lakini anapingana na Paulo katika Waebrania 10:31, anaposema ni jambo la kutisha mtu kuangukia katika mikono ya Mungu aliye hai.

Jibu: Shalom, ukisoma kwa makini utaona kuwa sio kwamba maandiko yanapingana, kwamfano

Tukijifunza hicho kisa cha Daudi kwanini aseme ni heri kuangukia katika mikono ya Mungu, ndipo tutaelewa vizuri.

Kama tunavyoijua habari, Daudi alifanya kosa na Mungu akamwekea mapigo matatu mbele yake achague moja; Taifa lake lipigwe na njaa miaka 7, au Taifa lake lipigwe na ugonjwa wa Tauni siku tatu, au yeye mwenyewe akimbizwe na maadui zake miezi 3.

Sasa katika hizo adhabu tatu alizoambiwa achague, mbili kati ya hizo ni mkono wa Mungu na moja ni mkono wa mwanadamu.. Kwamfano hiyo ya njaa miaka saba na Tauni siku tatu, ni mkono wa Bwana, lakini hiyo ya kukimbizwa na maadui zake miezi 3, ni mkono wa mwanadamu.

Hivyo Daudi kwa uzoefu alioupata katika maisha yake, kupitia kufukuzwa na Sauli nyika kwa nyika, alijifunza kuwa kuwindwa na mwanadamu ni kubaya sana kwasababu mwanadamu hana rehema wala huruma..atakutafuta usiku na mchana, na hata akikushika hatakuhurumia.. Lakini kwa Mungu zipo rehema, huwa anaghairi mabaya, hata kama kashayanena, huwa ana huruma.

Kwahiyo Daudi alipopewa adhabu hizo tatu achague moja, ndipo yeye akachagua kuangukia mikononi mwa Mungu, kwasababu kuna rehema, Maana yake aidha Taifa lake lipigwe na njaa miaka 7 au wapigwe na tauni siku 3, kwasababu pengine wakiwa katikati ya hiyo adhabu Mungu anaweza kuwahurumia na kuikatisha adhabu hiyo, lakini asiangukie mikononi mwa wanadamu wamfukuze na kumwinda, kwani huwa hawakati tamaa na hawanaga huruma.

Na kweli, alipochagua kuangukia mikononi mwa Mungu, Tunasoma Mungu aliwapiga kweli kwa Tauni, lakini tunasoma hazikumalizika  siku zote tatu, Mungu aliizuilia ile Tauni, kwasababu ni mwingi wa rehema.

Tusome kidogo,

2Samweli 24:13 “Basi Gadi akamwendea Daudi, akamweleza, akamwambia, Basi, miaka saba ya njaa ikujie katika nchi yako? Au miezi mitatu ukimbie mbele ya adui zako, huku wakikufuatia? Au siku tatu iwe tauni katika nchi yako? Fanya shauri sasa, ufikiri, ni jawabu gani nimrudishie yeye aliyenituma.

14 Naye Daudi akamwambia Gadi, Nimeingia katika mashaka sana; basi sasa na TUANGUKE KATIKA MKONO WA BWANA; kwa kuwa rehema zake ni nyingi; wala nisianguke katika mkono wa wanadamu.

15 Basi Bwana akawaletea Israeli tauni tangu asubuhi hata wakati ulioamriwa; nao wakafa watu toka Dani mpaka Beer-sheba sabini elfu.

16 LAKINI HUYO MALAIKA ALIPONYOSHA MKONO WAKE KUELEKEA YERUSALEMU ILI AUHARIBU, BWANA AKAGHAIRI KATIKA MABAYA, AKAMWAMBIA HUYO MALAIKA MWENYE KUWAHARIBU WATU, YATOSHA, SASA ULEGEZE MKONO WAKO. NAYE YULE MALAIKA WA BWANA ALIKUWAKO KARIBU NA KIWANJA CHA KUPURIA CHA ARAUNA, MYEBUSI”.

Umeona hapo?, Bwana kaghairi mabaya!!.. Lakini hiyo haizifanyi adhabu zake kuwa HERI, Hata kama ataghairi mabaya lakini tayari kashaadhibu wengi, (hapo wameshaanguka watu elfu sabini, pengine walikusudiwa kuanguka watu laki tatu), lakini pamoja na hayo watu elfu sabini si wachache..Ni wengi sana, ni heri Daudi angeangukia kwenye kukimbizwa miezi mitatu yeye peke yake kuliko kuruhusu vifo vya watu elfu sabini..

Hivyo suala bado lipo pale pale kwamba ni jambo la kutisha kuangukia kwenye mikono ya Mungu hata kama ana rehema nyingi, kwasababu ni kweli anaweza akaghairi mabaya, lakini tayari atakuwa ameshaadhibu na kuharibu pakubwa sana..(watu elfu sabi). Ndicho Mtume Paulo alichokisema katika kitabu cha Waebrania…

Waebrania 10:30 “Maana twamjua yeye aliyesema, Kupatiliza kisasi ni juu yangu, mimi nitalipa. Na tena, Bwana atawahukumu watu wake.

31 Ni jambo la kutisha kuanguka katika mikono ya Mungu aliye hai”.

Kwahiyo mistari hiyo haikinzani bali inakubaliana katika jambo moja…Na Daudi alipochagua kuangukia katika mikono ya Mungu, si kwasababu adhabu za Mungu ni ndogo, bali ni kwasababu zina rehema ndani yake, kulinganisha na zile za wanadamu. Lakini hukumu za Mungu zinatisha na za kuogopwa, na ni kubwa kuliko za wanadamu, kwaufupi si za kutamani kabisa, kama Mtume Paulo alivyosema.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Je! Daudi hakuwa mtoto wa ndoa wa Yese? (Zab 51:5)

AINA TATU ZA WAKRISTO.

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 10 (Kitabu cha Zaburi).

JE! HAMPOTEI KWA SABABU HII?

JE! NI KWELI UMEMFUATA YESU?

Rudi nyumbani

Print this post

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA TITO.

Kitabu cha Tito ni waraka ulioandikwa na Mtume Paulo, kwa mtu anayejulikana kama Tito. Tito alikuwa ni mmoja wa watu waliogeuzwa kumgeukia Kristo, kupitia injili ya Mtume Paulo. Na mtu huyu alikuwa ni mwenyeji wa mji ulioitwa Krete.

Krete ni kisiwa kilichopo kusini mwa nchi ya Ugiriki, zamani kilikuwa kinaitwa Krete na hata leo hii bado kinaitwa hivyo hivyo Krete.

Kwahiyo Mtume Paulo katika ziara zake za kuhubiri, alifika pia katika kisiwa hicho, na hatimaye huyu Tito akawa mmoja wa matunda yake katika Injili. Na kwa kuwa alikuwa na bidii Zaidi  kuliko wengine, akachaguliwa kwa uongozo wa Roho Mtakatifu kuwa mwangalizi wa makanisa ya huo miji.

Na Paulo na wenzake baada ya kuondoka katika huo mji, kwenda kwenye miji mingine kwajili ya kuhubiri injili, ilibidi amwandikie waraka Tito, na kumpa maagizo machache ya namna ya kulijenga kanisa, Na maagizo hayo yalikuwa yamegawanyika katika vipengele viwili. 1) Maagizo jinsi ya kuteua viongozi wa kanisa na 2) Maagizo kwa waumini wote wa kanisa.

 1. MAAGIZO JINSI YA KUTEUA VIONGOZI WA KANISA.

Uteuzi wa viongozi ulitegemea vigezo fulani vya kimaandiko, hivyo ilibidi Paulo amfundishe Tito vigezo vya maaskofu, wachungaji na wazee wa kanisa, wanavyopaswa wawe, ili kanisa lisije likaanguka kwa kukosa uongozi thabiti, kutokana na kuwa viongozi wasio na vigezo. Hivyo Paulo kwa uongozo wa Roho akamwandikia Tito waraka huo na baadhi ya mambo aliyomwambia ni kama yafuatayo..

Tito 1:4 “ Tito, mwanangu hasa katika imani tuishirikiyo. Neema na iwe kwako na amani zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Mwokozi wetu.

5 Kwa sababu hii nalikuacha Krete, ili uyatengeneze yaliyopunguka, na kuweka wazee katika kila mji kama vile nilivyokuamuru;

6 ikiwa mtu hakushitakiwa neno, naye ni mume wa mke mmoja, ana watoto waaminio, wasioshitakiwa kuwa ni wafisadi wala wasiotii.

7 Maana imempasa askofu awe mtu asiyeshitakiwa neno ,kwa kuwa ni wakili wa MUNGU;asiwe mtu wa kujipendeza nafsi yake,asiwe mwepesi wa hasira, asiwe mlevi wala mgomvi, asiwe mpenda mapato ya aibu.

8 bali awe mkaribishaji, mpenda wema, mwenye kiasi, mwenye haki, mtakatifu, mwenye kudhibiti nafsi yake;

9 akilishika lile neno la imani vile vile kama alivyofundishwa, apate kuweza kuwaonya watu kwa mafundisho yenye uzima, na kuwashinda wenye kupinga.

10 Kwa maana kuna wengi wasiotii, wenye maneno yasiyo na maana, wadanganyaji, na hasa wale wa tohara, ambao yapasa wazibwe vinywa vyao.

11 Hao wanapindua watu wa nyumba nzima, wakifundisha yasiyowapasa kwa ajili ya mapato ya aibu”

 2. MAAGIZO KWA WAUMINI WOTE WA KANISA.

Na pamoja na hayo, Paulo alimpa maagizo ndugu Tito, Na maagizo hayo yalikuwa ni maonyo kwa waumini wote, wazee wakike kwa wa kiume, na vijana wa kike kwa wakiume, na watumwa.

Aliwaonya wazee wanawake wawe katika utakatifu, ili wawe vielelezo kwa wanawake vijana, kadhalika na watumwa wawatii Bwana zao.

Tito 2:1 “Lakini wewe nena mambo yapasayo mafundisho yenye uzima;

2 ya kwamba wazee wawe wenye kiasi, wastahivu, wenye busara, wazima katika imani na katika upendo na katika saburi.

3 Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na mwenendo wa utakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye kutumia mvinyo nyingi, bali wafundishao mema;

4 ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao;

5 na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe.

6 Vivyo hivyo na vijana waume uwaonye kuwa na kiasi;

7 katika mambo yote ukijionyesha wewe mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo mema, na katika mafundisho yako ukionyesha usahihi na ustahivu,

8 na maneno yenye uzima yasiyoweza kuhukumiwa makosa, ili yule mwenye kupinga atahayarike, kwa kuwa hana neno baya la kunena juu yetu.

9 Watumwa na wawatii bwana zao, wakiwapendeza katika mambo yote; wasiwe wenye kujibu,

10 wasiwe waibaji; bali wauonyeshe uaminifu mwema wote, ili wayapambe mafundisho ya Mwokozi wetu Mungu katika mambo yote.

11 Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa”.

Na pia Mtume Paulo, alimpa maagizo Tito, kuwa awakumbushe watu kunyenyekea kwa wenye mamlaka..

Tito 3:1 “Uwakumbushe watu kunyenyekea kwa wenye uwezo na mamlaka, na kutii, na kuwa tayari kwa kila kazi njema;

2 wasimtukane mtu ye yote, wasiwe wagomvi, wawe wema, wakionyesha upole wote kwa watu wote”.

Na mwisho, akamwambia maneno haya..

Tito 2: 15 “Nena maneno hayo, onya na kukaripia kwa mamlaka yote; asikudharau mtu awaye yote”.

Katika waraka huu tunajifunza mambo kadhaa.

 1. Kwanza tunajifunza kanisa la Kristo linaongozwa na maaskofu, wachungaji, walio na vigezo vya kimaandiko, kama tulivyovisoma hapo juu..

2. Na pia kila mshirika wa kanisa, ni lazima ajifunze kuishi maisha ya utakatifu, Kama ni mzee fahamu kuwa kuna vijana chini yako na watoto, ambao wanapaswa kujifunza kutoka kwako, wakikuona wewe mzee una mizaa je watajifunza nini kutoka kwako?..wakikuona wewe mzee unavaa vibaya watajifunza nini kutoka kwako?.

Vivyo hivyo kama wewe ni mtumwa, labda unafanya kazi katika shirika fulani, au na juu yako wapo wakubwa kuliko wewe, halafu wanakuona huna adabu, ni mwizi, na sio mnyenyekevu, je unawatengenezea picha gani kuhusu ukristo?

Na pia kinatufundisha sisi kama washirika wa mwili wa Kristo, kunyenyekea kwa wenye mamlaka. Haijalishi mwenye mamlaka ni nani, biblia imetuonya tuwaheshimu na kuwanyenyekea, unyeyekevu unaozungumziwa hapo sio kuwaabudu au kuwaogopa kiasi kwamba hata wakikuambia usimwabudu Mungu wako uwatii.. Hapana! Bali unyenyekevu unaozungumziwa hapo ni ule wa wewe kufuata na kutii maelekezo yao yote ambayo yanaelekeza kufanya mema, na kuwaheshimu kama unavyowaheshimu watu wengine wote.

Kwamfano mwenye mamlaka katika mji wako amesema  “siku fulani ni ya kufanya usafi” hapo huna budi kutii.

 3. Na jambo la mwisho tunaloweza kujifunza ni kukaripia, na kuonya kwa mamlaka yote watu wote wanaokwenda kinyume na Neno la Mungu ndani ya kanisa. Paulo alimwambia Tito akaripie, hivyo hata leo tuna jukumu hilo hilo, la kukaripia uzinzi na wazinzi waliopo kanisani, kukaripia walevi waliopo kanisani, kukaripia watukanaji na wavaaji vibaya kanisani, tena biblia imesema kwa tufanye hivyo kwa mamlaka yote, bila hofu kwasababu si dhambi. Wengi wanaogopa kukaripia kwasababu wanahisi kwamba watakuwa wanawahukumu watu. Hapana!. Kuambiwa ukweli sio kuhukumiwa bali ni kuonywa. Na biblia na ukristo kwa ujumla, dhima yake kubwa ni maonyo! Hakuna kitu kingine, kama hutaki maonyo, basi ukristo haukufai.

Bwana atubariki.

Kama hujampokea Yesu, kama bado unavaa vimini, kama bado ni mlevi, mshirikina,  mwizi n.k fahamu kuwa ukifa leo unakwenda jehanamu. Hivyo ni bora ukampokea Yesu leo kwa kutubu, na kuacha kufanya dhambi, ili upate wokovu na msamaha wa dhambi.

Yesu Kristo yupo mlangoni kurudi !!!.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA FILEMONI.

KUJIPAMBA NI DHAMBI?

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

JINSI MTUME PAULO ALIVYOUTHAMINI WITO WAKE, JUU YA WENYE VYEO.

UFUNUO Mlango wa 2: Sehemu ya pili.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya siku moja kwa Bwana ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja? (2Petro 3:8)

Tusome,

2Petro 3:8 “Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja”.

Kama ukiendelea mbele kidogo kusoma mstari wa 9, utaona Mtume Petro anajaribu kumwelezea Mungu kwamba huwa hakawii kuzitimiza ahadi zake kwetu sisi wanadamu.  

2Petro 3:8 “Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja.

 9 Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba”.

Aliona kuna watu wengi wanaona kama Mungu huwa anachelewa sana kutimiza aliyoyasema.. Alisema atarudi, mbona harudi na imeshapita miaka mingi? N.k

Ndipo akazungumza maneno hayo, ambayo pia yalizungumzwa kwa sehemu na Mfalme Daudi katika Zaburi..

Zaburi 90:4 “Maana miaka elfu machoni pako Ni kama siku ya jana ikiisha kupita, Na kama kesha la usiku”.

Maana yake ni kwamba tunapodhania kwamba Miaka elfu ni kipindi kirefu sana, kwa Mungu kwake ni kama siku moja tu ya jana iliyoisha. Na kwanini Kristo hajarudi mpaka miaka hii, sababu imeshatolewa hapo juu, kwamba “hapendi mtu yoyote apotee, bali wote waifikilie toba”. Hivyo anatuvumilia ili watu wote tuingie katika neema ya wokovu, kabla ya ule mwisho kufika,  maana ule mwisho ukifika kama hatutakuwa ndani ya wokovu, hakutakuwa na nafasi ya pili.

Lakini pia kama tukifikiri Mungu kawahi sana, basi tusisahau kuwa siku moja kwa Mungu ni sawa na miaka elfu, maana yake, tunaishi nje ya muda, (muda umeenda sana), na ule mwisho upo karibu sana. Kristo yupo mlangoni..

Na ndio maana biblia inasema “saa ya wokovu ni sasa”.

2Wakorintho 6.2 “Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa”

Kadhalika katika mambo mengine ya kimaisha, tunapoona siku moja ni fupi sana kwetu Mungu kufanya jambo, tujue kuwa kwa Mungu ni kama miaka elfu, maana yake ahadi zake alizotuahidi anaweza kuzitimiza  ndani ya siku moja… Kwahiyo hatupaswi kumkosea Mungu Imani, hata kama tumeona siku inakaribia kuisha na hatujapata kile tunachokitafuta, tufahamu kuwa Mungu anaweza kufanya jambo kubwa ndani ya siku hiyo hiyo moja kabla haijaisha yote, kwasababu kwake yeye ni kama miaka elfu.

Bwana atubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko siku elfu”?

IMESALIA RAHA YA SABATO KWA WATU WA MUNGU.

Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?

Je! Kuna malaika wangapi mbinguni?

LAKINI NINYI, NDUGU, MSIKATE TAMAA KATIKA KUTENDA MEMA.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

NGUVU YA MNADHIRI WA BWANA.

Jina la Mwokozi wetu Yesu, libarikiwe.

Mnadhiri ni mtu aliyejitenga na mambo fulani ili atimize nadhiri/Ahadi aliyoiweka kwa Mungu wake. Kwamfano katika agano la kale, kama mtu ameweka nadhiri fulani kwa Mungu, labda  ya kumtolea sadaka Fulani, na akatamka kwa kinywa chake mwenyewe mbele za Mungu, basi yalikuwepo maagizo Fulani ya kufanya ambayo yanaambatana na nadhiri hiyo aliyoiweka ili asije akaisahau nadhiri hiyo aliyoiweka.

Na agizo la kwanza kwa mtu aliyeweka nadhiri, ni kwamba hakupaswa kabisa kunywa divai wala kilevi cha aina yoyote ile.

Hesabu 6: 1 “Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,

2 Nena na watu wa Israeli, uwaambie, Mtu mume au mtu mke atakapoweka nadhiri kubwa, nadhiri ya Mnadhiri, ili ajiweke wakfu kwa Bwana;

3 atajitenga na divai na vileo; hatakunywa siki ya divai, wala siki ya kileo, wala asinywe maji yo yote ya zabibu, wala asile zabibu, mbichi wala zilizokauka.

 4 Siku zote za kujitenga kwake asile kitu cho chote kilichoandaliwa kwa mzabibu, tangu kokwa hata maganda”.

Na kwanini Mungu akataze mtu asinywe kileo chochote, wakati wa nadhiri yake? . Ni kwasababu kileo kinamtoa mtu ufahamu, na kumfanya ajisahau, hata ajikute anazungumza maneno au anafanya vitendo ambavyo ni kinyume na ile nadhiri aliyomwekea Mungu, hivyo ikawa dhambi kubwa kwake. Maana yake ni kwamba mtu aliyemwekea Mungu nadhiri ni lazima awe katika akili yake timamu wakati wote, hapaswi hata dakika moja kujitoa nje ya ufahamu wake kwa kileo, au kwa kitu kingine chochote.

2. Sheria ya Mnadhiri (yaani mtu aliyeweka nadhiri) ilikuwa ni lazima, aziache nywele zake ziwe ndefu, (Hapaswi kuzikata kabisa).

Hesabu 6: 5 Siku zote za nadhiri yake ya kujitenga, wembe usimfikilie kichwani mwake; hata hizo siku zitakapotimia, ambazo alijiweka wakfu kwa Bwana, atakuwa mtakatifu, ataziacha nywele za kichwani mwake zikue ziwe ndefu”.

Siku zote nywele ni ishara ya uwepo wa Mungu juu yetu. Na nywele huwa ni nyingi kichwani, na zina tabia ya kukua, kila siku zinaongezeka kimo, Ndivyo rehema na Neema za Mungu zilivyo nyingi juu yetu, zinaongezeka kila kukicha.

Maombolezo 3: 22 “Ni huruma za Bwana kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi.

23 Ni mpya kila siku asubuhi; Uaminifu wako ni mkuu”

Kwahiyo mnadhiri yeyote, ambaye alikuwa amemwekea Mungu nadhiri, hakukata nywele zake, mpaka siku ambayo atatimiza nadhiri hiyo ndipo ataruhusiwa kuzikata. (Matendo 18:18, matendo 21:23).

Sasa kama ukiendelea kusoma zaidi juu ya sheria hizo za mnadhiri, utaona kuwa pia mnadhiri yeyote pamoja na kutokukata nywele zake na kunywa kileo, alipaswa pia siku zote ajitenge na kila aina ya unajisi, maana yake alipaswa ajiweke katika hali ya utakatifu. Na kama akishindwa kutimiza vigezo hivyo nadhiri yake hiyo inakuwa ni batili na ni dhambi kwake.

Lakini pia kulikuwa na Baraka za kipekee kwa mtu aliyemwekea Mungu nadhiri, kipindi chote wakati yupo katika hiyo nadhiri na hata baada ya kuimaliza hiyo nadhiri. Na baraka hiyo ya kipekee ilikuwa ni kutembea na nguvu za Mungu, kwa namna isiyokuwa ya kawaida..Na nguvu hiyo kazi yake ni kumweka mtu mbali na maadui wa kiroho.

Sasa leo kwa msaada wa Bwana tutajifunza mtu mmoja katika maandiko, ambaye alikaa katika nadhiri za Mungu, na kuzifurahia nguvu za Mungu, mpaka siku alipojisahau na kutoka nje ya nadhiri na kupata madhara, na kupitia mtu huyo tutajua umuhimu wa kukaa katika nadhiri kwa Mungu wetu tulizomwekea.

Na mtu huyo ambaye tutajifunza habari zake  si mwingine zaidi ya Samsoni.

Biblia inasema Samsoni alikuwa Mnadhiri wa Mungu tangu tumboni mwa mama yake.  Mungu mwenyewe ndiye aliyemfanya awe mnadhiri wake.

Na kama sheria ya Mnadhiri wa Mungu inavyosema, hakupaswa anywe divai, wala kileo kingine chochote, hivyo Samsoni hakunywa kileo chochote tangu akiwa tumboni mwa mama yake, ndio maana Mungu alimwambia mama yake asinywe divai wakati wa uja uzito wake, kadhalika kama mnadhiri wa Mungu hakupaswa kukatwa nywele zake, kulingana na maagizo Mungu aliyotoa katika torati kumhusu mnadhiri..

Waamuzi 13:3 “Malaika wa Bwana akamtokea yule mwanamke, akamwambia, Tazama, wewe sasa u tasa, huzai; lakini utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanamume.

4 Basi sasa, jihadhari, nakuomba, usinywe divai wala kileo, wala usile kitu kilicho najisi;

5 kwani tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanamume; na wembe usipite juu ya kichwa chake; maana mtoto huyo atakuwa mnadhiri wa Mungu tangu tumboni; naye ataanza kuwaokoa Israeli na mikono ya Wafilisti”.

Umeona hapo?..ni kwanini Samsoni nywele zake hazikupaswa kukatwa.? Si kwasababu alikuwa ni mtu maalumu sana, bali ni kwasababu tayari alikuwa ni Mnadhiri, na sheria ya mnadhiri tangu wakati wa Musa ni kutokukata nywele, wala kunywa divai. Hivyo Samsoni hakupaswa kukata nywele zake wala kunywa kileo chochote maisha yake yote, ili nadhiri yake iwe na maana.

Sasa imezoeleka kufahamika kwamba, Samsoni nguvu zake zilikuwa katika nywele tu!..Lakini kiuhalisia ni kwamba hazikuwa katika nywele zake tu, bali hata katika kitu alichokuwa anakunywa… Ndio maana alionywa asinywe kileo chochote tangu akiwa tumboni…

Maana yake ni kwamba hata kama Delila asingejua siri ya nywele zake, lakini akajua siri ya kutokunywa kwake kileo, na hivyo akaenda kumtengenezea kileo na kumpa, bado nguvu za Samsoni  zingeisha mpaka atakapolevuka na kurudia akili yake, Kwasababu siri za nguvu za Samsoni, zilikuwa katika Neno la Mungu, ambalo linatoa maagizo juu ya mnadhiri, na neno hilo Mungu alilizungumza tangu wakati wa Torati ya Musa…

Hesabu 6: 1 “Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,

2 Nena na watu wa Israeli, uwaambie, Mtu mume au mtu mke atakapoweka nadhiri kubwa, nadhiri ya Mnadhiri, ili ajiweke wakfu kwa Bwana;

3 atajitenga na divai na vileo; hatakunywa siki ya divai, wala siki ya kileo, wala asinywe maji yo yote ya zabibu, wala asile zabibu, mbichi wala zilizokauka.

 4 Siku zote za kujitenga kwake asile kitu cho chote kilichoandaliwa kwa mzabibu, tangu kokwa hata maganda

5 Siku zote za nadhiri yake ya kujitenga, wembe usimfikilie kichwani mwake; hata hizo siku zitakapotimia, ambazo alijiweka wakfu kwa Bwana, atakuwa mtakatifu, ataziacha nywele za kichwani mwake zikue ziwe ndefu”.

Kwahiyo kama mtu yupo katikati ya nadhiri halafu akakata nywele zake, anakuwa kashaharibu kila kitu…kadhalika kama yupo katikati ya nadhiri halafu akalewa na kilevi cha aina yoyote ile,  vile vile anakuwa kashaharibu kila kitu.. Kwahiyo Samsoni akiwa bado yupo katika nadhiri yake ambayo hiyo ilikuwa ni ya maisha, nywele zake  zilikatwa…na hivyo akawa amejiharibia mwenyewe.

Hiyo ilikuwa ni agano la kale, kwamba mtu akiweka nadhiri ni lazima aziache nywele zake zikue… na mtu akivunja maagizo hayo ya torati anakuwa amejiharibia mwenyewe.

Hali kadhali katika agano jipya, tunazo nadhiri; Zipo nadhiri ambazo sisi wenyewe tunaziweka…kwamfano zile za kuahidi kufanya jambo Fulani kwa Mungu, lakini zipo nadhiri ambazo sisi hatuamui kuziweka, bali Mungu mwenyewe ndiye anayeziweka katika maisha yetu, kama vile Samsoni.

 Samsoni hakumwekea Mungu nadhiri kwa kuamua yeye, isipokuwa Mungu mwenyewe ndiye aliyemwekea ile nadhiri tangu akiwa tumboni mwa mama yake,  yeye alijikuta tu tayari kazaliwa na ile nadhiri. Vivyo hivyo pia mtu anayezaliwa mara ya pili katika roho, tayari anakuwa na nadhiri ya Maisha,  ambayo hiyo ni Mungu anaiweka katika maisha yake, na inamfunga aishi katika sheria za Mungu, na wakati wote na ni lazima aishi kulingana na Neno la Mungu ili nguvu zake za rohoni zisipotee, wakati wote anapoishi hapa duniani.. Lakini kama akitoka nje ya neno la Mungu, na kuruhusu  adui shetani yake akate nywele zake za rohoni, kama alivyofanya kwa samsoni, atakuwa amejiweka katika hali ya hatari sana, ni heri hata asingezaliwa mara ya pili.

Sasa ifuatayo ni milango ambayo shetani anaitumia kuzikata nywele zetu za rohoni, na kututoa katika unadhiri mtakatifu.

1.Uzinzi na uasherati.

Unapofanya uzinzi au uasherati baada ya kuzaliwa mara ya pili,  au unapojihusisha na mahusiano yoyote ya kipepo, hapo tayari unakuwa umejiuza kwa shetani moja kwa moja.. Na hicho ndicho kilichomwangusha pia Samsoni…Biblia inasema katika Mithali 31:3 “Usiwape wanawake nguvu zako;…”.  Na inasema pia..

1Wakorintho 6:18  “Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe”.

Hapo inasema, ikimbieni sio ikemeeni…

Siku hizi ni fashion kila kijana kuwa na girlfriend, na binti kuwa na boyfriend, tena hayo yanafanyika kanisani, na kila mtu anajua..halafu huyo huyo analalamika siku hizi nguvu za kusali zimeisha, anasumbuliwa na mapepo, anaota ndoto mbaya, akisoma neno dakika mbili anasikia usingizi, anashindwa kujizuia kutenda dhambi, mambo yake hayaendi sawa n.k..Sasa hizo nguvu zitatoka wapi wakati tayari umeshampa shetani?…tayari shetani kashakata nywele zako, kwa uasherati wako huo, hiyo nguvu ya kuomba utatolea wapi?, hiyo nguvu ya kusoma neno utatolea wapi, hiyo nguvu ya kwenda kuhubiri utatolea wapi, hiyo nguvu ya kufunga utatolea wapi?, utakemea pepo gani litoke?..kwaufupi katika roho, shetani ameshakupofusha macho na anakusagisha ngano katika gereza lake kama alivyomfanya Samsoni. (Waamuzi 16:21).

2.Ibada za sanamu.

Huu ni mlango wa pili, shetani anaoutumia kututoa katika unadhiri mtakatifu. Kumbuka siku zote pale tunapozaliwa mara ya pili, hatupaswi kumwambudu mtu yeyote wala kitu chochote. Tunapomfanya mtu Fulani, achukue nafasi ya Mungu, au kitu Fulani tulichokitengeneza kwa mikono yetu kichukue nafasi ya Mungu..tayari tumemfungulia shetani mlango wa kutuondoa kwenye unadhiri wetu mtakatifu.

Na mambo mengine yote yaliyosalia yaliyo kinyume na Neno la Mungu, ni mlango wa adui kututoa kwenye unadhiri mtakatifu.

Sasa inawezekanana tayari shetani kashakutoa katika  unadhiri wako, ambao Bwana alikuwekea tangu siku ile ulipozaliwa mara ya pili, ndio maana ulikuwa unanguvu nyingi za rohoni, kuangusha ngome na mamlaka kwa jina la Yesu, hata adui akuzingire kiasi gani, hakukuweza, kama vile Samsoni, ulikuwa una nguvu za kusali na kusoma Neno, na kushinda dhambi.. Lakini ulimfungulia shetani mlango mahali Fulani na akaziondoa nguvu zako, na mpaka sasa huwezi tena kufanya yale uliyokuwa unafanya mwanzo.

Suluhisho ni moja, ni kuanguka chini na kujinyenyekeza kwa Mungu, kwa kutubu kama Samsoni alivyofanya, na kuachana na mambo yote yaliyo kinyume na Neno la Mungu, kama ulikuwa unaishi maisha ya uasherati unayaacha kwa vitendo, ikiwemo kukata mawasiliano na hao uliokuwa unafanya nao uashetari, kama ulikuwa unaabudu sanamu, unaacha na kutubu, kama udanganyifu wa mali ulikuwa umekushika, unapunguza muda wa kufanya shughuli na kuongeza muda wa kumtafuta Mungu n.k. Kama ukifanya hayo Mungu ni wa rehema, kama alivyomrehemu Samsoni, na kumrejeshea tena nguvu zake. Na wewe utarudia katika hali yako ya unadhiri mtakatifu,kama ule wakati ambapo majeshi ya adui yalikuwa hayawezi kusimama mbele yako.

Lakini kama bado unaupenda ulimwengu, fahamu kuwa upo gereza na macho yako yamepofushwa, na kama bado hujampokea Yesu kabisa maishani mwako, ni vyema ukampokea leo, maadamu anapatikana, itafika wakati utatamani siku moja ya mwana wa Adamu katika maisha yako usiione, kama ukiipuuzia sauti yake inayokuita leo.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

NADHIRI.

UTAKASO NI SEHEMU YA MAISHA YA MKRISTO YA KILA SIKU.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

Kwanini Mungu aliikubali sadaka ya Yeftha ya kumtoa binti yake kafara?

Fadhili ni nini? Nini maana ya “fadhili zake ni za milele” kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

NIFANYALO WEWE HUJUI SASA; LAKINI UTALIFAHAMU BAADAYE.

Wakati ule ambao Bwana Yesu anawatawadha wanafunzi wake miguu, Petro alimuuliza Bwana swali la mshangao sana, lililoashiria kugoma kutawadhwa miguu na Bwana, kwasababu alitazamia kuwa wao ndio wangepaswa wamtawaze yeye miguu, na sio yeye awatawadhe wao, Lakini Bwana alimwambia maneno haya;

Yohana 13:7 “Yesu akajibu, akamwambia, Nifanyalo wewe hujui sasa; lakini utalifahamu baadaye”.

Nachotaka uone hapo  kuhusu  Bwana Yesu ni kuwa, si kila jambo analolifanya katika maisha yako sasa, au unaloliona akilitenda nje kwa wengine, ambalo hulielewi utalipatia majibu yake leo leo. Mengine amekusudia uyafahamu baadaye.

Yapo maisha Mungu anaweza kukupitisha wewe kama mkristo uliyeokoka  yakawa ni nje kabisa na matarajio yako, na ukijiangalia, huna kasoro yoyote na Mungu, lakini bado unajiuliza, kwanini mimi, mbona wenye dhambi hayawakuti kama yaliyonikutuma mimi..Kwanini matatizo haya yamenipata wakati huu, kwanini ugonjwa huu umenikuta mimi kama mtumishi wa Bwana, kwanini Mungu anaruhusu nichukiwe na ndugu zangu kwasababu ya ukristo wangu, kwanini Mungu mpaka sasa hanipi kazi, japokuwa nimekuwa nikimtumikia muda wote huu..

Maswali kama hayo alijiuliza Ayubu wakati ule alipokumbana na matatizo yasiyoeleweka chanzo chake ni nini.

Nataka nikuambie ukishajiona upo katika mazingira kama hayo, na ndani yako unashuhudiwa kabisa wewe ni mtoto wa Mungu, ni heri tu utulie, kwasababu si kila jambo utapata majibu yake leo leo, pengine ni ushuhuda Mungu anautengeneza ndani yako, ili uje kuwa msaada mkubwa sana kwa watu wengine baadaye, watakaopitia hali kama za kwako ili waimarike.

Au hata kama ikiwa ni kwa ajili yako, basi ujue lipo jambo bora Zaidi litakuja mbele yako, Hivyo usikata tamaa ya kuendelea kumtumikia  Mungu,. Yeye mwenyewe alisema..

Yeremia 29:11 “Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho”.

Unaona kumbe lipo tumaini kwenye siku za mwisho, siku ambazo huwezi tena kufanya mabadiliko yoyote, siku ambazo huwezi tena kurekebisha chochote hapo ndipo tumaini linatokea.. Siku hizo zikifika utasema, ni heri wakati ule Mungu hakunipa kile, au ni heri wakati ule Mungu alinipitisha pale nione, au ni heri wakati ule Mungu hakunijibu maombi yale, leo hii ningeshakuwa nimepotea, au nimekufa, au nimepoteza kila kitu, au ningefanana na wale waliopata hasara ya nafsi zao.

Tunapaswa tusiwe watu wa kutafuta tafuta sababu za kila ugumu unaokuja mbele yetu mwisho wa siku tutakuwa ni watu wa kulaumu laumu, au kunung’unika nung’unika, si kila jambo utalipatia jawabu lake papo kwa papo, hivyo wewe ishi maisha yanayompendeza Mungu sikuzote, haijalishi mambo yatakuonyookea, au hayatakunyookea sasa.. Songa mbele na Bwana, kwasababu anajua mawazo anayokuwazia, kamwe hawezi kukuacha, utafahamu sababu za yeye kufanya hivyo mbeleni, lakini sasa mtazame Kristo.

Siku hizo ndio zile utasema ni heri nilichagua kumtafuta Mungu, faida yake leo hii nimeiona.

Vivyo hivyo yapo mambo mengi sana kama kanisa la Kristo, Bwana ametuficha leo, kuna maswali ambayo kwa namna ya kawaida hatuwezi kuwa na majibu yake sasa, lakini tutakuja kufahamu baadaye, aidha tukiwa hapa hapa duniani au tukishavuka ng’ambo.

1Wakorintho 13:12 “Maana wakati wa sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana”.

Kwahiyo, tuzidi kumtazama Bwana Yesu, tumpende, na tumwamini, kamwe hawezi kutuacha. Sifa, heshima na utufuku vina yeye milele na milele.

Amen.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

ILI NIWE KIELELEZO KWA WALE WATAKAOMWAMINI BAADAYE.

Nini maana ya “heri mtu asiyekaa barazani pa wenye mizaha?”

SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?

NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.

MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.

Rudi nyumbani

Print this post

Ni kweli Waliolala Katika Kristo Wamepotea?(1Wakor 15:18)

SWALI: Bwana Yesu Asifiwe Naombeni Ufafanuzi Je Maneno Haya Yana Maana Gani

1wakoritho15:18-19 “na Hapo Wao Nao Waliolala Katika Kristo Wamepotea , 19 “kama Katika Maisha Haya Tu Tumemtumaini Kristo, Sisi Tu Maskini Kuliko Watu Wote”


JIBU: Ni rahisi, kudhani mistari hiyo inathibitisha kuwa wale waliokufa katika Yesu Kristo wamepotea katika uwongo wa kiimani. Lakini mistari hiyo haimaanishi hivyo, ukianzia vifungu vya juu, na ukiendelea mpaka vile vya chini utalithibitisha hilo. Tusome..

1Wakorintho 15:12 “Basi, ikiwa Kristo anahubiriwa ya kwamba amefufuka katika wafu, mbona baadhi yenu husema kwamba hakuna kiyama ya wafu?

13 Lakini kama hakuna kiyama ya wafu, Kristo naye hakufufuka;

14 tena kama Kristo hakufufuka, basi, kuhubiri kwetu ni bure na imani yenu ni bure.

15 Naam, na sisi tumeonekana kuwa mashahidi wa uongo wa Mungu; kwa maana tulimshuhudia Mungu ya kuwa alimfufua Kristo, ambaye hakumfufua, ikiwa wafu hawafufuliwi.

16 Maana kama wafu hawafufuliwi, Kristo naye hakufufuka.

17 Na kama Kristo hakufufuka, imani yenu ni bure; mngalimo katika dhambi zenu.

18 Na hapo wao nao waliolala katika Kristo wamepotea.

19 Kama katika maisha haya tu tumemtumaini Kristo, sisi tu maskini kuliko watu wote.

20 Lakini sasa Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala.

Unaona, mistari hiyo inatuonyesha kuwa, wakati ule kulizuka kundi la Wakorintho ambao walianza kuamini kuwa hakuna kiyama ya wafu(yaani hakuna ufufuo wa wafu), Imani kama ile waliokuwa nayo masadukayo, kwamba mtu akifa amekufa, habari yake imeishia hapo. Isipokuwa tu tofauti yao na masadukayo ni kuwa masadukayo walikuwa hawamwamini Kristo, lakini hawa walikuwa wanamwamini, na tena walikuwa wanaamini kuwa alikufa akafufuka.

Sasa ndio hapo ukisoma mstari wa 13-18 utaona mtume Paulo anawauliza maswali, yanayokinzana na Imani yao, anawauliza kama hawamini kuwa kuna kiyama wa wafu, kwanini waamini kuwa Kristo alifufuka?. Na kama hakufufuka, basi Imani yao ni bure, hata hao waliolala katika Kristo wamepotea. Hawapaswi kuamini hata ufufuo wa Yesu.

Mpaka hapo utakuwa umeona kuwa, mstari huo wa 18 haumaanishi kuwa wale waliolala katika Kristo wamepotea.

Lakini mstari wa 19 anamalizia na kusema..

19 Kama katika maisha haya tu tumemtumaini Kristo, sisi tu maskini kuliko watu wote.

Neno maskini kama lilivyotumika hapo ni Zaidi ya kukosa fedha.. Yaani sisi tuliomwamini Kristo, kwasababu ya maamuzi yetu hayo ya kumwishia yeye, tutakuwa kama watu waliodharaulika, au watu waliotupwa chini kuliko watu wote ulimwenguni. Japo tu juu ya wote.

Swali ni je! Na wewe leo hii Unaogopa kuchekwa kwa ajili ya Yesu? Au kudharauliwa, au kutengwa, au kufukuzwa kazi kwa ajili yake? Mitume hawakujali hilo, kwanini wewe uogope?..Kumbuka kumwamini Yesu ni pamoja na kukubali shutma kwa ajili ya jina lake. Huko ndiko kujitwika msalaba wako alikokuzungumzia Bwana Yesu

Alisema.

Marko 8:38 “Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu”.

Lakini Zaidi ya yote alisema maneno haya kwa wale watakaoshinda….

Ufunuo 3:21 “Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.

VIKAANGUKA MACHONI PAKE VITU KAMA MAGAMBA.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

NITAUPATAJE UPENDO WA KI-MUNGU NDANI YANGU?

Je ni kweli imani ya mtu ndiyo itakayomuokoa, na si kitu kingine?

Rudi nyumbani

Print this post

Alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru

SWALI: Naomba kufahamu nini maana ya huu mstari?

Wakorintho 3:17 “Basi ‘Bwana’ ndiye Roho; walakini alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru”.


JIBU: Kauli hiyo kinyume chake ni kuwa, kama  Roho wa Bwana hayupo basi mahali hapo hapana uhuru wowote, kwa mujibu wa biblia.

Lakini ni uhuru wa aina gani Roho Mtakatifu analeta.

kibiblia Roho Mtakatifu alikuja kuleta Uhuru wa aina mbili.

  • Uhuru wa kutuondoa katika utumwa wa dhambi na mateso.

  • Uhuru wa kututoa katika utumwa wa sheria.

1). Tukianzana na uhuru wa kutuondoa katika utumwa wa dhambi;

Siku ile Bwana Yesu alipoanza huduma yake ya kuhubiri alisema maneno haya..

Luka 4:18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa,

19 Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa”.

Umeona hiyo ni kuonyesha kuwa Roho Mtakatifu aliposhuka juu ya watu wake na katika kanisa alikuwa na kazi ya kuwatoa watu katika vifungo vya dhambi na mateso ya  ibilisi, yaani waliokuwa wanasumbuliwa na mapepo, waliokuwa wanateswa na magonjwa, na hofu, na mauti, na shida  vyote hivyo vilikuja kuondolewa na Roho Mtakatifu mwenyewe,

na pia ukizidi kusoma tena katika Isaya 61:3-4 utaona unabii huo wa Roho Mtakatifu unaendelea kusema..

“…kuwafariji wote waliao; 3 kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti ya haki, iliyopandwa na Bwana, ili atukuzwe”.

Unaona anafanya pia kazi ya kuwatoa watu katika huzuni zao, kuwafariji,kuwapa mataji ya utukufu na sifa. huo ni Zaidi ya Uhuru, ambao hakuna mtu yeyote hapa duniani angeweza kuutoa.

2). Uhuru wa sheria;

Pia alikuja kutukomboa sisi tuliokuwa chini ya sharia, tutoke katika laana ya sheria..

Wagalatia 4:3 “Kadhalika na sisi, tulipokuwa watoto, tulikuwa tukitumikishwa na kawaida za kwanza za dunia.

4 Hata ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke, amezaliwa chini ya sheria,

5 kusudi awakomboe hao waliokuwa chini ya sheria, ili sisi tupate kupokea hali ya kuwa wana.

6 Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani, Baba.

7 Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu”.

Roho Mtakatifu alikuja kututoa katika utumwa wa sheria, ili tupate kuhesabiwa haki kwa njia ya kumwamini Yesu Kristo na sio kwa matendo yetu tena. Kwasababu hapo mwanzo tulijitahidi sana kumpendeza Mungu kwa kushika sheria, lakini sheria ilituzidi nguvu, kwasababu ya udhaifu wa miili yetu. Hivyo tangu enzi za agano la kale, hakuwahi kuonekana hata mmoja aliyeweza kumpendeza Mungu kwa matendo yake mwenyewe, haijalishi walijitahidi kiasi gani.

Hivyo ili Mungu kutuokoa,  alimtuma mwanawe Yesu Kristo duniani, ili yeye peke yake atende mema, pasipo kufanya dhambi yoyote, kisha Mungu amuhesabie haki yeye peke yake kwa matendo yake, na ndipo sasa sisi  tutakaomwamini Yesu baadaye tuhesabiwa haki kama vile yeye, kwa njia ya matendo yake na sio yetu..

Kwahiyo, ikiwa wewe umemwamini Yesu, na ukampokea Roho wake, basi ujue Mungu haangalii matendo yako, kama ndio kipimo cha yeye kukubali, bali anamwangalia mwana wake YESU KRISTO uliyemwamini, na hivyo unahesabiwa haki, kama vile hujawahi kumkosea Mungu, kwasababu VAZI la Yesu linakufunika mbele yako.

Huoni kama huo ni uhuru mkubwa sana? Unahesabiwa haki kwa kumwamini tu!  Lakini ikumbukwe kuwa hiyo haimaanishi kuwa tuendelee kutenda dhambi kisa tu hatuhesabiwi haki kwa matendo yetu, hapana, hata kwa namna ya kawaida, huwezi kwenda kupeleka mkono kwenye tundu la nyoka akung’ate kila saa, kisa tu dawa ya kutibu sumu ipo, hapana, vinginevyo utakuwa mwendawazimu, bali utachukua tahadhari kubwa sana, kwa kuzidi kukaa mbali na nyoka, kwasababu unajua sumu yake sikuzote ni kifo..

Na sisi vivyo hivyo maadamu tunahesabiwa haki kwa kumwamini Yesu Kristo ni jukumu letu sote, tukae mbali na dhambi, kwa kadiri tuwezavyo, katika utakatifu wote ili tupate kumzalia Mungu matunda. Na hiyo ndio ishara ya kuamini kwetu.

Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa Roho Mtakatifu ametuletea uhuru mkubwa sana hapa duniani.  kiasi kwamba mtu yeyote atakayempokea, atakuwa HURU KWELI KWELI. Jambo ambalo watu wengi hawalifahamu, wakidhani kwa Mungu ni utumwa.

Swali ni je wewe umeshampokea ndani yako? Kama jibu ni la, unasubiri nini? Kumbuka Pasipo Roho Mtakatifu huwezi kwenda katika unyakuo, na haji ndani yako isipokuwa  kwanza umemwamini  Yesu Kristo, kwa kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa na kuwa tayari kuyaacha mambo yako maovu uliyokuwa unayafanya huko nyuma. Na pili kwa kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji tele, na kwa jina la YESU KRISTO sawasawa na Matendo 2:38, Na hapo ndipo Mungu atakapokupa kipawa cha Roho Mtakatifu ndani yako bure.

Hivyo ikiwa utapenda kumkaribisha Yesu maishani mwako, basi tafuta mchungaji yoyote, au mtumishi yoyote aliyesimama katika Imani, akusaidie, au wasiliana nasi kwa namba hizi: +255693036618 / +255789001312

Mungu akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

JE NI KWELI SAMAKI NGUVA YUPO?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

UTENDAJI KAZI MWINGINE WA ROHO MTAKATIFU USIOUFAHAMU.

 Nini maana ya “Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati”

NGAZI 7 AMBAZO MKRISTO NI LAZIMA AZIPANDE KUUFIKIA UKAMILIFU.

Rudi nyumbani

Print this post

Sitara ni nini katika biblia?

Sitara limetokana na neno “sitiri”, na kusitiri maana yake ni “kuficha kitu au jambo” hivyo kitu chochote kinachositiri kinaitwa “Sitara”. Nguo ni mfano wa Sitara, kwani inasitiri maungo yetu.. Kadhalika pazia linalowekwa mlangoni ni mfano wa Sitara, kwani linasitiri mambo yaliyopo ndani, au yanayoendelea ndani n.k

Kwamfano katika biblia tunaona, sehemu ile ambapo Sanduku la Agano lilikuwa linawekwa, paliwekwa pazia ambalo lilikuwa linatenganisha patakatifu, na patakatifu pa patakatifu, ili kulisitiri sanduku la agano lililokuwa ndani, sasa pazia lile lilikuwa linajulikana kama PAZIA LA SITARA.

Hesabu 4:5 “hapo watakapong’oa safari, Haruni ataingia ndani, na wanawe, nao watalishusha PAZIA LA SITARA, na kulifunika sanduku la ushahidi kwa hilo pazia;”

Pia unaweza kusoma juu ya pazia hilo katika Kutoka 35:12, Kutoka 39:34, Kutoka 40:21 na Kutoka 36:37.

Na katika wakati wetu huu, sitara yetu ni YESU KRISTO. Yeye pekee ndiye aliyechukua dhambi zetu, na kusitiri uovu wetu kupitia msalaba, maana yake pale tunapomwamini na kutubu, dhambi zetu zote zinasitirika mbele za Baba, na tunaonekana kama hatujawahi kutenda dhambi kabisa, yeye ndio kama vazi letu , kufahamu zaidi, ni kwa namna gani Yesu ni vazi letu (Sitara yetu) fungua hapa >> Mtakatifu ni nani?.

Pamoja na hayo, Yesu ni sitara yetu dhidi ya madhara yote yanayoletwa na yule adui yetu shetani, kama  vile shida, magonjwa na adha.

Zaburi 32:7 “Ndiwe sitara yangu, utanihifadhi na mateso, Utanizungusha nyimbo za wokovu”.

Zaburi 119:114 “Ndiwe sitara yangu na ngao yangu, Neno lako nimelingojea”.

Hivyo ni Baraka kubwa kumfanya Bwana, sitara yetu…Lakini ni laana kubwa kumfanya shetani au wanadamu kuwa sitara yetu.

Yeremia 17:5 “Bwana asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha Bwana

6 Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani palipo ukame, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.

 7 Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake.

  8 Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji, Uenezao mizizi yake karibu na mto; Hautaona hofu wakati wa hari ujapo, Bali jani lake litakuwa bichi; Wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua, Wala hautaacha kuzaa matunda”

Ukimkataa Bwana moyoni mwako, na kuikubali sayansi, hutaona mema yatakapotokea, utakuwa umelaaniwa biblia inasema hivyo.

Bwana atusaidie tuzidi kumfanya yeye SITARA YETU YA DAIMA. Ngome yetu, kimbilio letu, msaada wetu na jabali letu.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

WAPE WATU WANGU RUHUSA ILI WAPATE KUNITUMIKIA.

KUNA MAJIRA MUNGU ATAIVURUGA MIPANGO YETU.

NI KWA NAMNA GANI ROHO HUTUTAMANI KIASI CHA KUONA WIVU?

MANA ILIYOSHUSHWA KUTOKA MBINGUNI.

Rudi nyumbani

Print this post