Adhama ni nini katika biblia?

Adhama ni nini katika biblia?

Adhama ni neno lenye maana ya “Uzuri wa hali ya juu sana”. Na huu uzuri ni Bwana Yesu tu peke yake ndio anao, yeye ndiye mwenye adhama.

Zaburi 93: 1 “Bwana ametamalaki, amejivika adhama, Bwana amejivika, na kujikaza nguvu. Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike;

2 Kiti chako kimekuwa thabiti tokea zamani; Wewe ndiwe uliye tangu milele”

Mistari mingine michache inayozungumzia adhama ni kama ifuatayo..

Zaburi 96:6 “Heshima na adhama ziko mbele zake, Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake”.

Zaburi 104:1 “ Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Wewe, Bwana, Mungu wangu, Umejifanya mkuu sana; Umejivika heshima na adhama.

2 Umejivika nuru kama vazi; Umezitandika mbingu kama pazia;”

Isaya 33:21 “ Bali huko Bwana atakuwa pamoja nasi, mwenye adhama; mahali penye mito mipana na vijito, pasipopita mashua na makasia yake; wala hapana merikebu ya vita itakayopita hapo”.

2Wakorintho 4:7 “Lakini tuna hazina hii katika vyombo vya udongo, ili adhama kuu ya uwezo iwe ya Mungu, wala si kutoka kwetu”.

Mistari mingine iliyotaja neno hilo ni pamoja na 1Nyakati 16:27, Zaburi 21:5, Zaburi 113:3,  Zaburi 148:13 na Zaburi 29:4.

Hivyo Bwana Yesu, peke yake ndiye mwenye heshima yote na adhama yote, na wala hakuna mwingine.

Ufunuo 5:9 “Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa”

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 10 (Kitabu cha Zaburi).

Nini maana ya..“wakiwazuia watu wasioe” (1Timotheo 4:1)

UTUKUFU NA HESHIMA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments