Title November 2020

OLE WAKO KORAZINI NA BETHSAIDA.

Korazini na Bethsaida ilikuwa ni miji iliyokuwepo kandokando ya bahari ya Galilaya.. Sasa Bahari ya Galalilaya, iliitwa hivyo bahari lakini kiuhalisia sio bahari bali ni ziwa, kwasababu bahari ni lazima iwe na maji ya chumvi, lakini Hili la Galilaya lilikuwa na maji yasiyo chumvi (yaani maji barini), hivyo lilikuwa ni ziwa mfano wa Ziwa Victoria, isipokuwa halikuwa kubwa kama ziwa Victoria, Ziwa hilo la Galilaya mpaka leo lipo huko kaskazini mwa Israeli.

Sasa kando ya hilo ziwa la Galilaya (au Bahari ya Galilaya) kulikuwepo na miji maarufu mitatu, ambayo ni Korazini, Bethsaida na Kapernaumu. Miji hiyo kwamfano mrahisi tuseme Mji wa Mwanza, Mara na Kagera, iliyoizunguka ziwa Victoria, na ndio hivyo hivyo miji hiyo mitatu ilikuwa imeizunguka hiyo bahari ya Galilaya.

Sasa kipindi ambacho Bwana Yesu yupo duniani, sehemu za kwanza kwanza kabisa kuhubiri injili zilikuwa ni katika hiyo miji mitatu kwasababu haikuwa mbali sana na mji wa Nazareti aliokulia Bwana Yesu. Hivyo miji hii mitatu ilipata neema isiyokuwa ya kawaida kuona miujiza mikubwa. Tofauti na miji mingine yoyote ya Israeli kama Yerusalemu na Bethania au Samaria. Hivyo kwa miujiza iliyoiona ilitegemewa iwe ndio miji ya kwanza kutubu na kumkubali Mwokozi, lakini ilikuwa kinyume chake…Ndipo Bwana Yesu akaiambia siku moja maneno haya…

Mathayo 11:20  “Ndipo akaanza kuikemea miji ile ambamo ndani yake ilifanyika miujiza yake iliyo mingi, kwa sababu haikutubu.

21  Ole wako, Korazini! Ole wako, Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika katika Tiro na Sidoni, wangalitubu zamani kwa kuvaa magunia na majivu.

22  Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi Tiro na Sidoni kustahimili adhabu zao siku ya hukumu kuliko ninyi.

23  Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa mpaka mbinguni? Utashushwa mpaka kuzimu; kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwako ingalifanyika katika Sodoma, ungalikuwapo mji huo hata leo.

24  Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma kustahimili adhabu yake siku ya hukumu kuliko wewe”.

Maandiko hayo yanatuonyesha kuwa japokuwa watu wa Sodoma na Gomora walihukumiwa kwa adhabu ya moto, na kuchomeka kikatili, kutokana na dhambi zao, lakini kumbe bado haitoshi, wataendelea tena kuadhibiwa baadaye.

Hiyo inaogopesha sana, kama uliwahi kuona picha za ajali ya watu walioungua kwa moto, huwezi kufikiri kwamba watu kama hao wanaweza tena kwenda kuadhibiwa huko wanakokwenda…Lakini biblia inatufundisha kuwa watenda dhambi hata wakifa hapa kwa kuadhibiwa na Mungu, huko wanakokwenda watakutana na adhabu iliyo kubwa kuliko hiyo walioadhibiwa hapa..Ndicho Bwana Yesu alichokisema hapo kwenye huo mstari wa 24.

“Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma kustahimili adhabu yake siku ya hukumu kuliko wewe”.

Maana yake watu wa Sodoma, wataendelea kuadhibiwa..na sasa wapo kuzimu wanateseka, na siku ile ya Mwisho katika hukumu ya kiti cheupe cha enzi cha mwanakondoo, watahukumiwa na kutupwa kwenye ziwa la moto lenye mateso mara nyingi zaidi.

Lakini, Bwana Yesu anazidi kusema… “itakuwa heri kwa watu wa Sodoma kustahimili adhabu siku ile kuliko wewe”. Yaani hiyo miji ambayo ilihubiriwa na kuona miujiza mingi lakini haikutubu.

Hiyo inatupa picha nyingine kuwa, katika ziwa la moto, viwango vya kuadhibiwa vitatofautiana…wapo watakaoteseka sana kuliko wengine… Shetani hawezi kuteswa sawa na mzinzi, wala nabii wa uongo hawezi kuteswa sawa na kahaba..viwango vitatofautiana.

Lakini hapo Bwana anasema adhabu ya wale ambao hawatatubu, baada ya kuona miujiza mingi ya ki-Mungu ikitendeka..hao Bwana anasema dhambi yao ni kubwa kuliko ya watu wa Sodoma na Gomora, hivyo watahukumiwa zaidi kuliko watu wa Sodoma na Gomora,.

Hii ni tafakari fupi tu ya leo, ambayo ningependa tuitafakari pamoja leo. Na kujua kuwa miujiza Roho Mtakatifu anayoifanya kwenye maisha yetu, tunayoina kila mahali, sio kwa lengo la kutuburudisha, bali ni kwa lengo la kulihakikisha Neno lake kuwa ni kweli. Hivyo ni wajibu wetu kutubu na kujitakasa sana. Na kama bado Yesu yupo nje ya maisha yetu, huu ndio wakati wa kumkaribisha ili tusiangukie mikononi mwa hukumu ya Mungu.

Kwasababu ni dhahiri kuwa sisi tunaoishi sasa tunaona miujiza mikubwa ya Bwana Yesu kuliko wale watu wa kanisa la kwanza, Mpaka tunaizoelea. Kristo atusaidie tuchue hatua sahihi.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MADHARA YA KUTAFUTA ISHARA.

CHUKI ULIZO NAZO KWA MAADUI ZAKO, SIZO ALIZONAZO MUNGU JUU YAO.

Yuko azuiaye sasa hata atakapoondolewa! ni nani huyo?

Nguo za magunia katika biblia ni zipi?

Wevi na wanyanga’anyi waliomtangulia Yesu walikuwa ni wapi?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mungu anaposema “nitaliweka jina langu” ana maana gani?

SWALI: Kwanini kila mahali Mungu anasema, “mahali Fulani nitaliweka jina langu au nimeliweka jina langu”, Je ana maana gani kusema hivyo, ni kwamba lile jina lake la YEHOVA, anakuwa analiweka ndani ya  sehemu hizo au?


JIBU: Mahali popote Mungu anaposema nitaliweka jina langu, anamaanisha kuwa sehemu hiyo, au kitu hicho amekichagua, au amekiweka wakfu kitumiwe kwa ajili ya aidha kumtangaza yeye , au kuwambudu, au kumfanyia ibada, n.k. hakuna cha zaida.

Hivyo sehemu yoyote au kitu chochote, au mtu yoyote aliyewekwa wakfu na Mungu (au ametiwa mafuta ya utumishi), basi ujue  kuwa tayari mtu huyo au kitu hicho Mungu kashakiwekea jina lake ndani yake. Na mtu huyo, au kitu hicho kinapaswa kichukuliwe kwa umakini sana, kwasababu kikighafilikishwa, aidha na mtu mwenyewe, au mtu mwingine ni rahisi kupata adhabu kali sana kutoka kwa Mungu.

 * Kwa mfano katika biblia utaona Mungu aliweka jina lake ndani ya malaika wake kwa kusudi la kuwahudumia wana wa Israeli, na hichi ndicho alichowaambia wakiwa kule jangwani;

Kutoka 23:20 “Tazama, mimi namtuma malaika aende mbele yako, ili akulinde njiani na kukupeleka mpaka mahali pale nilipokutengezea.

21 Jitunzeni mbele yake, mwisikize sauti yake; wala msimtie kasirani; maana, hatawasamehe makosa yenu; KWA KUWA JINA LANGU LIMO NDANI YAKE”.

* Utaona tena Mungu aliliweka jina lake pia juu ya wana wote wa Israeli,. Yaani waisraeli wote walikuwa ni  wakfu kwa Mungu kati ya mataifa yote ulimwenguni. Hivyo mtu yeyote au taifa lolote ambalo liliwakosesha, au kuwafadhaisha, lilishiriki adhabu kali kutoka kwa Mungu.

Hesabu 6:27 “Ndivyo watakavyoweka jina langu juu ya wana wa Israeli; nami nitawabarikia”.

 Mtu yeyote aliyeilaani Israeli, Mungu alimlaani, na yeyote aliyeibariki Mungu alimbariki, kwasababu Mungu aliliweka jina lake juu yao. Hata sasa Baraka hizi na laana zinaendelea kwa yeyote atakayeitakia heri au shari Israeli.

* Utaona tena Mungu aliliweka jina lake, katika lile Hekalu lililojengwa na Mfalme Sulemani pale Yerusalemu.

2Wafalme 21:4 “Akazijenga madhabahu ndani ya nyumba ya Bwana, napo ndipo alipopanena Bwana, Katika Yerusalemu nitaliweka jina langu”.

Hivyo, wote ambao walikuwa wanalinajisi hekalu la Mungu, mauti au adhabu kali walikumbana navyo.

Lakini wakati mwingine Mungu aliahirisha hasira yake juu ya wana wa Israeli, sio kwasababu walimpendeza sana, hapana lakini ni kwasababu tu alishaliweka jina lake ndani yao. Soma vifungu hivi, utaliona hilo, Ezekieli 36:21, Isaya 48:9-12, Ezekieli 20:9-10,

Vivyo hivyo na katika agano jipya, Mungu ameweka jina lake katika vitu kikuu viwili.

Cha kwanza ni Kanisa lake; Palipo na Kanisa hai la Kristo ujue jina la Mungu lipo mahali hapo. Lile ni hekalu la Mungu. Ambapo Mungu amepaweka pawe wafku kwa ajili ya ibada, sala na dua, na shukrani, sasa ikitokea mtu analinajisi kanisa la Kristo, kwa namna yoyote ile, ajue kuwa anashindana na mkono wa Mungu wenyewe, na bila shaka yoyote, atakuwa matatizoni.

Pili, ni Mungu analiweka jina lake ndani ya mwaminio. Yaani ndani mtu aliyeokoka. Mtu aliyeokoka, moja kwa moja anapokea kibali cha Mungu kuja ndani yake, kwa yule Roho Mtakatifu anayeachiliwa juu yake. Hivyo mtu wa namna hiyo anakuwa ni wakfu kwa Mungu, chombo kiteule cha Mungu. Na mtu yeyote akitajiribu kumfadhaisha, atakuwa anajitafutia madhara mwenyewe kutoka kwa Mungu. Kwasababu tayari Mungu alishaliweka jina lake ndani yake.

Na mtu anaokoka, kwanza kwa kutubu, kwa kumaanisha kabisa kuziacha dhambi zake, na pili, kwa kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi, na kwa jina la Yesu Kristo sawasawa na Matendo 2:38

Akishakamilisha hayo, Roho Mtakatifu atakuja juu yake, na kuanzia huo wakati, jina la Mungu litakuwa limeshawekwa ndani yake. Na yeye atakuwa mtiwa mafuta wa Bwana.

Je, na wewe upo tayari leo kuokoka? Kama jibu ni ndio basi fungua hapa, kwa ajili ya kupata maelekezo ya namna ya kutubu. >>>> SALA YA TOBA

Bwana akakubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Hayawani ni nini katika biblia?

Je ni wanyang’anyi wawili waliomtukana Bwana Yesu au mmoja?

Shekina ni nini? Na Je! Utukufu wa shekina unamaana gani?

Baadhi ya watu  na misemo ambayo haipo katika biblia.

JINA LA MUNGU NI LIPI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Hayawani ni nini katika biblia?

Mwanzo 3:14 “Bwana Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako”

Hayawani ni wanyama wa mwituni, ambao sio wa kufugwa…Wanyama wa kufungwa ni kama Kondoo, Mbuzi, Ng’ombe, Ngamia, punda n.k. Hawa wameumbwa mahususi kuishi na wanadamu, na kunyenyekea chini ya mikono ya wanadamu. Lakini wanyama wengine wote ambao kamwe hawewezi kujinyenyekeza chini ya uongozo wa wanadamu, na hivyo hawaishi na wanadamu bali mwituni kama simba, chui, nyati, fisi, mbwa-mwitu n.k Hao ndio wanaoitwa hayawani, ni wanyama wasiofugika.

Kwamfano Swala ni kama mbuzi tu, lakini huwezi kumfuga, kwanza akikuona atakimbia…kadhalika Nyati, ni kama ng’ombe tu, lakini huwezi kumfuga na kumtumikisha kama ng’ombe akikuona atatatufa kukudhuru, badala ya kukutii. Kama biblia inavyosema..

Ayubu 39: 9 “Je! Nyati atakubali kukutumikia? Au atakaa katika zizi lako?

10 Je! Waweza kumfunga nyati kwa kamba matutani? Au, yeye atayalima mabonde nyuma yako?

 11 Je! Utamtumaini kwa sababu ana nguvu nyingi? Au, utamwachia yeye kazi yako?

 12 Je! Utamtumaini kwamba ataileta mbegu yako nyumbani. Na kukusanya nafaka ya kiwanja chako cha kupuria?”.

Baadhi ya mistari katika biblia inayozungumzia juu ya hayawani ni pamoja Mwanzo 3:14, Mwanzo 31:39, Ayubu 35:11, Zaburi 50:10, Isaya 13:21, Isaya 23:13 n.k.

Lakini pia biblia imewafananisha Maadui wa Injili kama Hayawani wa mwituni. Maadui wa Injili ni pamoja na manabii wote wa uongo na waalimu wote wa uongo, ni pamoja na watu wote wanaoipinga injili ya msalaba. Wale Bwana Yesu aliosema katika Mathayo  7:15.

Mathayo  7:15 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali”.

Hivyo manabii wote wa uongo ni hayawani ambao kazi yao kubwa ni kuingia katikati ya kundi la kulidhuru, hawa hawafugiki chini ya zizi la Mchungaji mkuu Yesu Kristo, ni wanyama wa mwituni katika roho, sio miongoni mwa kondoo wake.

1Wakorintho 15: 32 “Ikiwa, kwa jinsi ya kibinadamu, nalipigana na hayawani wakali kule Efeso….”.

Hali kadhalika, mtu yeyote ambaye kwa nje anaonekana ni mkristo, lakini kwa siri ni mtu anayefanya uchafu, biblia inasema huyo naye ni hayawani..

Tito 1:12  “Mtu wa kwao, nabii wao wenyewe, amesema, Wakrete ni waongo siku zote, HAYAWANİ WABAYA, walafi wavivu”.

Hivyo tujitahiti tusiwe wanyama wasiofugiga (hayawani) bali tuwe miongoni mwa kondoo wa Yesu. Na pia tujihadhari na hayawani wote wanaojigueza na kuwa mfano mfano wa kondoo wa Yesu, biblia imesema tutawatambua kwa Matunda yao.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

TABIA YAKO NI YA MNYAMA GANI?

CHAPA YA MNYAMA

Roho za Wanyama zinakwenda wapi baada ya kifo? Je! Watafufuliwa?

FAHAMU MAJIRA ULIYOPO NA NINI UNAPASWA UWE NACHO.

KWANINI AWE PUNDA NA SI MNYAMA MWINGINE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je ni wanyang’anyi wawili waliomtukana Bwana Yesu au mmoja?

SWALI: Kitabu cha Mathayo 27:44 na Marko 15:32b inazungumzia wale wanyang’anyi walioteswa pamoja na Yesu kuwa wote wawili walimtukana Yesu pia, ila tukisoma Luka 23:39 inasema ni mmoja ndiye alimtukana sasa kwanini inakuwa hivyo naomba unisaidie nielewe?.

JIBU: Tuvipitie vifungu vyenyewe;

Mathayo 27:44 “Pia wale wanyang’anyi waliosulibiwa pamoja naye walimshutumu vile vile.

Marko 15:32 Kristo, mfalme wa Israeli, na ashuke sasa msalabani tupate kuona na kuamini. Hata wale waliosulibiwa pamoja naye wakamfyolea.

Luka 23:39 “Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi.

40 Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo?

41 Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.

42 Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.

43 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”.

JIBU: Ukisoma juu juu ni rahisi kusema maandiko yanajichanganya, lakini hakuna kinachojichanganya isipokuwa ni sisi wenyewe tunakosa shabaha ya kuyaelewa maandiko.

Habari hii inafanana na ile, ya wale watu wawili ambao Yesu alikutana nao kule makaburini wenye pepo, ukisoma pale utaona injili moja inaonyesha Bwana alikutana na vichaa wawili, wakati injili nyingine inaonyesha alikutana ni kichaa mmoja, Sasa habari hizo sio kwamba zinajichanganya, hivyo Ili kupata ufafanuzi wake basi fungua hapa >>> Wenye pepo

Sasa tukirudi kwenye habari hiyo tunaona Injili ya Mathayo na Marko inaonyesha kuwa wale wahalifu wawili walimdhihaki  Bwana Yesu akiwa pale msalabani, bila upingamizi wowote . Lakini Injili ya Luka inaonyesha mmoja ndiye aliyemtukana lakini yule mwingine alimwomba rehema.

Kabla hatujalijibu swali, Tukumbuke kuwa Bwana Yesu alikuwa pale msalabani kwa muda mrefu sana usiopungua masaa 6, na wakati huo wote, wale wahalifu waliosulibiwa naye walikuwa wanautazama mwitikio wake, alipokuwa katika hali kama ya kwao, ni wazi kuwa  mwanzoni wote walidhani Yesu ni kama mmojawapo wa wahalifu wenzao, na hiyo haikuwa shida wote kutoa kauli za kudhihaki na kukebehi na ndio maana injili ya Mathayo na Marko zinaonyesha kuwa wote walimkebehi..

Lakini ni wazi kuwa baadaye kidogo yule mmoja alitubu, akageuka, na hiyo ni  pengine baada ya kuona utofauti wa Yesu na matendo aliyokuwa anayaonyesha  pale msalabani, alipoona aliposhutumiwa hakurudisha majibu, alipoona anawaombea msamaha, akisema Baba wasamehe kwa kuwa hawajui watendalo, pengine hilo lilimgusa sana, alipoona upendo wake wa kipekee, japokuwa alikuwa matesoni..Hilo ndilo lililomfanya yule muhalifu mmoja ageuze mtazamo wake na kujua kabisa Kristo hakuwa na kosa lolote..

Na zaidi ya yote  alipoona mpaka giza limeingia mchana kweupe, jambo ambalo si la kawaida.. Alitubu saa ile ile na mpaka kumwambia yule wenzake sisi ni kweli tumekosea, lakini huyu hakufanya kosa lolote linalomstahili yeye kuuawa. Ee Yesu unikumbuke katika ufalme wako.

Ni kitu gani tunajifunza?

Hiyo inatuonyesha uvumilivu wa Mungu jinsi ulivyo kwa wenye dhambi. Hata wewe mwenye dhambi Inawezekana  umekuwa ukimdhihaki Mungu mara nyingi, ukizipuuzia njia zake na kuziona ni za watu waliorukwa na akili mara nyingi, hata umefikia hatua ya kuutukana wokovu waziwazi na Mungu mwenyewe., lakini bado Mungu anakupa nafasi ya kutubu leo. Lakini nafasi hiyo haitadumu milele. Kumbuka wahalifu wale wote walikufa baada ya muda mfupi, lakini mpaka sasa tunaongea mmoja yupo peponi mwingine yupo motoni.

Yule aliye motoni alipuuzia wokovu mpaka dakika ya mwisho hakujua kuwa hana muda mrefu wa kuishi. Swali ni Je! Wewe pia unatambua muda uliobakiwa nao hapa duniani? Kama hufahamu ni kwanini basi bado upo kwenye dhambi? Hivyo tubu leo Yesu akuokoe akuoshe dhambi zako, ufanyike mtoto wake kweli kweli. Hizi ni nyakati za mwisho. Majira haya ni ya kumalizia. Hivyo usiruhusu, dhambi iendelee kuwa sehemu ya maisha yako.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Je! ile habari ya watu wawili wenye pepo inajichanganya?

Wevi na wanyanga’anyi waliomtangulia Yesu walikuwa ni wapi?

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

USIIGEUZE NYUMBA YA MUNGU KUWA PANGO LA WANYANG’ANYI.

UFUNUO: Mlango wa 11

Rudi Nyumbani:

Print this post

Shekina ni nini? Na Je! Utukufu wa shekina unamaana gani?

Shekina au Shekhinah / schechinah, Ni neno la kiyahudi linalomaanisha, “kutua” au “kuweka makao” au “makazi” ya uwepo wa Mungu duniani. Hivyo utukufu wa Shekina maana yake ni kujifunua kwa uwepo wa Mungu kwa dhahiri duniani, ambapo kuonekana kwake kunaweza kuchukua mfumo wa vitu mbalimbali vya asili , kama vile moto, wingu,moshi,mwanga, kijiti kinachoteketea n.k.,..

Neno hili huwezi kulikuta kwenye biblia, lakini maudhui yake ipo ndani ya biblia. Ni neno lililoanzishwa,  na waalimu wa kiyahudi , (Marabi) , na yalionekana  kwenye fasihi zao na maandishi yao ya kale, kipindi cha pale katikati kutoka agano la kale kuelekea agano jipya..

  • Mara ya kwanza utukufu wa Shekina kuonekana ilikuwa ni siku ile wana wa Israeli walipokuwa wanatoka Misri, kuelekea Jangwani walipokuwa pale Sukothi, siku hiyo ndio ilikuwa mara yao ya kwanza kuuona uwepo wa  Mungu dhahiri katika wingu na nguzo ya moto,

Kutoka 13:20 “Nao wakasafiri kutoka Sukothi, wakapiga kambi Ethamu, kwenye mpaka wa ile jangwa.

21 Bwana naye akawatangulia mchana ndani ya wingu mfano wa nguzo, ili awaongoze njia; na usiku, ndani ya moto mfano wa nguzo, ili kuwapa nuru; wapate kusafiri mchana na usiku;

22 ile nguzo ya wingu haikuondoka mchana, wala ile nguzo ya moto haikuondoka usiku, mbele ya hao watu”.

  • Ulikuja kuonekana tena ndani ya hema ya kukutania, kule jangwani;  Soma (Walawi 16:2, 1Wafalme 8:10-11)
  • Ulikuja kuonekana tena Hekaluni, kipindi kile ambacho Sulemani analiweka wakfu hekalu la Bwana (1Wafalme 8:10-11)
  • Ulionekana tena siku ile Mungu alipomthibitishia Ibrahimu agano lake alipokuwa amelala, na moto ukashuja juu ya madhabahu,aliyokuwa ameitengeneza, Mwanzo 15:17
  • Ulionekana pia kwa Ayubu wakati ule Mungu alipomtokea katika upepo wa kisulisuli na kuzungumza naye dhahiri (Ayubu 38-42)
  • Katika agano jipya tunaona ulionekana kwa Paulo siku ile alipokuwa anatoka Yerusalemu na kuelekea Dameski ili kuliharibu kanisa la Mungu, ndipo utukufu wa Mungu ukamtokea katika mwanga mkali na Kristo kuongea naye.. Matendo 9:3
  • Na utaonekana pia katika ile Yerusalemu mpya ambayo  tunayoingojea huko mbeleni (Ufunuo 21:23-)

Nakadhalika, na Kadhalika..

JE! NA SISI TUNAWEZA KUKUTANA NA UTUKUFU WA SHEKINA?

Pamoja na kwamba Mungu alijifunua dhahiri katika vitu vingi vya asili, kwa watu wachache, lakini kuna wakati ambao aliuweka mahususi kwa ajili ya kujifunua kwa watu wote, katika viwango vya juu kabisa vya utukufu wake ambao havijawahi kutokea hapa duniani.. Utukufu ambao ni zaidi ya wingu, au nguzo ya moto, au moshi, au tufani..na huo sio mwingine zaidi ya mwili wa Mwanadamu, ulioitwa YESU KRISTO. Biblia inatuambia kabisa kuwa Yesu alikuwa ni Mungu mwenyewe aliyechukua umbo la kibinadamu na kuishi na sisi (1Timotheo 3:16)

Na yeye ndiye utukufu pekee wa Mungu ambao  alishawahi kufunua hapa duniani tangu dunia iumbwe..

Yohana 1:14 “Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli”.

Soma tena..

Wakolosai 2:9 “Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili”.

Hivyo kwa kifupi tunaweza kusema utukufu wa shekina tulionao sasa ni YESU KRISTO. Na kila mmoja wetu ameweza kumwona Mungu zaidi hata ya wale waliotokewa katika nguzo ya moto, ikiwa tu atakubali kuingia katika neema yake..

Swali ni Je! Utukufu huo umefunuliwa ndani yako? Je Umempokea Yesu katika maisha yako?. Kumbuka hakuna njia yoyote utakayoweza kumfikia Mungu, au hata kumjua Mungu isipokuwa kwa njia ya Yesu Kristo. Jiulize, ulimwengu umekuahidia nini tangu umeanza kuutumikia? Ukweli ni kwamba haujakupa ahadi yoyote, ya kuendelea kuishi, Lakini Kristo anakuahidia uzima wa milele baada ya kufa, kwanini usichague uzima, na mengine mengi?

Kama upo tayari leo hii kuyakabidhi maisha yako kwa Yesu, ili utukufu huu halisi wa Shekina ukujue juu yako, basi huo ni uamuzi wa busara sana kwako. Ikiwa jibu ni ndio, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba na kupokea maagizo mengine.>>>  SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312/ +255 693036618

Mada Nyinginezo:

JINA LA MUNGU NI LIPI?

VIGEZO VYA KUWA KARIBU NA YESU KRISTO KATIKA ULIMWENGU UJAO.

LIPO LA KUJIFUNZA KWA WALE MASHUJAA 37 WA DAUDI.

TUMEPEWA AMRI YA KUKANYAGA NGE NA NYOKA.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

LIPO LA KUJIFUNZA KWA WALE MASHUJAA 37 WA DAUDI.

Kama vile Daudi alivyokuwa shujaa, vivyo hivyo yeye naye alikuwa na mashujaa wake wengine 37 waliokuwa chini yake wakimzunguka wakati wote,walipokuwa vitani kushindana na maadui zao .

Kwa ufupi mashujaa hao waligawanyika katika makundi makuu matatu (3), Kundi la kwanza lilikuwa na mashujaa watatu wa juu, kundi la pili lilikuwa na mashujaa wawili, na kundi la tatu lilikuwa na mashujaa wengine thelathini na mbili.

Hilo kundi la kwanza la juu lenye mashujaa watatu,.mtu wa kwanza aliitwa Yashobeamu Mhakmoni, mwingine ni Eleazari na wa mwisho ni Shama.. Hawa walikuwa mashujaa kweli kweli, na kundi la chini yake kidogo alikuwepo mtu mmoja aliyeitwa Abishai na mwingine ni Benaya, hawa nao walikuwa ni mashujaa sana, halafu lile kundi la mwisho, ndio alikuwepo Uria Mhiti, na wengine, yule ambaye Daudi alimtamani mke wake, hivyo akamweka kwenye vita vikali ili auwe kisha amchukue mke wake.. Huyu alikuwa mmojawapo wa wale wengine..

Sasa embu tuwatazame baadhi ya matendo ya mashujaa hawa kwa ufupi mambo waliyoyafanya, kisha mwishoni tutapata somo la kujifunza..

1) Yashobeamu Mhakmoni:

Huyu ndio Yule shujaa wa juu zaidi ya wote, katika vita alifanikiwa kuwaua wanajeshi 800 kwa mkuki wake mmoja, Jaribu kutengeneza picha mtu mmoja anaua watu 800, huyo ni shujaa kweli kweli mfano wa Samsoni,(2Samweli 23:8)

2) Eleazari, mwana wa Dodai.

Huyu naye alifanya mambo ya kustaajabisha, walipokuwa wamekusanyika ili kupigana na wafilisti kule kondeni, Israeli wote wakakimbia akabaki yeye peke yake na Daudi tu, lakini alinyanyuka na kuwapiga wafilisti, wengi kiasi kwamba hadi mkono wake ukachoka kuua, hata alipojaribu kuuachia upanga mkono wake bado umeshikamana na upanga, tu, (1Nyakati 11:12)

2Samweli 23:9 Na baada yake kulikuwa na Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu waliokuwa pamoja na Daudi; walipowatukana Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko ili kupigana, na watu wa Israeli walikuwa wamekwenda zao;

10 huyo aliinuka, akawapiga Wafilisti hata mkono wake ukachoka, na mkono wake ukaambatana na upanga; naye Bwana akafanya wokovu mkuu siku ile; nao watu wakarudi nyuma yake ili kuteka nyara tu.

3) Shama, mwana wa Agee.

Huyu naye alikuwa kwenye mashamba ya midengu pamoja na waisraeli wengine, lakini wafilisti walipotokea wakakimbia, akabaki yeye tu peke yake kondeni, akapigana na wafilisti wengi sana akawaua yeye peke yake, hivyo akafanikiwa kulilinda lile shamba la midengu lisichukuliwe na wafilisti.(2Samweli 23:11-12)

  1. Mwingine aliitwa Abishai, nduguye Yoabu,

Aliwaua kwa wakati mmoja watu 300 kwa mkuki wake,(2Samweli 23:18)

II. Benaya, mwana wa Yehoyada:

Aliwaua majitu mawili wa Kimoabu, pia alimuua simba katikati ya pango, vilevile alimuua Mmisri ambaye alikuwa mrefu sana mfano wa Goliathi, kwa kutumia silaha ya adui yake.

2Samweli 23:20…..”aliwaua simba wakali wawili wa Moabu, pia akashuka akamwua simba katikati ya shimo wakati wa theruji.

21 huyo naye akamwua Mmisri, mtu mrefu; naye huyo Mmisri alikuwa na mkuki mkononi; lakini yeye alimshukia na gongo, akamnyakulia Mmisri mkuki mkononi mwake, akamwua kwa mkuki wake mwenyewe”.

III. Mwingine ni Elhanani ambaye alimwangusha Goliathi, mfano wa yule aliyeangushwa na Daudi.

2Samweli 21:19 “Kulikuwa na vita tena na Wafilisti huko Gobu; na Elhanani, mwana wa Yairi, Mbethlehemi, alimwua Goliathi, Mgiti, ambaye mti wa mkuki wake ulikuwa kama mti wa mfumaji.

20 Kulikuwa na vita tena huko Gathi; ambako kulikuwa na mtu mrefu sana, mwenye vidole sita katika kila mkono, na vidole sita katika kila mguu, jumla yake ishirini na vinne; yeye naye alizaliwa kwa Mrefai.

21 Naye huyo alipowatukana Israeli, ndipo Yonathani, mwana wa Shama, nduguye Daudi, akamwua.

22 Hao wanne walizaliwa kwake huyo Mrefai wa Gathi; wakaanguka kwa mkono wa Daudi, na kwa mikono ya watumishi wake.

IV. Na mashujaa wengine ambao walifanya matendo ya kishujaa unaweza kuwasoma katika..2Samweli 23:14-17..

Lakini tunavyousoma ushujaa wao watu hawa, tunaweza kujiuliza Daudi aliwatolea wapi? Je aliwaiba katikati ya jeshi la Sauli?, au alienda kuwatafuta miongoni mwa watu waliokuwa na nguvu sana Israeli? Jibu ni la!

Mashujaa hawa 37, Daudi aliokuwa nao, hakuwatoa katikati ya kambi za kivita, bali walikuwa ni watu wa kawaida sana wasiokuwa na uelekeo wowote wa ki maisha, watu hohe-hahe tu, watu waliokuwa katika umaskini, wenye dhiki nyingi, wenye madeni, watu dhaifu, watu wasio na raha moyoni, ndio waliokusanyika wakawa pamoja na Daudi, na kati ya hao ndio likanyanyuka wimbi kubwa la mashujaa namna ile ambao waliogopeka na majeshi makubwa yaliyokuwepo wakati ule.

1Samweli 22:1 “Basi Daudi akaondoka huko, akakimbilia pango la Adulamu; na ndugu zake na watu wote wa mbari ya baba yake waliposikia habari hiyo, wakamwendea huko.

2 Na kila mtu aliyekuwa katika hali ya dhiki, na kila mtu aliyekuwa na deni, na watu wote wenye uchungu mioyoni mwao, wakakusanyika kwake; naye akawa jemadari wao; nao waliokuwa pamoja naye walipata kama watu mia nne”.

Sasa Daudi ni mfano wa Kristo, hata sasa Bwana anao mashujaa wake wa Injili, na bado anaendelea kuwatafuta, lakini maandiko yanatuambia mashujaa hao hawatafuti katikati ya watu wenye vyeo, watu matajiri, watu wenye ujuzi mwingi, badala yake anawatafuta katikati ya watu wasiokuwa na uelekeo wowote, watu wa kawaida sana…

1Wakoritho 1:26 “Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa;

27 bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu;

28 tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko;

29 mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu”.

Unaona, hivyo ndugu.. Mimi na wewe tunayo nafasi sana kubwa ya kuwa mashujaa wa Kristo ikiwa tu tutakubali kuambatana naye, hilo tu, umaskini wako sio kigezo, madeni yako sio sababu, dhiki zako sio sababu za wewe kutokuwa shujaa wa Bwana. Usije ukasema ooh! Mimi nilikuwa sina pesa ndio maana nikashindwa kukutumikia..Siku ile mashujaa kama hao watatuhukumu.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 10 (Kitabu cha Zaburi).

Jina la Bwana wetu na Mwokozi wetu, Yesu Kristo libarikiwe…Karibu katika kuyatafakari maandiko, tumekwisha kuvipitia vitabu kadhaa vya Mwanzo, naomba kama hujavipitia na ungependa kuvipitia, basi fungua hapa >> VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Leo kwa neema za Bwana tutasonga mbele kitabu kingine kimoja, ambacho ni kitabu cha Zaburi.

Kitabu cha Zaburi ndio kitabu kirefu kuliko vitabu vyote katika biblia, na ndio kitabu ambacho kipo katikati ya Biblia. Sehemu kubwa ya kitabu hichi imeandikwa na Mfalme Daudi, mwana wa Yese.  Lakini sio Milango yote imeandikwa na Daudi, la!..milango mingine imeandikwa na Sulemani, Mfalme Hezekia, Asafu,Musa, Ethani na Hemani.

Kitabu hichi kimeandikwa katika mfumo wa beti za nyimbo. Kwasababu maana tu ya neno lenyewe Zaburi ni “Nyimbo takatifu zilizoimbwa kwa vyombo vya muziki vya nyuzi nyuzi, kama vile santuri, kinubi na zeze”. Kama utapenda kuvijua vyombo hivyo vya nyuzi nyuzi vya muziki kwa urefu utatutumie ujumbe inbox.

Hivyo nyimbo hizi za Zaburi, ziliandikwa si kwa lengo la kuburudisha bali kwa lengo la kumshukuru Mungu, kumtukuza Mungu, kumwomba Mungu, kumsifu Mungu, kuomba ulinzi na haki .

Mfalme Daudi alizitunga nyimbo hizi katika kipindi chote cha maisha yake aliyoishi (yaani miaka 70). Hivyo hakikuandikwa kwa siku moja, au wiki moja. Kila hatua ya maisha Daudi aliyoipitia Roho ya Mungu ilishuka juu yake na kumsukuma kuandika beti za nyimbo hizo, ambazo leo tunazisoma katika biblia.

Sasa swali ni kwanini zimeandikwa katika mfumo wa Nyimbo?

Ikumbukwe kuwa Daudi tangu akiwa mdogo alikuwa na kipaji cha kupiga filimbi na kinubi..Hivyo alijifunza kumwimbia Mungu tangu akiwa mdogo, na kipaji chake hicho Mungu alichompa, kuna kipindi kilivuma mpaka hadi kikamfikia Mfalme Sauli..

1Samweli 16:14 “Basi, roho ya Bwana ilikuwa imemwacha Sauli, na roho mbaya kutoka kwa Bwana ikamsumbua.

 15 Nao watumishi wa Sauli wakamwambia, Angalia, sasa roho mbaya kutoka kwa Mungu inakusumbua.

 16 Basi bwana wetu na atuamuru sisi watumishi wake waliopo hapa mbele yako watafute mtu aliye stadi wa kupiga kinubi; basi itakuwa, roho ile mbaya kutoka kwa Mungu itakapokujilia, yeye atapiga kinubi kwa mkono wake, nawe utapona.

17 Basi Sauli akawaambia, VEMA, NITAFUTIENI MTU ALIYE STADI WA KUPIGA KINUBI, MKANILETEE.

 18 Ndipo akajibu mmoja wa watumishi wake akasema, Tazama, nimemwona mwana mmoja wa Yese, Mbethlehemi, ALIYE STADI WA KUPIGA KINUBI, tena ni mtu shujaa, hodari wa vita, anenaye kwa busara, mtu mzuri, ambaye Bwana yu pamoja naye.

19 Basi Sauli akampelekea Yese wajumbe, akasema, Nipelekee Daudi mwanao, aliye pamoja na kondoo……….

23 Ikawa, ile roho mbaya kutoka kwa Mungu ilipomjilia Sauli, NDIPO DAUDI AKAKISHIKA KINUBI, AKAKIPIGA KWA MKONO WAKE, naye Sauli akaburudishwa, na ile roho mbaya ikamwacha”.

Hivyo kipaji hicho cha kupiga vinubi na kuimba, alichokuwa nacho Daudi, aliendelea kukitumia mpaka anaondoka Duniani.

Sasa ni Mazingira gani aliyokuwa mfalme Daudi wakati anaandika hizo Zaburi.

Daudi hakuwa anakaa tu ndani, na ghafla anaanza kujikuta anaandika nyimbo hizo.  Hapana, mfano wa mazingira aliyokuwa anaandika beti hizo, ni wakati labda ametoka vitani na Mungu kampa ushindi dhidi ya maadui zake ambao pengine walikuwa ni hodari kupita wao, hivyo ile furaha anayoipata na huku anaona kama sio Mungu wasingeshinda, ile furaha inamsukuma kuandika nyimbo za kumshukuru Mungu.

Kwamfano hebu tuziangalie beti chache za Daudi katika Zaburi kasha tuzitafute ziliandikwa kipindi gani.

Tuanze na Zaburi ya 105, inasema hivi..

Zaburi 105:1 “Haleluya. Mshukuruni Bwana,liitieni jina ,Wajulisheni watu matendo yake.

2 Mwimbieni, mwimbieni kwa zaburi, Zitafakarini ajabu zake zote.

 3 Jisifuni kwa jina lake takatifu, Na ufurahi moyo wao wamtafutao Bwana.

  4 Mtakeni Bwana na nguvu zake, Utafuteni uso wake sikuzote ”

Je ni kwamba Daudi alikaa tu ndani?..na akachukua tu kalamu na karatasi kuandika ubeti huo?..Jibu ni la!..Ubeti huo uliandikwa kipindi Mfalme Daudi Analitoa sanduku la Agano kwa Obed-odemu kwenda mjini kwake yaani (Yerusalemu).. Hivyo kwa furaha kubwa wakati sanduku la agano linaingia tu mjini mwake, alicheza mpaka nguo zikamtoka, na alilisindikiza Sanduku hilo la agano, kwa nyimbo nyingi za santuri na vinubi…

Tusome…

1Nyakati 15:25 “ Basi Daudi, na wazee wa Israeli, na maakida wa maelfu, wakaenda, ili kulipandisha sanduku la agano la Bwana kutoka nyumbani mwa Obed-edomu kwa furaha kuu;

26 hata ikawa, Mungu alipowajalia Walawi waliolichukua sanduku la agano la Bwana, wakachinja ng’ombe saba, na kondoo waume saba.

 27 Naye Daudi alikuwa amevaa joho ya kitani safi, na Walawi wote waliolichukua sanduku, na waimbaji, na Kenania msimamizi wa uchukuzi, na waimbaji; naye Daudi alikuwa amevaa naivera ya kitani.

28 Ndivyo Israeli wote walivyolipandisha sanduku la agano la Bwana kwa shangwe na kwa sauti ya tarumbeta, na kwa baragumu, na kwa matoazi, wakipiga sauti kuu kwa vinanda na vinubi.

 29 Hata ikawa, sanduku la agano la Bwana lilipofika mjini kwa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani, akamwona mfalme Daudi, akicheza na kushangilia; akamdharau moyoni mwake”.

Sasa tukiendelea mlango wa 16 kuanzia mstari wa 9 ndiyo tunaiona Zaburi hiyo ya 105 ilipotokea.

Tusome..

1Nyakati 16:1 “Wakaliingiza sanduku la Mungu, na kuliweka katikati ya hema aliyoipiga Daudi kwa ajili yake; wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.

2 Na Daudi alipokwisha kuitoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani, akawabariki watu kwa jina la Bwana.

 3 Kisha akawagawia kila mtu wa Israeli, waume kwa wake, kila mtu mkate wa ngano, na kipande cha nyama, na mkate wa zabibu.

4 Akawaagiza baadhi ya Walawi kwamba watumike mbele ya sanduku la Bwana, wamfanyie ukumbusho, na shukrani, na sifa, Bwana, Mungu wa Israeli;

5 Asafu mkuu wao, na wa pili wake Zekaria, na Yeieli, na Shemiramothi, na Yehieli, na Matithiya, na Eliabu, na Benaya, na Obed-edomu, na Yeieli, wenye vinanda na vinubi; naye Asafu mwenye kupiga matoazi;

 6 nao makuhani Benaya na Yahazieli wenye baragumu daima, mbele ya sanduku la agano la Mungu.  7 Ndipo siku hiyo Daudi alipoagiza kwanza kumshukuru Bwana, kwa mkono wa Asafu na nduguze.

 8 Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; Wajulisheni watu matendo yake.

  9 Mwimbieni, mwimbieni kwa zaburi; Zitafakarini ajabu zake zote.

 10 Jisifuni kwa jina lake takatifu; Na ufurahi moyo wao wamtafutao Bwana.

 11 Mtakeni Bwana na nguvu zake; Utafuteni uso wake siku zote.

12 Zikumbukeni ajabu zake alizozifanya; Miujiza yake na hukumu za kinywa chake;

13 Enyi wazao wa Israeli, mtumishi wake, Enyi wana wa Yakobo, wateule wake.

14 Yeye, Bwana, ndiye Mungu wetu; Duniani mwote mna hukumu zake.

 15 Likumbukeni agano lake milele, Neno lile aliloviamuru vizazi elfu.  16 Agano alilofanya na Ibrahimu, Na uapo wake kwa Isaka;

17 Alilomthibitishia Yakobo kuwa amri, Na Israeli liwe agano la milele”

Umeona?..Kwahiyo Zaburi hazikutungwa tu pasipo sababu yoyote, bali zilitungwa kila baada ya tukio fulani la ki-Mungu lililotokea katika maisha ya Daudi. Zaburi zote 150, zilindikwa kwa msukumo wa Roho baada ya tukio fulani la ki-Mungu.

Zaburi nyingine Daudi aliziandika, baada ya kuokoka kimiujiza kwenye mikono ya Sauli aliyekuwa anatafuta kumuua, hivyo akaandika nyimbo hizo kumshukuru Mungu. Na sehemu kubwa ya Zaburi ya Daudi aliandika baada ya kupata ushindi dhidi ya Maadui zake (Yaani mataifa yaliyokuwa yanafanya vita dhidi ya Israeli)

Lakini pamoja na hayo nyimbo hizo za Zaburi, licha tu ni nyimbo katika mfumo wa maombi, shukrani, sifa  n.k. kwa Mungu lakini pia zina unabii ndani yake.

Na unabii wa kwanza na Mkuu ziliobeba ni unabii wa kuja kwa Masihi, yaani Yesu Kristo, na unabii wa Wana wa Israeli kuchukuliwa mateka Babeli.

  • Kitabu cha Zaburi pekee ndio kimetabiri neno la Mwisho la Bwana Yesu pale Kalvari alilosema “Mungu wangu..Mungu wangu mbona umeniacha. Kasome Zaburi 22:1, linganisha na Marko15:34”.
  • Kadhalika kitabu cha Zaburi pekee ndicho kilichotabiri usaliti wa Yuda, hakuna kitabu kingine kilichozungumzia usaliti wa Yuda zaidi ya hichi cha Zaburi..

Zaburi 41:9 “Msiri wangu tena niliyemtumaini, Aliyekula chakula changu, Ameniinulia kisigino chake”. Linganisha na maneno ya Bwana Yesu katika Yohana 13:18

Yohana 13:18  “Sisemi habari za ninyi nyote; nawajua wale niliowachagua; lakini andiko lipate kutimizwa, Aliyekula chakula changu Ameniinulia kisigino chake”.

  • Pia kitabu hichi ndio kitabu pekee kilichotabiri juu ya mavazi ya Yesu kupigiwa kura na wale askari pale msalabani…

Zaburi 22:18 “Wanagawanya nguo zangu, Na vazi langu wanalipigia kura”…Linganisha na Mathayo 27:35

  • Kitabu cha Zaburi  pia ndio kitabu pekee kilichotabiri kufufuka kwa Bwana Yesu, na kwamba Kristo hataona uharibifu soma..Matendo 2:27-33. Hakuna kitabu kingine chochote kilichotabiri kufufuka kwa Yesu, hata kitabu cha Isaya hakikutabiri.

Hivyo kitabu hiki kwa sehemu kubwa kimebeba Ufunuo juu ya Yesu..Ndio maana Baada ya Yesu kufufuka alitaja kuwa yote aliyoandikiwa katika Zaburi na torati lazima yatimie..

Luka 24:44  “Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika Manabii na Zaburi”

Mbali na hayo, Kitabu cha Zaburi kinatufundisha Mambo yafuatayo.

  • Kuomba: Zab. 51 ni mfano wa zaburi inayotufundisha sisi namna ya kuomba na kujisongeza mbele za Mungu kwa unyenyekevu.
  • Kumshukuru Mungu:
  • Kumsifu Mungu; Kwamba tunapaswa tumsifu Mungu sio tu kwa midomo mikavu bali kwa kumwimbia kwa vinanda vya nyuzi kumi, na vinubi na santuri…Kwa nyakati zetu hizi ni kwa kutumia vyombo vyote vya muziki kama guitar,vinanda, matarumbeta, piano n.k. na kwa nguvu sana pamoja na vigelegele vya shange na nderemo.(Soma Zab.33:2, Zab 144:9).
  • Kumtegemea Mungu, na kutohofu chochote: “ Zab. 23:4 Nijapopita kando ya bonde la uvuli wa mauti sitaogopa mabaya kwa maana wewe upo pamoja nami” na “Zab. 27:1 Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? Bwana ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nao

Bwana akubariki.

Usikose mwendelezo wa vitabu vinavyofuata…

Maran atha!

Kwa maombezi/ Ushauri/ Ratiba za Ibada/Maswali/ Whatsapp/ Piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

UFUNUO: Mlango wa 1

MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.

NA BAADA YA LILE TONGE, SHETANI AKAMWINGIA.

REKEBISHA YAFUATAYO ILI MAMBO YAENDE SAWA.

JINSI YA KUEPUKA KUUMIZWA MOYO KUSIKOKUWA NA SABABU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Bahari mbalimbali zilizoorodheshwa kwenye biblia.

Biblia inaziorodhesha bahari kuu nne, tuzisome;

1 ) Bahari ya shamu: Kwa sasa inajulikana kama bahari nyekundu, (Kwa kiingereza red sea). Hii ni ile bahari ambayo wana wa Israeli waliivuka baada ya Mungu kuipasua pale walipokuwa wanafuatiliwa na maadui zao, ambapo tunaona baadaye walikuja kumezwa na bahari ile.

bahari ya shamu

Kutoka 15:22 “Musa akawaongoza Israeli waende mbele kutoka Bahari ya Shamu, nao wakatokea kwa jangwa la Shuri; wakaenda safari ya siku tatu jangwani wasione maji”.

2) Bahari kubwa , au bahari ya Wafilisti, (Kutoka 23:31): Kwasasa inajulikana kama habari ya Mediteranea. Ipo upande wa Magharibi wa taifa la Israeli. Hii ndio bahari kubwa kuliko zote zinazoorodheshwa kwenye biblia.

bahari kubwa, ya wafilisti, au mediterenia

Hesabu 34:6 “Kisha mpaka wenu wa upande wa magharibi mtakuwa na bahari kubwa na mpaka wake; hii ndiyo mpaka wenu upande wa magharibi”.

Soma pia Yoshua 9:1, 15:47, 23:4, Ezekieli 47:19

3) Bahari ya Galilaya; Au kwa jina lingine Bahari ya Tiberia, au ziwa la Genesareti au Bahari ya Kinerethi Yoshua 12:3, 13:27, 34:11. Hii ndio ile bahari ambayo Bwana Yesu alitembea juu ya maji.

bahari ya galilaya

Luka 5:1 “Ikawa makutano walipomsonga wakilisikiliza neno la Mungu, yeye alikuwa amesimama kando ya ziwa la Genesareti,”

Mathayo 4:18 “Naye alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galilaya, aliona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea nduguye, wakitupa jarife baharini; kwa maana walikuwa wavuvi”.

4) Bahari ya chumvi: Hii ni habari ndogo sana, ambapo ipo chini ya mto Yordani, maji yake ni ya chumvi nyingi sana, jambo ambalo linaifanya bahari hiyo isiwe na kiumbe wa kuishi ndani yake kama samaki, sehemu nyingine wanaiita ‘bahari mfu’(Dead Sea)

bahari ya chumvi

 Hesabu 34:3 “ndipo upande wenu wa kusini utakuwa tangu bara ya Sini kupita kando ya Edomu, na mpaka wenu wa kusini utakuwa tangu mwisho wa Bahari ya Chumvi kuelekea mashariki”;

 Kumbukumbu 3:17, Yoshua 15:2.

Shalom, tazama maeneo mengine mbalimbali ya biblia chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Mto Frati upo nchi gani, Umuhimu wake katika biblia ni upi?

MTO YORDANI UKO NCHI GANI KWA SASA?

Sharoni ni nini au ni wapi kibiblia?(1Nyakati 5:16)

JIEPUSHE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Sharoni ni nini au ni wapi kibiblia?(1Nyakati 5:16)

Maana ya Neno Sharoni ni “uwanda” au “nchi tambarare”. Katika biblia, tunaona lipo eneo (wilaya) lililojulikana sana na waisraeli kama Sharoni, japokuwa biblia haijatolea maelezo yake mengi, Lakini ni eneo lililokuwa na rubuta nyingi, na lilikuwa lipo karibu na fukwe za ile bahari kubwa(yaani bahari ya Mediterenia), tazama ramani.

Utalisoma Neno hilo kwenye vifungu hivi vya biblia;

1Nyakati 5:16 “Nao wakakaa huko Gileadi, katika Bashani, na katika miji yake, na katika viunga vyote vya Sharoni, hata kufika mipakani mwake”.

1Nyakati 27:29 “na juu ya makundi ya ng’ombe waliolishwa katika Sharoni alikuwa Shitrai, Msharoni; na juu ya makundi waliokuwamo mabondeni alikuwa Shafati mwana wa Adlai”;

Isaya 33:9 “Nchi inaomboleza, na kulegea; Lebanoni imetahayarika na kunyauka; Sharoni imekuwa kama jangwa; Bashani na Karmeli zimepukutika majani”.

Isaya 65:10 “Na Sharoni itakuwa zizi la makundi ya kondoo, na bonde la Akori mahali pa kulala makundi ya ng’ombe, kwa ajili ya watu wangu walionitafuta”.

Na katika agano jipya utalisoma katika kifungu hichi;

Matendo 9:35 “Na watu wote waliokaa Lida na Sharoni wakamwona, wakamgeukia Bwana”.

UA LA UWANDANI

Lakini tukisoma kitabu cha wimbo ulio bora, tunaona, lipo Ua moja linatajwa kama Ua la Uwandani, au kwa jina lingine Ua la Sharoni (Rose of Sharon). Mwandishi wa kitabu hichi, anajifananisha yeye na Ua hilo ambalo limechipuka katika nchi hiyo ya Sharoni.

Wimbo 2:1 “Mimi ni ua la uwandani, Ni nyinyoro ya mabondeni.

2 Kama nyinyoro kati ya miiba, Kadhalika mpenzi wangu kati ya binti”.

Na bila shaka Ua hili ni Kristo, yeye ndiye aliyechipuka katika bonde la ulimwengu, na uzuri wake, na mwonekano wake ulikuwa ni tofauti na mwanadamu yoyote ulimwenguni. Yeye ndiye aliye Nuru ya ulimwengu, yeye ndiye aliyeiondoa harufu mbaya ya huu ulimwengu wa dhambi, hata tukapata kibali cha kumkaribia Mungu, yeye ndiye mwokozi wa ulimwengu.

Je! Na wewe umeliona Ua hilo?, Je umempata mwokozi moyoni mwako? Kumbuka hakuna njia nyingine yoyote utakayoweza kumfikia Mungu isipokuwa kwa njia yake yeye. Hakuna mwanadamu yoyote anayeweza kumpendeza Mungu kwa nguvu zake mwenyewe isipokuwa Yesu Kristo peke yake. Ukimkosa Kristo maishani mwako, haijalishi umepata ulimwengu mzima, hesabu kuwa umepoteza kila kitu. Lakini ukimpokea yeye, hata ukikosa vyote hesabu kuwa umevipata vyote.

Uamuzi ni wako,  kumbuka hizi ni siku za mwisho, Lakini ikiwa leo utapenda kuyakabidhi maisha yako kwake, Huo utakuwa ni uamuzi wa busara sana, Basi fungua hapa kwa ajili ya maelekezo ya Toba>>>  SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Uwanda wa dura ni nini?

Konde la Soani ni nini? (Zaburi 78:12,43)

Bisi ni nini? (Walawi 23:14, Ruthu 2:14)

Jaa ni nini katika biblia?

IKO NJIA IONEKANAYO KUWA SAWA MACHONI PA MTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

LANGO LIMEBADILIKA.

Ezekieli 44:1 “Kisha akanirudisha kwa njia ya lango lile la nje, la mahali patakatifu lililoelekea upande wa mashariki; nalo lilikuwa limefungwa.

2 Bwana akaniambia, Lango hili litafungwa, halitafunguliwa, wala mtu awaye yote hataingia kwa lango hili, kwa maana Bwana, Mungu wa Israeli, ameingia kwa hilo; basi kwa sababu hiyo litafungwa”.

Shalom,

Kwa jinsi tunavyozidi kuishi hapa duniani ndivyo dunia inavyozidi badilika kwa kasi sana mbele ya macho yetu, na haibadiliki kuelekea pazuri, bali inabadilika kuelekea pabaya..Inabadilika kuelekea kwenye maovu mengi zaidi…Maovu ya jana ni heri kuliko ya leo…Na hiyo ndiyo inayopelekea wokovu kuwa mgumu kupatikana mioyoni mwa watu siku baada ya siku.

Ukitazama mistari hiyo, ambayo iliandikwa katika agano lake, na nabii Ezekieli inazungumzia juu ya unabii wa Masihi siku atakapokuja na kuingia hekaluni kupitia lango la mashariki, unabii huo upo mwilini na rohoni, lakini lengo leo sio kuzungumzia habari hizo .. Nachotaka uone ni huyo ujumbe uliopo hapo, kwamba, hilo lango lipo wazi lakini siku moja litafungwa, na likishafungwa kamwe halitakaa lifunguliwe tena daima.. Huo ndio ujumbe, Na wote tunajua kuwa lango hilo ni Neema ya wokovu.

Sasa   tukirudi kipindi cha agano jipya, tunaona  tena Yesu akilitaja lango hilo, lakini safari hii yeye halitaji tena kama “Lango”Kana kwamba ni kubwa sana.. bali analitaja kama mlango, na tena sio mlango tu, bali ni mlango mwembamba sana..tusome..

Luka 13:24 “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze

25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango,…..”.

Unaona? Sasa utajiuliza ni nini kimetokea mpaka sio lango tena bali ni mlango?

Ni kwasababu majira yanabadilika, Mlango wa mbinguni tangu zamani, Mungu aliukusudia uwe mpana ili watu wote waingie na ndivyo ulivyo, alikusudia uwe mwepesi kwa watu wote na mataifa yote kuuingia, ni LANGO pana sana. Hilo ndio lengo la Mungu hata sasa, Mungu hawezi kumminya mtu kwa makusudi kwamba akipate kile kitu kwa shida, sasa atufanyie hivyo ili iweje?.

Lakini kutokana na maovu na mambo mengi yaliyopo ulimwenguni sasa imepelekea mlango huu kuwa mwembamba sana, na hyo ni kutokana na kuzuka kwa milango mingine mingi sana ya upotevuni, na watu wamekuwa wakiiangalia kwa hiyo, na kusahau lile lango moja tu la Mungu.

Ndugu yangu, hizi ni nyakati mbaya sana tunazoishi, leo utaudharau wokovu wa Yesu Kristo, lakini alishatabiri kuwa kuna siku ataufunga mlango huu, na siku hiyo utakapofungwa ndipo watu watakapogundua kuwa walikuwa wanapuuzia kitu cha msingi sana, cha uzima wa roho zao.. Ndipo watakapoanza kubisha wafunguliwe, kumbe hawakujua  kuwa lango hilo likishafungwa mara moja, halitafunguliwa tena daima. Kitakachofuata baada ya hapo ni matujo makubwa sana ambayo hayajawahi kutokea duniani kote.

Luka 13:24 “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.

25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;

26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.

27 Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.

28 Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje.

29 Nao watakuja watu toka mashariki na magharibi, na toka kaskazini na kusini, nao wataketi chakulani katika ufalme wa Mungu.”

Hivyo wokovu sio wa kukwepwa, injili si ya kudharauliwa wala kupuuziwa kabisa, huu si wakati wa kumwangalia jirani, au ndugu, au mzazi, katika suala lako la wokovu, Ni wakati wa kumkimbilia Kristo na kumwangalia yeye tu, kwasababu muda uliobakia ni mchache, nani ajuaye lango hilo litafungwa leo usiku, au kesho asubuhi. Jiulize Unyakuo ukipita leo halafu ukabaki, na injili zote hizo ulizosikia, na mafundisho yote hayo uliyofundishwa na kujifunza, utaenda kujibu nini mbele ya kiti cha hukumu.

Usikubali kusongwa na jambo lolote, huu mlango umeshakuwa finyu sana.  Kuiingia sio mrahisi tena kama tunavyodhani, hivyo  ni wakati wa kufanya maamuzi magumu, wa kukubali kujitwika msalaba na kumfuata Yesu, na uwe tayari kwenda kubatizwa na  kupokea Mtakatifu.

Bwana akubariki sana.

Ikiwa bado hujabatizwa, na utapenda kupata huduma hiyo ya ubatizo, au kumpa Kristo maisha yako, basi wasiliana nasi inbox au kwa namba hizi +255789001312


Mada Nyinginezo:

Biblia inamaana gani kusema;aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi?

Mlango uitwao “Mzuri” Unaozungumziwa katika Matendo 3:2 ndio upi?

Naomba kujua watakaoenda mbinguni je! ni wengi au wachache?

NI NANI ANAYEUFUNGA MLANGO WA MAARIFA?.

YONA: Mlango 1

Rudi Nyumbani:

Print this post