Title May 2024

Siri za Mungu ni zipi? (1Wakorintho 4:1)

Swali: Biblia inataja siri za Mungu katika 1Wakorintho 4:1, je hizi siri ni zipi na zipo ngapi?

Jibu: Turejee,

1Wakorintho 4:1 “Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu”

Awali ya yote tujue maana ya uwakili unaozungumziwa hapo?…. Uwakili unaozungumziwa hapo sio mfano wa ule wa “mahakamani” La! bali unamaanisha “Usimamizi”… Kibiblia mtu aliyepewa usimamizi wa nyumba au kazi Fulani, aliitwa “Wakili”..soma Luka 12:43-48 na Luka 16:1-13

Hivyo hapo Mtume Paulo, aliposema “.. sisi ni mawakili wa siri za Mungu” maana yake “wameweka kuisimamia nyumba ya Mungu kwa kuzifundisha siri za Mungu”….Kwa urefu Zaidi kuhusu Uwakili katika biblia fungua hapa >>> Wakili ni nani kibiblia? Uwakili ni nini?

Sasa tukirudi katika swali letu, SIRI ZA MUNGU NI ZIPI na ZIPO NGAPI?

Jibu ni kwamba “SIRI ZA MUNGU” zimetajwa MBILI TU (2), katika biblia. Ambazo ni 1)YESU NI MUNGU.   2) MATAIFA NI WARITHI WA AHADI ZA MUNGU… Tutazame moja baada ya nyingine.

  1.YESU NI MUNGU.

Wakolosai 2:2 “ili wafarijiwe mioyo yao, wakiunganishwa katika upendo, wakapate utajiri wote wa kufahamu kwa hakika, WAPATE KUJUA KABISA SIRI YA MUNGU, YAANI, KRISTO;

3  ambaye ndani yake yeye HAZINA ZOTE ZA HEKIMA NA MAARIFA ZIMESITIRIKA”.

Kwanini au kivipi “KRISTO” ni “SIRI YA MUNGU”?.. Kwasababu ndani yake hazina zote na hekima na maarifa zimesitirika..maana yake yeye ndio kila kitu, NDIYE MUNGU MWENYEWE katika mwili wa kibinadamu!!!!..Kiasi kwamba laiti Pilato angelijua hilo, asingeruhusu hukumu ipite juu yake, laiti wale makuhani na maaskari wangelijua hilo wasingepitisha misubari katika mikono yake na miguu yake, lakini walifumbwa macho ili tupate wokovu.

1Wakorintho 2:7 “bali twanena hekima ya Mungu KATIKA SIRI, ile hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiazimu tangu milele, kwa utukufu wetu;

8  AMBAYO WENYE KUITAWALA DUNIA HII HAWAIJUI HATA MMOJA; MAANA KAMA WANGALIIJUA, WASINGALIMSULIBISHA BWANA WA UTUKUFU”.

Siri hii ya kwamba KRISTO NI MUNGU, inaanzia katika Isaya 9:6, na kisha Yohana 1:1, Yohana 14:9, Yohana 20:28, Tito 2:13, 1Timotheo 3:16 na Ufunuo 22:13-13.

Siri ya Bwana YESU Kuwa MUNGU, inajulikana pia kama “Siri ya Utauwa/Uungu” ambayo Mtume Paulo aliitaja katika 1Timotheo 3:16..

1Timotheo 3:16 “Na bila shaka SIRI YA UTAUWA NI KUU. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu”.

Kwahiyo BWANA YESU KRISTO ni MUNGU ALIYEDHIHIRISHWA KATIKA MWILI, na wote tunaomwamini tunapaswa tuwe mawakili wa SIRI HIYO, Maana yake “KUIAMINI na KUIHUBIRI KWA WENGINE, wasiofahamu” .

  2. MATAIFA NI WARITHI WA AHADI ZA MUNGU.

Hii ni Siri ya pili (2) ambayo ilifichwa kwa vizazi vingi, lakini ikaja kufunuliwa baada ya KRISTO kupaa juu mbinguni.. Tangu wakati wa Musa mpaka wakati wa Yohana, manabii wote na wayahudi wote walikuwa wanajua na kuamini kuwa “hakuna namna yoyote, wala njia yoyote” itakayofanyika kwa watu wa mataifa wakubaliwe na MUNGU.

Wote walijua Taifa Teule la Mungu ni ISRAELI peke yake, na mataifa mengine yote ni watu najisi, lakini baada ya Bwana YESU kuondoka alianza kumfunulia Petro siri hiyo kuwa hata mataifa ni warithi sawa tu na wayahudi, kupitia msalaba wake (Bwana YESU).. Na alimfunulia siri hiyo wakati ule alipokwenda nyumbani kwa Kornelio aliyekuwa mtu wa mataifa (Matendo 10)..

Na baadaye Bwana YESU akaja kumfunulia Mtume Paulo siri hiyohiyo kuwa Mataifa nao ni warithi, tena wa ahadi moja na wayahudi, hivyo wanastahili injili, na kuhubiriwa habari njema..

Waefeso 3:5 “Siri hiyo hawakujulishwa wanadamu katika vizazi vingine; kama walivyofunuliwa mitume wake watakatifu na manabii zamani hizi katika Roho;

6  YA KWAMBA MATAIFA NI WARITHI PAMOJA NASI WA URITHI MMOJA, NA WA MWILI MMOJA, NA WASHIRIKI PAMOJA NASI WA AHADI YAKE ILIYO KATIKA KRISTO YESU KWA NJIA YA INJILI;

7  Injili hiyo ambayo nalifanywa mhudumu wake, kwa kadiri ya kipawa cha neema ya Mungu niliyopewa kwa kadiri ya utendaji wa uweza wake”.

Na sisi lazima tuwe wahudumu (Mawakili) wa siri hii kwamba “Wokovu ni haki ya watu wote” na Mungu anawapokea watu wote, ikiwa tu watakubali kutii na kunyenyekea mbele zake.

Kwahiyo kwa hitimisho, ni kwamba “Siri za Mungu” Si zile siri za kanisa, au zile za watumishi, au wapendwa kanisani…La! Bali ni hizo zilizotajwa hapo katika maandiko…Na kumbuka, shetani naye ana siri yake ijulikanayo kama “Siri ya Kuasi” iliyotajwa katika biblia ambayo inafanya kazi kwa kasi sana nyakati hizi…

Je umempokea YESU?..Kumbuka kipindi tulichopo ni cha Neema, lakini hii neema haitadumu milele, itafika wakati itaisha.. baada ya unyakuo hakuna neema tena, vile vile baada ya kifo hakuna Neema tena. Ni heri ukayasalimisha maisha yako kwa Bwana YESU maadamu unaishi, baada ya kifo hakuna nafasi ya pili.

Warumi 10:8 “Lakini yanenaje? Lile neno li karibu nawe, katika kinywa chako, na katika moyo wako; yaani, ni lile neno la imani tulihubirilo.

9  Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.

10  Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.

11  Kwa maana andiko lanena, Kila amwaminiye hatatahayarika

12  Kwa maana hakuna tofauti ya Myahudi na Myunani; maana yeye yule ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao;

13  KWA KUWA, KILA ATAKAYELIITIA JINA LA BWANA ATAOKOKA”

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUWA MAKINI NA MITANDAO, NI SHIMO REFU.

Hazina za gizani ni zipi? (Isaya 45:3).

SIRI YA KUASI KATIKA KANISA LA MUNGU.

UFUNUO: Mlango wa 10.

KUWA MAKINI, HATUA ZA UNYAKUO ZINAENDELEA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Adabu ni nini biblia?

Adabu, ni kitendo cha kuonyesha staha, kufuata miiko, kuonyeshaAdabu ni nini biblia? ustaarabu mzuri kwa wengine.

Adabu huonyeshwa kwa Mungu, lakini pia kwa wanadamu.

Adabu kwa Mungu.

> Ni pamoja na mwonekano wako uwapo ibadani.

 Petro alipomwona Yesu akiwa uchi alijivika vazi lake kwasababu alitambua anahitaji kuonyesha adabu kwa Mungu wake. (Yohana 21:7).

 >Ni pamoja na kuwa mtulivu: Uwapo ibadani, mazungumzo ya ovyo, yasiyo ya kiibada yaepuke, minong’ono madhabahuni kwa Mungu acha, kuchati, mizunguko zunguko, kutafuna tafutana.havihitajiki,

Adabu kwa wanadamu:

>Ni pamoja na Kuwasalimia wengine. Yesu alisema.

Mathayo 5:47  Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo? 48  Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.

>Vilevile ni pamoja na kuwasikiliza wengine, kuzuia kinywa chako kunena zaidi ya wastani (Kiasi), kuonyesha upole, kuonyesha kujali, kuonyesha maadili, na kutojishughulisha na mambo ya wengine.

Maandiko yanatufundisha tunda mojawapo la upendo ni adabu.

1Wakorintho 13:4  Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; 5  HAUKOSI KUWA NA ADABU; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya.

>Vilevile Imetoa agizo kwa wanawake wacha Mungu,kwamba pambo lao mojawapo liwe ni adabu nzuri (1Timotheo 2:9). Ambapo huusisha pia Uvaaji wako kilemba uwapo ibadani ni adabu kwa Mungu wako kwasababu maandiko yameagiza hivyo. (1Wakorintho 11:5). Kujisitiri kwako ni adabu pia.

Lakini zaidi sana imetoa  agizo kwa watawakatifu wote, tuenende kwa adabu kwa wale walio nje (1Wathesalonike 4:12).

Hivyo, sote kwa pamoja tuipe adabu nafasi maishani mwetu,ili tujengwe.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima; (Mithali 11:16)

Chamchela ni nini kwenye biblia?(Zaburi 58:9, Amosi 1:14)

UMETEKWA NA UPENDO WA KRISTO?

Rudi Nyumbani

Print this post

Heshima ni nini kibiblia?

Heshima ni kitendo cha kumpa mtu hadhi yake, au uthamani wake anaostahili. Kwa kawaida kila mwanadamu anastahili heshima. Na hivyo kama mwamini huna budi kujua jinsi ya kuigawanya heshima kulingana na mtu husika. Kwasababu ukosefu wa heshimu, kwanza ni zao la kiburi (Mithali 15:33), lakini pia hukuondolea Baraka na kibali  popote pale uendapo. Lakini pia ukitoa heshima isiyompa mtu ni kosa pia.

Warumi 13:7  Wapeni wote haki zao; mtu wa kodi, kodi; mtu wa ushuru, ushuru; astahiliye hofu, hofu; astahiliye heshima, heshima

Heshima kwa Mungu ipo wapi?

  1. Ipo katika kuliamini na kuliishi Neno lake: Si katika kulipamba jina lake, na huku hufanyi anayokuambia. Alisema. Luka 6:46  Na kwa nini mnaniita, Bwana, Bwana, walakini hamyatendi nisemayo? 47  Kila mtu ajaye kwangu, na kuyasikia maneno yangu na kuyatenda, nitawaonyesha mfano wake.
  2. Ipo katika uaminifu katika  utoaji: Mithali 3:9 Mheshimu Bwana kwa mali yako, Na kwa malimbuko ya mazao yako yote
  3. Ipo katika ibada :  Anayestahili kuabudiwa, kusujudiwa, kupigiwa magoti, kuhimidiwa ni Mungu tu peke yake, na wala si mwanadamu au kiumbe kingine pamoja naye, heshima hii inamuhusu yeye peke yake. Ufunuo 4:11 “ Umestahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kuupokea utukufu na heshima na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako, navyo vikaumbwa”

Heshima kwa Wazazi ipo wapi?

  1. Kuwasaidia. Biblia inasema kuwaheshimu wazazi ni pamoja na kuwasaidia kimahitaji (Mathayo 15:1-7)
  2. Kuwasikiliza na kushika maagizo yao: Mithali 1: 8 Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,

Heshima kwa Viongozi wako wa kiroho ipo wapi?

Kutii maelekezo yao.

Waebrania 13:17  Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi.

Heshima kwa watoto ipo wapi?.

Kutowakwaza,

Waefeso 6:4  Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana.

Heshima kwa Viongozi wa nchi.

Kutenda agizo lao.

Warumi 13:1  Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu. 2  Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu

Heshima kwa Mabwana ipo wapi?

Kuwatumikia kwa uaminifu na adabu. (Waefeso 6:5-8)

Hivyo kwa hitimisho, ni kwamba kila mwanadamu anastahili heshima, haijalishi, tajiri, au maskini, mrefu au mfupi, mgonjwa au mzima, mwenye elimu au asiye na elimu, bwana au mtumwa, ameokoka au hajaokoka. Wote ni agizo tuheshimiane.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?

CHUJIO HILI NI LA AJABU SANA!

JIWE LILILO HAI.

Rudi Nyumbani

Print this post

FUNDISHA NENO KANISANI NA NYUMBANI.

(Masomo maalumu kwa wazazi/walezi).

Ni nini unafanya kama mzazi uwapo nyumbani?.. Je maisha yako ndani ya kanisa ni sawa na yale nje ya kanisa?..Je kile unachokifanya kanisani ndicho unachokifanya nyumbani?…je nyumbani kwako ni sehemu ya kuishi tu au ni sehemu pia ya ibada?.

Kama wewe ni mwalimu kanisani, ni lazima pia uwe mwalimu nyumbani kwako…kama wewe ni kiongozi katika nyumba ya Mungu ni lazima pia uwe kiongozi katika nyumba yako, kama wewe ni mchungaji katika nyumba ya Mungu ni lazima pia uwe mchungaji katika nyumba yako mwenyewe…Ndivyo biblia inavyotufundisha.

Mitume wa Bwana YESU ni kielelezo kwetu, wao walikuwa wakihubiri Neno HEKALUNI NA NYUMBANI, kama maandiko yanavyosema, hivyo kama na sisi tumejengwa juu ya msingi wao ni lazima tufanye kama wao walivyofanya..

Matendo 5:42 “Na kila siku, NDANI YA HEKALU na NYUMBANI MWAO, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema za Yesu kwamba ni Kristo”.

Umeona?.. Si hekaluni tu!, bali hata nyumbani…. Uharibifu mkubwa shetani anauanzia nyumbani… Hivyo ni lazima uwe na AMRI, katika nyumba yako mwenyewe… Ni lazima pafanyike ibada nyumbani kila siku, ni lazima pafanyike maombi, ni lazima watoto na wengine wanaoishi katika nyumba yako wajue kuomba na kuombea wengine.

Ni lazima watoto wajifunze biblia na kufundisha biblia tangu wakiwa wadogo, ni lazima pia wajifunze kutoa.. ni lazima wote wawe wa kiroho, ni lazima uwafundishe wawe vipaumbele katika Imani wawapo shuleni, maana yake wakiwa shuleni wawe vipaumbele katika kuongoza maombi kwa wanafunzi wenzao, na kuomba vile vile kufunga… Na si kuwaacha jumapili kwa jumapili  tu wafundishwe kanisani hayo mambo..

Jenga tabia ya kuwafuatilia mienendo yao ya kiimani wakiwa mashuleni, fuatilia sifa zao za kiimani wawapo mashuleni, (na si tu taaluma yao)..wapo watoto taaluma zao zinaonekana nzuri lakini shetani kashawaharibu kitabia muda mrefu (matokeo yake yatakuja kuonekana baadaye).

Hivyo kama mzazi au mlezi, simama katika hiyo nafasi… kiasi kwamba NENO LA MUNGU nyumbani kwako ni AMRI sio OMBI!. Kama Nabii Yoshua alivyoazimia zamani zile..

Yoshua 24:15 “Nanyi kama mkiona ni vibaya kumtumikia Bwana, chagueni hivi leo mtakayemtumikia; kwamba ni miungu ile ambayo baba zenu waliitumikia ng’ambo ya Mto, au kwamba ni miungu ya wale Waamori ambao mnakaa katika nchi yao; LAKINI MIMI NA NYUMBA YANGU TUTAMTUMIKIA BWANA.

16 Hao watu wakajibu wakasema, Hasha! Tusimwache Bwana, ili kuitumikia miungu mingine”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUOTA UPO KANISANI.

UWE MWAMINIFU HATA KUFA.

NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?

YESU HAYUPO KATIKA MAZINGIRA YALEYALE TU SIKUZOTE, USIJISAHAU.

Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?

Rudi Nyumbani

Print this post

Lalama kwa uhai wa watoto wako wachanga wazimiao kwa njaa(Maombolezo 2:19)

Mafundisho maalumu kwa watumishi wa Mungu na Watenda kazi wote katika shamba la Bwana.

Maombolezo 2:19

[19]Inuka, ulalamike usiku, Mwanzo wa makesha yake; Mimina moyo wako kama maji usoni pa Bwana; Umwinulie mikono yako; KWA UHAI WA WATOTO WAKO WACHANGA WAZIMIAO KWA NJAA, Mwanzo wa kila njia kuu. 

Ikiwa wewe ni mzazi au mlezi unaelewa ni uchungu mwingi kiasi gani  unakupata  pale unapoona mtoto wako anaangamia kwa kukosa mahitaji yake muhimu, mfano  wa chakula. Ndicho kilichotokea kwa mama Hajiri siku alipofukuzwa kwa Ibrahimu, akiwa kule jangwani amepotea hali ilikuwa mbaya sana, kwani chakula na maji viliwaishia kabisa, huwenda zilipita siku kadhaa hawakuona dalili yoyote ya kupata msaada. Hivyo alichokifanya Hajiri, ni kwenda mbali kidogo na kumlilia sana Mungu wake, na Mungu akasikia, akaonyeshwa palipo na maji, akaenda kumpa mwanae, kuonyesha ni jinsi gani alivyouthamini uhai wa Ishmaeli.

Mwanzo 21:14 Ibrahimu akaamka asubuhi na mapema akatwaa mkate na kiriba cha maji, akampa Hajiri akimtwika begani pake, na kijana, akamruhusu; naye akatoka, akapotea katika jangwa la Beer-sheba. 

15 Yale maji yakaisha katika kiriba, akamlaza kijana chini ya kijiti kimoja. 

16 Akaenda akakaa akimkabili, mbali naye kadiri ya mtupo wa mshale; maana alisema, Nisimwone kijana akifa; naye akakaa akimkabili, AKAPAZA SAUTI YAKE, AKALIA. 

17 Mungu akasikia sauti ya kijana. Malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, Una nini, Hajiri? Usiogope, maana Mungu amesikia sauti ya kijana huko aliko. 

18 Ondoka, ukamwinue kijana, ukamshike mkononi mwako, kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa. 

19 Mungu akamfumbua macho, naye akaona kisima cha maji; akaenda akakijaza kiriba maji, akamnywesha kijana. 

Umeona kama Hajiri asingemtafuta Mungu katika hali ile, ni wazi kuwa Yule kijana ambaye alikuwa amekusudiwa awe taifa kubwa angefia jangwani na yale maono yasingetokea.

Ndicho tunachojifunza katika vifungu hivyo, kwenye kitabu cha Maombolezo, anasema kesha, ulie, kwa ajili ya watoto wako wachanga wazimiao kwa njaa. Leo hii tuna watu wengi ambao wameokoka kwa kuisikia injili yetu. Lakini je, watu hao wanasimama au wanakufa?, Unapomhubiria mtu, hatutakiwi kusema yaliyobaki namwachia Mungu, bali ni kuhakikisha hafi kiroho kwa kukosa chakula cha uzima. Na hiyo inakuja kwa kuendelea kumfuatilia kumfundisha, Lakini zaidi sana KUMWOMBEA kwa Mungu usiku na mchana akue kiroho.

Tukiiga mfano wa Epafra jinsi alivyokuwa akiwaombea sana watu wa kolosai walioamini kwa injili yao.

Wakolosai 4:12  Epafra, aliye mtu wa kwenu, mtumwa wa Yesu Kristo, awasalimu, akifanya bidii siku zote kwa ajili yenu katika maombi yake, ili kwamba msimame wakamilifu na kuthibitika sana katika mapenzi yote ya Mungu.

Umeona? Ukomavu wa watu walio wachanga wa kiroho hutegemea sana maombi ya kina kwa waliowazaa. Hivyo wewe kama mtenda kazi hakikisha unakuwa na maombi mengi kwa ajili ya wale uliowahubiria injili wakaokoka vinginevyo watakufa kiroho, katika ulimwengu huu wa njaa na kiu ya Neno la Mungu, tenga masaa kuwaombea. Na maombi hayo yawe ya rohoni kabisa, sio ya juu juu, bali ya kuzama, ili Mungu awakuze, na matokeo ya kazi yako utayaona tu baada ya kipindi fulani, jinsi watakavyozidi kubadilika na kukomaa kidogo kidogo, hatimaye kuwa watumishi imara katika shamba la Mungu.

Bwana akubariki.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.

NJAA ILIYOPO SASA.

LISHA KONDOO WANGU, LISHA WANA-KONDOO WANGU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 25:25 Kama vile maji ya baridi kwa mtu mwenye kiu 

SWALI: Nini maana ya

Mithali 25:25 Kama vile maji ya baridi kwa mtu mwenye kiu, Ndivyo ilivyo habari njema itokayo katika nchi ya mbali.

JIBU: Biblia inalinganisha burudiko kubwa mtu analolipata pale anaposikia habari fulani njema na mfano wa mtu mwenye kiu halafu ghafla akaletewa kikombe cha maji ya baridi, sasa katika mazungira kama hayo ni wazi kuwa maji yale atayafurahia sana kwasababu yupo katika kiu.

lakini kiini cha mstari huo ni hapo anaposema ni habari njema ITOKAYO KATIKA NCHI YA MBALI.

Tukumbuke kuwa zipo habari njema nyingi..kwamfano habari za kupewa tenda fulani ya kibiashara ni habari njema, habari za kufaulu darasani ni habari njema, habari za kuzaliwa mtoto duniani ni habari njema, habari za kupandishwa cheo ni habari njema n.k…lakini zote hizi hazina jipya kwasababu ni za hapa hapa tu duniani.

Bali zipo habari njema zinazotoka katika nchi ya mbali na huko si kwingine zaidi ya MBINGUNI, hizo ndizo watu wana kiu nazo, wakizisikia tu ni lazima mioyo yao ni lazima iburudike sana.

Na habari zenyewe ni zile zinazomuhusu  Yesu Kristo.

Alisema.

Yohana 6:33-35

[33]Kwa maana chakula cha Mungu ni kile kishukacho kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.

[34]Basi wakamwambia, Bwana, sikuzote utupe chakula hiki. 

[35]Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe.

Yesu ndio maji yakatao kiu, alileta habari njema iliyotoka mbinguni, alikuja kutuletea ukombozi na msamaha wa dhambi, alikuja kutufungua katika vifungo vyetu, na shida zetu mbalimbali, na kutumwagia karama za rohoni, mambo ambayo mwingine yoyote hawezi kutoa. Lakini zaidi sana alikuja kutuambia habari za ufalme wake, kwa habari ya mambo yanayokuja, kuhusu mbingu mpya na nchi mpya, na Yerusalemu mpya, na umilele, na uzuri na thawabu alizotuandalia sisi tuliomwamini. Mambo ambayo ukisikia kama wewe unapenda kweli maisha…utayafurahia sana.

hivyo yatupasa mimi na wewe tuwe na mwitikio huu, wa habari hizi njema kwa kuwashuhudia pia na wengine maji haya, kwasababu ni wazi kuwa wengi wana kiu, na hivyo wanahaja ya kuzisikia hizi habari njema zimuhusuyo Yesu Kristo.

Sote kwa pamoja tuamke tukahubiri injili. Tukijua kuwa inahitajiwa sana.

shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

INJILI NI NINI?

Maana ya Mithali 17:22 Moyo uliochangamka ni dawa nzuri;

KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Je! mtu anaweza kumbariki Mungu au kulibariki jina lake?

Swali: Tumekuwa tukisikia na kuona watu wakisema “Tunalibariki jina la Mungu” na wengine wanasema “tunambariki Mungu”.. Je mtu anaweza kubariki Mungu au jina lake?..au ni Mungu ndiye anayeweza kumbariki mtu na kulibariki jina la mtu?


Jibu: Mungu anaweza kulibariki jina la mtu na vile vile mtu anaweza kulibariki jina la MUNGU. Isipokuwa tafsiri ya neno “baraka” ndiyo inayoleta ukinzani kwetu!.

Neno “Baraka” maana yake ni “kukiongezea kitu au mtu thamani, au heshima au fursa” ambacho hakikuwa nacho au hakuwa nayo!… Na thamani hiyo/heshima hiyo inaweza kuwa ni zawadi, au nafasi, au hadhi.

Mtu anapompa mwingine zawadi, tafsiri yake ni kwamba “amembariki mtu yule” vile vile mtu anapompa mtu mwingine heshima ya juu au fursa ya juu “maana yake amembariki mtu yule”.

Vile vile na sisi Mungu anaweza kutupa fursa, au heshima au zawadi ya jambo Fulani tulitendalo..Na sisi pia tunaweza kumpa heshima Mungu wetu, au fursa au zawadi kwa jambo Fulani atutendealo,…sasa kitendo hicho cha kumheshimu Mungu kwa kumpa kitu Fulani, ndicho kinachoitwa KUMBARIKI BWANA.

Na zawadi kubwa ambayo tunaweza kumpa MUNGU ikawa ni Baraka kwake ni Maisha yetu, pamoja na SIFA za midomo yetu.

Pengine utauliza ni wapi katika maandiko watu walimbariki Bwana…

2Nyakati 20:25 “Nao Yehoshafati na watu wake walipokuja kuchukua nyara zao, wakaona kati yao wingi wa mali, na mavazi, na johari za thamani, walivyojivulia, zaidi kuliko wawezavyo kuchukua; wakawa siku tatu katika kuteka nyara, maana zilikuwa nyingi sana.

26 Hata siku ya nne wakakusanyika katika bonde la baraka; MAANA NDIPO WALIPOMBARIKIA BWANA; kwa hiyo jina lake mahali pale pakaitwa Bonde la Baraka hata leo”.

Umeona hapo mstari wa 26, biblia inasema “MAANA NDIPO WALIPOMBARIKIA BWANA”..Na walimbaki kwa njia gani??… si nyingine Zaidi ya SIFA…

2Nyakati 20:18 “Yehoshafati akainama kichwa, kifulifuli; wakaanguka mbele za Bwana Yuda wote na wakaao Yerusalemu, wakimsujudia Bwana.

19 Na Walawi, wa wana wa Wakohathi na wa wana wa Wakorahi, wakasimama ili wamsifu Bwana, Mungu wa Israeli, KWA SAUTI KUU SANA”.

Na pia katika Zaburi ya 63 tunazidi kulithibitisha hilo…

Zaburi 63:3 “Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai; Midomo yangu itakusifu.

4 NDIVYO NITAKAVYOKUBARIKI MAADAMU NI HAI; Kwa jina lako nitaiinua mikono yangu.”

Kwahiyo SIFA, tuimbazo ikiwa tunaziimba katika roho na kweli basi zinalibariki jina lake..utalisoma hilo Zaidi katika Zaburi ile  ya 96 na Ayubu 1:21.

Zaburi 96:1 “Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Mwimbieni Bwana, nchi yote.

2 Mwimbieni Bwana, LIBARIKINI JINA LAKE, Tangazeni wokovu wake siku kwa siku”.

Ila kumbuka jambo moja!.. Wewe au Mimi tusipolibariki jina la Mungu kwa kumpa yeye utukufu kwa vinywa vyetu au maisha yetu.. hatumpunguzii chochote, kwani anao mabilioni ya Malaika mbinguni wanaomsifu… Zaidi sana ni kwa hasara yetu wenyewe!!.. YEYE DAIMA ATABAKI KUWA MUNGU, NA WA KUABUDIWA, NA KUPEWA UTUKUFU  HATA PASIPO SISI!!.

2Timotheo 2:12 “Kama tukistahimili, tutamiliki pamoja naye; Kama tukimkana yeye, yeye naye atatukana sisi;

13  KAMA SISI HATUAMINI, YEYE HUDUMU WA KUAMINIWA. Kwa maana hawezi kujikana mwenyewe”.

Bwana atubariki.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JINA LAKO NI LA NANI?

Je Mungu anaweza kumdanganya mtu?

Je shetani anaweza kushusha moto kutoka mbinguni?

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

Rudi Nyumbani

Print this post

Nini maana ya ufalme wa Mungu hauwi katika neno bali katika nguvu?(1Wakorintho 4:20).

Swali: Je, Mtume Paulo alimaanisha Nini kusema Maana ufalme wa Mungu hauwi katika neno Bali katika nguvu?.


Jibu: Turejee mstari huo..

1 Wakorintho 4:20 “Maana ufalme wa Mungu hauwi katika neno, bali katika nguvu”.

Hapo anaposema kuwa Ufalme wa Mungu hauwi katika “neno” hamaanishi “Neno la Mungu”...kwasababu Ufalme wa Mbinguni unajengwa na NENO LA MUNGU kama nguzo ya msingi…na pasipo hilo hakuna ufalme wa Mungu…kinyume chake ni ufalme wa giza unajengwa.

Hivyo biblia inaposema ufalme wa Mungu hauwi katika neno, inamaanisha kuwa hauwi katika “MANENO MATUPU YASIYO NA NGUVU ZA MUNGU”...Bali unakuwa katika maneno yenye nguvu za Mungu.

Maana yake ishara na miujiza inafuatana na Neno la Ufalme…

Mtume Paulo kwa ufunuo wa Roho alizidi kuliweka hilo vizuri katika 1Wathesalonike 1:5.

1 Wathesalonike 1:5 “ya kwamba injili yetu haikuwafikia katika MANENO TU, bali na KATIKA NGUVU, na KATIKA ROHO MTAKATIFU, na uthibitifu mwingi; kama vile mnavyojua jinsi zilivyokuwa tabia zetu kwenu, kwa ajili yenu”.

Vile vile na sisi tunapaswa tuhubiri injili isiyo ya maneno matupu au yenye ushawishi wa maneno ili kuvuta watu… bali yenye dalili na udhihirisho wa Roho.

Maana yake ishara na miujiza vifuatane nasi…Na muujiza wa kwanza ni watu kutubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha…

1 Wakorintho 2:4 “Na neno langu na kuhubiri kwangu hakukuwa kwa maneno ya hekima yenye kushawishi akili za watu, bali kwa dalili za Roho na za nguvu”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

AINA TATU ZA IBADA ZA SANAMU.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze biblia Neno la Mungu wetu, lililo Taa ya njia zetu na Mwanga wa njia yetu (Zab. 119:105).

Zipo aina tatu (3) za sanamu zinazoabudiwa na watu.

1.Sanamu zenye mfano wa Mtu

2.Sanamu-watu

3.Sanamu-vitu

Tutazame moja baada ya nyingine.

      1.SANAMU ZENYE MFANO WA MTU.

Hivi ni vitu vyote visivyo na uhai vyenye mfano wa mtu, ambavyo vinatengenezwa na watu kwa lengo la kuabudiwa.

Tabia ya hizi sanamu kulingana na biblia ni kwamba zina midomo lakini hazisemi, zina macho lakini hazioni, zina masikio lakini hazisikii, zina pua lakini hazinusi..na wanaoziabudu wanafanana na hizo kiroho.

Zaburi 115:4 “Sanamu zao ni fedha na dhahabu, Kazi ya mikono ya wanadamu.

5 Zina vinywa lakini hazisemi, Zina macho lakini hazioni,

6 Zina masikio lakini hazisikii, Zina pua lakini hazisikii harufu,

7 Mikono lakini hazishiki, miguu lakini haziendi, Wala hazitoi sauti kwa koo zake.

8 Wazifanyao watafanana nazo, Kila mmoja anayezitumainia”

Hizi ndio zile zote zinazoabudiwa na wapagani, pamoja na baadhi ya madhehebu yajiitayo ya kikristo. Utakuta sanamu imewekwa ndani ya nyumba ya ibada, na watu wanakwenda kuiangukia na kuisujudia, hata kuitolea sadaka na kuiomba, jambo ambalo ni machukizo makubwa..

Ni dhambi kubwa kusujudia sanamu yoyote ile, Kasome Kutoka 20:1-6.

2. SANAMU-WATU.

Hii ni aina  ya pili ya sanamu ambayo ni tofauti kidogo na ile ya kwanza… ile ya kwanza ina midomo lakini haisemi, ina macho lakini haioni, ina masikio lakini haisikii…. Hii ya pili nayo ni hivyo hivyo, ina macho lakini haioni, ina masikio lakini haisikii, ina macho lakini haioni..tofauti tu ni kwamba ile ya kwanza ile ya kwanza haipumui ila hii ya pili inapumua, ile ya kwanza imetengenezwa kwa miti, udongo, chuma, fedha au dhahabu lakini hii ya pili ni Wanadamu.

Sasa tunaisoma wapi katika biblia…

Ezekieli 12: 1 “Neno la Bwana likanijia tena, kusema,

2 Mwanadamu, wewe unakaa kati ya nyumba iliyoasi, WATU AMBAO WANA MACHO YA KUONA, ILA HAWAONI, WANA MASIKIO YA KUSIKIA, ILA HAWASIKII; kwa maana ni nyumba iliyoasi”.

Umeona? Kumbe sanamu sio tu mawe na udongo vinavyoweza kuwa sanamu bali hata watu..

Kama hujamaanisha kumfuata YESU wewe ni SANAMU.. Kwasababu una macho lakini huoni mambo ya rohoni, una masikio lakini husikii sauti ya MUNGU, Una kinywa lakini hakineni mambo ya Mungu, Hivyo wewe ni sanamu pamoja na viungo vyako vyote.

“KICHWA” chako ni sanamu/mungu wako, ndio maana unakitumikia kwa vitu vya kidunia kama YEZEBELI..

“MASIKIO” yako ni sanamu/mungu wako, ndio maana unayatumikia kwa kubadilisha vipuli kila siku.

“MACHO” yako ni sanamu/mungu wako, ndio maana unayatumikia usiku na mchana kupaka uwanja, na kupadilisha kope pamoja na kuchonga nyusi.

“MDOMO” wako ni sanamu/mungu wako, ndio maana unautumika kwa rangi na kila aina ya lipstick

“MIKONO” yako na “MIGUU” ni sanamu/mungu wako, ndio maana unaitumika kwa bangili na kucha za bandia..

“TUMBO” lako ni mungu wako ndio maana unalitumikia kwa kulinywesha pombe na kuliburudisha kwa kila linachohitaji usiku na mchana… Huna muda wa kufunga na kuomba walau kwa wiki mara moja, kwako kufunga ni adhabu kubwa!!..

Wafilipi 3:19  “mwisho wao ni uharibifu, MUNGU WAO NI TUMBO, utukufu wao u katika fedheha yao, waniao mambo ya duniani”.

Ikiwa hujamaanisha kumfuata YESU kila kiungo katika mwili wako ni sanamu/mungu.. Ndio maana biblia inasema tuvifishe viungo vyetu vilivyo katika nchi, maana kwa hivyo huzaa dhambi na NDIO ibada ya sanamu.

Wakolosai 3:5 “Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu;

6  kwa ajili ya mambo hayo huja ghadhabu ya Mungu”.

     3. SANAMU-VITU.

Hizi ni sanamu zote zisizo na mwonekano au maumbile ya mwanadamu lakni zinaabudiwa.

Mfano wa hizi ni kazi, fedha, umaarufu, Elimu, Mali kama nyumba, magari, ardhi n.k. Mtu akiwa na hivi na hana KRISTO maishani mwake ni mwabudu sanamu tu!

KUMBUKA: Usipomwabudu MUNGU  WA KWELI, basi unaabudu sanamu, na usipoabudu sanamu basi unamwabudu MUNGU WA KWELI, Hakunaga hapo katikati! Ni aidha uwe wa shetani au wa Mungu.

Kama kazi yako inaheshima kuliko Mungu kiasi kwamba unakosa hata siku moja ya wiki kumtolea Mungu wako, hiyo kazi ni sanamu/mungu kwako.

Kama elimu yako, au umaarufu wako au cheo chako kina nguvu kuliko Neno la MUNGU, basi hicho ulichonacho tayari ni mungu wako.

Je umeokoka?…Kumbuka wote wanaoabudu sanamu sehemu yao ni katika lilwe ziwa liwakalo moto na kiberiti kulingana na biblia.

Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, NA HAO WAABUDUO SANAMU, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

Biblia inamaanisha nini kusema Yeye aliye na sikio, na asikie?

USIMWABUDU SHETANI!

MAJARIBU MATANO (5) YA MKRISTO.

DANIELI: Mlango wa 3

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 17:22 Moyo uliochangamka ni dawa nzuri;

SWALI: Nini maana ya

Mithali 17:22 Moyo uliochangamka ni dawa nzuri; Bali roho iliyopondeka huikausha mifupa.


JIBU: Mstari huu unatuonyesha jinsi gani hali ya moyo inavyoweza kuathiri hali za nje za mwili. Si kila wakati dawa itatibu, ikiwa moyo umepondeka afya inaweza kuathiriwa pia. Kwamfano labda mtu yupo katika nyumba au makazi ambayo hana amani, anateswa, anaudhiwa, anaabishwa, muda wote anakuwa mnyonge, utaona pia kwa namna Fulani afya yake itaathirika, labda atasumbuliwa na ugonjwa Fulani ambao hauna sababu wala chanzo.

Lakini moyo ukichangamka, hata kama huyo mtu yupo katika hali/mazingira magumu kiasi gani, mwili wake pia baada ya mda utaitikia hali ya roho yake. Na hivyo atakuwa na afya yake.

Sasa Nitaufanyaje moyo wangu uchangamke?

1)    Kwa kutembea ndani ya ahadi za Mungu katika Neno lake. Mara kadhaa katika maandiko Bwana Yesu alisema” jipeni moyo”. Unapojipa moyo katika ahadi za Mungu ukijua kabisa, ni hakika atatenda,hasemi uongo, Fahamu kuwa utakuwa ni mwanzo wa kuchangamka kwako. Kwamfano ukikumbuka kuwa alisema hatatuacha wala kutupungukia, unakuwa na amani wakati wote, nyakati zote, ukiwa na vingi ukiwa umepungukiwa yote yatakuwa sawa tu, kwasababu sikuzote yupo pamoja na wewe. Furaha inakutawala.

Hata upitiapo magonjwa, ukikumbuka ahadi zake kuwa atakuponya, ukaendelea kuzishika kwa imani, afya yako hurejea.

Yeremia 30:17 Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema Bwana, kwa sababu wamekuita, mwenye kutupwa, wakisema, Ni Sayuni, ambao hapana mtu autakaye. 

18 Bwana asema hivi, Tazama, nitarudisha tena hema za Yakobo zilizohamishwa, na kuyahurumia makao yake; nao mji huo utajengwa juu ya magofu yake wenyewe, nalo jumba litakaliwa, kama ilivyokuwa desturi yake. 

19 Tena kwao itasikiwa shukrani, na sauti yao WACHANGAMKAO; nami nitawazidisha, wala hawatakuwa wachache; tena nitawatukuza, wala hawatakuwa wanyonge.

Hivyo ishi kwa kushikilia ahadi za Mungu kwenye Neno lake, zipo nyingi sana, na zimefika katika kila Nyanja ya maisha yetu. Hakuna sababu ya kutochangamka, wakati Neno la ahadi lipo. Aliyekuahidia ni Mungu wa miungu muumba wa mbingu na nchi hakuna lolote linalomshinda, kwanini uogope?

2) Pili, kwa kupenda ushirika na wengine. Kamwe usiishushe wala kuipuuzia  nguvu iliyopo ndani ya ndugu katika Kristo. Zipo nyakati utahitaji kutiwa nguvu na wenzako, hata kukaa pamoja tu, kutafakari Neno la Mungu na kumwimbia Mungu ni tiba nzuri sana, itakayochangamsha moyo wako, tofauti na kama ungekuwa mwenyewe mwenyewe tu wakati wote.

Ndivyo ilivyokuwa hata kwa Paulo, wakati ule..

Matendo 28:15  Na kutoka huko ndugu, waliposikia habari zetu, wakaja kutulaki mpaka Soko la Apio na Mikahawa Mitatu. Paulo alipowaona alimshukuru Mungu, AKACHANGAMKA.

Chuma hunoa chuma, tuwapo pamoja, tunajengana nafsi, na matokeo ya kufanya hivyo yataonekana mpaka nje.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

PALE AHADI ZA MUNGU ZINAPOKUJARIBU.

JE! UNAIONA ILE NCHI NZURI YA KUMETA-META MBELE YAKO?

Je sisi wakristo tunaruhusiwa kufanya 40 za marehemu?

Rudi Nyumbani

Print this post