Ipi tofuati kati ya UTAKATIFU na UKAMILIFU?

Ipi tofuati kati ya UTAKATIFU na UKAMILIFU?

Swali: Ipi tofuati kati ya kuwa MTAKATIFU (1Petro 1:15-16) na kuwa MKAMILIFU (Mathayo 5:48)?

Jibu: MTAKATIFU ni Mtu aliyetakaswa, aliye safi, asiye na mawaa na anayefanya matendo mema.. Na biblia inatufundisha tuwe watakatifu kama Baba wa mbinguni alivyo mtakatifu…

1Petro 1:15  “bali kama yeye aliyewaita ALIVYO MTAKATIFU, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;

16  kwa maana imeandikwa, MTAKUWA WATAKATIFU KWA KUWA MIMI NI MTAKATIFU”.

Na tena Mambo ya Walawi 19:2  inarudia jambo hilo hilo..

Walawi 19:2 “Nena na mkutano wote wa wana wa Israeli, uwaambie, Mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana, Mungu wenu, ni mtakatifu”.

Lakini MKAMILIFU ni Mtakatifu aliye kamilika….. Wapo Watakatifu waliokamilika na ambao hawajakamilika.

Mtakatifu aliye kamilika ni yule ni anayefanya JAMBO LA ZIADA katika UTAKATIFU WAKE linalomtofautisha na wengine na kufanya afanane na MUNGU … Mfano wa mambo hayo ni kama yale yote Bwana YESU aliyoyataja katika Mathayo 5.

Mathayo 5:43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;

44  lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,

45  ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.

46  Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?

47  Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, MNATENDA TENDO GANI LA ZIADA? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?

48  Basi ninyi MTAKUWA WAKAMILIFU, KAMA BABA YENU WA MBINGUNI ALIVYO MKAMILIFU

Kwahiyo na sisi ni Lazima tuutafute UKAMILIFU na si UTAKATIFU TU!.

> “Mtakatifu” anafunga na kuomba kwaajili yake peke yake, lakini “Mkamilifu” anafunga na kuomba kwaajili yake na kwaajili ya wengine,

> “Mtakatifu”  anasoma neno na kuomba basi!…Lakini “Mkamilifu”  anasoma Neno na kuomba na kuwafundisha wengine mambo aliyojifunza, ili nao wabarikiwe kama yeye.

> “Mtakatifu”  anafanya kazi ya Mungu kwa moyo ili akapate thawabu mbinguni, lakini “Mkamilifu”  pamoja na kufikiri thawabu mbinguni lililo kubwa zaidi analolifikiri ni ndugu zake wasiangamie katika moto wa milele (moyo wake unaugua juu ya roho za wengine kupotea).

> “Mtakatifu”  atampa Mungu siku moja katika wiki ya kukusanyika nyumbani kwa Mungu, lakini “Mkamilifu”  atafikiri Zaidi ya siku moja.

> Mtakatifu” atazishika AMRI ZOTE ZA MUNGU, lakini Moyo wake utakuwa pia katika mali…. Lakini “Mkamilifu” Atazishika Amri zote na Moyo wake hautakuwa katika mali kama yule kijana aliyekutana na Bwana YESU.

Mathayo 19:16 “Na tazama, mtu mmoja akamwendea akamwambia, Mwalimu, nitende jambo gani jema, ili nipate uzima wa milele?

17  Akamwambia Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri.

18  Akamwambia, Zipi? Yesu akasema, Ni hizi, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo,

19  Waheshimu baba yako na mama yako, na, Mpende jirani yako kama nafsi yako.

20  Yule kijana akamwambia, Haya yote nimeyashika; nimepungukiwa na nini tena?

21  Yesu akamwambia, UKITAKA KUWA MKAMILIFU, enenda ukauze ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate.

22  Yule kijana alipolisikia neno lile, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi”.

Hivyo hatuna budi kuutafuta UKAMILIFU na sio UTAKATIFU tu peke yake!!.

Biblia inasema Nuhu alikuwa mtu Mkamilifu katika vizazi vyake ndio maana akapona katika ile gharika (Mwanzo 6:9),  Daudi alikuwa mkamilifu ndio maana alipendwa na Mungu zaidi ya wafalme wote (2Samweli 22:24), Ayubu alikuwa mkamilifu ndio maana alimwona Mungu katikati ya majaribu (Ayubu 1:1).

Na hata sisi tukiwa WAKAMILIFU tutamwona Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MADARAKA YA WAKATI MKAMILIFU.

BABA UWASAMEHE

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.

Nini maana ya Mungu amemfanya mwanadamu mnyofu?

NENO LA MUNGU NI UFUNUO MKAMILIFU.

Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments