Title April 2020

Did Paul truly worship the angel who he was walking with?

Let’s read that verse…

Acts 27:23 For there stood by me this night the angel of God, whose I am, and whom I serve,


If you quickly jump into this verse You would think Paul meant he was worshipping that angel who is always walking with him, but if you read closely you will be noticed he never meant that… rather he worships the God of that angel.


For better understanding we can put that word like this.
For there stood by me this night the angel of God… Which God?…The God (of that angel) whom I serve.

Now read again that statement plainly you will grab the meaning…

Furthermore, we are advised to study the bible diligently, so we can understand the word the God wants us to understand. Because there also many other verses which are hard to understand unless we are willing to sit down and ask the Holy Spirit for the interpretation. By doing so the holy spirit surely help us with the correct interpretations, and therefore we will win Satan from misleading us.

he succeeded to mislead many people in wrong interpretations from canonizing drinking of alcohol to polygamy marriages in the church and even going further to idol worshipping.

May the grace of God help us.

Shalom.

Related articles:

EVERY ONE SHALL GIVE ACCOUNT OF HIMSELF

THE ANCIENT DRAGON/SERPENT

WHO IS ANTI-CHRIST

THE BOOK OF LIFE.

Home:

Print this post

Je kuweka mapambo kama mikufu, vikuku na kutoboa pua ni dhambi?

SWALI: Ezekiel. 16:11 “Nikakupamba kwa mapambo pia nikakutia vikuku mikononi mwako na Mkufu shingoni mwako 12.nikatia Hazama puani mwako na pete masikioni mwako na Taji nzuri juu ya kichwa chako.

1Timotheo 2:9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri pamoja na adabu nzuri na moyo wa kiasi si kwa kusuka nywele wala kwa dhahabu na lulu wala kwa nguo za thamani 10.bali Kwa matendo mema kama iwapasavyo wanawake wanao ukili uchaji wa mungu”

Swali! Ni kosa kwetu kujipamba au Kuna aina ya mapambo tunayopaswa na mengine hatupaswi naomba ufafanuzi wako?”


JIBU: Mstari huu wa Ezekiel 16, ndio unaotumika na wengi wanaoamini kuwa kujipamba na kujitia wanja na kutia mapambo na kutoboa pua na masikio sio dhambi, kwasababu Mungu kahalalisha hapo kwenye Ezekieli..Hali kadhalika wanaoamini sio sahihi kwa mwanamke wa kikristo kujipamba na kuwa kama mwanamke wa kidunia, wanasimamia mstari huo wa 1Timotheo 2:9.

Kwa ufupi biblia haijichanganyi, kwasababu Mungu ni mkamilifu, na kila anachokizungumza ni Kweli, hivyo kinachojichanganya ni ufahamu wetu sisi… Sasa hilo andiko la kwenye Ezekieli na hilo la Timotheo yote ni maneno ya Mungu hakuna lililokosewa, wala hakuna linalokinzana na lingine, unaokinzana ni uelewa wetu na si Neno la Mungu. Sasa tofauti iliyopo katika hiyo mistari miwili ni kwamba katika Ezekieli ule ni mfano na katika Timotheo ni Agizo…

Katika Ezekieli ukianza kusoma kuanzia juu mstari wa kwanza, utaona Mungu alikuwa analifananisha Taifa la Israeli(na mji wake mkuu Yerusalemu) na mwanamke, na katika mfano huo akatumia utaratibu wa wanawake wa kidunia jinsi wanavyopambwa na kupendezwa na kuvalishwa vikuku, na kuvishwa mikufu, na kuvalishwa pete za masikio wanapoolewa…na Mungu akajiweka katika nafasi hiyo jinsi alivyolipenda Taifa hilo kama mwanamke aliyepambwa katika roho…lakini kama vile wanawake wa kidunia wasio waaminifu wanavyozisaliti ndoa zao kwa kiburi cha uzuri wao, ndivyo Yerusalemu ilivyofanya mbele za Mungu, na sio sehemu moja Mungu analifananisha Taifa la Israeli na mwanamke,

Utaona sehemu nyingine nyingi analiita binti Sayuni, Ukisoma katika Hosea utaona analifananisha taifa hilo na mwanamke aliyemwacha mumewe n.k..Hivyo huo ulikuwa ni mfano tu! Na sio amri, hivyo haimaanishi kwamba wanawake wanapaswa wajitie mapambo, watoboe pua na masikio na kujifananisha na wanawake wa kidunia. Hapana bali mapambo yao yanapaswa yawe ya rohoni, kama biblia inavyoagiza.

Ili kuelewa vizuri kuwa mfano sio amri, turudi tena kutafakari mfano mwingine katika Agano jipya, ambao huo utatufumbua macho zaidi.

Tuutafakari mfano ule wa wanawali kumi…ambao tunaupata katika Mathayo 25, katika mfano ule kama wengi wetu tunavyoujua, kulikuwa na Bwana mmoja mwenye wanawali 10, (maana yake mabikra)..Hawa wote walikuwa wameposwa tayari kwa kuolewa na Bwana huyu mmoja…lakini baadhi yao walikuwa werevu na wengine wapumbavu…

Sasa katika mfano huo, Bwana Yesu ndiye aliyejifananisha na huyo Bwana harusi kwenye mfano huo, na wale wanawali 10, ndio sisi kanisa lake, ambao miongoni mwao wapo werevu na wapumbavu…Sasa kwa mfano huo basi wa mtu mmoja kuwa na wake 10, kwamba Bwana Yesu alikuwa anahalalisha ndoa za mitara…Kwamba kila mmoja sasa ni sawa kwenda kuoa wanawake 10 si Bwana alisema pale?…Unaona? Ule Bwana alioutoa ni mfano tu!..ambapo alitumia desturi za watu wa mataifa za kuoa wake wengi ili kupitisha tu ujumbe…na sio kutoa amri kwamba na sisi tupose au tuoe wanawake 10.

Na ndio maana Bwana Yesu mwenyewe alisema katika Marko

Marko 10:5 “Yesu akawaambia, Kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu aliwaandikia amri hii.

6 Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke.

7 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe;

8 na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja”.

Umeona?..kwahiyo si sahihi kutumia mfano na kuufanya kuwa amri au Agizo (huko ni kutafsiri maandiko vibaya)…Pia utaona Bwana Yesu alitoa mfano mwingine kwamba atakuja kama mwivi usiku wa manane, hiyo haimaanishi kuwa wizi ni halali, au haimaanishi Bwana Yesu ni mwizi…hapana!. Anatumia matukio ya kiduni na kujiweka yeye au watu wake katika hizo nafasi, ili kufikisha tu ujumbe Fulani..

Kwa mantiki hiyo basi, ndio maana Mtume Paulo kwa kulijua hilo kwa ufunuo wa Roho …hakuchanganyikiwa na hayo maandiko ya kwenye Ezekieli kama sisi tulivyochanganyikiwa baadhi yetu sasa…ndio maana akatuandikia..kwamba

“…wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujistri pamoja na adabu nzuri na moyo wa kiasi si kwa kusuka nywele wala kwa dhahabu na lulu wala kwa nguo za thamani, bali Kwa metendo mema kama iwapasavyo wanawake wanao ukili uchaji wa mungu” .

Hivyo wewe mama/binti/mwanamke wa kikristo usidanganyike na uongo wa shetani uliozagaa huko na kule, mtaani kwamba Mungu haangalii mavazi na anapendezwa na wanawake wanaojichubua uso, au wanaopaka rangi mdomoni, au wanaotoboa masikio na pua, au wanaopaka wanja…au wanaovaa nguo za nusu uchi na za kubana. Wote wafanyayo mambo kama hayo ni machukizo na wanajifungulia milango ya kuingiliwa na maroho ya adui, na hatimaye kuishia katika jehanamu ya moto. Nyakati hizi ni za hatari na tunaishi katika siku za mwisho, mafundisho ya uongo yametabiriwa kuzagaa…shetani anafanya juhudi nyingi sana kuwavuta watu kwake, kwasababu anajua muda wake ni mchache sana.

Hivyo geuka leo, baada ya kuyaelewa haya maandiko…Mpe Yesu Kristo maisha yako kama bado hujaokoka, na upokee Roho Mtakatifu. Kwasababu Roho mtakatifu akishaingia ndani yako ndio atakufundisha hili andiko kuwa mwanamke anapaswa ajipambane ndani kwa matendo mema ya haki na sio nje kama wanawake wakileo wanavyofanya..

1Petro 3:3 “Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;

4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.

5 Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao”.

Bwana akubariki sana.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Je! ni vibaya kutaja Huduma kwa kujipa cheo? Mfano Mighty Prophet, Chief Apostle n.k.?

LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI.

Mwaloni ni nini? Na je unafunua nini rohoni?

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

LULU YA THAMANI.

INJILI YA KRISTO HAITANGAZWI KWA HATI MILIKI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

Shalom, karibu tujifunze maandiko katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo.

Leo tutajifunza jambo lingine ambalo kila mmoja wetu anapaswa kujua ni kwa nini tunapaswa tuihubiri injili wakati wote bila kujali ni nani tunayempelekea ujumbe huo.

Ukisoma Habari za wafalme katika biblia, utakutana na mfalme mmoja ambaye alimuudhi Mungu kwa viwango vya juu sana, naye si mwingine Zaidi ya mfalme Ahabu ambaye pia alichochewa na mke wake Yezebeli,

1Wafalme 11:25 “Lakini hapakuwa na mtu kama Ahabu, aliyejiuza atende maovu machoni pa Bwana ambaye Yezebeli mkewe alimchochea”.

Wote hawa wawili waliigeuza Israeli kuwa nchi ya waabudu sanamu, wakawafukuza na manabii wote wa Mungu, na kama hiyo haikutosha walikuwa wanamwaga damu nyingi za watu wasiokuwa na hatia..

Hivyo Mungu akakusudia kumuua Ahabu, kwa kumtolea kabisa unabii, kwa kinywa cha Nabii Eliya kuwa atakufa kifo cha aibu na damu yake italambwa na mbwa (1Wafalme 21:17-19)..Lakini miaka ilikwenda, miaka ikarudi, hakuna aliyejua mfalme huyu mwovu ni nani atamuua, wala atakufaje.

Lakini siku ya siku, akakusudia kwenda vitani, kupigana na maadui zake washamu, lakini safari hii hakwenda peke yake, bali alimtafuta Rafiki yake Yehoshafati ambaye yeye alikuwa ni mfalme wa Yuda wakati huo, isipokuwa Yehoshafati alikuwa anamcha Mungu kuliko yeye.. Hivyo akapanga njama, akamwambia Yehoshafati, kwamba yeye ndio ajifanye kuwa mfalme wa Israeli, avae nguo za kifalme, Na yeye atavaa nguo za kawaida, atajichanganya mule mule vitani..kwasababu alijua washami walikuwa hawana shida na watu, bali walikuwa na shida na mfalme wao..Maana ndivyo walivyopatana kuwa watakapokwenda vitani, wasihangaike na mtu yeyote bali wapeleke nguvu zao kwa mfalme wa Israeli tu, kwasababu walijua wakishamuua tu mfalme wao basi vita vitakuwa vimekwisha..

Lakini Ahabu yeye alikwenda kinyume chao, akamfanya mwenzake Yehoshafati awe shabaha ya maadui zao..Hivyo wakaingia wote vitani mapambano yakaanza, Na Yehoshafati alipoona maadui zao, wote wanamkimbilia kumfuata yeye, saa hiyo hiyo akamlilia Mungu amwepushe na ile mauti, Na Mungu akamsikia Hivyo wale washami walipoona kuwa yule wanayemfukuzia siye mfalme halisi wa Israeli waliachana naye, wakaendelea na mapambano..

Lakini sasa, wakiwa katika mapambano, hawajua mfalme ni yupi katikati ya umati, biblia inatuambia mtu mmoja akavuta upinde wake kwa kubahatisha tu, pengine yeye alikuwa na lengo la kumpinga, mwanajeshi mmoja wa kawaida tu aliyemwona mbali, akitimiza kusudi lake la kutupa silaha yake, kwa adui yake aliyemwona mbele yake..Lakini hakujua kuwe kumbe yule ndio Kichwa cha Adui wao, tusome…

1Wafalme 22:33 “Ikawa, wakuu wa magari walipoona ya kuwa siye mfalme wa Israeli, wakageuka nyuma wasimfuate.

34 Mtu mmoja akavuta upinde kwa kubahatisha, akampiga mfalme wa Israeli mahali pa kuungana mavazi yake ya chuma; kwa hiyo akamwambia mwendesha gari lake, Geuza mkono wako, unichukue kutoka katika majeshi; kwa kuwa nimejeruhiwa sana.

35 Pigano likazidi siku ile; mfalme akategemezwa garini mwake, kinyume cha Washami, hata jioni akafa; damu ikatoka katika jeraha yake ndani ya gari.

36 Ikapigwa mbiu jeshini, jua likichwa, kusema, Kila mtu aende mjini kwake, na kila mtu shambani kwake.

37 Hivyo akafa mfalme, akachukuliwa Samaria, wakamzika mfalme huko Samaria”

Unaona?..Ule upinde ulikwenda kupenya kwenye ile sehemu dhaifu kabisa ya mavazi yake ya chuma, yaani pale ambapo yanakutana, pale kwenye mkunjo hapo hapo ndipo mshale ukaingia..Na baadaye akafa kwa kuchurukiza damu, na mwisho wake ukawa umefikia hapo..

Sasa ni vizuri kufahamu kuwa habari zote tunazozisoma katika agano la kale, sio kutuburudisha sisi, hapana bali kila tukio lina ujumbe wa siri wa kanisa la Kristo katika agano jipya..

Hivyo katika Habari hiyo Bwana anatuonyesha, mojawapo ya njia ya kumshinda adui yetu ibilisi kiurahisi.. Tunajua ibilisi huwa anatumia mbinu nyingi katika kushindana na kanisa la Kristo, Na wakati mwingine haji kwa njia ya moja kwa moja ili kushindana na sisi, kwani anajua akija hivyo ni rahisi kumgundua na kumshinda..

Hivyo anatumika njia ya kujigeuza kama alivyofanya Ahabu..

Kwahiyo inahitajika njia nyingine ya kupambana naye, vinginevyo tutamkosa, nayo si nyingine Zaidi ya kurusha mishale mingi kwa kadiri tuwezavyo,.. Yaani maana yake tuihubiri injili kama watu wasio na malengo kwa sababu kwa njia hiyo Hujui Mungu atammalizia shetani katika engo ipi..

Unaweza ukakutana na mtu lakini hujui kuwa huyo ni ajenti mkubwa wa shetani, ambapo pengine angesikia injili yako kidogo tu, angegeuka, kutokwenda kusababisha maajali barabarani siku hiyo..

Au tunakutana na mtu ambaye anaonekana ni wa kidunia tu, tunaishia kusema huyu ni jambazi, au mlevi, au mshirikina na hawezi kubadilika, lakini hutujui shetani ndiye aliyempelekea mapepo mengi ya ushawishi ili aendeleee kuwa vile, kwasababu alishaona tangu zamani katika ulimwengu wa roho kuwa ikitokea akiiamini injili basi siku moja atakuwa mhubiri wa kimataifa wa kuwaleta wengi kwa Kristo, hivyo kaamua kumfanya vile awe muuaji, au mpingamizi mkubwa wa injili kama alivyofanya kwa mtume Paulo..Lakini kwasababu tunaogopa kurusha mishale, tukikisia kuwa haina faida yoyote hatujui kuwa ndivyo tunavyomkosa ibilisi hivyo vitani.

Kuna mhubiri mmoja wa kimataifa anaitwa Rick Jonyer, yeye alichukuliwa katika maono mbinguni akaonyeshwa, baadhi watu walio katika viti vya enzi, na alipotazama vizuri alimwona mtu mmoja aliyemjua,.akamuuliza Bwana Je! Imekuwaje mtu huyu mtu amefika hapa, Bwana akamfunulia historia ya Maisha yake, na jinsi yeye alivyokutana naye wakati fulani akamdharau, wala hakumhubiria kwasababu ya udhaifu wake wa kusikia..Lakini Yule mtu alipokuja kutubu dhambi zake, na kumtumikia Mungu kwa uaminifu wote katika madhaifu yake, ndio ikampelekea awe mtu mkubwa sana kule mbinguni.. Na mwisho kabisa Bwana akamwambia, kama usingekuwa na tabia hiyo ya kudharau watu, leo hii ungetambuliwa na mbingu kuwa wewe ndiwe mwalimu wa mfalme mkuu kama huyu.

Hivyo na sisi, tuhubiri kwa watu wote, bila kutazama ni nani aliye mbele yetu..Kwasababu hatujui kuwa ushindi mkubwa dhidi ya shetani tutaupata kupitia njia hiyo..

Mhubiri 11: 6 “Asubuhi panda mbegu zako, Wala jioni usiuzuie mkono wako. Kwa maana wewe hujui ni zipi zitakazofanikiwa,kama ni hii au hii, au kama zote zitafaa sawasawa”.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

IKIMBIE DHAMBI KWA GHARAMA ZOZOTE ZILE!

MUNGU KUSEMA NA WEWE PEKEE, HAITOSHI KUKUPA USHINDI.

Shetani ni nani?

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

Kwanini Mungu alisema hakuna mtu awazaye kuuona uso wake akaishi?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 3

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIHUSISHE HISIA KATIKA KUMTOLEA MUNGU.

Sadaka kubwa na ya kwanza ambayo ina thamani kubwa sana mbele za Mungu ni MAISHA YETU. Tunapoyatoa Maisha yetu kwake kwa kumwamini Mwanawe Yesu Kristo, na kuuacha ulimwengu, na kumuishia yeye kwa kuzishika amri zake na kuifanya kazi yake…hiyo ni sadaka kubwa na ya kwanza inayompendeza Mungu na sio mali zetu. Sadaka ya Maisha yetu ina majibu makubwa na thawabu kubwa sana…na thawabu yake kuu ni Uzima wa milele.. Yaani kuishi Maisha yasiyo na mwisho baada ya Maisha haya…Unayatoa Maisha yako sadaka ya miaka hii 80 au 90 au 100 tunayoishi…na unapata thawabu ya kuishi miaka milioni mara milioni…isiyo na uzee, shida, dhiki wala mateso.

Hivyo ni muhimu sana kuyatoa Maisha kuwa sadaka kwa Mungu wetu..Kwasababu hata yeye sadaka kubwa aliyoitoa kwa ajili yetu ni Maisha ya mwanawe mpendwa…Hivyo na sisi sadaka kubwa tunayoweza kumrudishia ni kuyatoa Maisha yetu kwake.

Lakini Pamoja na hayo, sadaka nyingine ya muhimu ni ya mali zetu. Tunapotoa mali zetu kwaajili ya Mungu wetu tunajitengenezea daraja kubwa la kubarikiwa hapa duniani. Wengi wanajiuliza je ni kiasi gani ninachopaswa kumtolea Mungu?…Kiasi mtu anachopaswa kumtolea Mungu ni kiwango chochote ambacho si kilema…Kilema maana yake ni kitu chenye kasoro/mapungufu.. Hicho hatupaswi kumpelekea Mungu wetu kwasababu tukifanya hivyo ni kumdharau na kumvunjia heshima..Mungu aliyeziumba nyota na mbingu hastahili makombo yetu..anastahili vilivyo bora.

Mfano wa sadaka kilema ni hii…Umepata laki mbili halafu unampa Mungu aliyekupa pumzi sh efu 1 tu au mia 5 na hiyo nyingine unaifanyia mambo yako ya kimaendeleo…Hiyo ni sadaka kilema..Hali kadhalika sadaka isiyo kilema ni ile umepata ya sh. Elfu 5 unamtolea Mungu elfu 2 au 3 au 4 au hata elfu 5 yote. Hivyo unaweza ukatoa kiwango sawa na mtu mwingine lakini sadaka yako ikawa ni kilema kutokana na mapato unayoyapata ukilinganishwa na mwenzako.

Sasa kuna jambo moja la muhimu la kujifunza. Wengi wanapenda kujionea huruma, au kuonea huruma wengine….Nataka nikuambie ndugu mpendwa…katika suala la kumtolea Mungu hakuna kuoneana huruma wala kumwonea mtu huruma…Umepata elfu 5, na umepanga kumtolea Mungu yote…basi fanya hivyo usianze kujionea huruma utabakiwa na nini, utakula nini, itakuwaje baada ya hapo!…Kama una moyo wa kujihurumia basi usitoe kabisa…lakini katika kumtolea Mungu hakunaga HISIA. Ni aidha unamtolea Mungu au humtolei..basi!.

Ibrahimu alipotaka kumtolea Mungu mwanawe..aliweka kando hisia. Ingawa alikuwa na chaguzi aidha kukubali au kukataa…lakini yeye alikubali kwa kuishinda hisia.

Eliya naye alipofika kwa yule mjane..alimwambia niandalie kwanza mimi na kisha ujifanyie wewe na mwanao, hakuanza kwa kuanza kumhurumia oo ampikie kwanza mwanawe ndipo na yeye apikiwe, hakikuwepo hicho kitu,.….Hivyo yule mwanamke naye alikuwa na chaguzi mbili mbele yake, kujihurumia kwanza yeye na mwana au kumsikiliza yule nabii mzee anayekuja kutaka kula chakula cha mwanae…alikuwa na chaguzi hakulazimishwa…Hivyo aliamua kuikataa huruma yake na mwanawe na kumtolea Mungu…Na kama tunavyoijua ile Habari…baada ya pale, lile pipa halikupunguka.

Utasema hiyo ni Agano la kale… watu walikuwa wagumu na sheria zilikuwa ni kali, vipi kuhusu agano jipya?

Katika Marko 12:41 tunasoma Habari, ifuatayo “Naye akaketi kulielekea sanduku la hazina, akatazama jinsi mkutano watiavyo mapesa katika sanduku. Matajiri wengi wakatia mengi. 42 Akaja mwanamke mmoja, mjane, maskini, akatia senti mbili, kiasi cha nusu pesa.

43 Akawaita wanafunzi wake, akawaambia, Amin, nawaambia, Huyu mjane maskini ametia zaidi kuliko wote wanaotia katika sanduku la hazina;

44 maana hao wote walitia baadhi ya mali iliyowazidi; bali huyu katika umaskini wake ametia vyote alivyokuwa navyo, ndiyo riziki yake yote pia”.

Huyo ni Bwana alikuwa ameketi karibu na chombo cha Sadaka anatazama….mbele yake anaona matajiri wanakuja na kutia noti zao humo…ghafla anatokea bibi maskini na mjane, huyo anamwona anakwenda kutia mule ndani ya hazina senti mbili, kiasi cha nusu pesa (maana yake hata haijakamilika kuitwa fedha kamili)..hicho alichokitoa huyo mama mjane biblia inasema ilikuwa ndiyo riziki yake yote..maana yake hana kitu baada ya pale hata chakula….na mbaya Zaidi alikuwa ni maskini na hana mume, na pengine ni kikongwe tayari.

Sasa tukio hilo Bwana alikuwa analitazama…Lakini tunasoma Bwana hakwenda kumzuia na kumwambia ooh! bibi maskini, ndio hicho tu ulichobakiwa nacho, usikitoe, nenda katumie kununua angalau unga ujipikie chakula chako ule…badala yake alimwacha akitoe hata hicho kidogo alichobakiwa nacho. Kwanini? kwasababu kutoa hakuhusiani na HISIA hata kidogo, hakuangalii hali mtu uliyo nayo au utakayokuwepo nayo baada ya hapo.

Hata Mungu wetu alipotaka kutuletea ukombozi kupitia mwanawe, mpendwa Yesu Kristo hakuangalia HISIA kwamba mwanawe anakwenda kuchapwa mijeledi na kusulubiwa uchi na kuuawa, tena mwanawe asiye na hatia…lakini alimtoa hivyo hivyo, kwasababu utoaji hauhusiani na hisia.

Na vivyo hivyo hata sasa, unapotaka kumtolea Mungu, usianze kujihurumia, kama una moyo wa kujihurumia basi ni heri usitoe kabisa!, hicho ulichopanga kumtolea Mungu kakifanyie shughuli nyingine, lakini kama umepanga kumtolea Mungu usianze kujiangalia hali yako, kwamba mimi niko hivi au vile, halafu bado nikitoe hichi, yaani mimi sina nyumba, sina chakula, sina hiki wala kile halafu bado nimtolee Mungu…ukidhani hizo hisia zako zinamgusa sana yeye!…Kama hazikumgusa kwa yule bibi kizee, aliyetoa senti mbili, ambaye alikuwa hana mume na ni maskini na bado ni mzee, sijui labda wewe matatizo yako ni makubwa zaidi kuliko yale, ambayo yanaweza kuugusa moyo wake akakuhurumia..

Hivyo usianze kutazama hali yako ni kujidanganya mwenyewe na kujizuilia baraka zako..shetani asikufumbe macho kukuletea orodha ya shida zako ili usimtolee Mungu, hayo mawazo yakija yakatae kwa Jina la Yesu. Ni mawazo ya shetani, hata mtu akikuletea hayo mawazo yakatae kwasababu mtu huyo pengine anatumika na shetani pasipo kujijua.

Lakini Pamoja na hayo yote, tunajua mwisho wa Bwana siku zote ni mzuri, Badala ya Isaka kufa badala yake alibarikiwa siku ile, vivyo hivyo badala ya yule mwanamke kufa njaa yeye na mwanae kipindi cha Eliya, alishiba na kusaza kipindi cha njaa na ukame…hali kadhalika hata huyu mjane ambaye alitoa senti mbili zake kwa siri, lakini Bwana alimwona na kumtangaza hadharani, bila shaka alipotoka pale alipewa vitu vingi na wale waliokuwa wanamheshimu Bwana, ingawa biblia haijasema..lakini ni wazi kuwa baraka zake zilianza palepale baada ya Bwana kumtangaza kiwango alichokitoa…Hivyo faida za kumtolea Mungu bila kuhusisha hisia ndio hizo mwisho wake…Lakini tukimsikiliza shetani na kuziheshimu hisia hatutaambulia chochote…Tutaishia kuona kwamba Mungu yeye anafilisi tu watu na hana huruma.

Bwana akubariki sana.

Mwisho kabisa, Kama bado hujaokoka, unasubiri nini?.. unasubiri kufa ghafla katika dhambi na kushuka kuzimu? Au unasubiri kuachwa kwenye unyakuo? Au unangoja dhiki kuu ambayo ipo karibuni kuanza?. Nakushauri uokoke kwasababu hizi ni siku za mwisho, sio wakati wa kujivuni dini wala dhehebu..Mifumo ya Dini na madhehebu, ndiyo itakayohusika kwa sehemu kubwa kuiunda ile chapa ya mnyama, ambapo itafika wakati mtu asipokuwa nayo hataweza kuuza wala kununua.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Je! ni vema kwa mkristo kwenda hospitali au kutumia miti shamba anapougua?

Je! kuchora tattoo ni dhambi?

Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

KWANINI MUNGU ALIMTUMIA MUSA KWA VIWANGO VILE?

UJIO WA BWANA YESU.

NAO WAKADHANI YA KUWA YUMO KATIKA MSAFARA;

Rudi Nyumbani:

Print this post

KATIKA SIKU HIYO WATASEMA,HUYU NDIYE BWANA TULIYEMNGOJA.

Isaya 25:8 “Amemeza mauti hata milele; na Bwana MUNGU atafuta machozi katika nyuso zote; na aibu ya watu wake ataiondoa katika ulimwengu wote; maana Bwana amenena hayo.

9 Katika siku hiyo watasema, Tazama, huyu ndiye Mungu wetu, Ndiye tuliyemngoja atusaidie; Huyu ndiye Bwana tuliyemngoja, Na tushangilie na kuufurahia wokovu wake”.

Upo wakati ambao, tutamwona Kristo uso kwa uso kwa mara ya kwanza, siku hiyo ya tarehe Fulani, na mwezi Fulani na mwaka Fulani, Tutaisikia Parapanda ya Mungu.. Parapanda hiyo haitamuhusu kila mtu, hapana, bali kwa wale ambao walikuwa wanaingojea kwa subira,..siku hiyo pengine itakuwa ni asubuhi kwa upande wako, wakati jua linachomoza mapema kabisa na ndege wanalia kwenye viota vyao, pengine utakuwa unakwenda kupiga mswaki, ajiandae kwenda kanisani, ghafla, utaanza kuona mabadiliko ya tofauti angani, utaanza kusikia sauti nzuri za parapanda, ikitokea mbali sana, pengine utajiuliza jambo hili ni nini? Wakati unaendelea kushangaa shangaa hivyo, ghafla utaona makaburi mengi yanafunguka, na wafu wengi wanafufuka, utawaona unaowajua na usio wajua..

Wakati huo utakuwa unajiuliza labda unaona maono au nini.. kwasababu utakuwa ni wewe tu peke yako ndio unayeyaona hayo yote, hakuna mwingine yoyote atakayeyaona..Saa hiyo hiyo utakuwa unawaona wale wafu nao wanakuja kukufuata kwa furaha, wanakuambia..Hii ndio ile siku tuliyokuwa tunaisubiria, kwa kipindi kirefu, kwa miaka mingi sasa imetimia..

Na wakati mnafikiria hayo, kwa mshangao mkubwa wa furaha isiyo na kifani, Mtaona juu mbinguni jeshi la malaika wengi, linatokea likiambatana na Bwana,(Bwana wetu Yesu)..na ghafla muda huo huo mnaanza kuona miili yenu inabadilishwa na kuwa miili mingine ya kimbinguni, inameta meta na ya utukufu, na bila kupoteza muda mnaanza kunyanyuka mnaiacha ardhi kwa mara ya kwanza, mnaanza kwenda juu kwa kasi sana, kumkaribia YESU mwenyewe Mafalme wa wafalme,..

Kisha wote tunakutana naye pale juu akitungojea kwa tabasamu la upendo wa ajabu, embu fikiria utakuwa na furaha kiasi gani, unamwona kwa mara ya kwanza Yesu uliyekuwa unamsubiria kwa miaka mingi, uso wake unauona uliyekuwa unatamani kuuona.. ndio hili neno litatimia.

Isaya 25:9 “Katika siku hiyo watasema, Tazama, huyu ndiye Mungu wetu, Ndiye tuliyemngoja atusaidie; Huyu ndiye Bwana tuliyemngoja, Na tushangilie na kuufurahia wokovu wake”.

Kumbuka kitendo cha wewe kuyashuhudia hayo yote, kwa watu wengine huku duniani kitakuwa ni kitendo cha kufumba na kufumbua..watashangaa tu haupo, umetoweka. Hawatasikia parapanda wala hawataona makaburi yakifunguka.

Na kwa jinsi watu watakaonyakuliwa watakavyokuwa ni wachache, hata ulimwengu hautasaidiki habari hizo, watasema tu wamepotea watu kadhaa, lakini watapatikana, hivyo watu wataendelea na shughuli zao kama kawaida, wakingojea dhiki kuu ya mpinga-Kristo.

1Wathesalonike 4;15 “Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti.

16 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.

17 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele”.

18 Basi, farijianeni kwa maneno hayo.

Wakati sisi tukichukuliwa na lile jeshi la malaika na kupelekwa mbinguni kwenye karama Yesu aliyotuandalia kwa zaid ya miaka 2000, mahali ambapo furaha isiyokuwa na kifani itakuwepo,.huku chini wanadamu wote watakuwa wanapita dhiki kuu, ambayo haijawahi kutokea mfano wake..

Tukose mengine yote,tusiikose siku hiyo ya unyakuo..

Unyakuo upo karibu sana ndugu, ni jambo la kushangaza, kama wewe bado mpaka leo hii, unapuuzia habari za wokovu.. Unasubiri siku ile ikujie kwa ghafla ndio uamini? Kama gonjwa hili la Corona lilivyoijia dunia kwa ghafla ndipo wakaamini kuwa dunia inaweza ikageuzwa na kuwa kitu kingine ndani ya muda mfupi?..Ndivyo unyakuo utakavyokuja na dhiki itakavyoanza!

Tubu dhambi zako sasahivi, mpokee YESU maishani mwako, ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO ili upokee kipawa cha Roho Mtakatifu, sawasawa na Matendo 2;38, uupate wokovu.. kisha uishi maisha ya kama mtu anayemngojea KRISTO..Ili siku ile na wewe uwe mmojawapo wa watakonyakuliwa na Bwana..

Hatuna muda mwingi, hapa duniani, mavuno ya dunia yamekwishakomaa (kulingana na maandiko),..siku yoyote hukumu ya Mungu itaanza kama vile tunavyoona dalili za kuanza kwake leo hii zilivyo, ikiwa bado unasubiria dalili nyingine ndio uamini basi ujue utajikuta umeingia katika dhiki kuu, na wakati upo katikati ya dhiki kuu ndio utauliza Habari za unyakuo, na utaambiwa..unyakuo ulishapita siku nyingi! Hivyo tubu leo ukabatizwe…

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

SIKU ILE NA SAA ILE.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

UFANYE NINI KAMA MKRISTO WAKATI HUU WA JANGA LA CORONA?

OLE WA NCHI NA BAHARI.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

TUNA WAJIBU WA KUOMBEANA KWA KINA.

Jina la Bwana Yesu libarikiwe. Karibu tujifunze Neno la Mungu..

Biblia inasema..katika Yakobo 5:16

“Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii”.

Maana yake ni kwamba tunapoombeana kuna neema ya ziada inashuka juu yetu…(Mungu anaachilia uponyaji)..Tunapomwomba Bwana atuhurumie sisi na kuwahurumia wengine, tunafungua wigo mpana wa Yule tunayemwombea kuponywa na kwetu sisi pia kuponywa pamoja na kufunika wingi wa dhambi..(Yakobo 5:20).

Hebu tukitafakari kile kisa cha Sodoma na Gomora…Kama wengi wetu tujuavyo kuwa kabla Mungu hajashusha moto kutoka mbinguni kuiteketeza miji ile..Mungu alimfunulia kwanza Ibrahimu makusudio yake hayo…lakini tunajua Ibrahimu kitu alichokifanya…japokuwa alikuwa anajua ni kweli Sodoma na Gomora kumeoza lakini hakuishitaki miji ile mbele za Mungu, na badala yake alitafuta njia ya kuiponya na ghadhabu ya Mungu…

Ndipo akaanza kwa kumwuliza Mungu kama watakuwepo wenye haki 50, je ataangamiza hao 50 pamoja na waovu…na kama tunavyojua Bwana alimwambia kama akikuta huko wenye haki 50 hataangamiza miji ile…lakini tunazidi kusoma Ibrahimu alimshusha Mungu idadi mpaka kufikia kwa wenye haki 10 kama watakuwepo…Lakini Mungu jibu lake lilikuwa ni lile lile…kwamba kama atakuta wenye haki 10 hataangamiza miji hiyo kwaajili ya hao wenye haki 10.(Mwanzo 18:23-33).

Lakini tunaona Ibrahimu aliishia idadi ya 10 tu!…Lakini hebu jiulize laiti angeendelea kidogo kuishusha ile idadi hadi tano na hata kufikia mmoja?..Labda pengine miji hiyo mpaka leo ingekuwepo…Kwasababu ndani ya miji ile alikuwepo mwenye haki mmoja LUTU.

Lakini kwasababu Ibrahimu hakulijua hilo, yeye alijua kwa namna yoyote ile mji mzima hauwezi ukakosa wenye haki 10, alijua watakuwepo wenye haki hata elfu…Hivyo aliachana na Mungu kwa amani kwasababu alijua Mungu huko aendako hawezi kukosa kabisa wenye haki 10, na hivyo miji ile itabaki salama tu, Hivyo Ibrahimu aliondoka akijua kuwa kwa maombi yale tayari kaiokoa Sodoma na Gomora…Lakini kumbe hakujua mwenye haki ni mmoja tu kule..ambaye ni ndugu yake aliyeitwa Lutu…Ndipo asubuhi anaamka na ghafla anaona upande wa mashariki moshi mkubwa unafuka juu!..kitendo hicho kilimuhuzunisha sana.

Lakini ni dhahiri kuwa laiti Ibrahimu angejua kuwa kuna mwenye haki mmoja tu ndani ya miji ile yote..asingemwacha Mungu bila kumwomba, wala asingeishia pale kwenye idadi ya watu kumi tu,…ni lazima angemshusha Mungu mpaka mtu mmoja na angezungumza na Mungu kwaajili ya huyo mwenye haki mmoja ili aunusuru mji wote, na suluhisho lingepatikana pale pale.

Tunachoweza kujifunza hapo ni kwamba ni lazima kuombeana sisi kwa sisi kwa kina, sio juu juu tu!..tusichukulie tu kwamba hali ni salama au shwari kwa ndugu zetu au kwa jamii ya watu wetu au kwa Taifa letu zima…Hali si shwari kama tunavyofikiri..Hivyo tusipoingia katika maombi ya kina ya kuomba rehema na Neema, uharibifu utashuka kwetu na kwa ndugu zetu ghafla.

Yakobo 5:16 “Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii”.

Ayubu alikuwa ni mwenye haki lakini hakuacha kuwaombea wanawe, vivyo hivyo na sisi kama Kanisa la Kristo hatuna budi kuombeana sisi kwa sisi, wakati mwingine kwa kutajana majina,..Ili Mungu asiishie kutuponya sisi tu bali mpaka na jamii nzima.

Bwana atubariki na kutusaidia.

Mada Nyinginezo:

USIWE NA HAKI KUPITA KIASI.

NDUGU,TUOMBEENI.

FAIDA ZA MAOMBI.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

CHAPA YA MNYAMA

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mwaloni ni nini? Na je unafunua nini rohoni?

Kwa lugha ya kiingereza unajulikana kama OAK tree, Kisayansi Kuna ziadi ya jamii 600 za mti huu.. Na unapatikana sehemu mbalimbali duniani sana sana zile za baridi, lakini katika ukanda wa mediterenia yaani Maeneo yote ya mashariki ya kati ikiwemo Israeli mti huu unaota kwa asili.

Mti wa mwaloni unatoa mbao zinazosifika kwa ugumu, katika ujenzi, na matumizi mbalimbali ikiwemo kutengenezea mapipa ya kuhifadhia divai, na mbao za mashua..Vile vile Mti huu unaweza kuishi miaka hata zaidi ya elfu moja..

Lakini Mti  wa mwaloni unaonekana pia ukitajwa sehemu nyingi katika biblia na baadhi ya vifungu hivyo ni kama vifuatavyo..

Mwanzo 35: 8 Akafa Debora mlezi wa Rebeka, akazikwa chini ya Betheli, chini ya mwaloni; na jina lake likaitwa Alon-bakuthi.

 

Yoshua 2: 25 Basi Yoshua akafanya agano na wale watu siku ile, akawapa amri na agizo huko Shekemu.

 

26 Yoshua akayaandika maneno haya katika kitabu cha torati ya Mungu; kisha akatwaa jiwe kubwa, akalisimamisha huko, chini ya ule mwaloni uliokuwa karibu na patakatifu pa Bwana.

 

Waamuzi 6:11 Malaika wa Bwana akaenda akaketi chini ya mwaloni uliokuwa katika Ofra, uliokuwa mali yake Yoashi, Mwabiezeri; na mwanawe Gideoni alikuwa akipepeta ngano ndani ya shinikizo, ili kuificha machoni pa Wamidiani.

 

2Samweli 18: 9 Na kwa bahati Absalomu akakutana na watumishi wa Daudi. Naye Absalomu alikuwa amepanda nyumbu wake, na yule nyumbu akapita chini ya matawi manene ya mwaloni mkubwa, hata kichwa chake kikakwama katika mwaloni huo, akanyakuliwa juu kati ya mbingu na nchi; na yule nyumbu aliyekuwa chini yake akaenda mbele.

Nakadhalika, na kadhalika…

Lakini Swali ni, Je mti wa mwaloni unayo maana yoyote rohoni?

Mti yote tunayoiona ikitajwa kwenye maandiko, ilikuwa na  kwa kazi maalumu katika jamii, vilevile ikifunua jambo Fulani katika roho kwa mfano ukisoma

Waamuzi 9;8-15.. utaona mwandishi akieleza jamii ya miti akifananisha na jamii za watu waliopo..

  • Kwamfano ukisoma pale mti kama Mzeutuni anasema ulikuwa unatumika kwa ajili ya kutolea mafuta, jambo lililofunua katika agano jipya, watiwa mafuta, au watumishi wa Bwana.(Soma Zekaria 4;11-14, Ufunuo 11)
  • Vilevile Mzabibu ulikuwa unatoa divai,.Ukimfunua Yesu Kristo na Roho Mtakatifu, Na sisi pia kama matawi ya ya mzabibu huo tunapaswa kutoa matunda ya Roho ndani yetu pale Kristo anapokaa ndani yetu (Yohana 15)
  • Pia Mtini, ni mti unaotoa tini, ikifunua taifa la Israeli kwa ujumla(Yeremia 24)
  • Miiba, au michongoma..Ni miti iliyofunua watawala wabovu au watumishi waovu mfano Abimeleki Yule mtoto wa Gideoni…

Sasa tukirudi kwenye maandiko kile kitabu cha Isaya 6:1-4  kinasema..

1 Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao.

2 Kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa, na siku ya kisasi cha Mungu wetu; kuwafariji wote waliao;

3 kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; WAPATE KUITWA MITI YA HAKI, iliyopandwa na Bwana, ili atukuzwe.

4 Nao watajenga mahali pa kale palipoharibiwa, watapainua mahali palipokuwa ukiwa zamani, watatengeneza miji iliyoharibiwa, mahali palipoachwa kizazi baada ya kizazi.

Ukisoma tafsiri nyingine nyingi za biblia, pale kwenye neno ‘miti ya haki’, limetumiwa neno mialoni ya haki..

Sasa kama tulivyokwisha kuona kule mwanzo mwaloni ni mti uliotumika hasahasa katika ujenzi, ni mti uliosifika kuwa na mbao ngumu, na zenye uwezo wa kuitunza divai vizuri.

Hivyo rohoni, ukiwa wewe ni mjenzi wa nyumba ya Mungu (Kanisa lake) unafananishwa na Mwaloni. Kama wewe ni mhubiri kwa Bwana ni mwaloni wake, kama wewe ni shujaa wa Bwana katika kuifanya kazi yake basi ni mwaloni kwa Bwana…Kama wewe unaifanya kazi kama ya Kristo ya kuhubiri injili basi ni mwaloni mzuri ufaaye kwa kazi ya ujezi wa nyumba ya Mungu inayodumu.. sawasawa na Isaya 61:4.

Ubarikiwe.

Mada Nyinginezo:

Pakanga ni nini?

Je! habari ya Yusufu, inabeba ujumbe gani kwa agano jipya?

JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

NINI MAANA YA KUSAGA MENO?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini Mungu alisema hakuna mtu awazaye kuuona uso wake akaishi?

SWALI: Kwanini Mungu alimwambia Musa hakuna mtu awazaye kuuona uso wake akaishi,(Kutoka 33:20) Je! Kwa Mungu kuna mauti, tunapaswa tujihadhari naye?


JIBU: Tunajua biblia inatuambia kuwa kwa Mungu ndipo chemchemi za maji ya uzima zinapotoka, na ndipo chanzo cha uhai kwa kila kiumbe hai kinapozaliwa..

Zaburi 104:29 “Wewe wauficha uso wako, Wao wanafadhaika; Waiondoa pumzi yao, wanakufa, Na kuyarudia mavumbi yao,

30 Waipeleka roho yako, wanaumbwa, Nawe waufanya upya uso wa nchi.

Hivyo kusema kwa Mungu kuna mauti, jibu ni La, badala yake ndio kuna uzima..

Lakini swali linakuja ni kwanini basi Mungu alimwambia Musa maneno yale, kuwa hakuna mtu atakayeuona uso wake na akaishi?? Je! Kila atakayemwona Mungu ni lazima afe?..Na ndio maana Mungu akamwonyesha tu Musa sehemu ya nyuma ya utukufu wake ili asife au?

Kauli hiyo ukiitafakari kwa haraka unaweza kudhani Mungu alimaanisha kifo, lakini si kweli, kwasababu Mungu sio Kifo, tukimwona Mungu katika utimilifu wote ndivyo tutakavyozidi kuishi, isipokuwa sasa hatutaishi tena katika hali hii ya Maisha ya kawaida tuliyonayo siku zote..

Yaani itatulizimu kuvuka viwango hivi, na kwenda viwango vingine kiasi kwamba hata haya Maisha ya hapa duniani yatakuwa hayana maana tena kwetu, kuyaishi hatutaweza kuendelea kuishi tena hapa duniani..tutahamishwa na kuingia katika Maisha ya ufalme wa Mungu wetu..

Chukulia mfano, mtoto mdogo labda wa miaka 5, halafu akiwa bado ni mdogo vilevile umwondolee akili yake ya kitoto, kisha umwekee ubongo wa mtu mzima wa miaka 40 ndani yake..halafu umpe toy, za kitoto au umnunulie midoli aichezee.. Wewe unadhani ataifurahia tena, au atacheza nayo tena?…Kinyume chake utamwona ananyanyuka, na kwenda kusikiliza BBC, akitoka hapo utaona anaanza kuzungumzia Habari za uwekezaji, na kupanga mipango ya kimaendeleo.., kamwe huwezi kumkuta anachezea tena matope, au anaruka ruka barabarani kama Watoto wengine..

Ni kwasababu gani? Ni kwasababu akili yake imevukishwa mipaka yake ya utoto, hivyo hawezi kuishi tena Maisha ya utoto aliyopaswa ayaishi kwa umri wake..

Vivyo hivyo tukimwona Mungu kwa utimilifu wote, Maisha ya hapa duniani ndivyo yatakavyokuwa hayana maana tena kwetu.kinachobakia ni Kuondoka tu..

Bwana wetu YESU KRISTO yeye peke yake ndiye aliyemwona Mungu katika utimilifu wote..

Yohana 1:18 “Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote; Mungu Mwana pekee aliye katika kifua cha Baba, huyu ndiye aliyemfunua”.

Na ndio maana aliondoka na kupaa na mpaka sasa, hajawahi kutokea mtu kama yeye, wakati huu wa sasa yupo kifuani mwa Mungu, hata makerubi na maserafi hajafikia bado hatua hiyo. Maisha yake hapa duniani yalikuwa ni ya kimiujiza tu, mpaka wengine wanadhani biblia iliongeza chumvi pale iliposema, mambo yote aliyoyafanya Yesu kama yangeandikwa moja moja sijui kama vitabu vyote duniani vingetosha..(Yohana 21:25)

Yesu alikuwa na uwezo wa kuuondoa uhai wake, na kuurudisha akiwa bado hapa hapa duniani,(Yohana 10:18), lakini hakutaka kufanya hivyo ili tu kutimiza kusudi la kutuokoa sisi, Je! Mtu huyo ni wa kawaida?

Na sisi pia tuzidi kumwomba Mungu azidi kujifunua kwetu, Zaidi na Zaidi, ili nasi tukifikie hatua ya kumjua yeye, mpaka kuifikia hatua ya kuondolewa duniani kwa tukio lile kuu la (UNYAKUO) alilotuahidia. Kama Bwana wetu alivyochukuliwa juu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:

MSHIKE SANA ELIMU.

JE VIBWENGO NI KWELI VIPO?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Zile mbao mbili za mawe Musa alizoambiwa achonge zilikuwaje?

SWALI: Zile Mbao za mawe Musa alizoambiwa achonge kwa ajili ya zile amri 10 zilikuwaje?..je ni mbao za miti zilichonganyikana na mawe au zilikuwa ni kitu gani?


JIBU: Neno mbao asili yake sio miti…bali ni kipande cha kitu chochote ambacho kipo bapa, ambacho kinaweza kufaa kwa matumizi mbali mbali kama uandishi au ujenzi. Umoja wa neno mbao ni UBAO. Hivyo ubao unaweza kuwa wa miti, chuma, mawe, glasi au chochote kile.

Hivyo Mbao mbili Musa alizoambiwa achonge hazikuwa za miti, bali za mawe. Na ndizo hizo Mungu alizozitumia kuandikia amri zake. Sasa Kwanini Mungu alitumia mawe na si miti? Ni kwasababu maandishi yaliyoandikwa kwenye mawe yanadumu kwa muda mrefu zaidi ya yale yanayoandikwa kwenye miti…kwasababu miti inaoza na kuharibika na kuliwa na mchwa lakini mawe yanadumu miaka mingi..Hivyo Mungu kuonyesha kwamba Amri zake ni za daima na milele na kwamba hazifutiki ndio maana alitumia mawe.

Lakini Pamoja na hayo mawe yanaweza kuharibika pia na maandishi yale yakapotea miaka inapozidi kuwa mingi…Hivyo Mungu aliruhusu pia amri zile zikae kwenye mawe kwa muda tu, kwasababu mbeleni alikuwa na mpango mwingine maalumu sana wa mahali pa kuziandikia ambapo zitadumu milele.

Hivyo wakati ulipofika, akaleta mpango mwingine wa kuandika amri zake si katika miti wala mawe ambayo yapo leo na kesho kupotea…Ndipo akaleta agano jipya kupitia mwana wake mpendwa ambapo ataziandika amri zake na sheria zake mioyoni mwa watu wake..Humo ndimo mahali pekee ambapo ahaziwezi kufutika kamwe kama maandiko yanavyosema..

Yeremia 31:31“Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda.

32 Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema Bwana. 33 Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; Nitatia SHERIA YANGU NDANI YAO, NA KATIKA MIOYO YAO NITAIANDIKA; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.

34 Wala hawatamfundisha kila mtu jirani yake, na kila mtu ndugu yake, wakisema, Mjue Bwana; kwa maana watanijua wote, tangu mtu aliye mdogo miongoni mwao hata aliye mkubwa miongoni mwao, asema Bwana; maana nitausamehe uovu wao, wala dhambi yao sitaikumbuka tena”

Hivyo ili tuzishike amri za Mungu hatuna budi ziandikwe ndani ya mioyo yetu….Na zinaandikwa tu pale tunamwamini Yesu Kristo na kupokea Roho Mtakatifu. Kumbuka Yesu ndiye mjumbe wa Agano jipya (Malaki 3:1) Hivyo yoyote aliyemwamini, na kupokea Roho wake Mtakatifu amri na sheria za Mungu zinaandikwa katika mbao za moyo wake…anakuwa anazitimiza sheria zile bila kujilazimisha wala kulazimishwa, wala hazimfanyi kuwa mtumwa, kiasi kwamba anapata tabu kuzishika sheria za Mungu…yeye mwenyewe tu anajikuta anazipenda sheria za Mungu na kuzitenda.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Sanduku la Agano lilikuwa linawakilisha nini katika Agano jipya?

HUDUMA YA (ELIFAZI, SOFARI, NA BILDADI).

Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

MUUNGANIKO WA MADHEHEBU NI MPANGO WA MPINGA-KRISTO.

IFANYE KAZI YA MUNGU PASIPO HOFU!

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIJITAFUTIE KULAMBWA NA MBWA KWA DHAMBI YA KUTAMANI.

Kutoka 20:17 “Usiitamani nyumba ya jirani yako, usimtamani mke wa jirani yako; wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng’ombe wake, wala punda wake, wala cho chote alicho nacho jirani yako”.

Bwana ameweka msisitizo mkubwa sana, katika jambo hili ‘Usitamani’..Na utaona ni karibu nyanja ya vitu vyote alivyonavyo jirani yako.

Sasa Usitamani kunako zungumiziwa hapo sio kutotamani kuwa na kitu kama cha jirani yako, hapana, bali ni kule kutamani kile kitu (chenyewe) jirani yako alichonavyo, na hivyo unatafuta kila namna na kila mbinu ya kukipata..(yaani kukitwaa na kiwe cha kwako) Hiyo ndiyo Mungu anaichukia.

Dhambi hii inagharimu sana na ndio maana Mungu aliisisitiza….

Wapo watu wawili katika biblia tunaweza kuwachukulia kama mfano jinsi waliitamia dhambi hii na ikawagharimu vibaya mno,

(1)Wa kwanza ni Mfalme Daudi na

(2)Wa pili Ni Mfalme Ahabu.

Daudi alimtamani mke wa Huria, na kama tunavyojua ikamfanya atafuta kila njia ya kumwangamiza ili amchukue mke wake, kuifanya habari iwe fupi, leo hii hakuna mtu asiyejua madhara yaliyompata Daudi..ambayo yalimfanya ajutie tendo lile kwa miaka mingi sana, licha ya kufukuzwa tu na kuachwa na Mungu kwa muda, lakini pia masuria wake 10 walifanyiwa kitendo kilekile na mtoto wake mwenyewe aliyemzaa(Absalomu)..Jaribu kufiria ni aibu kiasi gani?..mtoto wako anawabaka wake zako mbele ya taifa zima (2Samweli 11-18)…

Vile vile mwingine ni Mfalme ahabu, yeye naye alitamani kiwanja wa Nabothi Myezreeli, baada ya kukiona ni kizuri na kipo karibu na ikulu yake, hivyo baada ya kunyimwa ikamfanya akose raha kwa muda mrefu mpaka mkewe Yezebeli, akaamua kwenda kumuulia Nabothi ili tu akichukue kiwanja kile..Na ahabu alipoona vile Nabothi ameshauliwa, hakuchukua hatua yoyote ya kutubu badala yake akaenda kukichukua kile kiwanja na kukifanya kiwe chake..Lakini tunaijua habari yake jinsi ilivyokuja kuishia mbeleni, jinsi mbwa walivyokuja kuiliamba damu yake mbele ya kiwanja kile kile cha Nabothi alichomuulia..(1Wafalme 21)

Tunapaswa tujiepushe na roho hii ya tamaa, kwamfano mwanamke mmoja ataenda nyumba ya jirani yake, halafu kule akamwona mfanyakazi wa jirani yake jinsi alivyo mzuri, mchapa kazi, mpishi mzuri wala hana usumbufu wowote..akiangalia huku nyuma , wa kwake ni mvivu, hafanyi kazi, Sasa, badala ajitahidi akatafute mwingine, mwenye vigezo kama vya yule wa jirani yake, yeye anaingiwa na tamaa, na kutafuta kila mbinu ya kumpata yule wa jirani yake, anaanza kumwahidia mshahara mkubwa, ili aache kazi kwa boss wake wa kwanza ahamie kwake..

Na kweli anafanikiwa lakini hajui kuwa na yeye mwisho wake utakuwa kama wa Ahabu wa kuliwa na mbwa, au kama wa Daudi wa kuabishwa na kufukuzwa..pale unapowatamani wake wa wengine..

Mwingine ni katika mambo ya biashara, anaona tu, mwenzake, Mungu anamfanikisha sehemu Fulani wateja wanakuja..Yeye naye anaingiwa tamaa, na kwenda kumwahidia mwenye pango kuwa atamlipa kodi kubwa Zaidi ili yeye aingie pale mwenzake alipokuwepo afanye biashara hapo..Hiyo ni tamaa yenye adhabu..

Na nyingine nyingi za namna hiyo..Na ndio maana Bwana alihitimisha na kusema.. “wala cho chote alicho nacho jirani yako”

Biblia inatuambia..

1Timotheo 6:6 “Walakini utauwa pamoja na kuridhika ni faida kubwa”.

Tunapaswa tuwe watu wa kuridhika na vile tulivyonavyo..

Hivyo angalia je chochote, unachokitamani , Je, mwisho wa siku kitamuathiri jirani yako?. Kama ndivyo ni heri ukaacha..Uepukane na laana.. Na mapigo.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Ubatizo wa moto ni upi?

Kuota unafanya Mtihani.

“Ninyi ni chumvi ya dunia” Andiko hilo lina maana gani?

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

KWANINI MUNGU ALIMTUMIA MUSA KWA VIWANGO VILE?

Rudi Nyumbani:

Print this post