Pakanga ni nini?

Pakanga ni nini?

Pakanga ni mmea fulani mchungu uliokuwa unajulikana enzi za kale za biblia, ulikuwa ni mmea unaoota sehemu kame na ulikuwa ni mchungu sana..Hivyo kutokana na sifa ya mmea huo, chochote kile ambacho kingeleta uchungu mkali zamani kiliitwa jina la pakanga Kwa mfano kwenye biblia tunaona neno hilo likitumika sehemu mbali mbali…

Yeremia 23:15 “Basi Bwana wa majeshi asema hivi, katika habari ya manabii, Tazama, nitawalisha pakanga, nitawanywesha maji ya uchungu; kwa kuwa kutoka kwa manabii hao wa Yerusalemu kukufuru kumeingia katika nchi yote”.

Soma tena..

Mithali 5:3 “Maana midomo ya malaya hudondoza asali, Na kinywa chake ni laini kuliko mafuta; 4 Lakini mwisho wake ni mchungu kuliko pakanga; Ni mkali kama upanga wa makali kuwili”.

Yeremia 9:14 “bali wameenenda katika ushupavu wa mioyo yao wenyewe, na kuandamana na Mabaali, kama walivyofundishwa na baba zao.

15 Basi, Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tazama, nitawalisha pakanga, naam, watu hawa, nami nitawapa maji ya uchungu wayanywe.

16 Nami nitawatawanya kati ya mataifa, ambao wao hawakuwajua; wala baba zao, nami nitatuma upanga nyuma yao, hata nitakapowaangamiza kabisa”

Ufunuo 8:10 “Malaika wa tatu akapiga baragumu, nyota kubwa ikaanguka kutoka mbinguni, iliyokuwa ikiwaka kama taa, ikaanguka juu ya theluthi ya mito, na juu ya chemchemi za maji. 11 Na jina lake ile nyota yaitwa Pakanga; theluthi ya maji ikawa pakanga, na wanadamu wengi wakafa kwa maji hayo, kwa kuwa yalitiwa uchungu”.

Soma pia (Maombolezo 3:15,19), (Amosi 6:12), utaliona Neno hilo..

Hivyo biblia inapotumia hili Neno pakanga, inamaanisha uchungu mkali usio wa kawaida utakaowapata watu wanaotenda dhambi.. kama vile uasherati, uabuduji sanamu, utoaji wa unabii wa uongo n.k..

Hata leo Maisha yetu Mungu anaweza kuyatia pakanga, ikiwa tutaendelea kuishi Maisha ya kutokujali..Tuombe Bwana atuepushe na hayo mambo, huku tukikaa mbali na dhambi..Magonjwa haya tuyaonayo leo hii ni sehemu tu ndogo ya Pakanga, Ukilishangaisha ni hiyo itakayokuja kuachiliwa siku za mwisho ambapo watu watasaga ndimi, wakitamani vifo viwafikie, lakini mauti itawakimbia.. mambo hayo yatakuja baada ya unyakuo kupita.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?

Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?

NDUGU,TUOMBEENI.

Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?

TIMAZI NI NINI

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
9 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Anonymous
Anonymous
2 years ago

Naitwa Laban francis. naomba masomo. 0621697046

Amani Jeremia Sausi
Amani Jeremia Sausi
1 year ago
Reply to  Anonymous

Shalom Mtumishi/Watumishi wa Mungu Mkuu, naomba masomo kupitia email yangu

Anonymous
Anonymous
2 years ago

Naomba masomo kwa whatsapp 0621697046

Leonard
Leonard
2 years ago

Send also to me this doctrine

Respicius
Respicius
4 years ago

Naomba muwe mnanitumia hayo mafundisho alfu ntakuwa nawauliza maswali

Edward Mwaseba
Edward Mwaseba
3 years ago
Reply to  Admin

Naomba pia nipate masomo hayo. 0769417265