Moja la lango ambalo Mungu hulitumia sana, kutufikishia sisi taarifa zake, ni ndoto. Na kama ni lango la Mungu basi ni vema tufahamu kuwa ibilisi hatalipenda. Hivyo atahakikisha taarifa hizo anazivuruga au hazitufikii vema, kama tu vile anavyohakikisha watu hawaliewi Neno, au mahubiri, Ndivyo anavyofanya na kwenye ndoto pia.
Taarifa zitokazo kwa Mungu zinaangukia katika makundi matatu;
1) Tahadhari
Hizi ni taarifa za maonyo, au hatari zinazokuja mbeleni. Mfano wa taarifa hizi ni kama zile zilizomfikia Yusufu, alipokuwa Israeli, akaambiwa akimbilie Misri, kwasababu Herode anataka kumuua mtoto, na aliporudi baadaye, akaonywa tena asikae Yerusalemu, bali aende Nazareti.
Mathayo 2:19-22
19 Hata alipofariki Herode, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto huko Misri, 20 akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mamaye, ushike njia kwenda nchi ya Israeli; kwa maana wamekufa walioitafuta roho ya mtoto. 21 Akaondoka akamchukua mtoto na mamaye, akafika nchi ya Israeli. 22 Lakini aliposikia ya kwamba Arkelao anamiliki huko Uyahudi mahali pa Herode babaye, aliogopa kwenda huko; naye akiisha kuonywa katika ndoto, akasafiri pande za Galilaya,
Lengo la taarifa hizi ni mtu kuchukua hatua, aidha ya kivitendo au ya kimaombi.
Kwamfano Mungu anaweza kukuonyesha ajali, au msiba fulani. Hapo ujue hasaa unahitajika kuchukua hatua kimaombi kuharibu hizo roho za mauti, kwa kinywa chako.
2) Unabii
Hizi ni taarifa za mambo yajayo, Yale yatakayotokea baadaye, kwenye maisha yako, huduma, familia, nchi, au taifa. Mfano wa ndoto hizi, ni kama ile ya Farao juu ya miaka saba ya shibe na njaa, (Mwanzo 41) na Nebukadreza, juu ya ile sanamu kubwa, iliyowakilisha falme nne, zitakazokuja kusimama ulimwenguni (Danieli 2).
Halikadhalika Mungu anaweza kukuonyesha, maisha yako baadaye yatakuwaje, huduma yako baadaye, itasimamaje, maono yako baadaye yatafikia wapi, anaweza kukuonyesha mambo ya siku za mwisho, matukio yajayo, kuhusu nchi, watu, familia. Hatua unayopasa kuichukua ni kuomba, na kuandaa mazingira sasa. Mfano Farao aliposaidiwa tafsiri ya ndoto yake na Yusufu, alichukua hatua ya kuweka hazina ya vyakula kwasababu njaa ilikuwa inakuja mbele. Mungu akikuonyesha huduma yako itakuwa kubwa, anza leo kujiwekea hazina ya maarifa ya Neno la Mungu, anza kutendea kazi wito wako,. Akikuonyesha unawaombea watu wengi wanapona, anza leo kuwaombea watu hata kama hawaponi, omba hivyo hivyo kila siku, usikae tu ukasubiri ije kutimia huonyeshi jitahada yoyote, akikuonyesha biashara yako imekuwa, ongeza juhudi kufanya kazi.
3) Baraka
Mungu anaweza kuachia Neno la Baraka kwako, kwamfano ukaota, ndoto njema, labda unatiwa mafuta na Kristo, au unaambiwa maneno ya mafanikio kama vile Sulemani alipotokewa na Mungu na kuelezwa atapokea Hekima, na kuwa na mali nyingi. Uotapo ndoto ambazo ni za mafanikio kwako, uamkapo, hakikisha unazinenea kwa Imani. Unasema
“Na iwe kwangu kwa jina la Yesu Kristo”. Kama tu vile unavyobatilisha ndoto za maovu, labda mauti, vivyo hivyo hizi unazipokea kwa kinywa chako. Ni muhimu sana.
Ibrahimu aliota ndoto
Mwanzo 51:1-6
Baada ya mambo hayo neno la Bwana likamjia Abramu katika njozi, likinena, Usiogope, Abramu, Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana. 2 Abramu akasema, Ee Bwana MUNGU, utanipa nini, nami naenda zangu hali sina mtoto, na atakayeimiliki nyumba yangu ni huyu Eliezeri, Mdameski? 3 Abramu akasema, Tazama, hukunipa uzao, na mtu aliyezaliwa nyumbani mwangu ndiye mrithi wangu. 4 Nalo neno la Bwana likamjia likinena, Huyu hatakurithi, bali atakayetoka katika viuno vyako ndiye atakayekurithi. 5 Akamleta nje, akasema, Tazama sasa mbinguni, kazihesabu nyota, kama ukiweza kuzihesabu. Akamwambia, Ndivyo utakavyokuwa uzao wako. 6 Akamwamini Bwana, naye akamhesabia jambo hili kuwa haki.
Sasa kinachotokea ni kwamba ndoto nyingi sana, za taarifa mbalimbali kutoka kwa Mungu zinapotea akilini mwetu, na tunaona kawaida,
Ndoto hupotea kwa aidha namna mbili;
Namna mojawapo inaweza kutokea kwa mtu. Usikae ukafikiria kisa hukumbuki chochote, ukadhani hukuota ndoto yoyote. Zipo ndoto ulizoota. Hivyo ni vema ukajifunza namna ya kukabiliana na lango lako la ndoto. Ndio maana utaona wengine tukio likishatokea ndio anakumbuka kuwa alishawahi onyeshwa tukio hilo. Hiyo haitakiwi.
Nifanye nini ili nikumbuke ndoto zangu?
Njia tatu zinazoweza kumfanya mtu akumbuke ndoto.
i) Kuomba:
Kila asubuhi uamkapo, katika maombi yako, hakikisha unashika Kichwa chako, kisha unasema maneno haya
‘Baba, nafungua lango la ndoto zangu, yote uliyosema nami usiku nilipolala, ninayoyakumbuka na nisiyoyakumbuka yakawe bayana sasa kwa kwa jina la Yesu, ndoto zilizoibiwa na ibilisi, kumbukumbu zangu, na fikra zangu zilizofutika, navirejesha vyote ndani ya ufahamu wangu sasa kwa jina la Yesu Kristo’.
Ukijifunza kuomba namna hiyo, tayari umekaribisha msaada wa Mungu, mahususi katika eneo lako la ndoto na hivyo urahisi wa kukumbuka unakuja.
ii) Utulivu (Kutafakari)
Ukishaomba, pendelea kupata utulivu, kisha tafakari kwanza Neno la Mungu. Kila asubuhi hakikisha unapata kwanza mkate wa uzima ambao ni Neno, tafakari Neno kwa muda kidogo, jiulize vifungu hivi vinamaana gani, je! Siku ya leo nitaviwekaje katika maisha yangu? Fanya tu hivyo tembea maeneo mbalimbali ya kwenye biblia, kisha tafakari tena juu ya maisha yako ya rohoni, juu ya maono yako, juu ya familia yako utajiboreshaje, baadaye juu ya ratiba zako za siku..
Katika wingi wa kutafakari, mara nyingi Mungu hurejesha ndoto zilizosahaulika, utashangaa katika tafakari Fulani hapo hapo unakumbuka kuna jambo uliota, linaloendana na tukio hilo. Ujue huo ni ujumbe wa Mungu.
Ukikosa muda wa kutosha asubuhi, Fanya hivyo muda wa usiku kabla ya kulala, Pata utulivu mwingi peke yako, Utakumbushwa ndoto nyingi.
iii) Mazungumzo
Njia nyingine ambayo humfanya Mungu arejeshe ndoto zetu kirahisi, ni katika mazungumzo, kumbuka kila eneo la maisha yako au wengine, yamkini Bwana alishawahi kusema na wewe, kwa njia ya ndoto, lakini hujui.
Kwamfano ukiwa na mwenzako, au wenzako, mnazungumza sana, Habari njema za kanisa, katika mazungumzo ya muda mrefu ikiwa lipo ambalo Bwana alikuonyesha, utaona kumbukumbu hiyo inakujia, au labda mnazungumza kwa kina Habari ya siku za mwisho, Kumbukumbu ya ndoto kama hiyo itakujia, au malengo ya maono yako.
Hivyo mazungumzo mazuri na yenye maana hurejesha fikra zilizopotea. Kwahiyo, jijengee desturi ya kuwa na mazungumzo mema.
Zingatia pia si kila ndoto hutoka kwa Mungu, ili kuweza kutofautisha ndoto za Mungu na za shetani, fungua link hii, uweze kupitia..>>>> https://wingulamashahidi.org/2019/09/03/nitajuaje-kama-ndoto-ni-ya-mungu-au-ya-shetani/
Mungu akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kuna ndege anaitwa kiruka njia, ambaye anatajwa kama mmoja wa ndege najisi, kwenye Kumbukumbu 14:15, lakini ndege huyu anasifa moja ambayo, huwa ina funzo kubwa sana la kiroho.
Tofauti na ndege wengine, ambao huruka aidha mchana, au usiku, kujitafutia chakula, kwamfano mwewe, mbayuwayu, korongo, tai, ni ndege wa mchana, lakini pia bundi, popo, ni ndege wa usiku, wote hawa hufanya kazi aidha majira ya kutwa nzima ya mchana, au usiku kucha.
Lakini kiruka njia, huruka zaidi, majira ya alfajiri sana, na jioni sana. Majira haya huyapendelea kwasababu, ni wakati wa mageuko ya siku, ambayo ndege wote wawindaji hujitandaa Kwenda mapumziko, au kuamka. Kwamfano muda wa jioni kama vile saa 12, ndege wakali wawindaji kama vile tai, mwewe, kipanga, n.k. wanaacha uwindaji, na kutafuta makao yao kupumzika, lakini pia wakati huo huo ndege wakali wa usiku kama vile bundi, hujiandaa kutoka waende kwenye mawindo yao saa mbili, Kwahiyo huo muda hapo Katikati mazingira kwake huwa si ya upinzani mkubwa.
Kwasababu yeye ni ndege dhaifu, na anaweza kuwindwa na ndege wakubwa, majira hayo kwake ni salama zaidi. Vivyo hivyo ule muda wa alfajiri sana, miale ya jua inapoanza kuonekana kwa mbali sana, hutoka na Kwenda kuwinda, muda huo ndege wa usiku ndio wanakwenda kulala, huku ndege wa mchana wanajiandaa kutoka, mpaka inapofika saa 12 asubuhi, tayari ameshamaliza uwindaji wake.
Licha ya kuwa wakati huo, ndege wengi hawapo hewani, lakini wakati huo, wa alfajiri sana na jioni sana, ndio makundi ya wadudu wengi wa ardhini hutoka kuruka juu, ikiwemo mbu, kumbikumbi, mchwa, nondo, mende n.k. kwasababu yeye hula wadudu, anaweza kukamata wadudu hata elfu moja ndani ya saa moja tu. Hivyo kwa muda mfupi sana akawa ameshashiba, zaidi ya mihangaiko mingi ya kutwa nzima, kugombani vyakula, na masumbufu mengi.
Ndege huyu mchana hupumzika zake, kwenye miti, na usiku pia, lakini hutumia alfajiri yake na jioni yake vizuri. Ndio maana ni vigumu kujulikana, kwasababu shughuli zake anazifanya wakati anga ni tulivu.
Hutufundisha nini?
Bwana alituambia tuwatafakari ndege (Mathayo 6:26)
Ni lazima tuthamini mida hii miwili, kuitumia kuwa uweponi mwa Bwana, Bwana Yesu alipendelea sana, kuamka alfajiri kuomba,
Marko 1:35 Hata alfajiri na mapema sana akaondoka, akatoka akaenda zake mahali pasipokuwa na watu, akaomba huko.
Ipo faida kubwa sana kuamka mapema kuomba kwasababu, muda huo anga ni tulivu, wakati watu wamelala, wewe unapokea thawabu za siku kutoka kwa Bwana. Kuna usemi unaosema biashara ni asubuhi, kwasababu wameona Riziki nyingi huwaga majira hayo, vivyo hivyo rohoni, ukijifunza kuomba majira hayo, na jioni pia kabla hujaimaliza siku, Basi utaona tofauti kubwa sana, na wepesi mwingi wa masumbufu ya siku.
Hawa ndege katika Walawi 11:13-19 ndio ndege gani kwasasa?
MTEGO HUTEGWA BURE, MBELE YA MACHO YA NDEGE YE YOTE.
Je tamaa ni dhambi kulingana na Yakobo 1:15?
Jina la Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe sana, karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu wetu lililo taa na mwanga wa njia yetu (Zab.119:105).
Yeremia 18: 1 “Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, kusema, 2 Ondoka, ukashuke mpaka NYUMBA YA MFINYANZI, na huko nitakusikizisha maneno yangu.
Yeremia 18: 1 “Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, kusema,
2 Ondoka, ukashuke mpaka NYUMBA YA MFINYANZI, na huko nitakusikizisha maneno yangu.
3 Basi nikashuka mpaka nyumba ya mfinyanzi, na tazama, alikuwa akifanya kazi yake kwa magurudumu. 4 NA CHOMBO KILE, ALICHOKUWA AKIKIFINYANGA, KILIPOHARIBIKA MKONONI MWAKE YULE MFINYANZI, ALIKIFANYIZA TENA KUWA CHOMBO KINGINE, kama alivyoona vema yule mfinyanzi kukifanya”.
Katika mstari wa 4 tunasoma kuwa Mfinyazi alikifinyanga chombo kilichoharibika na kuwa chombo kingine, zingatia hilo neno “chombo kingine” maana yake sio tena chombo kile cha kwanza kilichoharibika.
Tuchukue mfano labda mfinyazi huyu alifinyanga kikombe cha maji hapo kwanza, na baadae akaone kimeharibika au kina kasoro, ndipo anapokivunja vunja kile kikombe cha udongo na kuutia tena maji na kuufinyanga tena kuwa sahani..
Sasa udongo ni ule ule umeweza kutoa chombo kingine kipya tofauti na kile cha kwanza, na MUNGU alimwambia hivo hivyo YEREMIA, lakini Yeremia hayupo sasa, ila sisi tupo, hivyo anatuambia sisi kuwa tujifunze kwa Mfinyanzi kwakuwe yeye (MUNGU) ndiye mfinyanzi mkuu wa maisha yetu.
Yeremia 18: 5 “Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema, 6 Ee nyumba ya Israeli, je! Siwezi mimi kuwatendea ninyi vile vile kama mfinyanzi huyu alivyotenda? Asema Bwana. Angalieni, KAMA UDONGO ULIVYO KATIKA MKONO WA MFINYANZI, NDIVYO MLIVYO NINYI KATIKA MKONO WANGU, EE NYUMBA YA ISRAELI”.
Yeremia 18: 5 “Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema,
6 Ee nyumba ya Israeli, je! Siwezi mimi kuwatendea ninyi vile vile kama mfinyanzi huyu alivyotenda? Asema Bwana. Angalieni, KAMA UDONGO ULIVYO KATIKA MKONO WA MFINYANZI, NDIVYO MLIVYO NINYI KATIKA MKONO WANGU, EE NYUMBA YA ISRAELI”.
Je wewe ni chombo cha aina gani?..
Kama maisha yako yametawaliwa na dhambi basi fahamu kuwa ni dhahiri kuwa wewe ni chombo kilichoharibika, kama maisha yako yametawaliwa na ugomvi, uasherati, wizi, masengenyo, kiburi na mambo mengine yote ambayo ni kinyume cha Neno la MUNGU (yaliyotajwa kwenye Wagalatia 5:19-20), huu ni wakati wa wewe kumkimbilia mfinyazi Mkuu YESU KRISTO, akufinyange kuwa chombo kingine cha heshima..
Warumi 9:21 “Au mfinyanzi je! Hana amri juu ya udongo, kwa fungu moja la udongo kuumba chombo kimoja kiwe cha heshima, na kimoja kiwe hakina heshima?”
Bwana YESU anaweza kukufanya kuwa mwingine kabisa, mtu wa maana kabisa, ambapo ile hali yako ya ulevi wa pombe au ulevi wa anasa inayokusumbua, kinachotakiwa tu ni kukiri kuwa wewe ni mkosaji mbele zake na unahitaji msaada wake, na baada ya hapo kutubu dhambi zako mbele yake huku ukidhamiria kabisa kuacha mambo yote mabaya, na kumwambia naomba unifinyange tena, kupitia Roho wake mtakatifu atakayeingia ndani yako atakugeuza na kuwa mtu mwingine.
Kumbuka toba isiyo ya kumaanisha haileti matokeo yoyote kwa mtu anayetaka mabadiliko, hakikisha unapotubu dhamiria kujitakasa, kwa kujitenga na vichocheo vyote vya dhambi, kama ulikuwa ni mlevi acha kwenda Bar, kama ulikuwa unajiuza jizuie kwa bidii kwenda vituo vya ulivyokuwa unafanya biashara hiyo, ili uumpe nafasi Roho Mtakatifu ndani yako kukufinganya upya kuwa chombo kingine.
2Timotheo 2:21 “Basi ikiwa mtu amejitakasa kwa kujitenga na hao, atakuwa chombo cha kupata heshima, kilichosafishwa, kimfaacho Bwana, kimetengenezwa kwa kila kazi iliyo njema”.
Bwana YESU akubariki sana.
Zaburi 145:19 “Atawafanyia wamchao matakwa yao, Naye atakisikia kilio chao na kuwaokoa”.
Pamoja na kwamba tumeagizwa kuomba “Mapenzi yake yatimie/yatimizwe (Mathayo 6:10”.
Lakini “Siri” moja kuu ni kwamba zaidi ya asilimia 90 ya Maombi ya wanaomcha MUNGU ni mapenzi ya MUNGU.Kwanini?..
Kwasababu maandiko yanatuambia hapo kuwa “Atawafanyia wamchao matakwa yao, Naye atakisikia kilio chao na kuwaokoa”.
Zingatia hilo neno “Atawafanyia wamchao matakwa yao”.
Kumbe Mungu anawapatia watu wake wanaomcha “Matakwa yao, yaani haja zao wanazozitaka”.
Kwa mtu anayemcha Mungu akiomba amani, ni asilimia kubwa ya hitaji lake hilo kuwa ni mapenzi ya MUNGU.
Mtu anayemcha MUNGU akiomba afya, ni asilimia zaidi ya nusu kuwa anaomba jambo ambalo ni mapenzi ya MUNGU.
Mtu anayemcha MUNGU akiomba akiomba mambo mengine yote ikiwemo mafanikio ya kiroho na kimwili ni mapenzi ya MUNGU, kwasababu MUNGU anawapa wamchao matakwa yao.
Je unataka kupewa matakwa yako na MUNGU?.Jibu ni rahisi “Mche Mungu tu”..Na Biblia inasema kumcha Mungu ndio hekima na kuepukana na uovu ndio ufahamu (Ayubu 28:28).
Sasa hatuwezi kumcha MUNGU kwa nguvu zetu, inahitajika kuwezeshwa na Roho Mtakatifu, kwasababu tabia ya kumcha MUNGU, ni zao la Roho Mtakatifu.Isaya 11:2 “Na roho ya BWANA atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, ROHO YA MAARIFA NA YA KUMCHA BWANA”.
Sasa kama kumcha Bwana ni zao la Roho Mtakatifu, je tunampataje Roho Mtakatifu..
Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? 38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”
Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”
Kumbe kanuni ya kupokea Roho ni kutubu na kubatizwa kwa jina la YESU KRISTO!.
Basi maana yake tukitubu na kubatizwa tutapokea Roho Mtakatifu kama ilivyoandikwa, na matokeo ya kujaa Roho Mtakatifu, ni uwezo wa kumcha MUNGU kuingia ndani yako.Na matokeo ya kumcha MUNGU sana ni kusikiwa maombi yako na Bwana kukupa matakwa yako.
Je umeokoka?..Je unamcha Bwana?.
Zaburi 112:1 “Haleluya. Heri mtu yule amchaye BWANA, Apendezwaye sana na maagizo yake. 2 Wazao wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa”. 3 Nyumbani mwake mna utajiri na mali, Na haki yake yakaa milele”.
Zaburi 112:1 “Haleluya. Heri mtu yule amchaye BWANA, Apendezwaye sana na maagizo yake.
2 Wazao wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa”.
3 Nyumbani mwake mna utajiri na mali, Na haki yake yakaa milele”.
Jina la Bwana YESU libarikiwe, karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu wetu, lililo taa na Mwanga wa njia yetu.
Utatamani kutembea na wenye vyeo vikubwa vya ulimwengu, ambao wengi wa hao ni wafu kiroho,
Utatamani kuolewa na wenye mali nyingi, na uwezo mkubwa ambao wengi wa hao ni wafu rohoni.
Utawadharau wanaoonekana dhaifu na wanyonge ambao Biblia inawataja kama matajiri wa imani na walio hai kiroho..
Yakobo 2:5 “Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni, Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao?”
Dada ni heri uambatane na huyo mtu ambaye unamwona leo ni maskini lakini anaye YESU, kuliko uende kuolewa na tajiri ambaye hana YESU maishani ( ni mfu kiroho).
Heri uwe na marafiki maskini lakini wanaye YESU kuliko uwe na marafiki matajiri ambao ndani yao hawana uzima.
Huyo tajiri kwako ni “Simba” na huyo maskini kwako ni “Mbwa”…ambaye ni kama hana hadhi mbele ya macho yako lakini Biblia inatufundisha kinyume na hilo..
Mhubiri 9:4 “Kwa kuwa liko tumaini kwa yule aliyeambatana na wote walio hai; (maana ni afadhali mbwa aliye hai kuliko simba aliyekufa)”.
Ni afadhali mbwa, anayeishi, maana yake ni heri mtu maskini na mdhaifu mwenye uhai wa rohoni kuliko mtu aliye simba (yaani mwenye nguvu na mkali) lakini ni mfu rohoni.
Chagua kwa makini nani wa kuambatana naye..
2 Wakorintho 6:14 “Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?
15 Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari?Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini?”
Bwana atusaidie..
Kitendo cha kumtia mtu adabu ndio kuadibu. Maana yake kuchukua hatua za makusudi kuadhibu, au kukaripia, au kuonyoosha mwenendo lakini kwa lengo la kujenga sio kulipiza kisasi.
Neno hilo utalipata kwenye vifungu hivi.
Zaburi 94:12
[12]Ee BWANA, heri mtu yule umwadibuye, Na kumfundisha kwa sheria yako;
Zaburi 94:10
[10]Awaadibuye mataifa asikemee? Amfundishaye mwanadamu asijue?
Mungu akiitwa Baba, basi tujue kuwa sisi ni watoto wake, na kama ni watoto wake basi atatuadabisha pale tunapokosea..
Kubali kuadibiwa na Bwana…
Shalom.
Beliari ni nini? (2Wakorintho 6:15)
‘laana ya torati’ maana yake ni nini?
Mapokeo ni nini?
Jina la Mwokozi YESU libarikiwe, karibu tujifunze Biblia, Neno la MUNGU wetu lililo taa na Mwanga wa njia yetu (Zab. 119:105).
Sayansi ya mwili inatuonesha kuwa “moyo” wa mtu upo upande wake wa “kushoto”..jambo ambalo ni kweli kabisa, ukiweka mkono wako kufuani utaona moyo ni kama umelalia upande wa kushoto.
Lakini katika roho ni kinyume chake, Kwani Biblia inatufundisha kuwa Moyo wa mwenye hekima upo upande wake wa kulia(kuume), na kinyume chake moyo wa mpumbavu upo upande wake wa kushoto.
Mhubiri 10:2 “MOYO WAKE MWENYE HEKIMA UPO UPANDE WA KUUME; Bali moyo wake mpumbavu upo mkono wa kushoto”.
Sasa kwanini inasema moyo wa mwenye hekima upo upande wake wa kuume na wa mpumbavu upo upande wake kushoto?..
Je kuna ubaya gani moyo kuwepo upande wa kushoto kiroho?.
Jibu ni la! Lakini Kibiblia mkono wa Kuume unawakilisha “WINGI WA SIKU” na mkono wa kushoto unawakilisha “UTAJIRI NA HESHIMA”.
Mithali 3:16 “Ana wingi WA SIKU KATIKA MKONO WAKE WA KUUME, Utajiri na heshima katika mkono wake wa kushoto”.
Wingi wa siku unaozungumziwa hapo ni “Uzima wa milele”….kwahiyo mtu mwenye hekima moyo wake utaegemea zaidi kufikiri habari za “Wingi wa siku” yaani uzima wa milele siku zote.
Yaani akose kila kitu lakini si uzima Uzima wa milele/Wingi wa siku..
Lakini kinyume chake mtu mpumbavu moyo wake utakuwa unaegemea zaidi habari za “Utajiri na heshima”..na wala hawazi sana juu ya “Wingi wa siku/Uzima wa milele).
Hawazi baada ya miaka yake kuisha hapa duniani atakuwa wapi huko anakokwenda…
Je moyo wako upo upande gani? Wa “Uzima wa milele” au mali na fahari za dunia?…Upo upande wa kuume au wa kushoto?.
Sasa si vibaya kuwa tajiri na kupata heshima duniani, ni vizuri lakini iwe ni sehemu ya kushoto ya maisha yetu, na si upande wetu wa kuume.
Kwasababu Bwana YESU alisema..
Marko 8:36 “Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake?
37 Ama mtu atoe nini badala ya nafsi yake?”
Kuna faida gani kupata utajiri wote na hauna uzima wa milele?..
Geuka leo hii na ufanye moyo wako ukae kuumeni mwako?..Fikiri zaidi kuhusu uzima wa milele, (wingi wa siku).
Kumbuka YESU anarudi, na uzima huu wa milele upo tu kwake na si kwa mwingine..
1 Yohana 5:11” Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe.
12 Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima”.
Zaburi 110:5 “Bwana yu mkono wako wa kuume; Ataseta wafalme, Siku ya ghadhabu yake”.
Bwana atusaidie.
Katika Biblia tunajifunza jambo kubwa sana kwa mwanamke “Hana” ambaye alikuwa tasa lakini baadae Bwana alimfungua tumbo lake na kuzaa watoto.
Katika usomaji wa kitabu cha 1Samweli mlango wa kwanza na wa pili, ni rahisi kufikiri kuwa Hana alimwekea MUNGU nadhiri ya kumtoa mtoto wake wa kwanza atumike kwenye nyumba ya MUNGU daima, bila kuwa na ufunuo au sababu yoyote (ni rahisi kufikiri hilo).
Lakini tukijifunza kwa undani, tunaona wazi kuwa sababu kuu ya Hana kumtoa mtoto wake wa kwanza (Samweli) atumike kwenye nyumba ya MUNGU daima, ni matatizo aliyoyaona ndani ya nyumba ya MUNGU, kwa wakati ule.
Kwani walikuwepo wana wawili wa kuhani Eli, walioitwa Hofni na Finehasi, vijana hawa hawakuwa waaminifu katika nyumba ya MUNGU,
Kwani walikuwa wanatumia vibaya dhabihu na sadaka zilizokuwa zinaletwa nyumbani mwa Bwana, na zaidi sana walikuwa wakizini na wanawake waliokuwa wakihudumu ndani ya nyumba ya MUNGU, na sifa zao hizo mbaya zilijulikana na watu wote, na hata mwanamke “Hana” aliwajua kwa sifa hiyo.
1 Samweli 2:22 “Basi Eli alikuwa mzee sana; naye alisikia habari za mambo yote ambayo wanawe waliwatenda Waisraeli; na jinsi walivyolala na wanawake waliokuwa wakitumika mlangoni pa hema ya kukutania.
23 Akawaambia, Mbona mnatenda mambo kama hayo? Maana nasikia habari za matendo yenu mabaya kwa watu hawa wote.
24 Sivyo hivyo, wanangu, kwa maana habari hii ninayoisikia si habari njema; mnawakosesha watu wa BWANA.
25 Mtu mmoja akimkosa mwenzake, Mungu atamhukumu; lakini mtu akimkosa BWANA, ni nani atakayemtetea? Lakini hawakuisikia sauti ya baba yao, kwa sababu BWANA amekusudia kuwaua”.
Kwasababu hiyo basi Hana, aliona shukrani pekee ambayo anaweza kumpa MUNGU endapo Mungu atamfungua tumbo lake si kutoa pesa, kwasababu hata akizipeleka madhabahuni nyumbani mwa MUNGU zitatumiwa vibaya na wale vijana wawili wa Eli (Hofni na Fineasi), wala si dhabihu kwasababu pia zinatumika vibaya.
Ndipo alipotafakari na kuona nadhiri bora na sadaka maalumu itakuwa ya kumtoa mwanae wa kwanza kwa Bwana akawe Mtumishi wa madhabahuni,
Hiyo aliona inaweza kuwa sadaka njema kwake kwa BWANA, Kwani mtoto yule atakuwa katika misingi sahihi ya kiMungu, na atasimama katika kazi ya nyumba ya Bwana kwa uaminifu na kuwa baraka kwa Israeli yote.
Ndivyo Hana alivyofanya, na kupitia sadaka yake hiyo ya kiufunuo, Mungu alisikia maombi yake na kumpa mtoto Samweli, ambaye ndiye aliyekuja kuwaa nabii mkuu Israeli kwa wakati ule.
Ni hivyo hivyo kwa MUNGU wetu, aliona baraka kubwa atakayoibarikia dunia si kuleta mvua nyingi yenye kustawisha nafaka ili matatizo ya njaa yaishe duniani, wala si kumfanya kila mtu kuwa milionea, bali ni kwa kumtoa mwanae pekee YESU KRISTO, Kama dhabihu iliyo hai na sadaka kuu, na kupitia sadaka hiyo leo hii tunabarikiwa kwa baraka zote.
Na sisi tunajifunza mambo hayo hayo, kutazama katika roho ni nini cha kumtolea BWANA, si kila wakati fedha au mali zitakuwa ni sadaka sahihi kwa MUNGU au kwa Nyumba yake au kazi ya MUNGU, wakati mwingine wewe mwenyewe unaweza kuwa sadaka bora kwa kujitoa mwili wako na muda wako kutumika.
Warumi 12:1 “Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.
Au si wewe bali mwanao anaweza kuwa bora zaidi na akawa sadaka yenye kumpendeza Bwana. (Kwa wewe kumuandaa kuwa mtumishi, kwa kumfundisha, kumwombea na kumtolea sadaka kwa MUNGU).
Kuna wakati ardhi inaweza kuwa sadaka nzuri kwa Bwana zaidi ya fedha, kuna wakati, kununua kitu na kukipeleka nyumbani mwa Bwana inaweza kuwa bora zaidi kuliko kutoa tu fedha, na kuna wakati fedha ni muhimu zaidi kuliko kitu utakachopeleka, hivyo ni muhimu kuwa na jicho la kiroho na kujua ni kipi kinafaa kutoa kwa wakati huo.
Na kumbuka siku zote, ni heri kutoa kuliko kupokea (Matendo 2:35).
Bwana YESU atusaidie katika kumtolea yeye matoleo yenye kumpendeza.
Biblia inatuonyesha Mungu ndiye muumba wa vitu vyote
Mwanzo 1:1 Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.
Lakini hatujui ni nini kilitokea baadaye kikaifanya dunia kuwa ukiwa, mpaka akaanza kuirekebisha tena dunia aliyoiumba mwanzo..
Kwasababu mstari wa 2..unasema nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji,
Mungu akaanza tena kuifanya ikaliwe na watu, akaleta tena nuru kutoka kwenye giza, akayatenga maji, na kuyaweka sehemu stahiki, akalitokeza anga..akamuumba mwanadamu.
Dunia ikawa nzuri tena, lakini baadaye mwanadamu akaasi, akaiharibu duniani, mpaka ikaangamia kwa maji.
Bado Mungu hakuikatia tamaa dunia yake, akawaongeza, Nuhu na wazao wake, baadaye akamchagua Ibrahimu ili kumwandaa mkombozi atakayeikomboa dunia kikamilifu, akaja Kristo ulimwenguni ndio mwokozi wetu.
Watu wakaokolewa, ijapokuwa waliendelea kuiharibu dunia, bado Mungu akawa kwenye mwendelezo wa uumbaji wake unaoharibiwa .
Na kama tunavyojua Kristo aliahidi kurudi tena duniani mara ya pili, kuwanyakua watu wake, kisha kuukarabati huu ulimwenguni na kuufanya kuwa mbingu mpya na nchi mpya.(Ufunuo 21)
Hivyo kama ukichunguza asili ya tabia ya Mungu, si kufanya kitu mara moja, kisha pale kinapoharibika anakikatia tamaa ..
Hapana utaona hukiumba tena na tena na tena…kwa miaka na miaka na miaka..tena huanzia mbali sana mpango wake wa ukarabati..
Na sisi ni lazima tujue tumeumbwa kwa mfano wake na sura yake..ikiwa unaona hakuna mwenye hekima duniani kumzidi Mungu, na kila lifanyalo ni bora, na kamilifu basi jifunze kuiga tabia zake ufanikiwe…
Mungu wetu alikuwa na siku moja katika juma ya kupumzika, wewe si ‘busy’ zaidi ya Mungu mpaka siku zote saba katika juma, mwaka mzima unafanya kazi mpaka unakosa muda wa kumwabudu Mungu wako.
Vivyo hivyo ni lazima kutambua kuwa kazi zake zimepitia changamoto nyingi sana za kuharibiwa zaidi ya zako lakini amekuwa katika uumbaji wake kila siku..Na wewe pia kuharibiwa kwa maono yako, si sababu ya kukata tamaa na kusema sitaendelea mbele…inuka anza tena na tena..
Unamtumikia Mungu, ile huduma iliyokaa ndani yako, ni kama imekufa, mwanzoni uliona hatua lakini sasa huoni, pengine ni kutokana na kuwa umedhulumiwa, umeibiwa, umefukuzwa..inuka tena na tena, anza upya..
Kuacha kazi uliyokwisha itaabikia na kuitolea jasho jingi, ni ishara ya kuwa bado tabia ya Mungu haijaumbika ndani yako.
Kumbuka mpaka leo hii Mungu anaendelea kufanya uumbaji wake, ijapokuwa kazi hizo zingepeswa zikamilike tangu kule mwanzo…Wewe ni nani usifanye matengenezo yako yaliyokufa kila siku?
Anza sasa. Fanya kazi na Mungu.
MBONA MMESIMAMA HAPA MCHANA KUTWA BILA KAZI?
USIMPE MWANAO VITU SASA.
2 Samweli 23:9-10
[9]Na baada yake kulikuwa na Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu waliokuwa pamoja na Daudi; walipowatukana Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko ili kupigana, na watu wa Israeli walikuwa wamekwenda zao; [10]huyo aliinuka, akawapiga Wafilisti hata mkono wake ukachoka, na mkono wake ukaambatana na upanga; naye BWANA akafanya wokovu mkuu siku ile; nao watu wakarudi nyuma yake ili kuteka nyara tu.
[9]Na baada yake kulikuwa na Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu waliokuwa pamoja na Daudi; walipowatukana Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko ili kupigana, na watu wa Israeli walikuwa wamekwenda zao;
[10]huyo aliinuka, akawapiga Wafilisti hata mkono wake ukachoka, na mkono wake ukaambatana na upanga; naye BWANA akafanya wokovu mkuu siku ile; nao watu wakarudi nyuma yake ili kuteka nyara tu.
Kibaolojia mwili wa mwanadamu unapokamata kitu, kwa muda mrefu sana, kwa nguvu, huwa unatabia ya kukakamaa katika hali hiyo hiyo hata kama mtu huyo hatakuwa na nia ya kuendelea kukishikilia kitu hicho.
Ndicho kilichomkuta huyu shujaa wa Daudi, alipokutana na jeshi la wafilisti angali yupo peke yake. Aligundua kitu pekee ambacho kingeweza kumtetea ni upanga wake. Hivyo aliukamata kwa nguvu sana bila kuuachia, akaanza kupambana na wafilisti wale kwa muda mrefu, hakujua kuwa mkono wake utabakia katika hali ile ile…yeye aliendelea tu kupigana vita, mpaka baadaye aliposhangaa kuona hana jitihada yoyote tena ya kuushika upanga, ni kama vile ulikuwa ni sehemu ya kiungo chake…kazi yake ilikuwa ni kurusha tu mkono kuupeleka anapotaka, huku upanga ukiwa tu pale pale kiganjani hautoki…
Kikawaida hali ikishafikia hatua hiyo huwa inamgharimu mtu masaa mengi hata siku, ili kung’atuka kutoka kwenye kitu kilichoshikamana naye..wakati mwingine ili kuharakisha uponyaji, wengine hutumia maji ya uvuguvugu na kuchua kiganja kwa muda baadaye kunyosha kidole kimoja baada ya kingine…
Sasa askari wa mwilini ni kivuli cha mtu wa rohoni. Yeye naye ana mikono na analazimika wakati wote kuwa na upanga…Lakini si upanga tu, wa kushika, bali ule Ugandao na mkono.
Waefeso 6:11-14,17
[11]Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. [12]Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. [13]Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.
[11]Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.
[12]Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.
[13]Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.
[14]Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,..
[17]Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;
Kama maandiko yanavyotuonyesha hapo Mtu wa rohoni, hulazimika kubeba upanga wake, ambao ni Neno la Mungu.
Tunapoonyesha nia ya kuling’ang’ania Neno la Mungu, mwanzoni ni kama tutatumia jitihada zetu, lakini haitakuwa hivyo mbeleni …baadaye litashikamana na sisi..maana yake haitakuwa jitihada tena kuliishi.
Jambo lolote la kiroho, mfano maombi ya masafa marefu, mwanzoni ukianza utaona kama ni jitihada zinatumika lakini ukiendelea mara mbili, mara tatu utaona ni kawaida..
Mambo yote ya rohoni iwe ni upendo, unyenyekevu, utaanza kwa jitihada fulani lakini Kwasababu umekusudia tu kung’ang’nia kwa nguvu, utagandamana navyo.
Kumbuka hakuna wepesi wowote utakuja bila mtu kutia nia kwanza. Anza sasa kutendea kazi Neno la Mungu.