NABII ALIYEHUDUMIWA NA NYUNI MCHAFU

Eliya alipoagizwa na Mungu kuzifunga mbingu kwa miaka mitatu na miezi sita, aliagizwa aelekee, karibu na kijito cha kedroni, na huko Mungu atamuhudumia kupitia kunguru kumleta mkate na nyama, asubuhi na jioni.

1 Wafalme 17:2-6

[2]Neno la BWANA likamjia, kusema,

[3]Ondoka hapa, geuka, uende upande wa mashariki, ujifiche karibu na kijito cha Kerithi kinachokabili Yordani.

[4]Itakuwa utakunywa maji ya kile kijito; nami nimewaamuru kunguru wakulishe huko.

[5]Basi akaenda akafanya kama alivyosema BWANA; kwa kuwa akaenda akakaa karibu na kijito cha Kerithi, kinachokabili Yordani.

[6]Kunguru wakamletea mkate na nyama asubuhi, na mkate na nyama jioni, akanywa maji ya kile kijito.

Unaweza ukajiuliza kwanini hakumwagizia malaika wake kama alivyomfanyia wakati ule anaelekea mlima Herobu (1Wafalme 19:4-8), au kwanini asimwagizie mtumishi wake, au mnyama safi kama huwa (njiwa), kinyume chake anamuagizia kunguru mnyama mchafu na najisi.

Kwa wakati ule ndege hawa waliwekwa miongoni mwa ndege wachafu wa hali ya juu sana. Hivyo chochote kilichoguswa na wanyama hawa hakikuliwa..lakini Mungu alimwagiza Kunguru huyo huyo amletee Eliya chakula.

Mara nyingi njia na kanuni za Mungu hazichunguziki, Si kila wakati Mungu atatumia watu wema sana, kama tunavyodhani kutuhudumia kimahitaji.

Kunguru hajui kusoma, hakujui kuandika, lakini alisikia agizo la Mungu.

Watu hawa rohoni si lazima wajue theolojia, wajue kanisa, wajue njia za haki, lakini Mungu akiwaamuru, watafanya tu.

Kwanini Mungu anafanya hivi wakati mwingine, ni kutushusha kiburi chetu, na kumwachia hukumu yote yeye mwenyewe.

Mungu anaweza kumwagiza mtu wa dini nyingine, kuisapoti huduma yako. Lakini hilo lisimaanishe kwamba Mungu amemkubali..

Anaweza kutumia maskini, kukutoa mahali fulani na kukupeleka kwingine, anaweza tumia mtu nje ya duara lako, kutenda kitu kwako wewe mwana wa Mungu.

Huyo unayemdhania kwenye akili yako, anaweza asifanye, yule usiyekuingia akilini ndio akatumiwa kufanya.

Eliya angeweza kusema Aah! Bwana…umeshindwa kuniletea Gabrieli, mbona nisingenajisika, lakini Bwana anasema kunguru ndiye nimemwagiza kwako.

Swali, vipi kama kunguru ndiye anayekufadhili kwasasa…Je utamlaumu Bwana?

Kumbuka uumbaji wote bado unamtii Mungu, haijalishi umetengwa naye, kwa umbali mrefu kiasi gani. Bado ni milki ya Bwana.

Mjue sana Mungu ili uwe na amani!

SALA.

Bwana Yesu! Asante kwa kunifumbua macho yangu na kunijuza kuwa ulimwengu wote unakutii wewe, naomba niwe mwepesi kupokea neema zako mbalimbali kwa namna ambayo zinatimiza mapenzi yako, bila mimi kunajisika. Asante kwa hilo, nimeamini, nimepokea. Amen.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Desturi ya maziko kibiblia ilikuwaje?.

Swali: Je Desturi ya kuzika ilikuwaje, ikiwemo upakaji wa manukato maiti?


Jibu: Awali ya yote ni muhimu kujua kuwa katika Biblia, hakukuwa na sheria ya kuvika sanda mwili wa mtu aliyekufa, wala kuupaka manukato,

Mtu akifa anakuwa amekufa, na liliobaki ni moja tu kwake, kwamba mwili wake uzikwe.

Desturi ya kuvika mwili wa marehemu sanda na kuupaka manukato ulikuja baada ya wana wa Israeli kurudi kutoka Babeli, ambapo marabi wa kiyahudi waliaanza kuutumia huo utaratibu wa kuuvika mwili wa marehemu kitambaa cheupe na kuupaka manukato.

Na pia katika nyakati za Biblia, watu hawakuzikwa kwenye majeneza ya mbao kama ilivyozoeleka leo, badala yake walizikwa kwenye mapango ya asili au makaburi yaliyochongwa kwenye miamba (kama lilivyokuwa kaburi la Abrahamu huko Makpela, Mwanzo 23:19 au kaburi la BWANA wetu YESU KRISTO)

Baada ya miaka kadhaa, miili ikishaoza na kubaki mifupa tu, mifupa hiyo ilikusanywa na kuwekwa kwenye sanduku dogo la mawe  au kuwekwa sehemu moja na mifupa ya mababu zao (ndio maana ya msemo wa kibiblia “alilazwa pamoja na mababu zake”).

Mwanzo 49:33 “Basi Yakobo alipokwisha kuwaagiza wanawe, akakunja miguu yake kitandani, akafa, akakusanywa pamoja na watu wake”.

Na katika Biblia pia hakukuwa na sheria ya kuchoma maiti bali miili yote ilizikwa kwa heshima.

Sasa swali?.. Ni kwanini akina Maramu Magdalena na wale wanawake wengine walikwenda kaburini mapema siku ya kwanza ya juma kumpaka Bwana Manukato?.

Marko 16:1 “Hata sabato ilipokwisha kupita, Mariamu Magdalene na Mariamu mamaye Yakobo, na Salome walinunua manukato wapate kwenda kumpaka.

2 Hata alfajiri mapema, siku ya kwanza ya juma, wakaenda kaburini, jua lilipoanza kuchomoza;

3 wakasemezana wao kwa wao, Ni nani atakayetuvingirishia lile jiwe mlangoni pa kaburi?”

Kulingana na mapokeo hayo ya wayahudi ambayo yalianza baada ya wao kutoka Babeli (lakini si agizo la Musa), ilikuwa ni sharti mwili uandaliwe kwa kupakwa manukato kabla ya kuzikwa.

Lengo la kufanya hivyo ni kupunguza harufu kipindi mwili unaanza kuoza, na kwasababu hawakuzika ardhini kama inavyofanyika sasa hivyo kama mwili usipopakwa hayo manukato harufu ingewasumbia wapita njia nje na mapango hayo, hivyo kulizuia hilo na kutunza heshima ya marehemu waliipaka miili manukato.

Na pia miili ya wanaume iliandaliwa na wanaume na wanawake iliandaliwa na wanawake, lakini katika mazingira fulani maalumu iliruhisiwa miili ya wanaume kuandaliwa na wanawake wa karibu sana, hususani wale wana familia wa karibu kutunza heshima na faragha ya marehemu., lakini haikuruhusiwa wanaume kuiandaa mikli ya wanawake kwa mazingira yoyote yale.

Sasa swali lingine kwanini akina Mariamu waende siku ya 3 na si ile siku aljyokufa?.

Jibu ni kuwa Kristo alikufa ijumaa jioni, hivyo nafasi ya kuuandaa mwili ilikuwa ni ndogo sabato ilikuwa imekaribia, na haikiruhisiwa kufanya maziko siku ya sabato.

Hivyo akina Yusufu na Nikodemo, waliuandaa ule mwili kwa hafaka haraka na kuufungua manukato, na wanawake walktama kuundaa vizur zaidi na kwa utaratibu.

Swali je na sisi ni kosa kuzika watu kwenye majeneza au ardhini? Au kutoipaka miili manukato? Au je ni lazima kuuvisha mwili sanda?.

Jibu ni la! Si kosa kuzika mtu kwenye jeneza  na pia si lazima kuvika maiti sanda kwani hata desturi hiyo haikutoka kwa MUNGU, asili yake ni wapagani ambapo ili kuweka usawa wa matajiri na masikini, wote walifungwa kwenye kitambaa cheupe, kwani hapo kwanza matajiri walizikwa na nguo za thamani na masikini kwa nguo za hadhi ya chini.

Kwahiyo si desturi ya lazima, na pia si kosa kuzika mwili kwa sanda kama Bwana YESU alivyozikiwa.

Lililo kubwa na la kuangalia sana ni wapo roho zetu zinapokwenda baada ya kufa, je tutaurithi uzima wa milele au tutapotea kwenye moto wa milele.

Lakini kufikiri juu ya maiti na mavazi yake, kwamba tutazikwaje ni tafakari dhaifu zisizotusaidia.

Je umeokoka?..una uhakika Bwana YESU akija leo unaenda naye?.

Kama hauna uhakika huo una subiri nini?. Mpe YESU maisha yako aiku ya leo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NENO NA MAOMBI~ Sehemu ya 3 (UTAKASO WA KINYWA)

Jina la Bwana YESU libarikiwe, karibu katika kujifunza Neno na Maombi.

Utangulizi: Kusoma Neno bila Maombi, au kuomba bila Neno la kusimama nalo ni sawa na kitamba cha bendera kisicho na mlingoti, kupitia mfululizo huu na tafakari hizi tutapata mwongozo sahihi wa kuomba kwa kusimama na maandiko ya Biblia.

Biblia inataja ulimi wa mtu, kama kiungo kiharibifu kuliko viungo vyote katika mwili.

 Yakobo 3:5 “Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana.

6 Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum”.

Sasa kwasababu ulimi ni kiungo hatarishi,maana yake kinaweza kumfanya mtu kuanguka moja kwa moja pasipo kuamka tena, hivyo andiko hili halijahifadhiwa ndai ya Biblia liwe tangazo la taarifa tu, kwamba tujue hatari ya ulimi halafu basi.

Hapana, si lengo la maandiko yote ya Biblia, bali maandiko yote yana lengo la sisi kusoma, na kujitengeneza kulingana na andiko hilo kwa njia ya kuomba…hivyo tumia muda kuomba maombi yafuatayo

 1. OMBA UTAKASO WA ULIMI.(tumia Dk. 30 au zaidi).

– Takasa kinywa chako, kwa kutubia maneno yote mabaya na mazungumzo yasiyofaa yaliyotoka kinywani mwako na omba utakaso kwa damu ya YESU.

 2. MWOMBE BWANA AKAKUTENGENEZE MANENO YA KINYWA CHAKO.

– Ukanene kwa hekima.

Zaburi 49:3 “Kinywa changu kitanena hekima,

Na fikira za moyo wangu zitakuwa za busara”

Ukanene kweli siku zote usiseme uongo.

Mithali 8:7 “Maana kinywa changu kitasema kweli, Na uovu ni chukizo kwa midomo yangu”.

  3. OMBA ULINZI WA KINYWA.

Mithali 13:3 “Yeye alindaye kinywa chake huilinda nafsi yake; Bali afunuaye midomo yake atapata uharibifu”.

– Usiwe mtu wa kupayuka.

Zaburi 141:3 “Ee BWANA, uweke mlinzi kinywani pangu, Mngojezi mlangoni pa midomo yangu”

– Usifanye dhambi (mf. Uongo, usengenyaji, matukanio, malalamiko na faraka).

Ayubu 31:30 “(Naam, sikukiacha kinywa changu kufanya dhambi Kwa kuutaka uhai wake kwa kuapiza);

   4. KEMEA KILA ROHO INAYOJIINUA KUKUKOSESHA KUPITIA ULIMI (KINYWA) CHAKO.

Kemea kwa jina la YESU KRISTO kila pando la la uongo, usengenyaji ndani  yako, kanisani kwako, familia yako  na wakristo wenzako wote.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

 

 

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ipi tofauti kati ya sherehe, Sikukuu na karamu kibiblia?.

Jibu: Tutazame moja baada ya nyingine.

     1. SHEREHE.

Katika Biblia hamna neno “sherehe” lakini kuna neno “sikukuu”.

Sherehe ni shughuli (tukio) la kijamii linayofanyika kwa lengo la kuadhimisha, kukumbuka jambo fulani  (kama vile  harusi, mahafali, siku ya kuzaliwa, ushindi n.k),

Na sherehe huwa inaambatana na michezo, au hotuba,  au ibada au michezo, kutegemea na aina ya sherehe..(na katika Biblia hatuna neno sherehe).

Kama jina sherehe lilivyo maana yake linahusisha “shangwe” au “shamra shamra”.

   2. SIKUKUU.

Sikuukuu ni neno linalopatikana kwenye Biblia, na tafsiri ya Neno Sikukuu ni “Siku iliyo kuu”. (Yaani siku yenye ubora kuliko nyingine)

Na katika Biblia zinatajwa sikukuu kadha wa kadha, ambazo hazikuwa kwa lengo la ibada na tafakari za kiMUNGU, mfano wa sikukuu hizo ni sikukuu ya vibanda, pasaka, na baragumu.

Kwa urefu juu ya Sikukuu hizo na maana zake kiroho fungua link ifuatavyo.

https://wingulamashahidi.org/archives/1858Karamu.

   3. KARAMU.

Karamu ni neno linalopatikana kwenye Biblia ambalo lina maana ya tafrija yenye mandalizi ya chakula.

Kwa ufupi ni shughuli yoyote ndogo au kubwa yenye malengo makuu ya kula vyakula na kufurahi kutokana na tukio fulani jema.

Katika Biblia kunatajwa karamu mbalimbali mfano wa hizo ni ile Abramu aliyowafanyia wale Malaika wawili waliomtembelea.

Mwanzo 19:1 “Basi, wale malaika wawili wakaja Sodoma jioni; na Lutu alikuwa amekaa mlangoni pa Sodoma. Lutu akawaona akaondoka akaenda kuwalaki, akainama kifudifudi.

2 Akasema, Bwana zangu, karibuni nawasihi mwingie nyumbani mwa mtumwa wenu, mkalale, mkanawe miguu yenu, hata asubuhi mwondoke na mapema mkaende zenu. Wakasema, Sivyo, lakini tutakaa uwanjani usiku kucha.

3 Akawasihi sana, nao wakaja, wakaingia nyumbani mwake. AKAWAFANYIA KARAMU, akawapikia mikate isiyochachwa nao wakala.”

Na ile Abramu aliyomfanyia mwanae baada ya kuachishwa maziwa.

Mwanzo 21:8 “Mtoto akakua, akaachishwa kunyonya; Ibrahimu akafanya karamu kuu siku ile Isaka alipoachishwa kunyonya.”

Lakini ipo karamu iliyo kuu katika Biblia ambayo haipaswi mtu yoyote kuikosa ambayo ni ile ya Mwanakondoo.

Kwa urefu juu ya karamu ya mwanakondoo ni fungua link ifuatayo..

https://wingulamashahidi.org/archives/1280

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE KUOMBA NI KARAMA?

Swali: Je kuomba ni moja ya karama za rohoni?..na kama ndio mbona hatuioni miongoni mwa zile tisa (9) zilizotajwa katika 1Wakorintho 12?.

Jibu: Kwa asili Kuomba sio karama bali ni “Agizo”.

Na agizo la kuomba si la mtu mmoja bali ni la watu wote wenye karama zote,

Kwasababu hata mwenye karama ya kinabii ni lazima awe mwombaji kwa lengo la kuinoa karama yake au kuwaombea wale aliowapa unabii..

Vile vile mwenye karama ya uponyaji ni lazima aombe na kufanya maombezi ili mgonjwa/wagonjwa wapone.

Mwenye karama za lugha ni ivyo hivyo ni lazima aombe ili anene kwa lugha, matendo ya miujiza ni ivyo hivyo ni lazima maombi yahusike ili miujiza itendeke.

Nabii Eliya hakushusha moto kutoka mbinguni kwa uweza wa MUNGU bila kuhusisha maombi, aliomba kwanza ndipo muujiza ukatendeka..na karama zote zinaendeshwa na maombi.

Sasa tunarudi kwenye swali, je kuna karama ya kuomba na maombezi?.

Jibu ni La! Hakuna hiyo karama, kwasababu agizo haliwezi kuwa karama..

Lakini sasa kama ni hivyo inakuwaje wapo watu wenye uwezo wa kuomba kwa kina na masafa marefu kuliko wengine?.

Kuna sababu kuu mbili (02) za hali hiyo ya baadhi ya watu kuwa na uwezo mkubwa zaidi ya wengine, na sababu ya pili ina uzito zaidi kwa mujibu wa swali Letu.

    1. MAZOEZI YA UTAUWA.

Najua unajiuliza mazoezi ya Utauwa ni kitu gani?…tusome maandiko yafuatayo kisha tufafanue.

1 Timotheo 4:7 “Bali hadithi za kizee, zisizokuwa za dini, uzikatae; NAWE UJIZOEZE KUPATA UTAUWA.

8 Kwa maana kujizoeza kupata nguvu za mwili kwafaa kidogo, lakini utauwa hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye”

Kiswahili kingine cha mazoezi ya utauwa ni “mazoezi ya uungu”.. yaani mtu anakuwa na mazoezi ya kutosha ya maagizo ya MUNGU kama maombi, mifungo, na uinjilisti…kiasi kwamba anakuwa ni mtu anayejizoeza kuhubiri mara kwa mara, au kuomba mara kwa mara jambo linalofanya uwezo wake wa kuomba, kuhubiri au kufunga kuongezeka kila iitwapo leo.

Sasa kundi hili linalojizoeza utauwa huwezi kushindana nalo wewe unayejizoeza kulala kutwa kuchwa au kula mara tatu kwa siku.

Wewe utasali dakika mbili na kulala mwenzio atasali masaa 5 bila kuchoka, wewe utabaki kusema fulani ana karama ya kuomba kumbe ni uvivu wako tu uliovikwa na ibilisi.

Hiyo ni sababu ya kwanza…

   2. KARAMA YA MASAIDIANO.

Hii ndio karama inayochanganywa na wengi..

1 Wakorintho 12:28 “Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha”.

Katika karama hii ya masaidiano ndio hapa kuna watu wanakuwa na mzigo wa kuomba kwaajili ya wengine kwa muda mrefu kwasababu ndani yao kuna msukumo wa kusaidia.

Ile roho ya kutamani kusaidia inamfanya mtu aidha atoe vitu vyake au muda wake katika maombi na kuomba mpaka ule mzigo utakapoisha ndani.

Kwahiyo kwa hitimisho hamna karama ya maombi kwenye Biblia, bali ya masaidiano ambayo inahusisha maombi au kitu kingine chochote cha kumsaidia mtu mwenye uhitaji.

Je wewe ni mwombaji?. Kama sio. fahamu shetani kafaulu pakubwa sana kukupata, kuelewa faida za maombi kwa undani wasiliana nasi kupitia namba zifuatazo, tutakupa masomo husika bure.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

BWANA, UNATUACHAJE?

Kuna  kauli ambayo tunayo sana kwenye vinywa vyetu…Hususani pale boss au kiongozi wetu anapomalizana nasi katika mpango fulani na kutuaga..tunasema “bwana unaniachaje”?

Maana yake, baada ya kukaa chini yake muda mrefu, au kumtumikia, kuna namna anapaswa akuandalie mazingira ya kukufanya uendeleze lile jambo lake, au lako mwenyewe.. ndio hapo utaona wanawaachia watumwa wao aidha viinua mgongo, mitaji, au fedha za matumizi. 

Hili linaonekana ni jambo zuri kufanywa na bwana au kiongozi yeyote mwenye busara. 

Lakini kwa Yesu mambo yalikuwa tofauti, kwenye kauli yake ya mwisho alipokuwa anapaa.. Mitume hawakuachwa na lolote, na zaidi wanaambiwa wakashuhudie habari zake kutoka pale Yerusalemu walipo, waende uyahudi, Samaria na mpaka mwisho wa nchi.

Ukitafakari kwa ukaribu jambo hilo linahitaji rasilimali nyingi za kifedha, kiuchumi n.k. lakini hawakuachiwa hata senti kumi.

Ukiwa na mawazo kuwa kiongozi wako wa kiroho akuandalie rasilimali za kujikimu kimaisha, ndio ukamtumikie Bwana vizuri, ndugu utavunjika moyo..kwasababu yeye mwenyewe alipoitwa hakuandaliwa rasilimali, Na hilo halikuanzia kwake, lilianzia kwa mitume, hadi kwa wote waliofuata baadaye yao. Tena ungekuwepo nyakati za mitume ungevunjika moyo mara kumi zaidi.

Kumbuka Yesu anaonekana kama  “Bwana mgumu” kwa baadhi ya watumwa. Usipokuwa makini unaweza kumwona pia hivyo.

Kivipi?

Mkumbuke yule aliyepewa talanta moja aliona ameachwa bila màandalizi mazuri kimtaji…akabakia tu kulalamika na kusema huyu Bwana wangu ni mgumu sana.… hii talanta moja aliyoniachia  nitafanyia nini, Hata chakula cha siku moja tu hainitoshi, Bado anataka nimletee vingi, anataka kuvuna asipopanda… Ninakwenda kumwekea pesa yake. Nikafanye mambo yangu akirudi nimpe sitaki lawama.

Hakujua uamuzi huo ni kosa kubwa..

Luka 19:20-26

[20]Akaja mwingine akasema, Bwana, hili ndilo fungu lako, ambalo nililiweka akiba katika leso. 

[21]Kwa maana nilikuogopa kwa kuwa u mtu mgumu; waondoa usichoweka, wavuna usichopanda. 

[22]Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, niondoaye nisichoweka, na kuvuna nisichopanda; 

[23]basi, mbona hukuiweka fedha yangu kwa watoao riba, ili nijapo niipate pamoja na faida yake? 

[24]Akawaambia waliosimama karibu, Mnyang’anyeni hilo fungu, mkampe yule mwenye mafungu kumi. 

[25]Wakamwambia, Bwana, anayo mafungu kumi. 

[26]Nawaambia, Kila aliye na kitu atapewa, bali yule asiye na kitu atanyang’anywa hata alicho nacho. 

Ukiona unasubiri ufanyiwe na Yesu kwanza kitu fulani ndipo uwe na hamasa ya kuifanya kazi. 

Kuwa makini. ROHO MTAKATIFU TAYARI YUPO NDANI YAKO UMESHAPEWA. Hakuna kingine zaidi ya hiko.  Simama kwenye huduma yako, Timiza utume wako.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

FUNDISHO, NI KUSEMA NENO USILOLIJUA

Ubora wa Kuhubiri au kufundisha haupimwi kwa elimu kubwa ya biblia, au mifano mizuri, au utashi fulani wa kupangilia maneno. Hapana, bali ni uwezo wa kupenya katika mioyo ya watu.

Haimaanishi kuwa na elimu ya biblia haichangii ubora wa fundisho au hubiri..inachangia sana lakini hiyo ni kama gamba la juu sana..ambalo linaweza lisitoe pia matokeo yoyote.

Pale fundisho linapoweza kuingia ndani ya moyo wa mtu, kupambanua, kuchoma, kulainisha, kupindua-pindua, kukarabati, kuponya hadi kumfanya mtu kuwa na mwitikio wa dhahiri wa nje. Hilo ndio linaitwa fundisho au hubiri kibiblia.

Sasa tendo hilo mpaka kufikiwa, si jambo rahisi hata kidogo, hakuna utashi wa kibinadamu unaweza kufanya hivyo.

Kwasababu hakuna anayejua ndani ya mtu mwingine kuna nini?

Lakini lililo gumu zaidi ni kuwa hata yeye mwenyewe hajijui vema, kama anahitaji matengenezo katika eneo fulani la moyo wake. Anaweza akawa ana hofu akadhani huwenda chanzo cha hofu hiyo ni ule ugonjwa uliomshika, kumbe chanzo ni kingine kabisa.

Kwasababu mwanadamu mwenyewe moyo wake ni fumbo kubwa.

Yeremia 17:9

[9]Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?

Umeona jinsi ilivyo ngumu sana. Ikiwa yeye mwenyewe hajijui, wewe mtu wa tatu utayajulia wapi yaliyomo moyoni mwake? Lakini Mungu anataka uyahubiri yahusuyo moyo wake.

Usifikiri unapomwona mtu, labda ana huzuni, au furaha au ana tabia za ulevi, wizi, , ukadhani anahitaji fundisho linaloendana na hiyo tabia unayoiona kwa nje.

Unaweza ukakosa shabaha kwa maili nyingi sana, ukifikiri tu hivyo.

Utamwona analia, pengine ni mgonjwa, amefiwa, amepoteza kila kitu kama ilivyokuwa kwa Ayubu na wewe unamfuata na fundisho la faraja, ukadhani kuwa ndio uponyaji wake utakapotokea.

Kumbe Mungu anajua anataka makemeo, na makaripio ili aponywe.

Wakati mwingine utasimama kwenye mkusanyiko wa watu wengi labda mia. Huko huko wapo wanaohitaji faraja, wanaohitaji unabii, wanaohitaji maonyo, wanaohitaji maarifa, wanaohitaji kufunguliwa. Sasa wewe unasimama na fundisho lako lenye mlengo mmoja wa makemeo, unadhani wote watahudumiwa na hilo. Kama ukikosa namna ya ki-ungu, unaweza ukawa unazungumza maneno yako.

Na lengo la Mungu ni watu wote wahudumiwe na Neno.

Hapo ndio linakuja suala la hakuna mbobezi wa fundisho au hubiri. Inahitaji hekima nyingine itokayo juu, ya kuhubiri usichokuwa na ufahamu nacho, au ujuzi nacho.

Siku ile ya Pentekoste, kilichotendeka mpaka ikapelekea watu wale kuchomwa mioyo, na hatimaye kuamini kwa idadi ile kubwa ya watu.

Haikuwa kwasababu walipaza sauti sana, au walihubiri kwa ujasiri sana, au maneno yao yalikuwa na elimu kubwa ya theolojia..

Hapana angalia utaona yalikuwa ni maneno ya kawaida kabisa… lakini yaliyoundwa na Roho Mtakatifu kwa namna ambayo yalipenya katika moyo wa kila mmoja.

Utaona, hatua ya kwanza walinena kwa lugha ambazo hata wao wenyewe hawakuzijua, lugha hizo zilikuwa zinawahubiria wengine.. zinanena mambo yao ya sirini, zinawakemea, zinawafariji, zinawaponya, zinawashuhudia Kristo.

Mpaka baadaye wanamaliza kunena tayari injili imeshahubiriwa wasijue ni kitu gani kimehubiriwa.

Petro aliposimama kumalizia maneno yake, wote wamenywea wanasubiri tu kupewa maelekezo ni nini cha kufanya baada ya pale..

Matendo ya Mitume 2:37

[37]Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

Hao ni watu wasio na elimu yoyote, walikuwapo waandishi, na mafarisayo wenye elimu lakini hakuna matokeo yoyote ya mafundisho yao.

Hata leo hii mimi na wewe.. Tujue kuwa kuhubiri na kufundisha hakutegemei sana ujuzi, au utashi, bali kunategemea zaidi Roho Mtakatifu.

Kwanini Roho Mtakatifu?

Kwasababu yeye ndiye anayeweza kuzama ndani ya mioyo ya watu na kujua shida zao, na kuwaponya.

Ni nini tunapaswa kufanya, ili fundisho likazame moyoni, lisitoke kwa makisio yetu?

Jambo kuu ni Kuwa na maandalizi ya kutosha.

Maandalizi hayo yapo kwa namna mbili.

1) Kumwandalia Roho Mtakatifu njia ya kuanzia..Ndio hapo unahitaji kwanza kusoma na kuandaa somo / fundisho. Kumbuka Ni lazama utenge muda kuandaa fundisho ambalo utalihubiri. Andika, na ujue pa kuanzia, bila kuwa na maandalizi hayo, unasema nitaenda tu kuzungumza. Ujue tayari umeizuia njia ya Roho Mtakatifu kufundisha.

2) Lakini hilo peke yake halitoshi, hatua nyingine ni kuomba maingilio ya Roho Mtakatifu yawe makubwa. Hapo ndipo unatenga muda mrefu wa kuomba, ili Roho Mtakatifu akatembee kwenye vyumba vya ndani kabisa ambavyo wewe hujui, wakati utakaposimama na kufundisha, kushuhudia.

Sasa ukimaliza hapo. Jiandae kwenda kusema ulichokusudia.. kumbuka mhubiri anayetumia dakika kumi kufundisha lakini amekuwa na maandalizi ya masaa matano kwenye kusoma na maombi. Ana nguvu zaidi ya yule atakayefundisha masaa matano, halafu alijiandaa kwa dakika tano.

Mwisho Ukienda kufundisha na kuona mazungumzo yako yanasogea nje ya mada, au taarifa nyingine zinakuja kichwani mwako tofauti na zile ulizoziandika kwenye daftari ujue ni kazi za Roho Mtakatifu usizizuie.

Baadaye utakuja kusikia tu shuhuda, na hata kama hazitasemwa, ujue Neno lako halijakwenda bure.

Tukiwa wahubiri na waalimu wa namna hii. Roho nyingi za watu zitaokolewa.

Kuhubiri ni kusema tusichokijua, cha wengine.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NENO NA MAOMBI~ Sehemu ya 2 (AMRI YA UPENDO)

Jina la Bwana YESU libarikiwe, karibu katika kujifunza Neno na Maombi. Kusoma Neno bila Maombi, au kuomba bila Neno ni sawa na kitamba cha bendera kisicho na mlingoti, kupitia mfululizo huu wa tafakari hizi tutapata mwongozo sahihi wa kuomba kupitia maandiko ya kwenye Biblia.

PENDO LA MUNGU.

Bwana YESU alitufundisha kuwa Amri ya kwanza ni “Kumpenda Bwana na ya pili ni kuwapenda majirani kama nafsi zetu”.

Mathayo 22:36 “Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu?

37 Akamwambia, MPENDE BWANA MUNGU WAKO KWA MOYO WAKO WOTE, NA KWA ROHO YAKO YOTE, NA KWA AKILI ZAKO ZOTE.

38 Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.

39 Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, MPENDE JIRANI YAKO KAMA NAFSI YAKO.

40 Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii”.

Na tena alisema…

Yohana 14:21 Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye; naye anipendaye atapendwa na Baba yangu; nami nitampenda na kujidhihirisha kwake.

 

   1. OMBA ONGEZEKO LA UPENDO WA MUNGU NDANI YAKO (Tumia dakika 30)

i. Kwa moyo wako wote.

  • Hapa utaomba Bwana akujalie kumtafuta kwa hiari bila shuruti, kwasababu hiyo ndio maana ya kumpenda kwa moyo wako wote.

     ii. Kwa roho yako yote

– Hapa utamwomba Bwana kuwa upendo wako ukatoke rohoni, katika kumtafuta kwasababu Neno linasema waabudua watamwabudu baba katika roho na kweli.

               iii.    Kwa akili zako zote.

                           – Hapa utaomba Bwana akuwezeshe kumtumikia yeye kwa ujuzi aliokupa, (ule wa asili na ule wa kujifunza) kama ni msomi basi kupitia elimu yako hiyo umtumikie MUNGU, na kuyafanya mapenzi yake.

          iv. Kwa Nguvu zako zote.

      – Nguvu zinaweza kuwa za mwili kama wewe ni kijana, lakini pia zinaweza kuwa za kifedha, katika maeneo hayo yote mwombe BWANA akusaidie uweze kumpenda MUNGU na kufanya mapenzi yake, Utoe muda wako au mali zako katika kumtumikia MUNGU.

            2. OMBA UPENDO KWA JIRANI. (Tumia dakika 30)

Neno la MUNGU linatufundisha kuwa “Tujaponena kwa lugha zote na kufanya ishara zote kama hatuna Upendo sisi sio kitu”

      1Wakorintho 13:1 “Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao”.

Na tena inasema…

Waebrania 13:1 “Upendano wa ndugu na udumu”.

    i. Omba Upendo kwa ndugu wa kiroho (Wachungaji na washirika wenzako)

  • Hapa utaomba Bwana akakukumbushe mema waliyokutendea.
  • Utaomba Bwana akuondolee chuki na kutokusamehe.
  • Utaomba Bwana akuoneshe kasoro zako ili pendo kati yako na wapendwa wenzako lidumu.
  • UOmbea kanisa na wakristo wenzako wakajawe na Upendo wa kiMungu.
  • Omba Bwana akaachie roho ya kusameheana.

     ii.   Omba Upendo kwa ndugu wa kimwili (Wana familia)

  • Hapa mwombe Bwana akuongezee upendo kwa wazazi, na ndugu wengine wadogo kwa wakubwa.
  • Waombee wana familia yako wajawe na upendo kama wewe unavyojiombea..

        3. KEMEA KILA ROHO INAYOJIINUA KUPOOZA UPENDO WA MUNGU, NA WA KINDUGU

Kemea kwa jina la YESU KRISTO kila pando la chuki kanisani kwako, katikati yako na wakristo wenzako, katikati yenu kama familia.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NENO NA MAOMBI~ Sehemu ya 1 (MAPENZI YA  MUNGU)

Jina la Bwana YESU libarikiwe, karibu katika kujifunza Neno na Maombi. Kusoma Neno bila Maombi, au kuomba bila Neno ni sawa na kitamba cha bendera kisicho na mlingoti, kupitia mfululizo huu wa tafakari tutapata mwongozo sahihi wa kuomba kupitia maandiko ya kwenye Biblia.

MAPENZI YA MUNGU.

Bwana YESU alisema si kila aniambiaye Bwana Bwana atakayeingia katika ufalme, bali yule afanyaye mapenzi ya Baba wa mbinguni.

Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Sasa basi kama kigezo cha kuingia mbinguni ni “KUFANYA MAPENZI YA MUNGU”, hivyo tukimwomba MUNGU atusaidie kuyajua na kuyafanya mapenzi yake tutakuwa tunaomba jambo sahihi kabisa.

      1. OMBA KUYAJUA MAPENZI YA MUNGU KWAKO (Tumia dakika 30)

Katika Eneo la kiroho.

  • Hapa utaomba Bwana akufunulie uyajue mapenzi yake katika kazi yake ya huduma, na wapi unapaswa utumike na utumikeje, pia kama bado haujaifahamu karama yako, mwombe Bwana akufunulie.

Katika Eneo la kimaisha.

  • Hapa utamwomba Bwana akufunulie kuyajua mapenzi yake katika kazi unazozifanya au elimu, ni kipi sahihi unapaswa ukifanye ukiwa hapo kazini, ni watu gani sahihi unapaswa ushirikiane nao ili usifanye kinyume jambo nje na mapenzi ya MUNGU pia kama unatafuta kazi, basi omba MUNGU akakufunulie kazi sahihi na kukuongoza hapo.

Katika Eneo la kifamilia.

  • Hapa omba Bwana akakuoneshe mapenzi yake kuishi na mke, mume, na watoto, au wazazi pia ombea wanafamilia yako wote wakayajue mapenzi ya MUNGU na kuyafanya.

 

  2. OMBA KUYATENDA MAPENZI YA MUNGU. (Tumia dakika 30)

Utauliza katika kuyatenda mapenzi ya MUNGU kuna haja ya kuomba?. Jibu ni Ndio! Kwasababu pasipo yeye kutusaidia sisi hatuwezi kufanya lolote. (Soma Yohana 15:5).

Katika Eneo la kifikra

  • Hapa utaomba Bwana akakusaidie fikra zako, Bwana akakupe uwezo wa kufikiri yanayompendeza yeye kila wakati akilini mwako (Waefeso 5:10).

Katika eneo la Viungo

  • Hapa mwombe Bwana akusaidie viungo vyako kama mikono, miguu, macho, masikio viwe vyepesi katika kufanya mapenzi ya MUNGU, baada ya kuyajua mapenzi ya MUNGU, ikiwa na maana kwamba miguu yako iwe tayari kukimbilia kuyafanya mapenzi ya MUNGU, mikono yako iwe tayari na mwepesi kufanya mapenzi ya MUNGU, macho yako yawe tayari kufanya mapenzi ya MUNGU.

 

     3. KEMEA KILA ROHO INAYOKUZUIA WEWE KUYAFANYA MAPENZI YA MUNGU.

Zipo roho za adui zinazozua kuyafanya mapenzi ya MUNGU, roho hizi zinazuia fikra zako za ndani zisifikiri, wala kupenda kuyafanya mapenzi ya MUNGU, ndio hapo utatamani kwenda kushuhudia habari za wokovu, ndani ya fikra zako woga unaingia au aibu au kukosa ujasiri, tumia muda kuzikemea.

Pia zinazuia viungo vyako visiwe tayari kufanya mapenzi ya MUNGU, ndio hapo utatamani kwenda kuhubiri au kwenda kufanya kazi yoyote iliyo halali na ghafla udhaifu wa mwili utaingia kama uchovu, uvivu, au ugonjwa. Hivyo chukua muda kukemea roho hizo na Bwana atakufungua.

1Petro 4:2 “Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.

3 Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;

4 mambo ambayo wao huona kuwa ni ajabu ya ninyi kutokwenda mbio pamoja nao katika ufisadi ule ule usio na kiasi, wakiwatukana”.

Bwana akubariki usikose sehemu ya Pili ya Mwongozo huu wa Neno na Maombi, kwa msaada zaidi wasiliana nasi kwa namba tajwa hapa chini.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NENO NA MAOMBI~ Sehemu ya 1 (MAPENZI YA  MUNGU)

 

Jina la Bwana YESU libarikiwe, karibu katika kujifunza Neno na Maombi. Kusoma Neno bila Maombi, au kuomba bila Neno ni sawa na kitamba cha bendera kisicho na mlingoti, kupitia mfululizo huu wa tafakari tutapata mwongozo sahihi wa kuomba kupitia maandiko ya kwenye Biblia.

MAPENZI YA MUNGU.

Bwana YESU alisema si kila aniambiaye Bwana Bwana atakayeingia katika ufalme, bali yule afanyaye mapenzi ya Baba wa mbinguni.

Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Sasa basi kama kigezo cha kuingia mbinguni ni “KUFANYA MAPENZI YA MUNGU”, hivyo tukimwomba MUNGU atusaidie kuyajua na kuyafanya mapenzi yake tutakuwa tunaomba jambo sahihi kabisa.

  1. OMBA KUYAJUA MAPENZI YA MUNGU KWAKO (Tumia dakika 30)

 

  1. Katika Eneo la kiroho.
  • Hapa utaomba Bwana akufunulie uyajue mapenzi yake katika kazi yake ya huduma, na wapi unapaswa utumike na utumikeje, pia kama bado haujaifahamu karama yako, mwombe Bwana akufunulie.
  1. Katika Eneo la kimaisha.

– Hapa utamwomba Bwana akufunulie kuyajua mapenzi yake katika kazi unazozifanya au elimu, ni kipi sahihi unapaswa ukifanye ukiwa hapo kazini, ni watu gani sahihi unapaswa ushirikiane nao ili usifanye kinyume jambo nje na mapenzi ya MUNGU pia kama unatafuta kazi, basi omba MUNGU akakufunulie kazi sahihi na kukuongoza hapo.

               iii.        Katika eneo la kifamilia.

                           – Hapa omba Bwana akakuoneshe mapenzi yake kuishi na mke, mume, na watoto, au wazazi pia ombea wanafamilia yako wote wakayajue mapenzi ya MUNGU na kuyafanya.

 

  1. OMBA KUYATENDA MAPENZI YA MUNGU. (Tumia dakika 30)

Utauliza katika kuyatenda mapenzi ya MUNGU kuna haja ya kuomba?. Jibu ni Ndio! Kwasababu pasipo yeye kutusaidia sisi hatuwezi kufanya lolote. (Soma Yohana 15:5).

  1. Katika Eneo la kifikra
  • Hapa utaomba Bwana akakusaidie fikra zako, Bwana akakupe uwezo wa kufikiri yanayompendeza yeye kila wakati akilini mwako (Waefeso 5:10).

 

  1. Katika eneo la Viungo
  • Hapa mwombe Bwana akusaidie viungo vyako kama mikono, miguu, macho, masikio viwe vyepesi katika kufanya mapenzi ya MUNGU, baada ya kuyajua mapenzi ya MUNGU, ikiwa na maana kwamba miguu yako iwe tayari kukimbilia kuyafanya mapenzi ya MUNGU, mikono yako iwe tayari na mwepesi kufanya mapenzi ya MUNGU, macho yako yawe tayari kufanya mapenzi ya MUNGU.

 

  1. KEMEA KILA ROHO INAYOKUZUIA WEWE KUYAFANYA MAPENZI YA MUNGU.

Zipo roho za adui zinazozua kuyafanya mapenzi ya MUNGU, roho hizi zinazuia fikra zako za ndani zisifikiri, wala kupenda kuyafanya mapenzi ya MUNGU, ndio hapo utatamani kwenda kushuhudia habari za wokovu, ndani ya fikra zako woga unaingia au aibu au kukosa ujasiri, tumia muda kuzikemea.

 

Pia zinazuia viungo vyako visiwe tayari kufanya mapenzi ya MUNGU, ndio hapo utatamani kwenda kuhubiri au kwenda kufanya kazi yoyote iliyo halali na ghafla udhaifu wa mwili utaingia kama uchovu, uvivu, au ugonjwa. Hivyo chukua muda kukemea roho hizo na Bwana atakufungua.

 

1Petro 4:2 “Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.

3 Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;

4 mambo ambayo wao huona kuwa ni ajabu ya ninyi kutokwenda mbio pamoja nao katika ufisadi ule ule usio na kiasi, wakiwatukana”.

 

Bwana akubariki usikose sehemu ya Pili ya Mwongozo huu wa Neno na Maombi, kwa msaada zaidi wasiliana nasi kwa namba tajwa hapa chini.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine: