Swali: Biblia inasema “Tukiongozwa na Roho hatupo chini ya sheria”(Wagalatia 5:18) maana yake nini andiko hili?
Jibu: Tuanzie ule mstari wa 16 ili tuelewe vizuri..
Wagalatia 5:16 “Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili. 17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka. 18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria”.
Wagalatia 5:16 “Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.
18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria”.
Awali ya yote ni vizuri kujua roho inayozungumziwa hapo ni roho gani?.. si roho ya mtu, bali roho ya MUNGU (Yaani Roho mtakatifu) ndio maana imeanza kwa herufu kubwa… maana yake “Tukiongozwa na Roho Mtakatifu hatupo chini ya sheria”
Sasa anaposema “tukiongozwa na Roho hatupo chini ya sheria” haimaanishi kuwa tunapookoka basi tuna ruhusa ya kufanya kila kitu, au kutenda jambo lolote, au kuvaa vyovyote au kuishi vyovyote, na kwamba tupo juu ya sheria.
La! Hiyo sio tafsiri yake.. ili tuelewe vizuri maana au tafsiri halisi ya andiko hilo, hebu takafakari mfano huu.
Mwalimu wa Hisabati anawaambia wanafunzi wake kuwa “Mkitumia kikokoteo (yaani calculator) hamtateseka na kanuni/sheria za mahesabu”.. maana yake ni kwamba mtafanya mahesabu yale yale lakini katika urahisi, lakini si kukwepa mahesabu… ikiwa na maana kuwa ile calculator inarahisisha kufanya mahesabu bila mwanafunzi kutumia kanuni.
Ni ivyo hivyo katika hilo andiko anaposema “Mkiongozwa na Roho hampo chini ya sheria”… maana yake sheria za kumcha MUNGU ambazo kwa udhaifu wa mwili ni ngumu, kama vile zile sheria za hisabati, kwa kupitia Roho Mtakatifu zinakuwa nyepesi.
Maana yake kama Biblia imesema “Usizini” au “Usiseme uongo”… kutimiza sheria hiyo ya kukaa bila kudanganya au bila kufanya zinaa ya nje au moyoni ni ngumu.. lakini kwa msaada wa Roho Mtakatifu inawezekana kutimiza sheria hiyo kirahisi,
Ndio maana hapo kwenye mstari wa 16 anasema “Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili”.
Na hapa ndipo tunapoona umuhimu mkubwa wa kujazwa Roho Mtakatifu kama Biblia inavyotufundisha..
Waefeso 5:18 “Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho”.
Watu waliojaa Roho Mtakatifu kweli kweli hawaoni shida kuishi maisha matakatifu yasiyo na dhambi, wengine wote wanaweza kuwashangaa wanawezaje kuishi bila wizi, matusi, rushwa, zinaa, ulevi na bado wanayafurahia hayo maisha, pasipo kujua siri kuwa ni Roho Mtakatifu aliye ndani yao, anawasaidia udhaifu wao.
Na ili tujae Roho Mtakatifu ni lazima tufahamu kanuni ya kumpata Roho Mtakatifu, kama tu ili tupate kikokoteo wepesi (calculator) itakachotusaidia kutatua mahesabu magumu kwa haraka na wepesi ni lazima tujue jinsi ya kuipata au mahali pa kuipata na gharama zake.
Sasa tunampataje Roho Mtakatifu ili tuwezi kuishi pasipo sheria??
Tunampata kwa kanuni ifuatayo..
Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? 38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.
Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.
Kwa njia ya kutubu dhambi kwa kumaanisha kuiacha!, na kubatizwa kwa Maji mengi kwa jina la Bwana YESU, yule Roho ataingia ndani ya kuwezesha uwezo huo mkubwa wa kuishi kwa utakatifu bila mapambano makubwa moyoni.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Mafundisho Mengine
ZIDI KUTAFUTA UJAZO WA ROHO MTAKATIFU.
Ahadi Ya Roho Mtakatifu.
KUWA NA MAFUTA YOTE YA ROHO MTAKATIFU NDANI YAKO.
ZIFAHAMU KARAMA 9 ZA ROHO MTAKATIFU NA UTENDAJI KAZI WAKE.
KAZI ZA ROHO MTAKATIFU
Shalom, jina la Mwokozi YESU libarikiwe, karibu tujifunze pamoja Biblia, Neno la Mungu wetu.
Maandiko yanatabiri kuwa siku za mwisho kutatokea aina ya watu wasiotaka “suluhu” katika nyanja mbalimbali za kifamilia hata kikanisa.
2 Timotheo 3:1 “Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. 2 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, 3 wasiowapenda wa kwao, WASIOTAKA KUFANYA SULUHU, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema”.
2 Timotheo 3:1 “Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.
2 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi,
3 wasiowapenda wa kwao, WASIOTAKA KUFANYA SULUHU, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema”.
Tabia ya kutotaka kufanya Suluhu imwsababisha ndoa nyingi kuvunjika, familia nyingi kutengana, makanisa kuanguka , undugu kuisha, na hata urafiki mwema kuisha..
Jambo ambalo si jema machoni pa MUNGU wetu.
Lakini pamoja na hayo yote, yawezekana zimetumika njia nyingi kuleta suluhu na mapatano imeshindikana..
Yawezekana mazungumzo na vikao vimefanyika vya kutosha lakini hakuna suluhu, yawezekana umejaribu au mmejaribu kuweka mambo sawa kwa kila njia lakini bado hakuna mapatano wala makubaliano.
Kama njia zote hizo hazijaleta matokeo basi ipo kanuni moja ya kibiblia nzuri sana ambayo mtu akisimama na hiyo vizuri basi hata wale maadui zake atapatana nao.
Na njia hiyo si nyingine zaidi ya ile tunayoisoma katika Mithali 16:7.
Mithali 16:7 “Njia za mtu zikimpendeza BWANA, Hata adui zake huwapatanisha naye”.
Ikiwa na maana kwamba Mtu akizitengeneza njia zake zikawa thabiti kwa MUNGU, na hata MUNGU akapendezwa naye, basi hatawale waliokuwa wanampiga vita, Mungu ataweka amani, hata wale waliokuwa wanamchukia Mungu ataweka upendo.
Lakini ni lazima njia za Mtu kwanza zimpendeze MUNGU,
Labda tujifunze mfano mmoja wa kwenye Biblia tuweze kuelewa zaidi, tumrejee Yakobo ndugu yake Esau,
Tunaona baada ya Yakobo kuchukua mbaraka wa ndugu yake, mara moja Esau aliapa kumuua, jambo lililomfanya Yakobo akimbie.
Lakini pamoja na kukimbia kwake Yakobo alijua fika kuwa hataweza kumkimbia ndugu yake milele, na hivyo alitamani mapatano naye.
Sasa Yakobk alichokifanya sio kuandika barua nyingi za kuomba msamaha kwa Esau, bali katika mazingira ya kujitenga alitengeneza njia zake kwa MUNGU, katika ukamilifu na usafi, na wala hakuketi kumsema kaka yake, na MUNGU akapendezwa naye na kumpatanisba na ndugu yake Esau ambaye aliapa kumuua hapo kwanza.
Mwanzo 33:1 “Yakobo akainua macho yake, akaona, na tazama, Esau anakuja na watu mia nne pamoja naye. Akawagawanyia Lea, na Raheli, na wale vijakazi wawili, wana wao…… 3 Akapita mwenyewe mbele yao, akainama mpaka nchi mara saba, hata alipomkaribia ndugu yake. 4 Esau akaja mbio kumlaki, akamkumbatia, na kumwangukia shingoni, akambusu; nao wakalia. 5 Akainua macho yake, akawaona wale wanawake na watoto, akauliza, Ni nani hawa walio pamoja nawe? Akasema, Ni watoto Mungu aliompa mtumwa wako kwa neema yake. 6 Ndipo wale vijakazi, na wana wao, wakakaribia wakainama. 7Lea naye, na wanawe, wakakaribia wakainama. Baadaye Yusufu na Raheli wakakaribia, wakainama. 8 Akasema, Kundi hili lote nililolikuta, maana yake ni nini? Akasema, Kunipatia kibali machoni pa bwana wangu. 9 Esau akasema, Ninayo tele, ndugu yangu, uliyo nayo na yawe yako. 10 Yakobo akasema, Sivyo; kama nimekubalika machoni pako tafadhali upokee zawadi yangu mkononi mwangu, iwapo nimeona uso wako kama kuona uso wa Mungu, ukapendezwa nami. 11 Pokea, tafadhali, mbaraka wangu, ulioletewa, kwa sababu Mungu amenineemesha, na kwa sababu ninavyo hivi vyote Akamshurutisha, naye akapokea. 12 Kisha Esau akamwambia, Twende zetu, tusafiri, nami nitakutangulia”.
Mwanzo 33:1 “Yakobo akainua macho yake, akaona, na tazama, Esau anakuja na watu mia nne pamoja naye. Akawagawanyia Lea, na Raheli, na wale vijakazi wawili, wana wao……
3 Akapita mwenyewe mbele yao, akainama mpaka nchi mara saba, hata alipomkaribia ndugu yake.
4 Esau akaja mbio kumlaki, akamkumbatia, na kumwangukia shingoni, akambusu; nao wakalia.
5 Akainua macho yake, akawaona wale wanawake na watoto, akauliza, Ni nani hawa walio pamoja nawe? Akasema, Ni watoto Mungu aliompa mtumwa wako kwa neema yake.
6 Ndipo wale vijakazi, na wana wao, wakakaribia wakainama.
7Lea naye, na wanawe, wakakaribia wakainama. Baadaye Yusufu na Raheli wakakaribia, wakainama.
8 Akasema, Kundi hili lote nililolikuta, maana yake ni nini? Akasema, Kunipatia kibali machoni pa bwana wangu.
9 Esau akasema, Ninayo tele, ndugu yangu, uliyo nayo na yawe yako.
10 Yakobo akasema, Sivyo; kama nimekubalika machoni pako tafadhali upokee zawadi yangu mkononi mwangu, iwapo nimeona uso wako kama kuona uso wa Mungu, ukapendezwa nami.
11 Pokea, tafadhali, mbaraka wangu, ulioletewa, kwa sababu Mungu amenineemesha, na kwa sababu ninavyo hivi vyote Akamshurutisha, naye akapokea.
12 Kisha Esau akamwambia, Twende zetu, tusafiri, nami nitakutangulia”.
Unaona hiyo kanuni?.. Kama njia za Yakobo zingekuwa mbovu nyumbani kwa Labani, hakika wakati huu wa kukuata na Esau ageuawa.
Yawezekana nawe ndoa yako haijakaa sawa na mke wako au mume wako. Usikimbilie manung’uniko na malalamiko na kusema umbea huku na kule, wala usitafute kujitetea sa a au kujionesha kuwa wewe ni mwenye haki.
Unaweza kujitenga kwa muda (si vibaya kujitenga kwa amani).. lakini ukiwa katika kujitenga ombi lako kuu liwe ni Kupata suluhu jema na patano zuri, huku ukizitengeneza njia zako lwa MUNGU.
Nakuhakikishia kukingana na Biblia kama njia zako zitampendeza Bwana, basi tegemea matokeo ya ajabu katika eneo hilo la mapatano au suluhu, utaona yule mume ambaye alikuwa anakusumbua sasa anatulia, yule mke rafiki, yule ndugu anakupenda na kuifuata imani yako.
Sasa Swali unatengenezaje njia yako kwa Bwana?. Si kwa njia nyingine bali kutii Neno la MUNGU.
Zaburi 119:9 “Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako”
Neno la MUNGU kwanza linasema tutubu, na kuimini injili (Marko 1:15). Na pia kubatizwa kwa maji na kwa Roho mtakatifu (Marko 16:16), na kuishi maisha ya utakatifu baada ya hapo (Waebrania 12:14).
Kwa kulitii hilo Neno basi mlango wa mapatano kwatu umefunguka?.
Je umempa Bwana YESU maisha yako?
Kama bado unasubiri nini?. Tubu leo na kuiamini injili.
Mafundisho mengine:
Katika maandiko ukikutana na kisa kinaishia kwa kusema ‘hata leo’. Basi kuwa makini hapo kwasababu lipo la kukusaidia.
Kwamfano Ibrahimu alipopanda kule mlimani kumtolea Mungu sadaka kwa Isaka, Mungu alimpa kondoo badala yake, Kwa tukio hilo Ibrahimu akapaita mahali pale Yehova-yire. (Maana yake Mungu-mpaji). Hivyo jambo lile maandiko yanasema liliendelea kutamkwa na watu kwa wakati mwingine mwingi sana kama usemi uliohai ‘Yehova-yire’, Mungu atupaye.
Mwanzo 22:13-14
[13]Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama, kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe. [14]Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-yire, kama watu wasemavyo hata leo, Katika mlima wa BWANA itapatikana.
[13]Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama, kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.
[14]Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-yire,
kama watu wasemavyo hata leo, Katika mlima wa BWANA itapatikana.
Mfano mwingi ni wakati wa Yoshua alipoiangamiza nyumba ya Akani, msaliti, biblia inasema;
Yoshua 7:26
[26]Kisha wakakusanya juu yake chungu kubwa ya mawe hata leo; naye BWANA akauacha ukali wa hasira yake. Kwa sababu hiyo jina la mahali pale likaitwa, Bonde la Akori, hata hivi leo.
Ikiwa na maana bonde hilo liliendelea kuitwa vile vile hadi wakati wa mwandishi. ‘Ipo sababu’.
Mfano mwingine ni kipindi cha Yehu alipoyavunja mahekalu ya Baali..
2 Wafalme 10:27
[27]Wakaibomoa nguzo ya Baali, na kuiangusha nyumba ya Baali, wakaifanya choo hata leo.
Ikiwa na maana mpaka wakati mwandishi anaandika hicho kitabu eneo hilo lilikuwa ni choo.
Mahali pengine ni hapa..
Israeli kuwa hatarini kuvamiwa na wamoabu, wakamlilia Mungu, kisha kawaambia hawatapigana vita bali watakwenda kuokota nyara, kazi yao iwe ni kusifu na kuimba tu. Maadui zao wakauana wao kwa wao Na eneo lile wakaliita bonde la baraka hata leo.
2 Mambo ya Nyakati 20:25-26
[25]Nao Yehoshafati na watu wake walipokuja kuchukua nyara zao, wakaona kati yao wingi wa mali, na mavazi, na johari za thamani, walivyojivulia, zaidi kuliko wawezavyo kuchukua; wakawa siku tatu katika kuteka nyara, maana zilikuwa nyingi sana. [26]Hata siku ya nne wakakusanyika katika bonde la Baraka; maana ndipo walipombarikia BWANA; kwa hiyo jina lake mahali pale pakaitwa Bonde la Baraka hata leo.
[25]Nao Yehoshafati na watu wake walipokuja kuchukua nyara zao, wakaona kati yao wingi wa mali, na mavazi, na johari za thamani, walivyojivulia, zaidi kuliko wawezavyo kuchukua; wakawa siku tatu katika kuteka nyara, maana zilikuwa nyingi sana.
[26]Hata siku ya nne wakakusanyika katika bonde la Baraka; maana ndipo walipombarikia BWANA; kwa hiyo jina lake mahali pale pakaitwa Bonde la Baraka hata leo.
Mahali pengine ni wakati wa kifo cha Yuda, lile shamba lililonunuliwa liliitwa konde la damu mpaka nyakati za mwandishi..
Mathayo 27:8
[8]Kwa hiyo konde lile huitwa konde la damu hata leo.
Sasa biblia kusema ‘hata leo’ sio tu kutoa uthibitisho wa tukio kwamba kweli lilitokea ..lakini ni vema kujua tafsiri yake rohoni…kwamba kuna minyororo aidha ya baraka au laana inatembea mpaka leo.
Kwamfano watu waliposema Yehova-yire walijua Mungu ni mpaji wakati wote…hivyo wakamwona katika mazingira hayo..ndio maana wakasema ‘hata sasa’ si tu wakati wa Ibrahimu.
Neno hilo lipo hai hata leo rohoni. Ukiamini Mungu aliyomtendea Ibrahimu anakwenda kukutendea na wewe, utapokea…kwasababu lipo hivyo hata leo.
Anaposema mahali pale pakaitwa bonde la baraka hata leo. Ni kweli rohoni hata leo bonde hilo lipo.
Ukiamini kwamba katika kumwimbia Mungu unaingia katika bonde la baraka. Utapokea vingi kwa Mungu, sawasawa na walivyopokea Israeli kipindi cha Yehoshafati vitani.
Hivyo mambo mengi na matukio mengi yanaendelea kutembea katika roho hata sasa…Je! Macho yako yanaona?
Ukiwa mwovu kama Akani, kumbuka bonde la Akori lipo mpaka leo, ikiwa utakuwa msaliti kama Yuda konde la damu lipo hata leo utazikiwa huko.
Chagua mema, yaishi mema, upokee mema
Shalom.
Jina la YESU KRISTO lenye nguvu libarikiwe.
Neno la MUNGU linatufundisha kuwa sote tuliomwamini YESU, tumefanywa kuwa “Wahudumu wa Agano jipya”, maana yake tu watumishi na wahudumu wa Agano jipya, ambalo ni Agano la Roho na sio la mwilini.
Na siri kubwa ni kwamba utumishi huu tuliopewa, “Umejitosheleza” asilimia zote, hauna kasoro, ni wenye nguvu wa kubadilisha visivyobadilika, na ni wenye thawabu kubwa kuliko kazi zote.
2Wakorintho 3:6 “Naye ndiye aliyetutosheleza kuwa wahudumu wa agano jipya; si wa andiko, bali wa roho; kwa maana andiko huua, bali roho huhuisha”.
Sasa kufahamu kwa undani nini maana ya “Andiko huua bali roho huhuisha” fungua hapa>>> Nini maana ya “Andiko huua, bali Roho huhuisha (2Wakorintho 3:6)
Lakini ninachotaka tuone siku ya leo ni “Utoshelevu huu tuliopewa” kwamba tunapokuwa wahudumu wa Agano hili jipya tumepata bahati kubwa sana, kwasababu umejaa utoshelevu usio elezeka, na hiyo ndio maana wote wanaomtumikia MUNGU ijapokuwa watapitia dhiki, au mateso, au adha, lakini ndani yao wanajihisi washindi siku zote,
Ndani yao wanajivunia injili, ndani yao wanazo nguvu, hata kama utu wao wa nje unachakaa..
2Wakorintho 4:12 “Basi hapo mauti hufanya kazi ndani yetu, bali uzima ndani yenu. …..16 Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku”.
2Wakorintho 4:12 “Basi hapo mauti hufanya kazi ndani yetu, bali uzima ndani yenu.
…..16 Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku”.
Kwa ufupi wana heri kubwa wamtumikiao Bwana katika Agano hili jipya kwa mujibu wa Biblia, kwasababu ni wenye thamani na thawabu kubwa mbinguni.
Je wewe ni mhudumu wa Agano jipya?..Je unaitumia karama yako vizuri?.. au umeificha talanta yako ardhini, umepewa huduma ya uinjilisti je unaufanya kwa bidii?.. umepewa karama nyingine yoyote je unaitumia kwa uaminifu?..
Huenda hujui hicho ulichopewa kina uthamani kiasi gani, lakini nataka nikuambie kuwa huduma iliyowekwa ndani yako baada ya wewe kuokoka ni kubwa, na imejitosheleza, kinachotakiwa ni wewe kuanza kazi na sio kuendelea kungoja.
Amka leo kama umelala, anza kuhudumu madhabahuni kwa Bwana, Nenda shambani kwa Bwana kavune watu, thawabu yako itakuwa ni kubwa mbinguni kwani kilichowekwa ndani yako ni kikubwa wala usijidharau au mtu asikudharau, simama mtumikie aliyekuita, kwani muda haukungoji na bado ule mwisho umekaribia sana.
Bwana akubariki na kukuongezea Neema, ikiwa utataka msaada hatua za kuanza katika kumtumikia MUNGU, basi unaweza kuwasiliana nasi kwa namba hizi 0789001312.
JE UTAKATIFU NI MATENDO YA SHERIA?
UKIMBIE UHURU WA ULIMWENGU
UPENDO WA KRISTO WATUBIDISHA;
Uradhi wa Mapenzi yake ni nini? (Waefeso 1:5)
UFANYE BIDII KATIKA KUSOMA.
WhatsApp
Jina la Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe sana, karibu tujifunze biblia neno la MUNGU wetu (Zab 119:102).
Siku zote penda kuhakiki jambo kabla ya kuliamini, au kulipokea.. Taarifa yoyote inayokufikia, au unayoihisi kabla ya kufanya maamuzi ya kuamini au kutenda jambo, fanya uhakiki kwanza, Desturi ya kuhakiki jambo sio “kukosa imani” kama inavyoaminika na wengi bali ndio kipimo cha “ukomavu”.
Katika Biblia tunajifunza kwa MUNGU wetu kuwa naye pia ni Mungu wa kuhakiki mambo.. kwamfano zile taarifa za maovu ya watu wa Sodoma na Gomora zilishatangulia kumfikia, lakini kabla ya kufanya maamuzi ya kuiangamiza miji ile pamoja na watu wake, alishuka kwanza yeye mwenyewe kuhakiki kwa kile kilichotangulia kumfikia.
Tusome habari..
Mwanzo 18: 20 “Bwana akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana, 21 BASI, NITASHUKA SASA NIONE KAMA WANAYOTENDA NI KIASI CHA KILIO KILICHONIJIA; NA KAMA SIVYO, NITAJUA. 22 Basi wale watu wakatoka huko wakaelekea Sodoma; lakini Ibrahimu alikuwa akali akisimama mbele za Bwana”.
Mwanzo 18: 20 “Bwana akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana,
21 BASI, NITASHUKA SASA NIONE KAMA WANAYOTENDA NI KIASI CHA KILIO KILICHONIJIA; NA KAMA SIVYO, NITAJUA.
22 Basi wale watu wakatoka huko wakaelekea Sodoma; lakini Ibrahimu alikuwa akali akisimama mbele za Bwana”.
Kupitia habari hiyo sio kwamba Bwana MUNGU alikuwa hayaamini masikio yake, wala malaika wake wala mashitaka yoyote yaliyopandishwa mbele zake juu ya watu wa Sodoma na Gomora, alikuwa anawaamini sana, lakini ilibidi yeye mwenyewe akahakiki ukweli na uzito wa mambo, ili hukumu yake iwe ya haki na kweli.
Ni mara ngapi umesikia habari za mtu fulani kuwa yuko hivi au yuko vile, na kabla haujachukua maamuzi juu yake umelifuatilia kwa undani uhakika wa maneno hayo?.. utaona kuwa ni mara chache sana.. Wengi tunaziamini sana taarifa za kuambiwa au kusimuliwa na si zile tulizozithibitisha wenyewe.
Tunapenda kuthibitishiwa mambo na si kuyathibitisha wenyewe, ni mara ngapi umefuatilia ukweli wa mambo kuhusu Mke wako kwa yale unayoyasikia?, au ya mume wako, au ya watoto wako au wazazi wako?.
Tumewahi kukutana na visa vya watoto kuaminishwa kuwa wazazi wao ni wachawi kwa maneno tu!, au kwa ndoto tu, na mwisho kuishia kuwachukia na kuwatenga wazazi wao jambo linalofunga Baraka na neema kwa mtoto asilimia mia moja.
Jifunze kuhakiki mambo yote, hata yale ya kiMUNGU, si kila hubiri ni la kuliamini au kulipokea asilimia zote bila kulihakiki, Ondoa ile desturi ya kuamini kila kitu, ndio tunajiandaa kuamini lakini si kuruhusu kuamini kila kinachotujia.
Kuhakiki mambo si dhambi.. Na kipimio kizuri cha kuhakiki mambo ni NENO LA MUNGU, kama wale watu wa Beroya.
Matendo 17:10 “Mara hao ndugu wakawapeleka Paulo na Sila usiku hata Beroya. Nao walipofika huko wakaingia katika sinagogi la Wayahudi. 11 Watu hawa walikuwa waungwana kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo”.
Matendo 17:10 “Mara hao ndugu wakawapeleka Paulo na Sila usiku hata Beroya. Nao walipofika huko wakaingia katika sinagogi la Wayahudi.
11 Watu hawa walikuwa waungwana kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo”.
Ukiwa na uwezo mkubwa wa kulijua NENO la MUNGU, utakuwa na uwezo mkubwa pia wa kuhakiki mambo, kwani Neno la Mungu (Biblia) ni kitabu kulichojaa mafunzo ya kila aina ya maisha.
Ukitaka kuhakiki ndoto unazoziota kama ni halisi au batili, Biblia pekee ndio kipimio chako, ukitaka kuhakiki fundisho au hubiri unalolisikia kama ni halisi au gugu, ni Biblia tu, ukitaka kuhakiki njia yako ya kiroho, kibiashara, au kielimu kama ni sahihi, ni Biblia tu.
Ukitaka kuhakiki mke, au mume au mtoto kama yupo katika njia sahihi au sio sahihi ni Biblia, ukitaka kuhakiki taarifa unazozijua kama ni njema au za kupotosha ni Biblia tu.
Biblia ndio kitabu cha Maisha, imejaa hekima, maarifa, mwanga, mashauri, na maelekezo sahihi ya maisha, ikiwemo majibu ya maswali magumu, Biblia pekee ndio kitabu kinachoelezea mambo yajayo kwa usahihi kwa mtu mmoja mmoja, au kundi na hata Taifa na Dunia kwa ujumla.
Ndio kitabu pekee ambacho ukikisoma ni kama yupo mtu mwingine pembeni yako anakusemesha, tofauti na vitabu vingine vyote, ndio kitabu pekee chenye taarifa zisizofifia uhalisia kwa jinsi muda unavyozidi kwenda.
Anza uhakiki wa mambo leo kwa kusoma Biblia, sauti ya MUNGU iliyo wazi.
Ikiwa utahitaji kusaidiwa mwongozo wa usomaji wa Biblia, basi waweza wasiliana nasi kwa namba hizi 0789001312.
MAMBO MANNE(4) YAFANYAYO NENO LA MUNGU.
NENO LA MUNGU NI UFUNUO MKAMILIFU.
Ipi tofauti ya Juhudi na bidii kibiblia. (Warumi 12:11)
Tofauti kati ya maandiko na Neno ni ipi?
Mgawanyo wa Vitabu vya Biblia
Jina la Bwana na Mwokozi wetu YESU KRISTO, libarikiwe daima.
Ipo faida kubwa sana ya kumwangalia Bwana, na Bwana kukuangalia wewe.. Wengi tunapenda Bwana atuangalie ila sisi tusimwangalie, hebu tutazame faida moja ya Bwana kutuangalia sisi na sisi kumwangalia Bwana, kwa kutafakari mfano ufuatao.
Mtu aliyesimama mbele yako ukimtazama naye akikutazama, ni wazi kuwa mbele yake ni nyuma yako wewe na nyuma yake ni mbele yako wewe, kwasababu mnatazamana, tofauti na kwamba mngetazama wote upande mmoja, endapo mngetazama wote upande mmoja mbele yako ingekuwa ni mbele yake pia, na nyuma yako ni nyuma yake pia.
Sasa Bwana anapotutazama sisi yale mambo yetu yaliyopita kwake ni kama yajayo, na yale yajayo ni kama yaliyopita… Kwahiyo wakati tunawaza nini kitatokea kesho, tayari Bwana alishakipanga na kukimaliza, wakati tunawaza ni mambo gani na gani yatatupata miaka 10 au 20 ijayo tayari Bwana alishashughulika nayo zamani, kwani mbele yetu sisi ni nyuma ya Bwana muda mrefu sana.
Vile vile mambo yetu yaliyopita ambayo yanaonekana kama hayawezi kutengenezekeka tena, hayawezi kurekebishika tena, kwa MUNGU wetu yanakuwa ni mambo yanayotengenezeka na ni mambo yanayopangika, kinachotakiwa ni kitu kimoja tu!… nacho ni kumwangalia Bwana.
Yeremia 31:28 “Tena itakuwa, kwa kadiri NILIVYOWAANGALIA, ili kung’oa, na kubomoa, na kuangusha, na kuangamiza, na kutesa; kwa kadiri iyo hiyo nitawaangalia, ili kujenga, na kupanda, asema Bwana”.
Tunamwangaliaje Bwana?.. Kwanza kwa kuungama makosa, na kutembea katika Neno lake, hapo Bwana pia atatuangalia kwasababu siku zote pia analitazama Neno lake apate kilitimiza (Yeremia 1:12).
Usiangalie matatizo yanayokuzunguka, bali mwangalie Bwana, usiangalie mambo ya kutisha yanayojiandaa kutokea wewe mtazame Bwana, usiangalie mambo yaliyopita yaliyoharibika wewe mwangalie, kwani unayoyaona kama hayawezi tena kurekebika BWANA anaweza kuyafanya upya tena, na unayoona kama hayataweza kutimia kwa Bwana mambo yako yajayo kwake ni kama yaliyopita, endapo ukimtazama.
Mtazame Bwana!, Mtazame Bwana!.
Maran atha!.
Je YESU KRISTO alikuwa na wadogo zake?
Tafsiri ya Wakolosai 2:18 Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu,
UJIO WA BWANA YESU.
Moja la lango ambalo Mungu hulitumia sana, kutufikishia sisi taarifa zake, ni ndoto. Na kama ni lango la Mungu basi ni vema tufahamu kuwa ibilisi hatalipenda. Hivyo atahakikisha taarifa hizo anazivuruga au hazitufikii vema, kama tu vile anavyohakikisha watu hawaliewi Neno, au mahubiri, Ndivyo anavyofanya na kwenye ndoto pia.
Taarifa zitokazo kwa Mungu zinaangukia katika makundi matatu;
1) Tahadhari
Hizi ni taarifa za maonyo, au hatari zinazokuja mbeleni. Mfano wa taarifa hizi ni kama zile zilizomfikia Yusufu, alipokuwa Israeli, akaambiwa akimbilie Misri, kwasababu Herode anataka kumuua mtoto, na aliporudi baadaye, akaonywa tena asikae Yerusalemu, bali aende Nazareti.
Mathayo 2:19-22
19 Hata alipofariki Herode, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto huko Misri, 20 akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mamaye, ushike njia kwenda nchi ya Israeli; kwa maana wamekufa walioitafuta roho ya mtoto. 21 Akaondoka akamchukua mtoto na mamaye, akafika nchi ya Israeli. 22 Lakini aliposikia ya kwamba Arkelao anamiliki huko Uyahudi mahali pa Herode babaye, aliogopa kwenda huko; naye akiisha kuonywa katika ndoto, akasafiri pande za Galilaya,
Lengo la taarifa hizi ni mtu kuchukua hatua, aidha ya kivitendo au ya kimaombi.
Kwamfano Mungu anaweza kukuonyesha ajali, au msiba fulani. Hapo ujue hasaa unahitajika kuchukua hatua kimaombi kuharibu hizo roho za mauti, kwa kinywa chako.
2) Unabii
Hizi ni taarifa za mambo yajayo, Yale yatakayotokea baadaye, kwenye maisha yako, huduma, familia, nchi, au taifa. Mfano wa ndoto hizi, ni kama ile ya Farao juu ya miaka saba ya shibe na njaa, (Mwanzo 41) na Nebukadreza, juu ya ile sanamu kubwa, iliyowakilisha falme nne, zitakazokuja kusimama ulimwenguni (Danieli 2).
Halikadhalika Mungu anaweza kukuonyesha, maisha yako baadaye yatakuwaje, huduma yako baadaye, itasimamaje, maono yako baadaye yatafikia wapi, anaweza kukuonyesha mambo ya siku za mwisho, matukio yajayo, kuhusu nchi, watu, familia. Hatua unayopasa kuichukua ni kuomba, na kuandaa mazingira sasa. Mfano Farao aliposaidiwa tafsiri ya ndoto yake na Yusufu, alichukua hatua ya kuweka hazina ya vyakula kwasababu njaa ilikuwa inakuja mbele. Mungu akikuonyesha huduma yako itakuwa kubwa, anza leo kujiwekea hazina ya maarifa ya Neno la Mungu, anza kutendea kazi wito wako,. Akikuonyesha unawaombea watu wengi wanapona, anza leo kuwaombea watu hata kama hawaponi, omba hivyo hivyo kila siku, usikae tu ukasubiri ije kutimia huonyeshi jitahada yoyote, akikuonyesha biashara yako imekuwa, ongeza juhudi kufanya kazi.
3) Baraka
Mungu anaweza kuachia Neno la Baraka kwako, kwamfano ukaota, ndoto njema, labda unatiwa mafuta na Kristo, au unaambiwa maneno ya mafanikio kama vile Sulemani alipotokewa na Mungu na kuelezwa atapokea Hekima, na kuwa na mali nyingi. Uotapo ndoto ambazo ni za mafanikio kwako, uamkapo, hakikisha unazinenea kwa Imani. Unasema
“Na iwe kwangu kwa jina la Yesu Kristo”. Kama tu vile unavyobatilisha ndoto za maovu, labda mauti, vivyo hivyo hizi unazipokea kwa kinywa chako. Ni muhimu sana.
Ibrahimu aliota ndoto
Mwanzo 51:1-6
Baada ya mambo hayo neno la Bwana likamjia Abramu katika njozi, likinena, Usiogope, Abramu, Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana. 2 Abramu akasema, Ee Bwana MUNGU, utanipa nini, nami naenda zangu hali sina mtoto, na atakayeimiliki nyumba yangu ni huyu Eliezeri, Mdameski? 3 Abramu akasema, Tazama, hukunipa uzao, na mtu aliyezaliwa nyumbani mwangu ndiye mrithi wangu. 4 Nalo neno la Bwana likamjia likinena, Huyu hatakurithi, bali atakayetoka katika viuno vyako ndiye atakayekurithi. 5 Akamleta nje, akasema, Tazama sasa mbinguni, kazihesabu nyota, kama ukiweza kuzihesabu. Akamwambia, Ndivyo utakavyokuwa uzao wako. 6 Akamwamini Bwana, naye akamhesabia jambo hili kuwa haki.
Sasa kinachotokea ni kwamba ndoto nyingi sana, za taarifa mbalimbali kutoka kwa Mungu zinapotea akilini mwetu, na tunaona kawaida,
Ndoto hupotea kwa aidha namna mbili;
Namna mojawapo inaweza kutokea kwa mtu. Usikae ukafikiria kisa hukumbuki chochote, ukadhani hukuota ndoto yoyote. Zipo ndoto ulizoota. Hivyo ni vema ukajifunza namna ya kukabiliana na lango lako la ndoto. Ndio maana utaona wengine tukio likishatokea ndio anakumbuka kuwa alishawahi onyeshwa tukio hilo. Hiyo haitakiwi.
Nifanye nini ili nikumbuke ndoto zangu?
Njia tatu zinazoweza kumfanya mtu akumbuke ndoto.
i) Kuomba:
Kila asubuhi uamkapo, katika maombi yako, hakikisha unashika Kichwa chako, kisha unasema maneno haya
‘Baba, nafungua lango la ndoto zangu, yote uliyosema nami usiku nilipolala, ninayoyakumbuka na nisiyoyakumbuka yakawe bayana sasa kwa kwa jina la Yesu, ndoto zilizoibiwa na ibilisi, kumbukumbu zangu, na fikra zangu zilizofutika, navirejesha vyote ndani ya ufahamu wangu sasa kwa jina la Yesu Kristo’.
Ukijifunza kuomba namna hiyo, tayari umekaribisha msaada wa Mungu, mahususi katika eneo lako la ndoto na hivyo urahisi wa kukumbuka unakuja.
ii) Utulivu (Kutafakari)
Ukishaomba, pendelea kupata utulivu, kisha tafakari kwanza Neno la Mungu. Kila asubuhi hakikisha unapata kwanza mkate wa uzima ambao ni Neno, tafakari Neno kwa muda kidogo, jiulize vifungu hivi vinamaana gani, je! Siku ya leo nitaviwekaje katika maisha yangu? Fanya tu hivyo tembea maeneo mbalimbali ya kwenye biblia, kisha tafakari tena juu ya maisha yako ya rohoni, juu ya maono yako, juu ya familia yako utajiboreshaje, baadaye juu ya ratiba zako za siku..
Katika wingi wa kutafakari, mara nyingi Mungu hurejesha ndoto zilizosahaulika, utashangaa katika tafakari Fulani hapo hapo unakumbuka kuna jambo uliota, linaloendana na tukio hilo. Ujue huo ni ujumbe wa Mungu.
Ukikosa muda wa kutosha asubuhi, Fanya hivyo muda wa usiku kabla ya kulala, Pata utulivu mwingi peke yako, Utakumbushwa ndoto nyingi.
iii) Mazungumzo
Njia nyingine ambayo humfanya Mungu arejeshe ndoto zetu kirahisi, ni katika mazungumzo, kumbuka kila eneo la maisha yako au wengine, yamkini Bwana alishawahi kusema na wewe, kwa njia ya ndoto, lakini hujui.
Kwamfano ukiwa na mwenzako, au wenzako, mnazungumza sana, Habari njema za kanisa, katika mazungumzo ya muda mrefu ikiwa lipo ambalo Bwana alikuonyesha, utaona kumbukumbu hiyo inakujia, au labda mnazungumza kwa kina Habari ya siku za mwisho, Kumbukumbu ya ndoto kama hiyo itakujia, au malengo ya maono yako.
Hivyo mazungumzo mazuri na yenye maana hurejesha fikra zilizopotea. Kwahiyo, jijengee desturi ya kuwa na mazungumzo mema.
Zingatia pia si kila ndoto hutoka kwa Mungu, ili kuweza kutofautisha ndoto za Mungu na za shetani, fungua link hii, uweze kupitia..>>>> https://wingulamashahidi.org/2019/09/03/nitajuaje-kama-ndoto-ni-ya-mungu-au-ya-shetani/
Mungu akubariki.
Kuna ndege anaitwa kiruka njia, ambaye anatajwa kama mmoja wa ndege najisi, kwenye Kumbukumbu 14:15, lakini ndege huyu anasifa moja ambayo, huwa ina funzo kubwa sana la kiroho.
Tofauti na ndege wengine, ambao huruka aidha mchana, au usiku, kujitafutia chakula, kwamfano mwewe, mbayuwayu, korongo, tai, ni ndege wa mchana, lakini pia bundi, popo, ni ndege wa usiku, wote hawa hufanya kazi aidha majira ya kutwa nzima ya mchana, au usiku kucha.
Lakini kiruka njia, huruka zaidi, majira ya alfajiri sana, na jioni sana. Majira haya huyapendelea kwasababu, ni wakati wa mageuko ya siku, ambayo ndege wote wawindaji hujiandaa Kwenda mapumziko, au kuamka. Kwamfano muda wa jioni kama vile saa 12, ndege wakali wawindaji kama vile tai, mwewe, kipanga, n.k. wanaacha uwindaji, na kutafuta makao yao kupumzika, lakini pia wakati huo huo ndege wakali wa usiku kama vile bundi, hujiandaa kutoka waende kwenye mawindo yao saa mbili, Kwahiyo huo muda hapo Katikati mazingira kwake huwa si ya upinzani mkubwa.
Kwasababu yeye ni ndege dhaifu, na anaweza kuwindwa na ndege wakubwa, majira hayo kwake ni salama zaidi. Vivyo hivyo ule muda wa alfajiri sana, miale ya jua inapoanza kuonekana kwa mbali sana, hutoka na Kwenda kuwinda, muda huo ndege wa usiku ndio wanakwenda kulala, huku ndege wa mchana wanajiandaa kutoka, mpaka inapofika saa 12 asubuhi, tayari ameshamaliza uwindaji wake.
Licha ya kuwa wakati huo, ndege wengi hawapo hewani, lakini wakati huo, wa alfajiri sana na jioni sana, ndio makundi ya wadudu wengi wa ardhini hutoka kuruka juu, ikiwemo mbu, kumbikumbi, mchwa, nondo, mende n.k. kwasababu yeye hula wadudu, anaweza kukamata wadudu hata elfu moja ndani ya saa moja tu. Hivyo kwa muda mfupi sana akawa ameshashiba, zaidi ya mihangaiko mingi ya kutwa nzima, kugombania vyakula, na masumbufu mengi.
Ndege huyu mchana hupumzika zake, kwenye miti, na usiku pia, lakini hutumia alfajiri yake na jioni yake vizuri. Ndio maana ni vigumu kujulikana, kwasababu shughuli zake anazifanya wakati anga ni tulivu.
Hutufundisha nini?
Bwana alituambia tuwatafakari ndege (Mathayo 6:26)
Ni lazima tuthamini mida hii miwili, kuitumia kuwa uweponi mwa Bwana, Bwana Yesu alipendelea sana, kuamka alfajiri kuomba,
Marko 1:35 Hata alfajiri na mapema sana akaondoka, akatoka akaenda zake mahali pasipokuwa na watu, akaomba huko.
Ipo faida kubwa sana kuamka mapema kuomba kwasababu, muda huo anga ni tulivu, wakati watu wamelala, wewe unapokea thawabu za siku kutoka kwa Bwana. Kuna usemi unaosema biashara ni asubuhi, kwasababu wameona Riziki nyingi huwaga majira hayo, vivyo hivyo rohoni, ukijifunza kuomba majira hayo, na jioni pia kabla hujaimaliza siku, Basi utaona tofauti kubwa sana, na wepesi mwingi wa masumbufu ya siku.
Hawa ndege katika Walawi 11:13-19 ndio ndege gani kwasasa?
MTEGO HUTEGWA BURE, MBELE YA MACHO YA NDEGE YE YOTE.
Je tamaa ni dhambi kulingana na Yakobo 1:15?
Jina la Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe sana, karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu wetu lililo taa na mwanga wa njia yetu (Zab.119:105).
Yeremia 18: 1 “Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, kusema, 2 Ondoka, ukashuke mpaka NYUMBA YA MFINYANZI, na huko nitakusikizisha maneno yangu.
Yeremia 18: 1 “Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, kusema,
2 Ondoka, ukashuke mpaka NYUMBA YA MFINYANZI, na huko nitakusikizisha maneno yangu.
3 Basi nikashuka mpaka nyumba ya mfinyanzi, na tazama, alikuwa akifanya kazi yake kwa magurudumu. 4 NA CHOMBO KILE, ALICHOKUWA AKIKIFINYANGA, KILIPOHARIBIKA MKONONI MWAKE YULE MFINYANZI, ALIKIFANYIZA TENA KUWA CHOMBO KINGINE, kama alivyoona vema yule mfinyanzi kukifanya”.
Katika mstari wa 4 tunasoma kuwa Mfinyazi alikifinyanga chombo kilichoharibika na kuwa chombo kingine, zingatia hilo neno “chombo kingine” maana yake sio tena chombo kile cha kwanza kilichoharibika.
Tuchukue mfano labda mfinyazi huyu alifinyanga kikombe cha maji hapo kwanza, na baadae akaone kimeharibika au kina kasoro, ndipo anapokivunja vunja kile kikombe cha udongo na kuutia tena maji na kuufinyanga tena kuwa sahani..
Sasa udongo ni ule ule umeweza kutoa chombo kingine kipya tofauti na kile cha kwanza, na MUNGU alimwambia hivo hivyo YEREMIA, lakini Yeremia hayupo sasa, ila sisi tupo, hivyo anatuambia sisi kuwa tujifunze kwa Mfinyanzi kwa kuwa yeye (MUNGU) ndiye mfinyanzi mkuu wa maisha yetu.
Yeremia 18: 5 “Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema, 6 Ee nyumba ya Israeli, je! Siwezi mimi kuwatendea ninyi vile vile kama mfinyanzi huyu alivyotenda? Asema Bwana. Angalieni, KAMA UDONGO ULIVYO KATIKA MKONO WA MFINYANZI, NDIVYO MLIVYO NINYI KATIKA MKONO WANGU, EE NYUMBA YA ISRAELI”.
Yeremia 18: 5 “Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema,
6 Ee nyumba ya Israeli, je! Siwezi mimi kuwatendea ninyi vile vile kama mfinyanzi huyu alivyotenda? Asema Bwana. Angalieni, KAMA UDONGO ULIVYO KATIKA MKONO WA MFINYANZI, NDIVYO MLIVYO NINYI KATIKA MKONO WANGU, EE NYUMBA YA ISRAELI”.
Je wewe ni chombo cha aina gani?..
Kama maisha yako yametawaliwa na dhambi basi fahamu kuwa ni dhahiri kuwa wewe ni chombo kilichoharibika, kama maisha yako yametawaliwa na ugomvi, uasherati, wizi, masengenyo, kiburi na mambo mengine yote ambayo ni kinyume cha Neno la MUNGU (yaliyotajwa kwenye Wagalatia 5:19-20), huu ni wakati wa wewe kumkimbilia mfinyazi Mkuu YESU KRISTO, akufinyange kuwa chombo kingine cha heshima..
Warumi 9:21 “Au mfinyanzi je! Hana amri juu ya udongo, kwa fungu moja la udongo kuumba chombo kimoja kiwe cha heshima, na kimoja kiwe hakina heshima?”
Bwana YESU anaweza kukufanya kuwa mwingine kabisa, mtu wa maana kabisa, ambapo ile hali yako ya ulevi wa pombe au ulevi wa anasa inayokusumbua, kinachotakiwa tu ni kukiri kuwa wewe ni mkosaji mbele zake na unahitaji msaada wake, na baada ya hapo kutubu dhambi zako mbele yake huku ukidhamiria kabisa kuacha mambo yote mabaya, na kumwambia naomba unifinyange tena, kupitia Roho wake mtakatifu atakayeingia ndani yako atakugeuza na kuwa mtu mwingine.
Kumbuka toba isiyo ya kumaanisha haileti matokeo yoyote kwa mtu anayetaka mabadiliko, hakikisha unapotubu dhamiria kujitakasa, kwa kujitenga na vichocheo vyote vya dhambi, kama ulikuwa ni mlevi acha kwenda Bar, kama ulikuwa unajiuza jizuie kwa bidii kwenda vituo vya ulivyokuwa unafanya biashara hiyo, ili uumpe nafasi Roho Mtakatifu ndani yako kukufinganya upya kuwa chombo kingine.
2Timotheo 2:21 “Basi ikiwa mtu amejitakasa kwa kujitenga na hao, atakuwa chombo cha kupata heshima, kilichosafishwa, kimfaacho Bwana, kimetengenezwa kwa kila kazi iliyo njema”.
Bwana YESU akubariki sana.
Zaburi 145:19 “Atawafanyia wamchao matakwa yao, Naye atakisikia kilio chao na kuwaokoa”.
Pamoja na kwamba tumeagizwa kuomba “Mapenzi yake yatimie/yatimizwe (Mathayo 6:10”.
Lakini “Siri” moja kuu ni kwamba zaidi ya asilimia 90 ya Maombi ya wanaomcha MUNGU ni mapenzi ya MUNGU.Kwanini?..
Kwasababu maandiko yanatuambia hapo kuwa “Atawafanyia wamchao matakwa yao, Naye atakisikia kilio chao na kuwaokoa”.
Zingatia hilo neno “Atawafanyia wamchao matakwa yao”.
Kumbe Mungu anawapatia watu wake wanaomcha “Matakwa yao, yaani haja zao wanazozitaka”.
Kwa mtu anayemcha Mungu akiomba amani, ni asilimia kubwa ya hitaji lake hilo kuwa ni mapenzi ya MUNGU.
Mtu anayemcha MUNGU akiomba afya, ni asilimia zaidi ya nusu kuwa anaomba jambo ambalo ni mapenzi ya MUNGU.
Mtu anayemcha MUNGU akiomba akiomba mambo mengine yote ikiwemo mafanikio ya kiroho na kimwili ni mapenzi ya MUNGU, kwasababu MUNGU anawapa wamchao matakwa yao.
Je unataka kupewa matakwa yako na MUNGU?.Jibu ni rahisi “Mche Mungu tu”..Na Biblia inasema kumcha Mungu ndio hekima na kuepukana na uovu ndio ufahamu (Ayubu 28:28).
Sasa hatuwezi kumcha MUNGU kwa nguvu zetu, inahitajika kuwezeshwa na Roho Mtakatifu, kwasababu tabia ya kumcha MUNGU, ni zao la Roho Mtakatifu.Isaya 11:2 “Na roho ya BWANA atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, ROHO YA MAARIFA NA YA KUMCHA BWANA”.
Sasa kama kumcha Bwana ni zao la Roho Mtakatifu, je tunampataje Roho Mtakatifu..
Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? 38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”
38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”
Kumbe kanuni ya kupokea Roho ni kutubu na kubatizwa kwa jina la YESU KRISTO!.
Basi maana yake tukitubu na kubatizwa tutapokea Roho Mtakatifu kama ilivyoandikwa, na matokeo ya kujaa Roho Mtakatifu, ni uwezo wa kumcha MUNGU kuingia ndani yako.Na matokeo ya kumcha MUNGU sana ni kusikiwa maombi yako na Bwana kukupa matakwa yako.
Je umeokoka?..Je unamcha Bwana?.
Zaburi 112:1 “Haleluya. Heri mtu yule amchaye BWANA, Apendezwaye sana na maagizo yake. 2 Wazao wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa”. 3 Nyumbani mwake mna utajiri na mali, Na haki yake yakaa milele”.
Zaburi 112:1 “Haleluya. Heri mtu yule amchaye BWANA, Apendezwaye sana na maagizo yake.
2 Wazao wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa”.
3 Nyumbani mwake mna utajiri na mali, Na haki yake yakaa milele”.