NENO NA MAOMBI~ Sehemu ya 2 (AMRI YA UPENDO)

NENO NA MAOMBI~ Sehemu ya 2 (AMRI YA UPENDO)

Jina la Bwana YESU libarikiwe, karibu katika kujifunza Neno na Maombi. Kusoma Neno bila Maombi, au kuomba bila Neno ni sawa na kitamba cha bendera kisicho na mlingoti, kupitia mfululizo huu wa tafakari hizi tutapata mwongozo sahihi wa kuomba kupitia maandiko ya kwenye Biblia.

PENDO LA MUNGU.

Bwana YESU alitufundisha kuwa Amri ya kwanza ni “Kumpenda Bwana na ya pili ni kuwapenda majirani kama nafsi zetu”.

Mathayo 22:36 “Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu?

37 Akamwambia, MPENDE BWANA MUNGU WAKO KWA MOYO WAKO WOTE, NA KWA ROHO YAKO YOTE, NA KWA AKILI ZAKO ZOTE.

38 Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.

39 Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, MPENDE JIRANI YAKO KAMA NAFSI YAKO.

40 Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii”.

Na tena alisema…

Yohana 14:21 Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye; naye anipendaye atapendwa na Baba yangu; nami nitampenda na kujidhihirisha kwake.

 

   1. OMBA ONGEZEKO LA UPENDO WA MUNGU NDANI YAKO (Tumia dakika 30)

i. Kwa moyo wako wote.

  • Hapa utaomba Bwana akujalie kumtafuta kwa hiari bila shuruti, kwasababu hiyo ndio maana ya kumpenda kwa moyo wako wote.

     ii. Kwa roho yako yote

– Hapa utamwomba Bwana kuwa upendo wako ukatoke rohoni, katika kumtafuta kwasababu Neno linasema waabudua watamwabudu baba katika roho na kweli.

               iii.    Kwa akili zako zote.

                           – Hapa utaomba Bwana akuwezeshe kumtumikia yeye kwa ujuzi aliokupa, (ule wa asili na ule wa kujifunza) kama ni msomi basi kupitia elimu yako hiyo umtumikie MUNGU, na kuyafanya mapenzi yake.

          iv. Kwa Nguvu zako zote.

      – Nguvu zinaweza kuwa za mwili kama wewe ni kijana, lakini pia zinaweza kuwa za kifedha, katika maeneo hayo yote mwombe BWANA akusaidie uweze kumpenda MUNGU na kufanya mapenzi yake, Utoe muda wako au mali zako katika kumtumikia MUNGU.

            2. OMBA UPENDO KWA JIRANI. (Tumia dakika 30)

Neno la MUNGU linatufundisha kuwa “Tujaponena kwa lugha zote na kufanya ishara zote kama hatuna Upendo sisi sio kitu”

      1Wakorintho 13:1 “Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao”.

Na tena inasema…

Waebrania 13:1 “Upendano wa ndugu na udumu”.

    i. Omba Upendo kwa ndugu wa kiroho (Wachungaji na washirika wenzako)

  • Hapa utaomba Bwana akakukumbushe mema waliyokutendea.
  • Utaomba Bwana akuondolee chuki na kutokusamehe.
  • Utaomba Bwana akuoneshe kasoro zako ili pendo kati yako na wapendwa wenzako lidumu.
  • UOmbea kanisa na wakristo wenzako wakajawe na Upendo wa kiMungu.
  • Omba Bwana akaachie roho ya kusameheana.

     ii.   Omba Upendo kwa ndugu wa kimwili (Wana familia)

  • Hapa mwombe Bwana akuongezee upendo kwa wazazi, na ndugu wengine wadogo kwa wakubwa.
  • Waombee wana familia yako wajawe na upendo kama wewe unavyojiombea..

        3. KEMEA KILA ROHO INAYOJIINUA KUPOOZA UPENDO WA MUNGU, NA WA KINDUGU

Kemea kwa jina la YESU KRISTO kila pando la chuki kanisani kwako, katikati yako na wakristo wenzako, katikati yenu kama familia.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

About the author

Nuru ya Upendo administrator

Leave a Reply