FAIDA ZA MAOMBI YA USIKU

FAIDA ZA MAOMBI YA USIKU

Kwanini maombi ya Usiku yana nguvu kuliko ya mchana?

  • Usiku watu wakiwa wamelala ndio muda ambao mawakala wa shetani (wachawi)  wanafanya kazi, kwahiyo kuna uhusiano mkubwa wa mtu akiwa amelala na kulogwa kwake…Maroho yanawaingia wengi wakati wamelala. Kwahiyo unapoomba usiku maana yake unakwenda kinyume na hizo nguvu.
  • Mtu akiwa amelala ndio wakati wa kilicho chake kuibiwa…Kwamfano wezi wanakuja kuiba usiku, mhusika akiamka asubuhi anakuta mali yake haipo, kadhalika Samsoni alinyolewa nywele zake na Delila alipokuwa amelala, alipoamka alijikuta nguvu zimemwisha, Kadhalika Operation nyingi mahospitalini zinafanyika wakati mtu akiwa amelala usingizi.

Kadhalika usiku wakati watu wamelala ndio wakati Adui anaiba vipawa vya watu..Kwahiyo unapokwenda kusali usiku, maana yake, unaingia kwenye uwanja wa mapambano uso kwa uso na Adui yako na ni rahisi kumwangusha..Kwahiyo yanakuwa ni maombi ya shabaha..Na yana madhara makubwa kwa shetani na ufalme wake. 

Shetani hapendi watu wasali usiku kwasababu anajua madhara yatakayomfikia.

Bwana akubariki. Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada Nyinginezo:

FAIDA ZA MAOMBI.

MAOMBI YA YABESI.

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

UPUMBAVU WA MUNGU.


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
6 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Nicholaus
Nicholaus
3 years ago

Ubarikiwe somo zuri

Anonymous
Anonymous
3 years ago

be blessed father infinitly

William Noel
William Noel
3 years ago

Ubarikiwe