Title April 2022

NJIA NYINGINE YA KUPATA REHEMA NA KIBALI KUTOKA KWA MUNGU.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, libarikiwe.

Zipo njia nyingi za kuvuta rehema za Mungu, juu yako.. baadhi ya hizo ni kuwa Mwombaji, mtoaji, na mtu wa kusamehe.

Lakini ipo njia nyingine ambayo tukiijua basi, siku zote tutakuwa watu wa kupata rehema kutoka kwa Bwana na hata kama kuna mabaya tuliyofanya mbele za Mungu, basi anatusamehe na kughairi kutuadhibu.

Na njia hiyo si nyingine Zaidi ya “kutojilipiza kisasa” au kutofurahia “anguko la wanaofanya vita nawe”.

Watu wengi leo hususani Wakristo, wanakosa maarifa kwa kudhani kuwa Mungu anapendezwa sana na anguko la maadui zao. Hivyo kila siku, na kila saa wanawaombea shari maadui zao, na kila siku wanakaa wakisubiria anguko lao ili wafurahi.. (Kama vile Nabii Yona alivyokaa chini ya mtango, akingoja kuona Ninawi inaangamizwa).

Na hiyo yote ni kutokana na jinsi tulivyofundishwa au kujifunza. Pasipo kujua kuwa hayo sio mapenzi ya Mungu kabisa.. Ingekuwa Mungu ana hasira sana na adui yako, nadhani asingemuumba kabisa.. Lakini mpaka unamwona anaishi, jua ni mapenzi ya Mungu yeye awepo pale..

Sasa hebu tujifunze mstari ufuatao ili tuweze kuelewa vizuri..

Mithali 24:17 “Usifurahi adui yako aangukapo; Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo;

18 Bwana asije akaliona hilo, likamkasirisha; Akageuzia mbali naye hasira yake”.

Umeona hapo?..Anasema usifurahi, ukimwona adui yako anaanguka!.. kwasababu Bwana kamwangusha kwa lengo la kumnyenyekeza na si kwa lengo la kumwangamiza kabisa!, kama wewe unavyofikiri..

Hivyo unaposhangilia anapoadhibiwa na Mungu, jambo hilo halimpendezi kabisa Mungu… na Bwana akiona unashangilia kuanguka kwake, basi anaghairi ule ubaya na kukugeukia wewe. (Kwasababu na wewe sio kwamba ni mkamilifu mbele zake, kwamba haustahili adhabu yoyote, unazo kasoro nyingi sana, isipokuwa Mungu ni mvumilivu kwako).

Vile vile, watu wanaofanya vita na wewe na kukushutumu, kukusengenya, kukulaumu, kukuudhi, kukuumiza, au hata kukutesa pasipo hatia yoyote, usijaribu kamwe kuwarudishia mabaya, wala kuwashitaki mbele za Mungu, wewe waombee rehema…na kubali mashutumu yao..Kwasababu kwa kufanya hivyo, Mungu, sio kwamba utakuona wewe ni mjinga mbele zake, kinyume chake utaonekana mwenye busara na hivyo utapata rehema Zaidi na kibali mbele zake.

Usichukizwe na laana watu wanazokulaani, kwasababu laana hizo kwako, ndio baraka kwako, mashutumu hayo unayoshutumiwa, Mungu anayasikiliza na yanamhuzisha, hivyo Bwana atakupa wewe rehema kwa mashutumu hayo, atakuhurumiwa kwa masengenyo hayo…N.k

Daudi aliijua hii siri, ndio maana kamwe hakuwahi kutoa Neno la laana kwa waliokuwa wanamlaani, wala hakuwahi kufurahia kuanguka kwa waliokuwa wanaitafuta roho yake, ndio maana utaona alilia sana, siku Sauli alipokufa, vile vile alilia sana Absalomu, mwanae alipokufa!..ambao hawa wote walifanyika maadui zake.

Sasa ni kwanini hakuwalaani waliokuwa wanamlaani?, ni kwasababu alijua KUWA KULAANIWA KWAKE NA WATU NDIO KUBARIKIWA KWAKE NA BWANA.

Utakumbuka wakati Fulani alipokuwa anamkimbia Mwanae Absalomu, alikutana na mtu mmoja aliyeitwa Shimei, mtu huyo alianza kumlaani, lakini Daudi hakurudisha laana hata moja, wala hakumwua ingawa alikuwa anao huo uwezo.

2 Samweli 16:5 “Basi mfalme Daudi alipofika Bahurimu, tazama, kulitoka huko mtu wa jamaa ya nyumba ya Sauli, jina lake akiitwa Shimei, mwana wa Gera; ALITOKA, AKALAANI ALIPOKUWA AKIENDA.

6 Tena akamtupia Daudi mawe, na watumishi wote wa mfalme Daudi; na watu wote na mashujaa wote walikuwako mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto.

7 Na Shimei alipolaani, alisema hivi, NENDA ZAKO! NENDA ZAKO! EWE MTU WA DAMU! EWE MTU USIYEFAA!

8 Bwana amerudisha juu yako damu yote ya nyumba ya sauli ambaye umetawala badala yake; naye bwana ametia ufalme katika mkono wa absalomu mwanao; kisha, angalia, wewe umetwaliwa katika uovu wako mwenyewe, kwa sababu umekuwa mtu wa damu.

9 Ndipo Abishai mwana wa Seruya, akamwambia mfalme, Mbona mbwa mfu huyu amlaani mfalme bwana wangu? Na nivuke, nakusihi, nikaondoe kichwa chake.

10 Mfalme akasema, Nina nini na ninyi, enyi wana wa Seruya? Kwa sababu yeye analaani, na kwa sababu Bwana amemwambia, Mlaani Daudi, basi, ni nani atakayesema, Mbona umetenda haya?

11 Daudi akamwambia Abishai, na watumishi wake wote, Angalieni, huyu mwanangu, aliyetoka viunoni mwangu, anautafuta uhai wangu; si zaidi Mbenyamini huyu sasa? MWACHENI ALAANI, KWA SABABU BWANA NDIYE ALIYEMWAGIZA.

12 LABDA BWANA ATAYAANGALIA MABAYA YALIYONIPATA, NAYE BWANA ATANILIPA MEMA KWA SABABU YA KUNILAANI KWAKE LEO.

13 Basi wakaendelea njiani Daudi na watu wake; SHIMEI NAYE AKAAENDELEA JUU YA UBAVU WA KILE KILIMA, KWA KUMKABILI, HUKU AKIENDELEA, AKILAANI, AKIMTUPIA MAWE, NA KURUSHA MAVUMBI”.

Je na sisi leo hii tunaweza kukubali mashutumu namna hii?.. kiasi kwamba wanaotusengenya na sisi hatuwarudishii masengenyo, wala kuwalaumu?.. kiasi kwamba tunahuzunika kuanguka kwa wanaoshindana nasi?

Tukifikia hatua hii tutapata kibali sana Mbele za Mungu. Unaona Daudi hapo baada ya kukubali mashutumu na laana anasema.. “MWACHENI ALAANI, KWA SABABU BWANA NDIYE ALIYEMWAGIZA.  LABDA BWANA ATAYAANGALIA MABAYA YALIYONIPATA, NAYE BWANA ATANILIPA MEMA KWA SABABU YA KUNILAANI KWAKE LEO. ”

Daudi alijua ili kupata Mema, hana budi kukubali laana, ili kupata kibali hana budi kukubali mashutumu. Na si Daudi peke yake, utaona pia na Ayubu, katika Maisha yake yote anasema hajawahi kufurahia anguko la wanaomchukia au wanaoshindana naye.. jambo lililomfanya apate kibali kikubwa sana mbele za Mungu, na kuonekana kuwa mkamilifu kuliko watu wote waliokuwepo chini ya jua katika kipindi chake..

Ayubu 31:29 “Kama nilifurahi kwa kuangamia kwake huyo aliyenichukia, Au kujitukuza alipopatikana na maovu;

30 (Naam, sikukiacha kinywa changu kufanya dhambi Kwa kuutaka uhai wake kwa kuapiza);”

Na sisi ili tupate rehema na kibali na baraka, na Mema kutoka kwa Mungu, hatuna budi kuwa kama Daudi na Ayubu..Ni kanuni inayoonekana kama ni ngumu, lakini ndio iliyokubalika mbele za Mungu. Injili za kupiga maadui, na kutwa kuchwa kushindana na maadui zako na kusubiria kuona shari yao ili ufurahie nataka nikuambie ni injili za kuzimu, ingawa kwa nje zinaonekana kama zina hekima.. Bwana Yesu Mkuu wa uzima alisema maneno haya..

Mathayo 5:43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;

44 lakini mimi nawaambia, WAPENDENI ADUI ZENU, WAOMBEENI WANAOWAUDHI,

45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.

46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?”

Unataka Rehema?, unataka kibali?, unataka Mema kutoka kwa Mungu??.. huna budi kukubali mashutumu, kwasababu Kristo naye alikubali mashutumu na kejeli na kudharauliwa lakini sasa ana utukufu kuliko vitu vyote.

Bwana YESU ANARUDI!!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

VITA DHIDI YA MAADUI

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

NJIA MUNGU ALIYOIWEKA KWA KILA JAMBO.

BASI, IWENI NA HURUMA, KAMA BABA YENU ALIVYO NA HURUMA

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

VIACHENI VYOTE VIKUE HATA WAKATI WA MAVUNO.

Jina la Bwana Yesu Kristo, Mkuu wa Uzima, libarikiwe.. karibu tujifunze biblia Neno la Mungu wetu, ambalo ni taa iongozayo miguu yetu na mwanga wa njia yetu (Zab.119:105).

Je unajua ni kwanini baadhi ya watu waovu, Mungu anaruhusu wafanikiwe katika ulimwengu huu, ijapokuwa wanalikufuru jina lake? Siri ipo katika mistari ifuatayo..

Mathayo 13:24 “Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;

25 lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.

26 Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.

27 Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu?

28 Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, Basi, wataka twende tukayakusanye?

29 AKASEMA, LA; MSIJE MKAKUSANYA MAGUGU, NA KUZING’OA NGANO PAMOJA NAYO.

30 VIACHENI VYOTE VIKUE HATA WAKATI WA MAVUNO; NA WAKATI WA MAVUNO NITAWAAMBIA WAVUNAO, YAKUSANYENI KWANZA MAGUGU, MYAFUNGE MATITA MATITA MKAYACHOME; BALI NGANO IKUSANYENI GHALANI MWANGU”.

Nataka tuone huo mstari wa 30 unaosema.. “VIACHENI VYOTE VIKUE”..

Hili ni Neno kubwa sana.. Yaani Mungu anaruhusu Magugu yasitawi ndani ya shamba lake?.. Si ajabu leo unaona waovu wanasitawi katika dunia yake, si ajabu unaona leo wachawi wanavuna, wauaji wanafanya biashara na kufanikiwa, waabudu sanamu wanaishi miaka mingi, walevi wanastawi katika dunia hii hii, wanayoishi watu wanaomcha Mungu.

Ukiona hivyo usishangae, kwasababu ni Mungu karuhusu wasitawi, wao ni magugu kati ya Ngano, ndani ya shamba lake, na Mungu kazuia wasiondolewe kwanza bali wakue Pamoja na Ngano, hata wakati wa mavuno, maana yake zile baraka za kumwagiwa maji na kuwekewa mbolea wacha nao wazifaidi mpaka wakati wa mavuno, na utakapofika wakati wa mavuno zitangamizwa milele..(Kwahiyo kumbe lengo la kuacha magugu yakue Pamoja na ngano, ni ili mwisho wa siku magugu hayo yale kuangamizwa)

Ndio maana sasa Daudi akasema maneno haya…

Zaburi 92:7 “Wasio haki wakichipuka kama majani Na wote watendao maovu wakistawi. Ni kwa kusudi waangamizwe milele”

Na Sulemani mwanae pia akasema…

Mithali 1:32 “…kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza”

Katika siku hizi za mwisho shetani anawafanya watu waangalie hali zao za kimaisha, na kuzifanya kuwa kipimo cha kwanza cha hali zao za kiroho. Kwamba ukipata mafanikio mengi basi ni Mungu kakubariki, na vile vile usipokuwa na mafaniko basi kuna tatizo, kwamba upo mbali na Mungu, Kufuatia 3 Yohana 1:2.

Ni kweli hali za kimaisha ni kipimo cha hali ya kiroho, lakini kipimo hichi si thabiti asilimia mia, kwasababu kuna matajiri wengi watakuwepo kuzimu, na vile vile kuna maskini wengi watakuwepo mbinguni (kasome Luka 16:19-31).

Hivyo kukubaliwa kwetu na Mungu hatukupimi kwa mafanikio, kwasababu yeye mwenyewe alisema “VIACHENI VYOTE VIKUE PAMOJA”. Ili wakati wa mavuno viangamizwe.

Sasa swali kama Mafanikio sio kipimo thabiti cha kukubaliwa na MUNGU, je kipimo thabiti kitakuwa ni kipi?

Kipimo kamili ni UTAKATIFU….Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, ambao hapana MTU ATAKAYEMWONA BWANA ASIPOKUWA NAO”.

Hicho ndio kipimo ambacho, kipo thabiti asilimia mia..Maana yake ukiwa mtakatifu utamwona Mungu, usipokuwa mtakatifu hutamwona Mungu, hakuna ambaye ataenda kuzimu akiwa mtakatifu..wala hakuna ambaye ataenda mbinguni kama si mtakatifu.. Tofauti na kipimo cha kwanza ambacho hakieleweki sana..kwasababu wapo matajiri kuzimu, na maskini mbinguni.

Kama ni hivyo, basi huu si wakati wa kutafuta kwanza mafanikio ya mwilini, bali wa kutafuta kwanza Utakatifu, ili tukae mbali na dhambi..kwasababu dhambi ndiyo itakayotutenga na Mungu milele.

Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,

20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,

21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, KATIKA HAYO NAWAAMBIA MAPEMA, KAMA NILIVYOKWISHA KUWAAMBIA, YA KWAMBA WATU WATENDAO MAMBO YA JINSI HIYO HAWATAURITHI UFALME WA MUNGU”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

UTENDAJI KAZI MWINGINE WA ROHO MTAKATIFU USIOUFAHAMU.

Je! Ni kweli Yesu alirejesha kila kitu kama pale Edeni?

 MAVUNO NI MENGI

MWISHO WA MAVUNO, NI MWISHO WA DUNIA.

UTENDAJI KAZI MWINGINE WA ROHO MTAKATIFU USIOUFAHAMU.

Rudi nyumbani

Print this post

Kuvyaza ni nini katika biblia? (Ayubu 21:10).

Ayubu 21:10 “Fahali wao HUVYAZA wala hapungukiwi na nguvu; Ng’ombe wao mke huzaa, asiharibu mimba”.

Kuvyaza ni lugha ya “kuzaliana” inayotumika kwa Wanyama wa kiume. Badala ya kusema “Ng’ombe dume anapanda”, lugha nzuri ni kusema “ng’ombe anavyaza” . Neno hili limeonekana mara moja tu katika biblia..

Ayubu aliiona njia ya wasio haki, kwamba  mali zao zinapongezeka, na mafahali yao YANAPOVYAZA na, na ng’ombe wao wa kike wanavyozaa kwa wingi, na huku wanamkataa Mungu.. mwisho wao utakuwa ni kushuka kuzimu kwa ghafla.

Ayubu 21:7 “Mbona waovu wanaishi, Na kuwa wazee, naam, na kuongezeka kuwa na nguvu?

8 Kizazi chao kinathibitika nao machoni pao, Na wazao wao mbele ya macho yao.

9 Nyumba zao zi salama pasina hofu, Wala fimbo ya Mungu haiwapigi.

10 Fahali wao huvyaza wala hapungukiwi na nguvu; Ng’ombe wao mke huzaa, asiharibu mimba.

11 Huwatoa kama kundi watoto wao. Na watoto wao hucheza.

12 Huimba kwa matari na kwa kinubi, Na kuifurahia sauti ya filimbi.

13 SIKU ZAO HUTUMIA KATIKA KUFANIKIWA, KISHA HUSHUKA KUZIMUNI GHAFULA.

14 Walakini walimwambia Mungu. Tuondokee; Kwani hatutaki kuzijua njia zako.

15 Huyo Mwenyezi ni nani, hata tumtumikie? Nasi tutafaidiwa nini tukimwomba?”.

Vile vile Daudi naye aliliona hilo hilo, kuwa mafaniko ya Mtu mwovu, mwisho wake ni kuangamia.

Zaburi 92:7 “Wasio haki wakichipuka kama majani Na wote watendao maovu wakistawi. Ni kwa kusudi waangamizwe milele”

Na Sulemani naye aliliona hilo na kwa uweza wa Roho akasema..

Mithali 1:32 “…kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza”.

Hii ikifunua kuwa mafanikio sio uthibitisho wa kwanza kwamba tumekubaliwa na Mungu, ukilima na kuvuna na huku moyoni umemwacha Mungu jua hayo mafaniko, yatakuangamiza..Ukifanya biashara na ukafanikiwa sana, sio uthibitisho wa kwanza kwamba njia zako ni sawa mbele za Mungu.. Zaidi sana Bwana Yesu alisema, itamfaidia nini mtu akiupata ulimwengu mzima, na kisha akapata hasara ya nafsi yake?.. kumbe inawezekana mtu akaupata hata ulimwengu mzima, lakini bado akapotea!. Hivyo mafanikio sio kitu cha kwanza cha kutafuta, bali tuutafute kwanza ufalme wake na haki yake.

Na ufalme wake na haki yake ni kumwamini Yesu, na kutubu na kubatizwa na kuishi Maisha matakatifu.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

KUOTA UNA MIMBA.

Je! Daudi hakuwa mtoto wa ndoa wa Yese? (Zab 51:5)

KWANINI DAUDI ALIKUWA NI MTU ALIYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU?

Maji ya Farakano ni nini katika biblia?

Nini maana ya usimfunge ng’ombe kinywa apurapo nafaka!.(Kumbukumbu 25:4)

Rudi nyumbani

Print this post

Kiyama ni nini?

Kiyama au kiama..maana yake ni ‘siku ya ufufuko’

Neno hilo linapatikana sehemu kadha wa kadha katika biblia. Kwamfano hivi ni baadhi ya vifungu ambavyo utakatana nalo;

Mathayo 22:23-28

[23] Siku ile Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, wakamwendea, wakamwuliza,

[24]wakisema, Mwalimu, Musa alisema, Mtu akifa, akiwa hana watoto, ndugu yake na amwoe yule mkewe, ili ampatie nduguye mzao.

[25]Basi, kwetu kulikuwa na ndugu saba; wa kwanza akaoa, akafariki, na kwa kuwa hana mzao, akamwachia nduguye mke wake.

[26]Vivyo hivyo wa pili naye, na wa tatu, hata wote saba.

[27]Mwisho wa wote yule mwanamke akafa naye.

[28]Basi, katika kiyama, atakuwa mke wa yupi katika wale saba? Maana wote walikuwa naye.

Hapo ni mafarisayo  walitaka kujua kutoka kwa Yesu siku ya ufufuo wa wafu, mambo ya ndoa yatakuwaje.?

Soma pia..Wafilipi 3:10-11

[10]ili nimjue yeye, na uweza wa kufufuka kwake, na ushirika wa mateso yake, nikifananishwa na kufa kwake;

[11]ili nipate kwa njia yo yote kuifikia kiyama ya wafu.

Akimaanisha afikie siku ya ufufuko wa wafu.

Neno hilo utalisoma pia katika vifungu hivi;

2 Timotheo 2:17-18,22

[17]na neno lao litaenea kama donda-ndugu. Miongoni mwa hao wamo Himenayo na Fileto,

[18]walioikosa ile kweli, wakisema ya kwamba kiyama imekwisha kuwapo, hata kuipindua imani ya watu kadha wa kadha.

Hivyo na sisi pia hatuna budi kuyaelekeza mawazo yetu katika ufufuo wa wafu..Tumaini hilo ni lazima liwepo ndani yetu. Na ufufuo huo utakuja siku ile ya UNYAKUO ambapo parapanda italia, kisha wafu wote waliokuwa makaburini waliompokea Kristo, watafufuliwa na  moja kwa moja wataungana na sisi tuliohai kisha kwa pamoja tutapaa kumlaki Bwana Yesu mawinguni.

Swali la kujiuliza. Je, tumejipangaje kwa ajili ya siku hiyo ya kiyama? Je matendo yetu wanastahili kukubaliwa?

Majibu sote tunayo.

Tukumbuke kuwa Siku ya kiyama ipo karibuni sana.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

NA JINA LAKE AITWA, NENO LA MUNGU.

Je mtu akifa anakuwa hana dhambi tena?

Rudi nyumbani

Print this post

NA JINA LAKE AITWA, NENO LA MUNGU.

Ufunuo  19:11-13

[11]Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.

[12]Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.

 [13]Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.

Ulishawahi kujiuliza ni kwanini mahali hapo Yesu hajitambulishi kwa jina lake la asili tulilolizoea, bali anajiita Neno la Mungu,?.

Ipo maana kubwa sana nyuma yake ambayo wakristo wengi hatuijui.

Ni muhimu tufahamu kuwa pale Tunapomtaja YESU, tunamlenga Yesu wa pande mbili.

  1. Yesu kama mtu
  2. Yesu kama Neno

Wakristo wengi tunaishia kumtambua Yesu kama mtu,  jinsi alivyokuwa na mamlaka, na uweza, na maajabu, jinsi alivyosulubiwa na kuzikwa na kufufuka na kupaa juu, na sasa hivi anatawala na kumiliki viumbe vyote vya mbinguni na vya duniani ..jambo ambalo ni zuri sana, kwasababu kwa kumtambua hivyo ndivyo tunavyomwamini na kupokea wokovu na kuponywa shida zetu.

Lakini kosa ni pale tunapoishia kumtambia Yesu-mtu tu, hatutaki kumtambua Yesu kama Yesu-Neno.

Utajiuliza huyu YESU-NENO ni yupi?

Ni Yesu katika maneno yake aliyokuwa anayafundisha. Leo hii ukiweza kuyaishi maneno hayo kikamilifu 100%, basi na wewe unabadilika na kuwa Yesu, mwenyewe.

Kiasi kwamba, wakati mwingine hutahitaji Yesu aje kukusaidia, bali wewe mwenyewe utaweza kufanya, kila kitu.

Wakristo wengi tunampenda Yesu tunapomsoma au kumsikia, lakini hatutaki kuwa kama yeye. Kwasababu tunaona ugumu kuyaishi maneno yake.

Tunafanana na mwanafunzi  anayetegemea tu kikokoteo  (calculator) kupigia mahesabu yake, lakini kichwani asiwe na maarifa yoyote ya kinachofanyika nyuma ya kikokoteo kile

 lakini mtu ambaye anajua kanuni  ya kikokoteo, huyo huwa anakuwa ni bora zaidi..kwasababu hata pasipo kuwa nacho anaweza tu kupiga mahesabu yake na kupata majibu. Atakihitaji kwa kurahisisha tu kazi zake, lakini pasipo hicho bado anaweza kufanya.

Lakini hiyo itamgharimu aende  shule, ajifunze misingi yote ya hisabati..tofauti na yule mwingine ambaye kazi yake ni kubofya tu. “Jibu hilo hapo!”

Ndivyo ilivyo kwa wakristo wanaomtegemea Yesu-mtu tu, na sio Yesu-Neno. Wanamgeuza Bwana Yesu kama calculator wanamwita awasaidie, lakini hawataki kuyaishi maneno yake..

Sio kila wakati tutamwitaji Yesu atusaidie, wakati mwingine anataka sisi wenyewe tufanye, ndivyo alivyowazoeza pia mitume wake ambao hapo mwanzo walizoelea kumtegemea tu yeye ilihali hawazingatii maneno yake

Mathayo 17:17

[17]Yesu akajibu, akasema, Enyi kizazi kisichoamini, kilichopotoka, nitakaa pamoja nanyi hata lini? Nitachukuliana nanyi hata lini? Mleteni huku kwangu.

Wakati mwingine tunamwita Yesu, atusaidie, na anakaa kimya hafanyi chochote..tunaita usiku kucha hajibu lolote. Ni kwasababu gani? Ni kwasababu hatutaki kuliishi Neno lake.

Kwamfano:  mmoja anaweza akawa anafunga na kukesha kumlilia Yesu ampe  mali (kwasababu anamjua Yesu-mtu anaweza yote)..lakini huku anaendelea na mambo yake ya kidunia.. Na mwingine akalizingatia lile Neno la Yesu linalosema;

Mathayo 6:32-33

[32]Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.

[33]Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.

Huyu wa pili, anaweza asimtaje Yesu wala mali mahali popote, lakini akapokea hitaji lake, kwasababu tu kajua kanuni ya roho.. Lakini yule wa kwanza kupewa/kutokupewa ni juu ya Yesu mwenyewe..sio juu yake.

Hivyo tujifunze kuyaishi maneno ya Yesu, kwamfano tunapoambiwa tusamehe huyo ndio Yesu-Neno., tunapoambiwa tusizini ndiye Yesu Neno.

Na Yesu mwenyewe alitusisitizia kwamba  maneno yake yakiwa ndani yetu, basi tukiomba lolote yeye atatupa.

Yohana 15:7

[7]Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

“Yodi” ni nini kama tunavyoisoma katika Mathayo 5:18?

BASI MUNGU ALIMWADHIMISHA MNO.

UNAMCHUKULIA YESU KWAKO KAMA NANI?

Unyenyekevu ni nini?

MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

Mshipi wa dhahabu matitini ni nini?.

Rudi nyumbani

Print this post

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 13 (Kitabu cha Hosea).

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, libarikiwe!…karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu wetu. Neno la Mungu ni Taa iongozayo hatua za miguu yetu na Mwanga unaoongoza Njia yetu.

Huu ni mwendelezo wa ufupisho wa vitabu vya Biblia, Tumeshavitazama vitabu kadhaa nyuma, kama bado hujapitia uchambuzi huo, basi Unaweza kufanya hivyo kwa kufungua link hii>>VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1. Au ukawasiliana nasi kupitia namba zilizopo mwisho wa somo hili, au katika tovuti yetu, ili tuweze kukutumia masomo hayo kwa njia ya Whatsapp.

Vile vile ni muhimu kujua kuwa huu ni Ufupisho tu!, na muhtasari, ambao utakuwezesha kuvielewa vitabu hivi kiurahisi, hivyo baada ya kusoma ufupisho huu ni vizuri kwenda kusoma kitabu husika, ili ukajazilishe vile vichache ulivyovitapata huku. Kwa kusoma ufupisho huu pekee yake bila kushika biblia, hakuna chochote utakachonufaika nacho, Zaidi sana ni afadhali kuisoma biblia bila ufupisho wowote, kuliko kusoma hapa na kutoishika kabisa biblia.

KITABU CHA HOSEA.

Kitabu cha Hosea, kimeandikwa na Hosea Mwenyewe na maana ya jina Hosea ni “Wokovu”.. Hosea alikuwa ni Nabii wa Mungu, kama vile alivyokuwa Yeremia, Isaya au Danieli.. Kitabu cha Hosea, kinakadiriwa kuandiwa kwa muda wa miaka 40. Ndani ya muda huo Hosea alipokea mfululizo wa maono kutoka kwa Mungu na akayaandika katika kitabu hicho chenye sura/milango 14.

Nabii Hosea ni moja ya manabii watatu ambao Bwana aliyatumia Maisha yao kama Ishara… Wengine ni Nabii Isaya, ambaye kuna wakati aliambiwa atembee uchi (kuelewa zaidi kwanini aambiwe atembee uchi fungua hapa >> KWANINI NABII ISAYA ALIAGIZWA KUHUBIRI UCHI? ), na mwingine ni Ezekieli ambaye aliambiwa ale mikate iliyookwa juu ya kinyesi cha Mwanadamu, na vile vile alale kwa upande mmoja kwa siku nyingi, kuwa ishara juu ya wana wa Israeli.

Lakini Nabii Hosea yeye Mungu aliyafanya Maisha yake kuwa ishara, kwa namna nyingine, na namna hiyo ni “katika eneo la Ndoa”.. Kwa kawaida Bwana hakuwahi kuwapa watu maagizo ya kuoa watu wazinzi au makahaba. Lakini Hosea aliambiwa akaoe mwanamke “Kahaba”..Mwanamke ambaye tabia yake si kutulia na mwanaume mmoja, Ambaye hawezi kukaa na mwanaume mmoja. Huyo ndio Bwana alimpa maagizo Hosea akamwoe kwa sababu maalumu..

Lengo la kumpa maagizo hayo ni ili kuwafundisha Israeli ni kwajinsi gani wanaonekana mbele zake, kwamba mbele za Mungu wanaonekena kama Mwanamke kahaba, ambaye hatulii ni mume wake mmoja. Na Taifa la Israeli katika roho linafananishwa na mwanamke, na Mungu ni kama MUME wake.

Yeremia 31:31 “Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda.

32 Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, INGAWA NALIKUWA MUME KWAO, asema Bwana”.

Umeona hapo?.. anasema tangu siku ile aliyowatoa Misri, yeye alikuwa ni MUME KWAO, lakini walilivunja agano lake..pia Yeremia 3:14, inazungumzia jambo hilo hilo…

Yeremia 3:14 “Rudini, enyi watoto wenye kuasi, asema Bwana; maana mimi ni MUME WENU; nami nitatwaa mtu mmoja wa mji mmoja, na wawili wa jamaa moja, nami nitawaleta hata Sayuni”

Kwahiyo Kwajinsi Israeli walivyokuwa wanamwacha Mungu, kiroho ni kama walikuwa wanamsaliti MUME WAO, ambaye ni Mungu. Na matendo yote mabaya waliyokuwa wanayafanya kiroho yalitafsirika kama UASHERATI.

Kwahiyo Hosea kuambiwa vile aoe kahaba, ni kuwapa ujumbe Israeli kuwa kama vile yeye (Hosea) anavyosumbuliwa na mwanamke Kahaba, (leo yupo na yeye ndani, kesho katoroka kwenda kufanya ukahaba)…ndivyo na Israeli inavyomsumbua Mungu kwa uzinzi wa kiroho inaoufanya..

Sasa ili kuzidi kuelewa kwa undani, juu ya Agizo hili Hosea alilopewa unaweza kufungua hapa >>> Kwanini MUNGU Anampa Nabii Hosea maagizo ya Kumuoa mwanamke kahaba?

Kwahiyo baada ya Israeli yote kuona Hosea kaoa mwanamke mzinzi na tabu anazozipata kwa mwanamke huyo, na jinsi Hosea alivyowapa majibu, baadhi ya wana wa Israeli walitubu, na kumgeukia Mungu, lakini wengine walishupaza shingo.

Kitabu cha Hosea tutakigawanya katika sehemu kuu 8.

SEHEMU YA KWANZA (mlango wa kwanza na wa pili).

 Unahusu maelekezo ya Bwana kwa Hosea, juu ya kutafuta MKE WA KIKAHABA ALIYEITWA GOMERI, na kuzaa naye Watoto watatu, mtoto wa Kwanza, ambaye atakuwa wa kiume atamwita YEZREELI (Yezreeli ulikuwa ni mji ya mfalme wa Israeli, aliyeitwa Ahabu na mkewe Yezebeli).  Ndipo palipokuwa kitovu cha maasi yote ya Isreali.

Na mtoto wa pili ambaye atakuwa wa kike ataitwa Lo-ruhama, ambayo tafsiri yake ni “Asiyehurumiwa”. Na mtoto wa tatu, ambaye ni wa kiume atamwita Lo-Ami, maana yake ni “Si watu wangu”.

Kupitia Watoto hao watatu, Pamoja na Mama yao, Mungu alipitisha ujumbe mzito sana kwa Israeli yote na Yuda. (Unaweza kupitia sura hizo mbili binafsi, kwa msaada wa Roho).

SEHEMU YA PILI (mlango wa tatu).

Unahusu maelekezo ya Bwana, kwa Hosea kuhusu kuoa mwanamke mwingine wa kizinzi, lakini huyu wa sasa, anapaswa akamchukue ambaye tayari anapendwa na mtu mwingine, lengo la kufanya hivyo ni kuwaonyesha ni jinsi gani, wana wa Israeli watatwaliwa na Mfalme Nebukadreza na kukaa siku nyingi mbali na uwepo wa Mungu aliye mume wao.

Hosea 3:1 “Bwana akaniambia, Enenda tena, mpende mwanamke apendwaye na rafiki yake, naye ni mzinzi; kama vile Bwana awapendavyo wana wa Israeli, ingawa wanaigeukia miungu mingine, na kupenda mikate ya zabibu kavu.

2 Basi nikajinunulia mwanamke huyo kwa vipande kumi na vitano vya fedha, na homeri moja ya shayiri, na nusu ya homeri ya shayiri;

3 nami nilimwambia, Utatawa kwa ajili yangu siku nyingi; hutafanya mambo ya ukahaba, wala hutakuwa mke wa mtu awaye yote; nami nitakuwa hali iyo hiyo kwa ajili yako.

4 Kwa maana wana wa Israeli watakaa siku nyingi bila mfalme, wala mtu mkuu, wala sadaka, wala nguzo, wala naivera, wala kinyago;

5 baada ya hayo wana wa Israeli watarejea, na kumtafuta Bwana, Mungu wao, na Daudi, mfalme wao; nao watamwendea Bwana na wema wake kwa kicho siku za mwisho”.

SEHEMU YA 3 (mlango wa 4-5).

Bwana anatoa OLE juu ya Israeli kutokana na dhambi zao wanazozifanya.

SEHEMU YA 4 (Mlango wa wa 6).

Bwana anatoa Shauri la Toba kwa Israeli, kwamba watubu naye atawarehemu..

Hosea 1 ‘Njoni, tumrudie Bwana; maana yeye amerarua, na yeye atatuponya; yeye amepiga, na yeye atatufunga jeraha zetu.

2 Baada ya siku mbili atatufufua; siku ya tatu atatuinua, nasi tutaishi mbele zake.

3 Nasi na tujue, naam, tukaendelee kumjua Bwana; kutokea kwake ni yakini kama asubuhi; naye atatujilia kama mvua, kama mvua ya vuli iinyweshayo nchi”.

SEHEMU YA 5 (Mlango wa 7-9).

Bwana anazidi kumwonyesha Nabii Hosea, makosa ya Israeli na jinsi wanavyoyategemea Mataifa kama Misri na Ashuru katika kupata msaada, zaidi ya kumtegemea Bwana.

Hosea 7:10 ‘Na kiburi cha Israeli chamshuhudia mbele ya uso wake; ila hata hivyo hawakumrudia Bwana, Mungu wao, wala hawakumtafuta kwa ajili ya hayo yote.

11 Naye Efraimu amekuwa kama njiwa mpumbavu, asiye na fahamu; humwita Misri, huenda Ashuru.

12 Watakapokwenda nitatandika wavu wangu juu yao; nitawashusha kama ndege wa angani; nitawarudi, kama vile mkutano wao ulivyosikia.

13 Ole wao! Kwa kuwa wamenikimbia; uharibifu na uwapate! Kwa kuwa wameniasi; ingawa ninataka kuwakomboa, hata hivyo wamenena uongo juu yangu.

14 Wala hawakunililia kwa moyo, lakini wanalalamika vitandani mwao; hujikutanisha ili kupata nafaka na divai; huniasi mimi”.

SEHEMU YA 6 (Mlango wa 10).

Unabii wa Israeli kuchukuliwa mateka kwenda Ashuru.

Kumbuka Israeli ilikuja kugawanyika katika sehemu kuu 2, kaskazini na kusini, kaskazini palibaki kuitwa Israeli lakini upande wa kusini kuliitwa Yuda. Sasa huu upande wa Kaskazini ulikuja kuchukuliwa mateka mpaka Taifa la Ashuru lililopo Kaskazini..kutokana na maasi kuwa mengi, lakini kabla ya kupelekwa huko Bwana alituma manabii wengi kuwaonya watubu, waache maasi, wairudie sheria ya Mungu, na mmojawapo wa manabii hao, Bwana aliowatuma kuwaonya Israeli ni huyu Nabii Hosea!.. aliwaambia maneno haya…

Hosea 10:5 “Wakaao Samaria wataona hofu kwa ajili ya ndama za Beth-Aveni; kwa maana watu wa mji huo wataulilia, na makuhani wake walioufurahia, kwa sababu ya utukufu wake; kwa maana umetoweka.

6 NAYO ITACHUKULIWA ASHURU, IWE ZAWADI KWA MFALME YAREBU; EFRAIMU ATAPATA AIBU, NA ISRAELI ATALIONEA HAYA SHAURI LAKE MWENYEWE.

7 Katika habari za Samaria, mfalme wake amekatiliwa mbali, kama povu usoni pa maji.

8 Mahali pa Aveni palipoinuka, yaani, dhambi ya Israeli, pataharibika; mwiba na mbigili itamea juu ya madhabahu zake; nao wataiambia milima, Tusitirini; na vilima, Tuangukieni.

9 Ee Israeli, umefanya dhambi tangu siku za Gibea; huko ndiko walikosimama; ili vita vilivyokuwa juu ya wana wa uovu visiwapate katika Gibea”.

SEHEMU YA 7 (Mlango wa 11-12).

Bwana anawakumbusha Israeli Huruma zake (Jinsi alivyowahurumia kipindi wakiwa katika nchi ya utumwa ya Misri), lakini sasa wamemwacha, na hawajui kama wapo kwenye hatari.

Hosea 11:1 “Israeli alipokuwa mtoto, nalikuwa nikimpenda, nikamwita mwanangu atoke Misri”.

SEHEMU YA 8 (Mlango wa 12-14).

Bwana anazidi kuwapa shauri Israeli la kumrudia yeye kutubu, vile vile anawatahadharisha juu ya Hukumu ijayo.

Hosea 14:1 “ee israeli, MRUDIE BWANA, MUNGU WAKO; MAANA UMEANGUKA KWA SABABU YA UOVU WAKO.

2 chukueni maneno pamoja nanyi, mkamrudie bwana; mkamwambie, ondoa maovu yote, uyatakabali yaliyo mema; na hivyo ndivyo mtakavyotoa sadaka za midomo yetu kana kwamba ni ng’ombe”.

Kwa hitimisho ni kwamba kitabu cha Hosea ni kitabu cha Maonyo ya Israeli kumrudia Mungu, na kwamba, watubu..

Na sisi (watu wa Mungu) tunafananishwa na Mwanamke, tena Bibi-arusi..na Yesu Kristo ni Bwana wetu..

2Wakorintho 11:2 “Maana nawaonea wivu, WIVU WA MUNGU; KWA KUWA NALIWAPOSEA MUME MMOJA, ILI NIMLETEE KRISTO BIKIRA SAFI.

3 Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo”.

Kama Bibiarusi wa Kristo, unapofanya anasa kwa makusudi, katika roho unatafsirika kuwa unafanya uasherati mbele za Bwana, kama ni mtukanaji, mwizi, mlevi, na huku unajiita umeokoka jua kuwa unamtia Bwana wivu, kwa uasherati huo wa kiroho unaoufanya.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)

KIELELEZO CHA MWANAMKE KATIKA NYUMBA.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe;

SWALI: Je ni kweli, mpagani akioa au akiolewa na yule aliyeamini, na yeye pia anahesabiwa kuwa mkamilifu kulingana na mstari huu?

1Wakorintho 7:13 Na mwanamke, ambaye ana mume asiyeamini, na mume huyo anakubali kukaa naye, asimwache mumewe.

14 Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi; bali sasa ni watakatifu

JIBU: Ifahamike kuwa hakuna mtu anayehesabiwa mkamilifu kwa ukamilifu wa mtu mwingine. Maandiko yapo wazi katika hilo; yanasema kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe, na kila mtu atatoa Habari zake mwenyewe siku ile, mbele za Mungu (Wagalatia 6:5, Warumi 14:12).

Lakini je! Mstari huo unamaanisha kwamba ikiwa umeolewa au kuoa mtu aliyeamini, hata kama wewe ni mtenda dhambi utahesabiwa mtakatifu kwa yeye?na ukifa utaenda mbinguni? Jibu ni hapana, ukisoma vifungu vya chini yake kidogo utaelewa vizuri..Tusome..

1Wakorintho 7:12 “Lakini watu wengine nawaambia mimi, wala si Bwana, ya kwamba iwapo ndugu mmoja ana mke asiyeamini, na mke huyo anakubali kukaa naye asimwache.

13 Na mwanamke, ambaye ana mume asiyeamini, na mume huyo anakubali kukaa naye, asimwache mumewe.

14 Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi; bali sasa ni watakatifu.

15 Lakini yule asiyeamini akiondoka, na aondoke. Hapo huyo ndugu mume au ndugu mke hafungiki. Lakini Mungu ametuita katika amani.

16 KWA MAANA WAJUAJE, WEWE MWANAMKE, KAMA UTAMWOKOA MUMEO? AU WAJUAJE, WEWE MWANAMUME, KAMA UTAMWOKOA MKEO”?

Paulo anamaanisha kwamba, ikiwa wewe umeamini, na mwezi wako hajaamini, hupaswi kumuacha na kwenda kuoa/kuolewa na mwingine. Bali unapaswa kuendelea kuishi naye ikiwa tu bado yupo radhi kuwa nawe. Kwasababu kwa kufanya hivyo ni rahisi yeye kuvutwa kwenye Imani yako, ikiwa ataona mwenendo wako mzuri,.. Na kwa matokeo hayo Paulo anasema ni nani ajuaje na yeye atashawishwa kuokoka kama wewe?

Na ni kweli ukisikiliza shuhuda za ndoa nyingi zilivyomrudia Mungu, utasikia moja inakuambia Baba aliokoka baada ya mkewe kuwa mcha Mungu, au mama alimrudia Mungu baada ya mumewe kuokoka. Umeona? Lakini hilo  haimaanishi kuwa moja kwa moja ndio tayari na yeye kaokoka,kisa tu mwenzake kaokoka hata kama ataendelea kutenda dhambi, hapana.

Wanaweza wakakaa hivyo, na bado mmoja akaendelea kutokuamini hadi kifo na kuzimu akaenda. Lakini hiyo nayo hutokea mara chache, ikiwa kweli huyo mwenzi mwingine, anaishi Maisha ya haki, na ya kumpendeza Mungu, na ya kumwombea kwa bidii mwenzake.

Lakini pia ni lazima tufahamu kuwa biblia hairuhusu, mkristo kuoa/kuolewa na mtu asiyeamini. Mazingira yanayozungumziwa hapo, ni yale ambayo wokovu umemkuta tayari yupo kwenye ndoa ya namna hiyo. Leo hii kumekuwa na migogoro mingi ya kindoa, kwasababu ya maamuzi mabaya, yanayofanywa na wakristo, ambao hawazingatii maagizo ya Mungu yaliyosema tusifungwe nira Pamoja na wasioamini (2Wakorintho 6:14).

Ulinzi wa kwanza unapaswa uwe katika Imani yako, sio katika familia. Hivyo ikiwa bado hujaoa/ au hujaolewa, Imani ndio iwe ni kipimo cha kwanza cha kumtambua mwenzi sahihi. Lakini wewe ambaye tayari upo kwenye ndoa ya namna hiyo. Unalojukumu la kumvuta huyo mwenzi wako, kimatendo, kimaombi, na kimafundisho. Kwasababu huwezi jua kama atavutwa au la!.

Bwana akubariki

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NDOA NA TALAKA:

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)

NDOA NI NINI?

Je! Ni halali kuoa/kuolewa na mtu ambaye tayari anao watoto?

Nini Tofauti kati ya uzinzi na uasherati ?

JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?

NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

Rudi nyumbani

Print this post

Tofauti kati ya maandiko na Neno ni ipi?

Wapo wanatofautisha maneno haya mawili, na wapo wanayoyaona kama ni kitu kimoja..

Ni kweli Bwana Yesu alituonyesha  kuwa  “maandiko na Neno” la Mungu ni kitu kilekile  kimoja, na ndivyo ilivyo..

Soma Yohana 10:35

Ikiwa aliwaita miungu wale waliojiliwa na neno la Mungu; (na maandiko hayawezi kutanguka);

Isipokuwa  tofauti yao ndogo ni kwamba maandiko yanajifunga tu katika maandishi.. lakini Neno la Mungu, ni aidha katika maandishi au kuzungumzwa.

Bwana anaweza kutoa ujumbe wake kwa sauti kinabii, vilevile anaweza kuzungumza kwa biblia (maandiko). Na zote zikawa sauti zake zenye majibu.

Lakini tulichopewa, na tunapaswa tukitegemee sana ni Neno la Mungu katika maandiko, alisema,  “maandiko hayawezi kutanguka”, yaani kilichoandikwa kimeandikwa. Lakini Neno lake katika sauti anaweza kulitangua mwenyewe, au akaghahiri, au likawa la muda tu, tofauti na Neno katika maandishi.

Hivyo ukiishi kwa hilo, utakuwa salama. Lakini tukiwa wavivu wa kujifunza biblia. Tuwe na uhakika kuwa tunapoteza maisha yetu.

Marko 12:24

[24]Yesu akajibu, akawaambia, Je! Hampotei kwa sababu hii, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu?

Tupende Biblia zaidi ya chakula, tuone kuwa hatuwezi kuishi bila hilo; Daudi alisema.

Zaburi 119:140

[140]Neno lako limesafika sana, Kwa hiyo mtumishi wako amelipenda.

Tuyapende maandiko, kwani ndio uhai wetu.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Gombo ni nini?

Chuo cha vita vya Bwana ni kipi?(Hesabu 21:14)

Kitabu cha YASHARI kinachozungumziwa katika 2Samweli 1:17-18, ni kitabu gani?

Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?

Nini maana ya “Torati na manabii”?

Yeshuruni ni nani katika biblia?

URIMU NA THUMIMU NI NINI KATIKA BIBLIA?

Rudi nyumbani

Print this post

Ni maneno gani Bwana Yesu aliyokuwa anayaandika ardhini? (Yohana 8:7).

Jibu: Tuisome Habari nyenyewe…

Yohana 8:3 “Waandishi na Mafarisayo wakamletea mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, wakamweka katikati.

4 Wakamwambia, Mwalimu, mwanamke huyu amefumaniwa alipokuwa akizini.

5 Basi katika torati, Musa alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake namna hii; nawe wasemaje?

6 Nao wakasema neno hilo wakimjaribu, ili wapate sababu ya kumshitaki. Lakini Yesu akainama, AKAANDIKA KWA KIDOLE CHAKE KATIKA NCHI.

7 Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe.

8 Akainama tena, AKAANDIKA KWA KIDOLE CHAKE KATIKA NCHI.

9 Nao waliposikia, wakashitakiwa na dhamiri zao, wakatoka mmoja mmoja, wakianzia tangu wazee hata wa mwisho wao; akabaki Yesu peke yake, na yule mwanamke amesimama katikati.

10 Yesu akajiinua asimwone mtu ila yule mwanamke, akamwambia, Mwanamke, wako wapi wale washitaki wako? Je! Hakuna aliyekuhukumu kuwa na hatia?

11 Akamwambia, Hakuna, Bwana. Yesu akamwambia, Wala mimi sikuhukumu. Enenda zako; wala usitende dhambi tena.]”.

Katika tukio hilo maandiko, hayajasema wala kutaja ni kitu gani Bwana Yesu alichokuwa anakiandika ardhini, ikifunua kuwa SIO KITU CHA MUHIMU SANA SISI KUKIJUA, maana ingekuwa ni cha muhimu sana kukijua basi Mtume Yohana asingeacha kukiandika kwa faida yake na yetu pia, au Marko au Mathayo, wangeviandika… Lakini hakikuwa kitu cha muhimu sana kwetu kukijua…Ni sawa tutafute ni aina gani ya udongo, Bwana aliyoitengenezea tope, kwaajili ya kumponya yule kipofu.

Yohana 9:6 “Alipokwisha kusema hayo, alitema mate chini, akafanya tope kwa yale mate. Akampaka kipofu tope za macho”.

Unaona?..kujua ni aina gani ya udongo iliyotumika hapo kutengenezea tope, haitusaidii sana, vile vile kujua ni aina gani ya Mti ulitumika kumsulubisha Bwana pale msalabani, pia haitusaidii chochote, kwamba tujue ule mti ulikuwa ni Mkoko, au Mtini, au Mpingo, au Mwerezi au Mwaloni haitusaidii chochote kiroho.. Ndio maana maandiko hayaeleza aina ya mti huo.

Vile vile ni maneno gani Bwana Yesu aliyokuwa anayaandika ardhini sio jambo la muhimu kulijua.. Wengi wanasema Bwana Yesu alikuwa anaandika dhambi za wale Mafarisayo na Masadukayo ardhini, kufuatia andiko la Yeremia 17:13..

Yeremia 17:13 “Ee Bwana, tumaini la Israeli, wote wakuachao watatahayarika. WAO WATAKAOJITENGA NAMI WATAANDIKWA KATIKA MCHANGA, kwa sababu wamemwacha Bwana, kisima cha maji yaliyo hai”.

Lakini bado hoja hii haina nguvu, kwasababu Bwana Yesu angekuwa kutwa kuchwa anashinda kuandika tu dhambi za watu mchangani, kwasababu waliokuwa wanamkataa ni wengi.

Hivyo alichokuwa anakiandika sio cha Muhimu kukifaham, lakini kilicho cha muhimu kujua ni KWANINI ALIKUWA ANAANDIKA ARDHINI, WAKATI WATU WANAMWONGELESHWA!. Hicho ndio cha muhimu kujua..

Sababu kuu ya  Bwana Yesu kushuka na kuanza kuandika chini, ilikuwa ni kwa “LENGO LA KUWAPA NAFASI YA KUJITAFAKARI na YA KUCHUKUA MAAMUZI THABITI”.

Ili tuelewe vizuri, tuutafakari huu mfano mrahisi.

“Mtu Fulani unayemjua amekuja kwako kukuuliza swali la mtego, au swali ambalo anayo majibu yake..na wewe ukajua anayo majibu yake…Hivyo ukaamua kukaa kimya, usimjibu swali lile, huku ukianza kuchezea chezea shilingi iliyopo mezani, pako mbele yako, au ukaendelea kuchezea simu…Na baadaye akazidi kukuhimiza umjibu… wewe ukamjibu, jibu fupi, la kumtafakarisha..na baada ya kumjibu ukaendelea kuchezea chezea ile shilingi iliyopo mezani au ukaendelea kuchezea simu yako”.

Je kwa tukio hilo kuna lolote la kujifunza katika hiyo shilingi au hiyo simu?.. kwamba tuanze kutafuta kujua ni shilingi ngapi uliyokuwa unaichezea, au ni mizunguko mingapi uliyokuwa unaizungusha au tuanze kutafuta kujua ni nini ulikuwa unakitazama kwenye simu wakati unaongeleshwa?.

Jibu ni la!.. wewe ulikuwa unarusha rusha ile shilingi, au unachezea simu ile kwa lengo la kumpa yule mtu nafasi ya kujitafakari swali alilouliza, hali kadhalika baada ya kumjibu kwa ufupi na kuendelea kuchezea simu yako ni ili kumpa nafasi ya nafasi ya kuondoka, na kutafakari ulichomwambia.. asiendelee kukuuliza maswali ambayo anayo majibu yake. (Na kwa njama hiyo fupi, basi utafanikiwa kumwondoa huyo mtu mbele yako, bila kutumia nguvu nyingi).

Ndicho Bwana Yesu alichowafanyia Mafarisayo, lengo lake ni kuwapa muda wa kujitafakari na kuacha kuuliza maswali ambayo wanayo majibu yake, na vile vile kuondoka pale. Lakini si kuandika dhambi zao ardhini.

Hivyo hiyo ni Hekima Bwana aliyoitumia kufupisha majadiliano marefu, na hoja zisizokuwa na Msingi.

Na sisi tunachoweza kujifunza hapo ni kuwa, sio kila hoja ni za kushiriki, nyingine ni kuzikatisha kwa Hekima.. Si kila swali ni la kujibu kwa urefu, na si kila mazungumzo ni ya kuyakumbatia kwa muda mrefu. Mazungumzo ambayo ni ya mashindano ya dini, hayo Mtume Paulo kwa ufunuo wa Roho alimwonya Timotheo na makanisa yote Kristo, kwamba wajiepushe nayo..

1Timotheo 6:20 “Ee Timotheo, ilinde hiyo amana; ujiepushe na maneno yasiyo ya dini, yasiyo na maana, na mashindano ya elimu iitwayo elimu kwa uongo”

2Timotheo 2:14 “Uwakumbushe mambo hayo, ukiwaonya machoni pa Mungu, wasiwe na mashindano ya maneno, ambayo hayana faida, bali huwaharibu wasikiao”

Bwana Yesu alipopelekwa mbele ya Makuhani na mbele ya Pilato, hakuwa mtu wa maneno mengi, mara zote alipoulizwa maswali ambayo hayana maana yoyote alikaa kimya!!..

Marko 15:4 “Nao wakuu wa makuhani walikuwa wakimshitaki mambo mengi.

4 Pilato akamwuliza tena akisema, HUJIBU NENO? Tazama ni mambo mangapi wanayokushitaki!

5 Wala Yesu HAKUJIBU NENO TENA, hata Pilato akastaajabu”.

Nasi pia pia hatuna budi kuwa watu wa maneno machache na watu wa kujiepusha na mashindano, ya dini.. Umeona, kwa matendo hayo mawili tu ya Bwana kuacha kuwazungumza na wale mafarisayo na kuendelea kuandika chini, ilitosha kuwaondoa Mafarisayo wale, Zaidi hata angetumia maneno mengi, lakini kwa maneno yale machache na tendo lile moja, alivifunga vyinywa vyao.

Tito 3:9 “Lakini maswali ya upuzi ujiepushe nayo, na nasaba, na magomvi, na mashindano ya sheria. Kwa kuwa hayana faida, tena hayana maana”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Je Musa yupo anawashitaki watu..kulingana na Yohana 5:45?

Je kauli ya Bwana Yesu inajichanganya? Katika Yohana 8:14 na Yohana 5:31?

NEEMA YA MUNGU KWA MARIAMU.

Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana?

Kwanini Yakobo na Yohana waliitwa “Wana wa Ngurumo”?

Rudi nyumbani

Print this post

UNYAKUO WA KANISA UMEPITA LEO!!

“Unyakuo wa kanisa umepita leo!. Hakuna tena toba”

Je taarifa hizi zimekushtua??.

Hebu jiulize Siku taarifa hizi zitakapokuwa kweli utakuwa katika hali gani?
Mpaka sasa, unyakuo bado, haujatokea lakini siku utakapotokea utakuwa katika hali gani, utakapopewa taarifa kuwa watakatifu wamenyakuliwa na wewe umewachwa???..

Je utashtuka kama ulivyoshtushwa leo au utaona kawaida?.

Kama umeshtuka leo, hiyo ni kuonyesha kuwa wewe hupaswi kuwa wa ulimwengu, nyumbani kwako sio huku..ndio maana umeshtuka na kuogopa kusikia umeachwa!.
Rudi leo utubu kwasababu Siku hiyo pengine utaamka asubuhi na kukutana na hizo taarifa “Unyakuo umepita”..ukikumbuka kuwa masaa kadhaa tu nyuma yaliyopita, ulisikia mahubiri na ulipuuzia.

Tubu leo hii na umpokee Yesu, kwasababu ni kweli upo karibuni kutokea.

Kama leo hii utatamani kumpa Yesu maisha yako, basi piga namba hizi, tuweze kuomba pamoja na kukuongoza sala ya Toba.
0789001312.

Print this post