Title April 2022

Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana?

SWALI: Yohana alimaanisha nini aliposema..10]Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana?

Je hiyo siku ya Bwana ni ipi? Na kwanini  itajwe pale?

Ufunuo wa Yohana 1:10

[10]Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana; nikasikia sauti kuu nyuma yangu, kama sauti ya baragumu,


JIBU: Mtume Yohana alikuwa katika kisiwa cha Patmo, kwa ajili ushuhuda wa Kristo, Na kwa mara ya kwanza alipotokewa na Bwana Yesu  na kuonyeshwa mambo yanayohusiana na siri za siku za mwisho na kanisa, anasema siku hiyo aliyotokewa iliangukia  siku ya Bwana.

Swali je siku hiyo ni siku ipi?

Ikumbukwe kuwa tangu awali wakristo wa kwanza, waliifanya siku ya kwanza ya juma( Yaani jumapili) kuwa ni siku ya Bwana, kufuatana na tukio la kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo, Na ni siku ambayo Bwana alikuwa akiwatokea wanafunzi wake (Soma Marko 16:9, Yohana 20:19 ).

Vilevile Siku hii hii ndio siku ambayo kanisa lilipokea ahadi ya Roho Mtakatifu kwa mara ya kwanza..Kwahiyo watakatifu wote, tangu enzi za mitume, hadi wakati wetu huu wa sasa waliifanya siku hii kuwa ni siku ya Bwana.

Soma vifungu hivi;

Matendo ya Mitume 20:7

[7]Hata siku ya kwanza ya juma, tulipokuwa tumekutana ili kumega mkate, Paulo akawahutubu, akiazimu kusafiri siku ya pili yake, naye akafuliza maneno yake hata usiku wa manane.

1 Wakorintho 16:2

[2]Siku ya kwanza ya juma kila mtu kwenu na aweke akiba kwake, kwa kadiri ya kufanikiwa kwake; ili kwamba michango isifanyike hapo nitakapokuja;

Na ndio hapa sasa  tunaona mtume Yohana anaeleza Kwamba alipokuwa katika Roho, siku ya Bwana (yaani jumapili) ndio alitokewa na maono hayo..

Zingatia:  Mtazamo ambao siku hiyo ilikuwa ni jumamosi, si sahihi. Jumamosi, haikuwahi kuadhimishwa na wakristo wa kwanza kwa shughuli rasmi za kibada, kwa mujibu wa maandiko.

Lakini kulikuwa na umuhimu gani habari ya siku hiyo kuandikwa?

Sio kwamba Bwana anaithamini jumapili, zaidi ya siku nyingine zote, hapana au siku hiyo ni takatifu zaidi ya nyingine zote, Hapana bali anachotaka kutuonyesha ni umuhimu wa siku tunazoziweka wakfu kwa ajili yake kwamba anaziheshimu na kwamba kwa kupitia hizo, ni rahisi yeye kujifunua kwetu.

Ikiwa siku yetu kwa Bwana ni jumamosi, basi tuithamini kwa kuwa katika Roho kama vile Yohana alivyokuwa mpaka Kristo akamtembelea siku hiyo..

Kama ni jumapili, tuifanye vivyo hivyo, kama ni jumatano tuipe heshima yake. Hizi siku tusizichukulie juu juu tu,

Lakini leo hii tunapuuzia ibada kuu za kila wiki (Jumapili), tunakosa mafundisho ya biblia kanisani, au hata tukienda siku hiyo hatuwi katika roho, tunaenda ili kutimiza tu wajibu . Halafu tunataka Bwana ajidhihirishe kwetu tunapokuwa nyumbani tunaangalia tv.

Kamwe Usiruhusu, siku yako ya ibada  iliwe na uvivu au mambo ya ulimwengu huu, kama vile anasa, na mihangaiko ya dunia, hata kama upo katika mazingira ambayo hayana watakatifu..Nenda milimani huko, au maporini ukasome biblia na kuomba kama Yohana..kuliko kumwachia shetani akupangie ratiba zake kwenye siku takatifu ya Bwana..

Ithamini siku ya ibada. Na kwa hakika atajidhihirisha kwako.

Ubarikiwe.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

Dini ni nini, na Imani ya kweli ni ipi?

UFUNUO: Mlango wa 1

Nini maana ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli?

JE KANISA LITAPITIA DHIKI KUU?

JIWE LILILO HAI.

Rudi nyumbani

Print this post

JIWE LILILO HAI.

Kwa kawaida Mawe, hayaishi.. ni vitu visivyo na uhai.. Kwasababu tabia mojawapo ya viumbe hai ni kukua, na nyingine ni kuzaliana na kuwa na hisia (yaani muitikio kwa mazingira ya nje).

Lakini Mawe tunayoyaona yote hayazai.. Hakuna jiwe linaloweza kuzaa..wala mawe hayakui, yapo vilevile siku zote..kwahiyo ni vitu visivyo hai.

Lakini biblia inasema lipo Jiwe moja la kipekee ambalo LINAISHI!!.. Hilo ni tofauti na mawe mengine,  mawe mengine ni magumu lakini hayaishi, ni mazuri kimwonekano lakini hayana uhai, ni ya gharama sana, lakini hayana uzima, hayakui, hayazai, hayaongezeki. Lakini lipo jiwe moja la gharama sana, na gumu sana, na lililo hai, linalokua na kuzaa..na jiwe hilo si jingine zaidi ya YESU KRISTO.

1Petro 2:4 “Mmwendee yeye, JIWE LILILO HAI, lililokataliwa na wanadamu, bali kwa Mungu ni teule, lenye heshima”.

Jiwe hili lilianza dogo sana, katika tumbo la Bikira Mariamu.. likazidi kukua katika uweza na nguvu.  Mpaka kufikia miaka 33 na nusu, liliongezeka nguvu, na thamani baada ya kushinda mauti, na sasahivi limeunuliwa juu sana, na siku moja litarushwa kutoka juu mpaka chini duniani na kuvunja vunja falme zote za ulimwengu, na litakuwa Mlima mkubwa, na litazaa milima mingine mingi, ambayo ndiyo sisi.

Danieli 2:34 “Nawe ukatazama hata jiwe likachongwa bila kazi ya mikono, nalo jiwe hilo likaipiga sanamu miguu yake, iliyokuwa ya chuma na udongo, likaivunja vipande vipande……………………

36 Hii ndiyo ile ndoto, nasi tutaihubiri tafsiri yake mbele ya mfalme.

44 Na katika siku za wafalme hao Mungu wa mbinguni ATAUSIMAMISHA UFALME AMBAO HAUTAANGAMIZWA MILELE, wala watu wengine hawataachiwa enzi yake; bali UTAVUNJA FALME HIZI ZOTE VIPANDE VIPANDE NA KUZIHARIBU, NAO UTASIMAMA MILELE NA MILELE.

45 NA KAMA VILE ULIVYOONA YA KUWA JIWE LILICHONGWA MLIMANI bila kazi ya mikono, na ya kuwa lilivunja-vunja kile chuma, na ile shaba na ule udongo, na ile fedha, na ile dhahabu; basi Mungu aliye mkuu amemjulisha mfalme mambo yatakayokuwa baadaye; na ndoto hii ni ya hakika, na tafsiri yake ni thabiti.”.

Jiwe hilo lililo hai ni YESU KRISTO. Linaishi, ndio maana unaona hapo katika maandiko, linaonekana kukua na kuwa mlima mkubwa, na hatimaye kuzaa mawe mengine na hayo mawe kuwa milima mingine mingi… na milima hiyo ndio sisi tuliomwamini, ambao tutakaokuja kutawala pamoja naye katika utawala wa miaka elfu.

1Petro 2:5 “NINYI NANYI, KAMA MAWE YALIYO HAI, MMEJENGWA MWE NYUMBA YA ROHO, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo”

Lakini wote ambao hawatamwamini Yesu katika maisha haya, Jiwe hili litakuja kuwaponda ponda..

1Petro 2:6 “Kwa kuwa imeandikwa katika maandiko Tazama, naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule, lenye heshima, Na kila amwaminiye hatatahayarika.

7 BASI, HESHIMA HII NI KWENU NINYI MNAOAMINI. BALI KWAO WASIOAMINI, JIWE WALILOLIKATAA WAASHI, LIMEKUWA JIWE KUU LA PEMBENI.

8 TENA, JIWE LA KUJIKWAZA MGUU, NA MWAMBA WA KUANGUSHA, KWA MAANA HUJIKWAZA KWA NENO LILE,WASILIAMINI,NAO WALIWEKWA KUSUDI WAPATE HAYO”.

Litumainie hili jiwe lililo hai, mengine yote yana thamani lakini hayana uzima, Wafalme wa dunia wana thamani lakini hawana uhai, ni mawe yasiyoishi, Wakuu na wenye mamlaka ni mawe magumu kama almasi yenye thamani nyingi lakini hayana uhai…(kwasababu almasi ijapokuwa ni ya thamani kuliko mawe yote, lakini si kitu kinachoishi). Lakini Yesu ni Jiwe lililo hai, tena lenye thamani, na linaloharibu. Hilo ndilo la kulitumainia na kulitafuta.

Kama umelipata hilo, basi wewe nawe ni jiwe kama yeye Bwana Yesu alivyo, katika ulimwengu wa roho unavunja vunja  na kuponda ponda ufalme wa giza na kuharibu na kuteka nyara kila kitu. Na unao uwezo wa kuzaa mawe mengine, kwasababu nawe ni jiwe lililo hai.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Group la whatsapp Jiunge na Group letu ya whatsapp, la masomo ya kila siku kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

Naye aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika-vunjika..

CHAGUA NI JIWE LIPI LITAKALO KUFAA KWA UJENZI.

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

Je Lutu alikwenda kuwahukumu watu wa Sodoma na Gomora? Kulingana na Mwanzo 19:9?

JIWE LA KUSAGIA

Rudi nyumbani

Print this post

NIFANYE NINI ILI NIPENDWE NA MUNGU?

Ni jambo la kawaida katika familia yoyote, si Watoto wote watakuwa na mahusiano sawa na wazazi wao. Wapo ambao wataonekana kuaminiwa Zaidi ya wengine, wapo ambao watapendwa Zaidi ya wengine, pia wapo ambao watategemewa na wazazi wao kuliko wengine,  n.k. Lakini hilo haliwafanyi wale wengine wasiwe Watoto wa wazazi wao.

Inatokea hivyo, kutokana na aidha tabia zao, ujuzi  au nafasi walizonazo. Vivyo hivyo na kwa Mungu katika familia yake ya watakatifu (Waliookoka), Si watakatifu wote watakuwa vipenzi wa Mungu, si wote wataaminiwa na Mungu, na si wote watategemewa na Bwana. Lakini hayo hayawafanyi hao wengine wasiwe Watoto wa Mungu.

Leo tutatazama mambo ambayo tukiwa nayo, basi tujue tutakuwa Watoto ambao tutapendwa sana na Mungu. Hivyo Ili tufahamu hayo tutaangalia katika biblia, mifano ya watu watatu (3) ambao, walipendwa na Mungu, ili na sisi tuige tabia kama zao tupendwa na Mungu.

Tabia ya kwanza ni Upendo.

Upendo ndio tabia ya kwanza itakayokuzogeza karibu na Mungu, na upendwe sana. Kati ya mitume 12 wa Bwana Yesu, Mtume Yohana peke yake ndiye aliyependwa na Yesu sana. Mpaka akawa muda wote anaegemea kifuani pake.

Yohana 21:20 “Petro akageuka akamwona yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu anafuata; (ndiye huyo aliyeegama kifuani pake wakati wa kula chakula cha jioni, akasema, Bwana, ni nani akusalitiye?)

21 Basi Petro akamwona huyo, akamwambia Yesu, Bwana, na huyu je?

Lakini lililomfanya apendwe na Yesu, ni upendo ambao aliuiga kutoka kwake. Na ndio maana utaona injili zake zote anahimiza upendo, kwasababu Mungu mwenyewe ni Upendo. Hivyo ili na sisi tupendwe na Bwana, hatuna budi kuonyesha bidii katika kupendana,

Na tabia za upendo tunazisoma katika 1Wakorintho 13:4-8….ambazo ni hizi;

13.4 Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;

13.5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;

13.6 haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;

13.7 huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.

13.8 Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.

Tabia ya pili ni Kuwa na moyo thabiti kwa Mungu.

Maana yake, ni kuwa tayari kukataa mambo yote yanayoweza kukukosesha na Mungu bila kujali gharama/hasara gani utakayoingia kwa kutokufanya hivyo. Huo ndio uthabiti wa moyo Mungu anaoutaka. Ambao alikuwa nao Danieli, ndio uliomfanya Mungu ampende sana.

Danieli 10:11 “Akaniambia, Ee Danieli, mtu upendwaye sana, yafahamu maneno nikuambiayo, ukasimame kiwima-wima; maana kwako nimetumwa sasa. Na aliponiambia neno hili, nalisimama nikitetemeka.

Soma pia Danieli 10:19,

Unaona Danieli, alikuwa ni mtu aliyependwa sana. Hiyo yote ni kutokana na moyo wake wa msimamo, tangu alipoingia kule Babeli wakati wayahudi wote, wapo vuguvugu, akiwa bado ni kijana mdogo alipoitwa akae katika milki za mfalme hakusita kutaa vyakula najisi vya kifalme..Na hata bado akiwa mzee, walipotaka kumzuia asimwabudu Mungu wake, bado aliendelea kumwabudu kutwa mara tatu, bila kuogopwa kutupwa katika tundu la simba.

Moyo kama huo unaonyesha upendo mkamilifu kwa Mungu wake, hivyo Mungu naye angeonyesha upendo wake tu. Na ndio maana Danieli kila alipotembelewa na Malaika alianza kwa kuambiwa mtu upendwaye sana.

Vivyo hivyo na sisi, katika mambo yetu, Ikiwa boss wako/ kazi yako vinakuzuia usiwe karibu na Mungu wako kwa ule muda unaokupasa umwabudu. Ukionyesha uthabiti, kwamba ni lazima ukamtumikie Bwana wako, ukamfanyie ibada, Bwana atakupenda..Ikiwa kazini kwako wanakulazimisha uvae suruali na vimini wewe kama binti uliyeokoka, ukakataa na kusema Imani yangu hainiruhusu bila kuogopa kufukuzwa kazi, basi ujue, upo katika njia ya kupendwa na Mungu kama Danieli.

Mwisho, Tafuta kuwa na Hekima, ya kuwasaidia watu wa Mungu.

Sulemani, ni mtu mwingine ambaye biblia inatuambia alipendwa na Mungu. Tunalithibitisha hilo katika,

Nehemia 13:26 Je! Sulemani, mwana wa Daudi, hakufanya dhambi kwa kutenda hayo? Lakini katika mataifa mengi hapakuwa na mfalme mwingine mfano wake. TENA ALIPENDWA NA MUNGU WAKE, naye Mungu akamfanya mfalme juu ya Israeli; walakini wanawake wageni walimkosesha hata yeye.

Ni kwasababu gani? Ni  kwasababu yeye hakuwa kama wafalme wengine, kama Sauli, ambao akili zao zilielekea katika kutawala tu, na vita  dhidi ya maadui. Bali yeye alitamani kupata njia ya namna ya kuyatengeneza mambo kwa hekima, watu wa Mungu wafurahi katika Bwana na kumtimikia katika utulivu. Ndipo Mungu akasikia ombi lake, akampatia. (1Wafalme 3:1-15)

Ndio hapo utaona hata vile ambavyo hakuomba, kama vile Mali Mungu alimpatia, kwasababu alipendwa sana na Mungu kwa kile alichokitamani. Na kama isingekuwa yeye mwenyewe kuja kukengeuka mwishoni, basi angekuwa ni mfano mkubwa sana wa kuigwa katika biblia nzima.

Vivyo hivyo na wewe, ukiitafuta hekima, ujue unatafuta kupendwa na Mungu, na hekima ya Mungu ipo katika Neno lake. Ukiwa ni mtu wa kujifunza biblia, na sio msomaji tu, kama gazeti, Hekima hiyo itaingia yenyewe moyoni mwako (Mithali 2:10). Na Mungu atakusaidia kuwapa wengine neema hiyo. Na mwisho wa siku utapendwa na Mungu.

Hekima zote za kimaisha, za kiutumishi, za kifamilia, za kijamii, zipo katika Neno la Mungu. Hivyo hakuna namna utaweza kuishi bila kusoma biblia.

Hivyo mambo hayo matatu tukiyachanganya. Yaani UPENDO, UTHABITI WA MOYO, NA HEKIMA.

Basi tujue kupendwa na Mungu, ni lazima kutatokea tu kwetu, . Na faida yake ni kuwa, tutaonyeshwa na mambo makubwa Zaidi ya tunayoyajua. Danieli na Yohana ndio waliopewa siri za nyakati za mbeleni. Na mpaka sasa tunagemea sana nabii zao ili kutambua nyakati na majira ya siku za Mwisho. Vilevile hata na vyote tunavyovisumbukia vya mwilini, ikiwa tutapendwa na Mungu basi yeye mwenyewe atavisogeza karibu na sisi. Kama alivyofanya kwa mtumwa wake Sulemani, na Danieli.

Bwana akubariki, na nikutakie kupendwa kwema na Bwana.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Group la whatsapp Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

Na ulimi laini huvunja mfupa.(Mithali 25:15)

NITAUPATAJE UPENDO WA KI-MUNGU NDANI YANGU?

Donda-Ndugu ni nini?

MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU

Kile kinara cha Taa ndani ya Hekalu la Sulemani kilikuwa kinawakilisha nini?

Moabu ni nchi gani kwasasa?

Kigao ni nini? Na Je kinafunua nini kwa agano jipya?

Rudi nyumbani

Print this post

Gumegume ni nini? (Isaya 50:7)

Gumegume ni jamii ya miamba ambayo ni migumu sana, inapatikana huko maeneo ya mashariki ya kati sana sana  nchi ya Palestina. Zamani ilitumika katika kutengeneza vifaa, kama nyundo, mashoka, visu, majembe, ncha za mikuki na michale n.k. hiyo yote ni kwasababu ya sifa ya ugumu wake.

Neno hili limetumika sehemu kadha wa kadha katika biblia kama tunavyoweza kulisoma katika vifungu hivi;

Yoshua 5:2 “Wakati huo Bwana akamwambia Yoshua, Haya, jifanyie visu vya mawe ya gumegume, watahiri tena wana wa Israeli mara ya pili.

Ayubu 28:9 “Huunyoshea mwamba wa gumegume mkono wake; Huipindua milima hata misingi yake”.

Isaya 5:28 “Mishale yao ni mikali, na pindi zao zote zimepindika; Kwato za farasi zao zitahesabika kama gumegume; Na gurudumu zao kama kisulisuli”;

Ezekieli 3:9 “Kama almasi ilivyo ngumu kuliko gumegume, ndivyo nilivyokifanya kipaji chako; usiwaogope, wala usifadhaike kwa sababu ya nyuso zao, wajapokuwa ni nyumba ya kuasi”.

Kumbukumbu 32:13 “Alimpandisha mahali pa nchi palipoinuka, Naye akala mazao ya mashamba; Akamnyonyesha asali iliyotoka jabalini, Na mafuta yaliyotoka katika mwamba wa gumegume;”

Lakini je Neno hili/ Mwamba huu unafunua nini rohoni?

Mungu anataka na sisi tuwe na mioyo ya gumegume kwake,(yaani mioyo migumu isiyokengeuka haraka), Kama ilivyokuwa kwa mwanawe mpendwa Yesu Kristo, ambaye tunamsoma unabii wake katika Isaya 50:7, akielezewa jinsi  moyo wake ulivyokuwa mgumu kwa Bwana kama gumegume, licha ya kuwa alipitia mateso makali namna ile.

Isaya 50:5 “Bwana MUNGU amenizibua sikio langu, wala sikuwa mkaidi, wala sikurudi nyuma.

6 Naliwatolea wapigao mgongo wangu, na wang’oao ndevu mashavu yangu; sikuficha uso wangu usipate fedheha na kutemewa mate

7 Maana Bwana MUNGU atanisaidia; kwa sababu hiyo sikutahayari, KWA SABABU HIYO NIMEKAZA USO WANGU KAMA GUMEGUME, nami najua ya kuwa sitaona haya.

Umeona, Bwana Yesu, japokuwa alipitia mateso makali, lakini bado moyo wake haukugeuka nyuma. Nasi pia ndivyo Mungu anavyotaka atuone.

Mtume Paulo pia alikuwa ni mtu wa namna hii, mpaka akadhubutu kusema hakuna jambo lolote linaloweza kumtenga yeye na upendo wa Kristo.

Warumi 8:38 “Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo,

39 wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.

Swali la kujiuliza, je! Na sisi, mioyo yetu ni ya gumegume kwa Bwana? Au ya Udongo?

Je! Dhiki na mateso vitakapotujia, bado tutaweza kung’ang’ana na Bwana?

Bwana atusaidie, tuwe watu na namna hii.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Group la whatsapp Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Shinikizo ni nini?

Donda-Ndugu ni nini?

MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.

Tofauti kati ya kukana na kusaliti ni ipi?

Matulizo ya mapenzi ni nini? (Wafilipi 2:1).

Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “Saa yangu haijawadia?”

Kwanini Bwana Yesu alivikwa taji ya miiba?

Rudi nyumbani

Print this post

Donda-Ndugu ni nini?

Tusome,

2Timotheo 2:16 “Jiepushe na maneno yasiyo na maana, ambayo si ya dini; kwa kuwa wataendelea zaidi katika maovu,

17 na neno lao litaenea kama DONDA-NDUGU. Miongoni mwa hao wamo Himenayo na Fileto,

18 walioikosa ile kweli, wakisema ya kwamba kiyama imekwisha kuwapo, hata kuipindua imani ya watu kadha wa kadha”.

Donda-ndugu ni kidonda kinachotokana na damu kuacha kupita katika kiungo kimojawapo cha mwili, husuani katika vidole au katika viungo vya ndani ya mwili kama Maini, na hivyo kusababisha kusababisha kiungo hicho kitengeneza kidonda kisichopona..

Na kiungo hicho kisipoondolewa basi kidonda hicho kinasambaa mwili mzima, na kusababisha matatizo mengine makubwa zaidi.  Ugonjwa wa donda-ndugu hauna tofauti na ugonjwa wa Kansa. Na suluhisho la kutibu ugonjwa huo ni kukikata hicho kiungo.

Mtume Paulo alifananisha mafundisho ya uongo ya Himenayo na Fileto na ugonjwa huo wa Donda-Ndugu.

FILETO na HIMENAYO walianza kuwafundisha watu kuwa Kiyama kimeshapita. Hakuna tena kiyama kinachokuja mbeleni, unyakuo umeshapita zamani, na hautakuja tena..

Na kwasababu mafundisho hayo ni mafundisho hatari, maana yake yasipokataliwa na kuzuiliwa vikali ni rahisi kusambaa kwa watu wengi na kusababisha imani za watu wengi kuvurugika na watu wengi kufa kiroho.

Watu wakishaamini kuwa hakuna tena unyakuo unaokuja, kitakachofuata ni kupoa na kuendelea na dhambi na anasa, hata kama watajiita bado ni wakristo, lakini ndani yao hakuna tena tumaini lolote la maisha yanayokuja. Utaona tena Mtume Paulo, analionya kanisa la Thesalonike juu ya mambo hayo hayo..

2Thesalonike 2:1 “Basi, ndugu, tunakusihini, kwa habari ya kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, na kukusanyika kwetu mbele zake,

2 kwamba msifadhaishwe upesi hata kuiacha nia yenu, wala msisitushwe, kwa roho, wala kwa neno, wala kwa waraka unaodhaniwa kuwa ni wetu, kana kwamba siku ya Bwana imekwisha kuwapo.

3 Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu;

4 yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa; hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu.

5 Je! Hamkumbuki ya kuwa wakati nilipokuwapo pamoja nanyi naliwaambieni hayo?

6 Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake”.

Hata sasa Unyakuo bado haujatokea, lakini siku yoyote kuanzia sasa, kanisa litaondolewa, na watakatifu wakweli walioukataa ulimwengu na kujitakasa kwa Neno, watanyakuliwa juu katika utukufu, na duniani kitakachokuwa kimesalia ni dhiki kuu ya Mpinga-Kristo.

Sasa hivi kuna mafundisho mengi yamezalika ndani ya Imani ya Kikristo, wapo wanaosema kwamba hakuna unyakuo wa kanisa, wapo wanaosema kuwa unyakuo umeshapita, na sasa tupo katika utawala wa miaka elfu moja, Wengine wanaamini kuwa mamlaka ya Bwana Yesu imeshapita, sasa tupo mamlaka nyingine,  ya Mungu Baba na mafundisho mengine mengi sana…

Na mafundisho haya katika siku hizi za mwisho yameenea kama donda-ndugu kiasi kwamba hata kuwabadilisha tena watu wayarudie maandiko inakuwa ni ngumu.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Group la whatsapp Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

Je! Siku ya unyakuo watoto wachanga watanyakuliwa?

TOFAUTISHA KATI YA MAFUNDISHO YA YESU, NA YA WAANDISHI.

Je ni lazima kupitia mafundisho ya muda mrefu kabla ya kubatizwa?

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

Sadaka ya Amani ilikuwaje?

Rudi nyumbani

Print this post

Tofauti kati ya kukana na kusaliti ni ipi?

Kukana ni kitendo cha kumkataa mtu aliyekaribu nawe, kwa hofu/shinikizo Fulani pengine aidha kwa hofu ya kuaibishwa, au kudharauliwa, au kuuliwa au kutengwa, au kuchekwa n.k. Lakini kimsingi sio kwamba humpendi au huyo mtu hana thamani yoyote kwako.

Lakini kusaliti, ni jambo  baya Zaidi, kwasababu linahusisha, kumkataa mtu Fulani aliye karibu nawe kwa hiari yako mwenyewe, pasipo shinikizo lolote, kwa maslahi yako binafsi, ni kitendo cha moyo-baridi kabisa.

Kwamfano Petro alimkana Bwana, kutokana na shinikizo la hofu ya yeye kukamatwa na kwenda kupigwa kama Bwana..Lakini hapo nyuma utaona, alidhubutu kumuhakikisha kabisa Bwana kwamba hata wenzake wote wajapomkana, yeye hatofanya hivyo (Mathayo 26:33-35)

Utaona tena hata baadaya ya kutubu kwake baadaye, alipokutana na Bwana kule baharini bado alimuhakikisha mara tatu kuwa anampenda yeye..(Yohana 21:15-17). Kuonyesha kuwa ni shinikizo ndio lililompeleka kufanya vile, lakini moyo wake bado upo kwa Yesu.

Lakini Yuda tangu mwanzo alikuwa hampendi Bwana, japokuwa yeye alipendwa sana, mahali pengine mpaka Yesu akawa anampa siri zake za ndani japokuwa alikuwa mwizi, biblia inasema hivyo katika Zaburi 41:9

9 Msiri wangu tena niliyemtumaini, Aliyekula chakula changu, Ameniinulia kisigino chake.

Lakini kinyume chake akarudisha mabaya badala ya mema. Utaona yeye mwenyewe kwa hiari yake akawafuata wakuu wa makuhani bila shinikizo lolote, akawaambia mtanipa nini, nikiwapa Kristo!. Wakamuahidia Pesa. (Mathayo 26.14-16)

Usaliti unafanana na mtu ambaye yupo tayari kumuua au kumletea madhara mzazi wake, kwa faida zake mwenyewe, pengine mali, au cheo, au heshima. Bila kujali kuwa yeye ndiye aliyemnyonyesha, aliyemtunza tangu akiwa tumboni, ndiye aliyemsomesha na kumvisha n.k.

Lakini kibiblia, vyote viwili yaani “kukana na kusaliti” hatupaswi kuwa navyo kwa Bwana wetu.

Leo hii wapo watu wanaomsaliti Bwana..Ndio hawa manabii na makristo wa uongo. Ambao wanajua kabisa waliokolewa kwa thamani, walitolewa chini matopeni, lakini wanapokuzwa kidogo, wanaanza kumgeuza Kristo kuwa biashara yao. Wanaacha utumishi walioitiwa, wanatumia fursa ya Kristo, kuyashibisha matumbo yao tu… Hawa ndio wakina Yuda.

Wafilipi 3:18 “Maana wengi huenenda, ambao nimewaambieni mara nyingi habari zao, na sasa nawaambia hata kwa machozi, kuwa ni adui za msalaba wa Kristo;

19 mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, utukufu wao u katika fedheha yao, waniao mambo ya duniani”.

Lakini Wakanaji, ni wakristo wote, ambao mioyo yao haipo kikamilifu kwa Bwana..wapo nusu nusu, ndio wale wakipitia dhiki kidogo, wapo tayari kumwacha Kristo, kisa ndugu, au wazazi, au shughuli, au ujana au anasa..hali na mazingira yanawafanya wamkane Bwana wao moja kwa moja, kwa matendo yao.

Na hii ni mbaya sana Bwana Yesu mwenyewe alisema..

Mathayo10:32 “Basi, kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, nami nitamkiri mbele za Baba yangu aliye mbinguni.

33 Bali mtu ye yote atakayenikana mbele ya watu, nami nitamkana mbele za Baba yangu aliye mbinguni.

34 Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani; la! Sikuja kuleta amani, bali upanga.

35 Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu;

36 na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.

37 Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.

38 Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili.

39 Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona”.

Umeona?..Lipi bora, uchukiwe na ulimwengu leo, lakini siku ile utukuzwe na Yesu, au leo hii umkane halafu siku ile ukwane naye? Majibu yanajulikana.

Hatupaswi kuogopa kuonekana washamba kisa tumeokoka, hatupaswi kuogopa kupigwa, au kuchekwa, au kuonekana tumerukwa na akili sababu ya Yesu, mwokozi wetu. Bali tumkiri yeye kwa matendo yetu, kwasababu hata yeye mwenyewe alidharauliwa lakini akayapuuzia maradhau yao (Isaya 53:3).

Hivyo sote tujifunze kujitwika misalaba yetu tumfuate Kristo. Ufalme wa mbinguni unapatikana kwa nguvu,.

Bwana atubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Group la whatsapp Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Je! Yuda atahukumiwa na Mungu kwa dhambi yake ya usaliti?

Chapa zake Yesu ni zipi hizo?

Na ulimi laini huvunja mfupa.(Mithali 25:15)

WAPENZI, MSIIAMINI KILA ROHO.

Neno ‘Kima’ linamaanisha nini Katika biblia? (Mathayo 27:9 )

Je! Ni kanisa lipi sahihi kumuabudia Mungu?

Matulizo ya mapenzi ni nini? (Wafilipi 2:1).

Rudi nyumbani

Print this post

Matulizo ya mapenzi ni nini? (Wafilipi 2:1).

Jibu: Tusome,

Wafilipi 2:1 “Basi ikiwako faraja yo yote katika Kristo, yakiwako MATULIZO YO YOTE YA MAPENZI, ukiwako ushirika wo wote wa Roho, ikiwako huruma yo yote na rehema,

2 ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkinia mamoja”.

Mapenzi yanayozungumziwa hapo ni ule Upendo wa Kristo kwetu, Matulizo ya mapenzi yanayonenwa  hapo sio matulizo ya mapenzi ya mwili, bali ni Matulizo ya mapenzi ya KRISTO, (Yaani ile hali ya kupata pumziko ndani ya Pendo la Kristo).

Tunapomfahamu Yesu, na jisni anavyotupenda kwa kiwango anachotaka yeye tumfahamu….basi tunapata pumziko kubwa sana na utulivu mkubwa sana ndani ya roho zetu… (roho zetu zinatulia na kuwa na amani).

Biblia (Neno la Mungu) linasema..

Warumi 8:38 “Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo,

39 wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Ukishajua kuwa hakuna Malaika yoyote anayeweza kumfanya Kristo akaacha kukupenda wewe baada ya kumuamini, ni lazima utapata Pumziko na utulivu ndani yako.

Ukishajua kuwa hakuna mwenye mamlaka yoyote duniani, awe kiongozi wa nchi au dunia, ambaye anaweza kumfanya Kristo akaacha kukupenda wewe, basi unapata utulivu ndani yako.

Ukishajua kuwa hakuna kiumbe chochote kilichopo duniani, au chini ya dunia..kitakachoweza kumfanya Kristo akakuchukia basi unapata Pumziko na utulivu usio wa kawaida. Unakuwa huangaiki tena..

Unapojua kuwa siku ile ulipomwamini Kristo, tayari dhambi zako zilifutwa, katika ulimwengu wa roho ulihamishwa kutoka katika nguvu za giza na kuingizwa katika Pendo hilo la Kristo.. basi unapata amani, utulivu na pumziko ndani yako.

Sasa pumziko hilo, na utulivu huo unaoupata kutokana na upendo wa Kristo kwako, ndio unaoitwa MATULIZO YA MAPENZI.

Nabii Isaya alilion Pendo la Yesu miaka mingi sana kabla ya kuja kwake, aliona Yerusalemu inakwenda kufarijiwa, mapigo yake ambayo Bwana alimwadhibu kutokana na dhambi zake, yanakwenda kuponywa, hofu yake inakwenda kuondolewa na Masihi ambaye atakuja.(na Yerusalemu itapokea Matulizo makubwa)..

Isaya 40:1 “Watulizeni mioyo, watulizeni mioyo, watu wangu, asema Mungu wenu.

2 Semeni na moyo wa Yerusalemu, kauambieni kwa sauti kuu ya kwamba vita vyake vimekwisha, uovu wake umeachiliwa; kwa kuwa amepokea kwa mkono wa Bwana adhabu maradufu kwa dhambi zake zote”.

Je Umeyapata Matulizo ya Mapenzi leo?. Umetulizwa na Bwana Yesu, au unataabishwa na shetani?.

Kama hujampokea Yesu, basi huna utulivu ndani yako..wachawi watakusumbua, mapepo yatakusumbua, na vile vile hofu ya mauti itakusumbua. Hivyo mpokee Yesu leo, upate pumziko ndani yako.

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami NITAWAPUMZISHA.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; NANYI MTAPATA RAHA NAFSINI MWENU;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Group la whatsapp Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

MAPENZI YA MUNGU NI YAPI?

JINSI YA KUMSIKIA MUNGU, NA KUPOKEA MAFUNUO AU JUMBE KUTOKA KWAKE.

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI:

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

Furaha ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

TOFAUTI YA MITUME, MANABII, WAINJILISTI, WACHUNGAJI NA WAALIMU NI IPI?

Huduma hizi 5 tunazisoma katika kitabu cha Waefeso..

Waefeso 4:11 “Naye alitoa wengine kuwa MITUME, na wengine kuwa MANABII; na wengine kuwa WAINJILISTI na wengine kuwa WACHUNGAJI na WAALIMU”.

Na madhumuni ya Bwana Yesu kuziweka huduma hizi tano (5), kama huduma za Uongozi katika kanisa ni kama mstari wa 12, unavyosema..

Tusome tena..

Wafeso 4:11 “naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu;

12 kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa kristo ujengwe”.

Kumbe lengo la kwanza ni “KUWAKAMILISHA WATAKATIFU”, na pili ni “KAZI YA HUDUMA ITENDEKE”, na tatu “MWILI WA KRISTO UJENGWE”.  Na sio ili Kuwaharibu watakatifu, au kujitafutia utajiri, au Umaarufu.

Mtu yeyote anayejiita mtumishi wa Mungu, kama hayo Maono matatu hayapo ndani yake, basi ni mtumishi wa shetani!

Sasa tuangalie kwa ufupi kazi za Hizi huduma tano.. Zinashirikianaje kuujenga mwili wakristo, na kuwakamilisha watakatifu.

 1. MITUME

Mitume kama jina lake lilivyo “ni watu waliotumwa”.. na kama wametumwa maana yake kuna aliyewatuma, na aliyewatuma ni lazima kawapa ujumbe.

Kwahiyo wahasisi wa Imani ya kikristo wa kwanza kabisa ni Mitume, Na mitume hao ni wale 11 pamoja na Mathiya wa 12. Hao ndio waliotumwa wa kwanza, kuitangaza Imani ya kikristo, kwa watu wote.

Lakini bado hao pekee wasingetosha kuitangaza Imani duniani kote, Hivyo Bwana Yesu alinyanyua Mitume wengine tofuati na hao 12, ambao ndani yake ndio akina Paulo na wengineo.

Hawa waliipeleka Imani ya kikristo duniani kote.

Na sio tu kulipeleka Neno la Mungu bali pia, kupanda Makanisa. Ndio maana utaona Mtume Paulo alipanda makanisa mengi sana, maeneno ya Galatia na Makedonia.

Na hata sasa Bwana anao mitume wake ambao anawatuma kuitangaza Imani ya kikristo mahali ambapo  haijasikiwa kabisa, na vile vile kupanda makanisa ya Kristo, na si makanisa yao wenyewe.

 2. MANABII

Manabii ni kundi lingine la watu ambalo Bwana anawaweka ndani ya Kanisa. Hawa kazi yao ni kulijenga kanisa kwa kutoa jumbe za Faraja na maonyo kutoka kwa Mungu moja kwa moja, na jumbe hizo ni kwaajili ya kulifariji kanisa na kulionya kwa mambo yanayoendelea au yanayokuja.

Kwamfano katika biblia, agano jipya tunamwona Nabii mmoja aliyeitwa Agabo, ambaye Bwana alikuwa anazungumza naye na kumpa jumbe za kulionya kanisa juu ya mambo yanayokuja..

Matendo 11:27 “Siku zizo hizo manabii walitelemka kutoka Yerusalemu hata Antiokia.

28 Na tulipokusanyika akasimama mmoja wao, jina lake Agabo, akaonyesha kwa uweza wa Roho Mtakatifu kwamba njaa kubwa itakuja karibu katika dunia nzima, nayo ikatukia katika siku za Klaudio.

29 Na wale wanafunzi, kila mtu kwa kadiri ya alivyofanikiwa, wakaazimu kupeleka msaada kwa ndugu zao waliokaa Uyahudi.

30 Wakafanya hivyo, wakawapelekea wazee kwa mikono ya Barnaba na Sauli”.

Umeona hapo?.. Manabii kazi yao ilikuwa ni kutoa taarifa za mambo yajayo na kuyaambia makanisa, kwa faida ya kanisa.. na kwa kujitakia umaarufu wao, wala kutaka fedha kutoka kwa watu.

Hapo taarifa za unabii huo, zilipofika kwa makanisa yote, ndipo kila mtu akajiandaa kwa akiba ya kutosha.. Huoni hapo kanisa limejengeka?..lakini leo kuna manabii ambao hawaoni mambo yanayokuja lakini wanaona mifuko na pochi za watu. Na Zaidi ya yote hawawafundishi watu utakatifu bali mafanikio tu! (hawa ndio manabii wa uongo waliotabiriwa kuja katika siku za mwisho).

Lakini Pamoja na kuwepo na jopo kubwa la manabii wa uongo, wapo pia manabii wa kweli, kwasababu Roho Mtakatifu wa kweli bado yupo duniani na anatenda kazi.

 3. WAINJILISTI.

Wainjilisti ni kundi lingine Bwana aliloliweka katika kanisa kwa lengo la kuwavuta watu katika Imani ya Kikristo, likitumia maandiko kumthibitisha Yesu Kristo ni Njia, kweli na Uzima. Vyombo hivi Bwana kaviweka maalumu kuvunja mapando ambayo yamepandwa na adui shetani ndani ya vichwa vya watu kuhusu Ukristo. Hivyo kupitia wainjilisti, watu wengi ambao, hawakuuelewa vizuri ukristo, au wamefundishwa isivyopaswa kuhusu Yesu, wanafunguka.

Mfano wa Wainjilisti katika biblia ni mtu mmoja aliyeitwa Apolo. Huyu alivunja misingi ya elimu za giza zilizokuwa zimepandwa ndani ya vichwa vya watu..

Matendo 18:23 “Hata akiisha kukaa huko siku kadha wa kadha akaondoka, akapita kati ya nchi ya Galatia na Frigia, mji kwa mji, akiwathibitisha wanafunzi.

24 Basi Myahudi mmoja, JINA LAKE APOLO, mzalia wa Iskanderia, MTU WA ELIMU, akafika Efeso; NAYE ALIKUWA HODARI KATIKA MAANDIKO.

25 Mtu huyo alikuwa amefundishwa njia ya Bwana; NA KWA KUWA ROHO YAKE ILIKUWA IKIMWAKA, alianza kunena na kufundisha kwa usahihi habari za Yesu; naye alijua ubatizo wa Yohana tu.

26 Akaanza kunena kwa ujasiri katika sinagogi; hata Prisila na Akila walipomsikia wakamchukua kwao, wakamweleza njia ya Bwana kwa usahihi zaidi.

27 Na alipotaka kuvuka bahari aende mpaka Akaya, ndugu wakamhimiza, wakawaandikia wale wanafunzi wamkaribishe, naye alipofika akawasaidia sana wale waliokwisha kuamini kwa neema ya Mungu.

28 Kwa maana aliwashinda Wayahudi kabisa kabisa mbele ya watu wote, akionyesha kwa maneno ya maandiko ya kuwa Yesu ni Kristo”.

Na tabia ya Wainjilisti ni kutokukaa sehemu moja, kwasababu Bwana ameweka ndani yao, roho ya kuhubiri, kama Apolo.

Na Wainjilisti wa kweli si wapenda fedha, wala wanaopenda umaarufu wala fasheni za kidunia. Wainjilisti wa kweli, ni wale wanaougua wanapoona watu wanafundishwa vitu visivyo sahihi kimaandiko kama Apolo.

 4. WACHUNGAJI

Wachungaji ni kundi lingine ambalo Bwana ameliweka ndani ya kanisa, kwa lengo la kulichunga kundi (kanisa). Baada ya mtu kuamini kutokana na injili ya mitume au wainjilisti, hana budi kukaa katika ushirika wa kanisa. Na atakapokuwa katika kanisa hana budi kuchungwa kama vile kondoo.

Sifa za wachungaji wa kweli ni zile zile za Uaskofu zinazotajwa katika kitabu cha 1Timotheo  3:1-7, kwamba asiwe mtu wa kupenda fedha, asiyekuwa mlevi,mwenye kuitunza nyumba yake vyema, na mwenye ushuhuda mzuri katikati ya watu.

Katika enzi za kanisa la kwanza wachungaji wa ukweli walikuwa ni wengi kuliko wa uongo, lakini katika siku hizi za mwisho, wachungaji wa uongo ni wengi kuliko wa ukweli, na hiyo yote ni kwasababu tunaishi katika siku za mwisho sawasawa na unabii, na siku yoyote Parapanda inalia.

 5. WAALIMU

Hili pia ni kundi lingine Bwana Yesu aliloliweka ndani ya kanisa. Lengo kuwepo  Waalimu ni kulifundisha Neno la Mungu, kwa watu walio makanisani. Waalimu wanakuwa na uwezo wa kufundisha, na kumfanya mtu aelewe, kama tu walimu wa elimu za kidunia walivyo. Lengo ni ili wakristo wajae ambayo Bwana anayahitaji..

Na siku hizi za mwisho waalimu wa uongo ni wengi, kuliko wa kweli. Kwasababu ile ile ya kuwa tunaishi katika siku za mwisho. Sifa kuu ya Waalimu wa Uongo ni kuhubiri mambo ya ulimwengu huu na kupenda fedha na mambo ya kiulimwengu.

Kwa hitimisho ni kuwa Roho Mtakatifu yupo mpaka sasa, na Mitume wa ukweli, Manabii wa ukweli, Wainjilisti wa ukweli, Wachungaji wa ukweli na Waalimu wa Ukweli, mpaka leo Bwana amewaweka katika makanisa yake.

Na pia karama huduma hizi zinaingiliana, kuna Mtu anaweza kuwa Mtume na pia akawa Mwinjilisti, hali kadhalika mwingine anaweza kuwa Mchungaji na akawa Mwalimu pia, na mwingine anaweza kuwa Mtume na kuwa mwalimu kama Mtume Paulo (1Timotheo 2:7), ndio maana utaona Mtupe Paulo, katoa mafundisho mengi sana katika nyaraka zake..na kwasababu alikuwa Mtume na hapo hapo Mwalimu.

Lakini kamwe hatupaswi kujisifia karama wala huduma tulizonazo, kwasababu Roho Mtakatifu hajavitoa vipawa hivyo kwa lengo la kutufanya sisi tuwe maarufu, au tuonekane wa tofauti..bali kwa lengo la kulijenga kanisa, na kuwakamilisha watakatifu.

Hekima ya Mungu ni kuu, sana. Na Bwana ni mzuri sana. Je! Umempokea Bwana Yesu, na kubatizwa? Na kupokea Roho Mtakatifu? Kama bado unasubiri nini?..kumbuka hizi ni siku za mwisho, na Yesu yupo mlangoni kurudi.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “Torati na manabii”?

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

Nini maana ya “Roho za manabii huwatii manabii?

AKAZIDI KUENDELEA KATIKA HEKIMA NA KIMO.

Nini maana ya “Torati na manabii”?

Rudi nyumbani

Print this post

Kusemethi ni nini katika biblia?

Kusemethi au kusemethu ni nafaka inayokaribia kufanana sana na Ngano kimwonekano na kiladha. Nafaka hii ni familia moja na nafaka ya Ngano.

Miaka ya zamani kabla ya Kristo, nafaka ya Kusemethi ndiyo iliyokuwa inatumika kama nafaka kuu ya kutengenezea mikate, Zaidi hata ya Ngano, lakini baada ya Kristo, Nafaka ya Ngano, ilianza kukubalika Zaidi duniani kote na kupata nguvu duniani kuliko Kusemethi. Kiasi kwamba mpaka kufikia leo hii ukitaja nafaka ya Kusemethi hakuna hata mtu anayeijua.

Ngano leo imepata nguvu kuliko Kusemethi, kama vile mafuta ya Alizeti, yalivyo na nguvu kuliko mafuta ya Mawese. Lakini Pamoja na hayo bado yapo maeneo machache ya dunia (Sehemu za Ulaya), wanalima Kusemethi na kuitumia kutengenezea mikate na vyakula vingine.

Katika biblia tunaona nafaka hii ikitajwa mara kadhaa, sehemu ya kwanza tunaona ikitajwa kipindi wana wa Israeli, wanaondolewa Misri na Bwana.

Kutoka 9:29 “Musa akamwambia, Mara nitakapotoka mjini nitamwinulia Bwana mikono yangu; na hizo ngurumo zitakoma, wala haitanyesha mvua ya mawe tena; ili upate kujua ya kuwa dunia hii ni ya Bwana.

30 Lakini, wewe na watumishi wako, najua ya kuwa ninyi hamtamcha Bwana Mungu bado.

31 Kitani na shayiri zilipigwa; maana shayiri zilikuwa na masuke na kitani zilikuwa katika kutoa maua.

32 Lakini ngano na KUSEMETHU hazikupigwa; maana, zilikuwa hazijakua bado”

Vile vile tunaona ikitajwa katika kitabu cha Ezekieli.

Ezekieli 4:9 “Pia ujipatie ngano, na shayiri, na kunde, na dengu, na mtama, na KUSEMETHI, ukavitie vyote katika chombo kimoja, ukajifanyie mkate kwa vitu hivyo; kwa kadiri ya hesabu ya siku utakazolala ubavuni mwako; yaani, siku mia tatu na tisini utaula”.

Unaweza kusoma pia Isaya 28:23, utaona nafaka hiyo ikitajwa..

Kama kuna baadhi ya Mazao na vyakula vilivyokuwa vinakubalika zamani za kale, lakini leo hii vinaonekana havina thamani yoyote..vile vile vitu vingine vyote siku moja vitapita na kuwa si kitu, lakini wamtumainio Bwana watadumu milele.

1Yohana 2:17 “Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, BALI YEYE AFANYAYE MAPENZI YA MUNGU ADUMU HATA MILELE”.

Zaburi 125:1 “Wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, Ambao hautatikisika, wakaa milele.

2 Kama milima inavyouzunguka Yerusalemu, NDIVYO BWANA ANAVYOWAZUNGUKA WATU WAKE, TANGU SASA NA HATA MILELE”.

Je na wewe unamtumainia Bwana? Au ulimwengu?..

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Nini maana ya usimfunge ng’ombe kinywa apurapo nafaka!.(Kumbukumbu 25:4)

Masuke ni nini? (Luka 6:1, Marko 4:28)

Uga ni nini? Na kazi yake ni ipi kibiblia?

Bisi ni nini? (Walawi 23:14, Ruthu 2:14)

YEYE ALIYEUWASHA HUO MOTO LAZIMA ATALIPA.

Rudi nyumbani

Print this post

Ijumaa kuu ni nini? Na kwanini iitwe kuu?

Ijumaa kuu ni ijumaa ya mwisho kabisa ya Bwana wetu Yesu Kristo kuwepo hapa duniani, ni siku ile ambayo alipitia mateso mengi, na kusulibiwa, na kufa na kisha kuzikwa. Siku hii huadhimishwa na wakristo wengi ulimwengu, kama kukumbuka la mateso ya Bwana wetu Yesu Kristo kila mwaka.

Kwanini iitwe ijumaa kuu?

Lakini swali ni kwanini iitwe ijumaa kuu na sio ijumaa ya mateso au ya huzuni? Kwanini iwe kuu? Wakati siku hiyo ilikuwa ni siku mbaya sana ya mamlaka ya giza, ya huzuni na masumbufu ya Yesu mwokozi wetu?

Ni kweli kwa jicho la nje! Ni siku isiyo nzuri, lakini kwa jicho la Roho ni siku ya furaha sana tena sana kwetu sisi wanadamu, Kwani ni siku ambayo kwa mara ya kwanza tulifutiwa mashtaka yetu ya hukumu, tangu tulipopoteza uzima pale Edeni. Kwani asingekufa Yesu, tusingepata msamaha wa dhambi.. Hivyo kifo chake, kilileta ukombozi mkuu sana kwetu, na matokeo yake hatupaswi kulia, kinyume chake tufurahie, kwani siku kama ya leo, karibia miaka 2000 iliyopita, tuliwekwa huru…Hivyo ni sahihi kuitwa ijumaa kuu na sio ijumaa ya mateso.

Ni sawa na mfano wa Samaki anayevuliwa, yeye kwa upande wakw kweli atapitia mateso ya kufa, lakini yule anayemvua atafurahia kupata kitoweo. Hivyo tunaweza kusema ni uchungu kwa Samaki lakini furaha kwa mvuvi..

Kifo cha Bwana wetu Yesu kilikuwa ni faida kubwa kwetu, kwasababu kama damu yake isingemwagika, tusingepata ondoleo la dhambi zetu (Waebrania 9:22).

Na je! kuna agizo lolote la kutokula nyama siku hii ya ijumaa kuu?

Jibu ni La, desturi ya kutokula nyama (ya wanyama-damu moto), ni pokeo tu la kanisa katoliki, ambao kwa mujibu wao, wanafanya hivyo kwa heshima ya Kristo, kuutoa mwili wake, kama sadaka kwetu, kwasababu nyama ni chakula cha starehe, hawafanyi hivyo ili kuyatafakari mateso ya Bwana, na sio tu katika siku ya ijumaa kuu, bali  pia siku ya jumatano ya majivu, pamoja na ijumaa nyingine zote, zinazofuata katika mfungo  hawali nyama .

Lakini agizo hilo halipo mahali popote katika maandiko. Kama ukila haufanyi makosa, au usipokula vilevile haufanya makosa.

Lakini swali lingine ni je! Kuadhimisha sikukuu hii ni dhambi?

Jibu ni la!, Biblia haijatupa agizo wala katazo la mtu kuiadhimishi siku Fulani kwa Mungu wake.

 Ni kwa jinsi yeye anavyoamini tu!.

Warumi 14:5 “Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku, mwingine aona siku zote kuwa sawasawa. Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe.

6 Yeye aadhimishaye siku, huiadhimisha kwa Bwana; naye alaye, hula kwa Bwana, kwa maana amshukuru Mungu; tena asiyekula, hali kwa Bwana, naye pia amshukuru Mungu”.

Hivyo ikiwa wewe hauoni kama siku ya ijumaa kuu inafaida yoyote kwako, basi usimuhukumu yule ambaye anaiadhimisha kwa Mungu wake, lakini pia wewe ambaye unaidhimisha usimuhukumu yule ambaye haiadhimishi. . Ikiwa unaona mfungo huo kwa kipindi hicho cha pasaka hauna maana kwako, hufanyi kosa, lakini pia usimuhukumu yule ambaye anafunga kwa ajili ya Bwana wake aliyemfia msalaba.Ndivyo ilivyo

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Easter ni nini?. Na je tunaruhusiwa kuisheherekea?

PASAKA NI NINI? NA JE TUNARUHUSIWA KUSHEHEREKEA PASAKA?

Je! kuna sikukuu za pasaka mbili? (Hesabu 9:11)

SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?

Mwandamo wa mwezi/Mwezi mpya Ni nini kibiblia?

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

KRISIMASI (CHRISTMAS) NI NINI? JE IPO KATIKA BIBLIA?

Panda/ Sauti ya panda ni nini kibiblia?(Danieli 3:5)

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

Rudi nyumbani

Print this post