Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

Jibu: Yakobo 3:1  “Ndugu zangu, msiwe waalimu wengi, mkijua ya kuwa mtapata hukumu kubwa zaidi”.

Sentensi hiyo ili ieleweke vizuri ni sawa na kusema “pasiwepo na waalimu wengi katikati yenu”.

Maneno hayo aliyazungumza Yakobo kwa uongozo wa Roho, kuifunua tabia inayoendelea katika kanisa leo . Pale ambapo kanisani kila mtu ni Mjuaji..(hakuna utaratibu). Jambo ambalo ni hatari sana…Kwasababu kanisa linaongozwa na karama za Roho.. Haiwezekani wote tukawa na karama moja, haiwezekani wote tukawa wainjilisti, au wote tukawa waalimu au wote wachungaji au wote manabii.

Lakini inapotokea ndani ya kanisa kila mtu ni mchungaji, au kila mtu ni mwalimu..Kitakachozalika hapo ni roho ya machafuko. Kwasababu mmoja labda karama yake ni matendo ya Miujiza, lakini atataka asimame na yeye afundishe na kuongoza na yeye kama mchungaji, mwisho wa siku kitakachozaliwa hapo ni machafuko, kwasababu vitafundishwa vitu ambavyo vingine hata havipo kwenye Neno, na kupata hatia ya kuliongeza au kulipunguza Neno la Mungu. Na hivyo kujitafutia hukumu.

Ufunuo 22:18  “Namshuhudia kila mtu ayasikiaye maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mtu ye yote akiyaongeza, Mungu atamwongezea hayo mapigo yaliyoandikwa katika kitabu hiki.

19  Na mtu ye yote akiondoa lo lote katika maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mungu atamwondolea sehemu yake katika ule mti wa uzima, na katika ule mji mtakatifu, ambao habari zake zimeandikwa katika kitabu hiki”.

Hivyo hilo ni neno la kutuonya na kutukumbusha na kututahadharisha tukae katika nafasi zetu, kila mmoja aliyoitiwa,  kama ni Mwalimu, mwalimu, kama ni mchungaji mchungaji, kama ni muinjilisti, muinjilisti n.k Sio umepewa karama ya uimbaji na wewe unatafuta kuwa mwalimu, Utajitafutia hukumu.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

USINIE MAKUU.

JE NI LAZIMA KUBADILISHA JINA BAADA YA KUOKOKA?

JE UPENDO WAKO UMEPOA?

BABA YANGU ANATENDA KAZI HATA SASA!.

Je! ni halali kwa mtu wa Mungu kutumia njia za uzazi wa mpango,ikiwamo mipira?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
JUMA R. MAFUMBA
JUMA R. MAFUMBA
10 months ago

Mwenyezi Mungu ni mwenye nguvu hivo tumtumaini yeye make ndo uzima wa milele