Category Archive Vijana

KAMA WEWE NI KIJANA, BASI FAHAMU YAFUATAYO NA UCHUKUE TAHADHARI!

Ikiwa wewe ni kijana basi fahamu basi fahamu mambo yafuatayo.

1.MAWAZO MABAYA YANAANZIA UJANANI.

Mwanzo 8:21 “Bwana akasikia harufu ya kumridhisha; Bwana akasema moyoni, Sitailaani nchi tena baada ya hayo kwa sababu ya wanadamu, MAANA MAWAZO YA MOYO WA MWANADAMU NI MABAYA TANGU UJANA WAKE; wala sitapiga tena baada ya hayo kila kilicho hai kama nilivyofanya”.

Mawazo ya kuidharau injili, mawazo ya ukaidi wa moyo na kiburi cha uzima yanaanzia ujanani.

Yeremia 22: 21 “Mimi nalisema nawe wakati wa kufanikiwa kwako; lakini ulisema, Sitaki kusikia. Hii ndiyo iliyokuwa desturi yako TANGU UJANA WAKO, KUTOKUITII SAUTI YANGU”.

   2. MUNGU ANATAFUTWA UJANANI NA SI UZEENI!.

Mhubiri 12: 1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo”.

Maana yake katika uzee “haitawezekana kabisa” kumtafuta Mungu kama utapuuzia wito wa Mungu katika ujana wako!!!. Wakati wa Ujana ndio wakati wa kujifunga NIRA YA MUNGU iliyotajwa na BWANA YESU katika Mathayo 11:29.

Maombolezo 3:27 “Ni vema mwanadamu aichukue NIRA WAKATI WA UJANA WAKE.

28 Na akae peke yake na kunyamaza kimya; Kwa sababu Bwana ameweka hayo juu yake”.

   3. KAMA UTACHAGUA ANASA, BASI FAHAMU KUWA SIKU YA MWISHO UTASIMAMA HUKUMUNI.

Mhubiri 11:9 “Wewe kijana, uufurahie ujana wako, na moyo wako ukuchangamshe siku za ujana wako, ukaziendee njia za moyo wako, na katika maono ya macho yako, lakini ujue wewe ya KWAMBA KWA AJILI YA HAYO YOTE MUNGU ATAKULETA HUKUMUNI”

Maana yake kama utachagua uzinzi katika ujana wako, au ulevi, au anasa nyingine yeyote basi pia jiweke tayari kusimama mbele ya kiti cha hukumu siku ile ya mwisho, ambapo maandiko yanasema kila mtu atatoa habari zake mwenyewe (Warumi 14:12), na tena kila neno la upuuzi litatolewa hesabu yake siku ile ya hukumu (Mathayo 12:36).

  4. NEEMA YA WOKOVU HAIKUBEMBELEZI.

Ufunuo 22:10 “ Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.

11  MWENYE KUDHULUMU NA AZIDI KUDHULUMU; NA MWENYE UCHAFU NA AZIDI KUWA MCHAFU; NA MWENYE HAKI NA AZIDI KUFANYA HAKI; NA MTAKATIFU NA AZIDI KUTAKASWA”.

Ikiwa umechagua uchafu!, basi usiufanye kidogo!..ufanya sana, lakini kama umechagua USAFI, basi JITAKASE SANA, usiwe hapo katikati (vuguvugu!)..

   5. UTAKAPOKUWA MZEE UTAPELEKWA USIKOTAKA.

Yohana 21:18  “Akasema, Amin, amin, nakuambia, Wakati ulipokuwa kijana, ulikuwa ukijifunga mwenyewe na kwenda utakako; lakini utakapokuwa mzee, utainyosha mikono yako, na mwingine atakufunga na kukuchukua usikotaka”.

Uhuru ulionao si wa Daima, ipo siku utaisha, na wengine watakuwa na mamlaka juu yako…….

Je wewe kama kijana sasa umejipangaje?..je unawaza nini katika ujana wako huu? au unafikiri nini?…Kwanini usiamua kumgeukia Muumba wako leo!, na kuachana na udunia, na tamaa za ujanani, ambazo hazina faida yoyote Zaidi sana zina hasara nyingi?

2Timotheo 2:22 “Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi”.

Bwana Yesu akubariki.

Ikiwa unahitaji msaada wa kuokoka na ubatizo basi wasiliana nasi kwa namba zetu tajwa hapo chini.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.

Je! Mke wa ujana wako ni yupi kibiblia?

ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

Nini tofauti ya Majira na Wakati?

Rudi nyumbani

Print this post

EPUKA MAKUNDI ILI UTAKATIFU WAKO UDUMU!.

Silaha moja shetani anayoitumia kuharibu maisha ya kiroho ya watu wengi, hususani vijana ni MAKUNDI!..

Na mtu mkamilifu ni Yule anayeweza kuchagua aina ya watu wa kutembea naye. Biblia inatufundisha kuwapenda watu wote, lakini si kuambatana na watu wote.

2Wakorintho  6:14  “Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani KATI YA HAKI NA UASI? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?”

Umeona?..maana yake ni kwamba kama unaambatana na mtu ambaye si wa aina yako, basi unajiharibu mwenyewe!, Baada tu ya kumkiri Yesu, jambo lingine la muhimu linalopasa kufuata ni KUCHAGUA AINA YA WATU, utakaoanza kuwa nao karibu, kuanzia huo wakati na kuendelea.

Wengi wanalikwepa hili na mwisho wa siku wanajikuta wameurudia ulimwengu tena kwa kasi kubwa.. Ndugu ukishaokoka yale makundi ya walevi uliyokuwa unashinda nayo, ni sharti uyaache!, ukishaokoka zile saluni ulizokuwa unaenda ambazo kutwa kuchwa ni kuzungumzia mambo ya watu wengine, unaziacha.. Ukishaokoka wale watu uliokuwa unakula nao rushwa, au unaiba nao unawaacha!

Sasa unawaachaje?

Awali ya yote unapaswa uwaambie na uikiri imani yako mbele yao, na endapo wakikusikia na wao wakakubali kubadilika na kuwa kama wewe basi utakuwa umewapata, lakini kama hawataki kubadilika na zaidi sana njia zao ni zile zile, basi hapo UNAPASWA UWAACHE!!, Kwa usalama wa roho yako, anza kutafuta marafiki wengine wa imani moja na wewe, hao panga ratiba mara chache chache kwenda kuwatembelea na utakapowatembelea habari utakazowapelekea ni za injili kuanzia mwanzo wako hadi mwisho wako.

Na kamwe usijaribu kuwaza kuwa unaweza kuwa shujaa na kwamba hawataweza kukurudisha nyuma endapo utashikamana nao..Ni kweli katika siku za mwanzo unaweza kujiona wewe ni mshindi, lakini nataka nikuambie kwa kadiri siku zitakavyozidi kwenda tabia yako njema kidogo kidogo itaanza kuathirika, na baada ya kipindi fulani, utajioni umepoa kabisa na kufanana na hao, au kuishia kuwa mkristo vuguvugu tu!.

Ukitaka ukristo wako uimarike siku baada ya siku, watafute wakristo wa kweli ungana nao!..na iache kampani mbaya!.. binti ukitaka udumu katika kuvaa vizuri na kwa heshima, na katika usafi watafute mabinti wenzako wa imani kama yako hiyo, dumu nao hao!.. utautunza utakatifu wako kwa viwango vya juu.. lakini ukitaka kuanza na moto na kuishia baridi, basi endelea na makundi yale yale uliyonayo baada ya kuokoka. (Maisha yako ya wokovu hayatafika mbali).

Vile vile ukitaka kudumu katika eneo la Maombi, yaani uzidi kuwa mwombaji, na mtu wa ibadani na mtu wa kumpenda Mungu, sharti uwatafute watu wa namna yako!.. ambao ni wacha Mungu tena wanaopenda maombi, lakini kama hutawatafuta hao na ukasema mimi ninaweza kuendelea kuwa mwombaji hata nikiwa na makundi yangu yale yale, nataka nikuambie ndugu yangu, unapoteza muda.. mwisho wako utakuwa mbaya sana, na hautajua ni saangapi umepoa kiroho au umeanguka kabisa.

Sasa tunazidi kulithibitisha vipi hili kimaandiko?

Tusome,

2Timotheo 2:22  “Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, PAMOJA NA WALE WAMWITAO BWANA KWA MOYO SAFI”.

Hapo anasema tuzikimbie tamaa za ujanani, tukatafute “haki, imani, upendo  na amani.” Lakini sasa tunatafuta hii haki, imani, upendo na amani pamoja na watu gani???..je! pamoja na walevi?, au pamoja na wazinzi?, au pamoja na watu wenye mizaa? Au pamoja na wahuni?..jibu ni la! Bali pamoja na WALE WAMWITAO BWANA KWA MOYO SAFI!!... Na wanaomwita Bwana kwa moyo safi si wengine zaidi ya wale wakristo waliosimama kikweli kweli, ambao Bwana kawapanda kila mahali.

Ukidhani kuwa unaweza kulirekebisha hilo andiko na kwamba  wewe unaweza kwenda kutafuta Imani pamoja na walevi, unapoteza muda!, ukidhani unaweza kuitafuta amani na kuipata pamoja na wazinzi,  au wahuni, au wauaji, au watu wa masengenyo basi nataka nikuambia kuwa unapoteza muda wako mwingi..Hata mwanafunzi hawezi kupata maarifa yoyote ya darasani endapo akikaa na wanafunzi wasiopenda shule, lakini akikaa na wenzake wapendao shule basi atapata faida anayoitafuta.

Vile vile na wewe leo hii, punguza makundi ya watu wa kidunia, na ongeza makundi ya watu wamwitao Bwana kwa moyo safi.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

EPUKA MUHURI WA SHETANI

EPUKA KUCHELEWA IBADA.

NI LIPI KATI YA MAKUNDI HAYA, WEWE UPO?

EPUKA KUUNDA MATARAJIO YAKO, KWENYE AHADI ZA MUNGU.

EPUKA KUPELELEZA KILA KITU MUNGU ANACHOKUAHIDIA.

Rudi nyumbani

Print this post

UTAKAPOKUWA MZEE, UTAINYOSHA MIKONO YAKO. NA MWINGINE ATAKUFUNGA

Bwana Yesu asifiwe,

Ufukufu na Heshimu ni vyake milele na milele. Amina.

Napenda tutafakari, Pamoja kwa makini maneno haya ambayo Bwana Yesu alimfunulia mtume wake Petro, ni maneno ambayo yatakufaa sasa wewe kijana ambaye bado una nguvu za kufanya utakalo hivi sasa..

Embu Tusome;

Yohana 21:18 “Akasema, Amin, amin, nakuambia, Wakati ulipokuwa kijana, ulikuwa ukijifunga mwenyewe na kwenda utakako; lakini utakapokuwa mzee, utainyosha mikono yako, na MWINGINE atakufunga na kukuchukua usikotaka”.

Hii kauli ni ya kuitafakari sana, sio ya kuichukulia juu juu, Hapa Bwana anamweleza Petro jinsi ujana wake unavyoweza kumpa uhuru wa ‘nani wa kujifunga chini yake’, na kumtumikia, mfano akiamua, ajifunge na kuwa mtumwa wa mali, uamuzi ni wake, akitaka ajifungue kisha ajifunge kwa mwingine tena, bado uwezo huo anao, leo anaweza akajifunga kwa Mungu, kesho kwa shetani, ni jinsi apendavyo kwasababu nguvu hizo anazo rohoni.

Hapo ndipo lile neno linalosema, “nimewaandikia ninyi vijana kwasababu mna nguvu ya kumshinda yule mwovu”(1Yohana 2:14), linapotimia, maana yake, uwezo wa kujifungua au kujifunga kwa shetani, unao, angali  bado una nguvu..

Lakini tunaona Bwana Yesu anampa angalizo lingine na kumwambia, utakapokuwa mzee, “MWINGINE”..Atakufunga na kukuchukua usikotaka..

Sasa ulishawahi kutafakari huyo ‘mwingine’ ni nani?

Huyo mwingine ni Aidha “Mungu” au “Shetani”.. Maana yake ni kuwa utafika wakati, ambapo kama hutajiweka chini ya Mungu tangu sasa, shetani atakuweka chini yake kipindi hicho, penda usipende,..yaani utamilikiwa na shetani asilimia mia ya Maisha yako, na kukufanyia chochote apendacho juu yako..

Ukishafikia hii hatua, kamwe huwezi tena kumgeukia Mungu, wala hata kuzielewa Habari za Mungu, kwasababu tayari wewe ni mfungwa wa shetani.

Hali kadhalika kinyume chake ni kweli, unapofanyika chombo cha Mungu sasa angali una nguvu..utafika wakati huna nguvu, Mungu atakuchukua moja kwa moja na kukupeleka atakapo yeye.. Huko ndipo wakati ambapo uzee wako unaishia vema..hata kama ni kwa kifo kwasababu ya ushuhuda, lakini kamwe hutakaa upotee tena milele..kwasababu umeshafungwa tayari na Mungu, hivyo hakuna namna yoyote utakaa upotee au uanguke mikononi mwa shetani.

Ndio maana biblia inasema..

Mhubiri 12:1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo”.

Maana yake ni kwamba usipomkumbuka muumba wako leo, wakati una nguvu (wakati wa ujana wako) utafikia wakati, utapoteza furaha yako yote ya maisha.. Hicho ndicho kipindi cha kufungwa na ibilisi, na kupelekwa usipotaka..Angalia vema utaona wazee wengi ambao wamekuwa wakipuuzia injili tangu ujanani, mwisho wao huwa hauwi mzuri, kunakuwa na ugumu mkubwa sana kuwashawishi kwa Habari ya wokovu. Huwa wanapitia wakati mgumu sana kiroho kwasababu tayari “mwingine” ameshawafunga na kuwachukua wasipotaka..

Hivyo Bwana Yesu alikuwa anamtahadharisha Mtume Petro, sio tu kwa Habari ya kifo chake, lakini pia kwa maamuzi anayoyachukua sasa..lazima yawe ya busara.. Utumwa anaouchagua sasa, ndio utakaomuhifadhi baadaye..

Kama ni Kristo, basi Kristo atamwokoa, lakini kama ni shetani basi shetani atampeleka alipo yeye..

Ndugu, siku hizi ambazo waweza kusikia injili, na ukashawishika moyoni, ndizo siku zako za ujana, embu sasa anza kujiweka chini ya Kristo, akuongoze, achana na ulimwengu na mambo yake, wanadamu hawawezi kukufaidia chochote kwa siku zijazo.

Anza kuisafisha njia yako sasa, kama vile biblia inavyotushauri katika..

Zaburi 119:9 “Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako”.

Kumbuka, ni kipindi kifupi sana tumebakiwa nacho hadi kurudi kwa Bwana Yesu mara ya pili, Kama unadhani, Unyakuo bado sana, fikiria mara mbili, dalili zote zimeshatimia, injili inayoendelea sasa sio ya kubembelezewa wokovu, bali ni ya kujiingiza katika ufalme kwa nguvu. Huna sababu ya kuendelea kufichwa uhalisia, dakika hizi ni za majeruhi, siku yoyote, parapanda  inalia, PARAPANDA INALIA!!

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

PETRO AKAMWAMBIA YESU “BWANA NA HUYU JE”?

NI YESU YUPI UMEMPOKEA?, NI ROHO IPI UMEIPOKEA? NA INJILI IPI UMEIPOKEA?

Je! Ni kanisa lipi sahihi kumuabudia Mungu?

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita.

Ni sahihi kusema sikuitiwa kuhubiri ubatizo kama Paulo alivyosema (1Wakorintho 1:17)?.

LAKINI WAKATI WA TAABU WATASEMA, SIMAMA UKATUOKOE.

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

Rudi nyumbani

Print this post

EE MUNGU, MUNGU WANGU, NITAKUTAFUTA MAPEMA:

Daudi alikuwa ni kijana mdogo, lakini aliona jinsi muda unavyokimbia kweli kweli, aliona jinsi, siku zinavyotoweka kwa kasi, na huku bado hajatengeneza mambo yake sawa na Mungu.

Japokuwa katika hatua aliyofikia tayari alikuwa ni kipenzi cha Mungu, lakini hakuridhika na hali yake ya kiroho, akataka ayatengeneze mapema mambo yake na Mungu, asiwe na doa lolote kwake, Ndipo akaandika Zaburi hii akasema;

ZABURI 63:1 “Ee MUNGU, Mungu wangu, NITAKUTAFUTA MAPEMA, Nafsi yangu inakuonea kiu, Mwili wangu wakuonea shauku, Katika nchi kame na uchovu, isiyo na maji”.

Alijua thamani ya ujana wake, kwamba akiuacha tu ukiyeyuka, mpaka kufikia uzee bila kumtafuta muumba wake, atakuwa ameshindwa vita vikubwa vya Maisha.. Ndio maana akatia bidii sana, kumtafuta Muumba wake mapema, angali bado ni kijana mdogo. Akawa siriazi na Mungu wake,

Alilitambua vizuri lile andiko linalosema..

Mhubiri 12:1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo”.

Kwamba ipo miaka ambayo akiifikia mtu hatapata raha yoyote Maishani mwake, kama ujana wake uliishia katika mambo yasiyokuwa na maana.. Hivyo akasema, nitamtafuta Mungu wangu mapema, haijalishi ni mateso gani au vikwazo gani nitavipitia sasa, na akalithibitisha kweli lile alilolisema kwa vitendo.

Hakungojea uzee, au afikishe umri Fulani wa makamo ndio aache njia za uovu, hakufikia uzee ndio amfanye Bwana kuwa ngao yake.. Bali umri wake ule ule wa ujana alimtafuta Mungu wake kwa bidii.

Swali la kujiuliza na wewe kama kijana, au wewe kama mtu mzima, bado unaona una muda wa kusubiri kwa Mungu wako?

Mtafute Mungu wako mapema, kesho si yako. Hizo nguvu za kiroho Mungu alizoziweka ndani yako, hazitakuwepo kesho. Neema ya wokovu, huwa haidumu milele.
Inatabia ya kuzunguka na kuhamia kwa wengine, jambo ambalo watu wengi hawalijui. Ilikuwepo kwa wayahudi, lakini sasa ipo kwetu. Na Mungu ameahidi siku hizi za mwisho itaondoka kwetu itarudi kwa wayahudi tena. Je unalifahamu hilo?

Bwana Yesu alisema..

Yohana 11:9 “… Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu.
10 Bali akienda usiku hujikwaa; kwa sababu nuru haimo ndani yake”.

Akimaanisha kuwa, nuru ya ulimwengu (yaani JUA) huwa linafanya kazi saa 12 tu. Baada ya hapo ni giza. Na ndivyo Yesu anavyoifananisha neema yake na JUA. Kwamba inadumu kwa kipindi Fulani tu, baada ya hapo haitaonekana tena.

Leo hii unaipuuzia injili, hutaki kutubu dhambi zako, kuna wakati nguvu ya kuvutwa kwa Yesu itaondoka kwako na kuamia kwa wengine. Kipindi hicho kikifika, milele hutakaa umgeukie Kristo utabakia kuwa mtu wa kudhihaki na kejeli kwenye mambo ya ki-Mungu. Kwasababu neema iliyokuwa inakuvuta imeshaondoka.

Kuwa makini sana na nyakati hizi za majeruhi. Mtafute Mungu wako mapema. Muda tuliobakiwa nao ni mchache mpaka Kristo atakapokuja, kizazi tunachoishi mimi na wewe, kimekidhi vigezo vyote vya kinabii kushuhudia tukio la unyakuo, na lile la kurudi kwa pili kwa Yesu duniani.. Unadhani tutakuwa na kizazi kingine? Soma biblia vizuri uone.

Unangoja nini?, Unamsubiria nani? Mgeukie Yesu mapema hii. Kanisa tulilopo ndio la saba na la mwisho lijulikanalo kama Laodikia, (Ufunuo 3:14-21), Na hakutakuwa na kanisa lingine Zaidi ya hili.

Tubu dhambi zako kwa kumaanisha,kweli kweli, mimina moyo wako kwa Bwana, salimisha ujana wako kwake, jitwike msalaba wako angali una kipindi kifupi bado, saa ya wokovu ni sasa, sio kesho, kama maandiko yasemavyo.

Ndugu, ikiwa unataka leo, kurudi kwa Bwana wako, na umedhamiria kwa dhati kufanya hivyo, basi fahamu Bwana Yesu anaweza kukupokea na kukusamehe dhambi zako.

Ni wewe tu kumaanisha kufungua moyo wako, kwani leo leo anaweza kukusamehe na kukupokea kama kiumbe kipya kwake. Akakusamehe kabisa dhambi zako. Basi Ikiwa upo tayari kufanya hivyo unaweza tafuta mahali pa utulivu, kisha piga goti, hata kwa machozi fuatisha sala hii ya toba kwa Imani, na Bwana atakusamehe;

Sema…

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.

Unaweza kirudia tena hiyo sala, hata mara mbili au tatu, mpaka utakaposikia amani moyoni mwako.

Basi ikiwa umekamilisha hilo..Hatua iliyobakia kwako ni ubatizo, kama hukubatizwa ipasavyo kwa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo.

Ikiwa utahitaji msaada huo na mafundisho ya kuukulia wokovu basi unaweza wasiliana nasi kwa namba zetu hizi;

+255693036618/ +255789001312

Tafadhali shea na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU:

TUNAMHITAJI SANA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUYAELEWA MAANDIKO.

NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?

WAPE WATU WANGU RUHUSA ILI WAPATE KUNITUMIKIA.

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

VIJANA NA MAHUSIANO.

Karibu katika darasa fupi, linalohusu vijana na mahusiano.

Yapo maswali kadhaa ya kujifunza kwa kijana kabla ya kuanza mahusiano ya aina yoyote ile, na mambo yenyewe ni haya;

 1. Je ni wakati gani ulio sahihi wa kuanza mahusiano?

 2. Je ni mtu gani sahihi wa kujiingiza naye katika mahusiano?

 3. Je mambo gani ninapaswa niyafanye na yapi sipaswi kuyafanya ninapoingia katika uhusiano?

Awali ya yote ni muhimu kufahamu kuwa darasa hili linawahusu/linawafaa zaidi vijana wa kiume na wa kike ambao tayari wameshaokoka!, yaani wametubu na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu na wanaitazamia mbingu mpya na nchi mpya. Kama bado hujampokea Bwana Yesu basi mafunzo haya yanaweza yasikusaidie, hivyo ni vyema kwanza ukampokea Bwana Yesu (ukaokoka), na ndipo mambo mengine yafuate baadaye.

Mahusiano yamegawanyika katika sehemu kuu (2),  Yapo Mahusiano kabla ya Ndoa, na Mahusiano baada ya Ndoa. Mahusiano kabla ya ndoa, yanaitwa Uchumba ambayo tutajikita sana kujifunza juu ya haya katika siku ya leo.


  1. Ni wakati gani ulio sahihi wa kuanza mahusiano Kwa kijana wa kiume:

Kama wewe ni kijana wa kiume na umeokoka, wakati sahihi wa kuanza mahusiano ni wakati ambao tayari unajitegemea mwenyewe. Maana yake una sehemu yako mwenyewe ya kuishi na una kipato chako mwenyewe, haumtegemei mzazi au ndugu!, kwasababu hatua ya uchumba ndio hatua ya awali kabla ya kuoa, na huwezi kuoa ukiwa bado hata wewe mwenyewe huwezi kujitunza, utamtuzaje huyo mke anayekuja?.

Kwasababu hiyo basi si wakati sahihi wa kuanza mahusiano yoyote ukiwa bado ni Mwanafunzi,  au ukiwa bado upo kwa wazazi wako, au ukiwa huna shughuli yoyote ya kukuingizia kipato!.

Ni umri gani sahihi wa kuanza Mahusiano, kwa kijana wa kiume?

Hapa inategemea na umri ulioanza kujitegemea mwenyewe, katika zama hizi vijana wengi wa kiume kuanzia miaka 25 na zaidi ndio wanaanza kujitegemeana hiyo ni kutokana na mifumo ya Elimu. Mtu atamaliza shule akiwa na zaidi ya miaka 20, na kujikuta kuanza kufanya kazi za mikono akiwa na zaidi ya miaka hata 25, wakati huo unaweza kuwa wakati sahihi wa kuanza uchumba.

Wapo wengine wanawahi kuanza kujitegemea wenyewe kabla ya umri huo!, hao wanaweza kuwahi kuanza mahusiano..lakini mahusiano ya mapema ni hatari sana, kwasababu akili ya kijana bado haijakomaa vizuri katika kujua mambo mengi ya kimaisha na wengi wanaingia huko kutokana na tamaa za kimwili tu!,.. Hivyo Ni vizuri kijana wa kiume akaanza mahusiano zaidi ya miaka 25.


Kwa kijana wa kike:

Wakati sahihi wa kuanza mahusiano kwa kijana wa kike, si wakati upo shule, bali wakati ambao umemaliza shule,

Vile vile umri sahihi wa kuanza mahusiano ni miaka 20 na zaidi!.. Zamani kidogo ilikuwa ni mapema, lakini zama hizi, shule zimewafanya watu wachelewe kuanza maisha yao kujitegemea. Lakini vijana wengi wa kike walio chini ya miaka 20 sasa wanaojiingiza kwenye mahusiano ya uchumba wengi wanaongozwa na tamaa tu!, aidha kwa kujua au kwa kutokujua. Na wengi wa hao wakifikisha miaka 30, akili zao zinapofika hatua ya kupevuka wanajigundua kuwa walikuwa wanafanya vitu vya kitoto na vya kipumbavu.


 2. Je ni mtu gani sahihi wa kujiingiza naye katika mahusiano?

Kwa kijana wa kiume:

Mtu sahihi wa kuanza naye mahusiano sio yule uliyeoneshwa na Nabii, au Mchungaji, au uliyechaguliwa na mtu. Kamwe usianze mahusiano na mtu yeyote ambaye umesaidiwa kuchaguliwa. Uchaguzi utachagua wewe!, Yule Bwana aliyekuchagulia atakuja kwako na wewe utajikuta unampenda, anakidhi vigezo vyako!..Hivyo ndivyo Bwana anavyowapa watu wenza wao na sio kuchaguliwa na mchungaji au Nabii, au kuoteshwa ndoto.

Vile  vile usianze mahusiano na msichana/ mwanamke yeyote ambaye yeye ndiye anayekuomba au kukulazimisha umwoe!.

Kwa kijana wa kike:

Kwa kijana wa kike mtu sahihi wa kuanza naye mahusiano si mwanafunzi,  haijalishi anaonesha kukupenda kiasi gani, bado sio mtu sahihi, hapa sizungumzii wale watu ambao ni wafanyakazi lakini wanajiongezea elimu ya juu (hili tayari ni kundi la watu wazima wanaojitambua), wanafunzi tunaowazungumzia hapa ni wale wa sekondari, na wale waliotoka sekondari na moja kwa moja chuo.


 4. Je mambo gani napaswa niyafanye na yapi sipaswi kuyafanya ninapoanza mahusiano?

Fanya mambo yafuatayo unapoanza mahusiano.

Kwa kijana wa kiume!

Mfahamu huyo mtu kwanza, na kama ameokoka anza naye urafiki kama wa dada na kaka tu Kama hajaokoka au si mtu wa imani moja nawe!, mhubirie kwanza aokoke, akimkubali Bwana Yesu, atakukubali na wewe, akimkataa Bwana Yesu hawezi kukukubali na wewe!. Usimwahidi kwamba utamwoa endapo akiokoka maana kwa kufanya hivyo atakukubali ilimradi tu aolewe na wewe!, hivyo mvute kwa Kristo kama unavyowavuta wengine wote.

Akikubali kumtii Kristo na kumpata Roho Mtakatifu ambaye umempokea wewe, na hata kushiriki kanisa moja nawe, hapo unaweza kuanza naye urafiki kama wa kaka na dada tu!, wa kuheshimiana, wakati huo unaweza kuongeza kumjali zaidi kuliko wengine wote wanaomzunguka, kwa kufanya hivyo atakuwa ameshaanza kujua kuwa unamjali, na hivyo atakupenda na hapo ni rahisi kuendelea na hatua nyingine.

Kwa kijana wa kike!

Kwasababu ni mwanaume ndiye anayemchagua mwanamke!, kijana wa kike hupaswi kujiweka au kujitangaza kwamba unatafuta mchumba.. Kaa katika hali yako ya asili, umri usikuogopeshe wala kukutatanisha, wapo wanaoolewa hata na miaka 60, na wanakuwa na furaha, hivyo usijitafutishe mchumba.. usijipendekeze sana kwa vijana wa kiume!, bali dumu katika usafi wa Rohoni na wa Mwilini, jiweke katika mazingira ya usafi na ya upole!, Bwana atakuletea mtu sahihi ambaye atakuheshimu, kwa wakati sahihi. (www wingulamashahidi org).

Hali kadhalika utakayemwona anakuja kwako kuwa naye makini, kwasababu Matunda mazuri si mtu tu anayeyapenda bali hata nyani, na ndege na popo na bundi wanayapenda!, (maana yake hata watu waovu wanawapenda wanawake wanaojiheshimu na watakatifu), hivyo kuwa makini, Kama hajaokoka mkaribishe kanisani, na jitahidi usimhubirie wewe, kwamaana ni rahisi kukubali kuokoka ili akupate!, bali mwunganishe na mchungaji wa kiume kanisani, au na mtu yeyote aliyesimama pale kanisani, kama akimsikiliza huyo na kumkubali Kristo, ni rahisi kuwa mtu sahihi Bwana aliyekukusudia, lakini kama hataki kujihusisha na mchungaji au mtu yeyote kanisani, jitenge naye, usitazame uzuri wake au fedha zake, ni pando la adui, anakutafuta kwa faida zake tu!

Mambo yafuatayo usiyafanye unapokuwa katika Mahusiano ya uchumba!


Kwa kijana wa kiume/kike.

1/ Usikutane kimwili na huyo uliyeanza naye mahusiano, wala msishikane wala kubusiana, (Kujaliana tayari ni ujumbe tosha kwamba kila mmoja anampenda mwenzie, na sio kufanya hayo mambo)

2/ Usimtembelee huyo kijana/binti nyumbani kwake akiwa peke yake, tafuta mwenzako muwe wawili ndipo umtembelee, hiyo itaongeza heshima yenu na vile vile shetani hatapata nafasi. Vile vile tafuta masomo mazuri yanayohusu mahusiano, yaliyofundishwa na watumishi wa Mungu wa kweli, mshirikishe mwenzio asikilize mafundisho hayo, au asome, au ahudhurie semina ili aanze kujiandaa na kuwa mume au mke.

Baada ya kuhakiki kuwa huyu mwenzangu ananifaa kimaisha na vile vile ananifaa kiroho, vile vile amekukubali uwe mwenza wake, basi hatua ya ndoa inaweza kufuata. Mambo yafuatayo yatakufaa baada ya mwenzako kukubali kufunga ndoa naye.

 1. Tangaza kwa wazazi: Kumbuka unapoenda kutangaza isiwe ni jambo la kushtusha kwa wazazi wako au walezi, ni vizuri wawe wanamjua huyu mwenza wako hata kabla ya hapo, ili wawe na amani naye.

2. Baada ya kutangaza kwa wazazi, Ndoa inapaswa utangazwe kanisani. Baada ya kanisa kujua na kupewa taratibu zote za ndoa, Mahari zitapangwa (Ni lazima kijana wa kiume ulipe mahari, ikiwa kubwa sana omba upunguziwe au kopa mahali ulipe), ni kinyume na maandiko kijana wa kiume kutolipa mahari, Kristo aliingia Gharama kutukomboa sisi (ndio damu yake) ambayo inafananishwa na mahari kwetu sisi bibiarusi wake, kwahiyo ni lazima kijana ulipe mahari.

 3. Baada ya Mahari na ndoa kutangazwa na kufungwa, kanisani. Hapo Mmekuwa Bwana arusi na Bibi-Arusi, mnaweza kufanya mambo yote yanayowahusu wana-ndoa. Hampaswi kuishi kama wachumba tena.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

JINSI YA KUUHARIBU UJANA WAKO.

MAMA, TAZAMA, MWANAO.

kwanini yule kijana aliitupa ile nguo ya kitani chini na kukimbia uchi?

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

Rudi nyumbani

Print this post

Je suruali ni vazi la kiume tu?

Ni wapi katika biblia panaonyesha kuwa suruali ni vazi la kiume tu? Na vipi juu ya kanzu!, mbona kama ni mfano wa gauni lakini linavaliwa na wanaume, kwanini Suruali isivaliwe pia na wanawake!


Jibu: Vazi la Suruali mara ya kwanza katika biblia lilivaliwa na Makuhani.

Mungu aliwapa amri makuhani watengeneze suruali ambazo zilitofautiana kimaumbile, waliambiwa watengeneze suruali fupi (yaani kaptula), Na vile vile walikuwa wanavaa zile ndefu ambazo zilifika kabisa mpaka chini kwenye viiko vya miguu.

Kutoka 28:41 “Nawe mvike huyo nduguyo Haruni na wanawe nao mavazi hayo; nawe watie mafuta, na kuwaweka kwa kazi takatifu, na kuwatakasa, ili wapate kunitumikia mimi katika kazi ya ukuhani.

42 Nawe wafanyie SURUALI ZA NGUO YA KITANI, ili kufunika tupu ya miili yao; suruali hizo zitafika tangu kiunoni hata mapajani;

43 na Haruni na wanawe watazivaa, hapo watakapoingia katika hema ya kukutania, au hapo watakapoikaribia madhabahu ili watumike katika mahali patakatifu; wasije wakachukua uovu, wakafa; hii itakuwa ni amri ya milele kwake yeye, na kwa wazao wake”.

Na katika Israeli hakukuwa na Kuhani Mwanamke!, Makuhani wote walikuwa ni wanaume. Hivyo lilikuwa ni vazi la kiume. (Soma pia Kutoka 39:27, na Walawi 6:10)

Vile vile tunaweza kulithibitisha hilo kipindi kile cha akina Shedraka, Meshaki na Abednego. Wakati Mfalme Nebukadneza alivyowatupa katika lile tanuru la moto, maandiko yanasema walitupwa kule hali wamevaa suruali zao na kanzu zao na joho zao.

Danieli 3:21 “Basi watu hao wakafungwa, hali wamevaa SURUALI ZAO, na kanzu zao, na joho zao, na mavazi yao mengine, wakatupwa katikati ya ile tanuru iliyokuwa ikiwaka moto.

22 Basi kwa sababu amri ya mfalme ilikuwa ni kali, na ile tanuru ilikuwa ina moto sana, mwako wa ule moto ukawaua wale watu waliowashika Shadraka, na Meshaki, na Abednego”.

Sasa Shedraka, Meshaki na Abednego hawakuwa wanawake, bali wanaume!, na hakuna popote katika biblia panataja au kuonyesha mwanamke kavaa suruali, kama hawa wakina Shedraki au kaagizwa kuvaa suruali kama hawa Makuhani.Hakuna!!. Ikifunua kuwa hilo ni vazi la kiume!

Maandiko yanasema.

Kumbukumbu 22:5 “Mwanamke asivae mavazi yampasayo mwanamume, wala mwanamume asivae mavazi ya mwanamke; kwa maana kila afanyaye mambo hayo ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako”.

Mwanamke yeyote kuvaa suruali ni machukizo mbele za Mungu, Suruali sio vazi la kumsitiri mwanamke, hakuna mwanamke yeyote anayevaa suruali na kuonekana kama kajisitiri, badala yake ataonekana kama kajidhalilisha au kajifunua..Na maandiko yanasema wanawake na wavae mavazi ya kujisitiri.

1Timotheo 2:9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani”

Hivyo mwanamke yeyote hapaswi kuvaa suruali, wala vimini wala nguo zozote zinazochora maungo yake.

Na pia Kanzu, halikuwa vazi la kike!, kanzu lilitumika kama vazi la Nje!, kama vile mtu anavyovaa koti!.. Ndio maana utaona hapo wakina shedraka, Meshaki na Abednego walikuwa wamevaa suruali na kanzu kwa nje. Kwahiyo Kanzu halikuwa gauni, Gauni ni vazi la kike lililotengenezwa mahususi kufuatia maumbile ya mwanamke!. Na ndilo wanawake wa kikristo wanapaswa walivae.

Sasa inawezekana ulikuwa hulijui hili kuwa hilo ni vazi la kiume, lakini leo umejua na ndani ya kabati lako kumejaa suruali, nataka nikuambie, usingoje kesho, leo leo zitoe kazichome moto!, wala usimpe mtu!.. zichome na tafuta magauno au sketi ndefu!, usiogope kuonekana mshamba mbele ya ulimwengu!. Ni heri uonekane mshamba lakini unakwenda mbinguni kuliko kuonekana wa kisasa lakini sehemu yako ni katika lile ziwa la moto!.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

USIYAACHE MAVAZI YAKO NA KWENDA UCHI!

Kwanini wale dubu waliowauwa vijana wa Elisha walikuwa wa kike?

Kwanini wale dubu waliowauwa vijana wa Elisha walikuwa wa kike?

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

VAZI LA YESU HALIGAWANYWI.

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI YA KUUHARIBU UJANA WAKO.

Hizi  ni baadhi ya njia zitakazokusaidia kuuharibu ujana wako kwa wepesi.

  1. Pendelea makundi yasiyojenga.

Wahuni ni ndio wawe marafiki zako, wazinzi ndio wawe kampani yako, walevi ndio wawe watu wa kukupa raha, wanawake wasengenyaji ndio wawe wajoli wako, njia hii ukiitumia vizuri itakufanikisha haraka sana kwenye malengo yako. Huna haja ya kukaa na vijana  wenye hekima, wanaomcha Mungu ya nini?

Ukiliondoa neno hili katika akili yako utafanikiwa..

Zaburi 1:1 Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.

2) Usimpende Mungu, wala usilitii Neno lake.

Wakati wale vijana wengine washamba wanajibidiisha kumpendeza Mungu, sawasawa na

Zaburi 119:9 Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako.

Basi wewe, nenda kinyume tu, kataa kulifuata neno la Mungu. Tafuta namna nyingine ya kuisafisha njia yako, Pale unapoambiwa usizini, ona kama huo ni udhaifu, kazini na kila kahaba au mwanamume unayemwona, kwasababu wewe ni mrembo sana,  si ndio? kijana maji ya moto.

3) Fanya chochote unachojisikia kufanya.

Kile roho yako inapenda, huna haja ya kujizuia. Usijizuie wala usiwe na kiasi, Ukijisikia kwenda Disko nenda, ukijisikia kuvuta sigara vuta, ukijisikia utukane, fanya hivyo, ukijisikia kutembea nusu uchi barabarani tembea, ukijisikia kujichubua tumia mikorogo yote, kwasababu andiko linalokusapoti kufanya hivyo;

Mhubiri 9:8 Mavazi yako na yawe meupe sikuzote; wala kichwa chako kisikose marhamu.

9 Uishi kwa furaha pamoja na mke umpendaye, siku zote za maisha yako ya ubatili, ulizopewa chini ya jua; siku zote za ubatili wako, kwa maana huo ni sehemu yako ya maisha; na katika taabu zako ulizozitaabika chini ya jua.

10 Lo lote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; KWA KUWA HAKUNA KAZI, WALA SHAURI, WALA MAARIFA, WALA HEKIMA, HUKO KUZIMU UENDAKO WEWE.

4) Endelea kufikiria wewe ndio bora kuliko watu wote duniani, hakuna mwingine kama wewe:

Kati ya watu 7,00,000,000 waliopo duniani leo, zidi kufikiri hakukuwahi kuwa na warembo zaidi yako wewe, na wakajuta, wazuri kupita wewe, wote hao waliokufa walikuwa wadhaifu sana, endelea kudharau maonyo ya waliokutangulia, ona mawazo yao ni ya kizee,

Hata hili andiko usilizingatie,

Mhubiri 12: 12 Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo;..”

Biblia iendelee kuwa kwako ni kitabu cha wazee,

5) Usipende kujishughulisha na chochote, kwasababu muda sikuzote unao.

Kwasababu kujishughulisha na kazi ya Mungu ni ushamba kwako, basi hata na mambo mengine, hayana haraka sana, si umri bado mdogo, utasoma tu siku moja, sasahivi ponda starehe, utafanya kazi tu siku moja, kesha kwenye muvi, chat instagramu, zururazurura, ruka ruka tu huku na huko, kwasababu muda bado upo, .

Wale wanaolishika hili neno achana nao.

Waefeso 5:15 Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; 16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.

Ukiyafanikisha haya kwa bidii ,mafanikio yako yapo mbioni.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Hizi  ni baadhi ya njia zitakazokusaidia kuuharibu ujana wako kwa wepesi.

  1. Pendelea makundi yasiyojenga.

Wahuni ni ndio wawe marafiki zako, wazinzi ndio wawe kampani yako, walevi ndio wawe watu wa kukupa raha, wanawake wasengenyaji ndio wawe wajoli wako, njia hii ukiitumia vizuri itakufanikisha haraka sana kwenye malengo yako. Huna haja ya kukaa na vijana  wenye hekima, wanaomcha Mungu ya nini?

Liondoe kabisa neno hili akilini mwako, utafanikiwa..

Zaburi 1:1 Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.

2) Usimpende Mungu, wala usilitii Neno lake.

Wakati wale vijana wengine washamba wanajibidiisha kumpendeza Mungu, sawasawa na

Zaburi 119:9 Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako.

Basi wewe, nenda kinyume tu, kataa kulifuata neno la Mungu. Njia yako utaisafisha vizuri sana, Pale unapoambiwa usizini, ona kama huo ni udhaifu, kadange na kila kahaba au mwanamume unayemwona, kwasababu wewe ni mrembo sana,  si ndio? kijana maji ya moto.

3) Fanya chochote unachojisikia kufanya.

Kile roho yako inapenda, huna haja ya kujizuia. Ukijisikia kwenda Disko nenda, ukijisikia kuvuta sigara vuta, ukijisikia utukane, fanya hivyo, ukijisikia kutembea nusu uchi barabarani tembea, ukijisikia kujichubua tumia mikorogo yote, kwasababu andiko linalokusapoti ni hili;

Mhubiri 9:8 Mavazi yako na yawe meupe sikuzote; wala kichwa chako kisikose marhamu.

9 Uishi kwa furaha pamoja na mke umpendaye, siku zote za maisha yako ya ubatili, ulizopewa chini ya jua; siku zote za ubatili wako, kwa maana huo ni sehemu yako ya maisha; na katika taabu zako ulizozitaabika chini ya jua.

10 Lo lote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; KWA KUWA HAKUNA KAZI, WALA SHAURI, WALA MAARIFA, WALA HEKIMA, HUKO KUZIMU UENDAKO WEWE.

4) Endelea kufikiria wewe ndio bora kuliko watu wote duniani, hakuna mwingine kama wewe duniani:

Kati ya watu 7,00,000,000 waliopo duniani leo, zidi kufikiri hakukuwahi kuwa na warembo zaidi yako wewe, wazuri kupita wewe, wote hao waliokufa walikuwa wadhaifu sana, endelea kudharau maonyo ya waliokutangulia, ona mawazo yao ni ya kizee, Kwasababu wewe ni wewe..

Hata hili andiko usilizingatie,

Mhubiri 12: 12 Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo;..”

Biblia ni kitabu cha wazee,

5) Usipende kujishughulisha na chochote, kwasababu muda sikuzote unao.

Kwasababu kujishughulisha na kazi ya Mungu ni ushamba kwako, basi hata na mambo mengine, hayana haraka sana, si umri bado mdogo, utasoma tu siku moja, sasahivi ponda starehe, utakuja kufanya kazi tu siku moja, kesha kwenye muvi, chat instagramu, zururazurura, ruka ruka tu huku na huko, kwasababu muda bado upo, .

Wale wanaolishika hili neno achana nao.

Waefeso 5:15 Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; 16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.

Ukiyafanikisha haya kwa bidii bado,mafanikio yako yapo mbioni.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.

Je! Ni dhambi kwa kijana aliyeokoka kuvaa suruali za kubana (model), kunyoa mitindo (mfano kiduku), ?

AGENDA KUBWA YA SHETANI KWA KANISA HILI LA LAODIKIA.

UFUNUO: Mlango wa 3 part 3

Rudi nyumbani

Print this post

TATIZO LA NDANI LINALOWASUMBUA VIJANA, WALIOOKOKA.

Kuna tatizo sugu ambalo linalowasumbua watu wengi , hususani vijana pindi wanapookoka, Na pengine linakusumbua hata na wewe.

Vijana kadha wa kadha waliookoka, wamekuwa wakinipigia  simu, wengine wakinitumia meseji wakisema mtumishi, tangu nilipookoka, nimejitahidi kweli kuacha uasherati na kutazama picha chafu (za ngono) mitandaoni, Lakini naona kama ninamkosea Mungu kwasababu, zile taswira za yale niliyokuwa ninayafanya au ninayatazama, zinanijia mara kwa mara akilini mwangu, wakati mwingine hata wakati nikiwa naomba, au najifunza Neno.

Hivyo naona kama bado sijakamilika, Mungu hajanisamehe na kuniosha dhambi zangu, najisikia vibaya sana, imenipelekea kukosa nguvu ya kumtumikia Mungu.. Nifanye nini?

Kama na wewe umekuwa na tatizo kama hili nataka nikuambie, wewe sio wa kwanza,  Biblia inasema mtaifahamu kweli nayo hiyo kweli itawaweka huru.(Yohana 8:32)

Jambo ambalo wengi hatufahamu ni kuwa, Utakaso wa Mungu  umegawanyika katika sehemu mbili.

  1. Upo utakaso ambao utaupokea moja kwa moja siku ile unapookoka
  2. Upo utakaso ambao Unachukua muda kutimilika.

Tukianzana na huo wa kwanza, zipo hali ndani yako, ambazo Mungu anaziondoa, mara moja pindi tu unapookoka, kwamfano kiu ya kutenda yale maovu uliyokuwa unayatenda huko nyuma, kama vile wizi, matusi, uvaaji mbaya, pombe  n.k.

Lakini upo utakaso ambapo itakupasa upitishwe mahali Fulani kwanza kwa muda, ndipo uwe safi kabisa. Na ndio maana utaona katika agano la kale kuna unajisi ambapo ulikuwa ukishatakasika, ilikupasa usubirie mpaka ifike jioni ndio uwe safi, mwingine siku tatu, mwingine wiki mbili, inategemeana na unajisi wenyewe. Utajiuliza ni kwanini usiwe na saa hiyo hiyo?

Kwamfano embu soma vifungu hivi;

Walawi 11:25” na mtu awaye yote atakayechukua cho chote cha mizoga yao atafua nguo zake, naye atakuwa najisi hata jioni”.

Walawi 15:27 “Na mtu ye yote atakayevigusa vitu vile atakuwa najisi, naye atazifua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa najisi hata jioni.

28 Lakini huyo mwanamke kwamba ametakaswa na kule kutoka damu kwake, ndipo atakapojihesabia siku saba, na baadaye atakuwa safi”.

Sasa katika suala kama hilo, la picha chafu kuondoka ndani yako, hupaswi, kudhani kuwa Mungu hajakusamehe, Umeshasamehewa, dhambi zako, tangu siku ile ulipookoka na kuacha kufanya hayo mambo, lakini ule utakaso kamili haujakamilika ndani yako, hivyo itakuchukua muda kidogo, hivyo kwa jinsi unavyozidi kujitenga na hayo mambo, ndivyo Mungu anakusafisha mpaka utafika wakati hizo picha hazitakujia tena katika akili yako.

Utajiuliza ni kwanini Musa alipelekwa jangwani miaka 40, kabla ya kuitwa kwenda kuwaokoa wana wa Israeli. Ilikuwa ni kwa kusudi la kuondoa, kiburi na majivuno ndani yake  ambayo pengine yasingeweza kuondoka kwa siku moja au wiki moja. Vilevile wana wa Israeli walizungushwa jangwani kwa miaka 40, ilikuwa ni ili kuindoa miungu iliyokuwa mioyo mwao, wajifunze kumtegemea Yehova tu.

Hata gari lililo spidi haliwezi kuchuna breki na kusimamia hapo hapo tu, ni lazima litaendelea mbele kidogo, kwasababu lilikuwa katika mwendo kasi. Halikadhalika, ikiwa umeokoka leo, au hivi karibuni, hizo picha chafu ulizokuwa unazitazama, zilishaiharibu nafsi yako kwa muda mrefu sana, hivyo zinaweza kuchukua muda Fulani mpaka ziondoke kabisa. Ndio ujue dhambi sio jambo la kulichukuliwa kirahisi rahisi tu.

1Wathesalonike 4:3 “Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati;

4 kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima;

5 si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu”.

Lakini usihofu wewe endelea kukaa mbali na uchafu wote, na kidogo kidogo, Bwana atayasafisha mawazo yako, na kuna wakati utafika, hata hayo mawazo au hizo picha zitakuwa kama ni Habari za utotoni.

Dhambi  inagharama. Hivyo, usirudi nyuma, wala usifadhaike, songa mbele, zidisha ukaribu wako na Mungu, kaa tu mbali na vyanzo vyote vya uzinzi, tamthilia za kidunia acha, movie zote  zenye maudhui hayo acha, mazungumzo yenye uzinzi ndani yake, kampani za marafiki wahuni achana nazo, mitandao ya kijamii kama instagramu, ikiwa huna jambo la maana unafuata kule, ondoa, kwasababu vingi vilivyomo kule havikujengi,.. vyote hivyo jitenge navyo.. Kwasababu biblia inasema moto hufa kwa kukosa kuni.

Mithali 26:20a “Moto hufa kwa kukosa kuni;..”

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.

MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI.HATA UASHERATI NAO

KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI:

MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.

Rudi nyumbani

Print this post

MUME / MKE BORA KUTOKA KWA BWANA UTAMWONA UKIWA KATIKA MAZINGIRA GANI?

Nakusalimu katika jina kuu sana la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze Neno la Mungu ili tupate maarifa sahihi ya kuishi hapa duniani.

Na leo tutaona mazingira ambayo ukikaa katika hayo basi Mungu atakujalia umwone mke/mume sahihi aliyekuchagulia toka mbali.

Tofauti na mazingira ya kiulimwengu ambayo yenyewe ili yakupe mke/mume wa kidunia ni sharti uwe katika mazingira ya kidunia..yaani uvae vimini, ujitembeze na suruali barabarani, unyoe viduku, uishi kama wasanii wa kidunia, uwepo disco na kwenye party party kila wakati n.k. ili uonekane.

Ukikaa katika mazingira kama hayo hakika dunia itakupatia unachokitafuta..

Lakini leo tutajifunza mazingira ya ki-Mungu… Ili Mungu akuonyeshe mke/mume sahihi tokea mbali je! Ukae katika mazingira gani.?

Tutamtazama Isaka mtoto wa Ibrahimu. Kama wewe ni msomaji wa biblia utakumbuka mpaka wakati mama yake anakufa hakuwa na mke bado.

Lakini siku moja Baba yake alipoona ni wakati sasa wa Isaka kuwa na mke alimtuma Kijakazi wake mmoja kwenda kumtafutia mke kutoka katika nchi ya mbali nchi sana ya baba zake. ..kwani hakutaka kumpatia mke kutoka katika miji ile waliyokuwepo.

Kuonyesha kuwa haijalishi utazungukwa na vijana wengi wazuri mahali ulipo, hiyo bado haikufanyi udhani mke/mume Mungu aliyekuchagulia ni lazima atoke hapo.

Sasa utaona mara baada ya yule kijakazi kutumwa kwenda kumtafutia Isaka mke na kumpata alipokuwa anarudi..Huku nyuma kuna tabia na desturi ambayo Isaka alikuwa nayo ambayo nataka leo tuione kwasababu hapa ndipo kiini cha somo letu kilipo.. Tusome..

Mwanzo 24:62-66

[62]Basi Isaka alikuwa amekuja kwa njia ya Beer-lahai-roi, maana alikaa katika nchi ya kusini.
[63]Isaka akatoka ili kutafakari kondeni wakati wa jioni; akainua macho yake, akaona, kuna ngamia wanakuja.
[64]Rebeka akainua macho, naye alipomwona Isaka, alishuka juu ya ngamia.
[65]Akamwambia mtumishi, Ni nani mtu huyu ajaye kondeni kutulaki? Mtumishi akasema, Huyu ndiye bwana wangu. Basi akatwaa shela yake akajifunika.
[66]Yule mtumishi akamwambia Isaka mambo yote aliyoyatenda.

Rudia tena Mstari wa 62 unasema…

‘Isaka akatoka ili kutafakari kondeni wakati wa jioni’.

Unaona, Pindi tu alipotoa mguu wake na kwenda kondeni kutafakari..alipojijengea desturi ya kwenda maporini mbali na makazi ya watu ili tu kupata utulivu na Mungu wake, kuutafakari ukuu wake na uweza wake na maajabu yake na ahadi zake..huko huko Mke wake alitokea..na akamwona tokea mbali..

Pengine yeye alidhani mjini alikoondoka ndipo wake wanapotokea lakini..alishangaa kule kule kondeni kwa mbali sana ngamia wanakuja wamembeba bibi arusi wake..

Hiyo ni kuonyesha Isaka haukuwa na hulka kama za vijana wengine walizokuwa nazo..alipendelea zaidi kumtafakari Mungu kuliko kuzurura zurura huko na huko.

Matokeo yake akampata Rebeka, mwanamke ambaye tunamsoma mpaka leo, licha ya kuwa alikuwa ni mwanamke anayemcha Mungu lakini bado alikuwa ni mzuri sana wa uso..Mwanzo 26:6-7

Ndugu, ikiwa unamuhitaji mke mzuri na anaye mcha Mungu basi kuwa kama Isaka..lakini ikiwa unamuhitaji Yezebeli basi ishi mfano wa hao vijana wa kidunia wanavyoishi leo hii..

Na hili pia lipo kwa upande wa pili wa mabinti..ikiwa unataka uolewe na mwanamume ilimradi tu mwanamume basi jiweke kama hao mabinti wa kidunia wanavyojiweka wanaotembea nusu uchi barabarani na kujipambapamba kama vile Yezebeli ili waonekane wanavutia..
Utampata unayemtafuta.

Lakini kinyume chake ni kuwa ukitulia katika kusudi la Mungu..unatumia muda mrefu kwa Mungu wako kuliko kutanga tanga..unamtakafakari tu yeye..nakwambia Mungu utakuongoza kwa Isaka wako tokea mbali..kama vile Rebeka alivyomwona Isaka akimfuta kutokea mbali..

Uhitaji kujionyesha onyesha ovyo..kwasababu anayekuletea mke/mume ni Mungu, si mwanadamu..wewe kaa katika kumtakafakari yeye maisha yako yote.

Kuoa utaoa, kuolewa utaolewa tu!..ukiishi maisha yanayopendeza Mungu si uongo utakutendea tu.

Daudi alisema..

Zaburi 37:25
[25]Nalikuwa kijana nami sasa ni mzee,
Lakini sijamwona mwenye haki ameachwa
Wala mzao wake akiomba chakula.

Mungu hawezi kuacha kumpa mteule wake kitu kilicho chema, na kizuri.. Hawezi kuruhusu mke/mume pasua kichwa atokee mbele ya njia yake, mtu anayemcha yeye. Hilo haliwezekani..

Hivyo kama bado hujaokoka. Tubu leo anza maisha yako upya na Bwana Yesu kwa kumaanisha kabisa..Toba ya kweli inaambatana na kuucha ulimwenguni, mkatae shetani na kazi zake zote na vimini vyake vyote, na suruali zote na viduku vyote..kamtafakari Mungu huko makondeni, hata kama utaonekana mshamba..

Ishi maisha ya kumlingana Bwana..Na bila shaka wakati utafika atamtuma malaika wake kwenda kukuletea mwenzi sahihi..Kama Ibrahimu alivyomtuma kijakazi wake, kumletea Isaka Rebeka.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

Sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji zilikuwaje?

Je! “Mke wa ujana wako” ni yupi kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Je kwa mkristo aliyeokoka, ni dhambi kunyoa ndevu zake?

SWALI: Je kwa mkristo aliyeokoka, ni dhambi kunyoa ndevu zake kulingana na huu mstari?

Walawi 19:26 “Msile kitu cho chote pamoja na damu yake; wala msifanye kuloga, wala kutumia utambuzi.

27 MSINYOE DENGE PEMBE ZA VICHWANI, WALA MSIHARIBU PEMBE ZA NDEVU ZENU.

28 Msichanje chale yo yote katika nyama ya miili yenu kwa ajili ya wafu, wala msiandike alama miilini mwenu; mimi ndimi Bwana.

29 Usimnajisi binti yako, ili kumfanya awe kahaba; isiwe hiyo nchi kuuandama ukahaba, na nchi kujawa na uovu mkuu”.

JIBU: Wana wa Israeli wakiwa jangwani Mungu aliwapa maagizo hayo, ya kutokunyoa ndege(para) kwenye pembe za vichwa vyao, na wala wasichonge ndevu (kwa pembeni) wanyoapo.

Sasa Mungu kuwapa maagizo hayo, haikuwa kwasababu wataonekana na mwonekano tofauti, hapana bali mitindo hiyo ilikuwa ni inamaana kubwa Zaidi kwa watu wale, kwani ziliwakilisha ibada za miungu yao ya kipagani na ushirikina.  Wakati ule wamisri na waarabu waliokuwa wanaishi majangwani, walikuwa wananyolewa nywele zote za pembeni na kuachwa na KIDUKU cha mvuringo hapo juu, na wengine walikuwa wananyoa para kabisa,(Isaya 15:2, Yeremia 48:37) walifanya hivyo  kwa heshima ya miungu yao. Vilevile na kuchongwa kwa pembe za ndevu zao, kwa lengo hilo hilo.

Sasa Ili Mungu kuwatofautisha watu wake na mionekano ya kipagani, akawazuia wasifanye vile kama wao. Mungu alilichagua taifa la Israeli liwe takatifu, lijulikane kama ni taifa la Yehova, sio taifa ambalo watu akilitazama waone desturi za miungu ya kipagani ndani yao. Na ndio maana utaona mpaka “chale” alikataza wasichanjwe, mpaka michoro ya mwilini (Tatoo) wasichore, kwasababu zote hizo zilikuwa ni desturi za wachawi na miungu ya kipagani.

Kama vile wafanyavyo wachina leo hii, utawaona wamenyoa vichwa vyao vyote, na kuacha kifuniko kidogo cha nywele hapo juu, sio kwamba ni fashion hapana, bali ni wanatangaza desturi za miungu yao.

Hata leo hii, Ni ajabu sana kumuona mkristo ananyoa KIDUKU, wala hata hajui asili yake ni nini au anatangaza nini.. Na hata kama hana nia ya kutangaza upagani, lakini pia hajui kuwa Mungu ametuita kujitofautisha na watu wa ulimwenguni, kama alivyofanya kwa waisraeli.

kunyoa kiduku

Unaponyoa kiduku, halafu ni mkristo, unatoa nuru gani kwa jamii inayokuzunguka.  Ni wazi kuwa unatangaza usanii wa wanamiziki, unapovaa nguo iliyochanika chanika magotini, unatangaza nini?.. Unapofuga rasta, unamtangaza Mungu gani hapo, wewe kama mkristo unatangaza nini..? Kumbuka sisi ni barua tunayosomwa na watu wote.

Pia upo unyoaji wa ndevu wa kisasa ambao unaweza ukawa hauna maana ya ibada ya kipagani, lakini staili ya unyoaji wake zikakutambulisha wewe ni nani, kama utanyoa ndevu kwengine kote  halafu hapo katikati  unaziacha zirefuke ziwe kama za mbuzi, au unanyoa kisha unaziwekea mitindo mitindo uonekane kama msanii Fulani kwenye tv, wewe kama mkristo unapaswa ujue bado ni rafiki wa dunia. Na sio wa Mungu.

Hivyo kama wewe ni mnyoaji wa viduku, au wa hizo staili ni heri ukaacha, kwasababu Mungu hapendezwi ni mkristo wa namna hiyo.

Warumi 12:1 “Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.

2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Je kuweka mapambo kama mikufu, vikuku na kutoboa pua ni dhambi?

Kikuku/vikuku ni nini katika biblia?

Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.

UFUNUO: Mlango wa 15

Swali: Je Ni sahihi kwa Mkristo kupeleka kesi mahakamani?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

Rudi nyumbani

Print this post