NI YESU YUPI UMEMPOKEA?, NI ROHO IPI UMEIPOKEA? NA INJILI IPI UMEIPOKEA?

NI YESU YUPI UMEMPOKEA?, NI ROHO IPI UMEIPOKEA? NA INJILI IPI UMEIPOKEA?

Jina la Bwana Yesu libarikiwe, karibu katika kuyatafakari maandiko..

2Wakorintho 11:4 “Maana yeye ajaye akihubiri YESU MWINGINE ambaye sisi hatukumhubiri, au mkipokea ROHO NYINGINE msiyoipokea, au INJILI NYINGINE msiyoikubali, mnatenda vema kuvumiliana naye”!

Hapo katika  sentensi hiyo, Mtume Paulo aliposema “mnatenda vema kuvumiliana naye”..hakuwa anawasifu watu wa Korintho kwa wao kupokea roho nyingine, au kumkubali Yesu mwingine, bali kinyume chake! Alikuwa ANAWASHUTUMU!.

Sentensi hiyo ili ieleweke vizuri tunaweza kuiweka hivi ….“Mnachukuliana na mtu anayekuja kwenu na kuwahubiria yesu mwingine au injili nyingine msiyoikubali)” yaani “mnaona ni sawa na tena mnakubaliana naye”.

Hapo Mtume Paulo, alimaanisha kwamba, hawapaswi kuchukuliana na mtu yeyote anayekuja kwao na kuwaletea yesu Mwingine au roho nyingine au injili nyingine ambayo hawakuhubiriwa na mitume..kinyume chake wawakatae watu hao na wakatae injili yao na kuipuuzia…lakini hawa watu Wa Korintho walikuwa hawafanyi hivyo!.. walikuwa wanakaa na kuwasikiliza!..jambo ambalo ni hatari kwa roho zao.

Na hata sasa kuna yesu mwingine anayehubiriwa tofauti na Yule Yesu wa kwenye biblia, kadhalika kuna roho nyingine tofauti na Yule Roho Mtakatifu anayehubiriwa katika biblia, na vile vile kuna injili nyingine tofauti na injili halisi ya kwenye biblia..

yesu mwingine ni yupi?

Bwana Yesu halisi anasema wa kwenye biblia anasema.. “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi (Yohana 14:6)”…lakini yesu mwingine anasema “zipo njia nyingi za kufika kwa baba, ikiwemo kupitia mtakatifu Fulani au kupitia maombi ya mtakatifu Fulani aliyekufa, au kupitia kanisa Fulani au kupitia dini nyingine yeyote”

Kadhalika Bwana Yesu halisi wa kwenye biblia alisema… “mtu yeyote akitaka kunifuata ajikane mwenyewe ajitwike msalaba wake anifuate(Mathayo 16:24) na tena anasema “itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake? Ama mtu atoe nini badala ya nafsi yake?(Marko 8:36)”..lakini yesu mwingine anasema.. “sio lazima kujikana nafsi, sio lazima kuacha dhambi, sio lazima kubadilika kimwonekano, Mungu anatazama roho hatazami mwili” n.k

Huyo ndio mfano wa yesu Mwingine ambaye Paulo, aliwaonya watu wa Korintho kwamba wasimkubali,na wala wasichukuliana naye kwasababu ni shetani.

Kadhalika ipo roho Nyingine.

Roho Mtakatifu wa kweli wa kwenye biblia, akija juu ya mtu, jambo la kwanza analolifanya ni kumgeuza Yule mtu na kuwa mtakatifu, kama jina lake lilivyo.. “Roho Mtakatifu”..sifa yake ni utakatifu, na kazi ya pili ni kutuongoza na kututia katika kweli yote ya maandiko, na ya tatu ni kutukumbusha maandiko ..

lakini zipo roho ambazo mtu anapozipokea hazimfanyi kuwa mtakatifu, badala yake ndio zinampa kibali cha kutenda dhambi, kuvaa vibaya,(nusu uchi), kutukana, kuwa na kinyongo na visasi..kadhalika hazimwongozi mtu katika kusoma Neno na kulijua katika ukweli wote. Badala yake ndio zinamletea uvivu wa kuisoma biblia na kuijua..Hizo roho ni roho nyingine, ambazo sio Roho Mtakatifu, ni roho za adui, ambazo zinajigeuza na kujifananisha na Roho Mtakatifu.

Kadhalika kuna Injili nyingine.

Injili maana yake ni “habari njema za Yesu Kristo” ambazo zinaleta WOKOVU kwa mtu.(Warumi 1:16). Na wokovu ni kupata kuokoka kutoka katika hatari Fulani ijayo, au iliyopo.

Zipo injili ambazo hazimfanyi mtu aokoke kutoka katika hatari ya adhabu ya milele (katika Jehanamu ya moto), badala yake zinamfanya astahili kwenda Jehanamu.

Mfano wa injili hizo ni “injili za kutokusamehe, vinyongo na visasi”. Siku hizi hadi makanisani zinahubiriwa. Bwana Yesu alisema, msipowasamehe watu makosa yao, hata baba yenu wa mbinguni hatawasamehe (Mathayo 6:15)..Kwahiyo kutokusamehe tayari ni tiketi ya kwenda jehanamu moja kwa moja..Na injili yeyote inayohubiri kutokusamehe ni injili nyingine ya kuzimu.

Leo hii utakuta mkristo kajaa uchungu, na vinyongo..kwa mambo baadhi tu aliyofanyiwa mabaya..na anakwenda kanisani anakutana na injili ya kupiga adui zake, na kuipokea akidhani yupo salama..kumbe yupo hatarini?

Jiulize ndugu, Umempokea Yesu yupi? Wa kwenye biblia au Yule mwingine?..na umeipokea roho ipi?, Ni Roho Mtakatifu au ya adui?.. na ni Injili gani umeipokea?..ile iletayo wokovu, au ikupelekayo kuzimu?

Maandiko yanatuasa kuwa “tuzipime roho”, na sio roho tu!, bali pia tumpime Bwana yupo tumempokea Yesu Kristo au yesu kristo, na ni injili ipi tumeipokea.

Maran atha!

Group la whatsapp Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Je! Watu ambao hawajawahi kusikia injili kabisa siku ya mwisho watahukumiwa?

Ni kwa namna gani malaika wa mbinguni wanaweza kutuhubiria sisi injili?

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

Matoazi na Matari ni nini? (Kutoka 15:20)

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Anonymous
Anonymous
2 years ago

Ameeeen Mtumishi,Mungu azidi kukubariki.