Baali alikuwa nani?

Baali alikuwa nani?

Baali alikuwa ni aina ya mungu aliyekuwa anaabudiwa na watu wa kaanani na nchi za Tiro na Sidoni, ambaye kulingana na historia za wakaanani, anatajwa kuwa mwana wa mungu aliyeulikana kwa jina la El na mkewe aliyejulikana kwa jina la Ashera..hawa ndio waliomzaa huyu Baali ambaye baadaye alikuja kuabudiwa kama mungu.

Tafsiri ya jina “Baali” ni “bwana” na aliaminika kama mungu wa rutuba na wa uzao.

Aliaminika kusaidia kuongeza rutuba ya nchi, pale ambapo chakula hakikupatikana kutokana na ardhi kutozaa..basi walimwomba huyu mungu baali, ili nchi iweze kuzaa mazao.

Kadhalika pale ambapo mtu au watu walipatwa na matatizo ya kutokupata watoto, walimwomba na kumtegemea mungu huyu kwaajili ya kupata uzao.

Mungu huyu aliabudiwa sana na watu wa kimataifa, lakini ulifika wakati hata wana wa Israeli wakaanza kumwabudu.
Wana wa Israeli walianza kumwabudu baali kwa mara ya kwanza katika kile kipindi cha Waamuzi.

Waamuzi 2:11 “Wana wa Israeli walifanya yaliyokuwa ni maovu mbele za macho ya BWANA, nao wakawatumikia Mabaali.

12 Wakamwacha BWANA, Mungu wa baba zao, aliyewaleta kutoka katika nchi ya Misri, wakafuata miungu mingine, baadhi ya miungu ya watu wale waliokaa karibu nao pande zote, wakajiinamisha mbele yao; wakamkasirisha BWANA, akaghadhibika.

13 Wakamwacha BWANA, wakamtumikia Baali na Maashtorethi”.

Waliendelea hivyo na ibada hizo za mabaali, lakini si kwa kiwango kikubwa..

Hali ilikuja kuwa mbaya zaidi ulipofika wakati wa Mfalme mmoja wa Israeli aliyeitwa Ahabu, ndipo kipindi hicho ibada hizo zilishika hatamu mpaka Bwana Mungu akamtuma Eliya Nabii.

Mfalme Ahabu aliabudu baali kwa kiwango ambacho hakuna mfalme yeyote alikifikia.

1 Wafalme 16:30“ Ahabu mwana wa Omri akafanya yaliyo mabaya machoni pa BWANA kuliko wote waliomtangulia.

31 Ikawa, kama ingalikuwa neno dogo tu kuyaendea makosa ya Yeroboamu mwana wa Nebati, akamwoa Yezebeli binti Ethbaali, mfalme wa Wasidoni, akaenda akamtumikia Baali, akamsujudia.

32 Akamjengea Baali madhabahu katika nyumba ya Baali, aliyoijenga huko Samaria.

33 Ahabu akaifanya Ashera; Ahabu akazidi kumghadhibisha BWANA, Mungu wa Israeli, kuliko wafalme wote wa Israeli waliomtangulia”.

Lakini je! Baali alikuwa ni mungu kweli?

Jibu ni la!.

Mungu ni mmoja tu, aliyeziumba mbingu na nchi, jina lake YEHOVA. Hao wengine sio miungu bali ni roho za mapepo..BAALI ni pepo!..

Ndio maana haikuweza kujibu chochote mbele za uwepo wa Bwana wa majeshi, wakati ule wa Eliya.

1 Wafalme 18:26
“ Wakamtwaa yule ng’ombe waliyepewa, wakamtengeza, wakaliitia jina la Baali tangu asubuhi hata adhuhuri, wakisema, Ee Baali, utusikie. Lakini hapakuwa na sauti, wala aliyejibu. Nao wakaruka-ruka juu ya madhabahu waliyoifanya”.

Hiyo inatufundisha kuwa ibada zote za miungu na za sanamu ni chukizo kwa Bwana.

Na wote wanaoabudu sanamu, na miungu hawataurithi uzima wa milele, maandiko yanasema hivyo.

Bwana atubariki.

Group la whatsapp Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Je Mungu anaweza kumdanganya mtu?

Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?

Maashera na Maashtorethi ni nini?

Mlima Gerizimu na Ebali ni ipi, na umuhimu wao rohoni ni upi?

Je Mungu anaweza kumdanganya mtu?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments