Maashera na Maashtorethi ni nini?

Maashera na Maashtorethi ni nini?

Ashera au kwa jina lingine anajulikana kama Ashtorethi, Ni mungu-mke wa kipagani ambaye alikuwa anabudiwa katika nchi ya wakaanani, Waashuru na mataifa mengine ya kando kando pale mashariki ya kati..

Ashera pamoja na Baali ni moja ya miungu ambayo ilikuwa ni maarufu sana duniani kwa wakati huo.

Katika nchi ya Kaanani walikuwa wanamwabudu katika mfumo wa mti, ambao ulipandwa chini, na kuchongwa katika maumbile ya mwanamke, kumwakilisha yeye. Wakimwona kama ndiye mti wa uzima.

Sasa tunaona katika maandiko, Wana wa Israeli wakiwa bado jangwani Mungu aliwaonya sana, juu ya miungu ya nchi hiyo ya Kaanani wanayoiendea, kwamba wasijichanganye nayo, badala yake wakifika huko  waivunje vunje, na kuiondoa, kwasababu yeye ni Mungu mwenye wivu;

Kutoka 34:12 “Ujihadhari nafsi yako, usije ukafanya agano na wenyeji wa nchi ile unayoiendea, lisiwe mtego katikati yako.

13 Bali utabomoa madhabahu zao, na kuvunja-vunja nguzo zao, na kuyakata-kata maashera yao.

14 Maana hutamwabudu mungu mwingine, kwa kuwa Bwana, ambaye jina lake ni mwenye wivu, ni Mungu mwenye wivu”.

Lakini tunaona walipofika nchi ya ahadi hilo hawakulizingatia badala yake, nao wao pia wakaanza kuiga desturi za wale wafiisti ambao hawakuwamaliza wote, wakaanza na wao kuabudu Maashera..

2Wafalme 17:9 “Tena, wana wa Israeli wakafanya kwa siri mambo yasiyokuwa mema juu ya Bwana, Mungu wao, wakajijengea mahali pa juu katika miji yao yote, kutoka mnara wa walinzi hata katika miji yenye boma.

10 Wakajisimamishia nguzo na maashera juu ya kila mlima mrefu, na chini ya kila mti wenye majani mabichi”;

Ikafikia hatua mpaka wafalme wengine wakawa sio tu wanaibudia nje kwa siri, bali waliichukua kabisa nguzo zake na kuipeleka katika hekalu la Mungu, mahali ambapo Mungu ameliweka jina lake, watu wamwabudu na kumfanyia dua, wao wanaingiza miungu migeni, Matokeo yake wakamtia Mungu wivu mkubwa zaidi, wakapewa adhabu ambayo isiyosameheka, na adhabu yenyewe ilikuwa kuuliwa, mji kuteketezwa na kuchukuliwa utumwani Babeli.

Mfalme ambaye alifanya kitendo hicho aliitwa Manase;

2Wafalme 21:7 “Akaiweka sanamu ya kuchongwa ya Ashera aliyoifanya ndani ya nyumba, ambayo Bwana alimwambia Daudi, na Sulemani mwanawe, Katika nyumba hii, na katika Yerusalemu, niliouchagua miongoni mwa kabila zote za Israeli, nitaliweka jina langu milele”;

Utasoma habari za maashera katika vifungu hivi;

2Nyakati 14:2,17:6, 19:3, 24:18, 23:14

Je hadi leo kuna maashera yanayoabudiwa?

Hata sasa Mambo hayo yanatendeka katika Kanisa la Kristo hata leo, na cha kusikitisha zaidi ni kuwa wanajua kabisa Mungu amekataza lakini wao wanafanya.

Unapoliweka sanamu la mtakatifu fulani (tuseme bikira Mariamu), na kuanza kulihusianisha na ibada, unaomba kwa kupitia hilo, unaeleza shida zao kwa kutazama sanamu hilo, ujue kuwa unamwabudu Ashera moja kwa moja.

Na tendo hilo linamtia wivu Mungu sana, wivu ambao unaweza kukusababishia mauti.  Ni heri ukutane na hasira ya Mungu kuliko Wivu wake..Kwasababu wivu unakula na hivyo mapigo yake ni makali zaidi.

Wimbo 8:6b..Kwa maana upendo una nguvu kama mauti, Na wivu ni mkali kama ahera.

Biblia inasema tena…

Mithali 27:4 “Ghadhabu ni kali, na hasira ni gharika; Lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu”.

Unaona?, shida inakuja ni pale mtu anapoelezwa ukweli kama huu, anadhani dini yake inashutumiwa..Nakwambia ni heri dini ishutumiwe roho yako ipone, kuliko roho iangamie dini yako iendelee kumtia Mungu wivu, faida yake itakuwa ni nini sasa?  Tubu mgeukie Kristo, uokoke. Hizi ni nyakati za mwisho.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

HISIA YA MUNGU ILIYO MBAYA KULIKO ZOTE.

USIIGEUZE NYUMBA YA MUNGU KUWA PANGO LA WANYANG’ANYI.

KUABUDU SANAMU/IBADA ZA SANAMU.

JIEPUSHE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

Nini maana ya uvuvio?.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Cecil Mapunda
Cecil Mapunda
3 years ago

Napenda kujifunza neno la Mungu.

MGOWOLE, Simon
MGOWOLE, Simon
3 years ago

Thank you so much MUNGU awabariki