Title June 2021

VIPINDI VINNE VYA MAISHA VILIVYO VIGUMU MTU KUMKUMBUKA MUUMBA WAKE.

Jina la Bwana wetu Yesu, libarikiwe karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu, ambalo ndio mwanga wa njia zetu na taa iongozayo miguu yetu. Leo tutajifunza vipindi VINNE ambavyo ni vigumu mtu kumkumbuka muumba wake.

Biblia inasema..

Mhubiri 12: 1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, KABLA HAZIJAJA SIKU ZILIZO MBAYA, WALA HAIJAKARIBIA MIAKA UTAKAPOSEMA, MIMI SINA FURAHA KATIKA HIYO.

2 KABLA JUA, NA NURU, NA MWEZI, NA NYOTA, HAVIJATIWA GIZA; KABLA YA KURUDI MAWINGU BAADA YA MVUA; ……

 6 KABLA HAIJAKATIKA KAMBA YA FEDHA; Au kuvunjwa bakuli la dhahabu; Au mtungi kuvunjika kisimani; Au gurudumu kuvunjika birikani”

7 NAYO MAVUMBI KUIRUDIA NCHI KAMA YALIVYOKUWA, NAYO ROHO KUMRUDIA MUNGU ALIYEITOA”

Biblia inaposema mkumbuke muumba wako “KABLA”. Maana yake ni kwamba kama hutamkumbuka katika hicho kipindi, basi utafika wakati itakuwa ni ngumu wewe kumkumbuka Muumba wako. Ikimaanisha kuwa kitendo cha mtu kumkumbuka Mungu, ni neema, na huwa hakidumu muda wote!, ni cha kitambo tu!..tofauti na wengi wanavyofikiri kuwa watakapofikia miaka fulani watamkumbuka Mungu, pasipo kujua kuwa nguvu ya mtu kuvutwa kwa Mungu inatoka kwa Mungu, na si kama mtu apendavyo yeye..

Yohana 6: 44 “Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka;..”.

Ndio maana leo hii kuna idadi kubwa ya vijana na watoto wanaompokea Yesu, kuliko wazee!.

Sasa kufuatia hiyo mistari katika kitabu hicho cha Mhubiri, biblia imetupa vipindi 6 ambavyo tunapaswa tufanye maamuzi, maana yake ndani ya hivyo vipindi, tunatakiwa tuwe tumeshafanya maamuzi  thabiti ya kumkumbuka muumba wetu na kumtumikia.

  1. KABLA HAZIJAJA SIKU NA MIAKA UTAKAYOKOSA FURAHA.

Mhubiri 12: 1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo”.

Nyakati za utoto na ujana, ni nyakati ambazo mtu anapokosa furaha, ni rahisi kumrudia Mungu, mtu anapopitia matatizo Fulani ndipo anapomkumbuka Mungu, kwasababu bado yupo katika miaka ya ujana, lakini sivyo atakavyokuwa mzee. Miaka ya uzee ni miaka ambayo mtu anapopitia matatizo au shida ndivyo anavyozidi kukaa mbali na Mungu. Ndio maana ni ngumu sana kumbadilisha mzee ampokee Yesu, hata akiwa katikati ya mateso na tabu!.. kwanini?..Ni kwasababu ile nguvu ya kumfanya amrudie muumba wako inakuwa haipo!.. Na mara nyingi ni kwasababu muda wa ujana, hakuutumia kumkumbuka muumba wake.

Lakini pia hapa biblia inatuonya kwamba tumkumbuke muumba kabla haijakaribia hiyo miaka!..sio haijafika!.. bali haijakaribia!!..maana yake hata kabla ya kuifikia hiyo miaka, bado kuna shughuli kumkumbuka Mungu..ikiwa na maana kuwa hii neema ya sisi kuvutwa kwa Mungu, haidumu juu yetu milele, inawahi kuondoka kabla hata ya sisi kufikia uzee. Ni wazee wachache sana, wanaopata neema ya kumpokea Yesu katika miaka ya uzee.. Na wengi wa hao ni kwasababu labda katika ujana, waliishi katika mazingira ambayo hawakufikiwa na injili sana.. Lakini wengi ambao wapo tangu ujana wao wanaisikia injili, lakini wanaipuuzia, katika uzee ni ngumu pia kumrudia Mungu.

  1. KABLA JUA, NA NURU, NA MWEZI, NA NYOTA, HAVIJATIWA GIZA; Kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;

Mhubiri 12:2 “Kabla jua, na nuru, na mwezi, Na nyota, havijatiwa giza; Kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua”

Kipindi ambacho Jua litatiwa giza kwa mtu, ni kipindi cha uzee.. Ni kipindi ambacho Mwili wako umeisha nguvu, macho yako hayana nguvu, miguu yako haina nguvu, mikono yako haina nguvu..

Bwana Yesu alimwambia Petro maneno haya..

Yohana 21:18  “Akasema, Amin, amin, nakuambia, Wakati ulipokuwa kijana, ulikuwa ukijifunga mwenyewe na kwenda utakako; lakini utakapokuwa mzee, utainyosha mikono yako, na mwingine atakufunga na kukuchukua usikotaka”

Kipindi hichi ni kipindi ambacho ni ngumu kumkumbuka muumba wako!.. ile kiu, hamu, au motisha ya kumtafuta Mungu inakuwa haipo, kadhalika uwezo wa kutafakari mambo ya Mungu unakuwa ni hafifu!.. kwahiyo Mungu anatupa tahadhari kuwa tumkumbuke yeye kabla hiyo miaka haijakaribia!..kwasababu itakapofika tofauti na tunavyofikiri kwamba tutakuwa na nguvu za kumkumbuka Mungu, kumbe la! Kinyume chake ndio tutakwenda mbali naye..

Na kipindi ambacho mawingu yatarudi baada ya mvua, ni kipindi hicho hicho ambacho, mvua ya neema imeisha juu ya mtu..hivyo mawingu yanarudi kama kawaida na kiangazi kinaanza.

  1. KABLA HAIJAKATIKA KAMBA YA FEDHA.

Mhubiri 12:6 “kabla haijakatika kamba ya fedha; Au kuvunjwa bakuli la dhahabu; Au mtungi kuvunjika kisimani; Au gurudumu kuvunjika birikani”

Kikawaida umri wa kukatika kamba ya fedha ni miaka 60, huo ndio umri wa kustaafu!…wengine wanastaafu kabla ya huo umri miaka 55, na wengine baada ya huo kidogo, miaka 65 na hapo anasema kukatika kamba ya fedha, na si kukatika fedha!..kamba ya fedha ni shughuli unayoifanya inayokuingizia kipato Fulani cha kila mwezi.. wengi!, kamba hiyo inakatika miaka 60.

Hivyo kabla ya hiyo miaka haijafika, Bwana Mungu anatupa tahadhari, tumkumbuke yeye kabla ya kuifikia hiyo miaka..kwasababu tusipomkumbuka na katika hiyo, na huku maisha yetu yote tumeisikia injili, baada ya miaka hiyo, hakutakuwa tena na nafasi ya sisi kumgeukia yeye.. kwasababu nguvu ya kuvutwa kwake haitokani na sisi, bali inatoka kwake.. hivyo hatupaswi kuipuuzia kipindi hichi cha ujana..

  1. Kabla MAVUMBI KUIRUDIA NCHI KAMA YALIVYOKUWA, NAYO ROHO KUMRUDIA MUNGU ALIYEITOA.

Hili ni neno la kuhitimisha. Kuwa tumkumbuke muumba kabla hatujamaliza maisha yetu hapa duniani. Baada ya kifo hakuna wokovu tena, biblia inasema “mti uangukiapo huko huko utalala Mhubiri 11:3”.

Hakuna nafasi ya pili baada ya kifo!. Bwana anasema tumkumbuke yeye kabla “roho zetu hazijamrudia yeye”. Kwasababu hakutakuwa na nafasi ya pili, kwamba tufufuliwe tutubu, ndipo tufe.. biblia inasema “tumewekewa kufa mara moja na baada ya kifo hukumu (Waebrania 9:27)”

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba Bwana Mungu anatuonya kwamba tuutumie muda wetu vizuri tukiwa hapa duniani!.. Na yale mawazo adui aliyoyaweka katika vichwa vyetu kwamba tutakapokuwa wazee ndipo tutamrudia Mungu, hayo mawazo tuyakatae!, kwasababu ni ya adui.. kiufupi!, kwajinsi muda unavyozidi kwenda ndivyo ile njia ya wokovu inasonga!, na kuzidi kuwa nyembamba.. Ndio maana Bwana akatuambia..

2Wakorintho 6:2  “(Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa”

Tubu na kumpokea Kristo leo, usiseme ngoja nimalizie kuiba kidogo, au ngoja niendele kufanya ukahaba, au ngoja nimalizie kunywa pombe, baada ya kipindi Fulani nitaokoka!.. Ndugu hayo ni mahubiri ya shetani anayokuhubiria kichwani pako. Pia usiseme ngoja nitakapostaafu, nitapata muda mwingi wa kumtafuta Mungu..jambo hilo lifute kwenye akili yako kuanzia sasa, “mkumbuke muumba wako kabla kamba ya fedha haijakatika”.

Kwa kadiri muda unavyozidi kwenda ndivyo ile njia inavyozidi kusonga na kuwa nyembamba, wakati uliokubalika ndio huu!, saa ya wokovu ndio sasa. Kumbuka pia hujui siku yako ya kuondoka duniani ni lini!, na yeye anasema mkumbuke kabla roho yako haijamrudia yeye!.

Je upo tayari kumkumbuka leo!, na kusema siutaki tena ulimwengu na tamaa zake zote?.. Pengine umri wako ni mkubwa lakini bado unaisikia hii sauti ikikuambia tubu tubu!.. hiyo ni neema fahamu kuwa ndio upo kipindi cha kumalizia!… muda si mrefu hutaisikia tena! Kwasababu hatuamui sisi kipindi cha kumfuata Yesu, bali neema ya Mungu ndiyo inayoamua juu ya maisha yetu. Ikiisha hiyo, hata tufanyaje hatutaweza kumtafuta Mungu.

Kama upo tayari kumpokea Yesu leo, hapo ulipo jitenge kwa muda mchache, kisha tubu dhambi zako zote kwa Bwana Yesu, na dhamiria kuziacha, kama ni ulevi, uzinzi, wizi, uuaji, uvaaji mbaya, utukuanaji, kamari, na mambo mengine yote yasiyompendeza Mungu, unadhamiria kuacha yote, na baada ya kutubu kwa dhati kabisa, hatua inayofuata ni kwenda kubatizwa, kumbuka ubatizo sahihi ni ule wa maji mengi na kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo kulingana na matendo 2:38, na Roho Mtakatifu ataingia ndani yako kukupa uwezo wa kushinda dhambi, na kukuongoza katika kweli yote.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?

YEZEBELI ALIKUWA NANI

Biblia ituambia tusalimiane kwa busu takatifu. Hili busu ndio lipi?

MTEGO HUTEGWA BURE, MBELE YA MACHO YA NDEGE YE YOTE.

Rudi nyumbani

Print this post

SISI NI WINDO BORA SANA, LA DHAMBI.

Dhambi inafananishwa na mnyama mkali sana wa porini, kama vile simba au chui, au chatu. Utagundua tabia moja waliyonayo hawa wanyama pale wanapowinda ni kuwa hawana papara, Wanakuwa wavumilivu sana mbele ya kitoweo chao, hawakurupuki  ovyo kwa  kuanza kukikimbiza kutokea mbali, hapana, bali utaona wanajisogoza karibu navyo, taratibu na kwa upole sana, na kwa kuvizia,kana kwamba hawana habari navyo, kiasi kwamba yule anayewindwa, hawezi kugundua chochote.. Hadi pale anapokaribiwa sana, na kurukiwa, au kikimbizwa kwa ghafla ndipo anapogundua haa, kumbe adui yangu alikuwa karibu sana na mimi. Akiwa  anajiandaa kukimbia  tayari ameshakamatwa..

Na ndivyo ilivyo dhambi tabia yake, haina papara.. Wakati ule kabla Kaini hajamuua ndugu yake Habili, kuna maneno ambayo Mungu alimwambia, embu tusome..

Mwanzo 4:3 “Ikawa hatimaye Kaini akaleta mazao ya ardhi, sadaka kwa Bwana.

4 Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. Bwana akamtakabali Habili na sadaka yake;

5 bali Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana.

6 Bwana akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana?

7 Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? USIPOTENDA VYEMA DHAMBI IKO, INAKUOTEA MLANGONI, NAYO INAKUTAMANI WEWE, WALAKINI YAPASA UISHINDE,

8 Kaini akamwambia Habili nduguye, [Twende uwandani]Ikawa walipokuwapo uwandani,Kaini akamwinukia Habili nduguye,akamwua.”.

Unaona? Kumbe dhambi ilikuwa imeshamsogelea sana Kaini mlangoni kama chui, lakini yeye hakuiona, ilikuwa inasubiria tu afungue mlango Fulani katika maisha yake, kisha yenyewe imrukie kwa ghafla, na habari yake iwe imekwisha. Hivyo Mungu akamtahadharisha mapema lakini yeye hakusikia, Na kama tunavyosoma biblia, Kaini hakutubu na kugeuka kuachana na mahasira zake na wivu, badala yake, siku moja akamwambia ndugu yake twenda huko maporini, walipofika kule, alishangaa nguvu ya ajabu ya kuua imemwingia ndani yake kwa ghafla, na moja kwa moja, akachukua kisu akamchinja ndugu yake bila hata huruma.

Jiulize swali ni nani alimfundisha Kaini kuua?, hakuna aliyemfundisha bali ni ile dhambi iliyomnasa ndio ilitekeleza hayo yote. Unapoona mauaji ya kikatili yanatekelezwa na watu usidhani kuwa ni akili zao ziliwatuma hivyo,.Unapoona Yuda anakwenda kumsaliti Bwana wake, tena kwa kumbusu macho makavu, usidhani mwanadamu wa kawaida anaweza kufanya kitendo kama kile  hapana, bali dhambi ikishakaba koo, huwezi kunasuka tena, ni sharti utimize mapenzi yake.

Ndugu yangu, leo hii, tabia ya dhambi bado ni ile ile.. Unapohubiriwa utubu dhambi, sio kwa faida ya mchungaji wako, au mwalimu wako, ni kwa faida yako mwenyewe. Kwasababu mimi na wewe sasa hivi tunawindwa vikali sana,..Na kama tutafungua milango yetu kuruhusu kila aina ya dhambi ituchezee tu, tufahamu kuwa mwisho wetu upo mlangoni.

Dhambi ina shinikizo kubwa sana, ikishafanikiwa kukuvaa kama Kaini, au Yuda, ujue hutoki tena, hutajali kifo, hutajali chochote. Kama unaendelea kutoka nje ya ndoa yako, kumbuka upo hatarini kufa, kama unazini zini ovyo, ujue dhambi imeshakuandalia mauti yako. Hatujui itakuwa ni kwa njia ya ukimwi, au kifo, au mapepo, lakini safari yako ipo ukingoni.

Hatupaswi kumwogopa shetani hata kidogo, lakini tunapaswa tuiogope dhambi kweli kweli. Kwasababu yeye ndio yule mnyama atuwindaye. Shetani kazi yake ni kututengenezea mazingira ya sisi kunaswa na dhambi, lakini yeye hana nguvu yoyote ya kukushinda.

Hivyo, tuwe makini, kama hujatubu, ni heri ukatubu sasa, na sio kesho. Hakuna wokovu wa kesho au ule wa “siku moja nitaokoka”. Wokovu wa namna hiyo haupo, wala hautakaa uje milele. Tubu mpendwa ukabatizwe, ukaoshwe dhambi zako, upokee na Roho Mtakatifu, hizi si zama za kutanga tanga na huu ulimwengu wa dhambi, mitandao inawaharibu watu wengi sana. Yesu alituambia, tumkumbuke mke wa Lutu. Tukitaka kuziponya nafsi zetu tutaziangamiza, na tukiziangamiza kwa ajili yake tutaziponya.

Acha mambo ya dunia yakupite, acha fashion zikupitie, acha anasa zikupite, ipoteze nafsi yako kwa Mungu, lakini mwisho wa siku utapona, kuliko kuupata ulimwengu mzima halafu baadaye unakwenda kuzimu milele itakusaidia nini?. Dhambi ni mnyama katili sana.

Bwana atusaidie sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

SI KWA UWEZA WALA KWA NGUVU BALI KWA ROHO YANGU, ASEMA BWANA.

NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.

Je aliyezungumza na Musa kule jangwani ni Mungu mwenyewe au malaika wake?

Je aliyezungumza na Musa kule jangwani ni Mungu mwenyewe au malaika wake?

 

UTAKUWA MTORO NA MTU ASIYE NA KIKAO DUNIANI.

HUDUMA YA UPATANISHO.

Rudi nyumbani

Print this post

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)

Karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu, ambalo ndio taa iongozayo miguu yetu, na mwanga wa njia yetu. Tumekwisha kuvipitia vitabu 20 vya mwanzo, hivyo kama hujavipitia basi ni vyema ukavipitia kwanza, ili tuweze kwenda pamoja katika vitabu hivi vinavyofuata.

Leo tutavitazama vitabu vitatu vya mbele, ambavyo ni Mithali, Mhubiri na Wimbo ulio bora. Vitabu hivi vitatu vimeandikwa na mtu mmoja anayeitwa Sulemani, katika majira tofauti tofauti. Kitabu cha Mithali na Wimbo ulio bora viliandikwa na Sulemani katika kipindi cha ujana wake, lakini kitabu cha Mhubiri alikiandika karibia na mwisho wa maisha yake. Hivyo leo tutakitazama kimoja baada ya kingine. (Lakini pia kabla ya kwenda kuvitazama ni vyema ukaavipitia wewe mwenyewe binafsi, ndipo uufuatilie ufupisho huu)

  1. Kitabu cha Mithali:

Kitabu cha Mithali kama tulivyosema ni kitabu kilichoandikwa kwa sehemu kubwa na Mfalme Sulemani na alikiandika katika ujana wake.. Zipo sehemu chache za kitabu hicho zilizoandikwa na Mtu aliyeitwa Aguri, na mfalme Lemueli (Mithali 30 na Mithali 31), lakini Kwingine kote kuliandikwa na Mfalme Sulemani.

 Ikumbukwe kuwa Sulemani, alimwomba Mungu hekima badala ya mali, na hivyo Mungu akampa vyote viwili, hekima pamoja na Mali ambazo hakuziomba (1Wafalme 3:11). Na hekima ni neno la kiujumla lenye maana ya “akili, na uwezo wa kupambanua mambo”. Na kuna hekima ya kiMungu na hekima ya kiulimwengu!. Sulemani alipewa hekima zote mbili! (Za kiMungu na za kiulimwengu).

Hekima za Kiulimwengu, zinamwezesha mtu aweze kuishi maisha ya mafanikio katika huu ulimwengu! Jinsi ya kutumia malighafi za ulimwengu huu, kufanikisha mambo yake. Kwamfano  watu waliogundua gari, au ndege, au simu wametumia hekima ya kiulimwengu kugundua vitu hivyo, ili viwasaidie katika changamoto za usafiri, na mawasiliano, kadhalika walioweka Methali kama “Asiyefunza na mamaye hufunzwa na ulimwengu” au “asiyesikia la mkuu, huvunjika guu” au “mtoto akililia wembe,mpe umkate”.. wametumia hekima za kibinadamu kujiwekea tahadhari wao na watoto wao, kiasi kwamba mtu yeyote akiisikia hiyo hekima na kuitii basi hatafunzwa na ulimwengu!. Sasa hekima kama hiyo sio hekima ya kiMungu, bali ya kiulimwengu lakini ina ukweli ndani yake.

Kwahiyo Mfalme Sulemani alipewa hekima za aina zote mbili (za KiMungu na za kiulimwengu). Ni muhimu kuufahamu huu msingi kwasababu, utatusaidia huko mbele kuelewa kwanini Sulemani alisema hekima zilimpoteza…(kwamba hazikuwa za kiMungu zilizompoteza bali za kiulimwengu).

Hivyo kwa akili nyingi Sulemani alizopewa na Mungu aliweza kutazama watoto, akatunga mithali za kidunia na kiMungu kuwahusu wao, vile vile aliweza kutazama watu wazima na wazee akatunga mithali kuhusu wao, kadhalika aliweza kutazama wafanya biashara akaweza kutunga mithali na kutunga mashauri kuwahusu wao na vile vile aliweza kutazama maisha ya watu waovu na wema, wapumbavu na werevu, pamoja na viumbe kama wanyama na miti, akatunga mithali juu ya hivyo vyote na akawapa wana wa Israeli wazitumie katika kuendesha maisha yao..

1Wafalme 4:29 “Mungu akampa Sulemani hekima, na akili nyingi sana, na moyo mkuu, kama mchanga ulioko pwani.

 30 Hekima ya Sulemani ikapita hekima ya wana wote wa mashariki, na hekima zote za Misri.

 31 Kwa kuwa alikuwa na hekima kuliko watu wote; kuliko Ethani Mwezrahi, na Hemani, na Kalkoli, na Darda, wana wa Maholi; zikaenea sifa zake kati ya mataifa yote yaliyozunguka.

 32 Naye akanena mifano elfu tatu, na nyimbo zake zilikuwa elfu moja na tano.

 33 Akanena habari za miti tangu mwerezi ulioko Lebanoni hata hisopo umeao ukutani; pia akanena habari za wanyama, na za ndege, na vitambaavyo, na samaki.

34 Wakaja wa mataifa yote ili waisikie hekima ya Sulemani, toka wafalme wote wa ulimwengu, waliokuwa wamepata habari za hekima yake”

Sasa kwa uwezo huo Mungu aliompa Sulemani na akili hizo, alijikuta anaweza kufanya biashara na kufanikiwa sana kwasababu alipewa akili za jinsi ya kuendesha biashara na zikafanikiwa, (Hicho ndio kilikuwa chanzo cha utajiri wa Sulemani), biblia inasema Sulemani alifanya biashara sana… Alifahamu siri nyingi za jinsi ya kufanya biashara na kufanikiwa!, mpaka wafalme wa dunia wakawa wanamfuata kutaka kujua anafanyaje fanyaje mpaka anafanikiwa…(hakuwa amekaa tu! Na kujikuta mali zinamjia, hapana bali alikuwa ni mtu mwenye uwezo mkubwa wa akili wa jinsi ya kutafuta mali).

1Wafalme 10:22 “Kwa kuwa mfalme alikuwa na merikebu za Tarshishi baharini pamoja na merikebu za Hiramu; mara moja katika miaka mitatu huja merikebu za Tarshishi, zikileta dhahabu, na fedha, na pembe, na nyani, na tausi.

23 Basi mfalme Sulemani akawapita wafalme wote wa duniani kwa mali, na kwa hekima.

24 Ulimwengu wote ukamtafuta Sulemani uso wake, ili waisikie hekima yake, Mungu aliyomtia moyoni.  25 Wakaleta kila mtu zawadi yake, vyombo vya fedha, na vyombo vya dhahabu, na mavazi, na silaha, na manukato, na farasi, na nyumbu, hesabu yake ya mwaka kwa mwaka.

26 Sulemani akakusanya magari na wapandao farasi; naye alikuwa na magari elfu na mia nne, na wapandao farasi kumi na mbili elfu, aliowaweka katika miji ya magari, na pamoja na mfalme huko Yerusalemu.

 27 Mfalme akafanya fedha humo Yerusalemu kuwa kama mawe, na mierezi akaifinya kuwa kama mikuyu iliyomo Shefela, kwa kuwa mingi.

28 Nao farasi aliokuwa nao Sulemani wakaletwa toka Misri; wakapewa wafanya biashara wake mfalme kwa makundi, kila kundi na thamani yake.

29 Tena gari huja kutoka katika Misri kwa shekeli mia sita za fedha, na farasi mmoja kwa mia hamsini; vivyo watu wakawaletea wafalme wote wa Wahiti, na wafalme wa Shamu, mikononi mwao”.

Vile vile Sulemani alikuwa na akili nyingi za “Jinsi ya kushinda vita”. Tofauti na wafalme wengine ambao jambo kidogo tu likizuka suluhisho ni kwenda vitani!.. Sulemani hakuwa hivyo, aliweza kutatua mambo kwa hekima tu!..Hivyo ikamfanya kuwa Mfalme katika Israeli ambaye hakuwahi kwenda vitani kupigana pigana hovyo!, hivyo uchumi wake ukastawi na watu wake!. Baba yake Daudi hakuwa na hiyo hekima!, yeye lolote likitokea kwamba maadui zake wamepanga vita, basi na yeye alipanga vita!, pasipo kufikiri sana njia mbadala ya kuvimaliza hivyo vita. Lakini Sulemani Mungu alimpa hiyo hekima..hakupigana vita katika ufalme wake wote na aliishi kwa amani.

Vile vile hakupungukiwa chakula wala mifugo, kwasababu alikuwa na akili za jinsi ya kuiongeza hiyo mifugo. Na aliyatimiza malengo yake hayo kwa kuwalazimisha watu wake kufanya kazi kwa nguvu (Israeli hawakupumzika), walifanyishwa kazi sana. (1Wafalme 12:4),

Kwa muhtasari huo basi, tutakuwa tumeshaanza kujua ni nini kimeandikwa katika kitabu cha MITHALI. Kwamba ni kitabu kilichojaa hekima za kiMungu na hekima za kidunia.

Hivyo tunaweza kukigawanya kitabu cha Mithali katika makundi hayo mawili.

  1. Mifano ya hekima za kiMungu, zilizoandikwa na Sulemani ndani ya kitabu cha Mithali

Mithali 1:7“Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu”.. Mithali kama hii haiwezi kukubaliwa na wenye hekima ya ulimwengu huu…

Mithali 18:10 “Jina la Bwana ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia, akawa salama”.

Soma pia Mithali 19:23, Mithali 16:5, Mithali 3:11 n.k

  1. Mifano ya hekima za kiulimwengu, Sulemani alizoziandika ingawa zina ukweli ndani yake ni kama ifuatavyo..

Mithali 5:6 “Ewe mvivu, mwendee chungu, Zitafakari njia zake ukapate hekima.

 7 Kwa maana yeye hana akida, Wala msimamizi, wala mkuu,

 8 Lakini hujiwekea akiba ya chakula wakati wa jua; Hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.

 9 Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaondoka lini katika usingizi wako?

Mithali12: 27 “Mtu mvivu hapiki mawindo yake; Bali mwenye bidii anazo mali za thamani”

Mithali 18:18 “Kura hukomesha mashindano; Hukata maneno ya wakuu”

Mithali 19: 7 “Ndugu zote wa maskini humchukia; Jinsi gani rafiki zake huzidi kujitenga naye! Huwafuata kwa maneno, lakini wametoweka”

Mithali 27: 7 “Nafsi iliyoshiba hukinai sega la asali; Bali nafsi yenye njaa huona kila kitu kichungu kuwa kitamu”.

Soma pia Mithali 26:13, Mithali 26:20 n.k

Ni jambo gani tunajifunza katika kitabu cha Mithali?

Jambo kuu na la kwanza tunalojifunza ni hekima za KiMungu, ambazo zinatupeleka moja kwa moja kumpenda Mungu, kumtafuta, na kumtumikia. Kadhalika pia tunajifunza hekima za kidunia, ambazo zitatusaidia katika maisha yetu ya hapa duniani, hayo ndiyo mambo mawili makuu, tunayoweza kujifunza katika kitabu hichi.

  1. KITABU CHA WIMBO ULIOBORA.

Kama jina lake lilivyo “wimbo ulio bora”.. maana yake kuna nyimbo nyingi..lakini upo ulio bora!.. Zamani na hata sasa, nyimbo zilitungwa kwa lengo pia la kufikisha ujumbe!.. Na mara nyingi nyimbo zinakuwa ni jambo fulani la kama igizo lakini limebeba ujumbe Fulani ndani yake.. Sasa Sulemani alitunga nyimbo nyingi, biblia inasema alitunga nyimbo elfu moja na tano (1005), zinazohusu miti, mimea, maisha ya watu (soma 1Wafalme 4:30) lakini katika hizo zote, alikuwa na wimbo mmoja ambao aliuona ni bora kuliko mwingine wote.. Na huo ndio tunaousoma katika kitabu hicho cha Wimbo ulio bora.. (Ni wimbo unaomhusu Mtu na Mpenzi wake).

Hata sasa nyimbo zinazoonekana ni bora na watu wa kidunia ni nyimbo zinazohusu mahusiano zinazidi sana nyimbo za kawaida za kuelimisha au za Taifa. Kwanini?…kwasababu shetani naye anajua “wimbo ulio bora”

Hivyo kitabu cha Wimbo ulio bora ni kitabu chenye mashairi na Mwanaume mmoja, anayemsifia mke wake (yaani bibi arusi wake), na vile vile bibiarusi anamsifia mume wake.. kwa ufupi ni kitabu chenye mpangilio wa mashairi na majibizano, baina watu wawili, mume na mke. Na kimegawanyika katika sehemu kuu tatu. (Uchumba, ndoa changa na Ndoa iliyokomaa).

Kuanzia Mlango wa 1-3, inazungumzia mazungumzo ya wapenzi hao wakiwa bado katika hatua ya uchumba, Kuanzia Mlango wa 3 hadi wa 5, ni mazungumzo ya wapenzi hao wawili wakiwa tayari ndani ya ndoa, na kuanzia Mlango wa 5-8 ni Mazungumzo ya wapenzi hao wakiwa katika kilele cha ndoa yao.

Kitabu hichi kwa namna ya kimwili kinahubiri sana sana upendo kwa wana-ndoa, Maana yake watu waliofunga ndoa, kitabu hichi kimejaa maonyo na mafundisho kuwahusu wao(Jinsi inavyowapasa kupendana na kutunzana). Vile vile kimejaa maonyo na mashauri kwa watu ambao bado hawajaingia kwenye ndoa..kwamba wasiyaamshe mapenzi wala kuyachochoe mpaka wakati wake utakapofika.

Wimbo 2:7 “Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Kwa paa na kwa ayala wa porini, Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe”.

Mbali na mafunzo tunayoyapata kuhusu wana ndoa na wale ambao hawayaingia bado kwenye ndoa, Mungu aliruhusu pia kitabu hiki kiwepo miongoni mwa vitabu vya biblia, na kiitwe wimbo uliobora kwasababu katika roho pia Kuna wimbo ulio bora ambao Mungu analiimbia kanisa lake!!, na kanisa vile vile kanisa linamwimbia yeye.

Ikumbukwe kuwa katika roho kanisa la Yesu linafananishwa na bibiarusi, na Kristo ndiye Bwana arusi mwenyewe..(soma 2Wakorintho 11:2, Ufunuo 21:9, Yohana 3:29), Kwahiyo upo wimbo unaoimbwa katika roho sasa, wimbo wa Bwana arusi kumrejesha mkewe, Bwana anawaita watu wake sasa, kwa sauti ya upole, na ya upendo kwa mashairi mazuri, anawaita watu katika hatua zote tatu…(hatua kabla ya kumpokea yeye, hapo ndio pale Bwana anamtumia mtu wahubiri wa kumvuta kwake, na mtu Yule anapotii, basi Bwana anakwenda naye katika hatua ya pili ya ndoa, hapo ndio pale mtu anapoamua kumpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yake na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu, na baada ya hatua hiyo, Mungu anamwongoza katika hatua nyingine ya mwisho ya kukua kiroho..

Ni nini tunajifunza katika kitabu cha Wimbo ulio bora?

Cha kwanza ni kwamba sisi (kanisa) tuliompokea tunafananishwa na bibi-arusi wa Yesu, na kama ni bibiarusi maana yake hatupaswi kuudharau wito wake, unapotuita…ambao umekuwa kama wimbo kwetu!..vile vile tunapaswa tuushikilie wokovu na kudumu katika huo, kwasababu uhusiano wetu na Mungu wetu hauishii tu katika kumwamini, bali pia katika kudumu katika imani(ndio kudumu katika ndoa)….na hatupaswi kufanya uasherati, ukifanya uasherati wa kiroho kwa kumwacha Mungu na kwenda kuabudu miungu mingine, tukifanya hivyo basi tunamtia Bwana wivu..na wivu wa kimahusiano ni mbaya kuliko mwingine wowote ule.. kama yeye mwenyewe alivyosema

Wimbo 8: 6 “…Kwa maana upendo una nguvu kama mauti, Na wivu ni mkali kama ahera. Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni miali ya Yahu”.

Pia tunajifunza kuwa na upendo na kuwa waaminifu kwa wapenzi wetu, tuliofunga nao ndoa!..

Na mwisho kitabu hichi kinawafunza wale ambao bado hawajaingia kwenye ndoa!, kwamba wasiyachochee mapenzi, kuyachochea mapenzi ni pamoja na kutazama picha chafu (pornography), kutazama filamu za kidunia ambazo nyingi sehemu kubwa zina maudhui ya mapenzi, vile vile kuzungumza mazungumzo machafu na kuwa na kampani ya watu ambao muda wote mada zao ni uasherati, hivyo ndio baadhi ya vichocheo vya mapenzi, ambavyo mwisho wake ni kuanguka katika uasherati na uzinzi.

  1. KITABU CHA MHUBIRI

Hichi ndio kitabu cha mwisho kilichoandikwa na Sulemani. Sulemani alikiandika kitabu hichi katika uzee wake..na ni kitabu cha hitimisho na kutoa jumla ya mambo yote!.. baada ya yeye kujaribu mambo yote, kuzipima hekima zote za kidunia, kufanya biashara nyingi na kufanikiwa, kujiongezea mali nyingi kuliko watu wote waliotangulia…mwisho wa siku anakuja na hitimisho!..na hitimisho hilo analiandika kama mahubiri!.. Anawahubiri wana wa Israeli.. anasema..

Mhubiri 1:1 “Maneno ya Mhubiri mwana wa Daudi, mfalme katika Yerusalemu.

 2 Mhubiri asema, Ubatili mtupu, ubatili mtupu, mambo yote ni ubatili.

3 Mtu ana faida gani ya kazi yake yote aifanyayo chini ya jua”

Anaendelea kwa kusema..

Mhubiri 1:12 “Mimi, Mhubiri, nalikuwa Mfalme wa Israeli katika Yerusalemu.

13 Nikatia moyo wangu ili kuyatafuta yote yanayotendeka chini ya mbingu, na kuyavumbua kwa hekima; ni taabu kubwa ambayo Mungu amewapa wanadamu, ili kutaabika ndani yake.

14 Nimeziona kazi zote zifanywazo chini ya jua; na, tazama, MAMBO YOTE NI UBATILI NA KUJILISHA UPEPO.

15 Yaliyopotoka hayawezi kunyoshwa, Wala yasiyokuwapo hayahesabiki.

16 Nikatafakari nikisema, Nimejipatia hekima nyingi kupita wote walionitangulia katika Yerusalemu; naam, moyo wangu umeona kwa wingi hekima na maarifa.

17 Nikatia moyo wangu ili kuijua hekima, na kujua wazimu na upumbavu; nikatambua ya kwamba hayo yote nayo ni kujilisha upepo.

18 YAANI, KATIKA WINGI WA HEKIMA MNA WINGI WA HUZUNI, Naye aongezaye maarifa huongeza masikitiko”.

Ukikitafakari kwa makini maneno hayo, utaona ni maneno ya kama mtu ambaye alikuwa anatamani jambo Fulani sana, kisha akalipata hilo jambo, halafu mwisho wa siku akaja kuliona kuwa si la maana sana kama alivyolitazamia!..

Kama tulivyojifunza mwanzo Sulemani alipewa hekima ya kiMungu na pia ya kidunia, hivyo kwa akili zake nyingi aliweza kuvumbua njia nyingi za kufanya biashara, na kufanikiwa.. akawa mwanauchumi mkubwa mpaka watu wa mataifa mengine wakaja kutaka kujua siri ya mafanikio yake, hata akapendwa na wanawake wengi wa kiulimwengu, na yeye pia akawapenda, na mwisho wa siku wakaja kumgeuza moyo,.. hivyo hekima za kidunia zikampotosha Sulemani, hata akamsahau Mungu na kusahau kufanya mema.. akazitumainia hekima zake za kidunia.

 Lakini alipokuwa mzee akagundua kuwa siku moja atakufa!, na mwingine atakuja kuvirithi hivyo vyote!.. na kama akifa na huku moyoni mwake hana utajiri kwa Mungu!.. ni sawa na kazi bure!..ni kujilisha upepo tu!!..hakuna faida yoyote ya yeye kuwa na kila kitu halafu anakuwa hajajaa mema??

Mhubiri 2:1 “Nikauambia moyo wangu, Haya, nitakujaribu kwa njia ya furaha basi ujifurahishe kwa anasa. Na tazama, hayo nayo yakawa ubatili.

 2 Nikasema juu ya kicheko, Ni wazimu; na juu ya furaha, Yafaa nini?

3 Moyoni mwangu nikapeleleza jinsi ya kuuburudisha mwili kwa mvinyo, na (moyo wangu ukali ukiniongoza kwa hekima) jinsi ya kushikana na upumbavu, hata niyaone yaliyo mema ya kuwafaa wanadamu, ili wayafanye hayo chini ya mbingu siku zote za maisha yao.

 4 Nikajifanyizia kazi zilizo kubwa; nikajijengea nyumba; nikajipandia mashamba ya mizabibu;

 5 nikajifanyizia bustani na viunga, na kuipanda humo miti yenye matunda ya kila namna;

 6 nikajifanyizia birika za maji, ya kuunyweshea mwitu mlimopandwa miti michanga.

 7 Nami nikanunua watumwa na wajakazi, nikawa na wazalia nyumbani mwangu; tena nikawa na mali nyingi za ng’ombe na kondoo, kupita wote walionitangulia katika Yerusalemu;

 8 tena nikajikusanyia fedha na dhahabu, na tunu za kifalme na za kutoka katika majimbo. Nikajipatia waimbaji, waume kwa wake, nao wale ambao wanadamu wanawatunuka, masuria wengi sana.

9 Basi nikawa mkuu, nikaongezeka kupita wote walionitangulia katika Yerusalemu; pia hekima yangu nikakaa nayo.

 10 Wala sikuyanyima macho yangu cho chote yalichokitamani; wala sikuuzuia moyo wangu katika furaha yo yote; maana moyo wangu ulifurahi kwa sababu ya kazi yangu yote, na hii ilikuwa sehemu yangu katika kazi yangu yote.

 11 Kisha nikaziangalia kazi zote zilizofanywa kwa mikono yangu, na taabu yote niliyotaabika katika kuzitenda; na tazama, yote ni ubatili na kujilisha upepo, wala faida hakuna chini ya jua”.

Ukiendelea kusoma kitabu hicho utaona Sulemani, anauchukia mpaka uhai.. anaona hakuna faida yoyote kujitumainisha katika hekima ya kidunia, ambayo hapo kwanza alikuwa anaiona ya maana!.. Magari, na majumba aliyokuwa anayatafuta!, mwisho wa siku anakuja kusema ni upumbavu yote!.. wanawake wengi aliokuwa anawatafuta mwisho wa siku anakuja kujuta anasema ni upumbavu!..biashara anazozifanya anakuja kusema ni kujilisha upepo!… Maana yake ni kwamba laiti kama angerudishwa nyuma, angefanya marekebisho makubwa sana!.. lakini tayari kashakuwa mzee, hivyo anatoa mahubiri wa Israeli.. anawashauri jambo jema la kutafuta!.. kwamba si hekima ya kidunia bali wamtafute Bwana..

Mhubiri 12:8 “Mhubiri asema, Ubatili mtupu; mambo yote ni ubatili!

9 Walakini, kwa sababu huyo Mhubiri alikuwa na hekima, aliendelea kuwafundisha watu maarifa, naam, akatafakari, akatafuta-tafuta, akatunga mithali nyingi.

 10 Huyo Mhubiri akatafuta-tafuta ili apate kuona maneno yapendezayo, na yale yaliyoandikwa kwa unyofu, yaani, maneno ya kweli.

 11 Maneno yao wenye hekima huwa mfano wa michokoo; na kama misumari iliyogongomewa sana; ndivyo yalivyo maneno yao walio wakuu wa makusanyiko, ambayo yatoka kwa mchungaji mmoja.

12 Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; na kusoma sana huuchosha mwili.

13 HII NDIYO JUMLA YA MANENO; YOTE YAMEKWISHA SIKIWA; MCHE MUNGU, NAWE UZISHIKE AMRI ZAKE, MAANA KWA JUMLA NDIYO IMPASAYO MTU.

 14 KWA MAANA MUNGU ATALETA HUKUMUNI KILA KAZI, PAMOJA NA KILA NENO LA SIRI, LIKIWA JEMA AU LIKIWA BAYA”.

Umeona hapo jumla ya mambo yote Sulemani anayoitoa??….Anasema Mche Bwana na uepukane na uovu!.. hasemi tafuta mali, hasemi tena wala hashauri watu kutafuta utajiri, wala hagusii hekima yoyote ya kiulimwengu, bali anahitimisha kwa kusema maneno hayo mawili tu!!!..” MCHE MUNGU, NAWE UZISHIKE AMRI ZAKE, MAANA KWA JUMLA NDIYO IMPASAYO MTU”

Je! Unamcha Mungu na kuzishika amri zake?.. Huyu ni Sulemani ambaye alikuwa ni tajiri kupita sisi, ambaye ameonja kila kitu, ndio anahitimisha hivi, kashatusaidia kufanya utafiti, hatuhitaji tena sisi kufanya utafiti, yeye kafanya utafiti wa kupata mali nyingi na mwisho wa siku kaona ni ubatili!, na kujilisha upepo!.. basi na sisi hatuna haja ya kurudia hayo hayo, kwamaana tukirudia hayo hayo mwisho wa siku tutafika kwenye jibu hilo hilo la Sulemani, na wakati huo tutakuwa tumeshapoteza muda wa kutosha.

Bwana Yesu ambaye alikuwa na hekima kuliko Sulemani alisema maneno haya..

Marko 10: 24  “Wanafunzi wakashangaa kwa maneno yake. Yesu akajibu tena, akawaambia, Watoto, jinsi ilivyo shida wenye kutegemea mali kuingia katika ufalme wa Mungu!

25  Ni rahisi ngamia kupenya katika tundu ya sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu”

Na tena akasema..

Marko 8:36 “ Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake?

37  Ama mtu atoe nini badala ya nafsi yake?

38  Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu”.

Imemfaidia nini Sulemani kuwa na hekima za kufanya biashara kuliko watu wote duniani, halafu hekima hizo zimekuja kumfanya akengeuke na kuabudu miungu mingine mwishoni?.. Ndio maana mwisho anasema na kutushauri kuwa ni ubatili hayo yote..tusiyatafute hayo!..kwasababu tutakufa na kuyaacha..bali tuutafute kwanza kutenda mapenzi ya Mungu hapa duniani.

Ndugu kama hujampokea Yesu, huu ndio wakati wako sasa wa kufanya hivyo, Yesu yupo mlangoni, Utafutaji wa mali usikusonge hata ukajikuta unaikosa mbingu!, kiungo chako kimoja kikikukosesha kikate!.. Ni heri ukose mali nyingi lakini uingie mbinguni kuliko upate dunia nzima halafu ukose uzima wa milele.

Hivyo kama hujaokoka!, hapo ulipo tubu, na kisha tafuta ubatizo sahihi ambao ni wa maji mengi na kwa jina la Yesu, na baada ya hapo Roho Mtakatifu atakuongoza katika kweli yote.

Maran atha!

Usikose mwendelezo wa vitabu vinavyofuata!!!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Nini maana ya “katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni”.

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

Nini maana ya “Mwenye hekima huvuta roho za watu”.

Pambaja ni nini katika Biblia kama tunavyosoma katika kitabu cha Wimbo ulio bora 1:2?

Rudi nyumbani

Print this post

INAYOENDELEA SASA NI HUDUMA YA RUTHU.

Ukweli ni kwamba hatuishi tena wakati wa mavuno, kama ilivyokuwa kipindi cha mitume. Bali tunaishi wakati wa makusanyo ya masazo. Utauliza ni kwa namna gani?

Zamani kulingana na desturi za wayahudi kulikuwa na makundi mawili ya watendaji kazi shambani, kundi la kwanza ni lile lililoajiriwa rasmi kwa kazi ya uvunaji, hilo lilikuwa linatangulia mwanzoni kabisa mwa uvunaji, na lilikuwa linavuna kila kitu kilichoonekana mbele yao.. Hivyo mpaka wafike mwisho wa shamba, walikuwa na magunia kwa magunia ya mavuno. Lakini pamoja na kuwa wanafanikiwa  kuvuna mavuno mengi, bado hawakuweza kumaliza kila kitu shambani.

Hapo ndipo linaporuhusiwa kundi la pili la wavunaji, sasa tabia ya hili kundi la pili ni kuwa lenyewe linatembea likizunguka zunguka kwenye shamba lote, kuangalia walau kama kuna kitu kimebakishwa na wavunaji nyuma, wakichukue wakatumie kwa ajili ya matumizi yao na chakula. Watu hawa waliokuwa ni  wale maskini waliokuwa wanaishi katika nchi na wageni  (Walawi 19:9)..Kazi yao ilikuwa ni ngumu kwasababu walikuwa wanaweza kuzunguka shamba nzima lenye ekari hata 100 wakaumbulia tu kadebe kamoja cha mahindi, kwasababu mavuno mengi yalishavunwa na wanavunaji wa kwanza.

Ruthu alikuwa ni mmojawapo wa hili kundi la pili la wavunaji. Wakati ule utaona alikwenda kukusanya masazo hayo katika shamba la tajiri mmoja aliyeitwa Boazi.

Ruthu 2:2 “Naye Ruthu Mmoabi akamwambia Naomi, Sasa niende kondeni, niokote masazo ya masuke nyuma yake yule ambaye nitaona kibali machoni pake. Akamwambia, Haya, mwanangu, nenda.

3 Basi akaenda, akaja akaokota masazo kondeni nyuma ya wavunaji; na bahati yake ikamtukia kwamba akaifika sehemu ya shamba iliyokuwa mali yake huyo Boazi, ambaye alikuwa wa jamaa yake Elimeleki.

4 Na tazama, Boazi akaja kutoka Bethlehemu kawaamkia wavunaji, akasema, Bwana akae nanyi. Nao wakamwitikia, Bwana na akubariki”.

Sasa kibiblia Wavunaji wa kwanza waliwawakilisha mitume wa Bwana. Na ndio maana utakumbuka wakati ule, wakihubiri injili kidogo tu, idadi ya maelfu ya watu ilikuwa inakuja kwa Kristo ndani ya siku moja.. Hiyo ni kuonyesha kuwa hao ndio waliokuwa wavunaji, Mungu aliowachagua.

Lakini leo hii hujiulizi licha ya kuwa kila mtu ameshasikia habari za Kristo, ameshasoma mafundisho ya mitume kwenye biblia takatifu, ameshaona miujiza mingi Kristo aliyotenda, lakini bado hawageuki, wala hawana mpango wa kutubu..hata ikitokea wamegeuka basi ni mmoja kati elfu.. Hiyo ni kuonyesha kuwa hakuna mavuno tena shambani.

Wanaopita leo hii ni akina Ruthu,(ambao ndio watumishi wa Mungu wa wakati huu) kukusanya masalio machache sana..Vinginevyo kama yasingekuwepo hadi wakati huu, Mungu angeshakuwa ameshauangamiza ulimwengu wote kwa moto. Soma

Isaya 1:9 “Kama Bwana wa majeshi ASINGALITUACHIA MABAKI MACHACHE SANA, tungalikuwa kama Sodoma, tungalifanana na Gomora”.

Ndugu kama wakati wa mavuno ya kwanza ulikupita, basi usifanye mchezo na huu wakati wa mwisho wa masalia tuliobakiwa nao, Ni neema kubwa sana tumepewa sisi, vinginevyo habari yetu ilikuwa tayari imeshakwisha..Si unakumbuka hili andiko linavyosema..

Yeremia 8:20 “Mavuno yamepita, wakati wa hari umekwisha, wala sisi hatukuokoka”.

Umeona? Lakini Mungu ameahidi yatakuwepo masalia machache sana…

Lakini hivi karibuni huduma ya Ruthu, inakwenda kuisha. Boazi wetu ambaye anamwakilisha YESU KRISTO, anakaribia kurudi shambani mwake, kukagua kazi yake.

Kristo atakaporudi, katika awamu hii, halafu akakuta bado hujaingia ghalani mwake, Ujue, adhabu yako itakuwa ni kubwa sana kwenye lile ziwa la moto siku ile. Kwasababu umejua likupasalo kutenda na hujatenda kwa wakati..

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana.

48 Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, atapigwa kidogo. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na Zaidi”.

Unangoja nini? Unasubiri nini usimgeukie Kristo. Huu ulimwengu hauna muda mrefu sana, Kristo yupo mlangoni kurudi, dalili zote zinaonyesha, mwisho umefika, Tubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa, kubali kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kwa jina la Yesu Kristo upate ondoleo la dhambi zako. Na Bwana akutie muhuri kwa Roho wake Mtakatifu, ili uwe salama katika nyakati hizi za hatari.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

JE! UNAIONA ILE NCHI NZURI YA KUMETA-META MBELE YAKO?

SINA PESA SASA, YESU ATANISAIDIA NINI?

JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI, AU KUTOA TALAKA?

Rudi nyumbani

Print this post

Zeri ya Gileadi ni nini?

Zeri ni dawa ambayo ilikuwa inakamuliwa kutoka katika aina Fulani ya mmea uliokuwa unapatikana sana sana huko Gileadi. Kwasasa haujulikani mmea huo ulikuwa hasaa ni wa aina gani, kama ni mti au jani, lakini biblia inachoeleza ni thamani yake na  sifa zake katika kuponya.

Ukisoma katika biblia kipindi kile wale watoto wa Yakobo walipomuuza ndugu yao kwa wale waarabu waishmaeli, biblia inatuambia, katika safari yao ya biashara ya kwenda Misri walikuwa wamebeba na Zeri pia.

Mwanzo 37:25 “Nao wakakaa kitako kula chakula; wakainua macho yao, wakaona, msafara wa Waishmaeli wanakuja wakitoka Gileadi na ngamia zao, wakichukua ubani na zeri na manemane, wakisafiri kuvichukua mpaka Misri”.

Lakini ukisoma pia kitabu cha Yeremia sura ya 8 inaeleza jinsi Yeremia alipokuwa akiwalilia ndugu zake wayahudi kwa jinsi watakavyochukuliwa na wababiloni mateka, Na ndio katika kulia kwake akisema Je! Kuna zeri ya Gileadi awapake watu wake ili waponywe na majeraha hayo makubwa  yatakayowapata.. Akimaanisha kama kuna tiba yoyote nzuri ya rohoni, itakayowaponya watu wake na msiba huo mkubwa utakaowakuta mbeleni.

Yeremia 8:21 “Kwa sababu ya maumivu ya binti ya watu wangu nimeumia mimi; nimevaa kaniki; ushangao umenishika.

22 Je! Hapana zeri katika Gileadi? Huko hakuna tabibu? Mbona, basi, haijarejea afya ya binti ya watu wangu”?

Ukisoma, tena ile sura ya 46 Utaona Mungu anawaambia waisraeli kwa kinywa hicho hicho cha Yeremia kwamba wakachukue Zeri ya Gileadi ili wajipake, kwasababu wamejiharibu kupitiliza, kwa makosa yao mengi.

Yeremia 46:11 “Panda uende Gileadi, ukatwae zeri, Ee binti, bikira wa Misri; unatumia dawa nyingi bure tu; hupati kupona kamwe”.

Soma pia Yeremia 51:8, Ezekieli 27:17 utakutana na Neno hilo.

 Lakini tunajua, Mungu hakumaanisha, Zeri kama dawa ya mitishamba, ndio ingewaponya watu wake, kwa dhiki zao, na dhambi zao, hapana. Bali alikuwa anamaanisha Zeri ya Rohoni.

Na huyo si mwingine Zaidi ya BWANA wetu YESU KRISTO. Yeye ndiye tiba ya kweli. Akimganga mtu amemganga kweli kweli roho yake, na vilevile hata mwili wake, anaponyeka kweli kweli.

1Petro 2:24 “Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa”.

Upendo wa kweli upo kwa Kristo, tumaini la kweli lipo kwake, furaha ya kudumu inatoka kwake.

Je! Umempokea Kristo maishani mwako? Au unategemea Zeri  nyingine zikuponye? Kumbuka fedha haiwezi kuiponya roho yako, mke hawezi kuyaponya hayo majeraha yaliyoko ndani yako,, Ndugu, au rafiki hawezi kuzifuta hizo hatia zilizouchafua moyo wako. Ni Yesu Kristo tu peke ndiye anayeweza kufanya hivyo?

Mpokee Leo ayageuze maisha yako.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

SIFONGO NA SIKI NI NINI?

Hisopu/ Hisopo ni nini katika biblia?(Zaburi 51:7)

NI LAZIMA KUISHIKILIA IMANI MPAKA MWISHO.

INJILI YA MANENO LAINI ITAKUGHARIMU.

Aina za dhambi

Rudi nyumbani

Print this post

JE! UNAIONA ILE NCHI NZURI YA KUMETA-META MBELE YAKO?

Tofauti na makabila mengine 11 ambayo Yakobo aliyabariki kama tunavyosoma katika kitabu cha Mwanzo ile sura ya 49. Kabila la Isakari ndio kabila, lililokubali utumishi, tena sio utumishi tu ilimradi utumishi bali utumishi kama wa Punda kwa watu wa Mungu. Unaweza kusema wana wa Isakari walikuwa wajinga, kuongozwa na roho ya punda kama wasemavyo watu sasa hivi. Lakini maandiko yanatuambia, walifanya hivyo kwasababu waliona ni nini kipo mbele yao. Waliona nchi nzuri ya utukufu ikiwangojea, waliona mahali pa mapumziko ya milele pako mbele yao panawasubiri, na hivyo ili kufikia nchi hiyo ni sharti leo hii watumike sana. Soma..

Mwanzo 49:14 “Isakari ni punda hodari, Ajilazaye kati ya mazizi ya kondoo;

15 Akaona mahali pa raha, kuwa pema, Na nchi, ya kuwa ni nzuri, Akainama bega lake lichukue mizigo, Akawa mtumishi kwa kazi ngumu”.

Unaona, alikubali kujishusha, ili awe mtumishi wa kazi ngumu. Kama vile Punda moja anayebeba chakula cha kondoo wengi zizini. Ndivyo alivyojiona kwa wengine.  Na matokeo yake biblia inatuambia, wana wa Isakari walikuja kuwa wenye akili nyingi za kujua majira ya nyakati Zaidi ya wote. Ndio waliokuwa wanategemewa na Israeli nzima, kutoa taarifa juu ya nyakati za neema na hukumu zilizoamriwa na Mungu. Akili hizo na hekima hizo walipewa na Mungu mwenyewe.

1Nyakati 12:32 “Na wa wana wa Isakari, watu wenye akili za kujua nyakati, kuyajua yawapasayo Israeli wayatende; vichwa vyao walikuwa watu mia mbili na ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao”.

Je! Na sisi tunaweza kufananishwa na wana wa Isakari? Unajua ni kwanini leo watu hatutaki kumtumikia Mungu, ni kwasababu hatuoni yaliyo mbele yetu, tunaona ya hapa hapa tu, hatuona majira ya neema yanayokuja huko mbeleni, hatuioni Yerusalemu mpya na nchi mpya tuliyoahidiwa na Mungu. Hatuoni Karamu ya mwanakondoo ambayo Yesu alikwenda kutuandalia kwa miaka 2000 sasa ipo karibuni kuanza. Na ndio maana hatutaki leo hii kujitia katika utumishi wa Mungu. Tunachojua ni kujitia katika utumishi wa kusumbukia maisha, tupate magari, tupate majumba, mashamba, tuwe mabilionea., hayo tu, Mambo ambayo fahari yake inaishia hapa hapa duniani.

Hata kuhudhuria ibada tunaona ni mzigo mzito, lakini tupo radhi kufanya kazi siku 365 bila kuchoka, usiku na mchana, tupo radhi kutazama Tv kila siku, lakini kusoma aya moja ya biblia na kuitafakari ni mtihani kwetu..Kama hayo yakitushinda tutawezaje, kuwa watumishi wa Mungu?

Wana wa Isakari waliitambua ile kauli ya Bwana Yesu kabla hata ya yeye mwenyewe kuja..kwamba ukubwa katika ufalme wa mbinguni, sio kuwa na sifa, na ujuzi, na vyeo, na kutumikiwa, hapa duniani, bali ni katika utumishi kwa wengine.. ndio maana wao wakaamua kuwa vile.

Mathayo 20:25 “Lakini Yesu akawaita, akasema, Mwajua ya kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha.

26 Lakini haitakuwa hivyo kwenu; bali mtu ye yote anayetaka kuwa mkubwa kwenu, na awe mtumishi wenu;

27 na mtu ye yote anayetaka kuwa wa kwanza kwenu na awe mtumwa wenu;”

Je! Na sisi tunaiona sawasawa hiyo nchi nzuri na ya kumeta meta kule ng’ambo? Kama ndivyo basi tuwe radhi kuwa Punda kwa kondoo wa Mungu, kama ilivyokuwa kwa wana wa Isakari. Tukubali kumtumikia Mungu,bila kutafuta faida zetu wenyewe. Tukubali kuwatanguliza wengine, na sio sisi tu wenyewe na matumbo yetu, kila siku. Ili siku ile Kristo akaketi  pamoja na sisi katika kiti chake cha enzi mbinguni.

Kumbuka hizi ni siku za kumalizia, wakati tuliobakiwa nao ni mfupi sana,Injili tuliyonayo sio ya kuliliwa liliwa tena uokoke. Kwasababu muda wake umeshaisha, tumebakiwa na injili ya Ushuhuda tu. Ili siku ile watu wasije wakasema hawakuhubiriwa injili. Embu jiulize wewe ambaye upo kwenye mawazo mawili mawili, ni ujasiri gani unapata kuishi maisha ya namna hiyo?

Unyakuo ukipita leo hii usiku na ukaachwa utamweleza nini Kristo? Au kifo kikikuta ghafla, huko unapokwenda utakuwa mgeni wa nani? Kuzimu ipo na haishi watu kama maandiko yanavyosema. Na ibilisi anataka uendelee katika hali hiyo hiyo, ili mabaya yakukute kwa ghafla, kama yalivyowakuta wenye dhambi wote waliotangulia kuzimu.

Tubu dhambi zako, na Zaidi sana ukawe mtumishi wa Mungu, ufanye kusudi lake hapa duniani. Kwasababu hilo ndilo uliloitiwa.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

WAENDEE WANA WA ISAKARI, UWE SALAMA.

UFUNUO: Mlango wa 17

NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

Wibari ni nani?(Mithali 30:26)

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya “Roho za manabii huwatii manabii?

SWALI: Shalom naomba kujua nini maana ya huu mstari “Roho za manabii huwatii manabii? (1Wakorintho 14:34)


JIBU: Labda tusome kuanzia juu kidogo ili tupate picha kamili mstari huo ulikuwa unamaana gani..

1Wakorintho 14:26 “Basi, ndugu, imekuwaje? Mkutanapo pamoja, kila mmoja ana zaburi, ana fundisho, ana ufunuo, ana lugha, ana tafsiri. Mambo yote na yatendeke kwa kusudi la kujenga.

27 Kama mtu akinena kwa lugha, wanene wawili au watatu, si zaidi, tena zamu kwa zamu, na mmoja na afasiri.

28 Lakini asipokuwapo mwenye kufasiri na anyamaze katika kanisa; aseme na nafsi yake tena na Mungu.

29 Na manabii wanene wawili, au watatu, na wengine wapambanue.

30 Lakini mwingine aliyeketi akifunuliwa neno, yule wa kwanza na anyamaze.

31 Kwa maana ninyi nyote mwaweza kuhutubu mmoja mmoja, ili wote wapate kujifunza, na wote wafarijiwe.

32 NA ROHO ZA MANABII HUWATII MANABII.

33 Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani; vile vile kama ilivyo katika makanisa yote ya watakatifu”.

Ukisoma hapo utaona kuna ustaarabu ulizuka miongoni mwa wakristo wa kanisa la Korintho. Walipokuwa kutanika kanisani, kila mtu alikuwa na neno la kusema, kila mtu alikuwa na wimbo wake spesheli wa kumwabudu Mungu, kila mtu alikuwa na ufunuo wake, kila mtu alikuwa na fundisho lake jipya la kuliwasilisha kanisani, kila mtu alikuwa na lugha na tafsiri yake mwenyewe..

Embu tengeneza picha, kila mtu kanisani anazo karama zote, wote wanataka kufundisha kwasababu wamepokea mafunuo, wote wanataka kutabiri kwasababu ni manabii, wote wanataka kufasiri lugha, wote wanataka kuwa waongozaji kwaya n.k…

Utagundua jambo kama hilo likiwepo kanisani, ni wazi kuwa hakutakuwa na kujengana tena, bali mavurugano tu, kwasababu hakuna utaratibu, hivyo hata kuielewa sauti ya Mungu itakuwa ni shida.

Kwamfano tengeneza picha umeenda kwenye shule yenye waalimu wengi, halafu kila mwalimu anataka afundishe masomo yote, hesabati, yeye, kemia yeye, baolojia yeye, na mwingine hivyo hivyo, jiulize wanafunzi wataelewaje? Hawawezi kuelewa bali watachanyikiwa, ni wapi wajifunze,  au mwalimu yupi wamsikilize…

Halikadhalika na katika kanisa la wakorintho, Paulo aliwaagiza, wasiwe na utaratibu huo, hata kama imetokea watu 10 au 20 au  50 katika kanisa wamepewa ufunuo kwa wakati mmoja, hawapaswi wanene wote, bali wawape ruhusa walau wawili au watatu tu, na hao wengine wabakie kupambanua..

Na kama ikitokea hao ambao hawajapewa nafasi ya kunena na bado wanang’ang’ania tu wanene na wao, wanapaswa wakumbuke huo msemo wa Paulo kwamba “ROHO ZA MANABII HUWATII MANABII”

Maana yake ni kuwa kama wao ni manabii, wanapaswa watii utaratibu wa manabii wenzao uliowekwa. Hata kama wao hawajapewa nafasi. Kwasababu Mungu sio Mungu wa machafuko,. Na vilevile kama ikatokea mwingine aliyeketi amefunuliwa jambo kubwa zaidi, basi yule wa kwanza, anapaswa awe radhi kumpisha mwenzake, na yeye atulie, kwasababu mambo yote yanafanywa kwa lengo la kulijenga kanisa, na sio kwa lengo la mashindano, au kwa lengo la kutoa mafunuo mengi, ambayo yatafanya kanisa likose shabaha ya kujua kusudi la Mungu ni nini.

Hata sasa, utaratibu huu unapaswa uwe mwendelevu katika makanisa, sio maono yote au mafunuo yote watu waanaoonyeshwa na Mungu yanapaswa yafundishwe ndani ya kanisa kwa wakati huo huo, hapana, vinginevyo tutazama kwenye machafuko na mikanganyiko mingi, bali vichaguliwe viungo viwili au vitatu katika vyenye karama hiyo, kisha sisi wengine tubakie kupambua, na hao wengine wapewe nafasi  wakati mwingine..Ili tuweze kumwelewa Mungu.

Lakini kama ikitokea mmojawetu anataka kujiona na yeye ni lazima ya kwake isemwe, akumbuke usemi ule..”Roho za Manabii, huwatii manabii”. Awe tayari kuwatanguliza wenzake kwanza, Kwasababu Mungu si Mungu wa machafuko bali wa utaratibu.

Bwana akubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Ampokeaye nabii kwa kuwa ni nabii, atapata thawabu ya nabii; Mstari huu unamaana gani?.

MATARAJIO YA KILA MWANADAMU DUNIANI NI YAPI?

SI KWA UWEZA WALA KWA NGUVU BALI KWA ROHO YANGU, ASEMA BWANA.

JE UNAIFANYA KAZI YA MUNGU?

HAKUNA MTU ANIONDOLEAYE, BALI MIMI NAUTOA MWENYEWE

Rudi nyumbani

Print this post

NI LAZIMA KUISHIKILIA IMANI MPAKA MWISHO.

Nabii Eliya alikuwa na Imani ya kutosha hata kushusha moto kutoka mbinguni, kuwaangamiza maadui zake, lakini masaa machache tu! baada  ya kushusha moto juu ya dhabihu ile, alimkimbia mwanamke mmoja mchawi aliyeitwa Yezebeli (alimkimbia kwa hofu kabisa), ili kujiokoa nafsi yake (1Wafalme 19). Ni sawa na fahali la ng’ombe na nguvu zake zote, halimwogopi fahali mwenzake, linapigana naye, lakini linamwogopa mbwa na kumkimbia kabisa..ndicho kilichomtokea Nabii Eliya. Alikuwa na Imani ya kuangushwa maadui zake walio magwiji, lakini aliizimisha kwa kumwogopa mwanamke mmoja tu!.

Pia tunaweza kujifunza kwa Petro, mtume wa Bwana Yesu..

Mathayo 14:24 “Na kile chombo kimekwisha kufika katikati ya bahari, kinataabika sana na mawimbi; maana upepo ulikuwa wa mbisho.

25  Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari.

26  Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli; wakapiga yowe kwa hofu.

27  Mara Yesu alinena, akawaambia, Jipeni moyo ni mimi; msiogope.

28  Petro akamjibu, akasema, Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji.

29  Akasema, Njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu.

30  Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe, akisema, Bwana, niokoe.

31  Mara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, EWE MWENYE IMANI HABA, MBONA ULIONA SHAKA?”

Hapo Mtume Petro, alikuwa na imani ya kuanzia lakini ya kumalizia hakuwa nayo, hatimaye akaanza kuzama kabla ya lengo lake kutimia.

Nasi pia tukumbuke Moto tuliokuwa nao wakati tunamwamini Yesu, ni lazima tuwe nao huo huo, tena na zaidi wakati wa mwisho wa maisha yetu..Hatupaswi hata kidogo kubaki na historia kichwani tu kwamba, miaka Fulani nilikuwa moto sana, miaka Fulani nilikuwa naweza kukesha kusali, miaka Fulani nilikuwa nashuhudia sana, miaka Fulani nilikuwa nasoma Neno sana.

Ukijiona juzi, au mwaka jana ulikuwa moto kuliko mwaka huu, tambua kuwa tayari umeshaanza kuzama…Imani yako imeshaanza kuwa haba!.. Unahitaji kumpigia yowe Bwana Yesu leo! Akusaidie.. Ukiona zile dhambi ambazo ulikuwa unaweza kuzishinda kirahisi mwaka jana lakini mwaka huu huwezi, leo ni wakati wa kupiga yowe, kabla ya hujamalizikia kuzama kabisa..Ukiona ulikuwa unaweza kusali masaa kadhaa lakini leo nusu saa tu ni shida!, unasinzia!, nguvu ya kulisoma Neno huna tena…hapo huna budi kupiga yowe kuomba msaada..kwasababu imani yako imeanza kupungua.

Ukiona ule ujasiri dhidi ya dhoruba zote za shetani, unaanza kupotea ndani yako, unahitaji kumlilia Bwana, ukiona hofu ya wachawi na madhara ya adui yamekuzingira, tofauti na hapo kwanza, ambapo ulikuwa na ujasiri wa kutohofu chochote, basi jua imani yako imeanza kutindika!.. huna budi kumpigia Bwana yowe! Kama ishara ya kutaka msaada..

Poteza kila kitu lakini usipoteze imani yako…kwasababu Imani ni ulinzi. Kamwe huwezi kumshinda adui shetani,  na dhoruba zake kama imani yako ipo chini.

Hivyo chunguza maisha yako leo!.. Je! Bado unayo imani ya kumalizia? Kama huna..leo hii kumbuka uliko toka, kumbuka uweza wa Mungu, mwanzo ulipomwamini, na mlilie Bwana, umwambie unahitaji Imani ya kwanza, na fanya hivyo kwa kumaanisha huku, ukirekebisha makosa yako yote ambayo yalikufanya urudi nyuma..Na Bwana atakusaidia kama alivyomsaidia Petro.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

AHADI YA ROHO ILIYOSALIA SASA KWA KIPINDI CHETU.

NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.

Je aliyezungumza na Musa kule jangwani ni Mungu mwenyewe au malaika wake?

KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!

KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.

Rudi nyumbani

Print this post

Je aliyezungumza na Musa kule jangwani ni Mungu mwenyewe au malaika wake?

Katika kitabu cha Kutoka 3:2, tunasoma ni Malaika wa Mungu ndiye aliyemtokea Musa, lakini tukiendelea mbele katika Mstari wa 4, tunaona ni Mungu ndiye anayezungumza na Musa, na si Yule malaika tena, hapo imekaaje?

Jibu: Tuisome habari hiyo…

Kutoka 3: 2 “Malaika wa Bwana akamtokea, katika mwali wa moto uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea

3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei.

4 Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa.

5 Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu.

 6 Tena akasema, Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu”.

Aliyemtokea Musa ni Malaika wa Mungu, na si Mungu mwenyewe… na malaika huyo alimtokea katika mwonekano wa Moto.. (kumbuka malaika wanaweza kuchukua mfano wa umbile lolote, wanaweza kuchukua umbile la mtu, au moto, au mwanga), wanapochukua umbile la kibinadamu wanaonekana kama wanadamu, mfano wa yule aliyemtokea Yoshua katika kitabu cha Yoshua 5:14, wanapokuja katika maumbile haya wanakuwa kama watu kabisa, wanaweza kuonekana na kuzungumza. Kadhalika wanaweza kuja katika maumbile kama ya mwanga au moto..katika maumbile haya, unaweza kusikia sauti tu na usione mtu..ukaona tu huo mwanga au moto!. N.k

Sasa Malaika huyu alitumwa na Mungu kwa Musa akiwa amebeba ujumbe wa Mungu, na alimtokea Musa katika umbile la Moto, maana yake Musa aliona moto tu kwenye kile kijiti na kusikia sauti lakini hakuwa anaona mtu.

Sasa jambo moja la kujifunza ni kwamba, Malaika wanapobeba ujumbe wa Mungu, na Mungu anapoweka jina lake ndani yako,na kuwatuma, wanaweza kutoa ujumbe kana kwamba ni Mungu mwenyewe ndiye anasema ndani yao..Sasa katika huyu Malaika aliyezungumza na Musa, Mungu alikuwa ameweka neno lake ndani yake, kiasi kwamba lolote atakalozungumza ni Mungu ndio kazungumza…(Sasa sio kwamba ni lolote atakalojiamulia tu yeye kusema!..hapana..bali ni lile ambalo Mungu atakalomwambia alifanye na kulisema ndilo atakalolisema).. Tunaweza kusoma hilo vizuri…

Kutoka 23:20 “Tazama, mimi namtuma malaika aende mbele yako, ili akulinde njiani na kukupeleka mpaka mahali pale nilipokutengezea.

 21 Jitunzeni mbele yake, MWISIKIZE SAUTI YAKE; wala msimtie kasirani; maana, hatawasamehe makosa yenu; kwa kuwa JINA LANGU LIMO NDANI YAKE.

22 LAKINI UKIISIKIZA SAUTI YAKE KWELI, NA KUYATENDA YOTE NINENAYO MIMI; ndipo mimi nitakuwa ni adui wa adui zako, na mtesi wa hao wakutesao”.

Hapo mstari wa 22, anasema “lakini ukiisikiza sauti yake kweli, na kuyatenda yote ninenayo mimi”..Maana yake “Bwana atanena kupitia yule malaika, chochote Yule malaika atakachokisema ni Bwana kakisema”. Jambo hilo liliwezekana kwa malaika tu! ila kwa sehemu ndogo! (si wakati wote Mungu alizungumza na watu kupitia malaika wake kama alivyofanya kwa Musa hapo)..…

Lakini zamani hizi limewezekana kwa asilimia zote kupitia mmoja tu YESU KRISTO!! MKUU WA UZIMA.. Huyo amefanyika bora kupita malaika, akisema ni Mungu kasema asilimia 100!, Maneno yake ni Maneno ya Mungu,..kwasababu amefanyika Bora kupita malaika haleluya!!! (Tutakuja kuliona hilo vizuri mbeleni kidogo!!).

Lakini tukirudi katika upande wa Malaika aliyezungumza na Musa, tunaona baadaye, mbeleni kabisa wana wa Israeli walipoanza kuzembea kuwafukuza wale wenyeji wa miji ile, tunaona Yule malaika aliyepewa maneno ya Bwana kinywani mwake, akitokea na kuanza kuzungumza, kana kwamba ni Bwana mwenyewe ndiye anayezungumza…

Waamuzi 2:1 “Kisha malaika wa Bwana alikwea juu kutoka Gilgali kwenda Bokimu. Akasema, Mimi nimewaleta ninyi mkwee juu kutoka nchi ya Misri, nami nimewaleta hata nchi niliyowaapia baba zenu; nami nilisema, Mimi milele sitalivunja hilo agano langu nililoagana nanyi;

2 nanyi msifanye agano lo lote na hawa wenyeji wa nchi hii; zipomosheni nchi madhabahu zao; lakini hamkuisikia sauti yangu; je! Mmefanya haya kwa sababu gani?

 3 Basi kwa ajili ya hayo mimi nilisema zaidi, Mimi sitawafukuza watoke mbele zenu; lakini watakuwa kama miiba mbavuni mwenu, na miungu yao itakuwa ni tanzi kwenu.

4 Ikawa, hapo huyo malaika wa Bwana alipoyanena maneno haya, kuwaambia wana wa Israeli wote, ndipo hao watu wakainua sauti zao na kulia

5 Nao wakaliita jina la mahali pale Bokimu; nao wakamchinjia Bwana sadaka huko”.

Umeona hapo?..aliyewatoa wana wa Israeli Misri kuwapeleka Kaanani ni Bwana, na si malaika, lakini Bwana alimpa Malaika wake jukumu zima, na vile vile, aliweka maneno yake ndani ya Yule malaika, kiasi kwamba atakachokinena Malaika yule, ni Bwana kakinena, na atakachokifanya malaika Yule ni Bwana kakifanya, vile vile Agano lake aliliweka ndani ya Yule malaika, kiasi kwamba atakayevunja agano lile la Yule malaika, ni sawa kalivunja agano la Mungu..kwasababu Neno lake limejaa ndani ya Malaika yule, anakuwa si yeye tena, bali ni Mungu anazungumza ndani yake.

Sasa katika agano hilo la kwanza, Mungu alizungumza ndani ya Malaika, lakini si wakati wote,(wakati mwingine Bwana alisema pasipo kuwatumia hao malaika).. lakini katika agano jipya, Mungu amejitwalia chombo chake, ambacho ametia maneno yake yote ndani yake, na agano lake lote ndani yake, zaidi ya alivyofanya kwa malaika…Chombo hicho hakina pumziko, wakati wote kikinena ni Mungu kanena..na chombo hicho si kingine zaidi ya Bwana Yesu…Huyu kafanyika bora kuliko malaika!!..

Waebrania 1:1  “Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi,

2  mwisho wa siku hizi AMESEMA NA SISI KATIKA MWANA, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu.

3  Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu;

4  AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA, KWA KADIRI JINA ALILOLIRITHI LILIVYO TUKUFU KULIKO LAO”

Umeona sauti ya Mungu leo ipo wapi?..umeona agano la Mungu leo lipo wapi?..si kwa mwingine zaidi ya kwa YESU!.. Huyo ni zaidi ya Yule malaika aliyezungumza na Musa pale kwenye ule mwali wa Moto.. Na kama agano la kwanza ambalo Bwana alinena kupitia malaika lilikuwa na utukufu mkubwa vile, kiasi kwamba yeyote atakayelivunja neno la malaika Yule alikufa,. hili la pili ni mara nyingi zaidi..biblia inasema hivyo..

Waebrania 2:1 “Kwa hiyo imetupasa kuyaangalia zaidi hayo yaliyosikiwa tusije tukayakosa.

2  Kwa maana, IKIWA LILE NENO LILILONENWA NA MALAIKA LILIKUWA IMARA, na kila kosa na uasi ULIPATA UJIRA WA HAKI,

3  sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? AMBAO KWANZA ULINENWA NA BWANA, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia”.

Je umempokea Yesu?.. Je! Umeyakabidhi maisha yako yote kwake?..fahamu kuwa Mamlaka yote ya mbinguni na duniani kapewa yeye..na yeye ndiye sauti ya Mungu kwetu!, ukimkataa yeye umemkataa Mungu, ukimkubali yeye umemkubali Mungu..

Kama bado hujamwamini, nafasi yako ya kumpokea ndio sasa, unachopaswa kufanya hapo ulipo ni kujitenga kwa muda, kisha kupiga magoti binafsi na kumkiri Yesu kwa kinywa chako kuwa ndiye Bwana na mwokozi wa ulimwengu, na kisha kukiri makosa yako kwa kutubu, huku umedhamiria kutofanya tena dhambi hizo, na baada ya hapo haraka sana bila kuchelewa tafuta ubatizo sahihi kama bado hujabatizwa ubatizo sahihi, kumbuka ubatizo ulioagizwa na Bwana Yesu ni ule wa maji mengi na kwa jina la YESU (Matendo 2:38), na baada ya hapo, Roho Mtakatifu atakuongoza katika yote yaliyosalia, ikiwemo kukupa uwezo wa kushinda dhambi.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Naomba kufahamu maana ya “sura ya kijiti” katika Marko 12:26.

Ni kweli Waliolala Katika Kristo Wamepotea?(1Wakor 15:18)

NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA!

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Naomba kufahamu maana ya “sura ya kijiti” katika Marko 12:26.

Jibu: Tusome,

Marko 12:26  “Na kwa habari ya wafu ya kwamba wafufuliwa, hamjasoma katika kitabu cha Musa, SURA YA KIJITI, jinsi Mungu alivyomwambia, akisema, Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo?”

Neno “sura” kama lilivyotumika hapo sio “uso”..kama huu wenye pua, na macho na masikio.. bali limetumika kuwakilisha “mlango fulani” katika maandiko.. Kama tunavyojua tukitaka kupata habari Fulani katika maandiko, huwa tunafungua biblia na kusema fungua kitabu Fulani, mlango Fulani utapata habari hiyo.

Kwamfano tukitaka kupata habari ya kufufuka kwa Bwana tunazipata katika kitabu cha Luka Mlango wa 24..Sasa badala ya kutumia neno mlango, wakati mwingine tunatumia neno “Sura”..hivyo ni sawasawa na kusema “habari za kufufuka kwa Bwana Yesu tunazipata katika kitabu cha Luka sura ya 24”.

Kadhalika hapo Mtume Paulo alikuwa anamaanisha “Sura ile katika maandiko ambayo Mungu alizungumza na Musa kupitia kile kijiti kilichokuwa kinawaka moto lakini hakiteketei”.. Na hiyo si nyingine zaidi ya ile sura ya 3 katika kitabu cha “Kutoka”…tusome.

Kutoka 3:1 “Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu.

 2 Malaika wa Bwana akamtokea, katika mwali wa moto uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea.

3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu KIJITI HIKI HAKITEKETEI.

4 Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka KATIKATI YA KILE KIJITI, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa.

 5 Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu.

6 Tena akasema, Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu.

 7 Bwana akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri”

Kwahiyo  “Sura” ni “Mlango”..Na kijiti kilichozungumziwa hapo sio kipande kidogo cha mti, bali ni “kichaka”.

Hivyo kikubwa tunachoweza kujifunza hapo ni kwamba Mungu ni Mungu wa walio hai… Alijitambulisha kwa Musa kama Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo.. Kwasababu Watu hao ingawa wamekufa sasa, lakini huko waliko wanaishi…kama Bwana Yesu mwenyewe alivyosema katika kitabu cha Yohana..

Yohana 11:25  “Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi”

Hivyo Ibrahimu, Isaka na Yakobo wanaishi sasa, na hivyo Mungu ni Mungu wao hata sasa… kadhalika na sisi tukiishi kwa kumwamini Yesu, na kuishi kulingana na mapenzi yake hapa duniani, tutakapokufa bado tutakuwa tunaishi katika paradiso ya raha, na baadaye tutafufuliwa kutoka huko paradiso na kuvikwa miili ya utukufu na kwenda na Bwana mbinguni, katika siku ile ya unyakuo..

Waebrania 11:16  “Lakini sasa waitamani nchi iliyo bora, yaani, ya mbinguni. KWA HIYO MUNGU HAONI HAYA KUITWA MUNGU WAO; maana amewatengenezea mji”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Kwanini Yakobo alimshinda Mungu, Je! Mungu huwa anashindwa na wanadamu?

Kwanini Yakobo alimshinda Mungu, Je! Mungu huwa anashindwa na wanadamu?

Naye aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika-vunjika..

MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Rudi nyumbani

Print this post