Zeri ya Gileadi ni nini?

Zeri ya Gileadi ni nini?

Zeri ni dawa ambayo ilikuwa inakamuliwa kutoka katika aina Fulani ya mmea uliokuwa unapatikana sana sana huko Gileadi. Kwasasa haujulikani mmea huo ulikuwa hasaa ni wa aina gani, kama ni mti au jani, lakini biblia inachoeleza ni thamani yake na  sifa zake katika kuponya.

Ukisoma katika biblia kipindi kile wale watoto wa Yakobo walipomuuza ndugu yao kwa wale waarabu waishmaeli, biblia inatuambia, katika safari yao ya biashara ya kwenda Misri walikuwa wamebeba na Zeri pia.

Mwanzo 37:25 “Nao wakakaa kitako kula chakula; wakainua macho yao, wakaona, msafara wa Waishmaeli wanakuja wakitoka Gileadi na ngamia zao, wakichukua ubani na zeri na manemane, wakisafiri kuvichukua mpaka Misri”.

Lakini ukisoma pia kitabu cha Yeremia sura ya 8 inaeleza jinsi Yeremia alipokuwa akiwalilia ndugu zake wayahudi kwa jinsi watakavyochukuliwa na wababiloni mateka, Na ndio katika kulia kwake akisema Je! Kuna zeri ya Gileadi awapake watu wake ili waponywe na majeraha hayo makubwa  yatakayowapata.. Akimaanisha kama kuna tiba yoyote nzuri ya rohoni, itakayowaponya watu wake na msiba huo mkubwa utakaowakuta mbeleni.

Yeremia 8:21 “Kwa sababu ya maumivu ya binti ya watu wangu nimeumia mimi; nimevaa kaniki; ushangao umenishika.

22 Je! Hapana zeri katika Gileadi? Huko hakuna tabibu? Mbona, basi, haijarejea afya ya binti ya watu wangu”?

Ukisoma, tena ile sura ya 46 Utaona Mungu anawaambia waisraeli kwa kinywa hicho hicho cha Yeremia kwamba wakachukue Zeri ya Gileadi ili wajipake, kwasababu wamejiharibu kupitiliza, kwa makosa yao mengi.

Yeremia 46:11 “Panda uende Gileadi, ukatwae zeri, Ee binti, bikira wa Misri; unatumia dawa nyingi bure tu; hupati kupona kamwe”.

Soma pia Yeremia 51:8, Ezekieli 27:17 utakutana na Neno hilo.

 Lakini tunajua, Mungu hakumaanisha, Zeri kama dawa ya mitishamba, ndio ingewaponya watu wake, kwa dhiki zao, na dhambi zao, hapana. Bali alikuwa anamaanisha Zeri ya Rohoni.

Na huyo si mwingine Zaidi ya BWANA wetu YESU KRISTO. Yeye ndiye tiba ya kweli. Akimganga mtu amemganga kweli kweli roho yake, na vilevile hata mwili wake, anaponyeka kweli kweli.

1Petro 2:24 “Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa”.

Upendo wa kweli upo kwa Kristo, tumaini la kweli lipo kwake, furaha ya kudumu inatoka kwake.

Je! Umempokea Kristo maishani mwako? Au unategemea Zeri  nyingine zikuponye? Kumbuka fedha haiwezi kuiponya roho yako, mke hawezi kuyaponya hayo majeraha yaliyoko ndani yako,, Ndugu, au rafiki hawezi kuzifuta hizo hatia zilizouchafua moyo wako. Ni Yesu Kristo tu peke ndiye anayeweza kufanya hivyo?

Mpokee Leo ayageuze maisha yako.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

SIFONGO NA SIKI NI NINI?

Hisopu/ Hisopo ni nini katika biblia?(Zaburi 51:7)

NI LAZIMA KUISHIKILIA IMANI MPAKA MWISHO.

INJILI YA MANENO LAINI ITAKUGHARIMU.

Aina za dhambi

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments