NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.

NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima, Ni siku nyingine tena Mungu ametupa neema ya kujifunza, hivyo nakukaribisha tuyatafakari pamoja maneno ya uzima maadamu siku ile inazidi kujongea.

Lipo jambo alilizungumza Petro, wakati ule ambao Bwana Yesu aliwachukua yeye pamoja na Yakobo na Yohana juu ya ule mlima mrefu.. Tukilisoma naamini litatupwa mwanga wa jinsi ya kutembea  vema katika safari yetu hii ya wokovu, Tusome habari yenyewe kwa ufupi na mbeleni kuna jambo kubwa ambalo Mungu atatufundisha siku ya leo.

Luka 9:28 “Baada ya maneno hayo yapata siku nane, aliwatwaa Petro na Yohana na Yakobo, akapanda mlimani ili kuomba.

29 Ikawa katika kusali kwake sura ya uso wake ikageuka, mavazi yake yakawa meupe, yakimeta-meta.

30 Na tazama, watu wawili walikuwa wakizungumza naye, nao ni Musa na Eliya;

31 walioonekana katika utukufu, wakanena habari za kufariki kwake atakakotimiza Yerusalemu.

32 Petro na wale waliokuwa pamoja naye walikuwa wamelemewa na usingizi; lakini walipokwisha amka waliuona utukufu wake, na wale wawili waliosimama pamoja naye.

33 Ikawa hao walipokuwa wakijitenga naye, PETRO ALIMWAMBIA YESU, BWANA MKUBWA, NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA; NA TUFANYE VIBANDA VITATU; KIMOJA CHAKO WEWE, NA KIMOJA CHA MUSA, NA KIMOJA CHA ELIYA; HALI HAJUI ASEMALO.

34 Alipokuwa akisema hayo, lilitokea wingu likawatia uvuli, wakaogopa walipoingia katika wingu hilo.

35 Sauti ikatoka katika wingu, ikisema, Huyu ni Mwanangu, mteule wangu, msikieni yeye.

36 Na sauti hiyo ilipokwisha, Yesu alionekana yu peke yake. Nao wakanyamaza, wasitangaze kwa mtu siku zile lo lote katika hayo waliyoyaona”.

Katika mazingira hayo utaona, wakati Yesu akiwa uweponi mwa Mungu, ghafla Musa na Eliya walitokea wakaanza kuzungumza naye.. Mazungumzo hayo inaelekea yalikuwa ni marefu kidogo, kwasababu hawakuja kama malaika kuleta ujumbe tu na kuondoka hapana, bali walikuja kama wageni, kuzungumza naye, na mada kuu ilikuwa ni kuhusu kifo chake, jinsi atakavyoteswa na kukataliwa na watu kule Yerusalemu.

Kumbuka wakati huo mitume walikuwa wamelala, lakini walipoamka ghafla, wakamwona Yesu waliyemzoea akiwa katika mwonekano mwingine kabisa, na pembeni yake walikuwa watu wengine wawili wamesimama, na cha kushangaza walikuwa wakiongea naye kama vile wanajuana.

Hivyo Petro kuona tukio kama lile Bwana akiwa na wageni wa kimbinguni, huku akitazama na mazingira ya pale mlimani, hakuna hata chochote CHA KUWATIA UVULI, akaona si vema, asikae tu hivi hivi akimtazama Bwana akizungumza na wageni wake kwenye jua.

Ghafla akajikuta tu anazungumza, na kumwambia Bwana, Ni vizuri sisi kuwapo hapa.. akiwa na maana ni kama vile bahati wao kupanda naye kule mlimani kwasababu, walau wanaweza kumsaidia kufanya kitu.. Ndipo Petro akasema wacha tuwatengenezee vibanda vitatu, kimoja chako wewe, kimoja cha Eliya na kingine cha Musa.. Ili walau mpate uvuli juu ya mlima huu mrefu, mwendelee kuzungumza kwa utulivu zaidi.. hivyo wacha sisi tushuke chini tukachukue vifito tuanze kazi..

Embu tengeneza picha, Petro alijua Bwana amepatwa na ugeni wa kimbinguni, alijua wale watu hawana haja ya kukaa kwenye vibanda,, lakini kutokana na mazungumzo yao kuwa eneo tupu la wazi kama lile hakuona aibu kuonyesha kujali kwake kwao… Kama vile Ibrahimu wakati ule alipotembelewa na wale watu watatu, alipowaalika na kuwanjia ndama.

Na biblia inatuambia mara baada ya Petro kuzungumza maneno yale.. saa hiyo hiyo, wingu kubwa jeupe, likashuka mahali pale, likawatia UVULI wote, walipoona vile waliogopa sana, kukaribia kuzimia kwasababu jambo kama hilo hawajawahi kuliona katika maisha yao yote, na saa hiyo hiyo, sauti ikatoka KATIKATI ya lile wingu ikisema..

“Huyu ni mwanangu mpendwa wangu msikieni yeye”…Maneno kama hayo kuyasikia ilihitaji mbingu ikupasukie kwanza, walioweza kusikia sauti ya Mungu moja kwa moja kutoka mbinguni ikimshuhudia Yesu ni hawa watatu, pamoja na Yohana mbatizaji Ambaye yeye wakati anambatiza Yesu, mbingu zilimpasukia na kusikia maneno hayo hayo.(Mathayo 3:16-17)

Lakini hiyo yote, ilikuwa ni kwasababu gani?

Ni kwasababu alifikiria kwanza kumwekea Bwana uvuli kwa vile vibanda walivyokuwa wanataka kumjengea yeye. Ndipo Mungu akawatia UVULI halisi wa Mbinguni kwa wingu lake yeye mwenyewe.

Tengeneza picha mfano wasingejaribu kufikiria vile kwa ajili ya Bwana wao.. Ni wazi kuwa wasingeshukiwa na wingu lolote na wala wasingekaa waisikie sauti ya Mungu moja kwa moja ikuzungumza nao. Ushuhuda ambao wangebakiwa nao ni ule wa kumwona Eliya na Musa, na Yesu kuwa na mavazi meupe basi. Hakuna Zaidi.

Vivyo hivyo na sisi leo, Je, tunamtazama Kristo akihudumu katika hali gani? Na sisi tutakuwa  ni watu wa kutazama tu, au wa kusikiliza tu, au tutasema kama Petro, NI VEMA SISI KUWAPO MAHALI HAPA. Tukifikiria hata kwa uchache Mungu aliotujalia, au alivyotupa hivyo vinatosha kwa Mungu, ahitaji wingi wako, anahitaji nia yako, na moyo wako wa dhati.. Kama wafuasi wa Kristo hatupaswi kukaa kuangalia injili inahubiriwa katika hali ya taabu. Ni kweli utukufu wa Mungu utaendelea kuonekana, lakini zipo faida ambazo tutazikosa kama hatutakuwa na mawazo  kama ya Petro, alivyosema NI VEMA MIMI KUWEPO HAPA, wacha nikachukue fito nimwekee Bwana kivuli, sihitaji niwe na matofauti kwanza.

Wakati mwingine tunashindwa kumsikia Mungu kipekee kwasababu ya sisi kutoelewa kanuni za utendaji kazi wake.

Kumbuka Neno la Mungu (BIBLIA) ndiyo dira ya safari yetu hapa duniani. Siri zote za Mungu na njia zote za  kumfikia yeye utazipata huko tu, na sio kwa mwanadamu yoyote, au kwa mwanazuoni yeyote, au msomi yoyote, au kwenye kitabu kingine chochote.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

CHANGIA SASA.

PATANA NA MSHITAKI WAKO KWANZA.

ESTA: Mlango wa 8, 9 & 10. (SIKU KUU YA PURIMU)

UFUNUO: Mlango wa 19

TUMTOLEE MUNGU VILE VINAVYOTUGHARIMU ZAIDI.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
JEAN DE DIEU MUNYAMBABAZI
JEAN DE DIEU MUNYAMBABAZI
1 year ago

Bwana Yesu asifiwe mpendwa! Asante kwa mafundisho ya kila wakati mubarikiwe.
Nimekuwa na swali ndani ya Kitabu ya mwanzo sura ya 1:26- na kwa sura 2:18 mbona ni habari ambazo zinapingana ukweli ni upi? Mfano: Mtu na minyama kipi kilichotanguliwa kuumbwa? Je nyuma ya siku ya saba ya kupumzika mbona kwa sura 2 tunaona kuumbwa tena kwa Adamu na hawa kutoshwa ubavuni mwake je nyuma ya siku 7 Mungu alifanya kazi tena? Munisaidie kuhusu hii .Nashukuru

Anonymous
Anonymous
1 year ago

Je, pombe ni dhambi?