Fuawe ni nini? Kama tunavyosoma katika Isaya 41:7

Fuawe ni nini? Kama tunavyosoma katika Isaya 41:7

Isaya 41:7 “Seremala akamtia moyo mfua dhahabu, na yeye alainishaye kwa nyundo AKAMHIMIZA YULE APIGAYE FUAWE, akiisifu kazi ya kuunga, akisema, ni kazi njema; naye akaikaza kwa misumari isitikisike. ”.


JIBU: Fuawe ni chuma kizito, zilichotengenezwa na wafuaji kwa ajili ya kazi ya kuchonga au kukarabati vitu vyenye asili ya chuma, kama fedha, dhahabu, shaba, n.k. kwa kuviponda ponda  juu ya chuma hicho ili vitokee katika  maumbile waliyoyatazamia Tazama picha chini.

Ilikuwa kama wanataka kuunda umbile Fulani la chuma au shaba au fedha, walikiingiza kwanza kwenye moto kiyeyuke ili kiwe kirahisi kupondwa.. Ndipo kikishatolewa kililetwa kwenye hii fuawe sasa kwa ajili ya kugongwa kwa lengo la kukipa umbile lake.

Hivyo tukirudi katika mstari huo, anasema seremala akamtia moyo mfua dhahabu, hapa alikuwa anamzungumzia mtengeneza vinyago, vya mbao, ambaye baada ya kuvichonga sasa alikuwa tayari kuvipeleka vinyago vyake kwa walainishao yaani wafuaji, ili wawandalie dhahabu au fedha ya  kuvifunika vinyago vyake na huyo mfua fedha, aishaiweka dhahabu aliipeleka  sasa kwa huyu mpiga fuawe, mchongaji wa mwisho wa kinyago, ili kuleta umbo kamili la kinyago kile, Soma pia (Isaya 40:19)

chuma kizito fuawe

Lakini Mungu hapo alikuwa anaonyesha taabu zao, na gharama zao nyingi wanazoingia kwa mambo yasiyokuwa na faida, Kwa kujiundia vinyago visivyoweza kuzungumza wala kusikia, wala kuokoa, wala kutoa ahadi za ulinzi baadaye.. Lakini tunaona hapo mistari iliyofuata Mungu akiwaahidia watu wake Israeli ahadi nono, ambazo vinyago haviwezi kutoa, akiwaambia..

Isaya 41:8 “Nawe, Israeli, mtumishi wangu; Yakobo, niliyekuchagua; mzao wa Ibrahimu, rafiki yangu;

9 wewe niliyekushika toka miisho ya dunia, na kukuita toka pembe zake, nikikuambia, Wewe u mtumishi wangu; nimekuchagua wala sikukutupa;

10 usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu”.

11 Tazama, wote walioona hasira juu yako watatahayarika na kufadhaika; watu washindanao nawe watakuwa si kitu, na kuangamia.

12 Utawatafuta wala hutawaona wale wapiganao nawe; watakuwa si kitu; watakuwa kama kitu kisichokuwa, wale waliofanya vita juu yako.

13 Kwa maana mimi, Bwana, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia.

14 Usiogope, Yakobo uliye mdudu, nanyi watu wa Israeli; mimi nitakusaidia, asema Bwana, na mkombozi wako ni Mtakatifu wa Israeli.

15 Tazama, nitakufanya kuwa chombo kikali kipya cha kupuria, chenye meno; utaifikicha milima, na kuisaga; nawe utafanya vilima kuwa kama makapi.

16 Utawapepeta, na upepo utawapeperusha; upepo wa kisulisuli utawatawanya; nawe utamfurahia Bwana, utajitukuza katika Mtakatifu wa Israeli.

17 Maskini na wahitaji wanatafuta maji, wala hapana; ndimi zao zimekauka kwa kiu; mimi, Bwana, nitawasikia, mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha.

18 Nitafunua vijito vya maji juu ya vilima, na chemchemi katikati ya mabonde; nitageuza jangwa kuwa ziwa la maji, na mahali pakavu kuwa vijito vya maji.

19 Nitapanda katika jangwa mwerezi, mshita, mhadasi, na mbono; nitatia katika nyika mberoshi, mtidhari, na mteashuri pamoja;”

Na sisi je, tunaweza kuweka kando ibada zote za sanamu za rohoni na mwilini, mpaka ifikie hatua ya Mungu kutuahidia ulinzi mnono kama huo aliowaahidia wana wa Israeli?

Jibu tunalo,

Je umeokoka? Je, unatambua kuwa nyakati hizi ni za mwisho?.. Na kanisa tunaloishi ndio kanisa la mwisho lijulikanalo kama Laodikia? Kama unayatambua hayo sasa Unangoja nini usimkaribishe Kristo leo maishani mwako. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo. Basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

kwanini Yakobo amefananishwa na mdudu?(Isa 42:14)

Kwanini biblia inaitaja mara kwa mara dhahabu ya Ofiri?

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Njuga ni nini (Isaya 3:16, Zekaria 14:20)?

Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “Saa yangu haijawadia?”

Ni nani aliyesema “Nitume mimi”? katika (Isaya 6:8)

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments