Title October 2021

Mizimu ni nini?

Ni kweli mizimu ipo?, Na tunawezaje kujihadhari nayo?.


Katika tafsiri inayojulikana na wengi ni kwamba Mzimu/Mizimu ni roho za watu waliokufa ambazo zinaweza kurudi na kuwatokea wengi.

Roho hizo zinaweza kurudi zenyewe au kurudishwa na mtu, kwa lengo fulani, aidha kutatua tatizo lililoshindikana katikati ya mtu au jamii ya watu, au kujilipiza kisasi kwa mambo aliyofanyiwa mtu huyo kabla ya kufa.

Lakini je! Kibiblia MIZIMU ni kweli ipo?

Jibu ni la! Hakuna roho yoyote ya mtu aliyekufa, inayoweza kurudi yenyewe au kurudishwa na mtu, na kisha kutatua jambo fulani la kimaisha.

Jambo hilo liliwezekana kwa sehemu katika agano la kale kabla ya Bwana Yesu kuja, shetani alikuwa na uwezo wa kuzipandisha juu za watu waliokufa. Utaona katika maandiko aliweza kumpandisha juu nabii Samweli (1Samweli 28:11-14).

Lakini katika agano jipya, baada ya Bwana Yesu kushuka kuzimu na kuzichukua zile funguo za mauti na kuzimu, ambazo mara ya kwanza zilikuwa mikononi mwa shetani, kukawa kuanzia huo wakati na kuendelea hakuna yeyote anayeweza kuzipandisha juu roho za watu waliokufa..

Hata shetani mwenyewe hawezi tena, kwasababu funguo za kuzimu na mauti anazo Kristo mwenyewe..yeye ndiye anayewamiliki wafu wote, wema na waovu.

 Warumi 14:9 “Maana Kristo alikufa akawa hai tena kwa sababu hii, awamiliki waliokufa na walio hai pia”.

Sasa swali linakuja, kama wafu hawawezi kurudi kama mizimu, hivyo tunavyoviona, au tunavyovisikia vikiwatokea watu vikiwa na sura za wapendwa wao waliowahi kuishi ni vitu gani?

Jibu rahisi ni MAPEPO yaliyojigeuza na kuvaa sura za watu waliokufa.

Maandiko yanasema shetani anaweza kujigeuza akawa kama Malaika wa Nuru, atashindwaje kujigeuza na kuvaa sura ya mtu fulani aliyekufa?. Ni kitu kirahisi sana kwake.

2 Wakorintho 11:14
“Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru”.

Kwahiyo shetani na mapepo yake wanachokifanya ni kuvaa sura za watu waliokufa na sauti zao, na kuigiza kama ndio wale watu halisi, na watu wanapowaona au kuwasikia wanaamini ni wafu wao wamerudi (Mizimu).. lakini kiuhalisia kumbe sio, bali ni mapepo yaliyojigeuza.

Na kwasababu shetani ni yule yule, anapenda kukaa nyuma ya kitu na kutafuta kuabudiwa..anakaa nyuma ya wote wanaoabudu sanamu, wanaoabudu miti wakidhani ni Mungu, wanaoabudu mizimu, wanaoabudu jua n.k

Hivyo hatuna budi tuwe macho na tujihadhari na kumwabudu shetani bila kujua, kwa kukosa maarifa.

Kadhalika kama bado tupo nje ya wokovu, hakuna namna yoyote tunaweza kujiepusha na madhara ya roho hizo chafu, ambazo zinazunguka huku na huko, kuuharibu ulimwengu.

Bwana atubariki.

Maran atha!

Group la whatsapp Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Noeli ni nini, na je! Neno hili linapatikana katika biblia?

THAWABU ZA SIRI, ZA WATAKATIFU MBINGUNI.

WAKAMCHA BWANA, NA KUITUMIKIA MIUNGU YAO WENYEWE.

MAJINI WAZURI WAPO?

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Eliya alijulikana kama “Eliya Mtishbi”?

Je! Mtishbi ni jina la Baba yake au?

Jibu: Tishbi sio jina la mtu bali la mji, kama vile ulivyo mji wa Samaria au Nazareti.

Kwahiyo kama vile mtu aliyetoka mji wa Nazareti anavyoitwa Mnazareti, au aliyetokea mji wa Samaria anavyoitwa Msamaria, kadhalika mtu yeyote aliyetokea mji huo wa Tishbi aliitwa Mtishbi.

Mji huo wa Tishbi, ulikuwepo katika nchi ya Gileadi, iliyopo ng’ambo ya pili ya mto Yordani. Kwasasa ni maeneo ya nchi ya Yordani (Jordan).

Na katika mji huo mdogo wa Tishbi ndiko Nabii Eliya alikokulia na kuishi sehemu kubwa ya maisha yake.

1 Wafalme 17:1
“Basi Eliya Mtishbi, wa wageni wa Gileadi, akamwambia Ahabu, Kama BWANA, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninasimama mbele zake, hakutakuwa na umande wala mvua miaka hii, ila kwa neno langu”

Maandiko hayajaeleza kwa undani maisha ya Nabii Eliya, ya utotoni, na ujanani, na vile vile hayajaeleza kama alikuwa na mke au watoto.

Lakini kikubwa tunachoweza kujifunza kwa Nabii huyu, ni roho ya kuomba kwa bidii..mbali na kwamba Mungu alimtumia kwa viwango vya juu sana, lakini pia alikuwa ni mtu wa kuomba kwa bidii sana, maandiko yanasema hivyo..

Yakobo 5:16
“Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.

17 Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi, akaomba kwa bidii mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya nchi muda wa miaka mitatu na miezi sita.

18 Akaomba tena, mbingu zikatoa mvua, nayo nchi ikazaa matunda yake”.

Na sisi tunajifunza tuwe watu wa kuomba kwa bidii kwasababu Eliya alikuwa ni MTU tu! Kama sisi na si malaika, au mtu fulani aliyeumbwa kipekee tofauti na sisi..alichokuwa na cha ziada ni bidii ya kuomba.

Hivyo na sisi tunajifunza tuwe watu wa kuomba kwa bidii, na sio tu kuomba bali pia kuombeana. Kwasababu kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana kama akiomba kwa bidii.

Bwana atujalie tuwe na bidii kama za hawa mashujaa wa Imani.

Maran atha!

Group la whatsapp Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

KUJIFUNUA KWA YESU KWA PILI.

Zeri ya Gileadi ni nini?

Sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji zilikuwaje?

Rudi nyumbani

Print this post

Baali alikuwa nani?

Baali alikuwa ni aina ya mungu aliyekuwa anaabudiwa na watu wa kaanani na nchi za Tiro na Sidoni, ambaye kulingana na historia za wakaanani, anatajwa kuwa mwana wa mungu aliyeulikana kwa jina la El na mkewe aliyejulikana kwa jina la Ashera..hawa ndio waliomzaa huyu Baali ambaye baadaye alikuja kuabudiwa kama mungu.

Tafsiri ya jina “Baali” ni “bwana” na aliaminika kama mungu wa rutuba na wa uzao.

Aliaminika kusaidia kuongeza rutuba ya nchi, pale ambapo chakula hakikupatikana kutokana na ardhi kutozaa..basi walimwomba huyu mungu baali, ili nchi iweze kuzaa mazao.

Kadhalika pale ambapo mtu au watu walipatwa na matatizo ya kutokupata watoto, walimwomba na kumtegemea mungu huyu kwaajili ya kupata uzao.

Mungu huyu aliabudiwa sana na watu wa kimataifa, lakini ulifika wakati hata wana wa Israeli wakaanza kumwabudu.
Wana wa Israeli walianza kumwabudu baali kwa mara ya kwanza katika kile kipindi cha Waamuzi.

Waamuzi 2:11 “Wana wa Israeli walifanya yaliyokuwa ni maovu mbele za macho ya BWANA, nao wakawatumikia Mabaali.

12 Wakamwacha BWANA, Mungu wa baba zao, aliyewaleta kutoka katika nchi ya Misri, wakafuata miungu mingine, baadhi ya miungu ya watu wale waliokaa karibu nao pande zote, wakajiinamisha mbele yao; wakamkasirisha BWANA, akaghadhibika.

13 Wakamwacha BWANA, wakamtumikia Baali na Maashtorethi”.

Waliendelea hivyo na ibada hizo za mabaali, lakini si kwa kiwango kikubwa..

Hali ilikuja kuwa mbaya zaidi ulipofika wakati wa Mfalme mmoja wa Israeli aliyeitwa Ahabu, ndipo kipindi hicho ibada hizo zilishika hatamu mpaka Bwana Mungu akamtuma Eliya Nabii.

Mfalme Ahabu aliabudu baali kwa kiwango ambacho hakuna mfalme yeyote alikifikia.

1 Wafalme 16:30“ Ahabu mwana wa Omri akafanya yaliyo mabaya machoni pa BWANA kuliko wote waliomtangulia.

31 Ikawa, kama ingalikuwa neno dogo tu kuyaendea makosa ya Yeroboamu mwana wa Nebati, akamwoa Yezebeli binti Ethbaali, mfalme wa Wasidoni, akaenda akamtumikia Baali, akamsujudia.

32 Akamjengea Baali madhabahu katika nyumba ya Baali, aliyoijenga huko Samaria.

33 Ahabu akaifanya Ashera; Ahabu akazidi kumghadhibisha BWANA, Mungu wa Israeli, kuliko wafalme wote wa Israeli waliomtangulia”.

Lakini je! Baali alikuwa ni mungu kweli?

Jibu ni la!.

Mungu ni mmoja tu, aliyeziumba mbingu na nchi, jina lake YEHOVA. Hao wengine sio miungu bali ni roho za mapepo..BAALI ni pepo!..

Ndio maana haikuweza kujibu chochote mbele za uwepo wa Bwana wa majeshi, wakati ule wa Eliya.

1 Wafalme 18:26
“ Wakamtwaa yule ng’ombe waliyepewa, wakamtengeza, wakaliitia jina la Baali tangu asubuhi hata adhuhuri, wakisema, Ee Baali, utusikie. Lakini hapakuwa na sauti, wala aliyejibu. Nao wakaruka-ruka juu ya madhabahu waliyoifanya”.

Hiyo inatufundisha kuwa ibada zote za miungu na za sanamu ni chukizo kwa Bwana.

Na wote wanaoabudu sanamu, na miungu hawataurithi uzima wa milele, maandiko yanasema hivyo.

Bwana atubariki.

Group la whatsapp Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Je Mungu anaweza kumdanganya mtu?

Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?

Maashera na Maashtorethi ni nini?

Mlima Gerizimu na Ebali ni ipi, na umuhimu wao rohoni ni upi?

Je Mungu anaweza kumdanganya mtu?

Rudi nyumbani

Print this post

NI YESU YUPI UMEMPOKEA?, NI ROHO IPI UMEIPOKEA? NA INJILI IPI UMEIPOKEA?

Jina la Bwana Yesu libarikiwe, karibu katika kuyatafakari maandiko..

2Wakorintho 11:4 “Maana yeye ajaye akihubiri YESU MWINGINE ambaye sisi hatukumhubiri, au mkipokea ROHO NYINGINE msiyoipokea, au INJILI NYINGINE msiyoikubali, mnatenda vema kuvumiliana naye”!

Hapo katika  sentensi hiyo, Mtume Paulo aliposema “mnatenda vema kuvumiliana naye”..hakuwa anawasifu watu wa Korintho kwa wao kupokea roho nyingine, au kumkubali Yesu mwingine, bali kinyume chake! Alikuwa ANAWASHUTUMU!.

Sentensi hiyo ili ieleweke vizuri tunaweza kuiweka hivi ….“Mnachukuliana na mtu anayekuja kwenu na kuwahubiria yesu mwingine au injili nyingine msiyoikubali)” yaani “mnaona ni sawa na tena mnakubaliana naye”.

Hapo Mtume Paulo, alimaanisha kwamba, hawapaswi kuchukuliana na mtu yeyote anayekuja kwao na kuwaletea yesu Mwingine au roho nyingine au injili nyingine ambayo hawakuhubiriwa na mitume..kinyume chake wawakatae watu hao na wakatae injili yao na kuipuuzia…lakini hawa watu Wa Korintho walikuwa hawafanyi hivyo!.. walikuwa wanakaa na kuwasikiliza!..jambo ambalo ni hatari kwa roho zao.

Na hata sasa kuna yesu mwingine anayehubiriwa tofauti na Yule Yesu wa kwenye biblia, kadhalika kuna roho nyingine tofauti na Yule Roho Mtakatifu anayehubiriwa katika biblia, na vile vile kuna injili nyingine tofauti na injili halisi ya kwenye biblia..

yesu mwingine ni yupi?

Bwana Yesu halisi anasema wa kwenye biblia anasema.. “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi (Yohana 14:6)”…lakini yesu mwingine anasema “zipo njia nyingi za kufika kwa baba, ikiwemo kupitia mtakatifu Fulani au kupitia maombi ya mtakatifu Fulani aliyekufa, au kupitia kanisa Fulani au kupitia dini nyingine yeyote”

Kadhalika Bwana Yesu halisi wa kwenye biblia alisema… “mtu yeyote akitaka kunifuata ajikane mwenyewe ajitwike msalaba wake anifuate(Mathayo 16:24) na tena anasema “itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake? Ama mtu atoe nini badala ya nafsi yake?(Marko 8:36)”..lakini yesu mwingine anasema.. “sio lazima kujikana nafsi, sio lazima kuacha dhambi, sio lazima kubadilika kimwonekano, Mungu anatazama roho hatazami mwili” n.k

Huyo ndio mfano wa yesu Mwingine ambaye Paulo, aliwaonya watu wa Korintho kwamba wasimkubali,na wala wasichukuliana naye kwasababu ni shetani.

Kadhalika ipo roho Nyingine.

Roho Mtakatifu wa kweli wa kwenye biblia, akija juu ya mtu, jambo la kwanza analolifanya ni kumgeuza Yule mtu na kuwa mtakatifu, kama jina lake lilivyo.. “Roho Mtakatifu”..sifa yake ni utakatifu, na kazi ya pili ni kutuongoza na kututia katika kweli yote ya maandiko, na ya tatu ni kutukumbusha maandiko ..

lakini zipo roho ambazo mtu anapozipokea hazimfanyi kuwa mtakatifu, badala yake ndio zinampa kibali cha kutenda dhambi, kuvaa vibaya,(nusu uchi), kutukana, kuwa na kinyongo na visasi..kadhalika hazimwongozi mtu katika kusoma Neno na kulijua katika ukweli wote. Badala yake ndio zinamletea uvivu wa kuisoma biblia na kuijua..Hizo roho ni roho nyingine, ambazo sio Roho Mtakatifu, ni roho za adui, ambazo zinajigeuza na kujifananisha na Roho Mtakatifu.

Kadhalika kuna Injili nyingine.

Injili maana yake ni “habari njema za Yesu Kristo” ambazo zinaleta WOKOVU kwa mtu.(Warumi 1:16). Na wokovu ni kupata kuokoka kutoka katika hatari Fulani ijayo, au iliyopo.

Zipo injili ambazo hazimfanyi mtu aokoke kutoka katika hatari ya adhabu ya milele (katika Jehanamu ya moto), badala yake zinamfanya astahili kwenda Jehanamu.

Mfano wa injili hizo ni “injili za kutokusamehe, vinyongo na visasi”. Siku hizi hadi makanisani zinahubiriwa. Bwana Yesu alisema, msipowasamehe watu makosa yao, hata baba yenu wa mbinguni hatawasamehe (Mathayo 6:15)..Kwahiyo kutokusamehe tayari ni tiketi ya kwenda jehanamu moja kwa moja..Na injili yeyote inayohubiri kutokusamehe ni injili nyingine ya kuzimu.

Leo hii utakuta mkristo kajaa uchungu, na vinyongo..kwa mambo baadhi tu aliyofanyiwa mabaya..na anakwenda kanisani anakutana na injili ya kupiga adui zake, na kuipokea akidhani yupo salama..kumbe yupo hatarini?

Jiulize ndugu, Umempokea Yesu yupi? Wa kwenye biblia au Yule mwingine?..na umeipokea roho ipi?, Ni Roho Mtakatifu au ya adui?.. na ni Injili gani umeipokea?..ile iletayo wokovu, au ikupelekayo kuzimu?

Maandiko yanatuasa kuwa “tuzipime roho”, na sio roho tu!, bali pia tumpime Bwana yupo tumempokea Yesu Kristo au yesu kristo, na ni injili ipi tumeipokea.

Maran atha!

Group la whatsapp Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Je! Watu ambao hawajawahi kusikia injili kabisa siku ya mwisho watahukumiwa?

Ni kwa namna gani malaika wa mbinguni wanaweza kutuhubiria sisi injili?

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

Matoazi na Matari ni nini? (Kutoka 15:20)

Rudi nyumbani

Print this post

Ni nani aliyemshawishi Daudi akawahesabu Israeli? Ni Mungu au shetani?

Katika 2Samweli 24:1 tunaona maandiko yanasema ni Mungu ndiye aliyemtia Daudi nia, lakini tukirudi katika 1Nyakati 21:1, tunaona maandiko yanasema ni shetani.


Tuanze na 2Samweli 24:1..

2Samweli 24:1 “Tena hasira ya BWANA IKAWAKA JUU YA ISRAELI, AKAMTIA DAUDI NIA JUU YAO, AKISEMA, NENDA, UKAWAHESABU ISRAELI NA YUDA”.

Tusome pia…

1Nyakati 21:1 “TENA SHETANI AKASIMAMA JUU YA ISRAELI, AKAMSHAWISHI DAUDI KUWAHESABU ISRAELI.

2 Basi Daudi akamwambia Yoabu, na wakuu wa watu, Nendeni kawahesabu Israeli toka Beer-sheba mpaka Dani; mkanipashe habari, nipate kujua jumla yao”.

Hapo tukiangalia tunaona ni kweli sentensi mbili zinajichanganya..lakini je! Ni kweli zinajichanganya?

Jibu ni la! Hazijichanganyi..fahamu zetu ndizo zinazojichanganya..lakini biblia siku zote itabaki kuwa Neno la Mungu, lililohakikiwa na Roho Mtakatifu na lisiloweza kukosewa.

Ili tuelewe vizuri maana ya mistari hiyo, hebu tutafakari katika mfano wa kawaida wa kimaisha.

Watu wawili tofauti wameshuhudia ajali barabarani.. Mmoja akatoa ushuhuda akasema “Yule mtu alipokuwa anavuka gari lilimgonga na halikusimama”…Na mwingine akatoa ushuhuda akasema.. “Yule mtu alipokuwa anavuka, Yule dereva alimgonga na hakusimama..akakimbia ”. Je! Katika hao mashuhuda wawili kuna ambaye hayupo sahihi?.. Bila shaka wote wapo sahihi!!.. aliyesema “gari limemgonga” na aliyesema “dereva kamgonga”..wote wapo sahihi..

Kwasababu Yule aliyesema gari limemgonga, hajahusisha dereva aliyekuwa analiendesha lile gari, kadhalika Yule aliyesema ni dereva kamgonga hajahusisha kifaa kilichotumika kumgongea Yule mvuka barabara, ambacho ni gari.

Kadhalika katika mistari hiyo hapo juu..Tunaona mmoja kamtaja kuwa ni Bwana Mungu ndiye aliyemtia nia Daudi, bila kuhusisha chombo alichokitumia (yaani shetani)..kadhalika mwandishi mwingine wa kitabu cha Mambo ya Nyakati, kakitaja chombo tu (yaani shetani)na bila kumhusisha aliyekitumia hicho chombo (yaani Mungu).

Kwahiyo kwa ujumla aliyeleta hayo yote ni Mungu, na shetani katumika tu kama chombo!..na hiyo yote ni kwasababu ya makosa ya Israeli. Na pia ilikuwepo sababu kwanini iwe ni kosa Daudi kwenda kuwahesabu Israeli kama utapenda kujua zaidi juu ya hilo, unaweza kufungua hapa >>>> USIZITEGEMEE NGUVU ZAKO

Kwahiyo tunachoweza kujifunza ni kwamba, Mungu anaweza kutumia chombo chochote kile kutimiza kusudi lake.

Kwamfano utaona Mungu alipotaka kuwatoa Israeli kuwapeleka Babeli, hakushuka yeye mwenyewe na kuwaondoa, bali utaona alimtumia Nebukadneza kama chombo chake cha kufanya hiyo kazi.

Kadhalika Bwana Mungu anaweza kumtumia shetani kutimiza kusudi lake.

Kwamfano mtu anayemkataa Mungu kwa makusudi, anaweza kuruhusu shetani ayaharibu maisha yake, mpaka atakapofikia hatua ya kujitambua.. Na hata wakati mwingine kama mtu huyo kama bado anazidi kushupaza shingo, basi Mungu anaweza kumweka chini milki ya shetani moja kwa moja.

Hivyo hatuna budi kukaa katika neema ya Mungu, na kuishi maisha yampendezayo, ili tusimkasirishe Bwana Mungu wetu aliyetuumba. Kwasababu maandiko yanasema.. yeye mwenyewe hapendi kumtesa mwadamu wala kumhuzunisha.. (Maombolezo 3:34).

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba kama bado hujampokea Yesu, fahamu kuwa hizi ni siku za mwisho. Na Kristo yupo mlangoni kurudi, unyakuo wa kanisa ni wakati wowote. Je akija leo na kukukuta katika hali hiyo ya dhambi, utakuwa mgeni wa nani?

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Ni miaka mingapi ya njaa Daudi aliyoambiwa achague? Ni miaka 7 au miaka 3?

Ni miaka mingapi ya njaa Daudi aliyoambiwa achague? Ni miaka 7 au miaka 3?

KUOTA UNAENDESHA GARI.

KUOTA NYOKA.

Rudi nyumbani

Print this post

KUOTA AJALI, KUNAMAANISHA NINI?

Ndoto za ajali zinaweza kuja katika maumbile mengi tofauti tofauti, wengine wanaota ajali za pikipiki, wengine za magari, wengi ndege, wengine meli, wengine treni, katika namna tofauti tofauti. Wengine wanaota mtu kagongwa na gari, au magari yanagonga gongana n.k… kwa vyovyote vile, ndoto hizo zinabeba maudhui moja nayo ni “AJALI”

Sasa ili kupata tafsiri sahihi ya ndoto hiyo ni vizuri ukajitambua wewe upo katika kundi gani.

1.) Kundi la kwanza ni waliookoka.

2) Kundi la pili ni wenye dhambi.

Tukianzana na kundi la kwanza: Ikiwa wewe, umeokoka (yaani unao uhakika umesimama ndani ya Kristo).  Basi fahamu kuwa ni Mungu anakutahadharisha tukio lililopo mbele yako, aidha kuna ajali utakutana nayo, au itatokea kwa mtu mwingine, au mahali fulani. Hivyo  unachopaswa kufanya, ni kuingia katika maomba ya kuvunja hiyo mipango ya adui. Ambayo pengine imepangwa kwako au kwa mtu mwingine..kemea kwa bidii kwa mamlaka uliyopewa katika jina la Yesu. Na Mungu ataisambaratisha hiyo mipango yote.

Ikiwa ndoto hiyo imekuja kwa uzito usiipuuzie, kwasababu Mungu kukuonyesha hivyo, ni ili usimame kama askari wa Mungu kushindana na hizo nyakati mbaya kabla hazijafika.( Soma Ayubu 33:14-15)

Kundi la Pili: Mwenye dhambi.

Ikiwa wewe ni mwenye dhambi(yaani hujaokoka, Kristo hayupo ndani yako). Ujue ndoto hiyo ni ishara ya tahadhari kubwa sana kwako. Kwamba kipindi si kirefu Mungu atakuadhibu, na kuadhibu kwake, kunaweza kukawa ni kifo cha ghafla, au kunaswa katika dhambi zako unazozifanya, na ukashindwa kutoka huko milele.

Soma hii Habari kwa makini;

Ezekieli 7: 6 “Mwisho umekuja, mwisho huu umekuja; unaamka ukupate; angalia, unakuja.

7 AJALI YAKO IMEKUJIA, wewe ukaaye katika nchi hii; majira yamewadia, siku ile inakaribia; siku ya fujo, wala si ya shangwe milimani.

8 BASI HIVI KARIBU NITAMWAGA GHADHABU YANGU JUU YAKO, nitazitimiza hasira zangu juu yako, nami nitakuhukumu sawasawa na njia zako; nami nitakupatiliza machukizo yako yote.

9 Jicho langu halitaachilia, wala sitaona huruma; nitakupatiliza njia zako na machukizo yako yote yatakuwa katikati yako; nanyi mtajua ya kuwa mimi, Bwana, napiga.

10 ANGALIA, SIKU HIYO; ANGALIA, INAKUJA; AJALI YAKO IMETOKEA; fimbo imechanua, kiburi kimechipuka”.

Umeona? Hayo maandiko yenyewe yanajieleza, ikiwa wewe ni mzinzi, fahamu kubwa ajali ya Ukimwi ipo mbele yako, wewe ni fisadi ajali ya vifungo ipo mbele yako, wewe ni mwizi ajali ya kifo ipo mbele yako, wewe ni mshirikina ajali ya jehanum ipo mbele yako.

Kwa ujumla kama wewe ni mwenye dhambi ujue mwisho wako upo karibuni sana. Na ukifa ni motoni. Ndio tafsiri ya ndoto hiyo.

Unasubiri nini mpaka hayo yote yakukute, ikiwa upo tayari leo kutubu dhambi, basi, Bwana Yesu atakusamehe, na kukuepusha na madhara hayo yote aliyokuonyesha mbele yako. Angeweza kukaa kimya tu, hayo mambo yakukute kwa ghafla, lakini kwasababu hataki uangamie ndio maana amekutahadharisha mapema.. Hivyo leo hii fungua moyo wako, kubali kugeuka, na uache dhambi zako zote, ili Kristo ayatengeneze tena Maisha yako.

Ikiwa upo tayari kutubu leo, basi fungua hapa, kwa ajili ya mwongozo wa SALA YA TOBA. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Angalia pia Kuota Unajenga nyumba

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)

Nakusalimu katika jina kuu, la Bwana wetu Yesu Kristo karibu katika sehemu ya pili ya Makala hii inayohusu migogoro katika ndoa. Sehemu ya kwanza tuliona Upande wa mwanaume, Leo tutaangazia upande wa mwanamke. Kwa kurejea mgogoro uliozuka katika ndoa ya kwanza ya Adamu. Kama hukupata sehemu ya kwanza tutumie msg inbox tukutumie uchambuzi wake.

Wewe kama mke.

Unapaswa utambue kuwa mume ndio kichwa cha Familia, Ndoa ya kwanza ulitikiswa na mwanamke, kuonyesha kuwa vyanzo vya migororo ya ndoa nyingi hadi sasa ni WANAWAKE.

Na hiyo yote ni kwasababu wepesi kufungua milango kwa shetani kuwadanganya kirahisi. Kwamba wao pia wajione wanauwezo wa kujiamulia tu mambo yao bila hata ya waume zao au kumshirikisha Mungu ? Hiyo ni hatari kubwa sana.

Usijaribu kufanya hivyo mwanamke, utaiharibu ndoa yako kwa mikono yako mwenyewe. Kinyume chake, anza kuwa MTIIFU kwa mume wako kama biblia inavyosema katika..

Waefeso 5:22 “ENYI WAKE, WATIINI WAUME ZENU KAMA KUMTII BWANA WETU.

23 Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili.

24 Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo”.

Kuwa mtiifu, mume wako anapokutakana uwahi kurudi nyumbani, TII, anapokuambia nipikie chakula, Tii, anapokuambia nifulie nguo, usimwambie housegirl si yupo, anapokuambia fanya hivi, au fanya vile wewe tenda, anapokushauri usifanye shughuli Fulani, sio nzuri, tii pia, kwasababu yule ndio kichwa chao. Ondoa kiburi ndani yako, wewe sio kichwa, ukijaribu kufanya hivyo, ndipo hapo shetani atakupa mbinu mbadala, utafute marafiki/wanaume wengine nje ya ndoa yako wenye pesa, ili kumkomoa mume wako, kumbe hujui kuwa ndio unajiangamiza wewe mwenyewe. Ndicho alichokiwaza Hawa alipokwenda kutafuta mashauri kwa nyoka.

Kwahiyo, simama katika nafasi yako, ya utiifu. Mbinu aliyotumia shetani kumwangamiza Hawa, ndio hiyo hiyo ataitumia na kwako, isiposimama katika nafasi yako kama mwanandoa. Na majuto utayaona baadaye sio sasa wakati una kiburi.

Kumbuka, mwanamke hutakaa ufanikiwe kwa kujitenga na mume wako? Kamwe halitawezekana.  Mwanaume anaweza kujaribu kuishi,  japo itakuwa kwa shida sana, lakini wewe sahau kuishi kwasababu Ubavu hauna ubongo,wala mikono, wala miguu, wala pua, wala macho,. Ni kipande cha nyama tu. Ndivyo ilivyo kwako wewe, ujue kuwa huna Maisha nje ya mume wako wa ndoa. Ukimwacha leo, haijalishi, una kipato kikubwa kuliko yeye, au ni mjanja kuliko yeye, nataka nikuambie hauna Maisha wewe duniani.

Na mwisho kabisa, hayo yote unaweza kuyafikia, ikiwa tu upo ndani ya Kristo, Haiwezekani kuwa mtiifu, au mwombaji, au mtakatifu, au mtu wa kusamehe, kama hutakuwa  ndani ya Kristo. Kwahiyo hatua ya kwanza ni kumpa Kristo Maisha yako.

Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo. Basi unaweza kufuatisha sala hii kwa Imani. Ukiifuatisha kwa kumaanisha kabisa ujue kabisa Bwana Yesu atakusamehe leo na kuja ndani yako….Tafuta sehemu ya utulivu kisha piga magoti, na useme sala hii kwa sauti.

“EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU, (KWA KUIJERUHI NDOA YANGU). LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.”

Ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani, ujue kuwa Kristo ameshakusamehe na kuanzia sasa anza kuwajibika kwa ajili ya ndoa yako. Na kama hujabatizwa, na unahitaji kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi, na kwa jina la Yesu Kristo, basi wasiliana na sisi kwa namba hizi, +255693036618 au +255789001312 Tukusaidie.

Mungu akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)

Nini maana ya..“wakiwazuia watu wasioe” (1Timotheo 4:1)

Kwanini wajane vijana hawakupaswa kuandikwa?

NDOA NA TALAKA:

NINI TUNAJIFUNZA KWA THEOFILO MTUKUFU?

Rudi nyumbani

Print this post

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

Katika siku hizi za mwisho, migogoro ya kindoa imekuwa ni mingi sana, kiasi kwamba ndoa kudumu hata mwaka mmoja, ni jambo la kushukuru sana. Kila kukicha mikwaruzano, hakuna amani, kila mmoja amemchoka mwenzake. Mpaka wengine kudhani huyo mwenzi aliyemuoa au aliyeolewa naye halikuwa chaguo sahihi kutoka kwa Mungu, hivyo  suluhisho pekee ni kuachana.

Nataka nikuambie, kabla hujafikiria kuachana na huyo mwenzi wako, Tafuta kwanza kama kuna watu walishapitia tatizo kama hilo la kwako, na uone walilitatuaje tatuaje, au mwisho wao ulikuwaje..

Kumbuka kuvunjika kwa ndoa, ni kushindwa kwa pande zote mbili (au moja), kujua wajibu wake katika ndoa kama Neno la Mungu linavyoagiza..

Ndoa inafananishwa na safari ya Maisha/ ya wokovu, si wakati wote, itakuwa ni “HONEY MOON”, si wakati wote mtakuwa ni vijana, si wakati wote mtakuwa Pamoja, na si wakati wote mambo yataenda sawa.. Haijalishi ndoa hiyo, atakuwa ameifungishwa Mungu mwenyewe Kanisani au la.  Kushuka na kupanda kutakuwa ni sehemu ya Maisha yenu.

Leo hii tutajifunza, mfano wa ndoa moja maarufu katika biblia, na jinsi ilivyokumbana  na migogoro mikubwa sana, ambayo naamini ni Zaidi ya migogoro ya ndoa zote zilizowahi kutokea ulimwenguni, lakini Pamoja na hayo  bado iliendelea kudumu hadi dakika ya mwisho, naamini kwa kupitia hiyo itakuponya na wewe pia ambaye kwenye ndoa yako zimeshaanza kuonekana dalili za nyufa.

Na ndoa hiyo si nyingine Zaidi  ya ile ya ADAMU.

Adamu alichaguliwa mke na Mungu mwenyewe, tena aliyeumbwa kutoka katika ubavu wake kabisa,kuonyesha kuwa ni wake kweli kweli,. Lakini waliishi kwa kipindi Fulani kirefu kwa raha na furaha bila taabu wala shida yoyote,  hadi siku mambo yalipoanza kubadilika,

Na yalibadilika, kwa kukengeuka kwa mwanamke kwanza, pale ambapo aliacha kusikiliza maagizo ya mume wake(aliyopewa na Mungu), ya kutokula matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya, lakini yeye akayala kwa tamaa ya kutaka kuwa kama Mungu, ya kutaka kuwa kichwa (yaani kumzidi hata mume wake),ya kutaka kumiliki,  akayala bila kumshirikisha mume wake, lakini kinyume chake ni kuwa tamaa hiyo Mungu aliipindua na kuihamishia kwa mume wake badala yake, na ndio maana utaona leo hii  kwanini wanaume wanauchu wa kutawala, kuwa vichwa, hiyo tamaa mwanzoni haikuwepo kwao bali ilikuwa kwa mwanamke, baada ya kuasi Mungu ndio akamuadhibu mwanamke kwa kosa hilo la kumuhamishia mwanaume.

Mwanzo 3:16 “Akamwambia mwanamke, Hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala”.

Sasa na baadaye Adamu alipoona, mke wake kaharibu, ameasi, akakubali na yeye, kuingia katika matatizo ya mke wake kwa hiari yake yeye mwenyewe (kwasababu yeye hakudanganywa), na baada ya hapo, Mungu akamlaani naye pia.

Tangu huo wakati, Maisha yakawa magumu kweli, kwasababu dhambi imeshaingia, kulima kwa shida kukanza, magonjwa yakazuka, vifo vikaingia, kila aina ya shida ikazuka tangu huo wakati na kuendelea, kila kukicha hali ndio ilizidi kuwa mbaya, hadi kwa Watoto waliowazaa, hakuna amani katikati yao, wakawa wanauana.. Embu tengeneza picha ingekuwa wewe ni Adamu ungemfanyaje huyo mwanamke baada ya hapo?

Ni wazi kuwa ungempa talaka siku ile ile ya kwanza alipofanya kosa lile si ndio?. Tena baada ya hapo ungekuwa ni wa kulaumu Maisha yako yote, kwamba Mungu amekupa mkosi na balaa, ni heri ungebakia tu peke yako bila kuoa, lakini tangu ulipompata huyo mwanamke, mambo yako ndio yameenda kombo kabisa kabisa…

Lile kampuni amelifilisi, mali zote zimepukutika umerudia umaskini ambao ulikuwa umeshauaga zamani, amekuletea gonjwa la ukimwi kwa kutanga tanga kwake, amekufanya utengane sio tu na ndugu zako, bali hata na Mungu wako. Mwanzoni ulikuwa  ukifanya ibada vizuri, lakini tangu umuoe yule mwanamke, muda kusali haupo! Kila kitu unakipata kwa shida, tofauti na ulivyokuwa ‘Single’.

Lawama kama hizo Adamu angestahili kuwa nazo kwa mke wake, Lakini hatuoni mahali popote Adamu alimwacha mke wake, na kutamani kuishi na wanyama kama hapo mwanzo, bali alimkumbatia, akakubaliana na hali, akamsamehe, akayapanga tena upya. Akijua kuwa ule tayari ni ubavu wake. Na Mungu hakukosea kumpa, lilikuwa ni chaguo sahihi.

Mwanaume,

Kumbuka kuwa, mpaka umefikia hatua ya kumwoa huyo binti/ mwanamke, ujue kuwa ndio UBAVU wako huo Mungu aliokupa, usidhani kumtambua mke mwema ni mpaka uishi naye bila migogoro, sikuzote za Maisha yako, si kweli. Huyo ambaye upo naye katika migogoro, ni wako, na atabakia kuwa wako mpaka kifo kitakapowatenganisha.

Unachopaswa kufanya ni wewe kusimama katika nafasi yako kama ADAMU.

Suluhisho sio kumwacha, kumbuka ukimwacha huyo maana yake, unataka kurudia kuishi na Wanyama, Mpende mke wako, kwasababu hakuna kitu kinachojenga Zaidi ya upendo, mkumbatie, msamehe, mjenge upya, mvumilie, pale anapokosa, hata kama alikuletea balaa kubwa namna gani, mkumbuke Adamu, alivyoweza kuwa mvumilivu, kwa kunyang’anywa kila kitu na Mungu lakini hakumwacha Hawa. Kwani biblia inasema aliishi miaka 930, na unajua mara nyingi wanawake huwa wanakuwa na umri mrefu kuliko wanaume, kwahiyo si ajabu kuona Adamu aliishi na mke wake kwa Zaidi ya miaka hata 800, lakini sisi miaka 3 tu tumeshachokana.

Biblia inasema..

Waefeso 5:25 “Enyi waume, WAPENDENI WAKE ZENU, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;

26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;

27 apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa.

28 Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe.

29 Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa.

30 Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake.

31 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja”.

UPENDO KWA MKE wako, ni agizo kutoka kwa Mungu, na sio ihari yako tu mwenyewe. Ukiwa mwanaume wa namna hii, nataka nikuambie utaiponya ndoa yako, na itadumu sana. Wanawake kukengeuka haraka, ni jambo la kawaida, lakini wakisharudi, wanakuwa ni lulu nzuri kwako. Jifunze kusamehe, na vilevile kumpenda.

Lakini hayo yote huwezi kuyafikia kama upo nje ya Kristo. Hivyo Okoka, mkaribishe Yesu katika Maisha yako, tubu dhambi zako, kwa kumaanisha kabisa, kisha ubatizwe, upokee Roho Mtakatifu, na Kristo atakupa uwezo huo, wa kumpenda mkeo kama alivyokuwa Adamu.

Bwana akubariki.

Usikose, sehemu ya pili ya Makala hii.. Ambayo inamlenga mwanamke, kama chanzo cha migogoro ndani ya ndoa, na afanye nini ili aweze kuiponya ndoa yake.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Je! “Mke wa ujana wako” ni yupi kibiblia?

Ndoa ya serikali ni halali?

NDOA NA HARUSI TAKATIFU.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.

Rudi nyumbani

Print this post

Ni miaka mingapi ya njaa Daudi aliyoambiwa achague? Ni miaka 7 au miaka 3?

 Tukisoma 2Samweli 24:13, tunaona biblia imesema ni miaka 7 imewekwa mbele ya Dauidi, Lakini tukienda kusoma tena habari hiyo hiyo katika kitabu cha 1Nyakati 21:12, tunaona biblia inataja miaka 3 ya njaa na si 7 tena. Je! Ipi ni ipi?


Labda tuanze kusoma habari hiyo katika kitabu cha 2 Samweli..

2Samweli 24:11 “Na Daudi alipoondoka asubuhi, neno la Bwana likamjia nabii Gadi, mwonaji wake Daudi, kusema,

12 Nenda, ukanene na Daudi, Bwana asema hivi, Nakuwekea mambo matatu; katika haya uchague moja, nikutendee hilo.

13 Basi Gadi akamwendea Daudi, akamweleza, akamwambia, Basi, MIAKA SABA YA NJAA ikujie katika nchi yako? Au miezi mitatu ukimbie mbele ya adui zako, huku wakikufuatia? Au siku tatu iwe tauni katika nchi yako? Fanya shauri sasa, ufikiri, ni jawabu gani nimrudishie yeye aliyenituma”.

Hapo tunaona kweli ni miaka 7, Lakini tusome tena habari hiyo katika Mambo ya Nyakati.

1Nyakati 21:11 “Basi Gadi akamwendea Daudi, akamwambia, Bwana asema hivi, Kubali upendavyo;

12 MIAKA MITATU YA NJAA; au miezi mitatu kuangamia mbele ya adui zako, ukipatwa na upanga wa watesi wako; au siku tatu upanga wa Bwana, yaani tauni katika nchi, na malaika wa Bwana akiharibu kati ya mipaka yote ya Israeli. Haya basi ufikiri ni jawabu gani nimrudishie yeye aliyenituma”.

Kwa mistari hiyo ni rahisi kusema biblia inajichanganya.. Lakini kiuhalisia, biblia haijichanganyi mahali popote, wala haijakosewa mahali popote.

Katika habari hiyo, waandishi wote wawili wa vitabu hivyo, walikuwa wapo sahihi.. hakuna ambaye hakuwa sahihi, kwasababu wote walikuwa wanaongozwa na Roho Mtakatifu katika kuandika. Isipokuwa kila mmoja aliandika katika mazingira tofauti na mwenzake, na hawakunakiliana hivyo, ushuhuda wa mmoja hauwezi kufanana asilimia mia na wa mwingine.

Hebu chukua mfano, umefungua taarifa ya habari katika vyombo viwili tofauti, ni wazi kuwa unaweza kusikia habari moja lakini imefafanuliwa tofauti katika vyombo vyote viwili lakini habari ni ile ile moja.

Habari hizo haziwezi kufanana asilimia mia, vinginevyo kimoja kitakuwa kimenakili habari ya mwingine kama ilivyo.

Kadhalika kitabu cha Samweli sio nakala ya kitabu cha Mambo ya Nyakati, kadhalika kitabu cha Luka sio nakala ya kitabu cha Mathayo..ingawa vyote vinaweza kuwa vinaelezea matukio yanayofanana, lakini haviwezi kufanana asilimia mia, kwasababu ni mashahidi wawili tofauti. Ndio maana unaona Ushuhuda wa Luka haifananini asilimia mia na wa Mathayo au Marko.

Sasa labda turudi katika habari hiyo ya Daudi..

Tukianza na kitabu hicho cha 2Samweli 24, labda turudi sura mbili nyuma, tuone ni tukio gani lilitokea.. kisha tutaanza kuelewa ni kwasababu gani Mwandishi hapa kataja miaka 7 badala ya 3..

Tusome,

2Samweli 21:1 “Kulikuwa na njaa siku za Daudi MUDA WA MIAKA MITATU, MWAKA KWA MWAKA; naye Daudi akautafuta uso wa Bwana. Bwana akasema, Ni kwa ajili ya Sauli, na kwa nyumba yake yenye damu, kwa kuwa aliwaua hao Wagibeoni”.

Umeona hapo? Kabla Daudi kutaka kwenda kuwahesabu watu, kulitangulia njaa miaka 3, ambapo njaa hiyo ilisababishwa na Sauli kuwaua wagibeoni.

Sasa baada ya Daudi kutafuta utatuzi wa njaa hiyo, maandiko yanatuambia alifanya kosa lingine la kwenda kuwahesabu Israeli, jambo ambalo lingeiingiza tena Israeli katika baa la njaa kwa miaka mingine 3 mbele. Na kama ukisoma pale, Sensa ya kuwahesabu Israeli ilichukua miezi kama 9 na siku 20 (2Samweli 24:8).

Kwahiyo ukichukua Miaka 3 ya njaa iliyosababishwa na Sauli,  ukijumlisha na hiyo miezi 9.. utaona ni kipindi cha takribani Miaka 4. Na maandiko yanasema baada ya Daudi kuwahesabu Israeli ndipo Neno la Bwana likamjia..kwahiyo inawezekana ikawa siku ile ile alipomaliza kuwahesabu au wiki moja baadaye au mwezi mmoja baadaye ndipo Neno la Bwana likamjia.. Lakini yote katika yote miaka 4 iliisha ambayo ilikuwa ya njaa..kabla ya kuja mingine 3 kwaajili ya kosa hilo la kwenda kuwahesabu.

Kwahiyo ukichukua hiyo miaka 3 ya Sauli, ukajumlisha KIPINDI CHA MWAKA MZIMA cha SENSA, Pamoja na Neno la Bwana kumjia Daudi, Ukajumlisha na MIAKA HIYO 3 Daudi aliyoambiwa achague, Jumla yake utapata ni miaka 7.

Kwahiyo Mwandishi wa katika kitabu hicho cha Samweli alichokuwa anakimaanisha ni kwamba Endapo Daudi atachagua janga la miaka 3 ya njaa.. atakuwa amefanya JUMLA ya miaka ya njaa katika Israeli kuwa SABA.

Lakini tukirudi kwa mwandishi wa kitabu cha Mambo ya Nyakati, yeye alikwenda moja kwa moja kwenye hiyo miaka 3 ya mwisho, pasipo kuhesabu ile 3 ya kwanza iliyotangulia, pamoja na ule mmoja wa Sensa. Na ndio maana utaona katika kitabu hicho cha Mambo ya Nyakati hajaeleza popote kuhusu Njaa hiyo ya kwanza iliyosababishwa na Sauli…kama alivyoeleza mwandishi wa kitabu cha Samweli.

Kwahiyo hakuna utata wowote katika hiyo mistari.

Sasa ilikuwepo sababu kwanini Mungu achukizwe na Daudi katika kwenda kuwahesabu Israeli..Sababu hiyo kwa urefu unaweza kuisoma hapa>> USIZITEGEMEE NGUVU ZAKO KUKUSAIDIA

Mwisho, tukumbuke kuwa Kristo yupo mlangoni kurudi kulinyakua kanisa lake.. na atakuja kama mwivi, Je! umejiandaa?. Kama bado mwamini Yesu leo, na kubatizwa, upate ondoleo la dhambi.

Bwana atubariki.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

NJAA ILIYOPO SASA.

HUYU MELKIZEDEKI NI NANI?

HUYU MELKIZEDEKI NI NANI?

RUDIA, TENA NA TENA KUMWOMBA MUNGU USIKATE TAMAA.

KUJIPAMBA NI DHAMBI?

Rudi nyumbani

Print this post

MWANAMKE, BINTI, MAMA. (Sehemu ya 3)

Hii ni sehemu ya tatu ya mfululizo wa masomo kwa wanawake, katika sehemu ya kwanza  na ya pili tumeona, ni kwanini Bwana aliwatambua baadhi ya wanawake, kwa jinsia zao, na sio kwa majina yao, kwa kuwaita “wanawake”, na sehemu nyingine kuwatambua kwa mionekano yao kwa kuwaita “Binti” na sio labda kwa majina yao..ipo sababu, ikiwa hujapata bado, chambuzi zake, basi tutumie msg inbox tukutumie..

Lakini leo tutasonga mbele tena, kuona ni kwanini baadhi ya wanawake, aliwatambua kwa majina ya “MAMA”.

Mama ni cheo cha ukomavu, kwasababu mpaka uitwe mama ni wazi kuwa lazima utakuwa na watoto uliowazaa au unaowalea chini yako. Sasa tukirudi kwa Bwana Yesu, kuna wanawake aliwaona ni “Wamama rohoni”, sio mwilini, kwasababu kulikuwa na wanawake wengi, lakini si wote aliwaita “Mama” kama tu vile si wote aliwaita “Binti yangu”, bali baadhi tu.

Sasa embu twende tukasome baadhi ya Habari katika biblia kisha tuone, ni nini Bwana anatufundisha katika Habari husika. Mwanamke wa kwanza tutakayemtazama ni yule mkananayo. Tusome;

Mathayo 15:21 “Yesu akaondoka huko, akaenda kando pande za Tiro na Sidoni.

22 Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.

23 Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.

24 Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.

25 Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie.

26 Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.

27 Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.

28 Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, MAMA, IMANI YAKO NI KUBWA; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile”.

Angalia asili ya huyu mwanamke, hakumtafuta Bwana kwa shida zake mwenyewe, au kwa matatizo yake mwenyewe, bali alimtafuta Bwana Yesu kwa shida za mwanawe.. Japokuwa mwanzoni hakujibiwa chochote, hata baada ya pale alipewa na maneno ya kukatishwa tamaa ya kuitwa mbwa, lakini bado hakuacha kuomba kwa shida ya mtu mwingine, kwasababu uzito wa mwanae ulikuwa kama wakwake.

Hiyo ni kuonyesha ni jinsi gani asivyojali vya kwake tu, bali hata vya wengine…

Mwanamke mwingine ni Mama yake Yesu mwenyewe, ambaye tunamsoma katika Yohana 2:1-4 siku ile alipoalikwa katika Harusi..

Yohana 2:1 “Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo.

2 Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.

3 Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai. 4 Yesu akamwambia, MAMA, TUNA NINI MIMI NAWE? Saa yangu haijawadia”.

Angalia tabia yake alijali shida za wengine, aibu za wengine, akazifanya kama ni za kwake. Na kumpelekea Kristo, na muda huo huo akamwita “mama”

Mwingine ni Mariamu Magdalena, asubuhi ile ya kufufuka kwa Bwana, alikuwa akilia pale makaburini ndipo Yesu akamtokea na kumwambia “Mama unalilia nini?” Saa hiyo hiyo Yesu akamtuma kwa ndugu zake kwenda kuwatangazia injili. Akawa mtu wa kwanza kupewa neema ya kuwahubiria watu wengine Habari za kufufuka kwa Bwana Yesu. (Yohana 20:11-18)..

Neema hiyo si kila mwanamke atapewa, bali ni wale “wamama rohoni tu” Wanawake waliokomaa kiroho,ambao wanajua wajibu wao kwa Bwana, wanajua kuwaongoza wengine katika njia za Mungu, haijalishi umri wao Rohoni watu kama hawa, wanawekwa kundi moja na akina Sara, na Rebeka, na Mariamu, na Elizabeti na wengineo. Kwasababu wamevuka viwango cha utoto, hadi kufikia hatua ya utu uzima ya kuzaa na kulea.

Swali ni je! Wewe, dada upo katika kundi gani? Bwana anapokuona anakutambuaje? msichana? Au Mtu? Mtoto? Au Mama?. Kabla hujafikiria kuyatazama Maisha ya mitume wa Yesu mfano wakina Petro waliishije, embu tafakari kwanza, Maisha ya wanawake wacha Mungu katika biblia waliishije. Hiyo itakusaidia sana mwanamke.

Tamani sana, Kristo akutambue kama “Mama” Ni heshima ya juu sana, Kristo anaweza kumpa mwanamke, iliyosawa na ya “Kitume”. Kua kiroho timiza wajibu wako wa kuitangaza injili na pia kuwasaidia wengine kumjua Mungu rohoni.

Bwana akubariki.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post