Je! Watu ambao hawajawahi kusikia injili kabisa siku ya mwisho watahukumiwa?

Je! Watu ambao hawajawahi kusikia injili kabisa siku ya mwisho watahukumiwa?

JIBU: Kumbuka Mungu ameiandika injili yake katika sehemu kuu mbili. Sehemu ya kwanza ni katika kitabu, na sehemu ya pili ni katika moyo wa mwanadamu.

Watu wengi tunadhani, ni mpaka tusikie ndio tutahukumiwa hapana, hiyo ni sehemu ya kwanza, lakini kuna sheria ambayo Mungu tayari kashiweka katika moyo wa kila mwanadamu ajapo hapa duniani, ambayo hiyo inathibitishwa na kutetewa na “dhamiri na mawazo” ya mtu mwenyewe.

Biblia inasema..

Warumi 2:14 “Kwa maana watu wa Mataifa wasio na sheria wafanyapo kwa tabia zao yaliyo ndani ya torati, hao wasio na sheria wamekuwa sheria kwa nafsi zao wenyewe.

15 Hao waionyesha KAZI YA TORATI ILIYOANDIKWA MIOYONI MWAO, dhamiri yao ikiwashuhudia, na mawazo yao, yenyewe kwa yenyewe, yakiwashitaki au kuwatetea;”

Umeona? Ikiwa na maana kuwa, hata ukienda katika jamii za watu ambao wamejitenga kabisa huko maporini, hawajui chochote kinachoendelea ulimwenguni, kazi yao ni kuwinda na kukusanya tu..bado utawakuta na tabia ambazo zinaendana kabisa na sheria za Mungu, kana kwamba wanaijui torati. Kwamfano utakuta wanapinga vitendo vya uuaji, wizi, au uzinzi n.k.

Mambo kama hayo, hawakuyasoma kwanza kwenye biblia, bali tayari yalishaandikwa mioyoni mwao kana kwamba walikuwa wanaijua biblia. Na ndio katika hayo Mungu atawahukumu. Kwasababu kama tulivyosoma hapo, kwamba kama mtu atafanya yaliyo ndani ya sheria, hata kama hajaisikia, basi tayari anaitenda sheria hiyo ndani ya moyo wake.

Lakini wakati wasasa tunaoishi, injili ya Kristo imeshasambaa ulimwenguni kote, Tumesikia, na bado mioyo yetu inatushuhudia. Haijalishi utaiamini, au huiamini,  Hivyo tujue kuwa tusipoitii hatutakuwa na udhuru siku ile ya hukumu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

JE! WATOTO WACHANGA WANAWEZA KUHUKUMIWA NA KUTUPWA MOTONI.

Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

NI LIPI KATI YA MAKUNDI HAYA, WEWE UPO?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments