Je mbinguni itakuwa ni kuimba tu wakati wote?.

Je mbinguni itakuwa ni kuimba tu wakati wote?.

Jibu: Hakuna andiko lolote katika biblia linalosema mbinguni ni mahali pa kuimba tu wakati wote!. Bwana Yesu alisema anakwenda kutuandalia makao..

Yohana 14:1 “Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.

2  Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali.

3  Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo”.

Umeona hapo anasema anaenda kutuandalia Makao, maana yake makazi..Na tena anasema yapo makao Mengi! (Si machache)…Na sehemu yoyote yenye makao/ makazi maana yake kuna shughuli nyingi, sio kuimba tu!. Kwa ufupi mbinguni itakuwa ni sehemu yenye upeo mkubwa kuliko duniani, vinginevyo basi duniani pangekuwa bora kuliko mbinguni.

Kama duniani tu! Vipo vitu vingi ambavyo vinavyowapa wanadamu raha, (ambavyo kimojawapo ndio hiyo kuimba) basi mbinguni hapawezi kuwa panyonge kuliko duniani, maana yake kule ni mara elfu elfu ya hapa.. zitakuwepo shughuli nyingi, na mambo mengi yatakayotupa raha na furaha, na sio kuimba tu!..kuimba itakuwa ni sehemu ya vitu hivyo!..Ndio maana mpaka sasa Bwana anatuandalia makao hayo, tukifika huko tutamfurahia Mungu katika viwango ambavyo hatujawahi kumfurahia.

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba mbinguni hapatakuwa ni mahali pa kuimba tu usiku na mchana, bali kutakuwepo na mambo mengine mengi, ambayo biblia inasema jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia.

1Wakorintho 2:9 “ lakini, kama ilivyoandikwa, Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, (Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,) Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao”

Kwahiyo hatuna budi kutafuta kuingia mbinguni kwa gharama zozote zile, ili tusiyakose hayo mambo mazuri tuliyoahidiwa na Baba. Na lango la kuingia mbinguni ni moja tu!, nalo ni YESU KRISTO, alisema..

Yohana 14:5 “Tomaso akamwambia, Bwana, sisi hatujui uendako; nasi twaijuaje njia?

6  Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi”

Kwa kumwamini Yesu, na kuungama dhambi zetu zote, na kubatizwa katika ubatizo sahihi, na kupokea Roho Mtakatifu, hapo tayari tutakuwa tumeshaanza safari ya kwenda mbinguni. Tutakuwa tumeshaiona njia.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

TABIA ZITAKAZOMTAMBULISHA MPINGA-KRISTO AJAYE.

BASI TUENDELEE KUMJUA MUNGU,NAYE ATATUJILIA KAMA MVUA YA VULI.

Jiepushe na tamaa ya Mali/kupenda fedha.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments