JE! WATOTO WACHANGA WANAWEZA KUHUKUMIWA NA KUTUPWA MOTONI.

JE! WATOTO WACHANGA WANAWEZA KUHUKUMIWA NA KUTUPWA MOTONI.

Je! watoto wachanga wanaweza kuhukumiwa na kutupwa motoni.


Biblia inatuonyesha kuwa watoto wachanga wanaweza kushiriki adhabu za watu wengine waovu wakiwa hapa hapa duniani kama tu vile wanavyoweza kushiriki baraka za watu wema wakiwa hapa hapa duniani ..Lakini baada ya kifo biblia haisemi kama watoto wachanga watatupwa motoni au watakwenda mbinguni..

Ipo mifano kadha wa kadha katika biblia ya watoto kuadhibiwa kwa makosa ya wengine, kwa mfano tukisoma habari za Nuhu, Tunaweza kuona Nuhu aliambiwa aingie katika Safina yeye na familia yake tu ( jumla, watu 8)..Jiulize huko nje kulikuwa na Watoto wangapi wachanga, au wanawake wangapi waliotoka tu kujifungua muda mfupi kabla ya gharika kuanza,..Lakini ulipofika wakati wa Mungu kuuondoa uovu ulimwenguni kote, waliarithiwa na Watoto nao ambao kwa jicho letu la kibinadamu tunaweza kusema walikuwa hawana hatia yoyote..

Vivyo hivyo katika Sodoma na Gomora, walipona watu watatu (3) tu kati ya maelfu kama sio mamilioni ya Watu (ikiwemo na Watoto wadogo) waliokuwepo katika miji ile.

Utaona sehemu nyingi katika biblia, Mungu akitoa laana kwa mtu mwovu ambayo wakati mwingine  haiishii kwake tu, bali inakwenda kuwaarithi mpaka wazao wake wote. Soma (2Samweli 21:1-10, Yoshua 7:1-26,)

Daudi alipomwasi Mungu na kwenda kuzini na mke wa Uria, kilichotokea, ni Mungu kumpiga yule mtoto aliyemzaa kwa maradhi hadi mwisho wa siku akafa, hiyo yote ilikuwa ni kwasababu ya kosa la Daudi kuimwaga damu isiyo na hatia na kulala na mwanamke ambaye hakuwa mke wake.

Vilevile hata katika kipindi cha Yona kutumwa Ninawi, alipoambiwa awahubirie watu wale kuwa  zimebakia siku 40  tu mji ule uteketezwe wote…Bila shaka jambo lingejirudia lile lile, kisingesalia kitu, sio tu Watoto, bali pia mifugo ambayo haina hatia yoyote, lakini walipotubu Mungu akaurehemu mji ule..Na sikia Mungu alichomwambia Yona..

Yona 4:11 “na mimi, je! Haikunipasa kuuhurumia Ninawi, mji ule mkubwa; ambao ndani yake wamo watu zaidi ya mia na ishirini elfu, wasioweza kupambanua katika mkono wao wa kulia na mkono wao wa kushoto; tena wamo wanyama wa kufugwa wengi sana”?

Unaona hao wasioweza kupambanua mkono wao wa kulia kutoka katika mkono wao wa kushoto wengi wao ni Watoto.

Hivyo dhambi ni mbaya sana, Na inatabia ya kuambukiza,,Na ndivyo itakavyokuja kuwa hata katika mwisho wa dunia..Siku Mungu atakapokuja kuteketeza kila kitu, Adhabu itawakuta wote…

Lakini kuhusu hukumu ya Watoto kwenda kutupwa katika ziwa la moto. Hilo hatulijui, lakini tunachojua ni  kuwa Mungu ni Mungu wa haki. Hawezi kumuhukumu mtu kwa kosa ambalo halijui. Watoto wachanga hawawezi kutofautisha kati ya jema na baya, kama ni hivyo basi hapo  tunaweza kusema hakuna hukumu ya adhabu juu yao..

Mithali 8:20 “Natembea katika njia ya haki, Katikati ya mapito ya hukumu”.

Zaidi ya yote biblia inawachukulia Watoto wachanga kama mfano mzuri wa kuigwa kwa wale watakourithi ufalme wa mbinguni..

Mathayo 19:14  “Lakini Yesu akasema, Waacheni watoto wadogo waje kwangu; wala msiwazuie; kwa maana walio mfano wa hao, ufalme wa mbinguni ni wao”

Unaona anasema tena. …

Mathayo 18:2  Ni nani basi aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni? Akaita mtoto mmoja, akamweka katikati yao,

3  akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.

Unaona, tabia za Watoto  ni tabia zenye sifa njema mbinguni kwahiyo hapo tunaweza kupata picha kuwa Watoto ambao bado hawajajitambua, wanaweza kuwepo mbinguni wote, lakini pale wanapojitambua tu, kwamba wanaweza kutofautisha kati ya mabaya na mema haijalishi watakuwa katika umri gani iwe ni miaka 6 au 10, hao moja kwa moja watapanda hukumuni. Na kama wamestahili kuzimu watakwenda kuzimu,  kama wamestahili uzima watakwenda uzimani.

Kwasababu biblia inasema, siku ile ya hukumu watakuwepo wakubwa kwa wadogo ili wahukumiwe..

Ufunuo 20:12  “Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao”

Hivyo kwa kuhitimisha. Upo uwezekano mkubwa  kwa Watoto wote wachanga wanaokufa kuwepo mbinguni. Japo suala la hukumu tunamwachia Mungu mwenyewe..hivyo Kikubwa tu tuwalee Watoto wetu katika njia iwapasayo, ili  atakapofikia umri ule wa kuweza kupambanua mema na mabaya basi wawe katika mstari mzuri wa kumtii Mungu ili hata ikitokea kwa bahati mbaya amefariki hapo katikati basi tuwe na uhakika wapo katika mikono ya Mungu.

Ubarikiwe sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Mbona Mungu anaruhusu watu wapate shida, ilhali ana uwezo wa kutuepusha?

KILEMBA CHA NEEMA, JE! UMEMVIKA MWANAO?

LENGO LA SHETANI KWA WATOTO WA KIZAZI HIKI.

JE! UNAYO NAFASI MBINGUNI?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

USIWE NA HAKI KUPITA KIASI.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Awey
Awey
1 year ago

Aminaa hii pia ilikua moja Kati ya swali nililo kuwa najiuliza mara Kwa mara sasa nimeelewa jambo hapo

M
M
1 year ago

Amina