Sasa mambo hayo yalikuwa ni zamani wakati utandawazi haujawa mkubwa je! leo hii itakuwaje? Kwa watoto wa leo, siku hizi sio TV tu peke yake, kuna simu tena zenye internet, Kuna magemu, ya kila aina kwenye simu za wazazi, na kibaya zaidi magemu yenyewe ukiangalia karibu yote yanadhima za kipepo ndani yake, kwamfano, magemu kama , House of the dead, mortal combat, spiderman, Zuma, Diablo.Titan n.k.Pia Kuna magemu mengine yanakuwepo sana kwenye simu unakuta mtu analiendesha au anakimbizwa na limnyama fulani la ajabu kutoka pangoni , na yeye anajaribu kulikimbia,(Nadhani utakuwa unalifahamu) sasa vitu kama hivi watu waliovitengeneza hawajavibuni tu ilimradi hapana bali wamevitoa kama vilivyo katika ulimwengu wa roho wa kishetani (ni vikundi maalumu kabisa vya kishetani vinavyofanya hizi kazi), wanachofanya ni kuchukua taswira yenye uwezo wa kama hayo mapepo na kuyatengenezea magemu yanayofanana nao pamoja na kazi zao.