Inaruhusiwa Kula nyama ya Nguruwe kwa Mkristo wa Kweli?

Inaruhusiwa Kula nyama ya Nguruwe kwa Mkristo wa Kweli?

1).Inaruhusiwa Kula nyama ya Nguruwe kwa Mkristo wa Kweli? 2).Mkristo wa Kweli Anaruhusiwa Kunywa Pombe/kuvuta sigara? 3).Ubatizo Wa Mkristo Wa Kweli Ni Wa Namna Gani?

JIBU: Kwa ufahamu hakuna tatizo lolote kula nyama ya nguruwe au chakula chochote ambacho mtu anaweza kukipokea kwa shukrani mbele za Mungu…biblia inasema viumbe vyote vimetakaswa na Mungu, Tukisoma

1Timotheo 4:1-5 inasema..

“Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;

2 kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe;

3 wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru WAJIEPUSHE NA VYAKULA, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli.

4 Kwa maana kila kiumbe cha Mungu ni kizuri, wala hakuna cha kukataliwa, kama kikipokewa kwa shukrani; 5 kwa kuwa kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba.”

Hivyo vyakula vyote ni halali lakini biblia inasema tule tu kwa IMANI, ila tukila kwa mashaka ni dhambi, na pia biblia inasema anayekula asimuhukumu yeye asiyekula, wala asiyekula asimuhukumu anayekula, kwasababu tumetofautiana ujuzi, haupaswi kumkwaza mwenzako(Ndugu yako) kwa ujuzi ulionao, ukimkosea mwenzako kisa hali nguruwe ni sawa na kumkosea Kristo mwenyewe

1wakorintho 8:13 inasema “Kwa hiyo, chakula kikimkwaza ndugu yangu, hakika sitakula nyama hata milele, nisije nikamkwaza ndugu yangu.”…..

8:8 Lakini chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu; maana, tusipokula hatupunguziwi kitu, wala tukila, hatuongezewi kitu.    

Hivyo tunafundishwa tuwe na hekima tunapokuwa katikati ya jamii fulani ya watu, iwe ni wakristo au isiwe wakristo, sio tunapofika mahali na kukuta jamii fulani hawali chakula fulani (nguruwe), na sisi tunaanza kula mbele yao na kuwaudhi. Hivyo ni sawa na kumkosea Kristo, ndio maana Paulo anasema ni “heri nisile nyama kabisa kama itakuwa ni kikwazo kwa ndugu yangu.”  

Na pia tukisoma.

Warumi 14:14 “Najua, TENA NIMEHAKIKISHWA SANA KATIKA BWANA YESU, YA KUWA HAKUNA KILICHO NAJISI KWA ASILI YAKE, lakini kwake yeye akionaye kitu kuwa najisi, kwake huyo kitu kile ni najisi.

15 Na ndugu yako akiingia huzuni kwa sababu ya chakula, umeacha kwenda katika upendo. Kwa chakula chako usimharibu mtu yule ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake.

16 Basi, huo wema wenu usitajwe kwa ubaya.

17 Maana ufalme wa Mungu si kula wala kunywa, bali ni haki na amani na furaha katika Roho Mtakatifu. ” 

Hivyo katika agano la kale Mungu kukataza vyakula fulani visiliwe ni kwa ajili ya kutufundisha sisi wa agano jipya mambo kadha wa kadha, kwamfano, kama vile Bwana alivyotenga vyakula najisi na visafi, ilifunua rohoni kuwa kuna vyakula vilivyo visafi na najisi (mafundisho) hivyo wajitenge na vile vichafu, na kudumu katika vile vilivyo safi, kadhalika pia, ilifunua aina mbili za watu yaani waliowasafi(wayahudi), na walionajisi kwa wakati ule (mataifa) lakini Bwana alipokuja aliwatakasa wanadamu wote,(soma Matendo 10:9) kama aliwatakasa wanadamu je! si zaidi viumbe vyake vyote?..n.k.  

2) Mkristo wa kweli haruhusiwi kunywa pombe wala kuvuta sigara wala kuuharibu mwili wake kwa namna yoyote ikiwemo kuchora alama kwenye miili(Tatoo),uzinzi, mustarbation n.k. kwasababu biblia inasema miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, hivyo hekalu la Mungu lazima liwe ni safi.

 1Wakorintho 3:16 “Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?

17 Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, MUNGU ATAMHARIBU MTU HUYO. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi”.

  3) Kuhusu ubatizo, ubatizo sahihi kulingana na maandiko ni wa kuzamishwa katika maji mengi, na inapaswa iwe ni katika JINA LA YESU KRISTO, kulingana na maandiko na sio kwa jina la BABA na Mwana na Roho Mtakatifu, kama inafanyika kimakosa na makanisa mengi, kwa ufafanuzi mrefu kuhusu UBATIZO SAHIHI fuata link hii  >> https://wingulamashahidi.org/2018/07/19/ubatizo-sahihi/

Ubarikiwe sana. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada zinazoendana:

USITAFUTE FAIDA YAKO MWENYEWE BALI YA WENGINE.

BWANA YESU ANAMAANISHA NINI KUSEMA MKAIHUBIRI INJILI KWA KILA KIUMBE?

UMEITIKIA WITO INAVYOPASWA?

BABA YANGU ANATENDA KAZI HATA SASA!.

MAMBO (2) YATAKAYOKUTENGA NA IMANI SIKU HIZI ZA MWISHO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
14 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
vigey B Venas
vigey B Venas
1 year ago

sijaelewa kabisa kuhusu ubatizo mahana kuna ubatizo wa aina nyingi sana kuna wa maji mengi na

Prosper
Prosper
1 year ago

Vipi sasa kuhusu Ili andiko mimi sijaielewa vizuri ni fafanulia
Kumbukumbu la torati 14:8 inasema
Na nguruwe,kwa kuwa amepasuliwa ukwato lakini hacheui,huyu ni najisi kwenu msile nyama zao, wala mizoga yao msiiguse

Bonventure shibonje
5 months ago
Reply to  Admin

Ningependa kujua ni kwa sababu gani katika agano la kale Mungu kakataza watu Kula nguruwe na baadhi ya wanyama?

Japhet nyanga
Japhet nyanga
1 year ago

Ndo kwa imani ya maelezo yako unamaanisha bibilia inaruhusu kula kila kiumbe akiwemo nguruwe?

Nema
Nema
1 year ago
Reply to  Japhet nyanga

Upo kama mim najua yakwamba agano la kale limekataza baadh ya vitu ila kuusu agano jipya baada ya Yesu Kristo kuja tunaambiwa vmetakaswa hakuna alivo vitakasa Mungu usivinene ni najisi
Matendo 11.5-10
Petro aliletewa wanyama na ndege achinje akasema hajawahi kula kilicho kichafu au najis ila roho mtaka tifu alimjibu alivo vtakasa Mungu usiviite najis

Erastus ouma
Erastus ouma
2 years ago

Asante sana ndugu zangu watanzania naomba kujua njia ya kumjua Mungu kama mwokozi wa maisha yangu

Anonymous
Anonymous
1 year ago
Reply to  Admin

sijaelewa kabisa kuhusu ubatizo mahana kuna ubatizo wa aina nyingi sana kuna wa maji mengi na

elifuraha
elifuraha
2 years ago

Agizo la Yesu Kristo kwenye Mathayo 28: 18-20 inasemaje kuhusu kubatiza?
“Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi, nendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari”.
kwa ufupi ni kwamba Mungu Baba, Mwana (Yesu Kristo) pamoja na Roho Mtakatifu wote ni wamoja yaani hunia mamoja, hupatana kwa shauri moja. Hivyo Kubatizwa kwa Jina La Yesu Kristo ni sawa na Kubatizwa kwa majina yote matatu. ubarikiwe sana

Anonymous
Anonymous
1 year ago
Reply to  elifuraha

Amen asante kwa kumsahihisha kidogo

Anna
Anna
10 months ago
Reply to  Anonymous

Wapo madhehebu wanaobatizwa kwa maji mengi kwa nilivyoelewa andiko ni kwamba kabla Yesu kuja duniani ,watu walibatizwa kwa maji mengi lakini baada ya Yesu kuja akaagiza watu wabatizwe kwa jina la baba na la mwana na la Roho Mtakatifu kwa sababu Yesu tayari alikua ameshapewa mamlaka yote baada ya kifo na kufufuka kwake