Title July 2022

NI NINI TUNAJIFUNZA KWA YOANA NA MANAENI?

Kama unadhani mazingira ni sababu ya wewe kutokuwa Mwanafunzi wa Yesu, basi tafakari mara mbili!.

Unaweza kusema labda Nimezaliwa katika dini inayompinga Kristo, nawezaje kuwa Mkristo tena yule wa kujikana nafsi?..nimeolewa na mtu ambaye anampinga Bwana Yesu? Na familia yangu yote haimwamini Yesu wala haiamini Ukristo..je inawezekana mimi kuwa mkristo na kuanza kwenda kanisani na hata kumtumikia yeye?

Jibu ni Ndio! Yote yanawezekana endapo utaamua kujikana nafsi kwa kumaanisha kumfuata Yesu..

Inawezekana kabisa kuwa mwanafunzi wa Yesu, na hata kuifanya kazi yake. Wewe sio wa kwanza kukutana na  mazingira kama hayo, hata katika biblia walikuwepo watu wa namna kama yako, ambao walikutana na mazingira magumu kuliko yako, lakini walishinda…lakini pia walikuwepo  walioshindwa..

Hebu tujifunze katika makundi yote mawili, ya walioshindwa na walioshinda.

1 . WALIOSHINDWA.

Tusome,

Yohana 12:42 “Walakini hata katika wakuu walikuwamo wengi waliomwamini; lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakumkiri, wasije wakatengwa na sinagogi”.

Hawa ni Wayahudi, ambao walimwamini Kweli Yesu lakini, walihofia kutengwa na ndugu zao na zaidi sana masinagogi yao, yaani watu wa dini yao!. Hivyo wakaishia tu kumwamini Yesu lakini hakuna chochote walichozalisha.

2 . WALIOSHINDA.

Lilikuwepo ambalo lilikuwepo katika mazingira magumu, lakini lilishinda.

Mfano wa hao ni YOANA MKEWE KUZA, wakili wa Herode. Na MANIELI ndugu wa Herode.

YOANA, MKEWE KUZA.

Huyu Yoana, alikuwa ni mke wa mtu aliyeitwa Kuza, ambaye alikuwa ni wakili wa mfalme Herode. Sasa ili kujua vizuri familia ya Herode ilikuwa ni ya watu wa namna gani, tusome mistari ifuatayo..

Mathayo 2:16 “Ndipo Herode, alipoona ya kuwa amedhihakiwa na wale mamajusi, alighadhabika sana, akatuma watu akawaua watoto wote wanaume waliokuwako huko Bethlehemu na viungani mwake mwote, tangu wenye miaka miwili na waliopungua, kwa muda ule aliouhakikisha kwa wale mamajusi”.

Herode alimtafuta kumwua Bwana Yesu katika uchanga wake, na hata kipindi amekuwa mkubwa mwanae alimkata kichwa Yohana mbatizaji.(Mathayo 14:1-10), na Zaidi sana baadaye alikuja kumwua Yakobo, mtume wa Bwana Yesu (Matendo 12:1-2) na alitafuta kumwua na Petro pia, lakini Bwana alimwepusha na mauti yake hiyo..

Kwahiyo kwa ufupi ni kwamba Herode alikuwa ni mpinga Kristo kwa wakati huo, na endapo angesikia yeyote katika watu wake kajishikamanisha na Bwana Yesu, wazo lake ni lile lile la kuua.. lakini tunaona huyu mke wa Wakili wake, aliyajua hayo yote, na Pamoja na hayo, akaamua kumfuata Yesu na kuwa mwanafunzi wake, pasipo kujali atapitia nini mbeleni.

Na tena sio yule mwanafunzi wa siri siri, bali yule wa wazi kabisa..ambaye anaambatana na Bwana Yesu kila mahali, na tena anamhudumia..

Luka 8:1 “Ikawa baada ya hayo alikuwa akizunguka-zunguka katika miji na vijiji akihubiri na kuitangaza habari njema ya ufalme wa Mungu; na wale Thenashara walikuwa pamoja naye,

2 na wanawake kadha wa kadha ambao walikuwa na pepo wabaya na magonjwa wakaponywa; nao ni Mariamu aitwaye Magdalene aliyetokwa na pepo saba,

3 NA YOANA MKEWE KUZA, WAKILI WAKE HERODE, na Susana, na wengine wengi, waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao”.

Umeona?..Yoana alijua kuna kifo kinamgoja wakati wowote, lakini alijikana nafsi na akawa moja ya wanawake wa mbele kabisa walioheshimiwa na Bwana Yesu.

MANAENI

Sio huyo tu! Kulikuwepo na mwanaume mwingine anayeitwa Manaeni..Huyu maandiko yanasema alikuwa ni NDUGU WA KUNYONYA wa Mfalme Herode…maana yake wametoka katika familia moja na Herode, wanajuana ndani na nje!.. lakini pamoja na kwamba anajua ndugu yake ni mfalme tena Mpinga-Kristo, yeye hakumwogopa.. bali aliacha vyote akachukua msalaba wake, akamfuata Yesu, na hatimaye Bwana akamfanya kuwa NABII wake.

Matendo 13:1” Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na MANABII NA WAALIMU, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na MANAENI ALIYEKUWA NDUGU WA KUNYONYA WA MFALME HERODE, na Sauli.

2 Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia”.

Kupitia watu hawa wawili YOANA Pamoja na MANAENI, itoshe kutupa kila sababu ya sisi kujikana nafsi!.

Watu hawa watasimama siku  ya hukumu Pamoja na sisi, ambao tunasema tupo katika mazingira magumu ya kumfuata Yesu, watatuhukumu.

Hivyo ndugu kama wewe umeolewa na mtu asiye mkristo, na sasa umemwamini Yesu, usione aibu wala usiogope, mkiri Kristo hadharani…kama wewe unaishi na wapagani ambao hawamwamini Yesu au wanampinga!.. bali usiwaogope.. wewe mfuate Yesu, kuwa mwanafunzi wake, jikane nafsi kama Yoana na Manaeni. Na Bwana Yesu atakuheshimu kuliko kawaida, atakutukuza kama alivyowatukuza Yoana na Manaeni.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI.

Maherodi walikuwa ni akina nani, Na kazi yao ilikuwa ni ipi?

NI NANI ALIYEKUPA MAMLAKA HII UYATENDE HAYA?

Wanafunzi wa Yesu, walimaanisha nini kusema kama “Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa”?

Kwanini Herode aliwakasirikia watu wa Tiro na Sidoni? (Matendo 12:20)

Rudi nyumbani

Print this post

NA WATU WOTE WALIKUWA WAKIAMKA MAPEMA, WAENDE HEKALUNI.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe karibu tujifunze biblia,

Luka 21:37 “Basi, kila mchana alikuwa akifundisha hekaluni, na usiku huenda kulala katika mlima uitwao wa Mizeituni

38 NA WATU WOTE WALIKUWA WAKIAMKA MAPEMA WAENDE HEKALUNI ILI KUMSIKILIZA”.

Je unaijua sababu ya Bwana Yesu kulala juu ya mlima wa mizeituni?

Si kwasababu hakuwa na watu wa kumkaribisha kwake awe analala kwao? La! alikuwa nao tele!!, na wengine wenye uwezo mkubwa tu!.. mfano wa hao ni Yule Yusufu mwanafunzi wake ambaye alikwenda kumwomba Pilato auondoe mwili wake pale msalabani, maandiko yanasema alikuwa ni mtu tajiri.

Mathayo 27:57 “Hata ilipokuwa jioni akafika MTU TAJIRI wa Arimathaya, jina lake Yusufu, naye mwenyewe alikuwa mwanafunzi wa Yesu;

58 mtu huyu alimwendea Pilato akauomba mwili wa Yesu. Ndipo Pilato akaamuru apewe”.

Mwingine ni Yule aliyempa chumba Bwana Yesu wakati wa Pasaka, (maandiko yanasema mtu huyu alikuwa ni mtu anayemiliki ghorofa, na kuna chumba maalumu, juu ya ghorofa ambacho alikuwa amempa Bwana Yesu na wanafunzi wake).

Marko 14:13 “Akatuma wawili katika wanafunzi wake, akawaambia, Nendeni zenu mjini; atakutana nanyi mwanamume amechukua mtungi wa maji; mfuateni;

14 na po pote atakapoingia, mwambieni mwenye nyumba, Mwalimu asema, Ki wapi chumba changu cha wageni, niile pasaka humo, pamoja na wanafunzi wangu?

15 Naye mwenyewe atawaonyesha orofa kubwa, imeandikwa tayari; humo tuandalieni”.

Umeona?..watu hawa wote walikuwa wanaishi pale pale Yerusalemu, ambao wangeweza kumhifadhi Bwana kipindi yupo Yerusalemu…na sio hao tu, bali pia walikuwepo  na wengine wengi,

Lakini jiulize kwanini Bwana kipindi anakaribia kuteswa hakuwa anakwenda kulala katika nyumba zao?.. Sababu zipo mbili. 1) KUOMBA. na  2) KUWAHI IBADANI.

KUOMBA.

  Bwana Yesu alikuwa ni mtu wa kuomba sana..na alijua mazingira bora ya kuomba ni yapi?, si ghorofani wala nyumbani. Bali ni sehemu iliyo na utulivu. Alijua Nyumbani kunakuwa na usumbufu mwingi ambao ungeweza kumwondoa katika uwepo,(usumbufu wa watu na kimazingira), Ndio maana utaona mara kadhaa akipanda mlimani pamoja na wanafunzi wake kuomba.. Hiyo ikitufundisha na sisi tuwe watu wa kuchagua mazingira sahihi ya kuomba.

KUWAHI IBADANI.

Sababu ya pili ya Bwana Yesu kulala katika mlima wa Mizeituni, ni ili AWAHI IBADANI. Alijua mazingira ya nyumbani si mazingira ambayo si rafiki kwa yeye kuwahi hekaluni.. kwasababu ya maandalizi kuwa mengi..

 Utaona kipindi tu yupo kwa akina Miriamu na Martha, ni jinsi gani, Martha alivyokuwa anamhangaikia kumwandalia vyakula, mara  chai, mara maji ya kunawa na kadhalika…mahangaiko yale, yakachukua mpaka muda wa kuanza kujifunza, mwisho Bwana Yesu ikabidi aanze kufundisha kabla hata ya Martha kumaliza kupika.. na kilichofuata utaona Martha!, alikwazika!..

Sasa mambo kama hayo hayo Bwana Yesu aliyajua ndio maana akatafuta mlima uliopo na hekalu awe analala huko kipindi anaendesha semina ya Masomo pale Hekaluni.

Kwasababu kukisha pambazuka tu, kazi aliyo nayo ni yeye pengine ni kunawa tu uso na kuteremka hekaluni kufundisha, pengine ingemchukua tu robo saa, kufanya maandalizi, tofauti na angekuwa nyumbani kwa watu..kwasababu Mlima wa Mizeituni na hekaluni ni mita kadhaa tu, si mbali..!

Hivyo Bwana Yesu akawa anawahi hekaluni mapema sana, wa kwanza kabla ya wote!..na kuwafundisha wale waliowahi kama yeye (akawa kielelezo). Na wengine wote walipoona kuwa anawahi, na kumkuta akifundisha wachache waliowahi kama yeye, na wenyewe wakawa wanaamka asubuhi na mapema kwenda kumsikiliza, wasikose madarasa hayo ya asubuhi..

Luka 21:37 “Basi, kila mchana alikuwa akifundisha hekaluni, na usiku huenda kulala katika mlima uitwao wa Mizeituni. 38 NA WATU WOTE WALIKUWA WAKIAMKA MAPEMA WAENDE HEKALUNI ILI KUMSIKILIZA”.

Kristo hata leo anawahi asubuhi na mapema Nyumbani kwake!.. na wote walio wake kweli kweli, wanawahi nyumbani kwake kumsikiliza! Na wanapokea Baraka!.

Katika siku hizi za mwisho, shetani anawaharibu wengi katika eneo la USINGIZI, na KUTOKUJALI. Asilimia kubwa ya watu wanaochelewa ibadani, au wasiofika kabisa ibadani ni kwasababu ya Usingizi!, au Kutokujali.

Kama kweli unamjali Bwana Yesu na maneno yake, huna sababu yoyote ya KUCHELEWA IBADANI, hata kama unakaa mbali na kanisa!, Amka mapema wahi kanisani!, KATISHA USINGIZI!!..Tabia ya kupenda usingizi kimwili, inafunua tabia ya kupenda usingizi katika roho, ambayo ni mbaya sana.

Na kama ukiona mahali ulipo ni mbali sana, basi siku moja kabla ya ibada, hamia karibu na maeneo ya kanisa, au kisha kanisani omba, asubuhi yake uamkie nyumbani kwa Bwana, utakuwa umejizolea Baraka nyingi zaidi.

Lakini kama utafika  nyumbani kwa Bwana kwa kuchelewa kwasababu ya usingizi!.. basi ni heri usingefika kabisa kanisani hiyo siku, kwasababu hakuna chochote unachokwenda kupokea hiyo siku!!, ni heri urudi nyumbani ukamalizie usingizi wako tu!!. Tabia ya KUPENDA USINGIZI na ya KUTOKUJALI ni tabia zinazomchukiza Bwana kuliko zote (soma Luka 22:46, Marko 13:35-37).

Na kumbuka hakuna maombi ya kuondoa KUONDOA USINGIZI!!..Dawa ya kuushinda usingizi ni kuamua kubadilisha tabia tu!, na wala si kuombewa!!.. Bwana Yesu alipowakuta akina Petro wamelala muda wa kuomba, hakwenda kukemea mapepo ndani yao!.. alichofanya aliwaambia WAAMKE WAOMBE!.. Roho zao zi radhi, lakini miili ndio midhaifu, hivyo wajilazimishe waamke!.

Na wewe leo hii, Amka mapema nenda Ibadani, amka mapema nenda kwenye maombi, amka mapema nenda shambani kwa Bwana, Ukatae usingizi, na pia Acha kuwa mtu wa KUTOKUJALI.

Bwana atubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NAWAAMBIA MAPEMA!

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Mlima wa Mizeituni  unaumuhimu gani kwetu?

Rudi nyumbani

Print this post

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

Sehemu ya kwanza: LIA NA NYONYA.

Nakusalimu katika jina kuu lenye uweza la mwokozi wetu Yesu Kristo, sifa na heshima vina yeye milele na milele.

Haya ni Makala maalimu kwa waongofu wapya, ikiwa wewe umeokoka hivi karibuni, au una ndugu/mpendwa ambaye amempokea Bwana Yesu siku za karibuni basi Makala hizi ni muhimu sana kwako au kwa yule mwingine.

Tunaposema kuokoka, tunamaanisha Kuzaliwa mara ya pili. Na mtu anazaliwa mara ya pili, Kwa kutubu dhambi zake kwa kumaanisha kabisa kuuacha ulimwengu, na pia kwa kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi (Yohana 3:23), na kwa jina la Yesu Kristo (Matendo 2:38), Na kwa kupokea Roho Mtakatifu..Kwa kuzingatia hivyo vigezo, basi mtu huyo anakuwa ameshazaliwa mara ya pili.

Lakini sasa hilo peke yake halitoshi, Wengi wanapotimiliza maagizo hayo wanajisahau na kudhani ndio tayari wameshatimilika, hakuna cha ziada.. Hawajui kuwa  mtu unaweza ukawa kweli umezaliwa mara ya pili lakini ni kiumbe kilicho kufa.. Utajiuliza ni kwa namna gani inakuwa hivyo?

Mtu anayezaliwa mara ya pili katika roho anafananishwa na mtoto, anayezaliwa mara ya kwanza katika dunia. Kwa kawaida mtoto huyo, ni lazima aonyeshe tabia kuu mbili. Kabla hajaweza hata kuona, au kuzungumza, au kujitambua..Ni lazima

  1. ALIE.
  2. Baadaye ANYONYE.

ALIE kwa sababu gani.. Mtoto anapotoka tumboni mwa mama yake, anakuwa kama kiumbe mfu, wanachofanya wakunga ni kumpiga kidogo, kumshutua ila atoe sauti, wakisikia analia basi wanatambua kuwa kiumbe kilichozaliwa ni hai, hivyo baada ya muda kidogo wanamsogeza katika hatua nyingine,

Ambayo ni kunyonyeshwa.

Cha kushangaza ni kwamba mtoto yule anaposogezwa katika nyonyo ya mama yake, hakuna mtu yeyote anayemfundisha kunyonya, utaona ni yeye mwenyewe anajua wajibu wake, wa kula, ndio hapo utaona saa hiyo hiyo ataanza kufyonza maziwa kana kwamba alishawahi kufundishwa huko tumboni jukumu lake kabla hajafika duniani.

Sasa kiroho pia ndio ipo hivyo. Ikiwa wewe umezaliwa kweli mara ya pili, hizi ni hatua za awali kabisa ambazo utazionyesha. Na kupitia hizo sisi wengine tutathibitisha kweli wewe ni kiumbe kipya hai. Kwani  ni lazima utoe kelele Fulani rohoni.. Huwezi kutulia, ambao sisi tuliokomaa kiroho tutazitambua, japo wewe hutoweza kuzielewa katika hatua yako ya uchanga rohoni..

Sisi tutaona kuhangaika kwako kutaka kumsaada wa kumjua Mungu, Na sisi tukishalitambua hilo, basi tunakuwa na wajibu mkubwa sana wa kukusaidia, kukosegezea matiti (Neno la Mungu) unyonye..

Embu tujifunze kisa cha Musa, pindi anazaliwa..Biblia inatuambia, alipozaliwa, mama yake alimficha ili Farao asimuue, lakini alipoona hali imekuwa  mbaya, alimtengenezea kisafina kidogo, kisha, akamtupa mtoni.. Lakini mtoto yule alipokuwa katika kila kisafina, hakukaa kimya tu, bali alikuwa anapiga kilele, analia,sana na binti Farao aliposikia alikwenda kutazama na kufungua aone ni nini kipo ndani, akakaona katoto, wakakahurumia..Embu tusome kwa ufupi kisa hicho;

Kutoa 2:6 “Akakifungua, akamwona mtoto, na tazama, MTOTO YULE ANALIA. BASI AKAMHURUMIA, akasema, Huyu ni mmojawapo wa watoto wa Waebrania.

7 Basi umbu lake mtoto akamwambia binti Farao, Je! Niende nikamwite mlezi katika wanawake wa Kiebrania, aje kwako, akunyonyeshee mtoto huyu?

8 Binti Farao akamwambia, Haya! Enenda. Yule kijana akaenda akamwita mama yake yule mtoto.

9 Binti Farao akamwambia, Mchukue mtoto huyu, ukaninyonyeshee, nami nitakupa mshahara wako. Yule mwanamke akamtwaa mtoto, akamnyonyesha.

10 Mtoto akakua, naye akamleta kwa binti Farao, akawa mwanawe. Akamwita jina lake Musa, akasema, Ni kwa sababu nalimtoa majini”.

Umeona? Mtoto yule angeangamia kama asingelia, lakini alipolia, akahurumiwa akatafutiwa msaada mapema wa kunyonyeshwa, na hatimaye akakua akaja kuwa Mkombozi wa Israeli, ndiye Musa tunayemsoma.

Ndugu/Dada uliyeokoka hivi karibuni, kutojishughulisha kwako na mambo ya Mungu, kunathibitisha kuwa wewe ni kiumbe mfu, kutoulizia kwako Habari ya ibada, kunatuambia kuwa wewe si kiumbe hai..Hupaswi kujificha, hupaswi kujiepusha na kiongozi wako wa kiimani..hupaswi kukaa mbali na wapendwa, hupaswi kupitisha siku nyingi hujulikani upo wapi, au maendeleo yako ya kiroho hayatambuliki.. kataa hiyo hali kwa nguvu zote..

Wewe tayari ni kiumbe kipya, yatamani sana maziwa ya roho.. Usisubiri kukumbushwa kumbushwa kuhudhuria mafundisho ya kuukulia wokovu, kama mtoto mchanga ambaye hafundishwi na mtu kunyonya ni wajibu wako kutafuta kufundishwa Neno la Mungu, kwa bidi zote..Sio wewe utafutwe.

1Petro 2:2 “Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu;”

Hivyo anza sasa kubadili mwenendo wa Maisha yako.. Jifunze kuomba na wapendwa, jifunze, kusoma biblia mwenyewe kuanzia sasa, jifunze kuuliza maswali, jifunze kumshirikisha kiongozi wako wa kiroho maendeleo yako. Atakusaidia, na kukuonyesha njia sahihi.

Wagalatia 6:6 “Mwanafunzi na amshirikishe mkufunzi wake katika mema yote”.

Hivyo zingatia mambo hayo makuu mawili. Na Bwana akutie nguvu.

Shalom.

Sehemu ya pili itafuata…

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

Maziwa yasiyoghoshiwa ni nini? Kwanini biblia inatumia mfano huo?

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

UMEITIMIZA HAKI YOTE?

ILI TUONEKANE SAFI MBELE ZA MUNGU TUFANYE NINI?

Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya wokovu watoka kwa Wayahudi? (Yohana 4:22)

Swali: Bwana alimaanisha nini kusema wokovu watoka kwa Wayahudi?, kwani si tunajua Wokovu unatoka kwa Mungu, iweje hapo aseme unatoka kwa Wayahudi?

Jibu: Tusome,

Yohana 4:22 “Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.”

Wokovu unaozungumziwa hapo, ni “Wokovu wa Roho”..na si wokovu wa vita au kitu kingine!, na aliposema kuwa “unatoka kwa Wayahudi” hakumaanisha kuwa Wayahudi ndio wanaoutoa wokovu na kuwapatia wengine la!, hakuna mtu wala Taifa linaloweza kuiokoa roho ya mtu!!, bali alimaanisha kuwa “wokovu unaanzia kwa wayahudi”, na ndipo unaenda kwa wengine…(yaani kwa watu wa mataifa ikiwemo na wasamaria ndani yake).

Ndio maana utaona ni kwanini Bwana wetu Yesu hakuzaliwa nje na jamii ya Israeli, wala hakuzaliwa katika Samaria, au katika Taifa lingine lolote tofauti na Israeli, badala yake alizaliwa Israeli, sawasawa na unabii Mungu alioutoa kupitia manabii wake wa zamani kama Musa, Daudi, na wengineo.

Na baada ya kuzaliwa katika jamii ya Wayahudi (yaani waisraeli), hakuanza kuhubiri injili yake kwa jamii ya watu watu wa mataifa, halafu ndio afuate kwa watu wa jamii ya Israeli(wayahudi) bali badala yake alianza kwanza kwa Wayahudi, na walipokataa ndipo akaruhusu injili ihubiriwe pia kwa watu wa mataifa ambao ndani yake pia wapo wasamaria.

Mathayo 10:5 “Hao Thenashara Yesu aliwatuma, AKAWAAGIZA, AKISEMA, KATIKA NJIA YA MATAIFA MSIENDE, WALA KATIKA MJI WO WOTE WA WASAMARIA MSIINGIE.

6 Afadhali shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.

7 Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia”.

Umeona?..Wanafunzi walikatazwa na Bwana kuhubiri kwa watu wa Mataifa katika mwanzo wa Injili, lakini baadaye, baada ya Wayahudi kushiba, na kukinai….Bwana Yesu aliwaruhusu pia wanafunzi wake waende kwa watu wa mataifa duniani kote wakahubiri injili kwa kila kiumbe.

Marko 16:14 “Baadaye akaonekana na wale kumi na mmoja walipokuwa wakila, akawakemea kwa kutokuamini kwao na ugumu wa mioyo yao, kwa kuwa hawakuwasadiki wale waliomwona alipofufuka katika wafu.

15 Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.

16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”.

Tunazidi kulithibitisha hili pia, kipindi Mtume Paulo anawahubiria wayahudi wa Antioko..

Matendo 13:45 “Bali Wayahudi, walipowaona makutano, wakajaa wivu, wakayakanusha maneno yaliyonenwa na Paulo, wakibisha na kutukana.

46 Paulo na Barnaba wakanena kwa ushujaa wakasema, Ilikuwa LAZIMA NENO LA MUNGU LINENWE KWENU KWANZA; lakini kwa kuwa mnalisukumia mbali, na kujiona nafsi zenu kuwa hamkustahili uzima wa milele, angalieni, twawageukia Mataifa.

47 Kwa sababu ndivyo tulivyoamriwa na Bwana, Nimekuweka uwe nuru ya Mataifa, Upate kuwa wokovu hata mwisho wa dunia.

48 Mataifa waliposikia hayo wakafurahi, wakalitukuza neno la Bwana, nao waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini”.

Umeona?.. Wokovu umeanzia kwa Wahayudi, na ukaenda kwa watu wa Mataifa. Hiyo ndio sababu ya Bwana Yesu kusema.. “Yohana 4: 22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.”

Je umeupokea Wokovu wa Bwana Yesu ambao tumeletewa sisi watu wa mataifa, ambao hapo kwanza hatukustahili?. Kama bado unasubiri nini?.. Pengine kweli umeupata Wokovu, lakini je! Unaujali kwa kuutunza?.. Au ni kama tu utambulisho katika Maisha yako, lakini hauna thamani nyingine yoyote ya ziada katika Maisha yako?.

Kumbuka kama unavaa nusu uchi, au nguo ambazo si za kujisitiri, kama vile suruali(kwako wewe mwanamke) au vimini tambua kuwa unaudharau wokovu wa Bwana, kama unalewa, au unacheza kamari, au unazini, au unafanya uchawi, au unaiba baada ya kuisikia injili mara nyingi, au baada ya kubatizwa..tambua kuwa unaudharau wokovu wa Bwana.

Hatari ya kutouthamini Wokovu wa Bwana ni hii tunayoisoma katika Waebrania 2:1.

Waebrania 2:1 “Kwa hiyo imetupasa kuyaangalia zaidi hayo yaliyosikiwa tusije tukayakosa.

2 Kwa maana, ikiwa lile neno lililonenwa na malaika lilikuwa imara, na kila kosa na uasi ulipata ujira wa haki,

3 SISI JE! TUTAPATAJE KUPONA, TUSIPOJALI WOKOVU MKUU NAMNA HII? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia”

Utapataje kupona, wewe ambaye huujali Msalaba?..siku ile utakuwa mgeni wan ani?..ni heri ukatengeneza mambo yako leo ili uwe na uhakika wa maisha yako ya umilele.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Ni wayahudi wa aina gani wanaotajwa kuwa sinagogi la shetani? (Ufunuo 2:9, Ufunuo 3:9)

Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?

USIMPE NGUVU SHETANI.

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

Mataifa ni nini katika Biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

NI NINI KINATOKA KINYWANI MWA MTOTO WAKO?

Nakusalimu tena katika jina la Bwana Yesu mwokozi  wetu, karibu katika kutafakari Maneno ya uzima..huu ni mwendelezo wa Makala  zinazohusu malezo ya Watoto kwa mzazi.

 Ikiwa wewe ni mzazi au mlezi na unao Watoto wadogo chini yako wa kuwalea, au unatarajia kuwa na Watoto.. Basi Makala hii ni muhimu sana kwako,

Zipo Makala nyingine tulishazitazama huko nyuma ikiwa hukuzipitia, basi waweza waweza wasiliana nasi inbox kwa namba hizi +255693036618 tuweze kukutumia.

Leo tutaona umuhimu wa kuwafundisha, Watoto nyimbo za kumsifu Mungu au kumwimbia..Awali ya yote ni lazima ufahamu kuwa, kila mtoto amewekewa ibada ya sifa ndani yake, haijalishi utalipenda hilo au hautalipenda..Na ibada hiyo huwa inakamilika pale anapokutana na Watoto wenzake kwenye michezo sehemu za wazi..Hapo ndipo utajua hicho kitu kipo ndani yake.

Kaa chunguza kwa makini, mahali palipo na Watoto wengi wamekusanyika, utasikia wakiimba vi-nyimbo Fulani mbalimbali, kulingana na kile ambacho walifundishwa, au wanachokisikia watu wengine wakiimba..

Na ndio maana Bwana Yesu alitumia mfano wa Watoto wanaocheza, masokoni, kwa kuimba, kukifananisha kizazi hiki jinsi mienendo yao ilivyokuwa na mwitikio mdogo wa injili..

Luka 7:31 “Bwana akasema, Niwafananishe na nini watu wa kizazi hiki? Nao wamefanana na nini?

32 Wamefanana na watoto walioketi sokoni na kuitana, wakisema, Tuliwapigia filimbi wala hamkucheza; tuliomboleza, wala hamkulia”.

Sasa wewe ukiwaona wanaimba unaweza kuchukulia kirahisi rahisi sana ukasema wanacheza tu, wanajifurahisha..lakini rohoni wanaonekana wanasifu katika ukamilifu wote, na hivyo wanasababisha madhara makubwa sana, hata kwa upande wa pili.

Ili tuelewe vizuri embu tujifunze kisa kimoja, kilichotokea Yerusalemu kipindi kile Bwana Yesu, anaingia akiwa amepanda punda na mwanapunda..Biblia inasema, watu walimtandikia nguo zao chini, na wengine majani ya mitende, wakaanza kumsifu kwa nguvu, wakisema Hosana hosana, Mwana wa Daudi..

Lakini wakati huo huo kulikuwa na kundi la Watoto linaongozana nao pembeni likiwasikiliza.. linajifunza hizo nyimbo..ndipo tunaona mwishoni kabisa wale watu walipomaliza sifa zao, Bwana Yesu aliingia Hekaluni, Lakini kule hekaluni, Watoto, hawakukaa kimya, wakaanza kutoa walivyovisikia,..wakawa wanakiimba kile wachokisikia kule nje! Hosana hosana, mwana wa Daudi..

Tendo lile likawa bughza kwa maadui wa Kristo, walipokuwa wanawasikia Watoto wakipiga kelele kama nyuki hekaluni, wakiimba walichokuwa wanakisikia, ndipo wakamfuata Kristo, kumuonya.. Lakini tunaona, Bwana hakuwaambia sawa nitawanyamazisha kinyume chake akawapa siri nyingine ambayo walikuwa hawaijui..akawaambia maneno haya.. “HAMKUPATA KUSOMA, KWA VINYWA VYA WATOTO WACHANGA NA WANYONYAO UMEKAMILISHA SIFA”

Mathayo 21:9-10,15-16

 “9 Na makutano waliotangulia, na wale waliofuata, wakapaza sauti, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi; ndiye mbarikiwa, yeye ajaye kwa jina la Bwana; Hosana juu mbinguni.

10 Hata alipoingia Yerusalemu, mji wote ukataharuki, watu wakisema, Ni nani huyu?

11 Makutano wakasema, Huyu ni yule nabii, Yesu, wa Nazareti ya Galilaya…..

15 Lakini wakuu wa makuhani na waandishi walipoyaona maajabu aliyoyafanya, na watoto waliopaza sauti zao hekaluni, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi! Walikasirika,

16 wakamwambia, Wasikia hawa wasemavyo? Yesu akawaambia, Naam; hamkupata kusoma, Kwa vinywa vya watoto wachanga na wanyonyao umekamilisha sifa?”

Umeona? Kumbe sifa za kweli zimekamilika katika vinywa vya Watoto wachanga, sio ajabu kuona mapepo yale yakilipuka ndani ya wale waandishi na wakuu wa makuhani, na kutaka kumshambulia Yesu kwasababu yao..

Mapepo yaliyokuwa yameigeuza nyumba ya Mungu kuwa pango la wanyang’anyi, sasa yanakutana na waaabuduo halisi wanaomwabudu Mungu katika Roho na kweli wamefika..(watoto)..Ni lazima yataabikie tu..

Lakini Habari hii inatufundisha nini sisi wazazi na walezi?

Kama sifa za kweli zimekamilika katika vinywa vya Watoto wachanga, basi tunapaswa tutumie nguvu nyingi sana kuwafundisha Watoto kumwimbia na kumsifu Mungu,  Ni muhimu sana, kwasababu hizo tu zinatosha kumtikisa shetani na ufalme wake..

Lakini kinyume chake ni kweli, kama mtoto hatoimba nyimbo za Mungu, badala yake amekaririshwa, bongofleva, na manyimbo ya kidunia, tufahamu kuwa sifa hizo pia zinakuwa zimekamilika kwa shetani. Hivyo, shetani anatukuzwa, na ufalme wa Mungu unadidimia.

Inasikitisha leo hii, kuona makundi ya Watoto wengi barabarani wanaimba nyimbo za wasanii wa kidunia, ambazo hata wewe mtu mzima kusikiliza unaziba masikio, mpaka unajiuliza hivi wazazi au walezi wao wapo wapi?

Wazazi wapo buzy na kazi, wapo buzy na biashara, wanachozingatia kwao tu ni elimu za duniani basi..Hayo mengine hawahangahiki nayo, hawajui kuwa mapepo yanapata nafasi katika mahekalu yao( yaani Nyumba zao), kwasababu ya sifa za Watoto wao za kipepo, zinamtukuza Ibilisi mwenyewe..

Ndugu, ukitaka furaha katika nyumba yako, embu wafundishe Watoto wako kuimba mapambio, vichwa vyao vijae sifa na nyimbo, waimbe hizo wakati wote, wachezecheze wakiimba hizo sio bongofleva.. kataa mtoto wako kujifunza, hizo nyimbo, wala usimvumilie unapomwona anaziimba bali mkemee.. sio kila mahali umpeleke mtoto au uende naye, huko atajifunza manyimbo ya ibilisi..

Wakati huu ambao bado ni wachanga, vichwa vyao huwa vinakamata sana upesi, hivyo tumia fursa hiyo, kuwapeleka Watoto, Sunday school, na kwenye mafundisho yao, ili wafunze huko kuimba na kumtukuza Mungu..Amani ije nyumbani kwako.

Bwana atusaidie sana, kuliona hilo.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU WATOTO.

MALEZI YA MTOTO MCHANGA.

KAMA “MAMA” UMEBEBA HATIMA YA MTOTO WAKO WA KIUME.

Je! Siku ya unyakuo watoto wachanga watanyakuliwa?

Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote.

UMEITIMIZA HAKI YOTE?

MWANAMKE ULIYEKOMAA KI-UMRI, ITAMBUE HUDUMA YAKO.

Rudi nyumbani

Print this post

KALAMU YENYE UONGO YA WAANDISHI IMEIFANYA KUWA UONGO.

Wingu la Mashahidi
Wingu la Mashahidi
KALAMU YENYE UONGO YA WAANDISHI IMEIFANYA KUWA UONGO.
/

SWALI: Mstari huu una maana gani? Je, ni kweli waandishi waliweza kubadilisha baadhi ya maneno ya torati, Na hivyo inaifanya biblia isiamike hadi sasa?

Yeremia 8:8 “Mwasemaje, Sisi tuna akili, na torati ya Bwana tunayo pamoja nasi? Lakini, tazama, kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo.

JIBU: Hii ni hoja inayotumiwa sana na wapinga-biblia, au wapinga-ukristo. Wakisimamia mstari huu, na kusema, unaona? Biblia ilichakachuliwa, zamani na waandishi wa kiyahudi kwa kuongeza baadhi ya maneno katika torati  iliyoandikwa na mwenyezi Mungu,.. Kwahiyo hiyo inathibitisha kuwa  biblia ni kitabu chenye kasoro..

Lakini je tukisoma vifungu hivyo, vinatuambia waliibadilisha torati?

Kabla ya kuendelea kusoma zaidi, embu tuitafakari tena hiyo kauli hapo mwishoni, anasema  “kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo”. Ahaa Kumbe waandishi ndio wameifanya kuwa uongo..Lakini yenyewe kama yenyewe sio uongo.. Mfano nikikuambia, unanifanya kuwa mwongo mbele za ndugu zangu, haimaanishi kuwa mimi ni mwongo..maana yake ni kuwa, pengine ni kwasababu uliyawakilisha  maneno yangu isivyopaswa, aidha kwa kuongeza chumvi au kupunguza, na kwasababu hiyo basi, mimi nikaonekana nimeongopa, lakini sivyo, mimi nilisema ukweli mwanzo, isipokuwa wewe ndio umeniwakilisha vibaya.

Ndivyo ilivyokuwa hapo, waandishi, ambao kazi yao kubwa ilikuwa ni kufundisha na kuwaelezea watu, walianza, kutoa tafsiri zisizo sawa za torati, na kuwafundisha watu na kuwaandikia, mfano Bwana Yesu alisema, waliipindua amri ya tano;  inayosema waheshimu baba yako na mama yako, na kuwaambia watu, ikiwa kuna chochote umekiweka wakfu hupaswi kumsaidia mzazi wako, hata kama akiangamia kwa njaa ni sawa tu..Jambo ambalo Mungu hakuliagiza hata kidogo, ilikuwa ni wajibu wa kila mtu kumsaidia mzazi wake, awapo katika uhitaji (Soma Marko 7:7-13)

Umeona, sasa tukirudi kwenye ile habari ya mwanzo ili kuthibitisha hilo vizuri, ukiendelea kusoma vifungu vinavyofuata utaona Yeremia, anaeleza kwa undani jinsi kalamu za hao waandishi zilivyoweza kuipa torati tafsiri zisizo sahihi..

Yeremia 8:8 “Mwasemaje, Sisi tuna akili, na torati ya Bwana tunayo pamoja nasi? Lakini, tazama, kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo.

9 Wenye hekima wametahayari, wamefadhaika na kushikwa; tazama, wamelikataa neno la Bwana, wana akili gani ndani yao?

10 Basi, kwa hiyo nitawapa watu wengine wake zao na mashamba yao nitawapa wale watakaowamiliki; MAANA KILA MMOJA WAO, TANGU ALIYE MDOGO HATA ALIYE MKUBWA, NI MTAMANIFU; TANGU NABII HATA KUHANI, KILA MMOJA HUTENDA MAMBO YA UDANGANYIFU.

11 KWA MAANA WAMEIPONYA JERAHA YA BINTI YA WATU WANGU KWA JUU-JUU TU, WAKISEMA, AMANI, AMANI, WALA HAPANA AMANI.

12 Je! Walitahayarika, walipokuwa wametenda machukizo? La! Hawakutahayarika, wala hawakuweza kuona haya usoni; basi wataanguka miongoni mwao waangukao; wakati wa kujiliwa kwao wataangushwa chini, asema Bwana..

Umeona hapo? Anasema, hao waandishi na makuhani, wanawatabiria watu amani, amani, na kuwaambia mnaishi sawasawa na torati ya Mungu inavyosema, hivyo hamwezi kupatwa na madhara, ili hali ndani yao wanatamani, ni waovu, waabudu masanamu, wanakula rushwa n.k.. 

Wakati torati inakataza vikali vitu hivyo, wenyewe wanawatumainisha watu, Mungu anawapenda, ndio hapo anasema,  wanawaponya jeraha zao kwa juu juu tu, mwisho wa siku  wanaadhibiwa, halafu wanasema Mungu ni mwongo.. Mbona anatupiga bila sababu!.

Je! Waandishi wa namna hii wapo hadi sasa?

Jambo hili lipo hadi sasa katika kanisa la Mungu, Siku hizi za mwisho makristo na manabii wengi sana wa uongo wametokea, nao wanawaponya watu wa Mungu juu juu tu, hawawaelezi ukweli, mpaka inafikia hatua Mungu anaonekana mwongo, hasikii wala hajibu.

Wanawaambia,  utafanikiwa, utabarikiwa, kesho yako ni ya kung’ara kama jua, wanawaambia watoe sadaka nyingi, watumie maji ya upako, mafuta na chumvi, wakati mwingine wafunge mwaka mzima, Mungu atawabariki.. Lakini wanasahau kuwa hao watu wana mizigo ya dhambi, ndiyo inayowafanya wasijibiwe maombi yao.. Kama vile maandiko yanavyosema..

Isaya 59:1 “Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;

2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.

3 Kwa maana mikono yenu imetiwa unajisi kwa damu, na vidole vyenu vimetiwa unajisi kwa uovu; midomo yenu imenena uongo, ndimi zenu zimenong’ona ubaya”.

Hivyo hao watu wanataabika, januari mpaka disemba, lakini hawaona nuru yoyote, hawaona uzima wowote, ndio kwanza hali inakuwa mbaya, mwishoni wanakataa tamaa wanasema Mungu hajibu maombi, wanawageukia waganga wa kienyeji.

Ndugu, Neno la Mungu ni kweli kabisa, akisema atakuponya, atakuponya kweli, akisema atakubariki atakubariki kweli, lakini ni sharti ujue, anataka nini kwanza kwako ili hivyo vyote vikujie.. Anachotaka ni wewe uache dhambi, uache, rushwa, uache uzinzi, uache uongo, uache vimini, uache fashion za kidunia, anasa, uache ulevi, uwe mtakatifu. Ndipo hayo yote yatakapokujia..

Epuka injili zizisogusia dhambi katika maisha yako, ziepuke kama ukoma, hizo huwa zinakuja na maneno mazuri sana ya kushawishi na kufariji, lakini hazitakusaidia chochote, Mungu ni mtakatifu, kamwe hajibu maombi ya mwenye dhambi.

Je! Umeokoka?  Kweli kweli kwa kumaanisha kumfuata Kristo? Kama la! Basi huu ndio wakati wako sasa kuanza upya na Kristo. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi, waweza tupigia kwa namba uzionaza hapo chini.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAJIBU YA MASWALI YANAYOULIZWA NA WASIO WAKRISTO (Sehemu ya kwanza).

Je!Sisi kama wakristo Tunaruhusiwa kuchangia ujenzi wa Imani nyingine?

Yesu ni Mungu?, Na Kama ni Mungu kwanini alikufa?

Nini maana ya “Torati na manabii”?

Neno “Mashehe” tunaliona likitajwa katika biblia(Agano la kale); Hawa mashehe ni wakina nani?

Je! Karamu za ‘Idi’ ndio zipo hizo tunazozisoma katika Hosea (12:9)

KUONGOZWA SALA YA TOBA

Rudi nyumbani

Print this post

UNAWAZA NINI SASA, JUU YA UFALME WA MBINGUNI?

Wingu la Mashahidi
Wingu la Mashahidi
UNAWAZA NINI SASA, JUU YA UFALME WA MBINGUNI?
/

Unawaza nini juu ya kuipeleka injili mbele?..Je unafikiri nini juu ya hali ya kiroho ya  wanao miaka kadhaa mbele?, endapo parapanda itakuwa haijalia miaka 20 ijayo, je hali ya kiroho ya wanao itakuwaje, ukilinganisha na kasi ya maadili kuporomoka?.. Je umewahi kufikiri kufanya chochote leo hii, ili miaka ya mbeleni watoto wako au Watoto wa wengine, wasikose chakula cha uzima?…

Kizazi tulichopo ni kizazi kinachoharibika kila siku, umewahi kufikiri hali itakuwaje miaka 10 mbeleni?..kama umewahi kufikiri kwamba hali utakuwa mbaya Zaidi kuliko sasa, basi pia jiulize leo hii unafanya nini ili wakati huo utakapofika, shetani asipate nafasi inayoiona mbeleni.

Kumbuka wewe usipotumia muda wako leo, au akili zako leo, au nguvu zako leo, kufikiri na kufanya jambo lolote juu ya ufalme wa Mbinguni, Bwana atafanya kupitia wengine, (kwasababu kazi yake ni lazima iende mbele) lakini wewe wewe utakuwa umejipunguzia thawabu zako mbele zake.

Hebu Leo tujifunze juu ya watu wawili katika biblia, ambao kupitia hao, tutapata hamasa na hekima katika kufikiri kuujenga ufalme wa mbinguni.

Mtu wa kwanza ni DANIELI, na wa pili ni YUSUFU. Watu hawa wawili wote walijaliwa uwezo wa kutafsiri ndoto, lakini kila mmoja kwa namna yake.

DANIELI:

Kuna wakati Mfalme Nebkadneza, (Mfalme wa Babeli) aliota Ndoto, lakini akawa ameisahau ile ndoto, na Danieli alipomwomba Bwana, aliweza kufunuliwa ndoto ile Pamoja na Tafsiri yake..na akaenda kumwambia mfalme, na ndoto ile na tafsiri yake vikathibitika..Na Mfalme akamtukuza sana Danieli, lakini si kama Yusufu.

YUSUFU:

Farao Mfalme wa Misri, naye aliota ndoto kama Nebukadneza…na ndoto ile alipoamka aliikumbuka…lakini cha ajabu ni kwamba hakuwaficha watafsiri wake ndoto ile, bali aliwahadithia alichokiota..yeye alichokuwa anahitaji tu ni maana ya ile ndoto..

Na alikuwa anajua kuwa watatokea waongo wengi, ambao watamwambia uongo..na kweli walitokea wengi wakampa tafsiri ya ndoto yake..lakini tafsiri zote hizo alizikataa..

Sasa ni Siri gani iliyofanya Tafsiri ya Yusufu ikubalike Zaidi ya zile nyingine zote??

Siri yenyewe ni mikakati baada ya kuielezea ile tafsiri..

Yusufu baada ya kusema kuna miaka 7 ya neema inakuja na 7 ya Njaa.. hakuishia hapo tu!.. lakini alitoa mikakati ni NINI CHA KUFANYA KATIKA HIYO MIAKA 7 YA NEEMA NA MIAKA 7 YA NJAA. Ndio utaona akamshauri Farao atafute mtu mwenye akili amweke juu ya kazi zake zote akusanye chakula cha kutosha katika miaka ya neema, ili itakapokuja miaka ya njaa basi hazina iwepo kubwa. (Hilo ndio wazo lililompandisha hadhi Yusufu, na wala si tu tafsiri)!..

Farao aliona hata kama tafsiri itakuwa ni ya UONGO, lakini wazo alilotoa YUSUFU NI LA HEKIMA NA AKILI…, hata kama Njaa haitakuja kama alivyotafsiri, lakini wazo tu la kuweka chakula akiba ni wazo kubwa sana na la akili sana, ambalo pengine katika utawala wake wote Farao hajawahi kushauriwa hivyo…

Tusome..

Mwanzo 41:28 “ Ndivyo nilivyomwambia Farao, ya kwamba Mungu amemwonyesha Farao atakayoyafanya hivi karibu.

29 Tazama, miaka saba ya shibe inakuja, katika nchi yote ya Misri.

30 Kisha kutakuja miaka saba ya njaa baada yake; na shibe ile yote itasahauliwa katika nchi ya Misri, na njaa itaiharibu nchi.

31 Wala shibe ile haitajulikana katika nchi kwa sababu ya njaa inayokuja baadaye, maana itakuwa nzito sana.

32 Na ndoto ya Farao kwa vile ilivyokuja mara mbili, ni kwa sababu neno hilo Mungu amelithibitisha, na Mungu atalitimiza upesi.

33 BASI, FARAO NA AJITAFUTIE MTU WA AKILI NA HEKIMA AMWEKE JUU YA NCHI YA MISRI.

34 FARAO NA AFANYE HIVI, TENA AKAWEKE WASIMAMIZI JUU YA NCHI, NA KUTWAA SEHEMU YA TANO KATIKA NCHI YA MISRI, KATIKA MIAKA HII SABA YA KUSHIBA.

35 NA WAKUSANYE CHAKULA CHOTE CHA MIAKA HII MYEMA IJAYO, WAKAWEKE AKIBA YA NAFAKA MKONONI MWA FARAO WAKAKILINDE KUWA CHAKULA KATIKA MIJI.

36 NA HICHO CHAKULA KITAKUWA AKIBA YA NCHI KWA AJILI YA MIAKA HIYO SABA YA NJAA, ITAKAYOKUWA KATIKA NCHI YA MISRI, NCHI ISIHARIBIKE KWA NJAA.

37 NENO HILO LIKAWA JEMA MACHONI PA FARAO, NA MACHONI PA WATUMWA WAKE WOTE.

38 Farao akawaambia watumwa wake, Tupate wapi mtu kama huyu, mwenye roho ya Mungu ndani yake?

39 Farao akamwambia Yusufu, Kwa kuwa Mungu amekufahamisha hayo yote, hapana mwenye akili na hekima kama wewe.

40 Basi wewe utakuwa juu ya nyumba yangu, na kwa neno lako watu wangu watatawaliwa. Katika kiti cha enzi tu nitakuwa mkuu kuliko wewe”.

Umeona?.. watafsiri wengine walikuwa wanakuja na tafsiri zao lakini mwisho wa siku wanamshauri Farao mambo yasiyo na hekima, wala yasiyojenga, wala yasiyo na manufaa..ndio maana hata tafsiri zao Mfalme alizikataa.. Lakini  Yusufu alipotoa tafsiri na mikakati bora baada ya ile tafsiri ndipo hata tafsiri yake ikathibitika.

Na utaona Yusufu alipokea kibali sana mbele ya Farao, Zaidi hata ya Danieli alivyotukuzwa na Nebukadreza.

Je na wewe unataka kibali leo mbele za Mungu? Kama Yusufu alivyopata mbele ya Farao??..kama ndio! basi anza kufikiri kuhusu Injili ya Kristo, katika siku za mbeleni, na anza kufanya kitu kuanzia sasa. Kama ni mhubiri basi weka hazina kwa vizazi vinavyokuja… Kama ni mtu wa kukirimu, basi changia injili kwa mali zako kwa kadiri uwezavyo, ili kusudi Watoto wanaochipukia wasikue na kukuta idadi ya disco na bar zimezidi makanisa, wasije wakakuta idada ya vikundi vya wahuni vimezidi vya watu wema, wasije  wakakutana na ugumu wa kuitafuta injili ya kweli, Zaidi ya huu tulionao sisi katika kizazi chetu..

 shetani anayo mikakati sasahivi ya kuharibu kizazi hata cha tano kijacho..na hata sasa kashaanza kufanya juhudi hizo, inatupasaje sisi, tunaosema tumeokoka sasa? Kama wewe umeipata injili ya kweli, kiurahisi, basi rahisisha pia kwa wanaokuja, ambao kwa ambao hawajasikia..ndivyo Mungu atakavyokupa kibali.

Mithali 13:22 “Mtu mwema huwaachia wana wa wanawe urithi”

Tujifunze kwa Yusufu, ili na sisi tupate kibali mbele za Mungu.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

FAHAMU TAFSIRI ZA NDOTO MBALIMBALI.

ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.

UKIOKOKA, JIANDAE KUPITISHWA USIPOPATAZAMIA.

Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?

Kwanini  vizazi vya ukoo wa Yesu vinajipinga katika Mathayo na Luka.

Rudi nyumbani

Print this post

Vitabu vya Deuterokanoni ni vya kiMungu?

Swali: Deuterokanoni ni nini?  na je vitabu vya Deutorokanoni ni vitabu vya kiMungu? (ambavyo vimevuviwa na Roho Mtakatifu) na vyenye kufaa kwa mafundisho.?

Jibu: Deuterokanoni ni vitabu vingine saba (7) ambavyo vimeongezwa na kanisa Katoliki juu ya vitabu 66 vya Biblia takatifu, na hivyo kufanya jumla ya vitabu 73 katika biblia ya kikatoliki. Maana ya neno “Deuterokanoni” ni “Orodha ya pili” ambayo imekuja baada ya orodha ya kwanza yenye vitabu 66

Na ordha hiyo ya vitabu vya Deuterokanoni ni..

1. Tobiti

2. Yudith

3. Wamakabayo I

4. Wamakabayo II

5. Hekima

6. Yoshua bin Sira

7. Kitabu cha Baruk.

Vitabu vya Deuterokanoni, viliandikwa baada ya nabii wa Mwisho (Nabii Malaki) kupita!.. Na vitabu hivi hapo kabla havikuhesabiwa kuwa vitabu vitakatifu  na pia wakristo!!..na wala havikuwekwa katika orodha ya vitabu vitakatifu au vya mafundisho ya kiMungu.

Vilikuja kuongezwa katika orodha ya vitabu vitakatifu na Papa Damasus 1 katika karne ya 4.

Lakini swali ni je!.. Vitabu hivi ni vitabu vitakatifu? Na kama sio kwanini?

Jibu ni kwamba vitabu hivi si vitabu vitakatifu wala vilivyovuviwa na Roho Mtakatifu, kwasababu zifuatazo.

Vinakinzana na vitabu vingine vitakatifu.

Kamwe Mungu hajichanganyi, na wala Neno lake halijichanganyi..lakini vitabu hivi vina mafundisho ambayo yanakinzana na mafundisho ya kweli ya Roho mtakatifu yaliyopo ndani ya vitabu 66. (Vitabu 66 havipingani hata kimoja, bali vyote vinakubaliana katika jambo moja, kwasababu vimevuviwa na Roho huyo huyo mmoja), lakini vitabu vya Deuterokanoni vinapingana na vitabu hivi vingine 66.

Kwamfano kitabu cha 2 Wamakabayo 12:43-45 kinafundisha Maombi kwa Wafu, na mafundisho ya toharani, jambo ambalo halionekani katika vitabu vingine 66 vya biblia.

Hakuna mahali popote katika biblia, panaonyesha kuwa wafu waliombewa au wanaombewa.. Zaidi sana biblia inasema katika Waebrania 9:27 “ kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu”.

Kwahiyo kitabu hiki si cha kiMungu, kwasababu Mungu kamwe hawezi kujichanganya..huku aseme hivi, na kule aseme vingine..

Na pia vitabu hivi, kuna sura zinazofundisha “Ulevi”, “Uchawi” na “Mazungumzo ya uongo”. Kwahiyo kwa ufupi si vitabu vya kiMungu, bali ni vya adui, shetani..ambavyo lengo lake ni kuwapeleka watu mbali na Mungu.

Biblia yenye vitabu 66, ndio biblia pekee ambayo mwanzo wake hadi mwisho wake imevuviwa na Roho Mtakatifu, na Ndio Neno la Mungu pekee, lakini hiyo yenye vitabu vya Deuterokanoni na nyingine yoyote yenye vitabu Zaidi ya hivyo ni ya kishetani, na si ya kuisoma wala kusikiliza mahubiri yanayotumia vitabu hivyo.

1Timotheo 4:1 “Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani”

Bwana Yesu akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

Biblia ina vitabu vingapi?

KITABU CHA UZIMA

Je! tunapaswa kukiamini Kitabu cha Henoko?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Rudi nyumbani

Maran atha!

Print this post

ILI TUONEKANE SAFI MBELE ZA MUNGU TUFANYE NINI?

Atukuzwe Yesu Kristo Bwana wetu milele na milele. Sifa na utukufu ni vyake yeye sikuzote..

Biblia inatuambia, mambo yote yaliyoandikwa katika agano la kale, yalikuwa ni kivuli cha agano jipya la rohoni. Hivyo maagizo mengi ya mwilini, unayoyasoma kule, yalikuwa ni muhtasari wa agano jipya lili bora Zaidi.

Ni sawa na mwanafunzi anayeanza chekechea, ukitaka kumfundisha  Hesabu za KUJUMLISHA na KUTOA, huwezi moja kwa moja ukamwandikia  5-3=2. Ukadhani ataelewa, ni kweli kwa upande wako ni rahisi kwasababu tayari upeo wako ulishatanuka, lakini kwa mtoto, huna budi kutumia njia ya vitendo kwa mwanzoni..

Ndipo itabidi umwekee vijiti, au mawe, ahesabu kimoja mpaka cha tano, kisha aondoe hapo vitatu, ndipo vile viwili vinavyosalia, viwe jibu. Hivyo akilini mwake anajua hesabu ni vijiti na mawe, lakini kihalisia sio hivyo.. Atakapokomaa akili, ndipo atakuwa hana haja ya vijiti, au vidole, au mawe tena.

Vivyo hivyo katika biblia, agano la kale la mwilini lilikuwa ni hatua za awali za kulielewa agano lilibora la rohoni..(Waebrania 10:1, Wakolosai 2:16-17).

Sasa tukirudi katika kichwa cha somo letu. Tufanye nini ili tuonekane safi mbele za Mungu?.

Kumbuka, katika torati Mungu aliwaatenga Wanyama wote katika makundi mawili makuu.

  1. Kundi la kwanza ni Wanyama safi
  2. Kundi la pili ni Wanyama najisi

Sasa ili mnyama aitwe safi, ilikuwa ni sharti, akidhi vigezo maalumu Mungu alivyovioanisha.. Na vigezo vyenyewe zipo vitatu ambavyo ni hivi;

  1. Awe anacheua
  2. Awe na kwato
  3. Awe na kwato zilizogawanyika mara mbili

Ikiwa na maana kama hatokidhi vigezo vyote vitatu, basi huyo mnyama ni najisi, haijalishi atakuwa na kimoja au viwili kati ya hivyo. Hakuruhusiwa, kuliwa, na wengine kufugwa au  kuguswa mizoga yao.

Walawi 11:2 “Neneni na wana wa Israeli, mkiwaambia, Wanyama hawa ndio wanyama wenye uhai mtakaowala, katika hayawani wote walio juu ya nchi.

3 Kila mnyama mwenye kwato katika miguu yake, mwenye miguu ya kupasuka kati, mwenye kucheua, katika hayawani, hao ndio mtakaowala.

4 Pamoja na hayo, wanyama hawa hamtawala katika wale wenye kucheua, na katika wale walio na kwato; ngamia, kwa sababu yuacheua lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu.

5 Na wibari, kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu.

6 Na sungura, kwa sababu hucheua, lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu.

7 Na nguruwe, kwa sababu yeye anazo kwato, ni mwenye miguu iliyopasuka kati, lakini hacheui, yeye ni najisi kwenu.

8 Msiile nyama yao, wala msiiguse mizoga yao; hao ni najisi kwenu.

Sasa utajiuliza ni kwanini, Mungu aliwaona hawafai?

Sio kwamba aliwaona wana sumu kali, au wana madhara wakiliwa, kama wengi wanavyodhani hapana, kwasababu wengi wao wanaliwa hadi sasa, na hakuna madhara yoyote yanayowapata bali alikuwa anatufundisha jambo la rohoni, ili tutakapoingia katika agano jipya tuelewe vema, Mungu anapozungumzia unajisi anamaanisha nini.

Kwamfano, anaposema,

  1. Wasiocheua, ni najisi.

Kucheua ni nini? Ni ile hali ya mnyama kuwa na uwezo wa kukirejesha tena kile chakula alichokimeza na kukitafuta tena, kwa kawaida Wanyama kama ng’ombe, twiga, ngamia, hawa wanakuwa na tumbo la ziada, ambalo linawasaidia kurejesha na kutafuna tena kile walichokila.

Hii inafunua nini sasa katika agano jipya?. Ukiwa si mtu wa kutafakari na kukitendea kazi kile unacholishwa (Neno la Mungu), wewe ni kusikia tu kilasiku, lakini hakuna tendo lolote la ziada unalolionyesha kwa kile ulichofundishwa, huzalishi chochote, mbele za Mungu ni kama mnyama najisi, asiyeweza kucheua, Na kamwe hutoweza kuingia mbinguni (patakatifu pa Mungu), siku ukifa. Mungu anataka tutendee kazi Neno lake, pia tujifunze kuzikumbuka Fadhili zake alizotutendea huko nyuma, tusiwe hasahaulifu. Usahaulifu ni tabia ya unajisi.

Hivyo jiangalie ndani yako je! Wewe ni mtu wa kulitendea kazi Neno la Mungu? Tangu uliopoanza kusikia ni mangapi umeyatendea kazi, Kama sio, basi bado hujawa safi.

2) Awe na Kwato:

Kucheua tu haitoshi, walikuwepo Wanyama wenye uwezo huo kama ngamia, lakini walikosa kwato.. yaani ni kama nyama tu imeshuka mpaka chini, ni sawa na kusema hawana kiatu.

Awe na Kwato:

Hivyo, ni dhaifu kwa upande mmoja, kwasababu wamekosa ulinzi miguuni, ukipita msumari mrefu, basi safari yao imekwisha, hawawezi kutembea kila mahali, penye miiba, hawawezi kuruka, kwasababu miguuni ni wadhaifu.

Tofauti na mnyama  farasi,au swala, yeye ana kwato ndio maana ni mwepesi kutembea popote, ngombe anakwato, ndio maana anaweza kulima hata kwenye mashamba n.k.

Hii inatupa tafsiri gani rohoni?

Waefeso 6:14 “Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,

15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani”;

Hapo anasema, ukiwa askari wa Kristo ni lazima ujifunze kusimama ukiwa umejifungia utayari miguuni.. utayari wa nini? Utayari wa kumtumikia Mungu kwa hali zote. Na je utayari huo unatokea wapi? Unatokea kwenye kuisikia injili ya Yesu Kristo, kwa kupitia hiyo tunapokea hamasa, na nguvu na uweza wa kumtumikia yeye.

Wanajeshi, kwa kawaida ni lazima wavae viatu vigumu miguuni waendapo vitani, ili kuwasaidia kukatisha katika mazingira yoyote magumu, vinginevyo wakienda peku peku, hawataweza kwenda mbali

Halikadhalika na wewe, ukiwa umejivika UTAYARI huo wa kumtumikia Bwana katika mazingira yoyote, rohoni unaonekana kama ni mnyama mwenye kwato. Unafaa kwa kazi,

3) Mwisho, kwato ziwe zimegawanyika.

Wapo Wanyama ambao walikuwa wanacheua, walikuwa wana kwato, lakini kwato zao zilikuwa hazijagawanyika mara mbili. Hapo bado walikuwa ni najisi.

kwato zilizogawanyika

Ni kwanini, Bwana alitaka kwato za mnyama zigawanyike mara mbili, ili waonekane safi?  Ni siri gani ipo nyuma yake?

Kama tulivyotangulia, kuona kwato, Ni utayari tuupatao katika injili…

Lakini lazima tujifunze kuligawanya Neno la Mungu. Ndio maana biblia inayo agano la kale na jipya. Ili tuweze kuwa askari kamili ya Kristo, hatuna budi kufahamu kuweka injili ya Kristo kama atakavyo yeye, kwa uongozo wa Roho Mtakatifu.

Kwa kukosa, kuelewa ufunuo uliokatika agano lake, ndio inayopelekea, watu kufundisha kuwa vyakula ni najisi kwasasa..

1 Timotheo 4 : 1-5

1 Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;

2 kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe;

3 wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli.

4 Kwa maana kila kiumbe cha Mungu ni kizuri, wala hakuna cha kukataliwa, kama kikipokewa kwa shukrani;

5 kwa kuwa kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba.

Wengine wanaona Ibrahimu, Daudi, wameoa wake wengi, anadhani ndio hata sasa ndivyo ilivyo, na Mungu anapendezwa navyo. Hawajui ni ufunuo gani ulikuwa nyuma yake.

Hivyo biblia inatutaka sana tujifunze kuligawanya vema Neno la Mungu. (2Timotheo 2:15).

Ni muhimu sana. Na hiyo inamuhitaji Roho Mtakatifu.

Hivyo kwa kukidhi vigezo hivi vitatu; 1) Kutendea kazi Neno la Mungu 2) Kumtumika kwa Bwana 3) Kuwa na maarifa ya Neno la Mungu. Basi utakuwa mnyama safi mbele za Mungu.

Na hivyo tutamkaribia Mungu.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Lumbwi ni nini katika biblia?

Wibari ni nani?(Mithali 30:26)

Bwana alimaanisha nini aliposema enendeni mkaihubiri injili kwa kila kiumbe?

Maji ya Farakano ni nini katika biblia?

NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

Rudi nyumbani

Print this post

Mti wa Mshita ni mti wa namna gani?

Wingu la Mashahidi
Wingu la Mashahidi
Mti wa Mshita ni mti wa namna gani?
/

Swali: Mti wa Mshita uliotengenezea sanduku la Agano ndio upi kwasasa?(Kutoka 25:10)

Jibu: Tusome

Kutoka 25:10 “Nao na wafanye sanduku la MTI WA MSHITA; urefu wake na uwe dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu, na kwenda juu kwake dhiraa moja na nusu.

11 Nawe ulifunike kwa dhahabu safi, ulifunike ndani na nje, nawe tia na ukingo wa dhahabu kulizunguka pande zote”.

Mshita ni jamii ya miti ambayo hata sasa ipo, na inapatikana katika sehemu nyingi za dunia, ikiwemo katika bara letu la Afrika, na hata katika Afrika mashariki.  (Tazama picha juu). Mti wa Mshita ni mti unaostahimili ukame zaidi ya miti mingi.

Tabia za mti wa mshita, ni kwamba ni moja ya miti migumu, na vile vile ni mti ambao hauharibiwi  na wadudu wala maji, wala hauingiaa fangasi kirahisi, jambo linaloifanya mbao ya mti huo iweze kutumika kutengenezea baadhi ya vyombo vya kuhifadhia vyakula, na sifa nyingine ya mbao ya mti wa Mshita ni rahisi kupakika rangi, kwasababu uso wake ni mwororo.

Sasa Kwanini Sanduku la Agano lilitengenezwa kwa mti wa Mshita?

Jibu, ni kwasababu ya tabia au sifa za mti huo.

Ndani ya Sanduku la Agano kulihifadhiwa chakula (yaani ile pishi ya mana) kwaajili ya ukumbusho wa vizazi vijavyo vya wana wa Israeli..Hivyo ni lazima chakula hicho kihifadhiwe ndani ya sanduku lililo imara lisiloingia fangasi wala wadudu waharibifu. Mbao nyingine zaidi ya Mshita, hazina sifa hizo!

Vile vile ndani ya Sanduku kulikuwa na zile mbao mbili, ambazo Musa aliambiwa azitengeneze, zilizoandikwa Amri kumi na chanda cha Mungu mwenywe, Mbao hizo ziliwekwa ndani ya Sanduku kuwa ukumbusho wa daima, hivyo ni lazima zihifadhiwe katika Sanduku lililo gumu ambalo haliharibiki haraka..

Na vile vile kulikuwa na ile fimbo ya Haruni iliyochipuka, ambayo ilihifadhiwa nayo pia kama ukumbusho wa utumishi wa kikuhani wa nyumba ya Lawi.. Fimbo hiyo nayo ilipaswa ihifadhiwe ndani ya sanduku imara lisiloruhusu unyevunyevu au maji kuingia.

Na sanduku la Agano linafananishwa na mioyo yetu..  Katika kitabu cha Yeremia 31:31, Biblia ilitabiri kuwa katika Agano jipya tulilopo sisi, sheria za Mungu zimeandikwa mioyoni mwetu.. Mioyo yetu kwa Bwana ni kama mti wa Mshita, Hivyo hatuna budi kuzidi kuiimarisha mioyo yetu, kwa kukaa mbali na dhambi ili tuzidi kuzidumisha sheria za Mungu katika mioyo yetu.

Maran atha!

Mada Nyinginezo:

Mwaloni ni nini? Na je unafunua nini rohoni?

Mwerezi ni nini?

FANYA BIDII ZOTE ULE MATUNDA YA UZIMA.

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

Je Adamu na Hawa, walikuwa hawafanyi mema kabla ya kula tunda?

Rudi Nyumbani:

Print this post

UTAPENDA KUCHANGIA HUDUMA HII?

Tutamshukuru Mungu kwa ajili yako, kwa mchango wako, ili kuifanya injili hii isonge mbele Tuma sadaka yako kwa namba hizi:
Airtel:+255789001312 -Devis Magembe
Mpesa: +255767992434-Denis Magembe


This will close in 315 seconds