Je! Karamu za ‘Idi’ ndio zipo hizo tunazozisoma katika Hosea (12:9)

Je! Karamu za ‘Idi’ ndio zipo hizo tunazozisoma katika Hosea (12:9)

Hosea 12:9 Lakini mimi ni Bwana, Mungu wako tangu ulipotoka katika nchi ya Misri; nitakukalisha tena katika hema, kama siku za KARAMU YA IDI.


JIBU: Tofauti na inavyodhaniwa hapo, na watu wa dini tofauti, kwamba Biblia inazitambua sherehe za kiislamu!. Jambo ambalo si kweli.

Ni vizuri kufahamu kuwa lugha yetu ya Kiswahili imetohoa maneno mengi sana kutoka katika lugha ya kiharabu, hata wakati ambapo biblia inatafsiriwa katika Kiswahili ilifuata mkondo huo huo. Kwamfano Sehemu nyingine utaona neno “shehe” likitajwa (1Samweli 5:8), na hapa unaona pia Neno “Idi” .

Kulingana na lugha ya  kiharabu neno IDI, linamaanisha “Sherehe”. Haijalishi ni sherehe ya aina gani, inaweza ikawa ni ya kidini au ya kitaifa, au ya kitamaduni, au ya kimuungano..

Hivyo imezoeleka na watu wengi wasioilewa lugha ya kiharabu kudhani kuwa Idi ni neno la sikukuu ya kiislamu, kumbe sio.

Katika biblia ya kiharabu, mahali popote, kulipotajwa sherehe ya kiyahudi, Neno Idi liliandikwa pale. Mfano, palipoandikwa sikukuu ya pasaka, iliandikwa “idi ya pasaka” n.k..

Hivyo, hatushangai na Neno hilo kuonekana katika baadhi ya vifungu kwenye biblia. Hiyo yote ni kwasababu lugha yetu ya Kiswahili, imeundwa kutoka katika lugha nyingi mbalimbali. Kwahiyo inayozungumziwa hapo sio sikukuu ya kiislamu, bali ni sikukuu ya vibanda, ambayo wana wa Israeli walikuwa wakiisheherekea kwa katika vibanda pindi walipokuwa jangwani.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?

UFUNUO: Mlango wa 19

ESTA: Mlango wa 5, 6 & 7

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Je kunena kwa Lugha mpya kukoje?.Na hizi lugha ni zipi, na je! ni lazima kila mkristo aliyepokea Roho Mtakatifu anene kwa lugha mpya?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments