Ni kweli hakuna mtu aliyewahi kuuona uso wa Mungu Zaidi ya Bwana Yesu?

Ni kweli hakuna mtu aliyewahi kuuona uso wa Mungu Zaidi ya Bwana Yesu?

SWALI: Musa alikuwa na mawasiliano ya ana kwa ana na Mungu, hata kuuona uso wake lakini katika Yohana 1:18, inaonekana Yohana anakanusha kuwa hakuna mtu aliyewahi kumwona Mungu isipokuwa Kristo pekee.


Jibu: Kumwona Mungu kunakozungumziwa hapo sio KUMTAZAMA USONI, kwamba anaonekanaje, mwonekano wake ukoje, uso wake unafananaje fananaje n.k. La! Sio kwa namna hiyo. Bali kumwona kunakozungumziwa hapo ni kwa ufahamu.

Kwamfano tunaposema TUMEUONA MKONO WA BWANA, haimaanishi tumeenda mbinguni tukauona mkono wake jinsi ulivyo, au umeshuka chini tukauona jinsi ulivyo, rangi yake na idadi ya vidole alivyo navyo! N.k. La! Bali tunamaanisha tumeona uweza wake mkuu!. Vile vile tunaposema tumemwona Bwana katika maisha yetu, haimaanishi ameshuka mbele yetu na tukamwona sura yake, bali tunamaanisha tumeona uwepo wake na kuutambua.

Kadhalika maandiko hapo yanaposema hakuna aliyemwona Mungu haimaanishi “aliyemwona Uso wake jinsi ulivyo” bali inamaanisha “hakuna aliyemjua Mungu na kumfahamu, kiuweza na kimamlaka kikamilifu” isipokuwa Kristo peke yake. Wengine wamemwona na kumwelewa lakini si kwa kiwango ambacho Mungu mwenyewe, alikuwa anataka watu wamwelewe.. Hivyo ni sawa na hawakumwona kabisa! Au kumwelewa. Ni Bwana Yesu pekee ndiye aliyemwelewa na kumfunua Baba, kikamilifu…

Luka 10:22 “Akasema, Nimekabidhiwa vyote na Baba yangu, wala hakuna amjuaye Mwana ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba ila Mwana, na ye yote ambaye Mwana apenda kumfunulia”.

Umeona? Kristo pekee ndiye aliyemjua Mungu, jinsi inavyopaswa kumjua.. Musa hakumjua Mungu, ndio maana torati ya Musa havikuweza kumkamilisha mwanadamu!.. Kristo ndiye aliyekuja kumfunua Mungu kwetu jinsi inavyopaswa, na kutuonyesha mapenzi yake kamili..

Yohana 1:17 “Kwa kuwa torati ilitolewa kwa mkono wa Musa; neema na kweli zilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo”.

Kwamfano Wanafunzi wa Yesu walikuwa wanamwona Bwana Yesu kila siku, lakini walikuwa hawamjui, macho ya mioyo yao yalikuwa yamefumbwa. Ndio maana alipowauliza Yeye ni nani, wakawa wanakosa jibu sahihi, mpaka Petro ambaye alifunuliwa na Baba, aliposema yeye ni Mwana wa Mungu, ili litimie hilo neno “WALA HAKUNA AMJUAYE MWANA ILA BABA”; WALA HAKUNA AMJUAYE BABA ILA MWANA, na ye yote ambaye Mwana apenda kumfunulia”.

Hivyo Bwana Yesu(Mwana wa Mungu).. ndio kila kitu katika haya maisha. Hakuna mtu mwingine yeyote, au nabii mwingine yeyote ambaye tunaweza kumfuata au kumtegemea maneno yake tukafika mbinguni. Injili ya Musa haikumhaidia mtu kufika kule Baba aliko, wala ya Nabii mwingine yeyote.. Ni Yesu pekee ndiye aliyetoa njia ya Watu kumfikia Baba Mbinguni!!..kwasababu yeye ndiye anayemjua.. Na njia hiyo ya kumfikia Baba ni YEYE MWENYEWE, yaani maisha yake na Neno lake.

Yohana 14:5 “Tomaso akamwambia, Bwana, sisi hatujui uendako; nasi twaijuaje njia?

6 Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi”

Je! Unataka kwenda mbinguni kwa Baba?

Kama ni ndio!, basi tambua NJIA NI YESU. Hakuna elimu nyingine yeyote, wala dini nyingine yeyote, wala maarifa mengine yeyote, ambayo yataweza kukufikisha mbinguni.. isipokuwa ni YESU TU!. Huyo ndiye aliyemwona Baba na Baba mwenyewe akamthibitisha.. hivyo hakuna njia ya mkato ya kufika mbinguni.

Hivyo kama hujampokea, mpokee leo na utubu na kubatizwa, ili aingia maishani mwako na kukuongoza katika njia ya uzima wa milele.

Maran atha!

[embedyt] https://www.youtube.com/embed?listType=playlist&list=PLIIhnDzXkeEcXSNPlq09Q5yonU3MOLI0h&v=kuCSAZcnM80&layout=gallery[/embedyt]

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Mlima Gerizimu na Ebali ni ipi, na umuhimu wao rohoni ni upi?

MJUE SANA YESU KRISTO.

Kama Mungu ndiye kaumba kila kitu, je ni yeye huyo huyo ndiye aliyeumba dhambi pia?

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments