Majukumu ya Mzazi ni kumlea mtoto katika njia inayompasa, kwasababu hekima ya Mungu inasema, hataiacha njia hiyo hata atakapokuwa mzee.
Mithali 22:6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”
Lakini pamoja na kumlea mtoto katika njia impasayo ya kiMungu, mzazi pia hapaswi kumchokoza mwanae sawasawa na maandiko yafuatayo…
Waefeso 6:4 “Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana”.
Wakolosai 3:21 “Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa”
Sasa utauliza nini maana ya kuchokoza?
Kuchokoza kama ilivyotumika hapo, ni “kitendo cha kumfanya mtoto awake hasira, pasipo kuwa na sababu ya msingi”
Na baadhi ya sababu hizo ambazo zinaweza kumfanya mtoto awake hasira, hata kufikia hatua ya kukata tamaa au kufanya dhambi kama za kutoa maneno mabaya mdomoni au moyoni..ni kama zifuatazo.
1.Ukali wa mzazi uliopitiliza.
Mzazi anapokuwa mtu wa kufoka mara kwa mara, na kushutumu kwa ukali mambo yasiyo na mashiko ni rahisi kumfanya mtoto akate tamaa au awake hasira, na kitendo hicho kibiblia kinatafsirika kama “Mzazi kamchokoza mwanae”.
2. Kumwadhibu mtoto mara kwa mara bila kuwa na sababu ya msingi.
Wapo wazazi ambao mtoto akifanya kosa dogo tu, tayari wamekamata kiboko na kutoa adhabu kali. Ni lazima mzazi apime kosa, kama linastahili adhabu au linastahili kuonya tu!.. Lakini sio kila kosa hukumu yake iwe viboko!. Hilo linaweza kumfanya mtoto achukizwe sana badala ya kujengeka, na kibiblia ikahesabika kama umemchokoza mwanao na si kumjenga.
3. Kumdhalilisha mtoto
Wapo wazazi wasiowatia moyo watoto wao, badala yake wanawadhalilisha mbele ya watoto wenzao, au mbele ya jamii.. Jambo kama hili pia kibiblia linatafsirika kama mzazi kamchokoza mwanae.
Tunapaswa siku zote kuwathaminisha watoto wetu mbele ya watoto wengine, vile vile kuwatia moyo katika mambo mazuri wanayoyafanya.
Na wazazi wengi hawajui kama wanawachokoza watoto wao, na kuwaharibu utu wao wa ndani kwa ukali wao.
Hivyo kama mzazi, zingatia mambo hayo (Usiwachokoze watoto wako) na Bwana atakubariki na vile vile kuwabariki watoto wako.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Mada Nyinginezo:
NINI MAANA YA SISI KUWA WATOTO WA MUNGU?
MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.
TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!
Je! Wana wenu huwatoa kwa nani? maana yake ni nini?
KILEMBA CHA NEEMA, JE! UMEMVIKA MWANAO?
Rudi nyumbani
Print this post
Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu, lihimidiwe.. karibu tujifunze biblia..
Neno la Mungu linasema..
Faida ya kumlea mtoto wako katika njia inayompasa ni kwamba atakapokuwa mzee hataiacha, na maana yake zaidi ni kwamba hawezi kufikia uzee kabla na yeye kuwa na watoto wake.. hivyo na wajukuu wako pia watanufaika kwa malezi yako wewe kwa mwanao, kwasababu kile mwanao alichokipokea kutoka kwako, na yeye atawafundisha watoto wake, hivyo kizazi chako chote hata cha tatu na cha nne au zaidi ya hapo kitakuwa kitakatifu na cha baraka.
Ukiona kuna shida kwa mjukuu, basi ujue kuwa shida ilianzia kwa bibi au babu, ikaingia kwa mtoto na kisha ikamalizikia kwa mjukuu.. Lakini kama babu au bibi alimlea mwanae katika njia inayompasa, ya kumcha Mungu na kumpenda Mungu, huyo mtoto naye pia ni lazima atawafundisha watoto wake njia hiyo hiyo, na hivyo wajukuu watakaozaliwa basi watakuwa wenye mwenendo mwema wa kumpendeza Mungu.
Tuangalie mfano mmoja wa kwenye biblia wa mtu aliyemlea vyema mtoto wake, na hata mjukuu aliyezaliwa akawa na mwenendo mzuri.
Mtu huyo si mwingine zaidi ya BIBI LOISI, ambaye alikuwa na binti yake aliyeitwa EUNIKE, ambaye ndiye aliyemzaa Askofu Timotheo, mtumwa wa Bwana..
2Timotheo 1:4 “Nami natamani sana kukuona, nikiyakumbuka machozi yako, ili nijae furaha; 5 nikiikumbuka imani uliyo nayo isiyo na unafiki, ambayo ilikaa kwanza katika bibi yako Loisi, na katika mama yako Eunike, nami nasadiki wewe nawe unayo”.
2Timotheo 1:4 “Nami natamani sana kukuona, nikiyakumbuka machozi yako, ili nijae furaha;
5 nikiikumbuka imani uliyo nayo isiyo na unafiki, ambayo ilikaa kwanza katika bibi yako Loisi, na katika mama yako Eunike, nami nasadiki wewe nawe unayo”.
Hapa tunaona Paulo anamwandikia waraka Timotheo, na kukiri chanzo cha imani yake Timotheo, kwamba ilianzia kwa bibi yake Loisi, na hatimaye kwa mama yake aliyeitwa Eunike, na ndipo ikaja kwake, ikimaanisha kuwa msingi wa Timotheo kumpenda Mungu haukuanzia kwake, bali ulianzia kwa bibi yake huko.. Ndio maana ikawa hata vyepesi Timotheo kuiamini injili ya Bwana Yesu na hata kuja kuwa Askofu wa makanisa mengi, na ndiye aliyekuwa pamoja na Paulo mpaka hatua ya mwisho.
Timotheo hakuwa Mwisraeli moja kwa moja, bali mama yake ndiye aliyekuwa mwisraeli, lakini baba yake alikuwa myunani… pamoja na mchanganyiko huo lakini malezi ya bibi yake na mama yake yalimfanya awe mwenye mwenendo bora kuliko vijana wengi.
Matendo 16:1 “Basi akafika Derbe na Listra, na hapo palikuwa na mwanafunzi mmoja jina lake Timotheo, mwana wa mwanamke Myahudi aliyeamini; lakini babaye alikuwa Myunani. 2 Mtu huyo alishuhudiwa vema na ndugu waliokaa Listra na Ikonio. 3 Paulo akamtaka huyo afuatane naye, akamtwaa akamtahiri kwa ajili ya Wayahudi waliokuwako pande zile; kwa maana wote walijua ya kuwa babaye ni Myunani”.
Matendo 16:1 “Basi akafika Derbe na Listra, na hapo palikuwa na mwanafunzi mmoja jina lake Timotheo, mwana wa mwanamke Myahudi aliyeamini; lakini babaye alikuwa Myunani.
2 Mtu huyo alishuhudiwa vema na ndugu waliokaa Listra na Ikonio.
3 Paulo akamtaka huyo afuatane naye, akamtwaa akamtahiri kwa ajili ya Wayahudi waliokuwako pande zile; kwa maana wote walijua ya kuwa babaye ni Myunani”.
Je na wewe kama mzazi un akitu gani cha kuwarithisha watoto wako na wajukuu wako?… je ni elimu tu ndio unayoona ni ya muhimu kwao???….
Nataka nikuambie kama watakuwa na elimu ya kidunia halafu hawana Mungu, basi jua kuwa umewapoteza wanao, haijalishi watakuwa mamilionea huko mbeleni!!.. Bibi Loisi, aliona utukufu wa mjukuu wake mbeleni, na kwamba atakuja kuwa mtumishi wa MUNGU hodari katika kuwavuta watu kwa Mungu, hivyo akaanza kuweka msingi bora kwa binti yake Eunike, na Eunike akamfundisha mwanae Timotheo malezi bora.
Walikuwepo vijana wengi wenye elimu nyakati za akina Timotheo, lakini wapo wapi leo??..walikuwepo vijana mamilionea kipindi cha akina Timotheo, lakini hakuna hata mmoja habari yake tunaisoma leo, lakini Timotheo habari zake tunazisoma na zinawaponya mamilioni ya watu duniani hata leo. Bwana amempa Timotheo kumbukumbu lisilofutika..
Walikuwepo wamama wengi na wabibi wengi nyakati za akina Timotheo, lakini hakuna hata mmoja tunayezisoma habari zake, ila hawa wawili Loisi pamoja na mwanae Eunike, habari zao tunazosoma hadi leo..
Na Mungu ni yeye Yule, hajabadilika..ikiwa na sisi tutatembea katika kanuni zake atatupa kumbukumbu ambalo halitafutika. Ikiwa na sisi tutawalea watoto wetu katika njia zitupasazo basi kumbukumbu letu pamoja na watoto wetu, na wajukuu wetu, na vitukuu vyetu, na vilembewe na vilembwekeze litadumu milele na milele.
Anza kuwafunza watoto wako biblia, wafundishe wamjue Yesu zaidi ya Hisabati, wafundishe wazijue amri za Mungu, na kuwa waombaji na watu wa ibada zaidi hata ya shule za ulimwengu. Ukimfanya Mungu wa kwanza katika maisha yao, na Mungu atawafanya wa kwanza katika mambo yao.
Bwana atubariki sote.
Maran atha.
“Si watu wa kutumia mvinyo sana”, je tunaruhusiwa kutumia mvingo kidogo?(1Timotheo 3:8).
KWANINI UNAPASWA UWE BIBI ARUSI NYAKATI HIZI ZA MAJERUHI?
MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)
Je! Mfalme Abiya na Mfalme Asa walikuwa ni ndugu?
Tunaishi katika ulimwengu ambao, maadili yameporomoka sana, na bado yanaendelea kuporomoka kwa vijana na watoto..Na hiyo inatufanya tuelekeze lawama kwa watoto; tukisema watoto wa siku hizi wamebadilika sana, lakini ukweli ni kwamba wazazi ndio wamebadilika, watoto ni walewale.
Malezo ya mzazi kwa mtoto ni muhimu sana, mtoto si kama nyau, ambaye kitu pekee anachohitaji ni chakula tu na sehemu ya kulala, hata ukimwacha mwaka mzima bila kumjali kwa vingine, hakuna hasara yoyote, bado ataendelea kuwa paka..
Lakini kwa mwanadamu sivyo..yeye hafugwi, bali analelewa..na malezi ni zaidi ya chakula na nguo na mahali pa kulala.. Hapo ndipo wazazi wengi wanashindwa kuelewa.
Kwasababu mtoto atahitaji kuwa na maarifa, nidhamu, uadilifu, hekima, busara, upendo, utiifu, upambanuzi n.k. Ili aweze kuishi vema katika huu ulimwengu.
Hivi vyote hazaliwi navyo, bali anajifunza anapokuwa duniani..hivyo akikosa msaada sahihi, basi ibilisi atatumia fursa hiyo kumfundisha elimu yake na nidhamu yake hapa ulimwenguni.
Hivyo wewe kama mzazi au mlezi una jukumu kubwa sana zaidi ya lile la kumlisha na kumvisha na kumsomesha..hizo ni hatua 3 katika ya 1000, anazopaswa azijue.
Ikiwa hukupata masomo yaliyotangulia ya malezi ya watoto, basi waweza kututumia ujumbe kwa namba hii, ili tuweze kukutumia chambuzi za nyuma. Au tembelea website yetu hii www.wingulamashahidi.org. au tutumie ujumbe kwa namba hizi +255693036618
Leo tutaona njia nyingine ya kumlea mtoto vema.
Na njia yenyewe si nyingine zaidi ya kutumia KIBOKO.
Lugha hii inaweza isiwe nzuri masikioni mwa wazazi lakini ni tiba nzuri kwa malezo yao. Hata ‘panadol’ haina ladha nzuri mdomoni, lakini pale inapotutibu tunaishukuru, ndio maana tunayo siku zote majumbani kwetu.
Lakini ni kwanini utumie kiboko kwa mtoto?
Sababu zipo mbili.
Mithali 22:15
[15]Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali.
Ni vizuri ukafahamu kuwa mtoto kama mtoto huwa ana ujinga mwingi ndani yake..yule si kama wewe, unapoona anang’ang’ania kitu fulani kisichopendeza halafu wewe kama mzazi unaamua tu kumwachia kisa anakililia, usidhani kuwa anaelewa matokeo ya kile anachokitaka..
Kumbuka yule hatafakari, wewe unatafakari, hivyo basi ukimsikia anatukana, usisubiri apumzike bali hapo hapo shika kiboko chapa. Ukiona unamwagiza kitu hatii, chapa..ukiona hawaheshimu watu wazima hata baada ya kuonywa mara nyingi..chapa..usiogope labda atakufa…biblia inasema kiboko cha adili hakiui..
Mithali 23:13
[13]Usimnyime mtoto wako mapigo; [14] Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.
Hiyo itamsaidia sana kuundoa ujinga mwingi wa kipepo ambao mwingine kwa maneno tu, peke yake au kwa kufundishwa hauwezi kutoka..
Na sababu ya pili kwanini tuwaadhibu watoto wetu kwa kiboko pale wanapokosea..ni kwasababu Mungu naye anatuadhibu sisi watoto wake.
Biblia inasema hivyo..
Waebrania 12:6-7
[6]Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi, Naye humpiga kila mwana amkubaliye.[7]Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye?
[6]Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi, Naye humpiga kila mwana amkubaliye.
[7]Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye?
Umeona..Sisi hatuna hekima ya kumzidi Mungu, tengeneza picha Bwana angekuwa anatuona tunatukana wengine halafu hachukui hatua yoyote anacheka tu..si tungaangamia..Mungu alipomuona Daudi anamchukua mke wa Huria halafu anaendelea kusema wewe ni mtumishi wangu unayeupendeza moyo wangu..Daudi leo angekuwa wapi kama sio kuzimu? Lakini Mungu alimuadhibu vikali…na baadaye akatubu akapona..
Nasi pia biblia inatuambia tutakuwa wakamilifu kama Baba yetu wa mbinguni alivyomkamilifu..(Mathayo 5:48)
Mzazi unayemtazama mwanao, anafanya ujinga, unaogopa kumchapa atalia..bado hujawa mkamilifu kama Mungu.
Hivyo anza sasa kutimiza huduma hii, ili kesho mtoto huyo afanyike baraka na neema kwa ulimwengu.
Lakini zingatia: Haimaanishi kuwa umpige pige mtoto ovyo kila saa anapokosea..hapana zipo sehemu zinastahili kiboko, zipo zinazostahili maonyo, zipo zinazostahili kuelimishwa..Zote zina umuhimu wake mkubwa bila kupuuzia hata moja.
Bwana akubariki
Shalom
NI NINI KINATOKA KINYWANI MWA MTOTO WAKO?
MALEZI YA MTOTO MCHANGA.
Jina la Bwana Yesu libarikiwe, karibu tujifunze tena maneno ya Uzima ya Bwana wetu, Yesu Kristo. Neno la Mungu ni taa inayoongoza miguu yetu, na Mwanga wa njia zetu! (Zab. 119:105).
Ipo hali Fulani ambayo, Watoto wa kiume wengi wanakuwa na mapenzi mengi kwa mama zao, na kinyume chake asilimia kubwa ya Watoto wa kike wanakuwa na mapenzi Zaidi kwa baba zao kuliko mama zao. Ingawa si wakati wote au kwa Watoto wote inakuwa hivi, lakini asilimia kubwa inatokea kuwa hivyo.
Na biblia pia utaona imetaja au kuonyesha kuwepo kwa aina hii ya mahusiano kati ya wazazi na Watoto wa jinsia tofauti.
Hebu tusome visa kadhaa vya baadhi ya wafalme wa kwenye biblia, kisha kisha tuendelee mbele.
Yeremia 52:1 “SEDEKIA alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja hapo alipoanza kumiliki; naye akamiliki miaka kumi na mmoja huko Yerusalemu; NA JINA LA MAMA YAKE ALIITWA HAMUTALI, BINTI YEREMIA WA LIBNA. 2 NAYE ALITENDA YALIYO MABAYA MACHONI PA BWANA, sawasawa na yote aliyoyatenda Yehoyakimu. 3 Maana, kwa sababu ya hasira ya Bwana, mambo haya yalitokea katika Yerusalemu na katika Yuda, hata akawaondosha wasiwe mbele za uso wake, naye Sedekia akamwasi mfalme wa Babeli.
Yeremia 52:1 “SEDEKIA alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja hapo alipoanza kumiliki; naye akamiliki miaka kumi na mmoja huko Yerusalemu; NA JINA LA MAMA YAKE ALIITWA HAMUTALI, BINTI YEREMIA WA LIBNA.
2 NAYE ALITENDA YALIYO MABAYA MACHONI PA BWANA, sawasawa na yote aliyoyatenda Yehoyakimu.
3 Maana, kwa sababu ya hasira ya Bwana, mambo haya yalitokea katika Yerusalemu na katika Yuda, hata akawaondosha wasiwe mbele za uso wake, naye Sedekia akamwasi mfalme wa Babeli.
Hapa tunaona Mama wa Sedekia anatajwa kama sababu ya Ubaya wa Mfalme Sedekia… Sasa sio huyo tu!
1Wafalme 14:21 “Rehoboamu akaanza kutawala alipokuwa mwenye miaka arobaini na mmoja, akatawala miaka kumi na saba huko Yerusalemu, mji aliouchagua Bwana miongoni mwa kabila zote za Israeli, ili aliweke jina lake huko. NA JINA LA MAMAYE ALIITWA NAAMA, MWAMONI. 22 BASI YUDA WAKAFANYA MAOVU MACHONI PA BWANA; WAKAMTIA WIVU, KWA MAKOSA YAO WALIYOYAKOSA, KULIKO YOTE WALIYOYAFANYA BABA ZAO.
1Wafalme 14:21 “Rehoboamu akaanza kutawala alipokuwa mwenye miaka arobaini na mmoja, akatawala miaka kumi na saba huko Yerusalemu, mji aliouchagua Bwana miongoni mwa kabila zote za Israeli, ili aliweke jina lake huko. NA JINA LA MAMAYE ALIITWA NAAMA, MWAMONI.
22 BASI YUDA WAKAFANYA MAOVU MACHONI PA BWANA; WAKAMTIA WIVU, KWA MAKOSA YAO WALIYOYAKOSA, KULIKO YOTE WALIYOYAFANYA BABA ZAO.
Ijapokuwa Rehoboamu alikuwa ni mwana wa Sulemani, na mjukuu wa Daudi, lakini mama yake anatajwa kumfanya awe mbaya…(sasa sio huyo peke yake..)
1Wafalme 15:1 “Mwaka wa kumi na nane wa mfalme Yeroboamu mwana wa Nebati, Abiya alianza kutawala juu ya Yuda. 2 Miaka mitatu akatawala huko Yerusalemu; NA JINA LA MAMAYE ALIITWA MAAKA, BINTI ABSALOMU. 3 AKAZIENDEA DHAMBI ZOTE ZA BABAYE, ALIZOZIFANYA KABLA YAKE; wala moyo wake haukuwa mkamilifu na Bwana, Mungu wake, kama moyo wa Daudi babaye”.
1Wafalme 15:1 “Mwaka wa kumi na nane wa mfalme Yeroboamu mwana wa Nebati, Abiya alianza kutawala juu ya Yuda.
2 Miaka mitatu akatawala huko Yerusalemu; NA JINA LA MAMAYE ALIITWA MAAKA, BINTI ABSALOMU.
3 AKAZIENDEA DHAMBI ZOTE ZA BABAYE, ALIZOZIFANYA KABLA YAKE; wala moyo wake haukuwa mkamilifu na Bwana, Mungu wake, kama moyo wa Daudi babaye”.
Si huyu peke yake…
1Wafalme 8:26 “Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala; akatawala mwaka mmoja huko Yerusalemu. NA JINA LA MAMAYE ALIITWA ATHALIA BINTI OMRI MFALME WA ISRAELI. 27 Akaiendea njia ya nyumba ya Ahabu, AKAFANYA YALIYO MABAYA MACHONI PA BWANA, kama walivyofanya nyumba ya Ahabu, kwa kuwa alikuwa mkwe wa jamaa ya Ahabu”.
1Wafalme 8:26 “Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala; akatawala mwaka mmoja huko Yerusalemu. NA JINA LA MAMAYE ALIITWA ATHALIA BINTI OMRI MFALME WA ISRAELI.
27 Akaiendea njia ya nyumba ya Ahabu, AKAFANYA YALIYO MABAYA MACHONI PA BWANA, kama walivyofanya nyumba ya Ahabu, kwa kuwa alikuwa mkwe wa jamaa ya Ahabu”.
Sio hawa tu…Unaweza kusoma pia habari za Mfalme Yothamu (2Wafalme 15:33), na Mfalme Manase (2Wafalme 21:1-2) na wengine wengi katika biblia, ambao utaona Uovu wao umesababishwa na mama zao.
Vile vile walikuwepo watu wa kawaida ambao hawakuwa wafalme, ambao pia tabia zao ziliathiriwa na mama zao, mfano wa hao ni yule kijana wa mwanamke wa kiisraeli, ambaye Habari zake tunazisoma katika Walawi 24:10-14, kijana huyu alimtukana Mungu, na akapigwa mawe mpaka kufa, na wengine wengi.
Lakini pia walikuwepo wafalme ambao walifanya mazuri, na Uzuri wao huo, Pamoja na sifa zao mbele za Bwana zilisababishwa na Mama zao..
1Wafalme 22:42 “Yehoshafati alikuwa mwenye miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka ishirini na mitano huko Yerusalemu. NA JINA LA MAMAYE ALIITWA AZUBA BINTI SHILHI. 43 AKAIENDEA NJIA YOTE YA ASA BABAYE; WALA HAKUGEUKA, AKIFANYA YALIYO MEMA MACHONI PA BWANA…..”.
1Wafalme 22:42 “Yehoshafati alikuwa mwenye miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka ishirini na mitano huko Yerusalemu. NA JINA LA MAMAYE ALIITWA AZUBA BINTI SHILHI.
43 AKAIENDEA NJIA YOTE YA ASA BABAYE; WALA HAKUGEUKA, AKIFANYA YALIYO MEMA MACHONI PA BWANA…..”.
1Wafalme 14:2 “Naye alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka ishirini na kenda katika Yerusalemu; NA JINA LA MAMAYE ALIITWA YEHOADANI WA YERUSALEMU. 3 AKAFANYA YALIYO MEMA MACHONI PA BWANA, ila si kama babaye Daudi; akafanya kama yote aliyoyafanya baba yake Yoashi”.
1Wafalme 14:2 “Naye alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka ishirini na kenda katika Yerusalemu; NA JINA LA MAMAYE ALIITWA YEHOADANI WA YERUSALEMU.
3 AKAFANYA YALIYO MEMA MACHONI PA BWANA, ila si kama babaye Daudi; akafanya kama yote aliyoyafanya baba yake Yoashi”.
1Wafalme 15:2 “Alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala; akatawala miaka hamsini na miwili huko Yerusalemu. NA JINA LA MAMAYE ALIITWA YEKOLIA WA YERUSALEMU. 3 AKAFANYA YALIYO MEMA MACHONI PA BWANA, kama yote aliyoyafanya babaye Amazia”.
1Wafalme 15:2 “Alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala; akatawala miaka hamsini na miwili huko Yerusalemu. NA JINA LA MAMAYE ALIITWA YEKOLIA WA YERUSALEMU.
3 AKAFANYA YALIYO MEMA MACHONI PA BWANA, kama yote aliyoyafanya babaye Amazia”.
Sasa katika maandiko hayo yote, unaweza kujiuliza ni kwanini ni waMama, wanahusishwa na si waBaba?.. Ni kwasababu kuna muunganiko wa kipekee kati ya Mama na mtoto wake wa kiume, ambapo Mama asipoutumia vizuri huo muunganiko, anaweza kujikuta anaharibu hatima ya mtoto wake wa kiume moja kwa moja. (Ni vizuri kulijua hili mapema, ili mambo yatakapoharibika huko mbeleni, usije ukasema ulikuwa hujui!!)
Mama unapokuwa mtu wa kidunia, unakuwa mtu wa kumkataa Mungu, fahamu kuwa na mtoto wako wa kiume ni rahisi sana, kuamini hiyo njia yako kuwa ni njia sahihi, kuliko hata mtoto wako wa kike.
Lakini mtoto wako wa kiume anapokuona wewe ni mtu unayemcha Mungu, ni mtu unayeutafuta sana uso wa Mungu, na kuukataa ubaya, ni rahisi sana, mwanao wa kiume, na yeye kuwa kama wewe, hiyo ni (Siku zote weka hilo akilini).
Wafalme wote waliofanya machukizo kwa Bwana, waliharibiwa na Mama zao. Vile vile wafalme wote waliofanya Mema mbele za Bwana, na hata kusifiwa ni kutokana na Mama zao. Hakuna mahali popote wababa wametajwa, katika kutenengeneza hatima za Watoto wao wa kiume.
Hivyo kama Mama, Jifunze kuwapeleka Watoto wako Kanisani, ukiwapeleka wewe Zaidi ya baba hawawezi kuiacha hiyo njia, hata kama watakuja kuyumba kidogo, lakini watairudia tu njia hiyo siku moja!..
Vile vile wafundishe kusoma Neno, na kushika vifungu vya biblia, na kuomba.. Ukifanya hayo kwa Watoto wako wewe kama Mama, ni rahisi mambo hayo kuwaingia Zaidi kuliko kama angefanya Baba.
Halikadhalika msifie mwanao katika mambo ya ki-Mungu na mema, zaidi ya mambo ya ulimwengu huu tu…sauti yako ina thamani kubwa zaidi kwake kuliko baba yake, angefanya hivyo.
Na vile vile wewe Mtoto wa kiume, jifunze kumsikiliza Mama yako, anayekufundisha njia za Mungu, na kukuelekeza njia sahihi.. Kwasababu usipomsikiliza huyo, hakuna mwingine utakayekuja kumsikiliza tena katika Maisha yako.
Ipo methali ya watu wa ulimwengu isemayo “ASIYEFUNZWA NA MAMAYE, HUFUNZWA NA ULIMWENGU”. Ni watu wa kidunia wameitunga methali hii kufuatia uhalisia waliouona, kuwa kwa Mama kunayo mafunzo makuu, Zaidi ya kwa baba.
Hivyo Wewe kama Mama mtengeneze mwanao katika njia ya haki Mithali 22:6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”., ..na wewe kama mtoto wa kiume, msikilize Mama yako.
Maran atha!
MWANAMKE, BINTI, MAMA. (Sehemu ya 2)
Je suruali ni vazi la kiume tu?
Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?
VIJANA NA MAHUSIANO.
WhatsApp
Haya Mafungu ya biblia ambayo wazazi/walezi wanapaswa wayajue kuhusu watoto wao.
Zaburi 8:2a “Vinywani mwa watoto wachanga na wanyonyao Umeiweka misingi ya nguvu;..”
Mungu anaonyesha kuwa kupitia watoto wachanga, ambao unaweza kuwadharau hawajui kitu, hapo ndipo Mungu ameweka nguvu zake. Hivyo anza kumlea mtoto katika misingi ya kumcha Mungu tangu akiwa mdogo, kwasababu hapo ndipo Mungu anapoketi.
Na ndio maana biblia inasema..
Mithali 22:6 Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.
Tabia ya kudharau watoto, au kuona kama umri wao wa kumjua Mungu bado, Yesu aliukemea sana, tunalithibitisha hilo katika..
Marko 10:13 “Basi wakamletea watoto wadogo ili awaguse; wanafunzi wake wakawakemea.14 Ila Yesu alipoona alichukizwa sana, akawaambia, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie; kwa maana watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao.15 Amin, nawaambieni, Ye yote asiyeukubali ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hatauingia kabisa.16 Akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabarikia”.
Marko 10:13 “Basi wakamletea watoto wadogo ili awaguse; wanafunzi wake wakawakemea.
14 Ila Yesu alipoona alichukizwa sana, akawaambia, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie; kwa maana watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao.
15 Amin, nawaambieni, Ye yote asiyeukubali ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hatauingia kabisa.
16 Akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabarikia”.
Biblia inasema pia..
Zaburi 127:3 “Tazama, wana ndio urithi wa Bwana, Uzao wa tumbo ni thawabu”.
Biblia bado inasisitiza wazazi, wasiwaudhi watoto wao, kwasababu zisizo na msingi, kisa tu wao ni watoto,
Waefeso 6:4 “Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana.
Kwasababu malaika wao mbinguni wanawatazama uwatendeapo mabaya..
Mathayo 18:10 “Angalieni msidharau mmojawapo wadogo hawa; kwa maana nawaambia ya kwamba malaika wao mbinguni siku zote huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni”.
Zaidi pia Bwana Yesu anataka wazazi/walezi wajifunze kupitia watoto walionao, hivyo kwa kupitia wao tutapata kujua siri kubwa za ufalme wa mbinguni.
Mathayo 18 : 1-5
“1 Saa ile wanafunzi wakamwendea Yesu wakisema,2 Ni nani basi aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni? Akaita mtoto mmoja, akamweka katikati yao,3 akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.4 Basi, ye yote ajinyenyekeshaye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni.5 Na ye yote atakayempokea mtoto mmoja mfano wa huyu kwa jina langu, anipokea mimi;”
“1 Saa ile wanafunzi wakamwendea Yesu wakisema,
2 Ni nani basi aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni? Akaita mtoto mmoja, akamweka katikati yao,
3 akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.
4 Basi, ye yote ajinyenyekeshaye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni.
5 Na ye yote atakayempokea mtoto mmoja mfano wa huyu kwa jina langu, anipokea mimi;”
Lakini bado Mungu anasisitiza juu ya kuwarekebisha watoto, kwamba ni jukumu la kila mzazi/mlezi kumwadhibu mtoto wake, pale anapokosea . Hilo ni agizo la Mungu. Usipomwajibisha mtoto wako, Mungu atakuwajibisha wewe siku ile, kwa kutomtengeneza mwanao.
Mithali 22:15 “Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali”.
Mithali 23: 13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu”.
Mithali 23: 13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.
14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu”.
2) WAJIBU WA MTOTO.
Vilevile mzazi, unapaswa umfundishe mwanao wajibu wake kama mtoto, Sawasawa na Neno la Mungu linavyosema,
Na mojawapo ni kuwafundisha kukutii wewe.
Waefeso 6:1 “Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki.2 Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi,3 Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia”.
Waefeso 6:1 “Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki.
2 Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi,
3 Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia”.
Mithali 1:8 “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,9 Kwa maana hayo yatakuwa kilemba cha neema kichwani pako, Na mikufu shingoni mwako”.
Mithali 1:8 “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,
9 Kwa maana hayo yatakuwa kilemba cha neema kichwani pako, Na mikufu shingoni mwako”.
Pia umfundishe kujua wajibu wake wa kumtafuta Mungu tangu akiwa mdogo..kwasababu kwa Mungu hakuna utoto.
Yeremia 1:6 “Ndipo niliposema, Aa, Bwana MUNGU! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto.7 Lakini Bwana akaniambia, Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru”.
Yeremia 1:6 “Ndipo niliposema, Aa, Bwana MUNGU! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto.
7 Lakini Bwana akaniambia, Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru”.
Na mwisho Mkumbushe pia hata watoto watahukumiwa, na kuzimu wapo watoto ambao hawakuwajibika katika kuwatii wazazi wao, na kumcha Mungu.
Ufunuo 20:12 “Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao”.
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali. Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
LENGO LA SHETANI KWA WATOTO WA KIZAZI HIKI.
KWANINI NI NUHU, AYUBU NA DANIELI?
Shalom, Jina la Bwana wetu, Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu.
Katika ulimwengu wa sasa, ukitaja mama wa kambo, au baba wa kambo, tayari picha ya kwanza inayotengenezeka kwenye vichwa vya wengi ni MATESO.
Lakini leo napenda tujifunze kitu kingine tofauti na hicho, ili tusije tukajikuta tunazuia baraka zetu pasipo sisi kujua.
Jambo la kwanza la kufahamu kabla hatujaingia kwenye kiini cha somo ni kwamba, popote pale unapojikuta upo, au umezaliwa, na kulelewa..jua Mungu kakuweka hapo kwa kusudi maalumu, ambalo ni la baraka.
Sasa turudi kwenye swali letu!. Je! Ni laana au mkosi, kuzaliwa au kulelewa na mama wa kambo au baba wa kambo?.
Tutalijibu swali hili, kwa kujifunza juu ya maisha mmoja katika biblia, na huyo si mwingine zaidi ya Bwana Yesu, Mkuu wa uzima..
Maandiko yanasema “tujifunze kwake”..Maana yake tumtazame yeye, tuyaangalie maisha yake, na tupate masomo (Mathayo 11:29).
Na leo tutapata somo lingine kutoka katika maisha yake.
Sasa wengi wetu hatujui kuwa Bwana wetu Yesu, alilelewa na Baba wa kambo katika mwili (Ni lugha ngumu kidogo hii, lakini ndivyo ilivyo).
Yusufu hakuwa Baba kamili wa Bwana Yesu. Mimba aliyoipata Mariamu haikumhusisha baba, ilikuwa ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu (soma Mathayo 1:18).
Baba wa Bwana Yesu, alikuwa ni Roho Mtakatifu.
Hivyo ni sahihi kabisa kusema, Yusufu alikuwa ni baba wa kambo wa Bwana Yesu.
Lakini ulishawahi kujiuliza ni kwanini Mungu aruhusu aishi na baba wa kambo?, kwani alishindwa kumfungulia Mariamu mlango, aishi mwenyewe tu na mtoto Yesu?.. Mungu angeweza kufanya hivyo, kwani yeye ni mweza wa kila kitu.
Angeweza kufungua mlango wa mali nyingi, kipindi Bwana Yesu anazaliwa na kumfanya Mariamu aishi maisha ya kifahari peke yake na mtoto Yesu, na pia angeweza kuzuia Yusufu asipose Mariamu kabisa..
Lakini hakufanya hivyo bali kinyume chake, baada tu ya Mariamu kuposwa ndipo mimba inaonekana..Na baada ya Yesu kuzaliwa, akaanza kubebwa na baba huyo huyo wa kambo, na hata wakati wa kazi ya ufundi, alifanya kazi ya baba huyo huyo wa kambo!.
Bwana aliruhusu maisha yake yawe hayo, ili kutufundisha na sisi kuwa si laana kuishi hayo maisha.
Sasa kulikuwa kuna nini kwa Yusufu, mpaka mkuu wa Uzima, Yesu Kristo apitie pale?
Yusufu alikuwa ni maskini kweli, hakuwa tajiri, lakini alikuwa amebeba ahadi ya kifalme, kumbuka Mungu alimwahidi Daudi, kwamba kupitia uzao wake atatokea Mfalme. Na Yusufu alikuwa ni wa Uzao wa Daudi.
Hivyo ili Bwana Yesu awe mfalme kupitia ahadi hiyo ya Daudi, ilikuwa hana budi azaliwe katika Hema ya Yusufu..angezaliwa pengine popote, ahadi hiyo ya Mungu isingetimia.
Mpaka hapo utakuwa umeanza kuona hata wewe ni kwasababu gani… umelelewa na huyo baba wa kambo Au mama wa kambo.
Haijalishi anakutesa kiasi gani, au ni maskini kiasi gani, lipo kusudi kwanini upo hapo, au umelelewa hapo, kuna baraka ambazo huwezi kuziona kwa macho!..
Kuzaliwa kwa Bwana kwenye lile zizi, chini ya Bwana Yusufu asiyekuwa na kitu, kulikuwa na maana kubwa.
Na wewe vile vile..tengeneza mambo yako vizuri sasahivi kwasaababu kuna baraka tele, mbele yako.
Ishi na Baba yako huyo vizuri, mheshimu, mbariki kwasababu ni Mungu ndiye aliyekuweka hapo, hujajiweka mwenyewe..na Mungu ndiye anayeijua mbele yetu..
Usianze kuharibu mambo kwa kunung’unika, unapopitia vikasoro vidogo vidogo, wewe tazama mbele, ongeza utii na heshima.
Kadhalika na kama wewe ni baba au ni mama na una watoto wa kambo, ishi nao vizuri, kwasababu nao pia wamebeba ahadi, ahadi hiyo isingeweza kukamilika pasipo wewe. Na mwisho utaona faida kubwa mbeleni.
Utasema vipi na mama wa kambo?
Musa alilelewa na Mama wa kambo, Binti Farao, hakujua atakuja kuwa nani..lakini maandiko yanasema, baadaye Mungu alikuja kumfanya Musa kuwa kama “mungu kwa Farao”.
Kutoka 7:1 “BWANA akamwambia Musa, Angalia, nimekufanya wewe kuwa kama Mungu kwa Farao; na huyo ndugu yako Haruni atakuwa nabii wako”.
Alienda kwa binti Farao, ili kupata jina hilo MUSA, Jina hilo alipewa na “mama wa Kambo”…hakupewa na mama yake mzazi, wala halikuwa jina la kiyahudi..
Na cha ajabu ni kwamba, Mungu hakumbadilisha jina Musa…aliendelea nalo hilo hilo, Sauli alibadilishwa na kuwa Paulo, Yakobo alibadilishwa na kuwa Israeli, lakini Musa amebakia kuwa Musa mpaka leo…kumbe wito wake ulikamilishwa pia na mama wa kambo.
Hivyo tunachoweza kujifunza ni kuwa macho ya kiroho kuona mbele na si hapa tu..katika nafasi uliyopo kama unaishi na baba au mama wa kambo, mheshimu kama Baba yako na kama mama yako, unapoona shetani ananyayuka na kujaribu kuharibu uhusiano wenu.. basi ni wakati wa wewe nyanyuka na kuongeza maombi…usiende kusikiliza simulizi za kishetani zinazosimuliwa huko na huko katika mitandao na katika vijiwe kuhusu ubaya wamama au wababa wa kambo, utajizolea elimu zitakazoharibu maisha yako..Biblia ndio kitabu chetu na mwongozo wetu.
Kama Bwana Yesu aliishi na Baba wa kambo, na kufanya naye kazi moja na bado akawa mfalme, ni kitu gani kitakachokuzuia wewe kufikia baraka zako, kupitia huyo mzazi au mlezi ambaye si wako?.
Kadhalika na kama wewe ni mzazi, au mlezi wa mtoto ambaye si wako, usimkatae mtoto wa kambo, kwasababu hujui ana ahadi gani kupitia wewe.. Na Mungu amekuchagua wewe, kwasababu na wewe pia unabaraka juu yake.
Hivyo kwa hitimisho ni kwamba hakuna laana yoyote kuishi au kulelewa na Baba au mama wa kambo. Vile vile hakuna laana yoyote au mkosi, kulea mtoto wa kambo.
Ikiwa bado hujamwamini Bwana Yesu, ni vyema ukakata shauri sasa kwasababu siku tunazoishi hizi ni siku za mwisho.
Na Bwana Yesu alisema.. “Itatufaidia nini tupate ulimwengu mzima halafu tupate hasara ya nafsi zetu”
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
MWANAMKE, BINTI, MAMA. (Sehemu ya 3)
YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.
SWALI: Je! Siku ya unyakuo watoto wachanga watanyakuliwa? Na vipi kuhusu walio bado tumboni, na wenyewe watanyakuliwa au wataachwa?
JIBU: Hili ni moja ya swali gumu kwasababu biblia haijaeleza moja kwa moja ni nini kitawatokea watoto siku ile ya Unyakuo, Hivyo tutajaribu kueleza kwa kadiri ya tunavyoona katika baadhi ya vifungu kwenye maandiko.
Ukitazama katika biblia, utaona, wapo watoto walipata neema kutokana na haki za wazazi wao, mfano wa hawa ni watoto wa Nuhu, na Lutu, vilevile wapo watoto walioadhibiwa kutokana na makosa ya wazazi wao. Utaliona hilo pia katika vile vizazi vyote vya Sodoma na Gomora, pamoja na gharika vyote viliteketezwa, hadi watoto walipata adhabu kwa dhambi za wengine. Lakini hiyo haimaanishi kuwa wataadhibiwa tena baada ya kifo.
Pia tukumbuke kuwa hata katikati ya kipindi cha dhiki kuu, bado watu wataendelea kutungishwa mimba na kuzaliwa, hivyo litakuwepo kundi la vichanga ambavyo vitazaliwa katikati ya dhiki kuu na vitakufa katika maangamizi yao..Hilo tunalithibitisha katika andiko hili;
Mathayo 24:19 “Ole wao wenye mimba na wanyonyeshao siku hizo!20 Ombeni, ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi, wala siku ya sabato.21 Kwa kuwa wakati huo kutakuwapo dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe.22 Na kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu ye yote; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo”.
Mathayo 24:19 “Ole wao wenye mimba na wanyonyeshao siku hizo!
20 Ombeni, ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi, wala siku ya sabato.
21 Kwa kuwa wakati huo kutakuwapo dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe.
22 Na kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu ye yote; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo”.
Unaona? Kwahiyo siku ile ikifika, kuna uwezekano wa watoto wengine kunyakuliwa (hata wale walio tumboni), na vilevile wengine kubaki, japo hatuwezi kusema hivyo ndivyo ilivyo, Yote tunamwachia Mungu. Ikiwa ni wote watanyakuliwa, au ni baadhi, Tunachopaswa kufahamu ni kuwa Mungu ni wa haki, atayaleta yote katika mizani, na yote yatakuwa sawa tu mwisho wa siku, na tutaona kabisa hukumu zake ni za haki. Kama vile Malaika mbinguni wanavyokiri hivyo..
Ufunuo 16:7 “Nikaisikia hiyo madhabahu ikisema, Naam, Bwana Mungu Mwenyezi, ni za kweli, na za haki, hukumu zako”.
Cha muhimu tunachopaswa kujua ni kuwa sisi ambao tayari tumeshafikia kimo cha kuyajua mema na mabaya, Kama hatutayatengeneza mambo yetu sasa, kwa kumpokea Bwana Yesu Kristo kwa kumaanisha kabisa, na kujitwika misalaba yetu na kumfuata, tujue kuwa unyakuo ukipita tutaachwa. Na matokeo yake, yatakuwa ni kuingia katika mateso makali ya dhiki kuu pamoja na Jehanamu ya moto.
Je! Umeokoka? Je! Umebatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako? Kumbuka Unyakuo ni wakati wowote, tubu umruidie muumba wako. Parapanda ni siku yoyote inalia, hakuna dalili iliyosalia..
Bwana Yesu akubariki.
Maran Atha.
JE! WATOTO WACHANGA WANAWEZA KUHUKUMIWA NA KUTUPWA MOTONI.
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote.
NI LIPI KATI YA MAKUNDI HAYA, WEWE UPO?
Kuna pepo moja lililowasumbua sana mitume wa Yesu, hilo halikuwa sawa na pepo mengine waliyokutana nayo, walihangaika nalo mchana kutwa lakini hawakufua dafu mpaka alipokuja Bwana Yesu mwenyewe kulikemea na kulitoa.
Lakini leo hatutazungumzia juu ya pepo hilo kwasababu habari yenyewe tunaijua, ila katika habari hiyo lipo jambo ambalo ni vizuri sisi tukajifunza, husasani kwa wazazi au walezi, wanaoishi na watoto wadogo. embu tusome tena alichokifanya Yesu kisha, tuende kwenye ujumbe wenyewe..
Marko 9:20 “Wakamleta kwake; hata alipomwona, mara yule pepo alimtia kifafa; naye akaanguka chini, akagaa-gaa, akitokwa na povu. 21 Akamwuliza babaye, AMEPATWA NA HAYA TANGU LINI? Akasema, TANGU UTOTO. 22 Na mara nyingi amemtupa katika moto, na katika maji, amwangamize; lakini ukiweza neno lo lote, utuhurumie, na kutusaidia”.
Marko 9:20 “Wakamleta kwake; hata alipomwona, mara yule pepo alimtia kifafa; naye akaanguka chini, akagaa-gaa, akitokwa na povu.
21 Akamwuliza babaye, AMEPATWA NA HAYA TANGU LINI? Akasema, TANGU UTOTO.
22 Na mara nyingi amemtupa katika moto, na katika maji, amwangamize; lakini ukiweza neno lo lote, utuhurumie, na kutusaidia”.
Sasa katika habari hiyo, usidhani Yesu alikuwa hajui matatizo ya huyo mtoto ndio maana akamwuliza vile, Kumbuka Yesu alikuwa anajua kila kitu wala alikuwa hana haja ya mtu kumuadhithia chochote, biblia inatuambia hivyo katika Yohana 16:30, Lakini aliuliza vile kwa lengo la kutaka watu wote wajue matatizo ya Yule mtoto yalianzia wapi, na ndio maana akamuuliza vile yule mzazi “Amepatwa na haya tangu lini?”.
Ndipo yule mzee akamjibu na kusema, “amepatwa na haya tangu utotoni”. Ulishawahi kuutafakari vizuri huu mstari, tangu utotoni? ..Hiyo ni kutuonyesha kuwa kuna mapepo ambayo, agenda yao kuu, ni watoto. Kwasababu yanajua yakianzia katika msingi, baadaye yatakuwa ni magumu kutoka.
Inashangaza leo hii kuona wazazi hawajali maisha ya kiroho ya watoto wao, wanaona kama wao ni watoto tu, shetani hawezi kuwashambulia, hawajui kuwa wanapaswa kulindwa kwasababu shetani huwa hatambui cha mtoto au cha mzee, lengo lake ni kuharibu. Kama alimuingia Nyoka ambaye ni mnyama tu, ataachaje kumwingine mtoto ambaye ni mwanadamu? ndio target yake kubwa?
Mzazi, anamruhusu mtoto wako mdogo atezame tv masaa 24 wakati wote hata zile programu ambazo haziendani na umri wake anamwacha azitazame, anamwacha asikilize miziki ya kidunia, tena Zaidi ya yote unafurahi anapocheza, lakini nyimbo za tenzi hata moja haujui, Mzazi mwingine hata hampeleki mtoto wake Sunday school ili afundishwe njia ya kikristo angali akiwa mdogo, yeye anachojua ni kumnunulia mtoto wake nguo nzuri tu, kumtafutia nursery nzuri ya kusoma, anajali vya mwilini vya mwanawe anapuuzia na vile vya rohoni. Hata kumwombea mtoto wake anashindwa.
Nachotaka nikuambie ni kuwa tusipowawekea msingi mzuri watoto wetu, shetani atatusaidia kuwawekea wake, kama alivyofanya kwa mtoto wa huyu mzee tunayesoma habari zake. Lile pepo lina haki ya kuwa gumu kutoka kwasababu tayari lilikuwa na msingi tangu utotoni. Na ukiangalia lengo la hilo pepo si lingine zaidi ya kumwangamiza tu, mara litake kumtupa kwenye maji, kwa bahati nzuri pengine watu wanamuona wanamuokoa, mara litake kumtupa kwenye moto, lakini Mungu anafungua rehema zake anaepukika.
Leo hii utaona kumenyanyuka kundi kubwa la watoto ambao wanaonyesha tabia ambazo hazieleweki chanzo chake ni nini, na wewe unaweza ukadhani ni yeye anafanya kumbe ni pepo ambalo tayari lilishamvaa tangu utotoni ndio linaonyesha tabia hizo ndani yake.
Wazazi ndio wanapaswa waanze kubadilika, ndio watoto wabadilike. Wewe kama mzazi, kama hutaonyesha kujali maisha ya kiroho ya mtoto wako, usidhani mtoto atabadilika mwenyewe au atakuwa na tabia njema huko mbeleni.
SASA UTAYAZUIAJE MAPEPO YA UHARIBIFU KAMA HAYO YASIMWINGIE MWANAO?
Kwanza ni kwa kutumia kiboko: Biblia inasema hivyo, …Pale unapoona kuna tabia Fulani ambayo sio nzuri, mfano kiburi, anatukana, hana nidhamu, hapo hapo hupaswi kuiacha hiyo tabia imee, mpaka hilo pepo liumbike ndani yake.. Utalitoa hilo kwa kiboko.
Mithali 23:13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa. 14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu”.
Mithali 23:13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.
Pili Ni kwa kumfundisha kanuni za imani: Unamfundisha biblia, unamfundisha nyimbo za kikristo, unamfundisha kusali, unamfundisha hata kukariri vifungu vya biblia, hata kama hataelewa sasahivi lakini vitabaki moyoni mwake kama hazina itakayokuja kumsaidia baadaye. Na hakikisha pia unampelekea kwenye mafundisho ya watoto kanisani.
Tatu Unamwombea; Mara kwa mara unahakikisha unamfunika mwanao, kwa damu ya Yesu Kristo, unatenga muda mrefu wa kumuombea.
Na Nne unamzuia kufanya/kutazama mambo ambayo hayapasi: Si lazima kila unachokitazama wewe, mtoto naye akitazame, magemu anayoyacheza mtoto si yote yanamaudhui mazuri, vilevile nguo unazomvisha mtoto si zote ni njema. Hivyo jifunze kumchagulia mtoto vinavyomfaa.
Ukizingatia hayo, basi mapepo kama hayo ambayo ni hatari na sugu, hayatamkuta mwanao. Kumbuka biblia inasema shetani ni kama simba angurumaye, akitafuta mtu ammeze, hivyo usipuuzie haya maagizo, mjenge mwanao, mjenge mdogo wako, mjenge mtoto yoyote auishiye naye.
Na Bwana atakubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
AGENDA KUBWA YA SHETANI KWA KANISA HILI LA LAODIKIA.
RUDI KUMPA MUNGU UTUKUFU.
Rudi Nyumbani:
Yafahamu malezi ya mtoto mchanga kibiblia.
Ukitaka mtoto wako mchanga awe na afya na ukuaji bora, na baadaye aishi Maisha aliyokusudiwa na Mungu ya mafanikio rohoni..Basi ni vema ukatafuta ushauri wa kiblia, ili ujue ni jinsi gani unapaswa umlee mwanao tangu akiwa katika hatua za awali za uchanga wake.
Embu tukiangazie kisa kimoja katika biblia, naomba usome chote, na mwisho wa Habari hiyo utajifunza jambo kubwa sana ambalo pengine hata hukuwahi kulitafakari hapo kabla..Ni tukio linalomuhusu Sulemani na wanawake wale wawili makahaba.
Tusome..
1Wafalme 3:16 Ndipo wanawake wawili, makahaba, walimwendea mfalme, wakasimama mbele yake. 17 Na mwanamke mmoja akasema, Ee bwana wangu, mimi na mwanamke huyu tunakaa katika nyumba moja; nami nalizaa nilipokuwa pamoja naye nyumbani. 18 Kisha, siku ya tatu baada ya kuzaa kwangu, ikawa mwanamke huyu naye akazaa; na sisi tulikuwa pamoja; hapakuwa na mtu mwingine pamoja nasi nyumbani, isipokuwa sisi wawili tu. 19 Na mtoto wa mwanamke huyu akafa usiku, maana alimlalia. 20 Akaondoka kati ya usiku, akamwondoa mtoto wangu ubavuni pangu, mimi mjakazi wako nilipokuwa usingizini, akamweka kifuani pake, na mtoto wake mwenyewe, aliyekuwa amekufa, akamweka kifuani pangu. 21 Nilipoondoka asubuhi nimnyonyeshe mtoto wangu, kumbe? Amekufa. Hata asubuhi nilipomtazama sana, kumbe! Siye mtoto wangu niliyemzaa. 22 Ndipo yule mwanamke wa pili akasema, Sivyo hivyo; bali mtoto wangu ndiye aliye hai, na mtoto wako ndiye aliyekufa. Na mwenzake akasema, Sivyo hivyo; bali mtoto wako ndiye aliyekufa, na mtoto wangu ndiye aliye hai. Ndivyo walivyosema mbele ya mfalme. 23 Ndipo mfalme akasema, Huyu anasema, Mtoto wangu yu hai, na mtoto wako amekufa. Na huyu anasema, Sivyo hivyo; bali mtoto aliyekufa ni wako, na mtoto aliye hai ni wangu. 24 Mfalme akasema, Nileteeni upanga. Wakaleta upanga mbele ya mfalme. 25 Mfalme akasema, Mkate mtoto aliye hai vipande viwili, kampe huyu nusu, na huyu nusu. 26 Ndipo mwanamke yule, ambaye mtoto aliye hai ni wake, akamwambia mfalme kwa maana moyoni mwake alimwonea mtoto wake huruma, akasema, Ee bwana wangu, mpe huyu mtoto aliye hai, wala usimwue kamwe. Lakini yule mwingine akasema, Asiwe wangu wala wako; na akatwe. 27 Ndipo mfalme akajibu, akasema, Mpe huyu wa kwanza mtoto aliye hai, maana yeye ndiye mama yake. 28 Na Israeli wote wakapata habari za hukumu ile aliyoihukumu mfalme wakamwogopa mfalme; maana waliona ya kuwa hekima ya Mungu ilikuwa ndani yake, ili afanye hukumu.
Tukianzana na hilo la kwanza: Utaona mwanamke yule mwerevu, alikuwa kila alipolala alikiweka kichanga chake Ubavuni. Ikiwa na maana alijitahidi kwa kadiri awezavyo kulala chali, ili mtoto apate nafasi ya kumwegemea yeye aidha ubavuni pake au kifuani pake, na sio yeye amwegemee mtoto,..Lakini yule mwingine hakulijali hilo, alimgeuza mtoto kuwa godoro, akamlalia..Na matokeo yake yakawa ni kifo.
Pili: Kama yule mwanamke angekuwa “hamchunguzi/hamdadisi” sana mtoto wake: Basi angeibiwa mwanawe bila habari. Lakini yeye tangu siku ya kwanza alikuwa anamkagua hadi kufikia siku ya tatu tayari alikuwa ameshamjua mwanawe ndani nje..,!, alijua umbile la mwanawe, na alama zake,..Hata pale alipojaribu tu kuchanganyiwa mtoto alilimtambua hilo mara moja.
Malalamiko mengi, ya wazazi, kuhusu Watoto wao kudhalilishwa kijinsia yanatokana na wazazi kutokuwa na tabia ya kuwachunguza Watoto wao, wanakuja kugundua hali imeshakuwa mbaya sana hairekebishiki. Anza kujijengea tabia hiyo ni kwa heri yako na kwa usalama wa kichanga chako.
Tatu: wanawake wale walikuwa ni wanyonyeshaji wa maziwa yao wenyewe ya asili kwa vichanga vyao na sio ya ng’ombe.
Sasa ili mtoto wako mchanga awe na ulinzi wa ki-Mungu maishani mwake..Mchukue ukamweke wakfu mbele za Mungu. Hakikisha pia huendi mikono mitupu, ambatanisha na sadaka yako ya shukurani kwa Mungu kwa kile alichokupa/alichowapa.
Ipo mifano mingi ya kimaandiko ya wanawake wenye akili walipeleka Watoto wao wapeleka mbele za Bwana wabarikiwe, na mpaka leo tunaona Watoto hao jinsi walivyokuwa nguzo muhimu katika Imani, Ukimsoma Samweli, yeye hakuwa vile hivi hivi tu, bali ni baada ya mama yake kumpeleka mbele za Bwana (Soma Samweli 1&2).
Ukimsoma Yohana Mbatizaji naye vivyo hivyo,. Ukimsoma pia Bwana wetu Yesu Kristo naye vivyo hivyo, wote walipelekwa mbele za Bwana. Vivyo hivyo mchukue mwanao, mpeleke nyumbani kwa Bwana awekwe wakfu kwa Bwana kwa kuwekewa mikono na wachungaji au wazee wa kanisa..Hiyo itakuwa ni salama ya Maisha ya baadaye ya mwanao.(Luka 2:22-24).
Huhitaji kusubiri mpaka awe mkubwa, siku za mwanzoni mwanzoni, au wiki za mwanzoni haraka bila kukawia mpeleke kwa Bwana..Kumbuka mtoto mchanga habatizwi kulingana na maandiko, Hivyo usifanye hivyo kwasababu haitasaidia chochote. Mpeleke akawekewe mikono tu awe wakfu kwa Bwana.
Na hili ndio jambo kuu kuliko yote ya kuzingatia. Unaweza ukaijali afya yake, lakini kama Mungu hamtambui ni kazi bure.Kwasababu shetani ndiye atakayemtambua.
Vilevile ni jukumu lako kumwombea mwanao kila wakati, Tenga muda maalimu wa kumwombea, walau lisaa 1 kila kipindi. Mwombee afya yake, mwombee ukuaji wake, mwombee kila pembe ambayo Mungu atakuongoza. Vilevile unapomwimbia Mungu imba Pamoja naye, Na hiyo ndio dalili nzuri upendo Mungu anaotaka mazazi aonyeshe kwa vichanga vyao.
Hivyo kwa kuhitimisha zingatia hayo mambo makuu 5.
Lakini kumbuka pia yote hayo ili yawe na maana ni lazima na wewe kama mzazi/wazazi, muwe mmemkabidhi Kristo Maisha yenu (yaani muwe mmeokoka). Hizi ni nyakati za mwisho na za hatari sana kama ulikuwa hujui, Pale Bwana Yesu aliposema..
Mathayo 24:19 “Ole wao wenye mimba na wanyonyeshao siku hizo! 20 Ombeni, ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi, wala siku ya sabato. 21 Kwa kuwa wakati huo kutakuwapo dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe”.
Jiulize ni kwanini alisema, ole kwa wanyonyeshao kama wewe?..Alisema hivyo kwasababu alijua mwisho ukiwakuta watu wa namna kama ya kwako, wakati huo utakuwa ni mgumu sana kwao..Embu jiweke katika mazingira kama hayo halafu usikie YESU karudi kulinyakua kanisa..Umebaki hapa duniani , halafu mpinga-Kristo anaanza kuchinja watu utakuwa katika hali gani na mwanao.
Angalia magonjwa yanayotokea duniani ya ajabu (covid-19), angalia, majanga, angalia matetemeko makubwa, mauaji ya ajabu na ya kinyama, angalia tetesi za vita vya ki-atomiki na kuibuka kwa manabii wa uongo..Hapo hatuwezi kusema tuna vizazi vingine mbele vya kuishi, pengine mimi na wewe tutashuhudia tukio zima la Unyakuo..Sasa utakuwa wapi ikiwa leo hii hujaokoka ndugu yangu..
Lakini ukitubu sasa, Kristo yupo tayari kukusamehe, unachopaswa kufanya ni kumaanisha tu, kutoka katika moyo wako, na kusema kuanzia leo mimi ninaacha dhambi ninamgeukia..Na wakati huu huu Kristo ataanza kufanya kazi ndani ya Maisha yako, Hivyo kama upo tayari kufanya hivyo leo.
Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE. ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE. AMEN.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.
Ubarikiwe sana
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
kilemba cha neema, Je! Umemvika mwanao ?
Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe..Karibu tujikumbushe mambo muhimu katika maisha yetu..Na hayo si mengine zaidi ya maonyo ya Neno la Mungu…Leo kwa Neema za Bwana tutajikumbusha majukumu machache ya wazazi juu ya watoto wetu..
Kutoka 20: 12 “Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako”.
Neno hili ni Neno la Mungu kwa watoto wote ambao wanao wazazi…Na hata kama hawana wazazi labda wamefariki au hawaishi nao kwa namna moja au nyingine…Basi nafasi hiyo ya Baba na Mama itachukuliwa na walezi wao…Hao wanasimama kama Baba zao na Mama zao kihalali kabisa mbele za Mungu..hata kama wapo katika vituo vya malezi vya mayatima…hao walezi wao wanachukua nafasi hiyo ya Baba na Mama…wana amri kutoka kwa Mungu kuheshimiwa kama wazazi halisi…Kwasababu kuna Baraka kubwa sana katika kuwaheshimu wazazi na kuwasikiliza..
Kadhalika haijalishi mzazi ni mwovu kiasi gani lakini ni lazima kumheshimu, na kumtii haijalishi yeye hajiheshimu kiasi gani ni wajibu wa kila mtoto kumheshimu mzazi wake..Kwasababu ndio amri ya kwanza yenye ahadi…
Waefeso 6:1 “Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki. 2 Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi, 3 Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia”
3 Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia”
Kupata heri na kuishi siku nyingi ni vitu viwili tofauti…Unaweza kuishi siku nyingi lakini maisha yasiwe ya heri..Hivyo, vyote viwili vinapaswa viende pamoja…
Sasa Kitu cha Muhimu cha kufahamu kwa mzazi ni kwamba…Hatima ya mtoto, mzazi anaweza kuchangia kwa asilimia kubwa kuitengeneza au kuiharibu…Mzazi anaweza kukazana kweli kumpenda mwanawe, kumlipia karo, kumtafutia shule bora..kumpatia lishe bora, kumlinda..kumhakikishia bima ya afya n.k Lakini kama hatamtengenezea mwanawe mazingira ya kumheshimu au kumtii.. huyo mtoto hawezi kupata heri yoyote huko anakokwenda, wala hawezi kuishi maisha marefu…haijalishi atapatiwa elimu nzuri kiasi gani sasa…au atakuwa na afya nzuri kiasi gani sasa au maarufu kiasi gani…Maisha yake yatakatika katikati na yatakuwa ya tabu.
Hayo ndio mambo ya kwanza ya kuzingatia kabla hata ya kwenda kuangalia ufaulu wake wa darasani…usifurahie anapofaulu sana na huku adabu yake inazidi kwenda chini..furahia pale heshima yake na utii wake unapozidi kupanda kwasababu unajua..hata kama atapepesuka kiafya sasa..hatakufa!..ataishi muda mrefu kwasababu Neno la Mungu linasema hivyo..hata kama hana heri sasa, lakini atakuja kuwa na heri baadaye katika kipindi cha maisha yake yote..
Hivyo kazana kumfundisha awe na tabia ya kukusikiliza…chochote utakachomwambia akutii na afanye kwa kupenda na si kwa kulazimishwa lazimishwa..mfunze tabia nzuri na heshima na utiii kwako na kwa watu wengine, mvishe mavazi ya adabu na mfundishe kuwa mtii….Mjaribu mara kwa mara kuangalia utii wake umefikia wapi ukiona umepungua tafuta namna ya kuurudisha…..mtume dukani mrudishe hata mara mbili au tatu, mpime..ujue kiwango cha utii alichonacho na heshima.
Mpime anapokuwa na wageni na watu wengine anakuwa na tabia gani zisizofaa na zile zinazofaa mpongeze…ukiona kasoro tumia fimbo kidogo, maana biblia inasema ukimpiga hatakufa…Wengi hawatumii fimbo wakidhani wanamharibia ujasiri mtoto, fimbo isiyokuwa na mafunzo sahihi ndiyo inayomharibia ujasiri..lakini fimbo yenye ujumbe wa kujenga ndiyo inayomjenga zaidi mtoto…
Na Mungu alivyowaumba watoto hawana kinyongo ili kwamba waweze kutengenezeka..ukimwadhibu sasahivi baada ya nusu saa mnacheka na kufurahi, ule upumbavu utakuwa umendoka lakini upendo wake kwako bado upo…..ukimwacha sasa bila kumfunza atakapokuwa mtu mzima hali za kuwa na vinyongo na uchungu zitakapomjia itakuwa ni ngumu kumtengeneza….kila utakalomwambia atakuwa anakwambia unamnyanyasa,..mara unaingilia uhuru wake..mara hujali hisia zake, mara wewe ni mkoloni, mara unamwaibisha n.k
Pia katika utoto aliopo, mfundishe biblia..mpe mistari kadhaa ya kuikariri na kuishika kwasababu watoto wengi bado hawajaweza kuipambanua mistari..wape tu waikariri itawasaidia ukubwani..kuliko kukariri nyimbo za kidunia..pia wafundishe nyimbo za kuabudu, na kumsifu Mungu na wafundishe sala za kuomba muda wote na habari za Yesu ambazo ndizo za muhimu kuliko zote..Na wapime je hivyo unavyowafundisha au wanavyofundishwa na wengine wanavizingatia.??
Ukimpima mtoto vizuri na kujua kuwa anakutii na kukuheshimu na anaheshima kubwa ambayo mpaka watu wa nje wanaishuhudia na kusema Yule mtoto anaheshima na adabu…Basi, kuna Baraka ambazo Mungu anaziachia ambazo ulimwengu hauwezi ukaziona..hapo ndipo nyota njema ya mtoto inapoanzia..
Mithali 22: 6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”…
Wengi wanaogopa kuwafundisha wanao adabu na heshima kwasababu wanahisi wakishafikisha umri Fulani labda wa kuvunja ungo au kubalehe watakengeuka..Huo ni uongo wa shetani!!…Watoto wengi wanakengeuka ukubwani kwasababu wazazi wao ambao hapo kwanza walikuwa wanawalea vizuri leo wamekengeuka!..sasa kama mzazi kakengeuka mtoto atasalimikaje?..Mzazi alikuwa anakwenda kanisani na mwombaji sasa hafanyi hivyo tena..mtoto ataendeleaje kwenda kanisani?…Mtoto alikuwa amezoea nyumbani ni mahali pa ibada sasa nyumbani kunapigwa kila siku kwenye TV, nyimbo za kidunia, mtoto ataendeleaje kuwa mtakatifu?….Lakini kama mzazi akibaki vile vile Yule mtoto kamwe hawezi kukengeuka hata atakapokuwa mzee..biblia sio kitabu cha Uongo!… Haiwezi kusema mtoto hataiacha ile njia halafu aje kuiacha!..sasa Mungu atakuwa ni mwongo.
Sasa faida nyingine ya mwisho na kuu ambayo mtoto anaweza kuipata kutoka kwako mzazi kwa kumfanya akutii na hata akusikilize na kukuheshimu katika viwango vya juu ni KUVIKWA KILEMBA CHA NEEMA KICHWANI PAKE?.
Mithali 1: 8 “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako, 9 Kwa maana hayo yatakuwa KILEMBA CHA NEEMA KICHWANI PAKO, Na mikufu shingoni mwako”.
Mithali 1: 8 “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,
9 Kwa maana hayo yatakuwa KILEMBA CHA NEEMA KICHWANI PAKO, Na mikufu shingoni mwako”.
Hii ni Baraka kubwa sana ambayo wazazi wengi hawaijui…Hapa duniani tunaishi kwa Neema,…Hivyo Neema ya Kristo inapokuwa nyingi juu yetu..ndipo tunapokuwa na nafasi zaidi ya kumkaribia Mungu, ndipo tunapokuwa na nafasi kubwa zaidi ya kuwa watumishi wa Mungu…Na utumishi wa Mungu sio tu ule wa kuhubiri madhabahuni hapana! bali hata ule wa Danieli ni utumishi wa Mungu..Pale Mungu anapokuweka katika ngazi Fulani ya juu na huko anakutumia kuwatunza watu wake..Hivyo Neema kama hiyo ni njema kwa mtu yeyote…Mtu anayemtumikia Mungu,.. Mungu atamheshimu biblia inasema hivyo (katika Yohana 12:26).
Sasa ni nani asiyetaka kuheshimiwa na Mungu?..Je! unataka mwanao aheshimiwe na Mungu?…Kwa kuvikwa neema ya kuwa mtumishi wake?…Ni kwa kumfanya akutii na kukuheshimu..huku na wewe ukionyesha kielelezo cha kumcha Mungu maisha yako yote ili usimwangushe..
Kuwa na mtoto ni Baraka!..Hususani kama umemvisha kilemba hicho cha neema….Neno la Mungu linasema wapeni watu vitu nanyi mtapewa kipimo cha kujaa na kushindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika ndivyo watu watakavyowapa kifuani mwenu…..Na wewe umempa mwanao hicho kipimo cha Neema ya Mungu juu ya kichwa chake kubwa namna hiyo…Bwana atamtumia huyo huyo kukulipa..kukurudishia kipimo cha kujaa na kushindiliwa nakusukwasukwa hata kumwagika katika siku za mbeleni..Na kwasababu mwanao au wanao watakuwa wanatembea na hiyo NEEMA kubwa sana kichwani mwao basi kila watakalomwomba Mungu, Mungu na kila watakalolifanya litafanikiwa katika maisha yao.
Kama wewe mzazi hujaokoka!..Tambua kuwa huwezi kuwavika wanao KILEMBA HICHO CHA NEEMA vichwani mwao..Wataharibikiwa na kuwa na maisha mabaya..kwasababu maisha yako wewe ni mabaya!..Hivyo ni vizuri leo hii ukamgeukia Kristo akuoshe dhambi zako kweli kweli kwa damu yake..Ili uwe mzazi/mlezi bora…Unachopaswa kufanya ni kutubu kuanzia leo na kumwambia Bwana akusamehe..akusamehe, uasherati wako kama ulikuwa unaufanya..akusamehe kwa kutowajali wanao,..akusamehe kwa kila uchafu uliokuwa unaufanya..na hivyo unamwahidi kwamba utafanya tena..
Baada ya kutubu kabatizwe katika ubatizo sahihi kwaajili ya ondoleo la dhambi (Matendo 2:38)..Kumbuka ubatizo sahihi ni ule wa kuzamishwa mwili wote kwenye maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo. Baada ya kufanya hivyo Roho Ambaye atakuwa ndani yako atakuongoza kufanya mengine yote yaliyosalia na kukupa uelewa wa ajabu wa kuyaelewa maandiko na kukusaidia kushinda dhambi ambazo kwa nguvu zako ulikuwa huwezi.
Kumbuka pia Yesu Kristo atarudi..Biblia inasema “Itatufaidia nini tuupate ulimwengu mzima na kisha tupate hasara za nafsi zetu’’..Hivyo uwe unalitafakari hilo kila siku.
Maran atha!..Shalom.
MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI.HATA UASHERATI NAO
KIMBIA! KIMBIA! KIMBIA!
MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:
BONDE LA KUKATA MANENO.