Title November 2019

KISIMA CHA MAJI YA UZIMA NI KILE KILE CHA ZAMANI.

 kisima cha maji ya uzima ni kile kile cha zamani. Hakitachimbwa kingine.

Shalom, Jina la Bwana wetu YESU KRISTO libarikiwe daima. Leo tutajifunza tena habari ya Isaka,.. kisha tuone ni nini Bwana anataka tujifunze kwa Mababa zetu hawa wa Imani,.. Mungu kujiita, yeye ni Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo, halafu akagotea hapo hakuendelea mbele, alikuwa anayo maana kubwa, Hivyo tunapaswa tujifunze sana juu ya watu hao watatu kwasababu zipo siri nyingi za ufalme zimelala hapo…

Kuhama kwa Isaka:

Tukisoma Mwanzo 26 tunaona kuna wakati njaa kali ilipita katika nchi yake,..Hivyo Isaka akalazimika kuhamisha makao yake kwa muda na kwenda kukaa kwa wafilisti,. lakini huko alipofika Mungu akamfanikisha kupita kiasi akawa Tajiri kiasi cha kuogopesha mpaka wenyeji kumwonea wivu na kumfukuza mpikani mwao,.. lakini alipokuwa huko ilimpasa pia awe na visima vya maji vya kulisha mifugo yake pamoja na watumwa wake, na watu wa nyumbani mwake wote..Lakini tunasoma Isaka hakuchimba kisima chochote kipya katika nchi ile bali alivifukua vile vile vilivyokuwa vimechimbwa na baba yake Ibrahimu tangu zamani sana ambavyo wafilisti walikuwa wamevifukia, na hapo ndipo somo letu la leo lilipo…

Embu Tusome wote sasa:

Mwanzo 26:15 “Na vile visima vyote walivyochimba watumwa wa baba yake, siku za Ibrahimu babaye, Wafilisti walikuwa wamevifukia, wakavijaza kifusi.

16 Abimeleki akamwambia Isaka, Utoke kwetu, maana wewe una nguvu sana kuliko sisi.

17 Basi Isaka akatoka huko akapiga kambi katika bonde la Gerari, akakaa huko.

18 Isaka akarudi akavichimbua vile visima vya maji walivyovichimba siku za Ibrahimu babaye; maana wale Wafilisti walikuwa wamevifukia baada ya kufa kwake Ibrahimu; naye akaviita majina kufuata majina alivyoviita babaye.

19 Watumwa wa Isaka wakachimba katika lile bonde, wakapata kisima cha maji yanayobubujika.

20 Wachungaji wa Gerari wakagombana na wachungaji wa Isaka wakisema, Maji haya ni yetu. Ndipo akakiita jina la kile kisima Eseki, kwa sababu waligombana naye.

21 Wakachimba kisima kingine, wakagombania na hicho tena. Akakiita jina lake Sitna.

22 Akaondoka huko akachimba kisima kingine, wala hicho hawakukigombania. Akakiita jina lake Rehobothi, akasema, Kwa kuwa sasa Bwana ametufanyia nafasi, nasi tutazidi katika nchi.

23 Akapanda kutoka hapo mpaka Beer-sheba”.

Isaka japokuwa alikuwa ni Tajiri, mwenye uwezo wa kuchimba visima vingine vingi vipya,.. lakini yeye hakufanya hivyo bali alivifukua visima vilevile vilivyochimbwa na Baba yake zamani…japo vilikuwa vimeshafukiwa na wafilisti havifai tena, lakini yeye alivifukua hivyo hivyo..kwasababu alijua anachokitafuta

Alitambua kuwa si kila Kisima kilicho mbele yake ni cha kunywa maji yake..

TUNAJIFUNZA NINI SISI WATU WA AGANO JIPYA?

Hata leo hii vipo visima vingi, vinavyodai kutoa maji, wengine kwao elimu ndio Kisima pekee,.. wengine biashara, wengine uongozi, wengine kipaji..wengine umaarufu n.k…lakini kipo Kisima kimoja tu chenye uwezo wa kutoa maji yaliyo hai yenye uzima, ambacho mtu akinywa kwa kupitia hicho, hataona kiu milele..

Watu wengi wamejaribu kukifukia Kisima hiki tangu siku ile ya Pentekoste,..na kikaonekana kweli kama kimeshafukiwa na kupotea kabisa,.. wakati ule kanisa lilipopitia kipindi kirefu cha giza, kwa miaka Zaidi ya elfu moja..lakini kuanzia karne ya 15 kilianza kuchimbuliwa tena na wajenzi ambao Mungu alishaweka tayari kwa kazi kama hiyo, kama vile Calvin,Martin Luther, John Wesley, na wengineo, na mpaka kufikia karne ya 20 yaani kuanzia mwaka 1906 na kuendelea kikaonekana kikitoa maji tena, yale yale yaliyokuwa yanabubuja wakati wa Pentekoste ya kwanza ya mitume…yaani Mambo yale yale yaliyokuwa yanafanyika katika kanisa la Kwanza, yalianza kuonekana tena yakifanyika katika kanisa hili la mwisho…Ndiyo tuliyaona yakianza na wakina William Seymour, William Branham na wengineo…Na hata sasa yule yule anaendelea kufanya kazi…HALELUYA!!

Roho yule yule aliyeachiliwa kipindi cha Pentekoste ambaye Kristo alisema kuwa yeye ndiye atakayeleta chemi chemi ya maji uzima, ndiye aliyemwagwa tena katika kanisa letu hili la mwisho la Laodikia..

Yohana 7:37 “Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe.

38 Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.

39 Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea.”

Kamwe usikoje maji haya ya uzima.

Lakini cha kusikitisha ni kuwa bado watu wanatafuta maji katika visima vingine,.. japokuwa hichi tayari kinaonekana kutoa maji mengi ya uzima tena bure, sio kwa kulipiwa kama vingine..Kaka/Dada ikiwa bado unaichezea hii neema, ipo siku utaitamani, na kuililia lakini utaikosa…Upo wakati utayatamani haya maji hata tone moja tu yakupe uzima lakini utayakosa…

Yule Tajiri aliyekuwa kule kuzimu aliye mwomba Lazaro achovye ncha ya kidole chake katika maji amnyweshe alikuwa hazungumzii maji ya bombani..hapana bali maji ya uzima, walau kidogo tu,.. yaani arudishwe duniani kuhubiriwa injili kwa dakika moja tu atubu aokoke kisha afe tena..Lakini ilishindikana na ndio maana akaomba basi ndugu zake wahubiriwe injili ili wasifike pale alipo..hakuomba ndugu zake wapewe maji mengi sana na washibe vizuri, ili wakifa wasisikie kiu huko aliko, au hakuomba wabebe maji ya kunywa kusudi huko wanakokwenda wawe naye mengi.. hapana aliomba wahubiriwe injili…kwasababu alijua hayo ndio maji ya uzima..

Leo hii itakufaidia nini upate, utajiri wote, upate elimu yote, upate umaarufu wote,.. na ujuzi wote, halafu unakufa ghafla, au kwa uzee mwema na kujikuta upo kuzimu.?..Ni kwanini leo hii usitafute jambo ambalo litakulinda sio tu ukiwa hapa duniani, bali pia hata huko unapokwenda….

Usipuuzie maji ya uzima, maji yaleyale yaliyochimbwa na mababa zetu mitume…Hayo ndio tunayoyaamini, na kumethibitishwa maji mengine, ni batili.

Bwana Yesu alimalizia na kwa kusema..

Ufunuo 21:6 “Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure” Amen.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

KAZI YA UZURURAJI WA SHETANI.

SEHEMU ISIYO NA MAJI.

INGIENI KWA KUPITIA MLANGO ULIO MWEMBAMBA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

USITUMAINISHWE NA MANENO YA UONGO.

Kwanini usitumainishwe na maneno ya uongo?

Kipindi kifupi sana kabla ya Hukumu ya Mungu kuja juu ya mtu, au juu ya nchi , au juu ya ulimwengu. Shetani huwa ananyanyua wimbi kubwa la manabii wa uongo, ambao kazi yao inakuwa ni kupunguza makali ya hukumu inayokuja. Shetani anajua kabisa watu wakiitafakari sana hukumu ijayo watatubu na hivyo atawapoteza na yeye hataki hata mmoja akose kwenda jehanamu pamoja na yeye, ndio lengo lake kubwa.

Tuutazama mfano mmoja katika biblia ambao utatupa mwanga kamili juu ya jambo hili. Mfano huu tunaoutoa kwenye Biblia kwasababu kila neno ili liwe kweli ni lazima lilinganishwe na biblia. Neno lolote linalotoka au kuhubiriwa kama halilingani au halipo kwenye biblia basi Neno hilo ni uongo. Hivyo tutamua biblia kuthibitisha mambo yote.

Tukisoma kitabu cha Wafalme wa pili, tunaona kuna wakati Maovu ya Wana wa Israeli yalifikia kiwango kikubwa sana mpaka Mungu akawatabiria kwamba watachukuliwa tena utumwani kama walivyochukuliwa wakati wa Farao wa Misri. Hivyo aliwaonya kwa kutumia watumishi wake wengi(manabii) watubu lakini hawakutaka (Soma 2Nyakati 36:15-17). Na hivyo kufikia kiwango ghadhabu ya Mungu kuachiliwa juu yao, kwa kuchukuliwa kwenda utumwani Babeli, na wengi wao kuuawa.

Lakini ni kwanini hawakutubu na kuishia kuangamizwa?

Ni kwasababu waliwasikiliza manabii wa Uongo badala ya kuwasikiliza manabii wa kweli wa Mungu. Kipindi hicho kulikuwa na manabii wa kweli wa Mungu kama vile Nabii Isaya ambaye alikuwa anawaonya juu ya maangamizi yanayokuja mbele yao, na kwamba wasipotubu watachukuliwa utumwani, lakini walimdharau. Bwana akamtuma na Nabii Yeremia ambaye aliwaonya na kuwaambia katika hali waliyofikia, kwenda utumwani watakwenda tu.

Hivyo wasitafute hata kupigana bali wajinyenyekeze kwa Nebukadneza, lakini badala yake wakamfunga na kumwona kama mtu asiye na Uzalendo na nchi yake na ni nabii wa uongo na kibaraka wa Nebkadneza. Hivyo wakawasikiliza manabii wengine ambao waliwatabiria mema. Kwamba hawatakufa, hawatapatikana na madhara, watastawi katika nchi ya Ahadi waliyopewa. Waliowatabiria kwamba watajenga na kupanda na kustawi. Manabii hao hawakugusia habari za maasi yao na kwamba wasipotubu watauawa, wao wakawahubiria habari za raha tu na amani..

Tunamsoma Nabii mmoja wa uongo anayeitwa HANANIA. Huyu ni mmoja wa walioibuka kipindi hicho cha Nabii Yeremia ambaye alikuwa anawatabiria watu amani kwamba kutakuwa shwari. Watu wasiogope Mungu bado yupo na wao, hajawaacha. Kamwe Nabii huyu hakuwahi kuwagusia habari za dhambi zao wanazozitenda zinazowafanya Mungu akae mbali nao, yeye aliwahubiria tu amani na mafanikio.

Tusome.

Yeremia 28:1 “Ikawa, katika mwaka ule ule, mwanzo wa kutawala kwake Sedekia, mfalme wa Yuda, mwaka wa nne, mwezi wa tano, HANANIA, mwana wa Azuri, nabii, wa Gibeoni, akasema nami ndani ya nyumba ya Bwana, mbele ya makuhani na watu wote, akisema,

2 Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nimeivunja nira ya mfalme wa Babeli.

3 Kabla haujatimia muda wa miaka miwili mizima, nitavirudisha mahali hapa vyombo vyote vya nyumba ya Bwana, ambavyo Nebukadreza, mfalme wa Babeli, aliviondoa katika mahali hapa, akavichukua mpaka Babeli.

4 Nami nitamrudisha hapa Yekonia, mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, pamoja na mateka wote wa Yuda, waliokwenda Babeli, asema Bwana; maana nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.

5 Ndipo nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, mbele ya makuhani, na mbele ya watu wote waliosimama ndani ya nyumba ya Bwana,

6 naam, nabii Yeremia akasema, Amina, Bwana na atende hivi; Bwana ayatimize maneno yako uliyotabiri, kuvirudisha hapa vyombo vya nyumba ya Bwana na watu wote waliofungwa, toka Babeli, hata mahali hapa.

7 Lakini lisikilize sasa neno hili nilisemalo, masikioni mwako, na masikioni mwa watu wote, 8 Manabii waliokuwako kabla ya zamani zangu, na zamani zako, walitabiri juu ya nchi nyingi, na juu ya falme kubwa, habari ya vita, na ya mabaya, na ya tauni.

9 Nabii atabiriye habari za amani, neno la nabii yule litakapotokea, ndipo nabii yule atakapojulikana, kuwa Bwana amemtuma kweli kweli.

10 Ndipo nabii Hanania akaitwaa hiyo nira iliyokuwa juu ya shingo ya Yeremia, akaivunja.

11 Naye Hanania akanena mbele ya watu wote, akisema, Bwana asema hivi, Hivyo ndivyo nitakavyoivunja nira ya Nebukadreza, mfalme wa Babeli, kabla haujatimia muda wa miaka miwili mizima, na kuiondoa shingoni mwa mataifa yote. Basi nabii Yeremia akaenda zake”.

Upotoshaji wa nabii Hanania.

Huyu (HANANIA), Nabii wa uongo… Kawadanganywa wana wa Israeli kwasababu wanapenda faraja, hawapendi kushutumiwa, hawakupenda kukemewa maisha yao ya dhambi, ya uasherati wanaoufanya, ya ulevi, ya anasa, ya wizi na ushoga na chuki, na uabuduji sanamu..moja kwa moja wakamwamini Hanania na hivyo wakapumbazika, kuamini kwamba katumwa na Mungu. Sasa sikia Bwana kipindi kifupi tu baadaye Bwana alichomwambia Nabii Yeremia.

Yeremia 28: 15 “Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, Sikia sasa, Ee Hanania; Bwana hakukutuma; lakini UNAWATUMAINISHA WATU HAWA MANENO YA UONGO.

16 Basi Bwana asema hivi, Tazama, nakutuma uende zako toka juu ya uso wa nchi; mwaka huu utakufa, kwa sababu umenena maneno ya uasi juu ya Bwana.

17 Basi nabii Hanania akafa, mwaka uo huo, mwezi wa saba”.

Kujirudia kwa yale yale duniani leo.

Umeona hapo?. Mambo yaliyotokea kipindi hicho ndiyo yanayotokea sasa kipindi hichi tunachoishi sasa. Shetani ameshajua tumeukaribia mwisho sana hivyo watu wote wanaanza kufikiri juu ya hukumu ijayo, ya moto wa umilele.

Na hataki mtu hata mmoja akose kuingia jehanamu, kwahiyo ili kuwapumbaza watu ananyanyua JOPO KUBWA LA MANABII WA UONGO!, Ambao kazi yao kubwa ni KUWATUMAINISHA WATU KWA MANENO YA UONGO..Kwamba hakuna hukumu!..Kwamba Dunia bado sana iishe, kwamba Mungu hawezi kuwatesa watu kwenye moto, kwamba usifikirie sana kuhusu mambo yajayo baada ya maisha haya…Watakazana kufundisha na kuhubiri namna ya kupata pesa!. Namna yakufunguliwa kiuchumi, namna ya kutoka kimaisha..Lakini kamwe hawatafundisha namna ya kutoka kwenye dhambi!!. Wana macho ya kuona kesho utaolewa, lakini hawana macho ya kuona kesho utakwenda jehanamu kama usipotubu. Wanaona maono ya wewe Kesho yako itakuwa ni ya kicheko, lakini hawaona maono kuwa Kesho yako itakuwa ni kilio na kusaga meno kama utaendelea kuishi na huyo mke ambaye si wa kwako, na huyo mume ambaye si wa kwako, na huo ulevi ambao unaufanya sasa, na hizo biashara haramu ambazo unazifanya sasa.

Ni wangapi leo hii wana maswali mengi yahusuyo maisha baada ya kifo na hawapati msaada wowote. Zaidi sana kila wanapokwenda wanaambiwa habari za kutabiriwa ndoa zao na biashara zao?. Huyo mtu akiwa tajiri namba moja duniani na akifa katika ulevi wake, au uasherati wake, au kutokusamehe kwake? au visasi vyake alivyonavyo moyoni. Huo utajiri vitakwenda kumsaidia nini huko?.

Tumeonywa tujihadhari.

Biblia inasema katika 1 Wathesalonike 5:3 “Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa”.

Kama hujasamehewa dhambi zako fahamu kuwa ni maelfu wamesamehewa dhambi zilizo nyingi kuliko za kwako bure na Bwana Yesu na anaendelea kutusamehe kila siku. Hivyo nafasi hiyo ya kipekee isikupite, kabla mlango wa Rehema kufungwa. Wakati ambao watu watatubu lakini hatawasikia. Hivyo unachopaswa kufanya ni kujitenga mahali ulipo kwa dakika chache. Na kutubu kwa kukiri makosa yako yote na kuahidi kutokutenda tena, na unaacha kwa vitendo. Hiyo ni hatua ya kwanza. Hatua ya pili kama hujabatizwa katafute ubatizo sahihi kwa maji mengi (Yohana 3:23) na kwa jina la Yesu kwaajili ya ondoleo la dhambi zako kulingana na (Matendo 2:38). Na baada ya hapo Roho Mtakatifu atakusaidia kufanya yaliyosalia ikiwemo kukupa uwezo wa ajabu kushinda dhambi, na kukupa uwezo mkubwa wa kuyaelewa maandiko.

Bwana akubariki.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Nitamjuaje nabii wa Uongo?

JIEPUSHE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

EPUKA MUHURI WA SHETANI

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

 

JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

SAUTI NI SAUTI YA YAKOBO, LAKINI MIKONO NI YA ESAU.

Sauti ni sauti ya Yakobo, lakini mikono ni ya Esau maana yake ni nini?

Shalom! Kama vile Zaburi 68:19 inavyosema… “Na ahimidiwe Bwana, ambaye Siku kwa siku hutuchukulia mzigo wetu;”

..Hivyo kila inapoitwa leo hatuachi kumshukuru Mungu kwa msaada wake anaotupa maishani.

Esau.

Tukisoma kitabu cha Mwanzo, tunaona maisha ya Isaka na wanawe wawili (Esau na Yakobo) jinsi yalivyokuwa,.. wengi wetu tunaifamu habari Esau kuwa alikuwa ni mtu aliyependwa sana na baba yake, na Yakobo alipendwa na mama yake, ..Isaka alimpenda Esau kwasababu alikuwa anamjali sana, ni mtu ambaye alikuwa radhi kupoteza muda wake mwingi ili tu kuhakikisha kuwa baba yake yupo katika hali nzuri, na nafsi yake inafurahi,.. alikuwa anamjali baba yake kiasi kwamba hakuruhusu hata mtu yeyote wa kawaida tu awe anamlisha baba yake, bali yeye mwenyewe alikuwa anatoka na kwenda kumtafutia mnyama mzuri,.. kisha anakuja kumwandaa mwenyewe, na kumtengea baba yake mezani, huo upendo sio wa kawaida..

Hivyo baba yake akampenda sana kwasababu alikuwa anatoa kilicho bora kwa ajili yake,..Esau hakuwa mtu wa kuingia tu zizini na kuchukua mbuzi au kondoo, na kuandaa kwa ajili ya baba yake..Kwake hicho aliona kama sio kitendo cha heshima, badala yake alijiota na kuingia porini mwenyewe kwenda kumtafutia baba yake chakula chenye ladha tofuati na vile ambavyo vinaliwa sikuzote nyumbani..Hata kama ingekuwa wewe ni mzazi ungeachaje kumpenda mtoto kama huyo….hakununulii tu suti zinazotoka labda Kariakoo, bali anafunga safari yeye mwenyewe kwenda kukutafutia suti nzuri nje ya nchi labda Ujerumani au Canada, ili tu nafsi yako ifurahi..

Hiyo ikamfanya baba yake amthamini sana Esau kuliko Yakobo, na ilipokaribia sasa wakati wa kufa kwake, akamwita Esau kisirisiri ili ambariki..hakumwambia hata Yakobo siri hiyo, lakini alimwita akamwambia amwandalie mawindo mazuri kama ilivyo desturi yake ya siku zote na mwisho aje kumbariki.. Esau akaondoka haraka pasipo kujua kuwa mama yake yupo karibu sana na Isaka kuliko yeye anavyodhani.. Ndipo mama yake akafanya haraka haraka kwenda kumweleza Yakobo mambo yote, na akampa siri ya kumfanya auchukue ule mbaraka wa Esau ..

Lakini Yakobo akamwambia mama yake, maneno haya:

Mwanzo 27:11 “Yakobo akamwambia Rebeka mamaye, Esau ndugu yangu ni mtu mwenye malaika, na mimi ni mtu laini.

12 Labda baba yangu atanipapasa, nami nitakuwa machoni pake kama mdanganyifu; nami nitaleta juu yangu laana wala si mbaraka.

13 Mamaye akamwambia, Laana yako na iwe juu yangu, mwanangu, usikie sauti yangu tu, enenda ukaniletee wana-mbuzi”.

Ukiendelea kusoma utaona, Rebeka alimwandalia Yakobo, mambo mawili makuu, moja ni vazi la mnyama, ili kuvaa shingoni na mikononi mwake, na pili ni vazi la Esau lenye harufu ya mawindo ili Isaka akimkaribia asikie harufu nzuri aliyozoea kumsikia nayo Esau kila alipokuwa akimletea mawindo mezani..

Mwanzo 27:21 “Isaka akamwambia Yakobo, Karibu, tafadhali, ili nikupapase, mwanangu, nione kwamba wewe ndiwe mwanangu Esau, ama siyo.

22 Basi Yakobo akamkaribia Isaka, babaye, naye akampapasa, akasema, Sauti ni sauti ya Yakobo, lakini mikono ni mikono ya Esau”.

JE! KUNA JAMBO LOLOTE TUNAWEZA KUJIFUNZA HAPO KATIKA AGANO JIPYA?

Pamoja na mengi yasiyofaa juu ya Esau ambayo tusingepaswa kuyaiga lakini pia upo ufunuo mwingine wa kipekee juu ya maisha ya Esau na Yakobo. Kama vile yasivyokuwa mengi ya kujifunza juu ya maisha ya yona (kwa tabia yake ya kutokutii), lakini pia kutokutii kwake kulibeba ufunuo wa Yesu kukaa kaburini siku tatu.(Soma Luka 11:30-31). Kadhalika na Esau ni hivyo hivyo, maisha yake yamebeba ufunuo juu ya Yesu.

Kumbuka Yakobo kama Yakobo ambaye tunamwona leo hii anayeitwa Israeli asingekuwa vile, wala asingekuwa na Baraka zile kama Sio Esau aliyemwandalia..Hivyo Esau ni mfano kamili wa Bwana wetu YESU KRISTO…Sisi tunaoitwa wakristo, tusingekuwa hivi tulivyo leo hii kama kusingekuwa na mtu ambaye tumemwibia Baraka zake..Na huyo si mwingine zaidi ya Bwana wetu YESU KRISTO…Yeye ndiye aliyempendeza Baba yetu (Mungu) kuliko mwanadamu yoyote hapa duniani, mpaka siku moja sauti ikasikika kutoka mbinguni ikisema huyu ni mwanangu mpendwa wangu niliyependezwa naye…Yeye ndiye mwana peke yake alistahili kupokea Baraka zote peke yake ndiye aliyestahili kubarikiwa na Mungu…Amefanyika kuwa laana kwa ajili yetu sisi, ili sisi tuzishiriki Baraka zake,..kama asingejitwika fedheha zetu, na dhambi zetu sisi leo hii sijui tungekuwa wapi..

LAKINI VIPO VIGEZO VYA SISI KUBARIKIWA.

Kumbuka halikuwa jambo la Yakobo kwenda tu kichwa kichwa kunyakuwa Baraka zile, kulikuwa na taratibu za kufuata. Kwanza ilimbidi avae mavazi ya Esau pili avae ngozi ya mnyama inayofanana na Esau vinginevyo angekumbana na laana ya baba yake badala ya baraka…Hata leo hii wapo watu wanamwendea Mungu bila kufuata kanuni Mungu aliyoiweka..na mwisho wa siku wanaangukia laana badala ya Baraka..Yaani kwa ufupi kama wewe upo nje ya Kristo, ni heri uendelee katika hali yako ya dhambi kuliko kumkaribia Mungu na kumfanyia ibada ukidhani kuwa ndio utampendeza….

Mungu hakuwahi kupendezwa na mwanadamu yoyote ni Yesu Kristo tu peke yake..Na hivyo ili na wewe uonekane unampendeza yeye ni sharti uvae vazi la YESU KRISTO..Kama sio Yesu Kristo sisi ni kama mbolea tu, hatustahili hata kulitaja jina la Mungu.

Tulishapotea siku nyingi kwenye dira za kiungu.

Hilo tu ndilo litakalo tufanya sisi tubarikiwe na Mungu..Na tunaweza kufanya hivyo kwa kutubu dhambi zetu zote kwa kudhamiria kuziacha kabisa kisha kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi (Yohana 3:23) na kwa jina la YESU KRISTO (Matendo 2:38), na baada ya hapo Roho Mtakatifu kuja juu yetu…Tukikamiliza hatua zote hizo tutakuwa na uhakika wote kuwa dhambi zetu zimeondolewa na sisi nasi tutazishiriki Baraka zile zile za Bwana wetu Yesu Kristo.

UTUKUFU UNA KRISTO YESU, BWANA WETU..MKUU WA WAFALME WA DUNIA (Ufunuo 1:5), Aliyetuosha dhambi zetu kwa Damu yake. Ubarikiwe sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

YONA: Mlango 1

TUMAINI NI NINI?

UWE MWAMINIFU HATA KUFA.

BUSTANI YA NEEMA.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Print this post

TENZI ZA ROHONI

Maana ya Neno “Tenzi” ni Tungo zilizokaa katika mfumo wa “Mashairi”..Kwahiyo Mashairi yote ni Tenzi…Na Tenzi zipo za aina mbili. Kuna Tenzi za Mwilini na TENZI ZA ROHONI.

TENZI ZA MWILINI.

Haya ni mashahiri yote ambayo yametungwa na watu kwa kufikisha ujumbe wa mambo yahusuyo ulimwengu huu…Nyimbo zote zinazoimbwa na wasanii wa kidunia ni tenzi za mwilini…Mashairi yote yanatungwa na Wanafalsafa wa ulimwengu huu ni tenzi za mwilini…

TENZI ZA ROHONI.

Pamoja na kuwepo kwa tenzi za Mwilini,..zipo pia Tenzi za rohoni. Tenzi hizi ni nyimbo za mashahiri ambazo zinatungwa kwa uongozo wa Roho Mtakatifu kwa lengo la kuzinufaisha roho za watu.

Madhara ya Tenzi za rohoni yapo katika roho. Nyimbo hizi hazijatungwa kwa lengo la kuinufaisha dunia, wala kisisimua dunia.Ni nyimbo zilizobeba maonyo na mahubiri ya rohoni. Kiasi kwamba mtu akisikia kama alikuwa hajampa Kristo Yesu maisha yake anaguswa moyo na kumgeukia Kristo.

Kadhalika kama alikuwa amevunjika moyo, au amejeruhiwa rohoni basi anajengeka upya na kufarijika na kupata amani mpya tena na nguvu mpya ya kuendelea mbele.

Kadhalika kama kulikuwa na mtu ambaye amerudi nyuma kiimani basi kwa kupitia nyimbo hizo zinamrejesha upya kwenye mstari..Na kumwonya kuhusu hatari za kupotea njia. n.k

Kama Biblia inavyosema katika..

Wakolosai 3:16 “Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu”.

Hivyo tunaonyana kwa Zaburi,  kwa Nyimbo (Ambazo hizi ni nyimbo za kawaida kama mapambio, sifa nk)..Na pia kwa Tenzi za Rohoni (Yaani Nyimbo za rohoni ambazo ni tofauti na sifa).

Katika Ukristo, kipo kitabu kimoja kijulikanacho kama TENZI ZA ROHONI.

Kitabu hichi kimebeba mkusanyiko wa baadhi ya Nyimbo hizo za rohoni (yaani tenzi za rohoni)..Wengi wa watunzi wa nyimbo hizo ndani ya kitabu hicho hawakuzitunga kwa lengo la kupata fedha au kwa lengo la kusisimua watu..Au hawakuamka asubuhi na kuamua kuzitunga tu..

Wengi waliziimba hizo nyimbo kwa ufunuo wa Roho kutokana na mambo fulani ya kiroho waliyopitia katika maisha yao…Wengine walipokuwa matatizoni na Bwana akawaokoa au akaonyesha mkono wake Ndipo wakasukumwa kuziimba…

Kwamfano mwandishi wa wimbo wa tenzi unaoitwa “Yesu kwetu ni Rafiki”…aliyeitwa Joseph Scriven huyu baada ya mpenzi wake kufa kwa kuzama bahati mbaya kwenye maji..siku moja kabla ya harusi yao..alihamia Canada na huko akapata taarifa mama yake kuwa ni mgonjwa sana..Hivyo katika hali ile ya matatizo anayoyapitia akamwandikia shairi la kumfariji mama yake linalosema “omba bila kukata tamaa”..shahiri hilo likaja kubadilishwa jina na kuwa “Yesu Kwetu ni Rafiki”..ambalo ndilo tunaloliimba leo katika vitabu vyetu vya tenzi..

Kwamfano tena wimbo wa tenzi unaoujulikana kama “NI SALAMA ROHONI MWANGU”..

Wimbo huu ulitungwa na mtu anayeitwa Horatio Spafford.. Huyu alikuwa ni Mwanasheria aliyefanikiwa sana..Mambo yalimbadilikia ghafla baada ya moto mkubwa kuzuka katika mji aliokuwa anafanyia kazi wa Chicago mwaka 1871..ukasababisha kuchoma nyaraka zake zote za kazi na hivyo kubaki bila nyaraka yoyote ya kazi…Baada ya tukio hilo akaanza kuporomoka kiuchumi kwani kibarua chake kiliota nyasi… na hivyo kuazimia kuhamia Ulaya.

Wakati anawatanguliza mkewe na wanawe wakike wanne Ulaya yeye alibaki Chicago kumalizia kuweka mambo yake sawa ndipo awafuate wanawe na mkewe huyo Ulaya..Wakati wanawe na mkewe wapo safarini kwenye meli,.. Meli yao ilipata ajali na kuzama na kusababisha kifo cha wanawe wote wanne…Kwa bahati nzuri mkewe aliwahiwa kuokolewa lakini alikuwa katika hali ya mahutihuti.. Horatio alipozipata hizo habari alihuzunika sana, ikambidi afunge safari akamwangalie mkewe hali yake katika hali ya huzuni sana…Wakati yupo kwenye meli akapita lile eneo ambalo ajali ilitokea…Msukumo fulani ndani ukamjia kuimba huu wimbo “

NI SALAMA ROHONI MWANGU

1.Nionapo amani kama shwari, Ama nionapo shida; Kwa mambo yote umenijulisha, Ni salama rohoni mwangu.

Salama rohoni, Ni salama rohoni mwangu.

2.Ingawa shetani atanitesa, Nitajipa moyo kwani Kristo ameona unyonge wangu, Amekufa kwa roho yangu.

Umeona?..Ni wimbo wa kuganga roho…na sio kuburudisha..Ni wimbo wa kutia nguvu roho zetu katika tabu tunazopitia au tutakazopitia, shetani anapotutesa tunajipa moyo na kusema, ijapokuwa nimepoteza vyote lakini ni salama rohoni mwangu, Ninaye Kristo, ingawa nje hakuna usalama lakini Rohoni mwangu kuna usalama n.k…Huo ndio mfano wa Tenzi za rohoni.

Na watunzi wengine wote waliosalia wa tenzi za rohoni…walisukumwa na nguvu fulani ya kiMungu kuziandika.(Tazama historia ya nyimbo nyingine chini mwisho wa somo hili)

Hivyo Ni nyimbo njema ambazo Neno linatuagiza tuwe tunaziimba..sio tuziimba kwa kutimiza wajibu fulani..hapana bali kwa kuzifaidisha roho zetu…Kwasababu lengo la nyimbo hizo siokuijenga Roho ya Mungu bali roho zetu. Na pia zipo nyimbo nyingi za rohoni (yaani tenzi za rohoni)…Tofauti na hizo tunazozijua za kwenye kitabu cha Tenzi..Hivyo zozote zile Roho atakazokuongoza kuzitumia zina matokeo yale yale katika roho.

Bwana akubariki sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali share na wengine.


Mada Nyinginezo:

CHA KUTUMAINI SINA lyrics

USINIPITE MWOKOZI Lyrics

MWAMBA WENYE IMARA

MATESO YA MWENYE HAKI

UWE MWAMINIFU HATA KUFA.

TULICHUNGUZE UMBO LA YESU NA MWENENDO WAKE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

TUNA WAJIBU WA KUOMBEA MAHALI TULIPO.

Tuna wajibu wa kuombea mahali tulipo. hata kama ni pabaya kiasi gani.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze Biblia, leo tutajifunza kwa ufupi umuhimu wa kuombea nchi tuliyopo, sehemu za kazi tulizopo, nyumba tunazoishi, mitaa tunayoishi hata kama ndani yake inatupa shida na mateso kiasi gani. Maadamu tunaishi ndani yake hatuna budi kuiombea.

Tunajifunza kwa wana wa Israeli kipindi kile walichomwudhi sana Mungu kwa dhambi zao. Mpaka kufikia hatua ya Mungu kuwaadhibu kwa kuwatoa katika nchi yao na kuwapeleka utumwani Babeli. Na tunaona tarehe za kwanza kwanza kabisa za wao kufika Babeli wakiwa na minyororo mikononi na miguuni, Mungu alimwambia Nabii Yeremia ambaye alibaki Israeli, kwamba awaandikie waraka waisraeli wote waliofungwa huko Babeli kwamba, hiyo nchi waliyoifikia waitakie mema.

Yeremia 29: 4 “Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, awaambia hivi watu wote waliochukuliwa mateka, niliowafanya wachukuliwe toka Yerusalemu mpaka Babeli;

5 Jengeni nyumba, mkakae ndani yake, kapandeni bustani, mkale matunda yake;

6 oeni wake, mkazae wana na binti; kawaozeni wake wana wenu, mkawaoze waume binti zenu, wazae wana na binti; mkaongezeke huko wala msipungue.

7 Kautakieni amani mji ule, ambao nimewafanya mchukuliwe mateka, MKAUOMBEE KWA BWANA; KWA MAANA KATIKA AMANI YAKE MJI HUO NINYI MTAPATA AMANI”.

Unaona hapo?. Ni mji wa shida ni mji wa mateso na mji wa Ugenini, Ni mji wa wapagani, waabudu mizimu, ni mji ambao uliuteketeza mji wao na kuuwa ndugu zao. Lakini Bwana anawaambia wauombee amani mji huo, wasiulaani.

Kwanini?

Ni kwasababu Mji huo ukiwa na Amani na wao watapata amani, na kinyume chake mji huo ukichafuka na wao watapata tabu. Hilo ni funzo tosha la hali tunazopitia sasa, kuna umuhimu mkubwa sana kuombea mahali tulipo, Nchi unayoishi, hata kama sio nchi yako lakini maadamu unaishi ndani ya hiyo nchi ni lazima uiombee. Kwasababu madhara yakija hata kama unamcha Mungu kiasi gani na wewe pia yatakuathiri tu.

Hebu fikiria vita vitokee ghafla katika nchi uliyopo, mabomu yakapigwa huku na kule. Barabara zikaharibika, miundombinu ya maji na umeme ikaharibika kiasi kwamba maji yakakosekana na umeme vilevile. Unadhani wewe unayemcha Mungu jambo hilo halitakuathiri?..Litakuathiri tu kwa namna moja au nyingine. Kwasababu unahitaji barabara kupitisha gari lako,..unahitaji umeme kuendesha shughuli zako..Unahitaji maji kwa matumizi yako binafsi na mifugo yako..Watoto wako wanahitaji kwenda shule, na sasa hawawezi kwenda tena kwasababu mji umechafuka n.k

Kwahiyo ni muhimu kuombea sehemu tulipo. Kadhalika unaishi kwenye nyumba ambayo si yako, wewe ni mgeni au mpangaji, au si mwanafamilia . Lakini umekaribishwa tu katika hiyo nyumba, Ni wajibu wako kuiombea hata kama hupati hisani wanazozipata wanafamilia. Ni wajibu wako kuiombea kwasababu Nyumba hiyo ikipata Amani nawe pia utanufaika kwahiyo amani…lakini usipoiombea ikipata shida na wewe hutasalimika utateseka mara mbili.

Sehemu zote ulizopo..

Vivyo hivyo katika sehemu ya kazi uliyopo. Una wajibu wa kuiombea hata kama wewe ndiye mfanyakazi unayelipwa mshahara kidogo kuliko wote..Kwasababu ukipaombea pakistawi na wewe pia utastawi..Lakini pakididimia na wewe utaathirika tu. Ndio maana Mungu akawaambia wana wa Israeli hapo juu “MKAUOMBEE KWA BWANA; KWA MAANA KATIKA AMANI YAKE MJI HUO NINYI MTAPATA AMANI”.

Ukiwa shuleni ni hivyo hivyo. Unaiombea shule uliyopo, au chuo. Kwasababu shule ikistawi na wewe utastawi ndani yake. Lakini usipoiombea na kuacha tu bila kujali, waalimu wakiwa wabaya itakuathiri na wewe… Miundo mbinu ikiwa mibovu itakuathiri na wewe… Wanafunzi wenzako wanaokuzunguka wakiwa wabaya utapata usumbufu usio wa lazima..Haijalishi wewe utakuwa mkamilifu kiasi gani, hizo tabu hutazikwepa. Na mambo mengine yote ni hivyo hivyo..Ni lazima kuyaombea. Ni lazima kuombea mahali tulipo Mpaka hapo Naamini utakuwa umeongeza kitu juu ya vile unavyovijua.

Bwana akubariki sana.

Kama hujampa Yesu Kristo Maisha yako. Mlango upo wazi ila hautakuwa hivyo siku zote. Wakati dunia inafurahia anasa…Ujio wa Kristo unazidi kukaribia kila sekunde inayosogea, ujio wake upo karibu kunashinda tunavyofikiri. Watu wa ulimwengu wataomboleza siku ile watakapokuja kugundua kwamba walikuwa wanapoteza muda kujifurahisha na anasa za ulimwengu. Bwana atusaidie tusiwe mimi na wewe. Hivyo Tubu kama hujatubu, na pia tafuta ubatizo kama hujabatizwa, na Upokee Roho Mtakatifu. Kwa hatua hizo tatu utakuwa umekamilisha wokovu wako.

Maran atha!jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Maandiko yanasema Eliya aliomba kwa bidii hadi akasimamisha mvua kunyesha kwa MUDA wa miaka 3 na nusu.(Yakobo5:17) Je! kuomba kwa bidii ni kuomba kwa namna gani?

UWE MWAMINIFU HATA KUFA.

SIKU ILE NA SAA ILE.

UMEPATANISHWA NA MAADUI ZAKO?

JIEPUSHE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

USISIKILIZE DHIHAKA ZA SHETANI, ZITAKUKWAMISHA.

Usisikilize dhihaka za shetani, zitakukwamisha.

Nehemia 4:1 “Lakini ikawa, Sanbalati aliposikia ya kwamba tulikuwa tukiujenga ukuta, akaghadhibika, akaingiwa na uchungu sana, akawadhihaki Wayahudi.

2 Akanena mbele ya nduguze na mbele ya jeshi la Samaria, akisema, Wayahudi hawa wanyonge wanafanyaje? Je! Watajifanyizia boma? Watatoa dhabihu? Au watamaliza katika siku moja? Je! Watayafufua mawe katika chungu hizi za kifusi, nayo yameteketezwa kwa moto?

3 Basi Tobia, Mwamoni, alikuwa karibu naye, akasema, HATA HIKI WANACHOKIJENGA, ANGEPANDA MBWEHA, ANGEUBOMOA UKUTA WAO WA MAWE.”

Ni kawaida ya shetani sikuzote huwa akishaona anakaribia kushindwa anazidisha ujasiri wake kwa kiwango cha hali ya juu sana, kiasi kwamba usipokuwa na moyo mkuu ni rahisi kukiacha kile unachokifanya au unachokiamini mara moja. Huwa anatumia mbinu ya kukishusha thamani kile kitu na ujione kama vile ulikuwa unafanya kazi bure, au umepoteza uelekeo wa Maisha yako mazuri moja kwa moja..

Ndivyo ilivyotokea kwa Daudi pale alipokutana na Goliathi. Utakumbuka Goliathi alimwambia Daudi maneno haya “Njoo huku kwangu; nyama yako nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni.”.. Unaona lakini Daudi hakuogopa badala yake alirudisha mapigo na kumwambia..

1Samweli 17:45 “Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina la Bwana wa majeshi, Mungu wa majeshi ya Israeli uliowatukana.

46 Siku hii ya leo Bwana atakuua mkononi mwangu, nami nitakupiga, na kukuondolea kichwa chako, nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya majeshi ya Wafilisti, ili kwamba dunia nzima wajue ya kuwa yuko Mungu katika Israeli.

47 Nao jamii ya watu wote pia wajue ya kwamba Bwana haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; maana vita ni vya Bwana, naye atawatia ninyi mikononi mwetu.”

Unaona? Ndivyo shetani alivyo sikuzote, Hata alipomwona Nehemia anafanya bidii kuukarabati ukuta wa Yerusalemu ambao ulikuwa umeshaharibika wa Nyumba ya Bwana..japo kweli walikuwa wanaonekana kama vile kazi ile hawataimaliza kwa jinsi walivyokuwa wachache na kwa jinsi walivyozungukwa na maadui…Shetani hakuweza kutulia kwasababau alijua yapo mafanikio makubwa sana katika ujenzi ule kuliko ujenzi wowote unaofanyika duniani kwa wakati ule hadi wakati wa mbeleeni..Hivyo kama kawaida alichokifanya ni kuwavunja tu moyo wakina Nehemia na kuwaambia…

Hicho wanachokifanya hata angepita Mbweha juu ya ukuta huo ungebomoka..Ni dhihaka za shetani kubwa kiasi gani, kumbuka mbweha ni mnyama mwepesi sana, hana hata uzito wa kumfikia mbwa wa kawaida…walau wangesema tembo ingekuwa sio dhihaka za shetani kubwa sana..Licha ya kwamba Nehemia na watu wake walikuwa wanafanya kazi kubwa usiku na mchana kuujenga ukuta. Lakini hapo hapo wanatokea watu na kuwaambia wanachofanya ni kazi bure, hata mbweha akipita juu ya ukuta ule utaanguka.

Lakini Sisi tuonaishi kizazi hiki ndio tunaojua vizuri kama ile kweli ilikuwa ni kazi bure au La!..Kama ulikuwa hujui ukuta ule waliokuwa wanaujenga wakina Nehemia sehemu yake ipo mpaka leo, na hapo ni Zaidi ya miaka 2,500 imeshapita (Tazama picha chini)…Katika wakati wao yalikuwepo majengo mazuri na imara Zaidi ya ule, lakini yalipita, yakaja mengine nayo, yakapita,. Yakaja tena mengine mapya nayo yakapita lakini sehemu ya ukuta ule inadumu mpaka sasa. Ndio ule ukuta uliyo Jerusalemu ambao leo hii maelfu na maelfu ya wayahudi wanakwenda kila mwaka kufanya ibada zao hapo, mbele ya ule ukuta kule Jerusalemu ujulikanao kama ukuta wa maombolezo (wailing wall)..Na ndio ukuta ulio maarufu Zaidi ya kuta zote sasa hivi duniani..

Je! Ukuta huo kweli ulikuwa ni dhaifu?

Ukishaokoka na kumwamini Kristo, shetani hawezi kuvumilia kukuona kuwa siku moja utakuja kuwa msaada mkuu kwa wengine katika mambo ya rohoni. Hivyo leo hii ni lazima atanyanyua tu maudhi na dhihaka fulani fulani ili tu kukukatisha tamaa usisonge mbele, uikane Imani. Ukishaona hivyo, wewe puuzia tu songa mbele..

Unaweza kuchekwa na kuambiwa umepoteza dira ya Maisha. Ukiona hivyo basi ndio ujue upo kwenye njia sahihi, unaweza kuambiwa umelogwa au umerukwa na akili…Ukishaona hivyo usiyatafakari sana hayo maneno yatakuumiza kichwa..ujue tu kuwa ni shetani huyo anatafuta njia ya kukutasha tamaa usisonge mbele kwasababu ameshaona kuna kitu kikubwa kinajiandaa kutokea mbele yako…Puuzia endelea na wokovu wako. Vilevile unaweza ukawa ni mgonjwa na shetani anakuambia huo ugonjwa mwaka huu humalizi utakufa….wewe usimsikilize ni lazima aje kwako kwa ujasiri mkubwa wa namna hiyo, ndio asili yake hiyo, ili tu akufanye uache kuamini…Wewe ziba masikio ikiwezekana mjibu kama vile Daudi alivyomjibu Golithi, “sitakufa bali nitaishi, wewe ndio utayekufa kwenye lile ziwa la moto kuzimu”.

Kwa kufanya hivyo utaweza kuizimisha hiyo mishale yake ya moto. Kumbuka Biblia inasema ufalme wa mbinguni unaanza kama chembe ya haradali…lakini ikishakuwa kuwa kubwa, ndege wa angani wanakuja kutua chini ya uvuli wake (Mathayo 13:31-32)..Lakini ulianza tu kama chembe ndogo sana ya kudharauliwa..Leo hii utaona wokovu wako kama vile hauna faida…Lakini ni jambo la muda tu..Vumilia, kubali kuchekwa, kubali kudharauliwa, kubali mashutumu yote, hayo hayakwepeki…Lakini kuna wakati utafika hiyo mbegu itakuwa mbuyu..

Ikiwa wewe upo ndani ya Kristo, nakutia moyo zidi kumwangalia yeye na songa mbele. Ikiwa bado haujamkabidhi Kristo Maisha yako, kumbuka wakati wa neema ndio huu. Na mlango bado upo wazi lakini hautakuwa wazi kwako siku zote, fanya maamuzi haraka kwasababu biblia inasema saa ya wokovu ni sasa, ukidhamiria kweli kuyasalimisha Maisha yako kwa Bwana, atakupokea na kukutengeneza na kukufanya kuwa mwana wake..

Yohana 3: 16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.

Bwana akubariki.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

YUDA ISKARIOTE! MTUME ALIYECHAGULIWA NA BWANA YESU.

KWANINI DAUDI ALIKUWA NI MTU ALIYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU?

BUSTANI YA NEEMA.

NAMNA YA KUMTAMBUA BIBI ARUSI WA KWELI WA KRISTO.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

WACHAWI

Je! Wachawi wapo?..Wachawi wanaua watu?, wachawi ni wengi?, Nitajikingaje na wachawi?.Je wachawi wanapaa kwa ungo?

Kuna maswali mengi sana yahusuyo wachawi..Lakini kabla ya kuyajibu maswali hayo hapo juu..Ni vema tukajua nini maana ya uchawi..Kwa kujua nini maana ya uchawi unaweza kubofya hapa usome kisha ndipo tuende pamoja. >> Nini maana ya uchawi

Je wachawi wapo?

Kwa ufupi uchawi upo.  Biblia Takatifu inathibitisha hilo.Ni kitu kinachoogopeka sana na wengi wasio na Maarifa ya kutosha yamhusuyo Mungu. Na kama uchawi upo maana yake na wachawi wapo pia. Kwasababu wanauoufanya huo uchawi ndio wanaoitwa Wachawi.

Biblia inawataja wachawi katika..

Kumbukumbu 18:10 “Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri,

11 wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu.

12 Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana, Mungu wako, anawafukuza mbele yako”.

Na katika kitabu cha Matendo tunamsoma mtu mmoja aliyekuwa mchawi.

Matendo 13:6 “Walipokwisha kupita katikati ya kisiwa chote mpaka Pafo, wakaona mtu mmoja, mchawi, nabii wa uongo, Myahudi jina lake Bar-Yesu;”

Kwahiyo wachawi wapo 

Je Wachawi wanaua watu?

Jibu ni ndio!..Wachawi wanaua watu na wanauwezo wa kumdhuru mtu yeyote aliye nje ya Kristo. Kwasababu mtu yeyote aliye nje ya Kristo hana ulinzi wowote wa KiMungu hivyo chochote kile kinauwezo wa kumdhuru..Na wachawi wanauwezo wa kumdhuru mtu kwa uchawi.

Je Wachawi ni wengi?

Ipo idadi kubwa ya wachawi ulimwenguni kote..Kikundi kimoja cha Freemason ambacho ni cha kichawi, kina washirika zaidi ya milioni 6 duniani kote. Na kuna maelfu ya vikundi hivyo katika kila nchi duniani kote. Hivyo kwa ufupi wachawi ni wengi.

Je wachawi wanapaa kwa ungo?

Kama vile maarifa ya wanadamu yalivyo na aina mbalimbali ya vyombo vya usafiri, kwamfano kuna magari, ndege, pikipiki, baiskeli n.k Vivyo hivyo elimu ya uchawi. Wapo wanaotumia ungo kusafiria, wapo wanaotumia ufagio, wapo wanaotumia fimbo, wanyama n.k

Lakini Elimu ya Uchawi ni dhaifu sana…Kiasi kwamba haistahili kulinganishwa na Elimu ya Mungu hata kidogo. Elimu ya Mungu ni kuu sana

Je wachawi ni wa kuogopwa?

Mchawi yoyote hawezi kumwingilia Mtu aliyeokoka…Kwanini? Kwasababu Elimu ya Mungu ni kuu sana..Mchawi ajaribupo kumwigia mtu aliyeokoka..Anaweza akakutana na moja ya mambo yafuatayo.

  1. Anaweza kuona chochote kisicho cha kawaida kikimzunguka yule mtu wa Mungu, inaweza ikawa moto, au mwanga mkali, au anaweza asimwone kabisa.
  2. Anaweza akaona Malaika..Wachawi wengi wanakutana na Malaika wakiwalinda watu wa Mungu, na wengi wa wachawi wanaoona hivyo huwa hawatangazi inaishia kuwa siri yao…Labda wakiokoka ndio wanaweza kutoa ushuhuda…

Je tutashindanaje na wachawi?

Tofauti na inavyodhaniwa na wengi kwamba wachawi tutawashinda tu kwa kuwatupia mishale ya moto katika maombi ya vita vikali vya mkesha…Lakini ukweli ni kwamba mtu tu aliyesimama katika Imani kamilifu,aliyemwaminifu kwa Bwana katika utakatifu na utauwa..Hata asipoomba ombi lolote katika maisha yake linalomhusisha mchawi…bado mtu huyo atakuwa yu salama dhidi ya wachawi.

Mungu hatulindi kwasababu tunawajua maadui zetu..Ndugu ukifunuliwa macho idadi ya maadui ulionao katika ulimwengu wa roho, na ukaambiwa uanze mmoja mmoja kupambana naye… utapambana vita milele na milele na bado hutamaliza hata robo yao..

Wakati wewe unawataja wachawi wako watano hapo mtaani wanakuzunguka…Nyuma ya pazia kuna jeshi la mapepo yanakuwinda usiku na mchana..Kuna pepo ambalo usiku na mchana linapambana tu ujikwae chooni uanguke ufe…Lipo ambalo shughuli yake ni kutafuta kila namna ya wewe kugongwa na gari kila unapotoka nje…lingine ufe na ajali..Pepo lingine ni ili ung’atwe hata na nyoka tu au mbwa mwenye kichaa barabarani…Usiku na mchana yanakufuatilia kila unapotoka, unapokwenda na Mungu anakuepushia nayo. Pasipo hata wewe kujua.

Kwahiyo kamwe usifikiri maombi yako ya vita ndiyo yanayokusaidia sana katika kukulinda..Wachawi ni moja ya maadui wadogo sana wa uzima wako.

Kitu kikubwa kinachokusaidia kukulinda ni wewe kukaa katika maisha yanayompendeza Mungu basii, kuzishika amri zake na kudumu katika Neno lake. Hata usipowataja hao wachawi katika maombi yako kwa miaka 10 hakuna watakalofanya litakalofanikiwa juu yako…Mapepo na wachawi kila watakachokipanga hakitafanikiwa..Uthibitisho utaona tu ni wewe upo salama..Kwasababu Mungu wetu anatupigania kwa namna isiyoonekana.

Je tunapaswa kuogopa kula nyumbani kwa mchawi?

Hatupaswi kuogopa kula chochote kilichopo mbele yetu, kwa hofu ya kulogwa, wala hatupaswi kuogopa kusafiri mkoa wowote au nchi yoyote kwa hofu ya kulogwa. Wala hatupaswi kuogopa kuwapa kuwashika mkono watu ambao tumeshajua ni wachawi au waganga wa kienyeji… Kwasababu tunaye Kristo ambaye anatupigania kwa namna isiyoonekana. 

Je tunapogundua fulani anajihusisha na Uchawi tumfanyeje?

Hatupaswi kumtenga wala kumuua?..wala kumchukia…Kwasababu Uchawi ni dhambi kama dhambi nyingine..Na dawa ya dhambi ni Toba, itokanayo na Injili ya Msalaba…Hivyo mtu yeyote ambaye ni mchawi anaweza tu kuacha uchawi kwa kuhubiriwa injili..ambayo hiyo ni silaha tosha kuifanya kila fikra iweze kumtii Kristo. Na baada yakuhubiriwa Roho Mtakatifu atamchoma ndani yake na kugundua alikuwa gizani na hivyo kuokoka na kuwa kiumbe kipya na kuifanya kazi ya Mungu. Hiyo ndiyo silaha ya kumvua mchawi uchawi wake..Na sio kumkemea wala kumuua.

2 Wakorintho 10:3 “Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili;

4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)

5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;”

Ikiwa hujaokoka!. Ni vyema ukafanya hivyo leo…Hakuna ulinzi wowote mtu anaweza kuupata akiwa nje ya Kristo..Mtu aliye nje ya Kristo kamwe hatawaweza wachawi, wala hataweza kushindana na roho ya uadui inayotenda kazi ndani ya mapepo wabaya…

Hivyo Kristo pekee ndiye anayetoa utakatifu..Mpokee leo na kisha Ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa waji mengi na kwa jina la Yesu Kristo kwa ajili ya ondoleo la dhambi na utakuwa umezaliwa mara ya pili kwa Roho atakayeingia ndani yako. Na hapo utakuwa chini ya mikono salama ya Bwana wetu Yesu Kristo.

Bwana akubariki sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.

JE NI KWELI MTU ANAWEZA KUTOKA NJE YA MWILI WAKE?.

https://wingulamashahidi.org/2019/08/30/maswali-na-majibu-2/

Rudi Nyumbani:

Print this post

NI KIPI MUNGU ANACHOKITAZAMA ZAIDI, MOYO AU MWILI?

Je! ni kipi Mungu anachokitazama zaidi, moyo au mwili?

Shalom. Jina la Bwana Yesu libarikiwe.

Karibu tujifunze Biblia. Neno la Mungu linasema katika..Waefeso 5:9-10 “kwa kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli; mkihakiki ni nini impendezayo Bwana”.

Hivyo kila siku ni wajibu wetu kuhakiki ni nini impendezayo Bwana. Kila tunachokifanya, kila tunachokisema na kila tunalichopanga kukifanya. Ni lazima tuwe na uhakika kwamba Je! kinampendeza Mungu.

Leo tutajifunza kuhusu mambo Mungu anayoyaangalia ndani ya mtu. Kama wengi wetu tunavyofahamu kuwa kuna usemi ambao upo kila mahali miongoni mwa wakristo wengi usemao kwamba “Mungu haangalii mambo ya nje kama mavazi bali anaangalia moyo”. Usemi huo upo kila mahali kama hujawahi kuusikia jaribu kufanya mahojiano na watu 5 au 10 hususani mabinti utalisikia Neno hilo likitoka vinywani mwao.

Kwanza kabisa ni muhimu kufahamu kuwa Mwanadamu kaumbwa katika sehemu kuu mbili ambazo ni UTU WA NDANI na UTU WA NJE. Utu wa ndani ndio unajumuisha Nafsi na Roho ya mtu. Na utu wa Nje ndio hii miili tuliyonayo. Hivyo kuna utu wa ndani na utu wa nje. Soma (Warumi 7:22, Waefeso 3:16),

Sasa aliyeufanya utu wa ndani ndio huyo huyo aliyeufanya utu wa nje. Hivyo vyote viwili kwake anavitazama. Lakini tukija katika suala la Ibada zetu sisi binafsi na Mungu ni ukweli usiopingika kwamba Mungu anatazama utu wetu wa ndani, na si nje. Ingekuwa anatazama miili yetu basi asingesikiliza sala zetu tunapojifungia vyumbani mwetu na kuomba tukiwa kifua wazi, au asingesikia sala zetu au sifa zetu tuwapo bafuni tunaoga. Hivyo hiyo ni wazi kuwa Mungu anaitazama mioyo yetu zaidi ya miili yetu.

Lakini linapokuja suala la kuwepo nje mahali ambapo pana mkusanyiko wa watu wengi. Kama kanisani au barabarani. Ni lazima ujifunike kwasababu haupo wewe na Mungu hapo..Bali upo wewe, Mungu pamoja na watu wengine. Mungu anatazama kweli moyo wako lakini hao wengine hawaoni moyo wako bali mwili wako, na wanapokuona upo nusu-uchi, au umevaa mavazi yasiyostahili au yasiyo na heshima, mioyoni mwao kutatokea tamaa, kutatoka shuku mbaya, kutatoka aibu, kutatokea kukwazika na wakati mwingine hasira na matusi.

Sasa mambo hayo ndiyo yanayomchukiza Mungu kwasababu unawakosesha wengine. Na ndio maana katuambia tuvae mavazi ya kujisitiri kila mahali tunapokwenda. 1Timotheo 2:9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi;”

Usipofanya hivyo, utakuwa unatenda dhambi kwa kuwakosesha wengine. Na Biblia inasema katika..

Marko 9.42 “Na ye yote atakayemkosesha mmojawapo wa wadogo hawa waniaminio, afadhali afungiwe jiwe la kusagia shingoni mwake, na kutupwa baharini.”..

Wewe hujali mwingine anatenda dhambi kwaajili yako. Lakini Mungu anajali sana, adhabu yake ndio hiyo hapo kwamba ni afadhali “kufungiwa jiwe la kusagia na kutupwa baharini”, kuliko kumfanya mtu mmoja akutamani kutokana na uvaaji wako.Kuliko kumfanya mtu mmoja aige uvaaji wako utahukumiwa kwaajili ya hayo.

Kama unasikia joto na unataka kuomba au kuabudu huku umevaa nguo fupi, basi nenda nyumbani kwako peke yako, vaa nguo zako fupi. Jifungie peke yako mahali asipoweza mtu hata mmoja kukuona omba unavyotaka na Sali unavyotaka. Hapo Mungu kweli hataangalia mavazi yako bali roho yako. Lakini unapotoka nje! Hiyo ni habari nyingine kabisa. Mavazi yako na mwonekano wako unajalisha sana. Bwana Yesu alisema..

Mathayo 5:16 “Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni”.

Sasa Ikiwa kuangaza kwako ni nusu-uchi barabarani, ni nani atayayatazama matendo yako na kumtukuza Mungu mbinguni?

Mtu mmoja tu unapomkosesha! Kumbuka sio watu 20, biblia inasema mmoja tu!! Ni huzuni kubwa sana kwa Mungu. Hakuna mtu anayeweza kukutamani ukivaa nguo za kujisitiri mwili wako wote. Usidanganyike na Semi za kishetani zinazokwambia na kukufundisha utembee nusu uchi barabarani au uingie ibadani na vimini hakuna shida. Huo ni uongo wa shetani 100%, ambao unatokana na upambanuzi mbaya wa maandiko…maswali ya moyo au mwili kwamba Mungu anaangalia moyo zaidi ya mwili yakatae.

Na tunapozungumzia uvaaji, tunalenga mavazi..sio mapambo!. Mapambo kama lipstick, wigi, hereni, make-up zote kama kujipaka hina, kuchora tattoo,kupaka wanja.kuchonga nyusi, kujichubua… hayo ni machukizo kabisa ambayo biblia imeyakataza (Soma 1Timotheo 2:9-10, Walawi 19:28). Hupaswi hata kujipamba na kumwomba Mungu ukiwa chumbani mwako peke yako. Kwasababu ni sanamu umeziweka juu ya mwili wako, na hivyo huwezi kumwomba Mungu na huku kuna sanamu kichwani mwako au mwilini mwako.

2Wakoritho 6:16 “Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.

17 Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha”.

Bwana akubariki sana.

Kama hujaokoka! Mlango wa Neema upo wazi, ila si karibuni, na ile njia ya uzima inazidi kuwa nyembamba. Kuokoka kesho ni ngumu kuliko leo, hivyo ni vyema ukafanya uamuzi leo, kwasababu biblia inasema saa ya wokovu ni sasa. Amua kwa dhati kutubu dhambi zako zote huku ukimaanisha kuziacha kabisa, na kisha baada ya kutubu tafuta ubatizo sahihi, ambao huo utakufanya ukamilishe wokovu wako. Ubatizo sahihi ni wa maji mengi na kwa Jina la Yesu kulingana na Matendo 2:38. Na kwa kufanya hivyo Roho Mtakatifu atakutia muhuri na kuwa wake milele, na kukupa uwezo wa kushinda dhambi.

Maran atha!jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

SAMEHE KUTOKA NDANI YA MOYO WAKO.

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

KAMA MUNGU ANABORESHA KAZI ZAKE, KWANINI WEWE USIBORESHE ZA KWAKO?.

Mpagani ni nani?

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE! MTUMISHI KUTOKUWA NA FEDHA NI ISHARA KUWA KUNA TATIZO KATIKA IMANI YAKE?

Jina kuu la Bwana wetu YESU KRISTO libarikiwe. Ni siku nyingine tena Bwana ametupa neema ya kuiona, Hivyo ninakukaribisha tujifunze tena maneno ya uzima maadamu siku ile inakaribia.

Watumishi wengi wa Mungu wameshakutana na changamoto kama hii ya watu kuwauliza mbona huyo Mungu wenu mnayemtumikia hawafanyi kuwa matajiri ikiwa yeye ni Tajiri…

Lakini mtu huyu huyu anayeuliza swali kama hili na yeye ukimuuliza Je! Wewe ni mkristo?. Atakuambia ndio, ukimuuliza Je unaiamini biblia unayoisoma atakuambia ndio ninaiamini.

Ukimuuliza tena Je! unamwamini Bwana Yesu? atakuambia ndio, Na vipi kuhusu mitume wake. Je unawaamini nao? atakuambia ndio ninawaamini asilimia mia kuwa walikuwa ni watumishi walioitwa na Mungu kutuletea sisi Imani ya kikiristo..

Lakini ukimwambia Je! Unajua hao unaowaamini sasa kuna wakati hawakuwa na chochote mfukoni mwao lakini Mungu alikuwa anawatumia bila matatizo yoyote. Atakuambia huo ni uongo..

Matendo 3:1 “Basi Petro na Yohana walikuwa wakikwea pamoja kwenda hekaluni, saa ya kusali, saa tisa.

2 Na mtu mmoja aliyekuwa kiwete toka tumboni mwa mamaye alichukuliwa na watu, ambaye walimweka kila siku katika mlango wa hekalu uitwao Mzuri, ili aombe sadaka kwa watu waingiao ndani ya hekalu.

3 Mtu huyu akiwaona Petro na Yohana wakiingia hekaluni aliomba apewe sadaka.

4 Na Petro, akimkazia macho, pamoja na Yohana, akasema, Tutazame sisi.

5 Akawaangalia, akitaraji kupata kitu kwao.

6 Lakini Petro akasema, MIMI SINA FEDHA, WALA DHAHABU, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende”.

Embu jaribu kifikiria kwa ukaribu mistari hiyo. Omba-omba huwa hahitaji pesa nyingi kama vile mtu wa kawaida anavyoweza kuomba. omba-omba huna wanahitaji vichenchi chenchi tu, vilivyobakia mfukoni shilingi 100, mia 200, mia 300 basi ikizidi sana 500. Na ukiwapa wanashukuru sana na kuona kama siku yao imekuwa nzuri sana. Ni hela ambazo mtu wa kawaida haziwezi kumshinda kutoa..

Lakini mitume wa Bwana Yesu Kristo, hawakuwa nazo, walikiri kwa vivywa vyao kuwa hawana fedha wala dhahabu, hawana chochote. Sio kwamba walikuwa nazo wakawa wanazuia kumpa hapana, ni kweli hawakuwa na kitu mfukoni… Lakini hilo halikuwafanya wajione kuwa sio watu walioitwa na Mungu..Badala yake wakamweleza walicho nacho…ambacho ni Jina la YESU KRISTO, na hilo ndilo waliloliona kuwa lina thamani kubwa kuliko fedha zote duniani.

Mtumishi wa kweli wa Mungu anacho kitu ambacho fedha haiwezi kufikia thamani yake, anazo habari za uzima. Injili inayoweza kumfanya mtu apate uzima wa milele jambo ambalo fedha haiwezi kufanya. Hakuna mtu anayeweza kuongeza muda wa Maisha yake kwa fedha. Na ndio maana na sisi tunaoujasiri kusema..Hatuna fedha wala dhahabu lakini tunalo Neno la Mungu linaloweza kuokoa roho za watu.

Hivyo kama mtumishi wa Mungu kwa fedha alizonazo kama uthibitisho wa utume wake, Na si kwa Neno la Mungu. Nataka nikuambie umepotea njia..kwasababu ni kweli wanaweza wasiwe na hicho unachotamani kukiona kwao..Lakini hao ndio watiwa Mafuta wa Mungu wanaokuletea wewe habari njema za wokovu..na uponyaji wa Roho yako, usiwadharau!.

Yule kiwete ambaye tangu kuzaliwa alikuwa hawezi kutembea. Laiti angewadharau wale Mitume na kulazimisha apate fedha kutoka kwao. Angekufa na hali yake, hata angepewa fedha za mchango na watu wote wa dunia nzima. Hakuna matibabu yoyote duniani ambayo yangeweza kumfanya atembee.

Biblia inasema siku za mwisho kutatokea kundi kubwa la watu watakaokuwa wanapenda fedha (2Timotheo 3:2)..Yaani kwao fedha itakuwa ni kipimo cha kila kitu, hadi katika mambo ya rohoni. kama mchungaji huna gari basi hakuna mtu atakayekuja kusikilza Neno la Mungu kanisani kwako hata kama unafundisha kweli kiasi gani..

Kama ukisimama barabarani kuhubiri upo na biskeli na spika yako, hata kama uwepo wa Mungu upo hapo kuwaokoa watu kiasi gani, na ishara na miujiza vinatendeka, watu watageuza vichwa upande wa pili na kuondoka zao. Lakini wakimuona nabii fulani wa uongo anatembea na walinzi, anafundisha mafundisho yake mwenyewe na kuuza chupa za maji ya upako, na Zaidi ya yote hawaambiwi chochote kuhusu Maisha yao ya dhambi. ndio anakuwa wa kwanza kwenda kumsikiliza na kukunua.

Sisemi watumishi wa Mungu wanapaswa wawe maskini, lakini leweke hilo akilini kuwa mambo ya ufalme wa mbinguni hayapimwi kwa mizani ya fedha au utajiri,..Tukilijua hilo tutaweza kujipima sisi na kuchagua ni wapi pa kudumu kujifunza na ni wapi tusidumu, kwa ajili ya usalama wa Roho zetu.. Hizi ni siku zile za hatari ambazo shetani amejikita Zaidi kuwapotosha watu nyuma ya vazi la uzuri na urembo, na utanashati, na mafanikio..lakini ndani yake ni shimo la kuzimu..Hivyo Bwana atusaidie sote.

Ubarikiwe sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

 

 

Mada Nyinginezo:

ALIYE MKUU KATIKA UFALME WA MBINGUNI.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

CHUKIZO LA UHARIBIFU

NGURUMO SABA

Rudi Nyumbani:

Print this post

UWE MWAMINIFU HATA KUFA.

Uwe mwaminifu hata kufa…

Ufunuo 2:2 “Nayajua matendo yako, na taabu yako, na subira yako, na ya kuwa huwezi kuchukuliana na watu wabaya, tena umewajaribu wale wajiitao mitume, nao sio, ukawaona kuwa waongo;

3 tena ulikuwa na subira na kuvumilia kwa ajili ya jina langu, wala hukuchoka”.

Wengi wanasema Kristo hatujali.. Lakini kiuhalisia ni kwamba anatujali kuliko sisi tunavyodhani. Kila kitu tunachokifanya anakiona, na anakihesabu. Hakuna kinachoenda bure mbele zake. Alisema katika Neno lake “lakini ninyi, hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote.( Mathayo 10:30)”. Sasa mtu anayejua idadi ya nywele zetu zote na hakuna hata moja inayopotea bila yeye kujua ataachaje kufahamu kila tendo jema tunalolifanya?

Ukiona mtu anasema naijua tabu yako. Ni wazi kuwa ni mtu anayejali….tena anakuambia najua Taabu yako na shida zako unazozipitia, anajua uvumilivu wako, na subira yako…Na anajua jitihada zako na jinsi gani huchoki kufanya mema. Ni wazi kuwa ni mtu anayekujali sana na anap moyo wa upendo na wewe.

Ndio maana tunasoma katika kitabu cha Ufunuo, Bwana Yesu alipotoa ujumbe kwa kila kanisa alianza na Neno hili “Nayajua matendo yako,”. Ikifunua kuwa Bwana anatujua sana, kila dakika anatuangalia..Kama ni mabaya tunayafanya anayaona, vile vile kama mema tunayafanya anayaona..Leo ulimhurumia mtu Fulani mnyonge anaona!. Na anarekodi, leo ulimsamehe mtu aliyekuudhi ingawa alikuumiza sana kiasi kwamba ilikuwa hata ni ngumu kumsamehe lakini ulimsamehe tu hivyo hivyo, anakuona. Na atalitaja tukio hilo siku ile mbele ya malaika wake watakatifu.

Ulimhurumia mtu Fulani na kumsaidia katika hali aliyokuwepo. Analiona tendo hilo.

Ulimwombea mwingine katika maombi yako, ingawa yeye hakuna lolote analokufanyia. Bwana anaona na analiandika katika kumbukumbu isiyoweza kusahaulika. Ulitukanwa ukavumilia na wala hukurudisha tusi anaandika. Ulimtolea sadaka yako ingawa ndio hiyo tu uliyokuwa nayo huna nyingine. Ameliweka moyoni mwake zitapita siku kadhaa wewe utasahau lakini yeye lipo moyoni mwake. Kila siku kila dakika linamrudia rudia katika mawazo yake milele na milele.

Wakati mwingine ingawa unaomba lakini majibu yanachelewa, lakini bado unamvumilia. Jambo hilo analiona na uvumilivu wako kwake, upo akilini mwake kila dakika. Mateso na dhiki unazopitia ambazo bado hujaona tumaini na bado hujaiachilia Imani. Nataka nikuambia anaona! Na inamwingia moyoni kuliko hata wewe inavyokusumbua.

Sehemu nyingine anasema “Nayajua matendo yako na upendo na imani na huduma na subira yako; tena kwamba matendo yako ya mwisho yamezidi yale ya kwanza. (Ufunuo 2:19)”

Ufunuo 2:8 “Haya ndiyo aneneyo yeye aliye wa kwanza na wa mwisho, aliyekuwa amekufa, kisha akawa hai.

9 Naijua dhiki yako na umaskini wako, (lakini u tajiri) najua na matukano ya hao wasemao ya kuwa ni Wayahudi, nao sio, bali ni sinagogi la Shetani.

10 Usiogope mambo yatakayokupata; tazama, huyo Ibilisi atawatupa baadhi yenu gerezani ili mjaribiwe, nanyi mtakuwa na dhiki siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima.”

Wakati mwingine huyu huyu Yesu wetu mwema anaruhusu tujaribiwe kwa dhiki na vifungo. Na wakati mwingine anakaa mbali kama vile hayupo. Tambua ya kwamba yupo pembeni yako hata wakati wa tabu. Na anaiona shida yako, Anasema Uwe mwaminifu tu hata kufa. Naye atakupa Taji ya Uzima,Usianze kunung’unika nung’unika kama walivyofanya wana wa Israeli kule jangwani. Ukifanya hivyo utapoteza Taji yako.

Bwana Yesu naye alipitia majaribu mazito kuliko hata sisi. Yeye alitiwa mikononi mwa shetani ili ajaribiwe, akatundikwa msalabani. Na wakati akiwa msalabani japo kuwa alikuwa ni mwana wa Mungu lakini alisikia hali Fulani ya ukame wa kiroho isiyokuwa ya kawaida mpaka akasema Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?. Lakini alikuwa mwaminifu mpaka kufa hakuikana imani wala kunung’unika akiwa pale msalabani. Na Mungu akampa Taji ya Uzima ambayo leo hii tunamtukuza kama MFALME MKUU ASIYESHINDWA. Haleluya!.

Kwahiyo na sisi wakati mwingine Mungu ataruhusu tujaribiwe. Ila tunapaswa na sisi tuwe waaminifu mpaka kufa. Tukifahamu kuwa Mwangalizi wetu yupo mbinguni akirekodi kila tukio na kila tendo jema tunalolipitia, akirekodi kila chozi, na kila tendo tunalolivumilia. Akirekodi kila jeraha tunaloumizwa na tunaposamehe. Tukilitambua hilo itatufanya tuishi maisha ya kujipa moyo kila siku Kuwa mateso ya Ulimwengu huu ni ya kitambo tu. Ipo taji tumewekewa mbinguni. Na upo wakati wa kufutwa machozi.

Malaki 3:13 “Maneno yenu yamekuwa magumu juu yangu, asema Bwana. Lakini ninyi mwasema, Tumesema maneno juu yako kwa namna gani?

14 Mmesema, Kumtumikia Mungu hakuna faida; na, Tumepata faida gani kwa kuyashika maagizo yake, na kwa kwenda kwa huzuni mbele za Bwana wa majeshi?

15 Na sasa twasema ya kwamba wenye kiburi ndio walio heri; naam, watendao uovu ndio wajengwao; naam, wamjaribuo Mungu ndio waponywao.

16 Ndipo wale waliomcha Bwana waliposemezana wao kwa wao. Naye Bwana akasikiliza, akasikia; na kitabu cha ukumbusho kikaandikwa mbele zake, kwa ajili ya hao waliomcha Bwana, na kulitafakari jina lake.

17 Nao watakuwa wangu, asema Bwana wa majeshi, katika siku ile niifanyayo; naam, watakuwa hazina yangu hasa; nami nitawaachilia, kama vile mtu amwachiliavyo mwanawe mwenyewe amtumikiaye”.

Bwana akubariki.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

KITABU CHA UKUMBUSHO

UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.

PENGINE MUNGU ALISHASEMA NAWE KWA NJIA HII.

INJILI YA KRISTO HAITANGAZWI KWA HATI MILIKI.

SIKU ILE NA SAA ILE.

WOKOVU NI SASA

Rudi Nyumbani:

Print this post