TUMAINI NI NINI?

TUMAINI NI NINI?

Tumaini ni moja ya nguzo tatu kuu katika Ukristo, Ya kwanza ikiwa ni UPENDO, Ya pili ni IMANI na ya tatu ni Tumaini. (1Wakorintho 13:13). Sasa hivi viwili vya mwisho vinatabia ya kwenda sambamba, kwani biblia inatumbia Imani ni kuwa na uhakika wa mambo YATARAJIWAYO, ni bayana ya mambo yasiyoonekana…(Waebrania 11:1)

Lakini kibiblia tumaini ni tarajio, au tazamio Fulani ambalo tayari unao uhakika nalo. Tofauti na tafsiri za kawaida kwamba tumaini ni tarajio la jambo ambalo pengine unaweza ukawa hata huna uhakika nalo, kwamfano, mtu anayeishi na virusi vya ukimwi, ipo kauli inayosema, watu wa namna hiyo huwa wanaishi kwa matumaini…Wakiwa na maana kuwa wanatumainia siku moja dawa itatokea, na kwamba isipotekea ndio basi tena…kwasababu wapo katika tarajio lisilo na uhakika.

Lakini katika ukristo ni kinyume  chake, hatusemi tunatumainia tukifa tutakwenda mbinguni, kana kwamba hatuna uhakika huo kuwa tutakwenda mbinguni au la,  hapana…Au hatusemi tunatumai Bwana Yesu atakuja hapana bali tunaamini kuwa atakuja, uhakika huo tunao kabisaa na hiyo ndio inayoitwa Imani…sasa katika kuamini huko ndipo tumaini halisi linazaliwa hapo ndipo tunaweza kusema   tunatumai moja ya hizi siku tutamwona Bwana Yesu akitokea mawinguni…Unaona hapo tunaamini kuwa ni lazima aje, isipokuwa tunatazamia atakuja hivi karibuni, na kama asipokuja leo wala kesho, basi ni sawa lakini mwisho wa siku ni lazima aje tu…

Kila mkristo ni lazima awe na kiwango kikubwa cha Tumaini ndani yake, katika safari hii ngumu na ya majaribu mengi hapa duniani ni lazima TUMAINI liumbike ndani yetu kwamba siku si nyingi Bwana wetu atatuokoa…Na ndio maana tunaimba..’’Ni salama rohoni mwangu, Bwana Himiza siku ya kuja,’’ ..tunatumai siku moja hayo yote yatakwisha, tunapopitia misiba ya ndugu zetu tunatumai siku moja tutawaona tena utukufuni uso kwa uso, na hivyo hiyo inatupa nguvu ya kuendelea mbele tusikate tamaa, tunapopitia mateso, na njaa na kuchukiwa na kutengwa, na kudharauliwa tunajua ni kwa muda tu tunatumai siku moja tutafutwa machozi na BWANA na hayo yote hatutayaona tena…Hilo ndilo tumaini hasaa linalotoka katika uhakika Fulani…ambao bado hatujaufikia maadamu tupo hapa duniani.

Bila tumaini, katika safari hii hatuwezi kufika mbali kama vile tu, bila Imani na Upendo, hakuna chochote tunachoweza kufanya.Kwasababu tumaini linavutwa na subira na uvumilivu.

Warumi 5:1  Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na mwe na amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,

2  ambaye kwa yeye tumepata kwa njia ya imani kuifikia neema hii ambayo mnasimama ndani yake; na kufurahi katika tumaini la utukufu wa Mungu.

3  Wala si hivyo tu, ila na mfurahi katika dhiki pia; mkijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi;

4  na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini;

5  na tumaini halitahayarishi; kwa maana pendo la Mungu limekwisha kumiminwa katika mioyo yetu na Roho Mtakatifu tuliyepewa sisi.

Biblia inaendelea kusema…

Wagalatia 5:5  Maana sisi kwa Roho tunalitazamia tumaini la haki kwa njia ya imani.

Wafilipi 3:20  Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena TUNAMTAZAMIA Mwokozi, Bwana Yesu Kristo;

21  atakayeubadili mwili wetu wa unyonge, upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote viwe chini yake.

Inasema tena…

2Petro 3:13  Lakini, kama ilivyo ahadi yake, MNATAZAMIA mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake. 14  Kwa hiyo, wapenzi, kwa kuwa mnatazamia mambo hayo, fanyeni bidii ili mwonekane katika amani kuwa hamna mawaa wala aibu mbele yake.

Hivyo kwa ufupi  tumaini ni matarajio au matazamio ya ahadi tulizoahidiwa, Lakini Imani ni uhakika wa matarajio hayo. Au tunaweza kusema uhakika wa tumaini letu.

Ubarikiwe sana. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

PENGINE MUNGU ALISHASEMA NAWE KWA NJIA HII.

UMEPATANISHWA NA MAADUI ZAKO?

Biblia inamaanisha nini kusema Yeye aliye na sikio, na asikie?

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
mawazo stanley
mawazo stanley
3 years ago

Ahsante sana nimejifunza mungu awabaliki kwa ujumbe huu mkubwa. Bila matumaini maishani ni sawa na kuwa na giza kubwa.