KUTAHIRIWA KIBIBLIA

KUTAHIRIWA KIBIBLIA

Kutahiriwa Ni nini?

Kutahiriwa kibiblia ni kitendo cha Sehemu ya nyama ya mbele ya uume wa mwanamume kukatwa. Mtoto yeyote wa kiume anapozaliwa anakuwa na sehemu ya nyama iliyozidi katika uume wake. Sehemu hiyo ya nyama ndiyo inayoitwa GOVI na ndiyo iliyokuwa inakatwa.

Katika Biblia Mungu alimpa Ibrahimu maagizo ya kufanya Tohara yake (Yaani kuiondoa hiyo sehemu ya nyama iliyozidi katika kila mtoto wa kiume) kuanzia yeye  binafsi na wazao wake pamoja na wote waliokuwepo katika malango yake. Na Tohara hiyo Mungu aliiruhusu ifanyike  kama Ishara ya Agano Mungu aliloingia nao.

Mwanzo 17:9 “Mungu akamwambia Ibrahimu, Nawe ulishike agano langu, wewe na uzao wako kwa vizazi vyao baada
yako.

10 Hili ndilo agano langu utakalolishika, kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, Kila mwanamume wa kwenu atatahiriwa.

11 Mtatahiriwa nyama ya magovi yenu, na jambo hilo litakuwa ishara ya agano kati ya mimi na ninyi.

12 Mtoto wa siku nane atatahiriwa kwenu, kila mwanamume katika vizazi vyenu, mzaliwa nyumbani, na mnunuliwa kwa fedha, kila mgeni asiyekuwa wa uzao wako.

13 Mzaliwa nyumbani mwako, na mnunuliwa kwa fedha yako, lazima atahiriwe; na agano langu litakuwa katika mwili wenu, kuwa agano la milele.

14 Na mwanamume mwenye govi asiyetahiriwa nyama ya govi lake, mtu yule atatengwa na watu wake; amelivunja agano langu”

Hivyo Tohara ilikuwa ni Ishara ya Agano la Mungu katika miili ya wana wa Israeli.

Na ni kwanini ifanyike katika kiungo cha Uzazi? 

Jibu ni kwamba sehemu ya uzazi, ni sehemu ya siri na ya muhimu sana kwa mtu.Ni sehemu ambayo inafunikwa kwa mavazi mengi. Jambo hilo linafunua kitu fulani katika Tohara ya pili ambayo tutakwenda kuiona hapo mbele.

Lakini sasa tukirudi katika Agano jipya la Yesu Kristo. Tohara ya mwilini sio tena ISHARA YA AGANO Mungu aliloingia nasi. Ipo tohara nyingine ya Rohoni ambayo ndiyo ya Muhimu kuliko zote. Ambayo ndio ISHARA Pekee ya Agano la Mungu. Na hiyo si nyingine zaidi ya TOHARA YA MOYONI.

Warumi 2:29 “bali yeye ni Myahudi aliye Myahudi kwa ndani, na tohara ni ya moyo, katika roho, si katika andiko; ambaye sifa yake haitoki kwa wanadamu bali kwa Mungu”. 

Tunapoisikia Injili na kuitii, Roho Mtakatifu anaondoa kile kipande cha nyama kilichozidi katika mioyo yetu. Kiburi kilichozidi ni govi, Uongo ambao haukupaswa uwepo ndani yako ni govi, hivyo Roho Mtakatifu anaukata. Kadhalika uasherati, ulevi, wizi na mambo mengine yote mabaya. Yanaondolewa na Roho Mtakatifu mwenyewe.

Wakolosai 2:10 “Na ninyi mmetimilika katika yeye aliye kichwa cha enzi yote na mamlaka.

11 Katika yeye mmetahiriwa kwa tohara isiyofanyika kwa mikono, kwa kuuvua mwili wa nyama, kwa tohara ya Kristo”

Tunasoma pia katika..

Matendo 7:7.51 Enyi wenye shingo gumu, msiotahiriwa mioyo wala masikio, siku zote mnampinga Roho Mtakatifu; kama baba zenu walivyofanya, na ninyi ni vivyo hivyo.

Hivyo kutahiriwa kibiblia ni kuondolewa sehemu isiyostahili kuwepo katika moyo wa mtu. Na kama vile jinsi ilivyofanyika kwenye viungo vya uzazi vilivyojificha. Kadhalika inafanyika pia katika MOYO ambao ndio umeficha mambo yote ya siri za mtu.

Je! Umetahiriwa moyoni mwako?..ulevi umeondolewa? rushwa imeondolewa?.. uasherati umeondolewa?. Kumbuka Tohara ya kwanza ilikuwa inawahusu wanaume tu..Lakini hii ya pili inahusu jinsia zote!.

Kama wewe bado unatoa mimba bado hujatahiriwa. Kama wewe mwanamke unasengenya na kuishi na mwanamume ambaye hamjafunga ndoa hapo bado unahitaji tohara ya moyoni.

Hivyo kama hujampa Yesu Kristo maisha yako. Ni wazi kuwa bado hujapokea Tohara hii ya moyoni yenye umuhimu mkubwa sana. Maana hiyo ndio ishara ya Agano la Mungu kwako. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JE! KUNA UMUHIMU WOWOTE WA KULIPA ZAKA?

Je! msalaba kaburini una umuhimu wowote?

SIKU ILE NA SAA ILE.

ROHO HUTUOMBEA KWA KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA!

JE BIKIRA MARIAMU ALIZAA WATOTO WENGINE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Agnes maganga
Agnes maganga
3 years ago

Thank you for the teaching am glad to know more about the word of God my question is how will I able to understand the bible coz am interested to know the word coz the word is our light