Title April 2023

Je! Mwendo wa Sabato ulikuwaje kibiblia?(Matendo 1:12)

Neno hili limetajwa mara moja katika biblia, kwenye kitabu cha;

Matendo 1:12 “Kisha wakarudi kwenda Yerusalemu kutoka mlima ulioitwa wa Mizeituni, ulio karibu na Yerusalemu, wapata mwendo wa sabato”.

Ni mwendo ambao ulitengwa maalumu wa mtu kusafiri siku ya sabato, ambao urefu wake ulikuwa ni dhiraa elfu mbili (2000), ambao ni sawa na Kilometa moja kwa makadirio.

Kutoka mlima wa mizetuni mpaka mjini Yerusalemu, ni umbali uliokuwa  ndani ya hiyo kilometa moja, ndio huo walisafiri mitume wa Bwana siku hiyo.

Lakini Je! Agizo hilo tunalipata wapi katika agano la kale?

Hakuna andiko la moja kwa moja katika torati ya Musa linaloeleza kuwa mwendo wa sabato, ulipaswa uwe ndani ya hizo dhiraa elfu mbili. Bali Marabi wa kiyahudi baadaye walidhani hivyo kulingana na uhalisia wa maandiko haya.

Kutoka 16:29 “Angalieni, kwa kuwa Bwana amewapa ninyi hiyo Sabato, kwa sababu hii huwapa siku ya sita chakula cha siku mbili; kaeni kila mtu mahali pake, mtu awaye yote asiondoke mahali pake kwa siku ya saba

Kwamba anaposema Usiondoke mahali pako, anamaanisha ndani ya mipaka ya mji wako, hii ikiwa na maana ukiwa ndani ya mipaka uliruhusiwa kutembea, utakavyo. Na kama ikitokea unatoka, basi hupaswi kusafiri Zaidi ya hizo dhiraa elfu 2000.

Na hiyo waliirithi kufuatana na sheria ya malisho ya nje ya mji ambayo walipewa walawi katika..

Hesabu 35:4 “Na yale malisho ya miji mtakayowapa Walawi, ukubwa wake utakuwa tangu ukuta wa mji kupima kiasi cha dhiraa elfu pande zote.  5 Nanyi mtapima hapo nje ya mji upande wa mashariki dhiraa elfu mbili, na upande wa kusini dhiraa elfu mbili, na upande wa magharibi dhiraa elfu mbili, na upande wa kaskazini dhiraa elfu mbili, huo mji ulio katikati. Hayo ndiyo yatakayokuwa kwao malisho ya miji”.

Hivyo kwa kurejea sheria hizo, wakahitimisha kuwa mwendo wa mtu kusafiri nje ya mji siku ya sabato ni hizo dhiraa elfu mbili(2000) au kilometa moja . Ndio Wakauita mwendo wa Sabato. Lakini hakukuwa na sheria ya moja kwa moja inayoeleza mwendo huo ulipaswa uwe katika vipimo hivyo.

Lengo la kufanya vile ni kuwafanya watu wasitawanyike mbali na eneo la kuabudia, ndani ya mji, siku hiyo ya Bwana.

Hata sasa. Ni lazima Kila mmoja wetu awe na mwendo wake wa sabato katika siku ya Bwana..kumbuka jumapili ni siku ya Bwana, hupaswi kwenda mbali na uwepo wa Mungu, siku hiyo sio siku ya kufanya biashara, sio siku ya kwenda kwenye mihangaiko isiyokuwa na lazima, Bali ni siku maalumu Kwa ajili ya ibada..penda kuwepo kanisani, mikutanoni, kwenye semina, kwenye mafundisho redioni,mitandaoni, kwenye vitabu vy ona kiroho.n.k.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MWENDO UNAOSHANGAZA SANA!

IMESALIA RAHA YA SABATO KWA WATU WA MUNGU.

Je ni kweli ilikuwa desturi ya Bwana kuishika sabato?(Luka 4:16)

Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

EPUKA KUCHELEWA IBADA.

Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?

NI NINI KITAKACHOTUFANYA TUPIGE MBIO BILA KUPUNGUZA MWENDO?

Rudi nyumbani

Print this post

Je ni kweli hakuna aliyepaa mbinguni zaidi ya Mwana wa Adamu? (Yohana 3:13)

Je ni kweli Yesu peke yake ndiye aliyepaa mbinguni, na Eliya hakupaa wala Henoko? Kulingana na Yohana 3:13?

Jibu: Tusome,

Yohana 3:13 “Wala hakuna mtu aliyepaa mbinguni, ila yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu”

Mstari huu lengo lake si kutoa taarifa za waliopaa mbinguni au ambao hawajapaa!, tukiusoma kwa lengo hilo basi ni rahisi kuchanganyikiwa, na kuona biblia inajichanganya…

Mfano mtu anaweza kusikika akitoa kauli hii “hakuna mtu aliyewahi kuja kwangu kunitazama, isipokuwa mtoto wangu tu”.. Kauli hiyo mtu asipojua kwanini imezungumzwa vile, anaweza kutafsiri kuwa “hakuna mtu yeyote aliyewahi kufika nyumbani kwake huyo ndugu, iwe mgeni au mwenyeji, isipokuwa mtoto wake tu…..maana yake anaishi tu peke yake peke yake, au nyumba yake ipo mafichoni mahali ambapo watu hawawezi kufika, au pengine amefunga mlango kwa wageni hivyo hakuna mtu yeyote anayeweza kumtembelea”…

Lakini kumbe hakumaanisha hivyo, yule aliyemsikia hakuanza kusikiliza mwanzo wa maneno yake bali alichukua kipande cha mwisho cha maneno yake… lakini kumbe maneno yake hasa yalianza hivi….. “Tangu nilipoanza kuugua, mpaka nilipopona hakuna mtu aliyewahi kuja kwangu kunitazama isipokuwa mtoto wangu tu “

Na kauli ya Bwana Yesu, aliposema hakuna aliyepaa juu ila aliyeshuka, ina mantiki hiyo hiyo…

Sasa Ili tuelewe vizuri, tuanzie kusoma mstari ule wa 12.

Yohana 3:12 “Ikiwa nimewaambia mambo ya duniani, wala hamsadiki, mtasadiki wapi niwaambiapo mambo ya mbinguni?

13  Wala hakuna mtu aliyepaa mbinguni, ila yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu”

Hapa tunaona ni Bwana Yesu anampa Nikodemu taarifa kuwa “yeye pekee ndio mwenye taarifa za mbinguni, yaani siri za ufalme wa mbinguni”  asizozijua mtu mwingine yeyote.

Na kwanini siri hizo anazo yeye tu peke yake?, na si mwingine yeyote?..Kwasababu ni yeye tu pekee ndiye aliyetokea mbinguni, wengine wote asili yao ni hapa duniani, hivyo hawawezi kujua mambo ya mbinguni wala siri za ndani za mbinguni, kwasababu hawakutokea huko. Lakini Yesu asili yake sio duniani..yeye alikuwepo mbinguni kabla hajazaliwa na Mariamu.

Nabii Eliya alipaa mbinguni lakini hakutokea mbinguni, hivyo hawezi kuyajua ya mbinguni, kwasababu asili yake ni duniani,  yeye  alizaliwa hapa  duniani kama wanadamu wengine wote, mbinguni alienda kama tu sehemu ya mwaliko.. Kama sisi tutakavyoalikwa siku ile ya mwisho ya parapanda.. Tutaenda kama wageni waalikwa, lakini Kristo si mgeni mwalikwa bali Mwalikaji/naye ni mwenyeji.

Ni sawa na Mtoto wa mfalme wa Taifa fulani, aje aishi Tanzania na baada ya muda arejee nchini mwake, halafu kuna kijana mwingine raia wa Tanzania, mzaliwa wa Tanzania apewe mwaliko wa kwenda kuishi Huko kwenye huo ufalme, kipindi chote cha maisha yake.. Je huyu kijana aliyealikwa anaweza kuwa sawa na yule kijana aliye mwana wa Mfalme?.. Au watakuwa na uelewa sawa kuhusiana na mambo ya huo ufalme?.

Jibu ni la! Ni wazi kuwa Huyu kijana wa Mfalme atakuwa  anajua siri nyingi za Taifa lake, kuliko huyu kijana aliyealikwa, kwasababu ni mzaliwa wa kule, na zaidi sana ni mwana wa mfalme, lakini huyu aliyealikwa hatajua sana mambo ya ufalme ule, kwasababu yeye ni kama mwalikwa tu.

Ni hivyo hivyo kwa Eliya na Henoko.. Hao ni waalikwa tu mbinguni, lakini hawakuwa wenyeji wa kule,

Lakini Yesu ni Mwalika, na tena ni mfalme.. hivyo Kristo pekee ndiye ajuaye mambo yote ya  mbinguni, siri zote za Ufalme wa mbinguni, kwasababu yeye ni mwana wa Mfalme na pia asili yake ni kwenye huo ufalme.

Ndio maana sasa biblia inasema hapo… “Ikiwa nimewaambia mambo ya duniani, wala hamsadiki, mtasadiki wapi niwaambiapo mambo ya mbinguni? Wala hakuna mtu aliyepaa mbinguni, ila yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu”.

Maana yake hakuna mtu aliepaa mbinguni kwenda kuzichukua siri na kutujuza sisi, isipokuwa Yule aliyeshuka kutoka kule, ambaye ni Yesu Kristo mwenyewe, Mwana wa Adamu.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

MJUE SANA YESU KRISTO.

Ni kweli hakuna mtu aliyewahi kuuona uso wa Mungu Zaidi ya Bwana Yesu?

Uishi kwa furaha pamoja na mke umpendaye, siku zote

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana yake, mpumbavu kuwa na fedha mikononi mwake ya kununulia hekima, Ikiwa hana moyo wa ufahamu?


Mithali 17:16 “Nini maana yake, mpumbavu kuwa na fedha mkononi mwake ya kununulia hekima, Ikiwa hana moyo wa ufahamu?”..

Hili andiko lina maana gani?

Jibu: Awali ni vizuri kufahamu hekima inayozungumziwa hapo ni hekima gani?

Hekima inayozungumziwa hapo si hekima ya kiMungu, kwasababu hekima ya Mungu haipatikani kwa fedha…bali hekima inayozungumziwa hapo ni ile ya kiulimwengu, ambayo hiyo inaweza kupatikana kutoka kwa watu,na kwa njia ya kununuliwa (kwa njia ya kwenda katika shule za wenye hekima)…ambapo mtu atalipa kiasi fulani cha Ada na kisha kufundishwa hiyo hekima.

Mfano wa shule za hekima, ni hizi tulizonazo sasa, ambapo mtu atajiunga na shule fulani na kwenda kupewa Maarifa katika eneo fulani la maisha, ambayo yatamfanya aishi vizuri na kupata mafanikio katika maisha.

Kwahiyo hapo biblia iliposema… “Nini maana yake, mpumbavu kuwa na fedha mkononi mwake ya kununulia hekima, Ikiwa hana moyo wa ufahamu?”

Tafsiri yake kwa lugha nyepesi ni hii………. “ina maana gani mpumbavu kuwa na fedha ya kulipia elimu yake na ikiwa hana Moyo wala Nia ya kuipata hiyo hekima?”

Ni jambo ambalo kweli halina Maana,…kwasababu hata akienda kutafuta kuinunua hiyo hekima hataipata kwasababu moyo wake haupo huko, hivyo ataenda kupoteza fedha tu…

Andiko hili linatufundisha umuhimu wa kufanya kitu kwa moyo (iwe cha kimwili Au cha kiroho)… Kama hujanuia kufanya kitu kwa moyo basi ni heri usikifanye kabisa kwasababu ni sawa na kupoteza muda au fedha.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwanini maombi kwa Marehemu si sahihi kibiblia?

Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia;Achukiaye mambo ya dhamana yu salama

TAFUTA HEKIMA, MAARIFA, UFAHAMU NA BUSARA.

Shetani anaishi wapi, Je! Amefungwa au yupo kuzimu?

WALA HAKUSIMAMA MTU PAMOJA NAYE, YUSUFU ALIPOJITAMBULISHA KWA NDUGUZE

Rudi nyumbani

Print this post

Mtiririko wa vitabu vya biblia kwanini upo vile?

SWALI: Kwanini vitabu vya biblia vipo katika mtiririko ule, na sio kinyume chake?

Ni vema kufahamu kuwa mtiririko wa kibiblia wa agano la kale na agano jipya, haukuwekwa na Mungu, kwamba kianze kitabu hiki kifuate hiki, kianze cha Mwanzo kisha kifuate cha Kutoka. Hapana bali ni utaratibu uliowekwa na wanadamu, ambao kimsingi unamaudhui mazuri, na uligawanya hivyo ili kumsaidia msomaji kufahamu vizuri, kuliko vingeorodheshwa  tu kila kimoja eneo lake, ingewia ngumu kwa msomaji anayependa kujifunza Biblia kuelewa kiwepesi.

Mtiririko ambao sisi tunaoutumia ni tofauti na mtiririko ambao Wayahudi wanautumia kwa vitabu vya agano la kale.

Kwa mfano mtiririko wetu (Ambao unajulikana kama mtiririko wa kiprotestanti), una vitabu 39 vya Agano la kale. Lakini mtitiriko wa Kiyahudi, una vitabu 24 kwa agano hilo hilo la kale,.

Vitabu vyetu ni kama vifuatavyo

Vitabu vya Sheria

  1. Mwanzo
  2. Kutoka
  3. Mambo ya Walawi
  4. Hesabu
  5. Kumbukumbu la Torati

Vitabu vya Historia

  • Yoshua
  • Waamuzi
  • Ruthu
  • 1Samweli
  • 2Samweli
  • 1Wafalme
  • 2Wafalme
  • 1Mambo ya Nyakati
  • 2Mambo ya Nyakati
  • Ezra
  • Nehemia
  • Esta

Vitabu vya Mashairi

  1. Ayubu
  2. Zaburi
  3. Mithali
  4. Mhubiri
  5. Wimbo ulio bora

Vitabu vya Manabii (Wakubwa)

  • Isaya
  • Yeremia
  • Maombolezi
  • Ezekieli
  • Danieli

Vitabu vya manabii (Wadogo)

  • Hosea
  • Yoeli
  • Amosi
  • Obadia
  • Yona
  • Mika
  • Nahumu
  • Habakuki
  • Sefania
  • Hagai
  • Zekaria
  • Malaki                                                     

Lakini utajiuliza kwanini biblia ya kiyahudi iwe na vitabu 24 na sio 39? Je vingine vimeondolewa? Jibu ni hapana, bali baadhi yao vilijumuishwa kama ni kitabu kimoja kwamfano.

> Vitabu viwili vya wafalme kwao ni kitabu kimoja.

> Vitabu viwili vya Mambo ya Nyakati kwao ni kitabu kimoja.

> Vitabu viwili vya Samweli kwao ni kitabu kimoja.

> Ezra na Nehemia vimeweka kama kitabu kimoja.

> Vitabu 12 vya Manabii wadogo kwao ni  kitabu kimoja.

Jumla yake ni vitabu 24 Badala ya 39.

Hivyo tukirudi katika biblia yetu, yenye vitabu 39 kwa agano la kale, Orodha ile haijawekwa kulingana na vipindi vilipoandikwa, bali kulingana na ‘asili ya vitabu’. Ndio hapo utaona hiyo migawanyo mikuu mitano (Yaani vitabu vya Sheria, vya historia, vya mashairi, vya Manabii wakubwa na wale wadogo).

Kutaja manabii wakubwa haimaanishi kuwa walikuwa na vyeo vya juu au walikuwa na nguvu zaidi ya wale wengine hapana, bali ni kutokana na wingi wa uandishi wao, yaani waliokuwa na uandishi mwingi waliwekwa katika kundi hilo la manabii wakubwa.

Tukirudi katika agano jipya.

Vipo vitabu 27, na vyenyewe pia havijaandikwa kulingana na wakati wa uandishi, japo havipishani sana na wakati wa uandishi.

Huu ndio mgawanyo wake.

Vitabu vya Injili

  1. Mathayo
  2. Marko
  3. Luka
  4. Yohana

Kitabu cha Historia

  • Matendo

Nyaraka za Paulo

  • Warumi
  • 1Wakorintho
  • 2Wakorintho
  • Wagalatia
  • Waefeso
  • Wafilipi
  • Wakolosai
  • 1Wathesalonike
  • 2Wathesalonike
  • 1Timotheo
  • 2Timotheo
  • Tito
  • Filemoni

Nyaraka kwa wote

  1. Waebrania
  2. Yakobo
  3. 1Petro
  4. 2Petro
  5. 1Yohana
  6. 2Yohana
  7. 3Yohana
  8. Yuda

Unabii

  • Ufunuo

Halikadhalika Nyaraka za Mtume Paulo ziliorodheshwa katika mpangilio ule kutoka na  urefu wa uandishi na sio umuhimu wa nyaraka Fulani zaidi ya nyingine, kwamfano utaona kitabu cha kwanza kwa urefu cha Mtume Paulo ni Warumi na ndio kilichowekwa cha kwanza. Vilevile kirefu zaidi ya vyote alivyoviandika kwa Watu, ni cha Timotheo ndicho kilichopangiliwa cha kwanza.

Lakini pamoja na kwamba havikuweka katika mpangalio wa nyakati za uandishi bado zinamtiririko mzuri unaelekeana na historia, kuanzia kitabu cha Mwanzo mpaka ufunuo.  Japo pia katika usomaji haimaanishi ufuate mtiririko huo, bali unaweza kuanza vyovyote upendavyo kwa jinsi Roho Mtakatifu atakavyokuongoza.Kwasababu hakuna sehemu yoyote katika maandiko tumewekewa mtiririko huo.

Pia zipo biblia nyingine mfano ile ya Kikatoliki yenye vitabu 73, ambayo kimsingi haijavuviwa na Roho wa Mungu kwani kuna baadhi ya vitabu vimeongezwa ambayo hukinzana na mafundisho ya msingi ya imani, na hivyo hatupaswi kuifuata. Biblia yetu ina vitabu 66 tu. Kama vilivyoorodheshwa hapo juu. Zaidi ya hivyo hutoka kwa Yule mwovu.

Bwana akubariki sana.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Tofauti kati ya maandiko na Neno ni ipi?

TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.

HISTORIA YA BIBLIA YA KING JAMES, INA FUNZO GANI KWETU?

Vitabu vya Deuterokanoni ni vya kiMungu?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

Mimbari ni nini? Je tofauti kati ya Mimbari na madhabahu ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

JE BWANA YESU ALIMTOKEA YUDA BAADA YA KUFUFUKA KWAKE?.

Je Bwana Yesu alimtokea Yuda baada ya kufufuka kwake?.. maana tunasoma katika 1Wakorintho 15:5 kuwa aliwatokea wale Thenashara ambao mmojawao alikuwa ni Yuda.

Jibu: Kwanza ni muhimu kujua maana ya Neno “Thenashara”.. Tafsiri ya Thenashara ni “kumi na mbili”. Maana yake popote biblia inapotaja neno hilo, iliwalenga wale Mitume 12 wa Bwana Yesu.

Na katika kipindi cha huduma ya Bwana Yesu, Yule Yuda aliyemsaliti alikuwa miongoni mwa hao Thenashara. Lakini tunaona baada ya kufa walibaki Mitume 11 tu..na kipindi Bwana Yesu anafufuka Yuda tayari alikuwa ni Marehemu kwani alijinyonga kabla hata ya Bwana kufufuka, hivyo hakuuona ufufuo wa Bwana,  Lakini tukienda mbele katika kitabu cha 1Wakorintho 15:3 tunasoma kuwa Bwana aliwatokea wote 12.. Je ni kwamba biblia inajichanganya au la?

Tusome..

1Wakorintho 15:3  “Kwa maana naliwatolea ninyi hapo mwanzo yale niliyoyapokea mimi mwenyewe, ya kuwa Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama yanenavyo maandiko;

4  na ya kuwa alizikwa; na ya kuwa alifufuka siku ya tatu, kama yanenavyo maandiko;

5 na ya kuwa alimtokea Kefa; TENA NA WALE THENASHARA;

6  baadaye aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano pamoja; katika hao wengi wanaishi hata sasa, ila baadhi yao wamelala”

Ni kweli Bwana aliwatokea wale Thenashara (yaani Mitume 12), lakini Yule wa 12 hakuwa Yuda kwasababu biblia inasema nafasi yake ilichukuliwa na mtu anayeitwa mwingine aliyeitwa Mathiya.

Tusome.

Matendo 1:23  “Wakaweka wawili, Yusufu, aitwaye Barsaba, aliyekuwa na jina la pili Yusto, na Mathiya. 24  Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuonyeshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili,

25  ashike mahali katika huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe. 26  Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye AKAHESABIWA KUWA PAMOJA NA MITUME KUMI NA MMOJA”

Hapo anasema Mathiya akahesabiwa kuwa pamoja na Mitume 11, maana yake yeye alikuwa wa 12. Kwahiyo Mathiya alihesabika miongoni mwa Thenashara, na ndio maana hapo katika 1Wakorintho 15:5 Mtume Paulo kataja kumi na Mbili, lakini Yule wa 12 hakumlenga Yuda bali Mathiya.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Thenashara ni nini? (Marko3:16)

Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?

Katika (Mathayo 25:8 na Marko 16:8) Wale wanawake walitangaza kufufuka kwa Bwana au walikaa kimya?

Je! tunapaswa kukiamini Kitabu cha Henoko?

Je! Bwana Yesu alisulubiwa juu ya msalaba au juu ya mti uliokuwa wima?

Rudi nyumbani

Print this post

Mimbari ni nini? Je tofauti kati ya Mimbari na madhabahu ni ipi?

SWALI: Mimbari ni nini? Je tofauti kati ya Mimbari na madhabahu ni ipi?


Mimbari ni eneo lililoinuka ambalo limetengwa rasmi katika kanisa kwa ajili ya Neno la Mungu kuhubiriwa, au taarifa za kikanisa kuwasilishwa, au huduma nyingine za kiibada kutendeka kama vile uimbaji wa kwaya.

Lakini Madhabahu ni eneo la kanisa ambalo watu huenda kuomba, kutoa sadaka, kupeleka shukrani na sifa, na kushiriki meza ya Bwana (yaani mahali pa kukutana na Mungu). Madhabahuni pa Mungu sio tu pale mbele ya kanisa, bali ni lile eneo lote la kanisa. Isipokuwa tu lile la mbele ndio linasimama kama kitovu cha madhabahu yote.

Mara nyingi mimbari pia huwa palepale madhabahuni. Hivyo unaweza kusikia mtu anasema nakwenda kusimama madhabahuni kuhubiri, mwingine utamsikia anasema nakwenda kusimama mimbari. Wote wawili hawajabadili maana.

Hivyo ikiwa unakwenda kwa kuhubiri, au kuhutubu, au kuimba kwaya kiuhalisia hapo ni sawa na unasimama mimbarani, lakini ikiwa unakwenda kwa ajili ya kuomba, kutoa sadaka, kufanya ibada kama kusifu na kuabudu, hapo huisogelei mimbara bali madhahabu ya Mungu.

Mimbarani ni mahali pa kusikilizwa, lakini madhabahuni, ni mahali pa kushiriki

Mambo ambayo hupaswi kufanya mimbarani kama mhubiri.

  • Kutoka toka sana nje ya mimbari pindi uhubiripo
  • Kufundisha maudhui ambayo ipo nje ya Neno la Mungu. Mfano, siasa, michezo
  • Kujigamba/ Kujisifu zaidi ya kumtukuza Kristo
  • Kupuuzia kujiandaa, kimaombi na kiroho, kabla ya kusimama mimbarani

Mambo ambayo hupaswi kufanya uwapo madhahabuni kama mshirika.

  • Usitoe sadaka yako kama una neno na ndugu yako.(Mathayo 5:23-24)
  • Usivae mavazi yasiyo na utukufu machoni pa Bwana
  • Usizunguke zunguke, au kuzungumza ovyo uwapo kanisani (kuwa mtulivu). Kumbuka eneo lote la kanisa ni madhabahu ya Mungu, na sio pale mbele tu.
  • Hakikisha huchelewi kufika madhabahuni pa Mungu, wala huikatishi ibada na kuondoka

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?

Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?

Kwanini madhabahu zilitengenezwa kwa mawe yasiyochongwa?

Biblia inasema tujihadhari na “Mbwa” hawa mbwa ni akina nani? (Wafilipi 3:2)

UPAKO NI NINI?

Rudi nyumbani

Print this post

USIJISIFIE KARAMA KWA UONGO.

Mithali 25:14 “Kama mawingu na upepo pasipo mvua; Ndivyo alivyo yeye ajisifiaye karama kwa uongo”.

Njia nyingine shetani anayoitumia kuwaangusha watu na kudanganya watu, ni kupitia “karama za uongo”.. Hii inatokea pale ambapo mtu anajipandikiza karama ambayo hana, na anajitangaza kuwa anayo kwa wote, jambo ambalo lina madhara makubwa sana kiroho.

Zifuatazo ni ishara za karama ya kweli ndani ya Mtu, maana yake mtu akikosa hizi ishara basi huenda hiyo karama hana au anayo lakini imeshambuliwa na kutumiwa na adui.

  1. KUWAKAMILISHA WATAKATIFU.

  Mtu mwenye karama ya kweli ya Mungu, ni lazima atakuwa na msukumo wa kuwafanya watu wazidi kukamilika katika Utakatifu, na kumcha Mungu…hata kufikia viwango ambavyo Mungu anataka (Waebrania 12:14), maana yake kila siku atakuwa anatafuta kutatua kasoro zinazofanya watu au yeye mwenyewe asiwe wakamilifu kwa Mungu..Lakini kama karama ya mtu inazidi kumfanya yeye mwenyewe asiwe mkamilifu, au kuwafanya watu wasiwe wakamilifu kwa Mungu, au wasihamasike kumtafuta Mungu zaidi, au kujitakasa… badala yake inawahamasisha kutafuta mambo ya kidunia, basi huyo mtu haijalishi anajiita Mchungaji au Mtume, au nabii kiuhalisia hana hiyo karama..

Utauliza tunalithibitisha vipi hilo kimaandiko… hebu tusome maandiko yafuatayo..

Waefeso 4:11  “Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu; KWA KUSUDI LA KUWAKAMILISHA WATAKATIFU….”

2. IPO KWA LENGO LA KUWAHUDUMIA WATU NA SI KUJIHUDUMIA YENYEWE.

Karama yoyote ya kweli ni lazima iwe na HUDUMA, na huduma maana yake ni kutoa msaada kwa wengine, na msaada tulioagizwa sisi wakristo tu utoe ni ule wa kiroho na usio na gharama.. Maana yake hatujaagizwa kuwatoza watu vitu ili wapokee kutoka kwetu.

Hiyo ikiwa na maana kuwa kama mtu yeyote anajiita Mchungaji, au Nabii, au Mwinjilisti au Mwimbaji, au Mwimbaji, halafu huduma yake anaitoa kwa malipo, ni wazi kuwa hana hiyo karama, haijalishi anajua kuimba kiasi gani au anajua kuhubiri kiasi gani, au anatoa unabii kiasi gani… Kama hatakuwa mtu wa kutoa Huduma bila kutazamia malipo, huyo atakuwa anahudumu kwa roho nyingine ya adui.

Utasema tulithibithisha vipi hili nalo  kimaandiko… Tuendelee na mstari ule wa 12..

Waefeso 4:11  “Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu;

12  kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, HATA KAZI YA HUDUMA ITENDEKE….”

3. IPO KWA LENGO LA KUUJENGA MWILI WA KRISTO.

Mwili wa Kristo inajengwa kwa viungo vyote na si kimoja au viwili.. Kristo alipokuwa hapa duniani hakuwa mlemavu.. wala hata baada ya kufa hakuwa mlemavu (maandiko yanaonyesha mifupa yake haikuvunjwa pale msalabani).. Na sisi ni viungo vya Kristo, hivyo ili tuujenge mwili mkamilifu wa Yesu ni lazima tuwepo wote pamoja..

Mtu akijiona Nabii, au Mtume, au Mwalimu na hayupo katika ushirika na viungo vingine katika kanisa, ni yeye tu kama yeye, mtu huyo si kiungo cha Kristo, na hana hiyo karama anayojivunia..

1Wakorintho 12:14  “Kwa maana mwili si kiungo kimoja, bali ni vingi.

15  Mguu ukisema, Kwa kuwa mimi si mkono, mimi si wa mwili; je! Si wa mwili kwa sababu hiyo?

16  Na sikio likisema, Kwa kuwa mimi si jicho, mimi si la mwili; je! Si la mwili kwa sababu hiyo?

17  Kama mwili wote ukiwa jicho, ku wapi kusikia? Kama wote ni sikio ku wapi kunusa?

18  Bali Mungu amevitia viungo kila kimoja katika mwili kama alivyotaka.

19  Lakini kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?

20  Lakini sasa viungo ni vingi, ila mwili ni mmoja.

21  Na jicho haliwezi kuuambia mkono, Sina haja na wewe; wala tena kichwa hakiwezi kuiambia miguu, Sina haja na ninyi”.

Tunazidi kulithibitsha hili katika mstari ule ule wa 12..

Waefeso 4:11 “Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu;

12 kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, HATA MWILI WA KRISTO UJENGWE”

Kama Karama haiujengi mwili wa Kristo ni karama ya uongo.

Kwahiyo ni lazima kila mtu mwenye karama Fulani ya Roho awe na sifa hizo, lakini kama hana hizo sifa basi huenda hana hiyo karama anayojivunia kuwa anayo au alikuwa nayo lakini sisi imeshambuliwa na inatumiwa na adui.

Na watu wote wanaojivunia karama za Uongo, biblia imesema ni kama mawingu yasiyo na maji.

Mithali 25:14 “Kama mawingu na upepo pasipo mvua; Ndivyo alivyo yeye ajisifiaye karama kwa uongo”.

Maana yake ni watu wanaotoa matumaini ya kusitawisha jambo lakini mwisho wao ni ukame tu.. Hivyo si wakuaminiwa.

Bwana atusaidie karama zetu ziwe za kweli.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?

ICHOCHEE KARAMA YAKO.

Nini tofauti kati ya Kipawa na Karama?

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.

Rudi nyumbani

Print this post

ISHARA YA KANISA LA LAODIKIA

Karibu katika mafunzo ya biblia.

Kwanini tunasema kuwa hili ni kanisa la Mwisho la Laodikia?, Je ni viashiria gani vinavyotutambulisha kuwa hali ya kanisa la Laodikia lile la saba ambalo Mtume Yohana alilonyeshwa kwenye Maono  katika kitabu cha Ufunuo ndio hali halisi ya kanisa letu la siku za mwisho?.

Awali ya yote hebu tujikumbushe historia ya yale makanisa saba, tunayoyasoma katika kitabu cha Ufunuo Mlango wa 2 na wa 3.

Makanisa saba tunayoyasoma katika kitabu cha Ufunuo ni makanisa ambayo yalikuwa katika miji 7 tofauti tofauti. (Efeso, Smirna, Pergano, Thiatira, Sardi, Filadelfia na Laodikia, Ufunuo 1:11).

Hivyo  na makanisa hayo yalijulikana kwa majina ya miji hiyo,  na Yote ilikuwa inapatikana katika eneo lijulikanalo kama “Asia Ndogo” ambapo kwasasa ni nchi ya “Uturuki”.

Sasa kila kanisa lilikuwa na tabia yake, kulingana na huo mji (unaweza kusoma tabia hizo katika Ufunuo 2-3). Na kanisa la Mwisho kabisa kutajwa ambalo ndio la saba lililoitwa Laodikia lilikuwa na tabia nyingine ya kipekee ambayo kwa hiyo ndiyo tutajua kuwa kanisa letu la sasa linafanana na kanisa la huo mji au la!.

Sasa kabla ya kwenda kusoma tabia za kanisa hilo katika kitabu cha Ufunuo, hebu kwanza tuweke msingi mwingine wa kuelewa jambo lingine, ambalo litatusaidia kuelewa hili vizuri.

Katika biblia maandiko yanatabiri kuwa dalili za siku za mwisho ni Maasi kuongezeka katika kiwango cha miji ya Sodoma na Gomora, au miji ya Nyakati za Nuhu (Soma Luka 17:26-28).

Maana yake ni kuwa kama hali ya maovu haijafikia kile kiwango cha maasi ya Sodoma na Gomora, basi bado ule mwisho utakuwa upo mbali, lakini kama hali ya mji itafikia kile kiwango cha maasi ya Sodoma na Gomora basi ni wazi kuwa ule mwisho umefika.

Kwahiyo ni sahihi kusema kuwa  Miji ya Sodoma na Gomora ni ishara au alama ya miji ya siku za mwisho, Hivyo tukitaka kujua kuwa tupo siku za mwisho basi tujilinganishe na miji ya Sodoma na Gomora. (2Petro 2:6 na Yuda 1:7).

Na sasa tunaona kabisa kuwa kizazi chetu ni kama kile cha Sodoma na Gomora na hata huenda kimepita, kwasababu katika miji ya Sodoma na Gomora kulikuwa na mwingiliano wa ndoa za jinsia moja..vile vile na sasa hali ni hiyo hiyo, ushoga upo kila mahali, mauaji, dhuluma n.k kwahiyo tupo siku za mwisho.

Vile vile na kanisa la Mji wa Laodikia, ambao ulikuwepo katika enzi  za kanisa la Kwanza,  lilikuwa ni Ishara ya kanisa la siku za mwisho. Maana yake ni kuwa tukitaka kujua kuwa tunaishi katika kanisa la mwisho, basi tunapaswa tujilinganishe kanisa letu na lile la Laodikia. Tukiona yanafanana kitabia basi tujue kuwa hili ndio kanisa la mwisho na unyakuo umekaribia.. lakini tukiona kuwa bado hatujafikia viwango vya kanisa lile basi tujue kuwa ule mwisho huenda bado sana.

Sasa hebu tusome tabia za kanisa la Laodikia katika biblia.

Laodikia 3:14 “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu.

15  NAYAJUA MATENDO YAKO, YA KUWA HU BARIDI WALA HU MOTO; INGEKUWA HERI KAMA UNGEKUWA BARIDI AU MOTO.

16  Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

17  Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi”.

Umeona tabia za kanisa la Laodikia?..Biblia inasema ni kanisa ambalo lilikuwa vuguvugu, si moto wala si bariki.. mfano kamili wa kanisa la wakati huu. (Kumbuka hapa tunazungumzia kanisa na si watu wa ulimwengu, watu wa ulimwengu ishara yao ni miji ya Sodoma na Gomora na sisi kanisa ishara yetu ni kanisa la mji wa Laodikia).

Kanisa la wakati huu utaona mtu mguu mmoja nje mguu mmoja ndani, leo yupo kanisani kesho disco, leo anamwabudu Bwana kesho anasikiliza miziki ya kidunia, simu yake nusu ina nyimbo za injili nusu nyimbo za kidunia, kabati lake nusu lina nguo za kujisitiri nusu lina nguo za nusu uchi, maneno yake nusu ya heshima nusu ya kihuni, biashara yake nusu ni halali nusu si haramu, duka lake nusu lina bidhaa njema nusu lina bidhaa haramu (pombe, na sigara), leo atatoa sadaka kesho anaonga/ anaogwa.n.k

Hiyo ndiyo ilikuwa hali ya kanisa la Laodikia na ndio hali ya kanisa la Sasa tulilopo.

Hiyo ndiyo alama pekee inayotutambulisha siku si nyingi unyakuo wa kanisa utatokea. Kwasababu hakutakuwa na kanisa lingine litakalotokea lenye tabia nyingine, hili la Laodikia biblia imetabiri ndio kanisa la Mwisho baada ya hapo ni unyakuo ndio maana utaona pale, baada ya ujumbe wake kumalizika kilichofuata ni Yohana kuchukuliwa juu mbinguni.

Ufunuo 4:1 “Baada ya hayo naliona, na tazama, mlango ukafunguka mbinguni, na sauti ile ya kwanza niliyoisikia kama sauti ya baragumu ikinena nami, ikisema, Panda hata huku, nami nitakuonyesha mambo ambayo hayana budi kuwako baada ya hayo”.

Wakati kanisa hili la Laodikia limechafuka hivi, Bwana analiandaa kundi lake dogo, na kuliambia litoke huko, kama vile alivyowaokoa Nuhu na Luthu..Vile vile kanisa la Laodikia litaingia katika dhiki kuu kwasababu ni kanisa vuguvugu lakini kundi dogo ambalo litakuwa safi na litakuwa Moto na si Vuguvugu hilo litaenda na Bwana katika unyakuo.

Ndugu unyakuo umekaribia sana, Yesu yupo Mlangoni kurudi, ondoka katika uvuguvugu, wa kidunia, kuwa Moto.. Ukiamua kumfuata Kristo basi mfuate kwelikweli, usiige desturi za kiduni, ukiamua kuwa mtu wa kujisitiri fanya hivyo kikweli kweli usiwe nusu nusu, ukiamua kumfuata Yesu basi jikane kweli kweli.

Uvuguvu Kristo anauchukia kuliko hata Yule mtu aliye baridi kabisa.. kwasababu yeye mwenyewe anasema ni heri mtu awe moto au baridi kuliko vuguvugu..

Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

AGENDA KUBWA YA SHETANI KWA KANISA HILI LA LAODIKIA.

SAUTI NI SAUTI YA YAKOBO, LAKINI MIKONO NI YA ESAU.

Babewatoto ni nani katika biblia?(Isaya 34:14).

Babeli ni nchi gani kwasasa?

JE NI KWELI SAMAKI NGUVA YUPO?

Rudi nyumbani

Print this post

USIKWEPE USHIRIKA NA MADHABAHU YA KRISTO.

Upo umuhimu wa kufanya ushirika.

Ushirika unatokana na neno kushiriki.  Na matokeo ya kushiriki ni kuambukizwa sifa au tabia ya kile kitu unachoshirikiana nacho.

Watu wengi hatujui hata Neno USHIRIKINA limetokana na neno kushiriki. Washirikina wanashiriki mambo ya kipepo, ili wapate sifa za kipepo, au waambukizwe tabia zao ndani yao na ndio maana wanaitwa washirikina. Ndio hapo utaona mtu anakwenda kwa mganga, kisha anapewa dawa Fulani anaambiwa anywe au aweke chini ya biashara yake, halafu itamfanya wateja wavutiwe na biashara yake. Mtu huyo analivuta pepo la mauti ndani yake, kwa ushirika anaoufanya kisa lile pepo linasimama pale na kushawishi watu waovu , kisha Yule mtu anapata anachokitafuta kwa muda, halafu mwisho wa siku pepo lile linageuka na kumuua,.kwasababu hatma ya shetani sikuzote ni kuchinja na kuiba. Lakini ikiwa mtu huyo hatofanya ushirikina wowote, hawezi kuwa na uwezo huo wa kipepo.

Sasa na katika Mungu ni vivyo hivyo. Unapokuwa nyumbani mwa Mungu Usiwe ni mtu wa kwenda na kutoka tu, kama mtembeleaji. Huna ushirika wowote na watakatifu wengine, huna ushirika wowote na Mungu,. Ukifanya hivyo hutakuwa na nguvu zozote au sifa au tabia zozote za ki-Mungu ndani yako.

Ushirika wa Kikristo Ni upi?

  1. Kuhudumu
  2. Meza ya Bwana
  3. Kutawadhana miguu

Kwamfano Unapohudumu, yaani unapojishughulisha na jambo Fulani ndani ya Kanisa labda kufundisha, kujitoa kwa ajili ya maendeleo ya kanisa kama kuchangia, kufagia, kujenga, kupiga deki, na vyovyote vile. Hapo ni sawa unafanya ushirika na watakatifu wengine katika kuujenga mwili wa Kristo. Na hivyo rohoni, unapokea uwezo au sifa nyingine ya ziada ambayo hapo kwanza ulikuwa huna. Na moja ya uwezo huo ni nguvu ya kuendelea mbele katika imani.

Na pia Meza ya Bwana. Huna budi kushiriki. Kwasababu hiyo inakuunganisha na Mungu moja kwa moja. Embu soma maandiko haya upate kuelewa vema;.

1Wakorintho 10:14  “Kwa ajili ya hayo, wapenzi wangu, ikimbieni ibada ya sanamu. 15  Nasema kama na watu wenye akili; lifikirini ninyi ninenalo.

16  Kikombe kile cha baraka tukibarikicho, JE! SI USHIRIKA wa damu ya Kristo? Mkate ule tuumegao, SI USHIRIKA wa mwili wa Kristo? 17  Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja; kwa maana sisi sote twapokea sehemu ya ule mkate mmoja.

18  Waangalieni hao Waisraeli walivyokuwa kwa jinsi ya mwili; wale wazilao dhabihu, je! Hawana shirika na madhabahu? 19  Basi niseme nini? Ya kwamba kile kilichotolewa sadaka kwa sanamu ni kitu? Au ya kwamba sanamu ni kitu?

20  Sivyo, lakini vitu vile wavitoavyo sadaka wavitoa kwa mashetani, wala si kwa Mungu; nami sipendi ninyi kushirikiana na mashetani. Hamwezi kunywea kikombe cha Bwana na kikombe cha mashetani”.

Umeona? Kumbe kikombe na mkate ule ni USHIRIKA.. ambao sisi tunafanya na Mungu. Na hivyo una matokeo yake makubwa rohoni. Yesu alisema mtu asipoula mwili wangu, na kuinywa damu yangu hana uzima ndani yake. (Yohana 6:53)

Vivyo hivyo na kutawadhana miguu watakatifu. Unapomwosha mwenzako miguu, maana yake ni kuwa unajishusha na kujinyenyekeza kwake, hivyo unapokea neema ya Upendano wa ndugu ndani yako.

Hivyo kwa ufupi ili utake kupokea tabia zote za Ki-Mungu ndani yako,  kama Upendo, utu wema, furaha, amani, Uvumilivu, huna budi kuwa katika ushirika wake. Nje ya hapo, huwezi.

Matendo 2:41  “Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu. 42  Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali”

Usiukwepe ushirika wa Bwana.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

HUNA SHIRIKA NAMI.

MEZA YA BWANA, NA KUTAWADHANA MIGUU.

KANUNI RAHISI YA KUPOKEA BARAKA MARA DUFU.

HISTORIA YA BIBLIA YA KING JAMES, INA FUNZO GANI KWETU?

WANNE WALIO WAONGO.

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?

Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima; (Mithali 11:16)

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini maombi kwa Marehemu si sahihi kibiblia?

Jibu: Katika biblia hakuna mahali popote panapoonyesha marehemu waliombewa..isipokuwa katika sehemu moja tu inaonyesha Marehemu mmoja aliyekuwepo katika mateso ya kuzimu aliomba ndugu zake walio hai wakahubiriwe injili ili wasifike katika dhambi na kwenda kule aliko, lakini tunaona maombi yake hayo hayakuwa na matokeo yoyote.
Hebu tuisome hiyo habari..

Luka 16:27 “Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu,
28 kwa kuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao pia wakafika mahali hapa pa mateso.
29 Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao.
30 Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu, watatubu.
31 Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishiwa hata na mtu akifufuka katika wafu”

Umeona?..Huyu Tajiri alijaribu kuwaombea watu walio hai wasifike alipo lakini maombi yake yalizuiliwa, halikadhalika Sisi tulio hai hatuwezi kuwaombea watu waliokufa kwamba watolewe katika mateso ya kuzimu.

Kama kuna maombi ya kuwaombea wafu watoke katika mateso ya kuzimu na kuingia paradiso, basi vile vile yatakuwepo pia maombi au sala za kuwatoa watu peponi na kuwapeleka kuzimu.. Lakini kama hakuna maombi ya mtu kumtoa mtu peponi(yaani paradiso) na kumpeleka kuzimu…vile vile hakuna maombi yoyote ya kuweza kumtoa mtu kuzimu na kumpeleka peponi.

Utasema tunazidi kulithibitisha vipi hilo kimaandiko?

Hebu tuzidi kuisoma hiyo habari ya Tajiri na Lazaro…Tuangalie maombi mengine aliyoomba kuhusiana na yeye kutolewa kule.

Luka 16:23 “Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu.
24 Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.
25 Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa.
26 Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ILI WALE WATAKAO KUTOKA HUKU KWENDA KWENU WASIWEZE; WALA WATU WA KWENU WASIVUKE KUJA KWETU”.

Hapo mwisho anasema..kati Yao (hao walio kuzimu na walio peponi)..KUMEWEKWA SHIMO KUBWA kama mpaka, ili walio kuzimu wasiweze kuvuka kuingia peponi na walio peponi wasivuke kwenda kuzimu..Ikiwa na maana kuwa hakuna mwingiliano wowote wa walio kuzimu na walio peponi..Hilo shimo katikati yao lipo mpaka sasa.

Hivyo kwa hitimisho, maombi ya kuwaombea heri Marehemu au kuwaombea wapunguziwe adhabu ni maombi yasiyo ya kimaandiko na hayana matokeo yoyote… Vile vile sala za kuwaomba watakatifu waliofariki watuombee halipo kimaandiko.

Ni vizuri kutengeneza maisha yetu hapa duniani kabla ya kufa, kwa kumwamini Bwana Yesu na kutubu dhambi, kwasababu tukishakufa hakutakuwa na nafasi nyingine ya pili.

Yohana 8:24 “Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba mtakufa katika dhambi zenu; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenu”.
Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je sisi wakristo tunaruhusiwa kufanya 40 za marehemu?

MATESO YA KUZIMU.

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

USIRUHUSU INZI WATUE JUU YA ROHO YAKO.

JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.

Rudi nyumbani

Print this post