(Masomo maalumu yahusuyo mifungo na maombi).
Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze Biblia Neno la Mungu wetu lililo taa ya miguu yetu na Mwanga wa njia yetu (Zab 119:105).
Biblia inatufundisha sehemu kadhaa FAIDA za kufunga (yaani kujizuia kula na kunywa kwa kitambo) kwamba kwa kufanya hivyo tunafungua milango mingi, ambayo isingeweza kufunguka kwa maombi ya kawaida tu.
Mathayo 17:20 “Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu. 21 [LAKINI NAMNA HII HAITOKI ILA KWA KUSALI NA KUFUNGA”.
Mathayo 17:20 “Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.
21 [LAKINI NAMNA HII HAITOKI ILA KWA KUSALI NA KUFUNGA”.
Lakini JE UNAJUA FAIDA ZA KUIFUNGISHA NA MIFUGO YAKO PIA? AU KAZI YAKO, AU BIASHARA YAKO?. Si watu tu wanaopaswa kufunga hata wanyama pia.. Utauliza hilo limekaaje?, hetu turejee biblia kidogo nyakati zile za Nabii Yona alipokwenda kuhubiri katika mji wa Ninawi.
Biblia inaonyesha kuwa Mfalme wa Ninawi alipiga mbiu kuwa wanadamu na wanyama wote walioko Ninawi wafunge wasile wala wasinywe (Zingatia hilo: si wanadamu tu bali hata wanyama wa kufungwa).
Yona 3:6 “Habari ikamfikia mfalme wa Ninawi, naye akaondoka katika kiti chake cha enzi, akavua vazi lake, akajivika nguo za magunia, na kuketi katika majivu. 7 Naye akapiga mbiu, akatangaza habari katika mji wa Ninawi, kwa amri ya mfalme na wakuu wake; kusema, Mwanadamu ASIONJE KITU, WALA MNYAMA WALA MAKUNDI YA NG’OMBE, WALA MAKUNDI YA KONDOO; WASILE, WALA WASINYWE MAJI; 8 bali na wafunikwe nguo za magunia, MWANADAMU NA MNYAMA PIA, nao wakamlilie Mungu kwa nguvu, naam, na wageuke, kila mtu akaache njia yake mbaya, na udhalimu ulio mikononi mwake. 9 Ni nani ajuaye kwamba Mungu hatageuka na kughairi, na kuiacha hasira yake kali, ili msiangamizwe? 10 Mungu akaona matendo yao, ya kuwa wameiacha njia yao mbaya. Basi Mungu akalighairi neno lile baya, ambalo alisema atawatenda; asilitende”.
Yona 3:6 “Habari ikamfikia mfalme wa Ninawi, naye akaondoka katika kiti chake cha enzi, akavua vazi lake, akajivika nguo za magunia, na kuketi katika majivu.
7 Naye akapiga mbiu, akatangaza habari katika mji wa Ninawi, kwa amri ya mfalme na wakuu wake; kusema, Mwanadamu ASIONJE KITU, WALA MNYAMA WALA MAKUNDI YA NG’OMBE, WALA MAKUNDI YA KONDOO; WASILE, WALA WASINYWE MAJI;
8 bali na wafunikwe nguo za magunia, MWANADAMU NA MNYAMA PIA, nao wakamlilie Mungu kwa nguvu, naam, na wageuke, kila mtu akaache njia yake mbaya, na udhalimu ulio mikononi mwake.
9 Ni nani ajuaye kwamba Mungu hatageuka na kughairi, na kuiacha hasira yake kali, ili msiangamizwe? 10 Mungu akaona matendo yao, ya kuwa wameiacha njia yao mbaya. Basi Mungu akalighairi neno lile baya, ambalo alisema atawatenda; asilitende”.
Unaona alichofanya Mfalme wa Ninawi??…Na matokeo yake tunaona baadaye Mungu anawataja wanyama kuwa wamestahili rehema kwa mfungo huo..Maana yake wanyama nao pia wasingefungishwa huenda wangepona watu tu lakini wanyama wangepigwa (wangekufa!!)..Maana yake uchumi wao watu wa Ninawi ungeharibika, hata baada ya wao kupokea msamaha!!.
Yona 4:10 “Bwana akamwambia, Wewe umeuhurumia mtango, ambao hukuufanyia kazi, wala kuuotesha; uliomea katika usiku mmoja, na kuangamia katika usiku mmoja; 11 na mimi, je! Haikunipasa kuuhurumia Ninawi, mji ule mkubwa; ambao ndani yake wamo watu zaidi YA MIA NA ISHIRINI ELFU, wasioweza kupambanua katika mkono wao wa kulia na mkono wao wa kushoto; TENA WAMO WANYAMA WA KUFUGWA WENGI SANA?”
Yona 4:10 “Bwana akamwambia, Wewe umeuhurumia mtango, ambao hukuufanyia kazi, wala kuuotesha; uliomea katika usiku mmoja, na kuangamia katika usiku mmoja;
11 na mimi, je! Haikunipasa kuuhurumia Ninawi, mji ule mkubwa; ambao ndani yake wamo watu zaidi YA MIA NA ISHIRINI ELFU, wasioweza kupambanua katika mkono wao wa kulia na mkono wao wa kushoto; TENA WAMO WANYAMA WA KUFUGWA WENGI SANA?”
Nataka uangalie hayo maneno ya mwisho ya Bwana… “TENA WAMO WANYAMA WA KUFUGWA WENGI SANA?”
Kumbe hata wanyama pia wanaweza kuingizwa kwenye mkondo wetu wa BARAKA AU LAANA!.. Mfalme wa Ninawi aliliona hili, alijua siku ile ya gharika ya Nuhu hata wanyama waliangamizwa na dunia, na yeye akajua dhambi zimewachafua si tu watu, bali hata na wanyama wao wa kufungwa, hivyo nao pia ni lazima watakaswe kwa toba na kwa kufunga, na utaona aliwavisha mpaka hao wanyama mavazi ya magunia!.
Ni vizuri kulijua hili ndugu, kuwa unapofunga fanya hivyo pia kwa wanyama wako (inaweza isiwe mara kwa mara lakini weka desturi hiyo)!!!
Unapofunga hebu pia funga pia na shamba lako, usinyeshee chochote siku hiyo, usiweke mboleo siku hiyo, wala usilipalilie, kama unafuga kuku, usiwalishe siku hiyo, usilishe ng’ombe wako siku hiyo, usilishe mbuzi zako siku hiyo, vile vile usifungue biashara yako siku hiyo, fanya hivyo kwa Imani na utaona matokeo makubwa sana baada ya hapo!.
Wengi hawaoni matokeo katika kazi zao kwasababu wanasahau kufunga biashara zao, badala yake wanafunga tu wao, pasipo kujua kuwa vifungo pia havipo tu katika mwili, bali pia katika biashara na mifugo, hivyo nayo pia inapaswa ifungishwe.
Bwana akubariki.
Maran atha
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.
HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.
NINI MAANA YA KUTUBU
Je tunaruhusiwa kutumia vidonge wakati wa kufunga?
Ninawi ni nchi gani kwasasa?
Rudi nyumbani
Print this post
JIBU: Ipo mitazamo mingi, ihusuyo eneo halisi la makaburi ya wazazi wetu wa kwanza, Kwamfano kwa mujibu wa hadithi za kiyahudi, wao wanaamini kuwa Adamu na Hawa walizikwa pale Israeli, mahali palipoitwa Hebroni katika pango lijulikano kama pango la Makpela. Ambalo baadaye Ibrahimu na Sara walikuja kulinunua likawa ni eneo la maziko yao ya kifamilia, (Mwanzo 49:29-31) kwa urefu wa habari hiyo fungua hapa usome >>> Pango la Makpela ni lipi,
Wengine, wanaamini kuwa pale Kristo aliposulubiwa Golgota, ndipo palipokuwa kaburi la Adamu, wakiamini kuwa kama Kristo alvyoitwa Adamu wa pili, maana yake ni alikuja kurudisha kile kitu ambacho Adamu wa kwanza alikipoteza, yaani uzima. Hivyo kama Adamu alileta kifo, Kristo alileta uzima kwa msalaba wake, na aliyafanya hayo juu ya kaburi la Adamu.
Lakini je! kuna usahihi kwa mitazamo hiyo.
Kwasababu biblia haijaeleza chochote, kuhusiana na kaburi la Adamu na Hawa, hii yote ni mitazamo, ambayo yaweza kuwa ukweli au uongo, tusiweke imani yetu moja kwa moja katika mitazamo. Kwasababu gharika ilipokuja ilivuruga ramani yote ya ulimwengu, isingekuwa rahisi kupatambua mahali sahihi alipozikwa Adamu, isipokuwa kwa ufunuo.
Na habari hiyo kutoandikwa ni kutuonyesha kuwa hakuna umuhimu sana kwa kujua Adamu alizikiwa wapi. Ushindi tulioupata kwa kifo cha Kristo, na kufufuka kwake, ni habari tosha tunayopaswa tuifakari usiku na mchana, zaidi ya kaburi la Adamu.
Lakini swali ni Je! Yesu amefufuka ndani yako? Fahamu kuwa Ikiwa bado hujazaliwa mara ya pili, kifo kina nguvu juu yako, ukifa hakuna maisha kwako, ni mateso katika moto wa jehanamu. Lakini ukizaliwa mara ya pili uzima wa milele unao na hata ukifa, utakuwa unaendelea kuishi.
Yohana 11:25 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi; 26 naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo?
Unasubiri nini? Usiokoke leo.
Saa ya wokovu ni sasa, ni pale tu unapotubu kwa kumaanisha kuacha dhambi, na kumwita Yesu ayatawale maisha yako, kisha kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu. Hapo unakuwa tayari umezaliwa mara ya pili. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo sasa, basi fungua hapa kwa mwongozo wa Sala hiyo ya toba.>>>KUONGOZWA SALA YA TOBA
Shalom.
KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?
Maziara ni nini? Je! Na Tunaruhusiwa kuyajenga kwenye makaburi yetu?
JINA LAKO NI LA NANI?
Kuhimidi ni nini?(Zaburi 31:21)
NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA
Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?
Rudi Nyumbani
Maelezo ya Mithali 28:20
“Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele; Lakini afanyaye haraka kuwa tajiri hakosi ataadhibiwa”.
Mstari huo unatufundisha jinsi pupa (kutaka vya haraka), inavyokinzana na neno “Uaminifu”. Ikiwa na maana mtu ambaye anataka wingi kwa muda mfupi, ni lazima tu atatumia njia isiyo ya haki, ili avipate anavyovitaka. Kwamfano viongozi wa nchi au waajiriwa wenye tamaa ya mafanikio ya haraka, wanaotaka mwezi huo huo wajenge, au wawe na miradi mikubwa, mwisho wa siku huwa wanatumia njia za wizi, ili kufikia mafanikio yao. Hiyo ndio sababu inayowafanya wapoteze uaminifu katika kile walichokabidhiwa.
Na hatma ya hawa watu, ni kukutana tu na matatizo, aidha kufungwa, au kufukuzwa kazi, au kutozwa faini, n.k.. na kuangukia hasara tu sio faida.
Ndio maana ya hili Neno
Mithali 28:20 Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele; Lakini afanyaye haraka kuwa tajiri hakosi ataadhibiwa.
Kwasababu mafanikio na pupa, havipatani kabisa. Bali achumaye kidogo-kidogo ndiye atakayefanikiwa(Mithali 13:11)
Yusufu alirekodiwa kuwa ni mwaminifu katika kazi yake. Na hivyo, akabarikiwa na Bwana mpaka akapewa nafasi ya uwaziri-mkuu wa taifa kubwa la Misri (Mwanzo 39:1-6). Danieli alirekodiwa kuwa muaminifu na hivyo akadumu katika falme zote mbili zilizotawala dunia wakati ule, yaani Babeli pamoja na Umedi na Uajemi (Danieli 6:4).
Lakini pia Neno hili linatafsirika rohoni.
Katika kazi ya Bwana, palipo na UAMINIFU, basi mwishowe Mungu huwa anabariki utumishi wa mtu huyo. Alisema maneno haya;
Luka 16:10 “Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia. 11 Basi, kama ninyi hamkuwa waaminifu katika mali ya udhalimu, ni nani atakayewapa amana mali ya kweli? 12 Na kama hamkuwa waaminifu katika mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewapa iliyo yenu wenyewe?
Umeona? Lakini ukikosa uaminifu, ndio utataka utumie njia zisizompendeza Mungu ili uone matokeo unayoyatarajia haraka, ndio hapo utaona mhubiri anatumia njia za undanganyifu kutengeneza shuhuda za uongo, ili watu wajue kuwa anao-upako wajae kwenye kanisa lake. Mambo kama haya hatma yake ni , uangamivu. Wengine, wanahubiri injili ya kisiasa, au vichekesho, wengine wanapachika staili za kidunia madhabahuni na kwenye kwaya, hawahubiri tena kweli, wala hawakemei dhambi, wakihofia watu kukimbia makanisa yao. Wanapoteza uaminifu ili wapate watu wengi kanisani. Hii ni hatari kubwa!
Hawajui kuwa ndani ya uaminifu, zipo Baraka. Na Mungu anaona, Mungu atamnyanyua tu mtu huyo.
Hivyo tupende kusimamia kweli, turidhike na nafasi zetu, tupinge mambo ya giza, TUWE WAAMINIFU katika yote na hakika tutaona Baraka za Bwana.
UAMINIFU NI KIGEZO KIKUBWA CHA KUTUMIWA NA MUNGU.
USIZISHIRIKI DHAMBI ZA WATU WENGINE.
Maana ya Mithali 9:17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu, Na mkate ulioliwa kwa siri hupendeza”
Vifungu vya biblia kuhusu Uongozi.
Nini maana ya Mithali 27:6 “Jeraha utiwazo na rafiki ni amini;
TABIA ZA NJIA YA MUNGU KWA MKRISTO
THAWABU YA UAMINIFU.
Katika biblia mtu ambaye alipokea taaarifa iliyofichwa kutoka Kwa Mungu na kuiwasilisha Kwa watu aliitwa mwonaji. Alipokea aidha kupitia, maono, ndoto, au kufunuliwa dhahiri, Mfano wa Hawa alikuwa ni Samweli…
1 Samweli 9:9-12
[9](Hapo zamani katika Israeli, mtu alipokwenda kuuliza neno kwa Mungu, husema hivi, Haya! Twende kwa mwonaji; maana mtu aitwaye sasa Nabii hapo zamani aliitwa Mwonaji.) [10]Basi Sauli akamwambia mtumishi wake, Umesema vema; haya! Twende. Wakaenda mpaka mji ule aliokuwamo mtu wa Mungu. [11]Hata walipokwea kwenda mjini, wakakutana na wasichana, wanatoka kwenda kuteka maji; wakawaambia, Je! Mwonaji yuko? [12]Nao wakawajibu, wakasema, Yuko; tazama, yuko huko mbele yako; fanyeni haraka sasa, maana hivi leo amekuja mjini; kwa sababu watu wana dhabihu leo katika mahali pa juu;
[9](Hapo zamani katika Israeli, mtu alipokwenda kuuliza neno kwa Mungu, husema hivi, Haya! Twende kwa mwonaji; maana mtu aitwaye sasa Nabii hapo zamani aliitwa Mwonaji.)
[10]Basi Sauli akamwambia mtumishi wake, Umesema vema; haya! Twende. Wakaenda mpaka mji ule aliokuwamo mtu wa Mungu.
[11]Hata walipokwea kwenda mjini, wakakutana na wasichana, wanatoka kwenda kuteka maji; wakawaambia, Je! Mwonaji yuko?
[12]Nao wakawajibu, wakasema, Yuko; tazama, yuko huko mbele yako; fanyeni haraka sasa, maana hivi leo amekuja mjini; kwa sababu watu wana dhabihu leo katika mahali pa juu;
Lakini baadaye watu Hawa walikuja pia kuitwa Manabii kama tunavyosoma kwenye vifungu hivyo
Isipokuwa Maana ya Nabii ni Pana zaidi sio tu kupokea taaarifa kutoka Kwa Mungu na kuiwasilisha Bali pia alisimama kufundisha na kuwarejesha watu, katika Sheria ya Mungu.ikiwemo kukaribia na kukemea, na kuonya. Mfano wa Hawa ni Isaya, Yeremia, Ezekieli, Yona, Hosea, Mika, Hagai, Malaki na wengine.
Hivyo nabii ni lazima pia awe mwonaji, kwamba apokee pia taaarifa za Moja Kwa Moja kutoka Kwa Mungu, na kufichua Siri zilizositirika lakini mwonaji haikuwa lazima afanye kazi ya kinabii, Bali ni kusema tu kile anachoelezwa, au kufichua Siri zilizojificha, au kuomba mwongozo wa Roho wa Mungu, Kwa ajili ya jambo/tatizo Fulani.
Hivyo kuhitimisha ni kwamba Kuna maandiko mengine yanawataja waonaji, lakini yalimaanisha pia ni manabii, na mengine yanabakia kumaanisha walewale tu waonaji.
Mfano wake ni Samweli, ambaye alikuwa ni mwonaji lakini pia ni Nabii.
1 Mambo ya Nyakati 29:29
[29]Basi habari za mfalme Daudi, mwanzo na mwisho, angalia, zimeandikwa katika tarehe ya Samweli, mwonaji, na katika tarehe ya Nathani, nabii, na katika tarehe ya Gadi, mwonaji;
Soma pia vifungu hivi, kufahamu zaidi.
(2Samweli 24:11, 2Nyakati 16:7, 29:30,)
Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
IELEWE SAUTI YA MUNGU.
TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.
NA TAA YA MUNGU ILIKUWA BADO HAIJAZIMIKA.
UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?
Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?
NA TAA YA MUNGU ILIKUWA BADO HAIJAZIMIKA
Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?
Maelezo ya Mithali 18:13 Yeye ajibuye kabla hajasikia, Ni upumbavu na aibu kwake.
Hekima inatufundisha tusiwe watu wa kujibu au kuzungumza kabla hatujasikia habari yote au taaarifa yote na kuitafakari kwanza..Kwamfano mwenzako anazungumza jambo Kisha wewe ukaingilia kati na kutaka kujibu, hoja ambayo haijakamilika..Matokeo yake hapo ni Nini kama sio kutoa majibu yasiyosahihi?. Au ambayo hayajakamilika?
Ndio hapo anasema ni upumbavu na aibu kwake.
Hii imeathiri hata kusambaa Kwa taaarifa za uongo. Mtu atasikia jambo, kwasababu Hana taaarifa nalo vizuri, atatoka muda huo huo na kwenda kumpasha mwingine, na yule mwingine atampasha mwingine..Hivyo taaarifa za uongo huzagaa Kwa upesi sana. Ndivyo ambavyo hata waandishi wa habari ambao hawawi makini wanavyosambaza habari ambazo bado hawajazifanyia uchambuzi yakinifu. Na matokeo yake husababisha matatizo makubwa katika jamii.
Mafarisayo na wayahudi walimpinga Yesu kwasababu walikuwa ni watu wa kupokea tu taaarifa ambazo hawazitafiti, walisikia Yesu anatokea Nazareti, wakahitimisha amezaliwa Nazareti, wengine wakamwita Msamaria. Lakini kama wangesubiri kutuatilia Kwa ukaribu mawazo Yao yangebadilika, na wasingekuwa wapumbavu kama tunavyowasoma kwenye biblia.
Hata wakati alipokuwa anazungumza nao, hawakutaka kusikiliza mpaka mwisho ni Nini Bwana anataka kuwaambia, kwamfano Kuna wakati aliwaambia, mtu akilishika Neno lake hataonja mauti milele. Lakini wao Hawakutaka ufafanuzi alimaanisha Nini.. hapo hapo wakarukia na kumwita ana Pepo;Kwa kauli Ile.
Yohana 8:52-53
[52]Basi Wayahudi wakamwambia, Sasa tumeng’amua ya kuwa una pepo. Ibrahimu amekufa, na manabii wamekufa; nawe wasema, Mtu akilishika neno langu, hataonja mauti milele. [53]Wewe u mkuu kuliko baba yetu Ibrahimu, ambaye amekufa? Nao manabii wamekufa. Wajifanya u nani?
[52]Basi Wayahudi wakamwambia, Sasa tumeng’amua ya kuwa una pepo. Ibrahimu amekufa, na manabii wamekufa; nawe wasema, Mtu akilishika neno langu, hataonja mauti milele.
[53]Wewe u mkuu kuliko baba yetu Ibrahimu, ambaye amekufa? Nao manabii wamekufa. Wajifanya u nani?
Wakati mwingine aliwaambia livunjeni hili hekalu,nami nitalisimamisha baada ya siku tatu. Wakairukia hiyo kauli bila kusubiria maelezo yake , ndio ikawa habari ya mji mzima Kuna mtu kasema anaweza kulijenga Kwa siku 3 hekalu lililojengwa Kwa miaka 46. Kumbe hawakujua Kristo anazungumzia habari ya mwili wake.(Yohana 2:20)
Biblia inatuasa tuwe wepesi wa kusikia, na si wa kusema; Ina faida nyingi.
Yakobo 1:19
[19]Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika;
HAUWEZI KURUKA MADARASA YA MUNGU!
KUOTA UPO UCHI.
FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.
FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.
Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?
Maana ya Mithali 19:15 ‘Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito;
Fahamu Maana ya;
Mithali 18:18 Kura hukomesha mashindano; Hukata maneno ya wakuu.
Kupiga kura ni Moja ya njia ambayo ilitumika kuleta suluhisho lenye utata, na wakati mwingine kuchagua viongozi/wamiliki. Pitia hapa ujue zaidi kuhusu kura zilivyopigwa zamani za biblia…>> Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo;
Na Mungu wakati mwingine aliingilia kati na kuleta majibu yake sahihi kwa kupitia njia hiyo. Kwamfano wakati ule Yona anamkimbia Mungu, Hali ilipochafuka kule baharini, utaona wale watu walipiga kura, ili kujua sababu ya mambo yale ni nani na Ile kura ikamwangukia Yona.
Mitume wa Bwana baada ya kuomba, kuhusu mrithi wa nafasi ya Yuda wakapiga kura katika ya wale wanafunzi wawili, nayo ikamwangukia Mathiya, na likawa kweli ni chaguo la Mungu.(Matendo 1:15-19),
Hata wakati wa nchi ya Israeli kugawanywa . Kura zilitumika kuamua nani akae wapi, na nani arithi wapi (Hesabu 26:55).
Hivyo kupiga kura ilikuwa ni mojawapo ya njia kuleta jibu lisilokuwa na upendeleo. Au lililoegemea upande Fulani mmoja. Na kwa kufanya hivyo malalamiko mengii yalikomeshwa kwasababu maamuzi hayakuamuliwa na upande wowote ule.
Ndio maana ya hili andiko
Mithali 18:18
[18]Kura hukomesha mashindano; Hukata maneno ya wakuu.
Hata kipindi Cha sasa njia ambayo hutumiwa kuchagua viongozi wengi ulimwenguni Huwa ni ya kura. Isipokuwa hii siyo ya kurusha SHILINGI, au kete angani inayomwangukia mmojawapo ndio anakuwa kiongozi..hapana Bali ni kuruhusu Kila mmoja kutia maoni yake..Kisha zinahesabiwa na yule mwenye nyingi hupewa. Na hivyo hakuna malalamiko.
Tofauti na Ile mtu atawadhwe tu Moja Kwa moja kuwa kiongozi, Hiyo huleta ukakasi mwingi.
Hivyo ni kutufundisha kua Bwana anaouwezo wa kuingilia kura zipigwazo na kuleta majibu yake sahihi..hususani pale anaposhirikwa Kwa maombi, na kama hakusema Kwa njia nyingine ya Moja Kwa moja.
Bwana akubariki
Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?
MKUU WA ANGA.
Mzushi ni nani kibiblia? (Tito 3:10).
Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?
Biblia inakataza kuapa kabisa, lakini kwanini watu wanaapa mahakamani na katika vifungo vya ndoa?
Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake
Nini maana ya Mithali 27:21 inaposema “mtu hujaribiwa kwa sifa zake?”
Hakuna namna utautenganisha “Moyo” na “hazina”.. vitu hivi vinaenda pamoja!.(ni sawa na miguu na mwili,..mahali miguu ilipo na mwili upo, miguu haiwezi kuwa mahali pengine na mwili mahali pengine) Vile vile Moyo wa mtu na hazina yake, vinaenda pamoja…Pale mtu alipojiwekea hazina, ni lazima (akili yake yote na fikra zake na hisia zake na mawazo yake yatakuwa huko).
Ndio maana mtu aliyejiwekea hazina kubwa ya mali za kidunia, halafu mali zile zikapotea zote ghafla, ni rahisi mtu huyo kuchanganyikiwa au kupoteza maisha maisha kabisa!.
Kwanini?..Kwasababu Moyo wake wote (fikra, mawazo, akili, malengo, uzima, hadhi) vilikuwepo katika mali zile, na sasa hana tena!, hata maisha kwake yanakuwa hayana maana tena!. Ndivyo ilivyo, kwamba Moyo siku zote unafuata hazina ilipo!, na unaishi kutokana na hazina mtu alizonazo. Ndivyo moyo wa mtu ulivyoumbwa!..
Vile vile mtu anayejiwekea hazina mbinguni, ni lazima fikra zake, mawazo yake, akili yake, malengo yake yote yatakuwa kule mbinguni hazina yake ilipo.
Sasa Bwana Yesu alitufundisha kanuni ya kuielekeza Mioyo yetu mbinguni, kwamba si kwa kuomba tu! Bali kwa kujiwekea hazina kule mbinguni,..kwanini?…kwasababu tutakapojiwekea hazina kule juu mbinguni basi mioyo yetu (yaani fikra, fahamu, akili, mawazo na hisia) zitaelekea kule Mbinguni, bila shuruti!.
Sasa swali, tunajiwekeaje hazina juu mbinguni?.. yeye mwenyewe (Bwana Yesu) alitufundisha kanuni katika Luka 18:18-22
Luka 18:18 “Tena, mtu mkubwa mmoja alimwuliza, akisema, Mwalimu mwema, nifanye nini ili nipate kuurithi uzima wa milele? 19 Yesu akamwambia, Mbona unaniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, naye ndiye Mungu. 20 Wazijua amri; Usizini, Usiue, Usiibe, Usishuhudie uongo, Waheshimu baba yako na mama yako. 21 Akasema, Hayo yote nimeyashika tangu utoto wangu 22 Yesu aliposikia hayo alimwambia, Umepungukiwa na neno moja bado; viuze ulivyo navyo vyote, ukawagawanyie maskini, NAWE UTAKUWA NA HAZINA MBINGUNI; kisha, njoo unifuate”.
Luka 18:18 “Tena, mtu mkubwa mmoja alimwuliza, akisema, Mwalimu mwema, nifanye nini ili nipate kuurithi uzima wa milele?
19 Yesu akamwambia, Mbona unaniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, naye ndiye Mungu.
20 Wazijua amri; Usizini, Usiue, Usiibe, Usishuhudie uongo, Waheshimu baba yako na mama yako.
21 Akasema, Hayo yote nimeyashika tangu utoto wangu
22 Yesu aliposikia hayo alimwambia, Umepungukiwa na neno moja bado; viuze ulivyo navyo vyote, ukawagawanyie maskini, NAWE UTAKUWA NA HAZINA MBINGUNI; kisha, njoo unifuate”.
Na tena anarudia maneno kama hayo hayo katika Luka 12:32-34…
Luka 12:32 “Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme. 33 Viuzeni mlivyo navyo, mtoe sadaka. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, AKIBA ISIYOPUNGUA katika mbingu, mahali pasipokaribia mwivi, wala nondo haharibu. 34 KWA KUWA HAZINA YENU ILIPO, NDIPO ITAKAPOKUWAPO NA MIOYO YENU”.
Luka 12:32 “Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme.
33 Viuzeni mlivyo navyo, mtoe sadaka. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, AKIBA ISIYOPUNGUA katika mbingu, mahali pasipokaribia mwivi, wala nondo haharibu.
34 KWA KUWA HAZINA YENU ILIPO, NDIPO ITAKAPOKUWAPO NA MIOYO YENU”.
Umeona?.. Kumbe kanuni ya kujiwekea hazina mbinguni ni kumtolea Mungu!..
Kwanini?.. Kwasababu tunapomtolea Mungu vile tulivyo navyo, mawazo yetu yatakuwa siku moja kwenda kupata thawabu mbinguni!, fikra zetu zitakuwa siku moja kwenda kuona miji mizuri tuliyoandwaliwa, mawazo yetu yatakuwa siku moja kwenda kuvikwa taji……hivyo muda wote tutakuwa tunafakari tu yaliyo ya juu na huko ndiko mioyo yetu itakapokuwepo!.
Ndio maana utaona watu wanaojitoa kwa Mungu kuanzia miili yao, mpaka mali zao, muda wote wanawaza unyakuo utakuwa lini?, muda wote wanawaza Kristo anakuja lini?.. ni kwanini wanakuwa hivyo?, si kwamba wanajilazimisha kuwa hivyo, ni kwamba tayari mioyo yao ipo mbinguni kwasababu wamejiwekea hazina huko.
Hii ni kanuni rahisi kabisa ya kuhamisha mioyo yetu kutoka kutafakari MAMBO YA CHINI na kuanza kutafakari MAMBO YA JUU!.
Ukitaka uwe mtu wa kutafakari mambo ya mbinguni sana, mtolee Mungu kuanzia muda wako, akili yako, mwili wako, ufahamu wako na hata vitu vyako!.. Hapo moyo wako wenyewe tu utaanza kuelekea mbinguni bila hata kutumia nguvu nyingi!,. Utajikuta tu unaanza kutamani kumwona Yesu, utajikuta unatamani ile siku ya mwisho ifike n.k
Laakini kinyume chake usipofanya hivyo na ukajitumainisha katika kujiwekea hazina katika mambo ya ulimwengu, basi fahamu kuwa moyo wako utaelekea tu katika mambo ya ulimwengu hata kama hupendi!.
Wakolosai 3:2 “Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi”.
Maran atha!
Hazina za gizani ni zipi? (Isaya 45:3).
YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.
Nondo ni nini kama tunavyosoma katika biblia?
UKIOKOKA, JIANDAE KUPITISHWA USIPOPATAZAMIA.
Yeshuruni ni nani katika biblia?
Swali: Biblia inatufundisha katika Wagalatia 5:23 kuwa “tuwe wapole kiasi”, sasa napenda kujua mtu utakuwaje mpole kiasi.
Jibu: Tusome,
Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, 23 UPOLE, KIASI; juu ya mambo kama hayo hakuna sharia”.
Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
23 UPOLE, KIASI; juu ya mambo kama hayo hakuna sharia”.
Hapa biblia haisemi kuwa tunda la Roho Mtakitifu kuwa ni “Upole kiasi” kana kwamba “upole unapaswa uwe na kiasi”…. La! Bali inasema tunda la Roho ni “Upole”, halafu “Kiasi”… hayo ni maneno mawili yaliyotengenishwa na alama ya mkato.
Maana yake “Upole” ni kitu kingine na “Kiasi” ni kitu kingine. Ikiwa na maana kuwa Tunda la Roho “Upole ulio wote” na sio upole kiasi.
Biblia inatufundisha tuwe watu wapole kama Hua (Njiwa).
Mathayo 10:16 “Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwa-mwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua”
Hua ni ndege mpole sana ndio maana Roho Mtakatifu alitumia umbile la Hua kushuka juu ya Bwana Yesu wakati ule alipobatizwa (Mathayo 3:16)... Na maandiko yanazidi kutufundisha kuwa Bwana Yesu ni Mpole..
Mathayo 21:5 “Mwambieni binti Sayuni Tazama, mfalme wako anakuja kwako, MPOLE, naye amepanda punda, Na mwana-punda, mtoto wa punda”.
Soma pia, Mathayo 11:29, utaona sifa hiyo ya Bwana ya upole ikitajwa..
Na sisi pia ni lazima tuwe na sifa hiyo ya “Upole” kama ishara mojawapo ya kuwa na Roho Mtakatifu ndani yetu… shetani kaligeuze Neno hili la Upole na kuweka “Upole kiasi” ili kuchochea ubaya ndani ya watu.. Kwamba ni vizuri kuwa wapole lakini tusiwe wapole sana, tuwe wapole tu kiasi!. Huo ni uongo wa adui!.
Na kumbuka kuna tofauti ya “upole” na “unyonge”. Biblia haitufundishi kuwa wanyonge, bali kuwa wapole, Mtu mpole ni yule ambaye ana uwezo wote wa kutumia ukali lakini hautumii!, kama alivyokuwa Bwana Yesu… Lakini mnyonge ni yule anayekuwa analazimika kuwa hivyo mpole kutokana tu na mazingira..na akitoka katika hayo mazingira basi tabia yake ya ubaya na ukali usio na maana na vurugu inajidhihirisha.
Bwana atusaidie .
Upole ni nini?
KIASI NI NINI KATIKA UKRISTO?
BWANA UNIJULISHE MWISHO WANGU.
Je Paulo na Petro walishindania nini? (Wagalatia 2:11).
Je ni kweli Musa alikuwa mtu mpole kuliko wote duniani?
Jibu: Tusome kuanzia mstari wa 5..
Zaburi 91:5 “Hutaogopa hofu ya usiku, Wala mshale urukao mchana, 6 Wala tauni ipitayo gizani, Wala uele uharibuo adhuhuri”.
Zaburi 91:5 “Hutaogopa hofu ya usiku, Wala mshale urukao mchana,
6 Wala tauni ipitayo gizani, Wala uele uharibuo adhuhuri”.
“Uele” ni janga linaloleta mauti linaloweza kumpata mtu.. ajali ya gari ni mfano wa Uele, Ajali ya kuzama kwenye maji ni mfano wa “Uele”, janga la kuungua moto mpaka kufa ni mfano wa “Uele”.
Maandiko yanatufundisha kuwa wote wamtumainio Bwana, na kumkimbilia na kumfanya kuwa ngome na msaada, hawatakuwa na hofu na majanga hayo, kwani Mungu ni ngome ya wote wanaomcha, naye ndiye awaokoaye na majanga.
Zaburi 121:4 “Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi, Yeye aliye mlinzi wa Israeli. 5 BWANA ndiye mlinzi wako; BWANA ni uvuli mkono wako wa kuume. 6 Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi wakati wa usiku. 7 BWANA atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako. 8 BWANA atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele”.
Zaburi 121:4 “Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi, Yeye aliye mlinzi wa Israeli.
5 BWANA ndiye mlinzi wako; BWANA ni uvuli mkono wako wa kuume.
6 Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi wakati wa usiku.
7 BWANA atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako.
8 BWANA atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele”.
Je una hofu na UELE?..Mpokee Yesu kwa kutubu dhambi na kujazwa Roho Mtakatifu, naye atakupa furaha nawe utaishi maisha ya raha na ya utulivu.
Zaburi 127:2 “……Yeye humpa mpenzi wake usingizi”
KUOTA AJALI, KUNAMAANISHA NINI?
Je! Mungu anasababisha ajali au Majanga?
MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.
Kaniki ni nini katika biblia? (Yeremia 8:21).
JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?
“Ganjo” ni mahali palipoharibika.. Jengo lililoharibika linaitwa “Ganjo” yakiwa mengi yanaitwa “maganjo”, mji ulioharibiwa aidha kwa vita au kwa janga fulani pia unaitwa “Ganjo”.
Katika biblia neno hili limeonekana mara kadhaa..
Walawi 26:30 “Nami nitapaharibu mahali penu palipoinuka, na kuziangusha sanamu zenu za jua, nami nitaitupa mizoga yenu juu ya mizoga ya sanamu zenu; na roho yangu itawachukia. 31 Nami nitaifanya MIJI YENU IWE MAGANJO, na mahali penu patakatifu nitapatia ukiwa; wala sitasikia harufu ya manukato yenu yapendezayo. 32 Nami nitaitia hiyo nchi ukiwa; na adui zenu watakaokaa huko wataistaajabia”
Walawi 26:30 “Nami nitapaharibu mahali penu palipoinuka, na kuziangusha sanamu zenu za jua, nami nitaitupa mizoga yenu juu ya mizoga ya sanamu zenu; na roho yangu itawachukia.
31 Nami nitaifanya MIJI YENU IWE MAGANJO, na mahali penu patakatifu nitapatia ukiwa; wala sitasikia harufu ya manukato yenu yapendezayo.
32 Nami nitaitia hiyo nchi ukiwa; na adui zenu watakaokaa huko wataistaajabia”
Tusome pia…
Ezekieli 29:12 “Nami nitaifanya nchi ya Misri kuwa ukiwa, kati ya nchi zilizo ukiwa, na miji yake, kati ya miji iliyoharibika, ITAKUWA MAGANJO muda wa miaka arobaini; nami nitawatawanya Wamisri kati ya mataifa, nami nitawatapanya kati ya nchi mbalimbali.”
Neno hili pia unaweza kulisoma katika mistari ifuatayo likiwa na maana hiyo hiyo..Walawi 26:33, 2Nyakati 34:6, Ayubu 3:14, Isaya 6:11, 7:19, Yeremia 4:7, Ezekieli 6:14, 36:38, na Amosi 9:14.
Vile vile hii dunia siku moja itafanyika kuwa “GANJO”, kutokana na dhambi!.. Bwana ataiharibu kwa moto kama alivyoiharibu nyakati za Nuhu, kwa maji.
2Petro 3:6 “kwa hayo dunia ile ya wakati ule iligharikishwa na maji, ikaangamia. 7 Lakini mbingu za sasa na nchi zimewekwa akiba kwa moto, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu”.
2Petro 3:6 “kwa hayo dunia ile ya wakati ule iligharikishwa na maji, ikaangamia.
7 Lakini mbingu za sasa na nchi zimewekwa akiba kwa moto, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu”.
Je umeokoka? Kama bado, saa ya wokovu ni sasa, tupo mwisho wa nyakati.
Maran atha.
Agano ni nini? na kuna aina ngapi za maagano?
Miji ya Tiro na Sidoni ni miji gani kwasasa?
Kama Malkia Esta alijipamba je! Kuna ubaya gani wanawake wa wakikristo wa leo kujipamba?.
TAA YA MWILI NI JICHO,
VICHEKESHO NA UTANI MADHABAHUNI