Title 2023

Mabibi wastahiki walikuwa ni watu gani? (Esta 1:18).

(Mada maalumu kwa wanawake)

Jibu: Mabibi Wastahiki ni “wanawake wa heshima”.. kundi hili la wanawake lilihusisha wake za Wafalme, Maliwali au Maakida au Majumbe..

Wakati mfalme Ahasuero alipowafanyia maakida wake na maliwali wake karamu, biblia inatuambia kuwa Malkia Vashti (mke wa mfalme), yeye naye aliwafanyia wanawake (ambao ni wake wa hao maakida na maliwali) karamu.

Esta 1:2 “siku zile mfalme Ahasuero alipoketi katika kiti cha enzi cha ufalme wake, huko Shushani ngomeni;

3 mwaka wa tatu wa kumiliki kwake, ikawa aliwafanyia karamu maakida wake wote na majumbe wake; wakuu wa Uajemi na Umedi, watu wenye cheo na maakida wa majimbo, wakihudhuria mbele zake. 

4 Akawaonyesha utajiri wa ufalme wake mtukufu, na heshima ya enzi yake bora siku nyingi, maana siku mia na themanini……………………..

9 Tena Vashti, malkia, naye akawafanyia karamu WANAWAKE NDANI YA NYUMBA YA KIFALME YA MFALME Ahasuero”.

Sasa hao wanawake waliokuwa wake za “maliwali na maakida” ndio waliojulikana kama “mabibi wastahiki”.. wakiongozwa na Malkia Vashti.

Lakini tunachoweza kujifunza ni kuwa ile karamu ya hawa wanawake haikuwa na utukufu wowote, kwani iliishia kuleta aibu kubwa katika ufalme wote wa Uajemi. Kwani Malkia Vashti alikosa utii kwa Mfalme alipoitwa, na Zaidi sana alionyesha dharau hizo mbele ya Mfalme na waliwali wake wote.

Na huenda pia kiburi hicho kilichochewa na jopo la wale wanawake wengine wastahiki waliohudhuria karamu hiyo ya Malkia Vashti. Hiyo ikifunua kuwa hakuna cha maana walichokuwa wanakizungumza au kukipanga katika hiyo karamu Vashti aliyowaandalia, huenda yaliyokuwa yanazungumziwa kule ni UMBEA TU na kusema mapungufu ya waume zao!

Hiyo ikamfanya Vashti apoteze umalkia wake, na hata hao wanawake wengine ambao wastahiki kuzidi kutawaliwa na waume zao.

Esta 1:16 “Basi Memukani akajibu mbele ya mfalme na maakida, Huyu Vashti, malkia, hakumkosa mfalme tu peke yake, ila na maakida wote, na watu wote pia walioko katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero. 

17 Kwa maana tendo hilo la malkia litajulikana na wanawake wote, hata waume zao watadharauliwa machoni pao, itakaponenwa ya kuwa mfalme Ahasuero aliamuru Vashti, malkia, aletwe mbele yake, bali hakuja. 

18 Hata na leo hivi mabibi wastahiki wa Uajemi na Umedi waliokwisha kuzisikia habari za tendo lake malkia watawaambia vivi hivi maakida wote wa mfalme. Hivyo kutatokea dharau nyingi na ghadhabu tele.

 19 Basi mfalme akiona vema, na itoke kwake amri ya kifalme, nayo iandikwe katika sheria za Waajemi na Wamedi isitanguke, ya kwamba Vashti asifike tena mbele ya mfalme Ahasuero; na umalkia wake mfalme ampe mwingine aliye mwema kuliko yeye.

 20 Basi mbiu ya mfalme atakayoipiga itakapotangazwa katika ufalme wake wote, nao ni mkubwa, wake wote watawaheshimu waume zao, wakubwa kwa wadogo.

 21 Basi neno hili likawapendeza mfalme na maakida; naye mfalme akafanya sawasawa na neno lake Memukani.

 22 Kwa maana alipeleka nyaraka katika majimbo yote ya mfalme, kila jimbo kwa mwandiko wake, na kila taifa kwa lugha yake, ya kwamba kila mwanamume atawale nyumbani mwake, na kuitangaza habari hii kwa lugha ya watu wake”.

Tabia kama hii inaendelea mpaka leo kwa baadhi ya wanawake walioolewa!, ambao baada ya kuolewa wanawaona waume zao kama si kitu tena, na hata kupoteza UTII kwao!. Pasipo kujua kuwa kwa kufanya hivyo wanazidi kujipotezea nafasi zao ndani ya familia zao, kwani badala ya kuwa kichwa Mungu anawaweka kuwa wa mwisho.

Neno la Mungu linasema wanawake na wawatii waume zao.

1Petro 3:1 “Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;

2  wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu.

3  Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;

4  bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.

5  Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, NA KUWATII WAUME ZAO”

Soma tena Waefeso 5:24 na Tito 2:5 utaona jambo hilo hilo, sasa mwana-mama unatolea wapi kiburi!!!. Badilika, na anza kuwa mtii, ikiwa haupo ndani yako, na hiyo ni kwa faida yako na familia yako. Kitabu cha Esta, huenda kingepaswa kiitwe kitabu cha Vashti, lakini kwa kiburi chake, umalkia wake akapewa Esta.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

ESTA: Mlango wa 5, 6 & 7

LITANIA YA BIKIRA MARIA JE! NI SALA YA KIMAANDIKO?

YESU ANAKWENDA KUIBADILISHA OFISI YAKE.

NI KIJIJI CHA AINA GANI UPO?

MAJESHI YA PEPO WABAYA.

Rudi nyumbani

Print this post

Kipuli ni nini, na kimebeba ujumbe gani?.(Mithali 25:12).

Jibu: Turejee,

Mithali 25:12 “KIPULI CHA DHAHABU, na pambo la dhahabu safi; Ndivyo alivyo mwonyaji mwenye hekima kwa sikio lisikialo”

“Kipuli” ni jina lingine la “hereni za masikioni”.

Neno hili limeonekana mara moja tu katika biblia, katika kitabu cha Mithali 25:12.

Na mwandishi wa Mithali (Sulemani) kwa hekima ya roho alipata kuelewa vipuli (hereni) sahihi wanazopaswa wavae watu, tofauti na hizi tuzijuazo.

Anasema… “KIPULI CHA DHAHABU, na pambo la dhahabu safi; Ndivyo alivyo MWONYAJI MWENYE HEKIMA KWA SIKIO LISIKIALO”.

Maana yake ni kuwa sikio linalosikia hekima kutoka kwa wenye hekima, linafananishwa na sikio lililovishwa hereni ya dhahabu au pambo la dhahabu.

Kwa lugha nyingine ni kwamba, kama tukitaka kupamba masikio yetu kwa vitu vya thamani, basi tuwe wasikilizaji wa maneno ya hekima. (Kwani maneno hayo yataonekana kama mapambo ya thamani katika masikio yetu).

Na maneno ya hekima hatuyapati pengine isipokuwa katika biblia takatifu (Humo ndimo tutakapopata lulu na mapamba ya thamani ya masikio yetu)..

Mithali 2:1 “Mwanangu, kama ukiyakubali maneno yangu, Na kuyaweka akiba maagizo yangu;

2 HATA UKATEGA SIKIO LAKO KUSIKIA HEKIMA, UKAUELEKEZA MOYO WAKO UPATE KUFAHAMU;

3 Naam, ukiita busara, Na kupaza sauti yako upate ufahamu;

4 Ukiutafuta kama fedha, Na kuutafutia kama hazina iliyositirika;

5 Ndipo utakapofahamu kumcha Bwana, Na kupata kumjua Mungu”

Soma tena  Mithali 4:20, Mithali 5:1, na  Mithali 22:17 utaona maneno yanayopatana na hayo..

Mithali hizi zinalingana kabisa na ujumbe wa Roho Mtakatifu tunaousoma katika kitabu cha 1Petro 3:3. Na 1 Timotheo 2:9.

1 Petro 3:3 “Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;

4 BALI KUWE UTU WA MOYONI USIOONEKANA, KATIKA MAPAMBO YASIYOHARIBIKA; YAANI, ROHO YA UPOLE NA UTULIVU, ILIYO YA THAMANI KUU MBELE ZA MUNGU.

5 Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao.

6 Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote”.

Mstari wa 4 unasema… “ BALI KUWE UTU WA MOYONI USIOONEKANA, KATIKA MAPAMBO YASIYOHARIBIKA; YAANI, ROHO YA UPOLE NA UTULIVU, ILIYO YA THAMANI KUU MBELE ZA MUNGU”.

Je ni vipuli gani vipo masikioni mwako?…vya chuma au vya maneno ya hekima?.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Rudi nyumbani

Print this post

WALAWI WALIKUWA WENYE MIOYO YA ADILI KWA KUJITAKASA KULIKO MAKUHANI.

2Nyakati 29:34 Lakini makuhani walikuwa wachache, wasiweze kuchuna sadaka zote za kuteketezwa; basi ndugu zao Walawi wakawasaidia, hata ilipokwisha kazi, na hata makuhani walipojitakasa; kwa kuwa Walawi walikuwa wenye mioyo ya adili kwa kujitakasa kuliko makuhani.

Nakusalimu katika jina la Bwana Yesu.

Fundisho hili linawahusu sana sana viongozi wa kiroho / Watumishi wa Mungu wanaohudumia kundi la Mungu. Mfano wachungaji au maaskofu.

Kuna wakati wale walioteuliwa kuwa viongozi wa juu kabisa wanaweza wasiwajibike ipasavyo katika nafasi zao, je! Wewe kama mwangalizi wao ufanye nini?

Mfano tukirejea habari hiyo tunaona Mfalme Hezekia alipokusudia kulitakasa hekalu la Mungu, ambalo lilikuwa limefungwa na kusahauliwa, na baba yake.

Alitafuta makuhani wa kuhudumu upya katika nyumba ya Mungu. Ikumbukwe kuwa makuhani tu ndio walioruhusiwa kufanya shughuli zote za madhahabuni, ikiwemo kuvukiza uvumba na kuandaa zile sadaka zilizoletwa mbele ya nyumba ya Bwana.

Lakini hapo biblia inatuambia, Makuhani walikuwa wachache!. Utajiuliza ni kwanini? Sio kwamba hawakuwepo kabisa, walikuwepo, lakini biblia inatuambia waliokuwa na mioyo ya adili ya kuipenda kazi ya Mungu ndio walikuwa wachache.

Pengine, wengine walikuwa na udhuru zao, wakiona kuahirisha shughuli zao, na kwenda kuhudumu madhabahuni  ni kuvugiwa ratiba ni kazi ya kuchosha, haina faida, wengine hawakuwa tayari kujitakasa, kwa kuacha mambo mabovu yasiyowapasa makuhani, wengine wakawa wazito, wanavutwa vutwa sana, kazi ambayo inapaswa ifanyike haraka n.k..

Hivyo hiyo ikapelekea kundi la viongozi wa juu kabisa likawa chache sana. Na kimsingi ni lazima wawepo wahudumu wa kutosha katika kazi hiyo ya madhabahuni. Sasa wafanyaje. Ndipo hapo utaona Walawi ambao kazi zao ni za nje, ya hema kama vile usimamizi wa malango, kulinda hekalu, na kuimba. Ikabidi sasa waingizwe ndani kwa ajili ya kusaidia kazi za kikuhani.

Na sababu ya kufanya hivyo biblia inasema, wenyewe walikuwa ni “wenye mioyo ya adili kwa kujitakasa kuliko makuhani”.

Walikuwa na moyo wa kumtumikia Mungu zaidi hata ya wale wanaostahili. Hivyo wakapewa kazi za juu zisizowastahili na wakafanya vizuri na Mungu akawabariki, ijapokuwa ilikuwa ni kinyume na taratibu.

Hata sasa katika kanisa, ni rahisi kuona wenye ngazi za chini, ni wepesi na wenye mioyo ya uaminifu katika nyumba ya Bwana kuliko wale viongozi wa juu. Utaona ni kiongozi wa wakina mama, lakini kwenye maombi haudhurii, kuwafuatilia wanawake wenzake haangahiki. Lakini hapo hapo utaona kabinti kadogo, kanajibidiisha, haachi maombi yapite, anawapigia simu yeye kuwakumbusha kana kwamba ndio kiongozi mkuu, anatoa taarifa za maboresho na changamoto kwa kiongozi wake, mambo  ambayo hata huyo kiongozi hajui.

Sasa katika mazingira kama haya? Unadhani kiongozi ni nani? …Uongozi sio cheo, uongozi ni MOYO, uaminifu na kujitoa. Ikiwa wewe ni mwangalizi, hakikisha huyu aliye na MOYO ndio unampa wajibu na majukumu yote ya uongozi katika nafasi hiyo. Hata kama hajawekewa mikono, au hana uzoefu wowote, au hajatambulika rasmi.

Huyo huyo ndiye Mungu aliyemchagua, hao wengine ni makapi.

Kwani Bwana Yesu alishatangulia kusema maneno haya.

Mathayo 19:30  “Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza”.

Sio kwamba Mungu anao upendeleo.. Lakini alisema.. “ walioalikwa hawakustahili”(Mathayo 22:8).

Halidhalika hata katika ngazi nyingine zote, ikiwa mchungaji msaidizi haipendi kazi yake, usione vibaya, kumpa kazi hiyo shemasi mwenye MOYO wa kuwahudumia watu. Mungu atamtengeneza mwenyewe. Lakini ikiwa wewe ni kiongozi-mlegevu, tubu geuka, ipende nafasi yako, hudumu hapo kwa uaminifu kwasababu umepewa dhamana ambayo utakuja kuitolea hesabu yake siku ile ya hukumu.

Bwana awe nawe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Uadilifu ni nini kibiblia?

Kwa namna gani tumefanyika Makuhani na Ufalme?.(Ufunuo 1:6)

Kwanini Yesu aliwaambia wale wakoma wakajionyeshe kwa makuhani?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji zilikuwaje?

Rudi nyumbani

Print this post

Kwa namna gani tumefanyika Makuhani na Ufalme?.(Ufunuo 1:6)

Swali: Biblia inasema katika Ufunuo 1:6 kuwa kupitia Bwana Yesu tumefanyika kuwa ufalme na makuhani, je tumefanyikaje kuwa hivyo?

Jibu: Awali ya yote tusome maandiko yafuatayo,

1 Yohana 4:17 “Katika hili pendo limekamilishwa kwetu, ili tuwe na ujasiri katika siku ya hukumu; kwa kuwa, KAMA YEYE ALIVYO, NDIVYO TULIVYO NA SISI ULIMWENGUNI HUMU”.

Hapo anasema “kama yeye alivyo ndivyo na sisi tulivyo”. Ikiwa na maana kuwa katika roho sisi tunafanana na Kristo kwa kila kitu.

Maana yake kama Kristo ni mwana wa Mungu basi na sisi ni wana wa Mungu sawasawa na Warumi 8:16.

Warumi 8:16 “Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu”.

Vile vile kama Kristo alikufa na kufufuka na kuketi katika kiti cha enzi, vile vile na sisi katika roho tulikufa pamoja naye kwa njia ya ubatizo (sawasawa na Warumi 6:4 na Warumi 6:8) kwa njia ya ubatizo

Warumi 6:4 “Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima”.

Na vile vile kama Kristo alifufuka na sisi pia tulifufuka  pamoja naye na sasa tumeketi pamoja naye katika ulimwengu wa roho.

Waefeso 2:6 “Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu”.

Kwahiyo kwa ufupi ni kwamba watu waliookoka kikamilifu wanafanana na Kristo kwa kila kitu, na hii ndio sababu kwanini shetani pamoja na mapepo yake yanawaogopa watu wa YESU KRISTO, ni kwasababu yanamwona Yesu Kristo ndani yao.

Sasa nafasi nyingine ya YESU iliyo kuu ni nafasi ya “ukuhani” na tena si kuhani tu, bali “KUHANI MKUU”.

Waebrania 8:1 “Basi, katika hayo tunayosema, neno lililo kuu ndilo hili: Tunaye kuhani mkuu wa namna hii, aliyeketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Ukuu mbinguni”.

Na kama Kristo alivyokuwa Kuhani, vile vile na sisi ni makuhani.

Na kumbuka kazi ya Makuhani ilikuwa ni kuwapatanisha watu na Mungu wao kwa njia ya SADAKA NA MAOMBI NA MAFUNDISHO.

Mfano Samweli, alifanya kazi ya kuwapatanisha Israeli kupitia sadaka zao , vilevile na kuwaombea na kuwafundisha njia iliyo sahihi..

1 Samweli 12:23 “Walakini mimi, hasha! Nisimtende BWANA dhambi kwa kuacha kuwaombea ninyi; lakini nitawaelimisha katika njia iliyo njema, na kunyoka”

Na Kristo ni hivyo kama Kuhani amesimama kutupatanisha na baba kwa njia ya kutuombea..

1 Yohana 2:1 “Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki”.

Soma pia Warumi 8:34, utaona jambo hilo hilo.

Na pia Yesu anatupatanisha kwa Baba kwa njia ya sadaka ya mwili  wake alioutoa kwaajili yetu.

Na sisi pia kwakuwa tunafanana na yeye katika roho sawasawa na hiyo 1 Yohana 4:1, basi na sisi ni makuhani kama yeye na tunaweza kuzifanya kazi zile zile anazozifanya yeye sasa za kikuhani.

Na kazi hizo ni kuwapatanisha watu na Baba kwa njia ya MAOMBI, MAFUNDISHO NA SADAKA. Hivyo tumepewa na sisi huduma ya upatanisho kama aliyonayo Bwana wetu YESU KRISTO.

Utauliza tunalithibitisha vipi hilo kibiblia?…Tusome maandiko yafuatayo..

2 Wakorintho 5:18 “Lakini vyote pia vyatokana na Mungu, aliyetupatanisha sisi na nafsi yake kwa Kristo, naye ALITUPA HUDUMA YA UPATANISHO;

19 yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; NAYE AMETIA NDANI YETU NENO LA UPATANISHO”

Ndio maana tunaweza kuombeana na Mungu akasikia (Yakobo 5:16) kwasababu na sisi ni makuhanimkama yeye, Vile vile kwa kujitoa miili yetu na vitu vyetu kama sadaka tunaweza kujipatanisha na kuwapatanishe wengine na Mungu.

Na hiyo yote ni kwasababu Kristo ametufanya na sisi kuwa makuhani kama yeye sawasawa na Ufunuo 1:6.

Tofauti ya Kristo na sisi ni kwamba Kristo yeye ni KUHANI MKUU, na sisi tunabaki kuwa makuhani, (yeye ni mkuu wa makuhani, utukufu na heshima zinabaki kwake, Bwana wa mabwana, mwamba imara!!!).

Na ni kwa namna gani sisi ni UFALME?.

Ni kwa namna ile jinsi Kristo alivyo…Yeye ni Mfalme, na tena si mfalme tu, bali Mfalme wa wafalme.

Ufunuo 19:16 “Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA”

Na kama yeye ni Mfalme wa wafalme, maana yake anao wafalme anaowatawala ambao nao pia ni wafalmena hao si wengine zaidi ya wale wanaomwamini..  (Kwamaana hawezi kuitwa mfalme wa wafalme kama hana wafalme chini yake anaowatawala).

Na utukufu wa ufalme tulionao sasa utakuja kudhuhirika zaidi katika ule utawala wa amani wa miaka 1000 wa YESU KRISTO.

Ufunuo 20:6 “Huo ndio ufufuo wa kwanza. Heri, na mtakatifu, ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hao mauti ya pili haina nguvu; BALI WATAKUWA MAKUHANI WA MUNGU NA WA KRISTO, NAO WATATAWALA PAMOJA NAYE HIYO MIAKA ELFU”

Je umeziona faida za kuwa ndani ya Kristo?.. Tunakuwa makuhani na tena wafalme…

Je! Tayari Umemwamini yeye?.

Kama bado unasubiri nini?..kumbuka tunaishi majira ya kurudi kwa Yesu mara ya pili.

Bwana akubariki.

Shalom..

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Rudi nyumbani

Print this post

Uadilifu ni nini kibiblia?

Uadilifu ni neno pana linalomaanisha, nidhamu, utu, auminifu, yaani kutenda kile ambacho jamii husika inataka wewe ukitende.

Kibiblia uadilifu ni utiifu katika sheria ya Mungu. Vilevile uaminifu na nidhamu katika mambo yote ya ki-Mungu.  Mtu wa namna hiyo anaitwa mwadilifu, au mcha Mungu.

Kwamfano watu ambao walikuwa waadilifu katika biblia ni kama Yusufu, Ayubu, Danieli pamoja na wengine, ambao waliweza kutembea katika sheria za Mungu bila lawama yoyote.

Baadhi ya vifungu ambavyo utakutana na Neno hilo ni hivi;

2Nyakati 26:3 Uzia alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala; akatawala huko Yerusalemu miaka hamsini na miwili; na jina la mamaye aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.  4 Akafanya yaliyo ya adili machoni pa Bwana, sawasawa na yote aliyoyafanya Amazia babaye

Zaburi 64: 10 “Mwenye haki atamfurahia Bwana na kumkimbilia, Na wote wenye moyo wa adili watajisifu”

Zaburi 112: 2 Wazao wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa.  3 Nyumbani mwake mna utajiri na mali, Na haki yake yakaa milele.  4 Nuru huwazukia wenye adili gizani; Ana fadhili na huruma na haki

Soma pia 2Nyakati 27:2,29:2 Zaburi 140:13.

Lakini cha kujua kuhusu tabia hii, ni kwamba Bwana Yesu alisema ni wajibu pia wa kila kiongozi wa kiroho/ Mhubiri kufundisha mafundisho ya adili, zaidi ya mafundisho ya utoaji.

Luka 11:42  Lakini, ole wenu, Mafarisayo, kwa kuwa mwatoa zaka za mnanaa na mchicha na kila mboga, na huku mwaacha mambo ya adili, na upendo wa Mungu; iliwapasa kuyafanya hayo ya kwanza, bila kuyaacha hayo ya pili.

Mafundisho ya adili, ni kama vile, utakatifu, auminifu, haki, utu wema, amani, umoja na kiasi, uvumilivu, fadhili, upole, unyenyekevu. na yote yanayofanana na hayo. Kwasababu ndicho Bwana anataka kukiona ndani ya mioyo ya watu wake, wawe waadilifu kama yeye alivyo mwadilifu (Zaburi 25:8).

Je! Wewe ni mwadilifu? Kumbuka huwezi kuwa hivyo kama upo nje ya Kristo. Yeye ndio pekee anayeweza kukupa nguvu ya kutenda mema. Hivyo ili uitwe mwadilifu sharti kwanza umpokee Yesu akuokoe, akusamehe dhambi zako. Ndipo Bwana akupe nguvu ya kumcha yeye.

Ikiwa upo tayari leo kuokoka, basi fungua hapa kwa mwongozo wa Sala ya Toba. >> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

IMANI YENYE MATENDO;

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

JE KUHUDUMU KWA NYIMBO ZA INJILI KUKOJE?

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

Ebenezeri/ Ebeneza maana yake ni nini?

Maana ya Neno Ebenezeri ni jiwe la msaada.

Wakati ule Israeli wanamlilia Bwana awarudie, Wafilisti walipata taarifa wakakusanyika pamoja ili wawaangamize, Israeli walivyoona hivyo wakaogopa sana, wakamsihi Samweli awalilie kwa Bwana ili wasaidiwe kwasababu wanakwenda kuangamia. Na Mungu akasikia kilio chao, akawatetea, kwa kutoa ngurumo kubwa sana, zilizowadhoofisha wafilisti, hivyo wakapigwa na kuharibiwa, mpaka miji ambayo wafilisti walikuwa wameiteka ikarudishwa yote kwa Israeli. Ndipo Samweli akachukua jiwe kubwa akalisimamisha Kati ya Mispa na Sheni, akaliita Ebenezeri, akasema hata sasa Bwana ametusaidia.

1Samweli 7:12 Ndipo Samweli akatwaa jiwe, na kulisimamisha kati ya Mispa na Sheni, akaliita jina lake Eben-ezeri, akisema, Hata sasa Bwana ametusaidia.

Lakini la kujiuliza kwanini Samweli anyanyue jiwe, na sio kitu kingine labda nguzo au bendera? Na pia alikuwa na maana gani kusema “Hata sasa Bwana ametusaidia”? Na sio maneno mengine?

JIBU: Alinyanyua jiwe kwasababu alipata ufunuo wa aliyemsaidia, na huyo si mwingine zaidi ya  Kristo ambaye ndio jiwe letu (Warumi 9:33). Alitambua ni yeye ndiye aliyewapigania vita kwa kunguruma, Kwasababu ndiye simba wa Yuda.

Lakini pia kwanini aseme “Hata sasa Bwana ametusaidia” ni kwasababu alitambua kuwa Mungu ni msaada wao sikuzote, hadi ule wakati walioufikia bado alikuwa ni msaada wao, ndio maana akasema “Hata sasa Bwana ametusaidia”, yaani sio tu jana, au zamani bali hata sasa Bwana yupo pamoja nasi.

Ikiwa na maana kuwa hata na sisi tukiwa ndani ya Kristo wakati wote atatulinda,  sio jana tu peke yake, hadi leo na hata kesho. Ni furaha iliyoje kuwekwa chini ya huu mwamba Yesu Kristo?

Je! Kristo ni jiwe lako? Je! Ni Ebenezeri wako? Kama sio, embu mkaribishe leo maishani mwako akuokoe, upate uzima wa milele. Akulinde mbali na Yule mwovu. Ikiwa upo tayari kutubu na kumpokea Yesu basi fungua hapa kwa msaada wa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

CHAGUA NI JIWE LIPI LITAKALO KUFAA KWA UJENZI.

BASI, IWENI NA HURUMA, KAMA BABA YENU ALIVYO NA HURUMA

LIONDOE JIWE.

Usimwache rafiki yako mwenyewe, wala rafiki ya baba yako.

Rudi nyumbani

Print this post

Mganda ni nini kama itumikavyo katika biblia?

Neno hili utalisoma katika vifungu kadha wa kadha,

Hivi ni baadhi ya vifungu hivyo ambavyo utakutana nalo;

Mwanzo 37:6 “akawaambia, Tafadhalini, sikieni ndoto hii niliyoiota.  7 Tazama, sisi tulikuwa tukifunga miganda shambani, kumbe! Mganda wangu ukaondoka ukasimama, na tazama, miganda yenu ikazunguka ikainama mbele ya mganda wangu.  8 Ndugu zake wakamwambia, Je! Kweli wewe utatumiliki sisi? Nawe utatutawala sisi? Wakazidi kumchukia kwa ajili ya ndoto yake, na kwa maneno yake”.

Walawi 23: 10 Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Hapo mtakapokuwa mmekwisha ingia hiyo nchi niwapayo, na kuyavuna mavuno yake, ndipo mtakapomletea kuhani mganda wa malimbuko ya mavuno yenu;  11 naye atautikisa mganda mbele za Bwana ili kwamba ukubaliwe kwa ajili yenu; siku ya pili baada ya Sabato kuhani atautikisa.  12 Na siku hiyo mtakayoutikisa mganda, mtamsongeza mwana-kondoo wa kiume mkamilifu wa mwaka wa kwanza awe sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana.

Tafsiri ya Neno mganda, ni matita ya mazao yoyote yaliyovunwa ambayo yamefungwa pamoja. Kwamfano ngano zilipovunwa, katika mashamba, zilifungwa kwanza katika matita matita, baadaye zikakusanywa zote pamoja, ndipo zikaenda kukobolewa na kusagwa. Sasa hayo matita matita ndio huitwa miganda. (Tazama picha juu)

Kwamfano katika vifungu vifuatavyo utaelewa biblia ilimaanisha nini;

Kumbukumbu 24: 19 Uvunapo mavuno yako katika shamba lako, ukasahau mganda shambani, usirudi kuuchukua; na uwe wa mgeni, au yatima, au mjane; ili Bwana, Mungu wako, akubariki katika kazi yote ya mikono yako.

Maana yake ni kuwa ikitokea, umeenda shambani kuvuna, ukafanikiwa kukusanya miganda kumi, sasa wakati unaondoka ukasahau mmoja, Ilikatazwa kurudi nyuma na kuuchukua, bali uuache kwa ajili ya mayatima na wageni. Kwasababu maskini waliruhusiwa kuingia kwenye mashamba kuokota vile vinavyosalia.

Hii inatufundisha nini?

Wakati mwingine Mungu ataruhusu usichukue kila kitu ulichonacho/ au ulichokikusanya, ikawa umesahau  fahamu kuwa ni Mungu ametaka, ili wengine wafaidike, usipende kukomba kila kitu, wakati mwingine utajiepusha na Baraka zako. Ukisafiri usiondoke na kabati lote la nguo, ulikuwa unakwenda mahali Fulani umebeba vingi, na kwa bahati mbaya ukakisahau kimoja, usiwe mwepesi kukirudia  kukichukua, hujui ni kwanini Mungu amekusahaulisha.

Wewe ni boss, umeona, vichenji vimebaki, si lazima uvikombe vyote, waachie waajiriwa wako. Itakuwa ni Baraka kwako.

Lakini pia ni kutuelekeza mioyo yetu imtegemee yeye zaidi ya miganda yetu. Utakumbuka mitume wa Kristo, walipofanyiwa miujiza ya mikate, wakaagizwa wakusanye vipande, kisipotee hata kimoja, lakini baadaye walipoondoka, wakakumbuka wamesahau,wakaanza kulalamikiana wao kwa wao watakula nini. Lakini Yesu akawaambia mmesahau miujiza Mungu aliyowafanyia kama hiyo? Mna wasiwasi gani? Mungu anaweza kuwapa na vingine.

Mathayo 16:5  Nao wanafunzi wakaenda hata ng’ambo, wakasahau kuchukua mikate. 6  Yesu akawaambia, Angalieni, jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo. 7  Wakabishana wao kwa wao, wakisema, Ni kwa sababu hatukuchukua mikate. 8  Naye Yesu akafahamu, akawaambia, Mbona mnabishana ninyi kwa ninyi, enyi wa imani chache, kwa sababu hamna mikate? 9  Hamjafahamu bado, wala hamkumbuki ile mikate mitano kwa wale elfu tano, na vikapu vingapi mlivyoviokota?

Hivyo na sisi pia tusiwe na tabia ya kubeba miganda yote.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Mofa ni nini? na inafunua nini kiroho?(1Samweli 28:24).

Mashonde ni nini? (Ezekieli 4:15).

YEYE ATAWABATIZA KWA ROHO MTAKATIFU NA KWA MOTO.

TUYATENDE MAMBO YOTE KWA UZURI NA UTARATIBU.

VIACHENI VYOTE VIKUE HATA WAKATI WA MAVUNO.

Rudi nyumbani

Print this post

Mashonde ni nini? (Ezekieli 4:15).

Swali: Mashonde ni kitu gani kama tunavyosoma katika Ezekieli 4:15, na yamebeba ufunuo gani?

Jibu: Turejee..

Ezekieli 4:12“Nawe utakila kama mkate wa shayiri, nawe utakioka mbele ya macho yao juu ya MASHONDE YATOKAYO KATIKA MWANADAMU”.

“Mashonde” ni jina lingine la “kinyesi kikavu” aidha cha mwadamu au mnyama.

Zamani na hata sasa katika maeneno baadhi, kinyesi kikavu kimetumika kama chanzo cha nishati, kwasababu kinawaka kwa haraka zaidi hata ya kuni, Hivyo kinaweza kutumika kama mbadala ya wa kuni kama kikiwa kwa wingi.

Katika maeneo ya mashariki ya kati, vinyesi vikavu vya ngamia na ng’ombe vilitumika kwa sana kama chanzo cha nishati, na nyakati chache chache sana (hususani vipindi vya ukame na dhiki), na vilitumika hata vya wanadamu lakini vyote vilikuwa ni vikavu….lakini sasa vinatumika hata vibichi kutokana na kukuwa kwa teknolojia.

Sasa tukirejea katika biblia, tunasoma Nabii Ezekieli akipewa maagizo na Mungu kuwa aoke mkate aina ya shayiri juu ya Mashonde (yaani kinyesi) cha mwanadamu, maana yake atumie kinyesi cha mwanadamu kama chanzo cha nishati, badala ya cha Wanyama. Sasa changamoto ya kutumia vinyesi, aidha vya mwanadamu au mnyama kama nishati ni “harufu”.

Maana yake kile kitakachopikwa juu ya mashonde(kinyesi) fulani kitabeba harufu ya kile kinyesi husika, kwahiyo kama mkate utaokwa juu ya kinyesi cha ngamia, basi ule mkate kwa sehemu utatoa harufu ya kinyesi cha ngamia, vile vile kama umeokwa juu ya kinyesi cha mwanadamu basi utatoa harufu ya kinyesi cha mwanadamu.

Hivyo Mungu alimwambia Ezekieli atumie kinyesi cha Mtu, kutengeneza huo mkate na kisha aule!.. Lengo la kumwambia vile si kumwadhibu Ezekieli, la! Kwani Ezekieli alikuwa ni nabii wa Mungu mwaminifu sana, hivyo aliambiwa afanye vile ili awe ishara kwa Taifa la Israeli kama Hosea alivyokuwa ishara kwa Taifa la Israeli alipoambia akaoe mwanamke wa uzinzi.

Maana yake kwa Ezekieli kula mkate uliookwa juu ya kinyesi cha mtu, ni ujumbe kwa wana wa Israeli kuwa na wao watakwenda utumwami mahali pa dhiki nyingi, na watapitia shida na njaa kali hata kufikia hatua ya kukosa chanzo bora cha nishati na hivyo kuona hata kinyesi chao wenyewe chaweza kufaa kwa nishati ya kuokea mikate ili tu waweze kuzishibisha nafsi zao wasife kwa njaa.

Hivyo Bwana Mungu alimchagulia Ezekieli hiyo ishara, lakini tunasoma Ezekieli alimsihi Bwana ambadilishie hiyo ishara kwani hakuwahi kula kitu najisi tangu amezaliwa, (kwasababu kulingana na desturi za kiyahudi kitu chochote kilichookwa juu ya kinyesi ni najisi), Hivyo akamsikia kwa ombi hilo, na Bwana Mungu akambadilishia, badala ya kutumia kinyesi cha mtu, basi atumie cha Ng’ombe, na ndivyo Ezekieli alivyofanya kama tunavyosoma…

Ezekieli 4:13 “Bwana akasema, Hivyo ndivyo wana wa Israeli watakavyokula chakula chao, hali kimetiwa unajisi, kati ya mataifa nitakakowafukuza

14 Ndipo nikasema, Ee Bwana MUNGU, tazama, roho yangu haikutiwa unajisi; maana tangu ujana wangu hata sasa sijala nyamafu, wala iliyoraruliwa na hayawani; wala nyama ichukizayo haikuingia kinywani mwangu.

15 Ndipo akaniambia, Tazama, NIMEKUPA MASHONDE YA NG’OMBE badala ya mashonde ya mwanadamu, nawe utakipika chakula chako juu ya hayo.

16 Tena akaniambia, Mwanadamu, tazama, nitalivunja tegemeo la chakula katika Yerusalemu; nao watakula mkate kwa kuupima, na kwa kuutunza sana; nao watakunywa maji kwa kuyapima, na kwa kushangaa;

17 wapate kupungukiwa na mkate na maji, na kustaajabiana, na kukonda kwa sababu ya uovu wao”.

Ni nini tunajifunza katika Habari hiyo?

Kikubwa tunachoweza kujifunza ni kuwa “tunapomwacha Mungu na kufuata mambo yote, tunajiweka katika hatari ya kuharibu Maisha yetu kuanzia ya rohoni mpaka ya mwilini”.  Wana wa Israeli hapa walimwacha Mungu na matokeo yake Maisha yao yaliharibika kwa njaa na umasikini na utumwa mpaka kufikia hatua ya kula mikate iliyookwa juu ya vinyesi vyao wenyewe, na ni hivyo hivyo hata leo, (kwasababu Mungu ni yule yule hajabadilika)… kama tukigeuka na kufuata mambo yetu, basi Maisha yetu yataharibika hata zaidi ya hayo ya wana wa Israeli nyakati hizo.

Je umempokea YESU KRISTO, kama Bwana na Mwokozi wa Maisha yako?

Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

EZEKIELI, ITABIRIE MIFUPA MIKAVU.

HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

Roho Mtakatifu ni nani?.

Kuna tofauti gani kati ya  “Edeni” na “Adeni”?

Bawa la mbuni hufurahi; Lakini mabawa yake na manyoya yake, je! Yana huruma? 

Rudi nyumbani

Print this post

Bwana alimaanisha nini kusema “atazamaye mwanamke kwa kumtamani” amezini naye?

Je! Kutamani kwa namna yoyote hakufai?

Mathayo 5:27  Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini; 28  lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.

JIBU: Ukitafakari hapo utaona mazingira Bwana anayoyazungumzia hapo ni ya uzinzi. Uzinzi ni kitendo cha kutoka nje ya mpango wa Mungu wa ki-ndoa katika eneo la kukutanika kimwili. ambao chanzo chake ni tamaa.

Sasa Bwana anaweka wazi kuwa uzinzi huanzia ndani kwenye mawazo ya mtu, moyoni mwake, tofauti na vile inavyodhaniwa kuwa mpaka wakutane dhahiri.

Lakini swali linaloulizwa je! Hatupaswi kutamani kabisa? Na kama tukitamani tutakuwa tunafanya kosa.

Kila kitu Mungu amekiweka katika utaratibu wake. Ni sawa na kusema kwanini ulafi ni dhambi, wakati Mungu ametuwekea ndani yetu hamu ya kula. Au kwanini nisile udongo wakati, najisikia hamu ya kuula mimi kama mjamzito, Au kwanini nisinywe pombe wakati ninajiona kabisa nini kiu nayo?. Kama Mungu angekuwa hapendi kwanini ameniwekea kiu hiyo?

Lakini unajua kabisa ukizidisha kula kuna madhara mwilini, pia ukila/ukinywa kitu kisichopasa utajisababishia madhara mwenyewe.

Vivyo hivyo katika tamaa. Haijawekwa, iwe ni “kutamani-tamani”, kila kitu kinachokatiza mbele. Bali Mungu aliiumba hiyo mahususi kwa wanandoa. Hivyo ikiwa upo humo huna budi kuzielekeza kwa mkeo/mumeo tu, na kama bado hujaingia humo, unapaswa uweze kuzitawala. Na hiyo inawezekana kabisa, usipozitengenezea mazingira, haziwezi kuamka na kukusumbua. Kwasababu maandiko yanasema moto hufa kwa kukosa kuni.

Ufanyeje.

Ni kujiepusha na mazingira yote, yatakayoweza kukupelekea kulipuka tamaa. Kwamfano, mazungumzo-zungumzo yasiyokuwa na maana na mtu wa jinsia nyingine, (kuchati), na kutazama video au picha zenye maudhui ya kizinzi, kuzungumza-zungumza habari hizo na marafiki zako, kuwa katika mazingira yasiyo ya kujishughulisha, kwamfano upo tu huna kazi yoyote umekaa, ni rahisi kupelekwa kwenye mawazo hayo na adui. Lakini pia kuwa msomaji wa Neno na mwombaji. Vitakusaidia sana kuwa mtu asiyetawaliwa na tamaa.

Na hivyo hata adui akitaka kukupeleka kwenye hali ya kutamani, kujengea picha, kutafakari,  basi unaweza kuyakataa hayo mawazo haraka, na ukaendelea kuwa salama, bila ya kuzini moyoni mwako. Kwasababu umevidhibiti.

Pia kumbuka jambo hili, si la wanaume tu, bali kwa jinsia zote. Hatupaswi kuishi maisha ya tamaa.

Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI.HATA UASHERATI NAO

Nini Tofauti kati ya uzinzi na uasherati ?

WAANDAA MEZA MBELE YANGU, MACHONI PA WATESI WANGU

Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Yesu alipopaa juu aliteka mateka, Kauli hiyo ina maana gani?

SWALI: Ni mateka yapi hayo aliyoyateka..na ni vipawa gani alivyowapa wanadamu.?

Waefeso 4:8 Hivyo husema, Alipopaa juu aliteka mateka, Akawapa wanadamu vipawa. 


JIBU: Ufalme wa Mbinguni umefananishwa na ngome Fulani, yenye hazina kubwa sana ambayo hupiganiwa na watu wengi kumilikiwa.

Na Ndio maana Bwana Yesu aliyasema maneno haya; 

Mathayo 11:12 Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka. 

Umeona unafananishwa na kitu cha kutekwa, sio kitu cha kuombwa, au kubembelezwa Fulani. Inahitaji kupambania.

Hivyo Kwa  maneno hayo utaelewa kuwa hata Bwana wetu Yesu Kristo, alikuwa katika operesheni hiyo ya kuuteka huo ufalme.

Na hiyo ilikuja kutimia siku ile aliposhinda pale Kalvari Kwa kifo chake na kufufuka katika wafu aliweza kumiliki vyote vya mbinguni na vya duniani…vyote viliwekwa chini yake.

Waefeso 1:20-23 aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho;  [21]juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia;  [22]akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo  [23]ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote. 

Sasa kwasababu ameteka Kila kitu cha mbinguni, aliteka pia na ‘uweza wote wa kiungu’ na kutupa sisi wanadamu, ndio vipawa au karama za Roho Mtakatifu, alizozitoa Kwa lengo la kuujenga mwili wa Kristo, kuhubiri injili, na kuhudumu.

Ndio hapo akawafanya wengine kuwa mitume, wengine kuwa manabii, wengine wainjilisti, wengine, wachungaji na wengine waalimu.(Waefeso 4:11)

Pamoja na karama zile 9, tunazozisoma katika 1Wakorintho 12.

1 Wakorintho 12:8 Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa, apendavyo Roho yeye yule; [9]mwingine imani katika Roho yeye yule; na mwingine karama za kuponya katika Roho yule mmoja;  [10]na mwingine matendo ya miujiza; na mwingine unabii; na mwingine kupambanua roho; mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha;  [11]lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye. 

Mambo ambayo hayakuwahi kuonekana zamani, hata za manabii..lakini Sasa twaziona zikidhihirika katika kanisa la Kristo.

Hivyo kumbuka Yesu hajateka mateka tu mbinguni. ni mpaka duniani. Maana yake ni kuwa sisi tuliomwamini hatuna budi pia kuwa watekaji. Hivyo popote pale uendapo kuhubiri injili, usiogope Wala usiwe mnyonge, vamia, hubiri Kwa ujasiri na hakika watu watabadilika kwasababu nguvu hizo tumepewa katika Kristo Yesu

2 Wakorintho 10:4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)  tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo; 

Bwana akubariki

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Wakaldayo ni watu gani?

TUNA JUKUMU LA KWENDA KUTEKA MATEKA.

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

TABIA ZA NJIA YA MUNGU KWA MKRISTO

MBINGUNI YUPO NANI SASA?

Rudi nyumbani

Print this post