HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

Luka 14:15 “Basi aliposikia hayo mmojawapo wa wale walioketi chakulani pamoja naye alimwambia, Heri yule atakayekula mkate katika ufalme wa Mungu”.

Enzi za biblia chakula kilichokuwa kinapewa heshima kubwa zaidi katika sherehe kilikuwa ni mkate uliookwa vizuri kwa upishi makini..Ni sawa na tuseme leo hii KEKI..Tunajua sherehe isiyokuwa na keki haijakamilika..miongoni mwa vyakula vyote vya kwenye sherehe keki huwa ndio inayopewa heshima kubwa kuliko zote na huwa inawekwa pale mbele kabisa, ili kuliwa na watu mahususi, Na sio na kila mtu tu aliyealikwa tu karamuni..bali wale walengwa tu..wengine wote watakula vyakula vingine vilivyoandaliwa kwa ajali yao..

Hivyo Keki huwa ndio inayofunua vyeo vya watu pale karamuni..Wale wanaopewa kipaumbele cha kwanza kuila ndio wanatambulika kuwa wale ni walengwa wa juu, au wenye kuheshimiwa ziadi, vivyo hivyo na wanao fuata na wanaofuata..

Sasa tukirudi katika mstari ule, tunapaswa tujiulize yule mtu aliona tukio gani mpaka ikamsukumwa kusema maneno kama yale “Heri yule atakayekula mkate katika ufalme wa Mungu”??..Tukisoma mistari ya juu kidogo tunaona alizungumza maneno yale baada ya kuona mfumo mzima wa karamu aliyokuwa amealikwa siku hiyo..Biblia inatuambia, Farisayo mmoja mkuu sana, aliyekuwa na cheo kikubwa, aliamua afanye karamu yake siku ya sabato, na alipofanya akawaalika ndugu zake tu, na watu wakubwa wakubwa tu, pengine mawaziri wa nchi, au wabunge wa nchi, na marafiki zake walio mtajiri na majirani zake wale wenye vyeo na fedha n.k. Na huko huko akamwalika huyu mtu na Bwana YESU pia..

Sherehe ile bila shaka ilikuwa ni ya kifahari sana, pengine walikuwa katika ukumbu uliopambwa sana. Sasa wakiwa huko baadhi ya watu walioalikwa wengine wakawa wanakimbilia viti vya mbeleni ili wawe wa kwanza kutambuliwa na kulishwa mkate au tuiite keki ya wakati huo..Utasema hilo tumelijuaje kuwa walikuwa wanakimbilia viti vya mbele?..Tumelijua hilo kwa maneno ya Bwana Yesu mwenyewe pale alipowaambia wale waliolikwa..

Luka 14:7 “Akawaambia mfano wale walioalikwa, alipoona jinsi walivyochagua viti vya mbele; akisema,

8 Ukialikwa na mtu arusini, usiketi katika kiti cha mbele; isiwe kwamba amealikwa mtu mwenye kustahiwa kuliko wewe,

9 akaja yule aliyewaalika wewe na yeye, na kukuambia, Mpishe huyu! Ndipo utakapoanza kwa haya kushika mahali pa nyuma.

10 Bali ukialikwa, nenda ukaketi mahali pa nyuma, ili ajapo yule aliyekualika akuambie, Rafiki yangu, njoo huku mbele zaidi; ndipo utakapokuwa na utukufu mbele ya wote walioketi pamoja nawe.

11 Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa”.

Unaona Vile vile utasema tumejuaje sherehe ile ilikuwa ni ya watu wakubwa tu..Tumelijua hilo kutoka katika kinywa chwa Bwana Yesu mwenyewe….

Luka 14:12 “Akamwambia na yule aliyemwalika, Ufanyapo chakula cha mchana au cha jioni, usiwaite rafiki zako, wala ndugu zako, wala jamaa zako, wala jirani zako wenye mali; wao wasije wakakualika wewe ukapata malipo.

13 Bali ufanyapo karamu waite maskini, vilema, viwete, vipofu,

14 nawe utakuwa heri, kwa kuwa hao hawana cha kukulipa; kwa maana utalipwa katika ufufuo wa wenye haki”.

Sasa, kutokana na hali nzima ya mazingira yaliyokuwa yanaendelea pale, kila mtu anatamani angepewa heshima ya mbele, aketi katika viti vya mbeleni, awe wa kwanza kulishwa keki, kutambuliwa..Ndio sasa tunaona huyu mtu mmoja aliyealikwa anatokea na kumwambia Bwana ama! kweli! HERI HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU..

Alipiga hesabu akasema kama duniani mambo ndio hivi, itakuwaje mbinguni mtu kupewa heshima ya juu zaidi katika karamu ile ya mwana-kondoo?.. Kuwa wa kwanza kulishwa MKATE wa mbinguni..Kupewa heshima ya viti vya mbele..Kuketi karibu kabisa na Kristo, kuzungumza naye kama mgeni rasmi mwalikwa..Utajisikiaje siku hiyo, kwenye meza moja na Ibrahimu, na manabii na mitume wa Kristo, mnacheka na kufurahi na Kristo akiwa katikati yenu…Ukiangalia wengi mmealikwa lakini si wote mpo katika meza moja na Bwana..

Mathayo 8:11 “Nami nawaambieni, ya kwamba wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi pamoja na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni;

12 bali wana wa ufalme watatupwa katika giza la nje, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”.

Leo hii yeye akiwa hapa duniani ataachaje kusema.. Heri yule atakayekula mkate katika ufalme wa Mungu?..Hata mtu yeyote anayejua thamani ya sherehe, anaelewa ni raha gani unajisikia unapopewa heshima ya juu zaidi katikati ya waalikwa.

Ndugu yangu karamu ya mwana-kondoo ipo karibu sana.. SIku ile ambayo parapanda italia, na wafu kufufuka, wakiungana na wale ambao watakuwa hai wakati huo, wote kwa pamoja wataisikia sauti ya Bwana Yesu ikiwaita hapo juu..Siku hiyo ndipo watakapoacha ardhi, na moja kwa moja safari ya kuelekea katika malango ya mbinguni itaanza..Siku hiyo wale walionyakuliwa hawataamini kwa macho yao kama kweli ndio siku hiyo imefika..Lakini ndivyo ilivyo wataanza safari mpaka mbinguni huku mabilioni kwa mabilioni ya malaika yakiwalaki..

Na moja kwa moja watapelekwa katika ukumbi wa kimbinguni usioelezeka kwa uzuri wake, miili yao wakati huo itakuwa imebadilishwa, watakuwa kama malaika..wana mavazi mazuri meupe yanayong’aa kama jua, wataketishwa katika sehemu waliyoandaliwa karamuni..Watayaona yale makao waliokuwa wamekwenda kuandaliwa kwa zaidi ya miaka 2000, na YESU.. Watazimia mioyo kwa furaha, wataketi watakula na kunywa na Bwana divai mpya..Watamwona Mungu,..watafurahi milele na milele.

Mathayo 26:29 “Lakini nawaambieni, Sitakunywa kabisa tangu sasa uzao huu wa mzabibu, hata siku ile nitakapokunywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu’’.

Lakini wakati huo huku chini, mambo yatakuwa tofauti wengine watakuwa wakilia na kusaga meno. Wakihangaika katika dhiki ya mpinga-kristo,.Wengine watakuwa wanajuta..

Ndugu dalili zote zimeshatimia, pengine sisi sote tutashuhudia tukio hili la kunyakuliwa kwa kanisa siku za hivi karibuni..Lakini swali linakuja Je! na wewe ni mmojawapo wa watakaonyakuliwa? Je! unaouhakika hata ukifa leo utakuwepo katikati ufufuo wa kwanza? Kama hujui basi ni ishara kuwa utabaki hapa duniani, ndugu umgeukie Mungu angali muda unao, Tubu dhambi zako kuwa maanisha kumuishia Mungu katika kipindi hichi kifupi cha kumalizia ili kama akirudi hapa katikati nawe uwe mmojawapo wa wale watakaokwenda naye.

Ufunuo 19:6 “Nikasikia sauti kama sauti ya makutano mengi, na kama sauti ya maji mengi, na kama sauti ya radi yenye nguvu, ikisema, Haleluya; kwa kuwa Bwana Mungu wetu, Mwenyezi, amemiliki.

7 Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondoo imekuja, na mkewe amejiweka tayari.

8 Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu.

9 Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo. Akaniambia, Maneno haya ni maneno ya kweli ya Mungu”.

Bwana akubariki.Tafadhali Share ujumbe huu na kwa wengine. Pia usiache kutembelea website yetu hii (www wingulamashahidi org) kwa mafundisho zaidi.

Maran Atha . Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

JE! UNAYO NAFASI MBINGUNI?

UFALME WA MUNGU HAUPATIKANI KIRAHISI.

Yeshuruni ni nani katika biblia?

JIEPUSHE NA MASHINDANO YA DINI.

MKUU WA ANGA.

ANTIPA SHAHIDI WANGU, MWAMINIFU WANGU.

Tofuati kati ya Myahudi, Mwisraeli na Muebrania ni ipi?

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments