Category Archive jehanamu

Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

Kifo ni ile hali ya uhai kutoka ndani ya kiumbe hai chochote. Kifo kinaweza kumtokea mtu, mnyama, bakteria, kirusi, mmea, jani n.k. Vyote hivi maadamu vina uhai ndani yao, vinapotokwa tu huo  uhai basi vinakuwa vimekufa.

Lakini Mauti ni nini?

Mauti ni kile kile kifo, isipokuwa ni mahususi tu kwa mwanadamu.. Huwezi kusema “mti” umekumbwa na mauti, au “mbwa” amepatwa na mauti.. Bali utasema, mti umekufa au mbwa amekufa. Ni mwanadamu tu ndiye anayekumbwa na mauti.

Lakini kwanini Kifo kitofautishwe na mauti?

Ni kuonyesha uzito wa hali hiyo kwa mwanadamu.. Kwamfano “Kilio” kinaweza kutokea kwa mtu yeyote yule, iwe ni mtoto au mtu mzima Lakini kikiwa kwa mtu mzima, hakiwezi kuchukuliwa kama kile cha mtoto, kwasababu kama vile wasemavyo wanajamii, “ukiona mtu mzima analia basi ujue kuna jambo”

Maana yake ni kuwa hadi mtu mzima anatoa machozi, ujue hayajaja bure bure tu, bali yana sababu nyuma yake, na matokeo mbele yake, kwasababu si desturi ya mtu mzima kulia. Nyuma yake utagundua aidha kuna msiba, au magonjwa, au kuumizwa moyo kusikoelezeka, kusalitiwa au kupoteza mali zake nyingi, au vitu, n.k.. Lakini mtoto mdogo anaweza akalia kwasababu zisizokuwa na maana au msingi wowote.

Vivyo hivyo katika kifo na mauti ni tendo lilelile..kuondoka kwa uhai.. isipokuwa linapokuja kwa mtu, linakuwa na uzito wa namna yake, kwasababu mwanadamu hakuumbiwa kifo, halidhalika kwa sifa yake na heshima na akili alizopewa na Mungu, jambo kama hilo ni anguko kubwa sana kwake..Mauti ni pigo kwa mwanadamu.

Sababu ya mauti kumpata mtu ni nini?

Ni dhambi..

Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Sisi wanadamu tulipoasi, adhabu hii ya mauti ilitukumba.. Hilo ni pigo kubwa sana kwetu, tofauti na Wanyama, wenyewe hawajui chochote, wala hawaelewi, kufa na kupotea kwao ni kitu cha kawaida, lakini sisi tunajua kwamba ipo siku uhai utatutoka..

Lakini heri ingekuwa ni kifo cha miili yetu tu halafu basi.. Lakini Huko mbeleni pia baada ya kifo, kuna adhabu ya kifo cha roho. Hiyo ndio inayoitwa mauti ya pili..Ambazo roho hizi zitamalizwa kabisa katika lile ziwa la moto..Hapo ndipo utaona, tofauti ya kifo cha mnyama, na kile cha mwanadamu.

Ndugu, ukikumbwa na mauti sasa, toa yale mawazo kwamba utakuwa kama mnyama tu.. Hapana, ukifa katika dhambi, utanyoshea moja kwa moja hadi jehanamu, ukisubiri siku ya ufufuo ifike uhukumiwe kisha utupwe katika ziwa la moto milele na milele.

Lakini Habari njema ni kwamba, Bwana Yesu alikuja kukomesha mauti kwa mwanadamu, na kwamba yeyote amwaminiye yeye, anakuwa amevuta kutoka katika mauti na kuingia kwenye uzima..

Yohana 5:24 “Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani”.

Umeona? Yaani Yesu akikuoa mauti inakuwa haina nguvu tena ndani yake..

Hivyo ndugu, wasubiri nini, leo usimkaribishe Yesu moyoni mwako.? Kumbuka hakuna mtu mwenye garantii ya kuishi milele. Au anayeijua kesho yake kama atakuwa duniani au la. Ukifa katika dhambi ni nani atakayekuponya na mauti ya roho yako? Huko utakapokwenda utakuwa mgeni wa nani. Kama huna uhakika, unajisikiaje kubaki katika hali hiyo?

Lakini nafasi sasa unayo, Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo, yaani kuongozwa sala ya toba ya kumpokea Yesu.. Basi fungua hapa kwa ajili ya mwongozo huo >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa kifo kinampata kiumbe hai chochote, lakini mauti ni mahususi kwa mwanadamu, kwasababu yenyewe inabeba maana kubwa zaidi ya kifo cha kutoka uhai tu. Mauti imebeba uchungu, majuto, masononeko, hukumu, nyuma yake, jambo ambalo kifo hakina.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

jiunge kwenye group la whatsapp la mafundisho ya kila siku kwa kubofya hapa >>> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Jehanamu ni nini?

Kuna hukumu za aina ngapi?

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

UNYAKUO.

DHAMBI YA MAUTI

BALI WANA WA UFALME WATATUPWA NJE!.

Rudi nyumbani

Print this post

MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.

SWALI: Kwanini watu watakaohukumiwa siku ile ya mwisho, wanaonekana kutofautishwa katika sehemu mbili, wengine watatokea “baharini”, na wengine katika “mauti na kuzimu”. Kwanini iwe hivyo na tofauti ya maeneo hayo ni ipi?

Ufunuo 20:11 “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana.

12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao.

13 BAHARI IKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE; NA MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.

14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto.

15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto”.


JIBU: Hukumu ya mwisho kabisa ni hukumu ijulikanayo kama “hukumu ya kiti cheupe cha enzi cha mwanakondoo”. Ni hukumu inayokamilisha wafu wote walioko makaburini, mbali na watakatifu.

Haitachagua wakubwa, wala wadogo, vijana au wazee. Waovu wote watafufuliwa wakati huu na kila mmoja atahukumiwa sawasawa na matendo  yake, kisha atatupwa katika lile ziwa la moto, aangamie huko milele.

Lakini biblia inatuonyesha siku hiyo waovu hao watatoka sehemu kuu mbili,

  1. ya kwanza, ni habarini,
  2. na ya pili ni Mauti na Kuzimu.

Kumbuka, lugha iliyotumika hapo ni lugha ya kinabii, na sio halisi kabisa kwamba bahari inayo wafu wake. Hapana.

Je Bahari ikawatoa wafu waliokuwa ndani yake, kunamaanisha nini?.

Tukianzana na wafu waliokuwa baharini. Tabia ya bahari sikuzote ni kubwa, haina mwisho, ukipotea humo, umepotea moja kwa moja. Na kibiblia maji mengi(bahari) inamaanisha ulimwengu.

Ufunuo 17:15 “Kisha akaniambia, Yale maji uliyoyaona, hapo aketipo yule kahaba, ni jamaa na makutano na mataifa na lugha”.

Hii ikiwa na maana sikuile ya mwisho, wafu wote, yaani waovu wa mataifa yote, wa lugha zote, waliokufa tangu Adamu, hadi wakati wa kurudi kwa Bwana Yesu kulinyakuwa kanisa lake (siku ya unyakuo). Wote hao watakuwa katika kundi la wafu watokao baharini. Watafufuliwa na kuhukumiwa.

Mauti na kuzimu kulifunua nini?

Lakini mara baada ya unyakuo kupita. Kuna tukio lingine litafuata, ambalo linajulikana kama dhiki kuu.

Kipindi  hichi kinajulikana kama kipindi cha utawala wa shetani(mpinga-kristo), watu wengi sana watauliwa, kutokana na dhiki ambayo Mungu ataruhusu shetani aisababishe, kwa waovu wote, watakaobakia duniani. (Tukiachia mbali wale ambao watakataa chapa ya mnyama). watauawa.

Ukisoma Ufunuo 6:8 inasema.

“Nikaona, na tazama, farasi wa rangi ya kijivujivu, na yeye aliyempanda JINA LAKE NI MAUTI, NA KUZIMU AKAFUATANA NAYE. Nao wakapewa mamlaka juu ya robo ya nchi, waue kwa upanga na kwa njaa na kwa tauni na kwa hayawani wa nchi”.

Umeona huyu farasi wa kijivujivu anaitwa mauti, akiambatana na kuzimu. Ambaye ni ibilisi akifanya kazi yake wakati huo. Naye atasababisha vifo vya robo ya watu waliopo duniani wakati huo. Kwamfano kwa dunia ya sasa ni Zaidi ya watu BILIONI 2, watauawa, na hiyo itakuwa ni katika mapigo ya ghadhabu ya Mungu, na vita vya Harmagedoni, na magonjwa, na wote hawa watakaokufa  moja kwa moja watakuwa chini ya “Mauti na kuzimu”.

Sasa biblia inaposema Mauti na Kuzimu ikatoa wafu wake, umeshaelewa kuwa ni wafu waliokufa katika hichi kipindi cha Dhiki kuu, ambao kimsingi walikuwa chini ya mpanda farasi wanne, aliyeitwa mauti na kuzimu.

Sasa kwanini sehemu zote mbili zitajwe?

Ni kuonyesha kuwa hukumu hiyo haitambakisha mfu hata mmoja. Itakuwa ni hukumu ya ulimwengu mzima kwa wale ambao hawakunyakuliwa, Au kuikataa cha ya mnyama.

Ikiwa leo hii umekufa kama mlevi, au fisadi, au kihaba, utakapokufa utakwenda katika Habari la kiroho. Lakini ikiwa utakufa katika dhiki kuu, vilevile utakwenda katika katika mauti na kuzimu. Na wote siku ya mwisho mtafufuliwa. Na kuhukumiwa, kila mmoja kwa kipimo chake. Kisha mtatupwa katika ziwa la moto.

Ndugu, hukumu ya Mungu ni ya kuiogopa sana, kwasababu hakuna nafasi ya pili baada ya kifo. Ukifa leo ghafla, ni moja kwa moja jehanamu ukisubiria siku hiyo ya ufufuo ifike, Kwanini hayo yote yatukute? Watu walio kuzimu leo hii Ni kilio na majuto ndivyo vinavyoendelea, wanatamani wangepata hata dakika 2 za kutubu lakini hawana. Wewe muda unao. Lakini unafurahia ulimwengu.

Mgeukie Kristo, leo akusamehe dhambi zako. Tubu kwa kumaanisha kabisa kuuacha ulimwengu na tamaa zake zote. Dhamiria kumfuata Yesu, naye atakuokoa, katika dakika hizi za majeruhi. Kumbuka Unyakuo ni wakati wowote, hilo linafahamika. Muda umeisha, dalili zote zimeshatimia. Mlango wa neema kwa mataifa hivi karibuni utafungwa.

Bwana atusaidie.

Maran Atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita.

MPINGA-KRISTO

UTAWALA WA MIAKA 1000.

JE MGOGORO WA URUSI NA UKRAINE,UMETABIRIWA KIBIBLIA?

Rudi nyumbani

Print this post

Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?

SWALI: Naomba kuelewa kwa undani Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?


JIBU:

Mbinguni,

Sehemu nyingi Biblia inaposema mbinguni, huwa inamaanisha moja kwa moja kule Mungu alipo Pamoja Malaika zake, Kule ambako Bwana Yesu alikwenda kutuandalia makao. Mahali ambapo sisi kama watakatifu bado hatujafika hata mmoja.

Ndio mbingu ya Tatu, ambayo Mtume Paulo alinyakuliwa kuonyeshwa baadhi ya vitu vilivyopo kule vipo kule ambavyo havielezeki kibinadamu, kwasababu upeo wetu ni mdogo. (2Wakorintho 12:1-4)

Ni juu sana, ambako, hatuna maelezo ya kutosha kupaelezea, mpaka tutakapofika.

2Nyakati 6:18 “Lakini Mungu je! Yamkini atakaa na watu duniani? Tazama, mbingu na mbingu za mbingu za mbingu hazikutoshi; siuze nyumba hii niliyoijenga!”

Peponi/Paradiso:

Ni mbingu ya mangojeo, ambayo sio makazi yetu ya kudumu. Mtakatifu anayekufa sasa hivi anakwenda mahali panapoitwa Peponi/Paradiso, akisubiria, siku ya unyakuo ifike, arudi kaburini achukue mwili wake, kisha aungane Pamoja na wale watakatifu watakaokuwa hai wakati huo, na moja kwa moja safari ya kwenda mbinguni ianze, kule Bwana Yesu alipo.

Yule mwizi pale msalabani, Bwana alimwambia maneno hayo;

Luka 23:42 “Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.

43 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”.

Wengine wanaiita mbingu ya pili, lakini vyovyote vile iitwavyo, bado ni mahali pa mangojeo pa watakatifu, Ndio kifuani pa Ibrahimu, yule maskini Lazaro alikwenda (Luka 16:19-31), ndio kule ambazo zile Roho zilizo chini ya madhahabu zilikuwa zinalia, zikiomba zilipiziwe kisasi kwa watesi wao.

Ufunuo 6:9 “Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao.

10 Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?

11 Nao wakapewa kila mmoja nguo ndefu, nyeupe, wakaambiwa wastarehe bado muda mchache, hata itakapotimia hesabu ya wajoli wao na ndugu zao, watakaouawa vile vile kama wao”.

Vilevile huku ndio kule wale wafu waliofufuka na Bwana Yesu walipoelekea kwa mara ya kwanza. (Mathayo 27:52-53)

Hivyo leo, hii ukifa katika Kristo, basi unakwenda katika eneo hili la mbingu, ambalo ni lizuri sana. Ukisubiri ufufuo wa mwisho.

Kuzimu:

Kuzimu kibiblia ni Neno lililomaanisha makao ya wafu  Au kaburini. Ambapo, waovu na wema walikuwa wanakwenda kabla ya Kristo kuja duniani, kuwatenganisha moja kwa moja kimakao,

 Ayubu anasema

Ayubu 14:13 “Laiti ungenificha kuzimuni, Ukanilinda kwa siri, hata ghadhabu zako zitakapopita, Na kuniandikia muda ulioamriwa, na kunikumbuka!”

Daudi pia alipazungumzia, (Zaburi 16:10), kwamba Bwana hatomwacha huko milele.

Lakini baada ya Bwana Yesu kuja, wakatifu walitoka huko  makaburini, na kwenda peponi/ Paradiso. Mahali pa raha Zaidi pa juu na si makaburini tena. Hivyo wanaobakia makaburini au kuzimu ni waovu.

Jehanamu:

Ni mahali pa mangojeo pa waovu, ni mahali pa mateso, kama vile Paradiso palivyo mahali pa raha pa mangojeo kwa watakatifu, vivyo hivyo jehanamu nako, ni mahali pa mangojeo pa watu waovu wanaokufa sasa. Wanaadhibiwa huko, wakingojea siku ile ya hukumu ya mwisho ifike. Ili wapewe hukumu yao, katika hukumu ya kile kiti cheupe cha enzi cha mwanakondoo, kisha wakatupwe kwenye lile ziwa la moto, ambalo ndio mauti ya pili ilipo.

Ni sawa na mhalifu anayekamatwa sasa hivi, kabla ya kuhukumiwa kifungo, huwa anawekwa kwanza mahabusu, akisubiria siku ya kupandishwa kizimbani ifike, ahukumiwe kisha akatumikie kifungo chake Jela, Ndivyo ilivyo kwa watu waovu wanaokufa sasa, na waliokufa zamani. Wanakwenda katika sehemu hii ya mateso, ambayo si ya kawaida.

Bwana Yesu alisema..

Marko 9:45 “Na mguu wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima, u kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili, na kutupwa katika jehanum; [

46 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]”

Je! Wewe ni wa makao yapi?

Swali, la kujiuliza ni Je! Tukifa leo, au Unyakuo ukitukuta leo, mimi na wewe tutakuwa wa upande upi? Katika mambo ambayo hupaswi kuyachukulia juu juu tu, basi ni mambo ya Maisha yako ya milele. Kwasababu ukishakufa hakuna nafasi ya pili tena. Kama umestahili Jehanamu basi utaendelea kuishi humo milele.

Ni heri ukamgeukie Kristo, maadamu muda mchache bado unao. Acha kutazama, mambo ya ulimwengu, kwani huwa yanapumbaza sana, kukufanya usione kama kuna mabaya yanakuja mbele, Moja ya hizi siku utajutia Maisha yako, uliishije endapo hukumpa Kristo Maisha yako leo.

Tubu dhambi zako, maanisha kumfuata Yesu.

Bwana atusaidie, kuyafahamu haya.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Je! kuna maombi yoyote ya kumtoa mtu aliyekufa kwenye mateso ya kuzimu?

MILANGO YA KUZIMU.

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

Rudi nyumbani

Print this post

MILANGO YA KUZIMU.

Milango ni wingi wa neno “mlango”..( Malango na Milango), ni neno moja. Katika biblia tunasoma Neno hilo likitajwa na Bwana Yesu..

Mathayo 16:18 “ Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; WALA MILANGO YA KUZIMU HAITALISHINDA.

19  Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni”.

Tunasoma Mamlaka hayo alipewa Mtume Petro,  na Mitume wengine pia walipewa mamlaka kama hayo (soma Yohana 20:23).

Sasa Mlango maana yake ni maingilio ya mahali, Vitu au watu wanaingia ndani ya nyumba au ndani ya mji kupitia milango yake, hakuna namna wanaweza kupitia kwingine.

Kwahiyo Kristo aliposema atalijenga kanisa ambalo milango ya kuzimu haitalishinda, Maana yake ni kwamba kanisa Bwana Yesu atakalolijenga, litakuwa na nguvu dhidi ya Milango yote ya kuzimu.

Sasa Milango ya kuzimu ni ipi?

Milango ya kuzimu ni mambo yote ambayo yanayompa mtu tiketi ya moja kwa moja kuingia kuzimu. Ifuatayo ni baadhi tu!

1Wakorintho 6:9  “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? MSIDANGANYIKE; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,

10  wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”

Kwahiyo Ibada za sanamu: Ni lango la kuzimu…Uasherani: ni lango la kuzimu!. Mtu anayefanya uasherati kajifungulia mlango wa kwenda kuzimu, Uuaji ni lango la kuzimu, Wizi ni lango la kuzimu, Anasa ni lango la kuzimu, Ulevi ni lango la kuzimu. Na mengine mengi yanayofanana na hayo!.. ndio maana Bwana Yesu kaitaja kama “Milango”..maana yake ipo mingi… Maana yake hata ukitenda mojawapo kati ya hayo bado utaingia kuzimu tu! Hata kama hutafanya hayo mengine yaliyosalia.. Ukiwa mzinzi tu, hata kama huibi, au sio mlevi, tayari utaenda kuzimu tu!..Kwasababu uzinzi, ni moja wapo ya lango la kuzimu..utafika kule kule tu, alipo mlevi na muuaji. Kwasababu kuzimu ina milango mingi.

Yakobo 2:10  “Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote.

11  Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria”.

Kwahiyo Kanisa Bwana atakalolitengeneza Maana yake litakuwa ni Kanisa Takatifu lisilo na kunyanzi wala hila, Kanisa ambalo litaliendea LANGO MOJA TU LA MBINGUNI (Yaani Yesu), na wala halivutwa na Malango ya kuzimu!. Kanisa la namna hiyo ndio Bwana aliahidi kulijenga.

Na alianza kulijenga siku ile ya Pentekoste, Roho Mtakatifu aliposhuka juu watu wake, akawajaza Roho Mtakatifu, na kuwapa nguvu za kushinda milango yote ya kuzimu.

Roho Mtakatifu ndio Muhuri wa Mungu, anaposhuka juu ya mtu, anaondoa ile kiu yote ya kufanya dhambi, kiasi kwamba dunia inamshangaa mtu huyo anawezaje kuishi bila kufanya zinaa katika kizazi hiki, anawezaje kuishi bila kuvuta sigara wala kunywa pombe, na hata hatumii nguvu kujizuia, anawezaje kuishi bila kutukana, bila kuiba, anawezaje kuishi maisha ya ustaarabu kiasi hicho, anawezaje kuwa na amani na huku hana kitu mfukoni, anawezaje kuwa na amani na huku kila mtu yupo kinyume naye, anawezaje kuishi bila kumkana huyo Yesu, anawezaje kuishi bila kuvutwa na anasa na starehe za dunia?..n.k pasipo kujua kuwa ipo nguvu waliyopewa ya kuishinda MILANGO YA KUZIMU.

Je na wewe unayo hiyo nguvu?. Au malango ya kuzimu yana nguvu juu yako?.

Kwa ufunuo Petro aliopewa ndio Bwana aliosema atalijenga kanisa lake juu yake, na  milango ya kuzimu haitalishinda…na ufunuo huo si mwingine zaidi ya YESU NDIYE MWANA WA MUNGU.

Mathayo 16:15  “Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?

16  Simoni Petro akajibu akasema, WEWE NDIWE KRISTO, MWANA WA MUNGU ALIYE HAI.

17  Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.

18  Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda”

Hivyo ukitaka milango ya kuzimu uishinde, njia ni moja tu, nayo ni KUMWAMINI YESU KUWA NDIYE MWANA WA MUNGU, Huo ndio Msingi, ambao kanisa la Mungu linajengwa juu yake. Ukitafuta msingi mwingine kamwe hutaweza kupata nguvu ya kuishinda milango ya kuzimu.

Na kumwamini Yesu, ni kutubu kwa kudhamiria kuacha kabisa dhambi zote, na baada ya hapo ubatizo, na mwisho kupokea Roho Mtakatifu, kama muhuri wa Mungu, ambaye huyo ndio ukamilifu wa kazi ya Mungu juu ya Mtu, ndiye anayetoa nguvu za kuyashinda malango ya kuzimu.

Kumbuka biblia inasema kuzimu haishibi..(Mithali 30:16), wanaoshuka huko ni wengi kila siku.Na ina milango mingi.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Je! kuna maombi yoyote ya kumtoa mtu aliyekufa kwenye mateso ya kuzimu?

LANGO LIMEBADILIKA.

WAOMBEENI WANAOWAUDHI.

UFUNUO: Mlango wa 3 part 3

Rudi nyumbani

Print this post

MATESO YA KUZIMU.

Je kuna uthibitisho wowote wa kimaandiko kwamba kutakuwa na mateso baada ya kifo kwa wale watakaokufa katika dhambi?.

Jibu ni ndio.. Tusome,

Luka 16:22 “Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.

23  Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, ALIPOKUWA KATIKA MATESO, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake.

24  Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu NINATESWA KATIKA MOTO HUU.

25  Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe UNAUMIZWA.”

Watu wote ambao watamkataa Yesu katika maisha haya, watakapokufa wataenda kuzimu kwenye mateso, watu wote wanaoliharibu hekalu la Roho Mtakatifu (yaani miili yao) kwa kuvaa vimini, nguo za utupu,  zinazochora maungo yao, wanaopaka wanja, wanaopaka hina, wanaoweka kucha za bandia, na wigi ili wafanane na wanawake wa ulimwengu huu, biblia imesema, wote wataingia katika lile ziwa la moto.

Na biblia inazidi kusema kuwa kuzimu haishibi watu na wala haijai,.. ni kubwa kuliko hii dunia tunayoishi.

Mithali 27:20 “KUZIMU NA UHARIBIFU HAVISHIBI;….”.

Mithali 30:15 “……………Kuna vitu vitatu visivyoshiba kamwe, Naam, vinne visivyosema, Basi!

 16 KUZIMU; na tumbo lisilozaa; Nchi isiyoshiba maji; na moto usiosema, Basi!“.

Kuzimu haishibi!!..Inapokea tu watu kila siku kila saa… Ipo nafasi kubwa mno kuzimu na watu wanaingia huko kila siku. Biblia haidanganyi.

Watu wote wanaofanya uasherati, na wanaopenda ulimwengu kuliko kumpenda Mungu, ikiwemo kutazama filamu za kidunia, na tamthilia za kidunia, wote wataenda katika ziwa la moto kama hawatatubu na kuacha njia zao mbaya, hiyo ni kulingana na Neno la Mungu.

Wote wanaocheza kamari, ikiwemo kubeti, na michezo yote ya bahati nasibu. Wakifa katika hiyo hali wataenda kuzimu.

Watu wote wanaoishi na wanawake/wanaume ambao si wake zao/waume zao, na wote wanaotazama picha za utupu katika mitandao, na wanaojichua, na walawiti wote.. hao wakifa sehemu yao itakuwa ni katika lile ziwa la moto, hiyo ni kulinga na Neno la Mungu.

Na wote watakaoingia kuzimu, hakuna mlango wa kurudi tena au kutoka huko, wakiwa katika mateso huko kuzimu watatamani kutubu lakini itakuwa wameshachelewa, watalia lakini hakuna atakayesikia, mateso yao yatakuwa makali usiku na mchana, watakuwa tu katika hali ya majuto, wakijutia kiburi chao, uchafu wao waliokuwa wanaufanya kwa siri au kwa wazi, uasherati wao waliokuwa wanaufanya bila hofu, ulevi wao waliokuwa wanaufanya kila siku, anasa zao N.k

Kwa uchungu na mateso mengi wakiwa huko, watajigundua kuwa shetani alikuwa amewapofusha macho na hivyo watamchukia shetani kwa ukomo wa chuki, lakini watakuwa wameshachelewa, wangepaswa wafanye hivyo kabla hawajaingia huko.

Ndugu hakuna maombi yoyote yanayopanda kutoka kuzimu kwenda kwa Mungu, hakuna kilio chochote kinachotoka kuzimu na kwenda kwa Mungu, wala hakuna utukufu wowote wa Mungu unaotoka kuzimu, hivyo Mungu hasikii kilio cha watu wanaolia kuzimu, wala kelele zao hazimfikii,  wala sifa zao kwa Mungu, hakuna mtandao kati ya kuzimu na mbingu. Walioingia huko ndio wamesahaulika hivyo.

Isaya 38:18 “Kwa kuwa kuzimu hakuwezi kukusifu; mauti haiwezi kukuadhimisha; Wale washukao shimoni hawawezi kuitarajia kweli yako.  19 Aliye hai, naam, aliye hai, ndiye atakayekusifu..”

Zaburi 6:5 “Maana mautini hapana kumbukumbu lako; Katika kuzimu ni nani atakayekushukuru?”

Shetani kanyanyua mahubiri, yanayosema kuwa kuna tumaini baada ya kifo, yaani wale watu waliokufa katika dhambi  na kuingia kuzimu, wanaweza kutolewa kutoka katika hayo mateso na kuingia peponi, kwasababu Mungu anasikia mateso yao na maumivu yao huko.. USIDANGANYIKE!!. Hakuna nafasi ya pili baada ya kifo, wala hakuna mageuzi wala mashauri kuzimu!!.. Wala hatuwezi kumwombea mtu aliyeshuka kuzimu, wala kumshauri Mungu juu ya hao waliopo kuzimu.

Mhubiri 9:10 “ Lo lote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; kwa kuwa hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, HUKO KUZIMU UENDAKO WEWE”.

Kaka/Dada unayesoma huu ujumbe, Iepuke kuzimu! Kwasababu kuzimu ipo kweli, sio nadharia, ni kitu halisi kabisa.  Na mtu akishuka huko hatatoka tena milele, na ndilo lengo kubwa la shetani, hataki kwenda mwenyewe kwenye moto wa milele, anataka kwenda na wengi.

Hivyo tusiruhusu hilo, aende peke yake na mapepo yake… Leo hii unapoisikia hii sauti nenda kachome hivyo vimini, na nguo zote za kikahaba, ikiwemo suruali, tupa hayo mawigi na mahereni unayovaa (mwili wako ni hekalu la Roho Mtakatifu).. usiangalie ni kundi kubwa kiasi gani linakiuka Neno la Mungu. Kuzimu utashuka peke yako, wala hutakuwa na jopo kubwa la watu, kama hutatubu. Wale funza wa kuzimu, ambao Bwana Yesu alisema hawafi watakutesa kule kuzimu usiku na mchana, na utalia wala sauti yako haitasikika popote, utakuwa peke yako, katikati ya giza nene, ukiungua tu, kwenye moto usiozimika.

Siku hiyo utasema heri ningesikia na kutubu, nisingekuwepo huku..lakini haitasaidia chochote.

Hivyo geuka leo na kutubu kwa vitendo, hiyo miziki unayoisikiliza ya kidunia  itakupeleka kuzimu, futa yote leo katika simu yako, na itoe katika nyumba yako, hizo filamu acha kuzitazama kuanzia muda huu, haijalishi zinapendwa na kusifiwa na wangapi. Kuanzia leo anza kumfuata Yesu kwa kumaanisha, na wala usiwe mshabiki wa Kristo, bali uwe mfuasi wake.

Kama umeamua kumfuata Yesu leo kwa kutubu, na kudhamiria kuacha vyote.. Bali uamuzi huo ni bora kuliko kitu kingine chochote ambacho ungeweza kukifanya, hivyo ili usirudi tena nyuma na uukulie wokovu, hakikisha unakishikilia kile ulicho nacho kwa bidii sana, kwa kusoma Neno la Mungu kwa bidii, na kutafuta kuzijua habari zake kwa bidii, mahali popote pale anapohubiriwa.

Na pia ili kuukamilisha wokovu wako, ni lazima ukabatizwe ubatizo sahihi kama bado hujabatizwa, Ubatizo sahihi ni ule wa maji mengi (Yohana 3:23), na kwa jina la YESU KRISTO, ambalo ndio jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu kulingana na Matendo 2:38, Matendo 8:16, na Matendo 19:5, kwaajili ya ondoleo la dhambi.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Ni kweli Waliolala Katika Kristo Wamepotea?(1Wakor 15:18)

Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “Saa yangu haijawadia?”

Kuota upo nchi nyingine.

FUNGUO ZA UZIMA, MAUTI NA KUZIMU.

KUZIMU NI WAPI

Je! kuna maombi yoyote ya kumtoa mtu aliyekufa kwenye mateso ya kuzimu?

Rudi nyumbani

Print this post

Maana yake nini “Wajapochimba waingie katika kuzimu, mkono wangu utawatoa huko”

SWALI: Huu mstari una maana gani? Amos 9:2 “Wajapochimba waingie katika kuzimu, mkono wangu utawatoa huko; nao wajapopanda hata mbinguni, nitawatelemsha toka huko”


JIBU: Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, Ni muhimu kufahamu sio kila mahali panapozungumzia Neno mbinguni katika biblia panamaanisha “mbinguni kule Malaika watakatifu walipo” Hususani katika agano la kale. Neno mbinguni pia linaweza kutumika na wapagani kumaanisha mbingu yao, kadhalika mbinguni kunaweza kumaanisha “sehemu iliyo inuka sana”.

Mtu aliyejiinua sana moyo wake katika roho anaonekana amepanda mpaka mbinguni.

Hali kadhalika sio kila mahali panalipoandikwa neno “kuzimu” katika biblia hususani agano la kale, kuna maanisha kule kuzimu, roho za viumbe walioasi zilipo!..hapana! sehemu nyingine panapotajwa neno kuzimu panamaanisha mahali pa chini sana. Kwamfano mtu aliye katika vifungo vingi vilivyomfanya awe chini sana, katika roho ni kama yupo kuzimu. (Yona na Mariamu na Hana).

Kwamfano tunaweza kusoma mistari ifuatayo ili tupate kuelewa vizuri.

Yona 2:1 “Ndipo Yona akamwomba Bwana, Mungu wake, katika tumbo la yule samaki,

  2 Akasema, Nalimlilia Bwana kwa sababu ya shida yangu, Naye akaniitikia; KATİKA TUMBO LA KUZİMU NALİOMBA, Nawe ukasikia sauti yangu.

3 Maana ulinitupa vilindini, Ndani ya moyo wa bahari; Gharika ya maji ikanizunguka pande zote; Mawimbi yako yote na gharika zako zote zimepita juu yangu”

Sasa hapo Yona sio kwamba alishuka kuzimu, mahali pa wafu, hapana, bali katika mazingira ya lile tumbo la samaki alilokuwemo ndio akakufananisha na KUZIMU. Mahali pabaja mfano wa kuzimu. Na mtu anapokuwa katika mazingira hayo yanayofananishwa na kuzimu, anaweza kupandishwa juu na kutoka huko, kama Yona na Hana mama yake Samweli.

1Samweli 2:6 “Bwana huua, naye hufanya kuwa hai; Hushusha hata kuzimu, tena huleta juu.

7 Bwana hufukarisha mtu, naye hutajirisha; Hushusha chini, tena huinua juu”

Na andiko lingine ndio hilo la kwenye Amosi 9:2 “Wajapochimba waingie katika kuzimu, mkono wangu utawatoa huko; nao wajapopanda hata mbinguni, nitawatelemsha toka huko”

Lakini mtu anayeshuka katika ile kuzimu halisi ya sehemu ya wafu walioasi, biblia inasema hawezi kurudi tena wala hawezi kutoka huko.

Ayubu 7:9 “Kama vile wingu likomavyo na kutoweka, Ni vivyo huyo ashukaye kuzimuni hatazuka tena kabisa.  Hatarudi tena nyumbani kwake, Wala mahali pake hapatamjua tena”.

Kwahiyo unaweza ukawa unapitia hali fulani katika hii dunia, ambapo mahali ulipo ni kama kuzimu, kila kona unaona giza limekuzunguka na mashaka, huoni unafuu popote, nataka nikuambie lipo tumaini kwa Kristo, maadamu bado unaishi, Bwana anaweza kukunyanyua tena na kukutoa huko Kuzimu, ulipo na kukupandisha juu, Hivyo Mwamini, omba kwa bidii na mshukuru, siku isiyokuwa na jina utaona miujiza.

Vivyo hivyo unaweza kuwa katika mahali fulani, au ukawa katika nafasi fulani na moyo wako  ukainuka sana, pengine ukajiona ni mungu-mtu, kila mtu anakuogopa, kila mtu anakuhofu au wewe ukajiona ni bora sana kuliko wengine wote wanaokuzunguka, nataka nikuambia mbele za Mungu, umejiinua na kufika mbinguni, na biblia inasema wote wajikwezao watashushwa (Luka 14:11).

Kwa maelezo marefu kuhusu  mbungini fungua hapa  >> mbinguni  ni wapi?

Hivyo mstari huo katika Amosi hauzungumzii Mbingu halisi, Malaika watakatifu waliopo, bali wala hauzungumzii Kuzimu halisi, wafu waliokufa katika dhambi walipo… Bali inazungumzia hali fulani ya maisha ambayo mtu yupo chini sana mfano wa kuzimu, na hali fulani ya maisha ambayo mtu kajiinua sana juu mfano wa mbingu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

FUNGUO ZA UZIMA, MAUTI NA KUZIMU.

ALIKUWAKO NAYE HAYUKO, NAYE YU TAYARI KUPANDA KUTOKA KUZIMU.

CHAPA YA MNYAMA

UJIO WA BWANA YESU.

MAMBO MANNE,YANAYODHOOFISHA UOMBAJI WAKO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

FUNGUO ZA UZIMA, MAUTI NA KUZIMU.

Shalom, mtu wa Mungu..karibu tujifunze Biblia…

Katika kisiwa cha Patmo, Bwana Yesu alimtokea Yohana alipokuwa ametelekezwa kule na kumwambia maneno mengi sana kama tunavyoyasoma katika kitabu cha Ufunuo. Na moja ya maneno aliyomwambia ni haya.

Ufunuo 1:17 “Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,

18 na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu”

Mtu aliye na funguo maana yake yeye ndie mwenye uwezo wa kuingia na kutoka, au ana uwezo wa kumruhusu mtu mwingine aingie au atoke. Ana uwezo pia wa kumfungia mtu nje au akamfungia ndani. Vilevile huwezi kuzungumzia funguo bila mlango.

Sasa kuna Malango makuu matatu katika maisha 1)  Lango la  MAUTI  na 2) Lango la KUZIMU na 3) Lango la UZIMA WA MILELE

  1. Lango la MAUTI.

Lango la mauti ni hatua ile ya mwisho kabisa mtu anapouacha mwili na kufa..Anakuwa anaingia katika upeo mwingine, ambao sio wa maisha haya ya duniani. Huko anakwenda kukutana na vitu vipya ambavyo havipo hapa duniani aidha vizuri au vibaya. Katika huu mlango au geti kabla ya agano jipya ilikuwa haiwezekani mtu aliyeenda huko arudie tena huku ulimwenguni. Ukifa hakuna kurudi, wanaoingia mautini wanakuwa wamefungiwa huko huko milele. Lakini baada ya Kristo na kuzitwaa funguo za Mauti, ndipo ukazaliwa uwezekano mpya wa wafu kurudia tena uhai… Na huo ulianza na Yesu mwenyewe kutoka kaburini na kurudia uhai, na siku ile tu alipokufa wapo wengine waliotoka makaburini Pamoja naye, wale waliokufa katika haki wakati wa agano la kwanza.

  1. Lango la Kuzimu.

Lango hili mtu analiingia baada ya kifo, Mtu aliyekufa katika dhambi, pasipo kutubu..anapokufa baada ya kuvuka lango la kwanza la Mauti, anaingia lango la pili la kuzimu. Huko ni sehemu mbaya isiyofaa. Na huko nako kuna malango mengine madogo madogo kumtenganisha mwovu na mwovu..hatutaingia huko sana. Lakini katika lango hili kuu la kuzimu, waliokuwa wamekufa katika uovu katika agano la kale, ilikuwa haiwezekani kutoka huko milele. Lakini Kristo alizitwaa funguo, na siku moja wafu waliopo kuzimu watatolewa huko kwaajili ya hukumu na wakiisha hukumiwa watatupwa katika ziwa la moto. 

Yohana 5:27  “Naye akampa amri ya kufanya hukumu kwa sababu ni Mwana wa Adamu. 

28  Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. 

29  Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu”.

Hivyo hata wafu waliopo kuzimu siku moja watatolewa huko kwaajili ya hukumu. Ufunuo 20:13  “Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake”. Ufufuo huu sio mzuri kabisa kwasababu ni wa hukumu.

Na roho ya malango ya kuzimu inafanya kazi hata kabla ya mauti, roho hiyo ndiyo inayowavuta watu wengi waiendee njia iliyopotea, shetani na majeshi yake wanafanya kazi kwa nguvu sana kuhakikisha ni kundi kubwa linataingia kuzimu.

  1. Lango la UZIMA WA MILELE:

Lango hili ni ndio la lenye maana  kwetu wanadamu, kwasababu ndio lango la uzima wa milele. Tofauti na malango hayo mengine ambayo yanahitaji kifo ndipo uyaingie.. Lango hili la uzima wa milele halihitaji mtu ufe, linaanzia hapa hapa duniani..wakati huu huu mtu anapumua na kuishi katika mwili wake. Lango hili ni bure kuingia lakini linahitaji kupambana sana, kwasababu yupo mwingine adui yetu ambaye hatamani hata mmoja wetu aingie.

Lango hili ni lile Bwana Yesu alilolisema katika kitabu cha Luka..

Luka 13:24  “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze. 

25  Wakati mwenye nyumba atakaposimama NA KUUFUNGA MLANGO, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako; 

26  ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu. 27  Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu. 

28  Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje”.

Kama tunapenda uzima wa milele basi lango hili lipo wazi mbele yetu leo, Bado Bwana Yesu hajalifunga na tunaingia ndani ya lango leo hili kwa kuyatii maneno yake yanayohubiriwa katika biblia takatifu na yanayohubiriwa na watumishi wake. Lakini tukiyakataa maneno yake basi mlango huu utafungwa mbele yetu.

Wapo watu wanaoishi hapa duniani ambao tayari wameshafungiwa mlango huu.(kwamfano watu waliomkufuru Roho Mtakatifu tayari wameshafungiwa, hao kamwe hawawezi kusamehewa tena kadhalika na watu baadhi ambao wameisikia injili kwa muda mrefu sana, wamepigiwa kelele sana, injili imerudiwa na kurudiwa masikioni mwao lakini hata kujigusa hawajigusi, wengi wameshafungiwa huu mlango hivyo kamwe hawataweza kusikia tena ile hamu ya kutubu na kuvutwa kwa Mungu).

Yesu ndiye mwenye funguo za hili lango na funguo hizo pia amewapa watumishi wake..Hebu tusome maandiko yafuatayao ili tuelewe Zaidi..

Yohana 20:21  “Basi Yesu akawaambia tena, Amani iwe kwenu; kama Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawapeleka ninyi. 

22  Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu. 

23  Wo wote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wo wote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa”.

Umeona hapo? Wale waliotumwa na Yesu kuhubiri wamepewa amri ya kuwafungia watu dhambi..Na hawawafungii kwa kutamka mdomoni kwamba “Fulani nakufungia dhambi” hapana hiyo sio tafsiri yake..Tafsiri ya kuwafungia watu dhambi iliyozungumziwa hapo ni hii >>

Mathayo 10:14  “Na mtu asipowakaribisha wala kuyasikiliza maneno yenu, mtokapo katika nyumba ile, au mji ule, kung’uteni mavumbi ya miguuni mwenu.

15  Amin, nawaambia, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma na Gomora kustahimili adhabu ya siku ya hukumu, kuliko mji ule”.

Kwahiyo mtu anaposikia injili na kuidharau tena kuikejeli..Yule mtumishi wa Mungu Roho Mtakatifu anapomwongoza aondoke mahali pale..hao waliosalia hapo nyuma, ndio Habari yao imeisha!..hawatapata tena neema kamwe, wataendelea katika njia hiyo hiyo! Mlango umefungwa tayari. Hali kadhalika wanapoikubali na kuitii, basi wanafunguliwa mlango ambao malango ya kuzimu hayataiweza..maana yake hao watu watakaoitii injili inayohubiriwa na mtu yule aliyetumwa na Mungu..basi ni ngumu sana kupotea…Watakuwa wana ulinzi Fulani wa daima ambao hata wakirudi nyuma kidogo nguvu ya Mungu itawarudisha kwenye mstari kwasababu tu! Waliitii injili ya Kristo. Bwana Yesu alimwambia maneno haya Petro.

Mathayo 16:18  “Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda. 

19  Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni”

Petro ni mfano wa watu wote waliothibitishwa na Mungu na kuwekwa wakfu kwa ajili ya kazi yake.

Hivyo dada/kaka unayesikia maneno haya. Kama unapenda kuishi Maisha yasiyo na mwisho…miaka milioni kwa mamilioni yasiyo na shida wala taabu, wala uchungu…Njia ni moja tu, nayo ni Yesu. Yeye ndiye mwenye funguo za Uzima wa Milele, na funguo hizo amewapa watumishi wake pia..Ukitaka kuishi, ukitaka uzima..Mkubali Yesu. Ukimkubali Yesu malango ya kuzimu yatakukwepa..kuna nguvu fulani itaachiliwa juu yako ambayo atakuweka katika mstari uliyoonyooka..Lakini kama hutaki kuishi milele, basi malango ya Mauti na kuzimu yanakungoja, hivyo chagua chaguo jema, Yesu ndiye lango na anakupenda!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

KUZIMU ni mahali pa namna gani, Je! huko wanaishi watu wakifa na kwenda kupata mateso au ni vinginevyo?

USIUZE URITHI WAKO.

HASIRA YA MUNGU KUKUWAKIA, KWA KUTOMZUNGUZIA TU MUNGU IPASAVYO.

FAHAMU MAJIRA ULIYOPO NA NINI UNAPASWA UWE NACHO.

MWANAMKE ULIYEKOMAA KI-UMRI, ITAMBUE HUDUMA YAKO.

NI KITU GANI PETRO NA YOHANA WALIKIGUNDUA KABURINI?

UHARIBIFU HAUNA KIFUNIKO.

Kuna ufufuo wa aina ngapi?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kuzimu kuna nini?

Kuzimu kuna nini?


Kuzimu sio mahali pa kupatamani hata kidogo, wala sio mahali ambapo utatamani hata adui yako aingie..

Na ndio maana Bwana Yesu alisema maneno haya..

Marko 9:43  “Na mkono wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima u kigutu, kuliko kuwa na mikono miwili, na kwenda zako jehanum, kwenye moto usiozimika;

44  ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]

45  Na mguu wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima, u kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili, na kutupwa katika jehanum;

[ 46  ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]

47  Na jicho lako likikukosesha, ling’oe, ulitupe; ni afadhali kuingia katika ufalme wa Mungu, una chongo, kuliko kuwa na macho mawili, na kutupwa katika jehanum;

48  ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki”.

Unaona, akiwa na maana kuwa kama itabidi kiungo chako kimoja tu cha thamani, kiondoke ni heri ukafanya hivyo kuliko uende kuishia huko milele.

Ikiwa unataka kujua kwa Urefu Jehanum ni nini? Unataka kujua hao funza wanamaanisha nini?, kuzimu kuna nini ,fungua hapa usome Habari yao.. >>>> Jehanamu ni nini?

Haya Maisha tuliyopewa ni ya kitambo kifupi sana, tunapaswa tujitathimini tukifa leo tutakwenda wapi ikiwa tupo nje ya Kristo? Biblia inatuambia Kuzimu haishibi watu, wala uharibifu hauna kifuniko, ikiwa na maana kuwa kila dakika, kila sekunde watu wanashuka huko wengi sana..

Lakini kwanini hayo yote yatukute angali bado tunao muda wa kutubu? Tutubu dhambi zetu, na kuyasalimisha Maisha yetu kwake, tuseme ulimwengu sasa basi, leo hii tunamgeukia Kristo.

Hivyo Ikiwa wewe ni mmojawapo ambaye unasema leo nipo tayari kumpa Yesu Maisha yangu, basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana.

Basi, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuwa na uhalali kwa kuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako.

Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwabudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Hongera kwa kuokoka.

Pia nakualika kutembelea tovuti hii mara kwa mara, yapo mafundisho mengi zaidi ya 1000, na maswali mengi sana yaliyojibiwa ya kwenye biblia..

Au kama utakuwa unapenda utumiwe kwa njia ya whatsapp basi utatumia ujumbe katika namba hii +255789001312 .. Bwana akubariki sana.

Mada Nyinginezo:

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

UTAWALA WA MIAKA 1000.

HAPO NDIPO WATU WALIPOANZA KULIITIA JINA LA BWANA.

Rudi Nyumbani

Print this post

NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.

Ufunuo 1: 17 “…Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,

18 na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu”.

Hayo ni Maneno ya Bwana wetu Yesu Kristo, akiliambia kanisa.. Sasa ukiona mpaka Bwana Yesu anasema anazo funguo za mauti, na kuzimu, ni dhahiri kuwa hapo mwanzo hakuwa nazo, zilikuwa kwa mwingine..Na huyo si mwingine zaidi ya Ibilisi.

Kumbuka Tahadhari ya kwanza Mungu aliyowapa Adamu na Hawa pale Edeni, kuhusu kula Tunda, haikuwa kwamba matokeo yake watakuwa uchi, au watajua mema na mabaya au watakula kwa jasho, au watazaa kuwa uchungu . Hapana, bali tahadhari aliyowapa ya kwanza na ya mwisho ilikuwa ni kuwa WATAKUFA(‘KIFO’)..Siku watakapokula matunda ya mti ule watakufa..akimaanisha watakufa kweli kweli..sio kwamba watakufa halafu siku moja watafufuka hapana, bali watakufa moja kwa moja..

Kwasababu Mungu alimwona muhasisi wa kifo hicho pale Edeni, Lakini wazazi wetu hawakuzingatia hilo badala yake wakala, Na matokeo yake ndio yale tuliyoyaona yalifuata baada ya pale..watu wakawa na makao mengine, baada ya pale yaliyoitwa KUZIMU. Chini ya mungu wao mpya aliyeitwa Ibilisi.

Na ndio maana katika agano la kale, hakukuwa na mtu aliyekuwa na uhakika wa maisha baada ya kifo, ni waisraeli tu ndio walifahamu hilo, nao si wote, isipokuwa wale tu waliokuwa wanafuatailia masuala ya Mesiya, ambaye alitabiriwa kuwa huko mbele atakuja kuwafufua wafu, lakini wengine waliosalia hawakujua hilo…

Na ndio maana tena utaona kulikuwa na mapambano makali kati ya mafarisayo na masadukayo, wengine waliamini kuna ufufuo wa wafu, na wengine hawakuamini hicho kitu (Soma, Matendo 4;1-2,23:7-8, Marko 12:18)..Ni kwasababu gani? Ni kwasababu suala la wafu kufufuliwa lilikuwa si jambo lililoandikwa kwa uwazi sana katika maandiko kama wengi wanavyodhani.. isipokuwa tu waliotambua jambo hilo ni wale waliokuwa wanafuatilia habari za Mesiya kuwa atakuja kufanya jambo hilo.

Kwahiyo wakati wote huo watu walikuwa wametawaliwa na roho ya mauti ya ibilisi.

Warumi 5:14 “walakini mauti ilitawala tangu Adamu mpaka Musa, nayo iliwatawala hata wao wasiofanya dhambi ifananayo na kosa la Adamu, aliye mfano wake yeye atakayekuja”.

Unaona wakati huo wote shetani alikuwa na funguo hizo, alikuwa wakati mwingine anao uwezo hata wa kuwaendea wafu walio watakatifu na kuzungumza nao, soma habari za samweli(1Samweli 28)..

Lakini sasa Kristo alipokuja alipindua kila kitu,(majira yakageuka), kwanza aliiondoa hofu ya mauti ambayo ilikuwa imewatawala wanadamu kwa muda mrefu tangu zamani..

Waebrania 2:14 “Basi, kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili, yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo, ili kwa njia ya mauti amharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi,

15 awaache huru wale ambao kwamba maisha yao yote kwa hofu ya mauti walikuwa katika hali ya utumwa”.

Na pili akaiteka ile Kuzimu iliyokuwa chini ya shetani, ambayo ndio ilikuwa makao ya wafu wote…

Na ndio maana siku ile alipokufa tu, utasoma makaburi yalipasuka na watakatifu wengi wakatoka makaburini

Mathayo 27:51 “Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;

52 makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala;

53 nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi”.

Tangu huo wakati hadi leo ibilisi hajui wafu wapo wapi na wanafanya nini saa hii, anachojua tu, ni kuwa wale watakatifu wapo upande wa PEPO(Paradiso) na wale waovu wapo sehemu ya mateso (Jehanum)..Hana uwezo wa kuleta mzimu wa mtu yeyote aliyekufa kwasababu sasahivi Kristo ndiye anayewamiliki walio hai na waliokufa soma Warumi 14:9. Kwahiyo hivyo vinavyoonekana na watu vyenye sura kama za wapendwa waliokufa..kiuhalisia sio wale watu wenyewe, bali ni roho tu za mapepo zilizovaa sura za watu waliokufa…

Kristo sasa ameshashikilia mamlaka yote, ya mbinguni, ya duniani na ya kuzimu..Haleluya.

Hivyo ikiwa wewe ni mtakatifu, kama utakufa leo basi ujue roho yako na nafsi yako itakwenda sehemu salama, yenye raha na pumziko la kweli, mahali pasipoelezeka panapoitwa Pepo, lakini wewe ambaye ni mwenye dhambi, ukifa leo, shetani hakuchukui bali utakayekuchuwa na Mungu mwenyewe na kwenda kukutupa katika jehanamu ya moto ukingoja hukumu ya siku ile ya mwisho..

Unatanga tanga nini kwa waganga wa kienyeji? Hao hawatakusaidia chochote, unawatafuta wanadamu, hao nao hawawezi kukuondolea hofu ya mauti na mashaka uliyonayo sasa, kwamba ukifa utakwenda wapi..Anayeweza kufanya hivyo ni Kristo tu peke yake, mwenye funguo za mauti na kuzimu.Yeye ndiye atakayeweza kukufanya uwe huru na hofu ya kifo, kiasi kwamba hata ikitokea unakufa leo, utakuwa na uhakika kuwa roho yako imekwenda sehemu salama. Ukingojea siku ile kuu ya kwenda mbinguni kwa Baba.

Hivyo leo mpe Kristo maisha yako kama bado hujampa, vivyo hivyo kama ni vuguvugu huu ni wakati wa kuwa moto!.. Tubu dhambi zao kwa kumaanisha kuziacha, hizi ni nyakati za mwisho, parapanda italia wakati wowote, na Yesu atawafufua kwanza wale waliokufa katika haki nao kwa pamoja na sisi tulio hai tutakwenda kumlaki mawinguni,..lakini jiulize wewe mwenye dhambi utakuwa wapi siku hiyo?..Au ukifa leo hii ni nani atayekusaidia huko uendako? Shetani anaivizia roho yako kwasababu anajua ukifa katika dhambi ni umepotea kwelikweli hata yeye mwenyewe hata kuona milele…Hivyo acha leo ulevi, wizi, rushwa, anasa, uasherati, vipodozi unavyopaka, vimini unavyovaa, matusi unayotukana na mambo yote yanayofanana na hayo..Na upokee Roho Mtakatifu ambaye ni ahadi kwetu tutakaomwamini Yesu.

Uamuzi ni wako, tafakari tena kisha chagua uzima. Wokovu ni bure kwa wote wanaouhitaji..Kristo anaokoa kweli.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

Nifanye nini ili niondokane na Hofu maishani mwangu?

SI KWA FAIDA YA MWENYEZI, BALI KWA FAIDA YETU.

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

NAO WAKADHANI YA KUWA YUMO KATIKA MSAFARA;

Nini maana ya maneno haya ya Bwana? “Nami nikiinuliwa juu ya nchi,NITAWAVUTA WOTE KWANGU”(Yohana12:32).

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! kuna maombi yoyote ya kumtoa mtu aliyekufa kwenye mateso ya kuzimu?

JIBU: Kama yatakuwepo maombi ya kumtoa mtu aliyekufa katika dhambi kuzimu …basi yatakuwepo pia maombi..au itakuwepo namna ya kumtoa mtu aliyekufa katika haki paradiso.

Lakini kama hakuna maombi yoyote au namna yoyote ya kumtoa mtu paradiso na kumpeleka kuzimu..kadhalika hakutakuwepo na maombi yoyote ya kumtoa mtu jehanum na kumpeleka paradiso.

Biblia inasema katika…

Luka 16: 22 “ Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.

23 Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake.

24 Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.

25 Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa.

26 Na zaidi ya hayo, KATI YETU SISI NA NINYI KUMEWEKWA SHIMO KUBWA, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu”.

Hapo inasema kumewekwa shimo kubwa…SHIMO Ni lugha ya kuonyesha kwamba haiwezekani kwa namna yoyote mtu aliyeko jehanamu kuvuka kuingia paradiso…wala aliyeko paradiso kwenda kuzimu..Ikifunua kwamba hata maombi hayawezi kumvusha mtu katika shimo hilo…

Nafasi ya kuvuka kutoka mautini kuingia uzimani tunayo tukiwa hapa hapa duniani. Tukishindwa kutengeneza mambo yetu tukiwa hapa duniani tukifika kule hakuna hiyo nafasi…Ibrahimu ambaye sisi sote tunamwita Baba wa Imani, ambaye ni mtakatifu na aliyekubaliwa na Mungu pengine kuliko mimi na wewe ameshindwa kumtoa huyo Tajiri kuzimu na kumwingiza paradiso…Je wewe au mimi ambaye tuna dhambi tutawezea wapi?…Ibrahimu ambaye sasa yupo utukufuni ambaye kashashinda vita vya ulimwengu huu, kashindwa kumtoa tajiri kuzimu… sisi ambao hata hatujui kinachoendelea ng’ambo..maombi yatu yatamtoaje mtu aliyekufa kutoka kuzimu kumpeleka peponi?.

Hivyo hiyo inatutahadharisha kuyaangalia Maisha yetu..Tujihakiki kila siku je tunampendeza Mungu?..Je tunastahili kuingia mbinguni?..Kama bado basi tutengeneze mambo yetu kabla siku zetu za kuishi hazijakwisha. Tusidanganywe na uongo wa shetani, ambao unakuja kwa kivuli cha faraja kwa ndugu zetu waliotangulia lakini kumbe nyuma yake kumejaa roho ya uongo na upotevu..Tuishi maisha masafi na ya kuwahubiria ndugu zetu kabla hawajaondoka duniani..Kwasababu hakuna nafasi ya pili baada ya kifo.

Hakuna kupitia kwanza ‘Toharani’ kisha ndio tuende mbinguni kama baadhi ya madhehebu yanavyoamini mfano wa Katoliki..Tukishakufa habari yetu ndio inakuwa imeisha hapo. kama tumeangukia upande wa uzima, basi tutabakia huko uzimani daima, kama tuliangukia upande wa mauti basi tutaishi mautini milele.

Tubu ikiwa bado hujatubu, angali nafasi ipo.

Bwana akubariki. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani?

DUNIANI MNAYO DHIKI.

USIFE NA DHAMBI ZAKO!

ALIJARIBIWA SAWASAWA NA SISI KATIKA MAMBO YOTE.

Je! Ni sahihi kuoa/kuolewa na mtu uliyemzidi umri?

Rudi Nyumbani:

Print this post