UHARIBIFU HAUNA KIFUNIKO.

UHARIBIFU HAUNA KIFUNIKO.

Ayubu 26:6 “Kaburi li wazi mbele yake, Uharibifu nao hauna kifuniko”.

Kama tunavyojua mashimo mengi yanayochimbwa huwa yanawekwa mifuniko juu, ili kusudi kwamba ikitokea mtu mgeni akapita kwa njia ile iwe ni mchana au usiku kwa bahati mbaya asitumbukie,

Lakini biblia inatumbia kaburi la mauti lipo wazi sikuzote, na uharibifu hauna kifuniko..

Uharibifu kwa jina lingine ni kuzimu.. Akimaanisha kuwa kuzimu haina mfuniko wowote, mfano ikitokea umepita katika njia hiyo kwa namna yoyote, basi kutelezea humo na kuzama ni mara moja..haijui huyu ni mgeni, au ni mwenyeji au ni mtoto. Ukizama umezama!.

Na ndio maana leo hii mtu akifa katika dhambi, moja kwa moja atajikuta ghafla tu yupo kuzimu, (Ayubu 21:13). atajiuliza amefikaje fikaje huko. Lakini ndio hivyo tayari ameshafika huko mahali ambapo hatatoka tena milele,.atakachokuwa anasema huko ni Laiti ningejua, laiti ningefahamu, nisingefanya hiki au kile..

Biblia inatuambia..

Isaya 5:14 “Kwa hiyo kuzimu kumeongeza tamaa yake, kumefunua kinywa chake bila kiasi; na utukufu wao, na wingi wao, na ghasia yao, naye pia afurahiye miongoni mwao, hushuka na kuingia humo”.

Unaona? Unashuka kwa ghafla sana, tusitamani tufike huko. Kila inapoitwa leo, tumwombe Mungu vilevile tujitahidi kukaa mbali na dhambi kwa kadiri tuwezavyo.

Watu wote wanaochukuliwa katika maono na kupelekwa kule, na kuonyeshwa sehemu tu ya mambo yanayoendelea humo, huwa hawatamani kuhadithia, kwasababu wote wanaowaona humo, ni vilio vya majuto tu, wanatamani wapewe dakika hata moja warudi watengeneze mambo yao lakini haiwezekani tena..

Ayubu 7:9 “Kama vile wingu likomavyo na kutoweka, NI VIVYO HUYO ASHUKAYE KUZIMUNI HATAZUKA TENA KABISA.

10 Hatarudi tena nyumbani kwake, Wala mahali pake hapatamjua tena”.

Utatamani urudi duniani siku hiyo itashindikana…Mfano tu wa Lazaro na yule Tajiri…Yule tajiri aliomba akawahubiriwe ndugu zake ili wasifike mahali pale alipo pa mateso lakini ilishindikana..Na Watu wanaoshuka huko ni wengi sana wasiohesabikia. Hivyo mimi na wewe tulio hai, tuikwepe dhambi…

Tusipende kufuata mikumbo ya watu, kisa wanakwenda Disko na sisi tuende, kisa wanavaa nguo za kikahaba na sisi tuvae, kisa wanafanya uasherati na sisi tufanye..kisa wanatumia pombe na sisi tutumie ..Kamwe usiwaige hao..Kwasababu wanaoshuka huko ni wengi sana, na kuzimu haijai watu..(Mithali 27:20, Mithali 30:16)

Kumbuka hizi ni zile siku zilizotabiriwa za maasi kuongezeka. Kwahiyo usishangae kuona wimbi kubwa la watu wanaofanya dhambi hadharani bila hofu.

Zaidi macho yetu yaelekee mbinguni, kwani unyakuo upo karibu, Au hata kama hautakukuta wakati wako, basi tufahamu kuwa kifo nacho hakipo mbali, Hivyo ni wajibu wetu kujiimarisha na kujithibitisha kwamba tupo katika mstari wa Imani.

Luka 12:35 “Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka;

36 nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara”.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

IELEWE SAUTI YA MUNGU.

KUOTA MTU AMEKUFA/NDUGU AMEKUFA.

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 2

MADHARA YA KUTOA MIMBA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Nasibu Saul Kottei
Nasibu Saul Kottei
2 years ago

Maran atha.!